Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110105 articles
Browse latest View live

TAHADHARI KWA WATUMIAJI WA VIVINJARI VYA “INERNET EXPLORER”

$
0
0
Mwishoni mwa juma pamegundulika hali mbaya ya kiusalama mtandao itakayo waathiri watumiaji wa kivinjari kijulikanacho kama "internet explorer" ambapo watumiaji wa kivinjari hicho wako hatarini kuweza kuingiliwa kirahisi computer zao na wahalifu mtandao.

Jumamosi tangazo hilo linalosomeka hapa "TANGAZO" limeweza kubainisha internet explorer toleo la 6 hadi la 11 yote yameweza kugundulika yanatoa mwanya kwa wahalifu mtandao kupenya kwa watumiaji na kuchukua taarifa zozote zitakazo patikana kwenye computer zao.

Aidha, Kampuni inayo jihusisha na na maswala ya ulinzi mtandao ya "FireEye" imeonyesha takwimu yakua asilimia 56 ya vi vinjari kwa hadi ilipofikia mwaka 2013 vilikua hatarini kuingiliwa na wahalifu. na kubainisha kwamba wahalifu wamekua na uwezo wa kutengeneza vivinjari visivyo sahihi vinavyo weza ruhusu wahalifu hao kuingilia computer za watu mara tu watumiaji wa vi vinjari hivyo wanapo vitumia.

Microsofti imeshindwa kupata suluhu ya tatizo hilo ambapo CERT ya marekani imetoa tahadhari linalosomeka hapa "CERT ALERT" yakuwa watumiaji vivinjari vya "internet explorer" wanapaswa kubadil vivinjari kwa sasa na badala yake watumie vingine hadi hapo tatizo litakapo rekebishwa na kutangazwa vingenevyo.

Aidha,Christian Tripputi Ametumia muda huu kuonya watumiaji wa Window XP yakuwa kwa sasa wako hatarini kwani hakuna tena huduma zitakazo endelea kutolewa kwa Window hiyo na wahalifu mtandao wamesha anza kuleta madhara kwa wote wanaoendelea na matumizi ya windo hiyo na kusisistiza hapata kuwa na msaada kwa waathirika. Taarifa ya awali ilyotelewa na Yusuph kileo kuhusiana na matumizi ya   Window XP inasomeka hapa “TAHADHARI KWA WATUMIAJI WA WINDOW XP"

SHEREHE ZA MIAKA 50 YA MUUNGANO ZAFANYIKA PARIS UFARANSA

$
0
0
Watanzania waishio nchini Ufaransa walikutana Jumamosi mchana tarehe 26 Aprili nyumbani kwa Balozi wa Tanzania mjini Paris ili kusherehekea miaka 50 ya muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika.
Balozi wa Tanzania Nchini Ufaranza,Mh. Begum Karim Taj akipokea keki maalum kwa ajili ya sherehe hizo za Muungano wa Tanzania katika hafla iliyofanyika nyumbani kwa Balozi,Mjini Paris Ufaransa.
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa akiwa na watoto mjini Paris.
Mh. Balozi Begum Taj akiwa na baadhi ya watanzania waishio nchini Ufaranza.

Vodacom yawaunganisha Buhigwe kwenye mtandao wa simu za mkononi

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli akiuzindua rasmi mnara wa Vodacom kuashiria kuanza kupatikana huduma za kampuni hiyo ya simu nchini katika kijiji cha Bukuba kilichopo Buhigwe mkoani Kigoma. Pembeni yake ni Meneja wa Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim. Wengine ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo Malcelina Mbehoma na Mwenyekiti wa Halmashauri Abel Kabona. Vodacom inaendeleza mkakati wake wa kuwaunganisha watanzania wa vijijini na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi ili kuwawezesha kuboresha maisha yao.
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma Charles Gishuli (mwenye koti) akitumia simu yake ya mkononi kutuma fedha kupitia huduma ya M-pesa mara tu baada ya kuzindua huduma za Vodacom katika kijiji cha Bukuba mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Abel Kabona. Vodacom inaendeleza mkakati wake wa kuwaunganisha watanzania wa vijijini na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi ili kuwawezesha kuboresha maisha yao.
Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli jinsi ambavyo wakazi wa kijiji cha Bukuba Mkoani Kigoma wanavyoweza kupata huduma za Intaneti kupitia mtandao wa Vodacom mara baada ya Mkuu huyo wa Wilaya kuzindua rasmi huduma za Vodacom kijijini hapo mwishoni mwa wiki. Kushoto (mwenye kofia nyekundu) ni Mhandisi wa Vodacom Mkoa wa Kigoma Adam Nyamgali.
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Charles Gishuli akiongea na wakazi wa kijiji cha Bukuba na vijiji jirani waliofika kushuhudia uzinduzi wa mnara wa mtandao wa Vodacom kijijini hapo mwishoni mwa wiki. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim. Wengine kutoka kuhsoto ni Mhandisi wa Vodacom Adam Nyamgali, Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya Renatus Mkasa na Kaimu Mkurgenzi Mtendaji wa Wilaya Malcelina Mbehoma. Kupatikana kwa huduma za Vodacom kijijini hapo kunatarajiwa kufungua ukurusa mpya wa maendeleo ya kiuchumi an kijamii kijijini hapo.

