Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

MATUKIO MBALIMBALI YA WAZIRI MKUU BUNGENI JIJINI DODOMA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Bungeni jijini Dodoma, Juni 25, 2019. 
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji akijibu hoja za Wabunge kuhusu Bajeti ya Serikali, Bungeni jijini Dodoma, Juni 25, 2019.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Kuteuliwa, Anne Kilango, Bungeni jijini Dodoma, Juni 25, 2019.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, Bungeni jijini Dodoma, Juni 25, 2019. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango na Naibu wake, Dkt. Ashatu Kijaji (kulia) baada ya Waziri wa Fedha na Naibu wake kujibu hoja za wabunge kuhusu Bajeti ya Serikali, Bungeni jijini Dodoma, Juni 25, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


StarTimes yatoa zawadi kwa Vijana kwenye tamasha la Twen’zetu kwa Yesu

$
0
0
Tamasha la dini ambalo linajulikana kama ‘Twen’zetu kwa Yesu’ lililofanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Tamasha hilo hufanyika kila mwaka likiwa na lengo la kukutanisha Vijana wa kikristo pamoja. Mwaka huu StarTimes walikuwa miongoni mwa wadhamini wa tamasha hilo ambalo lilihudhuriwa na maelfu ya washiriki kutoka sehemu mbali mbali jijini Dar es Salaam.

Zaidi ya udhamini StarTimes walitoa zawadi mbalimbali kwa Vijana waliohudhuria tamasha hilo. Miongoni mwa zawadi hizo vilikuwemo ving’amuzi vitano vya Antenna vya StarTimes, Smart TV ya StarTimes inch 50 ambayo ilienda kwa kijana wa Usharika wa KKKT Mbezi jijini Dar es Salaam.

“Nimefurahi sana kupata zawadi hii, kiukweli nilipokuwa nakuja kwenye tamasha la leo sikutegemea kama kutakuwa na kitu cha namna hii. Namshukuru sana Mungu pia nawashukuru StarTimes kwa zawadi hii.” Bariki Josephat, Mshindi wa Smart TV kwenye tamasha la Twen’zetu kwa Yesu.

Hata hivyo kijana Bariki baada ya kupokea zawadi hiyo yeye pamoja na ndugu zake waliomba kuiacha TV hiyo mikononi mwa StarTimes kwa sababu za kiusalama na kisha kufika kwenye ofisi zao siku ya Jumatatu kuichukua akiambatana na baba yake.

Mbali na tamasha hilo StarTimes wanaendelea kurusha michuano ya Copa America ambayo itaingia hatua ya robo fainali usiku wa kuamkia Ijumaa wiki hii kwa mechi kali ya Brazil vs Paraguay na Ijumaa usiku Venezuela vs Argentina. Zote kupitia chaneli za michezo za StarTimes kwa kiwango cha HD.
Kijana Bariki Josephat (aliyebeba begi) akiwa ameshikilia zawadi yake ya StarTimes Smart TV aliyopewa siku ya tamasha la Twenzetu kwa Yesu na wawakilishi kutoka StarTimes na viongozi wa dini.
Bariki Josephat akiwa kwenye ofisi za StarTimes alipofika kuchukua zawadi yake akiwa ameambatana na baba yake mzazi.

BUNGE LA TANZANIA LAPATA MSAADA WA LAPTOPS KUTOKA BUNGE LA CHINA

$
0
0
 Spika wa Bunge Job Ndugai (Mb), akimsikiliza Balozi wa China Nchini Tanzania Wang Ke wakati wa makabidhiano ya msaada wa kompyuta (Laptops)70 kutoka Bunge la China. Makabidhiano hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Spika Bungeni Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge Job Ndugai (Mb), akipokea msaada wa kompyuta (Laptops) 70 kutoka kwa Balozi wa China Nchini Tanzania,  Wang Ke, makabidhiano yalifanyika katika Ukumbi wa Spika Bungeni Mjini Dodoma na kushuhudiwa na Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson. Msaada huo wa Kompyuta 70 (laptops) umetolewa na Bunge la China  kwa Wabunge wa Bunge la Tanzania. 
 Spika wa Bunge Job Ndugai (Mb), akipokea msaada wa kompyuta (Laptops) 70 kutoka kwa Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, makabidhiano yalifanyika katika Ukumbi wa Spika Bungeni Mjini Dodoma na kushuhudiwa na Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson. Msaada huo wa Kompyuta 70 (laptops) umetolewa na Bunge la China  kwa Wabunge wa Bunge la Tanzania.
Spika wa Bunge Job Ndugai (Mb) na Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, wakisaini mkataba wa makabidhiano ya msaada wa kompyuta (Laptops) 70 makabidhiano yalifanyika katika Ukumbi wa Spika Bungeni Mjini Dodoma na kushuhudiwa na Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson na Wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge. Msaada huo wa Kompyuta 70 (laptops) umetolewa na Bunge la China  kwa Wabunge wa Bunge la Tanzania.

MKURABITA YAPIGA KAMBI ZANZIBAR KUKAGUA SHUGHULI ZAKE

$
0
0
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar 
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya Biashara na Viwanda, Tume ya Mipango Zanzibar na Ofisi ya Mpango wa kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Taanzania (MKURABITA) zitaendeleza azma yake muhimu ya kuhamasisha urasimishaji wa Wafanyabiashara wadogo wadogo wa Zanzibar ili kuzifanya biashara zao kutambulika kisheria.

Kwa kufanya hivyo kutawawezesha Wajasiriamali mbali mbali kufanya biashara endelevu zinazowakomboa kiuchumi na kuepuka kufanya biashara ya kimazoea zisizoleta tija.

Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda Juma Reli ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA iliyomtembelea Ofisini kwake Migombani ikiwa ni mwendelezo wa kukagua shughuli zinazofanywa na Kamati hiyo visiwani Zanzibar.

Amesema kwa Zanzibar kazi za urasimishaji hufanyika kwa kushirikiana na Ofisi za Wilaya na Halmashauri husika ambapo Wafanyabiashara hupatiwa mafunzo maalum ya urasimishaji.

“Unapokuwa rasmi unaweza kupata mkopo kirahisi, ukipata mkopo pia kuna uwezekanao wa biashara kukua na pato la Taifa pia huongezeka” alifafanua Katibu Juma Reli.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Biashara na ukuzaji masoko Khamis Ahmad Shauri amesema jumla ya Wafanyabiashara wadogo 154 walipatiwa mafunzo ya urasimishaji Unguja na Pemba kwa mwaka 2018/2019

Amefahamisha kuwa Wafanyabiashara wanaporasimishwa hupata fursa ya kuweza kukopa Mitaji katika vyanzo mbalimbali ikiwemo Benki ambayo huwasaidia kuziendeleza biashara zao kwa faida yao na vizazi vyao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya uongozi ya MKURABITA Balozi Daniel Ole Njolay ameishauri Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupunguza gharama za uanzishwaji wa biashara kwa wananchi ikiwemo ukataji wa Leseni ili kuyafanya mazingira ya biashara kuwa rahisi.

