Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109593 articles
Browse latest View live

Mfuko wa Mazingira kutatua changamoto za mabadiliko ya tabianchi

0
0
Serikali imesema Mfuko wa Dhamana ya Mazingira ulioanzishwa na Ofisi ya Makamu wa Rais utasaidia katika kutatua changamoto mbalimbali za kimazingira zikiwemo mabadiliko ya tabianchi.

Hayo yamesemwa leo Agost 30, 2019 na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mussa Sima wakati akiwasilisha taarifa kuhusu mabadiliko ya tabia nchi mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira.

Mhe. Sima alisema kuwa ni kweli zipo changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya mazingira na Ofisi hiyo imeona ni jambo zuri kuanzisha Mfuko huo utakaosaidia kuimarisha mapato na hivyo kuweza kuzitatua.     

Akitolea majibu kuhusu maoni ya baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo waliopendekeza kuwa taasisi zingine za Serikali zenye uhusiano wa moja kwa moja na masuala ya mazingira zichangie sehemu ya mapato yake kwenye Mfuko wa Mazingira ili uweze kufanya kazi zake.
"Mheshimiwa Mwenyekiti tumeyapokea maoni ya wajumbe wa Kamati hii tutayafanyia kazi na sisi tutakaa na wataalamu wetu tutayaweka vizuri kuyaleta kwenye Kamati hii ili," alisema Naibu Waziri.

Awali katika taarifa hiyo iliyowasilishwa ilibainisha juhudi za Serikali katika kubabiliana na mabadiliko ya tabianchi kuwa ni pamoja na kutekeleza miradi na programu mbalimbali inayosaidia katika utunzaji wa mazingira.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima akitolea ufafanuzi hoja mbalimbali katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira.

SERIKALI ITAENDELEA KUSHIRIKIANA NA UNHCR-MAJALIWA

0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim M. Majaliwa akiwa katika mzungumzo na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo Grandi. Mazungumzo hayo yamefanyika kando na mkutano wa TICAD7 Yokohoma,Japan.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akifuatilia mazungumzo kati ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim M. Majaliwa na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo Grandi(hayupo pichani) Yokohama, Japan.
Mazungumzo kati ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim M. Majaliwa na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo Grandi kuhusu wakimbizi waliopo Tanzania yakiendelea. Yokohama, Japan.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim M. Majaliwa akiagana na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo Grandi mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo baina yao kuhusu wakimbizi waliopo Tanzania. Mazungumzo hayo yamefanyika Yokohama, Japan.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akisalimiana na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo Grandimara baada ya kumaliza kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu mhe. Kassim M. Majaliwa. Yokohama, Japan.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiteta jambo na Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) Bw Filippo Grandi mara baada ya kumalizika mazungumzo ya Waziri Mkuu mhe. Kassim M. Majaliwa. Yokohama, Japan.


SERIKALI ya Tanzania itaendelea kushirikiana na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) katika kutatua changamoto zinazotokana na uwepo wa wakimbizi nchini pamoja na kutafuta suluhu ya kudumu kwenye nchi zao ili wakimbizi hao waweze kurejea makwao kuendelea na shughuli za maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo (Ijumaa, Agosti 30, 2019) katika mazungumzo yake na Kamishna Mkuu wa UNHCR, Bw. Filippo Grandikwenye Kituo cha Maonyesho cha Yokohama nchini Japan baada ya kuhitimishwa kwa Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (Tokyo International Conference on African Development – TICAD 7).

Katika mazungumzo hayo, Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa UNHCR kuisaidia mikoa inayokaliwa na wakambizi kutokana na kuharibiwa kwa mazingira. “Hata hivyo Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na UNHCR kuimarisha ulinzi wa maeneo ya wakimbizi ili wananchi wa maeneo hayo waendelee kuishi kwa amani na utulivu.”

Kwa upande wake, Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR), Bw. Filippo Grandi amesema amefurahishwa na utayari wa Serikali ya Tanzania katika kupokea wakimbizi na usikivu wa Rais Dkt. John Magufuli katika kushughulikia changamoto za wakimbizi. 

Waziri Mkuu yupo nchini Japan akimwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye Mkutano wa Kilele wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (Tokyo International Conference on African Development – TICAD 7) ambao umehitimishwa leo.

Waziri Mkuu ameambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi na viongozi mbalimbali kutoka Serikali ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Dk Mahiga ahitimisha mchakato wa maboresho ya sekta ndogo ya mfumo wa haki jinai

0
0
Charles James

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk Augustine Mahiga amefunga zoezi lilioanza Julai mwaka huu la kupitia mfumo wa haki jinai ili kuufanyia maboresho.

Dk Mahiga amesema Wataalamu kutoka Wizara, Taasisi za Serikali na Asasi za kiraia wamekua wakichambua na kujadili masuala mbalimbali katika mfumo wa haki jinai ambayo yamekua kikwazo katika kushughulikia na kusimamia masuala ya kijinai nchini.

" Kazi hii imefikia hatua ambayo mtapitishwa na kujadili maeneo yaliyopendekezwa kuboreshwa ili kuifanya mfumo huu kuwa rafiki Kwa wadau wa haki jinai," amesema Dk Mahiga.

Amesema mfumo huo kwa ujumla unahusisha mnyororo wa hatua mbalimbali zinazotokea wakati wa kushughulikia uhalifu kuanzia katika ngazi ya kuzuia uhalifu usitokee, kutambua unapotokea m, kukamata wale wanaofanya uhalifu, kupeleleza, kushitaki mahakamani na kutoa adhabu.

Katika mnyororo huo mambo mbalimbali yamewekwa kisheria ya namna ya kushughulikia wahalifu ambayo yanashughulikiwa na vyombo au Taasisi mbalimbali za jukwaa la haki na jinai.

Mara ya mwisho kupitia mfumo huo n kuufanyia maboresho ni takribani miaka 20 iliyopita hivyo ni muhimu kupitia mfumo huo na kuufanyia maboresho ili kuendana na wakati uliopo." Niwapongeze wataalamu wetu ambao mmekua hapa kwa miezi miwili na wote ambao mmeshiriki katika kazi hii hadi hatua hii ya leo.

" Niwashukuru Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala Mikoa kwa kutenga muda wao kutembelea wakati wa mchakato wa maboresho haya kwa ngazi ya watalaamu. Nimshukuru pia Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally ambaye nae alitenga muda wake na kutembelea wataalamu wakati wa mchakato," amesema Dk Mahiga.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Augustine Mahiga akizungumza wakati wa hitimisho la mchakato wa maboresho ya sekta ndogo ya haki jinai.
 Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Augustine Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa mchakato wa maboresho wa sekta ndogo ya mfumo wa haki jinai. Kushoto kwake ni Waziri wa Nchi Utumiahi, Kepteni George Mkuchika na kulia ni Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana, Anthony Mavunde.

MAHAKAMA YAELEZWA MWANDISHI ERICK KABENDERA AMEPOOZA MGUU, HAWEZI KUPUMUA VIZURI

0
0
Na Karama Kenyunko, Michuzi Tv.

UPANDE wa utetezi katika kesi ya Uhujumu Uchumi inayomkabili mwandishi wa habari za uchunguzi Erick Kabendera umeiomba mahakama kuliamurau Jeshi la Magereza kumpeleka mshtakiwa huyo hospitali yoyote ya serikali ikiwamo Muhimbili kupata vipimo kwani anasumbuliwa na maradhi yasiyojulikana kwani hawezi kupumua wala kutembea sababu amepooza mguu.

Wakili wa utetezi, Jebra Kambole amedai hayo leo Agosti 30,2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Janeth Mtega wakati kesi ilipokuja kwa ajili ya kutajwa baada ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwizile aliyepangiwa  kusikiliza kesi hiyo kuwa na udhuru wa kikazi.

Wakili Kambole amedai, mteja wao anasumbuliwa na maradhi yasiyojulikana ikiwamo kupoteza nguvu mwilini, kushindwa kupumua vizuri wakati wa usiku na kuzimia mara kwa mara.

Mapema, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon amedai mahakamani hapo kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa lakini kuna maeneo bado wanaendelea na uchunguzi kwa hiyo upelelezi wake bado haujakamilika.

Wakili wa utetezi, Kambole alidai kuwa wanaomba Jamhuri kuharakisha upelelezi kwa sababu mshtakiwa anakabiliwa na tuhuma ambazo hazina dhamana na pia mshtakiwa ana matatizo ya afya tangu usiku wa kuamkia Agosti 21, mwaka huu akiwa gerezani alianza kuumwa mpaka leo bado hali yake haijaimarika anapata shida kupumua inapofika usiku.

"Mheshimiwa mimi mwenyewe nilikwenda kumwona mshtakiwa, anashindwa kutembea anaishiwa nguvu na wakati mwingine anapoteza fahamu (kuzimia), mpaka sasa ndugu zake hawafahamu kinachomsumbua ni nini hivyotunaomba mahakama itoe amri kwa Jeshi la Magereza kumpeleka mshtakiwa hospitali yoyote ya serikali ikiwamo Muhimbili kwa ajili ya kupata vipimo vinavyostahili ili apate matibabu na ijulikane anaumwa nini, mshtakiwa ana haki ya kupata huduma bora. " amedai Kambole.

