Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

WAZIRI LUGOLA AONGOZA KIKAO CHA TUME YA UTUMISHI WA POLISI, UHAMIAJI NA MAGEREZA JIJINI DODOMA

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na Wajumbe  wa Tume ya Utumishi ya Polisi, Uhamiaji na Magereza wakati wa kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na Wajumbe  wa Tume ya Utumishi ya Polisi, Uhamiaji na Magereza (hawapo pichani), kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo Meja Jenerali Jacob Kingu.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu,akifafanua jambo mbele ya Wajumbe  wa Tume ya Utumishi ya Polisi, Uhamiaji na Magereza (hawapo pichani), wakati  wa  kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara. Kulia  ni Waziri wa wizara hiyo Kangi Lugola. Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia),Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Meja Jenerali Jacob Kingu na Kamishna wa Polisi Benedict  Wakulyamba, wakipitia vitabu wakati wa kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.
 Kamishna wa Magereza, Faustine Kasike  akizungumza wakati wa Kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kulia ni Kamishna wa Uhamiaji Dk. Anna Makakala.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.
 Kamishna wa Uhamiaji ,Dk. Anna Makakala akizungumza wakati wa kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kushoto  ni Kamishna wa Magereza  Faustine Kasike.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.
Kamishna wa Polisi, Benedict Wakulyamba akizungumza wakati wa kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

CGF ANDENGENYE APOKEA MSAADA WA VIFAA VYA KUZIMIA MOTO NA MAOKOZI

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, CGF Thobias Andengenye, amepokea msaada wa vifaa vya kuzimia moto na maokozi vitakavyotumika kwa shughuli mbalimbali za Jeshi hilo.

Amepokea msaada huo mapema hii leo Makao Makuu Ndogo ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam, kutoka kwa Kampuni ya Wilna International Japan.
Hata hivyo, Andengenye ameishukuru Kampuni hiyo kwa kutoa msaada huo na kushirikiana na Jeshi hilo katika Kuokoa Maisha na Mali za Watanzania.   
Aidha, Mwakilishi wa Kampuni ya Wilna International Japan, Bw. Martin Chuwa, amesema kuwa wameamua kutoa msaada huo wa vifaa vya kuzimia moto na maokozi ili kurahisisha utendaji kazi wa Jeshi hilo.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, (CGF) Thobias Andengenye, akipokea Sare za kuzimia moto (Fire suite), kutoka kwa Mwakilishi wa Kampuni ya Wilna International Japan, Bw. Martin Chuwa. Vifaa hivyo vimepokelewa Makao mapema hii leo Makuu Ndogo ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, (CGF) Thobias Andengenye, akipokea Mikanda maalum kwa ajili ya maokozi (Rescue Belt), kutoka Mwakilishi wa Kampuni ya Wilna International Japan, Bw. Martin Chuwa. Vifaa hivyo vimepokelewa mapema hii leo Makao Makuu Ndogo ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya vifaa vya kuzimia moto na maokozi vilivyotolewa na Kampuni ya Wilna International Japan na kukabidhiwa kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa Lengo la kuboresha utendaji kazi. (Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)

RAIS KENYATTA AMTUMIA UJUMBE RAIS DKT. MAGUFULI

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dany Kazungu, ofisini kwa Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es salaam, Julai 2, 2019. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dany Kazungu, ofisini kwa Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam, Julai 2, 2019. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea ujumbe maalum wa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya kwa naiba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, kutoka kwa Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dany Kazungu, ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Julai 2, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
…………………………. 
*Ni kuhusu kuchukizwa kwake na kauli ya Jaguar 

RAIS wa Kenya, Uhuru Kenyatta amemtumia ujumbe maalumu Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli unaoelezea msimamo wa Serikali yake kuhusu kukerwa na matamshi yaliyotolewa hivi karibuni na Mbunge wa jimbo la Starehe, Charles Njagua Kanyi maarufu kwa jina la Jaguar. 

Ujumbe huo wa maandishi umewasilishwa leo (Jumanne, Julai 02, 2019) na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dany Kazungu na kupokelewa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa niaba ya Rais Dkt. Magufuli, ofisini kwa Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar Es Salaam. 

Akipokea taarifa hiyo Waziri Mkuu amesema Watanzania wamefurahishwa na hatua mbalimbali zilizochukulia na Serikali ya Kenya dhidi ya mbunge huyo zinazodhihirisha kwamba matamshi hayo hayakuwa msimamo wa Serikali ya Kenya wala wananchi wake bali ulikuwa ni msimamo binafsi wa mbunge huyo. 

Amesema siku zote Watanzania na Wakenya wamekuwa huru kuishi na kufanya kazi au biashara katika nchi za Afrika ya Mashariki na pale yalipotokea matatizo au kutokukubaliana serikali husika zilikaa mezani na kumaliza tofauti hizo. 

“Uhusiano kati ya Kenya na Tanzania ni wa karibu mno na wa kidugu kwani kuna baadhi ya makabila yapo katika nchi mbili hizi kama vile Wamasai na Wakurya na Wajaluo hivyo ushirkiano katika masuala ya mbalimbali yakiwemo ya kabiashara na ya kijamii haukwepeki.” 

Hivyo, Waziri Mkuu ametoa wito kwa viongozi na wananchi wa nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki kujiepusha na kauli zenye viashiria vya kujenga chuki, uhasama na migongano miongoni mwa wananchi kwani kauli hizo zisipodhibitiwa mapema zinaweza kusabisha hofu na kutokuelewana miongoni mwao. 

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasihi Watanzania kuendelea kuishi kwa amani na upendo na ndugu zao wa Kenya na wageni wote kutoka nchi za Afrika ya Mashariki na duniani kwa ujumla ambao wapo nchini wakifanya shughuli mbalimbali kwa mujibu wa sheria za nchi. 

“Mambo yetu yote katika nchi za Afrika ya Mashariki hasa ya biashara na ya kiuchumi kwa ujumla yataenda vizuri endapo tutalinda na kudumisha amani, bila amani tutaogopana na tutashindwa kabisa kushirikiana”, amesisitiza Mheshimiwa Majaliwa. 

Waziri Mkuu ameahidi kuwa Serikali ya Tanzania kamwe ahaitaruhusu wala kufumbia macho kauli au vitendo vyovyote vyenye viashiria vya uchochezi dhidi ya nchi jirani ili na kulinda na kuunga mkono juhudi mbalimbali za ushirikiano wa kisiasa na kiuchumi zinazofanywa na viongozi wakuu wa Mataifa ya Afrika. 

Kwa upande wake Balozi Kazungu amemshukuru Waziri Mkuu kwa kauli yake aliyoitoa Bungeni jijini Dodoma iliyowataka Watanzania kuwa watulivu na wayachukulie matamshi ya Mbunge wa jimbo la Starehe nchini Kenya, Njagua kuwa ni msimamo wake binafsi na siyo msimamo wa Wakenya na Serikali yao. 

Balozi Njagua mesema Msimamo wa Rais Kenyatta siku zote umekuwa ni kuwapokea na kuwakubali ndugu zao wote wanaotoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki walioamua kuishi au kufanya biashara nchini Kenya. 

Mwanzoni mwa wiki iliyopita Mbunge wa jimbo la Starehe nchini Kenya Njagua alitoa matamshi ya kichochezi akiwataka raia wa kigeni kutoka Mataifa mbalimbali wanaofanya shughuli za kibiashara nchini Kenya wakiwemo Watanzania waondoke ndani ya muda wa saa 24.