Mratibu wa MKURABITA Tanzania Dkt. Seraphia Mgembe ameiomba Wizara ya Viwanda na Biashara Zanzibar kuandaa mijadala ya wazi kwa wananachi walionufaika na MKURABITA Zanzibar ili iwahamasishe wananchi wengine kurasimisha biashara na rasilimali zao.

Awali Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA walimtembelea Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar Mwita M. Mwita na kufanya mazungumzo naye ambapo aliwaeleza kuwa Ofisi yake tayari imeratibu na kufanya utambuzi wa Viwanja zaidi ya 10,000.

Amesema baada ya utambuzi huo Serikali ya Mapinduzi ipo mbioni kutoa hati za Viwanja hivyo kwa wananchi ili kufanya shughuli zao na kuepuka migogoro ya ardhi.

Kamati hiyo pia ilipata fursa ya kutembelea Wajasiriamali walionufaika na MKURABITA na kuona maendeleo yao ambapo pia walielezea changamoto ya masoko kwa bidhaa wanazozizalisha.

Mpango wa kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Taanzania (MKURABITA) ulianzishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2004 ikiwa ni mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini Tanzania MKUKUTA na MKUZA ambapo walengwa hutumia raslimali na biashara zao zilizorasmishwa katika kujipatia mitaji, soko na fursa zingine.
 Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar Mwita M. Mwita (mwenye Mkoba) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA waliomtembelea ofisini kwake Vuga mjini Zanzibar.

 Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda Juma Reli akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA iliyomtembelea Ofisini kwake Migombani ikiwa ni mwendelezo wa kukagua shughuli zinazofanywa na Kamati hiyo visiwani Zanzibar.
 Mkurugenzi wa Biashara na ukuzaji masoko Zanzibar Khamis Ahmad Shauri akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mpango wa kurasimisha biashara ndogo ndogo Zanzibar kwa mwaka 2018/19 mbele ya Kamati ya Uongozi ya MKURABITA.
 Mjasiriamali ambaye amepata mafunzo kutoka kwa MKURABITA Furaha Juma Abdalla akiwauzia bidhaa anazozalisha baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA waliomtembelea kwake Chukwani Zanzibar kujua maendeleo ya shughuli zake.
Mratibu wa MKURABITA Tanzania Dkt. Seraphia Mgembe akiangalia Mikoba inayotengenezwa na Mjasiriamali Neema Betraham wa Kikwajuni mjini Zanzibar mara baada ya kufika kuangalia shughuli za Wajasiriamali hao. Picha na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar

WAZIRI KABUDI ASHRIKI MKUTANO WA FOCAC BEIJING CHINA

$
0
0
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof Palamagamba John Kabudi (Mb) (katikati) akifuatilia mkutano wa waratibu wa jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC),Beijing -  China. June 25,2019 .
 Meza kuu watatu kushoto ni Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni ambaye ni mgeni wa heshima na Mkuu wa Nchi pekee kutoka Bara la Afrika akiwa katika mkutano wa waratibu wa jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika. Wa pili kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje China na Mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi. Mkutano huo umefanyika Beijing,China na Kuhudhuriwa na Mawaziri wa mambo ya Nje wa Nchi za Afrika 53. June 25, 2019.
 Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (watano kutoka kushoto) akiwa katika mkutano wa waratibu wa jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaohudhuriwa na Mawaziri wa Mambo ya NJe 53 kutoka Nchi za Afrika. Mkutano huo unafanyika Beijing – China. June 25, 2019. 
 Sehemu ya Mawaziri wa mambo ya Nje kutoka Nchi 53 za Afrika wanaohudhuria mkutano wa waratibu wa jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC).Mkutano huo unafanyika Beijing – China. June 25, 2019.


Nchi za Kiafrika zimeiomba China kuhakikisha kuwa ufadhili ama mikopo inayotoa kwa Nchi za Kiafrika inalenga katika miradi ya kikanda itakayoziunganisha na kuzinufaisha nchi hizo kiuchumi huku Tanzania ikiitaka China kuhakikisha kuwa miradi ya maendeleo inayowekeza nchini iwe ya manufaa kwa pande zote mbili.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) ameyasema hayo Beijing Nchini China katika mkutano wa waratibu wa jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) alipopata fursa ya kuzungumza katika mkutano huo na kuongeza kuwa endapo China itazisaidia kwa ufadhili ama kwa mikopo nafuu kuwekeza katika miradi hasa ya miundombinu itakayoziunganisha Nchi za kiafrika kwa kiasi kikubwa itazisaidia Nchi hizo kufanya biashara zenyewe kwa zenyewe itaziwezesha kupiga hatua za kimaendeleo na kiuchumi na hivyo kujitegemea.

Ameongeza kuwa Mkutano huo wa waratibu wa jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) umekuwa ni wa manufaa kwa kuwa Nchi zenyewe za kiafrika zimepata fursa ya kutaja baadhi ya miradi ya kipaumbele kutokana na uitaji wa Nchi husika huku akiitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji kwa kuwa Nchi nyingi za Kiafrika bado zina vyanzo vingi vya maji vinavyoweza kuzalisha umeme ambao utakuwa ni wa bei nafuu na kusaidia katika ujenzi wa viwanda.

Aidha katika mkutano huo wa siku mbili uliozikutanisha Nchi zipatazo 53 za Kiafrika na China zimeitaka China pia kuhakikisha inasaidia ama kufadhili katika kuinua uwezo wa kitaaluma utakaowawezesha vijana kwa Kiafrika kujiajiri na kupata wataalam wabobezi katika masuala mbalimbali kutokana na uwekezaji hasa wa viwanda na miundombinu utakaofanywa kwa pamoja na China na Nchi za Kiafrika.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) amesema katika mkutano huo wa waratibu wa jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) Tanzania imesisitiza kuwa katika miradi ya uwekezaji,ya misaada ama ile ya mikopo nafuu inayoelekezwa Tanzania iwe ni ile yenye manufaa kwa pande zote mbili yaani win win situation kama anavyosisitiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Akisoma hotuba kwa niaba ya Rais wa China Mhe. Xi Jimping, Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi amesema kuwa China haitatoa misaada yenye masharti magumu kwa Nchi za Afrika, badala yake itaendeleza ushirikiano wake na Afrika katika kutekeleza miradi ya maendeleo yenye manufaa kwa pande zote mbili.

