Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

BREAKING NEWS: BOT SUSPENDS APPOINTMENT OF MR. FRANK NYABUNDEGE AS MANAGING DIRECTOR OF TIB CORPORATE BANK LIMITED


BREAKING: BENKI KUU YA TANZANIA YASITISHA UTEUZI WA BW. FRANK NYABUNDEGE KAMA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA TIB CORPORATE

VOA Swahili: Watu 26 Wauawa Shambulizi La Bomu Somalia

LIVE: KINACHOENDELEA USIKU HUU MISS KINONDONI 2019

TAARIFA KWA UMMA: WAMILIKI WA MAJENGO NA WAFANYA BIASHARA WALIOKIDHI VIGEZO WANATAKIWA KUFIKA VITUO VYA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KUCHUKUA HATI ZA USALAMA DHIDI YA MOTO

$
0
0

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linapenda kuutaarifu Umma wa  Tanzania  kwamba, Wamiliki wa majengo na Wafanyabiashara waliofanyiwa ukaguzi wa kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto na kukidhi vigezo vya usalama wa moto, kufika au kuwasiliana na Ofisi ya Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa husika au kituo cha Jeshi hilo kilicho karibu yake, kwa ajili ya kuchukua Hati ya Usalama dhidi ya Moto (Fire SafetyCertificate).
Cheti cha Usalama dhidi ya Moto kinapatikana baada ya kufanyiwa ukaguzi wa kinga na tahadhari dhidi ya majanga kwenye majengo. Ukaguzi huo unafanyika kwa mujibu wa Sheria namba 14 ya mwaka 2007, ikisomwa pamoja na Kanuni ya Vyeti na Usalama wa moto ya Mwaka 2008 na marekebisho ya mwaka 2014 (FireandRescueForceSafetyInspectionsandCertificatesRegulations of2008GN.106anditsAmendmentGN63of2014.)PamojanaKanuniya tahadhari dhidi ya moto kwenye majengo ya mwaka 2015 (Fire and Rescue ForceFireSafetyPrecautioninBuildingRegulationsof2015GN516.)

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linatoa rai kwa Umma kujenga tabia ya kutembelea vituo vilivyo karibu kwa ajili ya kupata ushauri pamoja na kuchukua hati za usalama dhidi ya moto.
Imetolewa na,


Kitengo cha Habari, Uhusiano na Elimu kwa Umma Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,

Makao Makuu.


DKT BASHIRU AGAWA MABATI 200 MANYARA

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru Ally akishiriki ujenzi wa ofisi ya CCM Tawi la Songambele Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, ambapo alichangia mabati 100.
Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally akizungumza na wanachama wa Tawi la Oloshonyokie Kata ya Naisinyai Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, baada ya kulizindua na kuchangia mabati 100.
……………………….
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt Bashiru Ally Kakurwa ameyapatia mabati 200 matawi ya CCM ya Oloshonyokie Naisinyai na Songambele Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, kwa ajili kujenga ofisi mpya za matawi hayo.

Dk Bashiru akizungumza na wanachama wa matawi hayo alisema mabati hayo 200 yanatolewa kupitia mfuko wa kuendeleza chama wa Mwenyekiti wao Rais John Magufuli.

Alisema uhai wa chama hicho unategemea wanachama waliopo kwenye matawi na mashina hivyo wanayaunga mkono ili kuendelea kuifanya CCM iwe karibu zaidi na wananchi.

Pia, aliwapongeza baadhi ya wadau wa maendeleo wa mji mdogo wa Mirerani, ambao ni wana CCM, Paul Mollel na Siria Mepukori kwa kila mmoja kuchangia sh500,000 ya ujenzi wa tawi la CCM Songambele na diwani wa kata ya Loiborsiret Ezekiel Lesenga (Mardad) alijitolea mifuko 20 ya saruji kwa tawi la Songambele.

Mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti alijitolea mifuko 100 ya saruji ya tawi la Songambele, mbunge wa jimbo la Simanjiro, James Ole Millya alijitolea mifuko 40 kwenye tawi la Oloshonyokie na mifuko 20 ya saruji katika tawi la Songambele.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Yefred Myenzi alisema yeye binafsi anachangia mifuko 10 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa tawi la CCM Songambele.

Mbunge wa jimbo la Simanjiro James Ole Millya alisema amewatafutia wadau na amewachangia kwani matawi yote ni ya kwake, Naisinyai yote ni CCM japo hapo Songambele diwani ni Chadema.Kada wa chama hicho Siria Mepukori alisema yeye ni mdau wa maendeleo na aliamua kumuunga mkono Dk Bashiru kwa sh500,000 ili kufanikisha ujenzi wa tawi hilo la Songambele.

Kada mwingine Paul Mollel alisema amechangia sh500,000 kwenye ofisi hiyo ya Songambele ili kumuunga mkono Katibu Mkuu wa CCM ambaye ana lengo zuri la kuhakikisha matawi yanajengwa.

RAIS DKT.MAGUFULI AMTEUA BW.JULIUS MTATIRO KUWA DC TUNDURU

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JULAI 14,2019


DIAMOND PLUTNUMZ ANAYETAMBA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA.

$
0
0

Na Moshy Kiyungi,Dar es Salaam.


Licha ya Nogwa na maneno ya kumchafua kwenye mitandao ya kijamii, Diamond Platnumz anaendelea ‘kutesa’ katika gemu la muziki wa kizazi kipya humu nchini na sehemu nyingine duniani.

Diamond amekuwa akisafiri kwenda kutumbuiza katika nchi za Bara la Ulaya, Falme za Kiarabu na Asia.Nyota ya msanii huyu inaonesha ipo juu mno kwa kuwa kila sehemu anakokwenda, anakubalika.

Hivi karibuni alimshirikisha mwanamuziki toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Fally Ipupa katika wimbo wa “Inama”, unaotamba katika baadhi ya vituo vya redio humu nchini na kwenye mitandao ya kijamii.

Kufuatia umri wake wa miaka 30 hivi sasa, yaelekea siku zijazo ataweza kufanya mambo makubwa mno hata ya kuitangaza nchi yetu kwenye safari zake nje ya nchi.Baada ya kuzaliwa October 02, 1989 katika Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam, alipewa majina ya Nasibu Abdul Juma.

Kwa bahati mbaya hakupata malezi ya baba na mama yake kwakuwa akiwa na umri mdogo, wazazi wake walitengana.Baba yake alimuacha bila msaada wowote ikabidi yeye na mama yake mzazi wahamie Tandale Magharibi kwa Nyanya yake mzaa mama, hapo ndipo yakawa makazi yao.

Historia yake ni ya kusikitisha kama alivyoelezea kwenye wimbo wa “Binadamu wabaya”.Mnamo mwaka 1995 alianza kupata elimu ya Checheka katika shule ya Chakula bora iliyopo Tandale Uzuri.