UWE MZAWA UWE MWEKEZAJI WA NJE KWANGU HAKI YAKO UTAIPATA-BITEKO

$
0
0
Waziri wa Madini Doto Biteko katikati kulia na Katibu Mkuu Prof. Simon Msanjila katikati kushoto wakiwa wanasikiliza jambo huku Afisa Madini Mkazi mkoa wa Mara Nyaisaara Mgaya wakati wa kikao cha usuluhishi wa mgogoro baina ya wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu eneo la Ikungi mkoani Mara na Kampuni ya PolyGold (T) Ltd. 
Sosy Mgonya miongoni wa wachimbaji wadogo akijibu swali aliloulizwa na Katibu Mkuu Prof. Simon Msanjila wakati wa kikao hicho. 
Waziri wa Madini Doto Biteko katikati kulia, Katibu Mkuu Prof. Simon Msanjila katikati kushoto na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Madini Prof. Shukrani Manya wakiwa kwenye kikao cha usuluhishi wa mgogoro baina ya wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu eneo la Ikungi mkoani Mara na Kampuni ya PolyGold (T) Ltd hawapo pichani. 


………………………….. 
Na Issa Mtuwa -WM – Dodoma 
Uwe mzawa, uwe mwekezaji wa nje kwangu haki yako utaipata. Ni kauli ya Waziri wa Madini Doto Biteko wakati akisuluhisha mgogoro baina ya wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu eneo la Ikungi mkoani Mara na mwekezaji wa kampuni ya PolyGold (T) Ltd. 

Ametoa kauli hiyo leo Julai 2, 2019 ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma baada ya kukutana na pande hizo mbili ambazo awali zilikubaliana na kusainiana mkataba wa kuchimba madini kwa ushirika. Pande hizo zilishindana kabla ya kuanza kwa shuguli za uchimbaji kiasi cha kuwa na mgogoro mkubwa uliopelekea kufikishana kwa Waziri wa Madini ili kupata suluhu ya mgogoro wao ambao teyari umetatuliwa na Waziri Biteko. 
Akitumia staili ya ushirikishi wa kusikiliza kila upande, Biteko alitoa fursa ya kila upande kuongea na kubaini changamoto kadhaa. 

Baada ya kuwasikiliza, Biteko alifikia maamuzi ya kuwatoa nje wawakilishi wa Kampuni ya PolyGold (T) Ltd nje ya ukumbi wa kikao ili azungumze na wachimbaji wadogo baada ya kugundua changamoto kwa upande wao. 
Hali aikuwa shwari kwa muda baada ya Biteko kucharuka baada ya kubaini uwepo wa ujanja ujunja kwa upande wa wachimbaji wadogo na kuwataka waache ujanja ujanja na kusikiliza maneno ya watu walio nje na makubaliano na mshirika wao na kuwaambia waache tamaa badala yake waheshimu makubaliano waliyofikia kwa hiyari yao bila uwepo wa wizara. 

Amesema yapo malalamiko ya wawekezaji katika maeneo mbalimbali ya uwekezaji hivyo hataki kuruhusu ujanja ujanja huo utokee kwenye wizara anayo iongoza. Ameongeza kuwa hata kama wao ni kutoka nje wanayo haki ya msingi kupewe haki yao pale inapoonekana kukiukwa au kuonewa kwani shuguli zao ni halali na wanafuata sheria. 

“Ndugu zangu niwaambie ukweli, huyu mmoja mnae muona (Mwekezaji) ana haki kama nyinyi, akionewa huyo mjue anawatu yuma yake, ana ubalozi hapa kwa hiyo siko teyari kuchafua jina la serikali na wizara ninayo iongoza kwa kukiuka haki ya upande fulani. Uwe mzawa uwe mwekezaji wa nje kwangu haki yako utaipata, kwa hiyo kaeni na mkubaliane na mwekezaji wenu, mimi na wezangu tunatoka tunawacha nikirudi tupate majibu msimamo wangu nimewapa”. alisema Biteko huku akiwa amekasirika. 

Mara baada ya maelekezo hayo wachimbaji wadogo wakiongozwa na Edwin Mchihiyo na Sosy Mgonya ambae leseni yake imenusurika kufutwa na waziri walikaa pamoja na mwekezaji wao kampuni ya PolyGold (T) Ltd iliyo wakilishwa na Sergey Sagsyan na Benny Haule na kuzungumza kuhusu mvutano juu ya mgogoro wao na kufikia muafaka uliopelekea kuondoa mgogoro uliokuwepo. 

Akiongea kwa niaba ya wenzake kiongozi wa wachimbaji hao wadogo Edwin Mchihiyo amemshukuru Waziri kwa kusimamia kutatua mgogoro wao ambao umefikia tamati na kuahidi wanakwenda kutekeleza makubaliano yaliyokuwa yanaleta sinto fahau baina yao. 

Katika kikao hicho Waziri aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila, Mtendaji Mkuu wa Tume ya Madini Prof. Shukrani Manya, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Issa Nchasi na Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Edwin Igenge wote kutoka wizara ya madini na viongozi wengine wa Wizara na Tume ya Madini.

NYASA YAKOPESHA VIKUNDI KUMI NA MBILI

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Nyasa ndugu Jimson Mhagama akizungumza na wanufaika wa vikundi vilivyopatiwa mikopo hivi karibuni Ofisini kwake, ikiwa niasilimia kumi ya mapato ya ndani ya Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma.Picha na( Ofisi ya ded Nyasa) 
…………… 
Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa imetoa shilingi milioni thelathini na tano laki saba themanini na sita elfu mia nne tisini na mbili (35,786,492/=) kukopesha vikundi kumi na mbili (12) vya wanawake, vijana na walemavu ikiwa ni asilimia kumi (10%) ya mapato ya ndani ya Halmashauri. 

Akiongea na wanufaika wa mikopo hiyo ofisini kwake, Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Nyasa, Ndugu Jimson Mhagama amewataka wana vikundi hao kuzitumia fedha hizo vizuri kwa kuboresha shughuli mbali mbali za kiuchumi ili waweze kuzirudisha kwa wakati na ziendelee kukopeshwa kwa vikundi vingine vya ujasiriamali na kuinua uchumi wa wananchi wa Wilaya ya Nyasa. 

Mhagama alifafanua kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa, kwa mwaka wa Fedha wa 2018/2019, imetenga bajeti ya shilingi 42,081,692/= kwa ajili ya kukopesha vikundi vya kina mama, vijana na walemavu ikiwa ni asilimia kumi ya mapato ya ndani kama ilivyoagizwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Tawala za Serikali za Mitaa kupitia Tangazo la Serikali Namba 286 la tarehe 5/4/2019 ambayo imeainisha utoaji na usimamizi wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika Serikali za Mitaa ambapo inazitaka Halmashauri zote kutenga asilimia kumi (10%) ya mapato yake ya ndani kuwezesha vikundi hivyo. 

“Wilaya ya Nyasa tumefanikiwa kuto fedha zote tulizoweka kwenye Bajeti ya mwaka huu wa Fedha na tayari tumesha waingizia kwenye akaunti zenu za vikundi. Nawakumbusha Fedha hizi sio Ruzuku, huu ni mkopo na zinatakiwa kurudishwa ili na vikundi vingine viweze kunufaika na fedha mtakazorudisha”, alisema Mkurugenzi huyo. 

Alivitaja Vikundi vya wanawake vilivyopewa mikopo hiyo kuwa ni, Amani (Kata ya Chiwanda), Chakula barafu (Kata ya Mbamba-bay), Umoja Group (Kata ya Mpepo), Acha Tuanze (Kata ya Lumeme), Umoja (Kata ya Kihagara) na Upendo Kiwono (Kata ya Mpepo). 

Vikundi vingine ni vya vijana wa Kisasa (Kata ya Luhangarasi), Pikipiki (Kata ya Tingi), Tuungane Pamoja (Kata ya Liwundi), Dhahabu Kijani (Kata ya Mipotopoto) na Kikuso (Kata ya Mpepo) na kikundi kimoja cha walemavu cha Tuthaminiwe kutoka Kata ya Lipingo wilayani hapa. 