Akijibu hoja hizo, Wankyo alidai kuwa atafikisha taarifa mahali husika kuhusu kuharakisha upelelezi na pia kuhusu matibabu jeshi la magereza lina utaratibu wake wa kutoa huduma za matibabu kwa watuhumiwa.

"Si sahihi mahakama hii kutoa amri kulielekeza jeshi hilo kwamba apelekwe hospitali gani kwa sababu hajasema kama amekosa huduma hiyo gerezani, tuhuma zinazomkabili mshtakiwa zinasikilizwa na Mahakama kuu kwa hiyo mahakama hii haina mamlaka ya kusikiliza hoja na kutoa uamuzi"alidai Wankyo.

Akifafanua zaidi Wankyo alidai kuwa kama utetezi wana hoja wawasilishe mbele ya Hakimu anayesikiliza usikilizwaji wa awali wa kesi hii.

Hakimu Mtega amesema amesikiliza hoja za pande zote mbili, amezihifadhi mpaka hakimu anayehusika na jalada hilo atakaporudi,  mshtakiwa arudishwe mahabusu mpaka Septemba 2, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Kabendera anadaiwa katika siku tofauti kati ya Januari 2015 na Julai 2019 katika maeneo tofauti jijini Dar es Salaam, alitoa msaada katika genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia faida.

Pia anadaiwa kushindwa kulipa kodi ya sh. 173, 247,047.02 ambayo ilitakiwa ilipwe TRA huku pia anadaiwa kujipatia Sh. Milioni 173.2 wakati akijua kuwa fedha hizo ni za kutakatisha na zao la makosa tangulizi ya kukwepa Kodi na kujihusisha na genge la uhalifu.

Waziri Mwakyembe Akutana na Kujadiliana na Wahariri Juu ya Tamasha la JAMAFEST

0
0

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe akisisitiza jambo kwa Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakati alipokutana nao leo29 Agosti, 2019 jijini Dar es Salaam kuzungumzia Tamasha la nne la Utamaduni wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalotarajia kufanyika hapa nchini kuanzia tarehe 21 hadi 28, Septemba 2019.

  Baadhi ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakimsikiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) wakati alipokutana nao leo 29 Agosti, 2019 jijini Dar es Salaam kuzungumzia Tamasha la nne la Utamaduni wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalotarajia kufanyika hapa nchini kuanzia tarehe 21 hadi 28, Septemba 2019.

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe akifafanua  jambo kwa Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakati alipokutana nao leo29 Agosti, 2019  jijini Dar es Salaam kuzungumzia Tamasha la nne la Utamaduni wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalotarajia kufanyika hapa nchini kuanzia tarehe 21 hadi 28, Septemba 2019.
 Baadhi ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakimsikiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) wakati alipokutana nao leo29 Agosti, 2019  jijini Dar es Salaam kuzungumzia Tamasha la nne la Utamaduni wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalotarajia kufanyika hapa nchini kuanzia tarehe 21 hadi 28, Septemba 2019.
Mhariri Mkuu wa E. FM Radio, Scholastica Mazula akichangia mada wakati Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe alipokutana na Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari leo  29 Agosti, 2019 jijini Dar es Salaam kuzungumzia Tamasha la nne la Utamaduni wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalotarajia kufanyika hapa nchini kuanzia tarehe 21 hadi 28, Septemba 2019.
Picha na WHUSM – Dar es Salaam

Mfumo Shirikishi wa Kusimamia Shughuli na Rasilimali za Taasisi (ERMS).

WADAU WA NAFAKA WAKUTANA DAR KUJADILI FURSA

0
0



NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

MKUTANO wa siku mbili wa Wafanyabiashara wa Nafaka Ndani na Nje ya Nchi umefunguliwa na Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo Agosti 29, 2019.

Mkutano huo ambao umewajumuisha wasindikaji, wasafirishaji na wamiliki wa maghala ya nafaka Lengo lake ni kuangalia fursa zilizopo kwenye tasnia ya nafaka na jinsi ya kuzifikia ikiwa ni pamoja na masoko.

Akizungumza na washiriki wa mkutano huo uliowakutanisha  wadau kutoka mikoa mbalimbali  nchini, Mhe. Hasunga ambaye alifuatana na Manaibu wake, Mhe. Husein Bashe, na Mhe. Omary Mgumba alisema mkutano huo utatoa fursa kwa wajumbe kuelimishwa kuhusu fursa ya biashara ya mazao ya nafaka katika soko la Afrika, uwezo wa Tanzania kuzalisha na nafasi ya wafanyabiashara kushiriki kikamilifu lakini pia washiriki watapata fursa ya kujifunza athari za upotevu wa mazao ya nafaka baada yamavuno na mkakati wa serikali kudhibidi hali hiyo.

“Kitaalamu wanasema utafiti uliofanyika Tanzania na  nchi nyingi za Kusini asilimia 40 ya mazao yote yakiwemo ya nafaka yanapotea baada ya mavuno kwa kuharibika na matatizo mengine, hii haikubaliki mkulima amewekeza, amevuna halavu mazao yake yanaharibika, lazima tuwe na mkakati wa kuzuia hali hii.” Alitoa hakikisho Mhe. Waziri Hasunga na kuongeza.

Kulingana na uzalishaji uliopo, nafaka nyingi kama mahindi mtama na nafaka nyingine huhifadhiwa katika kiwango kisichoridhisha hali hii huchangia kupoteza ubora wa nafaka na hatimaye huchangia kuzorota kwa ustawi wa afya zetu, alifafanua zaidi Mheshimiwa Waziri.

Alisema Agosti 1, mwaka huu kwenye sherehe za Nanenane kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muunganow a Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alizindua mkakati wa namna ya kupambana na kudhibiti upotevu wa mazao baada ya mavuno.

Katika utafiti wake ilioufanya hivi karibuni Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) chini ya Mradi wa Rapid Response Implementation Support to the Ministry of Agriculture and Agriculture Sector Lead Ministry (RARIS) unaofadhiliwa na Taasisi ya Bill and Melinda Gates Foundation umebaini kuwa hali ya maghala mengi ya watu binafsi hayatoi taarifa serikalini na hii ni kutokana na mfumo wa sasa wa maghala.

Akitoa mada kuhusu mahusiano kati ya maghala (Storage facilities na upotevu wa mazao baada ya mavuno, post harvest losses), Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Dkt.Hoseana Lunogelo alisema ESRF ilifanya utafiti wa hali (status) ya maghala nchini na kubaini kuwa maghala ya watu binafsi hayalazimiki kisheria kutoa taarifa serikalini kuhusu nini kimehifadhiwa na kiasi gani cha nafaka kilichohifadhiwa ndani ya maghala hayo na hali hii serikali inategemea tu maghala ya Serikali yaani (Public Storage Facilities ) kupitia Werehouse Reseat Regulatory Board ili kujua takwimu za hali ya chakula nchini.

“Kwa sasa kuna maghala 3,430 yaliyopo kati ya hayo ni 185 tu ndiyo kuna uhakika wa kupata tawimu endapo zitahitajika lakini yaliyosalia huwezi kupata takwimu hizo kwa sababu hakuna sheria inayowalazimisha kufanya hivyo.” Alifafanua Dkt. Lunogelo.

Alisema hii ni changamoto kubwa, kama serikali inapata taarifa kutoka kwenye maghala machache sana nchini na yale mengi haipati taarifa zake, maana yake Serikali haiwezi kufanya maamuzi sahihi kuhusiana na upatikanaji wa chakula nchini na hiyo ina athari mbaya kwenye usalama wa chakula na pia ina athari mbaya pia kwenye biashara.” Alsiema Dkt. Lunogelo.
 Wadau wa mazao ya nafaka, wakimsikiliza Waziri wa Kilimo Mhe. Japhate Hasunga wakati akihutubia mkutano wa siku mbili wa Wafanyabiashara wa Nafaka Ndani na Nje ya Nchi  kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam 
 Mhe. Waziri Hasunga.
 Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga akihutubia mkutano huo.
 Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Dkt.Hoseana Lunogelo, akiwasilisha mada kuhusu mahusiano kati ya maghala (Storage facilities na upotevu wa mazao baada ya mavuno, post harvest losses).
 Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Dkt.Hoseana Lunogelo, akiwasilisha mada kuhusu mahusiano kati ya maghala (Storage facilities na upotevu wa mazao baada ya mavuno, post harvest losses).
 Bi. Margareth Nzuki (katikati), akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF akifuatilia kwa makini mada iliyokuwa inawasilishwa na Dkt. Bunogelo kuhusu utafiti ambao ulifanywa na Taasisi hiyo kuhusu mahusiano kati ya maghala (Storage facilities na upotevu wa mazao baada ya mavuno, post harvest losses).

 Mkuurgenzi Mtednaji wa Benki ya Kilimo Tanzania (TADB), Bw.Japhet Justine akipiga makofi wakati mkutano huo ukiendelea.
 Mjumbe akifuatilia kwa makini mkutano huo.
  Mjumbe akifuatilia kwa makini mkutano huo.
 Bi.Margareth Nzuki (kushoto), kutoka ESRF akibadilishana mawazo na Bi. Vumilia L. Zikankuba kutoka Wizara ya Kilimo wakati wa mkutano huo.
 Mshiriki akitoa maoni yake.
 Oswald Mashindani (kushoto), kutoka ESRF akizunhumza jambo mbele ya Katibu Mkuu (mstaafu) Wizxara ya Fedha, Bw. Paniel Lyimo (katikati) wakati wa mkutano huo.
 Mhe. Hadsunga (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na manaibu waziri makatibu wakuu na Mwenyekiti wa TPSF.
 Washiriki wakiwa kwenye mkutano huo unaofikia kilele leo Agosti 30, 2019.
 Washiriki wakiwa kwenye mkutano huo unaofikia kilele leo Agosti 30, 2019.
Washiriki wakiwa kwenye mkutano huo unaofikia kilele leo Agosti 30, 2019.

