Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109597 articles
Browse latest View live

SOMO MURUA: MUZIKI WA TANZANIA UILIVYOANZA HADI ULIPOFIKIA

0
0
Na: Moshy Kiyungi, Tabora.

Septemba, 2019. Baadhi ya maneno yanayotumika Kimataifa yametokana na lugha zetu za Kiafrika, mfano wa karibu neno IKULU.

Neno hilo limetokana na hadhi ya nyumba ya makazi ya mtawala wa Watemi wa kabila la Wanyamwezi toka mkoa wa Tabora. Ikulu  linaonekana kurasimishwa kutumika sehemu zote zilizopo ofisi za makao makuu ya Viongozi wakuu wa nchi.

Nyumba ya rais wa Marekani ‘White House’ inaitwa IKULU ya Marekani nk.

Maneno mengine yalitoholewa toka lugha za Wakoloni, mfano neno ‘Muziki’ ambalo lililetwa hapa nchini na Wajerumani.

Hii ilitokana na bendi zilizokuwa za askari na kuingizwa katika shule ya kwanza ya Serikali ya Tanga, ikiitwa ‘Tanga School’ wakati huo.

Madhehebu mbalimbali ya dini nayo yalichangiza kuingiza muziki na vyombo vya muziki vipya vilivyotoa mchango katika huu muziki.

Neno Kwaya lilitokana na neno la Kiingereza yaani ‘Choir’, nazo zikaanza kushika kasi.

Tofauti na hivi sasa ambapo baadhi ya makabila yanabeza nyimbo na ngoma za utamaduni wao wakidai ati zimepitwa na wakati!

Utakuta siku za sherehe za harusi wakipiga miziki ya taarab, hip hop, taradansi, na sasa hivi wamebuni ‘Singeli’

Mfano wa karibu ni watu wa kabila la Wanyamwezi toka Tabora, miaka hii hawahitaji kuzisikia kitu kinaitwa ngoma za asili za kabila lao Manyanga, Maswezi, Radu ama Ngelo ambazo zamani ndizo zilikuwa zikitoa burudani maridhawa katika sherehe mbalimbali.

Mbaya zaidi hata kuongea lugha yao ya Kinyamwezi wanajisikia ‘Kichefuchefu’, aibu ama eti ni ushamba kuzungumza lugha yao!

Lakini historia inaeleza kuwa Wajerumani hawakuzuia muziki au ngoma za kiasili, muziki mpya na wa kiasili vyote vilienda sambamba.

Ulipoingia utawala wa Mwingereza, ulileta mabadiliko mengi katika muziki kutokana na vita vya dunia. Askari waliotoka vitani (King Africans Riffles) maarufu kama KAR au KEA, walirudi wakiwa na hadithi kuhusu muziki,.

Vyombo vya muziki na hata mtindo wa muziki walioukuta katika safari zao za kivita, vyombo kama vile Akodian na Magitaa makavu (yasiyotumia umeme) yaliingia nchini.

Magitaa ya umeme katika bendi za muziki wa dansi yalianza kutumika kati ya mwaka 1957 na 1959.

Bendi ya Dar es Salaam Jazz hutajwa kama ilikuwa ya kwanza ya muziki wa dansi kuanza kutumia gitaa hilo, ikifuatiwa na bendi ya Western Jazz na zinginezo zikafuatia.

Wakati huohuo zaidi ya makabila mbalimbali kuchanganyikana na miji kuanzishwa, ndipo mwanzo wa kuzaliwa kwa Utamaduni mpya.

Muziki uliokubalika kwa makabila yote ni bendi mbalimbali zilizoanzishwa katika ukanda mzima wa Afrika ya Mashariki.

Wasomi wa Kiafrika wakawaiga Wazungu kwa kutengeneza klabu zao ambazo zilikuwa maarufu kama ‘Dancing Clubs’.

Huko zilipigwa nyimbo mbalimbali kwa kutumia santuri na kucheza mitindo mbalimbali kama vile Chacha, Tango, Foxtrot, Swing, Waltz na kadhalika.

Inaamainika klabu ya kwanza Tanganyika ilikuwa mjini Tanga iliyokuwa ikiitwa ‘Young Novelty Dancing Club’. Baadaye ikaanzishwa Dar es Salaam ‘Young Generation Dancing Club’.

Klabu hizo ndizo chanzo cha bendi ya kwanza ya

Dar es Salaam Social Orchestra, ambayo baadaye ikawa bendi maarufu yaani Dar es Salaam Jazz Band.

Bendi hiyo ilikuja kujizolea umaarufu mkubwa wakitumia mtindo wa ‘Mundo’ huku wakijita ‘Majini wa Bahari’.

Nyingine ilikuwa YMCA Social Orchestra, kati ya miaka ya 1920 na 1935.


Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia kumalizika mwaka 1945, Wamarekani waliweka radio yenye nguvu katika mji unaoitwa Kinshasa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.


Radio hiyo iliweza kusikika sehemu nyingi Afrika Mashariki, Kati na Magharibi, ikawa mwanzo wa Lebo maarufu ya Longisa nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo. Mwaka 1947 Lepodiville ambao sasa unaitwa Kinshasa, ukajulikana kama mji wa starehe.

Ikawa ndiyo sababu ya kuingwa muziki wa Kikongo, wakati huohuo Marekani ikijizatiti kueneza utamaduni wake sanjari na Ufaransa ikieneza muziki wa Jazz kwenye makoloni yake.

Lebo ya Galotone ya Afrika Kusini pia ilisambaza santuri ambazo ziliingiza mtindo wa Jive nchini.

Miaka mingi ya nyuma ilishuhudiwa vijana walikuwa na vikundi wakicheza mtindo huo wa Jive. Aidha bendi kadhaa ziliiga upigaji wa filimbi kumuiga mwanamuziki Spokes Mashiyane.

Mwaka wa 1954, Kenya ikaanza kuwa kituo cha kikubwa cha kurekodi muziki. Miaka mingi baadaye bendi za Afrika Mashariki zililazimika kwenda ili kufyatua santuri maeneo ya Kericho nchini Kenya.

Kuna baadhi ya wanamuziki hadi leo hufikiriwa kuwa ni Wakenya au walitoka Kenya. Mfano ni Frank Humplink na dada zake ambao walitoa vibao ambavyo bado vinasikika katika anga za muziki, kama ‘Embe dodo’, ‘Tufurahi Harusi’ na nyingine nyingi.

Mara baada ya nchi yetu kujipatia Uhuru mwaka 1961, pamoja na mapungufu yanayotajwa ya utawala wa Chama kimoja, kulikuwapo na mazuri mengi kutokana na chama hicho kuwa na dira inayoeleweka.

Kilielekeza kila kitu kadri ya matakwa yake jambo hilo lilikuza muziki humu nchini.

Sanaa ya Tanzania haikukwepa mwongozo wa chama tawala wakti huo cha TANU. Sehemu za kazi, vijiji, miji viliagizwa kuwa na vikundi vya utamaduni ambavyo vilikuwa ndivyo vikundi vya burudani baada ya kazi na pia kuelezea mipango na malengo ya chama na serikali.

Itakumbukwa kuwa miaka ya 1960, alikuwepo mhamasishaji maarufu mzee Makongoro, ambaye alikuwa akiimba nyimbo zenye mafunzo makubwa kwa jamii. Mmoja ya tungo yake ni ile “Dereva kalewa pombe”

Wakati huo ziliundwa bendi za majeshi kama vile Polisi Jazz



, Mwenge Jazz aliyo chini ya  JWTZ,  Magereza Jazz,  JKT Kimbunga na Kimulimuli pamonja na Uhamiaji.

Mashirika ya Umma nayo hayakuachwa kupewa maelekezo ya kuanzisha bendi. Shirika la Bima la Taifa (NIC), ilianzisha bendi ya Bima Lee, Shirika la Maenedeleo Dar es Salaam nalo likaanzisha bendi ya DDC Mlimani Parck Orchestra. Shirika la Usafiri Dar es Salaam nalo likawa na bendi ya UDA Jazz ikitumia mtindo wa ‘Bayankata’. Bodi ya Biashara ya Nje (BET) ilinzisha bendi ya Biashara Jazz, Kiwanda cha kukata Alimasi cha Iringa, nacho kilikuwa na bendi ya Tancut Alimasi Orchestra na nyingine nyingi.

Baadhi ya miji nayo yakaanzisha bendi zao kama ilikuwa bendi ya Kurugenzi ya Arusha na Kurugenzi ya Dodoma.

Bendi zilitunga na kuimba nyimbo zambazo zilipitiwa kabla ya kurekodiwa na kurushwa hewani tofauti na nyakati zilizofuatia.

Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD), ndiyo ilikuwa pekee ikitangaza na kupiga kila aina ya muziki wa nchi hii, tofauti na sasa ambapo kuna vituo vingi vya radio, lakini vimeshindwa kufanya kazi hiyo iliyoweza kufanywa na kituo kimoja cha Taifa. 

Mwanzoni mwa miaka ya 1960, baadhi ya bendi ziliingia kwenye utamaduni wa kunakili nyimbo za kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.  

Bendi hizo ziliiga mirindimo ya vyombo vya nyimbo walizonakiri kilichobadilika ni kuimba kwa lugha ya Kiswahili.

Mathalani nyimbo za “Lau Nafasi”, “Mtoto wacha kupiga Mayowe”, “Nachekacheka Kilwa”, “Rosa” na nyingine nyingi.

Pamoja na hayo kulikuwako na wanamuziki waliokuwa wakifuata nyayo za nchi za Magharibi na baadaye wakachangaya vyombo na milio ya kiasili, ukazaliwa muziki wa Afro Rock, sambamba na nchi nyingine katika Afrika.

Kipindi hicho mwanasiasa mmoja aliamua kupiga marufuku muziki wa Bugi, ambao ulikuwa ni maonesho ya muziki ya mchana yaliyokuwa yakimalizima majira ya saa kumi nambili jioni. Kupiga marufuku muziki huo ilikuwa ni sawa na leo upige marufuku wanamuziki wa kizazi kipya, pengo hilo halijazibika hasi leo.

Miaka ya 1980 na 1990 kulikuwa na mfumo wa utawala wa shughuli za utamaduni, ambao pamoja na kuweko maofisa Utamaduni wa Wilaya, Mkoa, pia kulikuweko na Baraza la Muziki la Taifa (BAMUTA).

Pia kulizaliwa vyama ambavyo vilifanya kazi kubwa ya kuunganisha wanamuziki kama vile Chama cha Muziki Tanzania (CHAMUDATA) na Tanzania Taarab Association.

CHAMUDATA ailiandaa maonesho makubwa yaliyounganisha wanamuziki nchi nzima, yaani “Top Ten Show” Kama ilivyo nchini Marekani.

