Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109609 articles
Browse latest View live

Sima: Ofisi ya Makamu wa Rais imeendelea kuchukua Hatua kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi

0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mussa Sima amesema Ofisi hiyo imeendeelea kuchukua hatua za makusudi kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Amesema hayo leo bungeni, Dodoma alipojibu swali la Mbunge wa Konde Mhe. Khatibu Said Haji aliyeuliza je hatua gani Serikali inachukua kudhibiti athari za uharibifu katika Bandari ya Tanga eneo la ‘Deep Sea’ lango kuu la kuingilia na kutokea.

Mhe. Sima alisema Ofisi hiyo imeandaa mkakati na kutekeleza mkakati wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi wa mwaka 2007 na mkakati wa kulinda wa mwaka 2012.Alisema mikakati hiyo inaelekeza hatua za haraka za kulinda sekta muhimu za maji, maliasili, miundombinu, afya, nishati, ukanda wa pwani na maeneo ya bahari.

“Eneo la ufukwe linalojulikana kama Deep Sea lililopo katika Jiji la Tanga linakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo athari za kimazingira kama vile utupaji wa taka hasa za plastiki na taka zingine ambazo huletwa na mifereji ya maji ya mvua inayoingia baharini kutoka maeneo mbalimbali ya Tanga hivyo Serikali ikishirikia na imechukua hatua za kutoa elimu kwa wananchi wakiwemo wavuvi kuhusu utunzaji wa mazingira,” alisema Naibu Waziri.

Serikali yaweka mikakati Viwanja vya Ndege

0
0

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Issac Kamwelwe leo akifungua Jukwaa la Pili la Kitaifa la Usafiri wa Anga linalofanyika kwa siku mbili kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. 


SERIKALI imesema imeweka mipango kabambe ya kuboresha viwanja vidogo vya ndege (Airstrips), ili viweze kutumika kirahisi na ndege ndogo zinazosafirisha Watalii kutembelea mbuga mbalimbali za wanyama na vivutio vilivyopo nchini. 

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Issac Kamwelwe katika Jukwaa la Pili la Kitaifa la Usafiri wa Anga linaloendelea kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), ambapo tayari imeundwa kamati kutembelea viwanja hivyo, ambavyo amesema vipo zaidi ya 600 vikiwemo vya makampuni binafsi. 

“Hivi viwanja ndivyo vinavyoingiza Watalii ndani ya mbuga na vivutio vingine baada ya kushuka pale KIA (Kilimanjaro International Airport) na hapa Dar es Salaam Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), sasa hivi vinatakiwa viwe katika ubora mzuri utakaofanya Watalii kujiona wapo sehemu nzuri na salama,” amesisitiza Mhandisi Kamwelwe. 

Hata hivyo, Mhandisi Kamwelwe amesema Idara ya Uhandisi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), itaimarishwa zaidi ili iweze kufanya marekebisho kwenye viwanja hivi, ikiwezekana kununuliwa vifaa ili kufanya kazi kwa ufanisi. 

Pia amesema tayari Serikali imeweza kusimamia vyema mradi wa ujenzi wa Jengo la Tatu la abiria la JNIA, ambao umekamilika na limeongeza uwezo wa kuhudumia abiria, ambapo itahudumia abiria milioni sita kwa mwaka. 

“Ninawataka wafanyabiashara na wadau wengine wote kuchangamkia fursa za
kibiashara zilizopo kwenye jengo letu hili la kisasa, ambapo sasa nimetaarifiwa wapo katika hatua za kuwapata watoa huduma ndio maana ninasema mjitokeze kwa wingi kuomba,” amesema Mhandisi Kamwelwe. 

Akizungumzia viwanja vingine amesema baada ya kukamilika kwa upanuzi na ukarabati wa viwanja vya ndege vya Songwe na Mwanza vitawekwa katika daraja la Kimataifa, kutokana na kuwa na miundombinu ya kisasa, ambapo kwa upande wa Mwanza ujenzi wa jengo la mizigo upo katika hatua ya mwisho kukamilika. 

Kwa sasa kiwanja cha ndege cha Songwe kipo daraja 3C na yakikamilika maboresho ya miundombinu kitakuwa daraja la 4D na Mwanza ni daraja 4C.

Maafisa Habari Taasisi za Umma Wapongeza TAGCO na Idara ya Habari MAELEZO Kuwatembelea

MAMLAKA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA YAELEZA ILIVYOFANIKIWA KUDHIBITI BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA

0
0

Na Said Mwishehe,Globu ya Jamii

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini Tanzania imesema imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kudhibiti uingizwaji wa dawa za kulevya huku ikieleza namna ambavyo wafanyabiashara wakubwa wa dawa hizo kufungwa na wengine kukimbia nchi.

Akizungumza kwenye mahojiano maalum na Michuzi Blog pamoja na Michuzi TV Kamishna wa Kinga na Tiba wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini Dk.Peter Mfisi amesema kwa sasa mamlaka imefanikiwa kudhibiti biashara ya dawa za kulevya.

Dk.Mfisi amefafanua hayo wakati Akifafanua zaidi kwenye Maadhimisho ya Siku ya Dawa za Kulevya Duniani ambayo hufanyika kila ifikapo Juni 26 ya kila mwaka ambapo kwa Tanzania kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Tangamano jijini Tanga ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan.

" Katika kuhakikisha tunadhibiti biashara ya dawa za kulevya nchini kwetu, Mamlaka yetu iliamua kuanza na kuwadhibiti wafanyabiashara wakubwa ambao wanajihusisha na biashara hii ikiwa pamoja na kuingiza nchini.

"Kulikuwa na wafanyabiashara waliokuwa anaingiza hadi kilo 100 za dawa za kulevya aina ya Herroin , baada ya kuwadhibiti hao kwa kuwakamata na kuwachukulia hatua ikiwa pamoja na kufungwa , tumefanikiwa kudhibiti biadhara hiyo.Pia kuna wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya ambao wamekimbia nchini yetu,"amesema Dk.Mfisi.

Pia amesema katika kukomesha biashara ya dawa za kulevya wanatambua kuna wale wafanyabiashara wadogo wadogo lakini hawakuanza na hao kwani walijua kuna mahali ambapo wanazipata, hivyo walianza na wakubwa.

"Ripoti ya taasisi za kimataifa za kudhibiti biashara ya dawa za kulevya zinaonesha Tanzania imefanikiwa kupunguza uingizwaji wa dawa za kulevya kwa asilimia 90 , hivyo imebaki asilimia 10 na ukweli tumefanikiwa sana,"amesema Dk.Mfis.

Pamoja na mambo mengine Dk.Mfisi amezungumzia hatua ambazo zimechukuliwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupamba na Dawa za Kulevya katika kuhakikisha inadhibiti njia ambazo zilikuwa zinatumika kupitisha dawa za kulevya.Amesema kuwa Mamlaka kwa sasa imekuwa makini kuhakikisha dawa za kulevya hazipiti kwenye mipaka ya nchi yetu kwa kuimatisha ulinzi ukiwemo kwenye Pwani ya Bahari ya Hindi ambayo ilikuwa inatumika sana huko nyuma.

"Tumefanikiwa kudhibiti Pwani ya Bahari ambako wafanyabiashara walikuwa wanatumia kama njia ya kupitisha dawa hizo.Hivyo wameamua kutumia Pwani ya Msumbiji na Afrika Kusini na kisha wanatumia njia barabara ili kuifikisha wanakotaka kuipeleka,"amesema Dk.Mfisi.

Amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk.John Magufuli iko makini katika kukabiliana na dawa za kulevya nchini na ukweli uliopo wote wanaojihusisha na biashara hiyo wamechukuliwa hatua stahiki.

WANUFAIKA WA TASAF WATAKIWA KUTOBWETEKA NA MAFANIKIO WALIYOYAPATA.

0
0
NA Estom Sanga-ZANZIBAR 

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Taifa ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF- Dr. Moses Kusiluka amewataka Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Serikali kupitia TASAF kutumia fursa hiyo kwa ukamilifu kwa kufanya kazi kwa bidii ili kutimiza azma ya serikali ya kupambana na umaskini nchini. 

Dr. Kusiluka ambaye pia ndiye Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-IKULU -ameyasema hayo katika shehia ya Kianga wilaya ya Magharibi ‘’A’’ Mkoa wa Mjini –Magharibi,Kisiwani Unguja ambako ameambatana na Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Taifa ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF- kujionea utekelezaji wa shughuli za Mfuko huo Kisiwani humo. 

Amesema Serikali ya Awamu ya Tano inafanya juhudi kubwa za kuweka mazingira mazuri kwa Wananchi kujiletea maendeleo na kuboresha maisha yao hivyo akawataka kutumia vizuri fursa hiyo kwa kufanya kazi za uzalishaji mali kwa bidi ili kukuza uchumi wao na hatimaye kuchangia katika pato la taifa na kuondoa kero ya umaskini miongoni mwao kwa vitendo. 

Dr. Kusiluka pia amewataka Walengwa wa TASAF kutobweteka na mafanikio waliyoanza kuyapata kutokana na huduma zinazotolewa na Serikali kupitia TASAF badala yake waendelee kuuchukia umaskini kwa vitendo kwa kufanya kazi kwa bidi ili hatimaye waweze kuboresha maisha yao huku akisisitiza ustawi wa jamii kwa ujumla hususani watoto kama ilivyo dhamira ya Serikali. 

Katika hatua nyingine Dr. Kusiluka ameuagiza Uongozi na Watumishi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu mkubwa na kuzingatia Uzalendo kwani amesema Mfuko huo unagusa nyanja muhimu za Maendeleo ya Wananchi katika sekta mbalimbali zikiwemo elimu, afya,maji,uchumi,kilimo,mifugo na hifadhi ya mazingira na hivyo kuwa miongoni mwa sekta zinazogusa maisha ya wananchi wengi moja kwa moja.“Serikali inathamini mchango wa taasisi hii katika jitihada zake za kupunguza umaskini nchini, endeleeni kufanya kazi kwa bidi ili kufikia malengo yaliyokusudiwa kwa haraka na ufanisi mkubwa” amesisitiza Dr. Kusiluka. 

Kwa upande wake, Naibu Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Mihayo Juma Nunga akizungumza na Wananchi baada ya Wajumbe wa Kamati hiyo kutembelea na kukagua ujenzi wa kituo cha Afya cha Shehia ya Kianga inayojengwa na TASAF kwa kushirikiana na Wananchi wa eneo hilo, amesema ujenzi huo ni miongoni mwa vielelezo vya namna serikali zote mbili,yaani ile ya Muungano na ile ya Mapinduzi zinavyowajali wananchi kwa kuondoa kero zao kwa vitendo. 