HammerQ ft kivurande "Kimbaumbau" (walete) Official Audio


MAKAMISHNA WASTAAFU WA JESHI LA MAGEREZA WALIOSTAAFU UTUMISHI WAO KWA MUJIBU WA SHERIA, WAAGWA JIJINI DAR

0
0
 Kamishna Mstaafu wa Magereza, Gedion Nkana(kushoto) na Kamishna Mstaafu wa Magereza, Augustine Mboje(kulia) wakiwa kwenye gari maalum wakipita katikati ya Gwaride likiwa katika umbo la OMEGA ikiwa ni ishara ya kuwaaga rasmi baada ya kustaafu utumishi wao Jeshini. Hafla hiyo imefanyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es Salaam Agosti 30, 2019.
 Makamishna Wastaafu wa Magereza wakipita katika gari maalum wakiwapungia mikono Maafisa na askari pamoja na Wageni mbalimbali waliofika katika hafla ya kuwaaga wastaafu hao iliyofanyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam Agosti 30, 2019.
 Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kushoto) akiwa na Maafisa Waandamizi kutoka Vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini wakiwapungia mikono  Makamishna Wastaafu wa Jeshi la Magereza(hawapo pichani) katika hafla ya kuwaaga wastaafu hao iliyofnyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam Agosti 30, 2019.
 Kamishna Mstaafu wa Magereza, Gedion Nkana akikagua Gwaride maalum lililoandaliwa na Maofisa na askari wa Jeshi la Magereza kwa ajili ya kuwaaga wastaafu wa Jeshi hilo leo Agosti 30, 2019.
  Gwaride maalum lililoundwa na Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza likipita kwa mwendo wa haraka mbele ya Makamishna Wastaafu wa Jeshi hilo ambao wamestaafu utumishi wao kwa mujibu wa Sheria.
 Kamishna Mstaafu wa Magereza, Gedion Nkana(kushoto) na Kamishna Mstaafu wa Magereza, Augustine Mboje(kulia) wakiwa katika jukwaa kuu wakipokea salaam ya heshima kutoka kwa Gwaride maalum la kuwaaga leo Agosti 30, 2019 katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es salaam.
 Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akiteta jambo na Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza, John Casmir Minja mara baada ya gwaride maalum la kuwaaga Makamishna wastaafu wa Jeshi hilo ambao wamestaafu utumishi wao Jeshini kwa mujibu wa Sheria. Hafla hiyo imefanyika katika Viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania, Ukonga jijini Dar es Salaam leo Agosti 30, 2019.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa tatu toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Makamishna Jenerali Wastaafu wa Jeshi la Magereza(walioketi) pamoja na Makamishna Waliopo wa Jeshi Magereza, Makamishna Wastaafu wa Magereza na Maafisa Waandamizi wastaafu wa Jeshi la Magereza(waliosimama mstari wa nyuma) mara baada ya ya Gwaride rasmi la kuwaaga Makamishna Wastaafu wa Jeshi hilo leo Agosti 30, 2019(Picha  zote na Jeshi la Magereza).

WAZIRI LUGOLA KUHUGHULIKIA VYAMA VYA SIASA VILIVYOTANGAZA KUFANYA MIKUTANO YA HADHARA KABLA YA MUDA

0
0
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na waandishi wa Kituo cha Channel Ten na Redio Magic (hawapo pichani), wakati walipokuwa wanamuhoji jijini Dar es Salaam, leo, kuhusu hali ya usalama wa nchi. Katika mahojiano hayo, Lugola alitoa onyo kali kwa vyama vya siasa nchini ambavyo vimetangaza kufanya mikutano ya hadhara kabla ya muda uliopangwa kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia) akimsikiliza Mtangazi wa Kituo cha Channel Ten na Redio Magic, Nelson Munema, alipokuwa anamuhoji kuhusu usalama wa nchi, ofisini kwa Waziri huyo, jijini Dar es Salaam, leo. Katika mahojiano hayo, Lugola alitoa onyo kali kwa vyama vya siasa nchini ambavyo vimetangaza kufanya mikutano ya hadhara kabla ya muda uliopangwa kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Na Felix Mwagara, MOHA
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ametoa onyo kali kwa vyama vya siasa nchini ambavyo vimetangaza kufanya mikutano ya hadhara kabla ya muda uliopangwa kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini.

Waziri Lugola ameyasema hayo wakati alipokuwa katika mahojiano maalum na chombo kimoja cha Habari jijini Dar es Salaam, leo, akisisitiza kuwa, Jeshi la Polisi lipo imara kipindi hiki tunapoelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa pamoja na Uchaguzi Mkuu mwakani, hivyo vyama vya siasa vilivyotangaza kuanza kufanya mikutano ya hadhara kabla ya muda Jeshi lake litavishughulikia ipasavyo. 

“Hii naomba eleweka na pia iwekwe akilini, mikutano ya hadhara bado haijaruhusiwa kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ni kosa kufanya mikutano ya hadhara kabla ya tarehe ya kufanya mikutano ya hadhara pamoja na kampeni haijatangazwa, jana kuna chama kimetangaza kuanza kufanya mkutano wa hadhara, sasa waendelee na mipango yao, alafu tuone nini kitawatokea,” alisema Lugola.

Waziri Lugola alisema Serikali haiwezi kuchezewa na kamwe wanaotaka kuichezea watashughulikiwa pamoja na kufunguliwa mashtaka kwa mujibu wa sheria za nchi.

“Kama wanataka kutikisa kiberiti cha Rais Magufuli watakikuta kimejaa, wasithubutu kuichezea Serikali ya awamu hii, tupo imara na pia tutahakikisha tunalinda amani ya nchi hii kwa nguvu zote, na amani hii tuliyonayo hatuwezi kuipoteza kamwe,” alisema Lugola na kuongeza kuwa;

“Nimekabidhiwa lindo hili na Rais Magufuli ili niweze kulilinda ipasavyo, hivyo basi, wanasiasa wasibiri muda wa kuanza kampeni, na sio kukurupa kufanya mikutano ya hadhara bila ya kufuata taratibu, hilo halikubaliki hata kidogo.”

Pia Waziri Lugola, alipoulizwa kuhusu vituo vya polisi kutotoa dhamana saa 24 kama alivyoelekeza kwa nchi nzima, alishangazwa kama kuna baadhi ya vituo hivyo kuendelea kuvunja maagizo yake, hivyo amewataka wananchi wampigie simu kwa mwananchi yeyote atakaye onewa na askari au mtu yeyote aliyopo ndani ya Wizara na Taasisi zake anazoziongoza. 

“Mwananchi yeyote atakayenyimwa dhamana, au atakaye onewa, akikisheni mnanipigia simu, na pia kuna njia nyingi za kutupa hapa Wizarani kupitia mitandao yetu ya kijamii, tovuti pamoja na makamanda mbalimbali walipo katika mikoa yote nchini,” alisema Lugola.

Aidha, Waziri Lugola amepiga marufuku tabia ya Watanzania kuchukua sheria mkononi katika matukio yoyote yanayotokea nchini, alisema kumvamia mharifu na kumpiga ni kosa kisheria pamoja na matukio mengineyo. 

JKCI wamwekea mgonjwa mwenye umri wa miaka 101 kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ya moyo

0
0
 Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Yona Gandye na Khuzeima Khanbai wakimwekea mgonjwa mwenye umri wa miaka 101  kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ya moyo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) kifaa hicho huwekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini ya asilimi 30 kwa dakika. Tangu kuanza kwa Taasisi hiyo mwaka 2015 hii ni mara ya kwanza kwa mgonjwa mwenye umri huo kuwekewa kifaa hicho.
 Madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Yona Gandye na Khuzeima Khanbai wakiangalia kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ya moyo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) ambacho kimewekwa kwa mgonjwa mwenye umri wa miaka 101 kifaa hicho huwekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini ya asilimi 30 kwa dakika. Tangu kuanza kwa Taasisi hiyo mwaka 2015 hii ni mara ya kwanza kwa mgonjwa mwenye umri huo kuwekewa kifaa hicho.
Madaktari, wauguzi na mafundi sanifu wa moyo wa mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wa chumba cha Cathlab wakiwa na nyuso za furaha mara baada  ya kumaliza kumwekea mgonjwa  kifaa maalum cha kurekebisha  mapigo ya moyo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker) ambacho kimewekwa kwa mgonjwa mwenye umri wa miaka 101 kifaa hicho huwekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini ya asilimi 30 kwa dakika. 
Na Ales Mbilinyi -JKCI
 KWA mara ya kwanza madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa
 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wamwekea mgonjwa mwenye umri wa miaka 101 kifaa maalum cha kurekebisha mapigo ya moyo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker).

Kifaa hicho kisaidizi cha moyo huwekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini ya asilimi 30 kwa dakika.

