Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

WAZIRI MAGUFULI AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA KUKAGUA NYUMBA ZINAZOJENGWA KWA AJILI YA WATUMISHI WA UMMA ENEO LA BUNJU B JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, amefanya ziara ya kushtukiza kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba 851 zinazojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) huko Bunju B katika wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. 
 Waziri Magufuli ambaye aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Alhaj Eng. Mussa Iyombe, ametembelea eneo hilo ambalo tayari kuna nyumba 130 zinazoendelea kujengwa katika hatua mbali mbali. 
 Akionyesha kuridhishwa kwake, Waziri Magufuli ameipongeza TBA kwa ubunifu wao na jinsi ambavyo wanautekeleza mradi huo kwani nyumba zinazojengwa zimepangwa vizuri na ujenzi wake pia ukitekelezwa kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa. 
 Awali akitoa taarifa ya maendeleo ya mradi huo ambao ni sehemu ya ujenzi wa nyumba 10,000 ambazo TBA inatarajia kuzijenga nchi nzima kwa ajili ya kuwakopesha watumishi wa umma, Mtendaji Mkuu wa TBA Architect Elius Mwakalinga alielezea kuwa kwa mwaka huu wa fedha wa 2013/14 jumla nyumba 2,500 zitajengwa katika mikoa 12 hapa nchini. Kati ya nyumba hizo mkoa wa Dar es Salaam utapata nyumba 1,400. 
 Hata hivyo, mbali na mafanikio hayo yaliyopatikana, changamoto kadhaa pia zimebainishwa ambazo zinahitaji kutafutiwa ufumbuzi ili kuweza kuutekeleza mradi huo kwa ufanisi. 
 Arch. Mwakalinga alibainisha kuwa mahitaji ya fedha kwa ajili ya kukamilisha mradi huo ni moja ya changamoto kubwa walionayo kwa sasa. Alibainisha kuwa, baada ya kuwa na mazungumzo na taasisi mbali mbali za fedha, TBA iliwasilisha Wizara ya Ujenzi mapendekezo ya kuomba mikopo kutoka vyombo hivyo ambapo udhamini wa Hazina ulihitajika kabla ya kuendelea na taratibu nyingine. 
Mapendekezo hayo yaliyowasilishwa yamechukua muda mrefu kiasi cha kuathiri maendeleo ya mradi huo. Kutokana na hali hiyo TBA imelazimika kuchukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kuangalia utaratibu wa kuuza kupitia mikopo ya benki, nyumba 155 ambazo ziko katika hatua za mwisho wa ujenzi. Tayari TBA imeanza mazungumzo na benki za CRDB, Azania Bancorp, Barclays, ABC, TIB na NMB kwa ajili ya kuwapatia mikopo watumishi wenye sifa ambao wamekwisha wasilisha maombi ya kuziwa nyumba hizo. 
Jumla wa maombi 3,000 yamepokelewa TBA kutoka kwa watumishi wa ngazi mbali mbali. Nyumba hizo zinatarajiwa kuuzwa kwa kiasi cha kuanzia Shilingi milioni 30 hadi milioni 180 kulingana na ukubwa wa nyumba. 
 Katika hatua nyingine Waziri Magufuli ameidhinisha kutolewa kwa fedha kiasi cha Shilingi milioni 800 zilizopatikana kutokana na mauzo ya nyumba ambapo ameagiza kuwa taratibu zikamilishwe mara moja ili fedha hizo zitumike kukamilisha ujenzi wa mradi huo wa Bunju B unaotekelezwa na TBA. 
Hadi sasa kiasi cha Shilingi bilioni 3.42 kimekwishatumika kwa ujenzi wa nyumba hizo pamoja na barabara zenye urefu wa kilometa 9.5 katika eneo hilo. 
 Waziri Magufuli hata hivyo imezitaka mamlaka zinazohusika na ujenzi na matengenezo ya barabara nchini ambazo ni TANROADS na Halmashauri mbali mbali kuhakikisha kuwa zinatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara katika maeneo ambayo yatajengwa nyumba zilizo katika miradi hii ya TBA kwani hilo ni jukumu lao na sio la TBA.
Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Elius Mwakalinga (kulia) akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Magufuli (katikati) akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Mussa Iyombe (kushoto) kuhusu utekelezaji wa ujenzi wa nyumba 851 zinazojengwa eneo la Bunju B jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Elius Mwakalinga (kushoto) akimwonyesha Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Magufuli (wa pili kulia) utekelezaji wa ujenzi wa nyumba 851 zinazojengwa eneo la Bunju B jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Magufuli (mbele kulia) akikagua utekelezaji wa ujenzi wa nyumba 851 zinazojengwa eneo la Bunju B jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Elius Mwakalinga.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Magufuli (katikati) akikagua utekelezaji wa ujenzi wa nyumba 851 zinazojengwa eneo la Bunju B jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Mussa Iyombe (kulia) na Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Elius Mwakalinga (kushoto) pamoja na Watendaji wengine kutoka Wizara ya Ujenzi.

