Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110016 articles
Browse latest View live

MKURUGENZI WA MASHITAKA AWASILISHA OMBI MAHAKAMA KUU YA TANZANIA KUTAKA KUTAIFISHA NYUMBA SABA ZA KIFAHARI

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Michuzi Globu

MKURUGENZI wa Mashitaka Nchini (DPP), amewasilisha maombi Mahakama Kuu ya Tanzania ya kutaka kutaifisha nyumba saba za mke wa aliyekuwa mmoja wa Wakurugenzi wa Kampuni Superior Financing Solutions Aloycious Gonzaga, Magreth Gonzaga.

Katika maombi hayo namba moja ya mwaka 2019 yanayotarajia kuanza kusikilizwa mbele Jaji Sirilius Matupa, Novemba 26, mwaka 2019 saa tatu asubuhi, DPP, anaomba kutaifisha Plot no.199, Block D, no.121302 iliyopo Tegeta jijini Dar es Salaam, Plot no.200 Block D no.39021 ya Tegeta, Plot No.1378, Block E Tegeta ikiwa namba za hati 41275 na Plot No.176 Block B iliyopo Aman Gomvu ikiwa na hati namba 138598. Nyumba nyingine ni ya Plot No.191, Block B iliyopo Aman Gomvu ikiwa na hati namba No.132797 na No.174 Block B iliyopo Aman Gomvu ikiwa na hati namba 138597.

Awali kabla kuwasilishwa kwa maombi hayo, TAKUKURU ilitangaza kumsaka mwanamke huyo anayedaiwa kumiliki nyumba tatu za kifahari jijini, huku akituhumiwa kutakatisha fedha haramu kinyume cha Kifungu Na. 12(d) na 13(a) cha Sheria ya Utakatishaji Fedha Haramu Na. 12 ya Mwaka 2006.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Diwani Athumani, amesema wanamsaka Magreth kupitia tangazo lililotolewa kwa amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inayosikiliza shauri la jinai namba 28 la mwaka 2019.

Alidai Magreth ambaye kwa sasa anadaiwa kukimbilia nje ya nchi, anatafutwa na TAKUKURU kwa tuhuma za kutakatisha fedha na kujipatia mali kupitia Kampuni ya Superior Financing Solution Limited (SFS) inayodaiwa kufanya biashara bila kulipa kodi ya serikali. "Wakati uchunguzi unaendelea, mtuhumiwa alitoroka nchini," Athumani alisema.

“Kisheria mtuhumiwa huyo anahesabiwa kama ni mtuhumiwa aliyetoroka. Kutokana na sababu hiyo, Takukuru inapaswa kutangaza kutafutwa kwake kabla ya kutaifisha mali alizojipatia kwa njia ya rushwa," aliongeza.

Aloycious Gonzaga na mwenzake Isaack Kasanga wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 5/2019 katika Mahakama Kuu Kitengo cha Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi 'Mahakama ya Mafisadi'.

Washitakiwa wanakabiliwa na mashitaka 45 ambayo ni kula njama kutenda kosa kosa moja, kughushi 12, kuwasilisha nyaraka za uongo tisa, kushindwa kulipa kodi na utakatishaji fedha mashitaka 30. Inadaiwa kati ya Machi 2, mwaka 2010 na Aprili 26, mwaka 2016 katika maeneo tofauti ndani ya Jiji la Dar es salaam washitakiwa hao walikula njama kwa kugushi,kukwepa kulipa kodi na kutakatisha.

Shirika lisilo la Kiserikali la Camfed la endesha semina ya wabunge

$
0
0
Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Camfed, Lydia Wilbard akizungumza wakati wa Semina na wabunge wa Kamati ya Bunge ya Huduma za maendeleo ya Jamii, iliyofanyika Bungeni jijini Dodoma leo. Semina hiyo iliandaliwa na shirika lisilo la kiserikali linalojishughurisha na Mtoto wa kike aliye katika mazingira magumu la Camfed.
Mnufaika na Shirika lisilo la kiserikali la Camfed, Stumai Kaguna akizungumza wakati wa Semina ya Wabunge wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Maendeleo ya Jamii.
Meneja Mradi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Camfed, Anna Sawaki akizungumza wakati wa semina ya Wabunge wa kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.
Afisa Miradi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Camfed, Diris Martin akizungumza wakati wa Semina kwa wabunge wa Kamati ya Huduma za Masendeleo ya Jamii.

MAMLAKA YA DAWA NA VIFAA TIBA (TMDA)YAFANYA UKAGUZI VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA, YANASA DAWA BANDIA SABA

$
0
0
MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), imefanya ukaguzi katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma za afya zikiwemo dawa na kugundua kuwepo kwa dawa bandia ambazo kwa sasa wanazishikilia.

Akizungumza leo Novemba 13,mwaka 2019 jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMDA,Akida Khea amesema kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Septemba 2019, baadhi ya dawa bandia zilizobainika na kutolewa taarifa ya kuwepo katika nchi za wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni pamoja na dawa aina ya Gentrisone Cream 10gm toleo namba GNTRO X030,Augmentin 625mg tables toleo namba 786627 na kapsuli za Cold caps.

"Viwanda halisi vinavyotengeneza dawa hizi vilithibitisha kuwa dawa hizo hazikutengenezwa na viwanda huzika,"amesema Khea. Aidha amesema kuwa kwa mujibu wa uchambuzi na uchunguzi uliofanywa na TMDA, matoleo ya dawa hizo husika yalithibitishwa kuwa ni bandia.

"Uchunguzi kupitia maabara ya TMDA kwa dawa ya Gentrisone cream 10gm toleo namba GNTRO XO30 ulionesha kuwa dawa hiyo haikuwa na viambato hai (active pharmaceutical ingrediets) vya dawa hiyo ambavyo ni Betamethasone Proprionate, Clotrimazole na Gentamycin sulfate,"amesema Khea.

Hata hivyo, Khea amesema kuwa katika operesheni ya ukaguzi katika Mikoa inayopakana na nchi za jirani ikiwemo mikoa ya Kigoma,Songwe,Kagera,Rukwa, Mbeya,Mara,Kilimanjaro, Arusha,Mwanza, Ruvuma,Mtwara na Tanga. Wakati mikoa mengine ni Dar es Salaam,Dodoma,Shinyanga,Geita,Singida ,Morogoro,Iringa, na Tabora

"Katika operesheni hii jumla ya maeneo 558 ikiwa ni famasi 209,maduka ya Dawa Muhimu 263, Vituo vya kutolea huduma za afya 27,Maduka ya Vifaa Tiba 21 na Vituo vya dawa asili na tiba mbadala 38 katika,"amesema Khea.
  Aina saba ya dawa duni na bandia zilizokamatwa katika ukaguzi maalum wa dawa ulioendeshwa na TMDA.
 Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo ya Teknolojia kutoka Wizara ya Mifugo na Uvivu,Chanasa Ngeleja akizungumza wakati wa uwasilishaji wa ripoti ya ukaguzi wa dawa leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka michuzi Tv)
aimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA), Akida Khea akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) mapema wakati wa kutangaza matokeo ya ukaguzi maalum wa dawa vifaa tiba, vitendanishi, dawa asili na tiba mbadala, tukio lililofanyika makao makuu ya TMDA, Mabibo Jijini Dar e Salaam.

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA), Akida Khea akionesha moja ya dawa zilizokanatwa katika tukio hilo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema wakati wa kutangaza matokeo ya ukaguzi maalum wa dawa vifaa tiba, vitendanishi, dawa asili na tiba mbadala, tukio lililofanyika makao makuu ya TMDA, Mabibo Jijini Dar e Salaam.

Duniani Leo November 13, 2019

UCHAMBUZI WA KITABU CHA HISTORIA YA MAISHA YA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA TATU MHE. BENJMAMIN WILLIAM MKAPA

$
0
0



NA PROFESA RWEKAZA MUKANDALA


Mtoto Benjamin William Mkapa, alifundishwa kupika chakula na mama mzazi Stephania akiwa mdogo. Alipokwenda shule hapo kijijini Lupaso, Ndanda na hatimaye St. Francis Pugu na Makerere, alifundishwa kupika, kufinyanga, kubuni na kuchambua mawazo na kuyaweka sawa kama msomi mbunifu na mwandishi. Kitabu hiki ni zao la mpishi wa mawazo mahiri aliyebobea.  Ni kitabu cha kurasa mia tatu na kumi na tisa, katika sura ya kumi na sita.   Kuna utangulizi ulioandikwa na Mheshimiwa Joaquim Chissano, Rais mstaafu wa Msumbiji, Pia kuna picha nyinge nzuri, na viambatisho viwili.  Mchapaji Mkuki na Nyota wamefanya kazi nzuri sana, sikubaini kosa hata moja. 

Wasilisho hili linamega simulizi hii katika sehemu kuu tatu. Kwanza tunapewa vionjo vitamu tukielezwa kuzaliwa kwake, kukua na kwenda shule. Hii ilikuwa matayarisho ya kufikia nia au azma yake ya maisha. Kisha tunaletewa mlo wenyewe (main course) uliosheheni kumbukumbu  na ngano za huyo kijana sasa mtu mzima akiwa kazini, mpaka akaukwaa urais wa Tanzania. Mwisho tunaelezwa kwa ufupi maisha yake baada ya kumaliza ngwe yake ya miaka kumi ya urais.