ZIARA YA SADIFA YATIKISA KATA YA KAWE

$
0
0
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM, Taifa, Sadifa Juma (wapili kushoto) akiwasili kwenye Uwanja wa Mkutano eneo la Tanganyika Packers, Kawe Dar es Salaam, Jumapili, Aprili 27, 2014 ambako mbali na kuhutubia mkutano wa hadhara, alikabidhi vifaa vya michezo kwa timu mbalimbali za soka katika kata ya Kawe. Kulia ni Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Kawe, Lilian Rwebangila na Katibu wa UVCCM wa kata hiyo, Aisha Katundu na kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Kata hiyo Said Herry.
 Vijana wa CCM na wananchi kwa jumla wakimsindikiza Sadifa, kwa hamasa kuingia uwanjani
 Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM (Bara) Mfaume Ali Kizigo akihutubia kwenye mkutano wa hadhara wa UVCCM uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe Dar es Salaam, Jumapili ya Aprili 27, 2014, kumkaribisha Sadifa kuhutubia.
 Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Kawe Lilian Rwebangila akimkaribisha Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Hamis Juma, kuhutubia mkutano huo wa hadhara kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe.
 Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Hamis Juma, akihutubia mkutano wa hadhara huku shamrashamra zikitawala, kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, Dar es Salaam, Jumapili Aprili 27, 2014.
 Sadifa (kushoto) akishuhudia wakati Katibu wa CCM wilaya ya Kinondoni, Athuman Shemsha, akimtawaza Kada wa CCM, Vincet Massawe, wakati wa mkutano wa hadhara wa UVCCM  uliofanyika Viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, Dar es Salaam, Jumapili, Aprili 27, 2014

PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Airtel yazindua whatsapp, Facebook na Twitter bure kupitia Vifurushi vya yatosha

$
0
0
·       Yatangaza facebook, whatsapp and twitter BURE
·       Sasa wateja kupata whatsapp, Facebook na Twitter bure kupitia yatosha bando
  kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inayoongoza kwa kutoa huduma bora imezindua huduma ya kibunifu itakayowawezesha wateja wake kupata na kuunganishwa kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook, Whatsapp na twitter BURE kupitia huduma ya Airtel yatosha.

Akiongelea kuhusu huduma hiyo Mkuu wa kitengo cha mawasiliano wa Airtel Bi Beatrice Singano Mallya alisema” sasa ni bure kabisa kwa wateja wetu wote wa Airtel kuunganishwa na mitandao ya kijamii ya Whatsapp, Facebook na Twitter. Airtel tunayofuraha kutoa nafasi kwa wateja wetu kuwasiliana na marafiki na familia kupitia mitandao hii ya kijamii bure bila makato yoyote, huku tukiendelea kuthibitisha kuwa Airtel Yatosha ni BABA LAO!”
Aliongeza kwa kusema mteja yoyote atakayenunua kifurushi cha data cha yatosha kuanzia sasa iwe ni cha siku, Wiki au Mwezi vifurushi vyao vya internet vya MB au GB  hazitakatwa katika matumizi ya Facebook, Whatsapp na Twitter na badala yake wataweza kutumia vifurushi vyao vya data kwenye kuperuzi katika mitandao mingine kama vile YouTube na mingine mingi kadri ya mahitaji yao”
Akiongea kuhusu namna ya kujiunga Meneja Masoko wa Airtel Bi Upendo Nkini alisema” ili kupata Whatsapp, Facebook na Twitter BURE wateja watatakiwa kupiga *149*99# kisha kuchagua kifurushi kinachowafaa na kuanza kufurahia BURE Whatsapp, Facebook na Twitter”
“Sambamba na hilo katika kuendeleza ubunifu na kurahisiaha upatikanaji wa vifurushi vya Yatosha,  tumewawezesha wateja wetu  kutumia simu za kununua vifurushi vya yatosha kwa ajili ya marafiki zao familia na kubaki wakiwa wameunganishwa na kufurahia mitandao hii ya kijamii ya Whatsapp, Facebook na  Twitter BURE, furahia kuunganishwa katika mawasiliano kupitia mtandao wa Airtel” aliongeza Nkini

Serikali yadhamiria kuboresha huduma kwa nchi jirani-Mwakyembe

$
0
0
Na Mwandishi wetu, Pwani
Serikali imesema imedhamiria kukabiliana kwa vitendo na changamoto ya kutotumia fursa na nafasi ya kijiografia ya nchi ya Tanzania na kuifanya kuwa shindani na hivyo kuleta maendeleo endelevu na ustawi wa jamii.
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe amesema jana mkoani Pwani kuwa hakuna sababu inayoifanya Tanzania isiwe taifa shindani kibiashara katika ukanda huu wa Afrika kutokana na nafasi yake kijiografia miongoni mwa sababu nyingine.