Aidha alisema kila kikundi kimekopeshwa Tsh milioni tatu (3,000,000/=), kwa vikundi vya kina mama na vijana na kikundi cha walemavu kimekopeshwa shilingi 2,786,492/= (milioni mbili laki saba themanini na sita elfu mia nne tisini na mbili), ambayo watarudisha bila riba kwa kipindi cha mwaka mmoja. 

Aliongeza kuwa tayari Halmashauri kwa kipindi cha robo ya kwanza imetoa shilingi 6,295,200/= kwa ajili ya vikundi vitatu vya Mamanilee, Upendo na Muongozo cha vijana wa Kata ya Lipingo. 

Baadhi ya wanufaika wa mikopo hiyo, Mwenyekiti wa kikundi cha pikipiki kutoka Kata ya Tingi, walisema wanaipongeza sana Serikali kwa kuwajali makundi maalum hasa ya vijana kina mama na watu wenye Ulemavu kwa kuwa makundi hayo ndio hasa yanayo shughulika na utafutaji mitaji kwa kuwa Serikali imewapa mitaji hawata iangusha kwa kuwa watalipa kwa wakati kukuza uchumi katika jamii. 

“Nachukua fursa hii kukupongeza sana Mkurugenzi wetu kwa kutupatia mikopo hii kwa kuwa makundi haya ndiyo haswa tunaohangaika kutafuta mitaji na hakuna mwaka ambao Halmashauri hii imetoa mikopo kwa vikundi kumi na tano, hayo ni maajabu. Sisi wanufaika hatuta kuangusha, tutafanya biashara vizuri na tutarudisha kwa wakati ili vukundi vingine vipewe mikopo hii isiyo na Riba”. 

Aliongeza kuwa tayari Halmashauri kwa kipindi cha robo ya kwanza ilishatoa shilingi 6,295,200/= kwa ajili ya Vikundi vitatu vya Mamanilee, Upendo na Muongozo cha vijana wa Kata ya Lipingo.

TASAC YATOA WITO KWA MAWAKALA WAFORODHA

$
0
0

 Na.Khadija seif ,Michuzi tv

SHIRIKA la uwakala wa meli nchini (TASAC) limebainisha majukumu yake .
Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Emmanuel ndambo amesema shirika limepewa majukumu ya kusimamia na kudhibiti shughuli za usafiri wa majini kwa ujumla wake ikiwa ni pamoja na kutoa leseni kwa watoa huduma hizo.

"Kuhakikisha watoa huduma wanazingatia masharti ya uendeshaji pamoja na kulinda mazingira na usalama wa abiria na mizigo yao,"

Hata hivyo ndomba ameeleza kuwa kuna sheria ambazo zilitungwa na shirika hilo ikiwemo uwakala wa forodha na uondoshaji wa shehena kwa bidhaa Kama madini ,makinikia,mitambo,petroli,silaha,wanyama hai na nyaraka za serikali.

" majukumu mengine ni udhibiti wa nyaraka za mizigo,uhakiki wa mizigo inayoingia na kutoka pamoja na uwakala wa meli," alisema ndomba


Ndomba amebainisha maamuzi makuu mawili ambayo bodi ya wakurugenzi iliyoteuliwa iliunda ni pamoja na kuhakikisha shirika la uwakala wa meli (TASAC) inafanya kazi kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kusimamia tozo zote zinazotozwa kwa wananchi .

Pia ametoa wito wakala wa forodha,pamoja na mawakala wote wa meli kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuleta ufanisi na kuboresha bandari zote.
Mkurugenzi mkuu wa shirika la uwakala wa meli nchini (TASAC) Emmanuel Ndambo akizungumza na waandishi wahabari wakati wa kutolea ufafanuzi sheria pamoja na majukumu yaliyoundwa na bodi hiyo

NUNDU APIGA HESABU ZA UBUNGE JIMBO LA TANGA 2020

$
0
0
ALIYEKUWA Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano katika serikali ya awamu ya nne Mhandisi Omari Nundu ametangaza nia ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Tanga mwaka 2020 mara baada ya kipenga kutangazwa rasmi. 

Mhandisi Nundu alitangaza nia hiyo wakati wa halfa ya kukabidhiwa vifaa vya Hospitali ya wilaya ya Tanga vilivyotolewa na wadau wa maendeleo mkoani Tanga kupitia magroup ya mitandao ya kijamii ya Whatsup. 

Alisema kwamba wakati ukifika wa kuchukua fomu atafanya hivyo kwa kuchukua na kujaza ikiwemo kuirudisha ili kuwa tayari kwa ajili ya kinyang’anyiro hicho ili kuomba ridhaa ya wananchi wamchague ili awatumikie. 

Mhandisi Nundu ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) kwa kipindi cha miaka mitano kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015 kubwagwa na mgombea kutoka Chama cha Wananchi (CUF) Alhaji Mussa Mbaruku. 

“Labda niwaambie kwamba ikifika mwaka 2020 wakati wa kugombea nitachukua fomu nitazijaza na kugombea lakini kwa sasa hamtoniona nikigawa fedha kwa watu elfu ishirikiniishirini wala futari “Alisema Waziri huyo wa zamani 

“Nimesikia maneno mtaani yanapita kwamba Nundu anataka kugombea ubunge niwaambie kwamba ikifika mwaka 2020 wakati wa kugombea nitachukua fomu nitaijaza na kurudisha”Alisema .Aidha alieleza kwamba hatawapa fedha watu lakini kwenye suala la maendeleo atashirikiana na wananchi kuhakikisha yanapatikana kwa kutatua baadhi ya changamoto. 

“Nitasimamia suala la maendeleo mpaka hatua ya mwisho sasa tuna Rais ambaye anasaidia na kusukuma maendeleo kwa kasi kubwa kwani matunda yake yameonekana kwenye sekta mbalimbali”Alisema 

Awali akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji alisema kwamba niwashukuru wote waliochangia vifaa hivyo vya matumizi ya hispiotali nikiri hivi sasa tutakuwa tunapokea vifaa kwa utaratibu wa kiserikali. 

Mayeji alisema kwamba wao serikali wanapokea misaada yoyote ile hasa isiyo na masharti watapokea na wanaingiza kwenye matumizi hawana sababu yoyote ya kukataa kitu ambacho kimekuwa kikitolewa na wadau. 
Watawakabidhi wataalamu waugavi kwa ajili ya kuvipokea huku akieleza kwamba wao kama serikali hawana masharti ya kutokupokea msaada wowote ambao umekuwa ukitolewa. 

“Kama kuna mtu anahitaji kutoa msaada kwenye Jiji la Tanga tupo tayari kupokea lakini kikubwa tufuate utaratibu ambao unatakiwa kwa kupeleka kunakohusika na watapokea na kupeleka kwenye matumizi yanayokusudiwa “Alisema Mkurugenzi huyo. 

Alisema wamevipokea na vitatumika kwenye matumizi yalyokusudiwa ili viendelee kutumika kwa kuwekewa uangalizi mzuri wa matumizi.

DKT.SHEIN AFUNGUA MAADHIMISHO WIKI YA UTUMISHI WA UMMA ZANZIBAR

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akimkabidhi Katibu Mkuu Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu kiongozi Abdulhamid Yahya Mzee Cheti maalum katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul-wakil kikwajuni Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akikabidhiwa Cheti maalum na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idi katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul-wakil kikwajuni Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akitoa hotuba ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul-wakil kikwajuni Zanzibar. 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala bora Yakut Hassan Yakut akitoa maelezo mafupi ya makaribisho katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul-wakil kikwajuni Zanzibar. 
Baadi ya Wageni waalikwa waliohudhuria katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul-wakil kikwajuni Zanzibar. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman akitoa hotuba ya makaribisho kwa Mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul-wakil kikwajuni Zanzibar. 
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dk,Mary Mwanjelwa akizungumza katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdul-wakil kikwajuni Zanzibar. 
PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

WACHINA KUWEKEZA KWENYE ULANGA MIRERANI

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara, James Ole Millya (kushoto) akiwa na wachina, maofisa wa madini na polisi wakikagua eneo la uwekezaji wa madini ya ulanga Mji mdogo wa Mirerani. 

