Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110135 articles
Browse latest View live

TANZANIA YAKABILIWA NA UPUNGUFU WA MARUBANI,WAOMBWA KUJITOKEZA KUSOMEA KOZI HIYO ADHIMU

$
0
0
Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha


MAMLAKA ya usafiri wa anga Tanzania (TCAA) imesema kuwa Tanzania ina
upungufu wa marubani na wataalamu wa mitambo ya ndege, hivyo ni fursa
kwa watanzania walio wengi kujitokeza kusomea fani hyo ili kuweza
kuziba pengo hilo.

Afisa Habari wa TCAA,Bestina Magutu aliyasema hayo juzi,alipokuwa
akizungumza na wanahabari katika banda la mamlaka hiyo,lililopo katika
maonyesho ya kilimo na sherehe za nanenane,katika viwanja vya nanenane
vilivyopo Themi jijini hapa.
Alisema kuwa wakati umefika kwa watanzania wengi kujitokeza kusomea
fani hiyo,ambapo ametoa wito kwa  wazazi na walezi kuwapeleka watoto
wao katika banda la mamlaka hiyo ili waweze kujifunza mambo mbalimbali
yanayohusiana na usafiri wa ndege.

“Unakuta mtoto anapokuwa mdogo ukimuuliza ukiwa mkubwa unataka kuja
kuwa nani anakwambia nataka kuwa rubani lakini ndoto zake zinatoweka
kutokana na kushindwa kujengewa msingi mzuri angali akiwa
mdogo”alisema Magutu.

Alisema kuwa mamlaka hiyo inamiliki na kuendesha chuocha usafiri wa
anga(CATC) kinachotoa mafunzo ya urubani,uongozaji ndege,taarifa za
usafiri wa anga,uhandisi na usimamizi wa shughuli katika viwanja vya
ndege hivyo watanzania wanapaswa kuchangamkia fursa hiyo.

“Mamlaka ya usafiri wa anga hapa nchini ina majukumu makuu mawili
ambayo ni udhibiti wa masuala ya kiusalama na kiuchumi pamoja na
utoaji wa huduma za uongozaji ndege kwa watoa huduma wote wa usafiri
wa anga katika viwanja vyote vya ndege”alisisitiza Afisa habari huyo
wa TCAA.

Aliongeza kuwa Mamlaka hiyo imekuwa makini sana katika kusimamia
masuala ya kiusalama kwa kuhakikisha kuwa ndege inaponunuliwa
ikaguliwa kwanza katika nchi ilipotengenezwa kabla ya kuingia nchini
ili kuhakikisha kuwa ina ubora unaotakiwa na kukagua huduma kwenye
viwanja vya ndege.

Alisema kuwa pia wanaangalia huduma zote zinazotolewa kwa
abiria,matumizi ya miundombinu ya kuruka na kutua ndege mafuta ya
ndege,huduma za uongozaji ndegeikiwa ni pamoja na utoaji wa
mawasilianoya taarifa za anga na mitambo ya kuongozea ndege na ile ya
kufanya uchunguzi katika anga.

Magutu alisema kuwa  pia mamlaka hiyo imekuwa ikiangalia na kukagua
mara kwa mara kuona kama makampuni ya ndege yana uwezo wa kufanya
biashara hiyo,kukagua huduma kwenye viwanja vya ndege pamoja na vyuo
mbalimbali vinavyotoa mafunzo yanayohusianana usafiri wa anga

WASAJILI WASAIDIZI MSAADA WA KISHERIA WASAIDIENI VIONGOZI KUTATUA KERO ZA WANANCHI-MHE. MTAKA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Watumishi wa wizara ya Katiba na Sheria baada ya kuwasili katika Banda la Wizara katika Viwanja vya Nyakabindi kwenye maonyesho ya kitaifa ya Wakulima Nane Nane yanayofanyika wilayani Batiadi mkoani Simiyu
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu akisalimiana na Wasajili Wasaidizi Msaada wa sheria kutoka katika wilaya za Mkoa wa Simiyu wanaoshiriki maonyesho ya Nane Nane yanayofanyika Kitaifa mkoani Simiyu
Mhe. Mtaka akizungumza na Wasajili Wasaidizi waliopo kulia alipotembelea Banda la Wizara ya Katiba na Sheria mjini Bariadi katika maonyesho ya kitaifa ya Wakulima maarufu Kama Nane Nane
Mhe. Mtaka akizungumza na Wasajili Wasaidizi waliopo kulia alipotembelea Banda la Wizara ya Katiba na Sheria mjini Bariadi katika maonyesho ya kitaifa ya Wakulima maarufu Kama Nane Nane
Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria bi Agness Tumbuchile akifafanua Jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu alipotembelea Banda la Wizara katika Viwanja vya Nyakabindi mjini Bariadi mkoani Simiyu ambako yanafanyika maonyesho ya kitaifa ya wakulima
Mhe.Mtaka alisisitiza kitu kwa Wasajili Wasaidizi Msaada wa sheria wa Mkoa wa Simiyu alipotembelea Banda la Wizara katika maonyesho ya wakulima Nane Name mjini Bariadi
………………………

Mkuu wa mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amewataka wasajili wasaidizi Msaada wa Sheria mkoani Simiyu kuwasaidia viongozi wa mkoa huo katika kutatua matataizo ya wananchi kwa kuwa wao wako na wananchi hao katika kazi zao za kila siku na kuwafikisha viongozi taarifa za utatuzi wa kero hizo.

Mhe. Mtaka ametoa rai hiyo alipotembelea banda la Wizara ya Katiba na Sheria katika viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu ambako yanafanyika maonyesho ya wakulima Nane Nane kitaifa.

Mhe. Mtaka alikuwa akiongea bandani hapo na wasajili wasaidizi hao ambao ni maafisa maendeleo ya jamii kutoka katika wilaya za Bariadi, Meatu ,Itilima, Busega na Maswa.

“Nimefurahi kuwakuta wote hapa, niwatake mfanye kazi hii ya Msajili Msaidizi kwa nguvu zote ili muisaidie serikali kutekeleza azma yake ya kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi na hivyo kupata haki zao, muwasaidie viongozi kutatua matatizo ya wananchi kwa sababu sisi wanasiasa leo tupo kesho hatupo lakini nyie mpo na mnayajua matatizo ya wananchi kwani ni sehemu ya kazi zenu za kila siku, Serikali ilipoamua nyiyi mfanye kazi hii ilikuwa inajua ina maana gani“ amesema mhe. Mtaka.

Amesema ataitisha kikao cha pamoja cha wasajili wasaidizi hao na viongozi wa mkoa na wilaya zote ili kuwasikiliza wasajili wasaidizi hao juu ya historia na mwenendo wa matatizo yanayowakabili wananchi kutoka katika maeneo yao na namna wanavyoyatatua ili kuwawezesha wananchi kupata utatuzi wa kudumu na sio kila siku wanapokuja viongozi wapya na matatizo ya wananchi yanakuwa yale yale.

“Nitawaita pamoja na viongozi wenzangu kuanzia mkoani hadi wilayani , mtuambie mwelekeo wa matatizo ya wananchi mliyoyasikia na namna mlivyowasaidia, illi sisi viongozi tuyajue na tuweze kusonga mbele na sio kila anapokuja kiongozi mpya mwananchi anarudia tatizo lile, mkifanya kazi yenu kwa umakini hayo hayatakuwepo, “ alisema Mhe Mtaka.

Amesema Serikali iliamua kuwapa majukumu hayo wasaidizi wa kisheria kwa kuwa ni watu ambao wanakutana na wananachi katika shughuli zao za kila siku na hivyo ni jukumu lao kuwajulisha viongozi wao juu ya kile kinachoendelea miongoni mwa wananchi na namna wanavyoyatatua matatizo ya wananchi.