KENYAN NITE @ THAI VILLAGE AT MASAKI IN DAR ON SATURDAY

$
0
0
If it's Kapuka, Genge, Dancehall, Mugithi, Chakacha, Benga, Kamba and much more from area code +254...then this is the place to be!

For further information and all updates: 
Like our page on Facebook "blisseventz255"

EALA SET TO VISIT 5 COUNTIES AS IT STARTS KENYA TOUR

$
0
0
East African Legislative Assembly
The East African Legislative Assembly (EALA) Members are set for a ten-day extensive tour of the Republic of Kenya beginning tomorrow. The tour which is being held with the support of the Kenya Government through the Ministry of East African Affairs, Commerce and Tourism, shall see theregional legislators’ tour projects and interface with various stakeholders in five counties. 
The visit takes the EALA to Mombasa, Kilifi and Nairobi counties in the first leg before winding up with a tour of Nakuru and Machakos counties.  
 The tour seeks to enable EALA to appreciate the diversity of the people and the development initiatives that Kenya has to offer to the region.  At the same time, the legislators shall interact directly with citizens and hear their views, aspirations and fears on the integration process.   Legislators are also expected to get first-hand experience on the workings of a devolved government following the promulgation of the Constitution in Kenya in 2010.
According to the Co-ordinator of the trip, EALA MP (Kenya), Hon Peter Mathuki, the visit shall enable the Members to fully apprise and acquaint themselves with developments in Kenya and key integration issues.

‘Article 5 of the Treaty envisages a People-Centred integration. In this regard, we must enhance involvement of the people in deciding on the matters of the Community. It is important for the Assembly to be in tandem with the needs of the people through structured interface and the working tour is one such avenue’, Hon Mathuki stated.

At the Coast, the legislators shall visit the Kenya Ports Authority and then call on the Mombasa County Government and the Kilifi County Government respectively.

While in Nairobi, EALA is to meet with a number of stakeholders including the top leadership of the Lamu Port Southern Sudan-Ethiopia Transport (LAPSSET) Corridor project, Project, Konza Techno City, Vision 2030 Secretariat as well as the officials of the Kenya Private Sector Alliance (KEPSA) and the East African Business Council (EABC).

They shall while in Nairobi also have a date with the University of Nairobi’s School of Health identified as one of the EAC Centres of Excellence and hold interactive sessions with Parliamentary and Senate Committees and civil society groupings. 
In Naivasha, Nakuru county, the EALA is expected to tour the Olkaria Geothermal station. The tour is to climax with a courtesy visit to the Machakos County Government and a trip to the Export Processing Zone and the Kenya Meat Commission in Athi-River. 
In his address to the 3rd Meeting of the 2nd Session of the 3rd Assembly in November 2013, President Uhuru Kenyatta pledged his Government’s support for the Kenya tour.
“Madam Speaker, my Government not only supports the Assembly’s working tours; we have committed ourselves to facilitate your tour of our country.  If East African integration is to be truly people-centred, the Assembly must be able to fully discharge it responsibility of sensitizing the Community’s citizens”, President Kenyatta remarked.  
Since, 2004, the Kenya Government has supported EALA Members to visit different parts of the country and to interact with the citizens while noting the progress that Kenya is making in the Integration process. The tours were held in 2004, 2005, 2006, 2007 and 2008.