Maonesho hayo yaliwezekana kwa ushirikiano mkubwa na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Umoja wa Vijana na Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD). Halijawahi kutokea tena maonesho hayo yenye ukubwa wa aina hiyo hadi leo.

Kuvurugika kwa mfumo wa uongozi wa utamaduni umeacha shughuli za utamaduni mkononi mwa wafanyabiashara pekee, ambao lengo ni kupata faida za kiuchumi, matatizo na matokeo ya kufa kwa utamaduni si lolote kwao.

Serikali inatakiwa ichukue mzigo huu wa kufadhili au kusimamia ukuaji na uendelezaji wa utamaduni. Kuacha shughuli za biashara ya kazi za sanaa kwa wafanyabishara peke yake, hivi sasa mtoto wa Kitanzania anauelewa zaidi muziki na Utamaduni wa nje hasa wa Kimagharibi kuliko wake.

Nyakati hizo ndizo zilizozaa muziki wa kizazi kipya, maarufu kama Bongo Fleva, ambapo kuna mapinduzi makubwa sana katika muziki wa nchini Tanzania.

Bendi nyingi za muziki wa dansi zimeanzishwa, hasa kwa wale wakongwe na kuunda bendi zao binafsi.

Mfano ni Mafumu Bilal, Hussein Jumbe, Rashid Pembe, Banana Zorro, LadyJay Dee, Deo Mwanambilimbi na wengine wengi.

Kila kizuri kina athari zake.

Kukua kwa teknolojia na kuanza matumizi ya kompyuta katika utayarishaji wa muziki, kumeua vipaji na muziki kwakuwa yeyote anaweza kurekodi pasipo kubughudhiwa.

Vijana wameshika hatamu na muziki huu wa kizazi kipya, bila utaalamu wa kutaka kupiga ala za muziki kwa kuwa kila kitu kinafanywa na mashine za kisasa.

Miaka ya nyuma tulishuhudia bendi kubwa ya OTTU Jazz wakati huo, ilitumia mtindo wa ‘Discipline’, walitingisha mno baadhi ya wapenzi wa muziki wa dansi miaka hiyo.

Mabadiliko makubwa yakaaza kuonekana baada  kuundwa kwa taasisi au kampuni kubwa za uburudishaji wa muziki kama vile Radio One, Clouds FM, Radio Uhuru, Times FM, Radio Free Africa (RFA) na nyingine nyingi.

Kati ya miaka ya 1970 na 1980, bendi za Maqius du Zaire, Makassy Orchestra, Orchestra Safari Sound, MK Group, Zaita Muzica, The Bantu Group, La Capitale, bado ipo ikiongozwa na King Kiki, Bana Maquis nayo ipo ikiongozwa na Tshimanga Assosa, Maquis Original, Orchestra Kamanyola ipo jijini Mwanza, zote zilikuwa na wanamuziki wengi toka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Baadhi ya wanamuziki hao ni Kitzengu Makassy ‘Mzee Makassy”, Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kiki’, Baziano Bweti,  Fred Ndala Kasheba, Ramadhan Mtoro Ongolla ‘Dk. Remy’, Kabeya Badu,  Mukumbule Lolembo ‘Parash’, Mutombo Lufungula ‘Audax’, Mbuya Makonga ‘Adios’Mukuna Roy, Mbombo wa Mbomboka, Kaumba Kalemba, Ilunga Lubaba. Ilunga Banza ‘Banza Mchafu’, Radi Massiya ‘Dikubakuba’, Maliki Star,  Pulukulu Wabandoki ‘Motto’ Kalala Mbwebwe, na Chimbwiza Mbangu ‘Nguza Vicking’.

Wengine ni pamoja na Chinyama Chiyaza, Massiya Radi ‘Dibakubakuba’, Dekula Kahanga ‘Vumbi’, Moses ‘Fan Fan’, Tchimanga Assosa, mapacha waliokuwa na mvuto wa kipekee Kasalo Kyanga na Kyanga Songa  na wengine wengi.

Idadi kubwa ya vijana waliozaliwa miaka ya 1980 na 1990 mwanzoni, walianza hamasa ya kuwa wanamuziki na kujishughulisha na kazi hiyo kwa kasi.

Kipindi hicho ndicho kulitokea makundi mbalimbali ya muziki wa Hip hop, hii ikiwa ni pamoja na Gangwe Mobb, Dewplomatz, S.O.S Kwanza Unity, Underground Soulz, Hard Blasters na nyingine kibao.

Ilipotimu miaka ya 2000 na 2010, muziki uliokuwa juu sana ni wa ‘Bongo Fleva’ na muziki wa dansi ambao hasa vijana wapya au kitambo wakarudi kwa kasi kipindi hicho.

Baadhi ya bendi zilizojaribu kuja kivingine katika kipindi cha miaka ya 1990 katikati na mwishoni, zilirudi ama kuvuma kupita kiasi.

Mathalani, African Revolution iliyotumia mtindo wa ‘Chumvi Chumvi Tutalamba’ ilirudi na mtindo wa ‘Tam-Tam’ chini ya uongozi wake Muumini Mwijuma ‘Kocha wa Dunia’, Mchinga Sound, Diamond Sound, Akudo Impact, Double Extra iliyokuwa ikiongiozwa na Ali Choki, Bwagamoyo Sound, Tanzania One Theatre (TOT Plus Band), Tabora Jazz ‘WanaSegere Matata’, Kiko Kidds, Nyanyembe Jazz, Dodoma International.  Tatu Nane, Butiama Jazz, The African Stars, African Survivors Band ikiwa na wimbo wao wa “Maproso”, Malaika Band, The Kilimanjaro  band  ‘Wana Njenje’, Inafrica Band na nyingine nyingi zilitingisha zama hizo.

Bendi ya Chuchu Sound ni miongoni mwa bendi zilizotamba sana mwanzoni mwa miaka ya 2000 ikiongozwa na Omar Mkali ‘Babu Chuchu’.

Waliimba na kucheza katika mtindo wao wa ‘Chakacha’ au ‘Mduara’ kwa lugha maarufu. Bendi hiyo ilikuwa tishio ‘ikikabana shingo na bendi ya The Kilimanjaro Band ‘Wana Njenje’ pamoja na bendi ya Kilimanjaro Connection.

Ushindani ulikuwa mkubwa mno wakati huo ambapo tulishuhudia wanamuziki au waimbaji wakihama kutoka bendi moja kwenda nyingine kufuatia utitiri wa bendi za muziki zilizokuwepo nchini.

Kipindi hicho ndicho alichokuja mkali wa sauti ‘King of Melody’ Christian Bella, akitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Ushindani katika muziki ulipamba moto, ikazaliwa bendi ya Stono Musica ‘Wanajelajela Original’ baadaye FM Academia chini ya uongozi wa Nyoshi El Sadat.

Kabla ya kuundwa kwa bendi hii, ilikuwa moja na Stono Musica kabla kutengena na Nyoshi akabaki na jina halisi lakini akaongezea neon la “The Dream Team”.

Marekani ikashika hatamu kueneza utamaduni wake duniani kwenye miaka ya 2000. Tanzania ikaupokea pakazaliwa neno muziki wa kizazi kipya, ukiacha wale walioanza kabla ya  mwaka 2000, wakapatikana akina Dully Sykes, Manzese Crew, Wandava Kumi Ngangari (W TEN N), Jay More, Ngwair, Daz Nundaz, Madee, Mandojo na Domo Kaya.

Wengine nia Mr. Blue, Complex, Dudu Baya, Mr. Nice, Juma Nature, FSG, AY, GK, Q Chilla, Mwanafalsafa, aliyejaribu kutunga mashairi ya asili, Malaika Band, Lady JDee, Rehema Chalamila ‘Ray C’ na wengine wengi.

LadyJDee na AY ni wasanii wa mwanzo wa kizazi kipya kuthubutu kutoka nje ya mipaka ya Tanzania, ilhali wakijivika wajihi wa Kimagharibi.

Kukosekana udhamini au kujitangaza vya kutosha, kundi kama Boyz from the Army, Born Crew, Hot Girls, Big Dog Pose(BDP), Hot Port Family, Wateule, Mambo Poa, Uswahili Matola na wengine walithubutu bila mafanikio, wakapotea.

Wachuja Nafaka lilikuwa kundi mradi tu (Super Group) lilodumu kwa kipindi kifupi. Wasanii wengine walitamba katika miaka ya 2001 hadi 2004 ni pamoja na Zahrani a.k.a Big Punisher, Spula, Bushoke, Mr. Nice ambaye kwa kweli alitamba kupita maelezo nyimbo za kuchukua ala za kitoto na kuzirudia katika mtindo wa Bongo Fleva, alitamba nao kwa jina la “TAKEU”.

Mr. Nice akauvusha muziki huo mbali sana, hususan katika nchi za Burundi, Kongo (DRC), Rwanda na nchi nyingine za Afrika, japokuwa hakudumu sana katika ‘game’ la muziki.

Profesa Jay, ambaye hivi sasa ni Mbunge, kwa upande wa msanii wa kiume, alionekana kuunyanyasa muziki wa kizazi kipya katika miaka ya 2001 hadi 2005. Zama hizo Profesa Jay alionekana kutokuwa na mpinzani, yasemekana  yeye ndiye aliyesababisha watu wazima wausikilize muziki wa kizazi kipya.

Hauwezi kuutaja muziki wa kizazi kipya pasi bila Profesa Jay, Mb Doggy, ndiye mwanzilisha wa muziki wa mapenzi mazito, hata kama waliimba lakini si kwa kiwango cha Mb Doggy.

Kati ya mwaka 2005 na 2006 Mb Doggy kutoka Tip Top Connection, ilikuwa kipindi chake cha kunyanyasa katika muziki wa kizazi kipya., alionesha uwezo wake mkubwa katika tasnia hiyo.

Miaka ya 2005 na 2006 Ferouz naye alikuja juu sana, lakini hakwenda mbali. Wakati huohuo waliibuka akina Matonya, Abby Skills, Enika, Ali Kiba, Queen Darleen (japokuwa alikuwapo katika game tangu enzi za Historia ya Kweli ya Dully Sykes), lakini hakuwa msanii wa uhakika kipindi hicho.

Bila kuusahau muziki wa Taarab uliopamba moto, kipindi hicho ambao wataalamu wa muziki wanautaja kuwa unafaa kuwa muziki wa asilia wa Kitanzania ingawa una mahadhi ya Kiarabu na Kihindi kwa mbali.

Mwaka 2006 kundi la Jahazi Morden Taarab lilianzishwa chini ya uongozi wa Mzee Yussuf, akuvusha muziki huo ukiwa na vionjo vya kisasa.