Katika kuonyesha dhamira hiyo kivitendo, Waziri huyo anaongoza ujumbe wa maafisa mbalimbali wa serikali katika kukagua njia kuu toka jijini Dar es Salaam-Tunduma hadi katika mji wa Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Barabara hiyo kuu ndiyo inayotumiwa na magari ya mizigo ya wafanyabiashara wa DRC toka bandari ya Dar es Salaam, hivyo kwa kukagua maeneo ya mizani, serikali inataka kuondoa kero zinazowakumba wafanyabiashara hao.
“Tanzania imebarikiwa kuzungukwa na nchi sita zisizo na bahari na tuna ukanda wa bahari wenye urefu zaidi ya kilometa 1500…lazima tutumie bahati hii kujiletea maendeleo,” aliwaambia waandishi wa habari mara baada ya kutembelea kituo cha kupimia magari cha Maili Moja, Kibaha, mkoani Pwani.
Ziara ya ujumbe huo ilianzia katika bandari ya Dar es Salaam ambapo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Madeni Kipande ulitoa taarifa fupi kwa Waziri huyo kuhusiana na shughuli bandarini hapo.
Pia ujumbe ulitembelea Kitengo cha kupakia na kupakua kontena (TICS) bandarini hapo.  Maeneo mengine yaliyotembelewa ni pamoja na bandari za nchi kavu (ICDs) maeneo ya Kurasini ambapo Waziri alishuhudia msongamano mkubwa wa malori ya mizigo katika njia hiyo. “Tunataka kubadilika, lazima tubadilike,” alisema Waziri Mwakyembe.
Ujumbe huo unaosafiri kwa barabara ili kupata taarifa za moja kwa moja toka kwa wahusika, unajumuisha pia Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Bw. Peter Serukamba pamoja na mjumbe wa kamati hiyo, Bi. Zarina Madabida.
Akiongea baada ya kukagua kituo cha mizani cha Mikese, Bw. Serukamba alisema wanataka kuangalia na kufahamu kila tatizo kwa kina ili hatimae ufumbuzi wa kudumu upatikane. “Tuko katika ushindani mkubwa, lazima kama nchi tubadilike kwa haraka,” alisema Mwenyekiti huyo wa kamati.
Kwa upande wake, akitoa mfano wa kasoro zilizopo katika vituo vya kupima mizigo alisema bado muda unaotumika kushughulikia gari moja ni mrefu na hivyo kupunguza ufanisi. Waziri Mwakyembe alisema kasoro hizo pamoja na nyingine zitapatiwa ufumbuzi hivi karibuni kutokana na mikakati iliyopo.
Ziara hiyo ya kikazi ya zaidi ya kilometa 2,000 itahitimishwa kwa kufunguliwa kwa ofisi ya TPA Alhamis wiki hii katika mji wa Lubumbashi ambayo ni moja ya mikakati ya kuongeza ufanisi wa bandari katika kuhudumia nchi jirani.
Pamoja na maafisa wengine, ujumbe huo unajumuisha pia maafisa waandamizi toka TPA na Mamlaka ya Usafiri wan chi kavu na Majini (SUMATRA).
Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kuwa shehena yote ya mizigo ya nchi 6 zitumiazo bandari ya Dar es salaam, (yaani Zambia, D R Congo, Burundi, Rwanda, Malawi na Uganda) imeongezeka kutoka tani millioni 3.55 mwaka 2011/12 hadi kufikia tani millioni 4.05 mwaka 2102/13, hiyo ikiwa ni ongezeko la asilimia 14.2.

New Mellinium Women Group yafanya Kampeni Maalumu ya Saratani Nchini

$
0
0

  Mke wa Makamu wa RaisMama Asha Bilal  (L)na Mlezi wa chama cha wake wa viongozi Mama Tunu Pinda wakipata maelezo kutoka kwa Prof Amyn Alidina ambaye ni mkuu wa kitengo kinachotoa   huduma ya matibabu ya ugonjwa wa Saratani inayo tolewa katika Hospitali ya Aga Khan iliyopo jijini Dar es salaam Wake wa viongozi walikuwa katika Hospitali ya Aga Khan katika kampeni ya kuhamasisha Watanzania kuwa natabia ya kuchunguza afya zao ilikujua mapema kama wanatatizo la Saratani  nawaweze kupata matibu matibabu yanyo stahili Picha na Chris Mfinanga
 Mke wa Makamu wa Rais Mama Asha Bilal (R) akiwa na mlezi wa chama cha Wake wa Viongozi Mama Tunu Pinda (C)wakipata maelezo kutoka kwa Dr Sittileila Twaha  kuhusu saratani aliyokuwa nayo  mgonjwa Rehema Hatibu (53) ambaye anapata matibu Wake wa viongozi walikuwa katika Hospitali ya Aga Khan katika kampeni ya kuhamasisha Watanzania kuwa natabia ya kuchunguza afya zao ilikujua mapema kama wanatatizo la Saratani nawaweze kupata matibabu yanyo stahili Picha na Chris Mfinanga. 

Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda akipokea zawadi ya uwa kutoka kwa Loveluck Mwasha ambaye ni  Muuguzi mkuu wa Hospitali ya Aga Khan kama ishara ya shukurani  katika kampeni ya ugonjwa wa saratani

======  =======  =======

 Kikundi cha wake wa Viongozi (New Mellinium Women Group) kimetembelea Hospitali ya Aghakan  jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya Kampeni Maalumu ya Uhamasishaji wa K ampeni ya Saratani ya Matiti iliyoanzishwa na Hospitali hiyo.


Kwa niaba ya wake wa Viongozi Mlezi wa chama hicho cha wake waviongozi ambaye ni Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda amesema , “Wake wa viongozi wameguswa na kuona kuwa wao ni mabalozi wa wakinamama kwa njia moja ama nyingine wanaweza  kutoa elimu kwa ndugu jamaa na jamii iliyowazunguka katika kutoa uhamasishaji wa Kampeni ya Saratani”.

Mama Pinda ,amesema ni vema wakinamama kujenga tabia ya kupima afya zao mara kwa mara kwani matibabu ya Saratani yanatibika hivyo kuwahi kupata vipimo na kugundua tatizo mapema itaweza kuponya kinamama wengi hapa nchini ambao hupoteza maisha kutokana na ugonjwa huo.

“Kansa haina umri, kuna kinga kuanzia kwa watoto wenye umri chini ya miaka 12 hivyo nawasihi wakina mama kutumia nafasi waliyopewa kwenda kufanya vipimo vya Saratani vilivyoanzishwa katika Hospitali ya Agakhan”, alisisitiza Mama Pinda.

Mama Gharib Bilali alisema, “miongoni mwa saratani inayosumbua kina mama ni saratani ya Shingo ya Uzazi, natoa wito kwa watanzania hasa kina mama kwenda kufanya vipimo vya Saratani hiyo ili kuweza kujua afya zao kwani mama ni sehemu muhimu sana katika familia nawasihi wakinamama kutumia nafasi hii adhimu iliyotolewa na Hospital ya Agakhan kwenye kufanya vipimo hivyo”.

Mapema Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Aga khan Bibi. Loveluck Mwasha alisema, ujio wa wake wa Viongozi (New Millenium Women Group) imeamsha ari na kutupa moyo na kuona ni jinsi gani wake hao wameguswa na jambo hili muhimu kwani wao ni mabalozi ambao wataweza kufikisha elimu na taarifa wlizopata juu ya upimaji wa Saratani ulionzishwa na hospitali ya Agakhan.

“Hospitali ya Agakhan imeanzisha Kampeni hii Maalumu ili kuweza kuwasaidia wakinamama wote wenye uwezo wakati, wachini na wasio na uwezo kwa kutumia vigezo walivyonavyo na kwa gharama nafuu inayojumuisha Uchunguzi wa aina tatu Kupapasa, Picha na Biopsy”, alisema bibi Mwasha.

 “Tunaunga mkono jitihada za Serikali katika kuboresha huduma za afya kwa jamii nchini kwa watu wote”, alisisitiza Bibi. Mwasha.

Huduma hizi zinatolewa kwa ujumla yaani (package) ili kuwawezesha kinamama kupata huduma ya upimaji. Kampeni hii ya Upimaji wa Saratani tayari imeshafanyika katika mikoa ya Mwanza, Mtwara, Lindi na tutaendelea na kampeni hii katika mikoa na mbalimbali haa nchini.

Maadhimisho sherehe za Miaka 50 ya Muungano wa Tanzania yafana jijini Kuala Lumpur,Malaysia

$
0
0
Watanzania waishio nchini Malaysia hivi karibuni walikutana pamoja katika hafla ya kusherehekea maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanzania zilizofanyika katika Hotel ya Prince jijini Kuala Lumpur- Malaysia,chini ya uongozi wa Balozi Dr. Aziz Ponary Mlima. Mgeni rasmi kwenye hafla hiyo alikuwa ni Naibu Waziri wa Usafiri na Uchukuzi wa Malaysia Dato Ab. Aziz Kaprawi.
Balozi wa Tanzania nchini Malaysia,Dr. Aziz Ponary Mlima pamoja na Maafisa wa Ubalozi wakiwakaribisha wageni waalikwa.