Katika hotuba hiyo,serikali ya China imeahidi kuongeza umoja na ushirikiano kati yake na Afrika katika masuala ya kikanda na kimataifa ikiwa ni pamoja na kudumisha amani na usalama ili kuleta maendeleo endelevu kwa watu na kuifanya dunia kuwa mahali salama pa kuishi.

Mkutano huo wa waratibu wa jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika limeazimia kwa pamoja kutekeleza miradi ya kipaumbele kulingana na uhitaji wa kila nchi kwa kufuata hatua nane zilizotangazwa katika mkutano wa wakuu wa nchi wa FOCAC uliofanyika mwezi September 2018 jijini Beijing.

Hatua hizo ni pamoja na program ya kuendeleza viwanda kupitia ujenzi wa maeneo maalum ya viwanda,ujenzi wa miundombinu ikiwemo nishati,reli,barabara na bandari,sambamba na ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi vitakavyosaidia kuzalisha nguvu kazi ya viwandani.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
BEIJNG - CHINA.

25 Juni 2019

MKAZI DAR KORTINI KWA TUHUMA ZA UHUJUMU UCHUMI,KUTAKATISHA SHILINGI BILIONI MOJA

$
0
0

Na Karama Kenyunko, globu ya jamii

MKAZI wa Magomeni jijini Dar es Salaam, Haji Msongela Juma (33) leo Juno 25, 2019  amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na kesi ya  Uhujumu Uchumi  likiwamo shtaka la kutakatisha dola za Marekani 750,000 ambazo zaidi  ya Sh. Bilioni moja

Akisoma hati ya mashtaka leo Juni 25 ,2019, Wakili wa wa Serikali Wankyo Simon amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Mfawidhi Kelvin Mhina kuwa, Juni 19, mwaka huu huko katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) mshtakiwa huyo, akiwa anaondika nchini alikutwa akiwa na dola za Marekani 750,000 na kutoa taarifa ya uongo kwamba fedha hizo zinamilikiwa na H.Haji (GSM. Company).

Aidha imeendelea kudaiwa kuwa, siku na mahali hapo, mshtakiwa alikutwa akiwa na kiasi hicho cha fedha  ambazo anadaiwa kuzipata kwa njia isiyohalali

Hata hivyo, mshtakiwa hakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mashtaka yanayomkabili mshtakiwa ni ya uhujumu uchumi na mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na pia mashtaka ya kutakatisha fedha hayana dhamana, kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 9,mwaka huu

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na Mshtakiwa amerudishwa rumande.

Makamu wa Rais ashiriki Dua ya pamoja msiba mke wa Dkt. Mabodi

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Juni 25,2019 ameshiriki katika Dua ya pamoja na Familia ya Naibu katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Abdallah Juma Sadallah Mabodi wakati Makamu wa Rais alipofika nyumbani kwa Dkt. Mabodi Mikocheni jijini Dar es salaam kumfariji kutokana na kifo cha mkewe Dkt. Badriya Abubakar Gurnah kilichotokea mwishoni mwa wiki iliyopita.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassani akizungumza na Dkt. Abdallah Juma Sadallah Mabodi
.
Makamu wa Rais Akisaini kitabu cha kumbukumbu
Makamu akiagana na Familia baada ya Dua.

WAZIRI WA AFYA ASISITIZA UBORA WA BIDHAA KATIKA KIWANDA KIPYA CHA DAWA NA VIFAATIBA SIMIYU

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kiwanda cha Dawa na Vifaatiba kwa Profesa Olipa David Ngassapa (kulia) leo Jijini Dodoma. 
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Zainab Chaula (aliyesimama) akisema jambo wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kiwanda cha Dawa na Vifaatiba cha Simiyu leo Jijini Dodoma kulia ni Wazir wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisema jambo wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kiwanda cha Dawa na Vifaatiba cha Simiyu leo Jijini Dodoma. 



Na.WAMJW.Dodoma 

Bodi ya wakurugenzi wa kiwanda cha vifaa tiba cha Simiyu(SIMIYU MEDICAL PRODUCTS) wametakiwa kuzalisha bidhaa zenye viwango na kukidhi mahitaji ya ndani nan je ya nchi. 

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa bodi ya wakurugenzi wa kiwanda hicho uliofanyika leo jijini hapa. 

Waziri Ummy amesema kuwa bidhaa zenye viwango itasaidia kuuza nje ya nchi na watanzania kuzitumia kwani lengo la serikali ya awamu ya tano ni ya kukuza uchumi wa viwanda 

“Lakini mhakikishe maamuzi yeyote mtakayofanya mjiridhishe je ni kwa ajili ya maslahi ya Taifa na je yatatufikisha kule tunapotaka kufika,jiridhisheni katika kuhakikisha mnatumia fedha hizi chache tulizonazo katika kuleta matokeo ya haraka haya ndiyo ya kuyazingatia”.Alisisitiza Waziri Ummy. 

Aidha, Waziri Ummy aliitaka bodi hiyo kuhakikisha wanaongeza thamani ya mazao ya nchi kwa kuzalisha bidhaa nchini na kuondokana na uagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi,kuongeza ajira na hata kuondokana na uagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi. 

Hata hivyo aliwataka wasiangalie bidhaa zinazotakana na pamba hivyo kwa baadae ni bora wakaangalia bidhaa zingine zinazohitajika ambazo zinanunuliwa kwa haraka sana kutoka MSD kwani bohari ya Dawa hivi sasa imepata mkataba wa kununua bidhaa za hospitali kwa niaba ya nchi kumi na sita za nchi ya SADC hivyo wahakikishe bidhaa zinazozalishwa zina viwango na ubora na uzalishaji unakidhi soko la ndani nan je ya Tanzania.

SERIKALI YA KENYA YAMKANA JAGUAR

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa Kauli ya Serikali kuhusu kauli ya Mbunge wa Starehe nchini Kenya, Charles Kanyi Njagua, maarufu kwa jina la Jaguar, Bungeni jijini Dodoma, Juni 25, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaamesema Serikali ya Kenya imesema kauli iliyotolewa na Mbunge wa jimbo la Starehe nchini humo, Charles Njagua Kanyi maarufu Jaguar si kauli ya Serikali, hivyo amewataka Watanzania wawe watulivu.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Juni 25, 2019) wakati akitoa kauli ya Serikali kuhusu kauli ya iliyotolewa na mbunge huyo ya kuwataka wafanyabiashara kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania waondoke nchini Kenya ndani ya saa 24.