Akizungumza baada ya kumfanyia upasuaji mdogo na kumwekea mgonjwa kifaa hicho Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa JKCI Yona Gandye alisema mara nyingi wanawawekea kifaa hicho wagonjwa wenye umri wa miaka 80 kushuka chini lakini leo hii wamevunja rekodi na na kuweka kwa mgonjwa wa umri wa miaka 101.

“Kabla ya kufanya upasuaji tulimfanyia mgonjwa uchunguzi wa kina na kugundua mfumo wake wa umeme wa moyo unahitilafu na mapigo ya moyo yapo chini ya asilimia 20 hivyo tumemuwekea kifaa ambacho kitausaidia moyo kuongeza mapigo yake na mara baada ya kumwekea kifaa hiki mapigo yake ya moyo yako vizuri kati ya asilimia 60 na 100 kwa dakika”, alisema Dkt. Gandye.

Akizungumza kwa furaha mara baada ya baba yake kuwekewa kifaa hicho Saimoni Maina alisema matatizo ya baba yake yameanza mwaka mmoja uliopita na kutibiwa katika hospitali mbalilmbali Mkoani Manyara na Arusha ambapo waligundua kuwa mapigo yake ya moyo yapo chini hivyo kumpa rufaa kwa ajili ya kutibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete.

“Baba alikuwa akianguka na kupoteza fahamu mara kwa mara ndipo tukaamua kumpeleka hospitalini kwa ajili ya matibabu ili kufahamu anasumbuliwa na tatizo gani, tunashukuru sana uwepo wa Taasisi hii kwani baba yetu ameweza kufanyiwa upasuaji na hali yake inaendelea vizuri kama mnavyomuona”, alisema Maina.

Kwa upande wake Mzee Benedict Maina alisema kabla ya kufanyiwa kwa upasuaji huo alikuwa akipata maumivu makali sehemu za moyo, kuanguka, kupoteza fahamu na kushindwa kutembea lakini baada ya kufanyiwa upasuaji huo hali yake imebadilika na maumivu kupungua ukilinganisha na ilivyokuwa awali na anaamini siku chache zijazo atarudi katika hali yake ya kawaida.

SERIKALI YAFUTA MILIKI YA MASHAMBA YA MOA MKINGA

0
0
Na Munir Shemweta, WANMM MKINGA
Serikali imefuta miliki ya Mashamba matatu ya Mkomazi Plantantions maarufu MOA yaliyopo wilaya ya Mkinga mkoani Tanga kutokana na kukiuka masharti ya uendelezaji ikiwemo kutelekezwa bila kufanyiwa maendelezo yaliyokusudiwa  na kutolipiwa kodi ya pango la ardhi.

Uamuzi huo umetangazwa leo tarehe 30 Agosti 2019 na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alipozungumza na wananchi wa Mayomboni wilayani Mkinga mkoani Tanga alipokwenda kutatua mgogoro wa muda mrefu katika eneo hilo.

Mashamba yaliyofutiwa ni lenye hati Na 9780  na ukubwa wa ekari 14,688, shamba  Na 4268  ekari 804 na Shamba lenye Hati Na 9781  ekari 246 ambapo mashamba yote matatu yana ukubwa wa ekari 15,738.

Kufuatia uamuzi huo, jumla ya vijiji kumi vyenye kaya 3,236 zilizo na wakazi 16,450 zitanufaika na uamuzi wa serikali kutokana na wananchi wake kuvamia mashamba hayo na kufanya maendelezo ya kujenga makazi, shule pamoja na kuendesha shughuli za kilimo cha mazao ya kudumu na ya muda mfupi.

Vijiji vilivyonufaika ni uamuzi wa Serikali kufuta mashamba ya Mkomazi Plantations ni kijiji cha Kilulu-Dunga, Zingibari, Mwaboza, Mwakikoya, Mhandakini, Nkanyeni, Sigaya, Mayomboni, Ndumbani pamona na kijiji cha Moa

Akizugumza wakati wa kutangaza uamuzi huo, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema uamuzi wa kufuta mashamba hayo matatu unafuatia maombi yaliyotumwa kwa Raisi John Pombe Magufuli ya kutaka kufutwa mashamba hayo kutokana na kutoendelezwa na wamiliki wake kwa muda mrefu.

Alisema, Rais ameridhia maombi hayo kwa kuwa serikali imekuwa ikisisitiza utekelezwaji wa sheria ya Ardhi Na 4 ya mwaka 1999 ikiwemo uendelezaji wa mashamba ambayo yamemilikishwa sehemu mbalimbali nchini.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliagiza kufanyika upimaji katika vijiji vyote kumi vilivyopo ndani ya shamba hilo sambamba na kuanishwa miapaka ya vijiji hivyo na kupatiwa hati ambapo alitaka wananchi wanaishi kwenye vijiji hivyo kutobughudhiwa.

Aidha, Waziri Lukuvi alitaka maeneo yaliyopangwa kwa ajili ya uwekezaji katika shamba yaliyofutwa kuachwa kwa ajili ya shughuli hiyo ikiwemo muwekezaji wa Katani Azka International Tanzania mwenye ekari mia tano pamoja na maeneo ya viwanda kama kile cha kuzalisha chumvi na kusisitiza kuwa serikali inataka uwekezaji utakaotoa ajira kwa vijana na wakati huo kupata mapato kupitia kodi ya pango la ardhi.

Katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi ameagiza kufanyika uhakiki wa mashamba mengine ya Kwa Mtili Estates Co Ltd yaliyopo Mkinga mkoani Tanga ambapo ekari 58 pekee ndizo zilizoombwa kufutwa kwa Rais kutokana na kutoendelezwa huku mmili wake ikidaiwa kumiliki ekari  2,841.

Hatua hiyo inafuatia Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili katika halmashauri ya wilaya ya Mkainga Obed Katonge kueleza kuwa, Kwa Mtili Estates Co Ltd inalo shamba la lenye ukubwa wa ekari 2,841 tofauti na inavyoonekana katika kumbukumbu za ofisi ya Msajili wa Hati Kanda ya Kaskazini ambazo ni 58.

Lukuvi aliagiza wataalamu wa ardhi kutoka Kanda ya Kaskazini kufanya uhakiki huo katika kipindi cha mwezi mmoja na kumpa taarifa ya uhakiki huo mwisho wa mwezi Septemba 2019 na kufafanua kuwa pale itakapothibitika kuna ujannja uliofanyika wa kumuongeza mmiliki wa shamba hilo hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wahusika.

Mbunge wa Jimbo la Mkinga mkoani Tanga Dustan Kitandula aliishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kusikiliza kilio cha muda mrefu cha wananchi wanaoishi eneo la shamba lililofutwa la kutaka kurejeshewa ardhi yao waliyokuwa wakiutumia kwa shughuli mbalimbali.

Alisema, mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wa mkinga na wamiliki wa mashamba ya Mkomazi Plantantions Co Ltd umekaa kwa muda mrefu na kuwafanya wananchi kuwa na ndoto isiyokuwa na majibu lakini uamuzi uliotolewa na Serikali umewafanya kuishi kwa furaha na amani .
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mayomboni kilichopo wilaya ya Mkinga mkoani Tanga alipokwenda kutangaza uamuzi wa Serikali kufuta Mashamba matatu ya Mkomazi Plantantions Co Ltd maarufu kama MOA leo tarehe 30 Agosti 2019.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mayomboni kilichopo wilaya ya Mkinga mkoani Tanga alipokwenda kutangaza uamuzi wa Serikali kufuta Mashamba matatu ya Mkomazi Plantantions Co Ltd maarufu kama MOA leo tarehe 30 Agosti 2019. Wa kwanza kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Mkinga mkoani Tanga Dustan Kitandula.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Mkinga mkoani Tanga Dustan Kitandula alipokwenda kutangaza uamuzi wa Serikali kufuta Mashamba matatu ya Mkomazi Plantantions Co Ltd maarufu kama MOA leo tarehe 30 Agosti 2019.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akimsikiliza Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Dustan Kitandula (kushoto) alipokwenda kutangaza uamuzi wa Serikali kufuta Mashamba matatu ya Mkomazi Plantantions Co Ltd maarufu MOA leo tarehe 30 Agosti 2019. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

Ahukumiwa Jela Miaka Ishirini

0
0
Na Editha Edward-Tabora 

Mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Tabora imemuhukumu kujana mmoja kutumikia kifungo cha miaka Ishirini na miezi sita Jela anayefahamika kwa jina la Fabian Francis Mkazi wa Kaliua baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na nyara za Serikali ndani ya hifadhi ya msitu wa Ugalla wilayani Kaliua 

Akisoma hukumu katika shauri hilo la uhujumu uchumi namba sita la mwaka 2019 hakimu mkazi Mfawidhi mkoa wa Tabora Chiganga Mashauri Tengwa amedai kuwa maamuzi hayo ya mahakama yamefikiwa baada ya kupitia maelezo ya pande zote mbili na kujiridhisha pasipo kuwa na shaka yoyote kuwa mshitakiwa Fabiani Francis amehusika kutenda makosa mawili baada ya kukutwa ndani ya hifadhi ya msitu wa Ugalla akiwa na nyara za Serikali nyama ya Wanyamapori 

Katika Kosa la kwanza hakimu Chiganga Tengwa amemuhukumu kulipa faini ya Shilingi laki moja au Jela miezi sita huku Kosa la pili katika kesi hiyo Fabian amehukumiwa kifungo cha miaka Ishirini Jela

Awali katika mwenendo wa shauri hilo Wakili upande wa Jamhuri Tito Mwakalinga ameieleza mahakama kuwa mshitakiwa Fabiani Francis alikamatwa ndani ya hifadhi ya Ugalla Wilayani Kaliua eneo la upango mnamo tarehe 2 January 2019 akiwa na nyama ya wanyama wa porini yenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni nne na silaha ndogo kinyume cha sheria ya hifadhi ya wanyama pori.
Pichani ni kijana Fabian Francis aliyehukumiwa miaka Ishirini  na miezi sita Jela kwa Kosa la kukutwa na nyara za serikali.

TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA

0
0



Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuujulisha Umma wa Watanzania kuwa, Programu ya Mazingira ya Umoja wa Mataifa (United Nations Environment Programme-UNEP) imetangaza nafasi 5 za ajira zifuatazo:-
  1. Senior Administrative Officer;
  2. Senior Programme Management Officer;
  3. Chief of Section;
  4. Human Resource and Management;
  5. Deputy Chief Officer.

Wizara inawahimiza Watanzania wenye vigezo na sifa stahiki kuomba nafasi hizi. Kupata taarifa zaidi na taratibu za kuomba nafasi hizo tafadhali bofyaHAPA


Imetolewa na:


Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,


Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika 
Mashariki

Dodoma, Tanzania.


30 Agosti 2019


KUMBUKIZI YA NGULI TX MOSHI WILLIAM

0
0

Na Moshy Kiyungi,Tabora.

Japokuwa imepita miaka 13, tangu TX Moshi William alipofariki dunia, hadi leo kumbukumbu hazijatoweka vichwani mwa wapenzi na washabiki wa mwanamuziki huyo.

Tungo zake zilizokuwa zimejaa maudhui mema kwa jamii, zilimuongezea sifa kemkem katika kipindi chote maisha yake katika muziki.

TX Moshi William alizaliwa Korogwe mkoani Tanga mwaka 1958, akapewa jina la Shaban Ally Mhoja Kishiwa, baadaye alikuja kubadilisaha akawa Moshi William.

Alivunjika mguu katika ajali ya gari baada ya kupata ajali ya gari lililoparamia mti wa Mvinje pale Mivinjeni, barabara ya Kilwa jijjini Desemba 16, 2005 iliyompelekea kuvunjika mguu.

Februari 13, 2006 akalazwa katika hospitali ya Burere iliyoko Kibaha mkoani Pwani.Siku zilivyokuwa zikisonga mbele, mguu huo kuanza kumsumbua kwa kutunga usaha, akahamishiwa katika Hospitali ya Regency Machi 15, 2006 baada ya kugundulika kuwa pia alikuwa na matatizo ya figo.

Matatizo yalipoendelea Machi 18, 2006 alihamishiwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwenye kitengo cha kushughulikia mifupa MOI.

Kwa mapenzi ya Mungu TX Moshi William aliaga dunia Machi 29, 2006 katika hospitali hiyo ya Muhimbili alikokuwa amelazwa.Baada ya kifo hicho mwili wake ulishushwa kwenye nyumba yake ya milele katika makaburi yaliyoko maeneo ya Keko Machungwa, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mjane wa mwanamuziki huyo, Bi Asha Seif, alisema chanzo cha kifo cha mumewe kilitokana na kadhia ya mguu pamoja na figo.

Kwa mujibu wa mmoja wa viongozi wa bendi hiyo Dk. Saidi Mabera, Moshi William maarufu kwa jina la TX alijiunga na bendi ya Juwata mwaka 1982, akitokea katika bendi ya Polisi Jazz.

Mwanamuziki huyo alijipatia umarufu mkubwa kwa kutunga nyimbo zilizokuwa na mafunzo katika jamii. Baadhi yake ni kama Ashibae, Mwaka wa Watoto, Msafiri Kakiri, Asha Mwanaseifu, Kaza Moyo, Ajuza, Ndoa Ndoano, Mwanamkiwa, Ajali, Nyongo mkaa na Ini, Isihaka Kibene, Harusi ya Kibene, Piga Ua Talaka Utatoa na nyimbo nyingine nyingi.

Moshi William hadi mauti yalipomfika, tayari alikuwa amefanikwa kurekodi albamu takriban 13

Baadhi ya wapenzi wa muziki wa dansi katika miji mbalimbali ya Afrika Mashariki na Kati, walikuwa wakimfananisha sana na marehemu Madilu System, aliyekuwa mwanamuziki toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kutokana na mitindo ya unyoaji wa nywele, uvaaji hadi namna ya ya uimbaji.

Kifo cha mwanamuziki Moshi William kiliacha pengo kubwa katika ulimwengu wa muziki wa dansi, ikizingatiwa sauti yake iliyokuwa ya kuvutia, akitunga nyimbo zenye hisia kali zilitokana na maswahibu ya maisha yake.

Wanamuziki wenzake wa bendi ya Msondo Ngoma wlisema kuwa pengo aliloliacha Mwanamuziki mwenzao TX Moshi William halitazibika kamwe.

Aidha kiongozi wa bendi hiyo Dokta Said Mabera alitamka kuwa Tx Moshi William miongoni mwa nyimbo alizotunga mara baada ya kujiunga na bendi hiyo ni pamoja na Ajuza, Asha Mwanaseif, (aliomtungia mkewe), na wimbo mwingine Ashibaye.

Mabera aliyefanya kazi kwa karibu na TX Moshi William alisema kuwa kama kuna kitu ambacho kilimpa sana heshima kubwa mwanamuziki huyo TX, ni uwezo wake wa kutunga na kuimba, tofauti na wanamuziki walio wengi ambao unaweza kukuta mwanamuziki anajua kuimba lakini hana uwezo wa kutunga nyimbo au ana uwezo wakutunga lakini hana sauti nzuri.

Alisema kuwa mwimbaji huyo alitunga nyimbo nyingi baada ya kuhamia kwenye bendi hiyo lakini alisisitiza kwamba nyimbo zilizotia fora sana ni pamoja na Kilio cha Mtu Mzima, Ndoa Ndoana, Piga Ua Talaka Utatoa, Isihaka Kibene, Kaza Moyo, Harusi ya Kibene, na Ajali.

Wimbo huu Ajali aliutunga akiwa kitandani amelazwa hospitalini kwa matibabu mara baada ya kupata ajali iliyompelekea kuvunjika mguu.

Mara baada ya mwanamuziki huyu kuonekana anapata nafuu, baadhi wapenzi wa bendi hiyo ya Msondo mkoani Tanga, waliomba akakafanyiwe tambiko maalumu ili kipenzi chao TX Moshi William ili apone na kuzidi kuwa na maisha marefu.

TX Moshi William wakati wa uhai wake aliwahi kusema kuwa amepitia katika bendi mbalimbali za muziki ambazo ni pamoja na Safari Trippers, Juwata Jazz, UDA Jazz, na Polisi Jazz, ambayo alipigia kabla kujiunga kundi hilo la Juwata Jazz.

Kufuatia weledi wake katika muziki, nguli huyo alitunukiwa Tuzo mbalimbali za muziki hasa zile zijulikanazo kama Kilimanjaro Music Award.

Baadhi ya vyombo vya habari nchini Tanzania vinakariri kuwa Moshi alibatizwa jina la TX, na aliyekuwa mtangazaji wa siku nyingi wa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) Julius Nyaisanga.

Nyaisanga alimbatiza jina hilo kutokana na tunzi zake za uhakika. Kwa sasa Nyaisanga ni marehemu.Mwimbajji huyo jina lake hasa ni Shaaban Mhoja Kishiwa, mwenye asili ya Wanyamwezi, ingawa alikuwa akijulikana zaidi kwa jina la TX Moshi William.

Mengi hayafahamiki kwenye maisha yake inagawa wakati fulani TX Moshi William alikaririwa akisema kuwa hali ya kutotulia sehemu moja hasa wakati akiwa mtoto, ilitokana na ugomvi baina ya mama na baba yake.

Ilielezwa kuwa alilelewa na baba yake wa kambo kwa kipindi kirefu cha utoto hadi alipokuwa mtu mzima.

Miongoni mwa wanamuziki ambao tayari wameisha aga dunia na kuacha masikitiko makubwa katika ulimwengu wa muziki wa bendi hiyo ni pamoja na Suleiman Mbwembwe, Mnenge Ramadhani, Muhidin Gurumo, Joseph Maina, Athuman Momba na wengine wengi.

Mbwembwe alikuwa ana sauti ya aina yake na mara nyingi aliimba kwa kupokezana pamoja na Moshi William.Sasa wengi wanahoji nini mstakabali wa bendi hii ya Msondo Music band baada ya kuondokewa na majabari hawa?

Kama alivyotamka Waziri Dewa ambaye ni mratibu wa shughuli za bendi hiyo ya Msondo, itakuwa kazi ngumu na isiyofikiriwa kumpata mwimbaji mwingine mwenye sauti yenye mvuto kama ya TX Moshi William.

Nguli huyo aliacha mjane na watoto watano, wawili wa kike na watatu wa kiume. Wanne wakiwa wa mama mmoja ambao ni Hassan, Maika, Ramadhani na Maada. Jina la mtoto mwingine bado halijafahamika.

Mwanawe Hassan Moshi William amekuwa akijaribu kuvaa viatu vya baba yake, kwa kuimba nyimbo alizokuwa akiimba baba yake, lakini kwa mujibu wa wapenzi wa Msondo Ngoma, wanasema kuwa bado hajamfikia kabisa.

