Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

Kaimu Mkurugenzi Benki ya NMB Ruth Zaipuna ashiriki mdahalo wa jinsia jijini Dar es salaam

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya NMB – Ruth Zaipuna akiongea kwenye mdahalo ulioandaliwa na shirika la ‘International Finance Corporation’ (IFC) kuhusu Usawa wa Kijinsia Kazini. Mdahalo huo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam, ulikutanisha Wakurugenzi kutoka taasisi za Fedha, Wajasiriamali na Jinsia nchini. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered – Sanjay Rughani na kushoto ni Bi. Hodan Addou kutoja Umoja wa Mataifa.

IMEKULETEA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO NOVEMBA 1,2019

$
0
0

                

RC SINGIDA AFUNGUA MKUTANO MKUU WA TATU WA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA (SIFACU LTD)

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt.Rehema Nchimbi, akihutubia wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Tatu wa Chama Kikuu cha Ushirika (SIFACU Ltd) mkoani hapa juzi. Kutoka kushoto ni Katibu Tawala Msaidizi Uzalishaji Mkoa wa Singida, Beatus Choaji,  Mkuu wa Wilaya ya Singida,  Mhandisi Paskasi Muragili, Mwenyekiti wa  chama kikuu cha ushirika mkoa wa Singida,  Khamis  Mwanjowa na  mrajisi msaidizi wa  vyama vya ushirika mkoa wa Singida,  Thomas Nyamba.
 Mrajisi msaidizi wa  vyama vya ushirika mkoa wa Singida,  Thomas Nyamba, akizungumza katika mkutano huo.
 Mwenyekiti wa  chama kikuu cha ushirika mkoa wa Singida,  Khamis  Mwanjowa, akizungumza.
 RC Nchimbi na wajumbe wa mkutano huo wakiserebuka.
 RC Nchimbi na wajumbe wa mkutano huo wakiserebuka.
 Mkutano ukiendelea.
 Mkutano ukiendelea. 
 RC Nchimbi akikagua bidhaa za wajasiriamali.
 Wajumbe wakiwa kwenye mkutano huo.
 Wajumbe wakiwa kwenye mkutano huo.
Picha ya pamoja. 

Na Waandishi Wetu, Singida
MKUU wa Mkoa wa Singida, Dkt.Rehema Nchimbi ametoa miezi miwili kwa Mrajisi wa Vyama vya Ushirika mkoani hapa kuhakikisha anafanya ukaguzi kwa vyama vyote ambavyo bado havijakaguliwa, na kinyume chake hataruhusu mchakato wowote wa mikopo kufanyika.

Dk.Nchimbi aliyasema hayo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa tatu wa Chama Kikuu cha Ushirika (SIFACU Ltd) mkoani hapa juzi.

“Ukaguzi kwenye vyama hivi ni lazima na sio hiari, nakuagiza mrajisi ndani ya miezi miwili vyama vyote  vilivyobaki viwe vimekaguliwa na  chama kisichokaguliwa kisipewe mkopo wowote,” alisema Nchimbi
Alisema kwa mkoa wa Singida inasikitisha kuona takwimu zinaonyesha kati ya jumla ya vyama 320 vilivyopo ni vyama 70 pekee ndivyo vilivyokaguliwa jambo ambalo ni hatari kwa mustakabali chanya  wa uhai wa ushirika na wanaushirika wenyewe.

Alisisitiza kuwa, ushirika pamoja na mambo mengine ni lazima utembee na ajenda ya mshikamano, nguvu, heshima na uhai endelevu sanjari na kuweka kando masuala yote yanayoweza kuufifisha ikiwemo ubinafsi na migogoro isiyokoma.

“Utakuta kila siku  vitu vinavyoleta utapiamlo kwenye vyama hivi vya ushirika ni ubinafsi…watu wamesahau kabisa kuwa ushirika ni utumishi ndio maana rushwa imetamalaki na matokeo yake ni kufifisha matarajio yake chanya,” alisema Nchimbi.

Alisema anatamani moja ya ajenda kubwa ya wanaushirika wote iwe ni kutafuta suluhisho la lishe bora kwa watoto waliopo mashuleni ili hatimaye kuwawezesha kujenga utulivu wa akili kuweza kumsikiliza vizuri mwalimu na kumudu masomo yao.

Dkt. Nchimbi aliwakumbusha wana ushirika wote nchini, hususan wale wa mkoa wa Singida kutambua kwamba wao ni nguzo na mkono wa serikali katika kushauri, kuongoza, kuelekeza na kuifikisha jamii na taifa kwenye uchumi wa viwanda kama ishara na tunda la serikali iliyopo madarakani kwa sasa.

Kwa upande wake, Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika mkoani hapa, Thomas Nyamba, alisema hali ya vyama vya ushirika ndani ya mkoa wa Singida inaendelea kuimarika ikilinganishwa na huko nyuma, huku idadi ya vyama hivyo ikifikia 320.

“Tuna jumla ya vyama vya ushirika mia tatu na ishirini, kati ya hivyo sitini na tisa ni vile vya mazao hususan pamba, huku upande wa saccos hali sio ya kuridhisha kutokana na vingi kati yake kukabiliwa na madeni,” alisema Nyamba.

Makamu Mwenyekiti wa SIFACU, Yahaya Ramadhan Khamis alibainisha pamoja na mambo mengine lengo la mkutano huo mkuu ni kutathmini shughuli zote zilizofanywa kwa mwaka uliopita na kupanga mipango ya mwaka unaoanza.

“Mwaka uliopita tumefaulu kuunganisha vyama na wanachama wakekutoka idadi ya vyama thelathini na sita hadi sitini na sita, tumeweza pia kutafuta masoko ya uhakika, kuwaunganisha wakulima kuweza kupata mikopo kwenye taasisi mbalimbali za fedha,” alisema Khamis

MRADI WA MAJI WA KISARAWE KUANZA KUTOA MAJI MWEZI UJAO

$
0
0
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akimsikiliza Mkurugenzi wa Uwekezaji na Miradi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), Mhandisi Ramadhani Mtindasi katika kituo cha kusukumia maji Kibamba, wilayani Ubungo.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb) pamoja na Mkuu wa Wilaya za Ubungo, Kisare Makori (kulia) na Mkuu Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo (kushoto) katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Kisarawe, katika Kata ya Kibamba, wilayani Ubungo.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akiwa na mkandarasi alipotaka maelezo kuhusu utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa kwake jana ya kukamilisha utaratibu wa malipo na kazi ya kuvuta umeme.
Tenki la maji la Kibamba lenye ujazo wa lita milioni kumi litakolotumika kuhifadhi maji yatakayo hudumia wakazi wa Kisarawe kupitia Mradi wa Maji wa Kisarawe.



Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akiwa na Msimamizi wa Ujenzi wa Mradi wa Maji wa Kisarawe, Mhandisi Ishmaeli Kakwezi wakati akikagua tenki la maji la Kibamba lenye ujazo wa lita milioni 10.

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akiwa kwenye eneo palipo na maunganisho ya bomba la tenki la Kibamba na bomba linalopeleka maji katika Mji wa Kisarawe.
…………………….

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb) ametembelea na kukagua utekelezaji wa kazi ndogo zilizobaki katika ujenzi wa Mradi wa Maji wa Kisarawe katika Kata ya Kibamba, wilayani Ubungo.

