Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110095 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AISIFU NMB KWA KUIUNGANISHA JAMII KWA HUDUMA ZAKE

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya soka ya Bunge, Cosato Chumi baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa 5-3 dhidi ya timu ya NMB katika Bonanza la Benki ya NMB na Wabunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya Mpira wa Kikapu ya Benki ya NMB – Danford Kisinda baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa vikapu 54-52 dhidi ya timu ya mpira wa Kikapu ya Bunge katika mechi ya Bonanza la Benki ya NMB na Wabunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania – Tulia Ackson na Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya NMB wakiwa pamoja na timu ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wakifurahia ushindi wa timu za bunge kwenye Bonanza la michezo la NMB na Bunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.

Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya NMB akishangilia ushindi wa Mpira wa Kikapu baada ya kuwashinda timu ya Bunge kwa Vikapu 54 kwa 52 kwenye Bonanza la michezo la NMB na Bunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.
 
……………………
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesifu juhudi za Benki ya NMB kwenye kuunganisha jamii kupitia huduma bora za kibenki, matukio ya michezo na hata misaada mbalimbali nia ikiwa kuona jamii ya kitanzania inashiriki kikamilifu kwenye ujenzi wa Taifa. 

Alitoa kauli hiyo juzi jijini Dodoma kwenye Bonanza la michezo lililowashirikisha wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wafanyakazi wa Benki ya NMB. Akizungumzia kuhusu utendaji wa benki ya NMB, amesema imekuwa ikishirikiana na Serikali kuwaelimisha wakulima umuhimu wa kufungua akaunti na kujiwekea akiba. 

“Benki ya NMB ni benki pekee iliyomudu kufungua matawi hadi maeneo ya vijijini, hivyo kurahisishha upatikanaji wa huduma kwa watumishi na wananchi waishio maeneo hayo.” Amesema ni muhimu kwa watumishi kushiriki katika michezo mbalimbali kwa kuwa inaimarisha afya pamoja na kudumisha mshikamano. 

Michezo iliyochezwa katika bonanza hilo ni mpira wa miguu ambapo timu ya Bunge ilishinda baada ya kuifunga timu ya benki ya NMB magoli matano kwa matatu. Kwa upande wa mchezo wa mpira wa pete timu ya Bunge iliibuka na ushindi baada ya kuifunga timu ya NMB magoli 25 kwa 18, huku katika mchezo wa mpira wa kikapu timu ya NMB ilishinda baada ya kuifunga Bunge vikapu 54 kwa 52. 


Katika mchezo wa kuvuta kamba timu ya Wabunge Wanawake na Wanaume waliibuka na ushindi baada ya kuzishinda timu za NMB.

RC MTAKA AWATAKA VIONGOZI WA SERIKALI SIMIYU KUISAIDIA, KUILEA SEKTA BINAFSI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na viongozi na watendaji wa Serikali na Sekta binafsi katika Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu ambayo imefanyika mjini Bariadi. 
Mkurugenzi wa Bodi ya Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo nchini(TCCIA), Dkt. Meshack Kulwa akifafanua jambo katika Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi. 
Baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali na sekta binafsi wakifuatilia Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi. 
Baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali na sekta binafsi wakifuatilia Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu iliyofanyika mjini Bariadi 
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Shule ya biashara, Khalidi Swabiri (mwezeshaji) akitoa mada katika Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu, iliyofanyika mwishoni mwa wiki Mjini Bariadi. 
Meneja wa Mamlaka ya Mapato(TRA) Mkoa wa Simiyu, Bw. Charles Mkumbwa akifafanua jambo katika Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu iliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Bariadi. 
Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi akichangia hoja katika Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu iliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Bariadi. 
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Shule ya biashara, Khalidi Swabiri (mwezeshaji) akitoa mada katika Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu, iliyofanyika mwishoni mwa wiki Mjini Bariadi. 
…………………. 

Na Stella Kalinga, Simiyu 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewataka viongozi wa Serikali mkoani Simiyu kuisaidia na kuilea Sekta Binafsi ili iendelee kukua na wahakikishe kuwa maamuzi wanayofanya hayawi vikwazo katika mazingira ya biashara na uwekezaji. 

Mtaka ameyasema hayo wakati akifungua Warsha ya Utetezi na majadiliano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa viongozi wa Serikali na sekta binafsi mkoani Simiyu ambayo imefanyika mjini Bariadi. 
Amesema viongozi wa Serikali mkoani humo wanapofanya maamuzi katika biashara za watu ni lazima wawe na nia ya dhati ya kuona sekta binafsi inakuwa, ili maamuzi ya viongozi hao yasiwe vikwazo kwa ukuaji wa Sekta binafsi na mazingira ya biashara na uwekezaji. 

