Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live

IN LOVING MEMORY OF MZEE JAMES GERALD MANDAWA

$
0
0
IT SEEMS LIKE YESTERDAY THOUGH IT IS TWELVE MONTHS SINCE OUR LORD TOOK YOU HOME, OUR LOVELY DAD, THE FACT THAT YOU ARE NO LONGER HERE WILL ALWAYS CAUSE US PAIN, HOWEVER WE TAKE REFUGE IN THE LOVE THAT BOUND US FOREVER.

OUR HEARTS ARE FULL OF FOND MEMORIES; YOU GAVE US SO MUCH TO REMEMBER.

WE REMEMBER ALL THE SUPPORT AND GUIDANCE YOU PROVIDED THAT HAS BUILT A SOLID FOUNDATION IN OUR LIVES AND HAS MADE US WHAT WE ARE TODAY. 

WE CHERISH THE GOOD TIMES WE HAVE HAD TOGETHER AND THE LOVE THAT YOU GAVE US SO UNCONDITIONALLY. YOU WILL REMAIN FOREVER IN OUR HEARTS. YOU ARE DEEPLY MISSED BY Ma GLORY, Ma THECLA YOUR CHILDREN MERCY, DICKSON, NEEMA AND MVANO, YOUR GRANDCHILDREN JOYCE, ESTHER, FAITH-FATUMA, LINDA-RACHEL, TALLE, IBRAHIM, MONICA AND JAMES; YOUR IN-LAWS AND RELATIVES.

THANKS GIVING MASS WILL BE HELD AT ST. THOMAS ANGLICAN CHURCH, YOMBO KIWALANI ON SATURDAY, 5TH APRIL, 2014 FROM 08.00am.
The Lord gave and the Lord has taken away; may the name of the Lord be praised, AMEN.

WENGI WAJITOKEZA KUJIUNGA NA NSSF

$
0
0
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka (wa pili kulia), akipata maelezo kutoka kwa Ofisa Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Carloyne Newa (kushoto), kuhusu kujiunga na Mfuko huo wakati wa uzinduzi wa michuano ya Kombe la NSSF kwa vyombo vya Habari. Michuano hiyo inafanyika katika viwanja vya TCC Chag'ombe jijini Dar es Salaam.
 Mkazi wa jijini Dar es Salaam akiulizia taratibu za kujiunga na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF.
 Ofisa Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Carloyne Newa  (kulia), akitoa maelezo kwa baadhi ya wakazi wa Dar es Salaam walipofika katika banda la NSSF, na kutaka kujiunga na mfuko huo, wakati wa michuano ya kopmbe la  NSSF kwa vyombo vya habari.
  Ofisa Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Carloyne Newa  (kulia), akitoa maelezo kwa baadhi ya wakazi wa Dar es Salaam walipofika katika banda la NSSF.
 Maofisa wa NSSF wakitoa ufafanu kuhusu mafao yanayotolewa na Shirika hilo.
 Mwanachama mpya aliyejiunga na Shirika la taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), akijaza fomu ya kujiunga na mfuko huo. 
Baadhi ya waandishi wa wakipata maelezo kabla ya kujiunga na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF.

TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI (TFF) LEO

WATANZANIA TAKRIBANI MILIONI 3.3 HUTUMIA HUDUMA ZA KIBENKI : GAVANA BENNO NDULU

$
0
0
Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imethibitisha kuwa watu takribani watu milioni 3.3 ni kwa kutumia huduma za kibenki, kulingana na matokeo ya FinScope 2013 utafiti uliofanywa na Financial Sector Deepening Trust (FSDT).

Hayo yamesemwa na jijini Dar es Salaam na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Prof Benno Ndulu , wakati akitoa hotuba wakati wa uzinduzi wa utafiti wa ripoti ya FinScope Tanzania 2013; habari zilizomo katika utafiti huu thamani ni muhimu kwa ajili yetu maendeleo ya kiuchumi. Utafiti huu wa FinScope ni wa tatu tangu mwaka 2006.

Hata hivyo, alisema nusu ya Watanzania wote watu wazima - watu milioni 12 - sasa kutumia simu zao kwa kuondoa , kupokea na kuokoa fedha, au kulipa bili. Wanaume na wanawake katika maeneo ya mijini na vijijini katika nchi nzima na upatikanaji wa haraka kwa aina mbalimbali ya huduma za kifedha katika bonyeza ya kifungo chache .

