Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109593 articles
Browse latest View live

HALMASHAURI MANISPAA YA ILALA YAPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA TATU MFULULIZO, MADIWANI WAKUTANA KUJADILI MAPENDEKEZO,USHAURI WA CAG

0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

HALMASHAURI ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam imepata hati safi kwa mwaka unaoishia Juni 30,2018 na kufanya halmashauri hiyo kuendelea kupata hati hiyo kwa mwaka wa tatu mfululizo.

Hayo yamesemwa leo Juni 28,2019 na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam Jumanne Shauri wakati anawasilisha taarifa ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) katika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo.

Shauri wakat anawalisha taarifa hiyo ya CAG kwa Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo, amesema kuwa kwa mujibu wa Katiba ya mwaka 1977 (Rev 2005) ibara ya 143 na sheria ya ukaguzi wa umma namba 11 ya 2918 kifungu cha 10(1) ni jukumu la la Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kufanya ukaguzi wa taarifa za mapato na matumizi ya fedha za umma Serikali Kuu,Serikali za Mitaa,Idara na mashirika ya umma.

Amefafanua baada ya ukaguzi huo anatakiwa kutoa matokeo ya ukaguzi na mapendekezo kutokana na ukaguzi huo na hatua zinazotakiwa kuchukuliwa na menejimenti zilizopo kwa mujibu wa sheria.

"Hati ya ukaguzi kwa mwaka wa 2017/2018 mwaka uliokaguliwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imepata hati safi na kufanya halmashauri yetu kuendelea kupata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo.Tulipata hati safi mwaka 2017/2018, mwaka 2016/2017 na mwaka 2015/2016.Kwa mwaka wa 2014/2015 tulipata hati yenye mashaka,"amesema Shauri mbele ya wajumbe wa kikao hicho.

Kuhusu mapendekezo ya CAG ambayo yapo kwenye ripoti yake, Shauri amesema kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imeweka mikakati mbalimbali kuhakikisha wanaishughulikia kikamilifu na kufafanua baada ya kupokea ripoti ya CAG ,Ofisi ya Rais-Tamisemi kupitia ofisi ya mikoa ilitoa ratiba ya kujadili taarifa hiyo kupitia vikao mbalimbali vya halmashauri.

Hivyo amesema Mei 20 mwaka huu kamati ya watalaam walifanya kikao, pia Kamati ya Ukaguzi nayo ikafanya kikao Juni 21 na Kamati ya Fedha na Utawala walifanya kikao Juni 26 mwaka huu.

"Hivyo leo hii baraza la madiwani kupitia kikao maalumu kimefanya kikoa ili kupata taarifa hiyo.Aidha halmashauri imejipanga kuzuia hoja zote kwa kuunda timu ya wataalam kushughulika na kushauri kuhusu kuzuia hoja zilizojitokeza zisijirudie tena na jinsi ya kutekeleza mapendekezo na ushauri wa Mkaguzi,"amesema Shauri.

Wakati huo huo akizungmza baada ya kufanyika kwa kikao hicho Shauri ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa wakati wa kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka wa fedha unaoishia Juni 30 , idadi kubwa ya walipa kodi wamejitokeza kulipa na kwao ni jambo la faraja kwani kuna muamko mkubwa wa wananchi wa kada mbalimbali kulipa kodi.

"Kasi ya ulipaji kodi kwa wananchi waliopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ni mkubwa, wengi wameendelea kulipa kodi ambazo wanatakiwa kulipa lakini tunaendelea kuhamasisha wananchi kuendelea kulipa kodi kwa maendeleo ya halmashauri yetu na Taifa kwa ujumla,"amesema.

YANGA KUTIKISA NA MATUKIO MATATU KILELE CHA SIKU YA MWANANCHI

0
0
Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga Dkt Mshindo Msolla amesema kuwa katika kilele cha siku ya mwananchi kutakuwa na matukio matatu muhimu.

Kilele cha siku ya mwananchi kinatarajiwa kuwa Julai 27 mwaka huu tutakuwa na matukio matatu ambapo kwanza kutambulisha jezi mpya za msimu wa 2019/20, pili ni utambulisho wa wachezaji wapya na wale waliosalia na tatu ni mchezo kimataifa wa kirafiki. 

Dkt Msolla amesema, katika kuelekea kilele cha siku ya mwananchi kutatanguliwa na shughuli mbalimbali za kijamii ndani ya wiki nzima ikiwemo kufanya usafi kwenye mahospitali.

Akizungumzia usajili wa msimu mpya na ripoti ya kocha mkuu Mwinyi Zahera, Dkt Msolla amesema wamesajili kulingana na matakwa ya mwalimu, pamoja na ukocha wake kwa miaka 40 wamesimamja uweledi na kufuata kile kocha alichokiandika kwenye ripoti yake.

"Naamini hata huko alipo lazima atakuwa anafuraha maana wachezaji wote wa nje na ndani aliokuwa akiwahitaji tumewapata pia siku tatu zilizopita mwalimu alituma program ya mazoezi ,sisi kama menejimenti tumejipanga kuhakikisha yote yanaenda sawa" amesema Dkt Msolla.

"Kwa wale wachezaji wote ambao hawatakuwa nao msimu ujao kila mmoja ameshapewa barua ya kujulishwa suala hilo na si jambo jema wachezaji hao kuwatangaza hadharani kwani huenda baadhi yao wakapokea taarifa hiyo kwa namna nyingine," amesema.

Mbali na hilo, uongozi wa Yanga kupitia kwa Mwenyekiti wake Dkt Msolla umetoa onyo na kutangaza rasmi kutokufumbia macho watengenezaji wa jezi feki wanaotumia nembo ya Klabu yao.

Amesema, amewapa siku nne wale wote wanaotumia nembo ya klabu kwa ajili ya utengenezaji wa jezi na vifaa mbalimbali kwa manufaa yao ya kibiashara na baada ya tarehe 30 mwezi huu mtu yeyote atakaejihusisha na uuzaji wa jezi feki hatua kali za kisheria zitachukuliwa juu yake.

Mwenyekiti amesema kuwa lengo ni kuwaita wafanyabiashara hao wa uuzaji wa jezi na kufanya nao mazungumzo kujua ni namna gani wanaweza kusaidiana kwenye swala hilo la mauzo ya jezi na vifaa mbalimbali vyenye nembo ya klabu.
Mwenyekiti wa Yanga Dkt Mshindo Msolla(kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuelekea kilele cha siku ya mwananchi Julai 27 mwaka huu.

WATANZANIA WAHAMASISHWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUTEMBELEA HIFADHI ZA TAIFA

0
0
Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha 

KAMISHNA Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi wa Taifa wa Ziwa Manyara Noel Myonga amesema mwitikio wa Watanzania kutembelea hifadhi za Taifa ni mdogo, hivyo ameshauri kuongeza kasi ya kutembelea vivutio vilivyopo nchini.

Akizungumza leo Juni 28,2019 na waandishi wa habari waliofanya ziara wakiwa na walimbwende wa taji la Mrembo wa Mkoa wa Arusha waliotembelea hifadhi hiyo Myonga amesema ni vema Watanzania wakajenga utamaduni wa kutemebela hifadhi zilizopo nchini.

"Kutembelea hifadhi zetu kunasaidia mambo mengi sana ikiwemo kujifunza jografia ya nchi yetu, kuona vivutio vilivyopo na hatimaye kuongeza pato la nchi pamoja a kujiburudisha kwani kuna kila kitu ambacho mhusika anataka kukiona kama sehemu ya kupata starehe,"amesema Myonga.

Amevitaja baadhi ya vivutio vinavyopatikana kwenye hifadhi ya Manyara ni pamoja na kuona Simba wapandao juu ya miti, Ziwa Manyara pamoja na chemchem ya maji moto.

Amesema wamekuwa wakiwahamasisha Watanzania wanaotutembelea hifadhi hiyo na kuwashawishi kwenda kwa wingi na kwamba katika kufanikisha hilo wamekuwa wakijitagaza mara nyigi lakini mwitikio ni mdogo.