Alisababisha takriban kila mtu asikilize Taarab hasa kwa tungo zake lakini hakuzingatia uhalisia wa taarab mwanana ya akina Shakira na Visiwa vya Zanzibar. Baadaye zikazuka bendi nyingine nyingi za akina Nasma Hamis Kidogo, Khadija Omar Kopa, Isha Mashauzi ambao yaelezwa kuwa waliua kabisa muziki wa taarabu, wao wakaita ni Tara dansi!

Mzee Yussuf ameachana na masuala ya muziki, ni Alhaj baada ya kwenda kuhiji Mecca.

Miaka ya 2010 muziki wa kizazi kipya na muziki wa dansi ulibadilika sana. Vijana wengi waligeukia katika muziki wa dansi. Lakini muziki wa Bongo Fleva umepiga hatua maradufu. Msanii Naseeb Abdul ‘ Diamond Platinumz, ameupeleka  mbali sana muziki wa Tanzania nje ya nchi kwa kiasi  kikubwa kupita msanii mwingine yeyote yule tangu muziki huu ulipoanza. Sambamba na Ali Kiba ‘King Kiba’ ingawa kwa muda aliamua kumuachia uwanja  Diamond , na kuamua kurudi tena kwa kishindo.

Wasanii hao wameshindwa kuvaa viatu vya kina Salifu Keita, Mory Kante na wengine wengi wanaotumia Kora katika muziki wao.

Huenda Darasa ni msanii pekee wa hip-hop aliyeweza kufikisha watazamaji wengi kwa muda mfupi katika Youtube, kuliko msanii yeyote Yule wa hip– hop ya Kitanzania, hasa kwa kufuatia kibao chake cha “Too  Much”.

Muziki wa Singeli umebadilisha mawazo ya baadhi ya vijana ambapo wanawatelekezea kina Man Fongo, Msaga Sumu, Sholo Mwamba, Dula Makabila wakiwa na matumaini ya kuirudisha Tanzania katika asili ya muziki wake.

Mwisho.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba 0784331200, 0767331200 na 0713331200.

HALI YA AURLUS MABELE SI NJEMA

0
0
Na: Moshy Kiyungi, Tabora.

Septemba, 2019. Imefahamika kuwa afya ya mwanamuziki Aurlus Mabele, haiko vizuri akisumbuliwa na maradhi ya Kupooza.

Mabele amekuwa maarufu miongoni wa wapenzi na mashabiki wa muziki wa dansi, kupitia uwezo wake wakuimba na kunengua kwa mbwembwe, licha ya umri wa miaka 65, kuwa mkubwa.

Mwanamuziki huyo ana talanta nyingi zikiwemo za utunzi, uimbaji kutoka Jamhuri ya Kongo.

Aurlus Mabele alizaliwa mnamo mwaka wa 1953 katika wilaya ya Poto-Poto nchini Jamhuri ya Kongo-Brazzaville.


Majina yake halisi anaitwa Aurélien Miatsonama. Mwanamuziki huyu alianzisha kundi liitwalo "Ndimbola Lokole".


Baada ya kushiriki sana kupiga muziki  barani Ulaya, mwaka wa 1986 yeye na mcharaza gitaa la solo, Diblo Dibala na Mav Cacharel, waliamua kuanzisha kundi la Loketo. Kwa pamoja wakatengeneza muziki maarufu wa soukous.


Mabele baadaye akatajwa kama mfalme, hivyo basi ikapelekea msemo wa kuwa "Aurlus Mabele ndiye mfalme wa soukous".

Katika miaka 25 ya kazi zake ameweza kuuza zaidi ya nakala milioni 10 za albamu duniani.

Aurlus alisaidia kwa kiasi kikubwa katika kuitambulisha na kuusukuma vilivyo muziki wa soukous nje ya mipaka ya bara la Afrika.

Maradhi yake  ya kupooza yamemsubua kwa takriban miaka mitano.

Alipopata nafuu kidogo, aliweza kujipanga ili kufanya matamasha na kundi zima la Loketo huko Ulaya kati ya mwezi Mei na Juni, 2009.

Mabele kwa kushirikiana na wapiga gitaa maarufu na wenye vipaji, ametengeneza dansi ya Kiafrika yenye ladha yake ya kipekee ya soukous.

Walitunga nyimbo kama vile Mousso Africa, Ivorian woman, Embargo, Betty De Asta, Evelyne, Loketo na kadhalika.

Baadhi ya albamu zake  ni pamoja na

Dossier X 2000, Compil two na Compil one za  mwaka 1999. Zingine ni Tour de contrôle ya mwaka 1998, Best of Aurlus Mabele ya mwaka 1997, Génération-Wachiwa encaisse tout ya mwaka 1994, 
Stop Arretez ya mwaka 1992 na Embargo 1990.

Mwanamuziki huyo hakuishia hapo kwani aliachia albamu zingine za Soukouss la terreur ya mwaka 1989, Sebene Africa mousso La Femme ivoirienne, Maracas d'or  ya mwaka 1988, Réconciliation, Cicatrice na Confirmation,

Kundi la Loketo lilikuwa na mkali wa kupiga gitaa la solo barani Afrika Diblo Dibala na wakongwe wengine kama Aurlus Mabele, Jean Baron, Lucien Bokilo, Mack Mackaire ambaye alikuwa anapiga Drums.

Kwa umoja wao walitikisa sehemu zote walizopita kufanya maonesho yao, na wengine waling’ara sana na kufanikiwa kuziteka nyoyo za wapenda midundo ya Afrika si tu kwa Kongo bali kwa Bara zima la Afrika.


Ronald Rubinel alikuwa anabofya kinanda enzi hizo wapiga vinanda mashuhuri walikuwa yeye na jamaa aliyetoka kwa Pepe Kalle, mwenye majina ya  Butamu.


Bendi hiyo ilikuwa imesheheni wanenguaji mahiri wawili ‘Wana Wandere’, wazungu ambao walikuwa wakicheza vilivyo.

Tafsiri ya neon Loketo kwa lugha ya Kilingala, inamaana ya chezesha hips zako “move your hips” na ndivyo Aurlus Mabere ndiyo ulikuwa mtindo wake wa kuchezesha.

Mwaka 1987 wakiwa wametiamia Loketo,  waliwasha moto kwenye klabu moja ijulikanayo kama Kennel Club huko San Francisco, nchini Marekani.

Inasemekana ile ilikuwa tamasha kubwa na iliyobamba sana. Baadaye wanamuziki hao wakaanza kutoa kila mmoja na solo albam yake.

Tumuombee dua ili aweze kupona haraka.

Mwisho.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba: 08713331200, 0767331200,0736331200 na 0784331200.

RAMAPHOSA ATOA NENO KUHUSU XENOPHOBIA AFRIKA KUSINI

0
0
Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

RAIS wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amezitaka Wizara zinazoshughulika na masuala ya ulinzi na usalama kuhakikisha wanaangaza katika matukio ya kikatili yaliyowalenga wageni nchini humo ikiwa ni pamoja na kukomesha kabisa matukio hayo.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Ramaphosa ameandika kuwa hakutakuwa na uhalali kwa raia wa Afrika kusini kuwadhuru watu kutoka nchi nyingine za Afrika na kueleza kuwa watu nchini humo wanatakiwa kuishi kwa amani hata kama kuna shida yoyote inatakiwa kumalizwa kwa kufuata misingi ya Kidemokrasia.
 

Kwa upande wa balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Richard Lupembe amesema kuwa hadi leo mchana hakuna tukio lolote la raia wa Tanzania kudhurika kwa namna yoyote katika vurugu hizo zilizowalenga wageni.

Chombo cha habari Cha Aljazeera kimeripoti kuwa katika mitaa ya Alexandra polisi walionekana wakidhibiti kikosi cha watu 50 waliokuwa wanarusha mawe.
Vurugu hizo ziliibuka jumatatu wakati vikosi vya uokoaji vikizima moto katika jengo la Jeppestown ambapo iliripotiwa kuwa watu kadhaa walipoteza maisha na majeruhi walipatikana, watu katika vikundi mbalimbali waliendeleza kuvamia sehemu za biashara na kuchoma moto na kupora huku ikielezwa kuwa waliathirika zaidi ni raia kutoka nchi za Nigeria, Somalia na Ethiopia.

TCRA YAVITAKA VYOMBO VIWILI VYA HABARI KUOMBA RADHI SIKU 7 MFULULIZO KWA MAKOSA YA MAUDHUI MTANDAO

0
0
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imevitaka vyombo vya habari viwili viombe radhi kwa siku saba mfululizo kutokana na makosa mbalimbali ya ukiukwaji wa Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (Maudhui Mtandaoni) ikiwemo kuonesha na kuchapisha picha mbalimbali za ajali ya gari la mafuta, iliyotokea Msamvu, Morogoro.

Kamati ya Maudhui ilitoa onyo hilo kwa Lemutuz Online Tv na Global Tv ambapo wametakiwa kuomba radhi kuanzia Septemba 4 mwaka huu.

Akisoma uamuzi huo, mwenyekiti wa kamati hiyo, Valeria Msoka alisema katika ajali iliyotokea Agosti 10 mwaka huu baadhi ya vyombo vya habari hususan Online TV zaidi ya 15 zilichapisha na kuonesha picha za miili ya watu wakiofariki katika ajali hiyo kinyume cha sheria, kanuni na maadili ya uandishi na utangazaji wa habari.

Alisema baadhi ya vyombo hivyo viligundua makosa yao na kuziondoa picha hizo na kwamba Lemutuz Online Tv na Global Tv walishindwa kujirekebisha na Agosti 28 mwaka huu walifika mbele ya kamati hiyo na kujieleza.

"Katika utetezi wao Lemutuz Online Tv ilieleza kuwa kosa hilo lilisababishwa na uzembe wa msimamizi wao wa maudhui ambaye hakutumia busara na kuzingatia weredi katika uchapishaji video ile,Global Tv ilisema ilichukua tahadhari kubwa ya kuziziba picha za miili ya watu waliokuwa wameungua katika ajali ile kwa kuweka vivuli lakini ilitokea tatizo la kiufundi na kuonesha picha hizo chini ya kivuli,"amesema Msoka

Ameongeza kuwa vyombo vyote hivyo vya habari vilikiri makosa yao na kuomba radhi na kuahidi kutorudia tena na baada ya kusikiliza kwa kina maelezo ya utetezi wao, kamati imeona imekiuka kanuni za mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (maudhui mtandaoni) ya mwaka 2018.

Msoka amesema, kutokana na hilo kamati ya maudhui imeamua kutoa onyo kali na kuamuru chaneli hizo mbili kuomba radhi kwa watazamaji kupitia chaneli zao kwa siku saba mfululizo kuanzia Septemba 4 mwaka huu.

Amesema imeshauri chaneli zote mbili kuimarisha usimamzi makini wa chaneli zao ili kuhakikisha maudhui yao ni salama kisheria na kimaadili kabla ya ya kuwekwa mtandaoni.

