Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110129 articles
Browse latest View live

WANANCHI SINGIDA WAMBEBA MBUNGE WASUKUMA GARI LAKE

$
0
0
Wananchi wa Kitongoji cha Kaugeri Kata ya Mwaru katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida wakimlaki Mbunge wao Elibariki Kingu baada ya kuwasili kwa ajili ya kufanya mikutano ya hadhara kwenye kata hiyo jana. 
Wananchi wa Kitongoji cha Kaugeri Kata ya Mwaru wakiwa wamembeba mbunge wao. 
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu akipata maelezo kutoka kwa Diwani wa Kata ya Mwaru, Iddi Makangale alipo kuwa akikagua ujenzi wa Zahanati ya Kitongoji cha Mlandala.
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu akizunfumza na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mlandala.
Diwani wa Kata ya Mwaru, Iddi Makangale akizungumza na Wananchi wa kitongoji cha Mlandala katika mkutano wa mbunge huyo.
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu akiwahutubia Wananchi wa kitongoji cha Mlandala
Mkutano ukiendelea kitongoji cha Mlandala.
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu akiwa katika picha na viongozi pamoja na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kaugeri baada ya kukagua ujenzi wa shule hiyo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kaugeri wakitoa burudani kwenye mkutano huo.





Na Dotto Mwaibale, Singida

WANANCHI wa Kitongoji cha Kaugeri Kata ya Mwaru katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida wameshindwa kujizuia furaha yao na kujikuta wakimbeba na kusukuma gari la Mbunge wao Elibariki Kingu kutokana na jitihada zake za kuwapelekea miradi ya maendeleo.

Wakiongea kwa nyakati tofauti jana kwenye mikutano ya hadhara aliyoandaa mbunge huyo katika vitongoji vya Kaugeri na Mlandala walisema haijawahi kutokea tangu vianzishwe vijiji hivyo kwa kupata maendeleo makubwa katika kipindi cha miaka minne tangu mbunge huyo aingie madarakani.

Akizungumza katika mkutano huo mmoja wa wananchi wa kitongoji cha Kaugeri aliyejitambulisha kwa jina moja la Maganga alisema haijawahi tokea mbunge wa mfano kama Kingu.

" Mbunge huyu hana wa kumlinganisha naye amejitahidi sana kutuletea maendeleo katika Kata yetu yenye vitongoji vitano vya Kaugeri, Mdughuyu, Mlandala, Mpugizi na Mwaru.

Alisema katika vitongoji hivyo ameweza kujenga shule, zahanati na sasa amewaletea mradi mkubwa wa maji ambao utasambaza maji kwenye vitongoji vyote vya kata hiyo.

Diwani wa Kata hiyo Iddi Makangale alisema tangu miaka 50 iliyopita hakujawahi kutokea Mbunge kama Kingu kwani kazi iliyofanywa na Rais John Magufuli na Mbunge huyo kwa kushirikiana na wananchi imewarahisishia upatikanaji wa kupata kura nyingi katika uchaguzi mkuu kwa chama chao cha Mapinduzi (CCM).

" Kwa kazi hii kubwa iliyofanyika hatuna wasiwasi CCM itapata ushindi mnono ambao haujawahi kupatikana katika uchaguzi wowote tuliowahi kuufanya" alisema Makangale.

Akizungumza katika mkutano huo Kingu aliwashukuru wananchi hao na kuwaambia maendeleo hayo wanayapata baada ya Rais John Magufuli kuwabana mafisadi na matumizi mabaya ya fedha na kuzielekeza kwa wananchi wanyonge kwa kuwapelekea miradi ya maendeleo.

Alisema haijawahi kutokea kwa kipindi chote kilicho pita katika jimbo hilo kufanyika kwa miradi mingi kiasi hicho ikiwemo miradi mikubwa ya maji 22 huku mchakato wa kupata umeme wa REA ukiendelea.


Kingu aliwataka wananchi wa kata hiyo kuacha majungu badala yake wafanye kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo.Katika hatua nyingine Kingu anatarajia kuitisha mkutano mkubwa wenye lengo la upigaji kura ya kuwabaini wahalifu wa mauaji ya watu katika Kata ya Mwaru kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Waziri Mkuu atembelea shamba la katani la Hassan Sisal Estate Makanya.

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa ameshika jani la katani, wakati alipotembelea shamba la katani la Hassan Sisal Estate Makanya, wilayani Same katika mkoa Kilimanjaro Julai 19.2019. Anayetoa maelezo ni Meneja Mshauri wa shamba hilo, Ndekirwa Nyari.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa ameshika katani iliyokua imeanikwa, wakati alipotembelea shamba la katani la Hassan Sisal Estate Makanya, wilayani Same katika mkoa Kilimanjaro Julai 19.2019. Anayetoa maelezo ni Meneja Mshauri wa shamba hilo, Ndekirwa Nyari.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa anakagua marobota ya katani, wakati alipotembelea shamba la katani la Hassan Sisal Estate Makanya, wilayani Same katika mkoa Kilimanjaro Julai 19.2019. Kushoto ni Meneja Mshauri wa shamba hilo, Ndekirwa Nyari.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na wafanyakazi wa shamba la katani la Hassan Sisal Estate Makanya pamoja na wananchi, wakati alipotembelea shamba hilo, wilayani Same Julai 19.2019.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akimsikiliza Meneja Mshauri wa shamba wa shamba la katani la Hassan Sisal Estate Makanya, Ndekirwa Nyari pamoja, baada ya kutembelea shamba hilo, wilayani Same Julai 19.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

WAZIRI MKUU AAGIZA SAME SEKONDARI IPEWE GARI

$
0
0
DED aahidi kuliwasilisha kesho kutwa jioni 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Bi. Anna-Clare Shija apeleke gari haraka katika shule ya sekondari ya wavulana ya bweni ya Same ili kumsaidia mwalimu mkuu endapo kutatokea dharura. 

“Shule hii ina wanafunzi zaidi ya 800 lazima iwe na chombo cha usafiri kitakachotumika kwa dharura za kuwapeleka hospitali wanafunzi pale wanapougua. Sasa hivi mwanafuzi akiugua, Mwalimu Mkuu anafanyaje? Ni kama ameachiwa jukumu hili peke yake,” alisema Waziri Mkuu. 

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana (Ijumaa, Julai 19, 2019) wakati alipotembelea shule hiyo na kuzindua mradi wa ukarabati wa shule kongwe ya sekondari ya Same na kisha kuzungumza na wanafunzi, walimu na baadhi ya wazazi waliokuwepo. 

Waziri Mkuu alimwita Mkurugenzi wa wilaya hiyo, Bi. Shija na kumtaka atoe jibu hadharani kwamba ni lini atapeleka gari hilo shuleni hapo. Mkurugenzi huyo aliahidi kulipeleka gari hilo ifikapo Jumatatu jioni (Julai 22, 2019). 

“Haya maelekezo ni kwa wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini wenye shule ambazo zina wanafunzi zaidi ya 700. Mnapaswa kuhakikisha kunakuwa na gari la shule ili ikitokea dharura, Mkuu wa Shule aweze kuingilia kati na kupata ufumbuzi.” 

“Wakurugenzi mnatakiwa kutambua shule hizi ni zenu, kwa hiyo mnalo jukumu la kuzihudumia. Shule hii ya Same ina wanafunzi zaidi ya 800 na wanalala hapa hapa, ni lazima kuwe na gari la kuwahudumia hasa wakati wa dharura.” 

Pia amemuagiza Mkurugenzi huyo atafute daktari na muuguzi mmoja na awapangie kwenye shule hiyo ili waweze kutoka huduma kwa wanafunzi na kuwapunguzia adha ya kwenda mjini kutafuta huduma hiyo. 

Waziri Mkuu alifikia uamuzi huo baada ya kupokea changamoto zilizowasilishwa na kijana Omary Said wa kidato cha sita mchepuo wa PCB ambaye alisema shule hiyo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji; uchakavu wa mabweni; ukosefu wa zahanati ya shule na uhaba wa walimu wa sayansi hasa wa masomo ya fizikia. 

Mapema, akitoa taarifa ya ukarabati, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Bw. Hoza Mgonja alisema ukarabati huo ambao umegharimu sh. milioni 919, ulifanikisha ukarabati wa majengo saba ya madarasa yenye vyumba 22; maabara tatu, vyoo viwili vyenye matundu tisa; jengo moja la walimu; maktaba yenye vyumba viwili na ofisi mbili; vyoo viwili vyenye matundu manne na miundombinu ya umeme na majitaka. 

Waziri Mkuu leo anaendelea na ziara yake mkoani Kilimanjaro kwa kutembelea wilaya ya Mwanga ambako atazungumza na watumishi na kisha ataenda kijiji cha Kirya, Nyumba ya Mungu kukagua mradi wa maji wa Same - Mwanga - Korogwe. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na wafanyakazi wa shamba la katani la Hassan Sisal Estate Makanya pamoja na wananchi, wakati alipotembelea shamba hilo, wilayani Same Julai 19.2019.

UVCCM Bahi waapa CCM kuibuka na ushindi uchaguzi wa Serikali za Mitaa

$
0
0
Na Charles James

Umoja wa vijana wa Chama cha mapinduzi [UVCCM] Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma umesema kuwa chama hicho kitashinda kwa kishindo kwa asilimia mia moja kwenye mitaa yote ya wilaya hiyo katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa .

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Bahi, Kadoke Hassan wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Wilayani humo.

Kadoke amebainisha misingi madhubuti itakayokipaisha chama hicho ni kutokana na Uongozi mzuri na Maridadi wa Rais Dk John Pombe Magufuli ikiwa ni pamoja na ununuzi wa ndege, mradi wa bomba la kusafirishia Mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga Tanzania pamoja na Mradi wa reli ya kisasa.

Mwenyekiti huyo wa UVCCM amehamasisha vijana wote kushikamana na kujitokeza katika ushiriki wa serikali za mitaa na wasisite kuyatangaza Mazuri yanayofanywa na Rais Magufuli.