Aidha amesema sio kwamba Watanzania hawana uwezo, bali utamaduni au mwamko wa kuwekeza fedha kwa ajili ya kutembelea kama wageni wa nje bado hawaoni thamani ya kufanya hivi, tukiamua tunaweza.

"Mtanzania anaona ni bora aende bar akatumie fedha kuliko kuja hifadhini ,ila naomba wabadilike kwa kuamua kutembelea hifadhi zetu badala ya kwenda kwenye maeneo mengine peke yake.Ukija hapa unalipa Sh.11,800 za kiingilio pamoja na VAT), gharama za usafiri ni kidogo kwa Mtanzania,"amesema Myonga.

Kwa upande wake Mhifadhi Ujirani mwema Ibrahimu Ninga ametumia nafasi hiyo kuzungumzia tatizo la ujangili katika hifadhi hiyo ambapo amesema moja ya jambo ambalo liliwahi kumnyima usingizi, ni matukio ya ujangili ambao kwa kweli yalisababisha wanyama kama vile tembo kuuawa kwa wingi

"Kazi ya kupambana na ujangili ni ngumu, lakini wao tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa, ndio maana mapaka sasa hali imetulia.Majangiri wana wanakuwa na mbinu nyingi kila kukicha, nasi tumejizitati kwelikweli, tumeimarisha doria zetu, tunashirikiana na wananchi ambao wanazunguka hifadhi hii na vyombo vingine vya dola kupambana na tatizo hili,"amesema Ninga.

Ameipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii  kwa kufanya kazi kubwa na wamekuwa hawalali ili kupambana na tatizo hilo."Nakumbuka ilifikia hatua majangili yalianza kutumia sumu kuua wanyama kwa wanyama ambao wanakula maboga kama tembo, wengi walikufa."
 kamishina msaidizi mwandamizi wa uhifadhi wa Taifa wa ziwa Manyara Noela Myonga akielezea historia ya ziwa manyara
 muhifadhi ujirani mwema Ibrahimu Ninga akiongoza watalii wa ndani kwenda kuona chem chem ya maji moto iliopo ndani ya hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara 
  Wageni kutoka nchi ya  Uingereza  waliotembelea hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara wakiwa katika moja ya kuvutio kili chopo ndani ya hifadhi hii wakiwa wanagusa maji ya chem chem ya maji moto kuhakikisha kama kweli  kama maji haya ni yamoto

TCRA yafunika kampeni ya Mnada kwa Mnada mkoani Kilimanjaro katika utoaji wa Elimu ya Usajili wa laini kwa kutumia alama za vidole

0
0
Wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro  na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi katika kampeni  ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu Mitandaoni  na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa ajili  ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa kuweka alama za vidole kwa laini za simu.

Mkuu wa TCRA Kanda ya Kaskazini  Julius Felix  amesema ni fursa kwa wananchi wa Kilimanjaro kupata huduma kutokana na kuwa na mnyororo wadau wa  mawasiliano. 

Amesema kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano. 

Felix mesema kuwa wananchi wasio kuwa na Vitambulisho vya NIDA wahakikishe  wanapata katika usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole. 
"TCRA iko karibu na wananchi katika utoaji wa elimu za utumiaji wa bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma hiyo" amesema ni fursa kwa wananchi wa Kilimanjaro kupata huduma kutokana na kuwa na mnyororo wadau wa  mawasiliano. 

Amesema kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano. 

Amesema kuwa wananchi wasio kuwa na Vitambulisho vya NIDA wahakikishe  wanapata katika usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole. 
"TCRA iko karibu na wananchi katika utoaji wa elimu za utumiaji wa bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma hiyo" Felix
 Afisa Masoko wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Doris Muhimbila akitoa maelezo kwa wananchi wakati kampeni ya Mnada kwa Mnada mkoani Kilimanjaro.
 Afisa wa Jeshi la Polisi Kitengo cha Makosa ya Mtandao akitoa maelezo kwa mwananchi kuhusiana na makosa ya mtandaoni yanayotokana na matumizi mabaya ya simu.
 Wananchi wakipata huduma mbalimbali katika kampeni ya Mnada Kwa Mnada inavyoendeshwa na TCRA.




Afisa Kusajili wa NIDA Mkoani wa Kilimanjaro Abubakar  kalinga akitoa maelezo wakati wananchi waliofika katika kampeni ya TCRA ya Mnada kwa Mnada.

SERIKALI YAIPOKEA KWA MIKONO MIWILI TAASISI YA 'WEFARM' NCHINI TANZANIA

0
0
Mkurugenzi Msaidizi wa Uinuaji wa  Mazao, Pembejeo na Ushirika wa Wizara ya Kilimo Bw. Beatus Malema (kushoto) akizindua taasisi ya 'Wefarm' kwa kushika nembo jijini Dar es Salaam. Pembeni wakwanza kulia ni Meneja Mkuu wa taasisi ya 'Wefarm' Bw. Nicholus John na Mkuu wa Idara ya ufuatiliaji wa taasisi ya We Farm Bi. Cyrila Anton.
Mkurugenzi Msaidizi wa Uinuaji wa  Mazao, Pembejeo na Ushirika wa Wizara ya Kilimo Bw. Beatus Malema akizungumza wakati wa uzinduzi wa taasisi ya 'Wefarm' iliyofanyika leo 28 Juni 2019 jijini Dar es Salaam.
Meneja Mkuu wa taasisi ya 'Wefarm' Bw. Nicholus John akizungumza na wakati wa uzinduzi wa taasisi hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Wageni waalikwa wakifuatilia uzinduzi huo.
Mkuu wa Idara ya ufuatiliaji wa taasisi ya We Farm Bi. Cyrila Anton (picha ya juu) akitoa ufafanuzi zaidi masuala mbalimbali ya wakulima.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.

Taasisi ya 'WEFARM' imezinduliwa itakayowawezesha wakulima kubadilishana taarifa kwa njia za kidigitali. Akizungumza na wanahabari wakati akizindua jukwaa la wakulima,Mkurugenzi Msaidizi wa Uinuaji wa  Mazao, Pembejeo na Ushirika wa Wizara ya Kilimo Bw. Beatus Malema

Amesema malengo ya serikali yetu nikuweza kufanya kazi pamoja na sekta binafsi, serikali za mitaa na watoa huduma wanaotoa huduma bora katika sekta ya Kilimo. "Tunakaribisha Wefarm naninaimani kuwa mmekwenda kwa wahusika katika sekta ya kilimo na wamewasaidia kujua changamoto zinazo wakabili," amesema Bw. Beatus Malema.

"Jukwaa la Wefarm limetengenezwa kwa uwazi na litawawezesha wakulima toka pande zote za Tanzania kuweza kupata elimu, maarifa, kupashana habari na kutatua matatizo ili kuuza bidhaa zilizo bora." amesema Bw. Malema. Kwa upande wake Meneja Mkuu wa WE FARM , Bw.Nicholaus John alisema huduma hiyo ni bure na mkulima atatuma ujumbe mfupi kupitia namba 15088.

“Mkulima ataweza kuuliza maswali na kupata majibu kutokana na matatizo mbalimbali yaliyopo shambani wkake, wazo hili lilikuja kutokana na kwamba wakulima wanachangamoto nyingin mashambani lakini wanakosa habari au ujuzi wa kuweza utatua matatizo yao.


TANESCO YAFANYA UPERESHENI MAALUM YA UKAGUZI JIJINI ARUSHA

0
0
Mhandisi Frederick Njavike ni Meneja wa wateja wakubwa Tanesco akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana namna ambavyo Shirika hilo limefanya ukaguzi wa mita zaidi ya 1000 katika maeneo mengi jijini Arusha ili kujiridhisha.
Zuberi Hassan ni Afisa Ukaguzi wa Mita amesema kuwa baada ya kufanya kama anavyoonekana akiendelea na ukaguzi huo ambapo wamegundua mita kadhaa zimechezewa ili zisiweze kusoma vizuri jambo ambalo ni hujuma kwa Shirika.