TX Moshi alikuwa ‘chakaramu’ na mbunifu wa kutunga vionjo ikiwemo mtindo ujulikanao wa ‘mambo hadharani’.

Aidha alibuni aina ya ‘Chombezo’ katika nyimbo zao ambapo alipenda kuweka vionjo vyenye kunogesha wimbo. Mfano utasikia "we nani", "kidogo tu..kidogo tu", "kwanini lakini", "watoto wanachezea umeme", "discipline", "fair play" na vingine vingi.

Wakazi wa Keko Machungwa hawawezi kumsahau nguli huyo takriban kila wimbo alikuwa hakosi kuitaja Keko Machungwa, ambako ndiko kulikuwa makazi yake.


Mwisho.

Mungu aipumzishe roho yake pahala pema peponi, Amina.



Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba: 0784331200, 0736331200, 0767331200 na 0713331200.

Watumishi Mloganzila wapatiwa chanjo ya Homa ya Ini

0
0
uuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Rither Msuya (kulia) akichukua sampuli kwa ajili kupima damu ili kugundua Virusi vya Homa ya Ini. Hospitali ya Mloganzila leo imewapima na kutoa chanjo ya Homa ya Ini kwa wafanyakazi wake
Muuguzi Magreth Zacharia (katikati) akimpatia chanjo ya Homa ya Ini mtumishi wa Muhimbili-Mloganzila, kushoto ni muuguzi Sarah Igira.
Wataalam wa Maabara Muhimbili-Mloganzila wakiendelea na zoezi la upimaji na utoaji wa majibu ya Virusi vya Homa ya Ini (Hepatitis).
Baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Mloganzila wakisubiri kupata huduma ya chanjo ya Homa ya Ini hii leo. 


Na Neema Wilson Mwangomo


Hospitali ya Taifa Muhimimbili-Mloganzila leo imetoa chanjo ya Homa ya Ini (Hepatitis) kwa wafanyakazi wake kwa lengo la kuwakinga watoa huduma mahala pa kazi ili wawe salama kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa.


Akizungumzia zoezi hilo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Prof. Lawrence Museru, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba MNH-Mloganzila Dkt. Mohamed Mohamed amesema dhamira ya hospitali ni kuhakikisha watumishi wake wote wanapatiwa chanjo hiyo muhimu.

“Zoezi linalofanyika hapa ni kupima kwanza Virusi vya Homa ya Ini kisha kutoa chanjo, lengo ni kuwapatia chanjo watumishi wote wa hospitali hii”amesema Dkt. Mohamed.

Ugonjwa wa homa ya Ini (Hepatitis) unasababishwa na virusi viitwavyo “Hepatitis B na C” na maambukizi ya ugonjwa huu yanashabiana na njia ya maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi kama vile kufanya ngono zisizo salama, kuchangia sindano au vikatio, kupewa damu isiyo pimwa, kupitia uzazi wa mama na mtoto hasa wakati wa kujifungua.

Ugonjwa huu sugu wa homa ya ini hauna tiba ya kuponya, isipokuwa dawa zilizo patikana hadi sasa zinaweza kupunguza kasi ya maambukizi mwilini na kuzuia madhara zaidi kwenye ini.

Ugonjwa huu unaweza kumpata mtu na kusababisha maradhi mwilini pasipo kuwa na dalili za aina yoyote ingawa kuna baadhi ya waathirika hupata dalili kama vile njano ya macho, kichefuchefu, tumbo kuuma kutapika na kuharisha kwa muda mfupi, mwili kuwashwa au kupata mkojo wa njano nyingi.

GRAND KALE ALIVYOENEZA MUZIKI WA RHUMBA DRC.

0
0
Na Moshy Kiyungi,Tabora.

Muziki wa rhumba umejizolea sifa na kupendwa na wapenzi wengi wa muziki humu nchini na Afrika kwa ujumla.

Sifa hizo zimetokana na baadhi ya wanamuziki waliokuwa hodari katika utunzi na upigaji wamuziki huo.

Makala hii inakujuza baadhi ya wanamuziki waliokuwa wakongwe, wanaokamilisha uhalisia wa simulizi hii.

Jina la Joseph Kabasele Tshama ‘Grand Kale’ ni miongoni mwa baadhi ya nguli aliyekuwa na Weledi mkubwa katika tasnia ya muziki hapa Afrika.

Hata hivyo baadhi wa watu kwa kutokuelewa kwao, wamekuwa wakichanganya majina ya Joseph Kabasele ‘Grand Kale’ na Kabasele Yampaya ‘Pepe Kalle’, wakidhani ni mtu mmoja ama ni ndugu.

Hao wote walikuwa ni wanamuziki mahiri wenye kupishana kwa mbali sana kwa umri.Joseph Kabasele ‘Grand Kale’ alizaliwa Desemba 16, 1930, mjini Matadi huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wakati Kabasele Yampanya ‘Pepe Kalle’ alizaliwa Novemba 28, 1951 jijini Kinshasa.

Wataalamu wa muziki wanaeleza kuwa historia ya muziki wa dansi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), haimuweki pembeni nguli Joseph Kabasele ‘Grand Kalle’.Mkongwe huyo alisaidia kwa kiasi kikubwa katika mwelekeo wa muziki wa kisasa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Grand Kale atakumbukwa kwa kuwa yeye alikuwa mwasisi na kiongozi wa bendi ya African Jazz,iliyokuwa kubwa nchini DRC wakati huo.

Bendi hiyo iliwajumuisha magwiji wengine akiwemo aliyekuwa mpiga gitaa mahiri, Dokta Nico Kasanda, aliyekuwa mtunzi na mwimbaji wa Kimataifa Tabu Ley Rochereau na mpiga saxophone maarufu Manu Dibango.

Kabasele alikuwa kinara wa muziki wa Kiafrika na miongoni mwa watunzi na mwimbaji mkubwa katika bara hili la Afrika ya watu weusi wanaozungumza Kifaransa.

Nguli huyo alizaliwa huko Matadi nchini DRC, katika familiya maarufu iliyomjumuisha Joseph Malula ambaye alitokea kuwa Askofu wa Kanisa Katoliki.Grand Kalle alikuwa miongoni mwa watu wa zama hizo waliopata elimu.

Alimaliza elimu ya sekondari na kuajiriwa kazi ya kuwa mpiga mashine (typist) kwenye Kampuni za biashara katika Jiji la Kinshasa.Muziki ulikuwa kama wito wake na akagundua mwanya wa kuufuatilia na kwenye mwaka 1950, akawepo katika studio mpya iliyojulikana kwa jina la OPIKA.

Akiwa katika studio ya OPIKA, Grand Kalle aliungana na wanamuziki wa muda, ambao walikuwa Jimmy ‘Zacharie Elenga’ ambaye alikuwa ndiye nyota wa wakati huo.Pia walikuwepo wapiga magitaa mashuhuri Georges Doula na Albert Yamba Yamba na baadhi ya wapigaji muziki waliokuwa wakichipukia.

Kama alivyokuwa yeye, Chipukizi hao waliona muziki ndio ufunguo wa mafanikio, baadaye wakiwa nje ya mihangaiko ya kazi na pia baada ya maonevu ya Ukoloni.Mojawapo ya bendi za mwanzoni ambayo iliibuka kutoka mseto huo wa Kabasele ni wanamuiziki Georges Doula na Yamba Yamba, waliunda bendi ikijulikana kwa jina OTC.

Baada ya kufanya ‘Promosheni’ ya filamu kwa ajili ya radio stesheni ya mjini hapo, ilikuwa ikitumia herufi hizo OTC.Kabasele ‘Grand Kalle’ umaarufu wake ukawa hauna mfano, aliweza kubuni mtindo wake baada ya kuhamasika na kumuona muimbaji machachari ‘Tino Rosi’.

Sauti ya Rosi wakati akighani, ilikuwa ni yenye mvuto kwenye nyimbo zake, ikawa kivutio kikubwa kwa wakazi wa mji wa Kinshasa.Nyimbo zake za mwanzoni zilizo ‘hit’ zilitokana na mjumuiko wa wanamuziki vijana wa OPIKA, hususan mpiga gitaa Nicolas Kasanda baadaye akajulikana kama Dokta Nico, akipiga gitaa la kati la rhythm.

Wimbo Parafifi uliofyatuliwa mwaka 1952, ambao maudhui yake uliimba kumsifia mtangazaji wa radio aliyekuwa nchini Jamhuri ya Kongo Brazzaville.Parafifi ulikuwa ni utunzi wa Joseph Kabasele ulioweza kutia fora pamoja na ule ‘Kale Kato’ uliokuwa ukihadithia juu ya penzi la Kabasele kwa kimwana mmoja aliyejulikana kwa jina la ‘Katherine’.

Katika kipindi cha kati ya mwaka 1953 hadi 1955, bendi mpya iliyomjumuisha Kabasele, Nico na Dechaud, iliibuka kutoka kwa wanamuziki wa muda wa studio ya OPIKA wakajiita African Jazz.

Wakiazima jina hilo ambalo halikushabihiyana na mtindo wa muziki wa Kimarekani wa ‘Jazz’ kama jina lilivyo.African Jazz ilicheza muziki wa nyimbo za Latini, ambapo bendi hiyo ilichangia kiasi kikubwa kukua kwa rumba la Kikongo.