Katika hatua nyingine, kamati hiyo imetoa onyo kali kwa Televisheni ya East Africa (EATV) kwa kurusha maudhui yasiyo na maadili Julai 2 mwaka huu kupitia kipindi chake cha 'Dadaz' kipengele cha Mtukati.

Pia ilitoa onyo kali kwa kituo cha TBC FM Radio , kwa kukiuka agizo la serikali la kutosoma habari za magazeti kwa undani.

Alisema radio hiyo ilitenda kosa hilo kupitia kipindi chake cha 'Busati' kipengele cha magazeti ambapo mtangazaji wa kipindi alisoma kwa undani habari mbalimbali zilizoandikwa katika magazeti ya uhuru na Habari Leo.

Alisema vyombo vyote vya habari viligundua nakukiri makosa yao na kuomba radhi ambapo kamati imevishauri kuimarisha na kuboresha usimamizi, utayarishaji na utangazaji wa vipindi vyao.

Mchungaji na wake zake wawili kizimbani.

0
0
Na Karama Kenyunko, Michuzi Tv.

MCHUNGAJI wa Kanisa la The Early Church of Lord Yeshwah, David Chirhuza (33) , na wake zake wawili, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka ya kuishi nchini Vila ya kibali na kufànya kazi za kanisa bila kibali.

Mbali na mchungaji huyo, washitakiwa wengine ambao ni wake zake ni, Easther Sebuyange (27), Kendewa Ruth (26) na Samwel Samy (22) mdogo wake.

Mchungaji Huyo ambae hivi karibuni video yake ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha kuwa na wake zake watatu ambao alidai walikuwa mbioni kumtafutia mke wa nne

Akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa serikali kutoka idara ya uhamiaji Godfrey Ngwilo akisaidiana na Sita Shija amedai mbele ya Hakimu Mkazi Kisutu Mwandamizi Agustino Mbando kuwa, Septemba 2 mwaka huu eneo la Salasala Kilimahewa, jijini Dar es Salam, mchungaji huyo na wenzake hao walibainika kuishi nchini bila kibali.

Katika shitaka la pili, linalomkabili mchungaji huyo pekee ilidaiwa kuwa, siku na mahali hapo, mshtakiwa alikutwa akijihusisha na kazi za kanisa kama mchungaji akiwa hana kibali cha kuishi nchini.

Baada ya kusomewa mashitaka hayo, mchungaji David amekana shitaka la kwanza na kukiri shitaka la pili huku washitakiwa wenzake wakikiri mashtaka yote.

Hata hivyo, washitakiwa wote walirudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ambapo mahakama iliwataka washtakiwa hao kuwa na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa serikali.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 9 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

MALINZI AIOMBA MAHAKAMA KUMUACHIA HURU KWANI HANA HATIA

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

ALIYEKUWA Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Jamal Malinzi ameendelea kujitetea na kuiomba  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumuachia huru kwa sababu hana hatia katika mashitaka 16 yanayomkabili ikiwemo ya utakatishaji fedha.

Malinzi amedai hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde wakati akijitetea. Akiongozwa na Wakili Richard Rweyongeza, Malinzi amedai wakati wa uongozi wake ndani ya TFF na taasisi zingine katika maisha yake hakuwahi kushiriki kutakatisha fedha.

Amedai, katika mashitaka ya utakatishaji yanaonesha kwamba alitakatisha Sh 43,100,000 kutokana na mashitaka ya kughushi ambayo  mahakama hiyo haijamuona kuwa na kesi ya kujibu.
Pia amedai  jumla ya fedha zilizoandikwa kwenye mashitaka ya kughushi si Sh 43,100,000 badala yake ni Sh 37,100,000 hivyo idadi iliyowekwa kwenye mashitaka hajui imetokea wapi.

Malinzi amedai fedha anazodaiwa kuzitakatisha alizipata kwa utaratibu halali wa TFF kwani zipo nyaraka mbalimbali zilizowasilishwa mahakamani hapo ikiwemo risiti na nyaraka za benki zinazothibitisha kwamba alipokea fedha kihalali.

Ameeleza kuwa, mpaka Desemba 31,2016  yeye ndio anayeidai TFF na kwamba katika mashitaka ya 15 hadi ya 26 ni ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na sio ya kughushi na mashitaka ya kughushi aliyonayo hayajaonesha kama alipata kitu chochote kutokana na makosa hayo.

Malinzi amedai  alifanya mabadiliko ya mtia saini kutoka Edger Masoud kwenda kwa Nsiande Mwanga kihalali kwa mamlaka aliyopewa kwa mujibu wa Katiba na kanuni za TFF na  si mamlaka ya kamati tendaji kujadili mtia saini badala yake ni Rais ndio anateua mtia saini na kupeleka katika bodi ya maamuzi kwa ajili ya kujadili na kisha hupelekwa benki.

"Nilisaini maamuzi ya kubadili mtia saini kwa mujibu wa katiba ya TFF kuonesha kuwakilisha shirikisho. Sikunufaika na kitu chochote kutokana na kubadilisha mtia saini badala yake mabadiliko haya yalinufaisha wengi," amedai Malinzi.

Pia amedai muhtasari wa Juni 5,2016 uliowasilishwa mahakamani hapo si sahihi na kwamba orodha sahihi ya wajumbe waliohudhuria kikao cha TFF inapatikana kwenye kitabu cha muhtasari na kwamba katika kikao hicho, mashahidi waliokuwepo hawakuhudhuria.

Amedai Mwanga hakuhusika kwa namna yoyote kuandaa maamuzi ya bodi na wala hakushiriki katika kufanya maamuzi kwani alikuwa mwajiriwa kama wengine.

Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Katibu Mtendaji wa TFF, Selestine Mwesigwa, Mhasibu wa TFF Nsiande Mwanga na  Karani Flora Rauya.

Kesi hiyo ya jinai namba 213 ya mwaka 2017 washitakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka 20 yakiwamo ya kula njama, kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji wa fedha wa Dola za Marekani 173,335.

Malinzi, Mwesigwa na Nsiande wapo rumande kwa sababu mmashitaka ya utakatishaji  fedha kuwa miongoni mwa mashitaka  ambayo kwa mujibu wa sheria hayana dhamana huku Rauya akiwa  nje kwa dhamana.

ZIARA YA KIKAZI YA KATIBU WA CCM MKOA WA MWANZA SALUM KALLI WILAYANI MISUNGWI

0
0
Vijana wa Chipukizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Misungwi wakimvisha skafu Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Salum Kalli alipokwenda kwenye ziara ya kikazi katika kata za Mbarika na Misasi jana.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli, akizungumza na Makatibu wa Kata na Matawi wa Chama (hawapo pichani) wa kata za Mbarika na Misasi kwenye tarafa ya Misiasi wilayani Misungwi.Wa pili kutoka kulia ni Katibu wa CCM Misungwi, Latifa Malimi.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Salum Kalli akisitiza jambo kwa makatibu wa matawi na kata za Misiasi na Mbarika wilayani Misungwi jana.
Katibu wa CCM Wilaya ya Misungwi, Latifa Malimi (kulia) akipokea bendera 550 kutoka kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli (kushoto), ukiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Katibu Mkuu Dk. Bashiru Ally, aliyoyatoa wakati wa ziara yake mapema mwezi Agosti mwaka huu.Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda.

Picha na Baltazar Mashaka

KAMPENI NYUMBA NI CHOO YAZINDULIWA SHINYANGA

0
0
Kampeni ya kuhamasisha wananchi wa mkoa wa Shinyanga kuwa na vyoo kwenye nyumba zao "Nyumba ni Choo", imezinduliwa na mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe.Zainab Telack, na kuwaonya wanasiasa ambao watawakingia kifua wananchi ambao watachukuliwa hatua kwa sababu ya kutokuwa na vyoo kwenye kaya zao kwa madai ni wapiga kura wao, kuwa atakaye fanya hivyo atashughulikiwa.

Kampeni hiyo ambayo itadumu ndani ya siku 21 imezinduliwa rasmi leo Septemba 3,2019 kwenye viwanja vya Zimamoto Mjini Shinyanga na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, mashirika, na wanasiasa. Akizindua kampeni ya 'Nyumba ni Choo', Telack amewaagiza maofisa afya wote wa mitaa kupeleka mipango kazi yao, ili waweze kupita kila Kaya za mkoa huo na kuzikagua nyumba ambazo hazina vyoo,na kuwachukulia hatua wahusika lengo likiwa ni kuhakikisha kaya zote ziwe na choo bora. 

Amesema anatambua kipindi hiki ni cha kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, hivyo wakati zoezi hilo la ukaguzi wa choo kwa kila nyumba likiendelea wanasiasa wanapaswa kutoliingilia, na kuanza kuzuia wananchi wasiwajibishwe kwa madai ni wapiga kura wao.

 “Kwenye kampeni hii ya nyumba ni choo hatutaki siasa, bali tunataka wananchi waishi salama wawe na vyoo bora kwenye nyumba zao, hivyo Mwanasiasa ambaye atamkingia kifua mwananchi ambaye atakutwa hana choo nipeni taarifa ili tuone namna ya kumshughulikia, hatutaki mzaa kwenye masuala ya maendeleo,” amesema Telack. “Hadi kufikia Desemba mwaka huu tunataka mkoa wetu, kaya zote ziwe na vyoo bora pamoja na kuvitumia, na kuondokana pia na dhana potofu ya kujisaidia vichakani kwa kuongopa kuchangia choo kimoja na mama mkwe, bali tunataka mkoa uwe safi kimazingira na wananachi wawe salama kiafya,” ameongeza.