Picha ya waliokaa, katikati ni mgeni rasmi ambaye ni Naibu Waziri wa Usafiri na Uchukuzi wa Malaysia Dato Ab. Aziz Kaprawi, kulia kwake ni Balozi Abdul Samad bin Othman ambaye ni Mkurugenzi wa Afrika katika wizara ya mambo ya nje ya Malaysia na kushoto kwake ni Dr. Aziz Ponary Mlima, Balozi wa Tanzania Malaysia. 
Balozi wa Tanzania nchini Malaysia,Dr. Aziz Ponary Mlima (kulia) pamoja na mgeni rasmi ambaye ni Naibu Waziri wa Usafiri na Uchukuzi wa Malaysia Dato Ab. Aziz Kaprawi wakikata keki kwenye hafla hiyo ya kusherehekea maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanzania zilizofanyika jijini Kuala Lumpur- Malaysia.
Sehemu ya watanzania waishio nchini Malaysia wakiwa pamoja na wageni wao katika hafla hiyo.


mkuu wa mkoa wa pwani afungua mkutano wa baraza la wafanyakazi wa uchukuzi

$
0
0
Mwenyekiti wa Baraza, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, akitoa hotuba ya utangulizi kabla ya Mkuu wa mkoa wa Pwani, B. Mwantumu Mahiza hajafungua rasmi Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Uchukuzi, lililofanyika mjini Bagamoyo katika hoteli ya Millenium Beach Resort, leo asubuhi.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Bi. Mwantumu Mahiza akitoa hotuba wakati akifungua Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Uchukuzi, lililofanyika mjini Bagamoyo, leo asubuhi katika Hoteli ya Millenium Beach Resort.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Bi. Mwantumu Mahiza (wa nne kutoka kulia waliokaa), akiwa katika picha ya Pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Uchukuzi, mara baada ya kulifungua katika Hotel ya MIllenium Beach Resort, mjini Bagamoyo, leo asubuhi. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-UCHUKUZI).

Juhudi za Seriali za kuboresha sekta ya Uchukuzi hazitachangia ipasavyo katika kuinua uchumi wa Taifa endapo watumishi  wa Serikali hawatabadilika na kuachana na tabia ya kufanya kazi kwa Mazoea.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Mwantumu Mahiza amesema hayo leo katika ufunguzi wa Baraza la Wafanayakazi la Wizara ya Uchukuzi mjini Bagamoyo.

Mhe Mahiza amesema kila mtumishi katika eneo lake la kazi anapaswa kufanya kazi kwa kujituma, weledi na kwa ubunifu ili kuboresha mchango wa wizara ya uchukuzi katika kuboresha na kukuza uchumi wa Taifa la Tanzania.

Amesema Wizara ya Uchukuzi ni Sekta nyeti katika maisha ya kila siku katika uendelezaji wa shuguli za kiuchumi na kijamii, hivyo wadau katika sekta hii wanapaswa kushiriki na kushikamana katika utendaji wa kazi hiyo.

‘Utekelezaji wa majukumu ya kazi kila mdau anatakiwa ajiulize yeye mwenyewe katika sehemu yake amechangia nini au ameleta mabadiliko gani katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi. Ili kuleta mabadiliko katika sehemu ya kazi. Wadau katika sekta ya Uchukuzi wanapaswa kuachana na kufanya kazi kwa mazoea na kufanya kazi kwa ubunifu na kujituma kwa kiwango cha juu’. Alisema Mhe. Mahiza.

Ili watumishi waweze kufanya kazi kwa matokeo makubwa, Mhe. Mahiza ameshauri Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Dkt.  Shaaban Mwinjaka kuwapa motisha kwa kuwapandisha vyeo na kuwasomesha na kuwapa fursa za kutembelea hifadhi za mbuga za wanayama ili kuwahamasisha na kuwaongezea mori na ari ya kufanya kazi.

Akizungumzia changamoto ambazo wizara ya Uchukuzi inakabilian nazo, Mkurugenzi Msaidizi, Usimamizi wa Rasilimali watu, Bi. Judith Ndaba amezitaja changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa watumishi katika Wizara.

‘Wizara inajitahidi kukabiliana na changamoto hiyo kwa kuhakikisha kuwa kila sehemu iliyo wazi imejazwa watumishi. Tayari Wizara imeomba kibali kuitaka Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma kwa lengo la kujaza nafasi hizo ili kuchangia ipasavyo katika utekelezaji wa mpango wa matokeo makubwa sasa(BRN)’.Alisema Bi Ndaba.


Mkutano wa Baraza la wafanyakazi la wizara ya uchukuzi,ambao umefanya kwa siku moja,ulipitia utekelezaji wa mpango mkakati wa mwaka 2013/14 na kupitisha mpango mkakati wa mwaka 2014/15.

FURSA: MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI KUANZA TENA MWEZI MEI

$
0
0
Action Music Tanzania (AMTz) inatangaza fursa kwa watu wote kujiunga na mafunzo ya kupiga ala za muziki yanayoanza tarehe 3/5/2014, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wanamuziki wa kupiga ala na kufanya maonesho kwa weledi na utaalamu zaidi.