Wasajili wasaidizi msaada wa kisheria ni maafisa maendeleo ya jamii kutoka katika mikoa, miji, majiji na halmashauri za wilaya nchini kote na wamekasimiwa mamlaka ya kuratibu na kusajili wasaidizi wa sheria na taasisi zinazotoa huduma za msaada wa sheria kwa wananchi nchini kama ambavyo Sheria ya Msaaada wa Sheria Na. 1 ya mwaka 2017 iliyoanza kutumika nchini Julai Mosi 2017 inavyosema.

Kupitia Sheria ya Msaada wa Sheria, Wizara ya Katiba na Sheria inafanya kazi kwa ukaribu na wasajili wasaidizi hao na kuhakikisha huduma za msaaada wa kisheria zinapatikana nchini kwa kila mwananchi mwenye uhitaji na ambaye hana uwezo wa kulipia huduma zinazotolewa na mawakili nchini.

Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na wasajili wasaidizi mkoa wa Simiyu inashiriki maonyesho ya wakulima ya Nane Nane mjini Bariadi ambako elimu juu ya sheria mbalimbali na msaada wa sheria vinatolewa bure kwa wananchi wanaotembelea banda la Wizara kwa kushirikiana na Wasajili Wasaidizi hao.

WANANCHI WA KIJIJI CHA NDULU MKOANI SINGIDA KUPATA BARABARA

$
0
0


Mbunge wa Singida Magharibi, Elibariki Kingu, akihutubia wananchi wa Kijiji cha Ndulu katika mkutano wahadhara uliofanyika wilayani Ikungi mkoani Singida jana.
Mbunge Kingu akikagua ujenzi wa nyumba ya Walimu katika Shule ya Msingi Ndulu ambapo pia alikagua Zahanati ya kijiji hicho.
Mbunge Kingu akikagua ujenzi wa matundu ya choo ya Shule ya Msingi Ndulu.
Burudani zikiendelea zikiongozwa na Msanii Monko Monko. 
Mwenyekiti wa Kijiji cha Ndulu, Joseph Mwanga akizungumza kwenye mkutano huo.
Viongozi wa Kata hiyo wakijitambulisha.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Kata ya Ihanja, Juma Ntandu, akizungumza kwenye mkutano huo.
Mbunge Kingu akikaribishwa kuhutubia kwa burudani za nyimbo.



Na Dotto Mwaibale, Singida.

Mbunge wa Singida Magharibi, Elibariki Kingu amesema Serikali inatarajia kujenga barabara ya kiwango cha changarawe kutoka Kata ya Ihanja iliyopo wilayani Ikungi mkoani Singida hadi Kijiji cha Ndulu yenye urefu wa zaidi ya kilomita 15.

Hatua hiyo imefikiwa kutokana na kilio cha muda mrefu cha wananchi wa kijiji hicho kutokuwa na barabara ya uhakika hivyo kuwa na changamogo kubwa hasa wakati wa mvua za masika.

Akizungumza jana katika mkutano wa hadhara Kingu alisema tayari Serikali imepitisha zaidi ya sh.milioni 287 za ujenzi wa barabara hiyo kinachofanyika hivi sasa ni kufanya usanifu na kumpata mkandarasi atakayeanza kazi hiyo haraka iwezekanavyo.

"Kazi hiyo itakapoanza vijana mkae mkao wa kula kwani mtapata ajira hivyo atakayehitaji kufanyakazi awe tayari kwani ni fursa hiyo kwenu" alisema Kingu.Katika hatua nyingine Kingu alisema Serikali imetoa sh.milioni 170 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na mabwalo ya wanafunzi wa Sekondari katika kata hiyo ya Ihanja.

Mbali ya miradi hiyo Kingu alisema wananchi wa kijiji hicho wakaetayari kupata Umeme wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao utatoka makao makuu ya Kata ya Ihanja hadi katika kijiji hicho ambapo pia aliahidi kuwapelekea jokofu la kutunzia dawa za chanjo katika Zahanati yao ili kuwapunguzia safari ndefu ya kwenda kupata dawa hizo Kituo cha Afya cha Ihanja.

" Nimesikia kilio chenu cha kutokuwa na jokofu nitakwenda Bohari ya Dawa (MSD) kuzungumza na Mkurugenzi Mkuu Laurian Bwanakunu ili nione atatusaidiaje kupata jokofu hilo" alisema Kingu.

Kingu alisema miradi yote hiyo inafafanywa na Serikali baada ya Rais Dkt.John Magufuli kubana mianya ya wizi wa fedha za selikali ambazo zilikuwa zikitumika vibaya na kuzielekeza kufanya miradi ya maendeleo ya wananchi.

WAZIRI HASUNGA ATEMBELEA BANDA LA PSSSF MAONESHO YA NANENANE NYAKABINDI, SIMIYU, HUKU MAONESHO KIKANDA NAKO MFUKO WAENDELEA KUELIMISHA KUHUSU HIFADHI YA JAMII

$
0
0
 Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga, (kulia), akisikiliza kuhusu elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, kutoka kwa Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bi. Rehema Mkamba alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye maonesho ya Nanenane viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
 Mheshimiwa Hasunga, akizungumza jambo na maafisa wa PSSSF kwenye banda la Mfuko huo alipolitembelea
 Afisa Mafao Mwandamizi PSSSF, Bi.Linda Balati (kushoto), akifafanua jambo kwa wanachama wa PSSSF kutoa Benki Kuu ya Tanzania BoT), walipotembeklea banda la Mfukjo huo katika maonesho ya Nanenane kitaifa, viwanja vya Nyakabidni nje kidogo ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSSSF, Bi. Rehema Mkamba akitoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa wanachama hawa waliotembelea banda la Mfuko huo Nanenane Nyakabindi, Simiyu.
 Meneja wa PSSF Mkoani Arusha, Bw. Rajabu Kinande (kushoto), akimhudumia mwanachama aliefika katika banda la Mfuko katika maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini viwanja vya Themi, jijini humo.
 Watumishi wa PSSSF wakihudumia wanachama kwenye maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro
Mfanyakazi wa PSSSF (kushoto), akimsikiliza kwa makini mwanachama huyu aliyetembeleabanda la Mfuko huo viwanja vya Themi, jijini Arusha.

VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KURUDISHA FADHILA KWA JAMII ISIOJIWEZA

$
0
0

Na Woinde Shizza Michuzi Tv ,Arusha 

Viongozi wa dini kote nchini wametakiwa kurejesha fadhila kwa waumini wao na kuwasaidia wananchi na watu wasio jiweza .

Hayo yamebainishwa na Nabii Mkuu Dr GeorDavie Wa huduma ya Ngurumo ya upako Jana wakati akigawa fedha za kuwaongezea mitaji baadhi ya wafanyabiashara wadogo wadogo Wa eneo La Kisongo lililopo ndani ya halmashauri ya Arusha wilaya ya Arumeru mkoani hapa.

Alisema kuwa viongozi wengi wadini wamekuwa hawarudishi fadhila kwa waumini wao ,huku wengine kusahau jamii inayowazunguka kitu ambacho ni kibaya kwani hata katika vitabu vya dini imeandikwa ,watu wasio jiweza , yatima na masikini wasaidiwe .