Mbunge wa jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara, James Ole Millya (kulia) akiwaonyesha wawekezaji wa China eneo mojawapo yanapopatikana madini ya ulanga Mji mdogo wa Mirerani. 

Mbunge wa jimbo la Simanjiro Mkoano Manyara, James Ole Millya (kulia) akiwasikiliza wawekezaji raia wa China kwenye eneo la madini ya ulanga Mji mdogo wa Mirerani. 

…………………. 
RAIA tisa wawekezaji wa China wanatarajia kuwekeza kwenye uchimbaji mkubwa wa madini ya Grafite (ulanga) Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. 

Madini hayo ya ulanga hutumika kwa ajili matengenezo ya vitu mbalimbali ikiwemo betri za simu, betri za kurunzi, kalamu ya risasi na mengineyo. 

Mbunge wa jimbo la Simanjiro, James Ole Millya, alisema wawekezaji hao wanatarajia kufanya uwekezaji mkubwa wa madini hayo ya viwandani katika eneo hilo. 

Ole Millya alisema uwekezaji huo utawanufaisha watanzania wengi hususan wa wilaya ya Simanjiro ikiwemo kuwapatia ajira za kudumu na za muda mfupi. 

Alisema awali wawekezaji hao walifika kwenye nchi ya Msumbiji na kukagua eneo la kuchimba madini hayo ya ulanga ndipo wakaja Tanzania kwa lengo la kukagua na kuwekeza. 

“Ninatarajia serikali itatoa ushirikiano mkubwa wa kutosha ili wawekezaji hao wafanikishe kuanzisha viwanda vikubwa katika uchimbaji wa madini hayo ya ulanga,” alisema Ole Millya. 

Hata hivyo, mkuu wa wilaya ya Simanjiro, Zephania Chaula alisema serikali itawapa ushirikiano mkubwa wawekezaji hao na kuwaandalia mazingira rafiki ya kuwekeza viwanda katika uchimbaji wa madini hayo. 

“Tunampongeza mbunge wetu kwa kufanikisha upatikanaji wa wawekezaji hao ambao kwa kiasi kikubwa watazalisha ajira kwa wana Simanjiro kupitia viwanda na kulipa kodi serikali,” alisema Chaula. 

Ofisa madini mkazi wa Mirerani, Daudi Ntalima alisema wametoa ushirikiano kwa wawekezaji hao ambao walikagua maeneo yote wanayotaka kuwekeza katika sekta hiyo. 

“Maofisa wangu wametembea mguu kwa mguu na wawekezaji hao ili kuhakikisha wanapata nafasi ya kufanya ukaguzi kabla ya kuwekeza pindi sheria, taratibu na kanuni zikifuatwa,” alisema Ntalima. 

Wilaya ya Simanjiro ina utajiri mkubwa wa aina mbalimbali ya madini zaidi ya 150 ikiwemo Tanzanite, Ruby, Green Tourmarine, Green Ginet, Saphure, Rose na mengineyo.

WAZIRI LUGOLA AONGOZA KIKAO CHA TUME YA UTUMISHI WA POLISI, UHAMIAJI NA MAGEREZA JIJINI DODOMA

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na Wajumbe  wa Tume ya Utumishi ya Polisi, Uhamiaji na Magereza wakati wa kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na Wajumbe  wa Tume ya Utumishi ya Polisi, Uhamiaji na Magereza (hawapo pichani), kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo Meja Jenerali Jacob Kingu.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu,akifafanua jambo mbele ya Wajumbe  wa Tume ya Utumishi ya Polisi, Uhamiaji na Magereza (hawapo pichani), wakati  wa  kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara. Kulia  ni Waziri wa wizara hiyo Kangi Lugola. Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia),Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Meja Jenerali Jacob Kingu na Kamishna wa Polisi Benedict  Wakulyamba, wakipitia vitabu wakati wa kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna wa Magereza, Faustine Kasike  akizungumza wakati wa Kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kulia ni Kamishna wa Uhamiaji Dk. Anna Makakala.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna wa Uhamiaji ,Dk. Anna Makakala akizungumza wakati wa kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kushoto  ni Kamishna wa Magereza  Faustine Kasike.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Kamishna wa Polisi, Benedict Wakulyamba akizungumza wakati wa kikao cha kujadili utendaji wa vyombo vilivyopo chini ya wizara.Kikao hicho kimefanyika Ukumbi wa wizara jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

SHIVYAWATA YAHITAJI MIUNDOMBINU RAFIKI,KUONDOA UNYANYAPAA WAKATI WA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA ,KIBAHA-MATAGI

$
0
0



NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA 

SHIRIKISHO la Watu Wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Kibaha,mkoani Pwani ,limetoa rai kwa Halmashauri ya Mji huo,kuweka miundombinu rafiki na kuondoa unyanyapaa wakati wa kupiga kura pamoja na kujitokeza kugombea, katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 . 

Anasema, kwa kuondoa changamoto hizo itasaidia makundi yote kushiriki bila vikwazo nyakati za chaguzi. 

Katibu wa shirikisho hilo ,Wilayani Kibaha, Happiness Matagi ,alitoa maoni hayo wakati wa kikao cha wadau wa uchaguzi wa serikali za mitaa,mjini Kibaha . 

Alisema, uchaguzi uliopita walishuhudia mazingira yasiyo rafiki kwao ,katika zoezi la upigaji kura kwani maeneo mengine yalikuwa ya ngazi, ukosefu wa msaada kwa wenye ulemavu wa macho na wasiosikia hali iliyosababisha kushindwa kushiriki vema kwenye zoezi hilo. 

“Elimu itolewe ili tushiriki na kuthubutu kugombea na tunataka tusinyanyapaliwe kwakuwa na sisi tuna haki ya kuchangamana na wengine katika masuala ya maendeleo na ngazi ya maamuzi”alisisitiza Happiness. 

Awali kaimu ofisa uchaguzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha ,Saidi Kayangu alisema ,wamejipanga kuweka mazingira rafiki na kusimamia haki kwa makundi yote ili kuondoa vikwazo wakati wa uchaguzi. 

Alifafanua,kwa kutambua hilo ndio maana hatua hii ya awali wameshirikisha asasi mbalimbali, wanawake,vijana ,walemavu na vyama vya siasa kwenye kikao cha wadau ili kupata maoni yao na kwenda kuyafanyia kazi. 

Katika hatua nyingine ,Kayangu alihimiza wananchi kujiorodhesha kwenye rejesta za wakazi katika mitaa yote 73 ili kupata takwimu kwa uhalisia hasa idadi ya kuanzia umri wa miaka 18 na kuendelea,:”hatua hii anaelezea itasaidia maandalizi ya uchaguzi kama vile idadi ya karatasi za kupiga kura. 

Nae mkurugenzi mtendaji wa asasi ya ushirikiano wa maendeleo ya vijana (YPC) Kibaha,Islael Ilunde aliwaasa vijana na wenye ulemavu kutumia haki yao ya kujitokeza kupiga kura na kugombea. 

Pia aliiomba jamii kuwa wakali, kukataa rushwa na badala yake wakati ukifika achaguliwe kiongozi bora na sio bora kiongozi.

WANAHABARI MKOANI ARUSHA WATAKIWA KUUNGANA KUTETEA MASLAHI YAO

$
0
0

Na Jusline Marco-Arusha

Wanachama wa chama cha wafanyakazi wanahabari Mkoani Arusha wametakiwa kuungana kwa pamoja katika kupigania na kutetea maslahi yao kupitia chama hicho.