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii,TASAF-Bw.Ladislaus Mwamanga amesema kumekuwa na mafanikio makubwa katika utekelezaji wa shughuli za Mfuko huo yaliyochangiwa kwa kiwango kikubwa na Serikali,Wadau wa Maendeleo na Wananchi hususani Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ambao amesema kwa sehemu kubwa wameanza kuboresha maisha yao na kuonyesha namna wanavyouchukia umaskini kwa vitendo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Taifa ya TASAF,Dr.Moses Kusiluka(mwenye  miwani ) akikagua  baadhi ya bidhaa zilizotengenezwa na Walengwa wa TASAF katika shehia ya Kianga, kisiwani Unguja kama mojawapo ya njia ya kujiongezea kipato .
  Mwenyekiti wa Kamati Uongozi wa  Taifa ya TASAF ( aliyevaa miwani) akikagua bidhaa zilizotengenezwa na Walengwa wa TASAF katika shehia ya Kianga,Unguja kama njia mojawapo ya kujiongeza kipato .Anayefuatia ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais-ZMZ- Mhe. Mihayo Juma Nunga.

 Wajumbe wa kamati ya uongozi ya taifa ya TASAF wakipata maelezo ya utekelezaji wa shughuli za TASAF kisiwani Unguja.

 Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Taifa ya TASAF Dr. Moses Kusiluka (aliyesimama ) akiwahutubia Wananchi wa Shehia ya Kianga kisiwani Unguja (hawapo pichani) wakati wa ziara ya kamati hiyo kukagua miradi ya TASAF kisiwani humo.

 Mwenyekiti wa kamati ya Uongozi ya taifa ya TASAF Dr.Moses Kusiluka  (alivaa koti) akiongoza wajumbe wa kamati hiyo kukagua ujenzi wa jengo la kituo cha Afya Kianga ,Unguja linalojengwa na TASAF kwa kushirikiana na wananchi, Katikati ni mmoja wa Wajumbe wa Kamati hiyo Dr.Gwajima ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia sekta ya Afya,kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Bw. Ladislaus Mwamanga.

 Sehemu ya Walengwa wa TASAF na wananchi wa shehia ya Kianga,Unguja wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya Taifa ya TASAFambaye pia ndiye Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-IKULU Dr. Moses Kusiluka (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kamati hiyo kukagua miradi ya TASAF kisiwani humo

VIONGOZI WASTAAFU WA MAGEREZA KUZINDUA VITABU VIWILI VINAVYOELEZEA HISTORIA YA JESHI LA MAGEREZA

0
0
 Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akionesha vitabu viwili ambavyo vimeandikwa na Viongozi Waandamizi wastaafu wa Jeshi la Magereza, akiwemo Kamishna Mkuu Mstaafu wa Magereza, Simon Mwanguku na Naibu Kamishna Mstaafu, John Nyoka, Viongozi hao wamekabidhi vitabu hivyo leo juni 24, 2019, Makao Makuu ya Magereza.  Vitabu hivyo vinaelezea historia ya Jeshi la Magereza pamoja na Programu za Urekebishaji vinatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni.
 Viongozi Waandamizi wastaafu wa Jeshi la Magereza,  akiwemo Kamishna Mkuu wa Magereza Mstaafu wa Magereza, Simon Mwanguku(kushoto), Kamishna Mkuu Mstaafu, Jumanne Mangala(katikati) na Naibu Kamishna Mstaafu wa Magereza, John Nyoka(kushoto) wakiwa Ofsini kwa Kamishna Jenerali wa Magereza katika mazungumzo maalum ya maandalizi ya uzinduzi wa vitabu viwili vinavyoelezea historia ya Magereza pamoja na Programu ya Urekebishaji.  
 Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Uwesu Ngarama akiwa na manaibu Kamishna wa Magereza kwa pamoja wakifuatilia mazungumzo maalum ya maandalizi ya uzinduzi wa vitabu viwili vilivyoandikwa na Viongozi Waandamizi wastaafu wa Magereza, leo Juni 24, 2019.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akizungumza na Viongozi Waandamizi wastaafu wa Jeshi la Magereza(kulia), leo Juni 24, 2019, Makao Makuu ya Magereza. Kushoto ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Uwesu Ngarama akiwa na manaibu Kamishna wa Magereza kwa pamoja wakifuatilia mazungumzo ya maandalizi ya uzinduzi wa vitabu viwili vilivyoandikwa na wastaafu wa Magereza(Picha na Jeshi la Magereza). 

Vodacom M-Pesa kunufaika na gawio la bilioni 27 za faida ya M-Pesa

0
0
Wateja  wa Vodacom M-Pesa taktribani milioni 8, kuanzia leo watapata sehemu ya faida ya bilioni 27 ikiwa ni bonus kutoka kwenye akaunti ya M-Pesa Trust. Mtandao huo unaoongoza nchini ulitangaza kwamba kwa mwezi mmoja na nusu kuaanzia leo, wateja wake wa M-Pesa watapata sehemu yao ya gawio hilo lililopatikana kama faida ya matumizi ya huduma hiyo. 
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa M-Commerce Epimack Mbeteni alisema, "tunashauku ya kugawana faida hii na wateja wetu kwani wao ndio sababu ya mafanikio ya huduma ya M-Pesa. Huduma ya M-Pesa imechangia maendeleo lukuki ya watanzania na mpango huu umedhamiria kuendelea kuwapa wateja wetu faida zaidi. Wateja wote wa Vodacom ambao wamekuwa wakitumia M-Pesa watafaidika na bonus hii ya bilioni 27 ambayo itagawiwa moja kwa moja kupitia M-Pesa”. 

Kuanzia sasa wateja wa Vodacom wanaweza kutuma SMS ya neno KIASI kwenda namba 15300 ili kujua kiwango gani cha faida watapokea. Baada ya kupata gawio hili, wateja wa M-Pesa wanaweza kukomboa faida hiyo kwa kuitoa kama fedha taslimu, kununua muda wa maongezi, vifurushi au kulipia bili.

"Kiasi ambacho mtu atapokea kama sehemu ya faida hiyo itategemea na idadi ya miamala aliyokuwa akifanya kwa kipindi fulani. Shughuli hizo ni kama miamala ya kuhamisha fedha, malipo ya bili mbalimbali au manunuzi ya muda wa maongezi. Napenda kuwahimiza wateja wetu kutuma SMS ili kujua ni kiasi gani cha gawio hili wanaostahili kupokea" alisisitiza Epimack.

M-Pesa inaumiliki wa soko wa asilimia 38.6% na inaongoza kwa kuwa huduma ya fedha za mkononi inayotumiwa na watanzania wengi zaidi ambao wanafanya hadi TZS 4.1 trilioni kwa mwezi. "Tumewekeza vilivyo katika M-Pesa ndani ya miaka kumi iliyopita na sasa huduma imekuwa na ufumbuzi wa kibunifu unaokidhi mahitaji ya watanzania kupitia bidhaa mbalimbali kama vile M-Koba, M-Pawa, Halal Pesa M-Pesa MasterCard na nyingine nyingi. Tunaendelea kuwa na nia ya kuboresha huduma hii kwa njia ya ubunifu huku tukishirikiana na makampuni pamoja na wavumbuzi mbalimbali ili kuendesha ajenda ya ujumuishwaji wa kifedha nchini" alimaliza Mbateni.

Mikoa 12 yafuzu fainali mbio za mita 1500 UMITASHUMTA 2019

0
0
Na Mathew Kwembe, Mtwara
Jumla ya washiriki 30 kutoka mikoa 12 nchini wamefuzu hatua ya fainali kushiriki mbio za mita 1500 zilizopangwa kufanyika kesho katika uwanja wa chuo cha ualimu Mtwara.

Washiriki hao 15 wavulana na 15 wasichana watashindana katika fainali za mbio ndefu za mita 1500 kwa ajili ya kuwapata washindi watatu kwa upande wa wavulana na washindi watatu kwa wasichana ambao wataibuka na medali za dhahabu, fedha na shaba.

Kwa mujibu wa Mratibu wa mashindano ya UMITASHUMTA taifa bwana Leonard Thadeo, mchezo huo wa riadha utachezwa kesho asubuhi ambapo utatanguliwa na fainali maalum za mbio fupi za mita 100 kwa wavulana na wasichana na kufuatiwa na mbio fupi za mita 200 kwa wavulana na wasichana.

Bwana Thadeo amewataja  waliofuzu fainali za mbio mita 1500 ni pamoja na Damian Christian wa Arusha, Hoja Samwel wa Simiyu, Robert Franciswa Singida, Frank Mashaka wa Mwanza, Paschal Juma wa Tabora  na Jackson Renatus wa Geita.

Wengine Amiri shaban wa Singida, Emanuel Ernest wa Manyara, Azari philipo wa Kigoma, Tululi Masanja wa Morogoro, Masanja Ngado wa Tabora, David Paulo wa Mara, Lenard Juma wa Geita, Saimon sangalali wa Mara na Maraba Madoshi wa Mwanza,

Kwa upande wa wasichana waliofuzu mita 1500 ni pamoja na Nyanzabe Mhalu wa Mara, Agnes Joseph wa Tabora, Salma Charles wa Shinyanga, Valaria wa Singida, Salma Musa Ismail wa Mwanza, na Faidha Ally wa Singida.

Washiriki wengine ni Grace Mpina wa Geita, Salome Ngogene wa Iringa, Taus Saimon wa Tabora, Hasja Mwinga wa Mbeya, Modesta Juma wa Geita, Winfrida Marwa wa Mara, Anita Fred wa Songwe na Veronica  Lubora wa Songwe.

Wakati huo huo michezo mbalimbali  imeendelea leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara ambapo katika matokeo ya mpira wa mikono kwa wavulana Tabora iliifunga Mtwara 13-05, Lindi waliwafunga Pwani 05-03, shinyanga  wasichana waliwafunga Rukwa 09-05, Kigoma wasichana walifungwa na shinyanga 07-10, na Njombe wavulana walifungwa na Lindi 09-12.

Matokeo mengine yanaonyesha Mwanza wasichana walifungwa na Mbeya 10-12, katavi wavulana walifungwa na Dodoma 10-19, Manyara wasichana waliwafunga Kagera 18-4, huku Simiyu wavulana wakiwafunga Songwe 11-06, Dodoma wasichana wametoka sare na Dar es salaam kwa 17-17, na Mwanza wavulana wamewafunga Manyara kwa 18-16.

Pia Mtwara wasichana imefungwa na Geita kwa 03-22, Arusha wavulana wamefungwa na Morogoro 10-35, Simiyu wasichana wamefungwa na Katavi kwa 03-06, Dar es salaam wavulana wamewafunga Singida kwa 27-13, Singida wasichana wamewafunga songwe kwa 08-05 na Pwani wavulana wamewafunga Kigoma kwa magoli 12-08, Songwe wavulana wamefungwa na Geita kwa 14-22, Mara wasichana wamewafunga Rukwa kwa 19-03, Mara wavulana wamewafunga Iringa 38-06, Geita wasichana wamewafunga Morogoro 13-11 na Mtwara wamefungwa na Tanga kwa 06-18
 Mwanariadha kutoka mkoa wa Arusha Damian Christian akiwaongoza wenzake katika mbio za mita 1500 hatua ya nusu fainali leo.
Washiriki wa mbio za kupokezana vijiti kutoka mikoa mbalimbali wakishiriki mbio za mita 400 leo.