Na Vero Ignatus,Arusha.

Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) mkoani Arusha limebaini kuwa zaidi ya Mita 1000 zimechakachuliwa mara baada shirika hilo kufanya Operesheni maalumu ya kukagua kubaini waliofanya hivyo ni njia ya kukwepa kulipa huduma stahiki za umeme hivyo wamechukuliwa hatua za kisheria

Zuberi Hassan ni Afisa Ukaguzi wa Mita amesema kuwa baada ya kufanya ukaguzi huo wamegundua kuwa mita kadhaa ambazo zimechezewa ili zisiweze kusoma vizuri matumizi ya umeme jambo ambalo ni hujuma kwa shirika hilo.

Joseph Shirima ni Mmiliki wa eneo ambalo lilikaguliwa na kukutwa na tatizo la mita kuchakachuliwa , amesema kuwa tatizo hilo lilisababishwa na baadhi ya wapangaji wasio waaminifu kufunga mita zao hivyo atashirikiana na shirika hilo ili kuhakikisha mita zinazowekwa zina kuwa na usahihi.

Mhandisi Frederick Njavike ni Meneja wa wateja wakubwa Tanesco amesema kuwa shirika hilo limefanya ukaguzi wa mita zaidi ya 1000 katika maeneo mengi jijini Arusha ili kujiridhisha na mita zilizopo pamoja na kuchukua hatua stahiki ikiwemo kusitisha huduma za umeme pamoja na kuchukua hatua Kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wateja wenye tabia ya kuchezea mita

RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN ATEMBELEA VIFAA VIPYA VYA UJENZI WA BARABARA VYA UUB ZANZIBAR. KIBELE WILAYA YA KATI UNGUJA

0
0
IS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Ujenzi na Utunzaji wa Barabara Zanzibar (UUB) Eng. Ali Tahir Fatawi, akitowa maelezo ya Vifaa vipya vya Ujenzi wa Barabara alipotembelea eneo la Kituo cha UUB Kibwele Wilaya ya Kati Unguja. 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Kituo cha Idara ya Ujenzi na Utunzaji wa Barabara Kibele Wilaya ya Kati Unguja kuangalia Vifaa Vipya vua Ujenzi wa Barabara Zanzibar. 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Ujenzi na Utunzaji wa Barabara Zanzibar Eng. Ali Tahir Fatawi, akitowa maelezo ya moja ya kifaa cha ujenzi wa barabara cha Idara ya Ujenzi na Utunzaji wa barabara alipotelmbelea Kituo hicho Kibele Wilaya ya Kati Unguja kuangalia vifaa hivyo vipya vilivoagiziwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kulia Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Dr.Sira Ubwa Mwamboya 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Vifaa vipya vya Idara ya Ujenzi na Utunzaji wa Barabara Zanzibar (UUB) katika Kituo cha Kibele Wilaya ya Kati Unguja kushoto Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibare Mhe. Dr. Sira Ubwa Mwamboya na Naibu Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Mhe. Mohammed Ahmed Salum. 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akipata maelezo ya Mtambo Mpya wa kupikia lami kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Ujenzi na Utunzaji wa Barabara Zanzibar Eng. Ali Tahir Fatawi, akitembelea Vifaa vipya vya Idara hiyo katika Kituo chao Kibele Wilaya ya Kati Unguja 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamerd Shein, akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar, wakati wa ziara yake kutembelea Kituo cha Idara ya UUB Kibele Wilaya ya Kati Unguja 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Ndg. Mustafa Aboud Jumbe na kushoto Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Mhe.Dr. Sira Ubwa Mwamboya 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar, alipofanya ziara kutembelea Kituo cha UUB Kibele kuangalia vifaa vipya vya Idara hiyo, kushoto Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Mhe.Dr. Sira Ubwa na Naibu Waziri Mhe Mohammed Ahmed Salum. 
WAZIRI wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Mhe.Dr,. Sira Ubwa akizungumza wakati wa ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, kutembelea Vifaa Vipya vya Kisasa vya Idara ya UUB Zanzibar,katika Kituo hicho Kibele Wilaya ya Kati Unguja. 
(Picha na Ikulu)

DK.TAIRO:UTAFITI WA GMO UNAENDELEA

0
0
Mratibu wa Tafiti za Kilimo kutoka Taasisi ya Kilimo Tanzania (TARI) Dk.Fred Tairo akielezea utafiti unaondelea kuhusu mbegu za Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO) kwa wadau mbalimbali walioshiri kongamano kuhusu GMO. 
Wadau wakifuatilia mjadala 
Waandishi wakimhoji Dk.Fred Tairo kuhusu utafiti wa GMO nchini. 


…………………… 
NA SULEIMAN MSUYA 

SERIKALI imesema utafiti kuhusu Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO), unaendelea katika Kituo vyake vya Utafiti Kilimo Mikocheni (MARI) na Shamba la Majaribio 
Makutupora Dodoma. 

Kauli ya Serikali kuendelea na utafiti wa GMO inakuja ikiwa ni takribani miezi minne imepita baada ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigimwa kutangaza uamuzi wa Serikaki kusitisha utafiti huo. 

Akizungumza na waandishi wa habari Mratibu wa Tafiti za Bioteknolojia za Kilimo nchini Dk. Fred Tairo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Mikocheni (TARI Mikocheni), wakati akiwasilisha mada ya hali ya utafiti wa GMO nchini kwenye mkutano wa mjadala wa wazi wa siasa za uchumi wa GMO ulioandaliwa na Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) alisema wao wanaendelea na utafiti katika vituo husika. 

Dkt. Tairo alisema TARI haijaacha kufanya utafiti wa GMO tangu walivyoanza na kwamba utafiti umeonesha matokeo chanya. 

Alisema taarifa zilizokuwa zimesambazwa kuwa utafiti huo umesitishwa hazikuwa sahihi na kwamba wanaendelea na utafiti katika hatua mbalimbali. 

“Baadhi ya vyombo vya habari na wananchi walielewa vibaya kauli iliyotolewa serikali ilitaka watafiti wafuate utaratibu wa kutoa matokeo waliyokuwa wanayapata kwenye majaribio hayo ili kuondoa mkanganyiko,” alisema Tairo. 

Mtafiti huyo alisema utafiti wa GMO TARI Mikocheni na Makutupora unaendelea na utakapokamilika matokeo yake yatawasilishwa serikalini kwaajili ya kufanyiwa maamuzi ya kuitumia au kitoitumia. 

Mratibu huyo wa Bioteknolojia alisema umuhimu wa serikali kufanya tafiti za GMO ni ili kukabiliana na changamoto sugu zinazotokana na madiliko ya tabia nchi ikiwemo ukame, wadudu na magonjwa sugu ili kuongeza tija kwa wakulima. 

Alisema kuwa majaribio yanayofanyika katika taasisi ya utafiti ya Makutupora Mkoani Dodoma unalenga kutafuta ufumbuzi wa changamoto ya ukame na bungua wa mahindi na kwa matokeo ya awali yameonyesha kufanikiwa pia kupambana pia na Viwavi jeshi vamizi. 

Dk.Tairo alisema TARI imefanya utafiti kwa upande wa zao la Muhogo ambao unalenga kuipa kinga mihogo kupambana na magonjwa sugu ya batobato kali na michirizi ya kahawai ambayo yanaathiri sana zao wakulima wa muhigo afrika hasa kusini mwa Jangwa la Sahara. 

Mtafiti huyo alisema GMO imeonesha kuwepo na matokeo chanya ya chakula, rutuba, usalama wa chakula na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. 

“Napenda kuweka wazi Tanzania ipo katika hatua ya pili ya utafiti ambao ni wa kwenye shamba maalum baada ya kumaliza ule wa ndani unaofanyika MARI. Nasisitiza kuwa hakuna bidhaa ya GMO inaayozalishwa nchini,” alisema. 

Kwa upande wake Mtafiti kutoka chuo kikuu cha Sayansi na teknolojia cha Nelson Mandela Mashamba Philipo alisema teknolojia hiyo ni nzuri ila serikali, wakulima na watafiti wanapaswa kukaa pamoja kuona kama ni muda muafaka wa teknolojia hiyo kutumika hapa nchini. 