 Alisema hii ni mapinduzi ya utulivu ambayo ni kuwa na madhara makubwa kwa mazingira ya fedha katika Tanzania . Mtandao wa simu operators kuendelea kufanya kazi na baadhi ya benki yetu ya kibiashara na kuendeleza bidhaa na huduma iliyoundwa na kukutana kutarajia kuongezeka kwa mahitaji katika muongo ujao.

Mkurugenzi wa Ufundi wa FSDT, Sosthene Kewe alisema zaidi ya nusu ya watu katika nchi kutumia huduma rasmi za kifedha, ikiwa ni pamoja na akiba na mikopo vikundi vidogo , maduka, ugavi mikopo na wakopeshaji fedha , ambayo bado ni mkubwa sana muhimu kwa nchi na mara nyingi pamoja na huduma nyingine.

" Ingawa hakuna miongoni mwao pia umewekwa au inasimamiwa na taasisi rasmi za fedha, akiba na mikopo ya vikundi inamilikiwa na kuendeshwa na watu ambao matumizi yao . Hii , kama vile bidhaa na huduma ambayo ni makini kulengwa kwa soko yao, inaweza kuelezea umaarufu wao "alisema.

Alisema matokeo ya utafiti inaonyesha kuna ongezeko la kuingizwa fedha na ufahamu juu ya huduma za benki za Mkono, ambapo zaidi ya watu 6.6m katika nchi kwa kutumia simu za kibenki.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Profesar Benno Ndulu akikata utepe kuzindua kitabu cha ripoti ya utafiti Tanzania katika masuala ya uchumi uliofanyika leo Aprili 2, 2014 katika ukumbi wa Makao Makuu ya Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Profesar Benno Ndulu akiongoza wageni waalikwa kuonyesha kitabu cha utafiti mara baada ya kumaliza kuzindua.
Wageni waalikwa waliohudhuria katika mkutano huo wa kutangaza ripoti ya utafiti Tanzania katika masuala ya uchumi.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

President Kikwete attends EU-Africa Summit in Brussels

$
0
0
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete shares a light moment with Swaziland King Mswati III shortly before the commencement of the Fourth European Union and Africa Summit held in Brussels Belgium this afternoon. The summit will illustrate how EU-Africa relations have evolved over the past years, will highlight the results achieved by the continental Partnership and will frame cooperation for the years to come.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete meets German leader Chancellor Angela Merkel during the Fourth European Union and Africa Summit held in Brussels Belgium this afternoon. President Kikwete arrived in Brussels today for a two days working visit.
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete greets French President Francois Hollande at the beginning of the EU Africa Summit held in the Belgium Capital Brussels this afternoon.Photos by Freddy Maro

MABILIONEA WA MAREKANI WAMALIZA ZIARA YAO SERENGETI

MKOA WA DODOMA WASHIRIKI SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA BODI YA HUDUMA ZA MAKTABA NCHINI

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dr. Rehema Nchimbi (mwenye kilemba kichwani) akikagua jengo la maktaba mkoa wa Dodoma kujionea mfumo wa vifaa vinavyotumika kutolea elimu na taarifa mbalimbali kwa njia ya video na sauti,  zoezi hili la ukaguzi lilifanyika mapema leo kwenye viwanja vya maktaba ya Dodoma wakati wa maadhimisho  ya miaka 50 ya bodi ya huduma za maktaba
 Watumishi wa maktaba ya mkoa Dodoma wakiwa tayari kupokea wananchi wenye mahitaji mbalimbali ya huduma za maktaba kwa ajili ya kuwapa maelekezo ya namna ya kupata taarifa na huduma nyingine mbalimbali mapema leo wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya bodi ya huduma za maktaba, maadhimisho mkoa Dodoma yalifanyika viwanja vya maktaba ya Dodoma.
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dr Rehema Nchimbi (mwenye kilemba kichwani) akikagua nyaraka na vitabu mbalimbali wakati akitembelea mabanda ya maonesho  ya vitabu wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya bodi ya huduma za maktaba Nchini, maadhimisho mkoa Dodoma yalifanyika viwanja vya maktaba ya mkoa.
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dr. Rehema Nchimbi (mwenye kilemba kichwani) akipata ufafanuzi kutoka kwa mtaalamu wa kutafsiri taarifa za vitabu na nyaraka mbalimbali katika lugha za watu wenye mahitaji maalumu/wenye ulemavu wa kuona (nukta nundu) Mwl. Charles Mtimatuku mapema wakati anatembelea mabanda ya maonesho wakati wa hafla ya maadhimisho ya miaka 50 ya bodi ya huduma za maktaba nchini  mkoani Dodoma. Huduma za maktaba nchini zimepiga hatua kiasi cha kuzalisha taarifa na nyaraka mbalimbali kwa watu wenye mahitaji maalumu.NA JOHN BANDA