Aidha ,UVCCM wilaya ya Bahi umechukua fursa ya kumpongeza Mathias Lyamunda aliyekuwa Mgombea wa Ubunge mwaka 2015 kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kwa uamuzi wake wa kujiuzulu nafasi zake ndani ya Chama hicho na kuhamia CCM ili kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Magufuli na Serikali ya CCM katika kuwaletea maendeleo Watanzania.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Bahi, Kadoke Hassaan akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akizungumzia uchaguzi wa Serikali za Mitaa na namna walivyojipanga kuhakikisha wanashinda mitaa yote.

Mkurugenzi Jiji la Dodoma atunukiwa cheti na Shirika la Machinga Nchini

$
0
0
Na Charles James

SHIRIKA la umoja wa Machinga Tanzania limetakiwa kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Mafuguli kutaka Machinga wafanye shughuli zao pasipo kusumbuliwa na mamlaka nyingine.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alipokuwa akiongea na kamati tendaji ya Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania walipomtembelea ofisini kwake kumkabidhi cheti cha shukrani leo.

Kunambi alisema “ndugu zangu, tunawajibu wa kumsaidia mhe Rais kama wadau. Mhe Rais amefanya jitihada kubwa katika kuhakikisha machinga wa nchi hii wanafanya shughuli zao katika mazingira mazuri. Tumeona utaratibu wake wa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo. Vitambulisho hivi vimekuwa msaada mkubwa kwa wafanyabiashara wadogo” alisema Kunambi.

Katika kuhakikisha Machinga wanafanya kazi zao vizuri, Mkurugenzi huyo alisema kuwa Jiji la Dodoma linataka kufanya Machinga wa kisasa. Machinga wanaofanya kazi zao vizuri kwa kuzingatia taratibu.

Aidha, aliwataka kufanya shughuli zao na kukua kimtaji. “Lazima tuwe na mpango wa kufanya mabadiliko kutoka Machinga kwenda kuwa wafanyabiashara. Hata Mbuyu ulianza kama mchicha” alisema Kunambi.

Nae mwenyekiti wa Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania, Ernest Masanja alisema kuwa umoja huo umeamua kumpatia cheti hicho kumshukuru Mkurugeni wa Jiji la Dodoma kutokana na ushirikiano ambao amekuwa akiutoa kwa Machinga katika kutekeleza majukumu yao. Jiji la Dodoma ni miongoni mwa Halmashauri ambazo zimemaliza kuuza vitambulisho vyote walivyopewa kwa ajili ya kuwauzia wafanyabiashara wadogo. Vitambulisho 15,173 vya wajasiliamali vimeshauzwa kwa wafanyabiashara kwa bei ya shilingi 20,000 kwa kila kimoja.

Rais John Magufuli aliamua kutoa vitambulisho na kuagiza mamlaka zinazohusika kuwa vitambulisho hivyo ni maalumu kwa wafanyabiashara ambao mtaji wao hauzidi Shilingi milioni nne (4) ili viwasaidie kuzitambulisha biashara zao.

Aidha, aliagiza kuwa wafanyabiashara watakaogawiwa vitambulisho hivyo wasisumbuliwe na mtu yeyote wakati wa kufanya shughuli zao. Lengo ni kuwafanya wafanyabiashara wadogo kutambuliwa rasmi na kutobughudhiwa wanapofanya biashara zao za halali.
 Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania (SHIUMA) walipomtembelea ofisini kwake n kumkabidhi Cheti cha Shukrani kwa kutambua mchango wake kwa machinga
Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi akizungumza na viongozi wa Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania walipomtembelea Ofisini kwake ambapo pia walimpatia cheti cha shukrani kwa mchango wake kwa Machinga

TADB WATAMBULISHA MFUMO JUMUISHI KAGERA, SASA MALIPO YA MKULIMA KURAHISISHWA.

$
0
0
Anaandika Abdullatif Yunus Michuzi TV. Kagera.

Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) inazidi kuweka mazingira mazuri ya kuhakikisha Mkulima hasa Mkulima wa zao la Kahawa Mkoani Kagera, ananufaika na Kilimo cha zao hilo ambapo Benki hiyo kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wametambulisha rasmi mfumo jumuishi utakaomsaidia Mkulima wa zao la Kahawa kupata huduma za kifedha.

Mfumo huu ni shirikishi kupitia Vyama vya ushirika (AMCOS) ambavyo vyama hivi vinamtambua Mkulima wa eneo husika, ukiwa na lengo la kuwawezesha wadau kumfikia mkulima kwa urahisi ili kumsogezea huduma mbalimbali za kifedha ikiwemo bei ya mazao, bima za afya na mikopo ya pembejeo kirahisi.

Mfumo Jumuishi unaowashirikisha wadau wa wa sekta ya fedha na mawasiliano zikiwemo Benki, mitandao ya Simu, Mfuko wa Bima, Wizara ya fedha, na wengineo, utamsaidia Mkulima katika kuhakikisha anapata Soko la uhakika, kujua bei ya soko, kuwa na mfumo wa kupata bei nzuri ya mazao, kulipwa fedha take yote kwa wakati na urahisi, kujikimu kimaisha na kiafya yeye na familia yake, kuwa mwekezaji kwenye Tanzania ya Viwanda, kuwa na fursa nyingi za kuwekeza kwa baadae na pia kumhakikishia Mkulima usalama wa fedha zake.

Mfumo jumuishi ni mpango wa wadau chini ya Benki ya Kilimo, kumuendea Mkulima kwa pamoja ambapo awali kila mdau alikuwa akimfuata Mkulima kwa njia zake, lakini lengo kubwa ni kumuondolea Mkulima Usumbufu na kuwa Tegemezi.

Tayari Mfumo jumuishi umeanzishwa na kufanikiwa katika zao la Korosho kwa Mikoa ya Kusini, Lindi Mtwara na Ruvuma, na sasa unatambulishwa rasmi kwa Mikoa ya Kanda ya ziwa kwa Kuanzia Kagera.
 Bwana Kazilahabi Jumanne Kaimu Meneja Benki ya maendeleo ya  Kilimo Kanda ya Ziwa akizungumza na vyombo vya habari juu ya Kampeni ya  mfumo Jumuishi iliyoanza Rasmi Mkoani Kagera.
 Pichani Kahawa iliyokobolewa baada ya kukusanywa na Vyama vya Msingi huko Wilayani, huletwa KCU kwa ajili ya hatua nyingine.
Pichani ni Ndg Kazilahabi Jumanne Kaimu Meneja Benki ya Wakulima Kanda ya Ziwa, akikagua Kahawa Iliyokobolewa tayari kwa hatua nyingine, kama alivyokutwa na Kamera yetu Ofisi za Chama kikuu cha Ushirika KCU 1990 ltd.

MJUKUU ATUHUMIWA KUMUUA BIBI YAKE BAADA YA KUMCHINJA KWA KUTENGANISHA SHINGO NA KIWILIWILI

$
0
0
Na, Editha Edward-Tabora 

KIJANA Athuman Khamis ambaye ni Mkazi wa Kijiji cha Usongwa katika Kata ya Bukene wilayani Nzega mkoani Tabora anatuhumiwa kumuua kwa kumchinja bibi yake Rahel Daud(67)mkazi wa kijiji hicho huku Sababu ikielezwa ni uvutaji wa bangi kwa kijana huyo

Tukio hilo la kikatili limetokea jana saa 12 jioni katika kijiji cha Usongwa kata ya Bukene wilayani Nzega Mjini 

Mkuu wa Wilaya ya Nzega Godfrey Ngupulla amesema kwa upelelezi aliofanya hadi chanzo cha mauaji hayo ni kuwa uliotokea ugomvi mdogo wa kurushiana maneno kwa bibi huyo na kijana huyo na ndipo alipomvizia ndani na kumchinja kwa kumtenganisha kiwiliwili na shingo

Esther Salum ambaye ni ndugu wa Rahel Daud ameiambia Michuzi Blog kuwa kitendo hicho alichofanyiwa ndugu yake si kizuri, hivyo anaiomba Serikali kumtafuta kijana aliyefanya kitendo hicho ili afikishwe kwenye sheria.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya Nzega George Mgarega amesema kuwa mwili huo ulivyofikishwa hospitalini hapo ulifanyiwa uchunguzi na kuonekana ulikuwa na majeraha ya kukatwa na kitu chenye ncha kali kwa kuanzia nyuma na kwenda mbele hivyo kusababisha kuvuja kwa damu nyingi na maumivu makali na hivyo kupoteza maisha.

Wakati huo huo Jeshi la Polisi wilayani Nzega linaendelea kufanya uchunguzi wa kumtafuta kijana huyo aliyefanya mauaji hayo.
 Pichani ni Ndugu wa Marehemu Esther Salum akielezea kitendo hicho.
 Pichani ni Mwili wa Marehemu Rahel Daud aliyepoteza maisha kwa kuchinjwa na kijana Athuman Khamis Wilayani Nzega.
 Mganga  Mfawidhi Hospitali ya Wilaya  Nzega,George Mgarega  akielezea baada ya kufanyiwa uchunguzi Mwili wa Marehemu.
Mkuu wa Wilaya ya Nzega,Mh.Godfrey Ngupulla  akielezea jinsi tukio la Mauaji hayo  lilivyotokea.

MAMENEJA UNGANISHENI WATEJA KWA SH 27,000 VIJIJI

$
0
0


Moja ya nyumba zilizowashwa umeme na Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu katika kijiji cha Mkindo Wilayani Kaliua mkoani Tabora.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu( mwenye kilemba) alizungumza na vijana wanaofanya kazi ya useremala kwa kutumia umeme wa jua katika kijiji cha Mgambo wilayani Sikonge, Naibu Waziri alifika kijijini hapo kutembelea kampuni ya uwekezaji inayozalisha umeme jua na kuwauzia wananchi.
Wakazi wa kijiji cha Wema mwenye ulemvu wakikabidhiwa kifaa cha umeme tayari ( UMETA) kutoka kwa Naibu Waziri wa Nishati , Subira Mgalu, aliyekuwa katika ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini wilayani Sikonge, mkoani Tabora.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu( katikati) akipata maeneo ya namna ya mtambo wa kuzalisha umeme jua unavyofanya kazi katika kijiji cha Mgambo, Mkola na Mwenge wilayani Sikonge mkoani Tabora.
Naibu Waziri Subira Mgalu( mwenye kilemba) na viongozi wengine wakikata utepe kuashirika kuwasha umeme katika moja ya taasisi za dini katika kijiji cha Mkindo wilayani Kaliua, mkoani Tabora.