Diamond alipomaliza elimu hiyo, akajiunga na elimu ya msingi mwaka 1996 katika shule ya Tandale Magharibi, jijiniDar es Salaam. 

Ilipofika mwaka 2000 akiwa darasa la tano, Diamond alionekana kuanza kupenda sana muziki, hivyo alianza kukopi baadhi na kukariri nyimbo za wasanii waliokuwa ‘wakihit’ ndani na nje ya nchi kwa kipindi hicho.

Nasseb akawa anaziimba nyimbo hizo sehemu mbalimbali.Mama yake mara nyingi alikuwa akimnunulia kanda za album za Wasanii tofauti waliokuwa ‘wakihit’ kipindi hicho.Alidiriki hata kumuandikia baadhi ya nyimbo za wasanii hao ili mwanawe aweze kuzishika na kuimba kirahisi.

Mama huyo wakati mwingine alikuwa akimpeleka katika matamasha tofauti tofauti ya kuonesha vipaji, ili Diamond apate nafasi ya kuimba.Baadhi ya ndugu wa familia yao waliona kama mama yake anampotosha na kumuharibu mtoto huyo badala ya kumuhimiza kimasomo.

Maisha yao yalikuwa ni ngumu sana, kwakuwa mama yake Diamond hakuwa hana njia ya kumuingizia kipato, ilibidi atumie kiasi kidogo anachokipata toka kwa kodi ya vyumba viwili alivyopewa na mama yake yaani Nyanya yake Diamond.

Aidha alikuwa akifanya biashara zake ndogondogo kwa mikopo, ili aweze kumsomeshea na kumlea mwanawe Diamond.Hali ilivyozidi ‘kubana’, walilazimika wote kuhamia katika chumba cha Nyanya huyo, wakapangisha vyumba vile viwili alivyopewa mama Diamond.Baada ya kuhitimu shule ya msingi mwaka 2002, Diamond akataka kuanza masomo ya Sekondari mwaka 2003.

Mama yake alimshauri aachane na mambo ya muziki kabisa, azingatie masomo ili apate elimu itayomsaidia hata katika muziki wake.Mama huyo akamwambia haiwezekani kushika vitu viwili kwa pamoja muda huo.

Diamond akaanza masomo ya sekondari huku akiendelea kufanya muziki kisirisiri bila mama yake kumbaini. Ilipofikia mwaka 2004 taratibu akaanza kujifunza kuandika nyimbo zake mwenyewe.

Baada ya kuhitimu elimu yake ya Sekondari mwaka 2006, mwaka uliofuatia wa 2007 Diamond akajikita rasmi katika shughuri za muziki ili kujaribu kutimiza ndoto zake.Hali ya maisha kwa Diamond aliyoyapitia hayakuwa rahisi kama alivyokuwa akitegemea.Ilifikia muda akaanza kutafuta vibarua sehemu tofauti ili aweze kupata riziki na kuepuka hali ya kushinda nyumbani.

Diamond alipitia kazi ya kuuza mitumba, kuuza mafuta katika vituo vya Shell, kupiga picha, kupigisha simu na kazi za viwandani.Alilazimika wakati mwingine kuingia kwenye makundi ya kucheza kamali za mitaani ili aweze kupata pesa ya kuingia studio kurekodi nyimbo zake.

Juhudi zake hizo hazikuweza kuzaa matunda. Diamond akiwa na ari ya kufikia malengo yake, ilimlazimu kuuza pete ya Dhahabu ambayo alipewa na mama yake mzazi.Baada ya tukio hilo, akamdanganya mama yake kuwa pete hiyo ameipoteza!Alifanikiwa kupata ‘fungu’ lililomuwezesha kuingia studio kurekodi wimbo wa kwanza uitwao “Toka mwanzo”.

Ukosefu wa mazoea ya kurekodi, ulisababisha kushindwa kutengeneza wimbo ambao unao ‘hit’ wapenzi wa muziki.Kwa bahati njema kwake wimbo huo watu walishangazwa jinsi Diamond alivyoingia kwa mara ya kwanza studio na kuweza kutengeneza wimbo kama mtu ambaye ni mzoefu.

Baadhi yao wakaamini kuwa akipata nafasi ya kurekodi mara kadhaa, angeweza kufanya vitu vikubwa zaidi.Wimbo ule ulimfanya aweze kukutana na Chizo Mapene ambaye alijitolea kumsimamia, Wakaanza kurekodi album. Wakiwa katikati ya kurekodi album hiyo anayemsaidia kwa bahati mbaya alipata matatizo ya kifedha na hakuweza tena kumsaidia.

Diamond ilimbidi aanze upya kuzunguuka katika studio tofauti kuomba kusiniwa kwenye rekodi label.Lakini kote alikopita hakuweza kufanikiwa, wote walimwambia bado hajafikia kiwango cha kuimba, wakaacha kumsikiliza kabisa.

Kilikuwa ni kipindi kigumu sana maana hata yule mpenzi wake ambaye alikuwa naye, alimukimbia baada ya kuchoshwa na ndoto hewa za Diamond ambazo alikuwa akiziota kila siku kuwa ipo siku atafanikiwa kimuziki.

Ndoto za Diamond zilikuwa kuwa atakuja kuwa mwanamuziki mkubwa, yeye na mpenzi wake huyo wataishi maisha mazuri.’Kitendo cha mpenzi wake huyo kilimchanganya na kumuumiza sana Diamond hususan kwa kauli aliyomuambia ya "sikiliza Diamond mi kwa sasa siwezi kuwa na mwanaume ambaye hana maslahi kwangu".

Kutwa ilikuwa ikimpitia kwenye kichwa chake, akajiona kama mwenye mikosi.Mwaka 2009 Diamond alikutana na Bwana Msafiri Peter maarufu kama Papaa Misifa ambae alikubali kumsaidia kimuziki na Kurecord wimbo wa kwanza ulioenda kwa jina la "Nenda kamwambie".

Wimbo huo aliuimbia kwa uchungu mpenzi wake Sarah Sadiki, aliyemuacha akielezea kiasi gani aliumia kwa yeye kumuacha.“Mungu si Athumani” usemi huu ulijionesha baada ya nyota ya Diamamond kuaza kuchomoza taratiibu.

Nenda Kamwambie ulikuwa ikichukua chati siku hadi siku, maisha ya Diamond yakaanza kubadilika hadi kuweza kununua gari aina ya Toyota Celica.Februari 14, 2010 Diamond aliachia album yake ya kwanza iliyokuwa na nyimbo 10 za Kamwambie , Mbagala , Nitarejea , Nalia na mengi , Binadamu , Nakupa , Usisahau , Uko tayari , Wakunesanesa , Toka mwanzo na Jisachi.