AKON KUONDOA GIZA BARANI AFRIKA.

0
0
Na Moshy Kiyungi
Licha ya kuwa ni mwanamuziki, Akon ni mwekezaji maarufu aliyeamua kutumia tasnia yake ya muziki kukabiliana na maendeleo endelevu ya watu wa barani Afrika. Nyota huyo wa R & B alizindua mpango maalum wa kutoa mafunzo unaoitwa ‘Akon Angaza Afrika’ ambao una lengo la kutumia nguvu ya Jua kuzalisha umeme.

Katika uzinduzi huo uliofanyika katika mjini mkuu wa Bamako nchini Mali, Akon anayomatumaini ya kuwafikia watu milioni 600 barani wa Afrika. Mafunzo hayo yatafundisha wadau wa mradi huo jinsi ya kutunza mifumo ya nishati hiyo inayoendeshwa kwa nguvu ya jua. Samba Bathily ambaye ni mwanzilishi msaidizi wa mradi huo, alisema jua na teknolojia hiyo ya ubunifu itasaidia kuleta umeme katika nyumba na kwenye jamii kwa ujumla.

Akon alielezea sababu ya kuwekeza zaidi kwenye nishati ya umeme, alisema kwamba ni moja ya njia ya kutoa fursa za kiuchumi na huduma za kijamii kwa Bara la Afrika, ambalo sehemu kubwa ni giza kutokana na ukosefu wa nishati ya umeme. Rapa wa huyo wa R & B Akon, alifanya ziara katika nchi ya Liberia kwa ajili ya kuweka umeme wa jua katika shule mbili za msingi katika taifa hilo lililo Magharibi ya Afrika.

Akon ambaye ni mwenye asili ya nchi ya Senegal, anashirikiana na kampuni ya Bridge International Academies pamoja na ushirikiano na mashirika mengine ya Kimatifa kusimamia shule 50 nchini Liberia. Wakati msafara wake wa magari ulipokuwa ukipita katika mji mkuu wa Monrovia, chini ya ulinzi wa maafisa wa polisi, Akon alisema kuwa inasikitisha kuona kwamba hakuna umeme katika barabara ya kilomita 50 kutoka uwanja wa ndege.

Mradi huo wa Akon utasaidia watu wa bara la Afrika kuweza kuwa na umeme tofauti na sasa ambapo changamoto za ukosefu umeme umekuwa mkubwa sana. Majina kamili ya mwekezaji huyu anaitwa Aliaumie Damala Badara Akon Thiam, Mmarekani mwenye asili ya Senegal. Ni mtunzi, mwimbaji wa nyimbo za R & B, mtayarishaji wa rekodi, mfanyabiashara mkubwa pia ni mhisani.

Baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kwamba Akon alizaliwa mwaka 1981, Taasisi zingine ikiwemo AP ilidai kuwa alizaliwa Aprili 30, 1973 mtaa wa St. Luis nchini Marekani. Ili kukwepa shughuli za kutafuta kibali cha uhamiaji, aliishi mjini Dakar, Senegal hadi alipofikisha umri wa miaka 7, kisha akabadilishana kati ya kuishi nchini Senegal na Marekani hadi alipofikisha umri wa miaka 15, alipohamia kabisa mjini Jersey, New Jersey huko Marekani.

Akon alikulia katika mandhari ya muziki na alifundishwa kucheza ala kadhaa ikiwemo djembe, kinanda, gitaa, ngoma na vingine vingi zaidi ya vyombo tano vya muziki. Alianza kutambua kipawa chake cha muziki, akaanza kujivunia historia ya muziki iliyokuwa kwenye familia yake kwakuwa alizaliwana wazazi Baba na mama yake wote walikuwa wanamuziki.

Mwaka 2003 alifungwa jela miaka mitatu kutokana na swala ya kuhusishwa ya wizi. Lakini makala ya jarida la Smoking Gun, ilieleza kuwa Akon hakushtakiwa na hatia yoyote ya uhalifu na hakutumikia kifungo chochote gerezani kati ya 1999 na 2002 kama alivyodai hapo awali. Yeye alisema kwamba jaribio la jarida la The Smoking Gun la kumharibia jina halikuwa na maana yoyote kwani hilo lilikuwa ni jambo alilojaribu kulisahau.

Akon alisema kuwa yeye hajawahi kukaa kwenye jela kipindi cha miaka 3 mfululizo, lakini amewahi kukaa kwa vipindi vifupi vifupi ambavyo vimefikia miaka mitatu. Baada ya kutoka jela alikutana na jamaa anayeitwa Stephen, ambaye ndiye aliyegundua kipaji chake kisha wakawa marafiki wakubwa. Kwa upendo alikuwanao Stephen, aliamua kumfundisha Akon maswala ya muziki akiwa huko Atlanta, Georgia nchini Marekani.

Kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi, Akon alishindwa kusaini katika record label ya rafiki yake Stephen, hivyo akabaki mtaani tu. Alianza kuandika na kurekodi nyimbo katika studio yake ya nyumbani. Tepu zake zilifika kwenye kampuni ya SRC/Universal, ambayo ilitoa albumu (LP) yake ya kwanza ya Trouble Juni 2004. Albamu hiyo ina nyimbo kama "Locked Up" na "Lonely", "Belly Dancer (Bananza)", "Pot of Gold", na "Ghetto."

Ilikuwa albamu ya kwanza kutolewa na kampuni yake mpya ya kurekodi ya Konvict Music. Wimbo wa "Locked Up" uliorodheshwa kwa nyimbo 10 bora nchini Marekani na tano bora nchini Uingereza Albamu hiyo ni mseto wa mtindo mwororo wa Akon wa Afrika Magharibi, ukichanganywa na MIDU kutoka Pwani ya Mashariki na Kusini. Nyimbo nyingi za Akon huanza kwa sauti ya kufunguka kwa mlango wa jela naye akitamka neno "Konvict".

Mwaka wa 2005 alitoa wimbo "Lonely" (ambao ni sampuli ya wimbo wa Bobby Vinton wa "Mr Lonely"). Wimbo huo uliorodheshwa miongoni mwa nyimbo tano bora kwenye orodha ya bango la nyimbo 100 mashuhuri, na ukaongoza kwenye chati katika nchi ya Australia, Uingereza na Ujerumani. Akon kisha alitoa wimbo mwingine ulioitwa 'Moonshine', akishirikiana na msanii kutoka New Zealand aliyeitwa Savage.

Wimbo huo ulivuma huko New Zealand na Australia, ukawa namba moja katika chati ya New Zealand. Akon hivi sasa ameanzisha kampuni mbili za kurekodi ambazo ni, Konvict Muzik na Kon Live Distribution. Anajulikana kama mmojawapo kati ya waimbaji waliofanikiwa kwa uhodari zaidi wa mtindo wa R & B karne ya 21. Msanii huyo Akon huingiza kibindoni zaidi ya dola milioni 30 kwa mwaka . Haya ni kulingana na jarida la Forbes.

Mwaka wa 2004 alipata umashuhuri kufuatia kutolewa kwa wimbo wa "Locked Up", uliokuwa wa kwanza kutoka kwa albamu yake ya kwanza iliyoitwa, Trouble. Albamu yake ya pili, Konvicted, ilimwezesha kuteuliwa kushindania Tuzo la Grammy kutokana na wimbo wa "Smack That". Albamu ya pili ya Akon, Konvicted ilitolewa tarehe 14 Novemba 2006, Ilikuwa na nyimbo alizoshirikisha waimbaji kama Eminem, Snoop Dogg na Styles P.

Albamu hiyo ya Konvicted ilipata kushika nafasi pili kwenye orodha ya Bango ' la nyimbo 200 mashuhuri, na kuuza nakala 286,000 katika wiki yake ya kwanza. Mwaka huohuo Akon alivunja rekodi ya orodha ya nyimbo 100 mashuhuri.

Wimbo wake wa "Smack That" ulipata mafanikio ya juu zaidi kwa kuruka kutoka namba 95 hadi namba 7. Ulipendekezwa kushindana katika kategoria ya Best Rap / Sung Collaboration katika mashindano ya 49 ya Grammy Awards, lakini ulishindwa na ule wa Justin Timberlake na wa T.I. wa "My Love". Msanii Akon mwaka wa 2006, alifungua kampuni yake mpya ya Kon Live Distribution chini ya Interscope Records. Msanii wake wa kwanza kusaini mkataba naye alikuwa ni Ray Lavender

Alishirikiana na msanii Chamillionaire kwenye tepu yake ya, Mixtape Messiah 2, akishiriki kwenye kibao "Ridin 'Overseas", ambacho alikuwa amekitayarisha. Julai 07, 2007 Akon alitumbuiza katika hafla ya American leg of Live Earth. Novemba 2007, Akon alirekodi toleo jipya la wimbo "Wanna Be Startin 'Somethin'" akiwa na Michael Jackson.

Ilipotimu Februari 2008, toleo jipya jingine la wimbo huo lilitolewa wakati wa maadhimisho ya 25 ya kutolewa upya kwa video ya Michael Jackson ya Thriller. Wimbo unaoitwa "Hold My Hand" wa R & B, Julai 2008, ulisambaa kwenye mtandao, ulioimbwa kwa ushirikiano kati ya Michael Jackson na Akon, na uliotungwa na Claude Kelly.

Baada ya kifo cha ghafla cha mfalme wa Pop Michael Jackson, ambaye Akon alikuwa akifanya kazi naye katika miaka ya mwisho, Akon alitoa wimbo wa kuonyesha heshima unaoitwa "Cry Out Of Joy". Akon na Michael Jackson walikuwa marafiki wa karibu katika wakati huo wa mwisho wa maisha ya Michael Jackon

Aidha aliwahi kufanyakazi na Whitney Houston katika kutayarisha albamu yake mpya ya mwaka wa 2009 iitwayo I Look To You. Yeye alishiriki katika wimbo wa "Like I Never Left". Inadaiwa kuwa Akon aliwahi kushiriki katika ulanguzi wa madawa ya kulevya, lakini yeye alikanusha akisema hajawahi kutumia madawa hayo, ingawa maneno ya baadhi ya nyimbo zake yanakinzana na makanusho yake.