Mtafiti huyo alisema teknolojia hiyo ina uwezo wa kuwezesha nyanya kuwekewa Jeni ambayo inauwezo wa kuifanya isiharibike ndani ya mwezi mmoja hata baada ya kuichuma na hivyo kumuongezea tija mkulima. 

Philipo alisema teknolojia hiyo sio ngeni duniani kwa kuwa inatumika nchi mbalimbali kama Marekani, China, Brazil na nyingine nyingi za afrika zinaitumia lakini ni muhimu wadau wote wapewe elimu ili kuondoa mashaka waliyona kuhusu teknolojia hiyo. 

Mtafiti Emmanuel Sulle ambaye ni Mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu katika Chuo Kikuu cha Western Cape Afrika Kusini alissema kuna haja ya serikali kuongeza bajeti kwenye tafiti za kilimo nchini ili kuwezesha watafiti kupatafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili wakulima. 

Sulle alisema pia Serikali inawajibu wa kuongeza idadi ya watafiti kwenye utafiti wa aina hiyo ambao unakuwa kwa kasi duniani ili waweze kuwa na uwezo wa kufanya tafiti hizo katika viwango vinavyotakiwa kimataifa. 

Alisema pamoja na kufanya tafiti za GMO lakini lazima watafiti waangalie mbinu zingine za asili wanazozitumia wakulima na kuziboresha na kuongeza uzalishaji 

Kwa upande Janet Maro wa Shirika la Sustainable Agriculture Tanzania (SAT) waliitaka Serikali kuongeza juhudi kwenye utafiti ili kuwepo na matokeo chanya ya utafiti huo. 

Alisema iwapo jitihada zitaongezeka katika kukabiliana na magonjwa yanayoshambulia mazoa usalama wa chakula utakuwepo. 

Abdallah Mkindi wa Shirika la TABIO alisema kilimo kinahitaji mikakati ya pamoja hivyo ni vema Serikali ijipange kwa kuongeza watafiti.

MWANZA,ARUSHA WANG’ARA RIADHA MITA 800 UMITASHUMTA 2019

0
0

Mwanariadha Damian Christian wa Arusha (kulia) ambaye alishika nafasi ya kwanza akiwaongoza wanariadha wenzake kumaliza mbio za mita 800 katika fainali zilizofanyika leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara. 
Wanariadha Lucia Nestory (kulia) na mwenzake Salima Mussa wote kutoka Mwanza wakimaliza mbio za mita 800 katika fainali iliyofanyika leo asubuhi katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara 
Msichana Shija Donard wa Mwanza (kushoto) akifuatiwa na Bertha Doto wa Geita, na Emiliana Ndele wa Mbeya kwenye fainali za mita 200 zilizofanyika leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara 
…………………. 

Na Mathew Kwembe, Mtwara 
Wanariadha Damian Christian wa Arusha na Lucia Nestory wa Mwanza wamefanikiwa kushinda fainali za mbio za mita 800 kwa wavulana na wasichana katika mashindano ya UMITASHUMTA yaliyofanyika leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara. 

Damian alitumia dakika 2:05:11 kujishindia medali ya dhahabu katika fainali hizo ambapo nafasi ya pili ilichukuliwa na mkimbiaji Tilulu masanja kutoka mkoa wa Morogoro ambaye alitumia dakika 2:05:32, huku mshindi wa tatu katika mbio hizo akiwa ni Masanja Ngado kutoka mkoa wa Tabora ambaye alitumia dakika 2:05:41 na hivyo kufanikiwa kushinda medali ya shaba. 

Kwa upande wa wasichana Lucia wa Mwanza aliyejishindia medali ya dhahabu alitumia dakika 2:21:00, ambapo nafasi ya pili pia ilichukuliwa Salima Mussa pia kutoka Mwanza ambaye alitumia dakika 2:21:16, na nafasi ya tatu ilishikwa na Nyanzobe Mrahi kutoka mkoa wa Mara ambaye alitumia dakika 2: 22:80 

Katika fainali za mita 200 kwa wavulana ambazo pia zilifanyika leo asubuhi, nafasi ya kwanza ilishikwa na mkimbiaji Steven Stephano wa Tabora ambaye alitumia muda wa sekunde 24:58 na hivyo kujitwalia medali ya dhahabu, nafasi ya pili ilichukuliwa na mwanariadha Hamis Hussein wa Geita aliyetumia muda wa sekunde 24:97, huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Daniel Emanuel wa Mwanza aliyetumia dakika 25:09. 

Kwa wasichana, nafasi ya kwanza katika mbio za mita 200 ilichukuliwa na Shija Donard wa Mwanza ambaye alikimbia kwa muda wa sekunde 27:94, nafasi ya pili ilishikwa na Bertha Doto wa Geita aliyetumia sekunde 28:40, na nafasi ya tatu ilienda kwa mwanariadha Emiliana Ndele wa Mbeya ambaye alitumia sekunde 28:45. 

Katika fainali za mbio za kupokezana kijiti mita 100 x 4 kwa wavulana nafasi ya kwanza imechukuliwa na mkoa wa Mwanza ambapo washiriki wake walitumia jumla ya sekunde 47:94, nafasi ya pili imechukuliwa na mkoa wa Tabora ambapo wanariadha wake walitumia sekunde 50:19, huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na washiriki kutokamkoa wa Mara ambapo walitumia sekunde 51:00. 

Kwa wasichana nafasi ya kwanza ilichukuliwa na washiriki wa mkoa wa Mwanza, wakifuatia na mkoa wa Mara na nafasi ya tatu imeshikwa na mkoa wa Geita. Wanariadha wa Mwanza walitumia jumla ya sekunde 54:78, Mara walitumia sekunde 55:15 na Geita walitumia sekunde 57:25. 

Katika mashindano ya kuruka chini kwa wavulana nafasi ya kwanza ilichukuliwa na mwanariadha Laurent Robert wa mkoa wa Geita ambaye alijishindia medali ya dhahabu baada ya kuruka urefu wa mita 5 na sentimita 57, nafasi ya pili ikienda mkoa wa Mwanza ambapo mwanariadha wake Kamdi Momona aliruka urefu wa mita 5 na sentimita 50, huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Leonard Vises kutoka mkoa wa Shinyanga ambaye aliruka urefu wa mita 5 na sentimita 47. 

Kwa upande wa wasichana katika mchezo wa kuruka chini nafasi ya kwanza ilinyakuliwa na Mosha Julius wa Mwanza ambaye aliruka urefu wa mita 4 na sentimita 57, nafasi ya pili ilichukuliwa Eliza Keraju kutoka mkoa wa Mara ambaye aliruka urefu wa mita 4 na sentimita 42, huku nafasi ya tatu ilichukuliwa na Shija Donard ambaye aliruka urefu wa mita 4 na sentimita 42. 
Katika mchezo wa kurusha kisahani kwa upande wa wavulana, nafasi ya kwanza ilichukuliwa na Kelvin John kutoka mkoa wa Mara ambaye alitwaa medali ya dhahabu aliyefanikiwa kurusha umbali wa mita 25 na sentimita 98, nafasi ya pili ikichukuliwa na Sadiki Mgale wa Songwe ambaye alirusha umbali wa mita 23na sentimita 73 na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Njendage Njanje wa Manyara aliyerusha umbali wa mita 23 na sentimita 23. 

Kwa wasichana, mshindi wa kwanza ni Debora Dambela wa Manyara ambaye alirusha kisahani umbali wa mita 20 na sentimita 46, nafasi ya pili ilichukuliwa na Mariam kumge wa Simiyu ambaye alirusha umbali wa mita 19 na sentimita 62, huku nafasi ya tatu ilichukuliwa na Shija Donard wa Mwanza ambaye alirusha umbali wa mita 19 na sentimita 59.