Ilipotimu Aprili 04, 2010, aliweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza Tanzania kushinda tunzo tatu za Tanzania Kili Music Awards.Tuzo hizo za Msanii bora Chipukizi, Wimbo bora wa mwaka Kamwambie, na Wimbo bora wa R&. Tunzo hizo zilimfanya achaguliwe kuwa balozi wa Malaria nchini Tanzania. 

Baada ya kuachia wimbo wake wa pili unaoitwa Mbagala, Diamond alichaguliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa mshereheshaji katika kampeni za kuwania urais. 

Diamond Oktoba 02, 2010 alipata mwaliko wa kwanza kwenda nchi uingereza katika miji ya London, Milton Keynes na Coventry 

Msanii huyo baada ya kuachia wimbo wake wa tatu mwaka 2011, alishinda Tuzo ya Nzumari Award nchini Kenya, akiwa kama Msanii bora wa Kiume toka Tanzania. Diamond Platnumz alifytaua wimbo wake wa nne, akaweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza na pekee kujaza Club Maisha, hadi watu kushindwa kuingia.

Baadhi ya watu walizirai baada kutokupata hewa ya kutosha kutokana na kujaa kwa ukumbi kupita kiasi.Siku ya mwaka mpya Januari 01, 2012 Diamond Platnumz, aliachia album yake ya pili na kuweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza Tanzania kuuza zaidi ya kopi 1200,000 za album.

Wakati huohuo aliweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza Tanzania kufanya show ya Corporate, iliyoitwa “Diamonds are forever" iliyofanyika Mlimani City, kwa kiingilio cha shilingi elfu hamsini za Kitanzania kwa mtu mmoja.

Katika onesho hilo ambalo alilifanya akiwa msanii peke yake, ziliuzwa zaidi ya tiketi 1,500.Mnamo mwezi wa tano mwaka 2012 , Diamond Platnumz aliweka record ya kuwa msanii wa kwanza kufanya show na kujaza zaidi ya watu 10'000 kwa kiingilio cha 20,000 katika kiwanja cha Darlive huku akishuka na Helicopter kwenye Stage. 

Mwaka huohuo Diamond alifanya ziara yake ya Europe ikiwemo Italy, Holland,Sweden , Greece na kumalizia ziara yake ya arabuni. nchini Masqat Oman. Mwishoni mwa mwaka 2012 ulikua mzuri kwa Diamond Platnumz kwani aliweza kuachia nyimbo mbili kwa mpigo za "Nataka kulewa " na "Kesho " zilizoambata na video zake.

Mwezi wa kumi na mbili mwaka 2012 diamond alitajwa kuwa ni msanii wa kwanza anaelipwa Pesa nyingi kwenye Show toka Tanzania Mwanzoni mwa mwaka 2013, Diamond Platnumz alichaguliwa na Cocacola kuwa Brand Ambassador wa Kinywaji Cha Cocacol.

Diamond akafanya na ziara yake ya kuzitembelea nchi za Afrima Mashariki zikiwemo Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Kenya n.k.Aliweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza Afrika Mashariki kufanikiwa kupiga show pekeake kwenye uwanja na kujaza zaidi ya watu 30,000.

Mnamo June 2013 Diamond alishinda tuzo mbili za Tanzania Kili Music Award, akiwa kama Msanii bora wa kiume Bongoflavour na Msanii bora wa kiume kwa wanamziki wote Tanzania.Julai 2013, aliachia singo yake iliyokwenda kwa jina la Number One, ambayo aliifanyia Video katika mji wa Cape Town South, Afrika ya Kusini chini ya kampuni ya Ogopa Videos.

Nasibu Juma ‘Diamond’ akaweka rekodi ya kuwa msanii wa kwanza kuzindua video bila kiingilio katika Hotel ya Serena, akiwa amewaalika CEO's , Mameneja na viongozi toka sehemu tofauti tofauti. Katika uzundi huo akamzawadia gari aliyekuwa mwanamuziki mkubwa nchini, marehemu Muhidin Maalim Gurumo.

Oktoba 10, 2013, Diamond aliifanya Collabo na msanii toka Nigeria Davido katika ngoma ya Number One, ikiwa ni remix.Baadaye alikwenda nchini Nigeria kwaajili ya kusomea Soko la Afrika Magharibi, pamoga na kushoot video ya wimbo huo kupitia Kampuni ya Capital Dreams iliyo chini ya Director Clarence Peter. 

Wimbo huo ulimtambulisha Diamond Platnumz nchini Nigeria na barani Afrika kwa ujumla, ikamuwezesha kupata kra nyingi kwenye tuzo za kimataifa ikiwemo MTV MAMA.Tuzo ambayo alicheza wimbo huo mubashara akiwa na Davido.

Julai 07, 2014 Diamond wakati akisherekea siku ya kuzaliwa ya mama yake, alimzawadia gari pamoja na kuachia video mbili za Mdogomdogo, aliyoifanyia nchini Uingereza na BumBum, aliyomshirikisha Iyanya kutoka Nigeria aliyoifanyia Afrika Kusini.Video hizo kwa pamoja zilimgarimu Diamond dola 78,000 za Kimarekani.

NYOKA LONGO ‘ALITOSWA’ MAREKANI.

$
0
0

Na: Moshy Kiyungi,Tabora.

Kundi la wanamuziki wa bendi ya Zaiko Langa Langa, walimuacha kiongozi wao Nyoka Longo, wakutokomea wakiwa nchini Marekani.

Kwa mujibu wa habari zilizotangazwa na mwanamuziki nguli Tshimanga Kalala Assosa, kupitia redio moja humu nchini hivi karibuni, alisema wanamuziki hao walikuwa katika ziara ya kikazi katika mji wa Los Angles nchini humo.

Walikuwa katika maonesho kadhaa, baada ya onesho lao la mwisho, wanamuziki wote walitoweka kusikojulikana huku wakimuacha kiongozi wao Nyoka Longo, asijiue la kufanya.

Zaiko Langa Langa ni bendi iliyojizolea sifa tangu na bado inaendeleza umaarufu wao tangu kuanzishwa kwake miaka ya sabini, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Bendi hiyo ‘imewapaisha’ wanamuziki wengi ambao nao walijipatia umaarufu mkubwa wakiwamo akina Papa Wemba, Bozi Boziana, Dindo Yogo, Evolocko Jocker na Nyoka Longo wote ni kizazi cha Zaiko Langalanga.

Kama ilivyo Wenge Musica na makundi yake, Zaiko nayo imefanikiwa kuzaa bendi nyingi kama Isifi Lokole, Viva La Musica, Langa Langa Stars, Zaiko Familia Dei, Anti Choc, Choc stars, and Zaiko Nkolo Mboka.

Zaiko Langa Langa ilianzishwa rasmi mwaka 1970 wakati huo ikijulikana kama Orchester Zaiko, waanzilishi wakiwa ni Papa Wemba, Evolocko Lay Lay, Zamungana na Nyoka Longo.