introducing 'Happy Day' by Mr Mossy - Prod Stide Bukobanyumbani.com

mhe bernad membe alivyoongea baada ya kuhojiwa na kamati ya maadili ya ccm

Shukurani za Asia Idarous Khamsin kwa kuiunga mkono "Lady in RED" 2014

$
0
0
Asia Idarous akipita kwenye red Carpet
Asia Idarous akipita kwenye red carpet

MAMA wa Mitindo nchini na Mkurugenzi wa Fabak Fashions, Asia Idarous Khamsin amewashukuru wadau mbali mbali kwa kuendelea kuliunga mkono onesho la Mitindo la kila mwaka la 'Lady in Red' ambalo kwa mwaka huu limetimiza miaka 10 tokea kuanzishwa kwake huku likiwa la mafanikio kwa kuibua wanamitindo wakubwa hapa nchini.

Akizungumza Dar es salaam, katika ofisi za Fabak zilizopo Msasani jirani na Kwa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam, Asia Idarous alishukuru wadau mbali mbali waliojitokeza siku hiyo sambamba na wadhamini waliofanikisha kwa shughuli hiyo kubwa hapa nchini.

Asia alisema ni jambo la fadhira kwa kushukuru huku akiahidi kuboresha kama kulikuwa na mapungufu ya hapa na pale. 
"Muungwana ni vitendo, ‘Lady in red Super brand, 10th Anniversary’ ilikuwa ni ya kipekee kwa mwaka huu, hivyo nawashukuru nyote kwa kuliunga mkono jukwaa la Lady in red 2014, kwa kutimiza miaka hii 10" alisema Asia Idarous.

Aliongeza kuwa, kuelekea onyesho la mwakani kwa mwaka 2015, jukwaa hilo la Lady in Red, linatarajia kuwa la kimataifa ikiwemo wabunifu wa kimataifa kuonyesha ubunifu wao hapa nchini.

"Kwa sasa tunaelekea anga za kimataifa kupitia jukwaa hili hili la Lady in red, zaidi ni kuendelea kuliunga mkono ilikutimiza ndoto hizi, na hii itasaidia kufungua milango ya wabunifu wetu kujiuza nje ya mipaka yetu" alisema Asia Idarous. 


waathirika wa kimbunga makete wazidi kupata msaada

$
0
0
Mkuu  Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro (kulia) akipokea msaada huo kwa niaba ya wananchi kutoka kwa mkurugenzi wa shirika la SUMASESU lililopo wilayani hapo
 Mkurugenzi wa shirika la SUMASESU Bw. Egnatio Mtawa akizungumza wakati akikabidhi msaada wa bati 25 na misumari kwa ajili ya waathirika wa kijiji cha Ndulamo
 mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro akizungumza wakati akipokea msaada huo kwa niaba ya wananchi

Na Edwin Moshi
Janga la kuezuliwa nyumba 11 katika kijiji cha Ndulamo wilayani Makete mkoa wa Njombe limeonesha kugusa wadau mbalimbali, ambapo shirika lisilo la kiserikali la SUMASESU lililopo wilayani hapo limetoa msaada wa bati 25 na kilo 5 ya misumari vyote vikiwa na thamani ya tsh. 325,000/=.
Akikabidhi msaada huo hii leo Mkurugenzi wa SUMASESU Bw. Egnatio Mtawa  amesema shirika lake limekuwa linafanya kazi kwa asilimia kubwa ndani ya wilaya ya Makete hasa na watu wazima (wasio na maradhi) hivyo wameguswa na janga hilo na kuona njia mojawapo ya kuwasaidia ni kutoa bati na misumari kulingana na uwezo wa shirika hilo.
Bw. Mtawa amesema kupitia matatizo mbalimbali yanayoigusa jamii ni vyema wanamakete wakawa na mshikamano na kuwasaidia wananchi pale wanapopata matatizo mbalimbali kwa kuwa hawajapenda kupata madhara hayo.

