Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live

KATIBU WA BUNGE AKUTANA NA MTAALAM MSHAURI KUTOKA CPA MAKAO MAKUU BUNGENI JIJINI DODOMA

$
0
0
 Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai akisalimiana na Mtaalam Mshauri Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola (CPA) kutoka Makao Makuu Uingereza, Ndg. Anthony Staddon alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
 Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai akimsikiliza Mtaalam Mshauri Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola (CPA) kutoka Makao Makuu Uingereza, Ndg. Anthony Staddon alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
 Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (kulia) akizungumza na Mtaalam Mshauri Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola (CPA) kutoka Makao Makuu Uingereza, Ndg. Anthony Staddon (wa pili kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Kuanzia kushoto ni Katibu Msaidizi wa Bunge, Ndg. Zainab Kihange, Katibu wa Spika wa Bunge, Ndg. Saidi Yakubu na Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Uhusiano wa Kimataifa na Itifaki, Ndg. Daniel Eliufoo. 
Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai akiagana na Mtaalam Mshauri Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola (CPA) kutoka Makao Makuu Uingereza, Ndg. Anthony Staddon baada ya mazungumzo yaliyofanyika leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

WAZIRI MKUU MSTAAFU MIZENGO PINDA ATEMBELEA UBALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WASHINGTON, DC

$
0
0
Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu pamoja na Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe aliofuatana nao siku ya Jumanne Novemba 5, 2019.
Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu akiwa na Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa na Watumishi wa Umma katika Ubalozi huo  siku ya Jumanne Novemba 5, 2019.

MKUU WA WILAYA YA DODOMA AINGILIA KATI MGOGORO WA MIRADHI WATOTO WA MAREHEMU HUSSEIN DIMA

$
0
0

Na Woinde Shizza Michuzi Tv

Mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjin Patrobas Katabi ameingilia kati mgogoro wa mirathi wa watoto wa marehemu Hussein Bakari Dima wanainde otaka kudhulumiwa nyumba yao na ndugu wa marehemu baba yao iliyopo eneo la Kizota Area A Dodoma mjini.

Suala hilo ambalo lilianza takribani miezi miwili iyopita ambapo Shangazi na baba mdogo yao walikuja na hoja ya kutaka kuwakabidhi mali za urithi wa marehemu baba yao kwa kuwa watoto hao wamekwisha kuwa wakubwa na umri Zaidi ya miaka 18 na waweza kujitegemea.

Wakielezea sakata hilo watoto hao Omar Hussein (29) na Shamila Hussein (26)walitaka kufahamu mali ambazo shangazi yao anataka kuwakabidhi,lakini kinyume na matarajio yao shangazi yao alikuja na watoto wengine wawili akidai ni watoto wa nje ya ndoa wa marehemu ambao wanastahili kugaiwa nyumba hiyo ambayo tangu marehemu baba yao akiwa hai alishawarithisha.

“Sisi tulikataa ombi la shangazi ndipo alipoamua kwenda mahakamani kufungua ombi la kutaka kuwa msimamizi wa mirathi bila kutushirikisha wala kuwa na kikao cha familia ambacho kimemteua na kuwa na muhtasari wa kumkubalia kuwa msimamizi wa mirathi”.alisema Omary

Omar alisema baada ya shangazi kufungua kesi hiyo iliyosikilizwa kwa siku mbili na kutolewa hukumu licha ya kuwa hawajui sheria lakini hawakuridhishwa na uamuzi huo uliompa shangazi yao haki zote za kuwa msimamizi wa mirathi ikiwemo kuiuza nyumba yao na kumgaia mtoto anaeona anafaa au angependa.

“licha ya kumuomba Rais wetu Magufuli atusaidie tusidhulumiwe haki yetu tuliamua kwenda kwa mkuu wa wilaya kupeleka malalamiko yetu tukijua kuwa ndipo tunaweza kupata haki,kwa kuwa hatuna uwezo nwa kifedha na mahakamani hatujasikilizwa licha ya kuwa na hati halali za umiliki wa nyumba yetu, lakini hakimu alisema ni za kughushi bila kututhibitishia, shangazi ambae hakuwa na nyaraka yeyote alisikilizwa na kupewa haki ya kuwa msimamizi wa mirathi”Alisema Omary

Baada ya kupokea malalamiko ya watoto wa marehemu yaliyofikishwa kwa mkuu wa wilaya ya Dodoma yakionesha kutoridhishwa na uamuzi wa mahakama ya mwanzo ya Makole iliyotolewa Oktoba 28 na hakimu Nduka iliyompa mamlaka shangazi yao Zakhia Said kuwa msimamizi wa mirathi bila wao kusikilizwa watoto hao.

Omary alisema nyumba hiyo ilijengwa na baba na mama yao wakati wa uhai wao,ambapo baba yao alifariki mwaka 1998 na mama yao alifariki mwaka 2010, ambapo wamesisitiza kuwa tangu baba afariki hii nyumba ilikuwa chini ya umiliki weo wakisimamiwa na marehemu mama kwa kuwa tulikuwa bado wadogo ambapo wamemshangaa shangazi kuja na hoja ya kutaka kugawa mali za marehemu baada ya miaka 21.

Akizungumzia suala hilo mkuu wa wilaya ya Dodoma baada ya kufikishiwa malalamiko hayo na kuyapitia alitumia uamuzi wa kumuita shangazi yao afike katika ofisi yao ili kujua undani wa suala hilo ambapo alidai kuwa yupo mkoani Kilimanjaro.

Katabi amesema kwa namna alivyolitazama suala hilo alibaini kuwepo dosari nyingi za kisheria baada ya kuangalia mlolongo wote ameona kumekuwepo na ujanja ujanja baada ya kuangalia nyaraka zote.

“Hatua ya kwanza nimona niongee na hakimu mfawidhi ili aweze kuangalia mwenendo mzima wa shauri hilo jinsi ambavyo limeenda”alisema Katabi

Aliongeza kuwa wao kama serikali hawana wajibu wala haki ya kuingilia mahakama ila tuna haki ya kusimamia utaratibu,sheria kwa maana utawala wa sheria pale wanapoona kwamba kuna viashiria vya kupindishwa kwa sheria au kutokuwepo kwa misingi mizuri ya usimamizi wa sheria na haki hapo ndipo wanaingia kama sehemu ya serikali.

“nimefika hapa ili kwanza nilielewe eneo lakini pia kupata nyaraka hizo na pili kuwapta hao wanaolalamikiwa ili tuweze kupima na kuangalia haki iko wapi kwa hiyo tutafanya vizuri kabisa kwa kushirikiana na mahakama kuweza kuona haki ya watoto hawa inapatikana na awadhulumiwi.”alisema Katabi.

WAZIRI HASUNGA AIVUNJA BODI YA KAMPUNI YA MBOLEA TFC, ATENGUA UTEUZI WA MENEJA MKUU TFC, MKURUGENZI BODI YA KAHAWA, BODI YA TUMBAKU NA MRAJIS WA USHIRIKA

$
0
0
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akisisitiza weledi katika kazi wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika Ofisi za Kampuni ya mbolea Tanzania-TFC iliyopo Masaki Jijini Dar es salaam leo tarehe 8 Novemba 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akizungumza jambo na Menejimenti ya kampuni ya Mbolea Tanzania - TFC kabla ya kikao kazi na watumishi wa kampuni hiyo iliyopo Masaki Jijini Dar es salaam leo tarehe 8 Novemba 2019.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akipitia taarifa, sheria na muongozo wa kampuni ya Mbolea Tanzania - TFC kabla ya kikao kazi na watumishi wa kampuni hiyo iliyopo Masaki Jijini Dar es salaam leo tarehe 8 Novemba 2019.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akizungumza na watumishi wa kampuni ya Mbolea Tanzania - TFC wakati wa kikao kazi na watumishi hao kilichofanyika eneo la Masaki Jijini Dar es salaam leo tarehe 8 Novemba 2019.


Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameivunja Bodi ya Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) iliyoteuliwa rasmi tarehe 1 Disemba 2017 ikiwa na wajumbe sita ambao ni Mhandisi Eli Pallangyo, Bw Nuru Ndile, Bi Rosemary Msabaha, Bw Peter Shao, Dkt Kadida Mashaushi na aliyekuwa Mwenyekiti Marehemu Prof Egid Mubofu.

