Mratibu wa Tamasha la Krismas Mkoani Dodoma, John Banda akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya kukamilika kwa maandalizi ya tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika leo kwenye Uwanja wa Jamhuri,Mkoani Dodoma, Kushoto ni Mmoja wa waimbaji kwenye tamasha hilo Beatrice Wiliam (BSS 2011) Maandalizi ya Tamasha la Chrismas ndani ya Dodoma Tayari yamekamilika wasanii kibao tayali wapo Dodoma na Asubuhi ya leo wameshiriki ibada ya pamoja katika kanisa la Mlima wa moto Sabasaba Dodoma.
Josephine Sudai akionyesha uwezo wake wa kuimba ndani ya kanisa la mlima wa moto Dodoma kabla ya kuelekea uwanja wa Jamhuri kwenye tamasha hilo.
Jubilee Lugobo toka jijini Dar es salaam nae yupo Dodoma kwa ajili ya tamasha hilo
Lusekelo Mwandiga akiimba kwa mbwembwe ndani ya kanisa la mlima wa moto sabasaba Dodoma kabla ya kushiriki tamasha hilo
Mwanadada Rose Kimaro ndani ya tamasha hilo na hapa ni mlima wa moto sabasaba.