Waimbaji wengine kadhaa walianza kuiga mtindo wake kiasi kwamba watu wakaanza kuzungumzia kuanzishwe kwa shule ‘mchapuo’ wa Kabasele au wa African Jazz.Aidha baadhi ya nyota wengine aliokuwa nao katika African Jazz zaidi ya Dokta Nico Kasanda, Tabu Ley, Dechaud na Manu Dibango. Wengine ni pamoja na waimbaji Joseph Mulamba Mujos, Bombenga na mpiga gitaa Tino Baroza.

African Jazz iliweza kuweka fursa nzuri kuwa ni uwanja wa mafunzo kwa wanamuziki vijana wa kizazi kilichofuatia huko DRC.

Hadi kufikia mwaka 1960, African Jazz ilikuwa bendi ya juu nchini mwao na kuweza kufyatua maelfu ya santuri zilizotolewa katika nembo ya ‘DECCA’ na kuweza kuwapata mashabiki wengi katika kumbi mbali mbali.

Joseph Kabasele alikuwa karibu sana na kundi la Rocka Mambo, hadi kuleta muungano mzuri na kundi lake la African Jazz. Alishirikiana nao na kuweza kutoa vibao vyenye viwango vizuri hasa alipokuwa ameshirikiana na Jean Serge Essous, Nino Malapet, Rossignol na kina Pandi.

January, 1960 Kabasele na kundi lake la African Jazz pamoja na wajumbe wawakilishi wa iliyokuwa ‘Belgian Congo’, walifanya kitu cha kihistoria ambacho ni kongomano la utambulisho la kisisasa huko Brussels.

Miongoni mwa tungo zake alizozifanya katika kongomano hilo la kisiasa la mwaka 1960, ni utunzi wa wimbo uliojulikana kama ‘Independence Cha Cha’ na ule wa ‘Le Table Ronde’.

Independence Cha Cha, ulitambulika kama wimbo wa Kitaifa kufikia uhuru.
Utunzi mwingine wa Kabasele ‘Bilombe Ba Gagne’ ukiwa na maana ya wenye kujiamini wameshinda, ulielezea maisha ya madhira chini ya utawala wa Wabelgiji.Kipindi ambapo uhuru ulibadilika na kuelekea kwenye vurugu.

Aidha Kabasele alitoa kibao kingine cha ‘Toyokana Tolimbisana na Kongo’ ukiwa na maana ya tuelewane na tusamehe yaliyopita, ukihimiza kuungana wakongomani.Mwaka 1961 kundi la African Jazz likiongozwa na Joseph Kabasele, lilifanya ziara ndefu katika nchi za Afrika Magharibi na kusambaza mitindo yao iliyochanganya mahadhi ya Kiafrika.

Kwa wasikilizaji wa nchi za Ghana, Nigeria, Ivory Coast, Sierra Leone na Guinea,ulileta athari kubwa kwa wanamuziki wa huko.

Mfano wa karibu ni kwa bendi ya Bembeya Jazz ya nchini Guinea, iliweza kufaidika kwa ziara hiyo ya Joseph Kabasele ya mwaka 1961. Katika kipindi hicho kuliweza kuzaliwa muziki mchanganyiko wa Afrika Magharibi na Latin Amerika kwa kupatikana mitindo ya High-Life, Juju na Afro-Beat.

Mwaka 1960 Grand Kale alirekodi kibao kilichojulikana ‘Okuka Lokole’ ambacho ni kwa heshima ya mwanamuziki ‘Louis Armstrong’ ambaye alitembelea nchi ya Kongo kwa ziara iliyodhaminiwa na Serikali ya Marekani.

Nguli huyo baadaye alibadilika akawa kiongozi mkali, tabia ambayo ilipelekea wanamuziki wote kuihama bendi ya African Jazz mwaka 1963.
Kabasele aliunganisha nguvu akishirikiana na mwimbaji Jean Bombenga, mwanafunzi wake aliekuwa na bendi ya Vox Africa, ambayo baadaye ilitambulika kama African Jazz.

Hata hivyo halikufanikiwa kufikia kiwango cha iliyokuwa African Jazz original.Baada ya kundi hilo kupiga muziki na kurekodi kwa uchache nyimbo pia kufanya maonesho kadhaa, lilisambaratika mwaka 1969.

Kabasele baadaye akaenda kurekodi huko Ulaya akiwa na kundi la wanamuziki walikuwepo studio na kulipa jina ‘African Team’.Kundi hilo lilikuwa na wanamuziki, Mkameruni, Manu Dibango na Jean Serge Essous wa Kongo Brazzaville waliokuwa wapulizaji wa saxophone.

Alikuwepo mpiga fluti toka nchini Cuba aliyekuwa akiitwa Don Gonzalo. Kwa pamoja walicheza muziki kwa miondoko ya Afro-Latin Jazz.Kwenye miaka ya mwanzo ya 1970, Kabasele akawa Rais wa chama cha haki miliki cha Kongo Kinshasa SONEKA.

Aidha alionekana jukwaani mara chache sana kutokana na maradhi ya ‘hypertension’ sugu ambayo yalimuandama sana.Aliwahi kwenda Paris mara mbili kwa matibabu lakini alipata nafuu ya muda.

Mwaka 1980 Kabasele alitunikiwa Nishani ya ‘Mwalimu Mkuu’ wa muziki wa Zaire na Umoja wa Wanamuziki UMUZA.Grand Kalle alikuwa na sauti pamoja na staili kigezo, ambayo waimbaji wote wa Kongo wangeweza kupimwa kwa hiyo.

Bendi yake ya African Jazz ilikuwa ni mfano kwa kila kundi la bendi za Wakongo waliofuatia.Mchango wake katika mwendelezo wa rumba la Kongo, uliwafanya Wakongo wote wamwite ‘Baba wa muziki wa Kongo’

Joseph Kabasele ‘Grand Kale’ anakuwa miongoni mwa wanamuziki wakubwa wa karne ya ishirini, alifariki February 11, 1983 akiwa katika mji wa Kinshasa, huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mungu aipumzishe roho yake pahala pema peponi, Amina.


Mwandishi wa makala haya anapatikana kwa namba: 0713331200, 0736331200, 0784331200 na 0767331200.

Dkt. Hussein Mwinyi aridhishwa na miradi ya SUMA JKT Kanda ya Ziwa

0
0
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Bw. Simon Berege (kushoto) akimwonesha Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi eneo la ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri hiyo mapema leo tarehe 30 Agosti, 2019 katika kata ya Ntobo.
Kaimu Mkurugenzi wa SUMA JKT Kaptain Fabian Buberwa (kulia) akimuelezea Waziri wa Ujenzi na Jeshi la kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi namna wanavyotekeleza mradi wa kujenga makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack wakiangalia ujenzi wa Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala leo tarehe 30 Agosti, 2019.
Sehemu ya ujenzi wa majengo ya Makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala inavyoonekana.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telacl na viongozi wengine wakiendelea kukagua ujenzi wa makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akizungumza na viongozi na watendaji katika eneo la ujenzi wa makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala.

****************

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi amesema anaridhishwa na kazi nzuri inayofanywa na miradi inayotekelezwa na SUMA JKT kanda ya Ziwa.

Dkt. Mwinyi akiwa kwenye ziara yake ya kukagua miradi inayotekelezwa na SUMA JKT pamoja na makampuni mengine yaliyo chini ya Wizara hiyo kanda ya Ziwa mapema leo tarehe 30/08/2019 katika Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga amesema kwa kiwango kikubwa ameridhishwa na kazi zinazofanywa na sehemu kubwa kazi zimekwenda kwa kiwango kinachotarajiwa na kuwa changamoto zilizopo zitafanyiwa kazi.

“Niwahakikishie Mikoa na Halmashauri zinazohusika na miradi inayotekelezwa na SUMA JKT changamoto zote zitafanyiwa kazi” amesema Dkt. Mwinyi.

Aidha, amemshukuru Mhe. Rais John Magufuli kwa kuiamini kampuni hiyo iliyo chini ya Wizara yake na ndiyo sababu ya yeye kufanya ziara hiyo ili kuhakikisha imani hiyo inadumu pamoja na kuwaomba viongozi wote wa Mikoa na Halmashauri kuendelea kuiamini.

Aidha, amewataka SUMA JKT kuongeza kazi ya ziada mara watakapopata fedha ili kukamilisha jengo la Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ambalo ujenzi wake umesimama kutokana na changamoto ya fedha.

Naye Mkurugenzi wa SUMA JKT Kanali Rajab Mabele amesema kuwa, kampuni hiyo imepiga hatua kubwa hasa katika nyanja ya ujenzi lakini pia inajihusisha na kazi nyingine mbalimbali ikiwemo kilimo na ufugaji.

Awali, akimkaribisha Dkt. Mwinyi Mkoani hapa, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amemuomba kupitia kampuni ya SUMA JKT kuangalia jinsi ya kuwa na miradi ya kuvuna maji ili wananchi waweze kujishughulisha na kilimo cha umwagiliaji.

“Pamoja na kiangazi kilichopo, tunapata mvua nyingi sana na tunavuna mpunga unaoweza kulisha nchi yote, sasa tuone namna bora ya kuvuna hayo maji na tayari baadhi ya wananchi wameshaanza kuchimba mashimo makubwa ya kuvuna maji, tumeona kama Mkoa tufanye hilo ili wananchi wetu waweze kupata mpunga” amesema Telack.