Ziara imelenga kufuatilia utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa jana kwa mkandarasi kukamilisha utaratibu wa malipo na kazi ya kuvuta umeme ifanyike haraka ili mradi uanze kufanya kazi mwezi ujao.

Malipo ya Shilingi milioni nane kwa TANESCO yameshafanyika na kazi ya kufunga umeme huo itaanza mara moja tayari kwa kufanya majaribio ya kusukuma maji (pump test) wiki ijayo.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri Aweso ameambatana na Wakuu wa Wilaya za Ubungo, Kisare Makori na Kisarawe, Jokate Mwegelo akiwasisitiza umoja na ushirikiano katika kufanikisha zoezi la utekelezaji wa mradi huo kwa maslahi mapana ya wananchi wa Kisarawe. 

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Makori ametoa rai kwa viongozi na watendaji wa wilaya za Ubungo na Kisarawe kujitoa na kusimamia miradi ya maendeleo inayotumia fedha nyingi, hatua itakayosaidia juhudi za Serikali kuzaa matunda.

SERIKALI KUWEKA KIPAUMBELE MICHEZO KWENYE MTAALA WA MAFUNZO YA UALIMU

$
0
0
Serikali ya Awamu ya Tano imeweka kipaumbele katika kuimarisha michezo kama eneo muhimu la mtaala wa mafunzo ya ualimu kutokana na ukweli kwamba michezo inaimarisha stadi za kujifunza, nidhamu na ni ajira pia.

Hayo yamesemwa Mkoani Mtwara na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha wakati wa kufunga Mashindano ya Kitaifa ya Michezo na Sanaa kwa Vyuo vya Ualimu Tanzania Bara (UMISAVUTA).

Amesema pamoja na kuwepo kwa mchepuo wa michezo katika baadhi ya vyuo vya Ualimu ni vizuri Vyuo hivyo kupitia Ofisi ya Kamishna wa Elimu wakaweka mikakati ya kuhakikisha kuwa ufundishaji na ujifunzaji wa michezo na sanaa unalenga kuwawezesha vijana kufanya vizuri katika eneo hilo kwa maendeleo yao na Taifa. 

Ametaja Vyuo ambavyo kwa sasa vinatoa mchepuo wa michezo kuwa ni Chuo cha Ualimu Tarime, Butiama, Butiama Mtwara Kawaida na Ilonga na kwamba Wizara itahakikisha kuwa michezo inaimarishwa katika vyuo vyote vya ualimu nchini.

Naibu Waziri Ole Nasha amevitaka vyuo vya ualimu kuhakikisha vinaendeleza michezo chuoni  kutokana na faida zitokanazo na michezo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha  wahitimu wa mafunzo ya ualimu wanapata mafunzo ambayo wakihitimu wanakwenda kuwa walimu mahiri wa michezo katika shule za msingi na sekondari ambapo ndipo wanamichezo na wasanii wanaandaliwa.

“Nimefarijika kuona mashindano ya michezo na sanaa kwa vyuo vya ualimu imerudi tena baada ya kutokuwepo kwa miaka 20 iliyopita, hatuna budi kuwekeza katika michezo kwa sababu ni fursa za kuweza kusaidia kukua kiuchumi. Nchi nyingi duniani michezo imekuwa sehemu kubwa ya kusaidia kukua kiuchumi,” alisema Naibu Waziri Ole Nasha. 

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambae pia ni Afisa Elimu Mkoa Germina Mng’aho amesema kufanyika kwa michezo hiyo ni utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo inataka kuwepo kwa mashindano ya michezo kwa shule na vyuo ili kuwezesha kuinua vipaji ambavyo vitaleta mafanikio katika michezo ya kitaifa na kimataifa.

Nae Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Seksheni ya Mafunzo ya Ualimu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Agusta Lupokela amesema anaishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutambua faida zinazopatikana katika michezo ikiwemo stadi za kujifunza na kuamua kurejesha mashindano ya michezo kwenye Vyuo vya Ualimu.

Akitoa taarifa ya mashindano hayo kwa  Naibu Waziri Mwenyekiti wa UMISAVUTA Taifa Agustine Sahili amesema kuwa michezo hiyo imeendeshwa kulingna na taratibu za michezo na matokeo yameamuliwa kwa weledi na haki katika kupata washindi.

Sahili ameiomba  Wizara  kuimarisha kozi ya michezo na fani mbalimbali za ndani katika vyuo vya ualimu ili wataalamu waweze kupatikana shuleni ambako ndiko chimbuko halisi la vipaji linapatikana lakini pia kuwajengea uwezo wasimamizi na waamuzi wa michezo kwa kuendesha kozi fupi na ndefu kwa kushirikiana na Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Pia ameiomba Wizara kuongeza wakufunzi wa michezo na Sanaa vyuoni kwani kwa sasa vyuo vingi havina wakufunzi wa aina hiyo hali inayodunisha uendeshaji wa michezo na ukuzaji wa vipaji kwa vijana chuoni ambapo pia inasababisha shule za msingi na sekondari kukosa walimu mahiri katika michezo na Sanaa.

Nae Mshiriki wa Mashindano ya Michezo na Sanaa  Albert Thomas kutoka Kanda ya Ziwa ameishukuru Serikali kwa kurejesha mashindano ya UMISAVUTA kwani inawasaidia kujenga  afya na akili lakini pia inawasaidia kuwa na uelewa wa masula ya michezo na kutoa elimu ya michezo kwa wanafunzi ambao watakwenda kuwafundisha  baada ya kumaliza masomo yao. Ameiomba Serikali kuendeleza vipaji vya wanamichezo wanaoshinda katika mashindano ya ngazi ya shule na vyuo ili visiishie kwenye ngazi ya kitaifa bali katika ngazi za kimataifa.

Ufungaji wa mashindano ya Kitaifa ya Michezo na Sanaa kwa vyuo vya ualimu yaliyoanza Oktoba 25, 2019 na kuhitimishwa Oktoba 31, 2019 yamepambwa na mechi kati ya Kanda ya ziwa na Kanda ya kusini ambapo Kanda ya ziwa wameibuka kidedea baada ya kuwafunga Kanda ya Kusini goli moja kwa sifuri.
Naibu waziri Wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha akitoa kombe la ushindi wa mpira wa miguu kwa wachezaji wa kanda ya ziwa wakati wa ufungaji wa mashindano ya kitaifa ya Michezo na Sanaa ya Vyuo vya Ualimu UMISAVUTA yaliyomalizika leo mkoani Mtwara.

 Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha akisalimiana na wachezaji kabla ya kuanza mechi wakati wa ufungaji wa Mashindano ya Kitaifa ya Michezo na Sanaa kwa Vyuo vya Ualimu Tanzania Bara ,yaliyofanyika Mkoani Mtwara.

WANANCHI MAKUNGU WAMSHUKURU RAIS MAGUFULI NA KINGU KUWACHIMBIA MAJI

$
0
0
 Mbunge Kingu akiwahutubia wananchi hao katika mkutano wa hadhara.