Amesema baada ya mbunge huyo kutoa kauli hiyo, Serikali ilianza kulifanyiakazi jambo hilo ambapo ilimuita Balozi wa Kenya nchini Tanzania ili kujua kama huo ni msimamo wa Serikali yao ama la, ambapo balozi huyo alimesema ile si kauli ya Serikali ya Kenya wala wananchi.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema mbali na kuwasiliana na Balozi huyo, pia Serikali imewasiliana na Balozi wa Tanzania nchini Kenya ili afuatilie kuhusu kauli ya Mbunge huyo, hivyo amewataka Watanzania waendelee kushirikiana na Wakenya.

“Si kauli nzuri na kauli hii iliyotolewa na mtu mmoja linajenga chuki baina ya mtu na mtu, nchi na nchi na tayari Serikali ya Kenya inalifanyia kazi suala hili na imetuomba Watanzania tuendelee kuwa wavumilivu.”

Waziri Mkuu amesema tamko lile linaweza kuibua chuki na vurugu miongoni mwa nchi mbalimbali zikiwemo za Afrika Mashariki na tayari Wabunge wa Bunge Afrika Mashariki wanaoendelea na kikao cha Bunge hilo jijini Arusha wamepinga na kulaani kauli hiyo.
Wamesema hawatoa nafasi kwa mtu yeyote kuvuruga nchi hizo.

Hivyo, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasihi Watanzania popote walipo waendelee kuishi vizuri na Wakenya kwa kuwa wao hawana chuki na Watanzania bali ni mtu binafsi. Pia amewatahadharisha wananchi wa Afrika Mashariki wawe makini na kauli zao ili kuepusha vurugu.

SPIKA NDUGAI AKIZUNGUMZA NA WAGENI KUTOKA KOGWA NA MBEYA WALIOKUJA KUTEMBELEA BUNGE

$
0
0


  Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Wageni kutoka Jimboni kwake Kogwa, Jijini Dodoma waliotembelea Bunge leo.
Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson (katikati waliokaa mbele) akizungumza na Wanawake Wajasiriamali kutoka Jijini Mbeya waliotembelea Bunge leo. Kulia ni Mbunge wa Chunya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka Mkoa wa Mbeya Mhe. Victor Mwambalasu.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai na Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson (katikati) katika picha ya pamoja na Wanawake Wajasiriamali kutoka Jijini Mbeya waliotembelea Bunge leo.

Arusha, Mwanza wazoa medali za dhahabu mbio za mita 1500 UMITASHUMTA

$
0
0

Washiriki wa mchezo wa riadha fainali maalum za UMITASHUMTA wakikimbia mbio za mita 100 leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara 
Mwanariadha Damian Christian wa Arusha (mbele) akiwaongoza wenzake Robert Francis wa Singida aliyeshika nafasi ya pili na Hoja Samwel wa Simiyu wakichuana vikali katika mbio za mita 1500.
Salma Ismail (392) kutoka Mwanza ambaye alishinda mbio za mita 1500 wasichana akiwa mbele ya wenzake Valaria charles (569) wa Singida ambaye alishika nafasi ya pili na Grace Mpina (080) kutoka Geita ambaye alishika nafasi ya tatu mara baada ya kumaliza mbio hizo leo asubuhi.



Na Mathew Kwembe, Mtwara 

Wanariadha Damian Christian kutoka mkoa wa Arusha na Salma Ismail wa Mwanza wameshinda medali za dhahabu kwa wavulana na wasichana kwenye fainali za mbio za mita 1500 zilizofanyika leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara. 

Damian alitumia dakika 4:16:47 kumaliza mbio hizo huku akifuatiwa kwa karibu na Mwanariadha Robert Francis kutoka Singida ambaye alitumia muda wa dakika 4:17:00, huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Hoja Samwel wa Simiyu ambaye alitumia dakika 4:19:88. 

Kutokana na matokeo hayo Damian amejinyakulia medali ya dhahabu, Robert atapata medali ya fedha ambapo Hoja atapata medali ya shaba. 

Kwa upande wa wasichana medali ya dhahabu imechukuliwa na mwanariadha Salma Ismail wa Mwanza ambaye alikimbia kwa muda wa dakika 4:46:65, ambapo medali ya fedha ilichukuliwa na mwanariadha Valaria Charles wa Singida ambaye alishika nafasi ya pili baada ya kutumia muda wa dakika 4:47:15 huku medali ya shaba ilikwenda kwa mwanariadha Grace Mpina wa Geita aliyetumia muda wa dakika 4:47:25. 

Katika mashindano ya kuruka juu ambayo yalifanyika leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara wanariadha watatu wa kutoka mikoa ya Mara, Kilimanjaro na Geita wamejinyakulia medali za dhahabu, fedha na shaba. 

Nafasi ya kwanza ilishikwa na Mwanariadha Yunus Chacha Mondera wa Mara ambaye aliruka urefu wa mita 1 na sentimita 38, nafasi ya pili imechukuliwa na mwanariadha Witness Martin kutoka Kilimanjaro ambaye aliruka urefu wa mita 1 na sentimita 37, huku nafasi ya tatu ilichukuliwa na Mectrida Kasandhao wa Geita. Matokeo hayo yamewawezesha wanariadha Yunus, Witnes na Mectrida kujinyakulia medali za dhahabu, fedha na shaba.

ZANZIBAR YAPATIWA MSAADA WA MASHINE 17 ZA KUSAFISHIA FIGO

$
0
0

Kaimu Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Ahmad Saleh Ghamdi akimkabidhi Waziri wa Afya Hamad Rashid Muhamed mashine za kusafishia Figo katika sherehe zilizofanyika Bohari Kuu ya Dawa Maruhubi nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Hamza (kushoto) akiwa na Waziri wa Afya Hamad Rashidi na Naibu wake Harusi Suleiman na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Halima (kulia) wakiangali mashine za kusafishia Figo zilizotolewa na Serikali ya Saudia Arabia katia Bohari kuu ya Dawa Maruhubi.
Baadhi ya mashine za kusafishia Figo zilizotlea na Serikali ya Saudi Arabia kwa ajili ya kutoa huduma katika Hospitali za Zanzibar.
Waziri wa Afya Hamad Rashid Muhamed akitoa shukrani baada ya kupokea mashine 17 za kusafishia Figo zilizotolewa na Serikali ya Saudi Arabia (kulia) ni Naibu Waziri wa Afya Harusi Suleiman na kushoto Kaimu Balizi wa Saudi Arabia nchi Tanzania Saleh Ghamdi

*******************

Na Ramadhani Ali – Maelezo 25.6.2019

Serikali ya Saudi Arabia imetoa msaada wa mashine 17 za kusafishia Figo (Dialysis Machines) kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zenye thamani ya shilingi milioni 400.