“Sekta binafsi ni lazima ilelewe anaeilea ni Serikali, Sekta binafsi ni lazima ilindwe anayeilinda ni Serikali,Sekta binafsi ni lazima isimamiwe anayeisimamia ni Serikali na Serikali inaisimamia kwa maana ya kuilea ili ifanye vizuri” alisema Mtaka. 

Aidha, ametoa wito kwa Wakuu wa Wilaya mkoani Simiyu kuendeleza utaratibu wa kukutana na wafanyabishara ili kupata nafasi ya kujadiliana juu ya fursa mbalimbali za uwekezaji na namna ya kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji, huku akisisitiza pia kuendelea kufanyika kwa mabaraza ya biashara ya wilaya. 

Katibu wa Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo nchini(TCCIA) Mkoa wa Simiyu, Bi. Christina Matulanya amesema ili kuboresha mazingira ya biashara Serikali inapaswa kuendelea kuvutia wawekezaji na kusimamia sheria, sera na kanuni zisipindishwe, huku akiupongeza Mkoa wa Simiyu kwa kuandaa mwongozo wa uwekezaji. 

Katika hatua nyingine Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Simiyu, Bw. Charles Mkumbwa ametoa wito kwa wafanyabiashara kuwa wazalendo, kutoa risiti ipasavyo, kufuata sheria za kodi na akaahidi kuwapa ushirikiano wafanyabiashara kila wanapohitaji. 

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Shule ya biashara, Khalidi Swabiri ambaye alikuwa mwezeshaji wa warsha hii amesema ni vema mabaraza ya biashara ya wilaya yakafanyika ili wafanyabiashara wapate muda wa kukutana na viongozi wa Serikali, sekta binafsi kwa lengo la kujadili changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika mazingira ya biashara na uwekezaji na ufumbuzi wake. 

Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo nchini(TCCIA), Dkt. Meshack Kulwa amesema pamoja na kuomba mabaraza ya biashara ya wilaya yafanye kazi, ameomba TCCIA mkoani Simiyu itafute viongozi watakaofanya kazi kwa kujituma ili TCCIA Simiyu iweze kuwa imara

Wakazi wa Makete watakiwa kuanzisha Kampuni ya Uwekezaji-TIC

$
0
0
Na Grace Semfuko, MAELEZO. 

Wito umetolewa kwa wakazi wa Makete waishio Jijini Dar es Salaam, kuanzisha Kampuni ya Uwekezaji na Mfuko wa Maendeleo wa Wilaya hiyo utakaoangalia fursa za kiuchumi zinazopatikana Makete, Mkoani Njombe, ili kukuza pato lao na Taifa kwa ujumla. 

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Geoffrey Mwambe, wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Wanachama wa Chama cha Maendeleo Makete (MDA) uliofanyika Jijini Dar es Salaam. 

Bwana Mwambe akasema, fursa ya kuanzisha kampuni na mfuko utawawezesha wakazi hao kununua hisa na umiliki pamoja na kuwapa fursa za kutafuta masoko ya bidhaa na huduma zitakazotolewa ikiwa ni sehemu ya kuitangaza Wilaya hiyo kwa wawekezaji wengine. 

“Makete mna fursa nyingi za uwekezaji, kuna kilimo cha ngano, pareto, viazi, matunda na mbogamboga, pia mnayo madini mbalimbali, mnao utalii wa ndege na maua kule kwenye hifadhi ya Kituro, ndugu zangu, uwekezaji katika sekta hizo inawezekana kabisa, pia mnayo ardhi ya kutosha, ni muhimu muwekeze nyumbani” alisema Mwambe. 

Mwambe aliwataka wakazi hao kushirikiana na kuongeza nguvu katika kutangaza fursa na vivutio vya utalii vilivyopo katika Wilaya hiyo ambayo imebarikiwa kuwa na hali nzuri ya hewa ya kuweza kuzalisha mazao mbalimbali ya chakula na biashara. 

“Ndugu zangu uwekezaji unawezekana sana Makete, mna ardhi yenye rutuba,mna hali nzuri ya hewa, umoja wenu ni bora zaidi kuliko utengano, nawaomba sana muungane na muanzishe Mfuko na Kampuni ya Wanamakete vitakayokuwa na malengo ya kuiletea maendeleo Wilaya ya yenu”alisema Mwambe. 