LINDI WATAKIWA KUSHIRIKI KATIKA ZOEZI LA UMEZAJI KINGATIBA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

0
0

NA WAMJW-LINDI 

WAKAZI wa Lindi na vitongoji vyake wametakiwa kushiriki katika kampeni ya kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa kumeza kingatiba za kutokomeza magonjwa hayo pamoja na kutunza mazingira kwa kuondoa mazalia ya mbu wanaenezao magonjwa hayo. 

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uzinduzi wa kambi ya upasuaji wa Mabusha na Ngirikokoto(Henia) unaofanyika mkoani Lindi. 

“Wakazi wa Lindi na Vitongoji vyake tunatakiwa kushiriki katika zoezi la kumeza dawa za kukinga magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele pamoja na kufanya usafi wa mazingira ili kuondoa mazalia ya mbu”alisema Dkt. Ndugulile 

Aidha, Dkt. Ndugulile amewataka wananchi wa Lindi kuondoa dhana potofu ya kuwa kila mwenye mabusha au ngirimaji basi atakuwa amerogwa ila ajue ugonjwa huo unasababishwa na vimelea vinavyotokana na mbu na kuzingatia umezaji wa dawa hizo. 

Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuhakikisha wanapambana kutokomeza ugonjwa huo Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya Utafiti ya uchimbani mafuta na gesi ya Statoil wamepata fedha za kuwafanyia upasuaji wagonjwa 200 wa mabusha na ngirikokoto kwa awamu ya kwanza ya mwaka 2017 na wagonjwa 200 kwa awamu ya pili ya mwaka 2018. 

Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amesema kuwa wananchi wa Lindi wanatakiwa kutoa taarifa sehemu husika pindi wanapoambiwa kuwa dawa muhimu hakuna kwenye vituo vya afya vya Serikali kwani dawa hizo zipo kwa asilimia 90 Mkoani humo. 

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Bw. Ramadhani Kaswa amesema kuwa umezajii wa kingatiba ya magonjwa hayo umefikia asilimia 70 kwa mwaka 2016/2017. 

Aidha, Bw. Kaswa amesema kuwa kutokana na zoezi la kuwatambua wagonjwa wenye mabusha na ngirikokoto wamejiandikisha wagonjwa 1294 kwa mkoa wa Lindi ikiwemo Manispaa ya Lindi wagonjwa 67,Wilaya ya Nachingwea wagonjwa 101,Halmashauri ya Lindi wagonjwa 633, Wilaya ya Liwale wagonjwa 387 na Wilaya ya Luongo wagonjwa 106. 

Uzinduzi huo uliambatana na zoezi la kumeza Kingatiba za magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ikiwemo mabusha na matende,usubi,minyoo,trakoma(vikope) na vichocho.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile


Serikali Iringa yapongeza diwani kwa kunusuru uhai wa familia zilizokosa matibabu

0
0
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela wa pili kushoto akiwa na diwani wa Mwangata Nguvu Chengula (mwenye suti nyeusi) na viongozi wengine wakimtazama mama wa watoto watatu ambao nusuru wapoteze maisha kwa kukosa huduma ya matibabu


Na Francis Godwin, Iringa 

Serikali ya wilaya ya Iringa imepongeza jitihada za diwani wa kata ya Mwangata Nguvu Chengula (CCM) za kuokoa maisha ya mkazi wa Mwangata D Amida Mgonakulima na wanae watatu wasife kwa kukosa matibabu baada ya kutelekezwa na ndugu wakiwa nyumbani. 

Pongezi hizo zimetolewa na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard kasesela leo baada ya kuwatembelea wagonjwa hao waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa wakiendelea na matibabu ,kuwa jitihada hizo zilizochukuliwa na diwani huyo ni za kupongezwa kwani bila kufanya hivyo uwezekano wa mwanamke huyo na wanae kupona ulikuwa ni mdogo. 

“Nimefarijika sana kuona hali ya wagonjwa hao ikiendelea vizuri maana huyo mama wa watoto alianza kuoza kuanzia kiunoni kushuka chini na hakuwa na uwezo hata wa kusimama kitandani lakini kwa sasa afya yake inazidi kwenda vizuri hakika diwani Chengula kanusuru uhai wao “ alisema Kasesela . 

Huku akitoa agizo kwa viongozi wa serikali za mitaa katika wilaya ya Iringa kufanya msako nyumba kwa nyumba ili kujua watoto ama wagonjwa waliotelekezwa kwa kukosa huduma za matibabu. 

“ Yawezekana kabisa wagonjwa hao ni baadhi tu ya wagonjwa wengi ambao wamefungiwa ndani bila kutibiwa sasa naagiza watendaji wa mitaa kupita nyumba kwa nyumba kukagua na kama kuna nyumba mlango utakutwa umefungwa fungueni kagueni ndani mkiwa na mwenye nyumba ili kujua ndani kuna nini “ alisema Kasesela 

Kasesela alisema tukio jingine kama hilo la Mwangata la mgonjwa kutelekezwa amelisikia kijiji cha Kisanga na amekwisha tuma watendaji kwenda kufuatilia na kuwa matukio yote hayo ni ya kikatili na hatakubali kuyasikia ama kuyaona ndani ya wilaya yake. 

Kwa upande wake diwani Chengula alisema uamuzi wa kunusuru uhai wa wagonjwa hao ulikuja baada ya wananchi wake kutoa taarifa na kuwa ataendelea kuwasaidia wagonjwa hao hadi watakapopona . 

Aidha Chengula ambae leo ameweza kuungana na mkuu huyo wa wilaya ya Iringa kukabidhi mahitaji mbali mbali zikiwemo nguo na mengine amejitolea kumsomesha motto wa darasa la tatu katika shule yake ya Sun Academy ambapo ada yake kwa mwaka ni zaidi ya shilingi milioni moja na kuwa atamlipia kwa miaka yote na kumwendeleza

WATENDAJI DUMISHENI NIDHAMU KATIKA UTENDAJI WENU-MAJALIWA

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisoma hotuba yake ya kuahirisha Bunge, jijini Dodoma Juni 28, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewatakaviongozi wote na watendaji wa Serikali kuanzia ngazi ya kijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa hadi wizara kuwajibika ipasavyo na kudumisha nidahmu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kuwahudumia wananchi.

Amesema ili kufikia lengo na dhamira ya kutekeleza Mpango na Bajeti ya Serikali ya 2019/2020 kwa ufanisi, viongozi hao wanatakiwa waendelee kuwasisitiza wananchi washiriki ipasavyo kulinda miundombinu inayojengwa kwa gharama kubwa na Serikali.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Juni 28) wakati akiahirisha mkutano wa 15 wa Bunge, Bungeni jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Septemba tatu mwaka huu.

Pia, Waziri Mkuu amezitaka mamlaka husika zishirikiane na wadau wengine katika kudhibiti uharibifu wa mazingira kwa kukomesha ukataji hovyo wa misitu, uchafuzi wa bahari, mito na maziwa na taka za plastiki ili kulinda mazingira asilia.

Akizungumzia kuhusu bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Waziri Mkuu amesema Serikali imepanga kutumia jumla ya sh. trilioni 33.11, kati yake sh. trilioni 20.86 zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida sawa na asilimia 63. “Aidha, sh. trilioni 12.25, sawa na asilimia 37 ya bajeti yote zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya maendeleo. 

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasihi Watanzania pamoja na Washirika wa Maendeleo waiunge mkono Serikali katika kutekeleza vipaumbele vilivyowekwa kwenye bajeti ya mwaka 2019/2020 ili viweze kutoa mchango wa haraka katika maendeleo ya uchumi na ya watu. 

Wakati huo huo,Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu uboreshwaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, ambapo amesema kwa sasa Tume ya Taifa ya Uchaguzi inakamilisha maandalizi hayo ikiwa sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani.

“Uboreshaji huo, unatarajiwa kuanza tarehe 18 Julai, 2019 katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro ambapo litafanyika kwa muda wa siku 7 kwa kila kituo na kuendelea hadi tarehe 5 Machi, 2020 litakapohitimishwa katika mkoa wa Dar es Salaam.” 