Kamanda Mpinga awafunda madereva wa UDA kuzingatia sheria za Usalama barabarani

$
0
0
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga ( aliyesimama) akifafanua kwa ufasaha vifungu vya sheria za usalama barabarani na miiko ya maadili ya udereva, wakati akifungua warsha ya mafunzo kwa maderva wa kampuni ya UDA jijini Dar es Salaam leo. Aliwafunda madereva hao kuwa wasafi, lugha nzuri na kutabasamu kwa abiria ambao ni wateja wao.Wengine pichani ni Mwenyekiti wa makampuni ya Simon Group,Robert Kisena (kulia) na David Mziray kutoka SUMATRA.
Mwenyekiti wa makampuni ya Simon Group,Robert Kisena (aliyesimama) akitoa neno la shukrani kwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga aliyefungua warsha ya mafunzo kwa madereva wa UDA leo jijini Dar es Salaam.
Madereva wa UDA wakifurahia mafunzo ya sheria za Usalama Barabarani yaliyofunguliwa na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mohamed Mpinga jijini Dar es Salaam leo.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa makampuni ya Simon Group, Robert Kisena wakati wa warsha ya mafunzo ya madereva wa shirika la UDA jijini Dar es Salaam leo.

kuelekea ukingoni mwa kampeni za Uchaguzi Jimbo la Chalinze,CCM yazidi kuzibomboa ngome za wapinzani wao

$
0
0
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye sambamba na Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete wakiyarudi magoma wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM uliofanyika leo April 2,2014 katika Kijiji cha Lugoba,Kata ya Lugoba.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubia Mamia ya wakazi wa Kijiji cha Lugoba waliofurika kwenye uwanja wa Mnadani,kusikiliza sera ya Mgombea Ubunge huyo leo April 2,2014.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini na Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Stephen Masele akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Lugoba wakati wa Mkutano wa Kampeni za CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,leo April 2,2014.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye akihutubia Mkutano wa hadhara wa Kampeni za CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete akiiangalia kadi ya CHADEMA ya Mzee Masoud Mtonga mara baada ya kukabidhiwa.
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ridhiwani Jakaya Kikwete akipokea kadi za Chama cha CUF kutoka kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Kata ya Msata,Idd Njema ambaye amejiunga na CCM sambamba na familia yake.katikati ni Meneja wa Kampeni za CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze,Steven Kazidi.

dkt hussein mwinyi na wadau wa london

$
0
0
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt Hussein Mwinyi akipata selfie na wadau wa London waliomtembelea hotelini kwake ili kumpa zawadi ya kitabu. Dkt Mwinyi alikuwa katika msafara wa Rais Kikwete alipofanya ziara ya kiserikali ya siku tatu Uingereza kwa mwaliko wa Waziri mkuu David Cameron

ankal avamia BBC London

$
0
0
 Ankal akiwa na Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC Bw. Ali Saleh alipovamia kituo hicho kuwataka hali wadau. Ankal alifarijika na kufurahi mno kukuta kumbe bosi huyu ni Bwawa la Maini damu kama yeye. Ila alimkuta hana furaha sana  kwa kuwa vijana wa Liverpool wameharibu plani ya kocha Brendan ya kubaki katika nne bora tu mwaka huu ili kucheza Europe Cup na sio kuchukua ubingwa mwaka huu. Maana inavyoelekea kombe linaenda Anfield, ambapo Ali Saleh anasema ah! tukishinda hatutolikataa ila sie tumepanga tulibebe mwakani na sio mwaka huu....!
 Charles Hilary Mkwanda akicheza na Ze Fulanazzzzzzz
 Ankal na Bi Zuhura Yunus. Kumbe bado katoto kadogoooo.....dah!
Ankal na  Salim Kikeke a.k.a 'Yul Bryner.
 