Aidha aliongeza Wilaya hiyo inao uwezo mkubwa wa kuzalisha ngano lakini bidhaa hiyo kwa asilimia kubwa inaagizwa kutoka nje ya nchi na kuwataka ikutafakari hilo ili kuzalisha ngano kwa wingi. 

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Makete, Bw. Burton Sinene alisema kwa sasa Wilaya hiyo inahitaji wawekezaji katika kiwanda cha kutengeneza njiti za meno (bamboo toothpick) kutokana na kuwepo kwa zao la mianzi, bidhaa ambayo kwa kiwango kikubwa inaagizwa nje ya nchi kwa ajili ya matumizi ya mezani wakati wa kula. 

Katika majadiliano ya kikao hicho wakazi hao waliiomba Serikali izidi kuimarisha miundombinu ya barabara ili kuweza kusafirisha mazao toka mashambani kwenda kwenye masoko mbalimbali, suala ambalo pia litawavutia wawekezaji wengi zaidi.

UJIO WA MAMEYA NCHINI, MWITA ATANGAZA NEEMA KWA WATANZANIA

$
0
0
* Awataka wafanyabiashara kutumia fursa hiyo kujitangaza zaidi.

Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
MEYA wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema kuwa siku ya kesho June 25 wanatarajia kupokea ugeni mkubwa wa Mameya wakiongozwa na mameya kutoka katika majiji ya Texas na Albama ya nchini Marekani ikiwa ni maandalizi ya mkutano mkuu utakaofanyika mwezi Desemba mwaka huu, ambapo mkutano huo utawakutanisha mameya wenye asili ya Afrika "Black Mayors" kote duniani.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mwita amesema kuwa mameya hao watakuwa nchini kwa siku 2, kuanzia Juni 25 na 26 na wataelekea Zanzibar na baadaye kurejea nchini kwa kufanya shughuli nyingine ikiwemo utalii.

Akieleza malengo ya ujio huo Mwita amesema kuwa ni kuhoji na kutaka kujua kama nchi itaweza kuwatambua kwa uraia pacha au namna yoyote ile kwa malengo ya kuwavutia wawe wawekezaji  na kuhamishia mitaji yao katika bara la Afrika.

 Pia amesema kuwa ugeni huo unakuja kwa malengo ya kuendeleza
 mahusiano bora na bara la Afrika na hiyo ni baada wamarekani hao wenye asili ya Uafrika "Wamarekani weusi"  kupoteza makazi yao na wazazi wao kuchukuliwa kama watumwa katika miaka ya 1619.

Pia amesema kuwa mameya hao wamekuja kufanya utalii ikiwemo kutembelea  Zanzibar ambako kunafahamika sana kwa usafirishaji wa watumwa.

Vilevile amesema kuwa ujio huo unafaida kwa Watanzania hasa katika kutangaza biashara za hoteli ambako inategemewa fedha nyingi zitaingizwa na amewataka watanzania kutumia nafasi hiyo adhimu kwa kutangaza biashara zao.

Mkutano mkuu wa mameya utafanyika mwezi Disemba mwaka huu ambao mameya wenye asili ya waafrika "The World Black Mayors conference" duniani kote watakutana nchini.

SERIKALI YAPELEKA BIL 8 JIJI LA TANGA KUTEKELEZA MIRADI YA AFYA NA ELIMU

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia akifuatilia hoja mbalimbali kwenye kikoa cha baraza la madiwani maalum la kujibu hoja za mkaguzi wa serikali CAG la Jiji hilo kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Selebosi
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Selebosi akizungumza wakati wa kikao hicho kushoto ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji akifuatiwa na Naibu Meya wa Jiji hilo Mohamed Haniu
Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji akizungumza wakati wa kikao hicho kulia ni Mstahiki Meya wa Jiji hilo Alhaji Mustapha Selebosi
DIWANI wa Kata ya Msambweni Jijini Tanga (CUF) Abdurahamani Mussa akichangia wakati wa kikao hicho
Sehemu ya Madiwani wa Jiji la Tanga wakifuatilia kikao hicho 


Serikali imepeleka kiasi cha sh Bil 8 kwa Halimashauri ya Jiji la Tanga kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Maendeleo kwenye sekta za Afya na elimu.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigela wakati wa baraza la madiwani maalum la kujibu hoja za mkaguzi wa serikali CAG la Jiji Hilo lilofanyika hapo Jana.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano imejipanga kuhakikisha wanatekeleza miradi ya Maendeleo kwa wakati ili kumaliza kero zinazowakabili wananchi.