Mwaka 2014 alifanya kampeni yake ya Akon Lighting Africa ambayo alifunga umeme katika nchi 15 za Afrika. Akon ana mipango ya kurekodi filamu nzima yenye jina Illegal Alien. Filamu hii imejikita katika baadhi ya matukio ya maisha yake na mwigizaji Mekhi Phifer atamwigiza yeye.

Mnamo 27 Aprili 2008, Akon alionekana na Colby O'Donis katika Dance on Sunset. Serikali ya Sri Lanka imemuwekea ‘ngumu’ msanii Akon kwa kile kinachodaiwa kuwa aliingilia imani ya dini ya Budha kwenye Video ya wimbo wake inayokwenda kwa jina la Sexy Bith, ambayo inaonyesha mdada mrembo akicheza mbele ya sanamu hiyo.

Mamia ya waandamanaji walijitokeza na kuandamana hadi kwenye jengo la Kampuni ambayo inaandaa ziara ya mwanamuziki huyo mapema mwezi wa nane. Alipoulizwa Akon alikaririwa na jarida moja akisema kuwa hana taarifa hizo na wala hakuwaza kufanya hilo kwa dhamira.

Hii ni mara ya pili wanamuziki wa Afrika kuleta ‘Kasheshe’ huko Asia, kuna wakati mamia ya watu waliandamana huko Darusalaam – Brunei, kwa madai wimbo wa JB Mpiana wa Sultan De Brunei Kastiko. Walidema kuwa wimbo huo umemkashifu Sultani wao kwa vile umemtaja na wanadada wanacheza nusu uchi.

Aidha Akon analo Shirika lake la kutoa msaada kwa watoto wasiojiweza barani Afrika liitwalo Konfidence Foundation pia anamiliki mgodi wa Almasi nchini Afrika ya Kusini. Aliwahi kushiriki katika mikutano kadhaa na viongozi waandamizi ili kujadili utekelezaji wa miradi ya kuzalisha umeme mjini Kigali, Rwanda

Mikutano hiyo ilifautia baada ya Akon kuanzisha mradi wake wa “Akon Lighting Africa”. Serikali ya Rwanda inakabiliwa na matatizo ya vyanzo vyakuzalisha nguvu ya umeme ambapo imepelekea kutumia njia mbadala ya nishati ya jua ambayo itafikisha angalau asilimia 60 ya matumizi ya nishati ifikapo mwaka 2020.

Vyanzo vya habari vilifahamisha kuwa lengo la nyota huyo wa muziki mwenye asili ya Senegal ni kuchunguza maeneo mapya ya uwekezaji katika miradi ya Nishati mbadala katika nchi 14 za Afrika zilizochaguliwa. Akon hivi karibuni alifungua 'Solar Academy' nchini Mali kwa lengo la kufanya uvumbuzi wa maendeleo katika teknolojia ya Nishati ya jua kwa kuwaelimisha wahandisi ambao hushughulikia kazi ya kufikisha umeme katika maeneo ya vijijini barani Afrika.

Rapa wa miondoko ya R&B anayeongoza katika chati za juu za muziki huo duniani, alifanya ziara nchini Liberia kuweka umeme wa jua katika shule mbili za msingi katika taifa hilo la Afrika Magharibi. Nchini humo anashirikiana na Kampuni ya Bridge International Academies pamoja na ushirikiano na mashirika mengine ya Kimatifa kusimamia shule 50 nchini Liberia.

Mradi huo wa Akon utasaidia watu wengi wa bara la Afrika kuweza kuwa na umeme tofauti na sasa ambapo changamoto za ukosefu umeme umekuwa mkubwa sana.

Kila la heri Akon kukumbuka asili yako Afrika.

Mwandishi wa makala hii anapatika kwa namba 0784331200, 0713331200, 0736331200, 0784331200 na 0767331200.

ZAIDI YA MIONGO MIWILI BILA PEPE KALLE

0
0
Na Moshy Kiyungi
Siku hazigandi ilikuwa wiki, miezi, miaka hadi zaidi ya miongo miwili imepita tangu Pepe Kalle alipofariki dunia!. Maradhi ya moyo ndiyo yaliyokatisha maisha ya nguli huyo Novemba 28, 1998 akiwa na umri wa miaka 47, itatimia miaka 21 tangu aiage dunia itakaofika Novemba 28, 2019.

Wasifu wa Pepe Kalle unaonesha kuwa alizaliwa Novemba 30, 1951 katika Jiji la Kinshasa huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, akapewa jina la Kabasele Yampanya. Ukiangalia mwezi aliozaliwa na ule aliofariki dunia ni uleule Novemba!

Sifa za mwanamuziki huyo ni kwamba wakati wa uhai wake alikuwa mtunzi, mwimbaji wa muziki wa soukous, pia aliongoza kundi la wanamuziki wa bendi ya Empire Bakuba, iliyokuwa maarufu nchini humo. Pepe Kalle lilikuwa na umbo kubwa lililokuwa na uzito wa Kilo 136 na urefu wake ulikuwa Sentimeta 190 ambazo ni sawa na futi sita na inchi tatu. Alijulikana kama ‘Tembo wa Afrika’

Sauti yake ilikuwa nyembamba na nyororo, mwenye uwezo mkubwa wa kughani, alikuwa mwepesi kunengua jukwaani licha ya umbo lake hilo. Watanzania wengi tutaendelea kumkumbuka mwanamuziki huyo hususan wakati alipokuja nchini mwetu, akatikisa majiji ya Arusha, Dar es Saalam na Mbeya.

Kwenye ziara hiyo Pepe Kalle alifuatana na wanamuziki akiwemo mipiga wa gitaa la besi Gode Lofombo na waimbaji akina Papy Tax na Dilu Dilumona. Aidha alifuatana na rapa wake mahiri na kiongozi wa wanenguaji Djouna Mombafu ‘Bileku Mpasi’ na mbilikimo wawili Emoro na Jolly Bebbe.

Kwa pamoja walitoa burudani za kutosha kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam mwaka 1991. Mwaka uliofuatia wa 1992, Emoro alifariki dunia akiwa na bendi yake nje ya nchi kwa safari za kikazi ya muziki. Historia yake katika muziki inaeleza kwamba alianza muziki rasmi kutunga na kuimba akiwa katika bendi ya African Jazz, iliyokuwa ikiongozwa na Joseph Kabasele ‘Grand Kalle’.

Grand Kalle, ndiye aliyemtengeneza vilivyo Pepe Kalle kimuziki, kuafuatia uzoefu wake mkubwa katika muziki. Baadhi ya watu wamekuwa wakichangaya majina yao, kwamba Joseph Kabasele ‘Grand Kalle’ alikuwa baba wa Kabasele Yampanya Pepe Kalle’ Hao wote walikuwa ni wanamuziki mahiri wenye kupishana kwa mbali sana kwa umri.

Joseph Kabasele ‘Grand Kalle’ alizaliwa Desemba 16, 1930 mjini Matadi huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kabasele Yampanya ‘Pepe Kalle’ alizaliwa Novemba 28, 1951 jijini Kinshasa. Baada ya kujiona kuwa amekomaa, akatimka na kwenda kujiunga na bendi ya Orchestra Lipua Lipua iliyokuwa ikifadhiliwa na Kiamunagana Mateta Wanzela Mbonga ‘Verckys’.

Verckys alikuwa akimiliki bendi ya Orchestra Veve, bendi za Lipua Lipua na Orchestra Kiam, alikuwa akizifadhili. Pepe Kalle akiwa na bendi hiyo hakuchukua kipindi kirefu akafanywa kuwa mwimbaji kiongozi, akishirikiana na mwimbaji mwingine Nyboma Mwandido. Pepe Kalla safari yake katika muziki haikuishia katika bendi ya Lipua Lipua, mwaka 1973 akiwa na Dilu Dilumona na Papy Tax waliondoka katika bendi hiyo wakaenda kuunda bendi yao iliyopewa jina la Empire Bakuba.

Jina la Empire Bakuba lilitokana na mashujaa wapiganaji wa makabila ya Kongo. Katika miaka hiyo ya 1970, Empire Bakuba na Zaiko Langa Langa ndizo zilikuwa zakiwika katika jiji la Kinshasa na kujizolea umaarufu mkubwa kwa wapenzi wa muziki wa rhumba. Vibao vya Dadou cha Pepe Kalle na Sango ya Mwa ya Papy Tex, iliiweka Empire Bakuba kwenye chati na ikaanzisha mtindo wa Kwasa kwasa.

Yalipofanyika maadhimisho ya miaka kumi ya bendi yao ya Empire Bakuba mwaka 1982, ilipigiwa kura na ikashinda kuwa bendi bora huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (zamani Zaire). Miaka ya 1980 Bakuba ilijizolea wapenzi na washabiki lukuki. Pepe Kalle alikishirikiana na Nyboma Mwandido kurekodi wimbo wa Moyibi mwaka 1988. Wimbo huo uliiongezea bendi hiyo umaarufu katika nchi zinazozungumza lugha ya Kifaransa huko Afrika ya Kati na Magharibi.

Album ya Roger Milla iliyokuwa ikimuenzi na kumsifia mchezaji wa mpira wa miguu Roger Milla ambaye alichezea timu yake ya Taifa ya Cameroon, akiwa na umri mkubwa kuliko wote mwaka 1990. Miaka ya 1990 Pepe Kale alitoa album zingine za Gigant Afrique Larger than Life na Cocktail.

Nyimbo zingine zilikuwa za Hidaya, Sintia, Reovisie, Guy guy na Yanga Afrika. Aliachia vibao vya La- rhumba, Don’t Cry, Yaja, Zouke Zouke Nakutuna na Pon moun Paka Buoge. Bendi ya Empire Bakuba iliwahi kufanya ziara sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi yao. Kama wanamuziki wengine, Pepe Kalle naye ailiwashirikisha wanamuziki wengine wakongwe katika tasnia ya muziki akiwemo Simaro Lutumba na Nyoka Longo.

Watanzania tutaendelea kumukumbuka Pepe Kalle ambaye alipotua Tanzania, ilitunga nyimbo kupitia lugha ya Kiswahili, za Yanga Afrika, akisifia Klabu ya Yanga iliyokuwa ikimtaja mfadhili wa klabu hiyo Abbas Gulamali, Hidaya, wimbo alioimba akilalamika kupoteza mkanda wake wa kiuno na mpenzi Bupe, aliutunga alipotoka jijini la Mbeya kufanya onyesho.

Wakati wa uhai wake Pepe Kalle alirekodi nyimbo zaidi wa 300 na kufyautua album 20 katika miongo miwili ya muziki wake. Bendi ya Empire Bakuba baada ya kifo cha kiongoizi wake Pepe Kalle kufariki dunia, haisikiki tene licha ya wanamuziki wake kuwapo.