Baadaye washabiki wakaanza kuwaita Langa Langa wakimaanisha ‘kulewa’ kwa kuwa nyimbo zao zilikuwa zikipigwa sana kwenye vilabu vya pombe kila kona.

Zaiko ndio waanzilishi wa sebene la leo ambapo wao walichukua mtindo wa kiasili na kuingiza ala kama magitaa, Chants, na rap kwa mbali jambo lililonogesha muziki wao na kuufanya kupendwa na rika lote.

Mwaka 1973 Zaiko walikuwa maarufu sana si tu kwa Zaire bali hata kwa nchi za jirani huku mwanamuziki wake Evolocko Jocker akiwa ni maarufu sana kwenye bendi hiyo ambapo aliweza kuingiza mtindo maarufu wa cavacha wa uchezaji ambao ulikuwa maarufu sana na kupendwa kote.

Miaka ya kati kati mwa sabini bendi hii ilianza kumong’onyoka ambapo waliondoka walikuwa wanamuziki wake maarufu kama Papa Wemba.

Wengine ni Bozi Boziana, Evolocko na Mavuela ambao kwa pamoja walianzisha Bendi iliyoitwa Isifi Lokole, ambayo hata hivyo haikukaa sana kwani nayo ilimeguka na kutoa bendi mbili Yoka Lokole, na Viva La Musica ya Papa Wemba.

Mwishoni mwa miaka ya sabini Bendi ilikuwa iko juu si mchezo huku wanamuziki wake wakiwa wanasifika kwa kila kitu, inakumbukwa wanamuziki kama Nyoka Longo, Lengi Lenga, Bimi Ombale, Dindo Yogo, Evolocko walileta laha sana kwenye bendi hii.

Ilienda mpaka miaka ya mwanzoni mwa 80 ambapo bendi ilimeguka tena. Hii ilitokana na wakongwe kama Meridjo, Nyoka Longo na Dindo Yogo kutokubaliana na mambo waliyoyaita mageuzi ambayo yaliletwa na vijana wapya kama Lengi Lenga, Ilo Pablo na Bimi Ombale.

Hii ilipelekea kusambaratika na kundi la akina Nyoka Longo likajiita Zaiko Langa Langa Nkolo Mboka, na lile la Bimi likajiita Zaiko Langa Langa Familia Dei.

Makundi yote kwa pamoja na mafanikio na mchango mkubwa kwenye ulimwengu wa muziki wa Kongo.

Mwisho.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba: 0767331200, 0736331200, 0784331200 na 0713331200.

Mbunge Mavunde amwaga vifaa vya uchaguzi Dodoma

$
0
0
Na Charles James, Michuzi TV

Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya Dodoma Mjini kimejipanga kuhakikisha kinapata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 kwa kuwafikia na kutatua kero,matatizo na changamoto zinazowakabili wananchi wake na pia kuwasimamia Viongozi wote wachaguliwa katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa CCMbna kutatua matatizo ya wananchi.

Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na Mwenyekiti wa CCM Wilaya Robert Mwinje wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya uenezi (Spika) na bendera kwa kata zote 41 vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

"Tunataka viongozi wote mliopo Serikalini na wawakikishi wa wananchi mnaotokana na CCM kuhakikisha mnatatua matatizo ya wananchi kuanzia ngazi ya chini kabisa ili tutengeneze uhalali kwa wananchi kuja kuwaomba ridhaa mwaka huu 2019 na mwakani 2020" amesema Mwinje

Akitoa maelezo ya awali,Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe Mavunde amesema kwamba vifaa hivyo alivyotoa leo kwa kila kata na Uongozi wa Wilaya wa Jumuiya Spika 45 zenye thamani ya Tsh 16,000,000 na bendera 1000 zenye thamani ya Tsh 3,500,000 ni maandalizi ya kampeni ya kisayansi ambayo wamepanga kuifanya katika Jimbo la Dodoma ili kuhakikisha CCM inashinda kwa kishindo katika uchaguzi huu wa serikali za Mitaa.

"Kupendeza kwetu kwa mashati ya kijani na kuimba kwetu vizuri nyimbo za CCM hakuna maana kama hatutakua Chama cha kujibu kero za wananchi. Nimejipanga vizuri kuhakikisha naendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuhakikisha Jimbo la Dodoma Mjini linaendelea kutoa kura nyingi kwa CCM katika uchaguzi wa Rais,Wabunge na Madiwani mwaka 2020.Rais Magufuli na CCM imetufanyia mambo makubwa sana hapa Dodoma hususani Jimbo la Dodoma Mjini shukrani yetu tutailipa kwenye sanduku la kura" amesema Mavunde

Wakati huo huo, Mbunge Mavunde ameahidi kutoa Tsh 20,500,000 kwa mgawanyo wa Tsh 500,000 kwa kata zote 41 katika kutunisha mfuko wa Uchaguzi wa Kata. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Viongozi wa Chama Wilaya na Viongozi wa Chama na Jumuiya zote kwa ngazi ya kata zote kwa Jimbo la Dodoma Mjini pamoja na Madiwani wa Kata na Viti Maalum.

Zanzibar International Film Festival (ZIFF) announces winners

$
0
0


Zanzibar International Film Festival (ZIFF) is East Africa’s largest film festival, exhibiting the latest and best films and promoting film talents from across the African continent, the Dhow countries and beyond.


For its 22nd edition it showed over 60 films from across Africa and the Dhow countries. Films were screened in Zanzibar’s ancient Stone Town, a UNESCO World Heritage Site, including in the open-air amphitheatre of the Old Fort, in Zan Cinema and in the Beach House.  



For each competition, the winner was selected by a jury of high-profile international film industry professionals, including:


Feature film jury:Lizelle Bisschoff (UK), lecturer in film and television studies at the University of Glasgow; Nadia Bulbulia (South Africa), executive Director of the National Association of Broadcasters South Africa; Peter Amina (UK), producer and director; and Mette Hjort(China) Chair Professor of Humanities and Dean of Arts at the Hong Konh Baptist University. 


Documentary film jury:Azza Elhosseiny (Egypt), director of Luxor African Film Festival; Amina Frense (South Africa) journalist, documentary filmmaker and executive producer; Salome Gregory (Tanzania) journalist for The Citizen Newspaper.


Short film jury:Mohamed Ghazala (Egypt) assistant professor of animation and the chair of the department of visual and digital production of Effat University, Saudi Arabia; Munier Parker (South Africa)filmmaker and producer from South Africa; Myriam Mouflih (UK) programmer, writer and filmmaker from Scotland.


Feature film winner:
Golden Dhow - Fatwa, dir. Mahmoud Ben Mahmoud, Tunisia 2018 


‘A poignant and powerful film with superb acting and impressive cinematography. The director succeeds in portraying the devastating effects of radicalisation in a seemingly liberal society. Relationships are layered and textured leaving the audience with a profound sense of despair and a reminder that society ought to nurture moderation if we are to stem extremism.’ – Nadia Bulbulia, jury member.    