"Mnachotakiwa Halimashauri ni kuhakikisha fedha hizo zinatumika katika malengo yaliyokusudiwa lakini na miradi hiyo iweze kuzingatia thamani halisi ya fedha hizo"alisema RC Shigela.

Awali akisoma hoja za CAG Mwekahazina wa Jiji la Tanga Corner Sima alisema kuwa ucheleweshaji wa fedha kwa ajili yautekelezaji wa miradi ya kimkakati yamajiji nchini umesababisha kushindwa kutekelezeka .

"Ucheleweshaji wa fedha hizo ilisababishia kuibua hoja kutoka kwa CAG kwani katika sh Bil 232.5 zilizotumwa kwa ajili yamiradi tuliweza kutumia sh Bil 4.7 sawa naasilimia 2% ya fedha hizo"alisema Sima..

Hivyo ofisi ya CAG imeielekeza Halimashauri ya Jiji hilo kuwasilisha mpango kazi wa matumizi ya fedha hizo na namna ambavyo zitaweza kutumika katika kutekeleza miradi hiyo ya kimaendeleo.

Nae Mstahiki Meya wa Jiji hilo Seleboss Mustafa alisema kuwa katika mwaka huu wa fedha wamejipanga kusimamia kwa ukaribu mapato pamoja na kuibua vyanzo vipya.

Huku akitilia mkazo namna walivyojipanga kuhakikisha wanatoa mikopo yenye masharti nafuu kwa makundi maalum ya vija a ,wanawake na Walemavu walioko katika kata 21 za Jiji hilo.

"Tumekuja na hari ya kuhakikisha tunamaliza changamoto za kimaendeleo kwa wananchi wetu huku kipaumbele kikubwa ikiwa ni ukusanyaji wa mapato ili kutekeleza miradi yetu ya Maendeleo na kuwaondolea adha wananchi wetu"alisema Meya huyo.

WADAU WA HAKI JINAI WAKUTANA KWA MABORESHO JIJINI DODOMA

$
0
0
 Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Balozi Augustine Mahiga akisoma hotuba yake kabla ya kufungua kikao kazi cha Maboresho ya Mfumo wa Haki jinai.
 Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome akimkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Balozi Augustine Mahiga kufungua Kikao kazi Wakuu wa Taasisi za Haki Jinai kuhusu Maboresho ya Mfumo wa Haki Jinai kinachofanyika katika Hoteli ya St. Gasper jijini Dodoma.
 Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Maboresho ya Mfumo wa Haki Jinai wakimsikiliza mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa kikao hicho.
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Balozi Augustine Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Kikao Kazi cha Maboresho ya Mfumo wa Haki Jinai.

Maajabu ya Mdalasini na Tangawizi katika Kuondoa Kitambi

TANZANIA YAWA MWENYEJI WA MAFUNZO YA UKAGUZI WA KODI

$
0
0
 Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo akifungua rasmi mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na African Tax Administration Forum (ATAF). Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika.  
 Meneja wa Mafunzo ya Ukaguzi wa Kodi kutoka African Tax Administration Forum (ATAF) Caroline Mutayabarwa akizungumza wakati wa hafla fupi ya ufunguzi wa mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na ATAF ambapo jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika.  Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na yatamalizika tarehe 28 Juni, 2019.
 Baadhi ya Wakaguzi wa Kodi kutoka Mamlaka za Mapato Afrika wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na African Tax Administration Forum (ATAF) ambapo jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika.  Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na yatamalizika tarehe 28 Juni, 2019.
  Wakaguzi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na African Tax Administration Forum (ATAF) ambapo jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika.  Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na yatamalizika tarehe 28 Juni, 2019.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya menejimenti ya TRA, wakufunzi na wakaguzi wa kodi mara baada ya ufunguzi rasmi wa mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na ATAF ambapo jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika.  Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na yatamalizika tarehe 28 Juni, 2019. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO)

KAFULILA: NAVOTAZAMA JPM NA SAFARI YETU KUTOKA 'UCHUMI WA MISSION-TOWN' KWENDA UCHUMI HALISI

$
0
0

- Pamoja na Changamoto ipo 'hangover' ya  'mission-towns' inasumbua  bado!

Na David KAFULILA Juni23/19

Nimewiwa  kuweka  neno katika  katika kipindi hiki cha mjadala huu wa Bajeti kutokana  na ukweli kwamba hii ni Bajeti ya nne kati ya tano zinazohitimisha  ngwe  ya kwanza  ya Rais Dr John Pombe  Magufuli  akiwatumikia  watanzania  katika nafasi  ya Mkuu wa nchi, Mkuu wa Serikali na Amiri Jeshi  Mkuu.  Kifupi ni muda unaoweza  kutoa picha ya kutosha kuhusu Taifa gani linasukwa chini ya awamu  ya tano! 