Aidha ametumia muda huo kumpongeza Rais Wa Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania Mh John Magufuli kwa jinsi anavyofanya Kazi pamoja na jinsi anavyo wajali wanyonge na watu wasiojiweza huku akibainisha kuwa ataendelea kumuombea pamoja na kumuunga mkono katika juhudi za kuleta maendeleo kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

" kutoa msaada huu ni njia moja wapo ya kumuunga mkono Rais wetu kwa Kazi nzuri anazofanya ,na tutaendelea kumuunga mkono ,Rais wetu ameonyesha njia ya kusaidia wanyonge na wasio jiweza na Mimi kama kiongozi Wa serikali ya ufalme wa mungu nimeamua kumuunga mkono na Leo sio mwanzo wala mwisho nitaendelea kutoa msaada kila Siku kadri mungu anavyo niongoza.

Alisema Katika serikali za duniani Wananchi wa Hali ya chini ndio wapiga kura na ndio walipa Kodi, vilevile katika serikali ya ufalme wa mungu wao ndio watoji wa kubwa wa sadaka na matoleo mbalimba, alisema wakiwezeshwa watafanya zaidi ya jinsi wanavyofanya Sasa katika serikali zote mbili

Nabii huyo ametoa zaidi ya shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwaongezea mitaji wajasiriamali wadogo Wa eneo La kisongo ikiwa Ni muendelezo wa kuwawezesha wafanyabiashara wadogo wadogo ambao kwa mwaka huu ametoa Zaidi ya milioni 200, ikiwa Ni pamoja na kuwajengea nyumba watu wasio nauwezo, kuwapa vijana pikipiki za biashara (bodaboda) pamoja na kutoa magari kwa watu mbalimbali huku akiahidi kutoa pesa na Mali kwa watu wengine kadri Mungu atakavyo muongoza .

Wakiongea Mara baada ya kupokea msaada huo Wa mitaji baadhi ya wajasiriamali wamemshukuru Nabii Mkuu kwa kuwawezesha kibiashara huku wakisema utawasaidia kukuza biashara zao.

"Kwakweli namshuru Mungu kwa kutuletea Huyu baba, Mimi nilikuwa na mitaji Wa machugwa Wa elfu kumi nimepewa hii laki moja kwa kweli nashukuru ,kwani sitauza machugwa tena Bali nitabadilisha biashara na nitaanza kuuza dagaa nashukuru sana" alisema Mary Kristofa

Kwa upande wake Marieta Daudi amemshukuru kwa msaada huo na kuwataka viongozi wengine Wa dini kuwa na moyo huo Wa kutoa ili kuweza kuwainua wananchi Wa chini na wasio jiweza.
Nabii Mkuu Dr GeorDavie Wa huduma ya Ngurumo ya upako akiwa anampa msaada Wa fedha mama mmoja mfanyabiashara Mdogo kwaajili ya kuongeza mtaji

MAGAZETI YA LEO AUGUST 6,2019

SONGAS YAKABIDHI MEDALI NA KOMBE KWA WASHINDI WA KITENGO CHA BIOLOJIA SHULE YA SEKONDARI MTWARA GIRLS

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Songas, Nigel Whittaker akikabidhi medali na kombe kwa Faudhia Juma Said na Zaina Yassin washindi wa kitengo cha Biolojia kutoka shule ya sekondari ya Mtwara Girls wakati wa maadhimisho ya mashindano ya sayansi yajulikanayo kama Young Scientist Tanzania, yaliyofanyika katika kumbi za JNICC, jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Songas imekuwa moja kati ya wadhamini wa mashindano hayo kwa muda wa miaka nane sasa na hii ni katika kuunga mkono juhudi za Serikali kuboresha sekta ya elimu.
Kheri Omar Sheha na Ally Yassin kutoka Shule ya Feza Zanzibar wakipiga picha (Selfie) na Mkurugenzi Mkuu wa Songas, Nigel Whittaker mara baada ya kushinda kitengo cha Biologia wakati wa mashindano ya Sayansi yajulikanayo kama Young Scientist Tanzania yaliyofanyika katika kumbi za JNICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Songas imekuwa moja kati ya wadhamini wa mashindano hayo kwa muda wa miaka nane sasa na hii ni katika kuunga mkono juhudi za Serikali kuboresha sekta ya elimu. 

SERIKALI YAWEKA MKAKATI KUHAKIKISHA WANUFAIKA WA TASAF WANAPATA RUZUKU STAHIKI NA KWA WAKATI

$
0
0
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na Wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika Kijiji cha Magata, wilayani Muleba mkoani Kagera wakati wa ziara ya kikazi yenye lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Magata baada ya kumaliza mkutano na wananchi na wanufaika wa TASAF katika Kijiji cha Magata, wilayani Muleba mkoani Kagera.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Mhe. Mhandisi Richard Ruyango na baadhi ya Watendaji wa TASAF wakielekea kwenye nyumba ya mnufaika wa TASAF kuona namna alivyotumia ruzuku inayotolewa na Serikali kupitia mfuko huo.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiwa na moja ya familia ya mnufaika wa TASAF katika Kijiji cha Magata wilayani Muleba ambaye alipata ulemavu wa viungo kutokana na ajali.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akiangalia banda la mifugo katika Kaya ya mmoja wa wanufaika wa TASAF, Bi. Nazifa Naziru katika Kijiji cha Magata wilayani Muleba.
……………………..
Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) imejipanga kikamilifu kuhakikisha inaweka mkakati madhubuti na endelevu wa kuwapata wanufaika stahiki wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na kuwapatia ruzuku zao kwa wakati.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakati akizungumza na wananchi na wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wa Vijiji vya Magata na Kyamyorwa, wilayani Muleba mkoani Kagera ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kikazi mkoani humo ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.
Dkt. Mwanjelwa amesema kuanzia sasa wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini watasajiliwa katika mfumo wa kielektroniki ikiwa ni pamoja na kupigwa picha kwa anayesajiliwa na anayesajili wakiwa katika makazi ya mnufaika ili kujiridhisha na sifa za mhusika.
Dkt. Mwanjelwa ameongeza kuwa, katika kuboresha utekelezaji wa Mpango wa TASAF awamu ya tatu sehemu ya pili, wanufaika wa Mpango watapatiwa ruzuku yao kwa njia ya miamala ya simu ili wapate stahiki zao kwa wakati.
“Wanufaika mnatakiwa kuwa na simu za viganjani zitakazowawezesha kupokea ruzuku zenu halisi na kwa wakati,” Dkt. Mwanjelwa amesema.
Dkt. Mwanjelwa amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua kuwajali wanyonge hivyo, itahakikisha kila mnufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini anapata stahiki yake.

BODI YA NAFAKA NA MAZAO MCHANGANYIKO MKOMBOZI KWA WAKULIMA: WAZIRI HASUNGA

$
0
0
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Simiyu

WAZIRI wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga amesema Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ni mkombozi kwa wakulima hapa nchini.

Mhe. Hasunga ameyasema hayo alipotembelea banda la bodi hiyo kwenye viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu ambako kunafanyika maonesho ya Nanenane kitaifa ambapo wakulima wanaonesha mazao yao lakini pia maonesho hayo yanatumika kuwaunganisha na wadau mbalimbali wa kilimo.

“Kwa wakulima bodi hii ni mkombozi kwa wakulima kwani jukumu lake ni kuhakikisha tunaongeza uzalishaji wa mazao ya nafaka, lakini pia bodi hii inanunua mazao ya nafaka na kuyaongezea thamani na sasa wameanzisha kiwanda kule Arusha cha kusaga nafaka na kuuza, lakini pia Dodoma watajenga kiwanda cha kuchakata Alizeti na nafaka na pia Mwanza watajenga kiwanda cha kuchakata mpunga na mazao mengine hivyo bodi hii ni muhimu kisekta.” Alisema. 

Mhe. Hasunga pia ameipongeza Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko kwa kutekeleza vema maelekezo ya Serikali ya kununua na kuuza Korosho.

