Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

GAVANA SHILATU AWAPA ZAWADI BODABODA

$
0
0

Na Mwandishi wetu Mihambwe

Vijana wengi nchini wamejiajiri katika sekta isiyo rasmi ya uendeshaji wa Pikipiki almaarufu Bodaboda ili kuweza kuyaendesha maisha yao pamoja na wategemezi wao.

Katika hali ya kutambua mchango wao kwa jamii na kwa Taifa, Afisa Tarafa Mihambwe Emmanuel Shilatu amewapa zawadi ya viakisi mwanga “Reflectors” bure kwa Bodaboda waliopo Tarafa ya Mihambwe ambao wana vitambulisho vya Wajasiriamali Wadogo kwani wameonyesha utii na heshima kubwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuvinunua vitambulisho vilivyotolewa nae.

“Bodaboda inabidi muelewe Serikali ya Rais Magufuli inawapenda sana na ndio maana Leo hii tunawazawadia reflectors bure kabisa kwa wote mliomuunga mkono Rais Magufuli kwa kununua vitambulisho vya Wajasiriamali vinavyouzwa kwa Tsh. Elfu ishirini tu. Serikali itahakikisha hamsumbuliwi wakati mnatimiza majukumu yenu, muhimu mzingatie sheria za usalama Barabarani.” Alisisitiza Gavana Shilatu huku akishangiliwa na Bodaboda.

Mpaka sasa kwenye Tarafa ya Mihambwe Bodaboda wa kata za Kitama, Miuta, Mihambwe na Mkoreha wameshapatiwa viakisi mwanga pamoja na kupewa Elimu ya usalama Barabarani toka kwa Askari wa usalama Barabarani (Trafiki) waliombatana nae kwenye ziara hiyo.

Mantrac Tanzania yaunga mkono sera ya Serikali ya viwanda

$
0
0
Huku Serikali ikipiga chapuo kwa ajili ya kuwa nchi ya viwanda na yenye uchumi wa kati, Mantrac Tanzania Limited imeweka historia mpya, ikiwa ya kwanza kwenye sekta ya uchimbaji.

Mantrac ndio waliopewa idhini ya kushughulikia bidhaa za Caterpillar nchini Tanzania, wakisambaza na kuhudumu katika mashine za CAT.

Akizungumza jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Meneja Mauzo wa Mantrac Tanzania, Butwa Sanga, alisema kwamba katika kujaribu kwenda kwa hali ya juu na kasi ya viwanda, kampuni hiyo inayoshughulikia mashine zenye uwezo mkubwa imekuja na chapa mpya ya Caterpillar yenye ufanisi mkubwa na inayookoa muda.

Alitambulisha mashine mpya kuwa ni New Generation Hydraulic Excavator (NGH) Caterpillar itakayoleta mapinduzi makubwa kwenye ajenda ya kuelekea kwenye nchi ya viwanda, kwa sababu ina ufanisi wa hali ya juu, gharama ndogo na inachukua muda mfupi kukamilisha kazi.

“Viwanda havijengwi kwa mkono, vinahitaji mashine zenye uwezo mkubwa kufanya hivyo,  na kwa kutumia mashine hizi mpya za NGH Caterpillar zilizoingia sokoni, tunatarajia kwamba watu waliojipanga kujenga viwanda vipya watapata kile kinachofaa sana kwa kazi hiyo ili kwenda haraka, tofauti na modeli zile za zamani,” alisema.

Bw. Sanga alikuwa akizungumza kwenye mafunzo ya siku tatu yanayokwenda kwa jina la ‘Changamoto ya Mafundi’ ambapo Mantrac inatoa mafunzo kwa mafundi 30 juu ya jinsi ya jinsi ya kutumia caterpillars hizo mpya zenye teknolojia ya hali ya juu.

Alisema kwamba makatapila hayo mapya ya NHG yanapunguza muda wa kazi kwa nusu na wakati huo huo kupunguza matumizi ya mafuta kwa kati ya asilimia 25 na 45 huku yakiongeza tija na uzalishaji.
 Mkufunzi kutoka Kampuni ya Mantrac, Ehab Abdelfatah Mohamed, (mwenye miwani) akitoa maelezo kwa baadhi ya waendeshaji kutoka makampuni tofauti  kuhusu mashine mpya za uchimbaji aina ya Caterpillar,  zinazosambazwa na kampuni hiyo jijini Dar es Salaam. Waendeshaji hao wanahudhuria mafunzo ya siku tatu yaiyoandaliwa na kampuni ya Mantrac Tanzania.  

Wamachinga Arusha wanufaika na Tigo Business,wakabidhiwa simu 247 na miamvuli 100

$
0
0
 
Meneja wa Tigo Kanda ya Kaskazini Lilian Mwalongo (kati kati) akikabidhi sehemu ya miavuli 200 kwa viongozi wa wafanya biashara wadogo wadogo mkoani Arusha maarufu kama Wamachinga. Kulian ni mwenyekiti wa umoja huo Amina Njoka na kushoto ni makamu mwenyekiti Iddi Hussein

Meneja wa Tigo Kanda ya Kaskazini Lilian Mwalongo (kati kati) akikabidhi moja ya boksi lenye simu 247 kwa viongozi wa wafanya biashara wadogo wadogo mkoani Arusha maarufu kama Wamachinga. Kulian ni mwenyekiti wa umoja huo Amina Njoka na kushoto ni makamu mwenyekiti Iddi Hussein.

Meneja wa Tigo Kanda ya Kaskazini Lilian Mwalongo (kati kati) akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi kabla ya kukabidhi zawadi za simu 247 kwa viongozi wa wafanya biashara wadogo wadogo mkoani Arusha maarufu kama Wamachinga. Kulian ni mwenyekiti wa umoja huo Amina Njoka.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Tigo mkoani Arusha wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Wamachinga muda mfupi bada ya kuwakabidhi simu 247 pamoja na miavuli 200 kwa ajili ya kusaidia kuboresha biashara zao jijini Arusha jana.



Kupitia Chama Cha Wamachinga Mkoa wa Arusha, leo tarehe 26/06/2019 kampuni ya Tigo kupiti kitengo chake cha Tigo Business imetoa simu 247 pamoja wa miavuli 100 kwa wateja wake ambao ni wanachama wa umoja huo wa wafanya biashara wadogo wadogo.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuwakabidi vifaa hivyo kwa wateja hao 247, Meneja wa Tigo Kanda ya Kaskazini Lilian Mwalongo alisema, zawadi hizo ni utaratibu wa kawaida wa kampuni hiyo kuwazawadia na kuwashukuru wateja wake waliopo kwenye vikundi na unalenga kuboresha biashara zao pamoja na mazingira wanayofanyia kazi.

“Leo kampuni ya Tigo inayofuraha kukabidhi vifaa hivi kwa wateja wetu ambao ni wanachama wa Umoja wa Wamachinga hapa mkoani Arusha. Ni utaratibu wetu wa kawaida kuwapa zawadi wateja waaminifu kama hawa na tunaamini vifaa hivi vitawasadia kuboresha biashara zao huku wakifurahia huduma bora kutoka Tigo,” alisema

Lilian alifafanua kuwa, kampuni ya Tigo hutoa zawadi mbali mbali ikiwamo simu za mkononi kwa wateja wa malipo ya baada waliopo kwenye vikundi na ambao hutumia huduma za Tigo wakiwa na mkataba wa miezi 12 au 24.