2.      KUZALIWA, MALEZI NA ELIMU

Baba yake mzazi Mheshimiwa Mzee William Matwani alikuwa mpishi msaidizi huko Mission Ndanda. Wamisionari wakambatiza, wakamfundisha kusoma, kuandika na kuhesabu, na kumfanya Katekista. Alipelekwa Lupaso, ambapo alieneza dini na kufundisha Bush school ya Wamisionari. Alimwoa Bibi Stephania Nambanga ambaye hakujua kusoma wala kuandika. Walijaliwa watoto wanne Benjamin akiwa wa mwisho. Kama ilivyo kwa kabila la Makua, Benjamin alipewa jina la ujombani, Mkapa. Mama hakuwa na muda wa kujifunza kusoma na kuandika kwani yeye ndiye alikuwa msingi wa familia, akihakikisha analima, kulisha familia, na kuwalea watoto.  Alikuwa mkali lakini msikivu na mpenda haki. Wazazi hawa ndio vinara wa sehemu hii ya kwanza ya simulizi hii. Waliishi pamoja kwa uadilifu na heshima kubwa, na mapenzi ya pamoja kwa watoto wao.

Ingawa wazazi hawakwenda shule, walipenda sana watoto wao wote waende shule. Hii pamoja na kwamba Baba Matwani alikuwa na kipato kidogo lakini cha uhakika kila mwezi, kiliifanya familia ionekane iko tofauti. Hii ilipelekea wivu na hatimaye chuki kutoka kwa jamii. Wivu huu na chuki ulisababisha tukio moja baya sana ambalo Mheshimiwa Mkapa analikumbuka kwa uchungu. Mwaka 1947, kulitokea ukame mkali, basi watu wakamleta mganga wa kienyeji akaamua kuwa mama mzazi, mama yake na bibi yake ndio walikuwa wameloga na kuzuia mvua. Walipigwa na kuteswa sana hadi Padri Mzungu alipofanikiwa kuwanasua. Bibi wa mama aliaga dunia muda mfupi baada ya tukio hilo.

Kijana Benjamini na mwenzie mmoja ndiyo waliopata bahati ya kuendelea na masomo ya Sekondari, kutoka darasa la watoto 25 hadi 30.   Kuchaguliwa ilikuwa bahati nasibu.

Shule ya sekondari ya Ndanda ilikuwa kilometa 60 kutoka Lupaso. Yeye na wenzie walitembea kwa miguu, bila viatu, kwa siku mbili, wakiwa wamebeba kichwani vitu vyao ambavyo vilikuwa vimefungwa katika mkeka. Baadae alipata sanduku la chuma.

Walimu wa Ndanda walikuwa wamisionari na walikazia sana sala na kazi “Ora et labora’’.   Wanafunzi walipika chakula chao wenyewe. Kwa kuwa kijana Benjamini alikuwa mdogo sana alipewa kazi ya kuosha vyombo. Kawaida alivibeba vyombo kichwani mpaka mahali pa kuvioshea, na kuvirudisha. Anasema kubeba vyombo hivyo ndiyo sababu ana upara hadi leo

Mwaka 1952, akiwa na umri wa miaka 15, aliamua kwenda Seminari darasa la nane. Baada ya muda mfupi aliamua kuwa upadre haukuwa wito wake, akarudi Ndanda kuendelea na shule. Mwaka 1957, alichaguliwa kwenda St. Francis College Pugu ikiwa ni shule kuu ya Wakatoliki Tanganyika.  Akiwa Pugu, kijana Benjamini alianza kupata mwamko wa kisiasa. Aliunga mkono harakati za kupata uhuru kwa kuandika barua kwa Mhariri wa Gazeti la “Tanganyika Standard” ambalo sasa ni Daily News akiunga mkono hoja ya Uhuru. Barua ilichapishwa. Ila kijana Benjamini alitumia jina bandia!

Mhe. Mkapa alishinda mitihani yake ya kujiunga Chuo Kikuu Makerere, kwa kupata daraja la kwanza, akiwa kati ya wanafunzi watatu bora katika darasa la wanafunzi 51.

Makerere alikumbana na mambo mengi mapya: Alikuwa darasani na wanafunzi wa rangi tofauti, kwa mara ya kwanza alikwenda kucheza dansi ya kisasa, alipangiwa chumba cha kulala nk.

Mwamko wake wa kisiasa uliendelea.   Alijiunga na Bodi ya Wahariri ya gazeti la “Transition”; alikuwa mwanachama hai wa kikundi cha wanafunzi cha TANU, akiwa katibu na hatimaye mwenyekiti wake. Alishiriki  kwenye siasa za wanafunzi hapo chuoni. Aligombea Urais na ingawa hakushinda, wanafunzi wa kike walimpigia kura nyingi si kwa sababu alikuwa  na rafiki wa kike, ila kwa jinsi alivyoweza kujieleza kuliko mpinzani wake. Alikuwa ‘More articulate!’ Aliteuliwa Makamu wa Rais wa Serikali ya wanafunzi, na hatimaye alikuwa mwenyekiti wa Baraza la wawakilishi la wanafunzi hapo Makerere. Alihitimu masomo yake Aprili 1962, miezi minne baada ya Tanganyika kupata Uhuru. Alipata shahada ya lugha na fasihi ya kiingereza na fonetiki.  Alikuwa tayari kuifukuzia nia na ndoto yake.

3.      MAISHA NA KAZI

Simulizi ya maisha ya utu uzima iko katika sehemu mbili.  Kwanza ni alipoanza kazi mpaka alipogombea Urais.  Pili ni maisha ya Urais.  Sehemu hii ya simulizi imejaa sifa heshima na upendo mwingi kwa Mwalimu. Anastaajabu kwa jinsi Mwalimu alivyoiunganisha nchi katika kupigania vita vya ukombozi wa bara la Africa.  Kama wazazi wake mzee Matwani na Bibi Nambanga walikuwa mashujaa wa sehemu ya kwanza ya maisha yake, hakika Mwalimu ndiye shujaa katika sehemu hii ya pili.   Anamueleza Mwalimu kama labda alitumwa na Mungu kwa makusudi (Almost divine intervention).

Akiwa mtu mzima na mhitimu wa Chuo Kikuu Makerere Mheshimiwa Mkapa alipenda kuajiliwa kwenye Wizara ya mambo ya nchi za nje: Kwanza ilishindikana lakini, baadae akaambiwa, itawezekana kama ataajiriwa kwanza kama bwana shauri mkufunzi wa Wilaya, wakati akisubiri.  Kwa hiyo aliajiriwa hivyo huko Dodoma April 1962.

Baada ya miezi minne August 1962 aliitwa Dar es salaam aende kujifunza udiplomasia Columbia Marekani.

Baada ya mwaka mmoja alirudi nchini akaajiriwa wizarani.  Kazi yake kubwa ilikuwa kuchukua muhtasari wa mazungumzo Waziri wake au Mhe. Rais alipopata wageni.  Anamsifia kwa ujasiri pale alipovunja uhusiano na Uingereza.   Wakati huu Mhe. Mkapa alitumia muda wake binafsi ama kusoma habari Radio Tanzania Dar es salam, ama kumchumbia Bi Anna.

Siku moja aliambiwa anaitwa Msasani kwa Mwalimu. Walipaita Msasani nyumbani kwa Mwalimu “The Clinic”.  Mwalimu akamwambia anamteua kuwa Mhariri Mtendaji wa gazeti la The Nationalist.  Ilibidi aende Uingereza kujifunza mambo ya magazeti kwenye magazeti ya The Mirror.

Alirudi na kuanza kazi chini ya Mwalimu kama Mhariri Mkuu, Mhe. Mkapa alikuwepo Arusha wakati wa Azimio mwenzie Nsa Kaisi ndiye aliyebuni neno la Arusha Declaration, walilitumia kwenye The Nationalist, Mwalimu akalipenda, basi hayo maamuzi yakaitwa hivyo.

Mhe. Mkapa aliruhusiwa kuhudhuria mikutano ya kamati kuu ya TANU, ambayo wakati ule ilitawaliwa na malumbano ya hoja na uchambuzi yakinifu ambao umepotea.  Alihusika katika kutayarisha sera mbalimbali za chama kutokana na umahiri wake wa kumudu lugha.

Mwalimu na msaidizi wake Joan Wicken ndio walio mfundisha ujamaa na alivutiwa na msimamo wa usawa na umuhimu wa kujitegemea.  Aliunga mkono wazo la Jeshi la Kujenga Taifa na akamuomba Mwalimu akamkubalia ajiunge kwa hiari.   Alijiunga na kuhitimu.  Siku ya kuhitimu Mwalimu alikuwa ndie mgeni rasmi.  Mheshimiwa Mkapa alichaguliwa na wenzie kusoma risala na Mwalimu alicheka sana alivyomtambua kuwa ni yeye kwani alikuwa amepoteza ratili nyingi za uzito.  Alikuwa slim fit.  Mheshimiwa Mkapa aliitwa huko “The Clinic” Msasani mara kadhaa.