Kaimu Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Ahmed Saleh Ghamdi alimkabidhi Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Muhamed msaada huo katika hafla iliyofanyika Bohari Kuu ya Dawa Marughubi.

Kaimu Balozi Ahmed alimpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Muhamed Shein na Serikali yake kwa juhudi kubwa wanazochukua katika kuimarisha uchumi na sekta ya afya.

Alisema Serikali ya nchi yake itaendelea kuunga mkono juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hasa katika kukuza sekta ya afya na elimu ambazo ni muhimu katika kuimarisha ustawi wa wananchi.

Aliongeza kusema kuwa Serikali ya Saudi Arabia itafikiria kutoa nafasi za masomo kwa madaktari wa Zanzibar hasa katika fani ambazo bado zinaupungufu wa wataalamu ili ziweze kuimarika katika kutoa huduma bora kwa wananchi.

Waziri wa Afya Hamad Rashidi Muhamed aliipongeza Serikali ya Saudi Arabia kwa misaada mbali mbali inayotoa kwa Zanzibar ikiwemo ya kuimarisha huduma za afya nchini.

Alisema mashine 17 za kusafishia Figo zilizotolewa na Serikali ya nchi hiyo zitawapunguzia na kuwarahisishia kazi watendaji na wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo kuipata kwa urahisi.

Aliongeza kuwa Zanzibar kama zilivyo nchi nyengine zinazoendelea, wagonjwa wa maradhi yasiyoambukiza ikiwemo matatizo ya Figo imekuwa ikiongezeka na kunahitajika kuongeza huduma za kuwahudumia wagonjwa wanaokabiliwa na matatizo hayo.

Alisema baada ya kupatikana msaada wa mashine hizo 17, Wizara itapeleka mashine 10 Pemba na inakusudia kuanzisha huduma ya kusafisha Figo

katika hospitali nyengine za Unguja ili kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali kuu ya Mnazimmoja.

Msaidizi Muuguzi wa Kitengo cha Figo Hospitali Kuu ya Mnazimmoja Zainab Ismail alisema kuongezeka kwa idadi ya mashine za kusafishia Figo katika Kitengo hicho kutawarahisishia utendaji wa kazi na wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo kuipata kwa haraka.

Alisema kazi ya kusafisha Figo huchukua karibu saa nne kwa mgonjwa mmoja na idadi ya wagonjwa waliopo Zanzibar hivi sasa ni wengi hivyo kulikuwa na umuhimu mkubwa kupata mashine nyengine kurahisisha utoaji wa huduma katika Kitengo hicho.

KAMPUNI YA CANDY& CONDY YATOA MSAADA WA VYAKULA,NGUO KWA YATIMA WANAOLELEWA KITUO CHA FARAJA JIJINI ARUSHA

$
0
0
 Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha 

KAMPUNI ya Candy & Candy imetoa  msaada wa vyakula, vinywaji baridi
na fedha za kununulia nguo za ndani watoto yatima wanaolelewa kwenye
kituo cha Faraja cha jijini Arusha.

Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Joe Kariuki aliongoza wafanyakazi wa kampuni hiyo kugawa vitu hivyo pamoja na kuzungumza na  watoto wa kituo hicho zaidi ya 200.

Akizungumza zaidi Kairuki amesema kampuni ya Candy & Candy itaendelea kuwa karibu na kituo hicho ambapo aliahidi kurudi kituoni hapo baada ya miezi miwili na endapo akiwakuta wamebadilika na kuwa na mwenendo mwema basi atawapatia zawadi ya luninga.

"Baba yenu (Faraja) ameniambia hapa kuna waliokuwa wamehukumiwa na
kufungwa, tunashukuru sasa mko kwenye hiki kituo mnalelewa vizuri basi
badilikeni tabia ili msirudi tena kule kwenye matatizo," amesema
Kariuki na kuongeza.

"Nitakuja hapa baada ya miezi miwili,  baba yenu akiniambia
mmebadilika tabia, hampigi watoto wa majirani na mnafanya usafi wa
mwili (kuoga) nitawanunulia TV nitaifunga hapo  (akionyesha
ukutani),".Walikabidhi kituoni hapo kilo 100 za mchele, unga wa mahindi gunia nne, mafuta ya kupikia ndoo mbili zenye lita 20 pamoja na juisi na biskuti ambazo waliwagawia watoto kituoni hapo.

Mkurugenzi huyo wa Candy& Candy ambaye kampuni hiyo ina matawi maeneo mbalimbali nchini huku makao makuu yake yakiwa nchini ,Uingereza alitoa fedha kwa ajili ya kusaidia masomo ya ziada ya mwanafunzi, Baraka Eli ambaye alidai kuwa endapo asingelipa kwa siku ya Jumatatu basi asingeruhusiwa kuingia darasani kujifunza.

Kariuki alilazimika kutoa fedha kwa ajili ya kuwanunulia nguo za ndani watoto wenye umri wa kati ya miaka tisa na 16 kwenye kituo hicho baada ya
kumweleza kuwa wengi wanayo moja huku wachache wakiwa na ambazo
hazizidi tano.Kwa upande wake Naye Rais wa programu ya U & I, (you and I) inayoendeshwa na Candy & Candy,  Nasra Swai akiongea na watoto wenye umri wa kati ya miaka tisa na 17 aliwaleza umuhimu wa kujitambua kama watoto.

Aidha aliwaeleza watoto hao jamii inawapenda na kuwathamini ndiyo
sababu wamefika kwenye kituo hicho  kuongea nao na  kubadilishana
mawazo ambapo aliwaahidi  kurudi tena kwenye kituo hicho kwa ajili ya
kuzungumza nao kuhusu masuala  mbalimbali ya makuzi.Akizungumza kwa niaba ya watoto kwa niaba ya wenzake mtoto, Barakaeli
Faraja amesema wanashukuru kampuni hiyo kuwasaidia kupata vitu
hivyo kwani wmekuwa wakivihitaji kwa muda mrefu.

Ameiomba kampuni hiyo iangalie uwezekano kuwasaidia zaidi kuwalipia
ada baadhi ya watoto, kupata vitanda kwani kwa sasa wanabanana mno,
kompyuta na runinga kwa ajili ya chumba cha watoto wakubwa.Wakati huo huo Mkurugenzi wa kituo hicho Faraja Mollel amesema kuwa wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa chakula cha kutosha kwa ajili ya watoto hao  ambapo wakati mwingine huwapa milo miwili tu kwa siku.