“Moja ya Jukumu tulioipatia Bodi mwaka huu ni kununua na kuuza Korosho kwa niaba ya Serikali na kazi hiyo wameifanya vizuri, wameweza kunua Korosho yote na wanayo.” Alifafanua.

Alisema, Bodi kama wafanyabiashara imeweza kununua Korosho na kuongeza thamani (Ku- process) kwa kuziweka kwenye vifungashio vya viwango mbalimbali na ndio maana wako kwenye maonesho ili kuzionesha na kutangaza masoko mbalimbali kwa wadau wa ndani na nje ili waweze kutoa Oda na hii itasaidia kupanua masoko ya Korosho.
Maonesho ya Nanenane kitaifa hapa Nyakabindi Mkoani Simiyu yalizinduliwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Agosti 1, na yatafikia Kilele Agosti 8, 2019 na yamebeba kauli mbiu isemayo "Kilimo, Ufugaji na Uvuvi kwa ukuaji w aUchumi wa Nchi.".
 Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga, akizungumza kwenye viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu ambako Maonesho ya Nanenane kitaifa yanafanyika mkoani humo.
 Wafanyakazi wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko, (kushoto), wakielimisha wakulima hawa wa Mkoani Simiyu walipotembelea banda la Bodi hiyo kwenye maonesho ya Nanenane kitaifa yanayofanyika viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu leo Agosti 5, 2019.
 Kikosi kazi cha Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko, ambacho kiko kwenye banda la bodi hiyo viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu tayari kutoa elimu kwa wananchi
 Wafanyakazi wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko, (kushoto), wakitoa elimu kuhusu shughuli za Bodi.

WAZIRI MKUU AWAHAMASISHA WATANZANIA KUENDELEA KUTEMBELEA KWA WINGI MAONESHO YA BIASHARA YA NCHI ZA SADC KUONA FURSA ZILIZOPO

$
0
0
Na Said Mwishehe,Michuzi TV

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewahamasisha Watanzania kutembelea Wiki ya Maonesho ya Biashara ya nchi za SADC yanayoendelea katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijjini Dar es Salaama ili kuona bidhaa mbalimbali zinazozalishwa.

Amesema ni fursa kubwa kwa Watanzania kuona bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi yao lakini pia wakaona bidhaa zinazozalishwa na nchi nyingine ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Bara la Afrika.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameyasema hayo leo Agosti 6,2019 baada ya kutembelea mabanda yaliyopo kwenye maonesho hayo ya SADC ambapo amefafanua kuwa ameona bidhaa za aina mbalimbali ambazo zinazozalishwa nchini zikiwa kwenye kiwango cha ubora wa hali ya juu na hivyo ameshauri Watanzania kujitokeza kwa wingi.

"Maonesho haya ni bure,nitoe rai kwa Watanzania wafike waone namna ambavyo bidhaa za hali ya juu ambazo zimetengenezwa na Watanzania.Pia wakifika wataona bidhaa zinazozalishwa na nchi nyingine.Ni fursa kubwa kwetu Tanzania kutumia nafasi hii kutangaza biadhaa zetu za ndani,"amesema Waziri Mkuu.

Amesema pia katika maonesho hayo kuna bidhaa mbalimbali zitokanazo na nafaka huku akutumia nafasi hiyo kueleza bidhaa hizo mbali ya kuwa kwenye maonesho watapata fursa ya kuuza bidhaa zao mwishoni mwa maonesho hayo

Amesema ni wakati mzuri wa kuhakikisha nchi yetu inaendelea kuhamasisha wawekezaji wa nje kuja kuwekeza nchini Tanzania kwani mazingira ni mzuri,huku akitoa rai kwa vyombo vya habari nchini kuendelea kuitangaza nchi yetu.

Wakati huo huo Waziri Mkuu ametumia nafasi hiyo kuwataka Watanzania kuwakarimu wageni wote ambao wamefika kwenye mikutano ya SADC na kwamba wageni wengi wameshafika na wengi e wanaendelea kuwasili.

Pia amezungumzia umuhimu wa kutangaza vivutio vya utalii wa nchi yetu ambavyo ni vingi na ni wakati muafaka kuhakikisha utalii wetu unaendelea kuzungumzwa na kuwahamasisha wageni kwenda kutembelea ma kuona maeneo ya utalii wetu.

Amesema nchini Tanzania kuna utali wa kila kiasi kwamba hata baadhi ya nchi wanatumia kivutio vyetu vya Utalii kutangaza vipo kwai,hivyo ni jukumu la wataanzania na kwa kutumia vyombo vya habari kueleza kuhusu kivutio vyetu.

"Tunajua Wizara ya Utalii inafanya kazi ya kutangaza Utalii wetu na vivutio vilivyopo lakini kwa kipindi hiki kila mmoja wetu kwa nafasi yake kutangaza utalii kwa wageni waliopo nchini kwetu,"amesema Waziri Mkuu.
 
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa akzungumza mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani),leo kuhusu kuwahamasisha Watanzania kutembelea Wiki ya Maonesho ya Biashara ya nchi za SADC yanayoendelea katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijjini Dar es Salaama ili kuona bidhaa mbalimbali zinazozalishwa.Pichanu kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh Prof.Palamagamba Kabudi,kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara ,Mh.Innocent Bashungwa 

DKT.GWAJIMA ATUMIA “ VIDEO CONFERENCE ” KUTOA MAAGIZO KWA WAJUMBE 234 WA TIMU ZA UENDESHAJI HUDUMA ZA AFYA MIKOA (RHMT)

$
0
0
Watumishi wa Idara ya afya Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia afya Dkt. Doroty Gwajima wakati akitoa maelekezo kuhusu sekta ya afya kupitia mfumo wa uendeshaji wa vikao kwa njia ya kielektroniki kwa Wajumbe 234 wa Timu za Uendeshaji Huduma za Afya Mikoa (RHMT).
Baadhi ya watumishi wa Idara ya afya Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia afya Dkt. Doroty Gwajima wakati akitoa maelekezo kuhusu sekta ya afya kupitia mfumo wa uendeshaji wa vikao kwa njia ya kielektroniki kwa Wajumbe 234 wa Timu za Uendeshaji Huduma za Afya Mikoa (RHMT) akiwa katika ziara ya kikazi katika Mkoa wa Kilimanjaro.

……………………..
Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Dkt. Dorothy Gwajima atumia mfumo wa uendeshaji wa vikao vya kazi kwa njia ya kielektroniki “video conferencing” kufanya mkutano na Wajumbe 234 wa Timu za Uendeshaji Huduma za Afya Mikoa, Wakurugenzi na Walezi wa Mikoa kutoka OR-TAMISEMI.

Mkutano huu ambao umefanyika kwa teknolojia hiyo ni wa mara ya kwanza na unalenga kupunguza gharama za safari kwa ajili ya vikao ambavyo, ajenda zake zinaweza kujadiliwa kwa njia ya kielektroniki na hivyo kuboresha ufanisi katika ufuatiliaji wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali.
Akiongea kwa njia ya Video Conference kutokea Mkoa wa Kilimanjaro alipokuwa kwenye ziara ya kikazi, Dkt. Dorothy Gwajima amesema, kuanzia sasa atakuwa akitumia njia ya kielektroniki “Video Conference” kwa ajili ya kuwakutanisha wadau wote wa sekta ya afya kujadili masuala yanayowahusu pia kutoa maelekezo na kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa majukumu.