April 1972 Mwalimu alimteua kuwa Mhariri Mtendaji wa Daily NewsMuda mfupi baadaye Mwalimu alimteua kuwa Press Secretary wa Rais.  Anasema huu ndio ulikuwa mwanzo wa maisha yake kama mwanasiasa.Mwaka huohuo, Mwalimu alimuagiza aanzishe Shirika la Habari Tanzania – SHIHATA na kuwa Mtendaji Mkuu wake.Mwaka 1976 akamteua Balozi huko NigeriaMwaka mmoja baadaye akaitwa tena “ The Clinic” na kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje.  Hapa alikuwa kama msaidizi wa Rais kwani Mwalimu ndiye aliyeendesha mambo ya Nchi za Nje. Alifanywa pia Mbunge wa kuteuliwa .Aliteuliwa kuwa Balozi wa Canada 1982Balozi Marekani 1983 – 1984Akateuliwa waziri wa habari na utamaduni 1980 – 1982Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje tena 1984.  Anabaini kuwa kwa kweli Mwalimu aliipa familia mtihani mkubwa na hii hamahama, lakini familia chini ya mama Anna walikubali na kupokea yote kwa mikono miwili

Hakika Mwalimu ndiye shujaa mkuu wa simulizi hii.  Mheshimiwa Mkapa anamueleza Mwalimu kuwa:

Alikuwa jasiri, na kiongozi lazima awe jasiriAlikuwa msikivu, kamwe hakumkatiza mtu hata kama alikuwa anaeleza pumba tu.Alikuwa mtu wa msimamo, hakuyumbayumbaAlikuwa mpatanishi na mjenga madaraja kuwaunganisha mahasimu.Alikuwa communicater wa ajabuAlikuwa fundi wa kutafuta sehemu za makubaliano kati ya wanao tofautianaAlikuwa mtaalamu wa kutumia mawazo ya wengine kurutubisha na kuboresha ya kwakeAliupa umuhimu wa kipekee Umoja wa KitaifaHakupenda ukandamizaji ndio sababu hakupenda kuikalia Uganda baada ya vita 1980

Mheshimiwa Mkapa anasema “Mwalimu alikuwa mwalimu wangu kwa kila kitu”.

Alikuwa mwana demokrasia mtu aliyempenda kama mrithi wake mwaka 1985  alipokataliwa na wenzie katika kamati Kuu, Mwalimu alikubali.Alikuwa kiongozi mwenye maono – visionary, alingalia maslahi na mustakabali wa Taifa ndani na nje ya mipaka yake.

Wazazi wa Mheshimiwa Mkapa walifariki akiwa Waziri, wakiwa na furaha na faraja kwa mafanikio yake, ingawa hakuwa Padre, Daktari au Mwalimu kama baba yake mzazi mzee Matwani alivyotaka.

URAIS

Baada ya kutafakari na kushauriana na rafiki zake, Mheshimiwa Mkapa kwanza alimwambia mama Anna juu ya kugombea Urais.  Mama Anna alisita kidogo ila akakubali.  Pili alimueleza Mwalimu kwa barua kwani alikuwa Butiama, kisha akukutana nae ana kwa ana.  Alimpa mwalimu sababu kuu nne za uamuzi wake wa kutaka kugombea. 

Kwanza alitaka kurekebisha na kurejesha uhusiano chanya kati ya chama na serikali yake, na vyama vya ushirika ambao ulikuwa umefifia. Pili, alitaka kuhimarisha uhusiano na vyama vya wafanyakazi ambao walikuwa wanatishia kugoma kwa mara ya kwanza. Tatu, ilikuwa kurekebisha mahusiano mabaya na wahisani kuhusiana na kushamiri kwa rushwa. Nne, alitaka kurudisha uhusiano na mashirika ya fedha ya kimataifa ambao walikuwa wamekataa kuanzisha miradi mipya.Mwisho aliwapima hao waliokuwa wamechukua fomu akaona atajilaumu hapo baadae kama naye hata gombea.

Mwalimu alimshukuru, akamwambia hakuwaza kuwa nae angegombea, alikuwa anamfikiria mtu mwingine ambaye alikuwa anasita sita.  Akamwambia hatamzuia kama amefanya uamuzi huo.  Mwalimu aliwaomba watu kadhaa kumuunga mkono, Mwalimu alipenda hasa uwezo wake wa kufanya maamuzi, Mwalimu alishiriki katika kampeni ambapo Mheshimiwa Mkapa alisisitiza ilani, sio mambo binafsi.  Mdahalo wa wagombea wote ambao ulirushwa mubashara ndio ulimfundisha njia ya  ushindi.   Ulikuwa “Game Changer” anasema.

November 23, 1995 aliapishwa kuwa Rais.  Katika kuunda Baraza la Mawaziri, Mwalimu alikataa kujihusisha hakuwa muingiliaji – interventionist.  Mheshimiwa hakuwa mgombea wa mtu kwa hivyo hakuna aliyetegemea fadhila. 

Hali ya nchi ya uchumi ilikuwa mbaya sana lakini anasema sikuogopa, kiongozi lazima awe jasiri.   Alikumbana na uzembe, kutowajibika na rushwa.

Kazi kubwa - kwanza ilikuwa kuwashawishi wahisani kuwa mambo yatabadilika.   Nchi ilikuwa na madeni makubwa sana.  Deni letu lilikuwa dola bilioni saba, tulisamehewa bilioni tatu, hii ilikuwa hatua kubwa sana na ilimfurahisha Mwalimu ambaye alishaanza kuumwa.

Mheshimiwa aliamini tulihitaji kujiangalia upya na kujifikiria kimkakati upya namna tulivyo kuwa tunaendesha nchi.

Mheshimiwa anasema kuwa walio iona staili yake ya “Kusema na kuelekeza” kuwa ilijaa kiburi na majivuno ilikuwa lazima kuonyesha kuwa hata tetereka.

Matokeo yake ni kwamba mapato yaliongezeka karibu mara tatu kutoka dola 612,587 mwaka 1995 kufikia dola 1,796,862 miaka kumi baadae. Fedha za kigeni ziliongezeka kutoka uwezo wa kununua bidhaa za mwezi mmoja na nusu kufikia uwezo wa kununua bidhaa za miezi mitano na theluthi moja.  Riba za benki ilishuka kutoka asilimia 36% kufikia asilimia 15% mwaka 2005.

Ilianzishwa TRA kuimarisha ukusanyaji wa mapato Julai 1996.Ukaanzishwa mfumo wa VAT Julai 1998Public Service and Act pamoja na Public Procurement Regulatory Authority vilianzishwa 2001Commision for Human Rights and Good Governance ilianzishwa Julai 2001Prevention of Corruption Bureau nayo ilianzishwa, Mheshimiwa akaitwa Mr cleanRegulatory Agencies nyingine zilianzishwa nyingi ikiwa ni pamoja na Brela, EWURA, TCCRA,SUMATRA, Viwanja vya ndege,Maji safi na taka, TANROADS,na National Business Council kuhimarisha mahusiano na wafanya biashara.

Kati ya mageuzi tuliyofanya yaliyokuwa na utata sana ni kubinafsisha mashirika ya Umma, mageuzi/maboresho ya utumishi, na uuzaji wa nyumba za Serikali.

Kwa kweli mashirika ya Umma yalikuwa yanaendeshwa kwa hasara. Kuna wanaodai kuwa Mwalimu hakkupenda ubinafsishwaji na alisema hivyo hasa wakati wa mtangulizi wake.  Mheshimiwa Mkapa anabaini kuwa, lakini Mwalimu hakunisema ana sijui kwa nini, ukweli ni kwamba Mwalimu alikuwa pragmatist na aliona hali halisi.  Kwa bahati mbaya sikufuatilia utendaji wa mashirika Mheshimiwa Mkapa anaendelea  mashirika tuliyo yaabinafsisha kama ambaavyo nilivyofanya kwa Regulatory Agencies.  Pia kweli kuwa tulibinafsisha kwa watu wan je kuliko wazawa. 

Pamoja na ugumu na utata wa baadhi ya mageuzi kura zake katika uchaguzi wa mwaka 2000 ziliongezeka kwa asilimia 100%.  Hii kwake ilikuwa kuambiwa “Songa mbele, endelea”  Na niliendelea, anasema.

Mheshimiwa Mkapa anasimulia kuwa maono yake:  ni maisha ya hali ya juu, amani, utulivu na umoja, utawala bora,jamii iliyoelimika na uchumi shindani wenye uwezo wa kukua kiendelevu na mgawanyo shirikishi wa kipato.  Ili kuyapata hayo ikaanzishwa

Vision 2025, MKUKUTA, MKURABITA, Mini Tiger Plan 2020, TASAF.  Wengi katika Baraza la Mawaziri, kwenye Chama na Serikali hawakuviunga mkono.  Lakini sasa naiona TASAF kama “High Point” ya Urais wangu, anasema Mheshimiwa Mkapa.Bima ya TaifaMageuzi katika Elimu, DEDP na SEDPMradi wa maji ziwa Victoria,

Kuhusu mahusiano ya ndani na nje, Mheshimiwa Mkapa anabaini kuwa uhusiano katika ya Bara na Zanzibar ulikuwa mgumu na tete lakini alifanikwa kutatua matatizo.

Anasema alikuwa na wasiwasi pale Rais wa Zanzibar Salmin Amour alipotaka kubadilisha sheria na kutawala kipindi cha tatu.  Lakini baadae yeye na wafuasi wake wakaamua yaishe.

Zanzibar ilianza kupeperusha bendera yake. 

Vifo vya watu 22 huko Pemba Januari 2001 vilinishtua na kumhuzunisha sana.  Anasema “hili litaendelea kuwa doa katika Urais wangu ingawa sikuwepo lilipotokea”.

Anabaini kuwa wakati wa utawala wake, wanadiplomasia walionyesha upendeleo kwa vyama vya upinzani na kukutana nao mara kwa mara,  Pia wapo walioamini walistahili upendeleo kuliko wengine.