"Tumesikia kwenye vyombo vya habari maafa yaliyowakumba wenzetu wa Ndulamo, kwa kweli ni janga kubwa na hawawezi kulimaliza wenyewe ila kwa mshikamano wetu wa pamoja ni hakika tutaweza kuwasaidia kuondkana na kero hii iliyowakumba" alisema Mtawa.
Akipokea msaada huo mbele ya viongozi wa kijiji hicho Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro amemshukuru mkurugenzi  huyo kupitia shirika lake la SUMASESU kwa kutoa msaada huo na kuongeza kuwa msaada huo utakuwa msaada mkubwa kwa waathirika hao.
Amesema anaimani wapo wananchi wenye uwezo na wenye mapenzi mema ya kusaidia kuendelea kujitokeza kwani muda bado upo na unahitajika ili usaidie kutatua tatizo hilo mapema.
"Kwa kweli kitendo kilichofanywa na SUMASESU kama wadau wa maendeleo wilayani Makete, ni cha kuigwa na kimesaidia sana, naomba wanamakete, ama wananchi wenye mapenzi mema kuendelea kutoa misaada yao ya hali na mali, si lazima uwe msaada mkubwa, hata bati moja linatosha" amesema Matiro.
Naye mwenyekiti wa kijiji hicho Bw. Liliyo Tweve ameshukuru kwa kijiji chake kupatiwa msaada huo na kusema kuwa hivi sasa kazi ya kujenga nyumba hizo zilizoezuliwa inaendelea vizuri na msaada huo utarahisisha ujenzi kukamilika mapema
Amesema Maazimio ya mkutano uliofanyika jana kijijini hapo yanaendelea vyema na inategemewa ndani ya wiki mbili zijazo kazi hiyo iwe imekwisha

hoja ya haja: Mimi wa Ughaibuni kama Diaspora pia ni Mtanzania

$
0
0
Swali muhimu tunaloulizwa Watanzania tunaoishi ughaibuni ni: tunataka nini hasa kwenye katiba mpya? Na ni kwa namna gani tunataka changamoto zetu ziingizwe kwenye katiba mpya? 

Katika kipindi hiki cha Bunge Maalumu la Katiba tumeonelea ni muafaka kuyapatia majibu maswali haya. Kwa kuanzia na bila kupoteza muda, Watanzania wa ughaibuni tunataka masuala yafuatayo yaingizwe kwenye katiba mpya: 
· Uraia wa nchi mbili; 
· Haki ya kurudi Tanzania kwa Watanzania na Watu wenye asili ya Kitanzania yaani “Right of Return”; 
· Haki ya kupiga kura yaani “voting rights”; 
· Kupata wawakilishi wa kuwawakilisha Watanzania wa ughaibuni serikalini na bungeni; 
· Haki ya kushiriki katika shughuli za kiuchumi na kimaendeleo za Tanzania. 

Katika kujibu swali la pili ambalo ni: ni kwa namna gani tunataka haya tunayoyataka yaingizwe bungeni? Jibu la swali hili ni rahisi sana. 

Tunawaomba Waheshimiwa wa Bunge Maalumu la Katiba pale watakapoanza kuyajadili masuala ya uraia na yale ya Watanzania waishio ughaibuni basi wakubaliane na maombi yetu yaliyotajwa hapo juu na wayapigie kura na kuyaingiza kwenye katiba. 

Mwakilishi wetu kwenye Bunge Maalumu la Katiba Mheshimiwa Kadari Singo naye anaomba msaada wa Waheshimiwa wabunge wa Bunge Maalumu la Katiba katika kuyapigia kura maoni haya na kuyaingiza kwenye katiba mpya.