Mafunzo yanayotolewa ni pamoja na upigaji wa ala za muziki zikiwemo gita, kinanda, tarumbeta, saxophone, konga, drum set, na upigaji wa ngoma za asili. Pia yatatolewa mafunzo ya ‘body percussion’ yaani matumizi ya mwili katika kutengeneza midundo ya muziki. Mafunzo hayo yanafanyika kwenye ofisi za AMTZ zilizopo maeneo ya Mwenge mtaa wa Umoja, nyuma ya magorofa ya jeshi na kwenye Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo ili kujiunga na mafunzo haya wasiliana nao kwa simu namba 0686928828/0653075791 ili kupata fomu za kujiunga na mafunzo.
 Baadhi ya wanafunzi wakiwa kwenye mazoezi

Baadhi ya wanafunzi wakiwa darasani

Tanzania Set to Test New Anti-Malaria Drug

$
0
0
BY ABDUEL ELINAZA, 29 APRIL 2014  ALLAFRICA.COM

Guangzhou — TANZANIA could be headed to a malaria-free country, thanks to Chinese medical research findings that target the disease-causing parasite itself instead of the mosquitoes which carry it. The current approach to deal with malaria is to control mosquitoes, which spread the disease by either killing them with insecticides or by draining bodies of stagnant water in which their larvae live.

However, Dr Li Guoqiao of the Guangzhou University of Chinese Medicine has developed a drug therapy based on artemisinin which attacks the malaria parasite to eradicate the disease.

According to General Manager, Mr Pan Longhua of Artepharm Company which manufactures the drug, after successfully eradicating malaria in the Comoros, a similar project was designed to be extended to Tanzania and talks to that end had reached an encouraging stage.

"I was in Tanzania two months ago where I met with the minister for health. We exchanged ideas and the prospects are good," Mr Pan told the 'Daily News.'"We are still exchanging ideas and other stakeholders are very supportive. Once everything has been agreed the pilot project will take off later this year," he added.

ASKARI TRAFIKI SITA WAPENDA RUSHWA MBEYA WATIMULIWA

$
0
0
Kamanda wa Polisi  Mkoani
Mbeya  SACP Ahmed Msangi

Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya limewafukuza kazi Askari sita  wa kikosi cha Usalama barabarani  Wilaya za Rungwe na Mbeya kwa tuhuma za kuomba,kushawishi na kupokea rushwa.
Kamanda wa Polisi  Mkoani Mbeya  SACP Ahmed Msangi amewatataja Askari hao kuwa ni pamoja na waliokuwa wakifanya kazi wilaya ya Mbeya barabara ya Mbeya/Tunduma eneo la Songwe ni Koplo  Jonson,PC Rymond na PC Simon.
Msangi amewataja wengine kuwa ni pamoja Sajini Hezron,PC Shaban na PC Kajolo ambao walikuwa wanafanya kazi barabara ya Mbeya/Rungwe wilaya ya Rungwe.
Askari hao walikuwa wanakabiliwa na makosa hayo na walifikishwa katika Mahakama ya Kijeshi na Hukumu kutolewa Aprili 24 mwaka huu na kupewa adhabu ya kufukuzwa kazi.
Aidha Kamanda Msangi amesema Jeshi lake halitasita kuwafukuza kazi Askari watakaokwenda kinyume na maadili ya Jeshi la Polisi na Askari yeyote atakayekwenda kinyume atakumbwa na adhabu kali ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi au kufikishwa mahakamani.
Askari wengine waliofukuzwa kazi hivi karibuni ni pamoja na PC James Kagomba ambaye amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa kutumia silaha,WP Prisca Kilwai anayekabiliwa na kesi ya wizi wa mtoto.
Wengine wliohukumiwa kifungo cha mwaka mmoja baada ya kukutwa na hatia ya kuua bila kukusudia ni DC Marcelino Venance mwenye namba 8084,PC Juma Idd mwenye namba 3117 na Askari wa Mgambo MG Jackson Mwakalobo ambao walidaiwa kusababisha kifo cha mwanafunzi Dentho Kajigili aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya Sekondari Ivumwe ya Jijini Mbeya. 

UTUMISHI YANYAKUA KOMBE KUPITIA MPIRA WA PETE MASHINDANO YA MEI MOSI 2014

$
0
0
Na. James Katubuka

Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma imetawazwa rasmi kuwa bingwa wa mpira wa Pete wa Mashindano ya Mei Mosi 2014.

Utumishi imefanikiwa kuwa bingwa baada ya kuisambaratisha timu ya Wizara ya Uchukuzi kwa ushindi wa magoli 33 dhidi ya 21. Mchezo huo wa fainali ulifanyika katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Katika mchezo huo mchezaji Fatuma Machenga (GS) wa Ofisi ya Rais Utumishi ndiye aliyekua tishio kwa kuongoza wachezaji wa timu yake kufanikisha ushindi huo. 

Mchezaji Subira Jumanne (WA) wa Uchukuzi akizungumzia hali ya mchezo baada ya mpira kumalizika alisema kuwa mchezo ulikuwa mgumu na wapinzani wao walikua wamejiandaa vyema.
 “Naamini wakati wa mashindano mengine tutafanya vizuri kwa kujiandaa vyakutosha, asiyekubali kushindwa si mshindani” Subira alisema.

Wakati huohuo, Fatuma Machenga (GS) wa Utumishi ameibuka kuwa mfungaji bora wa mpira wa Pete katika mashindano ya Mei Mosi 2014 kwa kufunga jumla ya magoli 136.
 “Tutahakikisha kuwa mwakani tunapambana zaidi kwa kufanya mazoezi ya kutosha ili kutetea ubingwa wetu” Machenga alisema.