Ujenzi ukiendelea katika kituo cha kupokea na kupoza umeme katika kijiji cha Uhuru, wilayani Urambo mkoani Tabora.
…………………..
Na Zuena Msuya, Tabora

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amesema mameneja wa Shirika la Umeme nchini, (Tanesco) waongeze idadi ya wateja kwa kuwaunganishia huduma ya umeme wananchi waliopo vijijini kwa bei ya shilingi 27,000.
Hatua hiyo ni kigezo cha kupima utendaji kazi wa mameneja hayo katika Kanda,Mikoa pamoja na Wilaya mbalimbali nchini.

Mgalu alisema hayo kwa nyakati tofauti, wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa mradi wa usambazaji wa Umeme Vijijini,( REA) katika Wilaya za Ulyankhulu, Kaliua, Urambo pamoja na Sikonge Mkoani Tabora, Julai 18,2019.

Katika Wilaya hizo, Mgalu aliwasha Umeme katika makazi ya watu, Nyumba za ibada,taasisi za umma, visima vya maji pamoja na kuzungumza na wananchi wa eneo hayo.Akiwa katika wilaya hizo, Mgalu aliwasha umeme katika kijiji cha Limbula na Kasunga wilayani ni Kaliua, vilevile katika kijiji cha Mfindo wilayani Ulyankhulu.

Aidha akiwa katika wilaya Urambo aliwasha umeme katika kijiji cha Wema, pia aliwsha umeme katika kijiji Kikungu wilayani Sikonge na kuzungumza na wananchi.Alisema Mameneja wa maeneo husika ndiyo wenye dhamana kubwa ya kuwafuata wateja katika makazi na kuwashawishi kuunganishwa na Umeme badala ya kukaa Ofisini na kusubiri wateja.

“Mradi wa REA umekwisha viunganisha na kuwasha umeme katika vijiji vingi vya Wilaya mbalimbali, naawaagiza mameneja kufanya kazi ya kuwafuata wananchi huko walipo mkawape elimu ili muwaunganishe na Umeme, kwa bei ya shilingi 27,000, tunataka kuona idadi ya watumiaji Umeme inaongezeka”, Alisema Mgalu.

Tangu mradi wa REA umeanza tayari zaidi ya wateja laki tisa(900,000) wameungamishwa na umeme na bado zoezi hilo linaendelea.

Katika ziara yake hiyo, Mgalu alikagua ujenzi wa kituo cha kupokea na kuponza umeme kilichopo katika kijiji cha Uhuru wilayani Urambo ambapo pamoja na mambo mengine alisema kuwa ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa kituo hicho inayoendelea.

Sambamba na hilo, alikagua eneo ambalo litajengwa kituo kingine cha kupokea na kupoza umeme katika kijiji cha Ipole wilayani Sikonge, ambacho kinatarajia kuanza kujengwa hivi karibuni.

Vituo hivyo vinajengwa mahsusi kwa lengo la kuimarisha upatikani wa umeme mwing na wakutosha katika Mikoa ya Tabora, Kigoma na pamoja na Katavi,pia mikoa hiyo nayo iunganishwe na gridi ya taifa, na kuacha kutumia umeme unaotokana na mafuta mazito.

Katika hatua nyingine alitembelea kagua kampuni ya Power Corner katika kijiji cha mgambo wilayani Sikonge, inayofanya kazi ya kuzalisha umeme kwa kutumia nguvu ya jua na kuwauzia wakazi wa kijiji cha Mgambo, Mwenge pamoja na Mkola.

Kituo hicho kilipata zabuni ya zaidi ya shilingi milioni 500 kutoka kwa Wakala wa Nishati Vijiji (REA) kwa lengo la kuchangia utekelezaji wa kituo hicho ikiwa ni kutekeleza azma ya serikali kuwainua wazalishaji wadogo wa umeme.

Naibu waziri aliwaagiza watendaji wa kituo hicho kutoa huduma bora zinazoendana na ghara wanazolipia wananchi ili mradi huo uwanufaishe wananchi na si kuwakandamiza.

NAIBU WAZIRI AWATOA HOFU WAKULIMA WA PAMBA MWANZA

$
0
0


Naibu Waziri wa Kilimo,akizungumza na wakulima wa pamba juzi wilayani Kwimba.Kulia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Salum Kalli na kushoto ni Mbunge wa Kwimba Shanif Mansoor.
……………………
NA BALTAZAR MASHAKA, KWIMBA
SERIKALI imewatoa hofu wakulima wa zao la pamba na kuwataka wasirubuniwe na walaghai, wapeleke pamba yao sokoni kwani fedha zipo, watalipwa na hakuna mkulima atadhulumiwa.

Pia imewahakikishia wanunuzi wa pamba kuwa hawatapata hasara baada ya serikali kuridhia kutoa ruzuku ya kuwafidia endapo bei ya pamba haitapanda kwenye soko la dunia ifikapo Agosti 15, mwaka huu.

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu wa Waziri wa Kilimo Omari Mkumba alipozungumza na wakulima wa vijiji vya wilaya za Magu na Kwimba na baadhi ya wanunuzi wa pamba kwenye wilaya hizo juzi kwa nyakati tofauti.

Mkumba ambaye aliambatana na Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Salum Kalli alisema kutokana na mdodoro wa bei ya pamba kwenye soko la dunia, msimamo wa serikali wakulima wauze pamba yao kwa bei dira ya sh. 1,200 kwa kilo na si vinginevyo.

Alisema imekubaliana na wanunuzi wanunue kwa bei hiyo na waichambue na kuihifadhi kisha waiuze kwa bei ya itakayokuwa sokoni lakini ikifika Agosti 15 mwaka huu, haijapanda wauze pamba yao na endapo wataiuza pungufu ya senti 69.4 USD serikali itawafidia.

“Licha ya wanunuzi kusuasua kutokana na mdororo wa bei na fedha zilizopo kutokidhi mahitaji ya mzigo uliopo sokoni, msirubiniwe kuwa pamba haina soko la hasha.Kilo ni sh. 1,200 na tunataka wakulima wapate tija kwa sababu wanatumia nguvu nyingi kulima pamba hadi wavune,”alisema Mkumba.Alieleza kuwa awali wanunuzi walisita kununua pamba kutokana na changamoto ya bei kubwa kulingana na mikataba waliyoingia na wanunuzi wakubwa hivyo waliona wanapata hasara.

Naibu waziri huyo alisema malalamiko ya wakulima kuwa hakuna fedha baada ya kuuza pamba yao yalitokana na benki kugoma kuwakopesha wanunuzi zikihofia kuzamisha fedha za watanzania, lakini serikali ilipoingilia kati zimeamua kuwakopesha wafanyabiashara ili waingie sokoni.

“Wanunuzi walikuwa hawana uhakika wa biashara na mitaji yao.Sasa serikali imebeba dhamana hiyo na yote hayo ni kumjali mkulima.Hivyo wakulima mnapaswa kumuunga mkono Rais John Magufuli kwa kuchapa kazi kwa ajili ya maendeleo ambayo hayaji bila kufanya kazi,”alisema Mkumba.

Pia aliwasisitiza wakulimakulipa madeni ya pembejeo ili mwakani waondokane na uhaba wa viaududu na mbegu ili walime kwa tija zaidi na kujiongezea kipato na kubadilisha maisha yao kiuchumi.Aidha, Katibu wa CCM, Kalli alisema Rais Magufuli analala na kuamka na shida za wananchi na kuwataka wakulima wasikubali kubabaishwa na kurubuniwa na wadanganyifu kwani serikali imewadhamini wanunuzi wa pamba licha ya bei kushuka kwenye soko.

“Wapo wapo vishoka waliingia kuwatisha wakulima kuwa pamba Mwanza ni siasa ili wauze kwa bei chee, lakini serikali imeingilia jambo hili kuwanusuru wakulima kwa kulipa fidia endapo watauza pamba kwenye soko chini ya senti Dola 68.Tuwatie shime wanunuzi wapate idea ya serikali waingie sokoni,”alisema Kalli.

Naye Mbunge wa Kwimba Shanif Mansoor alisema serikali kutoa ni faraja kwa wakulima baada ya serikali kutoa ruzuku kwenye pamba kwani kwa mara ya kwanza hiyo ni historia na ni vizuri wakulima wakaelezwa ili wanununuzi wasiwaonee.

“Nimefarijika kuona Serikali ya Rais John Magufuli ikitoa ruzuku kwenye pamba, wanunuzi watapata fidia na hakuna hasara na nadhani wataingia sokoni baada ya benki kukubali kutoa fedha.Lakini wanunuzi nao watoe bei halali,”alisema Mbunge huyo wa Kwimba

WAZIRI MKUU APOKEA TRENI YA MIZIGO NA KUZINDUA SAFARI ZA TRENI ZA MIZIGO KATIKA RELI YA KASKAZINI

$
0
0
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akipokea treni ya mizigo, iliyowasili tokea Tanga, kwenye uzinduzi wa treni hiyo katika reli ya Kaskazini Julai 20.2019.

 Wananchi wa Moshi, wakipokea treni ya mizigo kwa furaha kubwa, wakati ikiwasili tokea TangaJulai 20.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akikata utepe kuzindua treni ya mizigo katika reli ya Kaskazini Julai 20.2019. Uzinduzi huo umefanyika katika stesheni ya reli Moshi. 
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwapungia mikono wananchi waliyofika kushuhudia uzinduzi wa treni ya mizigo katika reli ya Kaskazini uliyofanyika katika stesheni ya reli Moshi, Julai 20.2019. 
 Wananchi wa Moshi, wakishangilia kwa furaha kubwa  baada ya kupokea treni ya mizigo katika reli ya Kaskazini, wakati ikiwasili tokea TangaJulai 20.2019

NIMERIDHISHWA NA MRADI WA MAJI WA CHANGANYIKENI- MZEE MKONGEA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv
Mbio za Mwenge Kitaifa 2019 zimeridhishwa na mradi wa usambazaji maji wa Makongo-Changanyikeni wenye thamani ya Bilion 75 unaosimamiwa na Mamlaka ya Maji safi na Majitaka Dar es Salaam DAWASA.