Dkt. Gwajima amefafanua kuwa iwapo angefanya kikao cha siku moja cha wadau hao wa afya , posho peke yake bila gharama za safari na ukumbi kwa siku moja ingegharimu takribani Tsh. milioni 30 na ukijumlisha na siku 2 za safari kuja Dodoma ingeweza fikia siyo chini ya Tsh. Milioni 100 au zaidi.
Anaendelea kufafanua kuwa, mfumo wa uendeshaji vikao kwa njia ya kieletroniki (video conference) utasaidia kudhibiti matumizi ya fedha nyingi zilizokuwa zikitumika katika uendeshaji wa vikao hivyo na kuwezesha kusaidia kutoa maagizo ambayo yatasaidia kufanya maboresho ya haraka na kuleta tija katika Sekta ya Afya nchini.

Amesema kuwa, kufanya vikao kwa kutumia mfumo huo kutasaidia kutatua changamoto zilizopo katika Mikoa na Halmashauri kwa kutoa ushauri wa haraka na kupokea taarifa za utekelezaji kwa ufanisi na kwa gharama nafuu zaidi ukilinganisha na gharama za safari kwa ajili ya kufanya vikao.

Wakati huohuo Dkt. Dorothy Gwajima amewaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa, Waganga Wakuu wa Wilaya na Timu za Uendeshaji Huduma za Afya nchini kuhakikisha wanafanya tathmini ya kina ili, kubaini changamoto wanazozisema kwa takwimu siyo kwa maneno tu ya jumla ambayo yanayoficha uhalisia wa changamoto husika.

“Kabla hatujasema upungufu wa watumishi tufanye mahesabu ya uwiano wa uwingi wa kazi kwa kila mtumishi kwa kutumia fomula ya WISN ambayo, tumefundishwa wote. Vinginevyo ukisubiri hadi Wizara ije ifanye basi hapo ni kwamba, RHMT/CHMT mtakuwa mmeshindwa kutekeleza wajibu wenu na badala yake mmegeuka chanzo cha changamoto” Amefafanua Dkt. Gwajima.
Dkt Gwajima amaesisitiza kufanya hesabu sahihi ili kuweza kuwapata baadhi ya wataalamu na kuwahamisha waende kwenye upungufu mkubwa zaidi wakati, zoezi la ajira likiendelea.

Vilevile, Dkt. Gwajima amewataka wajumbe hao kuhakikisha kabla ya kuandika changamoto ya ukosefu wa vifaa tiba, ni vyema wakahakiki maeneo yenye akiba ya vifaa ambavyo havitumiki ili vipelekwe maeneo yenye uhitaji mkubwa badala ya kila mara tunawaza kununua hivyo kusababisha baadhi ya vifaa kuharibika au kupotea.

Aidha amezitaka RHMT kumiliki taarifa wanazotuma Wizarani na kuhakikisha wanazituma kwa wakati kwa kuwa , kila mmoja atatetea taarifa aliyoituma kupitia vikao hivyo na uwajibikaji wake utawekwa wazi ambapo kwa sasa vikao hivyo vitakuwa vitafanyika kila mwezi kwa pamoja na kila wiki kutakuwa na ratiba ya mikoa kadhaa kuhudhuria vikao hivyo na kuwasilisha taarifa za maendeleo ya uwajibikaji.

Wakati huohuo Waganga Wakuu wa Mikoa wameupongeza mpango wa kuendesha vikao kwa njia ya Kielektroniki ambao umesaidia kutoa mtazamo mpya wa jinsi ya kukabiliana na changamoto mbalimbali za Sekta ya Afya nchini.

VIKUNDI VYA UWT WILAYA YA MUFINDI VYAFIKISHA MTAJI WA MILIONI MIAMBILI KUMI NA NNE

$
0
0
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rose Tweve akihutubia baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi wa jimbo la Mufindi Kaskazini wakati wa mkutano mkuu wa jimbo hilo
Baadhi ya viongoziwa chama cha mapinduzi wa jimbo la Mufindi Kaskazini wakati wa mkutano mkuu wa jimbo hilo


NA FREDY MGUNDA,IRINGA

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Rose Tweve ameendelea kuitunisha mifuko ya kimaendeleo ya wanawake wa UWT wilaya ya mufindi kwa kukuza mitaji waliyopewa na mbunge huyo.

Akizungumza kwenye mkutano mkuu wa jimbo la Mufindi kaskazini,mbunge Rose Tweve alisema kuwa vikundi vya wilaya ya Mufindi vinajumla ya mtaji wa milioni miambili kumi na nne (200,140,000) ambazo zinatokana na mtaji wa awali ambao mbunge huyo aliwapa.

Ikumbukwe kuwa mbunge Rose Tweve aliahidi kuviwezesha vikundi vyote vya UWT mkoa wa Iringa kwa kila kata akiwa na lengo la kuhakikisha kuwa wanawake wanajikomboa kiuchumi kupitia fedha hizo ambazo alikuwa amewaahidi.

Tweve aliwaomba wanawake wa UWT wilaya ya Mufindi waendelee kufanya kazi na kutunza mtaji huo kwa kuwa ndio mkombozi wa uchumi na amewapongeza kwa kuwa na nidhamu ya fedha ambayo wamekuwa na hadi hapo walipo fika.

“Hongereni sana wakinamama na nawaomba viongozi kuanzia ngazi ya kata hadi wilaya kuendelea kuwalea na kuwapa ushirikiano wa kutosha ili wafikie malengo yawalikusudia kwa kuwa wameonyesha nidhamu ya matumizi ya fedha” alisema Tweve

Awali mbunge huyo alitoa mitaji ya shilingi laki tano kwa vikundi vya wanawake wa kila kata kama mitaji ya kuanzia biashara zao ambazo zitasaidia kukuza uchumi wa moja moja na wa wilaya kwa ujumla.

Aidha Tweve amewataka Wanawake mkoa Iringa kujiunga katika vikundi mbalimbali vya kijasiliamali bila kujali itikadi za vyama vyao ili kuleta maendeleo.“Akina mama wasikate tamaa katika kujiunga katika vikundi mbalimbali kwani hiyo inasaidia kubadilishana mawazo katika suala la kutekeleza maendeleo yao” alisema Tweve

Tweve amewataka viongozi kuhakikisha wanawapigania wanawake katika kupata fursa na kuvunja mfumo dume uliopo.Katika hatua nyingine amewaasa wanawake wanapowezeshwa fedha wahakikishe wanazitumia vizuri ili kufikia malengo yao.

Waziri Simbachawene atoa wito kutangaza mafanikio ya Muungano

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. George Simbachawene akizungumza katika kikao na viongozi mbalimbali na watendaji kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar alipofanya ziara ya kujitambulisha.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Mohamed Aboud akimkaribisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. George Simbachawene, ujumbe wake, viongozi, watendaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Ofisi ya Makamu wa Rais.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. George Simbachawene akizungumza katika kikao na viongozi mbalimbali na watendaji kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Viongozi na watendaji wa Serikali wakifuatilia kikao kilichowakutanisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. George Simbachawene.

*************



Na Ofisi ya Makamu wa Rais

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. George Simbachawene amesema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni kipekee na kuwataka Watanzania kutangaza mazuri yake.

Ametoa kauli hiyo Agosti 5, 2019 wakati wa ziara yake visiwani Zanzibar alipofika kujitambulisha kwa viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Waziri Simbachawene alisema kuwa Muungano wetu unaishi na kuwa ni vyema sasa tuyape sauti kubwa yale mazuri yanayofanyika kutokana na Muungano huo kuliko changamoto.

“Mazuri ya Muungano ni mwngi kuliko changamoto na nina imani tutashirkiana vizuri na kaka yangu hapa Mheshimwa Aboud ambaye ni mwanadiplosia na tuna wataalamu hapa mtatusaidia ili tutekeleze wajibu. 