 Naye Afisa Afya wa mkoa wa Shinyanga Neema Simba, ametaja takwimu za kaya zenye vyoo mkoani humo kuwa ni asilimia 50.6 na kaya ambazo hazina vyoo ni asilimia 5.5 ambapo jumla ya kaya zote zipo 284,701. Kwa upande wake mratibu wa uhamasishaji wa kampeni hiyo kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Elizabeth Malingumu amesema wamezindua kampeni ya nyumba ni choo mkoani Shinyanga, ili wananchi wote wawe na vyoo bora ili waepukane na magonjwa ya mlipuko na kuishi salama. Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainabu Telack akizindua Kampeni ya nyumba ni choo na kuwataka wananchi wa mkoa huo wa Shinyanga kujenga vyoo bora pamoja na kuvitumia. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainab Telack akitoa onyo kwa wanasiasa kuingilia oparesheni ya ukaguzi wa choo kwa kila nyumba na kuwakingia kifua wale ambao watakutwa hawana vyoo kwa madai ni wapiga kura wao. Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mhe. Jasinta Mboneko, akizungumza akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Nyumba ni choo ambapo amesema wataisimamia na kuhakikisha inafanikiwa kwa wananchi wote kuwa na vyoo bora. Awali Afisa Afya wa mkoa wa Shinyanga Neema Simba akisoma taarifa ya usafi wa mazingira ya mkoa wa Shinyanga. ametaja Takwimu kuwa kati ya kaya za mkoa wa Shinyanga 284,701 wanaotumia vyoo ni asilimia 50.6 na wasio na vyoo ni asilimia 5.5. Mratibu wa uhamasishaji wa kampeni hiyo kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Elizabeth Malingumu akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Nyumba ni choo. Amesema wamezindua kampeni hiyo ili kuhamasisha wananchi wote wa mkoa wa Shinyanga wanakuwa na vyoo bora kwenye nyumba zao. Mwakilishi kutoka Shirika la Maendeleo la uholanzi (SNV) Elisekile Bwile, akielezea namna wanavyosaidiana na Serikali kuhakikisha nchi ya Tanzania wananchi wake wanakuwa kwenye mazingira ya usafi pamoja na kufadhili kujenga miradi ya kuhifadhia maji taka ukiwamo na mji wa Shinyanga. Balozi wa kampeni ya nyumba ni choo msanii Mrisho Mpoto akizungumza na wananchi wa mkoa wa Shinyanga na kuwataka wajenge vyoo bora, vilivyoezekwa mapaa juu, milango pamoja na kuwepo na maji ya kunawa mikono. Diwani wa Kata ya Kambarage manispaa ya Shinyanga Hassan Mwendapole akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo ya nyumba ni choo. Awali Katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela, akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo ya nyumba ni choo, kabla ya kuanza kutambulisha viongozi mbalimbali wa Serikali. Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack katikati, akiwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko (wa kwanza kushoto), pamoja na katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela kabla ya kuzindua kampeni hiyo ya nyumba ni choo. Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack awali kabla ya kwenda kwenye viwanja vya Zimamoto kuzindua kampeni ya nyumba ni choo akipiga picha ya pamoja na Balozi wa uhamasishaji wa kampeni hiyo Mrisho Mpoto kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa. Wananchi wa Shinyanga mjini wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya nyumba ni choo na kutakiwa wale ambao hawana vyoo, wajenge vyoo bora pamoja na kuvitumia ili waweze kujikinga na magonjwa mbalimbali ya mlipuko kikiwamo kipindupindu. Wananchi wa Shinyanga mjini wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya nyumba ni choo na kutakiwa wale ambao hawana vyoo, wajenge vyoo bora pamoja na kuvitumia ili waweze kujikinga na magonjwa mbalimbali ya mlipuko kikiwamo kipindupindu. Wananchi wa Shinyanga mjini wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya nyumba ni choo na kutakiwa wale ambao hawana vyoo, wajenge vyoo bora pamoja na kuvitumia ili waweze kujikinga na magonjwa mbalimbali ya mlipuko kikiwamo kipindupindu. Wananchi wa Shinyanga mjini wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya nyumba ni choo na kutakiwa wale ambao hawana vyoo, wajenge vyoo bora pamoja na kuvitumia ili waweze kujikinga na magonjwa mbalimbali ya mlipuko kikiwamo kipindupindu. Wananchi wa Shinyanga mjini wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya nyumba ni choo na kutakiwa wale ambao hawana vyoo, wajenge vyoo bora pamoja na kuvitumia ili waweze kujikinga na magonjwa mbalimbali ya mlipuko kikiwamo kipindupindu. Mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi (kushoto), akiwa na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Hoja Mahimba, wakishuhudia uzinduzi wa Kampeni ya nyumba ni choo, ya kuhamasisha wananchi wawe na vyoo bora kwenye nyumba zao. Viongozi mbalimbali wa kiserikali pamoja na vyombo vya dola, wakifurahia jambo kwenye uzinduzi huo wa Kampeni ya Nyumba ni choo mkoani Shinyanga, ya kuhamasisha wananchi wajenge vyoo bora pamoja na kuvitumia. Burudani zikitolewa kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo ya nyumba ni choo mkoani Shinyanga. Burudani zikiendelea kutolewa. Burudani zikiendelea kutolewa. Burudani zikiendelea kutolewa kwenye uzinduzi wa kampeni ya nyumba ni choo. Awali Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mhe. Zainabu Telack, wa pili kutoka kushoto, akiwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akifuatiwa na Katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela, pamoja na Mrisho Mpoto wa kwanza kushoto, akiongoza maandamano kwenda kuzindua kampeni ya nyumba ni choo. Waendesha Bodaboda wakiwa kwenye maandamano ya kwenda kuzindua kampeni ya nyumba ni choo, kwenye viwanja vya Zimamoto Shinyanga Mjini, kwa kuhamasisha wananchi wa mkoa wa Shinyanga wawe na vyoo bora pamoja na kuvitumia. Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

VIONGOZI WA CCM WALIPOKAGUA MIRADI MKAKATI YA UKARABATI NA UJENZI WA MELI

0
0
Meneja wa mradi wa ukabarati wa meli na ujenzi wa meli mpya,Meja, Mhandisi Abel Gwanafyo (wa pili kutoka kushoto) akitoa maelezo kwa uongozi wa CCM ulipokwenda kukagua miradi hiyo jana kwenye Bandari ya Mwanza Kusini.Kulia ni Mkujumbe wa NEC, Jamala Abdul Babu, wa pili ni Mwenyekiti wa Mkoa Dk. Anthony Diallo na wa tatu kutoka kushoto ni Katibu wa mkoa, Salum Kalli, aliyeinama ni Mtendaji Mkuu wa MSCL, Eric Hamis.
Ujumbe wa CCM Mkoa wa Mwanza ukiongozwa na meneja wa mradi wa ujenzi na ukarabati wa meli, Mhandisi Meja Abel Gwanafyo (wa kwanza kushoto) kukagua eneo linalojengwa chelezo ya meli mpya jana.Wa pili ni Mtendaji wa MSCL Eric Hamiss,wa tatu ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Dk. Anthony Diallo.Kutoka kulia wa pili ni Katibu wa mkoa Salum Kalli na wa tatu ni Mjumbe wa NEC, Jamal Abdul Babu.
Viongozi wa CCM Mkoa wa Mwanza, wakipata maelezo mafupi ya mradi wa ukarabati wa meli za MV. Victoria na MV. Butiama kutoka kwa Mhandisi Abel Gwanfyo (wa tatu kutoka kulia) jana kabla ya kukagua ukarabati huo wa meli.Kulia ni Katibu wa Mkoa Salum Kalli, wa pili ni mwenyekiti wa mkoa, Dk. Anthony Diallo.
Mwenyekiti na Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza, Dk. anthony Diallo na Salum Kalli, wakiiingia ndani ya meli ya MV. Victoria inayokarabatiwa kwa gharfama ya sh bilioni 22 na kampuni ya Korea Kusini ya KMTI.
Viongozi wa CCM Mkoa wa Mwanza wakiangalia mafundi (hawapo pichani) wakikata vyuma vinavyotumika kwenye ukarabati wa meli ya MV. Victoria jana. Mbele ni Mwenyekiti wa CCM Dk. Anthony Diallo na kulia ni Katibu Salum Kalli.
Mhandi wa MSCL Meja mstaafu Abel Gwanafyo, akiwapa maelezo ya mradi wa ukarabati wa meli ya MV. Victoria , viongozi wa CCM Mkoa wa Mwanza.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Dk. Anthony Diallo (kushoto) na Katibu wa mkoa Salum Kalli wakishuka kutoka kwenye meli y MV. Victoria baada ya kukagua na kujionea shughuli za ukarabati wa meli hiuo.Kushoto chini ni Mhandisi, Meja Abel Gwanfyo ambaye ni meneja wa mradi huo.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza. Salum Kalli akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kuhimisha ziara ya ukaguzi wa mradi wa ukarabati wa meli na ujenzi wa meli mpya.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Dk. Anhtony Diallo akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ukarabati na ujenzi wa meli katika Bandari ya Mwanza Kusini.





Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) Eric Hamiss (kushoto) akifafanua jambo kwa viongozi wa CCM wakiwemo watumishi wa kampuni hiyo kabla ya uongozi huo wa Chama kutembelea na kukagua miradi ya ujenzi wa meli na ukabati wa meli za MV. Butiamana MV. Victoria kwenye bandari ya Mwanza Kusini.picha zote na Baltazar Mashaka

MBULU WAMFAGILIA MAGUFULI

0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga, akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Joseph Mandoo akifungua kikao cha Baraza la madiwani.
Mkuu wa wilaya ya Mbulu Chelestino Mofuga akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani.
……………….
BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara limempongeza Rais John Magufuli kwa kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa hospitali ya wilaya na jengo jipya la utawala la makao makuu ya halmashauri hiyo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu, Joseph Guulo Mandoo alisema wanampongeza Rais Magufuli kutokana na kufanikisha miradi hiyo ya maendeleo.

Mandoo alisema hivi sasa halmashauri ya Mbulu imepiga hatua ya maendeleo kwenye sekta ya elimu, afya, utawala, miundombinu na maendeleo mengine.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mbulu, Hudson Starnley Kamoga alisema kutokana na kutengwa kwa fedha hizo na Rais Magufuli, hivi sasa wanazidi kupiga hatua ya maendeleo kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Jengo la utawala la makao makuu linaendelea vizuri na hospitali nayo inaendele kujengwa kule kata ya Dongobesh, natarajia tutamaliza kipindi cha miaka mitano tukiwa tumehamia Dongobesh,” alisema Mofuga.

Alisema wanatarajia kutenga eneo la kumbukumbu la kuandika majina yote ya madiwani waliokuwepo madarakani waliopo madarakani wakiongozwa na Mwenyekiti Mandoo na mkurugenzi Kamoga.

Mkuu wa wilaya ya Mbulu, Chelestino Mofuga alisema Rais Magufuli amefanya maendeleo mengi ikiwemo miradi ya kimkakati kwa muda mfupi wa miaka minne aliyoongoza, utadhani amekaa madarakani miaka 40.

“Tumeona barabara za gorofa, elimu bila malipo, reli ya kisasa, umeme, hospitali mpya za wilaya zimejengwa vituo vya afya, utadhani ameongoza kwa miaka 40 kumbe ni miaka minne,” alisema Mofuga.

List of Banned Cosmetics

Serikali kuendelea kupigania PSDS

0
0

Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Idara ya Maendeleo ya Sekta binafsi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Ezamo Maponde amesema serikali itaendelea kuwa mstari wa mbele kuwezesha mkakati wa maendeleo ya sekta binafsi katika nchi za Afrika Mashariki (PSDS) kufanikiwa.

Aidha alisema, serikali imekuwa mstari wa mbele kufanya mabadiliko mbalimbali ya sera zake ikiwemo mpango wa dira ya maendeleo ya taifa ya mwaka 2015 ili kusukuma mbele sekta za Kilimo na biashara.