 Ankal akila selfie na wadau Mariam Omar na Peter Musembi.
 Ankal akiwa na Alex Muriethi (aliyeketi) na 'shemeji' yetu Siraj Kalyango ambaye chupuchupu amuoe nanihii, ila alichelewa kuleta mahari, na mke kusombwa na maji mengine...
Ankal akila konozzzzz na Zawadi Machibya. Anatoa shukurani sana kwa BBC idhaa ya Kiswahili kwa ukarimu na ucheshi wao na kumpokea kwa moyo mkunjufu japo alifika hapo bila taarifa wala mihadi. Pia hapo BBC idhaa ya Kiswahili wana utamaduni wa kumkaribisha mdau yeyote kutoka Afrika kwa moyo mkunjufu na hata kumfanyia mahojiano kama inawezekana.

Ankal uso kwa uso na frida fashion jijini London

$
0
0
 Ankal akiwa na muasisi na mwanzilishi wa Fashion show nchini Tanzania Da' Farida Matata a.k.a Farida Fashion ambaye alianzisha mambo ya fashion show miaka ya 1986 na kuwatoa warembo wengi kitaifa na kimataifa. Hivi sasa anaendesha biashara kibao jijini London ikiwa ni pamoja na mkahawa wa vyakula vya Kiswahili sehemu ya Tottenham Hale wenye jina la hapo juu. Ankal  ametembelea hapo na kupata msosi wa nguvu wa wali wa nazi kwa samaki hapo chini

 Before....
 After.....

ankal na Aboubakar Faraj wa swift Freight UK LTD

$
0
0
Ankal akila selfie na mdau anayefanya vyema katika biashara ya usafirishaji mizigo dunia nzima kaka Abouibakar Faraji ofisini kwake Tottenham Hale..

meno tena!

$
0
0
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akiongea kwa uchungu kufuatia kukamatwa hivi karibuni katika Vijiji vya Kiyombo kilichopo Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora na Kijiji caha Chinangali Kilichopo Wiliaya Chamwino Mkoani Dodoma hivi karibuni.
  Mkuu wa Kitengo cha Hima Sheria Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Robert Mande (wapili kulia) akimwonyesha Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu Bunduli iliyokamtwa pamoja na meno ya Tembo katika kituo cha Kikosi dhidi ya  Ujangili  (KDU) cha Kanda ya Kati,  kjilichopo Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida juzi, yaliyokamtwa hivi karibuni katika Vijiji vya Kiyombo kilichopo Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora na Kijiji caha Chinangali Kilichopo Wiliaya Chamwino Mkoani Dodoma hivi karibuni.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro (wapili kushoto) na Mkuu wa Wilaya Mayoni Mkoani Singida, Fatma Toufiq (kushoto) wakiangalia meno ya Tembo katika kituo cha Kikosi dhidi ya Ujangili (KDU) cha Kanda ya Kati, kjilichopo Wilaya hiyo juzi, yaliyokamtwa hivi karibuni katika Vijiji vya Kiyombo kilichopo Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora na Kijiji caha Chinangali Kilichopo Wiliaya Chamwino Mkoani Dodoma hivi karibuni. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Hima Sheria Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Robert Mande.
Mkuu wa Kitengo cha Hima Sheria Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Robert Mande (wapili kushoto) akimwonyesha Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu meno ya Tembo katika kituo cha Kikosi dhidi ya Ujangili (KDU) cha Kanda ya Kati, kjilichopo Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida juzi, yaliyokamtwa hivi karibuni katika Kijiji vya Kiyombo kilichopo Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora na Kijiji caha Chinangali Kilichopo Wiliaya Chamwino Mkoani Dodoma hivi karibuni.

MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AKUTANA NA WAFUGAJI KUZUNGUMZIA MGOGORO KISHAPU NA IGUNGA

$
0
0


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Ally N. Rufunga amewataka wafugaji wanaoishi katika kijiji cha Magalata wilayani Kishapu mkoani Shinyanga kutovuka mto Manonga na kuingia katika wilaya ya Igunga wakati serikali inashughulikia suala la mpaka wa wilaya hizo mbili.