Ili mteja aweze kunufaika na zawadi hizi anatakiwa kujiandikisha kama mteja wa walipo ya baada (postpaid) na ni lazima awe katika kikundi au kampuni kubwa AU ndogo. Hivyo basi, tunakaribisha vikundi, makampuni pamoja na taasisi kwa ajili ya kupata huduma zetu nzuri na za uhakika za mawasiliano.

Meneja huyo pia aliwataka wanafuaika wa zawadi hizo kuendelea kutumia mtandao wa Tigo na kuongeza kuwa Tigo inajali na kuwekeza kwa wateja na wabia wake wa biashara ili kuhakikisha kuwa watanzania wote wawanufaika na huduma bora za mawasiliano.

KAMISHNA MPYA TIRA DKT JUMA AKABIDHIWA OFISI RASMI LEO JIJINI DAR

$
0
0
Aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) Dkt Baghayo Abdallah Saqware amekabidhi rasmi majukumu kwa Kamishna mpya Dkt Mussa Juma leo kwenye ofisi zao Jijini Dar es salaam.
Dkt Juma ameteuliwa mapema wiki hii na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ambapo uteuzi wake ulianza rasmi Juni 25, mwaka huu.
Kabla ya kuteuliwa kuchukua nafasi hiyo, Dkt Juma alikuwa Mkuu wa Idara ya Bima katika kitivo cha Bima na Hifadhi ya Jamii cha Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM). TIRA ni mamlaka ya inayosimamia  Bima zote nchini.
Aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) Dkt Baghayo Saqware(kulia) wakikumbatiana na   Kamishna mteule wa Mamlaka hiyo Dkt Mussa Juma baada ya  makabidhiano ya majukumu kwenye ofisi zao leo Jijini Dar es Salaam. Dkt Juma ameteuliwa Juni 25 mwaka huu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.
 Aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) Dkt Baghayo Saqware(kulia) akikabidhi taarifa za ofisi kwa Kamishna mteule wa Mamlaka hiyo Dkt Mussa Juma kwenye ofisi zao leo Jijini Dar es Salaam. Dkt Juma ameteuliwa Juni 25 mwaka huu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.
 Aliyekuwa Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) Dkt Baghayo Saqware(kushoto) akiweka saini kwenye nyaraka zenye taarifa za ofisi sambamba na Kamishna mteule wa Mamlaka hiyo Dkt Mussa Juma wakati wa makabidhiano ya majukumu kwenye ofisi zao leo Jijini Dar es Salaam. Dkt Juma ameteuliwa Juni 25 mwaka huu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

MISITU YA MIKOKO INASAIDIA KUZUIA MABADILIKO YA TABIANCHI- NAIBU WAZIRI SIMMA

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, Mhe. Mussa Simma amesema misitu ya mikoko husaidia kuzuia mabadiliko ya tabianchi kutokana na joto la dunia.

Mhe. Sima amesema hayo leo Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Chambani, Yussuf Salim Hussein aliyetaka kujua Serikali inafaidikaje na rasilimali ya miti ya kikoko iliyoanza katika Ukanda wa Pwani ya Tanga hadi Mtwara. 

Naibu Waziri Sima alisema mfumo wa ikolojia unaopatikana katika misitu ya mikoko unasaidia kuondoa kiwango kikubwa cha hewa ya ukaa ambayo ingeweza kuongeza joto la dunia na kusababisha mabadiliko ya tabianchi.

“Umuhimu wa misitu ya mikoko ni pamoja na kuwa na mazalia na makazi ya viumbe wa baharini na pia misitu hii huhifadhi fukwe na mazingira ya bahari na hivyo kuokoa mali na maisha ya wakazi wa pwani kuepukana na vimbunga, dhoruba na mawimbi ya bahari,” alisema.
Akuendelea kujibu swali hilo Mhe. Sima alisema mikoko husaidia kuchuja udongo, uchafu na sumu inayoweza kutiririshwa na maji na kuingia baharini na kuharibu matumbawe (mawe laini yanayopatikana baharini) ambayo ni makazi ya samaki.

Aidha, aliongeza kuwa misitu ya mikoko ni muhimu kwa Taifa kwani husaidia katika malighafi ya ujenzi yaani mbao, ufugaji nyuki, mapato ya Serikali kutokana na vibali vya mbao.

VODACOM TANZANIA FOUNDATION YAPONGEZWA KWA MCHANGO WAKE KATIKA KUSAIDIA JAMII

$
0
0
Vodacom Tanzania Foundation imezindua ripoti ya maendeleo ya jamii na mkakati mpya wa kuchochea ukuaji jumuishi leo Juni 27, 2019  ikiwa taasisi isiyo ya kiserikali ya Vodacom Tanzania Foundation ambayo imekuwa ikishiriki shughuli mbalimbali za kimaendeleo na leo imezindua ripoti yake ya mchango wa maendeleo ya jamii kwa miaka mitatu iliyopita (2014-2017) pamoja na mkakati mpya wa miaka mitatu 2019-2021 unaolenga kuchochea elimu jumuishi, ukuaji wa sekta ya kilimo, kuboresha mazingiza na ujumuishwaji wa watu kwenye mifumo rasmi ya kifedha.

Uzinduzi huo umefanyika leo katika tukio lililopewa jina la "Alama za upendo wa Vodacom" na kuhudhuriwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - Afya(TAMISEMI), Josephat Kandege, maafisa kutoka washirika wa maendeleo na wadau wa kitaifa na kimataifa imeelezwa kuwa.

Taasisi ya Vodacom Foundation imewekeza zaidi ya shilingu bilioni 11 katika miradi ya jamii ambayo imedhamiria  kuboresha maisha ya watu takribani milioni 3 nchini kupitia miradi mbalimbali hususani afya ya uzazi, elimu na huduma jumuishi za kifedha.

Akizungumza katika hafla hiyo Kandege amepongeza jitihada za Vodacom Tanzania Foundation katika kusaidia jamii na kusisitiza ushirikiano kati ya wadau mbalimbali.

 "Nawapongeza sana Vodacom kwa kuunga mkono jitihada za serikali katika kuboresha maisha ya watanzania na hasa katika sekta ya afya ya uzazi, elimu na uwezeshaji wa kiuchumi. Kuendeleza Tanzania ni jukumu letu sote hivyo basi ni muhimu sana tuungane pamoja kutimiza azma hii ya taifa letu. Natumai kwamba ripoti hii itatuhamasisha sote kuchangia Nguvu katika kuboresha maisha ya watanzania" ameeleza Kandege.

Aidha Kandege amesema kuwa ni jambo jema kwa makampuni ya namna hiyo kuiga mfano wa kampuni Vodacom kwa kushiriki katika kusaidia jamii katika masuala ya kijamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania,  Hisham Hendi amezungumzia juu ya mkakati huo mpya wa Taasisi hiyo na kueleza kuwa,
 "Mkakati wetu wa 2019-2021 umezingatia mipango ya maendeleo ya nchi (Tanzania) na malengo endelevu ya maendeleo (SDGs) huku tukilenga kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha, ubora wa elimu na kuchochea mabadiliko katika sekta ya kilimo. Kama mtandao wa simu unaoongoza nchini, tuna nafasi ya pekee kuchangia maendeleo ya jamii na ya kiuchumi nchini kwa kupitia matumizi ya teknolojia ya simu." Ameeleza.

Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa kampuni za simu zina fursa kubwa na wajibu wa kutumia teknolojia na uvumbuzi wa kidijitali kukuza uchumi wa nchi kwa kuongeza ufanisi wa watu. Kampuni ya Vodacom imekuwa ikifanya hivyo tangu mwaka 2000.

Pia Mkurugenzi wa Taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation, Bi. Rosalynn Mworia, amesisitiza mashirika kuwekeza katika miradi inayolenga kutatua changamoto mbalimbali za kijamii.