Kwakuwa mjadala wa Bajeti unagusa wadau wengi na hivyo niwajibu  kila mdau  kutoa  maoni, basi ieleweke vema  kwamba kutofautiana  maoni  miongoni mwa wadau  wa nchi ndio afya ya mjadala wenyewe. 


Binafsi nimependa  kutamka  kwa kifupi mafungu kumi (10) ya ukweli ambao ningependa  yaeleweke  kuwa ni kuweka  kumbukumbu sawa kwasababu katika mijadala hii wadau tunaweza kuzidiana  na kutofautiana  kiwango  cha taarifa. 


# Fungu la kwanza ninapenda  kutofautiana na maoni  ya chama fulani kuwa takwimu za ukuaji uchumi ( Pato la Taifa) zina walakini kwa hoja kwamba huwa haiwezekani  ukuaji  wa pato la mtu mmoja mmoja  kukua kwa kasi ndogo kuliko kasi ya ukuaji wa pato  la Taifa. Kwamba haiwezekani Serikali iseme  ukuaji uchumi ni asilimia7% kama ukuaji wa pato la mtu mmoja mmoja (per capita income) ni asilimia4.4%. 

# Naomba ieleweke  kwamba kwa mujibu  wa takwimu za Bank ya dunia, nchi kadhaa katika miaka kadhaa  zimepata  kuwa na asilimia kubwa ya ukuaji pato la Taifa kuliko pato la mtu mmoja mmoja.  Mfano; Kenya mwaka 2011 pato la Taifa lilikua  kwa asilimia 6.1% lakini Pato la mtu mmoja mmoja ( per capita income ) ilikua  asilimia  3.3%. Mwaka 2015 nchi hiyohiyo pato la Taifa lilikua  kwa asilimia 5.7% wakati pato la mtu mmoja mmoja lilikua kwa asilimia  3% . Sio Kenya tu, Botswana mwaka 2017 pato lake lilikua kwa asilimia 2.4% lakini pato la mtu mmoja mmoja lilikua kwa asilimia 0.5% au Ghana ambayo mwaka 2017 pato lake ilikua  kwa  asilimia 8.1% wakati pato la mtu mmoja mmoja lilikua  kwa asilimia 5.8%.Nikatika msingi huo hoja kwamba Pato  la Taifa Tanzania haliwezi  kukua kwa asilimia 7% kwakuwa pato la mtu mmoja mmoja ( per capita income ) ni asilimia4% inakosa  uzito. 

# Fungu la Pili; napongeza  uamuzi  wa Serikali kuongeza  kodi ya uagizaji  nje wa  nywele  bandia za kina mama . Nimeshangaa  kuona hata hilo  likipingwa  kwasababu ni moja ya mambo yasio na tija  kwa Taifa. Nimepata  kusoma  ripoti ya mtafiti  Sam  Piranty  ilochapwa  BBC Desemba2015 kuonesha  namna Afrika  inavopoteza  fedha za kigeni  kuagiza  vitu visio  lazma sana kutoka China.

# Katika ripoti  hiyo ilionesha  kwamba nchi ya Benin  mwaka huo iliongoza  kwa   kuagiiza  nywele  na ndevu  bandia  za thaman ya dola 411( zaidi ya bilioni900) kutoka China. Nigeria iliongoza kwa kuagiza  miswaki  milioni 159  kutoka China. Afrika kusini iliongoza  kwa kuagiza  chupi  za kiume  milioni16 na Kenya iliongoza kwa kuagiza  vyoo  vya  kukaa  kwa zaidi  ya dola milioni8 au bilioni20. 

# Ripoti hiyo ilikuwa mjadala mkubwa kwa misingi  kwamba afrika lazima ipunguze  matumizi  ya fedha za kigeni kuagiza vitu  visio lazma sana kiuchumi. .Hivyo uamuzi wa kuongeza  kodi katika uagizaji  nywele  bandia ni jambo la maana saana kwa lengo la kuhakikisha kama Taifa hatuingii  kundi la vinara wa matumizi makubwa ya fedha za kigeni kuagiza vitu visio muhimu sana kiuchumi .Nasisitiza bidhaa  hii  haina  umuhimu sana kuagizwa  nje  na ingebidi  kodi zaidi ya hiyo  ingekuwa afya ili kama nilazma  basi sizalishwe ndani