Silver Dhow - The Skier, dir. Fereydoun Najafi, Iran 2018
Bronze Dhow - Subira, dir. Sippy Chadha, Kenya 2018 
 
Special mention: 
Expelling, dir. Geng Changqing, China 2018 
Indigo, dir. Selma Bargach, Morocco 2018



Short Film winner: Sega, dir. Idil Ibrahim 2018, Senegal 

Special mention: Nada, dir. Adel Ahmed Yehia, 2017, Egypt 


Documentary winner: Someone to Blame - The Ahmed Timol Inquest, dir. Enver Samuel, 2018, South Africa


Media Contact: For further information, screeners, press tickets, hi-res images and interviews please contact: ziff@ziff.or.tz
Notes: 

For full programme please see ZIFF 2019 website: https://ziff2019.org/wp/ Project.




Mbio za hisani za Zanzibar Charity Marathon zafana

$
0
0
Na Andrew Chale, Zanzibbar

Watu zaidi ya 600 washiriki mbio za hisani za kuchangia malezi na elimu kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu kupitia Shirika la SOS Children’s Villages Zanzibar.

Awali mbio hizo zilizoanzia Ngome Kongwe majira ya asubuhi, washiriki hao kutoka maneo mbalimbali Zanzibar na nje ya Zanzibar wameweza kuanza na kumaliza huku wakipata medali za ushiriki.

Akizungumza na tuko Media, Mratibu wa mbio hizo David Lyamuya amesema kwa mwaka huu ni za mara ya kwanza na watu wadau wameonesha muitikio mkubwa wakiwemo wakimbiaji kutoka Arusha na maeneo mengine pamoja na wageni.

“Makampuni na mashirika ya hapa Zanzibar kwa ujumla wao wameweza kushiriki mbio hizi za kusaidia walio kwenye mazingira magumu. Tunawapongeza sana na watu wengine kwa kuchangia mbio kwani makusanyo yote ni kwa ajili ya watoto wetu.” Alieleza Lyamuya.

Lyamuya ameongeza kuwa, mbio hizo zinaongeza ufahamu wa malezi na ulinzi wa mtoto, kuimarisha mwili na pia kusaidia watoto na vijana ambao wamepoteza au ambao wapo katika hatari ya kupoteza malezi na uangalizi wa wazazi. Tunapenda kujivunia kwa kila mmoja aliyeshiriki kukimbia mbio hizi” alieleza Lyamuya.

Katika mbio hizo washiriki wote wameweza kukimbia mbio hizo na kumaliza ikiwemo mbio za Kilometa 5, Kilometa 10 na za Kilometa 21 zilizoanzia Ngome Kongwe na kuelekea SOS Mombasa kisha uwanja wa ndege, kilimani na kurejea kwenye viunga hivyo vya Ngome Kongwe.

Aidha, aliongeza kuwa SOS Children Village Zanzibar imeweza kujivunia kuweka mchango chanya katika ukuaji na ustawi wa watoto waishio kwenye mazingira hayo magumu zaidi kwani bado wanaweza kutimiza ndoto za kupitia fursa na elimu iliyo bora. 

Shirika hilo la SOS Children’s Villages Zanzibar kwa visiwani hapa lipo Unguja na Pemba limejikita katika kutoa malezi na ulinzi wa watoto, kwa sasa shirika lina hudumia watoto 186 katika kijiji cha SOS kilichopo Mombasa Unguja na watoto na vijana 1920 waliopo katika miradi ya kuimarisha familia.

Shirika hilo linauzoefu wa zaidi ya miaka 27 katika melezi ya mtoto haswa wale walio kwenye mazingira magumu,kuiimarisha familia kwa ajili ya kuepusha kutojali na utelekezaji wa watoto na mambo mengine mengi.

Kwa sasa, shirika hilo pia inatekeleza miradi katika maeneo mbalimbali ya Pemba, Unguja, Mwanza, Arusha, Dare Salaam, Mufindi, Iringa, huku miradi iliyowafikia watoto na vijana 5,236 na kuboresha familia 1215.






LONGRICH INTERNATIONAL INAYOFANYA BIASHARA MTANDAONI YATAMBULISHWA RASMI NCHINI

$
0
0
Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

Kampuni kutoka nchini China inayojishughulisha na masuala ya Bishara Mtandaoni imetambulishwa rasmi nchini Tanzania na kwa Watanzania kwa ujumla.

Longrich Internaltional yenye miaka 33 tangu kuzinduliwa ambapo Makao Makuu yake yapo nchini China imekuja nchini kutoa fursa katika suala la Biashara ya Mtandaoni.

Akizungumza wakati wa utambulisho wa Kampuni hiyo, Afisa Tarafa wa Wilaya ya Ilala, George Anthony amesema Serikali ya Tanzania ipo kwenye mkakati wakuvutia Wawekezaji na Biashara, amesema wanaikaribisha Longrich huku akisema Serikali inaahidi kuwa bega kwa bega kuweka mazingira sahihibya kufanya biashara.

Amewaomba Longrich wasiifanye Tanzania kama Soko, ametoa wito kwa Kampuni kama hizo kuja kuwekeza Viwanda vya Uzalishaji wa bidhaa zao hapa Tanzania, kama Serikali inavyojipambanua kuwa ya Viwanda.

Kwa Upande wake, Meneja wa Longrich Tanzania, Pino Zhang amesema Longrich ni moja ya Kampuni kubwa nchini China iliyo katika 10 Bora za Kampuni zilizopo nchini humo, amesema Longrich International ina matawi Ulimwenguni kote sio Tanzania pekee, pia ina Matawi katika nchi za Ghana, Afrika Kusini, Zambia, Kenya, Rwanda na Ivory Coast.