 "Tumeshirikisha wadau mbalimbali katika uzinduzi wa ripoti hii ili kuwahamasisha kuwekeza katika miradi ya kuboresha jamii na kuchochea ushirikiano zaidi baina yetu na wao ili kufikia lengo la kuwa taifa lenye maendeleo jumuishi.” amesema Rosalynn.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2006, Taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation imekuwa ikishirikiana na taasisi mbalimbali, imechangia vilivyo katika kuboresha maisha ya Watanzania kupunguza umasikini, kuboresha elimu, kuwezesha Wanawake na Wasichana, pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma za afya ya uzazi.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-Afya (TAMISEMI) Josephat Sinkamba Kandege( wa pili kulia) akizindua ripoti ya Taasisi isiyo ya kiserikali ya Vodacom Tanzania Foundation ya mchango wa maendeleo ya jamii kwa miaka mitatu iliyopita (2014-2017) pamoja na mkakati mpya wa miaka mitatu 2019-2021 unaolenga kuchochea elimu jumuishi, ukuaji wa sekta ya kilimo, kuboresha mazingiza na ujumuishwaji wa watu kwenye mifumo rasmi ya kifedha. Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jones Kilimbe, katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi, wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo na wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-Afya (TAMISEMI) Josephat Sinkamba Kandege( wa pili kulia) akifurahi mara baada ya kuzindua ripoti ya Taasisi isiyo ya kiserikali ya Vodacom Tanzania Foundation ya mchango wa maendeleo ya jamii kwa miaka mitatu iliyopita (2014-2017) pamoja na mkakati mpya wa miaka mitatu 2019-2021 unaolenga kuchochea elimu jumuishi, ukuaji wa sekta ya kilimo, kuboresha mazingiza na ujumuishwaji wa watu kwenye mifumo rasmi ya kifedha. Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jones Kilimbe, katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi, wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo na wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-Afya (TAMISEMI) Josephat Sinkamba Kandege( wa pili kulia) akizungumza na wadau mbalimbali wa maendeleo wakati wa uzinduzi ripoti ya Taasisi isiyo ya kiserikali ya Vodacom Tanzania Foundation ya mchango wa maendeleo ya jamii kwa miaka mitatu iliyopita (2014-2017) pamoja na mkakati mpya wa miaka mitatu 2019-2021 unaolenga kuchochea elimu jumuishi, ukuaji wa sekta ya kilimo, kuboresha mazingiza na ujumuishwaji wa watu kwenye mifumo rasmi ya kifedha.
Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi akisoma hotuba iliyokuwa inahusu Taasisi isiyo ya kiserikali ya Vodacom Tanzania Foundation wakati wa uzinduzi ripoti ya Taasisi hiyo ya mchango wa maendeleo ya jamii kwa miaka mitatu iliyopita (2014-2017) pamoja na mkakati mpya wa miaka mitatu 2019-2021.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jones Kilimbe akizungumza kuhusu mamlaka hiyo inavyofanya kazi bega kwa bega na Taasisi isiyo ya kiserikali ya Vodacom Tanzania Foundation wakati wa uzinduzi ripoti ya Taasisi hiyo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Meza kuu
Baadhi ya wadau wa maendeleo kutoka taasisi mbalimbali za hapa nchi wakiwa kwenye uzinduzi ripoti ya Taasisi isiyo ya kiserikali ya Vodacom Tanzania Foundation ya mchango wa maendeleo ya jamii kwa miaka mitatu iliyopita (2014-2017) pamoja na mkakati mpya wa miaka mitatu 2019-2021 unaolenga kuchochea elimu jumuishi, ukuaji wa sekta ya kilimo, kuboresha mazingiza na ujumuishwaji wa watu kwenye mifumo rasmi ya kifedha.
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi ripoti ya Taasisi isiyo ya kiserikali ya Vodacom Tanzania Foundation ya mchango wa maendeleo ya jamii kwa miaka mitatu iliyopita (2014-2017) pamoja na mkakati mpya wa miaka mitatu 2019-2021 unaolenga kuchochea elimu jumuishi, ukuaji wa sekta ya kilimo, kuboresha mazingiza na ujumuishwaji wa watu kwenye mifumo rasmi ya kifedha.

SERIKALI YAWAASA WANANCHI KUTOTUMIA DAWA ZA KULEVYA ILI KULINDA NGUVUKAZI YA TAIFA

$
0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewaasa wananchi wake kutojihusisha na matumizi ya dawa za kulevya ili kulinda nguvukazi ya Taifa kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George Mkuchika (Mb) kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya kupiga vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.

Mhe. Mkuchika amesema matumizi ya dawa za kulevya yanaleta athari kwa jamii nzima, kwani hushusha kiwango cha uzalishaji na hatimaye kukwamisha maendeleo ya Taifa.
 “Matumizi ya dawa za kulevya yanaathiri kwa kiasi kikubwa nguvukazi ya Taifa letu, ambayo ndio tegemeo katika uzalishaji na ukuzaji wa uchumi wa Taifa letu” Mhe. Mkuchika amesisitiza.

Mhe. Mkuchika amezitaja dawa za kulevya zinazotumika kwa wingi kuwa ni bangi, mirungi, heroin, cocaine na baadhi ya dawa za hospitali zenye asili ya kulevya kama vallium, ketamine, pethidine, indocile, morphine na tramadol.
Mhe. Mkuchika amewataka wananchi kuepuka matumizi ya dawa za kulevya ili kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano za kuijenga nchi kuwa ya viwanda na kufikia lengo la uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

“Jitihada za Serikali kuwa nchi ya viwanda zinahitaji fedha katika utekelezaji wake, hivyo badala ya kutumia fedha nyingi kukabiliana na tatizo la dawa za kulevya, tutumie fedha hizi kujenga miundombinu itakayotukuzia uchumi na kutuletea maendeleo katika Taifa letu” Mhe. Mkuchika amesema.
Aidha, Mhe. Mkuchika ametoa rai kwa wananchi kushirikiana na vyombo vya dola kutoa taarifa za uwepo wa matumizi na biashara ya dawa za kulevya katika maeneo wanayoishi ikiwa ni pamoja na kuwaomba viongozi wa dini kuungana na serikali kukemea matumizi ya dawa za kulevya kwani wanayo nafasi kubwa katika jamii kuwajenga vijana kiroho, kimwili na kisaikolojia ili wawe na tabia njema.

Naye, Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (Mb) akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu) Mhe. Jenista Mhagama (Mb) amesema tatizo la dawa za kulevya ni janga kubwa duniani kote na kwa bahati mbaya watumiaji wa dawa hizo kwa asilimia kubwa ni vijana ambao ndio tegemeo la uzalishaji na viongozi watarajiwa.

Maadhimisho ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya hufanyika kila mwaka Juni, 26 kwa lengo la kutoa fursa kwa umma kupata elimu kuhusu athari za matumizi na biashara ya dawa za kulevya kwa mustakabali wa maendeleo ya Taifa letu.
  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akizungumza na wananchi wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.
 Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) (hayupo pichani) wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (Mb) akizungumza na wananchi wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.
 Mmojawapo wa waathirika wa dawa za kulevya, Bw. Said Bandawa akitoa ushuhuda wa namna Serikali ilivyomsaidia kuondokana na matumizi ya dawa za kulevya wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya kupiga vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb) akiteta jambo na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (Mb) wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya kupiga vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.