 Mbunge wa Singida Magharibi, Elibariki Kingu (katikati) akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Makungu Wilaya ya Ikungi mkoani Singida juzi,  wakati akikagua mradi wa maji waliowezeshwa na Rais John Magufuli.
 Katibu Muenezi na Itikadi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Iyumbu, Lameck Maguni akizungumza kwenye mkutano huo.
 Wananchi wa Kijiji cha Iyumbu wakiwa kwenye mkutano.
 Katibu wa CCM Kata ya Iyumbu, Mohammed Itambu akizungumza.
 Mbunge Kingu akiserebuka katika mkutano huo.
 Mwenyekiti wa CCM Tawi la Makungu, Weja Ng'waya akizungumza.
 Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Kata ya Iyumbu, Njile Gasamalu akizungumza.
 Diwani wa Kata ya Iyumbu, Peter Gwiligwa akizungumza.
 Mwenyekiti wa CCM Kata ya Iyumbu, Juma Okumu akizungumza.
 Wananchi wa Kijiji cha Iyumbu wakiwa kwenye mkutano.
Kingu akiwahamasisha wananchi kwenda kujiandikisha.

Na Dotto Mwaibale, Singida
WANANCHI wa Kijiji cha Makungu Kata ya Iyumbu Wilaya ya Ikungi mkoani Singida wamemshukuru Rais John Magufuli na Mbunge wao Elibariki Kingu kwa kuwachimbia kisima cha 
maji.

Shukurani hizo walizitoa juzi katika mkutano wa hadhara aliouandaa mbunge huyo wakati akikagua miradi ya maendeleo pamoja na kuwahamasisha kujiandikisha kwa wingi ili waweze kuwachagua viongozi wa vijiji, vitongoji kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Mwishoni mwa mwaka jana wananchi hao walizuia msafara wa mbunge huyo na kumuonesha mabango yenye kero mbalimbali kubwa ikiwa ni kukosa maji ambapo aliipeleka kwa Rais Magufuli ambaye amewachimbia kisima hicho ambacho kitasambaza maji katika kijiji hicho na vitongoji vingine vya jirani.

Kingu alisema wanamshuru Rais John Magufuli kwa kusikia kilio chao hivyo kutokana na heshima hiyo aliowapa watahakikisha  viongozi wote katika uchaguzi wa serikali za mitaa vijiji na vitongoji wanatoka Chama Cha Mapinduzi (CCM)" Ndugu wananchi heshima pekee ya kumshukuru Rais wetu kwa kutuletea mradi huu wa maji ni  kuhakikisha tunakipa ushindi mkubwa chama chetu naombeni twendeni tukajiandikishe kwa wingi na siku ikifika ya kupiga kura basi tuwachague viongozi watakaounda serikali kupitia CCM" alisema Kingu.

Alisema serikali imewapendelea sana Jimbo la Singida Magharibi kwa kuwapelekea miradi ya  maji 24 na sasa hivi kuna magari mawili yenye mitambo ya kuchimba maji yapo maeneo mbalimbali ya jimbo hilo ambapo katika kijiji hicho maji yaliyopatikana yatakuwa yakitoka lita 11,000 kwa saa na kuwa sh.350 milioni zimetengwa kwa ajili ya miundo mbinu ya kusambaza maji kwenye kijiji hicho na kufunga DP.

RC DKT. REHEMA NCHIMBI AKABIDHI GARI KIKOSI CHA ZIMA MOTO NA UOKOAJI MKOA WA SINGIDA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akipeana mkono na Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani hapa, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACF), Ivo Ombella wakati akikabidhi gari aina ya‘Land Lover Defender’ kwa Jeshi hilo katika hafla iliyofanyika jana. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhandisi Paskasi Muragili.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACF), Ivo Ombella akizunguza baada ya kukabidhiwa gari hilo.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACF), Ivo Ombella (wa pili kulia) akiwa na maofisa wa jeshi hilo katika hafla ya kukabidhiwa gari hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi, akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa huo katika hafla ya kukabidhi gari hilo.
Gari aina ya ‘Land Lover Defender’ lililokabidhiwa kwa Jeshi la Zima moto na Uokoji mkoani hapa. 


Na Dotto Mwaibale, Singida

MKUU wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi amewataka wananchi kujiepusha na majanga ya moto yanayotokana na uzembe au makusudi kwa kigezo cha kutegemea uwepo wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

Dkt. Nchimbi aliyasema hayo jana wakati akikabidhi gari aina ya‘Land Lover Defender’kwa Jeshi la Zima moto na Uokoji mkoani hapa litakalotumika kwa shughuli mbalimbali za utawala.

“Natarajia gari hili liitasaidia kurahisisha majukumu ya kijeshi kwa Jeshi hili, hususan kwenye eneo la utoaji elimu na kujenga maarifa kwa jamii katika kuhakikisha suala la kinga linapewa kipaumbele ili kuepusha maafa na ajali zozote huko mbeleni,” alisema Nchimbi.

Kwa upande wake, Kamanda wa Jeshi hilo mkoani hapa, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACF), Ivo Ombella, alisema gari hilo litatumika kwa shughuli zote za dharula ndani ya jeshi hilo chini ya uratibu wa idaraya utawala.

“Ifahamike kuwa Jeshi la Zima moto na Uokoaji linahusika nadharula zote ikiwemo majanga ya moto, tetemeko la ardhi, mafuriko na uzazi isipokuwa jinai pekee,” alisema Ombella

Aidha, aliwatahadharisha wananchi kuwa makini kwa kujiepusha na majanga ya moto hasa nyakati za utayarishaji wa mashamba kwa kuzingatia usalama na utunzaji mzuri wa mazingira kulingana na eneo husika.

UZINDUZI WA KITABU NA FILAMU KUHUSU HISTORIA YA RELI YA TAZARA WAFANYIKA JIJINI BEIJING CHINA

$
0
0
Uzinduzi wa Kitabu na Filamu kuhusu historia ya Reli ya TAZARA umefanyika leo Beijing. 

Hafla hiyo ni sehemu ya matukio yanayoendelea ya Kumbukizi ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yanayofanywa na Chuo Kikuu cha Zhejiang Normal University. 

Ujenzi wa Reli ya TAZARA ni moja ya ‘legacy’ ya Baba wa Taifa inayoenziwa nchini China ikiwa ni alama ya urafiki kati ya China na Bara la Afrika.

Katika hafla hiyo Chuo Kikuu cha Zhejiang Normal University kimetangaza dhamira yake kuanzisha kozi ya lugha ya Kiswahili. Vilevile, wameeleza mpango wa kuanzia kituo cha mafunzo ya uongozi kitakachojulikana kama Julius Nyerere Study Centre.  

Kituo hicho kitashughulika na tafiti mbalimbali juu ya falsafa za Uongozi Barani Afrika.  Rais wa Zhejiang Normal University na  Balozi wa Zambia Mhe Winnie Chibesakunda, Mabalozi na Wanazuoni pia wameshiriki hafla hii. Habari/Picha kwa hisani ya Phelista Wegessa
 Balozi wa Tanzania nchini China,Mhe.Mbelwa Kairuki akizungumza kwenye hafla ya Uzinduzi wa Kitabu na Filamu kuhusu historia ya Reli ya TAZARA uliofanyika jijini Beijing. Hafla hiyo ni sehemu ya matukio yanayoendelea ya Kumbukizi ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yanayofanywa na Chuo Kikuu cha Zhejiang Normal University. 
Picha ya pamoja wakati wa uzinduzi 
 Wadau mbalimbali wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye uzinduzi huo





MLEMAVU WA MACHO ATAMANI KUWA MFANYABIASHARA MKUBWA

$
0
0
Na Woinde Shizza, Globu ya jamii Arusha
KIJANA Baraka Imanuel ni kijana mwenye umri wa miaka (24) mkazi wa ngaramtoni halmashauri Arusha iliopo wilayani Arumeru mkoani Arusha, kijana huyu ni mlemavu wa macho (kipofu ) na ni mfanyabiashara ndogomdogo na malengo yake ya kutoka kumiliki biashara ndogo anayoifanya na kuwa mfanyabiashara mkubwa.