Niwahakikishie nitachangia mawazo katika kuutunza na kuulinda, naomba ushirikiano,” alisisitiza Waziri Simbachawene. 

“Changamoto zilizokuwepo 15 hadi sasa zimebaki kama tano zingine zinapungua zaidi muungamo unaishi aina ya muungano ni haufanania na mingine ni vizuri kulinda kutunza na kuuendeleza na wakati mwingine ni vizuri kuangalia na kuona umuhimu wa kueleza mazuri yake.

“Wakati sasa umefika kwa kizazi kilichozaliwa ndani ya karne ya 21 kinapaswa kuelewa dhamira nzima ya waasisi wa Muungano ambao wengi kati yao wamesoma historia yake ndani ya vitabu,” alisisitiza.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Mohamed Aboud alisema Serikali hizi mbili zina jukumu la kuutunza na kuuendeleza Muungano.

Mhe. Aboud alisema Ofisi hizi za Makamu wa Rais na Makamu wa Pili zinahitaji kufanya kazi kwa pamoja na kuwa urafiki wetu utakuwa chachu ya kufanya kazi kwa ukaribu zaidi.

“Nakukukaribisha sana Mheshimwa Waziri na milango ipo wazi na tunaweza kushirkiana kwa karibu tufanye kazi pamoja ili tutekeleze wajibu wetu katika kusimamia mambo ya Muungano,” alisema Mhe. Aboud.

Zaidi ya wateja 6000 kuunganishiwa umeme wa mradi wa ‘Peri Urban’ mkoani Pwani

$
0
0

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) akiwasha umeme katika moja ya nyumba za Mkazi wa Kijiji cha Muheza katika Halmashauri ya Mji wa Kibaha ikiwa ni kuzindua Mradi wa Usambazaji wa Umeme katika vijiji vilivyopo pembezoni mwa Miji( Peri-Urban) katika wilaya hiyo.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu(kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Wakili Julias Bundala Kalolo( kulia) kabla ya kuwasha umeme na kuzindua Mradi wa Kusambaza umeme katika vijiji vilivyopo pembezoni mwa Miji ( Peri-Urban) katika Halmashauri ya Kibaha vijijini mkoani Pwani.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) akikata utepe kuashiria kuzindua Mradi wa Usambazaji wa Umeme katika vijiji vilivyopo pembezoni mwa miji( Peri-Urban) katika Kijiji cha Mwanabwito wilayani Kibaha vijijini.Uzinduzi huo umeshuhudiwa na Wajumbe bodi ya Wakurugenzi ya REA ,Viongozi wa Wizara ya Nishati na Taasisi zilizo chini yake ikiwemo REA na Tanesco.
Wasanii wa nyimbo za asili kutoka kabila asili ya Mkoa wa Pwani,wakiigiza kumtambikia Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu( kulia aliyekaa) wakati wa sherehe za kuzindua Mradi wa Usambazaji wa Umeme katika vijiji vilivyopo pembezoni mwa miji( Peri-Urban) wilayani Kibaha, mkoani Pwani.
Gari lililobeba nguzo mali ya Mkandarasi Sengerema zikiwa tayari zimewasili katika kijiji cha Mwanabwito, katika Halmashauri ya Kibaha vijijini kwa ajili ya mradi wa Peri-Urban.

……………………………………………………………..

Na Zuena Msuya, Pwani

Naibu waziri wa Nishati Subira Mgalu, amesema zaidi ya wateja 6000 mkoani Pwani wataunganishiwa umeme wa mradi wa kusambaza umeme katika vijiji vilivyopo pembezoni mwa Miji.

Mgalu alisema hayo, Augosti 05,2019, wakati akiwasha na kuzindua umeme katika kijiji cha Muheza katika Halmashauri ya Mji wa Kibaha na katika kijiji cha Mwanambwito katika Halmashauri ya Kibaha vijijini.

Alisema kuwa maeneo yote ya Wilaya ya Kibaha ikiwemo mitaa, vijiji pamoja na vitongoji vyate vitafikiwa na Mradi wa Peri-Urban.

Alifafanua kuwa mradi huo utangarimu zaidi ya shilingi bilioni 14 katika Mkoa wa Pwani pekee na unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 9 baada ya kuanza kwa utekelezaji wake.

Aliweka wazi kuwa mradi huo utaleta tija kubwa kwa taifa kwa kuwa utakuwa ukifanya kazi ya kuwaungashia umeme wananchi ambao hawakupitiwa na Mradi wa kusambaza umeme vijijini( REA) au hawakuweza kupata huduma hiyo kutokana na sababu mbalimbali.

“Mradi huu utafanya kazi kubwa sana kwa wananchi na utaleta manufaa makubwa sana kwa sababu wale wote walioshindwa kuunganishwa na umeme wa REA kwa namna moja au nyingine, au wale ambao hawakupitiwa kabisa, sasa mradi huu unamaliza kila kitu, utawaunganisha wote,jiandaeni kuupokea”,alisisitiza Mgalu.

Aliwaeleza wananchi wa Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani kuwa wataunganishwa na mradi huo kwa bei ya shilingi 27,000/= tu,ambayo inajumuisha gharama za nguzo, nyaya pamoja na LUKU, hivyo wananchi wasikubali kuchangia zaidi ya kiasi hicho cha fedha.

Sambasamba na hilo aliwaeleza kuwa mwananchi atalipia gharama ya kutandaza nyaya katika nyumba yake,kwa makubaliano na wakandarasi au mafundi waliothinishwa na shirika la Umeme nchini (TANESCO), kufanya shughuli hizo.

Mradi huu kwa Mkoa wa Pwani unatekelezwa na mkandarasi mzawa wa kampuni ya Sengerema na tayari ameanza kutekeleza mradi huo kwa kuwaungaishia wananchi huduma ya umeme huku akiendelea na ujenzi wa miundombinu katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Pwani.

IGP SIRRO AKUTANA NA MAKAMANDA WA POLISI WA MIKOA YOTE NCHINI JIJINI

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro akizungumza na makamanda wa Polisi hawapo pichani toka mikoa 35 Tanzania Bara na Visiwani katika ukumbi uliopo Polisi Makao Makuu jijini Dar Es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, akiwa katika picha ya pamoja na makamanda wa Polisi toka mikoa 35 baada ya kumaliza kikao cha utendaji kazi. (Picha na Jeshi la Polisi)