Amesema kuwa yeye aliguswa kuanzisha kituo hicho kutokana na historia
ya maisha yake ambapo yeye akiwa na umri mdogo aliwahi kuishi kwenye
mitaa ya jiji la Arusha akiwa na dd yake, Jenipher ambaye kwa sasa
anaishi Marekani.Amesema walipata msamaria mwema mama wa Kizungu aliyewachukua na kwenda kuishi nao ndipo maisha yao yalipobadilika, hivyo baada ya kufanikiwa akaguswa kuwasaidia watoto waliopitia magumu kama ya kwake.

Faraja amesema awali kwnye kituo hicho hapakuwa na shida ya ada
kwa watoto wa kituo hicho kwani kulikuwa na mfadhili aliyekuwa
akiwasaidia kununua chakula na kulipia ada baadhi ya watoto hao lakini
alifariki mwaka jana jambo linalowaweka katika wakati mgumu kwa sasa.
 Mkurugenzi wa kituo cha faraja wa pili kushoto akitoa maelezo ya jinsi kituo hicho kinavyowahudumia watoto hao

  Mkurugenzi wa kampuni ya Candy &Candy , Joe Kariuki akimkabidhi mkurugenzi wa kituo cha Faraja,Faraja Mollel baazi ya bidhaa waliopeleka katika kituo cha kulelea watoto yatima cha faraja

Young Tanzanian professionals from Vijana Think Tank attend leadership programme in Hong Kong, China

$
0
0
Tanzania's Ambassador to China H.E. Mbelwa Kairuki (third right, from row) poses with Young Tanzanian professionals from Vijana Think Tank(VTT) attending leadership program in Hong Kong, China as organized by the Institute of Advanced Executive Edu Poly University. The goal of the program is to enhance leadership skills in different sectors ranging from Manufacturing, Information and Communication Technology, Health to Tourism.

UNILEVER YAKAMILISHA KAMPENI TOA MKONO WA KA KWA KUSAIDIA YATIMA,WAZEE WASIOJIWEZA

$
0
0
Meneja Bidhaa ya Omo ya Kampuni ya Unilever, Upendo Mkusa (kushoto) akimkabidhi msaada wa sabuni, Sukari na Nguo kwa Mkurugenzi wa Kituo cha Kulelea Watoto yatima cha Children`s Home Msimbazi, Sista Etienne katika kuhitimisha Kampeni ya Kampuni hiyo ya Toa Mkono wa Ukarimu iliyofanyika Kipindi cha mwezi wa Ramadhani uliomalizika hivi karibuni. . Makabidhiano hayo yalifanyika kituoni hapo jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Bidhaa ya Omo wa Kampuni ya Unilever, Upendo Mkusa (katikati) akimkabidhi msaada wa sabuni, sukari na nguo Ofisa Mfawidhi wa Makazi ya wazee wasiojiweza ya Nunge, Jacklina Kanyamwenge katika kuhitimisha kampeni ya kampuni hiyo ya ‘Toa Mkono wa Ukarimu’ iliyofanyika kipindi cha Mwezi wa Ramadhani. Makabidhiano hayo yalifanyika kituoni Nunge, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Wanaoshuhudia ni Christabella Msangi na Nurdin Ally walioambata na meneja huyo.
Mmoja wa wazee wanaoishi katika Makazi ya wazee wasiojiweza ya Nunge, Vumilia Chambusho (kulia), akipokea msaada wa baadhi ya vyakula, nguo na sabuni kutoka kwa Meneja Bidhaa ya Omo wa Kampuni ya Unilever, Upendo Mkusa (watatu kushoto) vilivyotolewa na Unilever katika kuhitimisha kampeni ya kampuni hiyo ya ‘Toa Mkono wa Ukarimu’ iliyofanyika kipindi cha Mwezi wa Ramadhani. Makabidhiano hayo yalifanyika kituoni hapo, Nunge, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Wanaoshuhudia ni Christabella Msangi na Nurdin Ally walioambata na meneja huyo.
Meneja wa Bidhaa ya Omo wa Kampuni ya Unilever, Upendo Mkusa (kushoto) akisalimiana na baadhi ya wazee wanaoishi katika Makazi ya wazee wasiojiweza ya Nunge baada ya kukabidhi msaada wa sabuni, sukari na nguo vilivyotolewa na Unilever katika kuhitimisha kampeni ya kampuni hiyo ya ‘Toa Mkono wa Ukarimu’ iliyofanyika kipindi cha Mwezi wa Ramadhani. Makabidhiano hayo yalifanyika kituoni Nunge, Kigamboni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