UHABA DAWA ZA KULEVYA NCHINI WASABABISHA 'MATEJA' KUVUTA SUMU YA PANYA KUPATA STIMU

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya Jamii
IMEELEZWA  kwamba baada ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini kudhibiti uingizwaji na biashara ya dawa hizo hivi sasa waliokuwa wanajihusisha na utumiaji wa dawa hizo wanahaha kutafuta mbadala wake ili kupata stimu kiasi cha baadhi yao kuanza kuvuta sumu ya panya.

Baadhi ya wamiliki wa nyumba za kuhudumia walioathirika na utumiaji wa dawa za kulevya nchini wameiambia Michuzi Blog kwenye mahojiano maalumu kuwa upatikanaji wa dawa za kulevya kwa sasa umekuwa mgumu, hivyo wanaondelea na utumiaji wa dawa hizo wanahaha katika kuzipata kwake, hivyo wapo ambao wanatumia dawa za hospitali na wengine wanatumia sumu ya panya.

Mmoja wa wamiliki wa nyumba za Sober House kutoka New Vision Society Hamis Shuila amesema kazi nzuri ambayo inafanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini, kupitia Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, huko mtaani waliokuwa wanajihusisha na utumiaji wa dawa wapo katika wakati mgumu sana.

"Tunatoa huduma kwa walioathirika na dawa za kulevya na wameamua kuacha kwa hiyari yao.Hata hivyo hata wale ambao wanaendelea kutumia dawa za kulevya wanaishi maisha magumu.Ni ngumu sana kupata dawa ya kulevya kama ilivyokuwa huko nyuma.Ndio maana wengine wanalazimika kutumia dawa za hospitali kama mbadala wa dawa za kulevya.Wanatumia na wanapata stimu kama kawaida.

"Pia wapo ambao wao hawawezi kupata dawa za hospitalini, hivyo wanachokifanya wanachukua hii sumu ya panya ambayo unaijua wewe na kisha kuichanga kwenye kwenye bangi na baada ya hapo wanavuta na hakuna utofauti kati ya sumu ya panya  iliyochanganywa kwenye bangi na dawa za kulevya.Stimu ni ile ile tu na wanalewa vizuri,"amesema Shuila.

Amefafanua wanaotumia sumu ya panya kwa kuchanganya kwenye bangi na kisha kuvuta au kutumia dawa za hospitali si kwamba wanapenda ila kinachotokea watumiaji wa dawa za kulevya ni wagonjwa na hivyo wanatafuta mbinu yoyote kujitibu na hasa kwa kuzingatia akikosa kuvuta mwili unakuwa na maumivu makali sana.

"Hawa wanaotumia dawa za kulevya tunawaita ni wagonjwa na wakati mwingine wanakuwa kama wagonjwa wa akili.Hata hivyo akikosa dawa anakuwa na alosto ambayo hiyo itamfanya atumie mbinu yoyote kupata dawa, hata wale ambao unaona wamepora,wamejeruhi ili kupata fedha wanachotafuta ni kujitibu yale maamivu ambayo wanayasikia, hivyo wako tayari kufanya chochote na hajali hata kufa,"amesema Shuila.

Hata hivyo amesisitiza umuhimu wa Watanzania kuachana na utumiaji wa dawa za kulevya kwani madhara yake ni makubw kwa jamii, na kwamba wapo wengi waliokuwa wanatumia dawa hizo na sasa wameacha na kubaki kuwa watu weme na wanaendelea na majukumu yao ya ujenzi wa familia na nchi kwa ujumla.

Kwa upande wake Kamishna wa Kinga na Tiba wa Mamlaka ya Kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya Peter Mfisi amesema kutokana na kuzibwa kwa njia zote za kuingizwa kwa dawa za kulevya kumesababisha watumiaji kutafuta njia mbadala na hivyo wapo
wanaotumia dawa za hospitali kuvuta.

Hata hivyo ametoa ombi kwa watumishi wa  Hospitali, vituo vya afya, maduka ya dawa pamoja na Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kuhakikisha dawa zilizopo hospitalini zinatumika kwa mujibu wa utaratibu ikiwa pamoja na kutumiwa kwa wagonjwa husika na kwa maelekezo ya daktari na si kuacha zikaingia mtaani na kutumika kama dawa za kulevya.
Mmojawapo wa waathirika wa dawa za kulevya, Said Bandawa akitoa ushuhuda wa namna Serikali ilivyomsaidia kuondokana na matumizi ya dawa za kulevya wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya kupiga vita Dawa za Kulevya duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano, jijini Tanga.


MWENYEKITI WA MTANDAO WA SAUTI YA SOBER TANZANIA AIOMBA SERIKALI KUWASAIDIA MAENEO YA KUFANYA SHUGHULI ZA UCHUMI

$
0
0
Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii 
MWENYEKITI wa Mtandao wa Sauti ya Sober  House Tanzania Al-Karim Banji ameiomba  Serikali kusaidia upatikanaji wa maeneo ya ardhi kwa ajili ya shughuli za uchumi ikiwa pamoja na kuhakisha vijana ambao wanachana na matumizi ya dawa za kulevya wanajikita  kufanya kazi kwa bidii.

Amefafanua kazi ya Soba House pamoja na mambo mengine ni kuhakikisha aliyeathirika na  matumizi ya dawa za kulevya anaachana na dawa hizo na wanafanikisha hilo lakini  changamoto kubwa baada ya hapo walioamua kuacha dawa wanakosa kazi ya kufanya na matokeo yake akirudi mtaani anaanza kutumia tena.

Banji ametoa ombi hilo wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Dawa za Kulevya  Duniani ambayo hufanyika kila Juni 26 ya kila mwaka ambapo kitaifa yamefanyika katika Jiji  la Tanga na mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais Samia Suluh Hassan aliyewakilishwa na  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Mkuchika.

"Changamoto iliyopo wale ambao wanapata huduma baada ya kurudi mtaani wanarudia  tena kutokana na kukosa kasi .Hivyo inakuwa rahisi kushawishika na kurudi kwenye utumiaji dawa za kulevya.Ombi letu kubwa ni kupata maeneo ya shughuli za kiuchumi kama kufanya kilimo, ufugaji , ufyatuaji tofauli na aina nyingine ya kazi ambazo waliochana na dawa za kulevya watafanya wakiwa maeneo ya Soba,"amesema Banji.

Ametumia nafasi hiyo kuelezea viongozi wa ngazi mbalimbali wa Serikali waliotembelea banda la mtandao huo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Dawa za Kulevya Duniani ambayo kitaifa yamefanyika Tanga,Banji amesema iwapo Serikali itawasaidia kupata maeneo  hata katika suala la kujiendesha itakuwa na unafuu kwani kupitia kazi ambazo zitafanyika kwenye Soba zitawaingiza kipato na hivyo waliopo kujikumu.

Amesema huduma ambazo wanazitoa kwa walioathirika na dawa za kulevya kwenye Soba zinagharama yake ikiwemo ya mhusika kukaa katika soba wakati anapata huduma , hivyo pamoja na kwamba kuna gharama inayotolewa na mhusika kwa kila mwezi lakini kuna mahitaji mengine muhimu ambayo yanahitajika.

Banji ambaye yeye anamiliki Life and Hope Sober House Bagamoyo ametoa mfano kwake anao vijana walioathirika na dawa za kulevya na sasa wanapata huduma wapo 48 ambapo naamini wangekuwa na eneo la kutosha wangeshiriki kikamilifu kufanya kazi za kujipatia kipato na kuendelea na shughuli nyingine za kijamii.

Kuhusu mtandao wa Sauti ya sober House Tanzania, Banji amesema mtandao huo upo kwenye mikoa 11 nchini na wanaohudumiwa katika Sober hizo ni watu 15000 na malengo yao ni kuongeza idadi ya mikoa ili kuwafikia wengi zaidi.