SERIKALI YAJIPANGA KUONGEZA RASILIMALI WATU TRA

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu (kushoto), akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Fedha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA, Bi. Dinah Edward, alipofanya ziara ya kikazi katika Mamlaka hiyo kubaini changamoto za utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2018/19 na njia ya kuzitatua, katika ofisi za TRA jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Khatibu Kazungu (kushoto), akimsikiliza kwa makini Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA, Dkt. Edwin Mhede, kuhusu changamoto za Mamlaka hiyo hususani upungufu wa wafanyakazi wa kada mbalimbali takribani 2000, wakati wa mkutano katika Ofisi za Mamlaka hiyo Jijini Dar es Salaam.
Mkutano kati ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA, Dkt. Edwin Mhede, ukiendelea katika Ofisi za TRA jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu (kulia), Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Christopher Nkupama (kushoto) na Mtaalam wa Sera wa Wizara hiyo Bw. Msabaha Msabaha, wakimsikiliza Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA, Dkt. Edwin Mhede (hayupo pichani), alipokuwa akielezea mikakati ya ukusanyaji wa mapato.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu (kushoto), akihoji masuala mbalimbali ya utekelezaji wa Bajeti, wakati wa mkutano kati yake na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA, Dkt. Edwin Mhede (kulia), alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi za Mamlaka hiyo, Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Fedha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA, Bi. Dinah Edward (kushoto), akieleza changamoto za utekelezaji wa bajeti kwa mwaka 2018/19 wakati wa ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu (wa pili kushoto), jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Khatibu Kazungu (kulia) akiagana na Kaimu Mkurugenzi wa Fedha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA, Bi. Dinah Edward, baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi katika Mamlaka ya hiyo, jijini Dar es Salaam.
(Picha na Peter Haule, WFM, Dar es Salaam)
………………………
Na Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Serikali imejipanga kuongeza ufanisi wa kiutendaji na ukusanyaji wa Mapato wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA kwa kuongeza wafanyakazi na kuboresha makazi ya watumishi, ikiwa ni sehemu ya kutatua changamoto za utekelezaji wa Bajeti ya Mamlaka hiyo kwa mwaka wa Fedha 2018/19.
Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, wakati wa ziara ya kikazi ya kufuatilia mafanikio na changamoto za utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2018/19 kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania.
Dkt. Kazungu alisema kuwa, amebaini upungufu wa takribani wafanyakazi 2000 wa kada mbalimbali katika mamlaka hiyo, hivyo kufifisha ufanisi wa ukusanyaji wa mapato kwa kiwango toshelevu ili kufanikisha utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo.
“Kama Wizara ya Fedha na Mipango tumeona kuna umuhimu wa kuiwezesha TRA katika rasilimali watu na fedha ili kuongeza mapato ya Serikali katika muda mfupi ujao ili kuweza kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi na nchi kwa ujumla”, alieleza Dkt. Kazungu.
Alisema kuwa changamoto nyingine ni pamoja na upungufu wa vitendea kazi yakiwemo magari, ambapo ameahidi kulifanyia kazi suala hilo ili kurahisisha utendaji kazi wa Mamlaka hiyo muhimu katika mstakabali wa ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Dkt. Kazungu alisema ziara yake katika Mamlaka ya Mapato Tanzania ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara yake hususani katika eneo la changamoto zilizojitokeza kwa mwaka uliopita na kuangalia ni njia zipi zinaweza kutumika kuzitatua ili kuleta ufanisi kwa mwaka wa fedha 2019/20.
Kwa upande wake Kamishna Mkuu TRA, Dkt. Edwin Mhede, alimpongeza Dkt. Kazungu kwa kufanya ziara katika Taasisi yake na akamhakikishia kuwa amejipanga kimkakati kuhakikisha mapato yanaongezeka na pia iwapo suala la upungufu wa wafanyakazi litatatuliwa, ongezeko la makusanyo litakuwa sio jambo gumu kwa mamlaka yake.
Naibu Katibu Mkuu Dkt. Khatibu Kazungu, anafanya ziara katika Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Fedha kubaini changamoto za utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2018/19 na kuangalia utatuzi wake kwa mwaka wa fedha 2019/20.

RAIS MAGUFULI ATEMBELEA BANDA LA KAMPUNI YA MAFUTA YA PUMA TANZANIA, AWAPA UJUMBE KUHUSU GAWIO

$
0
0
*Puma nao wampongeza Rais kwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji

 Na Said Mwishehe, Michuzi TV

KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Energy Tanzania imemueleza Rais Dk.John Magufuli kuwa mazingira mazuri ya uwekezaji nchini yameifanya kampuni hiyo kuendelea kutengeneza faida mwaka hadi mwaka na hivyo imesababisha kuongezeka kwa gawio kwa Serikali.

Rais Magufuli alifika kwenye banda la Puma Energy Tanzania wakati anatembelea mabanda katika Maonesho ya Nne ya Wiki ya Viwanda ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika(SADC) yanayoendelea Ukumbi wa  Kimataifa wa Mwalim Nyerere jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika banda la Puma Energy Tanzania, Rais Magufuli pamoja na mambo mengine aliuliza maofisa wa kampuni hiyo mwaka huu wamejipanga kutoa gawio la shilingi ngaoi kwa Serikali, ambapo alijibiwa watatoa Sh.bilioni 22 ambapo  Sh.bilioni 11 zitakwenda kwa Serikali.

 "Mwaka jana mlitoa gawio kiasi gani?(Akajibiwa) basi mwaka huu uongezeni  ongezeni kidogo,"alisema Rais Magufuli ambapo maofisa wa Puma nao  wakamhakikishia Rais kuwa watajitajihidi kuongeza huku wakipongeza mazingira mazuri ya uwekezaji ambayo yamesababisha wao kuendelea kufanya vema siku hadi siku.

Akizungumza mbele ya Rais Meneja Operesheni wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania Lamecky Hiliyai amemwambia Rais kuwa kampuni hiyo kutokana na mazingira mazuri yaliyopo nchini katika uwekezaji wamekuwa wakiendelea kufanya biashara ya mafuta na kupata faida.

"Mheshmiwa Rais tunashukuru kwani kutokana na mazingira mazuri ya uwekezaji katika nchi yetu, nasi Kampuni ya Puma tumeendelea kufanya biashara, hivyo tumeendelea kupata faida na tunaahidi hata gawio kwa Serikali nalo tutaendelea kuongeza mwaka hadi mwaka,"alisema Hiliyai.

Kwa upande wake Meneja wa Sheria na Mahusiano ya kampuni hiyo, Godluck  Shirima amewaambia waandishi wa habari Kampuni yao inajivunia kufanya 

biashara katika nchi 13 za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).Kampuni hiyo ambayo inamilikiwa kwa ubia na Serikali ya Tanzania imesema  mbali na kudhamini maonesho ya wiki ya viwanda ya SADC pia imekuwa ikisaidia  jamii katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Shirima, alisema wamekuwa wakijiendesha kwa faida tangu walipoanza shughuli  zao mwaka 2011/12. Kwa mujibu wa Shirima mwaka 2011/12 walitoa gawio la Sh bilioni 3.5 kwa wanahisa wake na kati ya fedha gizo Serikali ilipata Sh bilioni 1.25.

Alisema mwaka 2018/19 wanatarajia kutoa gawio la Sh bilioni 22 na Serikali  itapata Sh bilioni 11. "Sisi ni wadau wakubwa wa SADC ndio maana tumedhamini maonesho haya na shughuli zingine za mikutano na tuko hapa kuonesha bidhaa  na huduma zetu kwa nchi wanachama," alisema Shirima.

Ameongeza hata katika uwekezaji unaofanywa na Serikali hasa katika ujenzi wa miundombinu wa kuwezesha usafirishaji wa malighafi na rasilimali za viwanda  umeiwezesha kampuni hiyo kuendelea kunufaika.

"Tumekuwa tukisambaza mafuta katika miradi ya ujenzi wa Reli ya Kisasa 
(SGR), Daraja la Salenda na tumejenga mfumo wa usafirishaji mafuta katika 
jengo la tatu la abiria Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,"amesema Shirima.
Rais Dk.John Magufuli akipata maelezo katika Banda la Kampuni ya Mafuta ya Puma Energy Tanzania akipata maelezo kutoka kwa Meneja Opereheni Lamecky Hiliyai kuhusu namna  ambavyo wanaonesha shughuli zao.Rais Magufuli ametumia nafasi hiyo kuwataka Puma kuendelea kuongeza gawio kwa Serikali ambapo maofisa wa Puma wamemhakikishia kutekeleza maagizo yake.Wa kwanza kushoto ni Meneja Sheria na Mahusiano wa kampuni hiyo Godluck Shirima.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimia na mmoja wa Wafanyakazi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma  EnerTanzania,alipotembelea banda hilo katika wiki ya maonesho ya Biashara kwa nchi za SADC yanayoendelea jijini Dar.