Waziri Hasunga amefanya maamuzi hayo leo tarehe 8 Novemba 2019 wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika Ofisi za Kampuni hiyo ya TFC zilizopo Masaki Jijini Dar es salaam huku akimuhamishia Wizarani Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo Ndg salum Mkumba ili kumalizia mkataba wa mwezi mmoja uliosalia.

Amesema kuwa Meneja huyo anatakiwa kuripoti Wizara ya Kilimo Jijini Dodoma kuanzia kesho tarehe 9 Novemba 2019 huku akieleza kuwa nafasi yake itasalia bila uteuzi mpaka atakapotoa maelekezo mengine.

Akizungumza katika kikao hicho Waziri Hasunga amesema kuwa ameivunja Bodi hiyo kutokana na kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kuagiza mbolea kutoka nje ya nchi hivyo kusababisha kampuni kushindwa kufanya biashara, kampuni kujiendesha kwa hasara hivyo kushindwa kufikia matakwa ya kuanzishwa kwa kampuni hiyo ya kuwa msambazaji kiongozi na anayeaminika kwa mbolea ya pembejeo zingine nchini kwa kuzingatia mahitaji ya mazao na afya ya udongo.

Kadhalika amesema kuwa Bodi hiyo pamoja na Meneja Mkuu imeshindwa kutekeleza wajibu wake ili kutoa suluhisho sahihi lenye gharama nafuu ya mbolea kwa wakulima na kwa wakati kwa kuzingatia hali ya udongo kwa mujibu wa Dira na Dhima ya Kampuni hiyo. Mengine ni kushindwa kuifufua na kuiendeleza kampuni hiyo

Kwa upande wa watumishi wengine wote waliobaki Waziri wa Kilimo amewapa wiki mbili kuhakikisha kuwa mbolea zilizopo bandarini zaidi ya makontena 127 ziwe zimetoka na kuwafikia wakulima kote nchini. “Tunahitaji mbolea lakini hiyo mbolea imekaa bandarini hivyo haraka iwezekanavyo ziende kwa wakulima” Alisisitiza Mhe Hasunga

Pia ametoa wiki moja kwa wafanyakazi hao kumpatia mabadiliko ya mtaji wa kampuni ili uendane na viwango vinavyotakiwa kwa mujibu wa sheria za makampuni hapa nchini, kuainisha mpangokazi unaoonyesha namna watakavyopata mbolea na kuisambaza mwaka huu, namna ya kusambaza viuatilifu na jinsi ya kuvipata vingine, kadhalika namna watakavyoisaidia serikali katika usambazaji wa mbegu na pembejeo nyingine.

“Ndani ya muda huo mkiniabia mmeshindwa nitajua hamuwezi kufanya kazi hivyo nitawapa kazi watu wengine ambao wengi wapo mtaani hawana kazi na wanaweza kufanya kazi hizo” Alisema

Waziri Hasunga amesema kuwa alimpatia maelekezo Meneja Mkuu wa kampuni hiyo ya mbolea (TFC) ya kutafuta eneo kwa ajili ya kujenga mtambo wa kuchanganyia mbolea lakini mpaka sasa Taasisi hiyo imeshindwa kutafuta eneo hilo kwa kipindi cha karibu miezi 9.

Katika hatua nyingine Waziri Hasunga amesema kuwa ataagiza wakaguzi maalumu kuikagua kampuni hiyo hususani kwenye majukumu ya kiutendaji kuangalia chanzo cha kushindwa kutekeleza majukumu yake na hatua zitachukuliwa kwa matokeo yatakayobainika.

Kadhalika amesema kuwa ametengua uteuzi wa Mrajis wa Vyama vya Ushirika Ndg Tito Haule, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Tanzania Ndg Primus Kimaryo, Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Tumbaku Dkt Julius Ningu wote kwa pamoja ni kutokana na kushindwa kutekeleza majukumu yao.

Waziri Hasunga amewataka watendaji hao kubadilika katika utendaji kazi ili kuongeza ufanisi na tija katika sekta ya kilimo ili kuwa na usalama wa chakula na kutofanya kazi kwa mazoea.

Serikali yaridhishwa na ubora ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ilemela

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR- TAMISEMI), Dkt. Dorothy Gwajima amekagua ujenzi wa Hospitali mpya ya Wilaya Ilemela mkoani Mwanza na kuridhishwa na ubora wa miundombinu ya majengo katika Hospitali hiyo. 

Dkt. Gwajima alifanya ziara ya kukagua ujenzi huo Novemba 07, 2019 na kisha kuelekeza Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kuanza taratibu za kuhakikisha Hospitali hiyo inaanza kutoa huduma kuanzia mwaka ujao 2020 ili kusogeza karibu huduma za afya kwa wananchi. 

Naye Msanifu Majengo Mwandamizi OR- TAMISEMI, Jonaphry Rwabagabo alitoa rai kwa wahandisi katika Halmashauri nyingine 67 nchini zinazojenga Hospitali za Wilaya kutimiza vyema majukumu yao ili kuhakikisha wanatekeleza kwa ubora miradi hiyo kama ilivyoonekana katika majengo ya Hospitali ya Wilaya Ilemela. 

Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ilemela ulianza mwezi Machi 2019 kwa kutumia mfumo wa "Force Account" ambapo Serikali ilitoa kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kutekeleza mradi huo.Na George Binagi-GB Pazzo, Mwanza
Majengo mbalimbali katika Hospitali ya Wilaya Ilemela inayojengwa katika Kata ya Sangabuye (eneo la Kabusungu-Isanzu).


Mwonekano wa majengo mbalimbali.

Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Ilemela uko katika hatua za mwisho ambazo ni pamoja na kuweka milango pamoja na madirisha.
Ukaguzi ukiendelea katika Hospitali ya Wilaya Ilemela.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR- TAMISEMI), Dkt. Dorothy Gwajima akiwa kwenye picha ya pamoja na watoa huduma za afya mkoani Mwanza.

Tazama Video hapa chini

JAFO AZIAGIZA HALMASHAURI NCHINI KUHARAKISHA VIBALI VYA AZAKI

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo,akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji, Wajibu, Bw.Ludovick Utuoh,kabla ya kufunga Mkutano wa Mijadala ya wiki ya AZAKI iliyohitimishwa leo jijini Dodoma baada ya kuanza Novemba 4 hadi 8 mwaka huu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo,akizungumza,na wadau kutoka Asasi za Kiraia wakati akifunga Mkutano wa Mijadala ya wiki ya AZAKI iliyohitimishwa leo jijini Dodoma baada ya kuanza Novemba 4 hadi 8 mwaka huu.
Rais wa Foundation for Civil Society, (FCS), Dkt Stigmata Tenga,akitoa taarifa kuhusu jinsi Wiki ya AZAKI ilivyokuwa katika maonesho hayo ambayo yalianza Novemba 4 hadi leo Novemba 8 ambapo yamefungwa na Waziri wa TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi CCM Mhe.Humphrey Polepole,Akizungumza wakati wa kufunga mkutano wa majadiliano ya Wiki ya AZAKI ambayo yalianza jijini Dodoma Novemba 4 hadi leo Novemba 8.
Mkurugenzi Mtendaji, Wajibu, Bw.Ludovick Utuoh, Akizungumza wakati wa kufunga Maonesho ya wiki ya AZAKI ambayo yalianza jijini Dodoma Novemba 4 hadi leo ambapo yamefungwa na Waziri wa TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo,akisisitiza jambo kwa washiriki kutoka Taasisi mbalimbali za Asasi za Kiraia wakati akifunga Mkutano wa Mijadala ya wiki ya AZAKI iliyohitimishwa leo jijini Dodoma baada ya kuanza Novemba 4 hadi 8 mwaka huu.
Sehemu ya washiriki wa Taasisi za Asasi za Kiraia wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo (hayupo pichani) wakati akifunga maonesho ya wiki ya AZAKI yaliyomalizika leo jijini Dodoma.
Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya uwezeshaji Asasi za kiraia(FCS), Francis Kiwanga,akizungumza na washiriki kutoka Taasisi mbalimbali za Asasi za Kiraia wakati wa kufunga mkutano wa majadiliano ya wiki ya AZAKI.
Mratibu ,Wiki ya AZAKI 2019 Justice Rutenge,akitoa taarifa ya hitimisho ya Wiki ya AZAKI ambapo maonesho hayo yamefikia mwisho na kufungwa na Waziri wa TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo yalianza jijini Dodoma Novemba 4 hadi leo Novemba 8,2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Asasi za Kiraia (AZAKI) ambapo maonesho hayo yameitimishwa leo jijini Dodoma.