Kwa upande wa vyombo vya habari ilibidi azoee kukosolewa, kwani waliamini alikuwa dictator ingawa alikuwa anashikilia msimamo. Anabaini kuwa alihitaji kuuza sera zake, kwa hiyo akaanzisha utaratibu wa kulihutubia Taifa kila mwezi lakini mhimili mkuu wa kupokea na kutoa mawazo na habari ilikuwa Chama chake CCM na vikao vyake mbalimbali.

Mheshimiwa Mkapa anakiri kuwa, Kabla hajawa Rais, hakujua kuwa kazi moja wapo ya Rais ni kutoa pole. Moja wapo ya mapungufu yangu ni kwamba si mwepesi wa kuonyesha hisia zangu. Mrithi wangu Rais kikwete ni mzuri sana katika hili.  “Anasema Mheshimiwa Mkapa.

Mwaka 1996 mafuriko yalisababisha maafa makubwa katika Nchi.Kuzama kwa Mv bukoba kulistua na kuhuwisha sana majanga mengine mengi.Niliwahurumia wafungwa wote waliostahili kunyongwa mpaka kufa.

Anasema ingawa hakatai kukosolewa kisiasa au kisera, kukosolewa binafsi kuliumiza sana.  Kwa mfano madai kwamba alimpendelea Baba mkwe wa mwanae katika kubinafsisha mgodi wa makaa ya mawe wa kiwira yalimuumiza sana.

Pia madai kuwa aliwapendelea NET GROUP solutions ltd  wakati wa kubinafisha TANESCO kwa sababu ya shemeji yake kulimuumiza sana pia  jambo moja lilojitokeza baada ya muheshimiwa kumaliza muda wake ni la External payment account (EPA). Mheshimiwa anaeleza kuwa, anavyoelewa urais wake haukuwa wa kwanza kuruhusu ununuzi  wa madeni kama huo. Anasema kwanza alisita ila Gavana wa Benki Kuu Daud Bilali alimuelewesha na akasema watakao nunua hayo madeni walikuwa tayari kuchangia mfuko wa kampeni za uchaguzi wa CCM. Wahuni walitumia uaminifu wake kwa chama kumshawishi akubali. “Ninajisikia kuwa nilitumika na kusalitiwa. Na ukweli ni kwamba mimi binafsi sikufaidika na sikupata chochote”.  Anasema Mheshimiwa Mkapa.

Kuna kukosolewa kuhusu matumizi ya anwani ya Ikulu wakati mimi na mke wangu tulipochukua mkopo NBC kununua nyumba. Ukweli ni kwamba wakati ule tulikuwa tunaishi Ikulu, tulichukua mkopo kwa mashart ya kawaida ya biashara.  Kabla sijaondoka Ikulu, nilimaliza malipo ya mkopo huo na mshahara wangu wa mwisho na mafao yangu, tukapewa hati ya nyumba hiyo.  Anasema Mheshimiwa Mkapa.

Kulikuwa pia na swala la RADAR ambayo ilkuwa lazima kuinunua kuimarisha ulinzi lakini manunuzi yaligubikwa na udanganyifu na hatimaye hela zilizolipwa za ziada zilirudishwa kwa Serikali.

Anafikiri ni muhimu kutazama upya suala la umiliki wa uchumi ili watu wengi zaidi wahusike.  Kuendelea kushamiri kwa umiliki hasa wa viwanda na mashamba makubwa na makampuni ya Kiasia au Kihindi inaweza ikaleta wivu, na kuleta shida kubwa.  Ana wasiwasi na siku za mbeleni kwani umaskini uenda bega kwa bega na uvunjifu wa amani.  Lazima tujiulize kama tunajikita katika utulivu na amani.

Anamalizia kwa kutoa ushauri kwa viongozi wa wakati ujao (future).

Onyesha nia na bidii kwa majukumu upewayo.Uwe tayari kuwashirikisha wengine katika mawazo, mafanikio, matatizo na upimaji utekelezaji, consult more.Usifanye kazi kwa kukurupuka na kutotabirikaFuata  na tii sheria na taratibuUwe tayari kusikilizaMtafute mlezi (mentor) kama mimi nilivyokuwa na Mwalimu.

Katika sehemu anabainisha umuhimu wa mke wake mama Anna Mkapa.  Mapema kabisa katika ukurasa wa 83.  Mheshimiwa anampa saluti mama Anna kwamba yeye ndiye gundi iliyo shikilia familia. Anakiri kuwa yeye Mheshimiwa Siyo mtu rahisi kuishi naye na anamshukuru kwa kuwa mtu wa subira na uwezo mkubwa.  Amevumilia mengi wakati wa safari za mara kwa mara, kutokuwepo nyumbani mara nyingi na  ndiye alibeba mzigo wa kuwalea watoto wao wawili.

4.      KUSTAAFU

Sehemu ya tatu naya mwisho ya simulizi hii, ni maisha ya mheshimiwa baada ya kustaafu Urais.

Kwanza Mheshimiwa ametumika sana Kimataifa katika nyadhifa na Taasisi mbalimbali ingawa hapendi kusafiri, Taasisi hizo ni pamoja na

Club de Madrid, The African Wildlife Foundation, Investment Climate Facility for Africa, UN Iniative “Delivering as One”UNCTAD,  Panel of Environment Persons, UN Commission on the Legal Empowerment of the Poor, Mwenyekiti wa Seventh Centre tangu 2006, Trustee wa the Aghakhan University na The Mkapa Foundation

Kote huku amejichanganya na watu wenye akili nyingi.
Pili, amehusika sana katika upatanisho wa migogoro huko South Sudan, Congo Mashariki, na Kenya.

Mheshimiwa Mkapa, anamalizia simulizi hii kwa kugusia mambo kadhaa.

Kwanza, anaona Rais mstaafu anathaminiwa zaidi uongozi na uwezo wake Kimataifa zaidi kuliko nyumbani, jambo ambalo hata Mwalimu aliliona.  Mara nyingi huitwa kwenye hafla ambapo anakuwa kama Ua au pambo ukutani, lakini natakiwa kwenye kazi muhimu na nyeti za kitaifa.Pili, anaongelea umuhimu wa kuanzishwa kwa Baraza dogo kama sehemu ya  Bunge kupitia miswada iliyopitishwa na Bunge kabla ya utekelezaji.Tatu, anazungumzia kukosekana kwa itikadi na fikra pevu za kina juu ya mustakabali wa Taifa letu.  Inabainishwa kuwa tunahitaji ukombozi wa pili, Kisiasa, Kiuchumi, Kiutamaduni.  Tunahitaji kama Taifa, na mtu mmoja mmoja kuona aibu kuwa ombaomba.  Tunahitaji kujitegemea na kuthamini uendelevu (sustainability) wa maendeleo.Nne, anagusia mwendo wa goigoi katika kuimarisha Jumuia ya Afrika Mashariki (EA).  Sioni juhudi kubwa, naona siasa tu, watu wamepoteza picha kubwa – Big Picture. Tano, anagusia Uongozi.  Anabainisha kuwa uongozi bora ni kipaji au karama na sayansi pia.  Unazaliwa na karama hizo lakini unajifunza pia.   Nia yaani commitment ni muhimu.  Kiongozi bora ni lazima awe mfano wa kuigwa katika utendaji kazi wake, uaminifu na uadilifu.

Anatilia mkazo swala la ongezeko la vijana na kwamba hakuna sera, ya namna ya kushughulikia ongezeko kubwa la watu.  Anagusia pia suala la siasa halaiki yaani Populism na athali zake.

Kuhusu siasa na demokrasia, anabainisha kuwa CCM bado kinajiona kama bado kipo kwenye siasa za chama kimoja, Kunahitajika more political interaction na engagement.

Mheshimiwa anaendelea kuwa, uwepo wa vyama vingi vya siasa unadhoofisha demokrasia.  Watu wanaingia katika siasa kusaka manufaa ya kiuchumi sio kwa nia tukufu ya kuwatumikia watu na taifa.  Wafanya biashara wanasaka na kulinda maslahi, wasomi hutafuta kusafiri na posho, Wabunge wachache wanajali maslahi ya jimbo, wengi wanapenda safari za nje.  Hakuna interaction ya Wabunge kuhusu sera na utekelezaji wake.

Mwisho Mheshimiwa anajiuliza kama tutaweza kudumisha amani na umoja wetu kama Taifa.  Anagusia kuibuka hapa na pale viashiria vya ukabila, udini, na ukanda.

Mwisho kabisa Mheshimiwa Mkapa, anamalizia kwa kusema; Nitamuachia Mungu wangu na nyinyi kuamua ni tofauti gani nimeifanya humu duniani.

NMB Bank Supports Chato Football Stadium

$
0
0

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Ziwa Abraham Augustino (katikati) akimkabidhi matofali Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhandisi - Charles Kabeho (wa pili kutoka kulia) kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa Chato. Kutoka kulia ni mwenyekiti wa halmashauri hiyo - Batholomeo Manunga na wa kwanza kushoto ni Diwani wa kata ya muungano - Johnson Kilimokwanza, hafla hiyo ilifanyika katika ofisi ya za mkuu wa wilaya Chato hivi karibuni
****************************

NMB Bank PLC has dished out construction materials worth 30m/- in support of a football Stadium Construction in Chato District, Geita region.

The materials handed over includes 500 bags of cement and 13,335 bricks promising to look into the possibility of dishing out more support for the project in the future.

In a brief handover ceremony of the materials in Chato over the weekend, the Bank( Manager for the Lake Zone – Abraham Augustino said the support of the materials is the bank’s recognition of the importance of sports in the promotion of good health among the people particularly the youths.

“This is in line with the Bank annual commitment to the public through its Corporate and Social Investment program which has spent over 900m/- for different projects countrywide so far,” said Mr Augustino.