Balozi wa Kampuni hiyo, Flora Vitalis amesema kuwa Longrich imeleta bidhaa za Mimea Asili kwa Watanzania, amesema tayari wamefungua milango kwa Watanzania wengi kujipatia bidhaa hizo zenye ubora, kama vile Taulo za Kike, Viatu.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Malkia wa Nguvu Tanzania, Grace Mpanduka ametoa wito kwa wanawake kutunza ngozi zao kwa kutumia bidhaa hizo za Mimea asilia kwani zina ubora wa hali ya juu.
Afisa Tarafa wa Wilaya ya Ilala, George Anthony (kulia) akizngungumza na waandishi wa bahari wakati wa utambulisho wa kampuni Longrich kutoka nchini China inayojishughulisha na masuala ya Bishara Mtandaoni leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)
Afisa Tarafa wa Wilaya ya Ilala, George Anthony (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Meneja wa Longrich Tanzania, Pino Zhang mara maada ya utambulisho wa kampuni hiyo kutoka nchini China inayojishughulisha na masuala ya bishara mtandaoni leo jijini Dar es Salaam. katika ni Mwenyekiti wa Chama cha Malkia wa Nguvu Tanzania,Grace Mpanduka
Afisa Tarafa wa Wilaya ya Ilala, George Anthony (kulia) akimkadhi zawadi mmoja wa washindi walio jishindia zawadi mbalimbali katika hafla ya utambulisho wa kampuni Longrich kutoka nchini China inayojishughulisha na masuala ya bishara mtandaoni leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Malkia wa Nguvu Tanzania, Grace Mpanduka wa (kwanza kuli) amewaomba wanawake kutunza ngozi zao kwa kutumia bidhaa za kampuni hiyo ambazo zinatengengenezwa kwa Mimea asilia kwa ubora wa hali ya juu.
washindi walio jishindia zawadi mbalimbal wakisoma vipeperushi mbalimbali leo katika afla ya utambulisho wa kampuni Longrich kutoka nchini China inayojishughulisha na masuala ya bishara mtandaoni leo jijini Dar es Salaam.
mkutano ukiendelea
Baadhi ya wangeni waliofika katika hafla ya utambulisho wa kampuni Longrich wakinunua bidhaa mbalimbali zinazo tengenezwa na kampuni hiyo.
picha ya pamoja

BENKI YA EXIMTANZANIA YASHIRIKI KIKAMILIFU MKUTANO MKUU WA KIMATAIFA WA WADAU WA KOROSHO MKOANI MTWARA.

$
0
0
Wafanyakazi wa Benki ya Exim Tanzania wakiwahudumia wateja waliotembelea banda la huduma za benki hiyo kwenye Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Wadau wa Korosho uliofanyika mkoani Mtwara mwishoni mwa wiki. Benki hiyo ni miongoni mwa wadau wakubwa wa zao la korosho hapa nchini ambapo imekuwa ikitoa huduma mbalimbali za kifedha kwa wakulima na wafanyabaishara wa zao hilo.
Wafanyakazi wa Benki ya Exim Tanzania wakiwahudumia wateja waliotembelea banda la huduma za benki hiyo kwenye Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Wadau wa Korosho uliofanyika mkoani Mtwara mwishoni mwa wiki. Benki hiyo ni miongoni mwa wadau wakubwa wa zao la korosho hapa nchini ambapo imekuwa ikitoa huduma mbalimbali za kifedha kwa wakulima na wafanyabaishara wa zao hilo.

Mavunde aungana na CWT Dodoma kuhamasisha utalii wa Ndani

$
0
0


 Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule za Wilaya ya Dodoma wakati walipotembelea michoro ya Male Kondoa.
 Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Mhe Anthony Mavunde na walimu wa shule za Wilaya hiyo wakipata maelekezo kwenye michoro ya Malikale wilayani Kondoa wakati wa ziara yao ya kutembelea vivutio vya ndani.




Na Charles James

Chama cha Walimu (CWT) Jiji la Dodoma kimewataka Watanzania kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya Utalii ili kukuza Utalii wa ndani hapa nchini Tanzania katika kumuunga Mkono Rais Dr John Pombe Joseph Magufuli kwenye azma yake ya kuhakikisha sekta ya Utalii inakua na kuchangia pato la Taifa na kuliingizia Taifa fedha nyingi za kigeni.

Hayo yamesemwa na Katibu wa CWT Wilaya ya Dodoma Mjini, Kelvin Mahundi kwa niaba ya walimu wenzake wakati wa ziara fupi ya Mafunzo katika Kituo cha Mali kale cha Michoro ya Miambani Wilayani Kondoa-Dodoma ambapo walimu hao kwa umoja wao walimshukuru Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Mhe Anthony Mavunde kwa kugharamia ziara yao ambapo wamewataka Watanzania kuonesha uzalendo kwa kutembelea vivutio vilivyopo nchini.

Kwa upande wake Mhe Mavunde ameungana na walimu hao kutoa wito kwa Jamii ya Watanzania kujiwekea utaratibu wa kutembelea vivutio vya Utalii kama ambavyo yeye aliona umuhimu wa kuwapeleka walimu wa Jiji la Dodoma kwenda kujifunza mambo ya Mali kale katika Michoro ya miambani-Kolo Kondoa.

"Hapa Kolo,Kondoa ni eneo zuri la kujifunza kuhusu historia na utamaduni wa jamii ya watu wanaoishi eneo hili kupitia hapa Kituoni.Awamu ya kwanza niliamua kuwaleta walimu na awamu ya pili sasa nitawaleta wanafunzi ili waje wajifunze nao pia.Nitaendelea kuwa Balozi mzuri katika kuhamasisha watu waje waone urithi huu wa Dunia kupitia michoro ya kwenye miamba hapa Kolo-Kondoa"Amesema Mavunde.

MIRADI YA MAJI YENYE WAKANDARASI WABABAISHAJI KURUDISHWA WIZARANI.

$
0
0

Anaandika Abdullatif Yunus wa Michuzi TV - Kagera.

Serikali kupitia Wizara ya Maji imesema haitakuwa tayari kuendelea kufanya kazi na Wakandarasi wasiokamilisha miradi ya Maji kwa wakati, badala yake wamekuwa hodari wa kuomba kulipwa pesa nyingi kabla ya utekelezaji wa Miradi husika.

Tamko hilo limetolewa na Waziri mwenye dhamana Profesa Makame Mabarawa Akiwa Wilayani Kyerwa akitokea Wilaya ya Karagwe katika ziara ya kikazi ambapo amesema kuwa, kwa miradi ya Maji Nchini ambayo inasua sua au imeshindwa kutoa Maji kama ilivyotarajiwa, Wakandarasi wataondolewa na Wizara yenyewe itahusika kutafuta Wakandarasi wapya wa kumalizia Miradi hiyo, tofauti na sasa ambapo Miradi inasimamiwa na Halmashauri au Mamlaka za Maji.

Akiwa Wilayani Kyerwa Mkoani Kagera, Waziri wa Maji Profesa Mbarawa ametembelea na kuijonea Ukarabati na Upanuzi wa Mradi wa Maji Mabira ambao ulianza kutekelezwa tangu Mwaka 2017 na Mkandarasi M/S Vumwe General Service and Supply Co.Ltd.

Mradi huo unaogharimu kiasi cha shilingi 586,747,480.00 unaosimamiwa na Halmashauri ya Wilaya Kyerwa, wenye lengo la kuhudumia wananchi wapatao 23,000 kufikia 2022, ulitakiwa kukamilika kwa sasa upo katika 80% na Mkandarasi tayari amelipwa zaidi ya Milioni 200.