JAFO AZIAGIZA HALMASHAURI NCHINI KUHARAKISHA VIBALI VYA AZAKI, "HAWA NI WADAU WA MAENDELEO"

Charles James, Michuzi TV

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe Selemani Jafo amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuhakikisha anasimamia zoezi la utoaji wa vibali vya usajili wa Asasi za Kiraia (Azaki) bila kuchelewesha.

Mhe Jafo amesema agizo hilo linakwenda pia kwa Mikoa na Halmashauri zote nchini kuharakisha kutoa vibali kwa Azaki zinazotuma maombi ya usajili ili kwa kuwa Azaki hizo zimekua mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali kuwaletea wananchi maendeleo.

Agizo hilo limetolewa leo jijini Dodoma wakati Mhe Jafo alipokua akifunga maadhimisho ya wiki ya Azaki yaliyodumu jijini hapa kwa juma zima na kuhudhuriwa na Azaki 500 na Taasisi 100.

Waziri Jafo amezitaka Asasi za kiraia nchini kuwa mabalozi wazuri katika kusemea mambo mema yanayofanywa na Serikali chini ya Rais Dk John Magufuli na kuzitama kusimamia malengo waliyojiwekea.

Mhe Jafo amesema kumekuepo na malalamiko kwenye Ofisi yake kuhusiana na kucheleweshwa kwa usajili wa Asasi hizo pindi wanavyoomba maombi ya usajili na kuwaahidi kuwa hata ikiwabidi kuomba kwenye Ofisi yake yupo tayari kusaini yeye mwenyewe.

Amesema maendeleo mengi yanayofanywa na Serikali hivi sasa kwenye sekta mbalimbali za Afya, Elimu, Miundombinu na Utawala bora yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na ukosoaji uliokua ukitolewa na Azaki hivyo ni vema wakapewa ushirikiano kwani wamekua ni wadau wa maendeleo nchini.

"Nakuagiza Katibu Mkuu wa Ofisi yangu hakikisha vibali vinatolewa bila vikwazo kwa Asasi hizi, ili mradi ina manufaa kwa Taifa na jamii kwa ujumla,na pia iwe na Sera zinazoeleweka katika kuchagiza maendeleo," amesema Jafo.

Amesema maendeleo mengi yanayofanywa na Serikali ya awamu ya tano,yametokana na mchango wa AZAKI wa kuibua changamoto zilizopo katika sekta mbalimbali hapa nchini,hivyo AZAKI zinastahili kupongezwa na kuskilizwa.

"Naomba niwapongeze sana AZAKI mmekuwa mkiibua matatizo yaliyopo sehemu tofauti, kwa mfano Hakielimu na tangazo lao la shule mbovu, yamesaidia serikali imeona na kuwekeza fedha nyingi katika sekta ya elimu kwa ajili ya kuziboresha na kufanya ujenzi.

"Katika sekta ya afya pia,barabara note mmekuwa mkipasemea na hivi sasa serikali inayafanyia kazi yote,na matokeo yanaonekana katika sekta hizo zilivyoimarika," Amesema Waziri Jafo.

Pamoja na hayo pia ameziagiza Asasi hizo za kiraia kuhakikisha wanasaidiana katika kuwezeshana na kurekebishana na sio kusemeana vibaya ili asasi nyingine zife jambo ambalo halikubaliki.

Amezitaka AZAKI hizo kuendelea kusaidia kulinda amani iliyopo kwa kutangaza mambo mema yenye ukweli ndani yake badala ya kutangaza mabaya wanayoyasikia bila kujua ukweli uliopo.

" Ndugu zangu kuna mambo mengi ambayo Rais Magufuli ameyafanya ndani ya kipindi kifupi cha uongozi wake, zaidi ya vituo vya Afya 360 vimejengwa, Hospitali 62 Nchi nzima na mpaka kufikia mwakani tutakua tumekamilisha nyingine 20 tena za kisasa kwa ajili ya kuhudumia wananchi wetu wanyonge.

Kama hiyo haitoshi Rais Magufuli ameamua kusimamia sera ya elimu bure kwa vitendo, Shule karibia zote kongwe zimefanyiwa ukarabati mkubwa na zaidi amekua akitoa elimu bila malipo kuanzia Elimu ya Msingi hadi Kidato cha Nne, kwenye miundombinu ndio usiseme hivi mnataka watanzania tupewe nini zaidi? Niwaombe tuendele kushirikiana, " Amesema Mhe Jafo.

Aidha amezitaka Azaki hizo kutumia Taasisi zao kutoa kuhamasisha wananchi kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 24 mwaka huu ili waweze kuwapata viongozi walio bora wenye kusimamia maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi Humphrey PolePole amesema
AZAKI na Serikali ni kitu kimoja hivyo haina haja ya kuogopana kama kuna suala lolote ambalo linapawa changamoto wasisite kushirikiana katika kukabiliana nalo na kulipatia ufumbuzi.

Nae Mkurugenzi wa Azaki nchini Francis Kiwanga amesema Azaki zipo kwa ajili ya kujenga na sio kubomoa kama baadhi ya watu wanavyofikiria na kuahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo.

" Sisi tunaishukuru sana Serikali kwa kuendelea kutusapoti, mmekua na sisi kwa wiki nzima hapa Dodoma, viongozi wa kiserikali, Wabunge na wadau mbalimbali wameungana nasi katika kujadili maslahi mapana ya Taifa letu hasa katika ubia wa maendeleo, tuwaahidi kwamba Azaki itazidisha mapambano ya kuwakomboa watanzania kifikra ili kuweza kufikia lengo Kuu ifikapo 2020," Amesema Kiwanga.

WAKURUGENZI WA HALMASHAURI WATAKIWA KUTOA ELIMU YA UJASIRIAMALI KWA WALEMAVU

$
0
0
Wakurugenzi wa Halmashauri na Maafisa Maendeleo ya Jamii nchini wametakiwa kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vikundi vya watu wenye ulemavu ili wanufaike na mikopo inayotolewa na Halmashauri hizo.

Agizo hilo limetolewa leo na Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga katika kongamano la asasi za kiraia (AZAKI) linaloendelea Jijini Dodoma.

Amesema watu wenye ulemavu wamekuwa hawatumii fursa ya mikopo inayotolewa na Halmashauri kutokana na wengi wao kutokuwa na elimu ya ujasiriamali.

“Matokeo yake wanaishia kuishi maisha ya utegemezi na kuomba omba mitaani, ninajua kabisa watu wenye ulemavu hawawezi kupata mikopo kwenye taasisi za kifedha ikiwemo mabenki kutokana na hali yao, ndio maana serikali kwa kuliona hilo iliamua kutenga asilimia 2 kati ya 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri zote nchini kwa ajili ya kutoa mikopo kwa makundi maalum yakiwemo ya watu wenye ulemavu,” amesema.

Ameeleza watu wengi wenye ulemavu bado hawajajitokeza vya kutosha kutumia fursa ya mikopo kwa ajili ya kujiimarisha kiuchumi hivyo wakurugenzi na maafisa hao wanatakiwa kutoa elimu ili waweze kujitokeza.

Amebainisha katika mwaka wa fedha 2018/19 Halmashauri nchini zilitenga jumla ya Sh. Bilioni 54.08  kwa ajili ya mikopo ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu lakini mpaka kufikia Juni 30, mwaka huu kiasi cha fedha kilichokuwa kimetolewa ni Sh.Bilioni 42.06  ambapo vikundi vya watu wenye ulemavu walipata kiasi cha fedha Sh.Bilioni 3.87.

“Kwa mwaka wa fedha 2019/20 serikali imetenga kiasi cha fedha Sh.Bilioni 62.22 ambapo wanawake na vijana  wametengewa Sh.Bilioni 24.9 na watu wenye ulemavu wametengewa Sh.Bilioni 12.4,”amesema.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga akizungumza katika mkutano wa majadiliano kuhusiana na fursa za mikopo kwa watu wenye mahitaji maalum kwenye wiki ya Asasi za Kiraia (Azaki) inayoendelea jijini Dodoma.

DC CHONGOLO ATEKELEZA AGIZO LA RAIS JPM LA KUSIMAMIA KURUDISHWA KWA NYUMBA YA BIBI MWENYE MIAKA ZAIDI YA 80.