# Fungu la tatu nigusie  kidogo kuhusu uimara wa uchumi !  ningependa  kuanza kwa kupongeza  uamuzi wa Serikali ya awamu ya tano mwaka jana2018 kukubali kufanyiwa  kitu inaitwa  CREDIT RATING...ambapo  Serikali inapimwa  katika mizania  ya kimataifa  kuona  uwezo  wake kumudu deni na kukopesheka  ambapo  kwa hakika  kinachopimwa  ni msuli  wa uchumi  wa nchi husika. Katika matokeo yake yalotolewa  Machi4,2018, matokeo yanayopatokana katika tovuti  ya Taasisi hiyo ambapo inaonesha  kwamba Tanzania ilifanya  vizuri  kuliko nchi zote afrika mashariki kwa uwezo wake kiuchumi  kumudu deni na kukopa zaidi..Ilikuwa habari nzito iliyozua  mjadala Kenya ambapo Gazeti la Daily Business  lilitoka  na kichwa  cha habari...." Tanzania Rated Higher than Kenya " kama inavyosomeka  kwenye mtandao wa Gazeti hilo hapa-

https://www.businessdailyafrica.com/markets/marketnews/US-agency-assigns-Tanzania-higher-credit-rating-than-Kenya/3815534-4329666-jpuyco/index.html 


Kwamba  wakati kwenye viwango  Tanzania ilionekana  kuwa na B1, nchi za Kenya na Uganda zilikuwa na B2.

# Kwa Tanzania hii ilikuwa mara ya kwanza tangu tupate Uhuru ambapo  kwa bahati nzuri tulifanyiwa  tathimini  huo na taasisi  ya Moody's  ambayo inaongoza  duniani katika kazi hizo  ambapo asilimia 45% ya kazi hizi duniani  inafanya yenyewe. Vema ieleweke  tu kwamba ripoti za taasisi hizi za credit rating ndio kwa kiasi kikubwa hutumiwa  na mataifa  mbalimbali  duniani yanayomgozwa kisasa( modern gorvenance).

#Fungu la nne; Nilipenda  nigusie  kwann kelele  kuhusu utitiri  wa leseni  na vibali zimekuwa  kubwa sasa kuliko zamani. Je  nikweli kwamba leseni na vibali husika vimeanza  leo au awamu hii ya5? Kwanza ieleweke  kwamba nakubaliana na ukweli kuwa utitiri  wa vibali na leseni ni changamoto  ktk urahisi wa kufanya Biashara. Lakini ieleweke  pia kwamba utitiri  huu  haujaletwa  na awamu  ya 5 bali usimamizi  madhubuti  wa taratibu katika awamu ya 5 na kuzibwa  kwa mianya  ndio sababu  ya utitiri  huu wa vibali kuonekana  machungu  yake.  Kabla ya awamu ya 5 nchi ilikuwa  inakwenda  kwa "mission-town" hivyo wingi huo wa vibali na leseni  usingeweza  kuleta  maumivu.

# Fungu la tano linatoka Fungu la nne ambapo linahusu  BLUEPRINT  na mazingira  ya Biashara. Kwamba  uamuzi  wa Serikali kukubali  kuanza  kutekeleza makubaliano  yake na sekta binafsi  yaliyomo  ndani ya kutabu  maarufu  kama BluePrint  ni uamuzi  wa kimapinduzi kwani mapungufu  ya kitaasisi, kimfumo, kisheria na kisera  yaliyokuwepo  tangu awamu ya tatu mpaka sasa yataanza  na yameanza  kufanyiwa kazi kurekebisha  mwendendo  wa biashara. Uamuzi wa kufuta  takribani  aina 54 za ushuru na tozo  ambazo zilikuwa kero ni sehemu ya dhamira  ya utekelezaji huo. 

Fungu la sita nimependa kugusia dhana ya Uchumi wa Vitu dhidi ya Uchumi  wa watu. Labda nianze kwa kurejea  hoja ya Mchumi Dambisa  Moyo kwenye kitabu  cha Edge  Of Chaos alichokizindua Aprili2018 na kusababisha mjadala mkali duniani ambapo  pamoja na mambo mengine amerejea hoja muhimu kwamba Afrika imendelea  kuwa tegemezi  kwasababu viongozi wake hawana uwezo kufanya  maamuzi makubwa kwa faida  ya vizazi  vijavyo  kwa hofu za uchaguzi.