Waziri Mkuu amesema uboreshaji huo hautahusisha wapiga kura walioandikishwa mwaka 2015 isipokuwa utawahusu wapiga kura wapya waliotimiza umri wa miaka 18 na kuendelea au watakaotimiza umri huo ifikapo siku ya uchaguzi mkuu ujao. 

Ametaja kundi lingine litakalohusika na zoezi hilo kuwa ni pamoja na wale watakaoboresha taarifa zao, kama waliohama jimbo au kata na kuhamia katika maeneo mengine ya kiuchaguzi, waliopoteza au kadi zao kuharibika, watakaorekebisha taarifa zao pamoja na kuwaondoa waliopoteza sifa kama vile kufariki.

Hivyo, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wananchi wote wenye sifa kutumia fursa hiyo kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura ili kutimiza haki yao ya kikatiba.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa Novemba mwaka huu kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambao ni sehemu muhimu katika kuimarisha utawala bora na demokrasia ambayo imeendelea kunawiri nchini. Amewataka wananchi wenye sifa kujitokeza wakati utakapofika.

Amesema Serikali imeendelea kutumia mbio za mwenge kuhamasisha wananchi washiriki uchaguzi huo kupitia kaulimbiu isemayo “Maji ni haki ya kila mtu, tutunze vyanzo vyake na tukumbuke kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa”.

“Napenda kutumia fursa hii kutoa wito kwa wadau mbalimbali na wananchi kwa ujumla hususan wale wenye sifa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kupiga kura ili waweze kutumia haki yao ya kidemokrasia ya kuchagua au kuchaguliwa katika uchaguzi huo.”

Kwa wananchi wenye nia ya kugombea katika uchaguzi huo, Waziri Mkuu amesema ni lazima wajue majukumu wanayoomba kwamba yanahitaji umakini mkubwa na uchapaji kazi kwa sababu Serikali imewekeza miradi mingi kote nchini, hivyo wanahitajika watu walio tayari kuhakikisha wanasimamia miradi hiyo ili itoe matokeo yanayokusudiwa.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuhakikisha uwepo wa mazingira salama na tulivu kwa kipindi chote cha uchaguzi.

TACAIDS - "MSIDANGANYIKE, HAKUNA MBADALA WA ARV"

0
0
Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) imewataka watu wanaoishi na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutodanganyika na kuacha kutumia dawa kupunguza makali ya VVU kwani hakuna mbadala wa ARV.

Rai hiyo imetolewa leo Juni 28,2019 na Mkurugenzi wa Uraghbishi na Habari wa TACAIDS, Bw. Jumanne Issango wakati akifunga Kambi ya Ariel 2019 iliyoandaliwa na asasi inayolenga kutokomeza UKIMWI kwa watoto na familia Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI).

Akizungumza kwenye kambi hiyo iliyojumuisha watoto na vijana 50 kutoka mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Mwanza na Mara Bw. Issango alisema kuwa inasikitisha kuona kuwa watu wengine wanaacha kutumia ARV na kisha kujikita kwenye dawa za kienyeji au maombi. “Matokeo yake ni VVU kuendelea kuwashambulia. Kinachosaidia kupunguza makali ya VVU mwilini ni ARV peke yake, hakuna mbadala,” alisisitiza.

Mkurugenzi huyo alisema, “Msidanganyike mkaacha kutumia dawa za ARV, mpaka sasa bado wanasayansi hawajapata dawa nyingine. Tunaamini ipo siku dawa itapatikana lakini kwa sasa wenye maambukizi ya VVU endeleeni kuwa wafuasi wazuri wa dawa na mtumie kwa usahihi.”

Akizungumzia vita dhidi ya maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kazi ambayo asasi ya Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) imekuwa ikiifanya tangu kuanzishwa kwake, Mkurugenzi huyo alisema kuwa hicho ni kipaumbele cha taifa hivyo hakina budi kufanyiwa kazi kwa juhudi.

Alisema kwa watoto na vijana wenye maambukizi, wataendelea kupata huduma za matunzo na tiba bila ubaguzi wowote ili kuhakikisha kuwa afya zao zinaendelea vizuri hivyo kuweza kufikia ndoto zao za baadaye.

“Kwa kazi zenu, AGPAHI mnagusa maisha ya Watanzania wengi. Kitendo cha kusaidia upatikanaji wa huduma za matunzo na tiba kwa wanaoishi na VVU ni cha utu. AGPAHI ni asasi ya kiutu na inajali Watanzania. Tunawashukuru kwa kuendelea kushirikiana na serikali kutoa huduma hizi muhimu,” alisema.

Aidha alikumbusha kwamba kuwa na maambukizi ya VVU siyo changamoto ya kumzuia mtu anayeishi na VVU kusonga mbele katika maisha yake na kutimiza ndoto zake, “Kinachotakiwa ni kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya,” alisema.

Kutokana na umuhimu wake, Bw. Issango aliziomba serikali za mikoa ambako AGPAHI inafanya kazi kushirikiana na asasi hiyo kikamilifu ili kuendelea kutoa msaada wa kisaikolojia kwa watu wanaoishi na maambukizi ya VVU.

Wakisoma risala yao, washiriki wa Ariel Camp 2019 waliiomba serikali kuiunga mkono AGPAHI ili huduma za kisaikolojia kwa watoto na vijana ziendelezwe na kuenezwa nchi nzima hivyo kuwafikia watoto wengi zaidi.
Mkurugenzi wa Uraghbishi na Habari wa TACAIDS, Bw. Jumanne Issango akifunga Kambi ya Ariel 2019 iliyoandaliwa na asasi inayolenga kutokomeza UKIMWI kwa watoto na familia Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) leo katika ukumbi wa Landmark Hotel jijini Dar es salaam. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Meneja Mawasiliano wa AGPAHI, Bi. Agnes Kabigi akizungumza wakati wa kufunga Ariel Camp 2019 iliyoanza Juni 23,2019.
Keki maalumu kwa ajili ya washiriki wa Kambi ya Ariel 2019.
Mkurugenzi wa Uraghbishi na Habari wa TACAIDS, Bw. Jumanne Issango na watoto wakikata keki ya Kambi ya Ariel 2019.
Mkurugenzi wa Uraghbishi na Habari wa TACAIDS, Bw. Jumanne Issango akilishana keki na mtoto aliyeshiriki Kambi ya Ariel 2019.
Mkurugenzi wa Uraghbishi na Habari wa TACAIDS, Bw. Jumanne Issango akiendelea na zoezi la kuwalisha keki washiriki wa Kambi ya Ariel 2019.
Kijana wa sarakasi kutoka kundi la Baba Watoto akitoa burudani ya kuzungusha meza kwa kutumia miguu wakati wa kufunga Kambi ya Ariel 2019.
Mshiriki wa Ariel Camp 2019 akitoa burudani ya kuimba.
Vijana wa sarakasi kutoka kundi la Baba Watoto wakitoa burudani.
Mkurugenzi wa Uraghbishi na Habari wa TACAIDS, Bw. Jumanne Issango akimkabidhi mtoto zawadi ya begi lenye vifaa vya shule.
Zoezi la kugawa zawadi likiendelea.
Vijana wakiangalia zawadi ya mabegi waliyopewa.
Walezi watoto nao walipata zawadi.
Mkurugenzi wa Uraghbishi na Habari wa TACAIDS, Bw. Jumanne Issango akiangalia michoro mbalimbali iliyochorwa na washiriki wa kambi ya Ariel 2019 inayoelezea historia ya maisha yao na ndoto zao katika maisha.
Washiriki wa Kambi ya Ariel 2019 wakiwa katika picha ya pamoja.
Washiriki wa Kambi ya Ariel 2019 wakiwa katika picha ya pamoja wakionesha zawadi ya mabegi yao.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Madaktari wa UN watembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuangalia huduma za matibabu ya moyo na mishipa ya damu wanazozitoa

0
0
Madaktari kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) wakimsikiliza Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo Khuzeima Khunbhai kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akiwaeleza jinsi wagonjwa waliolazwa katika chumba cha uangalizi maalum (CCU) wanavyotibiwa. Madaktari hao walifanya ziara ya kutembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo na mishipa ya damu wanazozitoa. 
Madaktari kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) wakimsikiliza Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tiba Shirikishi Delila Kimambo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akiwaeleza jinsi duka la dawa la Taasisi hiyo linavyotoa huduma kwa wagonjwa. Madaktari hao walifanya ziara ya kutembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo na mishipa ya damu wanazozitoa. 
Dk. Adarsh Tiwathia kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) akiongea jambo wakati wa kikao na viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa ziara yao ya kutembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo na mishipa ya damu wanazozitoa. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na madaktari kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) wakati wa ziara yao ya kutembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo na mishipa ya damu wanazozitoa.