$
0
0
Bi Amina Muhenga aliyekaa chini akimshukuru na kumuombea mungu Rais Dk. John Magufuli muda mchache kabla ya kukabidhiwa hati yake ya nyumba. Aliyesimama kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni , Mhe. Daniel Chongolo akimsalimia Bi Amina Muhenga ambaye alizurumiwa nyumba miaka zaidi ya 30 iliyopita muda mfupi kabla ya kumkabidhi hati ya umiliki wa nyumba. Wanaoshuhudia ni wananchi wa eneo la Mkoroshini Kata ya Msasani.

Nyumba aliyokabidhiwa Bi Amina Muhenga baada ya rais Dk. Magufuli kutoa agizo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo na hivyo kulifanyia kazi.
************************ 

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo ametekeleza agizo la Rais Dk. John Pombe Magufuli la kusimamia kurudishwa kwa nyumba ya Bi Amina Muhenga mwenye miaka zaidi ya 80 aliyozurumiwa kwa kipindi cha miaka zaidi ya 30 iliyopita.

Rais Dk. Magufuli alitoa agizo hilo zaidi ya miezi miwili iliyopita alipokuwa kwenye ibada ya jumapili katika kanisa la mtakatifu Petro ambapo Bi Amina alimfuata na kumueleza malalamiko yake kuhusiana na nyumba yake kuchukuliwa na mtu mwingine kinyume cha taratibu na hivyo kumsababishia kukosa makazi maalumu ya kuishi.

Mhe. Chongolo alieleza kuwa baada ya Rais kutoa maagizo hayo, kwakuwa ni waisaidizi wake ,walilifanyia kazi na hivyo kufanikisha kumrudishia Bi Amina nyumba yake pamoja na hati huku utaratibu mwingine ukiendelea kufanyika.

“Baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Bibi, Mhe rais kwakuwa sisi ni wasaidizi wake, alituagiza kulifanyia kazi na leo hii tumehitimisha kwa kumkabidhi hati za umiliki wa nyumba yake, na mambo mengine tunaendelea kuyakamilisha, kuanzia sasa bibi anarudi kwenye nyumba yake.” Amessema Mhe. Chongolo.

Aidha Mhe. Chongolo ameonyesha masikitiko yake ya baadhi ya wananchi wanaoishi katika Wilaya ya Kinondoni kuishi kwa ujanja ujanja na kusema kuwa kunaidadi kubwa ya watu wanaoishi kwenye mfumo huo na hivyo kutoa onyo la kuwataka kuacha mara moja tabia hiyo.

Amesema imekuwa ni jambo la kawaida kwa wananchi hao kwani kila siku ofisi yake imekuwa ikipokea malalamiko yanayohusiana na kuzurumiwa kwa nyumba zao kwakutumia kigezo cha hukumu ya Mahakama na hivyo kuacha watu wakiteseka.

Ameongeza kuwa,wakitoka Mahakamani wanakuja kuwatoa watu wenye haki, sijui niseme nini ila ukiangalia kunahali ya rushwa, ambayo imekuwa ikiwatesa sana baadhi ya wananchi, kazi yetu sisi ni kusimamia haki,nitahakikisha haki inasimamiwa na inatolewa kwa mwenye haki” amesema Mhe. Chongolo.

Kwa upande wake Bi Amina amemshukuru rais Magufuli kwa kumsaidia kupata nyumba yake, na hivyo kusema kuwa anamuombea kwa mungu aendelee kuwatumikia wanyonge.

WAZIRI MKUU MGENI RASMI BARAZA LA MAULIDI, ATOA NG’OMBE WATANO WA KITOWEO

$
0
0
Gari likiwa limebeba ng’ombe waliotolewa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Kassim kwa waumini wa Kiislamu pamoja na BAKWATA,kwa ajili ya kitoweo cha maulidi ya Mtume Muhammad S.A.W.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela,wa tatu kutoka kushoto akitoa neno wakati wa kukabidhi ng’ombe watano wa kitoweo waliotolewa kwa BAKWATA mkoani hapa kwa ajili ya sherehe za maulidi ya Mtume Muhammad S.A.W yanayofanyika kitaifa Mwanza, Novemba 9.

Kaimu Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, Alhaji Hassani Kabeke, wa kwanza kushoto akitoa shukurani kwa Mkuu wa Mkoa, John Mongela (wa pili kutoka kushoto) baada ya kumkabidi saruji mifuko 100 iliyotolewa na Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally kwa ajili ya ujenzi wa msikiri wa BAKWATA mkoani humu jana. Picha zote na Baltazar Mashaka





Kaimu sheikhe wa Mkoa wa Mwanza, alhaji Hassani Kabeke akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela, kukabidhi kitoweo kwa waumini wa dini hiyo kwa ajili ya maulidi lakini pia saruji ya ujenzi wa msikiti jijini humu.
.Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela, akizungumza na waumini wa dini ya Kiislamu kwenye viwanja vya Furahisha Kirumba, Manispaa ya Ilemela kabla ya kuwakabidhi ng’ombe watano wa kitoweo waliotolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Kassim lakini pia mifuko 100 kwa ajili ya ujenzi wa msikiti wa Bakwata mkoani huu jana.
…………………………………………………….

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa Kassim ametoa ng’ombe watano kwa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya sherehe za Maulidi.

Ng’ombe hao wa kitoweo walikabidhiwa juzi kwa kaimu Sheikhe wa Mkoa wa Mwanza,Alhaji Sheikhe Hassani Kabeke na Mkuu wa Mkoa huo John Mongela kwa niaba ya Waziri Mkuu.

Akizunguza wakati akikabidhi ng’ombe hao kwenyeViwanja vya Furahisha, Kata ya Kirumba katika Manispaa ya Ilemela zinakofanyikasherehe hizo kitaifa, Waziri Mkuualisema kitoweo hicho kitawasaidia Waislamu katika kipindi hiki cha kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad S.A.W.

Waziri Mkuu aliwataka waumini wa dini ya Kiislamu wanaposherehekea maulidi ya kuzaliwa kwa Mtume wahakikishe wanadumisha mshikamano,amani na utulivu wa nchi, tunu pekee inayoliliwa na mataifa mengi duniani.

“Niwatakie sherehe na maadhimisho mema ya maulidilakini jambo pekee na muhimu tuhakikishe tunafanya kwa utulivu, amani na mshikamano,ingawajambo hili kubwa ni kuwajenga watu kirohona kiimani,”alisema.

Sheikhe Kabeke akizungumza baada ya kupokea kitoweohicho kwa niaba ya BAKWATA na waislamu, alisema kitoweo hicho ni kafara njemaisiyo na doa.

“Serikali haina dini, ni faraja kwetu sisiWaislamu kutuunga mkono kwa kitoweo hiki ambacho ni kafara kubwa.Hii ndiyoserikali tunayoitaka na Tanzania tunayoifahamu ya watu wenye ukarimu,”alisema.


Alimshukuru Waziri Mkuu pamoja na serikali kwa kutambuamahitaji ya waislamu katika kipindi hikina kuamua kuwasaidia kitoweo kitakachowawezeshakutimiza jambo hilo la maulidi bila shida.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye Baraza la Maulidi litalofanyika jijini Mwanza baada ya sala itakayoswaliwa kwenye viwanja vya Furahisha.

Waziri Mkuu atawasili jijini Mwanza jioni kwa ajili ya shughuli hiyo akiungana na Waislamu wa jiji hilo na Watanzania wengine katika kumbukizi ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad S.A.

mahakama kuu kanda ya shinyanga yawaaga baadhi ya viongozi wa mahakama hiyo

$
0
0
Aliyekua Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga Mhe. Sekela Mwaiseje(aliyesimama) akizungumza jambo wakati wa hafla fupi ya kumuaga baada ya kuhamia Mahakama Kuu Kanda ya Arusha.

Bw. Bildars Ogenga akitoa salama za shukrani na kuwatakia heri viongozi wa Mahakama Kanda ya Shinyanga ambao wamehama kikazi kwa niaba ya watumishi wa Mahakama kuu Kanda ya Shinyanga.

Aliyekuwa Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga Bw. Ernest Masanja akiongea jambo wakati wa hafla fupi ya Kumuaga baada ya kuhamia Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba.