Gazeti hili lilipata nafasi ya kuzungumza na kijana huyu na alikuwa na
mengi yakueleza kuhusiana na namna anavyofanya biashara yake

Baraka anafanya biashara ya kuuza viberiti ndani ya jiji la Arusha, kila
asubuhi amekuwa akiamka na kwenda kununua viberiti na kuvitembeza kwa watu mbalimbali na kuuza ili apate chochote kitu kitakacho msaidia kutumia yeye na familia yake.

Baraka ni mtoto wa kwanza katika familia ya mama Beatrice Imanuel
akiwa na wadogo zake wawili mmoja wa kike alimtaja kwa jina la Jackile
Imanuel ambaye yeye yupo nyumbani tu hafanyi kazi yoyote pamoja na
wakiume aliyemtaja kwa jina la Steven Imanuel ambaye yeye ni
anajitolea kufanya kazi ya kusaidia mafundi wa ujenzi ili apate
chochote kitu cha kuwasukuma katika maisha.

Anafafanua kuwa mama yake mzazi anafanya bishara ya mamantile huku
baba yake aliemzaa aliikimbia familia na kutelekeza na kukimbili
pasipo julikana kwa kipindi cha mda mrefu.

Kwanini alianza biashara ilihali ni mlemavu wa macho?
Anaeleza kuwa kitu halisi kilichomsukuma mpaka akaamua kufanya
biashara ya kutembeza viberiti ni kuondokana na utegemezi, kitu
ambacho alisema anakichukia kuliko vitu vyote katika maisha yake japo
kuwa yeye ni kipofu.

Alisema kuwa aliamua kumuomba mama yake mtaji wa kuanza biashara hali kuwa mama yake alikuwa mgumu wa kumpa kutokana na hali yake lakini alimbembeleza hadi mama yake akaamua kumpa mtaji wa shilingi elfu 30, hela ambayo aliamua kwenda kununua nusu katoni ya viberiti na kuanza
kutembeza.

“Mama alinipa mtaji wa shilingi elfu 3o tu na niliamua kuanza
biashara bila kujali hali yangu na mpaka leo nafanya, nilianza na nusu
katoni ya viberiti na sasa hivi naweza nunua katoni moja nzima mbali na
hivyo pia nashukuru Mungu mtaji wangu umekuwa na umefikia kiasi cha
shilingi elfu 70 na hii inatokana na mimi kujali kazi yangu na
kuipenda na pia kuafanya maamuzi ya kutokuwa tegemezi”alibainisha
Baraka.

Anatambuaje Fedha anapopewa na mteja ?
Baraka alifafanua kuwa alibahatika kusoma hadi kidato cha nne ambapo
alisema kuwa elimu yake ya msingi aliipata katika shule ya msingi Longido mkoani Arusha, huku elimu ya sekondari akiipata katika shule ya Shaibushe iliopo mkoani Shinyanga ambapo walikuwa wakifundishwa na walimu wenye uzoefu wa kutoa elimu kwa wanafunzi wenye uhitaji.

“Nikipewa ela najua hii ni shilingi ngapi kutokana na elimu niliopewa
darasani pia nakisia na kutambua hii ni kiasi gani, pia nashukuru Mungu
maana wateja wengi nao wauzia viberiti wananionea huruma hivyo
hawawezi kunirusha kwani wanaona kabisa hali yangu ilivyo”,alisema

Alibainisha kuwa amekuwa anaamuka kila siku asubui na kwenda kununua
viberiti hivyo katika maduka ya Jumla na amekuwaanatembeza katika
maeneo mbalimbali ya jiji la Arusha ikiwemo standi, masokoni na hata
katika maeneo ya majumbani kwa watu.

Nini ombi lake kwa serikali na wadau ?
Baraka ameiomba serikali pamoja na wadau mbalimbali kujitokeza katika
kumsaidia kumuongezea mtaji na ikiwezekana kumfungulia sehemu moja
ambayo atakuwa anafanya biashara yake kwa kutulia na kuaachana na
kutembeza barabarani anavyofanya hivyo anahatarisha maisha yake
kwani anaweza kupata ajali kugongwa na hata kuibiwa mtaji wake mdogo
ambao ameukusanya kwa ajili ya kumkimu kimaisha.

Kwa upande wa mama yake Beatrice Imanuel alisema kuwa mtoto wake
Baraka alizaliwa na ulemavu wa macho lakini anashukuru Mungu
amejikubali na anajitambua pia anaweza kujituma hata kufanya biashara
tofauti na walemavu wengine ambao wengi wao wanaombamba omba tu
barabarani na hawana mawazo wa kugundua mradi wowote au biashara
yeyote ambayo inaweza kuwasaidia katika maisha.

Anaongeza kuwa kijana wake amekuwa ni mtu wa kumsaidia katika baadhi
ya maitaji hapo nyumbani kwani amekuwa akinunua vitu mbalimbali na
hata mda mungine wadogo zake wakiumwa na yeye anafedha za kuwapeleka hospitali amekuwa akimega sehemu ya mtaji wake na kuutumia kwa jili ya kuwapeleka hospitali.

Beatrice ametoa wito kwa baadhi ya watu wenye ulemavu na kuwaambia
wasijizarahu pindi wanapokuwa walemavu bali wajaribu kuangali kitu cha
kufanya ambacho kitawakwamua kimaisha na kuachana na biashara ya kukaa na kuomba omba barabarani, pia aliwataka wazazi ambao wanawatoto ambao wanaulemavu wasiwafiche watoto wao ndani bali wawatoe nje wakapate elimu kama vile watoto wengine wanavyopata elimu kwani iwapo watapata elimu itawasaidia kujiongeza katika maisha.

“Nina imani mtoto wangu kama angekuwa hajapata elimu basi asingeweza
kuniomba hela ya mtaji na kujiamini na kwenda kuanzisha biashara
ya kuuza viberiti hii imetokana na kujiamini kwakwe na ndio maana
akaamua kujitoa na kwenda barabarani kufanya biashara naimani huu
wote ni ujasiri ambao alijengewa na walimu wake wakati alipokuwa
shuleni, na kwakweli ananisaidia sana katika maitaji madogo madogo
hapa nyumbani “Alisema Beatrice.

Baadhi ya wananchi ambao wanamshuhudia kijana
Baraka walimpongeza jinsi anavyofanya kazi na kusema kuwa ni vijana
wachache wenye ulemavu ambao wanaweza kujiongeza na kuanza kufanya
biashara kama vile kijana Baraka anavyofanya biashara, huku wengine
wakisikika wakisema ni bora angetafuta biashara ya kukaa sehemu moja
na kufanya na sio kutembeza kwa ajili ya usalama wa maisha yake.


Picha zikionyesha kijana Baraka Imanuel akiendelea kufanya biashara yake ya viberiti katika maeneo mbalimbali ya jiji la Arusha.