Afisa Utamaduni Sumbawanga atoa kibao cha Kusifu Kasi ya Maendeleo nchini

0
0
Katika kuunga mkono na kuieleza jamii juu ya juhudi zinazofanya nwa serikali ya Awamu ya Tano chini ya Uongozi wa Dkt. John Pombe Magufuli, Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Sumbawanga Kiheka Charles a.k.a K Chars ameibuka na wimbo wa kuelezea mazuri yanayofanywa na serikali ya Tanzania. 

Katika kueleza malengo ya kutunga wimbo huo alioupa jina la Mchaka Mchaka na kumshirikisha msanii Mackpaul Sekimanga a.k.a Makamua, K Chars alisema kuwa kama kiongozi na mshauri wa wasanii ni jukumu lake kuwaonesha wasanii mada mbalimbali za kuimba na sio kujikita kuyaimbia mapenzi wakati wanaweza kuimba kuhusu kuhamasisha lishe bora, kuhimiza kilimo cha mazao mbalimbali na faida zake, kukemea mimba za mashuleni, ndoa za utotoni, kuboresha huduma za afya nakadhalika. 

“Hakuna msanii wa nje atakayekuja kusifu nchi yetu isipokuwa sisi wenyewe kusifia maendeleo yetu na kuyatangaza kwa wengine, hivyo nikaona niyaweke katika wimbo mazuri yaliyofanywa na serikali ambayo jamii inapaswa kuyafahamu, msanii ana nafasi kubwa ya kusikilizwa na jamii na yapo mengi ya kuyazungumzia katika maisha yetu, hivyo ni vyema wasanii wakajielekeza katika kuhamasisha mambo ya kimaendeleo, kuyaimba mazuri ya serikali na kuyaibua yale ambayo wanaona serikali inahitaji kuyafahamu ili yafanyiwe kazi,” Alisema 

Halikadhalika, alisifu juhudi za Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga, James Mtalitinya, kwa kumuunga mkono katika juhudi za kuibua vipaji vya wasanii wa Sumbawanga tangu kuanzishwa shindano la “Sumbawanga Talent Search” lililowahusisha wasanii wa kuimba, hadi kumalizika kwa shindano hilo. 

Katika Shindalo hilo ambalo fainali yake ilifanyika usiku wa mkesha wa Mwenge wa Uhuru 2019 na mshindi wa kwanza alipata shilingi 300,000/=, wa pili 200,000/= na wa tatu 100,000/= na walioingia kwenye kumi bora wamepewa fursa ya kurekodi wimbo wa kuelezea fursa za uwekezaji zinazopatikana katika Mkoa wa Rukwa pamoja na kusifu ukarimu wa watu wa mkoa huo, kibao kinachotarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi July,2019. 

K Chars ametumia fursa hiyo kuwaomba viongozi mbalimbali wa mkoa kuwasaidia na kuwaunga mkono wasanii wachanga wanaoutangaza mkoa.

WAZIRI KAMWELWE ATAKA MAJINA YA WASIMAMIZI WA MIRADI YA MAJENGO INAYOSIMAMIWA NA TBA.

0
0

Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

*Amuagiza Katibu Mkuu (Sekta ya Ujenzi) kupatiwa majina ya Wasimamizi wa miradi hiyo.

*Ujenzi wa Mradi Nyumba za Magomeni Kota, wakamilika kwa asilimia 40

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Ujenzi) kupatiwa majina ya Wasimamizi wa Miradi mbalimbali nchini inayosimamiwa na Wakala wa Majengo nchini (TBA) kuangalia Taaluma zao.

Waziri Kamwelwe ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari alipotembelea mradi wa ujenzi wa Nyumba maarufu Magomeni Kota unaoendelea jijini Dar es Salaam.Amesema Serikali imetoa jumla ya Shilingi Bilioni 2 kukamilika mradi huo, amesema kinachoonekana katika ujenzi wa nyumba hizo hakiridhishi.

"Nimebaini hakuona watu wanaofanya kazi, ujenzi umelala na sio kwa sababu ya fedha, kwani htiwezi kuingia mikataba halafu baadae tunawalipa?" amehoji Waziri Kamwelwe."Fedha ya Serikali haiwezi kufanya mafunzo kwa Wataalamu, sasa naagiza Miradi yote ya nchi nzima wale Wasimamizi wenye Taaluma nipate majina yao nataka kila mradi uwe na msimamizi wake", amesema Waziri Kamwelwe.

Hata hivyo, Waziri Kamwelwe amefanya ziara katika mradi wa nyumba uliopo Bunju B jijini Da es Salaam, ambapo amesifu ubora wa nyumba hizo zilizojengwa kwa viwango vinavyokubalika.Amesema amepeleka mapendekezo kwa Serikali Kuu kuhusu nyumba ambazo zimenunuliwa na Watumishi wa Serikali na tayari Watumishi hao wamehamia makao makuu Dodoma, amependekeza kwa Serikali kwa Watumishi hao kubadilishiwa nyumba hizo zilizopo Dar es Salaam na zile za Dodoma.

Mradi wa ujenzi wa Bunju B jijini Dar es Salaam una viwanja 851 kwa ajili ya makazi ya Watumishi na ujenzi huo unatekelezwa kulingana na Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM)

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe (aliyevaa suti nyeusi) akipata maelekezo kutoka kwa Mmoja wa Wataalamu wa Wakala wa Majengo nchini (TBA) kwenye mradi wa Nyumba za Makazi uliopo Magomeni Kota.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe akipata maelekezo ya sehemu ya ndani katika ujenzi wa Nyumba za Magomeni Kota.
 Majengo yanayoendelea kujengwa katika eneo la Magomeni Kota.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe akiwa ameongozana na Wataalamu wa TBA katika mradi wa ujenzi wa Nyumba za Bunju B jijini Dar es Salaam.

CHAKULA DAWA SULUHISHO LA UDUMAVU NA LISHE DUNI KAGERA .

0
0
Anaandika Abdullatif Yunus wa Michuzi TV.

Kufuatia hali ya Udumavu na Lishe duni kwa asilimia Kubwa ya Watoto katika Kaya nyingi zinazopatika Mkoani Kagera, Imeonekana kuwa Suluhisho pekee la kuondokana na changamoto hiyo ni Kutumia chakula dawa, chenye virutubishi maalum kwa ajili ya Afya ya Mtoto.

Shirika la Kimataifa linalohusiana na masuala ya Afya na Lishe Bora, lijulikanalo kama IMA World Health Tawi la Mkoa wa Kagera, kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara yenye dhamana, linaendelea na Kampeni yake Mkoani humo iitwayo "Mtoto Mwelevu, Ni Jukumu langu" lengo likiwa ni kuhakikisha tatizo la Udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano katika Mikoa ya kanda ya ziwa, Kagera ikiwa ni mmojawapo linapungua kwa asilimia kubwa.

Akizungumza Katika Tamasha la Mtoto Mwelevu Katika Kata ya Buyango Wilayani Missenyi, Juni 27, 2019. Afisa Afya Mkoa wa Kagera Nelson Lumberi kwa Niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa, amesema Jamii ina wajibu mkubwa katika kuzingatia suala la Lishe bora kwa watoto, ikiwa tunalenga kupunguza Udumavu Mkoani Kagera, na Lishe hiyo ni vyakula vya kawaida ambavyo upatikanaji wake ni rahisi kwani hupatikana zaidi katika mazingira yao, hivyo suala linabaki namna ya kupangilia mlo na hatimae kupatikana kwa matokeo Bora ya Mtoto anayekua, na Mtoto mwenye akili.