CHINA YAJA NA MKAKATI WA KUPAMBANA NA VITENDO VYA UJANGILI HIFADHI YA TAIFA YA MIKUMI

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwa na Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke (katikati) akimkabidhi Kamishna Mhifadhi wa Kanda ya Mashariki, Steria Ndaga moja ya kompyuta mpakato kati ya nne ambazo zimetolewa na Ubalozi wa China kwa ajili ya kusaidia katika mapambano dhidi ya Ujangili.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akikabidhi msaada wa runinga Kamishna Mhifadhi wa Kanda ya Mashariki, Steria Ndaga ambazo zitatumika kwa ajili ya kutolea elimu kwa njia ya video kwa wananchi wa kijiji cha Mhenda kuhusu athari zinazotokana na vitendo vya Ujangili. Kulia ni Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi ya Taifa ya Mikumi, Mathew Mombona kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kilosa Mhe.Adam Mgoi


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiteta jambo na Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe.Wang Ke kabla ya kukabidhi vifaa vya ujangili pamoja pembejeo za kilimo kwa wananchi wa Kijiji cha Mhende wilayani Kilosa mkoani Morogoro.


Balozi wa China nchini Tanzania , Wang Ke akizungumza mara baada ya kukabidhi mbegu mbalimbali za mazao kwa Diwani wa Kata ya Mhe. Ali Athuman kwa ajili ya kuwasaidia wananchi kujikita kwenye shughuli za kilimo na kuachana na vitendo vya ujangili.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe, Constantine Kanyasu akiwa pamoja na Balozi wa China nchini Tanzania, Wang KE wakiwa kwenye pamoja na baaadhgi ya wananchi pamoja na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Mikumi mkoani Morogoro.



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe, Constantine Kanyasu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mhende kinachopakana na Hifadhi ya Taifa ya Mikumi kabla ya kukabidhi Pembejeo za kilimo pamoja na vifaa vitakavyowasaidia Ulinzi shirikishi katika mapambano dhidi ya Ujangili.

Balozi wa China nchini Tanzania, WaNG KE akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mhende kinachopakana na Hifadhi ya Taifa ya Mikumi kabla akiwaeleza wananchi kuwa Mabalozi kwa kujikita katika kilimo kwa kuendesha shughuli za kilimo kwa njia ya kisasa kwa kutumia mbegu za kisasa walizopewa na Ubalozi huo.

(PICHA NA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII)

……………………..
Ubalozi wa China nchini Tanzania umeunga juhudi za Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya ujangili kwa kuziwezesha jamii zinazoishi karibu na Hifadhi ya Taifa ya Mikumi kwa kuzipa pembejeo za kilimo ikiwa pamoja na kuzijengea uwezo wa kulima kisasa ili kuwasaidia wananchi hao kuacha kujihusisha na vitendo vya ujangili.

Hayo yamebainishwa leo na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu wakati Ubalozi wa China nchini ukikabidhi msaada wa pembejeo za kilimo kwa wananchi wa kijiji cha Mhenda katika wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro

Ubalozi wa China nchini Tanzania umetoa msaada wa mbegu za mahindi yenye ujazo wa kilo 2500, mbegu za alizeti zenye ujazo wa kilo 150 pamoja mbegu za choroko zenye ujazo wa kilo 800

Mbali na msaada huo, Ubalozi huo umetoa jumla ya jozi 13 za sare za ulinzi shirikishi, buti 13, komputa mpakato nne pamoja runinga moja

Mhe.Kanyasu amesema lengo la vifaa hivyo ni kuwasaidia wananchi kujikita katika kilimo cha kisasa kwa kutumia mbegu zenye ubora wa hali ya juu.

Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Kanyasu amesema vifaa hivyo vitatumika katika kutoa elimu kwa wananchi katika mapambano dhidi ya vitendo vya ujangili.

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu ameipongeza Jamhuri ya watu wa China kukomesha soko la meno ya tembo na kuamua kutoa msaada kwa wanavijiji ili nao waweze kuachana na biashara hiyo haramu.

Awali, Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke amesema pembejeo za kilimo walizozitoa itakwenda sambamba na mafunzo yatakayotolewa na wataalam kutoka China watakaowafundisha wanakijiji kulima kwa kisasa ili waweze kuachana na vitendo vya ujangili.

Ameeleza kuwa Ubalozi wa China umeamua kuanza na kijiji hicho ili kuwasaidia wananchi kuweza kuzalisha mazao mengi ili wasiweze kujiingiza katika vitendo vya ujangili.

Amesema China imeamua kuisaidia Tanzania katika mapambano ya vita dhidi ya ujangilli kwa vile watalii wanakuja nchini kwa ajili ya kuangalia wanyama, hivyo vitendo vya ujangili vinakwamisha juhudi za serikali katika kujiletea maendeleo.

Aidha, Balozi huyo ameipongeza Taasisi ya Kova SUKOS Foundation inayoshughulikia majanga kwa kuratibu tukio hilo ikiwa pamoja na kujitoa kuhakikisha wananchi wa Mhende wanakabidhiwa misaada hiyo itakayowasaidia katika kujiondoa katika umasikini huku utalii ukizidi kushamiri.

Naye Diwani wa kata ya Mhenda, Ali Athumani amemshukuru Balozi wa China kwa msaada huo na kuahidi kuwa watakuwa mabalozi kwa vijiji vingine vilivyo karibu na Hifadhi hiyo.

WAZIRI LUKUVI AAGIZA MASHAMBA 24 KILOSA KUPELEKEWA ILANI YA KUFUTWA

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale wakati wa muendelezo wa ziara yake mkoani humo kutatua migogoro ya ardhi. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi.
Baadhi ya watendaji wa sekta ya ardhi mkoani Morogoro wakimsikiliza Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (hayupo pichani) alipokwenda wilayani Kilosa wakati wa muendelezo wa ziara yake kutatua migogoro ya ardhi mkoani Morogoro.(PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na uongozi wa wilaya ya Kilosa pamoja na Watendaji wa sekta ya ardhi katika wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro wakati wa muendelezo wa ziara yake ya kutatua migogoro ya ardhi mkoani Morogoro.

Baadhi ya watendaji wa sekta ya ardhi mkoani Morogoro wakimsikiliza Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (hayupo pichani) alipokwenda wilayani Kilosa wakati wa muendelezo wa ziara yake kutatua migogoro ya ardhi mkoani Morogoro.

……………..

Na Munir Shemweta, WANMM KILOSA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi ameagiza mashamba 24 yaliyopo katika wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro kupelekewa ilani ya kufutwa kutokana na kutoendelezwa na hivyo kukosa sifa ya kumilikiwa na wamiliki wake.

Lukuvi alitoa agizo hilo leo tarehe 8 Novemba 2019 wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro alipozungumza na uongozi wa wilaya ya Kilosa na watendaji wa sekta ya ardhi katika wilaya hiyo akiwa katika muendelezo wa ziara ya kutatua migogoro ya ardhi katika mkoa wa Morogoro.

Alisema, wilaya ya Kilosa haina kumbukumbu za mashamba jambo lilosababisha wizara yake kuamua kufanya upekeuzi maalum wa mashamba yote katika wilaya hiyo na kubaini mashamba 24 yasiyoendelezwa tofauti na mashamba 48 yaliyopendekezwa kufutwa awali.

Kufuatia agizo hilo la Lukuvi, sasa wilaya ya Kilosa itakuwa na mashamba 72 yanayotakiwa kufutwa baada ya mashamba 48 ya awali kupendekezwa kufutwa kutokana na kutoendelezwa.

‘’Maafisa Ardhi wa Wilaya ya Kilosa mfanye upekuzi wa mashama yote yasiyoendelezwa bila upendeleo wala kumuangalia mtu usoni na wala msitishwe na mtu yoyote kwa cheo chake au utajiri wakati wa kufanya kazi hiyo’’ alisema Lukuvi.

Waziri Lukuvi alisema, lengo la serikali kufuta mashamba yasiyoendelezwa ni kuwafikiria wananchi wanyonge wasiokuwa na ardhi kwa ajili ya shughuli za kilimo na kubainisha kuwa mashamba yatakatayofutwa yatagawiwa kwa wananchi na mengine yatatumika kama ardhi ya akiba itakayotumika kwa shughuli za uwekezaji.

Aidha, Lukuvi amekemea tabia ya baadhi ya wananchi wa wilaya ya Kilosa kuuza ama kukodisha mashamba wanayopatiwa na serikali na kusisitiza kuwa katika kukomesha tabia hiyo Wizara yake inaangalia namna ya kugawa mashamba yaliyofutwa kwa vikundi na kwa wale watakaopatiwa hawataruhusiwa kuuza na kuwataka Maafisa Ardhi kutofanya uhamisho wa shamba kwa yule aliyepatiwa .