MENEJA KLABU YA SIMBA ASIMULIA KIPIGO CHA MWADUI FC, AWEKA BAYANA MCHEZO DHIDI YA MBEYA CITY, KAGERE NJE

$
0
0
Kikosi cha Simba.

Na Said Mwishehe, Michuzi TV
BAADA ya kupokea kichapo cha goli moja kutoka kwa timu ya Mwadui FC ya Mjini Shinyanga, uongozi wa Klabu ya Simba umesema kwa sasa akili zote wamehamishia katika michezo inayofuata kwa kuanza na timu ya Mbeya City ya jijini Mbeya.

Tangu kuanza kwa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu Kikosi cha Simba kilikuwa hakijapoteza mchezo , hivyo Mwadui wamefanikiwa kushinda mchezo huo uliofanyika mkoani Shinyanga.

Akizungumza leo Novemba 1, 2019 jijini Dar es Salaam Meneja wa Klabu ya Simba Patrick Rweyemamu amesema kuwa baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Mwadui wameelekeza nguvu zao katika mchezo wao na Mbeya City utakaopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumapili ya wiki hii.

Amesisitiza kuwa wamejipanga na wachezaji wako fiti kukabiliana na Mbeya Citykwani wanachotaka ni kushnda mchezo huo na benchi la ufundi limejipanga vema. Hata hivyo amesema mshambuliaji wao Medie Kagere ataukosa mchezo dhidi ya Mbeya City kutokana na kuwa na kadi mbili za njano ikiwemo aliyoipata katika mchezo na Mwadui FC.

Kuhusu kufungwa na Mwadui FC, Meneja huyo wa Klabu ya Simba amesema hivi "Kwanza nieleze tu kufungwa na Mwanadui ni matokeo ya mchezo wa soka kama tunavyofahamu kuna kushinda, kufungwa au kutoka sare.Tumepoteza mchezo huo na ni matokeo ya mpira".

"Kipindi cha kwanza tulicheza vizuri lakini kipindi cha pili hatukucheza kama inavyotakiwa licha ya kufanya mashambulizi ya mara kwa mara.Benji la ufundi litafanyia kazi maana wameshajua tatizo lilikuwa wapi,"amesema.

Alipoulizwa huenda Simba wamepoteza mchezo huo kutokana na ubovu wa kiwanja kilichotumika kwenye mchezo huo, Rweyemamu amejibu sababu sio kiwanja na kwamba viwanja karibu vyote nchini vinafafa na ndio viwanja vyetu."Kiwanja haikuwa tatizo, tusitafute sababu."

Ameongeza anachoweza kueleza spidi ya klabu ya Simba imepunguzwa sana kutokana na kufungwa na mwadui. Hata hivyo mpira ni mchezo wa kushangaza kwani usiyemdhania ndio huyo huyo anaweza kukufunga na ndicho ambacho kimetokea.

KOCHA MKUU TAIFA STARS ATAJA MAMBO MATATU TANZANIA KUFANIKIWA KATIKA SOKA

$
0
0
Kocha Mkuu wa Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Etienne Ndayiragije

Na Said Mwishehe, Michuzi Blogu
KOCHA Mkuu wa Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Etienne Ndayiragije ametaja mambo matatu ya kufuatwa iwapo tunahitaji kuinua soka letu nchini.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Kocha Ndayiragije ameeleza kwa kina mambo ya msingi ambayo nchi yetu inatakiwa kufanya ambayo ni kuwekeza katika soka la vijana, pili viwanja vizuri vya soka na tatu kila mdau wa soka atimiwe wajibu wake.

Akifafanua zaidi amesema kuwa ili kuwa na timu nzuri kwenye vilabu vya Tanzania na kukuza soka, ni vema eneo la kuweka kwa vijana likapewa kipaumbele kwani ndioko ambako wachezaji wazuri wanaandaliwa vya kutosha na hatimaye kupata timu bora kwa ajili ya michuano ya kimataifa.

Kuhsuu viwanja vizuri, Kocha huyo amesema ili kuwa na wachezaji wazuri na walioandaliwa lazima wapate viwanja vilivyokuwa na viwango vya soka."Uzuri wa kiwanja cha soka ni eneo muhimu sana, hivyo ni vema kwa vilabu vya soka nchini Tanzania kuona ni namna gani wanaweza kuwa na viwanja vizuri kwa kushirikiana na wadau wengine wa soka.Kwangu ubora wa kiwanja ni jambo muhimu katika kukuza soka la nchi husika."

Pia amesema jambo la tatu ili kufanikiwa katika soka ni kuhakikisha wadau na wapenda soka wanatimiza wajibu wao kikamilifu ambapo amesema waandishi wa habari za michezo na wachambuzi wa soka wanatakiwa kutimiza wajibu wao, Shirikisho la Mpira wa Miguu nao watimize wajibu wao na makocha nao wafanye kazi yao kikamilifu.

"Kila mmoja akitimiza majukumu yake nina uhakika tutapiga hatua sana katika medani ya soka.Hivyo nishauri kila mmoja awe na jukumu la kuhakikisha anakuwa sehemu ya kufanikisha wajibu wake kwa ajili ya nchi,"amesema Kocha Ndayiragije.

Hata hivyo ametumia nafasi hiyo kueleza katika kazi yake ya ukocha amefundisha katika nchi tisa za Bara la Afrika lakini alichobaini Tanzania kuna vipaji vya hali ya juu vya soka, hivyo kikubwa ni kuwekwa mikakati thabiti kuendeleza vipaji hivyo.

Pamoja na uwepo wa vipaji vya soka, ameonesha hofu kutokana na vilabu vingi kukosa uwezo wa kutosha katika kuendeleza vipaji hivyo akitoa mfano kuwa mchezaji anaweza kuwa na kipaji na yuko katika klabu ambayo haina uwezo mkubwa kifedha, hivyo ikitokea klabu yenye uwezo inamchukua na akifka hapati nafasi, hivyo matokeo yake kipaji kinapotea.

MKURUGENZI MTENDAJI WA MCL FRANCIS NANAI ATOA SOMO KWA WAFABIASHARA KWENYE JUKWAA LA DAR BUSINESS EXPO 2019...

BENKI YA CRDB YATANGAZA KUPATA FAIDA YA BILIONI 92

HARMONIZE ALIVYOTAMBULISHA "UNO" KWA MARA KWANZA KWA MASHABIKI ZAKE, MBAGALA

Miezi 15 ya mradi wa elimu kwa vishikwambi wakamilika

$
0
0
SERIKALI imetaka watoto wote walioshiriki katika mradi wa XPRIZE-Unesco wa kujua Kuandika, Kusoma na Kuhesabu kwa kutumia Vishikwambi katika mradi wa majaribio mkoa wa Tanga kuhakikishwa wanaendelea na elimu katika shule shirikishi za mkoa huo.

Mradi huo wa XPRIZE umekamilisha awamu yake ya miezi 15 na mafanikio yake ni makubwa.

Akizungumza mjini Korogwe wakati wa kufunga mradi huo, Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said alisema kwamba mradi huo ulilenga kupeleka elimu kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu unastahili kuingia awamu ya pili kabla ya mafanikio yake kusambazwa nchi nzima.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Bi. Zena alisema kwamba kwa sasa wanafanya mchakato wa kuwa na awamu ya pili ya mradi huo ambao utaondoa changamoto zilizopo kabla ya kusambazwa nchini kote.