Akifunga mafunzo kwa wanahabari wanawake yaliyofanyika Mkoani Arusha Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Arusha Claud Gwandu amewataka wanahabari hao kuwa na ushirikiano katika kutetea maslahi yao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa muda wa Chama cha wafanyakazi kwenye vyombo vya habari Saidi Mmanga amesema kuwa waandishi wengi wa habari wanawake wanakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia,unyanyasaji wa kingono pamoja na mazingira yasiyoridhisha ya kazi hivyo mafunzo hayo yamelenga kuwapa uelewa waandishi hao nakuwakumbusha mikataba mbalimbali ya kimataifa ya masuala ya usawa wa kijinsia kwa wanawake.

Naye mmoja wa waandishi wa habari waliopatiwa mafunzo hayo,Veronica Ignatius akizungumza kwa niaba yao amewataka waandishi wa habari wanawake kufanya kazi kwa malengo na kupiga Vita rushwa ya ngono ili kuweza kuleta mageuzi kwa wengine na kuwa mfano hai kwao.

Hata hivyo mafunzo hayo yameandaliwa na chama cha wafanyakazi wanahabari Tanzania kwa ufadhili wa chama cha wafanyakazi wanahabari kutoka Norway kwa kushirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya wanahabari (IFS).

Hata hivyo takwimu zinaonyesha kuwa asilimia kubwa ya wanahabari wanawake hawapo katika mazingira bora ya kazi huku maslahi yao ikiwa duni hivyo kupitia mafunzo ya jinsia na usalama kwa wanahabari wanawake mahali pa kazi,wanahabari hao wametakiwa kuungana kwa pamoja ili kuweza kupaza sauti zao.
Waandishi wa habari wanawake Mkoani Arusha wapatiwa mafunzo ya jinsia na usalama mahali pa kazi na Chama cha wafanyakazi wanahabari Tanzania (JOWUTA)

WAKULIMA WASHAURIWA KUTUMIA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI KUPIMA UDONGO KWA LENGO LA KUPATA MAZAO BORA

$
0
0

Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MAMLAKA ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeshauri wakulima wasifanye kilimo cha zamani na badala yake watumie maabara yao kwa kupima udongo ili kuzalisha mazao yenye mahitaji ya kimataifa.

Imefafanua kwamba mazao yanapouzwa kimataifa lazima yawe yamekidhi viwango vya ili kuendana na soko la kimataifa.

Ushauri huo umetolewa leo kwenye Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea Sabasaba jijini Dar es Salaam na Ofisa Masoko na Mawasiliano wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Cletus Reuben Mnzava 

Mnzava amesema kuwa ni wakati muafaka kwa wakulima nchini kuitumia mamlaka hiyo kwa lengo la kulima kilimo chenye tija na kwamba kwa kutumia maabara ya mkemia mkuu wa Serikali kupima udongo.

"Tunawashauri wakulima nchini kuhakikisha wanatumia maabara ya mkemia mkuu wa serikali kupima udongo kabla ya kupanda mbegu za mazao.Tunahitaji kuona wakulima wanapata mazao yaliyobora," amesema Mnzava.

Ametumia nafasi hiyo pia kueleza kuwa kwa wanaokwenda maonesho ya Sabasaba wafike kwenye banda la Mamlaka hiyo kwani kuna mambo mengi ya kujifunza ambayo wameyaandaa kwa ajili ya wananchi wote.

Ameyataja baadhi ya mambo ambayo wameyaandaa kwa ajili ya wananchi ni pamoja na kueleza namna wanavyopima vinasaba vya binadamu na masuala ya ubora wa bidhaa.

Pia usimamizi na udhibiti wa kemikali na kufafanua wale wote wanaojihusisha na mnyororo wa majukumu yao watapatiwa maelezo mazuri kwa lengo la kuhakikisha shughuli wanazozifanya zinakuwa na tija kwa maendeleo ya viwanda nchini Tanzania.

Alipoulizwa kwa mwananchi mmoja wananufaika vipi na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali amesema kuna faida nyingi na baadhi ya faida ni ubora wa bidhaa kwani mamlaka inafanya uchunguzi kwa niaba yao kuchunguza ubora wa bidhaa.Pia wanasaidia katika namna bora ya kufanya kilimo pamoja na biashara kwa mfano za asali na mazao yanayosindikwa.

Pia wanasaidia katika ujasiriamali mdogomdogo hasa wa kutumia kemikal katika kutengeneza batiki na faida nyingine wanasaidia kwa kuelimisha umma kuhusu ubora wa nafaka na namna ambavyo zinatakiwa kutunzwa.

"Pia tunasaidia katika kuwaeleza namna nzuri ya kutumia kemikali bila kudhurika.Ujumbe wetu kwa wananchi waje kwenye banda letu kwa ajili ya kuwapatia elimu ya uchunguzi wa kisayansi wa maabara kwa ajili ya afya mazingira pamoja na maendeleo endelevu ya viwanda nchini Tanzania," amesema Mnzava.
 Ofisa Masoko na Mawasiliano wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Cletus Mnzava (katikati) wakijadiliana jambo na maofisa wengine wa mamlaka hiyo waliopo katika maonesho ya biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam
Mkemia Mwandamizi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Faustine Wanjala (kushoto)akiwa ameshika Muhogo na Karoti kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi waliofika kwenye banda lao lililopo maonesho ya Sabasaba jijini Dar es Salaam

JAJI OTHMAN CHANDE AAGWA RASMI BAADA YA KUSTAAFU,

$
0
0
Na Karama Kenyunko, globu ya jamii.

JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma amesema Jaji Mkuu Mstaafu, Othman Chande amechangia mabadiliko makubwa katika nyanja zote za mahakama ikiwemo kuhakikisha uhuru wa mahakama, kupambana na rushwa na kuondoa mrundikano wa mashauri.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuagwa kitaaluma kwa Jaji Chande leo jijini Dar es Salaam, Jaji Juma amesema, yeye ni miongoni mwa watu walioshuhudia mabadiliko makubwa ya mahakama yaliyosababishwa na Jaji mstaafu Chande tangu alipoteuliwa mwaka 2004 kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani na baadaye Rais Jakaya Kikwete alipomteua kuwa jaji mkuu mwaka 2010 hadi 2017alipostaafu.

Amesema katika kipindi hicho Jaji Chende alianzisha mpango mkakati wa kuhakikisha mahakama inajitawala na haki inatolewa kwa usawa na kuongeza kuwa, Jaji Chande alikuwa miongoni mwa walioandaa Mpango Mkakati wa miaka 10 wa mahakama kuanzia 2015 hadi 2020 wakiwa na lengo la kuhakikisha wanaondoa mrundikano wa kesi za zamani kwa kila jaji kusikiliza mashauri 250 kwa mwaka.

Ameongeza, mapaka sasa mahakama inaendelea kufuata muongozo huo kwa kuhakikisha kuwa Mahakama za Mwanzo zinasikiliza kesi kwa miezi sita hadi kwisha kwake na Mahakama za Wilaya na Mkoa husikiliza kwa mwaka mmoja na sasa kila Jaji anatakiwa kusikiliza mashauri 100 kwa mwaka.

Aidha amewaomba wananchi waendelee kuwaamini, kuwapima kwa hukumu zinazotolewa na mahakama na kama hawajaridhika wakate rufaa, kwani mahakama ni muhimili unaofanya kazi kwa uwazi zaidi. Aidha amesisitiza kuwa, mahakama imejipanga kuona kila mtumishi ana kitambulisho kinachoonesha majina yake hivyo, akiomba rushwa ni yeye binafsi na si watu wote hivyo anapaswa kujiwajibishwa kabla ya kupelekwa kwenye Tume ya maadili.

‘’Ukiombwa rushwa useme na uwe tayari kutoa ushahidi, nenda mpaka Takukuru, mtaje mla rushwa. Ninaahidi tutaendelea kuwasaidia wananchi wasiingie kwenye mitego ya rushwa na tunawaelimisha waelewe taratibu za mahakamani,’’ alisema.