Kwenye maombi yetu, karibu asilimia 95 ya Watanzania wanaoishi ughaibuni wanakubaliana nasi viongozi wao wa Jumuiya za Watanzania kwenye diaspora kuwa uraia wa nchi mbili unatoa suluhisho kwenye matatizo yao wanayokumbana nayo siku hadi siku huku ughaibuni. 

Vile vile uraia wa nchi mbili utalipatia taifa faida nyingi tu za kiuchumi, kiutamaduni, kielimu, kisayansi, kiteknolojia na katika masuala mengine mengi ambayo ni muhimu katika kuleta maendeleo ya Tanzania kwa ujumla. 

Suala la uraia wa nchi mbili na haki ya kurudi nyumbani kwa binadamu yeyote anayeishi kwenye nchi nyingine lipo vile vile kwenye “The Universal Declaration of Human Rights” kama haki ya msingi kwa kila binadamu. 

Kwenye haki za binadamu mtu yeyote ana haki ya kurudi katika nchi aliyozaliwa au katika nchi aliyo na ndugu na familia yake. Kwa mantiki hiyo “Right of Return” kama ilivyojadiliwa hapo juu ni muhimu sana kwa Watanzania wanaoishi ughaibuni na kuwakatalia haki hii, je si kukiuka misingi ya haki za binadamu? 

Watanzania tuna rekodi nzuri ya kuheshimu haki za binadamu na nadhani huu ni wakati muafaka kwa Bunge Maalumu la Katiba kuidhinisha uraia wa nchi mbili ili kutoa haki kwa Watanzania wa ughaibuni kurudi makwao watakapotaka kufanya hivyo. 

Vile vile huu ni wakati muafaka kwa Bunge Maalumu la Katiba na kwa Serikali kukubali kuwa Watanzania waishio ughaibuni wanatakiwa

kupewa haki yao ya kupiga kura. Hakuna sababu yeyote ya kimsingi ya kuwakatalia haki hii. 

Kama kukiwepo na “political will” basi itakuwa ni rahisi kwa Watanzania wa ughaibuni kuruhusiwa kupiga kura. Kupiga kura ni haki ya kila raia na watanzania wa ughaibuni wamekuwa wakinyimwa haki hii kwa muda mrefu. 

Tunaiomba serikali na Bunge Maalumu la Katiba kusikiliza kilio hiki kutoka ughaibuni na wahakikishe kuwa suala hili linaingizwa kwenye katiba mpya, ikiwa ni pamoja na kupatikana kwa wawakilishi wa Watanzania waishio ughaibuni watakaochaguliwa na Watanzania wa Ughaibuni kwa kufuata Katiba ya Tanzania na kwa kufuata sheria zitakazotungwa nchini Tanzania. 

Kwa kumalizia tunawaomba Watanzania wasaini “petition” ya kuomba uraia pacha iliyowekwa kwenye blogu mbalimbali. 

Tunaliomba Bunge Maalumu la Katiba liyaangalie maombi yetu haya na liyafanyie kazi ili yaingizwe kwenye katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Imeandaliwa na Deogratius Mhella, 
Katibu wa Vikao vya Muungano wa Jumuiya za Watanzania Marekani na DICOTA 
Katika kufikisha Maombi ya Watanzania wa Ughaibuni kwenye Vyombo vya habari ili kuelimisha umma wa Watanzania kuhusu maombi ya Watanzania waishio ughaibuni kwenye Bunge Maalumu la Katiba.

Mhe.Pandu Ameir Kificho ndiye Mwenyekiti wa Muda wa Bunge la Katiba.