Mradi huo ulioanza Desemba 2017 umefikia mwisho wake Aprili mwaka huu na umeelezwa kuwezesha watoto walioshiriki kufanya vyema katika masomo hayo waliojifunza bila Mwalimu kwa kutumia michezo iliyopo kwenye Vishikwambi.

Watoto wanaohusika ni wa miaka 5 mpaka 12. Imeelezwa kuwa kwa matumizi hayo ya Vishikwambi na mafanikio yake inaonesha kuwa njia nyingine ya kurejesha watoto wengi waliokosa elimu, darasani kwa kutumia teknolojia upo sahihi.

Bi. Zena alisema hakuna shaka kwamba elimu ni muhimu na kutokana na ukweli huo, mradi umedhirisha uwezo wake wa kusaidia wasioipata kwa kawaida kuipata. Katika kuimarisha kwenye mchakato wa pili kwa kuangalia matatizo yaliyopunguza kasi, serikali inaona Vishikwambi vibaki shule kwa usalama na pia walimu kutumika kuwezesha watoto wengi zaidi kujua kwa kasi KKK huku wakiimarisha uwezo wao wa kutumia teknolojia kujilete maendeleo.

Alisema pamoja na kunufaisha watoto mradi huo pia umefanikiwa kisaikolojia kushawishi watoto zaidi kupenda kusoma na kuanza mapema kutengeneza uongozi hasa kwa vijana ambao kutokana na kujua kusoma wamekuwa maarufu katika vijiji vyao.

Alitaka pamoja na kumalizika kwa mradi huo, wasimamizi wa sola katika vitongoji 170 kuhakikisha kwamba wanatunza sola hizo ili kusaidia vijana hao na watu wengine kufanyia kuchaji.

Mafanikio ya mradi huo kunaongeza nafasi zaidi kwa mujibu wa sera ya serikali ya kuhakikisha kwamba watoto wote hata wale ambao hawakuingia katika mfumo rasmi wanaingiza katika mfumo wa elimu kwa kupitia taratibu mbalimbali. Kwa sasa taratibu hizo ni utaratibu wa Memkwa kwa elimu ya msingi na Mespa kwa sekondari

Mradi huo ambao umefungwa ni sehemu ya mradi wa majaribio wa dunia ambapo teknolojia inajaribiwa kusaidia wale waliokosa nafasi ya kuingia shule.

Wakati mradi huo unaanza mwakilishi wa Global Learning Xprize, Elianne Philibert  alisema kwamba mafanikio yake yatawezeshwa kutengenezwa kwa moduli za kufundishia watoto walio nje ya mfumo rasmi wanaotumia lugha ya Kiswahili.

Washiriki wa mradi huo wa XPRIZE chini ya uangalizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula (WFP) na Kamati ya kitaifa inayohusisha pia Wizara ya Elimu imelenga kuwapata watoto ambao wanaweza kuingizwa darasa la pili na kuendelea na pia kuongeza uwezo wa kumudu masomo kwa watoto wa darasa la pili. Mradi huo ni matokeo ya mashindano Global Learning XPRIZE yaliyozinduliwa na Taasisi ya XPRIZE Septemba 2014.

Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos alisema katika hafla hiyo kwamba mradi huo  ulisohirikisha wilaya sita za Handeni, Korogwe, Lushoto, Mkinga, Muheza, na Pangani umekuwa na mafanikio kutokana na kujitoa kwa wadau wa mradi huo na wale ambao wamepelekewa.

Alishukuru serikali ya Tanzania kwua kushiriki katika shindano na pia kutekeleza malengo ya mradi huo. Alisema mradi huo ni utekelezaji wa wazo la UNESCO kwamba elimu ni tumaini jema  lakufikia maendeleo.

“Mradi wa XPRIZE umedhirisha kwamba mafunzo au utoaji elimu kwa watu ambao wamekosa au wana mazingira magumu unaweza kuboreshwa kwa ubunifu wa watoto kujifunza wenyewe kwa kutumia mifumo ya komyuta kama ilivyokuwa kwa vishikwambi “ alisema Tirso.

Alisema kabla ya mradi huo washiriki wake asilimia 74 walikuw ahawajwahi kugusa jingo inaloitwa shule, asilimia 80 walikuwa wanajifunza nyumbani na asiimia 90 walikuwahawawezi kusoma hata neon moja la Kiswahili ambalo ni lugha yataifa.

“Baada ya miezi 15  namba hizo zimepunguzwa kwa zaidi ya nusu huku watoto hao wakijifunza takribani sawa na watu walioshiriki darasani kwa kipindi cha mwaka mzima” alisema.

Kutokana na mafanikio hayo UNESCO imeitaka Wizara ya Elimu kusambaza zaidi wazo la mradi huo ili kuwafikia watoto wengi zaidi waliopemnbezoni na mazingira magumu yamaisha.

Naye Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais Tamisemi ambaye alimwakilisha Naibu Katibu Mkuu Elimu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Gerald Mweli, Bi Odilia Mushi alisema kwamba mradi huo umefanikiwa na kwamba nia ya serikali kuuimarisha na kuutambua zaidi kabla ya kuutawanya nchini.

Alisema pamoja na kuibua hamasa, ushuhuda wa watoto wenyewe unaonesha kwamba teknolojia inaweza kutumika kufungua maeneo yenye matatizo ya kufikika.

Aidha Ofisa Elimu mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu akimkaribisha mgeni rasmi alisema kwamba watoto ambao walikuwa wamekosa elimu wamepata faida kubwa ya mradi huo hasa wa kujua kuandika kusoma na kuhesabu.

“Hawawezi kuandika kwa kutumia kalamu lakini wanaweza kuandika kwa kutumia Vishikwambi na ni hatua kubwa ya kujua teknolojia na matumizi yake” alisema.

Mmoja wa wazazi Stella Ernest, aliishukuru serikali ya awamu ya Tano kwa kuwezesha kuwapo kwa programu hiyo ambayo imewatoa kimasomaso. Alisema watoto wamekuwa werevu zaidi na kutambua mambo katika hali ya kisasa kuliko awali.

Alisema hata mtoto wake mdogo siku hizi kwa kufurahishwa na michezo iliyopo katika Vishkwambi hivyo anapoamka humuuliza mama yake kama anajua kuandika Ameitaka serikali kuboresha zaidi mradi huo na kuufanya kuwa endelevu ili kusaidia watoto wengi zaidi. Aidha alitaka watoto waliobahatika kupata kujifunza wenyewe kupokewa na kuendelezwa zaidi.