‘’ Mkuu wa Wilaya komesha tabia ya udalali wa mashamba unaofanywa na baadhi ya wananchi wa Kilosa na yale mashamba yanayogawiwa kwa wananchi yatumike kwa shughuli zilizokusudiwa’’ alisema Lukuvi.

Vile vile, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ameagiza wafugaji wote wanaomiliki maeneo yenye hati kuweka uzio katika maeneo yao ili kuepuka mifugo yao kwenda maeneo ya wakulima na kusisitiza kufanyika ufugaji wa kisasa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ameomba kufanyika ukaguzi wa ardhi za vijiji kwa kuwa baadhi yake watu wamejimilikisha, wameuza na mengine kufanyika mgawanyo usio sahihi. Kwa mujibu wa Mgoyi halmashauri ya wilaya ya kilosa imeshindwa kufanya uhakiki kutokana na kutokuwa na fedha jambo alilolieleza kuwa limechangia migogoro ya ardhi katika wilaya hiyo na kusisitiza kuwa tegemeo la wilaya yake kwa sasa ni mashamba yaliyofutwa pekee.

Katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema vijijji viwili vilivyosajiliwa katika maeneo ya hifadhi wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro vitaendelea kubaki katika maeneo hayo kufuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuridhia vijiji 920 vilivyokuwa katika maeneo ya hifadhi kuendelea kubaki maeneo hayo.

Lukuvi amevitaja vijiji vya Mjambaa kilichoko katika shamba la Mbugani Estates lenye ukubwa wa ekari 1600 na kile cha Mambegwa kuwa vitaendelea kutambuliwa na kuagiza halmashauri ya wilaya ya Kilosa kwenda kuvipima na kuanisha shughuli za kilimo na makazi katika vijiji hivyo

WAZIRI LUGOLA AKUTANA NA WAJUMBE WA BODI YA SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA POLISI, JIJINI DODOMA, LEO

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza na
Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Uzalishaji Mali la Polisi, katika ukumbi
wa mikutano wa Wizara, jijini Dodoma, leo. Kulia meza kuu ni Naibu
Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima. Picha na Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani
Kailima akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Uzalishaji
Mali la Polisi, katika ukumbi wa mikutano wa Wizara, jijini Dodoma,
leo. Kulia kwa Kailima ni Waziri wa Wizara hiyo, Kangi Lugola. Lugola
alizungumza na Wajumbe hao, masuala mbalimbali ya uzalishaji mali
na kuwataka kufanya kazi kwa weledi. Picha na Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto),
akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhani
Kailima (kulia), pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Uzalishaji
Mali la Polisi, wakati alipokuwa anawasili katika ukumbi wa mikutano
wa Wizara, kuzungumza na Wajumbe wa Bodi hiyo, jijini Dodoma,
leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto meza
kuu), akimsikiliza Mjumbe wa Bodi ya Shirika la Uzalishaji Mali la
Polisi, Hilda Tegwa, alipokuwa anazungumza katika ukumbi wa
mikutano wa Wizara, jijini Dodoma, leo. Kulia meza kuu ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima. Picha na Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi.

DK. BASHIRU AUNGA MKONO UJENZI WA MSIKITI WA BAKWATA MWANZA KWA MIFUKO 100 YA SARUJI

$
0
0
NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ally, amekabidhi mifuko 100 ya saruji ili kushiriki ujenzi wa Msikiti wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Mwanza.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela, kwa niaba ya Dk. Bashiru alikabidhi saruji hiyo jana kwa Kaimu Sheikhe wa Mkoa Alhaji Sheikhe Hassani Kabeke.

Kwa mujibu wa Mongela, saruji hiyo ni ahadi ya Katibu Mkuu huyo wa CCM aliyoitoa mapema Agosti mwaka huu, alipotembelea na kuzungumza na viongozi wa taasisi mbalimbali za dini mkoani Mwanza.

Akiwa kwenye ofisi za BAKWATA zilizopo Mbungani katika Wilaya ya Nyaagana, Dk. Bashiru alikuta uongozi wa taasisi hiyo chini ya kaimu Sheikhe wa Mkoa, alhaji Kabeke ukiwa kwenye mchakato wa ujenzi wa msikiti wa baraza hilo na kuahidi kushiriki kwa kutoa mifuko 100 ya saruji.

Akipokea saruji hiyo, Sheikhe Kabeke alimshukuru Dk. Bashiru kwa kutekeleza ahadi yake kwa sababu siku ya kiama wote walioahidi watahojiwa.

Alisema serikali ya CCM chini ya Rais John Magufuli ni ya ahadi na vitendo kutokana na kutekeleza ahadi zake kwa wananchi ukweli uliodhihirishwa pia na Dk. Bashiru.

“Siku ya kiama ahadi zote wale waliaohidi wataulizwa lakini kwa kitendo hiki cha Katibu Mkuu kutimiza ahadi yake ni ishara njema kwa sababu tunaona serikali imetekeleza ahadi zake nyingi.Tunaamini mambo mengi yamefanyika na ahadi zitaendelea kutekelezwa na serikali yetu,”alisema.

Sheikhe Kabeke alisema kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24, mwaka huu, waislamu wajitokeze na kuwa mstari wa mbele siku hiyo ili kupiga kura kuchagua viongozi waadilifu, wazalendo na wenye uwezo wa kuleta maendeleo kwa jamii na kuyasimamia.

DK. BASHIRU ATIMIZA AHADI YA KINANA KATWE, AKABIDHI MIFUKO 26 YA SARUJI

$
0
0
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli (kulia), jana akikabidhi moja ya mifuko 26 ya saruji kwa uongoziwa CCM Tawi la Katwe Buchosa Sengerema.Saruji hiyo yenye tahamni ya sh. 507,000 ni ahadi ya Katibu Mkuu mstaafu Abdulrahiman Kinana aliyoitoa Juni 21, 2015 wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi ya tawi la CCM Katwe.
Kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Sengerema,Denis Luhende jana akizungumza kabla ya kumkaribisha Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Salum Kalli baada ya hafla ya makabidhiano ya saruji mifuko 26 ya saruji ya kukamilisha ujenzi wa ofisi ya tawi la Katwe.Saruji hiyo ilitolewa na Dk. Bashiru Ally.
.Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli (wa tatu kutoka kulia) akizungumza na wananchi na wana CCM wa Kijiji cha Katwe (hawapo pichani) jana baada ya kuwakabidhi ifuko 26 ya saruji ya kukamilisha ujenzi wa ofisi ya Chama ya tawi la Katwe.

Baadhi ya wajumbe wa Sekretarieti ya CCM tawi la Katwe wakiwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli, wa nne kutoka kushoto mbele ya jengo la tawi hilo.Wa tano kutoka kulia ni Mwenyekiti wa tawi hilo, Ruben Mchembe.

……………………………………………

NA BALTAZAR MASHAKA, SENGEREMA

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) tawi la Katwe wilayani Sengerema, wamesema uongozi wa Chama taifa umedhihirisha kuwa wa vitendo baada ya Dk. Bashiru Ally kutekeleza ahadi ya mtangulizi wake, Abdurahman Kinana.

Wamesema CCM chini ya Mwenyekiti wake Rais John Magufuli na Katibu Mkuu Dk. Bashiru, wameonyesha kwa vitendo badala ya maneno kutokana na kutekeleza ahadi nyingi zilizoahidiwa kwa wananchi na wana CCM iwe kwa Chama ama serikali.

“Tufikishie salama kwa Mwenyekiti Rais Magufuli tunaridhishwa na utendaji wake lakini pia Dk. Bashiru, ahadi hii ni ya muda mrefu na sasa ameitimiza na inaonyesha CCM na viongozi wake walivyo wa vitendo na si wa maneno.Tunamini jengo letu litakamilika,”alisema Mwenyekiti wa tawi la Katwe, Ruben Mchembe.

Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Salum, akikabidhi ahadi hiyo ya mifuko 26 ya saruji yenye thamani ya sh.507,000 jana alisema, Kinana (Katibu Mkuu mstaafu) Juni 21, 2015 aliahidi kuchangia sh. 500,000 za ujenzi wa ofisi ya tawi la Katwe wakati akiweka jiwe la msingi.

Alisema hadi anang’atuka hakuwa ametimiza ambapo Agosti Mosi, mwaka huu Dk. Bashiru akiwa ziarani Sengerema katika Jimbo la Buchosa aliahidi kutekeleza kwa asilimia 100 ahadi hiyo ya Kinana, baada ya viongozi wa tawi la Katwe kumueleza wakikumbushia ahadi hiyo ya kuchangia ujenzi wa ofisi ya Chama.