Receiving the items, the Chato District Commissioner – Charles Kabeho and Chato District Executive Director (DED) Eliud Mwaiteleke expressed gratitude to partners like NMB for coming forward to support sports development in the district.

DC Kabeho said the construction of the stadium was part of the initiatives targeting to boost sports development among other strategic programs in the district.

On his side DED Mwaiteleke hinted that the 3000 capacity stadium would lead to bigger sports facilities in the future remaining optimistic giants like Simba, Young Africans, Azam and others may one day use it when on transit for Premier league encounters.

“We are looking forward to hosting football giants like Simba and Young Africans who might decide to camp and train here as they travel for Premier league games. We ask for other supporters to join NMB and help us to complete the construction of this stadium,” he said.

GOBA KUNUFAIKA NA MRADI MKUBWA WA MAJI

$
0
0
 Maji yakititirika baada Mradi wa Maji kibululu Goba kukamilika..wananchi wa maeneo ya kibululu, Goba centre na Lasanza kunufaika na mradi huu.  Kukamilika kwa mradi huu kutanufaisha wananchi 5000 wa kata ya Goba na maeneo jirani

Hatua ilipofikia miradi ya Meli jijini Mwanza


INTRODUCING NEW VIDEO BY MADAM FLORA "WAKATI WAKE"

KILIMANJARO SAR YATOA MAFUNZO YA HUDUMA YA KWANZA KWA WAONGOZA WATALII ZAIDI YA 500.

$
0
0
Mtaalamu wa huduma ya kwanza kwa Magonjwa ya Mlima kutoka kampuni ya Utafutaji na Uokoaji ya Kilimanjaro SAR, Paul Gloy akionesha waongoza watalli namna ambavyo unaweza okoa maisha ya mtu aliyepata changamoto akiwa katika muinuko .
Mtaalamu wa Magonjwa ya Dharura na Uokoaji kutoka kampuni ya Kilimanjaro SAR,Dkt Hussein Abrodha akizungumza wakati akitoa mafunzo kwa waongoza watalii jijini Arusha. 
Baadhi ya Waongoza Watalii wakifuatilia mafunzo katika ukumbi wa mikutano wa hotel ya Rose Garden jijini Arusha .
 Mtaalamu wa Masoko wa Kampuni ya Utafutaji na uokoaji ya Kilimanjaro SAR ,akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Baadhi ya Washiriki 
Mtaalamu wa Huduma ya Kwanza wa Kampuni ya Kilimanjaro SAR ,Paul Gloy akiwalekeza waongoza Watalii namna ya kumhudumia mtu aliyepata changamoto ya kuvunjika Mguu.
Baada ya kupata mafunzo kutoka kwa Wataalamu wa Kampuni ya Utafutaji na Uokoaji ya Kilimanjaro ,Waongoza Watalii wakionesha namna ya kumhudumia mtu aliyepata changamoto ya kuvunjika uti wa mgongo .
Waongoza Watalii wakionesha namna ay kumuhudumia mtu aliyepatwa na Changamoto ya kuvunjika Mguu. 
Mtaalamu wa Magonjwa ya Dharura na Uokoaji kutoka Kilimanjaro SAR,Dkt Hussein Abrodha pamoja na Sarah Pascal wa kitengo cha simu za dharura (Waliosimama) wakitoa maelekezo kwa Waongoza watalii namna ya kurejesha uhai kwa mtu aliypatwa na tatizo la upumuaji .
Paul Gloy akiwaonesha Waongoza Watalii namna ya kumbeba mtu aliyepatwa na tatizo la kuvunjika Uti wa Mgongo . 
Sarah Pascal wa kituo cha MAwasiliano ya simu za Dharura katika kampuni ya Kilimanjaro SAR ,akitoa maelekezo ya namna ya kutumia kitabu kujaza taarifa za mtu aliefikwa na matatizo wakati wa kupanda Mlima.
 Afisa Uhusiano na Masoko wa Kampuni ay Utafutaji na Uokoaji ya Kilimanjaro SAR ,Abdulrahim Damian akitoa maelezo kwa washiriki wa mafunzo hayo kuhusu kampuni ya Kilimanjaro SAR.


Na Dixon Busagaga ,Arusha .



KATIKA kuongeza thamani ya Utalii wa milimani ,waongoza watalii zaidi ya 500 wa mikoa ya Arusha na Kilimanjaro wameanza kupatiwa mafunzo ya namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa wageni pindi wapatapo changamoto wakati wa kupanda.



Mafunzo hayo yanayofanyika kwa wiki mbili kwa kuanza na jiji la Arusha yanatolewa bila malipo na kampuni ya Utafutaji na Uokoaji ya Kilimanjaro SAR ya mkoani Kilimanjaro, mafunzo ambayo hutolewa kipindi cha mapumziko ya biashara ya utalii.



Mtaalamu wa Masoko wa kampuuni hiyo ,William Mbogo alisema Kilimanjaro SAR kwa miaka miwili ya mwanzo imeanza kutoa mafunzo kwa waongoza watalii wa milimani peke yake na kwamba baadae watafanya kwa waongoza watalii wa Safari za hifadhini.



“Kwenye mafunzo yetu haya tumeyagawanya katika sehemu kuu tatu ,sehemu ya kwanza tuna wataalamu wanaozungumzia namna ya kumpatia mtu huduma ya kwanza pale inapotokea mgeni amepata changamoto ,hatuishii hapo tu wanaingia kufanya pia kwa vitendo.”alisema Mbogo.



Alisema sehemu ya pili ya mafunzo hayo washiriki wanafundishwa namna ya kutambua aina mbalimbali ya magonjwa yatokanayo na mlima na pia namna ya kumrejeshea uhai mtu ambaye amepatwa na tatizo la upumuaji kwa kitaalamu wanaita CPR .



Mbogo alisema suala la usalama ni kivutio kikubwa cha wageni kwa kampuni zinazofanya shughuli za utalii huku usalama toa wito kwa kampuni hizo kuendelea kujenga imani na Kilimanjaro SAR ili kujiongezea thamani katika biashara ya utalii .



“Sasa hivi kampuni za utalii  zina ujasili wa kuuza mlima Kilimanjaro na Mlima Meru wakijua kabisa kwamba kuna huduma ya haraka tena ya uhakika kwa kutumia helkopta ambayo atapata mgeni wake na kampuni ya bima ya mgeni ndio itahusika kwenye malipo”alisema Mbogo .



Naye Afisa Uhusiano na Masoko wa kampuni ya Kilimanjaro SAR ,Abdulrahim Damian alisema kwa sasa mafunzo yanatolewa kwa waongoza watalii pekee kwa sababu wao ndio viongozi wa kundi linaloshiriki katika kuwapandisha wageni .



“Tunatoa mafunzo bure kwa hawa waongoza watalii ambao tunaamini ndio viongozi ,tunawapa maarifa waweze kuhudumia wageni lakini pia na watu wote ambao wanaongozana nao katika safari ya kupanda mlimani “ alisema Damian.



“Hii tunafanya kwa sababu mbili, ya kwanza tunashiriki katika uboreshaji wa huduma za kitalii hapa nchini  kwa kushirikiana na wadu wote wa utalii pamoja na serikali ili kuvutia wageni pindi wanapokuja nchini wasiwe na hofu juu ya usalama wao.”aliongeza Damian.



Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo , Waongoza watalii ,Jonas Luta ,Joyce Jacob na Hussein Paul wameishukuru Kampuni ya Kilimanjaro SAR kwa kuanzisha utaratibu wa kuwapa mafunzo hayo ambayo wameeleza hawakuwahi kuyapata hapo awali .



Mwisho


WAKAZI WAISHIO KANDO YA MTO NGERENGERE WAHAMA MAKAZI YAO KWA MUDA MANISPAA YA MOROGORO

$
0
0

Baadhi ya wakazi wa mtaa wa Yespa Manispaa ya Morogoro wakiwa nje ya nyumba zilizozingirwa na maji.

……………………………..


NA FARIDA SAIDY, MOROGORO


Baadhi ya kaya zilizo kandokando ya Mto Ngerengere Mtaa wa Yespa Manispaa ya Morogoro zimezingirwa na maji na kusababisha wakazi wa mtaa huu kuhama  kwa muda, ambapo imeelezwa hali hiyo imesababishwa na Maji kupoteza mwelekeo baada ya sehemu ya mto kuzibwa katika ujenzi wa Reli ya kisasa.


Wakiongea kwa nyakati tofauti wakazi hao wamesema kuwa hali hiyo imesababishwa na maji kupoteza mwelekeo kufuatia ujenzi wa miundombinu ya reli ya kisasa ambao imesababisha maji kujaa katika makazi ya watu.

Aidha wakazi hao wamesema kuwa  hali hiyo ya maji kuingia kwenye maeneo ya makazi imetajwa kusababisha hasara, ambapo licha ya baadhi ya watu kulazimika kuyahama makazi yao kwa muda, pia baadhi ya huduma zimesimama ikiwemo ibada.


Wakazi hawa walio pembezoni mwa mto Ngerengere wamesema kuwa wengi wao wameishi kwa muda mrefu katika maeneo hayo lakini  wajawahi kukutana na changamoto ya kuzingirwa na maji hivyo swala hilo kwao wanaliona ni tatizo hivyo wanaiomba mamlaka husika kulichulia hatua.