Hata hivyo amesema wale ambao wameamua kuachana na matumizi ya dawa za kulevya wanayo nafasi ya kuamua anataka kwenda kupata huduma wapi, hivyo wapo wanaokwenda kwenye Sober , wengine hospitalini  na maeneo mengine yanayotambulika kisheria.

Kutokana na ombi hilo la Banji kwa niaba ya mtandao huo wa sober, Serikali imewahakikisha kuyafanyia kazi maombi hayo na kukiri iko haja ya kuangalia na namna ambavyo inaweza kusaidia katika hilo huku Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akieleza wazi kuwa atasimamia hilo kwani lina tija kubwa.

"Ni kweli kuna sababu ya kuangalia namna ya kuwasaidia wenye Sober house, kwa hapa Mkoa wa Tanga kuna maeneo mengi ya ardhi ambayo hayatumiki, hivyo ni wakati sahihi  kuhakikisha wale ambao wameamua kuacha kutumia dawa za kulevya na wapo kenye hizi Sober wanapata maeneo ya kufanya shughuli za uchumi.Kuwasaidia maeneo kwa ajili ya 
kuwa na ofisi peke yake haitoshi, wapewe maeneo wafanye kazi,"amesema Waziri  Mwalim.

Kwa upande wake Waziri Mkuchika akizungumza akiwa katika banda la mtandao huo la Sauti za Sober Tanzania amekiri kuna wajibu kwa Serikali kuangalia na namna ya kuendeleakusaidiana na wadau kuhakikisha walioamua kuacha kutumia dawa za kulevya wanarudi kufanya kazi badala ya kukaa vijiweni.
 Mwenyekiti wa Mtandao wa Sauti ya Sober House Tanzania Al-Karim Banji (aliyevaa suti nyeusi) akizungumza mbele ya Mgeni rasmi Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais,Menejiment ya Utumishi wa Umma Umma Mkuchika ambaye amemuwakilisha Makamu wa Rais mama Samia Suluh Hassan wakati wa maadhimisho ya Siku ya Dawa za Kulevya Duniani ambayo kitaifa imefanyika Jiji la Tanga.
 Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais ,Menejimenti ya Utumishi wa Umma George Mkuchika aliyekuwa muwakilisha mgeni rasmi Mama Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye banda la Mtandao wa Saut za Sober Tanzania wakati wa maadhimisho ya siku ya Dawa za Kulevya Duniani
Mwenyekiti wa Mtandao wa Sauti ya Sober House Tanzania Al-Karim Banji akiwa na wajumbe wengine wa mtandao huo wakimsubiri Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Menijementi ya Utumishi wa Umma George Mkuchika aliyemuwakilisha Makamu wa Rais Samia Suluh Hassan aliyekuwa mgeni rasmi.

Mwenyekiti mpya wa bodi ya Airtel Tanzania PLC na Afisa mkuu mpya wa Ufundi kutoa ushirikiano kwa Uongozi kampuni hiyo

$
0
0
 Mwenyekiti mpya wa bodi ya Airtel Tanzania PLC Dkt Omary Nundu akisalimiana na Mkurugenzi mtendaji wa Airtel Tanzania alipotembelea Makuu ya ya Airtel Tanzania yaliyopo jijini Dar es salaam mtaa wa Morocco. Mwenyekiti huyo ameahidi kushirikiana na uongozi kuhakikisha kampuni hiyo inayomilikiwa na watanzania kwa asilimia 49% inaleta tija kwa watanzania.
 Afisa Mkuu wa Ufundi mpya wa Airtel Tanzania Dkt Prospa Mafole (kati) na Mwenyekiti mpya wa bodi ya Airtel Tanzania PLC Dkt Omary Nundu (kulia) wakisalimiana na mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Bw, Sunil Colaso walipotembelea yaliyopo jijini Dar es salaam mtaa wa Morocco hivi karibuni. Mkuu huyo wa ufundi anaendelea na kazi sasa baada ya kuteuliwa na serikali ili kujiunga na uongozi uliopo wa Airtel kuhakikisha kampuni hiyo inayomilikiwa na watanzania kwa asilimia 49% inatoa huduma bora zaidi na kuipa serikali mwekezaji faida .
 Mwenyekiti mpya wa bodi ya Airtel Tanzania PLC Dkt Omary Nundu (kulia) na Afisa mkuu mpya wa Ufundi Dkt Prospa Mafole wakisalimiana na Mkurugenzi mtendaji wa Airtel Tanzania Sunili Colaso (kushoto) leo walipotembelea yaliyopo jijini Dar es Salaam mtaa wa Morocco. Mwenyekiti bodi na Afisa ufuni Mpya walioteuliwa na serikali kushika nyadhifa hizo wameahidi kushirikiana na uongozi kuhakikisha kampuni hiyo inayomilikiwa na watanzania kwa asilimia 49% inaleta tija kwa watanzania.
Wakwanza tokea kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa Airtel Tanzania Sunil Colaso akifuatiwa na Mwenyekiti mpya wa bodi ya Airtel Tanzania PLC Dkt Omary Nundu na Afisa mkuu mpya wa Ufundi Dkt Prospa Mafole wakiwa kwenye kikao cha ukaribisho mara baada ya kutembelea Makuu ya Airtel Tanzania jijini Dar es Salaam mtaa wa Morocco leo na baadhi ya wakuu wavitengo mbalimbali wa Airtel Tanzania.

Balozi Seif amjulia hali Bibi Lela Ngozi

$
0
0
 Bwana Ramadhan Ali Foum (Rama Kimara) akimkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Hospitali ya Kijitonyama kumkagua Mkewe Bibi Lela Ngozi Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa aliyelazwa kupatiwa huduma za Afya.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimjulia hali Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Bibi Lela Ngozi aliyelazwa Hospitali ya Kijitonyama Dar es salaam akipatiwa huduma za Afya.
 Daktari dhamana wa Hospitali ya Kijitonyama Dkt. Nyamsogoro akimuelezea Balozi Seif maendeleo ya Afya ya Mgonjwa wao Bibi Lela Ngozi wanayempatia huduma za Matibabu Hospitalini hapo.
 Bibi Lela Ngozi akielezea faraja anayoipata kutokana na huduma za matibabu yake wakati akibadilishana mawazo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi. Picha na – OMPR – ZNZ.

RUNGU LA MOTO LAJA KWA VIJANA NA VIONGOZI WALIOSHIRIKI KUDANGANYA KATIKA ZOEZI LA UANDIKISHWAJI KWA VIJANA KATIKA JESHI

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
UANDIKISHWAJI wa vijana katika jeshi la kujenga taifa (JKT) unaoendelea katika Mikoa yote nchini na visiwani Zanzibar umeingia dosari baada ya kugubwika na udanganyifu wa hali ya juu hali iliyoilazimu jeshi hilo kutatua changamoto hiyo kwa kupitia upya vijana wote walioandikishwa kote nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi wa habari na mawasiliano Luteni Kanali Gaudance Gervas Ilonda amesema kuwa baada ya kutangaza nafasi kwa vijana kwa kujitolea katika jeshi hilo changamoto zimejitokeza katika zoezi la uandikishwaji huku akieleza changamoto mojawapo ni vijana kujiandikisha Mikoa tofauti na ile wanayoishi na hiyo ni shinikizo kutoka kwa wazazi na walezi hali inayosababisha vijana wa Mikoa husika kukosa nafasi hizo ambazo zimetolewa sawa kila sehemu kulingana na maeneo na idadi ya watu.