Kwa upande wake, Jaji mstaafu Chande, amesema mahakama ni taasisi ambayo inatakiwa kulindwa na kujilinda kwa kuwa huru ili kuhakikisha inafanya kazi kwa mujibu wa katiba na sheria na kutoa haki kwa usawa na uhuru hivyo ni lazima kulinda na kutetea uhuru wa mahakama kwani zipo taasisi nyingi zinazopima uhuru na zimeonesha kuwa unalindwa na kuheshimika hapa nchini.

Aidha ameongeza kua, mageuzi makubwa yameishafanyika na yanaendelea kufanyika ikiwemo kutenganisha majukumu ya wasajili na watendaji wake. Kwani kwa sasa mfumo mpya wa usikilizwaji wa malalamiko unasaidia ambapo asilimia 98 ya malalamiko yanasikilizwa kwa mwaka.

Naye, Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda amesema Jaji Chande ni chachu ya mabadiliko ya kimfumo katika mahakama kwani katika kipindi chake chote cha uongozi alihakikisha anasimamia masuala ya rushwa na mrundikano wa kesi na mahakama inakuwa na utawala binafsi katika utoaji wa haki kwa watu wote kwa usawa.

Akielezea safari yake ya uongozi, Jaji profesa Juma amesema, Jaji Chande alipata shahada ya Sheria kutoka Kitivo Cha Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1974, baadaye alisoma Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Webster huko Geneva mwaka 1982 na Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa alimteua kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Agosti 16, 2004 na Februari 6, 2008 aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.

Desemba 2, 2010 Rais mstaafu Jakaya Kikwete, alimteua kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, nafasi aliyoishika hadi alipofikia umri wa kustaafu kwa mujibu wa Katiba Januari 17, 2017.

Waliohitimu shahada ya Sheria pamoja na Jaji Mkuu Mstaafu Chande ni Pinda, Jaji mstaafu Dk Steven Bwana na wengine na baada ya kumaliza masomo yake alijiunga na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kama Mwanasheria wa Serikali alipokuwa Mwanasheria wa Serikali katika Benki Kuu ya Tanzania.

Pia Chande kwa kushirikiana na Reuben Mwaikinda, Maurice Pius Ndomba na Simon Ivasa-Merinyo Matafu walikuwa waendesha mashitaka wa makosa yanayohusu matumizi ya fedha za kigeni.

Pia alifanya kazi Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekudu huko Geneva Uswisi kama Mshauri Mwandamizi wa Mwendesha Mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai kuhusu Rwanda.

Aliteuliwa kuwa Mwendesha Mashitaka Mkuu katika Mahakama ya Rwanda kuanzia Juni Mosi, 1999 hadi Julai 31, 2000.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, Katibu Mkuu Kiongozi, John Kijazi, Jaji mstaafu, Augustino Ramadhan, Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), Mussa Assad, mawaziri, wastaafu serikalini na mahakamani na wanasheria.
 JAJI Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma  (kulia) akifurahi jambo na  Jaji Mkuu Mstaafu, Othman Chande








KIWANDA CHA A TO Z CHAIPA TUZO SIDO

$
0
0

Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha

Kiwanda cha kutengeneza nguo na vyandarua cha A to Z,kilichopo mkoani hapa kimelipongeza shirika la kuhudumia viwanda vidogo hapa nchini mkoani Arusha(SIDO) kwa mradi wao wa kaizen ambao unafadhiliwa na shirika la maendeleo la watu wa japan(JIKA) kwa kuwawezesha kupata mbinu mbalimbali za kuendesha kiwanda chao hali iliyopelekea kushinda tuzo ya kimataifa.

Akizungumza Meneja wa uzalishaji wa kiwanda hicho Marko Ayo alisema kwamba tulikua na tatizo la ubora katika kiwanda chetu ambapo
alisema Kaizen imewasaidia kutatua tatizo hilo na kuwaongezea ujuzi zaidi hivyo kuongeza uzalishaji na ubora zaidi.

Kwa upande wake meneja wa ubora wa kiwanda hicho Dominick Marike alisema kwamba kwa sasa wataongeza mashine katika kiwanda hicho na
kwamba afya na ubora katika kiwanda hicho zitasimamiwa vizuri ikiwa ni kuhakikisha kuwa ubora wa wafanyakazi utazingatiwa vizuri.

Naye Ruben Lyanga,Afisa usimamizi wa ubora amesema kuwa zana za kaizen wamezipata na kwamba ni bora hasa katika maendeleo ya viwanda na kuongeza kuwa kwa kuwa kwa kutumia ujuzi wa kaizen ndio kulikofanikisha kunyakua tuzo hiyo.

“Kiwanda chetu kimenufaika sana na mafunzo ya kaizen mliyotupatia,tumeyatekeleza kwa vitendo na ndio sababu tumetoa tuzo hii na imetufanya kuongeza uzalishaji zaidi na kwa ubora
mkubwa”alisema Lyanga.

Kwa upande wake meneja wa shirika la kuhudumia viwanda vidogo nchini mkoa wa Arusha(SIDO) Linah Nchimbi alikishukuru kiwanda hicho kwa tuzo
hiyo waliyowapatia ambapo aliwataka wadau wengine wa viwanda vingine wafike SIDO kupata mafunzo ya kaizen.

“Nampongeza sana rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa kuweka msisitizo juu ya uanzishaji wa viwanda vidogo na ndilo jukumu tunalolifanya sisi na tutahakikisha Tanzania ya viwanda inawezekana”alisema nchimbi.

Ameongeza kuwa wale wote wanaopata mafunzo hayo wanatakiwa waende katika maeneo ya uzalishaji na kuyafanyia kazi mafunzo hayo ili yawe
na tija na ufanisi zaidi.

“Tunahitaji wajasiriamali,wenye viwanda vidogo,vya kati wajitokeze zaidi ili kupata mafunzo ya kaizen kwani hadi sasa tuna wakufunzi zaidi ya 40 katoka wilaya zote za mkoa wetu wa Arusha”.
Meneja wa SIDO mkoa wa Arusha Linah Nchimbi akitoa mada kwa vijana kutoka majukwaa ya vijana wilaya ya Arusha waliotembelea makao makuu ya SIDO mkoa wa Arusha kujifunza mambo mbalimbali

WANANCHI WASHAURIWA KUJITOKEZA KWA WINGI MAONESHO YA SABASABA

$
0
0
WANANCHI wameshauliwa kujitokeza kwa wingi katika maonyesho ya sabasaba yanayoendelea jijini Dar Es Salaam ili kuweza kupata fursa ya kuona bidhaa mbalimbali ikiwa pamoja na kupata ushauri kuhusu afya na mambo mengine yanayohusu Binadamu.

Ushauri huo umetolewa leo na Mkurugenz wa huduma za kitabibu Aziza Bangoi Kutoka katika Kampuni ya Bangoi Natural Product ambaye naye nimiongoni mwa washiriki katika maonyesho hayo ya 43 ya kimataifa ya sabasaba ambapo yanafanyika kila mwaka mwezi kama huu.

Amesema ifike mahala Jamii ione umuhimu wa kuhudhuria kwa wingi kwenye maonyesho kama hayo kwani pamoja na mambo mengine lakini watapafursa ya kupata ushauri mbalimbali wa kiafya na hatimaye kuponya miiili yao ukizingatia miaka hii magonjwa yamekuwa mengi ukilinganisha na miaka mingi 

"Hapa kwenye maonyesho kuna vitu vingi wakiwamo matatibu tupo hapa waje wananchi wapate huduma kwa mfano Mimi hapa nina tiba za aina mbalimbali kama vile pumu,Ngili, virutubisho vya aina mbalimbali hivyo wafike hapa Banda la namba 32 la Ally Hassan Mwinyi watakutana na wataalumu wangu.amesema mama Bangoi.

Aziza amesema kuwa watanzania wanasumbuliwa na matatizo mbalimbali ya kiafya lakini tatizo kubwa ni watu ambao wanasubili hadi madhara wajitokeze waziwazi na ndio utaona wanahangaika kutafuta tiba badala ya kufanya hivyo mapema zaidi iwezekanavyo.