#Viongozi hao wanajikuta wanatafuta majibu  ya muda  mfupi  badala ufumbuzi  wa kudumu. Vema  ieleweke kwanza kwamba takwimu  za kiasi kinachotolewa  na serikali kwenye sekta za maji, elimu na afya tangu awamu  ha tano kuingia  madarakani  nikikubwa  kuliko tulikotoka.Pia vema ieleweke pia    kwamba  kwenye nchi lazma ujenge  kwanza msingi wa uzalishaji  kabla ya huduma. Kuita  ujenzi  wa reli ya kisasa  au Mradi  mkubwa wa umeme  wa zaidi ya 2100MW wa  Stirgglers  kuwa ni maendeleo ya vitu ni kutokuelewa  dhana nyepesi  kiuchumi  kwamba ni uchumi unaozalisha  unaoweza  kuhudumia  watu  na sio kinyume  chake.miradi hiyo mikubwa inaweka  misingi  ya kutanua  uzalishaji  na hatimaye  kuongeza  uwezo wa uchumi kutoa  huduma  zaidi.  

# Lakini zaidi ya ukweli huo, tukitaka  kujua  lini uchumi  wetu  ulihudumia  watu na lini ulihudumia  vitu ni kuangalia  upatikanaji  huduma  hizo.  Miradi  ya maji, umeme, elimu na afya  ni mikubwa Karibu kila Wilaya.  Wakati awamu  ya 5 inaingia madarakani  kiasi ambacho  kilitolewa  na serikali MSD  kwajili  ya kununua  dawa na vifaa tiba  hakikuzidi  shilingi 31bn  mwaka 2015 wakati leo kiasi kinachotolewa  na serikali kwajili ya kununua  dawa  na vifaa  tiba  ni zaidi ya 270bn sawa na ongezeko  la dawa  kwa zaidi  ya asilimia900%. Hizi dawa ni kwajili ya afya za watu sio vitu.

#Fungu la saba  ningependa kugusia  uwezo wa Serikali kukusanya kodi. Kwanza ieleweke  kuwa duniani kote huchukua  miongo  kadhaa  kwa mfanyabiashara  kutamani  kulipa  kodi kwa mapenzi yake. Ni ushindan siku zote.  Mapinduzi katika makusanyo ya kodi  kutoka shilingi  850bn kwa mwezi mpaka wastan wa shilingi 1300bn sawa na ongezeko la asilimia zaidi ya 52% yanaweza  yasitoshe  lakini ni makubwa kupata kutokea tena ndani ya muda mfupi . 

#Tumetoka kwenye kipindi ambacho serikali ilibidi  kukopa  ili kulipa  mshahara ya watumishi wake. Madhara yake ilikuwa ni pamoja na Serikali kukopa  mno kwenye hatifungani hata kufikia serikali kukopa kwa riba zaidi ya asilimia 17% kwa hatifungani za siku 365 . Madhara ya hali hiyo kwa sekta binafsi  ilikuwa  kusababisha  riba kwenye bank za biashara kupaa kwani Bank za biashara hutumia  kigezo  cha riba kwenye hatifungani  kuamua  riba kwenye bank  zao kwa sekta  binafsi. 

#Ndio sababu  ya riba kwenye bank kufika  asilimia 23% mwaka 2015 ni kwasababu serikali ilikopa  kwa asilimia17%.lakini kwasasa pamoja na deni kuongezeka  bado serikali haina kiu  na udharula  wa kukopa  kulinganisha  na tulikotoka. Ndio sababu inakopa  kwa riba ya asilimia 5% mwaka 208 kutoka asilimia17% mwaka 2015 na hiyo ndio sababu ya kwann sasa bank zinakopesha  kwa asilimia 13%mpaka 17% kutoka asilimia 23% kabla ya JPM. 

 # Fungu la nane nimependa kurejea kilichosemwa na Mkurugenzi  wa IMF, Bi  Christine  Legarde  alitembelea  Tume  ya Uchumi  wa Afrika  yenye makao yake makuu jijini Addis Ababa Ethiopia ,Disemba 2017  ambapo alipoulizwa  ni mataifa gani Afrika ambayo  mwelekeo wake kiuchumi unachukua  njia ya vietnam  kiviwanda  alitaja  Tanzania, Nigeria, Ethiopia na Kenya.  ( Rejea Jarida la Quartz , Disemba2017). Huu ndio mwelekeo.  Unachangamoto  nyingi lakini JPM yupo  kwenye njia  sahihi.