Hayo yamesemwa na Kiongozi wa Mwenge Mzee Mkongea Ali baada ya kutembelea kituo cha Usambazaji maji (booster Pump) na tenki la kuhifadhia maji.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa na kutembelea maeneo hayo, Mzee Mkongea amesema hizi ni jitihada za Rais John Pombe Magufuli za kuhakikisha wananchi wote wanapata maji ya uhakika.

"Jitihada zinazofanywa na Rais wetu ni kubwa, tuna mahusiano mazuri na Wenzetu wa India na tumeona katika ripoti fedha walizotupatia kwa ajili ya mradi huu imeondolewa kodi na hilo ni jambo jema kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi," Mkongea.

Amesema, "tulikuwa tukiona kwenye vyombo vya habari kuhusu mradi huu mkubwa na tulipofika na kupitia ripoti tumeona tenki la maji tukaamua kwenda kuliona niwapongeze DAWASA kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kusimamia miradi hii,"

Amempongeza pia Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Daniel Chongolo kwa kuweza kusimamia miradi hii mikubwa ya maji ndani ya Wilaya yake.

Kwa upande wa DAWASA, Afisa Mtendaji Mkuu Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema mradi huu umekamilika kwa asilimia 76 na umebakia kwenye hatua za mwisho.

Luhemeja amesema kukamilika kwa mradi huo kutanufaisha Manispaa za Kinondoni na Ubungo na Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo ukiwa unahusisha matenki matano yenye ujazo wa Lita Milioni 6.

Mbizo za mwenge mwaka huu zitetembelea miradi mbalimbali ya Maji ya Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani na kuizindua ikiwa tayari wameshaweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa tanki la maji la Pugu la ujazo wa Lita milion 2 na mradi wa Makongo-Changanyike.
 Kiongozi wa Mbio za Mwenge 2019 Mzee Mkongea Ali akiweka jiwe ka Msingi kwenye mradi wa usambazaji maji wa Makongo-Changanyikeni walipotembelea leo Jijini Dar es salaam.
 Kiongozi wa Mbio za Mwenge 2019 Mzee Mkongea Ali akizungumza baada ya kutembelea mradi wa usambazaji maji wa Makongo- Changanyikeni na kuridhishwa na mradi huo ulipofikia na kuwapongeza DAWASA kwa kuweza kusimamia mpaka hapo ulipofikia. Mwenge huo utatembelea miradi mbalimbali inayosimamiwana mamlaka hiyo.
 Afisa Mtendaji Mkuu ww DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja akielezea ramani ya mradi wa usambazaji maji wa Makongo-Changanyikeni wenye thamani ya bilioni 75 utakaohudumia wakazi wa Wilaya ya Kinondoni, Ubungo na Mji wa Bagamoyo.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Daniel Chongolo akiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja wakisikiliza jambo kutoka kwa Kaimu Meneja miradi wa Maji Ramadhani Mtindasi wakati wa Mbio za Mwenge zilipotembelea mradi wa usambazaji maji Makongo Changanyikeni.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja akitoa maelezo kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge 2019 Mzee Mkongea Ali alipotembelea tanki la maji lamradi wa usambazaji maji wa Makongo-Changanyikeni walipotembelea leo Jijini Dar es salaam

MUONGO UMETIMIA TOKA KIFO MICHAEL JACKSON

$
0
0
Na: Moshy Kiyungi,Tabora.

Mwaka huu 2019 imetimia miaka kumi tangu Michael Jackson alipoiaga dunia, Juni 25, 2009 nchini Marekani.

Alikuwa msanii mwenye vipaji vingi, aliyefahamika zaidi kwa jina bandia la kiheshima la ‘Mfalme wa Pop’Michael alipata mafanikio makubwa kwa muda wote pia alikuwa mmoja kati ya waburudishaji wenye mvuto na athira kubwa katika medani ya muziki.Michango yake katika muziki, fasheni, na hasa suala la kuanika hadharani maisha yake binafsi, vilimfanya awe kioo cha ulimwengu katika tamaduni maarufu kwa ziaidi ya miongo minne.

Wasifu wa Michael Jackson unaonesha kuwa alizaliwa Agosti 29, 1958 huko Gary, Indiana, nchini Marekani.Alitokea katika familia ya wanamuziki ya Jackson Five.

Michael Jackson alifariki mnamo Juni 25, 2009 katika hospitali ya UCLA Medical Center, nchini Marekani, alokokuwa amelazwa.Wakati wa uhai wake aliwahi kusimulia kuhusu miaka yake ya awali, mara kadhaa ilisema kuwa baba yake alimlazimisha kufanya mazoezi mno ya kucheza na uimbaji.

Michael akiwa pamoja na ndugu zake, alipewa uongozi wa uimbaji kwa mara ya kwanza akiwa mwanachama mdogo katika kundi la The Jackson 5 mnamo mwaka wa 1964.

Alianza kazi ya usanii wa kujitegemea kunako mwaka wa 1971, ambapo allbamu yake ya mwaka 1982 iliyopewa jina la ‘Thriller’, imebaki kuwa ni yenye mauzo bora kwa muda wote.Mchango wa Michael Jackson katika utengenezaji wa muziki wa video, ulimuinua kutoka katika hali ya kawaida hadi katika hali ya kisanii zaidi.

Video zake za Billie Jean, Beat It na Thriller zilimfanya kuwa msanii Mmarekani mweusi wa kwanza kupata kupigiwa nyimbo zake sana kwenye MTV.Michael Jackson alipata umaarufu kwa baadhi ya mitindo alipokuwa akicheza muziki huo kama vile Robot na Moon Walk.

Mitindo ya muziki, sauti yake na zile Koregrafia, zimetambulika vizazi kwa vizazi, kirangi na hata katika mipaka ya kitamaduni.Michael alikuwa mmoja kati ya wasanii wachache waliowekwa mara mbili kwenye Rock and Roll Hall of Fame.Mafanikio mengine yamejumlisha tuzo ya Guinness World Records (ikiwa ni pamoja Mburudishaji mwenye mafanikio kwa muda wote.

Nguli huyo alituzwa tuzo za Grammy 15 (ikiwa ni pamoja na ile ya Living Legend Award na ile ya Lifetime Achievement Award).Zingine ni pamoja na 26 American Music Awards akiwa kama msanii pekee ya kujitegemea, pamoja na moja kwa ajili ya Msanii wa Karne, zaidi ya msanii mwingine yeyote.Single zake 17 zilishika nafasi ya kwanza huko nchini Marekani, ikiwa ni pamoja na nne alizopaa akiwa kama mwanachama wa Jackson 5.

Inakadiriwa Michael Jackson alifanya mauzo ya rekodi zaidi ya milioni 750 duniani, yaliyomfanya kuwa miongoni mwa wasanii waliouza rekodi zao vilivyo kwa muda wote na haijawahi kutokea.Kuanzia katikati mwa miaka ya 1980 muonekano wa Michael Jackson ulikuwa unabadilika bila kificho.

Umbo la sura yake vilibadilika pia, madaktari wa upasuaji kadhaa walikisia ya kwamba, kunako miaka ya 1990, alipitia upasuaji kadhaa wa pua, kuinua paji la uso, kufanya midomo iwe myembaba, na upasuaji wa mfupashavu.

Michael Jackson alifanya upasuaji wa pua kwa mara ya kwanza baada ya kuvunja pua yake wakati anacheza mchezo wa hatari kunako mwaka wa 1979.Hata hivyo, upasuaji huo haukukamilika kisawasawa, alianza kulalamika ya kwamba upumuaji wake ni wa tabu, ungeathiri shughuli zake.

Michale akaelekezwa kwa Dk. Steven Hoefflin, ambaye alifanya upasuaji wa pua kwa mara ya pili mnamo mwaka wa 1981.Katherine Jackson alisema katika mahojiano kwamba Michael alipata madhila ya pua kwa makusudi hapo mara ya kwanza.

Yaelezwa kwamba Michael Jackson alifanya tena upasuaji wa pua kwa mara ya tatu na ya nne mnamo mwaka wa 1986.Mwamba huyo wa Pop, Michael Jackson aliandika katika wasifu wake mnamo 1988 Moonwalk, kwamba katika ongezeko la upasuaji wa pua, pia alipata kutengeneza kidimpo katika kidevu chake.

Toka 1986 na kuendelea, alikuwa mteja wa kawaida wa Arnold Klein, mtaalamu wa magonjwa ya ngozi ambaye amebobea katika tiba ya sindano za ugonjwa ngozi, utaratibu wa utoaji wa tiba ya upodozi bila upasuaji.

Katika kitabu chake, Michael alidhania kuwa madailiko ya sura yake ni matokeo ya kubalehe, mpangalio mkali wa mlo wa kutokula nyama, upungufu wa uzito, badiliko katika mtindo wa nyewele na taa za jukwaani.

Lakini Michael Jackson alikana madai yaliyotolewa na baadhi ya watu kwamba alibadilisha macho yake.Mwaka 1990, kiwango chote cha upasuaji wa Jackson kilijadiliwa mno, hayo yalikaribia kusema kwamba mwimbaji huyo amepitia karibia taratibu kumi za upasuaji ya kubadili umbo lake.

Ilivyofika mwezi Juni 1992, gazeti la Daily Mirror liliweka picha nzima katika ukurasa wake wa mbele, likidai sura ya Michael Jackson, ambayo walielezea kama "sura mbaya isiyo na umbo zuri" kwa kufanya upasuaji wa sura.

Michael Jackson akalishtaki jarida hilo na mwaka wa 1998, wakakubaliana kuondoa kesi mahakamani na kuyamaliza nje ya mahakama.Mnamo mwaka wa 1993 alishtakiwa kwa kosa la udhalilishaji wa kijinsia kwa mtoto, ingawa hakuna mashtaka yoyote yaliyotolewa dhidi yake.Michael Jackson aliwahi kufunga ndoa na Bi. Lisa Marie Presley, binti wa mwanamuziki Elvis Presley mnamo mwaka 1994.

Aidha alimuoa mwanamke mwingine Deborah Rowe mwaka 1996, ambaye alizaa naye watoto wawili wa mwanzo kati ya watatu.Baadaye mama huyo alitoboa siri ya ndoa yao na kuwaambia watoto wake kuwa Michael Jackson sio baba yao.Deborah Rowe aliyasema hayo wakati alipohojiwa kwa mara ya kwanza tangia kutangazwa kwa kifo cha Michael Jackson.