$
0
0

Bunge Maalumu la Katiba limemchagua Mhe. Pandu  Ameir Kificho (pichani) kuwa Mwenyekiti wa Muda wa Bunge la Katiba.
Katika uchaguzi wa nafasi hiyo uliofanyika  kwenye Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma, Mh.Kificho ameshinda kwa Kura 393 sawa na Asilimia 69.
Washindani wengine, Bi.Magret na Mhe.Mahalu wamepata Kura 84 kila mmoja sawa na Asilimia 15.79%.
Akitangaza matokeo hayo Katibu wa Bunge Dk Thomas Kashililah alisema Mhe. Kificho ameshinda baada ya kupata kura 393 sawa na 69.19% ya kura 558 zilizopigwa na kuwaacha kwa mbali washindani wake wa karibu, Mhe. Costa Mahalu na Mhe. Magdalena Rwebangira.

Awali Katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashilila alitangaza kuwa Kuna Wagombea 4 wa nafasi ya Uenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, lakini katika hatua za Mwisho za Kujinadi kwa Wajumbe, mgombea Mmoja Mh.Sadifa (Mwenyekiti wa UVCCM na Mbunge kutoka Zanzibar)aliamua kujitoa kwa Kusema anamheshimu Mzee Kificho hivyo anaona ni vyema akamuachia.
Mwenyekiti wa Bunge la Katiba ndiye atakayesimamia Kutunga Kanuni zitakazo tumika kwenye Bunge la Katiba. Mhe. Kificho pia ndiye Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar.. 

KIJANA MTANASHATI ATAFUTA MCHUMBA WA KUOA: Ona picha yake na sifa za mchumba huyo anayemtaka apo chini

$
0
0

Master Oscar John

Mimi ni kijana wa kitanzania ambaye nimekulia katika maadili ya kidini na malezi mazuri ya kifamia, napenda nichukue fursa hii nitangaze nafasi ya mchumba ambaye kama ata kidhi vigezo vyangu atakuwa ndio mke wangu wa ndoa. Kifupi mi ni mtaalam wa IT naishi Dar es salaam. 
Mchumba ninaye mtaka ni vema awe amekulia malezi ya kidini kwa sababu mimi ni mcha Mungu na napenda kusali kwa hiyo napenda na yeye awe hivyo, malezi yangu ni ya dini ya kikristo ni vema na yeye akawa huko ila itakapobidi anaweza akatoka dini tofauti na mimi, ila itamlazimu aamie kwenye dini yangu, napenda pia asiwe zaidi ya miaka 24, kwa upande wa elimu asiwe chini ya kidato cha nne. 
Namtanguliza Mungu mbele kwa yeyote ambaye anaona anafaa katika vigezo vyangu ili ambariki kabla hajafanya mawasiliano na mimi. 
Kwa mawasiliano na mimi: 
Mungu akutangulie wewe utakayeona 
unafaa kuishi na mimi kama mke na mume. 

Asanteni na karibu

TANZANIAN DIASPORA: We Tanzanians in the Diaspora , Believe That Dual Citizenship is a Great Thing for The Country

$
0
0
We Tanzanians in the  Diaspora , Believe That Dual Citizenship is a Great Thing for The Country. Please Support.
Dual Citizenship ni :
1. Kwa Ajili ya Wewe
2. Kwa Ajili ya Nchi
3. Kwa Ajili Ya Watoto Wako
4. Kwa Ajili Ya Maendeleo ya Nchi

The government has said that it is high time now for Tanzania to allow dual citizenships so as to enable the Diasporas contribute to the country’s development in terms of income and expertise.

It has been said that many wealthy and well educated Tanzanians living abroad fail to contribute to national development because they are denied the right to dual citizenship.

The Minister for Foreign Affairs and International Co-operation Bernard Membe said this when he was launching a new outreach project for Tanzanians living abroad prepared by the Tanzanian Diaspora department and International Organisation for Migration (IOM) called on all citizens, politicians and academics to support the inclusion of dual citizenship in the new constitution. 