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma imenyakua kombe hilo lililokuwa likishikiliwa na timu ya Wizara ya Ulinzi iliyokuwa bingwa katika mashindano yaliyopita Mwaka 2013. 
Mshindi wa Pili kwa mwaka 2014 ni Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mashindano hayo yalimalizika jana katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mabingwa wapya wa Mei Mosi 2014, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma wakiwa katika mazoezi mepesi kabla ya mchezo ambao waliifunga Uchukuzi na kunyaukua kombe la Mei Mosi 2014 iliyochezwa uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Mchezaji wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Sophia Komba akijiandaa kumdhibiti mchezaji wa Uchukuzi (C) (mwenye mpira) katika mechi ya fainali iliyochezwa katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Hekaheka ya kuwania mpira baina ya wachezaji wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma (jezi za kijani) na Uchukuzi (jezi za bluu) katika mechi ya fainali ya Mei Mosi 2014 iliyochezwa jana uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Baadhi ya wachezaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi Umma, pamoja na mashabiki wao wakipongezana baada ya kuibuka mabingwa wapya wa Mpira wa Pete kwa kuifunga Uchukuzi katika mashindano ya Mei Mosi 2014 yaliyomalizika katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Fatuma Machenga (GS) mfungaji bora katika Mpira wa Pete wa mashindano ya Mei Mosi 2014 akiwa na kikombe baada ya kutangazwa rasmi katika hafla fupi iliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuru mjini Morogoro.
Baadhi ya wachezaji wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma (jezi za kijani) wakishangilia kwa kutawazwa mabingwa wapya wa Mpira wa Pete Mei Mosi 2014 kwa kuifunga timu ya Uchukuzi. Mashindano hayo yalimalizika jana jioni katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mtangazaji Maarufu,Tshaka Ssali amtembelea Mh. Lowassa ofisini kwake leo

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli,Mh. Edward Lowassa (kushoto) akizungumza na mtangazaji maarufu wa Kituo Cha runinga Cha Serikali ya Marekani (VOA),Tshaka Ssali aliemtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo.Ssali ambaye amejijengea umaarufu duniani kwa kuwahoji viongozi maarufu hususan wa Afrika, alimtembelea Mh Lowassa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli,Mh. Edward Lowassa (kushoto) akifurahi jambo wakati akiwa katika mazungumzo na mtangazaji maarufu wa Kituo Cha runinga Cha Serikali ya Marekani (VOA),Tshaka Ssali.

President Kikwete has sent a congratulatory message to His Majesty King Willem-Alexander of the Kingdom of the Netherlands on the occasion of His Majesty’s Birthday

$
0
0
H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Majesty King Willem-Alexander of the Kingdom of the Netherlands on the occasion of His Majesty’s Birthday.
The message reads as follows:-

  “Your Majesty King Willem-Alexander R.,
   King of the Kingdom of the Netherlands,
   The Hague, 
   THE NETHERLANDS.
  
Your Majesty,
It is my great pleasure on behalf of the people and the Government of the United Republic of Tanzania to congratulate Your Majesty on the occasion of your 47th birthday.
As you celebrate your birthday let me take this opportunity to express my deep appreciation for the excellent bilateral relations that exist between our two countries and peoples. I reiterate my personal commitment and that of my Government to working with You and Your Government in strengthening further the long, close and historic relations for common aspirations.
Please accept Your Majesty, my best wishes for your continued good health and prosperity for the people of the Kingdom of the Netherlands”.


Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, 
Dar es Salaam.

29th April, 2013

UONGOZI WA OFISI YA MAKAMO WA KWANZA WA RAIS ZANZIBAR WAZUNGUMZA NA DK. SHEIN, IKULU

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Uongozi wa Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais katika kikao cha utekelezaji Mpango kazi wa Robo tatu ya mwaka Julai-Machi 2013/2014,katika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Unguja leo asubuhi.
Baadhi ya maafisa wa idara mbali mbali za Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais wakiwa katika kikao cha utekelezaji Mpango kazi wa Robo tatu ya mwaka Julai-Machi 2013/2014,katika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Unguja leo asubuhi,mwenyekiti wake akiwa ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein.(Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.)

maonesho ya 4 ya Tanzania Homes Expo kuanza Agosti 23 - 24,2014

$
0
0
Mkurugenzi wa Tanzania Homes Expo, Zenno Ngowi  akizungumza na waandishi (hawapo pichani)  jijini Dar es salaam leo kuhusu Uzinduzi wa maonesho ya 4 ya Tanzania Homes Expo na EAG Group Ltd yatakayofanyika Dar es Salaam kuanzia Agosti 23-24 mwaka huu. Kushoto ni Meneja Biashara,Mathew Gugai. (Picha Francis Dande)

Wanamichezo 45 waagwa rasmi kwa ajili ya kwenda nje kufanya maandalizi ya mashindano ya Jumuiya ya Madola