Alifunga ndoa na Michael Jackson na kupata watoto wawili Prince na Paris.
Deborah alifafanua kuwa watoto hao alizaa baada ya kupandikizwa mbegu za kiume za mwanaume asiyejulikana, aliyejitolea mbegu zake za kiume hospitalini.

Mwanamke huyo Deborah alikutana na Michael wakati alipokuwa akifanya kazi kwenye kliniki ya ngozi ya Beverly Hills, Marekani ambako Michael alikuwa akienda mara kwa mara kwa matibabu.

Rafiki wa zamani wa Michael Jackson ambaye pia alikuwa mtaalamu wa ngozi Arnold Klein, aliibuka na kusema kuwa mfalme huyo wa muziki wa Pop ulimwenguni Michael Jackson, hakuwa na uwezo wa kuzaa kutokana na kujeruhiwa mara mbili korodani zake.

Katika mahojiano yaliyorekodiwa na mtandao mmoja wa nchini Marekani, Paul Gohranson ambaye ni mtaalamu wa kuchua misuli na aliyewahi kuishi kimapenzi na Klein, amesema kuwa Jacko alipoteza uwezo wake wa kutengeneza mbegu za uzazi baada ya baba yake kumpiga korodani zake.

Gohranson alieleza kwamba hali hiyo ndiyo iliyopelekea rafiki yake wa zamani kujitolea mbegu zake ili kumwezesha Jacko kuwa baba.Alinukuliwa akimuuliza "Arnold kwanini Michael Jackson asitumie mbegu zake mwenyewe? alijibiwa kuwa Michael alikuwa hawezi kuzaa"

Akifafanua Arnold alisema kuwa Klein alimwambia na kumthibitishia mara mbili kuwa Michael Jackson aliwahi kumwambia kuwa alipigwa sehemu zake za siri mara mbili kwanza wakatia akiwa mtoto mdogo ambapo baba yake alimnyanyua mguu wake mmoja na kuanza kumpiga.Alisema kuwa Klein aliendelea kumueleza kuwa baba yake Michael hakudhamiria kumpiga sehemu zake hizo za siri wakati huo lakini ndiyo hivyo imetokea na ilimsababishia maumivu makali sana Michael.Mara ya pili ilikuwa pale Michael alipotoa albamu ya peke yake, kila mtu alimjia juu Jacko kuwa anapoteza sauti yake, mtazamo wake na huenda akaitia aibu familia ya Jackson.

Jamaa akiendelea kusimulia mkasa huo akasema baada ya Michael kumaliza kumwambi yote hayo, machozi yalikuwa yakimtoka na hayo aliyaeleza baada ya kufanyiwa vitendo hivyo alisema Klein.Hata hivyo baba yake Michael Joe Jackson, alikanusha kwamba aliwahi kupiga mtoto wake huyo kiasi hicho wakati wa utoto wake.

Familia ya Michael kwa muda mrefu ilikuwa ikilalamikiwa kwa ukatili dhidi ya mwanamuziki huyo hasa katika kipindi ambacho ilikuwa ikisimamia kazi za Jackson 5.Katika utetezi wake mzee Joe aliwahi kusikika akisema kuwa hakuwahi kuwa kuwafanyia vitendo vya kikatili watoto wake hao wakoseapo.

Kwenye mahojiano yake ya kwanza mara baada ya kuachiwa toka gerezani kwa kuhusishwa na kifo cha Michael Jackson, Dokta Conrad Murray alielezea kwenye mahojiano aliyofanya na The Mail kwamba, Michael hakuwa baba wa mtoto wake hata mmoja.

Nguli huyo Michael aliathiriwa na madawa kiasi cha kufikia hatua ya kuhitajika kuwa anavaa condom sababu mkojo ulikuwa unatoka wenyewe kwenye uume wake.Naamini aliamka na kuamua kufanya aliyozoea kufanya, akajidunga sindano haraka ambayo ilisababisha kumpeleka kwenye hali iliyomfika.

Michael Jackson alikuwa kwenye majanga mwishoni mwa maisha yake, akiwa na msongo wa kimawazo aliyekata tamaa japokuwa Dokta Muraay alijaribu kumlinda ila mwisho wa siku niliangushwa naye.

Jackson alikuwa ameingia kwenye matatizo ya kuathirika kiakili na kimwili kutokana na ziara yake ya London.’’ Alisema Dokta Conrad Murray.

Kifo cha Michael Jackson kilitokana na kuzidisha kiasi cha dawa wakati anajiandaa na ziara ya tamasha lake la This Is It. Tamasha ambalo lilitakiwa lianze katikati ya mwaka 2009, ikaripotiwa kwamba alitumia dawa aina ya Propofol na Afisa uchunguzi wa vifo wa Wilaya ya Los Angeles walielezwa kuwa kifo chake ni uuaji wa binadamu, na mashtaka yanakwenda kwa daktari wake binafsi kwa kosa la kuua bila kukusudia.

Kifo hicho cha Michael kiliamsha mihemko ya huzuni na huduma ya ukumbusho wake uliofanywa hadharani ulitangazwa ulitazamwa na maelfu ya watu moja kwa moja duniani.Mbabe huyo katika mambo ya sanaa Michael Jackson katika siku zake za mwisho kabla kifo chake, alikuwa akijua mambo yote yatakayomtokea.

Hii ni kwa mujibu wa dada yake La Tonya, ambaye aliamua kufunua mambo hadharani. Akiadai kuwa kaka yake hakufa kwa kifo cha kawaida na kwamba palikuwa na mapango kamambe wa kuondosha uhai wake.

Kwa mujibu wa La Tonya mfalme huyo wa Pop, aliyekuwa maarufu kwa jina la WackoJacko, alimuambia kwamba lazima atauawa kutokana na muziki wake.La Toya ambaye pia ni msanii maarufu alidai alimuambia Wacko Jacko kuwa “Watu wanakuingilia mpaka katika maisha yako, angalia mumo unavyoishi, ni lazima ujidhibiti hasa katika fedha zako. Wale wanaokufadhili, mapato yako na kila kitu kinachokuhuhusu.

Alidai kwamba baada ya kumwambia hivyo,Michael Jackson alimtazama na mwisho akamwambia “La Toya ,mimi nakwenda kuuawa na hasa kutokana na muziki na mali ninazozimiliki…”La Tonya alidai Wacko alikuwa anaogopa mno kuhusu maisha yake na akimshutumu Dk.Tohme Tohme ambaye ndiye aliyekuwa anamsimamia katika kuchangia kwa kiasi kikubwa kifo chake.

“Huyu alikuwa anajifanya mshauri wa kibiashara wa Michael Jackson, akafukuza watu wangu muhimu zaidi ambao walikuwa na Michael Jackson kwa muda mrefu…” Alitamka La Tonya.Mwanadada huyo alisema kuwa dunia itaendelea kumkumbuka Michael Jackson.

Historia ya Michael Jackson inaeleza kuwa kutokana na umahiri wake wa kuimba na kucheza, alipewa heshima ya kuwa Mfamle wa Pop.Aliingizwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Guiness kama mmja wa wanamziki wanaopendwa.

Alianza kuonesha cheche zake katika muziki akiwa mdogo kabisa pale alipoungana na ndugu zake na kuunda kundi la The Jackson 5, kabla hawajalibalisha jina na kuliita Jackosons mwaka 1964.Lakini miaka saba abaadaye aliamua kujiondoa katika kundi hilo, akaanza kupiga muziki peke yake.

Miaka ya 1980, Wacko Jacko akaja kuwa maaruru zaidi katika muziki hasa alipoibuka na Video za nyimbo zake za Beat It, Bile Jean na Thriller amabzo zilichangia kwa kiasi kikubwa kwa Televisheni mpya iliyokuwa imeanzishwa ya MTV.

Video nyingine kama Black or White na Scream zikaibeba MTV kiuifanya iendelee kung’ara zaid katika miaka ya 1990.

Album yake ya Thriller iliyotoka mwaka 1982, ndiyo iliyouza nakala nyingi mno kuliko nyingine zote, huku zile za Off the Wall (1979), Bad (1985), Dangerous,(1991) na History (1990) nazo pia ziilingiza mauzo makubwa duniani.

Wacko Jacko wakati wa uhai wake alitwaa mamia ya tuzo na kumfanya kuwa mmoja kati ya wasanii waliopata tuzo nyingi katika historia ya muziki. Pia alijulikana kwa jinsi alivyokuwa akisaidia jamii huku akiwa ametoa msaada kwa zaidi asasi 39.

Kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo, Wacko Jacko pia alichangia mamillioni ya dola kwa asasi mbalimbali zinazohusika na watoto. Michael Jackson alizunguuka katika hospitali nyingi mno kwa ajili ya kuwatembelea watoto.

Jacko mara nyingi alipokuwa akifanya zaira zake hizo, alipomaliza ni lazima alikuwa akiwauliza madaktari na wauguzi ni kitu gani walicho kuwa wanakihitaji kutoka kwake, akiambiwa vitu vya gharama kubwa, yeye alitimiza.

Mnamo mwaka 1993 alikumbwa na kashfa ya ngono na watoto, lakini kesi iliyofunguliwa ikamalizwa nje ya mahakama huku mwaka mwaka 2005, pia alikumbana na kesi nyingine kama hizo.

Aidha Kampuni ya Sony Music Entertainment ilisaini mkatataba wa milioni 250, ili iwe haki ya kusambaza haki zake mpaka 2017. Wacko Jacko alikuwa amejiandaa kufanya shoo moja kubwa kubwa iliyokuwa imepewa jina la This is It.Machael Jackson alikuwa mtoto wa nne kati ya kumi ambao ni Wamerekani wenye asili ya Afrika. Aliishi na ndugu zake katika nyumba moja ndogo ya vyumba vitatu iliyokuwa katika eneo la viwanda katika Jimbo la Chicago, nchini Marekani.

Mama yake Katherine Esther Scruse ni muumini mzuri wa mashahidi wa Yehova.Baba yake Joseph Walter ‘Joe’ Jackson, alikuwa mfanyakazi wa kwenye kiwanda cha chuma.Lakini pia alikuwa na bendi iliyokuwa ikijulikana kwa jia la The Falcon, ambayo alikuwa ikipiga katika mtindo wqa R&B.