Pia ameeleza kuwa baadhi ya viongozi wamekuwa wakipeleka majina ya vijana katika makao makuu ya jeshi la kujenga taifa na Mikoani kwa malengo ya kupata nafasi hizo kwa urahisi zaidi huku akieleza kuwa jeshi hilo halitoi ajira bali linawaandaa vijana hao kuwa wazalendo na viongozi bora kwa baadaye.

"Baadhi ya viongozi wamekuwa wakileta majina 10 hadi 20 ya vijana ili waweze kupata nafasi katika jeshi la wananchi, huku ni kujitengenezea kikosi kwa matumizi yao binafsi kwa baadaye jambo ambalo ni kinyume na kanuni za jeshi hilo" ameeleza Luteni Ilonda.

Aidha amesema kuwa changamoto nyingine katika zoezi hili la uandikishwaji ni udanganyifu wa vyeti vya elimu, vyeti vya kuzaliwa kwa kudanganya umri na afya pamoja na utapeli wakati wa uandikishwaji ambapo wazazi na walezi huombwa fedha ili kuweza kupata nafasi hizo.

"Katika baadhi ya maeneo ya uandikishwaji wazazi huombwa fedha ili kupata nafasi katika jeshi la kujenga taifa, kwa jeshi letu hatuna nafasi hizo na atakayebainika ataondoshwa mara moja" amesema Luteni Ilondo.

Vilevile amesema kuwa kufuatia dosari hizo ambazo hawataweza kuzifumbia macho jeshi la kujenga taifa kwa kushirikina na jeshi la wananchi, mamlaka ya vitambulisho vya taifa (NIDA), Wizara ya elimu, Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) pamoja na mamlaka nyingine watashirikiana katika zoezi kabambe la kupitia upya vijana wote walioandikisha kote nchini pamoja na kupitia nyaraka na vyeti vyote kwa lengo la kupata vijana halali, watanzania, wenye afya na wanaotoka maeneo husika ili waweze kuingia katika jeshi hilo na kupata mafunzo ya uzalendo, umoja, weledi, upendo na kujali mali za umma.

Luteni Ilonda amesema kuwa kwa watakaobainika wameshiriki katika udanganyifu huo kwa namna yoyote ile watakamatwa na kufunguliwa mashtaka na hakuna atakaye fumbiwa macho na hata wale waliotumia dhamana vibaya hawatastahimiliwa.

Mwisho amewataka wananchi kufuata taratibu za uombaji wa nafasi hizo ambazo sifa za kujiunga zimebandikwa katika maeneo ya Wilaya na ofisi husika huku akiwataka vijana wanaojiunga na jeshi  kuelewa kuwa hiyo sio tiketi ya ajira jeshini au serikalini bali ni sehemu ya kujifunza uzalendo na kuwa viongozi Bora wa baadaye.

NAIBU WAZIRI KWANDIKWA AMTAKA MKANDARASI KUONGEZA KASI YA UJENZI WA DARAJA LA NGUYAMI

$
0
0
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias John Kwandikwa (kulia), akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Morogoro Mhandisi Godwin Andalwisye (kushoto), kuhusu mradi wa ujenzi wa daraja la mfuto (drift) katika mto Nguyami linalounganisha kijiji cha Iyogwe na Gairo, wilayani Gairo.
 Ujenzi wa daraja la mfuto (drift) katika mto Nguyami linalounganisha kijiji cha Iyogwe na Gairo, mkoani Morogoro ukiendelea.
 Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Morogoro Mhandisi Godwin Andalwisye (wa pili kushoto), akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias John Kwandikwa (wa pili kulia), kuhusu mradi wa ujenzi wa daraja la mfuto (drift) katika mto Nguyami linalounganisha kijiji cha Iyogwe na Gairo. Mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias John Kwandikwa, akitoa maelekezo kwa mkandarasi M/S Superb Builders And General Supplires (hayupo pichani) anayejenga daraja la mfuto (drift) katika mto Nguyami linalounganisha kijiji cha Iyogwe na Gairo mkoani Morogoro. Daraja hilo linaunganisha barabara ya Iyogwe-Chakwale-Ngilori yenye urefu wa KM 42.

Naibu Waziri wa Ujenzi,  Elias Kwandikwa, amemtaka mkandarasi anayejenga daraja la mfuto (drift) katika mto Nguyami linalounganisha kijiji cha Iyogwe na Gairo kuongeza kasi ya ujenzi ili kuwaondolea kero wananchi wa eneo hilo.

Akizungumza na wananchi wa vijiji hivyo mara baada ya kukagua barabara ya Iyogwe-Chakwale-Ngilori yenye urefu wa KM 42, wilayani Gairo, Naibu Waziri Kwandikwa amesema Serikali imejipanga kuhakikisha madaraja matatu muhimu katika barabara hiyo yanakamilika kwa wakati na hivyo kuwezesha shughuli za kiuchumi  na uzalishaji.

“Tumejipanga kuhakikisha madaraja yote matatu ya Chakwale, Nguyami na Matale yanakamilika kwa wakati ili kurahisisha shughuli za usafiri na uchukuzi”, amesisitiza Naibu Waziri Kwandikwa.

Awali akitoa taarifa ya mradi wa madaraja hayo, Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Morogoro Mhandisi Godwin Andalwisye, amemueleza Naibu Waziri huyo kuwa TANROADS imejipanga kukamilisha ujenzi wa madaraja hayo kwa muda uliopangwa.

Madaraja matatu ya Chakwale, Nguyami na Matale yapo kwenye barabara ya Iyogwe-Chakwale-Ngilori yenye urefu wa KM 42 inaunganisha Wilaya za Gairo na Kilindi (Morogoro na Tanga), barabara hiyo ni muhimu kwa kuwa inapita eneo lenye uzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula na hivyo kuchochea uchumi wa wakazi wa maeneo hayo.

MKURUGENZI TAKUKURU ASEMA RUSHWA MARUFUKU KATIKA MAPAMBANO YA VITA DHIDI DAWA ZA KULEVYA

$
0
0

*Asema wanawafuatilia watumishi kwa karibu, watakaoabinika kukiona
*Waziri Mkuchika aitaja mikoa inayoongozwa kwa dawa za kulevya nchini

Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii
MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (TAKUKURU) Diwani Athumani amewataka Watanzania kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya huku akifafanua iwapo jamii ikaachwa itumie dawa za kulevya hatari zake ni nyingi ikiwemo ya uchumi kudorora na usalama wa nchi kuwa mashakani.

Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Dawa za Kulevya Duniani ambayo kitaifa yamefanyika katika Jiji la Tanga, Athumani amesema tatizo la dawa za kulevya lilikuwa kubwa lakini Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imefanya kazi kubwa kukomesha biashara ya dawa za kulevya nchini.

"Ni vema Watanzania wote tukaunga mkono mapambano dhidi ya dawa za kulevya na sio kuiachia mamlaka peke yake.Nguvu kazi kubwa ya Taifa ikiendelea kutumia dawa za kulevya maana yake uchumi utadorola na kwenda kuathiri uchumi wa nchi.Pia kundi kubwa likiachwa na kuingia kwenye dawa za kulevya usalama wa nchi unakuwa shakani,"amesema Diwani Athumani.

Akifafanua zaidi kuhusu ushiriki wa TAKUKURU kwenye mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini amesema rushwa inaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kukwamisha mapambano dhidi ya dawa hizo na kufafanua iwapo rushwa ikatumika mipakani maana yake wafanyabiashara hiyo watumia rushwa kuingiza dawa nchini.