Alisema hayo wakati wa kufunga kwa mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki , mradi uliokuwa ukiratibiwa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF).
Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu, Sera, Uratibu na Uwekezaji Ofisi ya Waziri Mkuu alisema kutokana na mabadiliko ya kisera na usimamizi wa utekelezaji wake Tanzania imefanikiwa kujiondoa katika utegemezi.

Alisema juhudi zilizofanyika kuweka msingi katika mradi huo kutatochoea kuimarishwa kwa Kilimo na kuwa na Kilimo biashara ili ndoto za kuwa na uchumi wa kati unaotegemea viwanda kufanikiwa.
Alisema kutokana na haja hiyo serikali imekuwa ikitengeneza sera na kubadili kanuni mbalimbali ili  kuhimiza uchumi wa kiushindani wa viwanda toka mwaka 1961 kwa lengo la kupunguza utegemezi katika bajeti. Sekta ya viwanda nchini imegawanyika katika maeneo matatu ya uzalishaji (53%) uchakataji (24 %) na uunganishaji (4%).

Kwa kuwa uchumi wa Tanzania unategemea mazao ya Kilimo kinachoajiri asilimia 75 ya wananchi, ndio nguzo ya uzalishaji wa bidhaa katika viwanda.
Kutokana na utegemezi huo viwanda vinavyochakata mazao ya Kilimo hasa chakula ni asilimia 24, viwanda vya nguyo na nyuzi asilimia 10 na kemikali asilimia 8.5.

Akizungumzia mradi huo Profesa Fortunata Makene, Mkuu wa kitengo cha utafiti mkakati na machapisho kutoka Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) alisema kwa kiasi kikubwa umesaidia katika kuleta tija katika sekta ya kilimo na biashara ikiwemo kuzishawishi serikali kufanya mabadiliko katika sera zake.

Akizungumza katika mkutano  huo uliowakutanisha  wadau mbalimbali wakiwemo watafiti wa masuala ya kiuchumi, wakulima na wafanyabiashara kujadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu  kuzinduliwa kwake, alisema mradi huo uliokuwa na lengo la kuzishawishi serikali katika masuala ya sera kupitia mpango ujulikanao kama 'National Reference Group'.

Alisema mradi huo ulilenga kuangalia namna ambavyo masuala ya mabadiliko ya tabia nchi  yanahusishwa na shughuli za kilimo na biashara ili kuleta tija kwa wakulima na wafanyabiashara kwa ujumla.

Profesa Makene alisema kimsingi mradi huo uliondeshwa kwa awamu mbili kwa vipindi vya miaka minne minne tangu kuanzishwa kwake umeweza kuchangia mabadiliko hayo  na kuongeza uelewa kwa wadau husika wakiwemo wanawake kutoka vikundi mbalimbali vinavyojishughulisha na kazi za usindikaji wa vyakula na bidhaa

Aidha alisema uwepo wa sera madhubuti katika kilimo na biashara kwa kiasi kikubwa kumeweza kuleta mabadiliko chanya kwa wakulima na wafanyabiashara ikiwemo kuongeza thamani katika mnyororo.

Nchi za Afrika Mashariki kwa sasa zipo katika kuendeleza mpango wa Private Sector Development Strategy (PSDS) 2018-2022 wenye lengo, la kuimarisha mazingira bora ya biashara na kuzifanya kuwa za ushindani.
 Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Sekta binafsi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Ezamo Maponde akizungumza wakati wa kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) katika hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa kitengo cha utafiti mkakati na machapisho kutoka Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Dk. Tausi Kida wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Sekta binafsi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Bw. Ezamo Maponde (kulia) na Mkuu wa kitengo cha utafiti mkakati na machapisho kutoka Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene wakiwa meza kuu wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

 Mtafiti mwandamizi wa ESRF Dk. Hoseana Bohela Lunogelo akizungumzia nafasi ya wadau katika mchakato wa PSDS wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mwakilishi wa Tanzania kwenye Shirika la Biashara Duniani (WTO) jijini Geneva , Uswis Bi. Neema Manongi akizungumzia kinachotarajiwa kutoka WTO za utengenezaji wa mnyororo wa thamani kwa bidhaa za mashambani wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF ambapo pia walijadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu kuzinduliwa kwake, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Dk Ladislaus Chang’a, kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) akiendesha majadiliano kuhusu namna ambavyo mazungumzo ya kimataifa kuhusu biashara na mabadiliko ya hali ya hewa yalivyochagiza uumbaji wa sera zinazotumiwa na serikali kuwezesha uchakataji wa bidhaa za kilimo pamoja na mabadiliko ya tabia nchi wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF ambapo pia walijadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu kuzinduliwa kwake, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Ofisa wa programu CUTS International, Nairobi Bw. Collins Owegi akizungumzia nini kilichofanyika na kufanikiwa katika PACTEAC2 wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF ambapo pia walijadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu kuzinduliwa kwake, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mratibu wa kitaifa wa TCSAA ambaye pia ni mshiriki majadiliano ya UNFCCC Bi. Shakwaanande Natai akizungumza kuhusu mabadiliko ya tabia nchi na uhuishaji wake kwenye kilimo chini ya makubaliano ya Koronivia wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF ambapo pia walijadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu kuzinduliwa kwake, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Dk. Donatilla Kaino wa ESRF akiendesha majadiliano ya mada kuhusu mradi PACTEAC 2 ambapo yaliangalia uwezeshaji uliofanyika na kipi kitaendelea wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF ambapo pia walijadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu kuzinduliwa kwake, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa kitengo cha utafiti mkakati na machapisho kutoka Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Profesa Fortunata Makene akifafanua jambo wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF ambapo pia walijadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu kuzinduliwa kwake, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.




 Baadh ya wadau mbalimbali wakiwemo watafiti wa masuala ya kiuchumi, wakulima na wafanyabiashara wakishiriki kutoa maoni wakati wa hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF ambapo pia walijadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu kuzinduliwa kwake, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.


 Baadhi ya wadau mbalimbali wakiwemo watafiti wa masuala ya kiuchumi, wakulima na wafanyabiashara walioshiriki hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF ambapo pia walijadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu kuzinduliwa kwake, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

Picha ya pamoja ya mgeni rasmi na wadau mbalimbali wakiwemo watafiti wa masuala ya kiuchumi, wakulima na wafanyabiashara walioshiriki hafla ya kufunga mradi wa miaka nane wa uhamasishaji kilimo, biashara pamoja na masuala ya tabia nchi katika nchi za Afrika Mashariki (PACTEAC 2), mradi uliokuwa ukiratibiwa na ESRF ambapo pia walijadili matokeo ya mradi huo awamu pili tangu kuzinduliwa kwake, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ESRF mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.

MVUA ZA VULI ZITAKUWA ZA WASTANI -MAMLAKA YA HALI YA HEWA.

0
0
Na Karama Kenyunko, Michuzi TV.

MAMLAKA ya Hali ya Hewa nchini (TMA) imesema kuwa, mvua za vuli zinazotarajia kuanza kunyesha kipindi cha Mwezi Oktoba hadi Desemba 2019 zitakuwa za wastani hadi chini ya wastani.

Mvua hizo zinatarajiwa kunyesha katika maeneo ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki na Pwani ya Kaskazini.Huku Mikoa ya Kanda ya Ziwa Viktoria pamoja na Kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma mvua zinatarajia kunyesha za wastani hadi juu ya wastani.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Agnes Kijazi amesema hayo leo Septemba 3, 2019 jijini Dar es Salaam, wakati akitoa utabiri wa Hali ya Hewa msimu wa mvua za vuli ambazo hupata misimu miwili ya mvua kwa mwaka (Nyanda za juu Kaskazini Mashariki, Pwani ya Kaskazini, Ukanda wa Ziwa Viktoria pamoja na Kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma.

Dkt. Kijazi amesema, joto la juu ya wastani katika bahari ya Hindi linatarajiwa kuongezeka katika kipindi hicho huku uwezekano wa matukio ya vimbunga katika maeneo ya Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi yanaweza kutokea.

Ameongeza kuwa kwa mikoa mingi mvua hizo zinatarajia kuanza kunyesha katika wiki ya pili ya mwezi Oktoba na kumalizika wiki ya nne ya mwezi Desemba 2019 katika baadhi ya maeneo

Amesema, mvua za nje ya misimu zinazoendelea kunyesha mkoani Kagera toka mwezi Agosti na zinatarajiwa kuendelea kunyeshaa hadi kufikia wiki ya pili ya mwezi Oktoba na hivyo zitaungana na msimu wa mvua za vuli ambazo zinatarajiwa kumalizika wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi Januari 2020.

"Mvua hizo zinatarajiwa kuendelea kusambaa katika Mikoa ya Mwanza, Geita, Mara, Simiyu na Shinyanga katika wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Oktoba. Kiwango cha mvua kinachotarajiwa katika msimu huu ni mvua za wastani hadi juu ya wastani katika maeneo mengi ya ukanda huo," amesema Dkt.Kijazi 

Amesema mvua katika ukanda wa Pwani ya Kaskazini katika mikoa ya Dar es salaam,Tanga,Pwani,Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Kaskazini mwa Mkoa wa Morogoro zinatarajiwa kuanza kunyesha katika wiki ya pili ya mwezi Oktoba ingawa mtawanyiko wake unatarajiwa kuwa hafifu.

Pia kutakuwepo vipindi virefu vya ukavu na mvua chache zinatarajiwa kuwepo katika maeneo mengi ya Ukanda wa Pwani ya Kaskazini ambapo kutakuwa na mvua za wastani kuanzia wiki ya pili ya mwezi Novemba na kuisha katika wiki ya nne ya mwezi Disemba.