Wacko Jacko alikuwa na dada watatu ambao ni Rbbie, La Toya na Janet huku wanaume wakiwa watano amabao ni akina Jackie, Tito, Jaremaine, Marlon, Randy na Kaka yake Brando, aliyekufa muda mfupi baada ya kuzaliwa kwake.

Michael Jackson alikuwa na msuguano katika uhusiano yake na baba yake, huku baba akidai alikuwa akitimiza majukumu yake kama mzazi.

Japokuwa ilikuwa imeripotiwa kudhalilishwa kwake wakati akiwa mtoto kwa miaka kadhaa, yeye binafsi alizungumza kinagaubaga kuhusu hilo katika mahojiano yake ya mwaka wa 1993 na Oprah Winfrey.

Alikunja uso kwa huzuni wakati anazungumzia mateso aliyokuwa ana pata kutoka katika mikono ya baba yake mzazi. Aliamini ya kwamba ameyakosa maisha yake ya utotoni kwa miaka kadhaa, akikubaliana na hali ya kwamba alikuwa akilia mara kwa mara hasusan kwa kufuatia upweke aliokuwa nao.

Walisema ya kwamba walikuwa wakinyanyasika sana kimwili na kihisia na baba yao.Katika moja ya mabishano makali ambayo baadaye yalikumbushiwa na Baba yake mzee Joseph, aliwahi kumning'iniza Michael miguu juu kichwa chini huku akimshika mguu mmoja tu na kumchapa vibiko kwa mkono wake na kumpiga vibako vya matakoni.

Mzee huyo alikuwa na kawaida ya kuwachukua vijana na kuwatupa ukutani.
Usiku mmoja wakati Michael Jackson kalala, baba yake mzee Joseph alipanda hadi chumbani kwa mwanae kwa kupitia dirilisha la bafuni, huku akiwa amevaa kinyago cha kutisha. Akaingia chumbani Michael akanza kupiga ukelele wa nguvu.

Mzee huyo alisema eti alitaka kuwafundisha watoto zake wasiache dirisha wazi wakati wanaenda kulala. Kwa miaka kadhaa baada ya hapo, Michael Jackson alikuwa akisumbuliwa na ndoto za kutisha za jinamizi likija kumchukua chumbani kwake, mwanzoni mwa miaka ya 1980

Mwaka wa 2003, baba yake alikiri kwamba alikuwa akimchapa viboko sana Michael Jackson wakati yu mtoto.

Michael Jackson alikuwa binadamu wa kwanza kukosa usingizi kamili kwa siku 60, wataalamu walibaini. Daktari wake binafsi wa Michael Jackson, Conrad Murray alikuwa akimpa dawa za kutuliza maumvu kwa miezi miwili mfululizo kila siku hali iliyopelekea mwili kuchoka kila wakati.

Inaelezwa kwamba dawa hizo zina kawaida ya kumyima mtu usingizi na zinaweza kumfamfanya kupoteza fahamu.Daktari bingwa na mtaalamu wa magonjwa ya kichwa, Charles Czeisler alisema kuwa Michael Jackson huenda alifariki aidha kwa sabababu ya kukosa usingizi muda mrefu, au kwa kuumia kwa muda mrefu dawa za kutuliza maumivu alizokuwa akipewa na Murray.

Siku chache kabla ya kifo chake, ilielezwa kuwa hakuweza kucheza japo kidogo au hata kukumbuka baadhi ya maneno kwenye nyimbo zake.Wakati fulani katika miaka ya 1990, ilionekana ya kwamba Michael Jackson alikuwa tegemezi kubwa la madawa mbalimbali, hasa dawa za kuua maumivu na vipoozeo vikalivikali ambapo afya yake ikaanza kuyumba waziwazi.

Wakati uchuguzi unaendelea, hali ya Jackson ilishughulikiwa na Stan Katz, mtaalamu wa masuala ya akili.Kwa mujibu wa Randy Taraborrelli, uchunguzi uliofanywa na Katz ulionesha Jackson akili yake imerudi kama mtoto mwenye miaka kumi.

Baadhi ya wataalamu wa tiba walithubutu kusema hadharani kwamba wanaamini mwimbaji huyo pia alikuwa na matatizo ya akili ya kujiona kama watu wengine wanamuona si yeye kutaka mwonekano wa mtu mwingine.

Hali ya kisaikolojia ambapo msumbuliwa hana wazo au uwezo wa kufikiria taswira yake jinsi watu wanavyochukulia.Michael Jackson alienda kujiswafi mwaka wa 1993 kwa msaada wa Elizabeth Taylor na Elton John, lakini ulevi wa dawa ulibaki palepale.

Wacko Jacko alikuwa hapendi kabisa kulizungumzia hilo, lakini pindi tu anapolisema, alikuwa na huzuni sana na kusema ya kwamba angetapika kabla ya kukutana na baba yake.

Mungu aiweke pahala pema peponi, Amina.


Makala hii imeandaliwa kwa msaada mkuwa wa mitandao.

Mwaandaji anapatikana kwa namba: 0784331200, 0767331200,0736331200 na 0713331200.

Mungu aipumzishe roho yake pahala pema peponi, Amina.


HALI YA UZALISHAJI WA MAZAO YA CHAKULA KWA MSIMU WA 2018/2019

$
0
0

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula kwa msimu wa 2018/2019 na upatikanaji wake kwa mwaka 2019/2020

Ndugu Wanahabari, 
Kila mwaka kati ya mwezi mei na juni, Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali hufanya tathmini ya hali ya uzalishaji wa chakula na upatikanaji ili kujua;

     i.        Hali ya kiujumla ya uzalishaji wa mazao na upatikanaji wa chakula kwa Mikoa na Halmashauri zote

    ii.        Uzalishaji wa mazao ya chakula na utekelezaji wa malengo ya uzalishaji hadi tarehe 31 Mei kila mwaka.

  iii.        Athari za visumbufu katika uzalishaji wa mazao

  iv.        Bei ya mazao ya chakula na hali ya upatikanaji wa chakula sokoni katika Halmashauri zote na kuainisha maeneo yenye dalili ya uhaba

   v.        Hali ya unyeshaji wa mvua na mwenendo wa uzalishaji wa mazao mashambani

Ndugu Wanahabari
hali ya uzalishaji na upatikanaji wa mazao ya chakula nchini imeendelea kuwa nzuri katika kipindi cha miaka mitano mfululizo kufuatia uzalishaji wa ziada wa mazao ya chakula kuanzia msimu wa kilimo wa 2013/2014 hadi 2017/2018 ambapo kwa msimu wa 2018/2019 nchi imejitosheleza ikilinganishwa na mahitaji.

Ndugu Wanahabari, 
katika kufanya tathmini ya hali ya chakula, hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula na usalama wa chakula tunaangalia baadhi ya mazao muhimu yanayohitajika zaidi kama vile mahindi, mtama na ulezi, mchele, mikunde, ngano, ndizi, muhogo na viazi.

Ndugu Wanahabari, 
katika kipindi hicho, nchi imekuwa na kiwango cha utoshelevu kati ya asilimia 120 hadi 125 na imekuwa ikizalisha ziada kati ya tani 2,582,717 hadi 3,322,689. Mafanikio hayo yanatokana na sababu mbalimbali ikiwemo hali ya hewa nzuri, pamoja na usimamizi na utekelezaji mzuri wa sera na mikakati mbalimbali inayotekelezwa na Serikali pamoja na Wadau wengine wa masuala ya kilimo ili kuongeza tija na uzalishaji.

Ndugu Wanahabari, 
Wizara ya Kilimo mwezi Mei hadi Juni 2019 ilifanya Tathmini ya Hali ya Uzalishaji wa Mazao ya Chakula kwa msimu wa 2018/2019 na Upatikanaji wa Chakula kwa  mwaka 2019/2020 katika mikoa yote 26 Tanzania Bara kwa lengo kubaini uzalishaji na mahitaji.

Matokeo yanaonesha kuwa hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula kitaifa katika msimu wa 2018/2019 utafikia tani16,408,309 kwa mlinganisho wa nafaka (Grain Equivalent) ambapo nafaka ni tani9,007,909 na siyo nafaka tani 7,400,400.

Ndugu Wanahabari, 
Ikilinganishwa na msimu uliopita, uzalishaji wa mazao ya chakula umeshukakwa tani 483,665 ambapo nafaka hususan mahindi yameshuka kwa tani 455,642 na mchele kwa tani 210,454. Aidha,uzalishaji wa siyonafaka (non cereals) umeongezeka kwa tani 46,283.

Ndugu Wanahabari, 
uzalishaji wa mazao ya nafaka ulifikia asilimia 103 na mazao yasiyo ya nafaka yalifikia asilimia 145. Hivyo, uzalishaji wa jumla wa mazao ya nafaka na yasiyo ya nafaka ulifikia asilimi 119.
Ndugu Wanahabari, 
Aidha mchango wa uzalishaji wa mazao ya chakula kitaifa katika msimu wa 2018/2019 unaonesha kuwa mahindi yamechangia kwa asilimia 35, muhogo kwa asilimia 17, mchele kwa asilimia 12, viazi kwa asilimia 10 na mazao mengine.
Ndugu Wanahabari, 
Pamoja na hali hiyo, utengamano wa usalama wa chakula unatarajiwa kuwa wa viwango tofauti kimkoa. Aidha, hali ya uwepo na upatikanaji wa chakula kwa sasa ni nzuri kutokana na uzalishaji mzuri wa msimu wa 2017/2018.

Ndugu Wanahabari

Kwa kuzingatia Kigezo cha Upimaji wa Kiwango cha Utoshelevu (Self Sufficiency Ratio– SSR), matokeo yanaonesha kuwa kwa mwaka wa chakula 2019/2020, nchi itakuwa na kiwango cha Utoshelevu cha asilimia119.

Ndugu Wanahabari

Tathmini imeonesha, hali ya chakula inatarajiwa kuwa ya kiwango cha Ziada kwenye mikoa 11 yaRukwa, Ruvuma, Songwe, Katavi, Njombe, Mbeya, Kigoma, Iringa, Kagera, Morogoro, na Mtwara kwa asilimia 128 hadi 227. Aidha, kutakuwa na hali ya Utoshelevu  kwenye mikoa 7 ya Geita, Simiyu, Pwani, Lindi, Manyara, Singida na Tanga kwa asilimia 109 hadi 119 naUpungufu kwenye mikoa 8 ya Dodoma, Mara, Mwanza, Arusha, Tabora, Shinyanga na Kilimanjaro kwa asilimia kati ya  98 hadi 99.