Djouna Mombafu ‘Bileku Mpasi’ ndiye pekee aliyejikwamua kwa kuunda bendi yake ya Orchestra Big One. Hivi sasa ni gumzo katika jiji la Kinshasa, wakitamba na albamu ya Tonnerre de Brest yenye kibao kikali cha ‘6600 Volts’. Bileku Mpasi akiwa na kundi hilo, amefanikiwa kufyatua albam nyingi kwa kipindi kifupi zilizopelekea kupata mialiko lukuki nje ya nchi yao hususan za Ulaya.

Amekuwa kivutio akionekana kwenye video zake nyingi kwa kuimba na kucheza akishirikiana na wanenguaji mbirikimo, Djuma Fatembo na mwanadada Jolly Bebe. Baadhi ya album alizoachia mwanamuziki huyo ni pamoja na Moun Baka Bouger, Karachiga, Tatou, Djouna Big One 6600Volts, Cupidon Brise , Tonnere de Best Onze na nyingine nyingi.

Ikumbukwe kwamba hapa nchini msanii aliyejulikana kwa jina la Kokoriko, aliweza kuiga miondoko ya uchezaji na uvaaji wa Bileku Mpasi, akapachikwa jina la Bileku Mpasi wa Tanzania.

Mungu aiweke roho yake pahala pema peponi, Amina.

Mwandishi wa makal hii anapatikana kwa namba: 0784331200, 0767331200, 07361331200 na 0713331200.

MANAMUZIKI STEVE WONDER MLEMAVU WA MACHO ANYETAMBA USA

0
0
Na Moshy Kiyungi
Baashi watu hukata tamaa pindi wanapojikuta wamezaliwa wakiwa na ulemavu wa aina yeyote ama kupatwa na ulemavu ukubwani. Kwa upande wa Steve Wonder ni tofauti kabisa, akiwa jukwaani kamwe huwezi kubaini kwamba anayepiga muziki ni mlemavu wa macho.

Ni pande na baba lenye upenzi wa kufuga nywele ndefu ‘rasta’ aliye na sauti ya juu na nyororo. Kila umuonapo hakosi kuwa na kuwa ni miwani mieusi usoni kwake. Wasifu wa Steve Wonder unaonesha kuwa alizaliwa Mei 13, 1950 mjini Saginaw, Michigan nchini Marekani.

Jina lake halisi ni Steveland Hardaway Judkins. Muziki anaopiga unatambulika na kukubalika Kimataifa, umletea sifa tele duniani kote. Talanata za mwanamuziki huyo ni mtunzi, mwimbaji wa nyimbo na pia ni mtayarishaji muziki.

Steve ana talanta za ziada za kupiga ala tofauti zikiwemo za upigaji wa ngoma, piano, gitaa, Kongas vilevile ni maarufu kwa kupiga Kinanda na Harmonica. Amekuwa miongoni mwa wasanii wakubwa wenye mafanikio wanaojulikana katika studio maarufu ya kurekodia ya Motown.

Wonder ni mwanaharakati wa haki za binadamu wa Kimarekani, ni kielelezo tosha kwamba ulemavu si kigezo cha kubweteka katika maisha. Kupitia nyimbo zake ameweza kuwa mmoja kati ya wanamuziki matajiri duniani, licha ya kuwa ulemavu huo.

Nguli huyo amekwisha rekodi zaidi ya albamu 23 na kutoa vibao vingi vilivyo maarufu, alizotunga na kuzirekodi. Baadhi ya nyimbo zake aliwashirikisha wanamuziki wengine wenye sifa kubwa katika muziki.

Machi 26, 1985 Serikali ya Afrika Kusini ilitangaza kutopiga miziki ya Steve Wonder kwa sababu ya kitendo alichokifanya wakati akipokea tuzo ya Oscar. Steve Wonder alishinda tuzo ya Oscar katika Category ya wimbo bora wa filamu 'I Just Called To Say I Love You' ulioandikwa kwenye filamu, 'The Woman In Red'.

Katika sherehe hizo Wonder alitamka kuwa anapokea tuzo hiyo kwa Jina la Nelson Mandela. Mandela wakati huo alikuwa bado mfungwa mweusi aliyetaka kuipindua serikali ya Wazungu. Nelson alikuwa wakili pekee aliyeanza kutetea haki za watu weusi wa Afrika ya Kusini.

Katika harakati zake hizo zilipelekea kuhukumiwa kifungo cha maisha mwaka 1964, kwa mashtaka ya kutaka kupindua serikali. Mwaka 1963 Wonder alitoka na wimbo "Fingertips” sehemu ya pili, na mwaka 1966, aliachia nyimbo za "Uptight (Everything's Alright)", "Blowin' in the Wind" na "A Place in the Sun".

Mwaka 1967 alikuja na wimbo wa "I Was Made to Love Her". Steve Wonder amekwisha tunga na kuimba nyimbo nyingi ambazo orodha yake ni ndefu mno. Msomaji wa makala haya nakuomba nikujuze baadhi ya nyimbo zake za karibuni zikiwemo za "From the Bottom of My Heart", "Shelter In The Rain", na So What The Fuss"

Nyimbo hizo zikiwa ni sehemu ya juhudi za Umoja wa Mataifa, kwa kushirikiana na Wasanii wa Kimataifa katika uwanja wa muziki. Katika kusisitiza umuhimu wa furaha katika maisha ya kila siku, Steve Wonder alizindua kampeni na ombi kwa raia wa duniani kuteua wimbo au muziki unaoweza kuleta tabasamu kwa kila mtu. Kampeni hiyo ililenga kuhamasisha matumaini bora.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wakati huo Ban Kin Moon, aliteua wimbo wenye ujumbe wa amani wa Steve Wonder , ambao kwake, unasikika kama sauti za furaha katika uwepo wa makubaliano mapya juu ya malengo ya maendeleo endelevu, katika yote ajenda za viongozi wa Kimataifa zilizoandaliwa kujadiliwa.

Alishiriki kutunga na kuimba wimbo uliowajumuisha magwiji wote wa kuimba Ulimwenguni, uliopewa jina la “We are The World” . Wakati huohuo mkongwe huyo Steve Wonder, amemkaribisha mtoto wake wa tisa ndani ya familia yake baada ya mpenzi wake kujifungua mtoto wa kike waliyempa jina la Nia.

Nia ni mtoto wa pili kwa mpenzi wake huyo anayejulikana kwa jina la Tomeeka Bracy. Kwa sasa Steve Wonder ni baba wa familia ya watoto tisa kutoka kwa wanawake tofauti tofauti aliowahi kuwa nao kipindi cha nyuma.

Bravo Steve Wonder, Mungu akupe maisha marefu.

Mwandishi wa makala haya anapatikana kwa namba: 0784331200, 0713331200, 0736331200 na 0767331200.

Muhimbili yaboresha huduma za ICU kutoka vitanda 25 hadi 78

0
0
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imeongeza idadi ya vitanda katika wodi za wagonjwa wanaohitaji huduma za uangalizi maalum (ICU) kutoka 25 hadi 78 ikiwa ni sehemu ya mkakati wa hospitali wa kuboresha miundombinu ya kutoa huduma kwa wagonjwa.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Kina mama wa MNH, Dkt. Vicenti Tarimo amesema lengo la kuboresha miundombinu inayotumika kutoa huduma ni kupunguza vifo vya kina mama wanaofariki dunia kutokana na kifafa cha mimba.

“Hospitali imetengeneza chumba cha kina mama wanaohitaji huduma ya uangalizi maalum (MAICU) chenye vitanda 10, pia imeweka mashine tano za kusaidia kupumua na ultrasound. Hivi sasa, huduma hii inapatikana kwenye jengo lao ukilinganisha na zamani ambapo mama alipaswa kupelekwa ICU ya kawaida ambayo ipo umbali wa mita 150. Hali hii ya upatikanaji wa huduma ilikuwa inahatarisha uhai wa mama na mtoto. Maisha ya kina mama wengi yameokolewa kupitia MAICU,” amesema Dkt. Tarimo. 

Dkt. Tarimo amefafanua kwamba kuwapo kwa huduma ya MAICU kumesaidia  kupunguza vifo vya kina mama kutoka 125 mwaka 2017/2018 hadi kufikia vifo 86 Julai 2018 hadi Juni 2019.  

Amesema uboreshaji wa huduma MNH ni sehemu ya kutekeleza malengo ya Serikali pamoja na malengo ya milenia ya kupunguza vifo vya kina mama.

“Hatua hii inaifanya MNH kuwa Hospitali ya kwanza ya umma hapa nchini kuwa na ICU ya kina mama wajawazito wenye kuhitaji uangalizi maalumu,” amesema Dkt. Tarimo.

Dkt. Tarimo amebainisha pia MNH ina ICU ya watoto wachanga (NICU) yenye vitanda 18, PICU ya watoto wenye umri wa kuanzia mwezi yenye vitanda 12, wodi ya wagonjwa wa tiba (MICU) ambayo ina vitanda 15, wodi ya wagonjwa wa upasuaji wanaohitaji uangalizi maalum (SICU) yenye vitanda 18, wodi ya wagonjwa wanaopandikizwa figo wanaohitaji uangalizi maalum ambayo ina vitanda 5 na ICU ya kina mama wajawazito (MAICU) ambayo ina vitanda 10.

“Shirika la Afya Duniani (WHO) linazitaka Hospitali kuwa na asilimia 10 ya vitanda vya ICU. MNH ina vitanda 1,550 hivyo inatakiwa kuwapo kwa vitanda 155 vya ICU. Hivi sasa MNH ina vitanda 78 sawa na asilimia 50 ya takwa la WHO. Hizi ni jitihada kubwa za uboreshaji huduma kwa wananchi,” amesema.

Dkt. Tarimo amesema kwamba uwapo wa miundombinu ya ICU, imesadia watalaam kutoka hospitali nyingine nchini kuja kujifunza namna bora ya kuanzisha na kuendesha vyumba vya wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum kwa makundi mbalimbali.

“Baadhi ya hospitali za rufaa za mikoa zimeanza kuleta watalaam wake kujifunza jinsi ya kutoa huduma kwenye ICU. Vilevile huduma hizi zitasaidia katika utafiti wa mahitaji halisi ya huduma za ICU pamoja na gharama zake na hivyo kusaidia Wizara ya Afya na Serikali kwa ujumla katika kuweka mipango ya upanuzi wa huduma hii hapa nchini,” amesema Dkt. Tarimo.