Amefafanua kuwa wa Serikali wameendelea kufanya vizuri katika kuenzi maonyesho hayo ambayo kimsingi dhamira kuu niwataka watanzania kupata wasaa kuja kuonyesha kile ambacho wanakifanya katika shughuli zao za kila siku na si vinginevyo hivyo niwajibu wa watanzania kujitokeza kwa wingi.

" ukifika katika Banda hili la Ally Hassan Mwinyi namba 32 utapata fursa ya kupata ushauri kwa magonjwa kama vile matatizo ya Meno,pumu,Mafuta ya nywele,ngozi ,dawa za nywele, fangasi,kupooza, ushauri wa namna ya kuacha pombe,na dawa zake zinapatikana hapa."amesisitiza Aziza

Pia katika eneo la vya kula lishe kama vile unga ya milonge,unga wa maboga,parachichi na pia anaondoa makemikali katika mwili wa binadamu hivyo wananchi wajitokeze kwa wingi katika viwanja hivyo vya sabasaba .

Aziza pia anatoa mwito kwa akina mama kuhamasika na kujitokeza kwa wingi kwani wao ndio wanamatatizo mengi na makubwa hivyo wasibaki makumbani watembelee viwanja vya maonyesho sabasaba.lakini hata msimu wa sabasaba ukimalizika wananchi wanaweza kufika maeneo ya Tandika nyumba na 47 Mtaa wa mwani Transfoma.
Mama Aziza Bangoi akiwa katika Banda lake namba 32 Banda la Ally Hassan Mwinyi akijaribu kutoa maelezo kwa mteja ambaye alifika katika Banda hilo ili kupata ushauri na tiba .kwenye viwanja hivyo vya maonyesho sabasaba .picha na Mpiga picha wetu.

WAZIRI LUGOLA AONGOZA KIKAO CHA KUFUATILIA MALI ZA MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA JIJINI DODOMA

$
0
0

Waziri  wa  Mambo  ya  Ndani  ya  Nchi, Kangi Lugola akizungumza wakati wa kikao na Uongozi  wa  Mamlaka  ya  Vitambulisho  vya  Taifa (NIDA), lengo la kikao hicho ni ukaguzi na utambuzi wa mali za mamlaka hiyo. Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Katibu  Mkuu  wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu,  akizungumza wakati wa kikao na Uongozi  wa  Mamlaka  ya  Vitambulisho  vya  Taifa (NIDA), lengo la kikao hicho ni ukaguzi  na  utambuzi wa  mali  za  mamlaka hiyo.Kushoto ni waziri wa wizara hiyo, Kangi Lugola. Kikao hicho kimefanyika  leo jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu  Katibu  Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima, akizungumza wakati wa kikao na Uongozi  wa  Mamlaka  ya  Vitambulisho  vya  Taifa (NIDA), lengo la kikao hicho ni ukaguzi na utambuzi wa mali za mamlaka hiyo. Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri  wa  Mambo  ya  Ndani  ya  Nchi, Kangi Lugola (katikati), Katibu Mkuu wa wizara, Meja Jenerali Jacob Kingu (kushoto)  na Naibu Katibu Mkuu ,Ramadhani Kailima (kulia) wakikagua orodha ya mali za Mamlaka  ya  Vitambulisho  vya  Taifa (NIDA),  wakati  wa  kikao  na uongozi wa mamlaka hiyo  lengo  ikiwa  ni ukaguzi  na utambuzi wa mali za mamlaka hiyo.Waliosimama ni Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dk. Anold Kihaule na Mkurugenzi wa Utawala na Fedha NIDA, Merckion Ndofi(kushoto). Kikao hicho kimefanyika  leo  jijini  Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mkurugenzi  wa  Sheria  wa  Wizara  ya  Mambo  ya  Ndani  ya Nchi, Merlin Komba, akizungumza wakati wa kikao na Uongozi  wa  Mamlaka  ya  Vitambulisho  vya  Taifa (NIDA),lengo  la  kikao  hicho  ni ukaguzi na utambuzi wa mali za mamlaka hiyo. Kikao  hicho  kimefanyika  leo  jijini  Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mkurugenzi  Mkuu  wa  Mamlaka  ya  Vitambulisho  vya  Taifa(NIDA), Dk. Arnold  Kihaule akiwasilisha muhtasari wa mali za mamlaka hiyo mbele ya uongozi  wa  juu  wa  Wizara  ya  Mambo  ya  Ndani  ya  Nchi, lengo la kikao hicho ni ukaguzi na utambuzi wa mali za mamlaka hiyo.Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Wasomi Waishukia Ripoti ya UNESCO,WWF

$
0
0
Na.Mwandishi Maalum. 

SERIKALI ya Tanzania inatakiwa kuchukua hatua madhubuti za ujenzi wa vyanzo vipya vya uzalishaji wa umeme wa uhakika ili iepuka kushindwa kufikia malengo ya kuwa taifa lenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. 

Sambamba na hilo, Tanzania inatakiwa kuwa na vyanzo vipya vya umeme wa uhakika ili kuepuka hatari ya maeneo ya misitu kugeuka jangwa na kuepuka athari za mabadiliko ya tabia ya nchi. 

Hayo yamebainishwa katika ripoti maalumu ya marafiki wa mazingira waliofanya utafiti kuhusu faida na hasara za ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa Rufiji unaofahamika zaidi kwa jina la Stiegler’s Gorge Hydropower Project unaotekelezwa katika eneo la hifadhi la Selous. 

Ripoti hiyo ya kitaalamu ambayo inatarajiwa kuzunduliwa hivi karibuni imeandaliwa na wataalamu wabobezi watano wa mazingira,uhifadhi na uchumi hapa nchini na imechambua upinzani wa ndani na wa kimataifa kuhusu ujenzi wa mradi wa Stiegler’s Gorge na hasa hoja zilizotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na Shirika la Kimataifa la Uhifadhi wa Mazingira na Wanyamapori (WWF) za kupinga mradi huo usitekelezwe. 

Mmoja wa wajumbe wa jopo hilo la wataalamu, Dk. Abubakar Rajabu katika mahojiano mafupi na waandishi wa habari yaliyofanyika jana jijini Dar es Salaam alisema yeye na wataalamu wenzake wamefanya utafiti wa kina na wa kitalaamu na kugundua kuwa upinzani unaoonyeshwa na mashirika hayo ya kimataifa dhidi ya ujenzi wa mradi huo umejikita zaidi katika hoja za upotoshaji ambazo lengo lake ni kutaka Tanzania iendelee kudumaa kiuchumi na kuharibu eneo la misitu kutokana na shughuli za kibinadamu. 

Dk Rajabu alisema katika utafiti wao wamebaini kuwa Tanzania ipo hatarini kugeuka jangwa na pia kukumbwa na athari mbaya za mabadiliko ya tabianchi kutokana na uharibifu wa mazingira unaosababishwa na shughuli za kibinadamu na hasa ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa na ili kuepuka hali hiyo ni lazima kutafuta njia mbadala aliyoitaja kuwa ni umeme wa uhakika na nafuu. 

Aidha, alisema ili Tanzania iweze kufikia malengo yake ya kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, serikali inalazimika kujenga vyanzo vipya vya umeme wa uhakika na rahisi ili kuziwezesha sekta nyeti za Viwanda, Kilimo na Madini kukua kwa kasi. 

“Serikali iko katika vita ya kiuchumi, vita hii si ya lelemama na kimsingi ni vita ya kila Mtanzania hivyo wote tuko kwenye vita hii. Sisi kama watalaamu kwenye mambo ya uhifadhi na mazingira tulipoona ripoti za UNESCO na WWF zilizokuwa zikipinga ujenzi wa mradi wa Stiegler’s Gorge ambao tulikusudia kuutekeleza tangu miaka ya 60 na tunajua manufaa yake tuliona tusipuuze utafiti wa wenzetu hawa, hebu tujiridhishe na hoja zao. 