“Nimekuja hapa kutekeleza ahadi hiyo kwa vitendo ambayo ni mifuko 26 ya saruji kwa maelekezo ya Katibu Mkuu ( Dk. Bashiru) ambaye pia ni mlezi wa CCM Mkoa wa Mwanza ili mkamilishe jengo hili.Ahadi hii imetekelezwa kwa asilimia 100,” alisema Kalli akiahidi kuwaletea rangi likamilika walipake na kuonekana la kisasa.

Aidha kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Sengerema, Denis Luhende alipongeza jitihada za wana CCM wa Katwe kujenga ofisi ya Chama na kwa jitihada walizozionyesha wakiungwa mkono na Dk. Bashiru, watawasogea na kulikamilisha jengo hilo.

Naye Katibu wa CCM Kata ya Katwe, Francis Mahuma, aliahidi kuwa watasaimamia kwa dhati ujenzi wa mradi huo na kwamba bado wana changamoto ya samani za ofisi na siyo rangi tu.

“Kwa niaba ya wananchi na wana CCM wa Katwe,tunaamini jengo letu kwa mchango huu sasa litakamilika na hivyo tufikishie salamu na shukurani zetu kwa Dk. Bashiru kuwa alichotoa tumekipokea,”alisema

MNYETI AWAKABIDHI PIKIPIKI WATENDAJI KATA BABATI MJINI

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amewakabidhi pikipiki watendaji sita kati ya nane wa Kata za Mjini Babati, waliokuwa wanafanya kazi zao kwa changamoto ya ukosefu wa usafiri, ili kuwafikia na kuwatumikia wananchi wengi zaidi. 

Pikipiki hizo sita zenye thamani ya sh14.3 milioni zimenunuliwa na halmashauri ya mji wa Babati, kupitia fedha za kujenga uwezo zinazotokana na kuendeleza miji (ULGSP).

Mnyeti akiwakabidhi maofisa watendaji hao wa kata sita za mjini Babati, alisema vitendea kazi hivyo viwe nyenzo za kuwafikia wananchi zaidi tofauti na awali. 

Alisema watendaji kata hao waliopo pembezoni mwa mji wa Babati wanapaswa kutokaa ofisini na kuwafikia wananchi kuwatumikia ili kuondokana na kisingizio cha ukosefu wa usafiri. 

“Tunataka tuone kero za wananchi zinatatuliwa, kama mimi nafika hadi vijijini, ninyi watendaji wa kata au vijiji mnapaswa kufika hadi kwenye ngazi ya kaya na kutatua changamoto zao,” alisema Mnyeti. 

Hata hivyo, alimuagiza mkurugenzi wa mji wa Babati, Fortunatus Fwema kuhakikisha maofisa watendaji wa kata za Babati na Bagara, nao wananunuliwa pikipiki kama wenzao.

Fwema alisema wapo kwenye mchakato wa kuhakikisha wanawanunulia pikipiki watendaji wa kata za Babati na Bagara. “Baada ya kuwanunulia pikipiki watendaji wa kata zilizo pembezoni tunaahidi kutekeleza agizo lako la kuwanunulia watendaji wawili wa Babati na Bagara ili kukamilisha kata zote nane,” alisema Fwema. 

Ofisa utumishi wa halmashauri ya mji wa Babati, Sadiki Mrisho alisema pikipiki hizo zinapaswa kutumiwa na maofisa watendaji wa kata sita kwa matumizi ya serikali pekee. Mrisho alisema pikipiki hizo zimetolewa kwa mkopo kwa watendaji hao utakaosaidia utunzaji na ununuzi wa pikipiki nyingine. 

Ofisa mtendaji wa kata ya Sigino, Evelin Panga alisema pikipiki hizo zitawasaidia kufika kiurahisi katika shughuli zao vijijini. 

Panga aliishukuru serikali kwa kuwapatia nyenzo hizo za usafiri kwani awali walikuwa wanatembea kwa miguu kutoka sehemu moja hadi nyingine.

WANANCHI WAMLILIA LUKUVI WAPATIWE SHAMBA LA MWEKEZAJI KILOSA

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Magomeni wilaya ya Kilosa mkoa wa Morogoro (hawapo pichani) jana alipokwenda kusikiliza malalamiko ya wakazi wa kijiji hicho kuhusiana na shamba la Mwekezaji Farm Africa Agro Focus Ltd. Kushoto ni ya Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale wakati akitoka eneo la Kiwanda cha Mwekezaji Farm Africa Agro Focus Ltd Kilosa Morogoro jana. Kulia kwa Lukuvi ni Mkuu wa wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi.
**********************************

Na Munir Shemweta, WANMM KILOSA

Wananchi wa kijiji cha Magomeni kilichopo tarafa ya Kilosa Mjini wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro wametoa kilio chao kwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi wakitaka kupatiwa shamba la Mwekezaji Farm Africa Agro Focus Ltd marufu kama kwa Karamagi kwa madai kuwa mwekezaji wa shamba hilo ameshindwa kuliendeleza.

Wananchi hao wamemueleza Lukuvi kuwa kijiji hicho hakina ardhi ya kutosha kuwawezesha wananch hao kujishughulisha na kilimo na eneo kubwa katika kijiji hicho ni eneo la shamba la Farm lenye ukubwa wa ekari 13,000.

Wananchi hao wa kijiji cha Magomeni walitoa kilio chao kwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi jana tarehe 08 Novemba 2019 wakati Lukuvi akiwa katika ziara yake wilayani Kilosa kuendelea na jitihada za kutatua migogoro ya ardhi katika mkoa wa Morogoro.

Wamedai kuwa pamoja na Muwekezaji kuwa na eneo kubwa lakini ameshindwa kuliendeleza kama taratibu zinavyotakiwa na badala yake sehemu kubwa ya shamba hilo imebakia kuwa pori ingawa limeendelezwa katika eneo la usoni.

Mmoja wa wananchi hao Ismail Masudi alimueleza Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa kwa muda mrefu wananchi wa kijiji cha magomeni wamekuwa wakiishi kwa hofu kubwa kutokana na mgogoro wa muda mrefu kati ya muwekezaji na wananchi wa kijiji hicho.

‘’Wananchi tumepiga kelele sana ya kusaidiwa, Mwekezaji ana eneo kubwa lakini wananchi wanakosa maeneo ya makazi na ya kufanyia shughuli za kilimo huku sehemu kubwa ya shamba ka mwekezaji ikiwa ni pori’’ alisema Masudi

Mwananchi mwingine Hatibu Musa alisema kilio kikubwa cha wakazi wa kijiji cha Magomeni ni eneo la kulimia wakati idadi ya wakazi inaongezeka na wananchi wamehangaika kwa takriban miaka 5 na mgogoro huku wakidai mwekezaji hana tija.

Kwa upande wake Wzairi wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alimtaka Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi kumuomba mwekezaji wa shamba hilo kupunguza ekari 3000 kati ya 10,000 alizokuwa nazo kwa ajili ya kuwapatia wananchi wa kijiji cha Magomeni.

‘’ Badala ya kuanza kufuta shamba, Mwekezaji arudishe ekari 3000 kati ya 13,000 alizokuwa nazo tunataka kasi ya uendelezaji uendelee maana haiwezekani miaka nanne ni ekari 2000 tu zilizoendelezwa’’ alisema Lukuvi

Alisema, haingilii maamuzi ya mahakama yaliyompa ushindi Mwekezaji na wala hataki wananchi kupingana na maamuzi ya mahakama bali hali hiyo inafuatia mwekezaji kushndwa kuliendeleza shamba kama taratibu zinavyotakiwa ambapo uendelezwaji unatakiwa kufanyika moja ya nane kila mwaka jambo alilolieleza muwekezaji huyo alishindwa kutekeleza.

Taarifa kuhusiana na shamba hilo zinaeleza kuwa Mwekezaji wa sasa Farm Africa Agro Focus alikabidhiwa shamba mwaka 2013 na hadi kufikia sasa ni ekari 2000 pekee kati ya 13,000 ndizo zilizoendelezwa kwa kulima zao la Korosho.

WALIOKUTWA NA NOTI BANDIA ZA MIL 11WILAYA YA HAI, WAPANDISHWA KIZIMBANI.

$
0
0
Na Dixon Busagaga,Moshi

MFANYABIASHARA Chartone Mushi (44) na wenzake wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi, wakikabiliwa na makosa matatu likiwamo la utakatishaji wa fedha kiasi cha Sh. milioni 11 ambazo ni noti bandia.

Wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo namba 11 ya Uhujumu Uchumi ya Mwaka 2019 ni Richard Mtui (38) na Togolai Kingazi (34), wote wakazi wa Wilaya ya hai, mkoani Kilimanjaro.

Akisoma hati ya mashtaka jana, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Bernazitha Maziku, Wakili wa Serikali, Ignas Mwinuka alidai mahakamani hapo kwamba Oktoba 19 mwaka huu huko katika maeneo ya Bomang’ombe, Wilaya ya Hai, mkoa wa Kilimanjaro,

Washtakiwa hao Richard Mtui, Chartone Mushi na Togolai Kingazi, kwa makusudi waliunda genge la wahalifu na kundi hilo kutenda uhalifu wa kupokea na kusambaza noti bandia.

Katika hati hiyo ya mashtaka, washtakiwa hao wanadaiwa kukutwa kinyume cha sheria na noti bandia zenye thamani ya Sh. milioni 11.

Wakili Mwinuka, alidai mahamani hapo kwamba kosa la tatu linalowakabili washtakiwa hao ni la utakatishaji wa fedha, ambalo ni kinyume na kifungu 3 (d), 12 (a) na 13 (1) (a) cha Sheria ya Kuzuia Utakatishaji wa Fedha Haramu, kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2012,

Ikisomwa pamoja na aya ya 22 ya jedwali la kwanza la Sheria ya Uhujumu Uchumi, Sura ya 200 ya Sheria iliyofanyiwa Marejeo Mwaka 2002 na kifungu cha 16 cha sheria hiyo.

Baada ya maelezo hayo, Hakimu Maziku, alisema kwa kwa kuwa kesi hiyo haina dhamana, washtakiwa wote watarejeshwa mahabusu.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 22, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena mahakamani hapo.



WANAFUNZI KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE WAKUMBUSHWA KUZINGATIA MASOMO, NIDHAMU

$
0
0

Na Said Mwishehe, Michuzi TV

MKUU wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Profesa. Shadrack Mwakalila amewataka wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa masomo 2019/20  kuhakikisha wanazingatia kile kilichowapeleka chuoni hapo kuwa ni kusoma na kufanya vizuri katika mitihani yao na si vinginevyo.

Prof. Mwakalila ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wanafunzi wanaosomea cheti, dipoloma na wale wa digrii ambapo kwa ujumla amewataka wanafunzi hao  kujiepusha  na vitendo vyote vinavyoashiria ubaguzi, masuala ya kisasa, kuhakikisha wanakuwa na nidhamu pamoja na kuwa na matumizi mazuri ya muda ili kufikia malengo wanayokusudia.

Taarifa ya Kitengo Cha Habari na Mawasiliano cha  Chuo Cha KumbuKumbu ya Mwalimu Nyerere imesema Prof. Mwakalila amesema lengo la kuzungumza na wanafunzi hao kwanza kuwapongeza kwa kuchaguliwa katika Chuo hicho kikongwe Cha Mwalimu Nyerere chenye  historia kubwa na kilichobeba jina  Muasisi wa Taifa letu.

"Hivyo hakikisheni kile kilichowaleta hapa kitaaluma mnakifanikisha ikiwa ni pamoja na kusoma kwa bidii na maarifa na kumtanguliza Mungu mbele, mambo ambayo hayana msingi achaneni nayo,"amesema Prof. Mwakalila.

"Msipoteze malengo ambayo yamewaleta hapa, mmekuja kusoma zingatieni hilo na wala msijiingize kwenye mambo ambayo yatawapotezea muda, na mnapopata changamoto mbalimbali basi viongozi wa Chuo tupo na hata Serikali ya Wanafunzi ipo kwa ajili ya kusikiliza na kupatia ufumbuzi changamoto hizoo,"amesema Prof. Mwakalila.

Mkuu huyo wa Chuo  amesema  Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kina historia iliyotukuka, kina jina kubwa, vijana wengi wanamsoma tu Baba wa Taifa kwenye vitabu lakini ni mtu muhimu sana kwa Taifa letu.

Amesema muasisi wa Chuo Cha Mwalimu Nyerere  ni Rais wa Kwanza wa Taifa hili ambaye ni hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambapo  mawazo  ya kujenga Chuo kwa ajili ya wazalendo yalianza mwaka 1958 ambapo Chuo kilifunguliwa rasmi Julai 29, mwaka 1961, hivyo Chuo hiki ni kikongwe.

Prof. Mwakalila ameongeza lengo la Chuo wakati kinaanzishwa ilikuwa ni  kwa ajili ya  kuandaa viongozi wazalendo ambao lazima waandaliwe, ili kwenda kuongoza nchi, hivyo amewahakikishia wanafunzi kuwa wapo kwenye Chuo ambacho kitawajenga kimaadili na kizalendo kwa ajili ya kuwa viongozi wazuri wa baadae.
 Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalim Nyerere jijini Dar es Salaam Profesa Shadrack Mwakalila akizungumza na wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo hicho ambapo amesisitiza nidhamu na kusimamia elimu ambayo imepeleka hapo

Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere wakifuatilia hotuba ya mkuu wa Chuo hicho Profesa Shadrack Mwakalila hayupo pichani wakati anazungumzia nao chuoni hapo

WABUNGE WAELIMISHWA KUHUSU UWEKEZAJI NCHINI, WAELEZWA NAFASI YA TANZANIA DUNIANI

$
0
0
KITUO cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimepata fursa ya kutoa elimu ya uwekezaji kwa wabunge kupitia semina iliyotolewa kwa wajumbe wa Kamati mbili za Bunge ikiwa ni mkakati maalumu wa kuwajengea uwezo kufahamu masuala ya uwekezaji nchini.

Semina hiyo imefanyika Mjini Dodoma na ilifunguliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki .Kamati hizo ni Kamati ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma na Kamati ya Katiba na Sheria. 

Hivyo wabunge hao walielimishwa kwa undani kuhusu majukumu ya TIC, namna kituo kinavyovutia uwekezaji kwa kuzingatia hitaji la mwekezaji, sababu za kuwekeza Tanzania, vigezo vya mwekezaji kujisajili na TIC, vivutio vya uwekezaji na namna ambavyo vinachangia kuvutia uwekezaji mpya.

Pia wameelezwa kuhusu umuhimu wa uwepo wa dirisha la huduma za mahala pamoja TIC kwa wawekezaji na namna linavyofanikisha uwekezaji, faida za uwekezaji na nafasi ya Tanzania katika masuala ya uwekezaji, mgawanyo wa miradi ya uwekezaji kimkoa.

Mengine yaliyoelewa kwa wabunge hao ni namna miundombinu mizuri inavyochangia kuvutia uwekezaji, na namna ambavyo uharaka wa upatikanaji wa idhini(vibali,vyeti na leseni) mbalimbali za kufanikisha uwekezaji zinavyovutia uwekezaji. 

Akizungumza mbele ya wabunge hao Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Goefrey Mwambe ameweka bayana namna ambavyo mataifa yote duniani yanavyoshindana kuvutia uwekezaji, changamoto za uwekezaji na mapendekezo ya maboresho ya mazingira ya uwekezaji nchini ili kuvutia uwekezaji zaidi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji kwa Umma Dk. Chegeni amesema kupitia semina wamepata picha kubwa ya mwenendo na nafasi ya Tanzania kiuwekezaji duniani, Afrika na Afrika Mashariki. 

Amesema, tayari kuna mikakati na jitihada zinazochukuliwa na Serikali kuboresha mazingira ya uwekezaji lakini tuongeze kasi ili kufanikisha uwekezaji zaidi. Semina imechangia kuwaongezea elimu zaidi kuhusu uwekezaji na watakuwa katika nafasi nzuri ya kuchangia pale hoja za uwekezaji zitakapowasilishwa Bungeni. 

Dk.Chegeni amehimiza TIC iendelee kutoa elimu ya uwekezaji kwa wadau wote wakieleza TIC na majukumu yake, faida za uwekezaji kwa nchi na faida za mwekezaji akijisajili na TIC katika kufanikisha uwekezaji wake.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Angellah Kairuki akitoa neno la ufunguzi kabla ya semina ya wabunge iliyoandaliwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) kuanza. Semina hiyo imefanyika Mjini Dodoma
 Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geoffrey Mwambe akitoa mada wakati wa semina hiyo iliyofanyika Mjini  Dodoma
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live




Latest Images