"Katika mikoa ya Nyanda za juu Kaskazini Mashariki Mikoa ya Kilimanjaro,Arusha na Manyara mvua zinatarajiwa kuanza katika wiki ya nne ya mwezi Oktoba kutarajiwa kuwa za wastani hadi chini ya wastani katika maeneo mengi ya mikoa hiyo ambapo Mvua hizi zinatarajiwa kuisha katika wiki ya nne ya mwezi Desemba 2019," amesema Dkt Kijazi

Dkt. Kijazi amesema, katika maeneo yanayotarajiwa kuwa na mvua nyingi matukio ya magonjwa ya mlipuko yanaweza kujitokeza na pia maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za wastani hadi chini ya wastani pia yanaweza kupata magonjwa ya mlipuko kutokana na uhaba wa Maji safi na salama

"Vipindi vifupi vya mvua kubwa vinarajiwa kujitokeza hata katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za wastani na chini ya wastani.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Dk. Agnes Kijazi akitangaza utabiri wa msimu wa mvua za vuli kwa waandishi wa habari katika kipindi, cha Octoba hadi Disemba, 2019 (OND). Utabiri huo umetangazwa leo Septemba 3, 2019 kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Hali ya hewa (TMA) Ubungo Plaza jijini Dar es salaam kulia kwake ni Mkurugenzi wa Huduma za utabiri, Hamza Kabelwa, na kushoto ni Meneja wa huduma za utabiri Samwel Mbuya.
baadhi ya wanahabari na wadau wa TMA wakifuatilia utabiri huo

TUTAFANYA MABADILIKO MAKUBWA KWENYE SEKTA YA KILIMO-WAZIRI HASUNGA

0
0


Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Katikati) akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe Job Daud Masima (Kulia) katika Ofisi za Ubalozi huo zilizopo katika mtaa wa 12, Abba Hillel Silver Jijini Tel Aviv nchini Israel. Mwingine ni Mwambata Jeshi Brigedia Jenerali Kahema Juni Mziray, Leo Tarehe 3 Septemba 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Kulia) akizungumza na Mkuu wa Mradi wa Umwagiji Afrika kampuni ya Netafim Ndg Shay Haxter mara baada ya kutembelea katika shamba la utafiti wa kilimo wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku sita nchini Israel. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe Job Daud Masima Leo Tarehe 3 Septemba 2019.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Tanzania walioshiriki mafunzo ya Kilimo nchini Israel kwenye shamba la mifugo la Jacob's Farm, Mwingine pichani ni Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe Job Daud Masima (Kulia), Leo Tarehe 3 Septemba 2019.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Israel zilizopo katika mtaa wa 12, Abba Hillel Silver Jijini Telaviv nchini Israel, Leo Tarehe 3 Septemba 2019.



Na Mathias Canal, Telaviv-Israel

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesema kuwa serikali YA Tanzania imejipanga kuikabili sekta ya kilimo ikiwa ni pamoja na kuona umuhimu wa kuwaandaa watanzania katika kubadilisha kilimo chao kutoka kwenye kilimo cha kujikimu na kuwa kilimo cha kibiashara.

Waziri Hasunga ameyasema hayo leo tarehe 3 Septemba 2019 wakati akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe Job Daud Masima katika Ofisi za Ubalozi huo zilizopo katika mtaa wa 12, Abba Hillel Silver Jijini Tel Aviv nchini Israel.

Alisema kuwa katika ziara yake hiyo amejifunza namna ambavyo nchi ya Israel imepiga hatua ya ujuzi katika sekta ya kilimo hivyo kuona umuhimu wa serikali ya Tanzania kuwekeza katika skimu za umwagiliaji.

Alisema kuwa asilimia kubwa ya wakulima nchini Tanzania wanatumia majembe ya mkono katika kilimo jambo ambalo haliwezi kuongeza tija na uzalishaji. “Tunatumia majembe ya mkono mbaya zaidi kilimo chetu kinategemea msimu wa mvua, hivyo kilimo cha namna hiyo bado kinatuchelewesha, tuna wajibu wa kujifunza kwa wenzetu walioendelea” Alisema Mhe Hasunga

Alisema kwa kuanza serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa kilimo inaweza kujenga mabwawa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji ili kuongeza uwezo wa kilimo cha umwagiliaji kitakachofanya kazi msimu mzima badala ya kilimo cha kutegemea mvua.

Mhe Hasunga alisema kuwa Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kadhalika wizara ya Viwanda na Biashara zitafanya kazi kwa pamoja ili kuona namna ya kuzalisha kwa tija mazao ya kilimo na kutoa malighafi nyingi zitakazochangia katika kuinua na kuchagiza matakwa ya serikali ya kuwa na serikali ya viwanda.

Kuhusu masoko ya mazao yanayozalishwa nchini Tanzania Mhe Hasunga alisema kuwa serikali inaendelea na mkakati maalumu wa kuimarisha masoko kwani imeanzisha kitengo maalumu katika wizara ya kilimo kitakachokuwa na wajibu wa kushughulikia masoko ya mazao ya wakulima.

Katika hatua nyingine Waziri Hasunga ameyaalika makampuni mbalimbali ya Israel yanayojishughulisha na kilimo kutembelea nchini Tanzania kwa ajili ya kujionea fursa za uwekezaji zilizopo nchini Tanzania.

“Tanzania ni nchi yenye rutuba nzuri, eneo kubwa kwa ajili ya uwekezaji wa kilimo, hivyo nayaalika makampuni yote yanayohusika na kilimo hususani yanayojishughulisha na utafiti, kutembelea Tanzania kwani ni nchi yenye eneo zuri na kubwa kwa ajili ya uwekezaji hususani katika sekta ya kiliumo” Alikaririwa Mhe Hasunga

Mhe Hasunga amesema kuwa Israel ni nchi yenye eneo dogo kwa ajili ya kilimo lakini wanazalisha chakula kinachotosheleza wananchi wake sambamba na kuuza mazao yao nje ya nchi jambo ambalo linaimarisha pato la serikali ya nchi hiyo na kipato cha mtu mmoja mmoja.

Vilevile, waziri Hasunga ameupongeza Ubalozi wa Tanzania nchini Israel unaoongozwa na Mhe Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe Job Daud Masima na watendaji wengine wote kwa kazi nzuri wanayoifanya ya uwakilishi wa Tanzania, Aidha Mhe Hasunga amemuomba Balozi huyo kutafuta fursa zaidi za makampuni ya kilimo na viwanda kwa ajili ya kuwekeza nchini Tanzania.

Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe Job Daud Masima amesema kuwa miongoni mwa mambo muhimu ya kuyafanyia kazi ni pamoja na kutafuta namna ya kuongeza idadi ya vijana wanaoshiriki katika mafunzo ya kilimo ya Agro Studies ili izidi kuongezeka maradufu.

Kadhalika, alisema kuwa ofisi yake inaendelea kufanya kazi kubwa kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea nchini Tanzania kwani idadi kubwa ya watalii inaongeza pato la kigeni la nchi.

Balozi Masima alisema kuwa nchi ya Israel ina mafanikio makubwa kwenye sekta ya teknolojia hivyo ni wajibu wa Tanzania kutumia fursa hiyo muhimu katika elimu ya ujuzi wa teknolojia za kilimo hususani umwagiliaji.

WAZIRI MWAKYEMBE AHAMASISHA UWEKEZAJI KATIKA VIWANDA, MADUKA MAKUBWA YA VIFAA VYA MICHEZO

0
0
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrson Mwakyembe akizungumza na wadau wa soka katika  uzinduzi wa tamasha la Kahama United Sport Academy

Na Mwandishi Wetu, Kahama

SERIKALI  kupitia Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo imewataka Watanzania na wawekezaji kutoka nje ya nchi  kuwekeza katika kujenga maduka makubwa ya vifaa vya michezo na viwanda  ili kupunguza gharama za kuagiza kutoka nchi za nje.

Kwa sasa Serikali ipo katika mazungumzo na baadhi ya wawekezaji kwa ajili ya kuona umuhimu wa kujenga viwanda na maduka makubwa ya vifaa vya michezo ili wananchi wanunue kwa bei ndogo na hatimaye kukuza sekta ya michezo nchini Tanzania ambayo ina nafasi kubwa ya kutoa ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi katika taifa.

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dk.Harison Mwakyembe aliyasema hayo wakati akizindua Kituo cha kulelea watoto cha Kahama United Spots Academy ambapo amesema kwa sasa nchi ipo katika mapinduzi makubwa ya michezo.

Dk.Mwakyembe amesema anawakaribisha watanzania na wawekezaji kutoka nje ya nchi  wenye uwezo wa kuwekeza kupitia  katika Wizara yake na kuzungumza nao ili kufanikisha upatikanaji wa vifaa vya michezo hapa hapa nchini na hivyo kupunguza bei ya kununua vifaa hivyo.

 Aidha amesema Tanzania ipo vizuri katika suala zima la michezo na kuongeza kuwa mradi huo ulioanzishwa na wadau wa soka wilayani Kahama ni mkubwa  na kwamba wilaya na mikoa mingine itaiga mfano huo huku akiwapongeza wadau wa michezo Wilaya ya Kahama kwa kuanzisha kituo hicho.

Hata hivyo Waziri Mwakyembe ameutaka uongozi wa Kahama Spots Academy kuhakikisha kuwa inatafuta maeneo makubwa nje ya mji kwa ajili ya uwekezaji wa michezo badala ya kung’ang’ania kuwekeza mijini ambapo maeneo ni madogo.

Awali akisoma risala ya kituo hicho Katibu wa Bodi ya Kahama Spots Academy Shabani Nguno amesema kuwa vijana waliopo katika kitu hicho ni wa umri wa kuanzia miaka 15, 17, pamoja na 20 huku wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa shuyle mbalimbali za sekondari katika Wilaya ya Kahama.

Nguno amesema kuwa vijana wote katika kituo hicho wanapata mafunzo ya kuanzia madarasani  na katika michezo na kuongeza kuwa watu matajiri kwa sasa wanatokana na michezo na hivyo wameamua kuwekeza ili kuwasaidia vijana hao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Kahama Spots Academy Khamis Mgeja amesema lengo kubwa la kituo hicho ni kuunga mkono jitihada za Rais John Magufuli kwa kutumia sekta ya michezo katika kukuza uchumi wa taifa kwa ujumla na wadau wa kahama wakaamua kujikita kuwekeza katika michezo.

Wakati huo huo Mkuu wa Wilaya Kahama Anamringi Macha amesema wazazi kuhakikisha kuwa wanawahimiza watoto wao kuwa na utamadumni wa kupenda michezo  kwani inasaidia katika kujenga mwili na kukuza akili kwa ujumla wake.

Macha amesema Kahama kuna fursa nyingi  na rasilimali za kutosha ikiwa ni pamoja na maeneo makubwa kwa ajili ya viwanja vya mpira  na michezo mingine na kuongeza kuwa kwa kufunguliwa kituo hicho ni moja ya matunda ya kukuza michezo kahama.

Katika hafla hiyo Waziri Mwakyembe alizawadiwa na Academy kupitia Mwenyekiti wake Alhaji Abed Salum jezi ya timu yenye jina la Mwakyembe.

TAMISEMI QUEENS YAPANIA KUFANYA MAKUBWA LIGI DARAJA LA KWANZA NETIBOLI TANZANIA BARA

0
0
Mfungaji tegemeo wa TAMISEMI QUEENS Lilian Jovin akifunga mojawapo ya magoli muhyaliyoiwezesha timu yake kushika nafasdi ya pili katika michuano ya netiboli ligi daraja la kwanza inayoendelea katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma

……………………

Na Mathew Kwembe, Dodoma

Timu ya netiboli ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ‘TAMISEMI QUEENS’ imejigamba kufanya vizuri katika michuano inayoendelea ya netiboli ligi daraja la kwanza inayoendelea katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Tayari timu hiyo imeshinda michezo minne kati ya sita iliyokwishacheza na hivi sasa inashika nafasi ya pili mbele ya vinara timu ya Mbweni JKT kutoka jijini Dar es salaam.