Katika hatua nyingine, Hospitali imefanya ukarabati mkubwa katika wodi 3 hadi 6 za Mwaisela na kuweka mfumo wa oxygen pamoja na vitanda 7 kila wodi sawa na vitanda 28 vya kutoa huduma kwa wagonjwa maalum (HDU). Uboreshaji huu utawasaidia wagonjwa wa kiharusi kuonwa kitalaam zaidi na kuwa  kwenye uangalizi wa karibu ikilinganishwa na awali walikuwa wakilazwa katika wodi za kawaida.
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Kina mama wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Vicenti Tarimo akizungumza na waandishi wa habari juu ya uboreshaji wa wodi zinazolaza wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU). Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Ukunga na Uzazi wa MNH, Bi. Mugara Mahungururo akiwa kwenye mkutano leo.
Meneja wa Jengo la Wazazi namba Moja wa MNH, Suzana Ndambala akitoa ufafanuzi katika kuhusu  huduma inayopatikana katika ICU ya kina mama wajawazito (MAICU) ina vitanda 10.
 Pichani ni waandishi wa habari wakimsikiliza Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Kina mama wa MNH, Dkt. Tarimo kuhusu uboreshaji wa miundimbinu inayotumika kutoa huduma kwa wagonjwa.

TANESCO yatenga Tshs. Bilioni 400 kupeleka umeme kwenye maeneo yaliyopitiwa na miundombinu

0
0
Na Teresia Mhagama, Dodoma
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetenga kiasi cha shilingi bilioni 400 kwa ajili ya kazi ya kusambaza umeme kwenye maeneo takribani 754 yaliyopitiwa na miundombinu ya umeme lakini hayana umeme.

Hayo yalisemwa tarehe 24 Juni, 2019 jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu wakati wa Majumuisho ya Semina ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti iliyohusu utekelelezaji wa miradi ya umeme vijijini na mradi wa Kinyerezi 1 Extension (MW 185).

Semina hiyo ya siku moja ilihudhuriwa na Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt.Hamisi Mwinyimvua, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Wakili Julius Kalolo, Menejimenti ya Wizara ya Nishati, REA na TANESCO.

“TANESCO imeshajipanga kufanya kazi hiyo na Wizara inaendelea kusimamia kazi hizi za usambazaji umeme ili kuhakikisha kuwa zinafanyika kwa ufanisi na tumeshafanya vikao mara kadhaa ili na wadau wanaohusika na usambazaji umeme wakiwemo Mameneja wa TANESCO nchi nzima lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata umeme.” Alisema Naibu Waziri.

Aliongeza kuwa, katika mwaka wa Fedha unaoanza mwezi wa Saba mwaka huu, kipaumbele kitakuwa ni usambazaji umeme katika maeneo mbalimbali nchini kwani kila siku kuna ziada ya umeme ya kiasi cha megawati 250 hadi 300 kwa siku.

Aidha kuhusu usambazaji umeme katika Taasisi za umma kwenye miradi ya umeme vijijini alisema kuwa, Serikali kupitia REA na TANESCO itaweka kipaumbele cha kupeleka umeme kwenye maeneo hayo ili uwepo wa nishati kwenye vijiji hivyo uwe na tija.

Katika Semina hiyo, wajumbe hao walielezwa mafanikio mbalimbali ya usambazaji umeme vijijini ambapo ilielezwa kuwa, hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Mei, 2019, jumla ya Vijiji 7,217 kati ya Vijiji 12,268 ambayo ni asilimia 58.9 ya Vijiji vyote vimefikiwa na miundombinu ya umeme.

Pia, hadi kufikia mwezi Juni 2020 jumla ya Vijiji 10,278 sawa na asilimia 84 ya Vijiji vyote vitakuwa vimepatiwa umeme.

Kuhusu utekelezaji wa mradi wa Kinyerezi I Extension (MW 185) ilielezwa kuwa, mradi huo utakamilika mwezi Agosti mwaka huu na mkandarasi ni kampuni ya Jacobsen Electro ya Norway.

Katika Semina hayo, Wajumbe hao walitoa maoni mbalimbali yatakayoboresha Sekta ya Nishati nchini ambayo Wizara ya Nishati kupitia Taasisi zake iliahidi kuyafanyia kazi.
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, akizungumza wakati wa Majumuisho ya Semina ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti iliyohusu miradi ya umeme vijijini na Kinyerezi 1 Extension, iliyofanyika jijini Dodoma. Kushoto kwa Naibu Waziri ni, Mkurugenzi Msaidizi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Nishati, Maseke Mabiki.
 Wataalam kutoka Wizara ya Nishati, REA na TANESCO wakiwa kwenye Semina ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti iliyohusu miradi ya umeme vijijini na Kinyerezi 1 Extension, iliyofanyika jijini Dodoma.
 Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Viongozi wa Wizara ya Nishati, REA na TANESCO wakiwa kwenye Semina iliyohusu miradi ya umeme vijijini na Kinyerezi 1 Extension, iliyofanyika jijini Dodoma.
 Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani, akizungumza wakati wa Semina ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti iliyohusu miradi ya umeme vijijini na Kinyerezi 1 Extension, iliyofanyika jijini Dodoma. Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt Hamisi Mwinyimvua.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Viongozi wa Wizara ya Nishati, REA na TANESCO wakiwa kwenye Semina iliyohusu miradi ya umeme vijijini na Kinyerezi 1 Extension, iliyofanyika jijini Dodoma.

WATUMISHI WAWILI WA TERURA WA MKOA WA SONGWE WAFA AJALINI IRINGA

0
0

 Na Datus Mahendeka Polisi Iringa


Wafanyakazi wawili wa Tarura Mkoa wa Songwe wamefariki kwa ajali ya kugongana uso kwa uso na Fuso wakitokea Mkoa wa Iringa wakielekea Dodoma.

Waliofariki ni Lodrick Richard, miaka 35, kabila Mchaga mkazi wa Dar es Salaam ambaye ni dereva wa gari waliokuwa wakisafiria pamoja na Joyce Enezer, miaka 45, kabila Mchaga mkazi wa Moshi.



Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Juma Bwire amesema ajali hiyo imetokea Juni 25 majira ya saa 11:45 alfajiri. 



"Wafanyakazi hawa waliokuwa wanaenda Dodoma kikazi ambapo waliofika maeneo ya Izazi Tarafa ya Isimani wakiwa kwenye gari lenye namba za kusajili Stl 3807 aina ya Toyota Hilux mali ya Tarura walikutana na Fuso.



Kwa mujibu wa Kamanda Bwire, Fuso hilo lenye namba za usajili T 146 BAZ  mali ya Wilson Msenga lilikuwa likiendeshwa na mtu mwenye kutambuliwa kwa jina moja la Amos, likitokea Dodoma kuja Iringa.

 Ndipo waligongana uso kwa uso ambao miili yao imekabidhiwa kwa Meneja wa Tarura Manispaa ya Iringa ili kupelekwa Dodoma kwa tararibu zingine.


Aidha alitaja majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni  Ernest Mgeni, miaka 49, kabila Mkinga, Gervas Myovela, miaka 44, kabila Mhehe na Jamadin Mikata, miaka 32 wote wakazi wa Mbozi ambao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa Iringa kwa matibabu.
Alisema dereva wa Fuso anatafutwa baada ya kulimbia mara baada ya ajali hiyo, kutokana na uzembe wake wa kuhama upande wake wa barabara.


AJALI YA KUGONGANA MAGARI MAWILI IRINGA YAUA WATUMISHI WA SERIKALI AKIWEMO DEREVA WA TARURA

0
0

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

 AJALI ya kugongana kwa magari miwili ikiwemo gari la  Wakala wa Barabara Vijijini (TARURA) ambapo watu watumishi wa umma wawili wamepoteza maisha na wengine kujeruhiwa.

Akizungumzia ajali hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Juma Makanya amesema magari hayo yamegongana leo eneo la Izazi wilayani Iringa ambapo gari aina ya Toyota Hilux mali ya TARURA yenye namba STL 3807 iliyokuwa ikiendeshwa na Lodrick Richard(35) ikitokea Iringa kuelekea Dodoma imegongana na gari aina ya Mistubishi Fuso namba T 146 BAZ mali ya Wilson Msenga .

Amesema gari hiyo ilikuwa inaendeshwa na Jumadin Mikata(32) mkazi wa Mbozi na kwamba katika ajali hiyo waliopoteza maisha ni dereva wa TARURA Lodrick Ricardh pamoja na Joyce Mlay (45) wakati waliojeruhiwa ni Ernest Mgeni, Gervas Myovela na  Jumadin Mikata.

"Miili ya marehemu imekadhiwa kwa Meneja wa TARURA katika Manispaa ya Iringa na  kuelekea Dodoma tayari kwa utaratibu  wa mazishi,"amesema.

Kuhusu chanzo cha ajali hiyo amesema ni uzembe wa dereva wa Fuso kushindwa kulimudu gari lake na kusababisha kuhama upande mmoja na kugongana uso kwa uso ambaye amekimbia baada ya ajali hiyo na sasa anatafutwa.

Ametoa  mwito kwa madereva kwa kuwa makini wanapokuwa barabarani na wasijione wako peke Yao bali waheshimu na watumiaji wengine wa barabara.

MIAKA 13 YA MAPAMBANO DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA NCHINI BILA AMINA CHIFUPA

0
0
*Alionesha ujasiri wa hali ya juu kuhakikisha biashara ya dawa za kulevya nchini inakoma

*Alifariki Dunia Juni 26 ambayo ndio Siku ya Maadhimisho ya Dawa za Kulevya Duniani

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii 


JUNI 26 ya kila mwaka hufanyika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Dawa za Kulevya Duniani.

Kwa mwaka huu nchini Tanzania maadhimisho hayo yanafanyika kitaifa katika Viwanja vya Tangamano jijini Tanga na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan.

Kwa kutumia maadhimisho hayo Mamlaka ya Kudhibiti na Kupamba na Dawa za Kulevya itatumia maadhimisho hayo kuendelea kutoa elimu kuhusu madhara yatokanayo na matumizi ya dawa za kulevya.

Pia ndio kipindi ambacho Mamlaka inatumia nafasi hiyo kuelezea hatua inazochukua katika kukomesha biashara hiyo ya dawa za kulevya.

Tunafahamu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa sehemu kubwa imefanikiwa kudhibiti biashara hiyo.Kuna sababu nyingi lakini kubwa ni utayari wa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk.John Magufuli kwa kuamua biadhara ya dawa za kulevya sasa basi.

Hata hivyo wakati tunaadhimisho Siku ya Dawa za Kulevya Duniani, hakika tunakumbuka mchango mkubwa wa aliyekuwa Mbunge Amina Chifupa Mpakanjia ambaye enzi za uhai wake alisimama kidete kuhakikisha anapiga vita biashara ya dawa hizo nchini kwetu.

Amina Chifupa kwasababu alijitoa mhanga licha ya kuwa na umri mdogo na katika Bunge la mwaka 2005 lakini alionesha namna anavyochukizwa na biashara ya dawa za kulevya.Hata hivyo wakati Jumanne ya Juni 26 mwaka huu wakati tuaadhimisha Siku ya Dawa za Kulevya, pia tunaadhimisha miaka 13 tangu kufarki kwa Amina Chifupa. Alifariki Dunia Juni 26 mwaka 2007.