Article 0

gado leo

Gari la JWTZ na Bus la Mohamed zagongana karibu na mizani ya Dodoma jioni hii

$
0
0
 Wananchi wakijaribu kumtoa dereva wa gari la JWTZ baada ya ajali na basi la Mohamed Trans jioni hii karibu na mizani ya Dodoma. Chini ni gari hilo la jeshi baada ya ajali. Picha kwa hisani ya JF

Article 22


R.I.P

HOSPITALI YA RUFAA YA KCMC YAZINDUA HUDUMA YA UPASUAJI KWA NJIA YA DARUBINI

$
0
0
 Madaktari bingwa wakifanya upasuaji kwa njia ya darubini ikiwa ni teknolojia mpya kufanyika katika Hospitali ya rufaa ya KCMC, Teknolojia hiyo inadaiwa kuokoa muda na gharama za upasuaji pamoja na kupunguza vifo.
 Madaktari KCMC wakimfanyia mgonjwa upasuaji kwa kutumia Teknolojia mpya Darubini.
 Dkt. Kondo Chilonga akiongoza madaktari wenzake kumfanyia mgonjwa upasuaji kwa kutumia teknolojia mpya ya Darubini ambayo inaruhusu upasuaji kufanyika bila ya kuchana ngozi.
 Zoezi linaendelea ukimya tafadhali!!! kwa mbali ni mtaalamu wa upasuaji wa Darubini (mzungu) kutoka Uingereza, Dkt. Liam Horgan.
Dkt. Kondo Chilonga akiongoza madaktari wenzake kumfanyia mgonjwa upasuaji kwa kutumia teknolojia mpya ya Darubini ambayo inaruhusu upasuaji kufanyika bila ya kuchana ngozi. 
Picha na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,  Moshi.

BENKI YA NMB YADHAMINI MKUTANO MKUU WA MAKAMANDA WA POLISI MOSHI

$
0
0
BENKI ya NMB imetoa kiasi cha shilingi milioni 75, kudhamini mkutano mkuu wa siku sita wa Maafisa wa Jeshi la Polisi nchini unaoendelea katika chuo cha taaluma ya Jeshi la Moshi (MPA), Mkoani Kilimanjaro. 
 Mkutano huo ambao unajumuisha makamishna, makamanda wa mikoa ya Tanzania bara na Visiwani pamoja na maafisa wakuu waandamizi wa Jeshi hilo kutoka Makao makuu, ulizinduliwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe.Pereira Sirima. 
 Akizungumza katika uzinduzi huo, Meneja wa NMB, kanda ya Kaskazini, Bi. Vicky Bishubo, alisema udhamini huo unajumuisha usafiri wa mabasi kwa washiriki wote kutoka mikoa yote ya Tanzania bara na Visiwani, pamoja na maandalizi ya mkutano huo. 
 Alisema pamoja na hayo, NMB imetoa Kompyuta mpakato nne zitakazowezesha mipango ya Jeshi ya kupambana na Uhalifu wa Mitandao, Mikoba, Notebook na kalamu za kutosha.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Pereira Sirima akiwasili katika viwanja vya chuo cha taaluma ya polisi Moshi (MPA), kufungua mkutano mkuu wa Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro, chuoni hapo. Mkutano huo unadhaminiwa na NMB.
Naibu waziri wa Mambo ya ndani, Pereira Sirima (katikati), IGP Ernest Mangu kulia kwake na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro katika uzinduzi wa mkutano wa Maafisa wa Jeshi la Polisi. 

Naibu Waziri wa Mambo ya ndani Mhe. Pereira Sirima (katikati), akifungua mkutano huo wa Maafisa wa Jeshi la Polisi. 

Naibu Waziri katika picha ya pamoja na wadau wa Jeshi la Polisi wakiwemo wadhamini wa mkutano huo benki ya NMB.
Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini Bi. Vicky Bishubo (kushoto) akifaruhia  jambo na maafisa wenzake wa benki hiyo, Meneja Mikopo  Tawi la Nelson Mandela Moshi, Saidi Pharseko,  Meneja Wateja Binafsi  Bi. Susan Shuma na Meneja Mawasiliano Bi. Josephine Kulwa.

Taarifa kwa Umma: Vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa.

Information to the Public: Heavy rains are expected.

Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images