Pamoja na kaya zilizo zingirwa na maji kuwa pembezoni mwa mto Ngerengere, Malalamiko ya wakazi hao ni ujenzi wa Reli ya kisasa, wakidai sehemu kubwa ya mto imezibwa ambapo kufuatia mvua zinazo endelea kunyesha mto huo umefurika na maji kusambaa baada ya kukosa mwelekeo.

SPIKA AFUNGUA MPANGO KAZI WA CHAMA CHA WABUNGE RAFIKI WA MAZINGIRA

$
0
0
  Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akifungua Mpango Kazi wa Chama cha Wabunge Rafiki wa Mazingira (TAPAFE), katika mkutano uliofanyika Ukumbi wa Msekwa Jijini Dodoma. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa chama hicho Mhe. Jitu Soni na Florentina Julius kutoka Jumuiko la Maliasili Tanzania.
Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge Rafiki wa Mazingira (TAPAFE), Mhe. Jitu Soni akitoa maelezo ya utanguzili kuhusiana na Mpango Kazi wa chama hicho kwa Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai kabla ya kuuzindua rasmi mpango huo katika mkutano uliofanyika Ukumbi wa Msekwa Jijini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akifuatilia uwasilishwaji wa mada katika Mkutano wa Chama cha Wabunge Rafiki wa Mazingira (TAPAFE), katika mkutano uliofanyika Ukumbi wa Msekwa Jijini Dodoma. Pembeni yake ni Mwenyekiti wa chama hicho Mhe. Jitu Soni.PICHA NA OFISI YA BUNGE

MBUNGE CCM AOMBA RADHI KWA KUSEMA WATUMISHI WA ATCL HAWANA MVUTO

$
0
0
MBUNGE wa Kigoma Kusini (CCM), Husna Mwilima, ameomba radhi kufuatia kauli yake ya kudai idadi kubwa ya watumishi wa kike katika Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) hawana mvuto, amedai kuwa lengo la kauli yake ilikuwa ni kushinikiza maboresho kwenye shirika hilo.

Mwilima ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma, leo Novemba 14, 2019, wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwenda kwa Wizara ya TAMISEMI, ambapo kabla ya kuuliza swali lake aliomba radhi kwa Watanzania.

"Nilitoa ile kauli lengo lilikuwa ni kuboresha Shirika letu la Ndege la ATCL, kwa kuwa ile kauli yangu iliwaboa sana Watanzania hasa wanawake nitumie nafasi hii kuomba radhi Watanzania hasa wanawake wenzangu", amesema Mbunge Mwilima

Mara baada ya kutoa kauli hiyo, Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai alimpongeza na kusema msamaha wake umepokelewa.

Kauli hiyo aliitoa Novemba 7, 2019 wakati akichangia kwenye mpango wa maendeleo ya Taifa Bungeni jijini Dodoma, Mbunge Mwilima alidai kuwa watumishi wanawake kwenye Shirika la Ndege la ATCL, hawana mvuto na kupelekea kutokuwa na hamasa kwa wateja.
Chanzo - EATV

MUONEKANO WA MANDHARI KATI KATI YA JIJI LA DAR.

$
0
0
Muonekano wa Mandhari  kati kati ya jiji la Dar leo asubuhi kama ilivyonaswa na mpiga picha wa Globu ya Jamii alipokuwa akikatiza kwenye moja ya jengo refu lililopo katikati ya jiji hilo.

CRDB Bank Becomes the First Bank in East & Central Africa’s to Receive the United Nations Green Climate Fund (GCF) Accreditation

$
0
0
SONGDO, South Korea Wednesday, Nov 13, 2019 -  Tanzania’s largest commercial bank, CRDB Bank Plc,  has today been accredited by the United Nations Green Climate Fund as the financial intermediary for the implementation of green financing in the United Republic of Tanzania.  

The accreditation was announced Wednesday during the 24th Green Climate Fund (GCF) Board Meeting, in Songdo, South Korea. This followed an extensive due-diligence assessment, conducted by GCF to ascertain the Bank’s preparedness in managing climate change programmes. 
Group CEO & Manging Director Abdulmajid Nsekela says the endorsement marks an important milestone in the Bank’s history and that of the Country. 

 “We are proud of this achievement and excited because it gives us a unique opportunity to make a huge impact in Tanzania,” quips Nsekela.  

GCF Director of Private Sector Facility, Ayaan Adam says CRDB Bank’s accreditation is highly merited, owing to the Bank’s portfolio strength and extensive client base within Tanzania and the Republic of Burundi.
“CRDB Bank is a very strong bank because it has a wide reach and presence, extending to two countries (and will hopefully go beyond). This means the bank is aware of the realities of what is happening in the country, ” says Adam. 
CRDB Bank becomes the 3rd commercial bank in Africa to obtain this accreditation, after Ecobank Ghana and Attijariwafa Bank of Morocco. Accredited entities carryout a range of activities that usually include the development of funding proposals and the management and monitoring of projects and programmes. Multiple projects  can be funded simultaneously.

“We want to take an active role in supporting development programs in our country. We are particularly keen to support the government initiatives in energy, transport and infrastructure, industrialisation, health and wellness, food security, safe cities and environment,” Nsekela explains.  

“We are ready to work with GCF to support both public and private entities in implementing sustainable development projects, through provision of affordable loans, guarantees and equity. With this endorsement, we are confident that CRDB Bank will be able to finance different vital green projects to the tune up to USD 250 million per single project funding proposal. This means that CRDB Bank will be able to finance multiple large scale projects with high impact to the social and economic development of Tanzania,” the CEO says.

Nsekela further says access to the Fund will empower the Bank to support the government of Tanzania sustainable development initiatives in the areas of renewable energy, mass mobility through rapid bus transit systems and railways, provide modern and sustainable housing estates in cities and  afforestation among others.  

The Chief Executive is upbeat that the implementation of sustainable initiatives will be an important step for the Bank’s Corprate Social Investment (CSI) approach and will go a long way in strengthening its position as a leading innovative bank in the region.  

CRDB Bank appreciates the continued support gained from the government of Tanzania and particularly nominating CRDB Bank for the accreditation and cooperation extended to the Bank by GCF to ensure that we sail smoothly to a successful accredition. The Bank will work in partnership with GCF and the government for the social and economic development of Tanzanians.

KITABU CHA HISTORIA YA MAISHA YA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA CHAAMSHA UPYA ARI YA KUJISOMEA

$
0
0
 Keki ya mfano ya Kitabu cha Mhe. Benjamin William Mkapa
 Msanii maarufu nchini Muzu Suleimanji akiwa na wadau wakiwa na nakala ya kitabu hicho.

 Profesa Saida Othman (kulia) akiwa na wadau wengine na nakala zao
 Profesa Semboje akielezea kitabu hicho kwa Bw. Ali Mufuruki na Mkurugenzi Mtendaji wa Standard Chartered Bw. Sanjay Rughan
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akinunua nakala yake.

Na Sultani Kipingo

Ujio wa Kitabu cha historia ya maisha ya Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa kumeelezwa kuwa ni mojawapo ya chachu za ajabu kupata kutokea hivi karibuni katika kuwahamasisha Watanzania kurudia upya hamu ya kujisomea vitabu ambayo inazidi kupotea kutokana na kile klnachoaminika kuwa ni utandawazi.

Uchunguzi uliofanyika mara baada ya uzinduzi wa kitabu hicho Novemba 12, 2019 jijini Dar es salaam umebaini kwamba wengi wanakisaka kitabu hicho kwa udi na uvumba ili kukisoma, kila mtu akiwa na sababu zake.

Wengine wanakitafuta ili kupata kwa undani mwandani wa “Mzee wa Ukweli na Uwazi”, wakati wengine wakitaka kuona endapo kweli “Che Nkapa” kafukua makaburi, wakati wengine wengi Zaidi wakijikuta wana hamu tu ya kumsikiliza kiongozi aliyevutiwa na usemi wa “Mtaji wa Maskini ni Nguvu zake mwenyewe.

“Tulim-miss Mzee wetu ndio maana tuna hamu ya kusoma maandiko yake” anasema Mariam Kindiko, mfanyabishara wa nguo na urembo maeneo ya Kijitonyama. “Wengi tuliobahatika kuwepo na akili zetu wakati wa enzi zake tunamkumbuka kwa jinsi alivyorejesha ghafla heshima ya mtu kufanya kazi”, anaongezea huku akicheka.

Watu wapatao sita hivi katika maeneo mbalimbali wanapita mle mle kwa Bi Mariam, na wengine wanaenda mbali Zaidi kuunga mkono ushauri alioutoa Rais Dkt. John Pombe Magufuli wa kutaka kitabu hicho cha Kiingereza kitafsiliwe kwa lugha ya Kiswahili ili wengi wafaidike nacho.

“Tunajua Che Nkapa alitaka kuwasiliana moja kwa moja na wasomi wenzie lakini sie walalahoi tusiojua Kiinglishi tunamwomba atufikirie kututafsiria kama alivyosema (Rais Magufuli) Ngosha” anasema Twalib Zakaria wa Kigamboni.

Uchunguzi huo umeonekwa kwamba ni kweli kwamba kitabu cha Mzee Mkapa kimezua mijadala kila kona ya nchi, ikiwemo kwa wanasiasa ambao kila lizukapo jambo jipya baadhi yao huwa wa kwanza kudandia treni kwa mbele, lakini si uwongo kwamba ghlafa bin vuuuup watu wamehamasika na  kutaka kukisoma hicho kitabu.

“Watanzania wamepata ari ya kusoma vitabu baada ya kukiona kitabu cha Mzee Mkapa na kumaizi kwamba mitandao na magazeti havina ujazo wa kutosha kikidhi kiu yao ya kujua mambo”,anasema mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam aliyeomba jina lihifadhiwe.