Kufuatia hatua hiyo Waziri Mbarawa amemuagiza Mhandisi wa Mkoa pamoja na Uongozi wa Halmashauri kutolipa kiasi kilichosalia mpaka kazi yote itakapokamilika kwa wakati, kwani Makandarasi wengi wamekuwa wakishindwa kumaliza kazi kwa wakati na huku wakidai kulipwa kiasi kikubwa cha pesa. Waziri Mbarawa yupo Kagera kwa ziara ya kikazi ya kutembelea na Kukagua Miradi ya Maji, baada ya Kuhitimisha ziara hiyo Wilayani Kyerwa sasa Yupo Wilayani Ngara.
Pichani Waziri Wa Maji Profesa Makame Mbarawa akifungulia maji katika mradi wa Maji Mabira uliokamilika Kwa 80% unaoendelea kukarabatiwa na kupanuliwa ili kukidhi mahitaji ya Wananchi 23,000 ifikapo 2022.
Kazi ni moja kumtua Mama ndoo kichwani, kama anayoonekana Waziri wa Maji Profesa Mbarawa akifanya tendo hilo baada ya kujiridhisha na hatua ya mradi wa Mabira Nyamilima Wilayani Kyerwa ulipofikia.
Pichani Waziri wa Maji Profesa Mbarawa akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Rashid Mwaimu, Mhandisi wa Maji Mkoa wa Kagera Avitus Exavery wakielekea kwenye Mradi wa Maji.
Pichani Waziri Mbarawa akionyesha moja kati ya Bei za vifaa vya mradi wa Maji kutoka Kiwandani, wakati akilinganisha na bei za mradi wa Maji Mabira uliopo Wilaya ya Kyerwa, alipotembelea mradi katika ziara yake.
Pichani ni tanki la Maji la Mradi wa Maji Mabira, unaosambazia Maji vijiji sita vya Rushe, Mabira, Omkagando, Kibimba, Makazi na Nyakatete wenye Gharama zaidi ya Shilingi Milioni 580, ukiendelelea kukarabatiwa na Kupanuliwa.

MAJALIWA AKABIDHI MSAADA WA SH. MILIONI 2.5 KWA MJASIRIAMALI WA KIGOMA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Bw. Leonard Nkamba wa kijiji cha Kambanga wilayani Kasulu msaada wa sh. milioni 2.5 ili zimwezesha kununua vitendea kazi vya kisasa vya kumsadia kufanya kazi yake ya kuchonga vyombo mbalimbali vya mezani kwa kutumia miti. Makabidhiano hayo yalifanyika mjini Kigoma Julai 24, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAOGELEAJI TANZANIA MORALI JUU,TSA YAIPONGEZA MOTISUN

$
0
0
Mkurugenzi wa kapuni ya Motisun Group Pawan Patel (wa pili kulia) akimkabidhi mfano wa hundi Katibu Mkuu wa Chama Cha Kuogelea Tanzania Inviolata Itatiro kwa ajili yakusaidia maandalizi ya timu ya Taifa itakayoshiriki mashindano ya kuogelea ya Dunia yaliyopangwa kufanyika mjini Gwangju, Korea Kusini.Kulia ni Meneja Mkuu wa Kampuni ya Sayona Drinks Nitin Menon na kushoto ni Maneja wa Masoko Erhard Mlyansi 
……………….. 
Na Mwandishi wetu 
Dar es Salaam. Waogeleaji wa Tanzania wanatarajia kuondoka nchini kesho kwenda Korea Kusini kwa ajili ya kushiriki katika mashindano ya Dunia. 
Safari hiyo itajumuisha waogeleaji wanne, Hilal Hemed Hilal, Collins Saliboko ambao watashindana kwa upande wa wanaume na Sylvia Caloiaro na Shivan Bhatt ambao watashindana kwa upande wa wanawake. 

Hilal na Collins watasafari mpaka Dubai na kukutana na waogeleaji wa kike, Sylvia Caloiaro na Shivan Bhatt ambao walikuwa wanafanya kambi ya mazoezi hapa nchini chini ya kocha Alex Mwaipasi na Michael Livingstone. 
Waogeleaji hao wapo morali ya juu baada ya kampuni ya Motisun Group kukabidhi mchango wao wa dola za kimarekani 2,000 (Sh 5 million) ili ziwasaidie katika mahitaji mbalimbali ya mashindano hayo. 

Meneja Mkuu wa kampuni ya Sayona Drinks Limited, Nitin Menon alikabidhi kiasi hicho cha fedha kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Kuogelea Nchini (TSA), Inviolata Itatiro na kuwaomba waogeleaji hao kupambana vilivyo kwa ajili ya Taifa. 

Menon alisema kuwa waogeleaji hao wanatakiwa kutambua kuwa Watanzania zaidi ya milioni 45 wanasubiri kuona matokeo mazuri kutoka kwao pamoja na ugumu wa mashindano. 

Alisema kuwa Motisun Group inajisikia fahari kubwa kuwa mdau wa michezo na kuahidi kuendelea kufanya hivyo nchini. “Naomba mkafanya vizuri katika mshindano haya na kuendelea kuleta hamasa kwa wanamichezo nchini, tupo pamoja nanyi katika kuendeleza gurudumu la maendeleo ya michezo nchini,” alisema Menon. 

Alisema kuwa hiyo si mara yao ya kwanza kusaidia michezo kwani waliweza kusaidia kambi ya timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars iliyokuwa inajiandaa na mashindano ya Afcon na pia kusaidia fainali za vijana wa chini ya miaka 17 za Afcon zilizofanyika hapa nchini. 

Katibu Mkuu wa TSA, Inviolata Itatiro aliipongeza kampuni hiyo na kuziomba kampuni nyingine kusaidia mchezo huo. “Ni fahari kwetu kuona Motisun Group imefungua njia. Bado tunahitaji msaada kutoka kwa wadau ili kufanikisha zoezi zima la kuwasafirisha waogeleaji wetu kwenda Korea,” alisema Inviolata.