Mhe Rufunga ametoa maelekezo mapema jana alipokutana na wafugaji hao katika kijiji cha Magalata wilayani Kishapu, ikiwa ni moja ya makubaliano ya kikao cha Kamati za ulinzi na usalama za mikoa ya Tabora na Shinyanga kuwa kila upande wananchi waelimishwe kutumia ardhi na kuwa watulivu wakati huu serikali inapofanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha mgogoro na kufuatilia mpaka halali wa eneo hilo.

Awali wafugaji waliieleza kamati ya Ulinzi na Usalama ambayo Mkuu wa mkoa ni mwenyekiti, kuwa mpaka halisi ni mto Mwanyerere (Manonga) lakini mto huo ulihama kutokana na mvua mwaka 1998 na sehemu kubwa uliingia eneo la Kishapu hivyo eneo lao la kitongoji cha Magogo likabaki upande mwingine na wamekuwa wakichungia huko kwa muda mrefu hadi hapo wakulima wa wilaya ya Igunga walipovamia eneo hilo ndipo vurugu zilianza.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha wafugaji Kanda ya Ziwa Bw. Mrida Mshota amewasihi wafugaji wa kijiji cha Magalata kutulia na kusubiri taratibu za serikali kwani suala hilo limeanza kushughulikiwa muda mrefu tangu serikali ilipopata taarifa za uvamizi huo, chama cha wafugaji pia kinashirikiana kwa karibu na serikali kuhakikisha haki inapatikana.

Mgogoro huo unatokana na kugombea eneo kati ya wakulima wa kijiji cha Isakamaliwa wilayani Igunga mkoani Tabora ambao ni wahitimu wa vyuo vikuu waliopewa eneo hilo na serikali ya mkoa ya Tabora kwa ajili ya kujiajiri kwa njia ya kilimo, wakati huohuo wafugaji wa kijiji cha Magalata wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga wenye asili ya Kitaturu wakidai wamevamiwa eneo hilo  kwani wamelisha mifugo yao kwa miaka mingi hapo.


Serikali ya Mkoa wa Shinyanga na Tabora zinaendelea kushughulikia tatizo hilo lililosababisha vifo vya watu watano na majeruhi mmoja ambapo tume ya watu 18 imeshaundwa na kupewa muda wa wiki nne kufanya uchunguzi wa chanzo hasa na kujua mpaka halali wakati wananchi wakiendelea kuelimishwa kuwa na subira.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe.Ally N. Rufunga akizungumza na wananchi wa kijiji cha Magalata wilayani Kishapu kuhusu vurugu zilizotokea za kugombea eneo la malisho na wakulima wa wilaya ya Igunga mkoani Tabora.
Mwenyekiti wa chama cha wafugaji Bw. Mrida Mshota akiwasihi wafugaji kuiamini serikali hivyo wawe na subira kufuatia mgogoro kati yao na wakulima wa Isakamaliwa Igunga.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Shinyanga ambaye ni Mkuu wa Mkoa (hayupo pichani) Ally N. Rufunga akitoa maelekezo kufuatia mgogoro wa eneo kati ya wafugaji wa Magalata na wakulima wa Isakamaliwa.

MAMA SALMA KIKWETE AKABIDHIWA CHETI CHA ULEZI WA HIARI WA CHAMA CHA WENZA WA MABALOZI WA AFRIKA WALIOKO UBELGIJI

$
0
0
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea cheti maalum cha ulezi wa heshima wa Chama cha wenza wa mabalozi wa nchi za Afrika walioko nchini Ubelgiji (Honory Patronese of the Association of the Spouses of African Ambassadors in Belgium) kutoka kwa Mke wa Balozi wa Cameroon nchini Ubelgiji Mama Christiane Eloundov de Evina wakati wa chakula cha mchana walichowaandalia wake wa Marais wa Afrika jijini Brussels tarehe 2.4.2014.
Mke wa Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Mama Adelaida Kamala akimkabidhi Cheti Maalum cha ulezi wa heshima cha wenza wa mabalozi wa Afrika walioko Ubelgiji, Mke wa Rais wa Cameroon Mama Chantal Biya wakati wa chakula cha mchana walichowaandalia wageni hao kwenye hoteli ya Sheraton tarehe 2.4.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wake wa Marais na Wakuu wa nchi za Afrika pamoja wa wenza wa Mabalozi wa nchi hizo mara baada ya kupata chakula cha mchana kilichoandaliwa na wenza hao tarehe 2.4.2014. 