"Rushwa ikiachwa na kutumika katika kupambana na dawa za kulevya maana yake ni kwamba dawa zitaendelea kuingizwa nchini na madhara yake ni kuathiri jamii katika nyanja mbalimbali.Ndio maana TAKUKURU tuko kila mahali kuhakisha hakuna rushwa katika kukomesha dawa za kulevya nchini,amesema Athumani na kufafanua Watanzania wanalo jukumu la kukemea dawa za kulevya na rushwa.

Ametoa rai kwa watumishi wote wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na dawa za kulevya kuhakikisha wanachukua rushwa katika utendaji wa kazi zao za kila siku na kwamba TAKUKURU iko kila mahali itaendelea kufuatilia na atakayepatikana ajue amepatikana.

Pia amewaomba viongozi wa dini kutumia karama ambazo wamepa na Mungu kuhakikisha wanaendelea kukumbusha waumini wao kuhusu madhara ya dawa za kulevya na rushwa katika nchi yetu kwani viongozi wa dini wanao mchango mkubwa katika harakati za kukomesha dawa hizo.

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalim amesema watanzania lazima wachukue dawa za kulevya nchini kwani madhara yake ni makubwa huku akifafanua kwa wale ambao wameatherik na utumiaji wa dawa hizo Serikali inayo wajibu wa kuwatibu na ndio maana kuna vituo vya kutoa huduma katika maeneo mbalimbali nchini na siku za karibuni kitajengwa kituo kingine katika jiji la Tanga.

"Katika nchi yetu tatizo la dawa za kulevya linashushulikiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya.Nitoe pongezi kwa Rais Dk.John Magufuli kwa uamuzi wake wa kukabiliana kwa vitendo na biashara ya dawa za kulevya kwa kuanzisha mamlaka hii ambayo inafanya kazi nzuri.Na tangu kuanzishwa kwa mamlaka kumewepo na ushirikiano mzuri kwa mihilimi yote mitatu katika nchi.

Wakati huo huo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma George Mkuchika akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi Samia Suluh Hassan amesema wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya wanao utajiri wa kutisha lakini athari zake kwa jamii ni kubwa, hivyo Watanzania lazima wachukue dawa hizo kwa nguvu zote.

"Kwa sasa uingizwaji wa dawa za kulevya nchini umepungua na ndio maana inaelezwa dawa kupanda bei kiasi cha wengine kuamua kuacha wenyewe na pale wanapopatikana wanaojihusisha na biashara hiyo wanakamatwa na sheria kuchukua mkondo wake wakati zamani wakikamatwa wanatoa rushwa na kuachwa,"amesema Mkuchika.

Hata hivyo amesema pamoja na mapambano ya dawa za kulevya kuwa na mafanikio makubwa Tanga inashika nafasi ya pili kwa kuwa na idadi kubwa ya wanaojihusisha na dawa za kulevya na nafasi ya kwanza inashika na Dar es Salaam.Hivyo ameendelea kuishauri jamii ya Watanzania kushiriki kikamilifu kwenye mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

Awali Kaimu Kamishna Jeneral wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Valite Mwachusa amesema kuwa mamlaka imeendelea kuweka mikakati ikiwemo ya kuhakikisha dawa za kulevya hazingizwi nchini , wakati mkakati mwingine ni kupunguza madhara yatonakayo na dawa za kulevya.

Mwachusa ameema pamoja na kufanikiwa kwa asilimia 90 kukabiliana na dawa za kulevya nchini bado tatizo ni kubwa na hivyo jamii ya Watanzania inayo nafasi ya kushiriki kikimalifu katika mapambano dhidi ya dawa hizo ambazo zikiachwa na kuingia nchini madhara yake ni makubwa.

'WE FARM' WAJA NA HUDUMA ZA KIDIGITALI KUWASAIDIA WAKULIMA TANZANIA

$
0
0
Katika kuhakikisha wakuliwa mbalimbali nchini wanapata taarifa za kilimo na kukifanya kiwe na tija, taasisi isiyo ya kiserikali iitwayo ‘We Farm’ imenzisha mradi unaowaunganisha wakulima kuwasiliana moja kwa moja na kupeana taarifa zitakazowawezesha kutimiza mahitaji yao ya kilimo.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Meneja Mkuu wa taasisi hiyo Nicholus John amesema ujio wa ‘We Farm’ zaidi umelenga kutatua changamoto zinazowakabili wakulima ikiwemo kukosa taarifa sahihi zinazohusiana na masuala ya kilimo hicho na kuwafanya wapate hasara kwa kukosa au mazao wanayoyalima kutokidhi makusudio yao.

Amesema mradi huo uliolenga kuwafikia wakuliza 400,000 ifikapo mwisho wa mwaka huu, zaidi utawaunganisha wakulima hao lupitia simu zao za mikononi huku ukitumia mwanya huo pia kupata majibu ya maswali mbalimbali yanayohusiana na kilimo wanachokifanya.

Nicholus amesema katika utekelezaji wa majukumu yake, ‘We Farm’ pia itafanya kazi kwa karibu na maafisa wa ugani waliopo katika halmashauri zote nchini ili kuleta tija zaidi katika kilimo hicho na hivyo kukuza uchumi wao pamoja na wa taifa kwa ujumla.

“Huduma hii inawawezesha wakulima kuwasiliana wao kwa wao na kuelezana changamoto zilizopo katika kilimo na kupaena majibu juu ya maswali mbalimbali yanayojitokeza, kikubwa ‘we farm’ ni ukumbi wa majadiliano kwa wakulima” aliongeza Nicholus.

Aidha amesema utafiti walioufanya hivi karibuni walibaini uwepo wa changamoto ya ukosefu wa taarifa kwa wakulima hao na hivyo kuwafanya washindwe kupata majibu katika masuala mbalimbali yanayohusiana na kilimo hicho.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya ufuatiliaji wa taasisi hiyo Cyrila Anton amesema kupitia huduma hiyo, wakulima wataweza kupiga hatua katika kilimo wanachokifanya na hivyo kuwawezesha kupata mafanikio yanayotokana kilimo wanachokifanya.
Meneja Mkuu wa taasisi ya 'We Farm' Bw. Nicholus John akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam waliofika katika mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya kuijua taasisi hiyo na malengo yake katika kutoka huduma kwa wakulima nchini Tanzania. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. Baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari wakisikiliza mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo.
Mkuu wa Idara ya ufuatiliaji wa taasisi ya We Farm Cyrila Anton akitoa ufafanuzi zaidi masuala mbalimbali ya wakulima.
Baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari wakisikiliza mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo.
Mmoja ya viongozi akiuliza maswali.
Viongozi wa taasisi ya We Farm wakiwa katika picha ya pamoja na wahariri wa vyombo vya habari mara baada ya kumaliza mafunzo ya kuwajenga uwezo. Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.


RC MBEYA ABATILISHA UHAMISHO WA MGANGA MKUU WA WILAYA YA KYELA

$
0
0
Na Emmanuel Madafa, MBEYA

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila amebatilisha uhamisho wa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Dk. Mariam Ngwere uliofanywa na Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwenda katika Halmashauri ya Wanging'ombe mkoani Njombe kwa madai kuwa uhamisho huo ni wa mashaka.

Akitangaza uamuzi huo leo  Juni 27 kwenye Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Kyela kilichoitishwa kwa ajili ya Kupitia na kujadili hoja zilizoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Chalamila alisema atawasiliana na Katibu Mkuu wa Tamisemi ili amshauri asitishe uhamisho huo na kwamba kama kuna ulazima wa mtumishi huyo kuhamishwa basi ni bora apandishwe cheo.