SAKATA LA KODI YA PANGO LA ARDHI LAZIDI KUWA CHUNGU KWA BAADHI YA KAMPUNI MWANZA

$
0
0

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza na Mmiliki wa shule za Musabe zilizoko mkoani Mwanza Daniel Musabe wakati wa oporesheni ya kufuatilia wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi katika mkoa wa Mawanza mwishoni mwa wiki. Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizarani Denis Masami na wa tatu kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa shule za Musabe Faustine Magabilo. 
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akihakiki deni la kodi ya pango la ardhi la kampuni ya Birchard Oil Limited pamoja na Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo Arshad Jetha (kushoto) wakati wa oporesheni za kuwatembelea wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi katika mkoa wa Mawanza mwishoni mwa wiki. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizarani Denis Masami. 
Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Ziwa Makwasa Biswalo (wa tatu kulia) akifafanua jambo kwa Meneja wa Kampuni ya Ideal Development Ltd Burnanuddin Rajbhai (wa kwanza kushoto) wakati Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alipoitembelea kampuni ya Ideal Development Limited katika operesheni ya kufuatilia wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi katika mkoa wa Mwanza mwishoni mwa wiki. Wa pili kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi Dorothy Mwanyika na wa pili kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizarani Denis Masami. 
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akihakiki deni la kodi ya pango la ardhi la kampuni ya Jesse and Company Ltd wakati wa oporesheni ya kufuatilia madeni ya kodi ya pango la ardhi katika mkoa wa Mawanza mwishoni mwa wiki. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Jesse and Company ltd Sundeep Bachu. 
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiagana na Afisa Mfawidhi wa Maabara ya Taifa ya Udhibiti Samaki na Mazao ya Uvuvi Emanuel Mundoko wakati wa oporesheni ya kufuatilia madeni ya kodi ya pango la ardhi katika mkoa wa Mawanza mwishoni mwa wiki. 
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akimpa maelekezo Meneja Rasilimali Watu wa kapmuni ya Synergy Tanzania Ltd ( wa kwanza kulia) wakati wa oporesheni ya kufuatilia wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi katika mkoa wa Mawanza mwishoni mwa wiki. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizarani Denis Masami. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI). 
……………………… 
Na Munir Shemweta, WANMM MWANZA 
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amezidi kuzibana Taasisi na Makampuni yenye madeni makubwa ya kodi ya pango la ardhi ambapo ametua mkoani Mwanza na kuyabana makampuni na taasisi nane ambazo kwa ujumla wake zinadaiwa zaidi ya milioni 900. 

Kampuni na taasisi alizotembelea Dkt Mabula ni Synergy Tanzania Ltd, Ideal Development Ltd, Birchard Oil Ltd, Shule za Musabe, Taasisi ya Taifa ya Utafiti Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Ndamavyo Auto Spares, Jesse & Company Ltd na Maabara ya Taifa ya Udhibiti Samaki na Mazao ya Uvuvi. 

Akizungumza katika ziara yake hiyo ya kufuatilia madeni ya kodi ya pango la ardhi mwishoni mwa wiki, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alisema ziara hiyo anayoifanya ya kuwafikia wale wenye madeni makubwa inafuatia baadhi ya kampuni na taasisi zinazodaiwa kushindwa kulipa ama kurekebisha madeni yao baada ya kikao cha Juni 11, 2019 kilichowakutanisha wadaiwa zaidi ya 200 jijini Dodoma
 
katika mwanzo wa ziara yake kwenye shule za Musabe, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alimueleza mmiliki wa shule hizo Daniel Musabe kulipa deni lake la kodi ya pango la ardhi linalofikia milioni 57.4 katika viwanja vyake vinne anavyomiliki kufikia tarehe 31 Julai 2019 ili kuepuka kufikishwa katika Baraza la Ardhi na Nyumba. 

Hata hivyo, Mmiliki wa Shule hizo ambazo ni za Chekechea, Msingi na Sekondari alimueleza Dkt Mabula kuwa yuko tayari kulipa deni la kodi ya pango la ardhi lakini alishindwa kufanya hivyo kutokana na changamoto za kibiashara ambapo hata hivyo aliahidi kulipa kiasi anachodaiwa kuanzia Agosti 2019 na kumaliza deni lote ifikapo Desemba 2019. 

Akiwa katika Kampuni ya Birchard Oil Limited, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Mabula ambaye aliambatana na Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizarani Denis Masami aliitaka kampuni hiyo kulipa kiasi inachodaiwa cha kodi ya pango la ardhi inayofikia milioni 85,235,050 ikiwa ni pamoja na malimbikizo ya kodi za miaka ya nyuma. 

Meneja uhusiano wa Kampuni hiyo inayojishughulisha na uzalishaji Mafuta na Marobota ya Pamba Arshad Jetha alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi kuwa kampuni yake pamoja na kudaiwa kodi ya pango la ardhi kwa baadhi ya viwanja inavyomiliki lakini baadhi yake alishalipia hivyo aliomba kuhakikiwa madeni yake ili kupata deni halisi. 

Ideal Development Ltd kupitia Meneja wake Burnanuddin Rajbhai alikiri deni la kodi ya pango la ardhi linalofikia milioni 79 na kuomba kupewa muda wa kulipa katika awamu tatu tofauti. Hata hivyo, Naibu Waziri wa Ardhi alizitaka kampuni na Taasisi zilizokubali kulipa madeni kuandika barua ya kueleza namna zitakavyolipa na muda wa mwisho wa kulipa madeni yao katika ofisi za ardhi za halmashauri husika na nakala za barua hizo ziende ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi wa Kanda ya Ziwa. 

Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Ziwa Makwasa Biswalo aliionya kampuni ya Ideal Development Ltd kwa kushindwa kutekeleza makubaliano yaliyofikia ya kulipa deni lake na kuieleza kuwa hatua itakayofuata kwa kampuni hiyo ni kufikishwa katika Baraza la Ardhi na suala la kuingia makubaliano ya malipo haliwezi kufanyika kwa mara ya pili. 

Kampuni ya Synergy Tanzania Ltd Kupitia kwa Meneja Utawala wake Florence Kivamba iliahidi kuandika barua ya makubaliano ya kulipa deni la milioni 43 inayodaiwa ingawa alioamba kufanya mawasiliano na uongozi wa juu kwa kuwa ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi ilikuwa ya kushtukiza na uongozi haukuwepo. 

Akiwa katika Taasisi ya Taifa ya Utafiti Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Mabula aliueleza uongozi wa Taasisi hiyo kuwa inadaiwa jumla ya shilingi milioni 515,713,900 ya kodi ya pango la ardhi na taasisi hiyo haijawahi kulipa kodi hiyo tangu mwaka 1996. 

Mkurugenzi wa NIMR mkoa wa Mwanza Safari Kinuhi alijitetea kwa kueleza kuwa taasisi yake inapaswa kusamehewa kulipa kodi ya pango la ardhi kwa kuwa haiko kibiashara bali inatoa huduma kwa wananchi na kuboresha afya ingawa aliahidi kuwasiliana na uongozi wa juu kuhusiana na suala hilo. 

Hata hivyo, Dkt Mabula alimueleza kuwa Taasisi yake inapaswa kufuata sheria wakati wa kuomba kusamehewa kodi ya pango la ardhi huku Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizarani Denis Masami akisisitiza kuwa hata kama Taasisi hiyo itasamehewa kulipa kodi hiyo lakini deni la nyuma lazima lilipwe kwa kuwa sheria ya msamaha itaanza pale tamko la msamaha lilipotoka. 

Maabara ya Taifa ya Udhibiti Samaki na Mazao ya Uvuvi iliyopo eneo la Nyegezi ilionekana kutokuwa na hati ya eneo inalomiliki ingawa Afisa Mfawidhi wa Taasisi hiyo Emanuel Mundoko alijitetea kwa kueleza kuwa awali Taasisi hiyo ilikuwa sehemu ya chuo cha Uvuvi na sasa inajitegemea hivyo hawajui madeni halisi wanayodaiwa.
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images