Article 17

APRM, MKAKATI MARIDHAWA KUDUMISHA UTAWALA BORA NA UCHUMI

$
0
0
Viongozi wa Nchi za Kiafrika katika Makao Makuu ya AU. Jumla ya nchi 34 kati ya 54 wanachama hai wa AU ni wanachama Mpango wa Afrika Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM).
Wajumbe wa Bodi na Sekretarieti ya APRM (Tanzania) wakiwa katika picha ya pamoja na Rais Dkt. Jakaya Kikwete. Kushoto kwa Rais ni Mwenyekiti wa APRM, Prof. Hassa Mlawa na kulia ni Katibu Mtendaji wa APRM, Bibi Rehema Twalib.

MAFANIKIO YA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI ARUSHA

$
0
0
Afisa Miradi wa IFAD nchini Dkt. Mwatima Juma pamoja na waratibu wa miradi mbalimbali akitoa maelezo kwa wakulima (Kulia) wanaotumia Skimu ya Maji ya Kabambe iliyopo katika jinsi ya kujipanga katika kilimo na kutunza chanzo cha Skimu hiyo iliyopo katika Wilaya ya Monduli katika kata ya Majengo Mkoani Arusha.
Skimu ya Maji ya Kabambe iliyojengwa katika Wilaya ya Monduli kata ya Majengo kuwasaidia wakulima kupata maji kwa ajili ya kilimo cha Mahindi, Ndizi na Mbogamboga, ikiwa ni sehemu ya miradi inayoratibiwa na ASDP na kusimamiwa na wadau wa maendeleo IFAD.
Shamba la Mbogamboga la Wakulima wa Monduli wanaotumia Skimu ya Maji ya Kabambe ikiwa ni sehemu ya mafanikio ya miradi ya ASDP inayosimamiwa na wadau wa maendeleo IFAD.

Tume ya Uchaguzi yavitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki kwenye Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze kuwatumia mawakala kutoka ndani ya jimbo hilo

$
0
0
TUME ya Taifa ya uchaguzi imevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki kwenye Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze kuhakikisha kuwa wanawatumia mawakala wanaotoka katika maeneo au vituo husika vya kupigia kura,ambao watawafahamua na kuwatambua wapiga kura wa eneo husika. 

Akizungumza katika mkutano baina ya vyama vya siasa na tume hiyo,Mwenyekiti wa Tume hiyo,Jaji mstaafu Damiani Lubuva amesema kuwa pamoja na kuwa sheria haikatazi kwa vyama kuteua mawakala wa vyama kutoka majimbo mengine ya uchaguzi,lakini ni vyema kuwateua wale wanaotoka katika maeneo hayo ili kuweza kuwatambua wapiga kura wao. 

“Kumekuwa na mazoea kwa baadhi ya vyama vya siasa kuteua mawakala wanaotoka majimbo mengine ya uchaguzi japokuwa sheria haikatazi lakini ni vema vyama vikatumia busara  ya kuwateua mawakala kutoka katika maeneo hayo ili kuweza kuwatambua wapiga kura”alisema Jaji Lubuva. 

Akizungumzia kuhusu umuhimu wa wananchi kujitokeza kupiga kura,Lubuva alisema kuwa tume inatambua juhudi za viongozi wa vyama vya siasa kuwahamasisha wananchi kujitokeza kushiriki katika uchaguzi lakini akawataka viongozi hao kuhakikisha kuwa wanawahamasisha zaidi wapiga kura kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura. 

Akizungumzia kuhusiana na maandalizi ya uchaguzi huo mdogo wa Chalinze,Msimamizi msaidizi wa uchaguzi wa jimbo hilo,ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo Samweli Sarianga alisema kuwa vifaa vyote na maandalizi yamekamilika japokuwa kumekuwako na changamoto nyingi ikiwamo uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha hivi karibuni na kusisitiza kuwa iwapo hali ya hewa itakuwa ni nzuri basi kuna uhakika wa vifaa vyote vya uchaguzi vitakuwa vimefikishwa katika maeneo husika tayari kwa ajili ya kusambazwa katika vituo vya kupigia kura. 

Jumla ya vyama 5 vinatarajiwa kushiriki katika uchaguzi huo mdogo wa Chalinze,ambapo vyama hivyo ni CCM,CHADEMA,NRA,CUF na AFP
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live




Latest Images