RAIS.DK. SHEIN AHUDHURIA MAADHIMISHO YA MIAKA 107 YA SKAUTI

$
0
0
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimvisha Nishani Mlezi wa Skauti Tanzania Rais Mstaaf wa Tanzania Mhe. Ali Hassan Mwinyi, wakati wa hafla hiyo ya maadhimisho ya Miaka 107 ya Sjauti Tanzania, zilizofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.(Picha na Ikulu).
IMG_3848
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Ali Mohamed Shein, akifungwa kiskafu na Vijana wa Skauti kushoto Halima Ali Makame na kulia Lutfia Juma Ali, baada ya kuwasili katika viwanja vya Mpira vya Maisara Suleiman Zanzibar kuhudhuria hafla ya  Maadhimisho ya Miaka 107 ya Skatu Tanzania.
IMG_3889
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Kambi ya Mfano ya Skauti wakati wa maadhimisho ya Miaka 1-7 ya Skauti Tanzania ziulizofanyika katika viwanja vya Maisara Suluiman, akimsikiliza Kijana Jaffar Mohammed, akitowa maelezo ya michuro ya ramani ya Tanzania.
IMG_3940
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Ndg. Alois Zengwe akitowa maelezo ya Kambi ya Mfano ya Skauti wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Skauti kutimiza Miaka 107 Tanzania tangu kuazishwa kwake kushoto Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Alali Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma.
IMG_3967
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akielekea katika eneo lililotayarishwa kwa ajili ya kuyapokea maandamano ya Vijana wa Skauti Tanzania katika viwanja vya Maisa Suleiman Zanzibar kushoto Mkuu wa Skauti Tanzania Mhe. Mwatumu Mahiza na Kiongozi wa Skauti Bi. Amina Clement Edward na kulia Makamu wa Rais wa Chama cha Skauti na Waziri wa Elimu na Mafuzo ya Amali Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma.
IMG_4060
 VIJANA wa Skauti Tanzania wakipita kwa ukakamavu kwa mgeni Raism Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.
IMG_4064
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akipokea maandamano ya Maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania yalioadhimishwa Kitaifa Zanzibar katika viwanja vya Maisara Suleiman
IMG_4095
IMG_4104
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Ali Mohamed Shein, akipokea gwaride Maalum la Vijana wa Skauti Tanzania kuadhimisha Miaka 107 zilizofanyika katika viwanja vya Maisa Suleiman Zanzibar.
IMG_4130
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi wa Meza Kuu wakiwa wamesimama wakati ukipigwa wimbo wa Taifa.
IMG_4137
 VIJANA wa Skauti wakitowa heshima wakati ukipigwa wimbo wa Taifa
IMG_4212
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla ya maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania yaliofanyika kataifa Zanzibar katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.
IMG_4153
 SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zuberia Ali Maulid, Rais Mstaaf wa Tanzania Mhe. Ali Hassan Mwinyi, Makamu wa Rais Mstaaf wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed GharibBilal na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, wakifuatilia hutuba ya mgeni rasmin Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia hayuko pichani.
IMG_4166
MKUU wa Skauti Tanzania Mhe Mwamtumu Mahiza akizungumza na kutowa maelezo ya Maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.
IMG_4172
 MKURUGENZI wa Skauti Kanda ya Afrika Ndg. Fedrick Kamakama  akizungumza na kutowa Salamu za Skauti Duniani wakati wa maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania zilizofanyika Kitaifa katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.
IMG_4184
  MAKAMU wa Rais wa Chama Cha Skauti Tanzania, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma ,akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmin kuhutubia hadhara hiyo ya Maadhimisho ya Miaka 107 ya Sakauti Tanzania zilizofanyika Kitaifa Zanzibar katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.
IMG_4193
IMG_4194
 WAGENI Waalikwa na Vijana wa Skauti Tanzania wakifuatilia hutuba ya mgeni rasmin Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla ya maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania.

Kampuni ya Candy & Candy yasaidia yatima kituio cha Faraja jijini Arusha

$
0
0

Na Woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha 

 KAMPUNI ya Candy & Candy imetoa misaada wa vyakula, vinywaji baridi na fedha za kununulia nguo za ndani watoto yatima wanaolelewa kwenye kituo cha Faraja cha jijini Arusha. Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Joe Kariuki aliongoza wafanyakazi wa kampuni hiyo kugawa vitu hivyo pamoja na kuongea na watoto wa kituo hicho zaidi ya 200. 
Alisema kuwa kampuni ya Candy & Candy itaendelea kuwa karibu na kituo hicho ambapo aliahidi kurudi kituoni hapo baada ya miezi miwili na endapo akiwakuta wamebadilika na kuwa na mwenendo mwema basi atawapatia zawadi ya luninga. 
"Baba yenu (Faraja) ameniambia hapa kuna waliokuwa wamehukumiwa na kufungwa, tunashukuru sasa mko kwenye hiki kituo mnalelewa vizuri basi badilikeni tabia ili msirudi tena kule kwenye matatizo," alisema Kariuki na kuongeza. 
 "Nitakuja hapa baada ya miezi miwili, baba yenu akiniambia mmebadilika tabia, hampigi watoto wa majirani na mnafanya usafi wa mwili (kuoga) nitawanunulia TV nitaifunga hapo (akionyesha ukutani),". 
Walikabidhi kituoni hapo kilo 100 za mchele, unga wa mahindi gunia nne, mafuta ya kupikia ndoo mbili zenye lita 20 pamoja na juisi na biskuti ambazo waliwagawia watoto kituoni hapo. 
 Mkurugenzi huyo wa Candy& Candy ambaye kampuni hiyo ina matawi nchi mbalimbali huku makao makuu yake yakiwa nchini Uingereza alitoa fedha kwa ajili ya kusaidia masomo ya ziada ya mwanafunzi, Baraka Eli ambaye alidai kuwa endapo asingelipa kwa siku ya Jumatatu basi asingeruhusiwa kuingia darasani kujifunza. 
 Kariuki alilazimika kutoa fedha kwa ajili ya kuwanunulia nguo za ndani watoto wenye umri wa kati ya miaka tisa na 16 kwenye kituo hicho baada ya kumweleza kuwa wengi wanayo moja huku wachache wakiwa na ambazo hazizidi tano. 
 Naye Rais wa programu ya U & I, (you and I) inayoendeshwa na Candy & Candy, Nasra Swai akiongea na watoto wenye umri wa kati ya miaka tisa na 17 aliwaleza umuhimu wa kujitambua kama watoto. 
 Aidha ali waeleza watoto hao jamii inawapenda na kuwathamini ndiyo sababu wamefika kwenye kituo hicho kuongea nao na kubadilishana mawazo ambapo aliwaahidi kurudi tena kwenye kituo hicho kwa ajili ya kuzungumza nao juu ya masuala mbalimbali ya makuzi. 
 Akiongea kwa niaba ya watoto kwa niaba ya wenzake mtoto, Barakaeli Faraja alisema kuwa wanashukuru kampuni hiyo kuwasaidia kupata vitu hivyo kwani wmekuwa wakivihitaji kwa muda mrefu. 
 Aliiomba kampuni hiyo iangalie uwezekano kuwasaidia zaidi kuwalipia ada baadhi ya watoto, kupata vitanda kwani kwa sasa wanabanana mno, kompyuta na runinga kwa ajili ya chumba cha watoto wakubwa. Mkurugenzi wa kituo hicho, Faraja Mollel alisema kuwa wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa chakula cha kutosha kwa ajili ya watoto hao ambapo wakati mwingine huwapa milo miwili tu kwa siku. 
 Alisema kuwa yeye aliguswa kuanzisha kituo hicho kutokana na historia ya maisha yake ambapo yeye akiwa na umri mdogo aliwahi kuishi kwenye mitaa ya jiji la Arusha akiwa na dd yake, Jenipher ambaye kwa sasa anaishi Marekani. 
 Alisema kuwa walipata msamaria mwema mama wa Kizungu ambaye aliwachukua na kwenda kuishi nao ndipo maisha yao yalipobadilika hivyo baada ya kufanikiwa akaguswa kuwasaidia watoto waliopitia magumu kama ya kwake. Faraja alisema kuwa awali kwnye kituo hicho hapakuwa na shida ya ada kwa watoto a kituo hicho kwani kulikuwa na mfadhili ambaye alikuwa akiwasaidia kununua chakula na kulipia ada baadhi ya watoto hao lakini alifariki mwaka jana jambo linalowaweka katika wakati mgumu kwa sasa.