Kauli hiyo pia imetolewa na mzazi mwingine Janeth Massawe ambaye alisema mradi huo ni wa mfano kwani umewasaidia kuwaondolea tatizo la elimu katika eneo lao. Alisema mradi huo umepokewa vyema na kwamba umewachagiza kutambua umuhimu wa elimu.
 Mgeni rasmi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Zena Said akitoa hotuba wakati wa kufunga wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE- uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos akitoa salamu za UNESCO wakati wa kufunga wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa kitengo cha Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Faith Shayo akifafanua jambo wakati wa kufunga wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI ambaye alimwakilisha Naibu Katibu Mkuu Elimu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Gerald Mweli , Bi Odilia Mushi akizungumza wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mtoto Habiba Athumani (13) mkazi wa kijiji cha Tabora wilayani Korogwe akitoa ushuhuda kwa wageni waalikwa kuhusu mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
Mtoto Ismail Adamu (13) mkazi wa kijiji cha Majengo wilayani Korogwe akitoa ushuhuda kwa wageni waalikwa kuhusu mradi wa XPRIZE- uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mmoja wa wazazi Stella Ernest ambaye mtoto wake amenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi akitoa ushuhuda wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mmoja wa wazazi Hassan Shomari ambaye mtoto wake amenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi akitoa ushuhuda wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na wazazi ambao watoto wao wamenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
Baadhi ya watoto ambao wamenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Baadhi ya wadau wa sekta ya elimu walioshiriki katika hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos wakitiliana saini na Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (kushoto) ya hati ya makabidhiano ya mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa kufunga mradi huo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (kulia) akimkabidhi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (wa pili kulia) ripoti ya utekelezaji wa mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Hilary Bitwaye (kushoto), Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi Odilia Mushi.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi Odilia Mushi (wa pili kulia) ripoti ya utekelezaji wa mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (wa pili kushoto) pamoja na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (kushoto).
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (kulia) akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Hilary Bitwaye (katikati) ripoti ya utekelezaji wa mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi Odilia Mushi.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (wa pili kulia) akimkabidhi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (katikati) funguo za gari la mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa kitengo cha Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Faith Shayo (kulia), Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi. Odilia Mushi (kushoto) pamoja na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (wa pili kushoto).
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (katikati) akimkabidhi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (wa pili kushoto) gari la mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bi. Odilia Mushi (kushoto), Ofisa Elimu mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu (wa pili kulia), Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (kulia).
 Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (aliyeshika usukani) na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bi. Odilia Mushi  wakiwa ndani ya gari la mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP mara baada ya kupokea gari hilo kutoka UNESCO wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
Meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto  wa halmashauri ya Korogwe walionufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.


Benki ya Exim Yajizatiti kuhudumia sekta korosho Mtwara

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mtwara-Mikindani  Bw. Emanuel Mwaigobeko akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki ya Exim Tanzania kwa ajili ya wadau wa zao la korosho mkoani Mtwara iliyolenga kupata wasaa wa kujadili fursa mbalimbali za kibiashara hususani katika zao hilo pamoja na  uboreshaji wa huduma zitolewazo na benki hiyo kwa wadau hao mkoani humo.

 Mmoja wa wadau wakubwa wa Korosho mkoani Mtwara Bw Ramesh Kennedy akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki ya Exim Tanzania kwa ajili ya wadau haoili kupata wasaa wa kujadili fursa mbalimbali za kibiashara hususani katika zao hilo pamoja na  uboreshaji wa huduma zitolewazo na benki hiyo kwa wadau hao mkoani humo.
Mkuu wa huduma ya rejareja wa benki ya Exim, Bw. Andrew Lyimo (wa kwanza kushoto) pamoja na Mkuu wa Hazina na Masoko ya Fedha wa benki hiyo Bw Arafat Haji (wa kwanza kulia) wakiwaongoza wageni waalikwa akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mtwara-Mikindani  Bw. Emanuel Mwaigobeko (alievaa suti nyeusi) kupata chakula wakati wa hafla hiyo.

Mtwara ; Octoba 31, 2019: Benki ya Exim Tanzania mapema wiki hii iliandaa hafla ya chakula maalum kwa ajili ya wadau mbalimbali wa zao la korosho mkoani Mtwara ili kupata wasaa wa kujadili fursa mbalimbali za kibiashara hususani katika zao hilo, mipango ya ukuaji na uboreshaji wa huduma zitolewazo na benki hiyo kwa wadau hao mkoani humo.
Akizungumza kwenye hafla hiyo iliyohudhuliwa na wadau mbalimbali wa zao la korosho wakiwemo viongozi wa kiserikali, wafanyabiashara wakubwa na wadogo pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo, Mkuu wa huduma ya rejareja wa benki ya Exim, Bw. Andrew Lyimo alisema kupitia hafla hiyo  walilenga pia  kutoa fursa miongoni mwa wateja hao ili waweze kufahamiana na kufungua wigo wa kufanya biashara pamoja.
“Pamoja na kushukuru kwa namna ambayo wateja wetu wamekuwa nasi hadi kufikia mafanikio ya kuikuaji na ubora wa huduma zetu, hafla hii inatoa fursa kwa wateja wetu pia kufahamiana wao kwa wao na hivyo kufungua milango ya fursa baina yao,’’ alisema Lyimo.
Alisema ukuaji wa benki hiyo unaoshuhudiwa kwasasa ni matokeo ya ushirikiano baina yake na wateja wake ambao kwa kiasi kikubwa wameonyesha imani kubwa kwa benki hiyo hali ambayo imekuwa ikiiwezesha benki hiyo kubuni huduma bora na rafiki za kibenki ili kulinda na kurejesha imani hiyo kwa wateja wa benki hiyo.
Pamoja na mambo mengine hafla hiyo ilipambwa na shuhuda mbalimbali kuhusu ubora wa huduma za benki hiyo kutoka kwa wadau hao.
Akizungumza kwenye hafla hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Bw. Emanuel Mwaigobeko alisema  mkoa huo umejipanga kwa dhati kuhakikisha ununuzi wa mkorosho unaenda vyema kwa kuzuia watu wachache kuharibu taswira ya serikali pamoja na sekta nzima ya kilimo cha zao hilo.
Pamoja na kuipongeza benki  ya Exim kwa namna inavyoshirikiana  na wadau wa zao hilo mkoani Mtwara, Bw Mwaigobeko alizitaka taasisi zinazohusika na masuala ya fedha mkoani humo kusaidia katika kuwajengea uelewa wa kutosha kuhusu masuala ya kifedha wakulima na wafanyabiashara wa zao hilo mkoani humo.
Alisema ni matarajio yake kwamba wakulima watakuwa waaminifu kupeleka korosho safi ili wasiharibu ubora wa korosho za Tanzania katika soko la ndani na nje.

MAHOJIANI YA BBC SWAHILI: MO DEWJI AWEKA WAZI SAKATA LA KUTEKWA

ACT WAZALENDO WAMSHAURI WAZIRI JAFO KUTATUA CHANGAMOTO KUELEKEA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

$
0
0
Mratibu wa Mawasiliano Taifa wa Chama cha ACT, Mbarala Maharagande (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Katibu wa Program za jamii taifa wa Chama cha ACT Wazalendo, Mwanaharusi Bunduki na kushoto ni Naibu katibu Mkuu Ngome ya  vijana Taifa ACT-Wazalendo, Boniphancia Mapunda.

Leandra Gabriel na Avila Kakingo,Globu ya Jamii
CHAMA cha ACT Wazalendo kimemshauri Waziri wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)Sulemani Jafo kutatua changamoto mbalimbali ndani ya siku zilizobaki kabla ya kuelekea uchaguuzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24 mwaka huu.

Akizungumza leo Novemba 1,2019 jijini Dar es Salaam Mratibu wa Mawasiliano Taifa wa Chama cha ACT, Mbarala Maharagande amesema kuwa Waziri Sulemani Jafo anapaswa kutambua kuwa kuna njama ovu na hujuma dhidi ya vyama vya upinzani kuhusu uchaguzi wa Serikali za mitaa unaoelekea kufanyika.