Kwa lugha nyingine Amina Chifupa alifariki Dunia ikiwa ndio siku ya Maadhimisho ya Siku ya Dawa za Kulevya. Binafsi naamini kuna siri kubwa hapa ambayo Mwenyezi Mungu ameificha kuhusu Amina Chifupa.Kama ambavyo nimeeleza enzi za uhai wake alisimama imara kukemea dawa za kulevya lakini kifo chkake kikawa ndio tarehe ya Siku ya Dawa za Kulevya.

Hivyo wakati Juni 26 tunaadhimisha Siku ya Dawa za Kulevya Duniani , tunayo nafasi ya kukumbuka mchango wa Amina Chifupa.Tunafahamu ni miaka 13 sasa mapambano ya dawa za kulevya yanaendelea bila uwepo wake.

Hata hivyo naomba nimwambie Amina Chifupa huko aliko kwamba sauti ambayo aliipaza miaka 13 iliyopita kuhusu biashara ya dawa za kulevya na madhara yake imepata Mamlaka sahihi ya kuisemea na hakika kwa sasa hali ni nzuri kwa kiwango kikubwa.Lala Amina Chifupa kwani Watanzania wanaendelea pale ulipoishia.Tunakuezi kwa vitendo.

Kwa kukumbusha tu Juni 26 ya mwaka 2007, ilikuwa hivi ...."Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na mumewe Mohamed Mpakanjia zinasema Mheshimiwa Amina Chifupa- Mpakanjia aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es Salaam amefariki dunia majira ya saa tatu kasorobo - Juni 26, 2007...."

Ndio ilikuwa habari kuu iliyotawala katika vyombo vyote vya habari nchini na kuitikisa Tanzania na kusababisha Watanzania wengi kutoamini amini macho na masikio yao wakati TV, Magazeti, Redio na mitandao vilipokuwa vikitangaza habari hiyo ya kusikitisha na kustua ya kufariki dunia kwa Amina Chifupa.

Amina Chifupa, aliyekuwa mtangazaji maarufu na mahiri sana wa kituo redio cha Clouds 88.5FM, hasa kwa vipindi vyake vya "Chei Chei Shangazi" na "Afrika Bambaataa", aliingia bungeni baada ya kushinda nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 kupitia tiketi ya Umoja wa Vijana wa CCM. 

Katika kipindi chake cha kifupi cha takribani miaka miwili Bungeni, alijizolea umaarufu mkubwa kutokana na hoja zake nzito sio tu za kutetea maslahi ya vijana na kukemea rushwa, bali pia kwa kuamua 'kumshika nyati mapembe' kwa kupambana na janga la dawa za kulevya kwa nguvu zake zote. 

Tunaweza sema kwa kujiamini hadi sasa hajatokea tena mbunge aliye shupavu kama Amina Chifupa katika kukemea na kusema kwa sauti kuhusu janga hilo la Dawa zyeye wa aliyekemea na kusema kwa sauti janga hilo kwa Taifa.

Kwa bahati mbaya Amina Chifupa aliaga dunia Siku ya Kilele cha Maadhimisho ya Kupambana na Madawa ya Kulevya Duniani, Juni 26. Hivyo ndio tunavyoweza kueleza wakati Tanzania inaadhimisha siku hiyo , inaadhimishwa bila uwepo wake.

Nachoweza kueleza ni hivi wakati tunaadhimisha Siku ya Dawa za Kulevya Dunani , tufahamu inakwenda sambamba na kabisa na Siku aliyofariki Dunia Amia Chifupa aliaga Dunia.Ni vema tukakumbuka machache kutoka kwake kuhusu harakati zake za kupambana na dawa za kulevya nchini.

Daima atakumbukwa kwa kujitolea kupambana na matajiri waliokuwa wanaofadhili au kujihusisha na uingizaji wa dawa za kulevya nchini.Alikuwa ni mbunge mdogo zaidi katika historia ya chombo hicho cha kutunga sheria na kupitisha bajeti ya nchi yetu kwa kipidi hicho.

Pia atakumbukwa kwa namna alivyosimama kidete na kutamka bayana angewataja hadharani vigogo wote wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na alienda mbali zaidi kwa kutamka hata kama angekuwa mume wake anahusika naye angemtaja. Hakika Amina Chifupa alikuwa jasiri kiasi hata alifikia uamuzi wa kuwasilisha majina ya vigogo waliokuwa wakifanya biashara hiyo ya "Unga" katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam.

Aliamua kujitoa mhanga kutetea kizazi cha vijana kinachoteketea kwa kutumia dawa za kulevya ilihali waoingiza wanazidi kuwa matajiri tishio na baadhi yao wana nguvu ya ushawishi katika nyanja mbalimbali serikalini.

Ukweli Amina alikuwa ni hazina kwa Taifa na mfano kwa vijana wenye umri mdogo kama wake kwamba inawezekana kujitoa pasipo woga kulitetea taifa na kuwaweka wazi wote wanaotumia utajiri wao, vyeo vyao kufanya au kuwezesha uhalifu hususani katika suala zima la dawa za kulevya. 

Hata hivyo cha kusikitisha ndoto yake hiyo na nyinginezo zilikatizwa ghafla na mauti yaliyomkuta saa tatu za usiku wa Juni 26, mwaka 2007 ambayo ilikuwa ni siku ya Jumanne katika hospitali kuu ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es salaam.

Wakati tunaadhimisha Siku ya Dawa za Kulevya, naomba kutumia nafasi hii kukusha historia ya Amina Chifupa kwa kueleza kuwa 

alizaliwa Mei 20, mwaka 1981 jijini Dar es Salaam, na alisoma Shule ya Msingi Ushindi, Mikocheni, Dar (1988-1994) kabla ya kujiunga na masomo ya sekondari ya kidato cha kwanza hadi cha nne katika Shule ya Wasichana ya Kisutu, Dar (1995-1998). 

Elimu yake ya Sekondari aliipata katika Shule ya Makongo (1999-2001) kabla ya kujiunga na Chuo cha Uandishi wa Habari cha Royal (2001-2003) ambako alifuzu Diploma ya Uandishi wa Habari.

Ilipofika mwaka 1999 alianza kazi ya utangazaji wa kituo cha redio cha Clouds FM cha jijini Dar na aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Mama Shughuli. 

Katika medani ya siasa alikuwa kada wa CCM, Kamanda wa CCM wa Umoja wa Vijana katika tawi la Mikocheni A jijini Dar, Katibu wa Kamati ya Uchumi ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoa wa Dar, Mama Mlezi wa UVCCM na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) matawi ya Bunju na Mbagala.

Mwaka 2005 aliteuliwa kuwa mbunge akiwakilisha kundi la vijana kupitia CCM ambako alidumu na cheo hicho kwa muda mfupi hadi mauti yalipomkuta Juni 26, 2007.

Amina Chifupa alizikwa Juni 28, 2007 kijijini Lupembe katika Wilaya ya Njombe mkoa wa Iringa (sasa ni mkoa a Njombe) karibu kabisa na eneo alilokuwa akiishi bibi yake. Mazishi yake yalihudhuriwa na watu wengi maarufu wakiiongozwa na aliyekuwa Spika wa Bunge wa wakati huo Samwel Sita, ambaye pia ni marehemu.

Miaka mitatu baadaye, aliyekuwa mume wa marehemu Amina Chifupa, Mohamed 'Medi' Mpakanjia, naye alifariki dunia. Wawili hao walijaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume anayeitwa Abdulrahman anayejulikana zaidi kama Rahman.

Baba mzazi wa marehemu Amina Chifupa, Mzee Hamisi Chifupa aalifariki dunia usiku wa kuamkia Mei 27, 2017 nyumbani kwa mwanaye wa kike, Upanga, jijini Dar es Salaam.

Mola aiweka mahali pema peponi roho ya marehemu Amina Chifupa wa Mpakanjia. WOTE NA TUSEME.... AMINA!

Pia Michuzi Blog na Michuzi TV inaungana na Watanzania wengine kuendelea kukuombea kwa Mwenyezi Mungu aiweke roho marehemu Amina Chifupa Mahala Pema ,Peponi .AMINA.

RAIS SHEIN AHUDHURIA MAADHIMISHO YA MIAKA 107 YA SKAUTI YAADHIMISHWA VIWANJA VYA MAISARA SULEIMAN ZANZIBAR

0
0
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Ali Mohamed Shein, akifungwa kiskafu na Vijana wa Skauti kushoto Halima Ali Makame na kulia Lutfia Juma Ali, baada ya kuwasili katika viwanja vya Mpira vya Maisara Suleiman Zanzibar kuhudhuria hafla ya  Maadhimisho ya Miaka 107 ya Skatu Tanzania.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Kambi ya Mfano ya Skauti wakati wa maadhimisho ya Miaka 1-7 ya Skauti Tanzania ziulizofanyika katika viwanja vya Maisara Suluiman, akimsikiliza Kijana Jaffar Mohammed, akitowa maelezo ya michuro ya ramani ya Tanzania.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Ndg. Alois Zengwe akitowa maelezo ya Kambi ya Mfano ya Skauti wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Skauti kutimiza Miaka 107 Tanzania tangu kuazishwa kwake kushoto Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Alali Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akielekea katika eneo lililotayarishwa kwa ajili ya kuyapokea maandamano ya Vijana wa Skauti Tanzania katika viwanja vya Maisa Suleiman Zanzibar kushoto Mkuu wa Skauti Tanzania Mhe. Mwatumu Mahiza na Kiongozi wa Skauti Bi. Amina Clement Edward na kulia Makamu wa Rais wa Chama cha Skauti na Waziri wa Elimu na Mafuzo ya Amali Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma.
 VIJANA wa Skauti Tanzania wakipita kwa ukakamavu kwa mgeni Raism Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akipokea maandamano ya Maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania yalioadhimishwa Kitaifa Zanzibar katika viwanja vya Maisara Suleiman

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Ali Mohamed Shein, akipokea gwaride Maalum la Vijana wa Skauti Tanzania kuadhimisha Miaka 107 zilizofanyika katika viwanja vya Maisa Suleiman Zanzibar.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi wa Meza Kuu wakiwa wamesimama wakati ukipigwa wimbo wa Taifa.
 VIJANA wa Skauti wakitowa heshima wakati ukipigwa wimbo wa Taifa
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla ya maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania yaliofanyika kataifa Zanzibar katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.
 SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zuberia Ali Maulid, Rais Mstaaf wa Tanzania Mhe. Ali Hassan Mwinyi, Makamu wa Rais Mstaaf wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed GharibBilal na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, wakifuatilia hutuba ya mgeni rasmin Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia hayuko pichani.
MKUU wa Skauti Tanzania Mhe Mwamtumu Mahiza akizungumza na kutowa maelezo ya Maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.
 MKURUGENZI wa Skauti Kanda ya Afrika Ndg. Fedrick Kamakama  akizungumza na kutowa Salamu za Skauti Duniani wakati wa maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania zilizofanyika Kitaifa katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.
  MAKAMU wa Rais wa Chama Cha Skauti Tanzania, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma ,akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmin kuhutubia hadhara hiyo ya Maadhimisho ya Miaka 107 ya Sakauti Tanzania zilizofanyika Kitaifa Zanzibar katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.