TAMISEMI QUEENS imekwishazifunga timu za Cocacola,Jiji la Dodoma, Jiji la Tanga na SMART na imepoteza michezo miwili hadi sasa ambayo ni ya Mbweni JKT na Jiji la Arusha.

Akizungumzia michuano hiyo kocha wa timu hiyo Maimuna Kitete amesema kuwa timu yake ina nafasi nzuri ya kushiriki ligi ya muungano kutokana na maandalizi mazuri ambayo timu yake imeyafanya.

Amesema kufikia sasa timu yake imeonyesha upinzani mzuri dhidi ya timu tishio kama Mbweni JKT na ameahidi kuzichapa timu zote tatu zilizosalia katika michuano hiyo.

Kwa upande wake Meneja wa timu hiyo Doto Bintaraba amesema kuwa timu ya ‘TAMISEMI QUEENS’ ina uhakika wa kushika nafasi tatu za juu kutokana na kuwaandaa vijana wake kufanya makubwa katika michuano ya ligi daraja la kwanza inayoendelea jijini Dodoma.

Amesema ari kubwa waliyo nayo wachezaji wake imempa imani ya kuendelea kufanya vizuri katika mechi tatu zilizosalia.

Naye mchezaji Lilian Jovin ambaye ndiye mfungaji tegemeo wa ‘TAMISEMI QUEENS’ amesema kuwa timu yake inaendelea kuimarika siku hadi siku na akaahidi kufanya vizuri katika michuano iliyobaki ya ligi daraja la kwanza.

Amesema kuwa kufikia sasa timu yake haiwaogopi timu yoyote na akawatahadharisha timu pinzani watakazokutana nazo wajipange kupata kipigo kitakatifu.

Kauli ya Lilian iliungwa mkono na mchezaji mkongwe wa timu hiyo Flora Odilo ambaye aliahidi ushindi mnono kwenye michezo mitatu iliyosalia katika michuano ya ligi hiyo.

‘TAMISEMI QUEENS’ imebakiza mechi dhidi ya Eagle, JKT Makutupora na JKT Mbweni.

Hadi sasa wanaoongoza ligi hiyo ni timu ya JKT Mbweni yenye pointi 10, ikifuatiwa na ‘TAMISEMI QUEENS’ikiwa na pointi 8, huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na timu ya JKT Makutupora iliyo na pointi 8 pia huku nafasi ya nne na ya tano zikichukuliwa na timu za Jeshi Stars na Jiji la Arusha.

Mbali na michuano hiyo kutoa bingwa wa mchezo wa netiboli Tanzania Bara, timu sita za juu zitafanikiwa moja kwa moja kushiriki ligi ya netiboli ya muungano iliyopangwa kufanyika mjini Zanzibar baadaye mwaka huu.

MKUU WA WILAYA YA UBUNGO APATIWA ELIMU KUHUSU MAHAKAMA INAYOTEMBEA

0
0
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Kisare Matiku Makori (kulia) akipatiwa elimu kuhusu gari maalum la Mahakama Inayotembea kwenye eneo la Kibamba jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kimara, Mhe.Geiza Mbeyu. (katikati) ni Karani wa Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Nise Mwasalemba.
Karani wa Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Nise Mwasalemba(kulia) akiwaelezea baadhi ya wakazi wa Kimara Stopover, jijini Da res Salaam kuhusu Mahakama Inayotembea Inavyofanya kazi baada ya kuwapatia elimu.(Picha na Aziza Muhali – SJMC)

RAIS WA ZANZIBAR DKT.SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI WA OFISI YA RAIS NA MWENEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI

0
0

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, wakati wa mkutano wa Utekelezaji wa Bajeti na Mpango Kazi wa Wizara hiyo kwa mwezi wa Julai 2018 hadi Juni 2019, uliofanyika Ikulu Zanzibar leo 3-9-2019

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Issa Haji Gavu, akiwasilisha ripoti ya Utekelezaji wa Bajeti na Mpango Kazi kwa Julai 2018 hadi Juni 2019, kulia Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ndg.Salum Kassim Ali


BAADHI ya Watendaji wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, wakifuatilia taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti na Mpango Kazi wa Ofisi yao kwa mwezi Julai 2018 hadi Juni 2019, uliofanyika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.


NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ndg Salum Kassim Ali, akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti na Mpango Kazi kwa mwezi Julai 2018 hadi Juni 2019, wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, , wakati wa mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar, ukiongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, hayuko pichani.


BAADHIU ya Wakurugenzi wa Wizara ya Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, wakifuatilia uwasilishwaji wa Ripoti ya Utekelezaji wa Bajeti na Mpango Kazi kwa Ofisi yao kwa mwezi Julai 2018 hadi Juni 2019, uliofanyika ukumbi wa Ikulu Zanzibar, ukiongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, hayupo pichani.


MSHAURI wa Rais Masuala ya Sanaa na Utamaduni Mhe. Chimbeni Kheri , akizungumza wakati wa mkutano wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, kuzungumzia Utekelezaji wa Bajeti na Mpango Kazi wa Ofisi hiyo kwa mwezi wa Julai 2018 hadi Juni 2019, uliofanyika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.(Picha na Ikulu)

MACHINGA KAZI KAZI

0
0


Mfanyabiashara ndogondogo maarufu kama Machinga amaye jina lake halikupatikana akitembeza bidhaa  wakati wakisaka wateja katika foleni ya magari, Barabara ya Bagamoyo eneo la Sayansi leo jijini Dar es Salaam. 
(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)
Wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Machinga wakiteta jambo wakati wakisaka wateja katika foleni ya magari, Barabara ya Bagamoyo,eneo la Sayansi leo jijini Dar es Salaam.

KINACHOENDELEA AFRIKA KUSINI,TATIZO LIPO,LINAHITAJI TIBA YA HARAKA

0
0



Ndugu zangu,

Nimeangalia picha za video na mnato kuhusu kinachoendelea Afrika Kusini. 

Xenophobia, ni hali ya wenyeji kujiona wana haki zaidi na kuwakataa wageni katika jamii. Huu ni ugonjwa, tunao umetuganda.

Tatizo lipo, tena kubwa na linahitaji tiba ya haraka. Ni namna tu ya kuliendea tatizo hilo. Hata sisi katika mikoa yetu tunazo chembe za Xenophobia ila pengine aina ya maamuzi tunayochukua ndiyo hayafanani.

Nakumbuka nikiwa mdogo mkoani Tanga, wakubwa zetu walitujengea mazingira ya kuwachukia Wasambaa. Kabila hili linatokea milimani Wilaya ya Lushoto.

Tulikuwa tunawachukia bila sababu, tuliwapa majina mabaya. Kila lisilofaa au kila tabia isiyofaa ilinasibishwa na kabila la wasambaa.

Walionekana watu wa hovyo, walionekana wana vurugu na kila baya. Wachafu, hawana staha na mengi ambayo naona haya hata kuyataja hapa 
Sababu ya hayo ni uvivu wa kaka na pengine baba zetu, hawakutaka kazi ngumu kama kubeba mizigo sokoni, kuuza mihogo na kutembeza kahawa barabarani.

Wasambaa walifanya kila kazi; mradi hawakuvunja sheria. Mbali ya kudharauliwa hawakuvunjika moyo.

Hivi nizungumzapo asilimia kubwa ya wale vijana wa Kisambaa ambao ni mahamia wa Tanga katika mika ya 1970 na 1980 hadi 1990 leo ndio matajiri wa Tanga.

Wanamiliki maduka, mabasi na biashara ya nafaka. Wanamiliki asilimia 80 ya biashara katika soko kuu la Ngamiani. Wana fedha.

Sisi watoto wa 'Kiungwana' tuliowabeza tumeishia kusubiri 'maa' (Mama) au 'baa' (Baba) atoe pesa ndio nyumbani kuliwe.

Sisemi vijana wote wa Tanga mjini hawataki kazi, la. Ila wapo waliojiendeleza kwq elimu, kazi za ajira au biashara. 

Hiki ndicho kinachotokea sasa Afrika Kusini. Baada ya uhuru mwaka 1994, wenyeji walidhani zile nyumba, magari, mashamba na biashara walizokuwa wakishikilia Makaburu watapewa wao; bure.

Nelson Mandela, akawaambia hawa Makaburu hapa ndio kwao. Hawana pa kwenda kwani walifika 'Cape of good hope' mwaka 1488.

Historia inasema mzungu wa kwanza kufika Caoe Town ni Mreno, Bartolomeu Dias mwaka huo wa 1488.

Baadaye mwaka 1497 Mdachi, Vasco da Gama alipita wakati akiitafuta India. Alikaa bandari ya St. Helena Bay kwa siku nane ndipo akavutiwa na mandhari ya Afrika Kusini.

Aidha, kampuni ya kwanza ya Kidachi ambao ndio asili ya Makaburu, ilianza biashara mwaka 1647. Ikiitwa The Dutch East India Company.

Sasa Mandela aliuliza watu hao unawaambia warudi kwao baada ya kukaa katika ardhi hiyo kwa miaka zaidi ya 400.

Hilo liliwavunja nguvu, wengi hawajui kama Mandela si maarufu na hapendwi sana Afrika Kusini kuliko nchi nyingine za Afrika. Sababu ni hiyo, anaonekana 'Snitch.'

Kuanzia miaka ya 1995 waafrika kutoka kila kona ya bara hili wakaanza kumiminika kutafuta fursa. Kutoka Tanzania, Zimbabwe, Nigeria, Kenya na kwengine kwingi.

Mwanzo raia wa Afrika Kusini waliona kawaida, ila kadiri siku zilivyokwenda mambo yakawawia magumu.

Raia wa kigeni hawana makuu, wakipanga nyumba ya vyumba vitano watakaa hata 50. Wakila mlo mmoja poa, wakikosa wanashukuru. Hivyo, ajira ya mshahara wowote kwake ni neema.

Wenye akili walifanya kazi kama mbwa bata kazi nne kwa siku. Kila wakilipwa wanatuma pesa kwao kujenga nyumba, kusomesha ndugu zao na kulea familia.

Sasa mambo yamegeuka. Raia wanataka kurudishiwa kazi zao. Wameshacheleqa maana serikali haina cha kuwapa. Na matajiri ambao asilimia kubwa ni wahindi na wazungu wameshazoea waahiriwa wanaotaka mshahara mdono na wanaofanya kazi kubwa.

Raia wao wanataka kazi na bata.

Makala hii kwa hisani ya Mhariri wa Jamvi la Habari-Hafidhi Kido
Viewing all 109597 articles
Browse latest View live




Latest Images