Mhadhiri huyo anasema kinadharia na kivitendo kiu ya kujua vitu ama mambo hufanya watu wategemee  ama wapendelee kilichopo mbele yao (mitandao, magazeti ya kawaida na udaku na soga za kijiweni), jambo ambalo limedhoofisha utamaduni wa kusoma vitabu.

“Kwa sehemu kubwa ni kwamba ukosefu wa vitabu vya kusisimua na vyenye mafundisho kumesababisha kufa ama kufifia kwa utamaduni wa kujisomea na ndio maana nasema kitabu cha Mheshimiwa Mkapa ni mfano hai kwamba kusoma kunaweza kuhamasishwa kwa kuwepo vitabu vyenye maudhui ya kuvutia”, amesema mhadhiri huyo.

Wahojiwa wengi pia wameshukuru kusikia kwamba Rais wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi na Rais wa Aamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete nao wako mbioni kuachia vitabu vya historia za maisha yao.

“Mbali na kuandika historia kwa ukamilifu pia hatua ya watu mashuhuri kuandika biography zao kunasaidia kuweka rekodi na kumbukumbu sawa kwani mambo muhimu hayo Watanzania tumeyapa kisogo sana” anasema msanii Nathan Mpangala.

Mwanamuziki mkongwe John Kitime anakubaliana na Mpangala, akiongezea kwamba iko haja kila mtu mashuhuri afanye kuandika historia ya maisha yake na kwa jinsi walivyo wengi utashangaa jinsi kila mtu atakavyopenda kusoma vitabu”, anaongezea.

Akielezea kitabu hicho, Profesa Rwekaza Mukandala anasema Mtoto Benjamin William Mkapa, alifundishwa kupika chakula na mama mzazi Stephania akiwa mdogo. Alipokwenda shule hapo kijijini Lupaso, Ndanda na hatimaye St. Francis Pugu na Makerere, alifundishwa kupika, kufinyanga, kubuni na kuchambua mawazo na kuyaweka sawa kama msomi mbunifu na mwandishi. Kitabu hiki ni zao la mpishi wa mawazo mahiri aliyebobea.  
"Ni kitabu cha kurasa mia tatu na kumi na tisa, katika sura ya kumi na sita.   Kuna utangulizi ulioandikwa na Mheshimiwa Joaquim Chissano, Rais mstaafu wa Msumbiji, Pia kuna picha nyinge nzuri, na viambatisho viwili.  Mchapaji Mkuki na Nyota wamefanya kazi nzuri sana, sikubaini kosa hata moja", anasema msomi huyo aliyepata kuwa Makama Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Profesa Mukandala anaweka bayana kwamba kitabu hicho kina sehemu kuu tatu. Kwanza tunapewa vionjo vitamu tukielezwa kuzaliwa kwake, kukua na kwenda shule. Hii ilikuwa matayarisho ya kufikia nia au azma yake ya maisha. 
Kisha tunaletewa mlo wenyewe (main course) uliosheheni kumbukumbu  na ngano za huyo kijana sasa mtu mzima akiwa kazini, mpaka akaukwaa urais wa Tanzania. Mwisho tunaelezwa kwa ufupi maisha yake baada ya kumaliza ngwe yake ya miaka kumi ya urais.




MWENYEKITI CABCT AWAASA WANAFUNZI KUSOMA KWA BIDII KUFIKIA MAENDELEO ENDELEVU

$
0
0
 Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara wa China nchini Tanzania (CABCT) akitoa cheti kwa mmoja ya wanafunzi waliomaliza elimu ya darasa la saba katika Shule ya Msingi Magoro iliyopo wilayani Rufiji.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara wa China nchini Tanzania (CABCT) Xian Ding akizungumza wakati wa mahafali ya 55 ya darasa la saba ya Shule ya Msingi Mahoro iliyopo Rufiji mkoani Pwani.Ding alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo.

Na Mwandishi Wetu
MWENYEKITI wa Umoja wa Wafanyabiashara wa China nchini Tanzania 
(CABCT)Xian Ding amesema ipo haja kwa wanafunzi kuanzia elimu ya awali hadi  vyuo vikuu nchini kusoma kwa bidii ili kufikia maendeleo endelevu ya kiuchumi  huku wakilenga kuanzisha biashara kubwa, kuajiriwa au kubuni teknolojia za kisasa katika kuendeleza nchi. 

Ameyasema hayo katika mahafali ya 55 ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi Mohoro iliyopo Rufiji mkoani Pwani alipokuwa mgeni rasmi ambapo pia ameipongeza Serikali kwa kuweka mazingira mazuri ya kufundishia katika shule hiyo.

 “Naipongeza Serikali kwa kuweka mazingira mazuri ya elimu kwenye shule 
hii na shule zingine, sisi wachina tutaendelea kusaidia kwenye jambo hili la 
elimu” alisema Bw. Ding.

Wakati anatoa hotuba yake Ding amewashauri wahitimu kuzingatia elimu na kuwaeleza bayana kuwa wazazi wamewekeza kwao. Aidha ameeleza ili uchumi uweze kukua mahali popote pale kunahitajika watu wabunifu waliobobea kwenye fani mbalimbali hatua inayotokana na kusoma kwa bidii na kujituma katika elimu. 

Pia Mwenyekiti huyo amewahamasiaha wahitimu mmoja mmoja kuzingatia elimu na kuwaambia kuwa hapo baadae utakapohitaji kuwa Daktari lazima usome, ukitaka kuwa Rubani lazima usome, ukitaka kuwa Waziri lazima usome, ukitaka kuwa Mbunge lazima usome, ukitaka kuwa Injinia lazima usome, ukitaka kuwa  Mwalimu lazima usome. 

“Nawaomba sana wanafunzi msome kwa bidii ili mje kujenga Taifa letu zuri la  Tanzania sambamba na kusimamia sera ya kukuza uchumi wa viwanda,” 
amesema Ding.

Ding ambaye pia ni Mkurugenzi wa kampuni ya Huatan Invesment Group 
inayomiliki miradi ya uwekezaji nchini ikiwamo kiwanda cha kutengeneza chakula  cha mifugo Pugu na kiwanda cha kuchakata betri zilizokwisha muda wake Rufiji.  

Katika kutekeleza Sera ya kushirikiana na jamii inayomzunguka, kwenye 
mahafali hayo, Mwenyekiti huyo ametoa msaada wa viatu kwa wanafunzi 
wanaobaki wa darasa la tatu na nne na fedha taslim kama zawadi kwa wahitimu waliofanya vizuri katika mitihani yao  ili kuwapa motisha wanafunzi wanaoendelea na masomo.

Katika hatua ya kusaidia maendeleo ya elimu Wilayani Rufiji, Mwenyenkiti huyo ametoa fedha kwa ajili ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Nyamwage waliokaa kambini kujisomea. 

Hata hivyo imekuwa ni kawaida kwa Mwenyekiti huyo wa CABCT kuunga mkono masuala mbalimbali ya jamii yanayojitokeza katika maeneo wanayofanyia  biashara na uwekezaji wao ikiwamo (usafiri, afya na elimu).  Jambo hili ni zuri na linapaswa kuungwa mkono na wadau wote wa maendeleo.

DC CHONGOLO AWAFUNDA VIJANA WAJASIRIAMALI

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongo amewataka vijana kutumia fursa inayotolewa na serikali kupitia halmashauri kupata mikopo isiyokuwa na riba ili waweze kujikwamua kiuchumi.

9Mhe. Chongolo alisema kuwa Manispaa ya Kinondoni inafungu la bajeti kwa ajili ya kutoa mikopo kwa Vijana, wakina mama na watu wenye ulemavu kwa lengo la kuwasaidia kujikwamua katika umasikini hivyo vijana wanapaswa kutumia nafasi hizo wanazozipata kwani itawawezesha kukuza mitaji yao na hivyo kufikia lengo la kuwa na viwanda huku akitolea mfano wa mfanyabiashara mkubwa Marehemu Dk. Reginal Mengi ambaye alifanikiwa kuwa na viwanda kupitia ujasiriamali.

Alifafanua kuwa iwapo watatumia vizuri mafunzo hayo yataleta tija katika kukuza uchumi wa ndani na kwamba serikali kupitia halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni itasimamia kupata mikopo hiyo na hivyo kuwawezesha kupata mashine pamoja na eneo la kujenga kiwanda chakutengeneza bidhaa za ngozi.

“ Nawapongeza sana idara husika ambayo imeandaa haya mafunzo sambamba na maonyesho ya bidhaa za ngozi, vijana mliopo hapa ,tumieni hii fursa mliyoipata, hakuna mafanikio ya siku moja, wote waliofanikiwa walianza kama nyie hapa” alisema Mhe. Chongolo.

“ Tunahitaji watu ambao watakuwa na nia ya kweli ya kujikwamua kiuchumi, inawezekana kuzalisha bidhaa za ngozi kwakuwa Tanzania tunaongoza kwakuwa na mifugo, ukiangalia Dar es Salaam ndio inaongoza kwa kula nyama,kwahiyo tunazana za kutengenezea bidhaa zetu” alifafanua.

Kwaupande wake , Meneja ukuzaji Bidhaa kutoka Tan Tredi , Masha Husein alisema kuwa wataendelea kushirikiana na manispaa ya Kinondoni katika kuwaelimisha wajasiriamali namna ya kufanya biashara kwenye maonesho kwani hiyo imekuwa ni changamoto kubwa kwao.