TCRA KANDA YA KASKAZINI YATAMBULISHA RASMI KWA WADAU MKATABA WA HUDUMA KWA WATEJA

$
0
0
Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha

MAMLAKA ya  Mawasiliano  Tanzania(TCRA)  Kanda ya Kaskazini imetambulisha rasmi kwa wadau wa mawasiliano mkataba   wa huduma kwa wateja ambao ulikwishazinduliwa tayari rasmi Mei 8 mwaka huu.

Akizungumzia na waandishi wa habari wakati wa kikao cha wadau wa sekta ya mawasiliano  kutoka Kanda ya Kaskazini ambacho kimefanyika leo Juni 26,2019 Kaimu Mkuu wa Kanda ya Kaskazini Mamlaka  ya Mawasiliano Tanzania( TCRA)Mhandisi Imelda Salum amesema lengo ni kubadili mambo mbalimbali yahusiyo taarifa za mawasiliano

Amesema kwamba mkataba huu unakusudia kuongeza uelewa wa wadau kuhusiana na mamlaka ,huduma zinazotolewa na mamlaka,haki na wajibu wa wateja na pia utaelezea jinsi ya kuhamasisha wadau wasioridhika na huduma wanazozitoa

Aidha amebainisha  pia mkataba huo utasaidia kuwafanya watumishi kuwa na mtazamo wa kujali na kuheshimu zaidi mahitaji ya wateja pamoja na wadau wote kwa kuwahudumia bila ubaguzi wowote ule

Amefafanua kuwa lengo kuu la kuboresha haya yote likiwa ni kuboresha maisha ya Watanzania kupitia uthibiti wenye ufanisi ambao unachochea na kukuza ubunifu ambao unahakikisha upatikanaji wa huduma bora na imara za mawasiliano ambazo zinatolewa kwa gharama nafuu zaidi.


Amesema mkataba huo utasaidia kujua namna gani ya kuhudumia jamii kwa ujumla na kuboresha  sekta ya mawasiliano pamoja na kutatua changamoto zilizopo.

Aidha amewashauri wadau wote wanaotumia huduma zinazotolewa na  mamlaka kuhakikisha wanajua vizuri sheria ,kanuni ,miongozo na taratibu za mamlaka ili kuzifuata vyema  sheria zinazongoza matumizi ya huduma za mawasiliano

Kikao hicho kimefunguliwa leo jijini Arusha na kimeshirikisha wadau wa mawasiliano kutoka mikoa  ya kanda ya kaskazini ambayo ni Tanga,Arusha Manyara na Kilimanjaro.
Kaimu mkuu wa kanda ya kaskazini mamlaka  ya mawasiliano TCRA Mhandisi Imelda Salum akimkabidhi leseni ya kurusha matangazo mkurugenzi  wa Radio Kicheko Live ,Phlaviana Kavishe ya mkoani kilimanjaro .
  kaimu mkuu wa kanda ya kaskazini mamlaka  ya mawasiliano TCRA Mhandisi Imelda Salum  akiongea na wadau wa mamlaka ya mawasiliano katika ukumbi wamkutano katika jengo la mkuu wa mkoa wa Arusha
wadau mbalimbali wakifuatilia mkutano huo
 

MAZOEZI MISS TANGA 2019 USIPIME, WAKAZI WA MKOA WA TANGA WAMIMINIKA NYUMBANI HOTEL KUWASHUHUDIA

$
0
0
WAREMBO wanaoshiriki Shindano ya Miss Tanga 2019 wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya mazoezi yao yanayofanyika kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Nyumbani leo
WAREMBO wanaoshiriki Shindano ya Miss Tanga 2019 wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya mazoezi yao yanayofanyika kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Nyumbani leo waliokaa mbele katikati ni Muandaaji wa Mashindano hayo Chuchu Hans
WAREMBO wanaoshiriki Shindano ya Miss Tanga 2019 wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya mazoezi yao yanayofanyika kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Nyumbani leo waliokaa mbele katikati ni Muandaaji wa Mashindano hayo Chuchu Hans
WAREMBO wanaoshiriki Shindano ya Miss Tanga 2019 wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya mazoezi yao yanayofanyika kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Nyumbani waliokaa mbele katikati ni Muandaaji wa Mashindano hayo Chuchu Hans
 
MAZOEZI ya Shindano la Miss Tanga 2019 yameendelea kupamba moto kwenye ukumbi wa Nyumbani Hotel ya Jijini Tanga huku wakazi wa mji huo wakijitokeza kwa wingi kushuhudia kutokana na kusheheni warembo bomba.

Shindano hilo linatarajiwa kufanyika Julai 6 mwaka huu kwenye Ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Resort iliyopo pembezoni mwa ufukwe wa bahari ya Hindi.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa mazoezi hayo Muandaaji wa Shindano hilo Chuchu Hans ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Chuchu Double Touch Entertainment alisema kwamba maandalizi ya shindano yanaendelea vizuri

Alisema kwamba warembo hao wanafanya mazoezi hayo kila siku jioni chini ya Mwalimu wao Pili na Rashida Wanjara.

Alisema kwamba katika shindano hilo warembo 18 watachuana ili kuweza kumpata Malkia wa Taji hilo ambayo atauwakilisha mkoa huo kwenye mashindano Kanda ya kaskazini,Miss Tanzania na Shindano la Miss World.

“Kwa kweli kwa sasa maandalizi yanaendelea vizuri na namshukuru Mungu tumepata warembo bomba ambao watashindana kwa lengo la kumpata mshindi wa Kinyang’anyiro hicho “Alisema.

Alisema kabla ya kufanyika kwa shindano hilo warembo hao watashiriki kwenye shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kufanya usafi kwenye vituo mbalimbali na vivutio vya Utalii vilivypo mkoani hapa kwa lengo la kuhamasisha utalii wa ndani.

Hata hivyo alisema kwamba onyesho hilo litapambwa na wasanii wa bongo movie na wengine ambao watatumbulishwa na Waandaaji wa Shindano hilo. 

GODSON KARIGO NA BONGO ZOZO WAHAMASISHA WATANZANIA KUSHAINGILIA TAIFA STARS

$
0
0
 Mwenyekiti wa chama cha Ushangiliaji nchini Godson Karigo (kushoto) na mwenzie Philemon Ntahilaja wakiwa kwenye kambi ya Taifa Stars jijini Cairo kuwahamasisha kwenye michuano ya AFCON
Mwenyekiti wa chama cha Ushangiliaji nchini Godson Karigo akiwa na mshabiki mkubwa wa Taifa Stars aishiye Uingereza Bongo Zozo wakiwa Misri


Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images