UJENZI WA BANDARI YA DAR ES SALAAM WAENDELEA VYEMA

$
0
0


Maendeleo ya ujenzi wa Bandari ya Dar es Salaam yanakwenda vizuri ambapo ujenzi wa magati 2 kati ya 7 yaliyopo umekamilika na kuanza kupokea meli kubwa za mizigo.


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Mhandisi Deusdedit Kakoko amesema mradi wa ujenzi wa magati hayo utakaogharimu takribani shilingi Trilioni moja utaiwezesha Bandari ya Dar es Salaam kuongeza ufanisi kwa kuongeza kasi ya upakuaji na upakiaji wa mizigo na kupokea meli yoyote duniani zikiwemo meli kubwa za kizazi cha saba (7th Generation).


Mhandisi Kakoko amefafanua kuwa kazi inayoendelea imewezesha kukamilika kwa ujenzi katika gati namba 1 na gati namba 2 ambazo zimeongezwa kina kutoka mita 8 hadi kufikia kati ya mita 15 na 19, kina ambacho ni kikubwa ikilinganishwa na kina kinahitajika kwa meli kubwa zaidi ambacho ni mita 12.


Aidha, Mhandisi Kakoko amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kutilia mkazo ujenzi wa Bandari ya Dar es Salaam na kuamua kujenga gati nyingine ya magari iitwayo RORO ambayo itaiwezesha bandari hiyo kupokea meli hata 2 kwa mpigo zenyewe uwezo wa kuchukua magari 10,000 ikilinganishwa na uwezo wa kuchukua magari 200 kabla ya mradi huo.


“Sasa maana yake nini, magari ni kati ya shehena inayoingiza tozo zaidi, kwa magari pekee yake tunaweza kukusanya tozo mara 2 au mara 3 ikilinganishwa na kipindi cha nyuma, ndio maana tunamshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kutuongezea hiyo gati ya RORO.


Kwa hiyo faida ya kwanza tunaipata katika kuongeza kina kwa maana meli kubwa zitaingia kwa mara moja, na kuna watu wamekuwa wakiona kuna Kijiji cha meli zinazosubiri kuingia bandari kushusha mizigo, hiyo haiwezi kuwepo tena” amesema Mhandisi Kakoko.


Mhandisi Kakoko amesema juhudi hizo zinakwenda sambamba na uboreshaji eneo la nyaraka (clearing) kupitia serikali mtandao ili kuondoa mianya ya udanganyifu ambao husababisha upotevu wa mapato.


“Sasa tutaweza kupata moja kwa moja Bill of Lading na hivyo kuondokana na baadhi ya wafanyabiashara au waagizaji mizigo ambao hudai makontena yana mitumba wakati ndani mna magari” amesema Mhandisi Kakoko na kubainisha kuwa uwekaji wa mfumo wa nyaraka unakwenda sambamba na uwekaji wa mitambo ya ukaguzi (scanner).


Amesema baada ya kukamilika kwa gati namba 1 na gati namba 2, ujenzi kwa sasa unaendelea katika gati namba 4 ambayo inakaribia kukabidhiwa TPA na gati namba 5 ambayo uchorongaji unaendelea.


Ameongeza kuwa baada ya kukamilika kwa ujenzi wa gati namba 3 na gati namba 4, ujenzi huo utaendelea kwa gati namba 5,6 na 7 na baada ya hapo kazi itaendelea kwa magati ambayo yapo chini ya Kampuni ya Kimataifa ya Huduma za Makontena Bandarini (TICTS) ambayo tayari Serikali ya Awamu ya Tano imeshafanya mazungumzo ya kurekebisha mkataba na sasa mrabaha unaolipwa ni mara 2 ikilinganishwa na zamani.


Mhandisi Kakoko amesema pamoja na kujenga gati hizo, Serikali pia inanunua mitambo mikubwa ya kupakulia na kupakia mizigo na hivyo kuongeza kasi na ufanisi zaidi wa bandari.


Kufuatia juhudi hizo amesema sasa bandari ya Dar es Salaam itakuwa na uwezo wa kutumia vizuri faida yake ya kijiografia kukabiliana na ushindani wa bandari zote zilizopo katika ukanda wa bandari ya Hindi na kuwa lango bora na muhimu kwa nchi za Afrika.


Mhandisi Kakoko amesema kazi hii ya uboreshaji wa Bandari a Dar es Salaam iliyopaswa kufanyika miaka 30 iliyopita imesababisha Tanzania kupoteza kiasi kikubwa cha mapato na kwamba kutokana na uboreshaji huu na hatua ambazo Serikali ya Awamu ya Tano imechukua, TPA itaendelea kuongoza katika utoaji wa gawio.


Ameahidi kuwa mwaka huu TPA inatarajia kutoa gawio la kati ya shilingi Bilioni 150 na shilingi Bilioni 200 na kwamba miaka michache ijayo TPA kwa kushirikiana na wadau wengine wa bandari watakuwa na uwezo wa kuzalisha fedha za kugharamia bajeti nzima ya Serikali ambayo ni takribani shilingi Trilioni 30 kwa mwaka.


Halikadhalika Mhandisi Kakoko amesema kazi ya ujenzi wa bandari pia inaendelea katika Bandari ya Mtwara na ujenzi katika Bandari ya Tanga utaanza mwezi huu (Agosti 2019)

WAZIRI MKUU AISHUKURU TIGO KWA KUWA MDHAMINI RASMI WA INTANETI KATIKA MKUTANO WA 39 WA SADC

$
0
0
Waziri Mkuu ameishukuru Tigo kwa kuwa mdhamini rasmi wa intaneti itakayotumiwa na wageni wanaohudhuria mkutano wa 39 wa jumuiya ya maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC. 

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametembelea banda la Tigo na kuwapongeza kwa kuwa wadhamini rasmi wa intaneti itakayotumika kwenye mkutano wa 39 wa jumuiya ya maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC ) unaondelea jijini Dar es Salaam, katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere. Tigo ndio kampuni ya mawasiliano pekee yenye mtandao wa kasi wa 4G+.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikaribishwa na Mkuu wa Mauzo – Tigo Business, Kadambara Maita  katika banda la Tigo, lililopo katika mkutano wa 39 wa jumuiya ya maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC unaondelea jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere.
Wafanyakazi wa Tigo wakimkaribisha Waziri Mkuu wa Tanzania, Mh.Kassim Majaliwa, katika banda la Tigo, lililopo katika mkutano wa 39 wa jumuiya ya maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC unaondelea jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere.

TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa) YANG’ARISHA USIKU WA SADC

$
0
0
Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kutoa burudani kwa wageni mbalimbali walioalikwa katika chakula cha jioni. Hafla iliyoandaliwa kwa ajili ya ukaribisho wa wageni wa Mkutano wa SADC hususan wa wale wa Wizara ya Viawanda na Biashara.
Mgeni Rasmi katika hafla hio alikua Mheshimiwa Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kikitoa burudani kwa wageni katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City. Ngoma hii inaitwa Druming Ensemble ambayo ni mchanganyo wa upigaji wa ngoma mbalimbali za kitanzania kwa kundi.

Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar Balozi Amina Salum Ali (aliyevaa miwani) alikua mmoja wa wageni waliohudhururia hafla hio na kuonyesha kufurahia uchezaji wa ngoma uliyofanywa na kikundi cha ngoma kutoka TaSUBa.
Waimbaji wa Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) wakiimba kwa kupokezana katika ngoma ya Nsimba ambayo inabebwa na uimbaji wa majibishano. 
Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kikicheza kwa madaha ngoma ya Nsimba ambayo huchezwa kwa kutumia ala ya vyungu ambayo asili yake huchezwa na wanawake wa kabila la kifipa. 
Viewing all 110135 articles
Browse latest View live




Latest Images