Alifafanua kuwa, wajasiriamali wengi hawana uelewa wa kutosha kuhusiana na namna ya kushiriki kwenye maonesho mbalimbali wanapopata nafasi jambo ambalo kama Tan Tredi imeliona na hivyo kusisitiza kuwa watahakikisha wanatoa elimu hiyo ili waweze kunufaika.

Naye Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi Dk. Patricia Henjewele alimpongeza Mhe. Chongolo kwakujali vijana na kusema kuwa katika maonesho ya nane nane waliona umuhimu wakukutana na wajasiriamali hao na hivyo kuandaa semina hiyo iliyoambatana na maonesho.

Dk. Henjewele aliwapongeza Tan Tredi kwakuwezesha maonesho hayo na hivyo kuahidi kuendeleza ushirikiano zaidi katika kutoa elimu kwa wajasiriamali hao.
 Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi, wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni , Dk. Patricia Henjewele akizungumza na washiriki vijana wajasiriamali wa bidhaa za ngozi wakati wa semina iliyofanyika jana katika ukumbi wa Manispaa. Kushoto ni mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Daniel Chongolo.
 Meneja ukuzaji bidhaa wa Tan Tred, Masha Hussein, akizungumza na vijana wajasiriamali jana wakati wa uzinduzi wa semina ya vijana wajasiriamali wa bidhaa za ngozi iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo akifuatilia kwa makini majadiliano ya semina ya vijana wajasiriamali wa bidhaa za ngozi kabla ya kufua kwa semina hiyo iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano. Kulia ni Mkuu wa Idara ya mifugo na Uvuvi Dk. Patricia Henjewele.
 Mmoja wa maafisa  Mifugo wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Deusdedit Nestory kutoka Idara ya Mifugo na Uvuvi akifafanua jambo kwa vijana wajasiria mali wa bidhaa za ngozi wakati wa semina iliyofanyika jana.
Mshiriki wa semina hiyo kijana anayejihusisha na utengenezaji wabidhaa za ngozi za kampuni ya asili asilia Viola Munishi akichangia mada iliyokuwa ikijadiliwa katika semina hiyo.

MTANDAO WA UTAFITI WA KISAYANSI LAZIMA UANZIE KATIKA VYUO VIKUU

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya utafiti ya taifa nchini Afrika Kusini, Dkt. Molapo Qhobela kulia akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano uliojumuisha wanasayansi wa nchi 15 za kusini mwa jangwa la Sahara.Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia , Amos Nungu.

Dkt. Qhobela amesema kuwa tafiti zitakazofanywa ziwe za afya, kilimo pamoja na chakula zote ziwe kwa kushirikiana ili kuleta matokeo mazuri kwa kujifunza kwa kila nchi ambayo hufanya utafiti kwa kubadilishana uzoefu katika utafiti.

Amesema ili utafiti ufanikiwe nilazima kuwe na ushirikiano na kubadilishana mawazo kati ya nchi zinazofanya utafiti za kisayansi.

Dkt. Qhobela nchi za kisayansi za Afrika zisifikiri kuwa hazina vitu vizuri vya kufanyia utafiti iwe katika Afya, Chakula, Kilimo na hata Mazingira.

"Sisi kama Jumuia Tunafanya kazi kwa karibu ili kuweka Sayansi iwe wazi  kwani Sayansi ya Afrika inategemea utafiti wa mwenzie". Amesema Dkt. Qhobela.
 Dkt. Merody Mentz, Coetzee akizungumza a waandishi wa habari jijini Dar es Salaam katika mkutano wa Sayansi, Teknolojia na ubunifu. amesema kuwa lazima mtandao wa utafiti kuanzia kuboreshwa katika vyuo vikuu mbalimbali katika nchi za Kusini mwa jangwa la Sahara ili kuweza kuwa na watafiti wengi ambao ni vijana.

Amesema changamoto kubwa ni kutokushirikia kwa watafiti endapo utafiti unafanywa. Ameshauri kuwa na ushirikiana kati ya watafiti wa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara.
Mwakilishi shirika la Canada linalofadhili Utafiti katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, Dkt.Ellie Osir akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu unaoendelea katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Dkt. Osir amesema kuwa Suala la kisayansi liwekewe kipaumbele  na ameshauri iwe ajenda ya nchi za Afrika katika kufanya utafiti wa Kisayansi, Teknolojia na ubunifu.

Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia, Dkt. Amos Nungu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu unaoendelea katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Dkt. Nungu amesema kuwa mijadala inayoendeshwa wabunifu kutoka katika Jangwa la Sahara wanachangia na mwisho wa siku kutakuwa na matokeo mazuri ya katika kubadilishana mawazo ya kiutafiti na ubunifu.

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba ameipongeza TCRA katika Kusogeza huduma kwa Wananchi

$
0
0
 MKuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman akikabidhiwa kitabu cha Muongozo wa Mawasiliano na Mkuu  wa Kanda ya Zanzibar wa  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)  Esuphatie Masinga (katikati) wakati wa Kampeni ya a Mnada kwa Mnada wa TCRA katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.K kushoto ni Mkuu wa Kanda ya Mashariki TCRA Mhandisi Lawi Odiero na watatu kutoka kushoto Afisa Habari Mwandamizi wa TCRA Makao Makuu Mabel Masasi.
 Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman akiweka alama ya vidole wa ajili ya usajili laini ya simu katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.
 Afisa Habari Mwandamizi wa TCRA Makao Makuu Mabel Masasi akimpa maelezo mwananchi wakati wa Kampeni ya Mnada kwa Mnada Katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.
 Afisa Habari wa TCRA Judith Shao akitoa maelezo kuhusiana vitabu vya Muongozo wa Mawasiliano Katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.
Wananchi wakipata maelezo kuhusiana na usajili kwa alama za vidole katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.

MKUU wa Mkoa  wa Kusini  Pemba Hemed Suleiman ameipongeza  Mamlaka ya  Mawasiliano Tanzania  kwa kuandaa kampeni ya Mnada kwa Mnada kwa kuwa inasaidia  sana wananchi  kupata  huduma  kirahisi

Mkuu huyo  ameyasema hayo wakati wa Kampeni ya Mnada kwa Mnada  wa TCRA katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba  amesema kwa kusogeza huduma zote  muhimu  pamoja  inawarahisishia wananchi kupata huduma jambo  ambalo  linamanufaa  kwa wananchi  na serikali kwa ujumla.

 Hemed Amewataka  wananchi kutumia vema  fursa ya kampeni huyo  inapofika katika  maeneo yao.

Kampeni ya Mnada kwa Mnada Pemba  katika utoaji wa Elimu ya Usajili wa laini kwa kutumia alama za vidole. 

Wakazi wa wilaya ya Pemba na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi katika kampeni  ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu Mitandaoni  na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Idara ya Uhamiaji  kwa ajili  ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa kuweka alama za vidole kwa laini za simu.

Kampeni tangu imeanzishwa imekwenda katika Mikoa 17 na Zanzibar lengo kuu ni nchi nzima kufikiwa na Kampeni hiyo.

 Mkuu wa TCRA Zanzibar Esuphatie Masinga amesema ni fursa kwa wananchi wa Pemba  kufika katika Viwanja vya Gombani  kwa ajili ya kusajili kwa alama za vidole pamoja na kujiandikisha kupata usajili wa vitambulisho vya Taifa  kutokana na kuwa na mnyororo wadau wa  mawasiliano. 

Masung amesema kuwa  Mnada kwa Mnada TCRA ilianzisha ili kutoa fursa ya Wananchi kuhudumiwa hasa wakati huu usajili wa laini za simu kwa alama za vidole pamoja Huduma zingine za mawasiliano..

Aidha amesema Kampeni hiyo ni kuimarisha ulinzi katika  huduma  za simu pamoja kufanya mawasiliano kuwa salama katika nchi.

Mkuu huyo amesema  kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano nchini.

Masinga  amesema kuwa wananchi wasio kuwa na Vitambulisho vya NIDA wahakikishe  wanapata katika usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole na huduma nyinginezo za Mawasiliano hayo.

Hata hivyo amesema kuwa
 kuna watu wengine wanatumia mawasiliano ya simu bila kujua ambapo Jeshi Polisi lipo katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada ili kutoa elimu kuhusiana  makosa ya jinai ya matumizi ya simu.

Aidha amesema Kampeni hiyo ni endelevu katika kuwafikia ikiwa kuhakikisha kila mwananchi anajisajili laini yake kwa alama za vidole kwa kutumia kitambulisho cha taifa.
TCRA iko kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi ili watumie Mawasiliano kwa usalama kutokana na elimu wanayoipata katika Kampeni mbalimbali.

Hata hivyo amesema kuwa wananchi wajitokeze katika kujisajili kwa alama za vidole kabla ya Desemba 31.

"TCRA  tunawafikia katika wananchi katika utoaji wa elimu za utumiaji wa bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma hiyo" amesema Masinga.

Nae Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa TCRA Mabel Masasi amesema kuwa mwitikio umekuwa mkubwa kwa Wananchi kutaka vitambulisho kwa ajili ya kusajili laini za simu kwa alama za vidole na kupata mwamko wa kutumia simu katika maendeleo.

Masasi amesema kuwa Wananchi wa watumie Kampeni ya Mnada kwa Mnada ya TCRA kupata elimu na baada ya kuisha Mnada sehemu husika waende katika mamlaka husika kupata vitambulisho.
Viewing all 110016 articles
Browse latest View live


Latest Images