Ndugu Wanahabari

Mkoa Dar es Salaam si miongoni mwa mikoa ya uzalishaji wa mazao na hivyo kujitosheleza kwa asilimia 3 tu kutokana na eneo dogo linalolimwa lisilokidhi mahitaji ya chakula ya wakaazi wake. Ingawa mkoa huu unawekwa kwenye upungufu wa chakula kwa maana ya uzalishaji katika mashamba, mkoa huu una vyakula vingi vinavyoingia sokoni kutoka katika mikoa 25 ya Tanzania bara na hivyo kuwa na Utoshelevu kwa vipindi vyote.  

Ndugu Wanahabari

Tathmini imebainisha kuwa uwepo wa maeneo (pockets)yenye dalili za upungufu wa chakula kwenye Halmashauri 46 katika mikoa 13kama ifuatavyo;

·      Mkoa wa Dodoma katika Halmashauri 7 za Bahi, Chamwino, Chemba, Kondoa, Kongwa na Mpwapwa;

·   Mkoa wa Mara katika Halmashauri 5 za Bunda DC, Bunda TC, Musoma DC, Musoma MC na Rorya;

·     Mkoa wa Tabora katika Halmashauri 5 za Uyuyi, Igunga, Nzega DC, Nzega TC na Kaliua;

·   Mkoa wa Shinyanga katika Halmashauri 4 za Kishapu, Shinyanga DC, Shinyanga MC na Msalala;

·     Mkoa wa Kilimanjaro katika Halmashauri 4 za Mwanga, Same, Siha na Hai,

·  Mkoa wa Mwaza katika Halmashauri 4 za Misungwi, Ukerewe, Kwimba na Sengerema;

·       Mkoa wa Manyara katika Halmashauri 4 za Simanjiro, Kiteto, Hanang na Mbulu TC;

·        Mkoa wa Simiyu katika Halamshauri 4 za Itilima, Maswa, Meatu na Busega;

·        Mkoa wa Arusha katika Halamshauri 3 za Longido, Ngorongoro na Monduli;

·        Mkoa wa Singida katika Halmashauri 3 za Ikungi, Manyoni na Singida DC;

·        Mkoa wa Tanga katika Halmshauri 1 ya Tanga jiji;

·        Mkoa wa Lindi katika Halmashauri 1 ya Lindi DC na

·        Mkoa wa Iringa katika Halmashauri 1 ya Iringa DC.

Ndugu Wanahabari

Msimu wa uzalishaji wa 2018/2019 ulikabiliwa na changamoto mbalimbali katika baadhi ya maeneo zilizoathiri uzalishaji wa mazao kwa viwango tofauti na kusababisha kushuka kwa uzalishaji wa mazao hususan zao la mahindi. Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na:-

(i)          Katika maeneo yanayopata mvua misimu miwili (Bimodal Areas) mvua za vuli katika maeneo mengi hazikufanya vizuri. Aidha, mvua za masika zilichelewa sana kuanza na hivyo kuathiri shughuli za kilimo katika maeneo hayo,

(ii)         Kuchelewa kuanza kunyesha kwa mvua na mtawanyiko usioridhisha kwenye baadhi ya maeneo ya nchi yanayopata mvua msimu mmoja (Unimodal Areas) hususan katika mikoa ya Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, na baadhi ya maeneo ya mikoa ya Morogoro, Mwanza, Mara, Simiyu na Manyara,

(iii)       Visumbufu hususan viwavijeshi vamizi (Fall Army Worm - FAW), panya na Kweleakwelea.

Ndugu Wanahabari

Kufuatia matokeo ya Tathmini hii, Serikali inachukua / itachukua hatua zifuatazo;

·        Kuimarisha Mfumo wa ukusanyaji taarifa za usalama wa chakula nchini ili kuweza kuchukua hatua stahiki pindi inapobidi,

·        Kufanya Tathmini ya Kina ya Hali ya Chakula na Lishe mapema katika Halmashauri zilizobainika kuwa na maeneo yenye viashiria vinavyoweza kusababisha upungufu wa chakula,

·        Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko wanatarajia kuanza ununuzi wa mazao ya chakula kutoka kwenye maeneo yenye ziada,

·        Kuimarisha mfumo wa upatikanaji na usambazaji wa pembejeo za kilimo ikiwemo viuatilifu, mbegu na mbolea.

·        TRA pamoja na Wataalam wa kilimo katika vituo vya mipaka ya nchi  kusimamia kikamilifu usafirishaji wa mazao yanayokwenda nje ya nchi ili kusaidia upatikanaji wa takwimu sahihi za kiasi kinachosafirishwa nje ya nchi.
Ndugu Wanahabari

Niwatake wananchi wote nchini kuzalisha mazao ya chakula kwa kuzingatia kanda za kiekolojia, kuwa na hulka ya kuhifadhi chakula kulingana na mahitaji ya kaya pamoja  kutumia  mazao ya chakula kilichopatikana vizuri kiweze kutumika hadi kufikia msimu mwingine wa uzalishaji.

Aidha, Wakulima waliopata chakula cha ziada wanashauriwa  wasiharakishe kuuza mazao yao mapema bali wasubiri hadi bei zitakapokuwa nzuri ndipo wauze na kwa wale wenye waliopata utoshelevu kidogo wa chakula watumie vizuri mazao hayo kwa ajili ya chakula na si vinginevyo.

ASANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA 
Japhet Ngailonga Hasunga (Mb)

WAZIRI WA KILIMO

18 Julai 2019
--

WAZIRI NDALICHAKO ATEMBELEA BANDA LA PSPTB KWENYE MAONESHO YA VYUO VIKUU

$
0
0
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako akipata maelezo kuhusu kazi zinazofanywa na  Bodi ya wataalamu wa ununuzi na Ugavi (PSPTB) kutoka kwa  Afisa mwandamiza Masoko na mahusiano kwa Umma wa PSPTB, Shamim Mdee alipotembelea banda la bodi hiyo wakati wa kufunga maonesho ya 14 ya Vyuo Vikuu yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako akipokea vipeperushi vya Bodi ya wataalamu wa ununuzi na Ugavi (PSPTB) kutoka kwa  Afisa mwandamiza Masoko na mahusiano kwa Umma wa PSPTB, Shamim Mdee alipotembelea banda la bodi hiyo wakati wa kufunga maonesho ya 14 ya Vyuo Vikuu yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

RC GAMBO:TAIFA LINAHITAJI VIONGOZI WA DINI WANAOHUBIRI HABARI NJEMA ZA AMANI.

$
0
0
Umati wa waumii waliofurika katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikhe Amri Abeid Karume Jijini Arusha kusikiliza neno la Mungu linaloendelea kuhubiriwa na Muhubiri wa Kimataifa kutoka nchini Sweeden Johannes Amrizer ambapo unakwenda sambamba na maadhimisho ya mika 80 ya Kanisa la Tanzania Assemblies of God Tanzania.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.Mrisho Gambo akisalimia wananchi waliohudhuria katika mkutano huo wa neno la Mungu ambao ulianza rasmi siku ya Jumatano ambapo siku ya kesho ndiyo Kilele chake.
Muhubiri wa Kimataifa kutoka nchini Sweeden Johannes Amrizer akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe.Mrisho Gambo jioni ya leo 


Na.Vero Ignatus,Arusha.

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema Taifa linahitaji viongozi wa dini wanaohubiri habari njema kuhusiana na Mungu kwaajili ya kuleta Amani katika Taifa na wananchi kwa ujumla.

Mhe. Gambo ameyasema hayo jioni ya leo katika mkutano wa Injili unaoendelea katika uwanja wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid alipokaribishwa kusalimia waumini waliokuwepo na muhubiri wa Kimataifa Johannes Amrizer kutoka nchini Sweeden."

Amesema kuwa kesho ni kilele cha maadhimisho miaka 80 ya Kanisa la Tanzania Assemblies of God Tanzania hivyo amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi ili kuungana na kanisa holo la TAG kusheherekea mwambie hata mwenzio aliyeko nyumbani.aje.kusikiliza.siyo.dhambi"

Waambieni wengine waliopo nyumbani wamechelewa angalau wajitahidi wafike siku ya kesho ili waweze kupata majumuisho ya kile kilichokuwa kinaendelea uwanjani hapa kwa wiki nzima"Alisema.Gambo.

Gambo amewahakikishia wananchi kuwa usalama upo wa kutosha na siku ya kesho wataimarisha usalama zaidi ,Amesema kanisa hilo la TAG wanalipenda kwasababu Askofu wake mkuu ni mtu mzuri,hana makuu,na ni mtu ambaye viongozi wa serikali wanamuheshimu,hivyo ni mfano mzuri wa kuigwa hata na viongozi wengine wa kidini.

Amesema kuwa wale ambao wakisikia neno la Mungu linahubiriwa wanasema ni kelele mapepo washindwe, kwani Mtu yeyote akikwambia huwezi kufanikiwa wewe jitikise kama punda utajitikisa mwisho utajikuta upo juu.

Kwa upande wake muhubiri huyo kutoka nchini Sweeden Johannes Amrizer amemshukuru mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kwa kumtia moyo akiwa katika mkoa huo wa Arusha

Viongozi wapya wa Jumuiya Kuu ya Wanzania waishio Uingereza na Ireland ya Kaskazini - ATUK

$
0
0
  Viongozi wapya wa Jumuiya Kuu ya Wanzania waishio Uingereza na Ireland ya Kaskazini  “ The Association of Tanzanians in the UNITED KINGDOM (ATUK). Kutoka kulia waliokaa ni  Dkt. Imani Kondo ambaye amechaguliwa kuwa Katibu, katikati ni Bi. Martha Mpangile ambaye anafanya kazi ya uanasheria mjini London amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Watanzania.
Kutoka kushoto ni Bi. Zuhura Adam Sapi Mkwawa Mtaalum wa Hisabati kutoka  mjini Leicester amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti. Waliosimama kutoka kulia ni Bi. Lucy Shigikile mfanyakazi toka Jumuiya ya Madola London anakuwa Mtunza Hazina, anayefuata katikati ni Bw. Frank Leo CEO wa Upendo Events ya mjini Coventry anakuwa Katibu  Msaidizi na mwisho kushoto ni Bw. Nelson Kampa Real Estates Agent toka Birmingham na ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Watanzania waishio Birmingham anakuwa Mtunza Hazina Msaidizi.
Uchaguzi wa Viongozi Wakuu hao ulifanyika katika ukumbi wa Ubalozi mjini London tarehe 14 Julai, 2019. Mhe. Balozi Asha- Rose Migiro ndiye mlezi wa Jumuiya Kuu ATUK.
Mwanasheria Bi. Mpangile atafanya mkutano wake wa kwanza Mjini Birmingham katika ukumbi wa Ibis Style Hotel NEC tarehe  28 Julai, 2019 ambako atakutana na viongozi wapya lakini pia atafanya mazungumzo ya makabidhiano toka Kamati Maalum katika  dhima ya kutekeleza dira na mwelekeo wa Jumuiya Kuu.