"Hatukatai watumishi wa umma kuhamishwa maana ni haki ya mtumishi yeyote kufanya kazi popote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tunachopinga ni uhamisho wenye mashaka, hivyo mimi kama Mkuu wa Mkoa siwezi kuwa laini kama mlenda natangaza kuanzia muda huu uhamisho huo ni batili," alisema Chalamila.

Aliwataka watumishi wa Halmashauri hiyo pamoja na madiwani kuungana na kuacha kuendekeza migogoro isiyokuwa ya lazima kwa maelezo kuwa migogoro hiyo inakwamisha shughuli za maendeleo.

WAZIRI MKUU AREJEA DODOMA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini, Patrobas Katambi  (kushoto) na  Mkuu wa wilaya ya Bahi, Mwanhamisi Mkunda wakati alipowasilli kwenye uwanja wa Ndege wa Dodoma akitoka Dar es salaam, Juni 27, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

BRELA YATOA MAFUNZO KWA WAFANYABIASHA MTWARA

$
0
0
 
  Msaidizi wa usajili mkuu katika wakala wa biashara na leseni hapa nchini (BRELA) George Chuwa aliyesimama akitoa elimu kwa wafanyabiashara mbalimbali mkoani Mtwara kuhusu kusajili biashara zao kwa njia ya mtandao mafunzo ambayo yamefanyika mjini Mtwara. 
Wafanyabiashara mbalimbali mkoani Mtwara wakijengewa uwezo katika mafunzo ya siku mbili  yanayoendeshwa na Wakala wa usajili wa biashara na leseni (BRELA) kuhusu namna ambavyo wanatakiwa kusajili biashara zao kwa njia ya mtandao mafunzo ambayo yamefanyika mjini Mtwara. (PICHA NA FATNA MWINYIMKUU)

WANAUME WATAJWA KUONGOZA KWA KUFANYA VITENDO VYA UKATILI

$
0
0
Jinsi ya kiume imetajwa kuwa ni moja kati ya watendaji wakubwa wa vitendo vingi vya ukatili dhidi ya Mwanamke na Mtoto katika jamii ambavyo vimekuwa vikiathiri malezi ya watoto na ustawi wa familia.

Hayo yamebainika leo jijini Dar es Salaam katika kikao katika ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Viongozi wa dini katika kujengewa uelewa kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia.

Akizungumza katika kikao hicho kwa niaba ya Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu, Kamishna wa Ustawi wa Jamii Dkt. Naftali Ng’ondi amesema kuwa kwa mujibu wa Utafiti wa hali ya ukatili dhidi ya watoto uliofanyika na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na UNICEF wa mwaka 2011 unaonesha kuwa mtoto 1 kati ya watoto 3 wa kike na 1 kati ya 7 wa kiume walifanyiwa vitendo vya ukatili kabla ya kufikisha umri wa miaka 18.

Dkt. Ng’ondi ameongeza kuwa asilimia 72 ya wasichana na asilimia 71 ya wavulana walifanyiwa ukatili wa kimwili na vilevile robo ya watoto walifanyiwa ukatili wa kiakili.

“Uandaji wa Ajenda hii umetokana na hali halisi ya ongezeko la changamoto zinazomkabili mtoto hasa zinzaoanzia katika ngazi ya familia” alisema

Kamishna Ng’ondi ameeleza kuwa vitendo vya ukatili pia vimekuwa vikisababishwa na ongezeko la migogoro ya ndoa ambapo imesababisha watoto kukosa malezi ya wazazi wote wawili ambapo amesema kwa mwaka kwa mujibu wa takwimu za Ofisi ya Ustawi wa Jamii inaonesha kwa muda wa miezi tisa kuanzia Julai, 2018 hadi Marchi 2019 jumla ya mashauri ya ndoa 16,832 ukilinganisha na mashauri 13,382 kwa mwaka 2017/2018.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Idara ya Manendeleo ya Mtoto kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Mwajuma Magwiza ameeleza kuwa jamii ya kitanzania inakumbwa na changamoto nyingi zikiwemo ukatili dhidi ya wanawake na watoto na Serikali imekuwa ikiandaa mikakati mbalimbali katika kukabiliana na changamoto hzio ikiwemo Ajenda ya Kitaifa ya Wajibu wa Wazazi/Walezi katika malezi na matunzo ya familia.

Naye Mwakilishi wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) Sheikh Hassan Said Chizenga amesema kuwa Ajenga hii inatakiwa kushirikisha Sekta nyingine kama vile utamaduni na michezo ili iweke misingi bora katika kujenga maadili ya watoto wetu katika malezi na makuzi yao.

Naye Mkurugenzi wa Huduma za Jamii kutoka Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) John Riziki amesema kuwa Baraza hilo limejidhatiti katika kuhakikisha wanasaidia na wazazi/walezi katika malezi kwa kufanya somo la dini kufundishwa katika shule za Msingi na Sekondari ili kuhakikisha watoto wanakuwa katika maadili mema.

Kikao hiki cha kuwajengea uelewa viongozi wa dini kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia ambayo kinakuja mara baada ya kuzinduliwa rasmi na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu(Mb) katika Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika mkoani Geita Juni, 16.
 Mwakilishi wa Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambaye ni Kamishna wa Ustawi wa Jamii Dkt. Naftali Ng’ondi akizungumza na viongozi wa dini wakati wa kikao baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika kikao cha kuwajengea uwezo viongozi hao kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Mtoto kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Mwajuma Magwiza akielezea lengo la kikao baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika na viongozi wa dini chenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi hao kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Mtoto kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Tausi Mwilima akichangia jambo katika kikao baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na viongozi wa dini chenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi hao kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
 Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi  kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Emmanuel Burton  akielezea athari za ukatili wa  kijinsia na Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia katika kikao baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na viongozi wa dini chenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi hao kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
 Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Mwelinde Kato akielezea umuhimu wa kitini cha malezi kwa Familia kuzuia ukatili dhidi ya watoto Tanzania  katika kikao baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na viongozi wa dini chenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi hao kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa TRCPT Mchungaji Canon Thomas Godda akichangia mada katika kikao baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika na viongozi wa dini chenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi hao kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.


  Sheikh Hemed Jawalii kutoka Taasisi ya Shia na Sharia Kigogo akichangia mada katika kikao baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na viongozi wa dini chenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi hao kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
  Viongozi wa dini wa kifuatilia mada mbalimbali katika kikao baina ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na viongozi hao chenye lengo la kuwajengea uwezo viongozi hao kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambaye ni Kamishana wa Ustawi wa Jamii Dkt. Naftali Ng’ondi (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na viongozi wa dini mara baada ya kikao kilichowakutanisha viongozi hao kuhusu Ajenda  ya  Kitaifa ya Wajibu wa  Wazazi /Walezi wa Malezi na Matunzo ya Familia kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu afungua Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Dodoma

$
0
0
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiangalia mvinyo, katika banda la Benki ya Maendeleo (TIB), kwenye Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Dodoma, lililofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma Juni 27.2019. Tokea kushoto ni Meneja Maendeleo ya Biashara (TIB), Joseph Chilambo na Mkurugenzi wa Mipango na Mikakati (TIB) Patric Mongela.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akioneshwa mkoba uliyobuniwa na Wajasiriamali wa Kitanzania na Meneja Mzalishaji wa Fay Fashion Gregory Mlay, kwenye Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Dodoma, lililofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma Juni 27.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akifafanuliwa jambo na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi, wakati akikagua mabanda, kwenye Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Dodoma, lililofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma Juni 27.2019.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images