 WAGENI Waalikwa na Vijana wa Skauti Tanzania wakifuatilia hutuba ya mgeni rasmin Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla ya maadhimisho ya Miaka 107 ya Skauti Tanzania.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimvisha Nishani Mlezi wa Skauti Tanzania Rais Mstaaf wa Tanzania Mhe. Ali Hassan Mwinyi, wakati wa hafla hiyo ya maadhimisho ya Miaka 107 ya Sjauti Tanzania, zilizofanyika katika viwanja vya Maisara Suleiman Zanzibar.(Picha na Ikulu)

TASAC:Mafunzo kwa wataalam wa vyombo vya usafiri wa Baharini na Maziwa yanahitajika.

0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Usalama wa vyombo vya usafirii wa Baharini na Maziwa unahitaji kuwa na Mafunzo ya mara kwa mara kwa ajili ya vyombo hivyo kwa wataalam ikiwa ni pamoja na kujifunza mbinu mbalimbali katika uokoaji pindi linapotokea kuweza kukabiliana.

Hayo ameyasema  Mkurugenzi wa Utawala na Rasilmali Watu wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji kwa  Zanzibar Rajab Yakub Uweja wakati akifunga Mafunzo ya  Wataalam wa Usalama na Uokoaji katika usafiri wa Baharini ulioshirikisha nchi Tisa uliofanyika Jijini Dar es Salaam.
Uweja amesema kuwa mafunzo ya usalama katika bahari na maziwa yanahitajika kutokana vyombo vya majini ni muhimu katika sekta ya usafirishaji  nchini.

Amesema kuwa Tanzania bado tuko vizuri lakini mafunzo bado ya yanahitajika kwa wataalam wa usalama na uokoaji.

Aidha amesema kuwa Shirika la Usafiri wa Meli Duniani (IMO) kutokana na utaratibu  wake limeonelea kuja kufanya mafunzo Tanzania kwa kutambua ni moja ya nchi inayopokea Meli  nyingi.

 Nae Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Meli Nchini (TASAC) Emmanuel Ndomba amesema usalama makosa yanayofanyika katika bahari asilimia 80 ni makosa ya kibinadamu hivyo wamiliki wa meli na vyombo vingine vya majini wanahitaji mafunzo.
Amesema kuwa Tanzania iko vizuri katika udhibiti wa usimamizi katika sekta ya usafirishaji wa Baharini na  Maziwa. 
 Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Stella Katondo akizungumza na waandishi wa habari namna Wizara hiyo walivyojipanga katika udhibiti wa  sekta ya usafirishaji katika mafunzo ya wataalam wa vyombo vya usafiri Baharini yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Wakala wa Meli Nchini (TASAC) Emmanuel Ndomba akizungumza kuhusiana mafunzo wataalam wa vyombo vya usafiri Baharini yaliyoshirikisha nchi Tisa yaliofanyika jijini Dar Salaam.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdullah Ulega akizungumza wakati akifungua mafunzo ya Watumishi wa Taasisi wa Sekta ya Uvuvi nchini Somalia wanaopata mafunzo katika Wakala ya Vyuo vya Uvuvi nchini (FETA) Mbegani wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
 Mkurugenzi wa Utawala na Rasilmali Watu wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Rajab Yakub Uweja akizungumza wakati akifunga Mafunzo ya Usalama na Uokoaji kwa wataalam wa vyombo vya usafiri Baharini yaliyoshirikisha nchi Tisa yalifanyika Jijini Dar es Salaam.



 Wadau wa Mafunzo ya Usalama na Uokoaji wa vyombo vya usafiri Baharini wakisiliza mada.

ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 30 KUSHINDANIWA SIMIYU JAMBO FESTIVAL 2019

0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu
Tamasha kubwa la michezo ambalo hufanyika kila mwaka Mkoani Simiyu (Simiyu Jambo Festival) linatarajiwa kufanyika Juni 30, mwaka huu katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi huku takribani shilingi milioni 32 zikishindaniwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 25, Mratibu wa tamasha hilo Bi. Zena Mchujuko amesema Mgeni rasmi katika Tamasha hili anatarajiwa kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson.

Amesema katika Tamasha hilo kutafanyika mashindano ya mbio za baiskeli wanaume na wanawake, mbio fupi kilometa tano wanaume na wanawake na mashindano ya mdahalo kwa wanafunzi wa shule za sekondari.

“Jumla ya shilingi milioni 32 zitashindaniwa kwa michezo yote, mshindi wa kwanza mbio za baiskeli kwa wanaume atapata 1,000,000, Wanawake 700, 000, walemavu 500, 000 na tutatoa zawadi mpaka kwa mshindi wa 25; ngoma za asili mshindi atapata 1,000,000” alisema Bi. Zena

Aidha, amesema fomu za ushiriki zinapatikana kataika ofisi ya Chama cha Baiskeli Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi na katika Tovuti: www.simiyutalent.co.tz kwa gharama za shilingi elfu tano(5000) kwa mashindano ya baiskeli na shilingi elfu mbili (2000) kwa ajili ya mashindano ya mbio fupi.

Katika hatua nyingine Bi. Mchujuko amesema kupitia Tamasha la Simiyu Jambo Festival jamii ya watu wa Simiyu itapata ujumbe wa kupinga mimba za utotoni jambo litakalopelekea watoto wa kike waweze kutimiza ndoto zao kupitia Kauli Mbiu ya Tamasha ambayo ni :-WEZESHA MTOTO WA KIKE ATIMIZE NDOTO ZAKE, INAWEZEKANA KUZUIA MIMBA KATIKA UMRI MDOGO”

Mratibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu Duniani(UNFPA) Mkoa wa Simiyu, Dkt. Amir Batenga amesema shirika hilo limekuwa likishirikiana na Serikali katika jitihada za kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi, ambapo waathirika wakubwa ni wasichana wenye umri mdogo, hivyo anaamini kupitia Tamasha hilo wananchi watapata ujumbe mahususi wa kukabiliana na mimba katika umri mdogo.

Naye Katibu wa Chama cha Mbio za Baiskeli Mkoa wa Simiyu, Bw, Samwel Richard washiriki takribani 260 kutoka mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Mara, Mwanza, Geita na Kagera wanatarajia kushirikia mashindano ya baiskeli, huku akiwahakikishia wananchi kuwa wachezaji wao wamejiandaa vizuri na wamekuwa kambi kwa takribani wiki mbili.

Kwa upande wake Kiongozi wa Ngoma za Asili Mkoa wa Simiyu, Bw. Buhimila Shala amesema kupitia ngoma za wagika na wagalu watatoa ujumbe uliobebwa na Kauli mbiu ya Tamasha kwa lengo la kuwaokoa wasichana kupata mimba katika umri mdogo.

Tamasha la Simiyu Festival mwaka 2019 limedhaminiwa na Jambo Food Products Company, Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani-UNFPA, NGM Gold Mine Limited, NGS Petroleum, Alliance Ginneries Limited, Busega Mazao Limited, Maswa Standard Chalk, Ms Hotel na Vetreces Company Limited.
 Mratibu wa Tamasha la Simiyu Jambo Festival Bi. Zena Mchujuko(kulia) akizungumza na waandishi wa habari na kutoa taarifa ya tamasha hilo ambalo linatarajiwa kufanyika Juni 30, 2019 Mjini Bariadi.
 Mratibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu Duniani(UNFPA) Mkoa wa Simiyu, Dkt. Amir Batenga(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari na kutoa taarifa ya namna Shirika hilo liakavyotumia Tamasha la Simiyu Jambo Festival kupeleka ujumbe wa Kupinga mimba za utotoni tamasha ambalo linatarajiwa kufanyika Juni 30, 2019 Mjini Bariadi.
 Kiongozi wa Ngoma za Asili, Bw. Buhimila Shala (kushoto) akizungumza katika Mkutano wa Waandishi wa Habari na kueleza namna ngoma za asili zitakavyopamba Tamasha la Simyu Jambo Festival ambalo linatarajiwa kufanyika Juni 30, 2019.
Katibu wa Chama cha Baiskeli Mkoa wa Simiyu, Bw. Samwel Richard(kulia) akizungumza na waandishi wa habari juu ya namna chama hicho kilivyojiandaa na mashindano ya baiskeli katika Tamasha la Simiyu Jambo Festival, linalotarajiwa kufanyika Juni 30, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI AZINDUA GHALA NA MITAMBO YA GESI YA KAMPUNI YA TAIFA GAS TANZANIA LIMITED KIGAMBONI, VIJIBWENI, JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Taifa Gas Tanzania Limited Bw. Rostam Aziz alipowasili kuzindua Ghala na Mitambo ya Gesi ya LPG vya Kampuni hiyo huko Vijibweni, Kigamboni, jijini Dar es salam leo Juni 25, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitembezwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Taifa Gas Tanzania Limited Bw. Rostam Aziz kuangalia Ghala na Mitambo ya Gesi ya LPG vya Kampuni hiyo kabla ya kuvizindua huko Vijibweni, Kigamboni, jijini Dar es salam leo Juni 25, 2019.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa uzinduzi wa Ghala na Mitambo ya kuchakata Gesi ya LPG vya Kampuni ya Taifa Gas Tanzania huko Vijibweni, Kigamboni, jijini Dar es salam leo Juni 25, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Taifa Gas Tanzania Limited Bw. Rostam Aziz na viongozi wengine wakikata utepe kuashiria kuzinduliwa kwa Ghala na Mitambo ya Gesi ya LPG vya Kampuni hiyo huko Vijibweni, Kigamboni, jijini Dar es salam leo Juni 25, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Taifa Gas Tanzania Limited Bw. Rostam Aziz baada ya kuzindua Ghala na Mitambo ya Gesi ya LPG vya Kampuni hiyo huko Vijibweni, Kigamboni, jijini Dar es salam leo Juni 25, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Taifa Gas Tanzania Limited Bw. Rostam Aziz na na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Bw. Hamisi Ramadhani wakisiliza maelezo ya namna mitambo ya kuchakata gesi inavyofanya kazi wakati wa uzinduzi wa Ghala na Mitambo ya Gesi ya LPG vya Kampuni hiyo huko Vijibweni, Kigamboni, jijini Dar es salam leo Juni 25, 2019. PICHA NA IKULU
Viewing all 109609 articles
Browse latest View live




Latest Images