“Mimi na wenzangu tukaingia kazini, tulifanyia kazi hoja zao zote na tulichogundua ni kwamba hoja zao ZOTE za kupinga mradi wa kuzalisha umeme wa maji wa Rufiji hazina ushahidi wa kutosha wa kisayansi bali upinzani huu lengo lake ni kutaka kuifanya Tanzania isipige hatua kimaendeleo, tuendelee kudumaa kiuchumi na katika nyanja zote muhimu. 

Lakini jambo kubwa kabisa tulilogundua ni hawa wenzetu wanataka miaka michache ijayo sehemu kubwa ya nchi yetu igeuke kuwa jangwa kwa sababu ya ukataji miti na hilo kwa ujumla litaharibu kabisa mazingira na kuifanya Tanzania kutofikia azma yake ya kuwa nchi ya uchumi wa kati na kuwarudisha nyuma watanzania kimaendeleo na Taifa liendelee kuwa tegemezi na pengine kutoweka kabisa katika ramani ya dunia:. 

Vyanzo vya maji vitakauka yote; mvua zitakuwa za kusadikika, kilimo kitadumaa, wanyama na ndege watakwisha wote, utalii hautakuwepo tena, viwanda vitayeyuka, ajira zitakuwa hadithi, mardhi na utapiamlo ndio itakuwa habari ya kila siku, nguvu kazi itapotea na Taifa litakuwa tegemezi nakadhalika. Na hayo yote yatachangia kuzorota kwa usalama wa taifa na nchi inaweza kutotawalika ”. 

“Niwape kidogo tu tulichogundua katika utafiti kwa sababu mengi mtayapata kwenye uzinduzi wa ripoti na mimi sitaki kumaliza uhondo, ni kwamba Tanzania ina eneo la misitu lenye kilomita za mraba 35,254 na kila mwaka eneo la misitu lipatalo kilomita za mraba 412 linateketezwa kwa ajili ya mkaa na kuni, ambacho ndio chanzo kikuu cha nishati kwa zaidi ya asilimia 85 ya watanzania wote. 

Kwa hiyo endapo hapatakuwa na nishati mbadala zaidi ya umeme na gasi, safari ya Tanzania kuelekea katika HATARI YA KUTOWEKA KATIKA RAMANI YA DUNIA ingekuwa imeanza rasmi, kama sio upeo mpana wa utawala kuona mbali na kuamua kutekeleza mradi mkubwa wa kufua umeme wa Rufiji. mpaka hapo nadhani mnaona hatari inayotunyemelea. 

“Lakini pia, katika utafiti wetu tumegundua kuwa asilimia 45 ya wafanyabiashara hapa Nchini wanamiliki jenereta ambazo zinatumia mafuta ya dizeli, moshi unaotokana na dizeli unachafua sana mazingira na hutuwezi kupiga hatua kiviwanda kama uzalishaji wetu utakuwa unategemea jenereta na hivyo kufanya gharama ya uzalishaji kuwa kubwa na hivyo kuongeza ughali wa maisha. Hivyo ni lazima tuwe na umeme wa uhakika alisema Dk Rajabu. 

Alisema ripoti inakuja kukata kiu ya maswali na kuondoa mashaka ya aina yoyote kuhusu utekelezaji wa mradi huo na umuhimu wa taifa kuwa na umeme wa uhakika na imeangalia nyanja zote zilizo tajwa kuwa na shaka na kupata ukweli wake. 

Alisisitiza kuwa hoja za kupinga mradi wa Stiegler’s Gorge zilizotolewa na wapinzani wa ndani na nje baada ya kuchujwa kisayansi zimekosa nguvu na hasa ikizingatiwa kuwa eneo la Selous lenye kilomita za mraba 50,000 ni pungufu ya asilimia mbili tu ndilo linalotumika kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa maji wa Rufiji. 

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan atembelea banda la NBC SabaSaba

$
0
0
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto) akipeana Mkono na Mkuu wa Idara ya Huduma za benki kidijitali na mageuzi ya kiteknolojia wa benki ya NBC Bw. Deogratius Lazari Mosha  kwenye banda la benki hiyo katika maonesho ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba 2019 viwanja vya Mwalimu Nyerere Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam.

Mpango wa Kuinua Elimu ya Msingi (Equip) wasaidia shule ya Muyegera kujikwamua na changamoto zake

$
0
0
Na Maureen Rogath, Michuzi TV, Kigoma 
Wanafunzi wa shule ya msingi ya Muyegera iliyopo wilayani hapa mkoani Kigoma wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa matundu ya choo, hali inayosababisha kukithiri kwa utoro shuleni hapo.  
Hayo yamebainishwa na mwalimu mkuu wa shule hiyo Bw. Issaya Ntahonkiliye wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa miradi iliyotekelezwa na Mpango wa Kuinua Elimu ya Msingi(Equip).  Alisema hali hiyo ya kukosekana kwa choo imesababisha wanafunzi kuumwa homa za matumbo na kushindwa kufika shule. 
 Alisema shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 927 ambapo wanatumia matundu ya choo 10, ambapo wanafunzi wavulana wapo 495 wanatumia matundu ya choo chenye matundu matano huku wanafunzi wasichana 452 nao wakitumia idadi hio hio ya matundu ya choo.
 “Kwa wastani wanafunzi wetu wanahitaji jumla ya  matundu ya choo 25 kwani vilivyopo haviwezi kutosheleza wanafunzi wote. Na wanafunzi wamekuwa wakiomba ruhusa mara kwa mara kutokana na kuumwa matumbo hali inayosababisha ongezeko la utoro,”alisema Ntahonkiliye. 
Makamu mkuu msaidizi wa shule hiyo Amani Emanuel, alisema mbali na kuwa na tatizo la matundu ya choo pia wanakabiliwa na upungufu wa madawati ambapo kwa sasa shule nzima ina jumla ya madawati 256 huku dawati moja likikaliwa na  wanafunzi wanne hadi watano  na wengine wakikaa chini.
 “Tumefikia hatua ya wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili tumewawekea utaratibu wa kuingia mchana kwani wakija wote kwa wakati mmoja madarasa hayatatosha kutokana na kukosekana kwa madawati na yanahitajika zaidi ya madawati 300 ambapo kila mwanafunzi ataweza kukaa kwenye dawati,”alisema Emanuel. 
 Mratibu elimu kata Yared Yowas, alisema Kutoakana na changamoto zinazoikabili shule hiyo walibuni mradi wa mashine ya kusaga na kukoboa pamoja na kuandaa shamba la miti kwa fedha walizopata kutoka kutoka Mpango wa Equip. 
 Alisema walipata kiasi cha Sh1.5 Milioni kutokana na andiko la mradi wa kuomba fedha ambapo waliweza kununua mashine hiyo na kwamba fedha itakayopatikana iweze kutatua changamoto za shule hiyo. 
 Alisema walipokea fedha kiasi cha Sh.550,000 kwa ajili ya shuguli za kuingizia kipato shule, ambazo waliweza kuandaa shamba la miti 6,000 kwa sh 350,000 ambapo miti hiyo ikikaribia kuvunwa wataweza kupata kiasi cha zaidi ya Sh.15 milioni.

 Mradi wa mashine ya kusaga na kukoboa uliobuniwa na waalimu na wazazi kwaajili ya shule ya msingi Muyegere  iliyopo wilayani Buhigwe kwa lengo la kujipatia kipato na kujiendesha yenyewe na kutatuta changamoto zinazowakabili
Mradi wa shamba la miti  uliobuniwa na waalimu na wazazi kwaajili ya shule ya msingi Muyegere  iliyopo wilayani Buhigwe kwa lengo la kujipatia kipato na kujiendesha yenyewe na kutatuta changamoto zinazowakabili
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>