$
0
0
Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe akizungumza na wanamichezo wanaoenda kuweka kambi katika nchi za New Zealand, Ethiopia, China na Uturuki ikiwa ni maandalizi ya mashindano ya Jumuiya ya Madola mapema mwezi julai. Kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Leornard Thadeo.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Leornard Thadeo akifafanua jambo wakati wa hafla ya kuwakabidhi bendera wanamichezo wanaokwenda nje ya nchi kwa ajili ya maandalizi ya mashindano ya Jumuiya ya Madola leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya njeya nchi na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe (wa tatu kutoka kushoto) akifurahia mara baada ya kuwa kabidhi Bendera ya Taifa wawakilishi wa wanamichezo wanaokwenda nchini New Zealand, Ethiopia,China na Uturuki kwa ajili ya kujiandaa na msahindano ya Jumuiya ya Madola. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Masuala ya Asia, Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Leornard Thadeo, Katibu wa Kamati ya Olympic Tanzania Filbert Bayi na mwakilishi wa wana michezo Neema Mwaisyula.

TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI (TFF) LEO

HALMASHAURI NA WADAU WA JIJI LA MWANZA WAANZA MAANDALIZI YA SHEREHE ZA KUADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA JUNI 16

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi inayoundwa na wadau wa watoto jijini Mwanza Bw. Godfrey Salumu akifafanua utaratibu mzima wa utendaji kazi wa kamati ndogo ndogo zilizoundwa kwa wajumbe (hawapo pichani) ili kuweza kufanikisha maadhimisho hayo.
Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya jiji la Mwanza Bi Eluminata Mwita akisikiliza jambo kwa makini toka kwa wajumbe (hawapo pichani).
Mkurugenzi wa Shirika la Kutetea Haki za Wanawake na Wasichana, KIVULINI Bw Ramadhani Masele (kushoto) ambae pia ni mjumbe wa kamati ya ndogo ya Uratibu, Mipango na Fedha akiteta jambo na mjumbe mwenzake wakati wa kikao hicho.
Wajumbe wa Kikao cha kwanza cha maandalizi ya Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika itakayofanyika Juni 16 chini ya kauli mbiu ya “Kuondoa Mila Zenye Kuleta Madhara kwa Watoto ni Jukumu Letu Sote”.
Uongozi wa kamati ya maandalizi ya sherehe ya siku ya Mtoto wa Afrika wilaya ya Nyamagana, Mwanza. Kulia ni Bw Godfrey Salumu ambae ni Mwenyekiti wa kamati, Bw. Devis Mrope (katikati) ambae na Katibu, kushoto ni Katibu Msaidizi Bi. Francisca Michael.

Halmashauri pamoja na wadau toka mashirika na taasisi za kutetea na kulinda haki za watoto jijini Mwanza wameanza rasmi vikao vya maandalizi ya kuadhimisha sherehe za siku ya mtoto wa Afrika inayoadhimishwa kila Mwaka Juni 16.

Kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri wa Jiji la Mwanza chini ya Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri hiyo Bi. Eluminatha Mwita wajumbe walikubaliana kuadhimisha siku hiyo katika Kata ya Buhongwa, kwa Wilaya ya Nyamagana.

Siku ya mtoto wa Afrika huadhimishwa kimataifa kote duniani kwa lengo la kutambua thamani, utu, na umuhimu wa mtoto duniani. Maadhimisho haya hufanywa kila juni 16 tangu ilipotangazwa kuwa siku rasmi mwaka 1991 na jumuiya ya umoja wa Afrika.

Akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho Afisa Maendeleo Jamii wa Jiji la Mwanza Bi. Eluminatha Mwita alisema kuwa kauli Mbiu ya mwaka huu ni “Kuondoa Mila Zenye Kuleta Madhara kwa Watoto ni Jukumu Letu Sote” na kufafanua kuwa kauli hiyo inalenga kuwasisitiza wazazi na walezi kuacha mila potofu zenye kuleta madhara kwa watoto.

Bi Eluminatha alisema kuwa “Kauli mbiu hiyo ina lenga kuangalia mila zote kandamizi na potofu zinazotokana na jamii husika katika malezi ya mtoto na kusababisha madhara mbalimbali ikiwemo kuongezeka kwa watoto wa mitaani, kubakwa kwa watoto, kukosa elimu, afya na malezi bora pamoja na vifo kwa watoto hawa”.

Kikao hicho cha kwanza kiliweza kuchagua viongozi wa kamati hiyo ya maandalizi, mwenyekiti aliyechaguliwa ni Godfrey Salum huku katibu ni Devis Mrope na katibu msaidizi akichaguliwa Francisca Michael, baada ya kupata viongozi kamati nne ziliundwa na wajumbe, Kamati ya Uratibu, Mipango na Fedha, Kamati ya Usafiri na Ulinzi, Kamati ya Mapambo na Burudani pamoja na kamati ya Hotuba na Habari.
Viewing all 110105 articles
Browse latest View live




Latest Images