Tayari IMA World Health wamekwishaanza utaratibu huo kwa kuziendea Kaya ambazo suala la lishe limekuwa changamoto katika Halmshauri za Mkoa wa Kagera, Missenyi, ikiwa mojawapo kwa kutoa mafunzo ya Lishe kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya hiyo, Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii (WAJA) Ambapo Jamii inaelekezwa namna ya kuandaa Chakula Dawa, ambapo katika Kata ya Buyango watoto waliofanyiwa tathimini na Mradi kwa kupimwa kiwango cha utapiamlo Jumla ni 541, kati ya hao waliogundulika na utapiamlo ni 114 ambapo waliingizwa kwenye Darasa la Chakula Dawa kwa Siku 12. 

Kati ya hao watoto 6 hawakuhudhuria na mmoja wapo kupoteza Maisha na kufanya idadi kuwa watoto 107 walioendelea na Kumaliza Darasa. Siku ya 12 asilimia 83 ya watoto waliongezeka uzito na asilimia 55 Afya zao ziliimarika. Wazazi mpaka sasa wanaendelea na zoezi hilo nyumbani ambapo Afya za watoto 107 zimeendelea kuimarika.

Hayo yanajiri ambapo Takwimu zikionesha kuwa hali ya Udumavu Nchini ni asilimia 34.7 wakati Mkoa wa Kagera Udumavu ni asilimia 41.7 hivyo Shirika la IMA World Health wakijitahidi kupunguza kiwango hicho kwa asilimia 7 kufifikia 2020.


Pichani ni Bi. Geniva Ereneus (30) Mama Wa watoto Mapacha Oliva na Olivia Ereneus akiendelea kuwalisha Chakula Dawa katika Tamasha la Mtoto Mwelevu Kata Buyango, Wilaya ya Missenyi.
Mtoto Safina Ahmad (4) akiendelea kunywa uji Wa lishe ambao ni Chakula dawa, wakati wa Tamasha la Mtoto Mwelevu Wilayani Missenyi kama alivyokutwa kamera yetu.
Pichani ni Afisa Afya Mkoa wa Kagera Nelson Lumberi akizungumza na wananchi waliohudhuria Tamasha la Mtoto Mwelevu, kwa niaba ya Mgeni rasmi Mganga Mkuu wa Mkoa Kagera.
Pichani ni Wadau kutoka IMA World Health na wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii (WAJA) wakifurahia Tamasha la Mtoto Mwelevu kwa kucheza ngoma ya asili, katika hafla iliyofanyika Wilayani Missenyi.
Pichani ni Sehemu ya Wazazi na walezi kutoka Kata Buyango, wakiwa katika Tamasha la Mtoto Mwelevu lililofanyika Katika Zahanati ya Kata Buyango, Wilayani Missenyi Juni 27, 2019.
Pichani ni mmoja kati ya akina mama waliohudhuria Tamasha la Mtoto Mwelevu, baada ya kumgawia mwanae Chakula Dawa.

TUNDU LISSU AVULIWA UBUNGE,JIMBO LIPO LAKE LATANGAZWA KUWA WAZI

MPANGO WA BLUEPRINT KUANZA JULAI MOSI MWAKA HUU-MAJALIWA

0
0
WAZIRI MKU Kassim Majaliwa amesema kuanzia Julai Mosi mwaka huu Serikali itaanza kutekeleza Mpango Kazi wa Utekelezaji wa Mpango wa Kuboresha Mfumo wa Udhibiti wa Biashara nchini (Blueprint) kwa lengo la kurahisisha mazingira ya kufanya biashara.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Juni 28) wakati akiahirisha mkutano wa 15 wa Bunge, jijini Dodoma. Amesema wakati kazi hiyo inaendelea Serikali itafanya ufutialiaji kuhusu utekelezaji wa mpango huo na kutathmini kama lengo limefikiwa.

”Utekelezaji wa mpango huo unakwenda sambamba na dhamira ya Serikali ya kurahisisha mazingira ya kufanya biashara nchini, unaojidhihirisha kupitia sheria ya fedha ya mwaka 2019 ambayo imefuta tozo kwamishi 54 zilizobainishwa kwenye mpango huo.”

Waziri Mkuu ametaja tozo zilizoondolewa au kupunguzwa ni pamoja na zinazosimamiwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), Wizara ya Mifugo na Uvuvi hususan kwenye Sekta ya Mifugo, Wizara ya Maliasili na Utalii na Wizara ya Maji

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema katika kuhakikisha utekelezaji wa mpango huo unaleta tija, ameielekeza Wizara ya Viwanda na Biashara ishirikiane na Ofisi ya Waziri Mkuu kusambaza blueprint pamoja na Mpango Kazi wa Utekelezaji kwa wizara zote kwa ajili ya kusimamia utekelezaji katika maeneo yao.

Amesema kupitia mpango wa bajeti ya 2019/2020, Serikali itaendelea kuweka mazingira rahisi ya ufanyaji biashara kwa kutoa unafuu katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi pamoja na shughuli nyingine jumuishi.

Wakati huohuo,Waziri Mkuu amesema katika kukabiliana na kilimo tegemezi cha mvua hususani kwenye zama hizi za mabadiliko ya tabia nchi, Serikali kwa sasa inaboresha kilimo cha umwagiliaji kwa lengo la kuwatoa wananchi katika kilimo hicho.

Amesema hatua zilizochukuliwa hadi sasa ni pamoja na kuunda upya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ambayo inalenga kuiwezesha tume hiyo kusimamia ipasavyo shughuli za umwagiliaji. Pia Serikali imehamishia tume hiyo Wizara ya Kilimo ambayo ndiyo yenye dhamana ya kuendeleza kilimo nchini.

”Ili tuweze kufikia lengo la kuongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji kutoka hekta 475,056 za sasa hadi hekta 1,000,000 ifikapo mwaka 2025, tayari nimeielekeza Wizara ya Kilimo isimamia kwa karibu na kutekeleza majukumu yake kwa weledi.”

Waziri Mkuu amesema Wizara ya Kilimo inatakiwa ihakikishe inasimamia vema miradi 22 ya umwagiliaji inayoendelea sasa pamoja na miradi mipya minane itakayojengwa nchini katika pindi cha mwaka wa fedha 2019/2020.

WAJUMBE KAMATI TENDAJI MABUNGE JUMUIYA YA MADOLA TAWI LA TANZANIA WAPATIWA SEMINA YA KUJENGEWA UWEZO BUNGENI JIJINI DODOMA

0
0


 Mjumbe wa kamati tendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika tawi la Tanzania, Mhe. Dkt. Sware Semesi (kulia) akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo (hawapo kwenye picha) wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati tendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika tawi la Tanzania iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bunge na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Mhe. Mussa Azzan Zungu
 Mwenyekiti wa Bunge na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Mhe. Mussa Azzan Zungu akifungua semina ya kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati tendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika tawi la Tanzania iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.
 Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dkt. Emmanuel Mallya akiwasilisha maada wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati tendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika tawi la Tanzania iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.
 Mjumbe wa kamati tendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika tawi la Tanzania, Mhe. Zainab Vullu akizungumza wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati tendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika tawi la Tanzania iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma. Kulia ni Mjumbe wa kamati tendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika tawi la Tanzania, Mhe. Mohamed Mchengerwa
Wajumbe wa kamati tendaji ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika tawi la Tanzania, Sekretarieti ya Mabunge ya Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika tawi la Tanzania pamoja na wawezeshaji wakiwa katika picha ya pamoja baada ya semina ya kujengewa uwezo iliyofanyika leo katika Ofisi za Bunge Jijini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Viewing all 109593 articles
Browse latest View live




Latest Images