Imetolewa na Uongozi ATUK.

VACANCY ANNOUNCEMENT FROM THE INTERNATIONAL TELECOMMUNICATION UNION (ITU)

$
0
0


The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received Vacancy Notice No. 21D-2019/BDT-DDR/External/D2 from the International Telecommunication Union (ITU) inviting qualified Tanzanians to apply for the post of  Deputy to the Director and Chief of the Administration and Operations Coordination Department (DDR).

Application details can be found through the ITU website: http://www.itu.int/employment/Recruitment/index.html

Closing date for application is Sunday 25th August 2019.


Issued by;
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dodoma.
18th July 2019.

WAZIRI MKUU AWAFUNDA WATUMISHI WA UMMA \

$
0
0

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiongea na Viongozi na Watumishi wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, katika ukumbi wa Halmashauri Julai 19.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akikagua darasa lililokarabatiwa la Shule Kongwe ya Same Sekondari, mkoani Kilimanjaro Julai 19.2019. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Same Sekondari Hoza Mgonja.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akikagua maabara katika Shule Kongwe ya Same Sekondari, kabla ya kuzindua mradi wa ukarabati wa shule hiyo kongwe, mkoani Kilimanjaro Julai 19.2019.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiangalia darasa lililokarabatiwa la Shule Kongwe ya Same Sekondari, katika mradi wa ukarabati wa shule hiyo kongwe mkoani Kilimanjaro, Julai 19.2019.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiangalia vitabu katika maktaba iliyokarabatiwa ya Shule Kongwe ya Same Sekondari, katika mradi wa ukarabati wa shule hiyo kongwe mkoani Kilimanjaro, Julai 19.2019. Kushoto ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Same Sekondari Hoza Mgonja.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizindua mradi wa ukarabati wa shule kongwe ya Same Sekondari, iliyoko wilayani Same katika mkoa wa Kilimanjaro, Julai 19.2019.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na wanafunzi wa Same Sekondari mara baada ya kuzindua mradi wa ukarabati wa shule hiyo kongwe, iliyoko wilayani Same katika mkoa wa Kilimanjaro, Julai 19.2019.

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akimsikiliza mwanafunzi wa Same Sekondari, Omari Pundugu, akielezea changamoto mafanikio na changamoto za shule hiyo mara baada ya uzinduzi wa mradi wa ukarabati wa shule hiyo kongwe, iliyoko wilayani Same katika mkoa wa Kilimanjaro, Julai 19.2019.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwasalimia wananchi, baada ya kuzindua mradi wa ukarabati wa shule kongwe ya Same Sekondari, mkoani Kilimanjaro Julai 19.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu). 
*Ataka wawe na mipango kazi, asema Serikali inapima matokeo
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa umma wawe na mipango ya kazi ambayo itaweza kupimika na kutoa matokeo.

“Kila mtumishi anapaswa awe na mpango kazi katika sekta yake na ni lazima aende kupima matokeo. Awamu hii, tunataka kuona matokeo ya kazi zenu." 

Ametoa kauli hiyo leo asubuhi (Ijumaa, Julai 19, 2019) wakati akizungumza na watumishi wa wilaya ya Same kwenye ukumbi wa Halmashauri ya wilaya hiyo, mjini Same. 

“Watumishi mmeletwa kwenye wilaya hii ili muwahudumie wananchi. Tulioajiriwa, kazi yetu kubwa ni kuwatumikia wananchi bila ubaguzi wowote uwe ni wa kabila, itikadi au rangi.” 

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwakumbusha watumishi hao kwamba baada ya mchujo wa watumishi hewa, waliobakia wanapaswa kufanya kazi kwa bidii. 

"Fanyeni kazi kwa bidii, msimamo wa Serikali hii ni kwamba hatumvumilii mtumishi ambaye si mwajibikaji, ni mwizi, mzembe au anaomba rushwa. Serikali hii hatuna muda wa kujadili matatizo ya watumishi, tunamalizana hapo hapo," amesema. 

Amewataka watumishi hao wasimamie utekelezaji wa ahadi zilizotolewa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwa sababu ndiyo chama tawala. 

"Mtumishi angalia sekta yako inasema nini, ifanyie kazi. Kama ni maji, tafuta ni wapi yanapatikana, changanua zinahitajika shilingi ngapi, tafuta njia ya kupata hizo fedha ili wananchi wapate maji." 

Kuhusu tabia ya kukaa ofisini, Waziri Mkuu amekemea tabia hiyo na kuwataka watumishi wote nchini waache tabia ya kukaa ofisini na badala yake waende vijijini kuwasikiliza wananchi. 

"Watumishi wa umma msikae ofisini. Nendeni vijijini walau kwa siku nne za juma. Hizo mbili zinazobakia, zitumieni kuandaa taarifa. Nendeni huko ili wananchi wasipate usumbufu wa kuja hapa mjini kuwatafuta," amesisitiza. 

"Mkuu wa Wilaya simamia zoezi la wakuu wa idara na wasaidizi wao kwenda vijijini. Wakienda vijijini ni lazima waonane na waheshimiwa madiwani, washirikiane kusikiliza kero na kutafuta majibu kwa wananchi. Huo ndiyo mshikamano wenyewe unaohitajika," amesema. 

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amewataka watumishi wa umma watambue mipaka yao na wajenge mahusiano baina yao na wengine. 

Alitoa kauli hiyo jana jioni (Alhamisi, Julai 18, 2019) wakati akizungumza na watumishi wa Manispaa ya Moshi, kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa. 

"Kila mmoja lazima atambue mipaka yake na mamlaka baina yake na wengine. Hapa mko wateuliwa, waajiriwa na wachaguliwa. Kila mtu ana nafasi yake ya kuwatumikia wananchi.

Aliwataka watumishi hao watambue falsafa ya Kiongozi mkuu wa nchi ambayo inahimiza uchapakazi. “Kwa hiyo tunaposema Hapa Kazi Tu, maana yake chapa kazi na tuone matokeo. Tunasisitiza kazi na tunataka kazi unayoifanya, itoe matokeo,” alisema.  

NEWZ ALERT:Rais Magufuli afanya uteuzi wa Waziri wa Muungano na Mazingira, Naibu Waziri wa Kilimo na Mwenyekiti wa PPRA

MBUNGE SINGIDA ASAKA MILIONI 480 ZA KUCHIMBA VISIMA

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu, akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana Kijiji cha Mtavira Kata ya Makilawa wilayani Ikungi mkoani Singida.
Wasanii wakitoa burudani kwenye mkutano huo
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu, akicheza sanjari na wasanii.
Mkutano ukiendelea
Wananchi wakinyoosha mikono kuipongeza Serikali kwa kuwapelekea maendeleo
Watoto wakiwa juu ya miti wakimsikiliza mbunge wao
Mkutano ukiendelea



Na DottoMwaibale, Singida

MBUNGE wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu anatafuta sh.milioni 480 kwa ajili ya kuchimba visima virefu vya maji katika vitongoji 12 vilivyopo Kata ya Makilawa wilayani Ikungi mkoani Singida.

Akizungumza jana katika mkutano wa hadhara wenye lengo la kuzungumzia miradi ya maendeleo iliyofanyika katani hapo pamoja na kujua changamoto zilizopo Kingu alisema wananchi waliopo mji wa Mtavira wameanza kupata maji hadi kufikia hatua ya kuosha magodoro.

"Hapa Mtavira mnapata maji mengi kupitia mradi wa Tanjet sasa hivi naelekeza nguvu zangu kupeleka maji katika vitongoji 12 vya kata hii ambapo nitachimba visima 12 vyenye thamani ya sh.milioni 480 pamoja na ujenzi wa sekondari" alisema Kingu.

Kingu alivitaja vitongoji hivyo kuwa ni Magohana A, Magohana B, Itulu, Kazizi, Munyu, Mpembu, Majengo, Mteva Kati, Songambele, Kasela, Kinyalambe na Darajani.

Akizungumzia kuhusu ujenzi wa sekondari alisema kwa kuanza atachangia mifuko ya saruji 150 huku madiwani wakiahidi kutoa mifuko 10 tu.Kingu alisema miradi yote hiyo inafanyika kwa msaada mkubwa wa Rais Dkt. John Magufuli baada ya kuziba mianya ya fedha za serikali ambazo zilizokuwa zikitumika vibaya na mafisadi.

Aliongeza kuwa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Serikali ya Rais Dkt.John Magufuli miradi mingi ya maendeleo imefanyika na mingine inaendelea kujengwa.

Alisema katika jimbo la Singida Magharibi baadhi ya miradi mikubwa iliyofanyika ni ya maji na ujenzi wa vituo vya afya vya kisasa Kata ya Sepuka na Ihanja ambacho kinavifaa tiba vya kisasa na wameajiriwa madaktari bingwa wanaotoa huduma za upasuaji kwa wananchi kutoka kata mbalimbali za jimbo hilo.

Kingu aliwahimiza wananchi kutunza miundombinu ya miradi hiyo baada ya kukamilika na kueleza kuwa itakuwa haina maana miradi iliyogharamiwa na serikali kwa fedha nyingi ikaachwa iharibike.

Diwani wa Kata ya Makilawa Hassan Mtakii alipongeza jitihada zinazofanywa na Serikali pamoja na mbunge huyo za kuwaletea maendeleo wananchi wa kata hiyo na nchi nzima kwa ujumla.
Viewing all 110129 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>