"Kuna tofauti kati ya hujuma au njama ovu na dosari au mapungufu, hujuma na njama ovu hizi zinafanywa dhidi ya vyama vya upinzani na wagombea wake pekee na hakuna lalamiko hata moja tulilolisikia au kushuhudia kutoka kwa CCM nchi nzima. Hii maana yake ni kwamba huenda hujuma hizo zinaratibiwa na Ofisi yake na wala hazitokei kwa bahati mbaya,"amesema Maharagande.

Amesema kuwa dosari zilizopo ofisi zinazosimamia uchakuguzi huo ikiwa ni kutokuwa na mihiri, kufungwa kwa ofisi, wagombea kutokupewa nakala za fomu za kugombea katika vijiji, kata na vitongoji. Ametaja maeneo yenye dosari hizo ambazo ni Ruangwa, Liwale, Bukombe, Songwe, Tabora, Busanda, Misungwi, Moshi Mjini, Morogoro Kusini Mashariki, Kasulu Vijijini, Tanga, Dar es Salaam, Newala, Mkoa wa Pwani na Mbeya.

"Tangu mchakato wa uchukuaji wa fomu uanze tarehe Oktoba 29, 2019 wanachama 276,401 wamejitokeza nchini kote kugombea nafasi za uongozi kupitia ACT-Wazalendo huku idadi hiyo ikiongezeka siku hadi siku na miongoni mwao kufanikiwa kuchukua fomu za kugombea".  Amesema Maharagande.

Pia Maharagande amesema Waziri Jafo achukue hatua dhidi ya viongozi watakaokiuka kanuni, taratibu, sheria na miongozo ya usimamizi wa uchaguzi.Hata hivyo amewaasa viongozi wa dini na wastaafu kuhimiza kutenda kwa Haki na kukemea viashiria vya kupotea kwa amani na utulivu kwani amani ni tunda la haki na pia kuamrisha kutenda mema kuendelea kukataza maovu.

Kwa upande wake Katibu wa Programu za Jamii Taifa wa ACT Mwanaharusi Bunduki amewashauri wasimamizi wa uchaguzi kupitia Serikali kuzingatia kanuni, sheria, taratibu na miongozo ya kusimamia uchaguzi hiyo ili kuendelea kuitunza amani ya nchi. 

Jeshi la polisi lamsaka mwananchi aliyetishia kwa bunduki

$
0
0

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii . 

Jeshi la Polisi limesema kuwa mtu aliyemtishia kwa bunduki anatafutwa na jeshi la polisi kutokana na kosa la kumiliki silaha. 

Kauli hiyo imetokana na kusambaa katika mitandao ya kijamii kuwepo kwa mtu mmoja kumtishia mwenzake kwa bunduki katika mazingira ambayo hayakuwa yanasababu ya mmiliki wa bunduki kutumia. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro amesema kuwa watu wamemilikishwa silaha sio kwa ajili ya kutishia watu wengine. 

Sirro amesema kuwa mtu huyo aliyemtishia anatafutwa, na silaha hiyo anatakiwa kunyang'anywa kutokana na kuitumia vibaya silaha hiyo ambayo  aliiomba. 

Aidha amesema kuwa wananchi wanaopewa silaha wanapaswa kuacha kutumia vibaya, kwani wanaomba kwa sababu maalum matokeo yake wanatumia silaha visivyo. 

"Watu wanatumia silaha visivyo,sasa Jeshi la polisi linamtafuta na popote akikamatwa sheria itashika mkondo wake kwa kutumia silaha vibaya kwa kutishia wananchi"amesema Sirro. 

Sirro amesema kuwa silaha hizo zimekuwa zikiombwa kwa sababu ambazo wanaamini ni kwa matumiza sahihi na salama,lakini kwa makosa yanayopatikana kwa baadhi ya watu wanaokiuka taratibu za matumizi ya silaha hiyo/hizo  hatua lazima zichukuliwe.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro 

TCRA yatoa elimu kwa Viziwi kuhusu matumizi salama ya mawasiliano

$
0
0
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa imeendesha semina ya siku moja kwa watu wenye matatizo ya kutosikia (Viziwi) katika Mkoa wa Simiyu yenye lengo la kuwajengea uelewa juu ya matumizi sahihi na salama ya mawasiliano.

Mafunzo hayo ambayo yamefanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ambapo zaidi ya viziwi 50 wameshirikia mafunzo hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa Kanda ya Ziwa wa TCRA, Mhandisi Francis Mihayo amesema kuwa TCRA imeandaa mafunzo hayo kwa viziwi ili waweze kuepuka na madhara ambayo wanaweza kupata ikiwa watatumia vibaya mawasiliano.

Mihayo ameongeza kuwa viziwi ni moja kati ya watu ambao wameendelea kukumbwa na tatizo la matumizi mabaya ya mitandao kama facebook, instagram, whatsap na twitter kwa kurusha vitu ambavyo siyo sahihi.

“ Mara nyingi wamekuwa wakijikuta wakichukuliwa hatua kali za kisheria kwa kikuka sheria zilizopo za matumizi sahihi ya mawasiliano, kutokana na hali tumeona ni vyema tukawapa elimu jinsi gani ya wanaweza kuepuka kwa kuzitambua sheria,” amesema Mhandisi Mihayo.

Aidha Mihayo amesema kuwa amekuwa wakipata malalamiko mengi kutoka kwa viziwi juu ya kutapeliwa kupitia simu, ambapo kupitia mafunzo hayo wataweza kuwafundisha namna bora ya kuepuka hali hiyo.

“ Tunawaelimisha pia umuhimu wa kusajili laini zao kwa njia ya alama za vidole, tunatambua changamoto wanazozipata katika zoezi hili, ndiyo maana tumewaita hapa ili kuwapatia elimu na kutatua changamoto hiyo,” alisema Mihayo.

Akizungumza kwa niaba ya viziwi hao Makamu mwenyekiti wa viziwi mkoa, Alex Benson viziwi wameeleza kukumbwa na tatizo la mawasiliano baina yao na watu wanaohusika katika zoezi la kusajili laini za simu kwa njia ya alama za vidole (Biometric Registration).

Wamesema kuwa tatizo hilo limesababisha viziwi wengi katika mkoa huo kushindwa kujisajili, kutokana na kushindwa kuelewana na watoa huduma wa makampuni mbalimbali ya simu wakati wa kujisajili kwa mfumo huo.

Bensoni amesema kuwa mbali na tatizo hilo, Bado Viziwi wameendelea kukumbwa na tatizo la kutapeliwa na watu wenye nia mbaya kupitia simu, ambapo alisema kupitia mafunzo hayo wataweza kutatuliwa changamoto hizo.

Akifungua mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga ameipongeza TCRA kwa kuona umuhimu wa zoezi hilo, kwani viziwi wanayo haki ya kupata elimu ya mawasiliano kama watu wengine.
 Afisa anayeshughulikia Masuala ya Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dorice Mhimbila akizungumza na watu wasiosikia wa mkoa wa Simiyu wakati mamlaka hiyo ilipokwenda kutoa elimu ya utumiaji wa mawasiliano


Baadhi watu wasiosikia (viziwi) wakiwa katika mafunzo ya utumiaji wa mawasiliano.
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images