JAJI KIONGOZI AZUNGUMZA NA WATALAAMU KUTOKA BENKI YA DUNIA KUHUSU MABORESHO YA MAHAKAMA

0
0
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe Eliezer Feleshi(wa pili kulia) akizungumza kuhusu mafanikio ya Mradi wa Maboresho ya Mahakama ya Tanzania wa Miaka Mitano (2015/2016 mpaka 2019/2020) kwa ujumbe kutoka Benki ya Dunia( wa kwanza kushoto) ni Mkuu wa Kitengo cha Maboresho ya Mahakama ya Tanzania, Mhe. Zahra Maruma. (watatu kushoto) Mtaalamu kutoka Benki ya Dunia, Benis Biseko (wanne kushoto) ni Msaidizi wa Mtendaji wa Mkuu wa Tanzania,Ginaweda Nashon.Kulia wa kwanza (kushoto) ni Mtaalamu kutoka Benki ya Dunia, Deborah Isser, wa pili kushoto ni Mtaalamu kutoka Benki ya Dunia, Waleed Malik na watatu (kushoto) ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Leonard Magacha.
Mkuu wa Kitengo cha Maboresho ya Mahakama ya Tanzania (JDU)Mhe. Zahara Maruma (wa kwanza kushoto) akijadiliana jambo na Wataalamu wa Benki ya Dunia, (wa pili) ni Deborah Isser, (wa pili kushoto) ni Waleed Malik na wa kwanza ni Denis Biseko.
Mtaalamu kutoka Benki ya Dunia,Deborah Isser(wa kwanza kulia ) akifafanua jambo kuhusu ueneshaji wa kesi kwa njia ya mtandao ‘Video Conference’,(wa pili kulia) ni Mtaalamu kutoka Benki ya Dunia, Waleed Malik na (watatu ni kulia) ni Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Leonard Magacha.

***************

Na Aziza Muhali (SJMC)

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt, Eliezer Feleshi, amefanya mazungumzo na wadau kutoka Benki ya Dunia(WB) juu ya tathmini ya Mradi wa Maboresho ya Mahakama ya Tanzania yanayofanywa chini, ambapo umeleta matokeo chanya katika shughuli za Mahakama.

Akizungumza na ujumbe wa benki hiyo, katika ofisi za Mahakama Kuu ya Tanzania, Jaji Kiongozi alisema mradi huo, umeweza kusaidia kuboresha shughuli za utendaji kazi wa Mahakama na kusogeza huduma karibu na wananchi.

“Tumeweza kusikiliza kesi kwa kutumia Mahakama Inayotembea (Mobile Court) jijini Mwanza, hivyo ni moja ya maboresho ya huduma za Mahakama, yaliyotokana na mradi huu,” alisema Jaji Kiongozi.

Aliongeza kuwa mradi huo unaofadhiliwa kwa fedha za mkopo kutoka benki hiyo, umewezesha Mahakama ya Tanzania,kusikiliza kesi kwa njia ya Mtandao ‘Video coference’, ambapo, ugeni huo, ulitaka kufahamu tathimini ya eneo hilo, alisema umeweza kutumika katika baadhi ya mikoa,ambayo ni Mbeya, Bukoba, na Kituo cha Mafunzo cha kilichopo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyo-Dar es Saalam, kikiwemo Chuo cha Uongozi wa Mahakama(IJA) Lushoto.

Jaji Kiongozi amefafanua mkakati wa kupata ukumbi(chumba maalum) kwa ajili ya kuanzisha kusikiliza kesi kwa njia ya mtandao katika gereza la Keko Jijini Dar es Salaam.

Jaji kiongozi amefafanua changamoto zinazoikabili Mahakama ikiwa ni pamoja na upungufu wa kumbi maalumu za kuendeshea kesi kwa njia hiyo,‘Tunakabiliwa na upungufu wa kumbi maalumu kwa ajili ya kuendeshea kesi, hivyo tunatakiwa tupate kumbi nyingi ili tuweze kuendesha kesi kwa wakati.

Aliongeza kwamba kwa hivi sasa ni ukumbi mmoja ndio unaotumika kuendesha kesi kwa njia hiyo’, alisema Mh. Dkt. Jaji Kiongozi.Aliyataja mafaniko mengine ni Mfumo wa Kusajili kesi kwa njia ya Kielektroniki(JSDS).

Dkt. Feleshi alisema eneo lingine, ambalo litafanyikazi ni kuhusu ambayo upelelezi wa kesi kuchukua muda mrefu ambapo kesi moja inaweza kuchukua kati ya mwaka mmoja au zaidi, hivyo litawekewa muda maalum.

Wadau hao , waliwasili nchini mnamo Agosti 23 mwaka huu , watakuwepo nchini hadi Agosti 31, mwaka huu, wamefanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya ujenzi wa Mahakama ikiwemo Mahakama ya Kuu ya Musoma, Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu na kufanya ziara Mkoani Dodoma na Mwanza ambako walijionea hali halisi ya utendaji kazi wa Mahakama Inayotembea.

BARA LA AFRIKA LINA NAFASI KUBWA YA KUPAMBANA NA UMASKINI NA KUYAFIKIA MAENDELEO KWA KASI KUBWA.

0
0
BARA la Afrika lina nafasi kubwa ya kupambana na umaskini na vikwazo vinavyozuia kuyafikia maendeleo, na hiyo ni kutokana na kizazi cha sasa kuwa cha kwanza kabisa kuishi katika bara hilo,huku  wakishuhudia ukuaji wa uchumi ukifikia asilimia 4 kwa nchi nyingi barani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ,Afisa Mtendaji mkuu wa taasisi ya The African Wildlife ,Kadu Sebunya amesema kuwa bara la Afrika tangu mwaka 1994 limeshuhudia vipindi virefu ya ukuaji wa kiuchumi tangu kipindi cha ukoloni katika miaka ya 60, lakini bara la Afrika limeendelea kukua na kubadilisha fikra pamoja na kuyabadilisha mataifa mengi ya Afrika kwa kuwa na uchumi unaojitegemea na unaokua kwa kasi ulimwenguni.

Amesema kuwa uwekezaji katika tafiti, uvumbuzi, elimu, na huduma za afya umeendelea kupunguza kasi ya kuenea kwa magonjwa pamoja na kuongeza kasi ya kujiandikisha shule, ambapo mamilioni ya watoto wanajiandikisha mashuleni kupata maarifa licha ya bara hilo kutokuwa katika nafasi nzuri katika masuala ya kisiasa.

Aidha amesema kuwa “Maendeleo ni Kuchagua” na hiyo itafanikiwa ikiwa viongozi wa Afrika na washirika wa maendeleo katika ngazi zote watapambana dhidi ya changamoto zinazozikumba nchi husika ikiwemo uchimbaji wa rasilimali, miundombinu hafifu, kilimo kisicho faafu, uharibifu wa mito, nyasi, mbuga za wanyama na misitu; vitu ambavyo wananchi wanavitegemea na hugharimu maendeleo.

Kadu amesema kuwa bara la Afrika ni mboni ya uhifadhi wa maliasili pamoja na viumbe wakiwemo robo tatu ya spishi za mamalia duniani wapatao 4700, ndege 2000,aina 2000 za samaki, na amfibia spishi 950 na hiyo ni pamoja na maelfu ya mimea yenye thamani pamoja na wanyama wa mwituni ambao wanawakilisha uasilia, uchumi na ikolojia.

"Utajiri wa Bara hilo umeelezwa zaidi hasa katika sekta za mafuta na gesi asilia na hiyo ni pamoja na kuwa na kampuni zenye umiliki wa hifadhi ya madini wa asilimia 40 duniani licha ya mlengo wa majadiliano ya sasa kuhusiana na maendeleo Afrika yameegemea zaidi katika unyonyanyi wa rasilimali na namna bora ya kuyafikia maendeleo",ameeleza Kadu.

Imeelezwa kuwa bara la Afrika ina maelfu ya utajiri katika sekta za utalii, madini na gesi na kwa sasa kinachotakiwa ni kuangaza macho katika mambo ya msingi ikiwemo madini, miundombinu, mafuta na gesi asilia, kilimo, makazi na mifumo ya wanyama kutegemeana pamoja na usimamizi endelevu wa rasilimali zake asili za kiafrika, mazingira, wanyama pori pamoja na ardhi.

Kupitia mkutano huo Kadu amewashukuru watoa mada wa mkutano huo akiwemo Rais mstaafu wa awamu ya tatu Rais Benjamin William Mkapa na Rais Mogae kwa kushirikiana na taasisi hiyo katika msingi wa wanyamapori wa kiafrika na katika mada zao wamesisitiza mambo muhimu sana kuhusiana mazingira, wanyamapori, na maeneo ya porini na kueleza kufikia mwaka 2063 Afrika litakua bara la maendeleo lenye kutumia rasilimali zake kukiletea maendeleo na kuyasimamia.
Afisa Mtendaji mkuu wa Taasisi ya The African Wildlife, Kadu Sebunya akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar, kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo namna Bara la Afrika linavvyoweza kujikwamua katika lindi la Umaskini ,kupiga hatua ya kimaendeleo na hatimaye kujenga uchumi wa kujitegemea.
Viewing all 109593 articles
Browse latest View live




Latest Images