Fungu la tisa niwakumbushe tu utafiti uliochapishwa kwenye Jarida la Havard Business Review  ukioonesha kwamba China inatarajiwa  kupoteza  ajira  kati  ya milioni 85 mpaka milioni100  kutokana  na gharama  ya ujira  kupanda. Ukweli huu ulisisitizwa  pia na Prof nguli  wa uchumi duniani, Joseph Stirglitz kwa msisitizo alipohutubia wanazuoni wa Tanzania ukumbi wa Nkurumah Chuokikuu cha Sar es Salaam mwaka jana kwamba mitaji  hiyo inaweza  kuelekea zaidi Afrika lakin nchi hizo ziwe na miundombinu  ya viwanda ambayo pamoja na rasilimali  watu ni pamoja ubora wa miundombinu kwa urahisi wa biashara

# Fungu la kumi nifunge  kwa kusema  hakuna   njia ya kujenga uchumi isiyo  na mbadala isipokuwa kinachozingatiwa ni gharama ya hiari( opportunity cost) isizidi gharama halisi. Ndio maana mijadala ya kiuchumi  ni yakudumu.  Walewale walioweza  kuhoji kwann  Serikali inakusanya  kiduchu  ndio wanalalamika  kwann  Serikali ikusanye  sana, inaumiza  wafanyabishara! Wale wale waliohoji iweje  nchi ya nusu karne toka ipate  Uhuru lakn imebaki  haina reli wala ndege ndio haohao  wanaohoji  kwann ijengwe  reli na kununuliwa ndege sio vitu vingine? Wale wale waliosema tunaporwa  kwenye madini miaka  yote ndio haohao  wanaopinga  kwann  wawekezaji  kwenye madini wafanyiwe  unyama  na kwamba ni kufifisha  sekta ya madini. Na vipindi  vyote wanaweza kuonekana  kuwa na hoja hasa katika nchi ambayo bado tabaka  la kati kiuchumi ni dogo hivyo kunakuwa  na changamoto ya wasikilizaji  wengi kutambua  nilichokiita gharama  ya hiari ( opportunity cost). 

# Imekuwa bahati kwamba kwenye sekta kama  ya madini iliyofanyiwa  mabadiliko na kupitia  msukosuko  mkubwa kuliko sekta  yoyote tangu awamu  ya 5 kuingia madarani, ndio sekta ambayo mauzo ya nje  yamezidi  kuongezeka  kinyume na ilivyokadiriwa na wakosoaji  wa JPM.  Sekta ya madini leo inachangia  pakubwa  kwenye pato la Taifa  kuliko  kabla na kwenye mauzo   ya nje  mchango  wake umezidi  kuongezeka  kutoka mauzo ya takribani  dola 1.2bn mwaka 2015 mpaka zaidi ya dola bilioni 1.6 mwaka 2018. Naam takwimu hazidanganyi lakini ni wazi kwamba ipo homa  ya mpito kutoka'uchumi wa 'mission-town kwenda uchumi  halisi '

TANZANIA YASAINI MKATABA WA KUPATIWA FEDHA ZA MSAADA BILIONI 60 ZA KITANZANIA KUTOKA SERIKALI YA CHINA

$
0
0
Tanzania imetia saini Mkataba wa kupatiwa fedha za Msaada wa Shilingi Bilioni 60 za kitanzania kutoka Serikali ya Watu wa China bila ya masharti yeyote ambapo Serikali ya Tanzania itaamua matumizi yake katika miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi wake. 

Mkataba huo umesainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi  ambaye ameiwakilisha Serikali ya Tanzania na Makamu Mwenyekiti wa Shirika la Kimataifa la Misaada ya Maendeleo la China Bw. Zhou Liujun kwa upande wa Serikali ya China. Mkataba huo umesainiwa punde tu mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya Waziri  Prof Palmagamba John Kabudi na Waziri wa Mambo ya Nje wa China na Mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi.

Mazungumzo ya Mawaziri hao yalilenga kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia baina ya China na Tanzania sambamba na  kuibua maeneo ya kipaumbele na kimkakati yatakayotekelezwa kwa ushirikiano baina ya China na Tanzania.

Maeneo hayo ni pamoja na upembuzi yakinifu kwa ajili ya upanuzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ili kuwa  Taasisi Mahiri ya Tiba ya Moyo Kusini mwa Jangwa la Sahara, ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme ya Ruhudji (megawatt 358) na Rumakali (megawatt 222) mkoani yaliyoko mkoani Iringa na Njombe ambayo yote kwa pamoja yatakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa takribani megawati 580,pamoja na upembuzi yakinifu wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa (standard gauge railway) sambamba na ukarabati wa reli ya TAZARA.

Aidha, katika mazungumzo yao, Serikali ya China imeahidi pia kuunga mkono katika ujenzi wa miundombinu muhimu katika mji mpya wa Serikali katika makao makuu Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Nje wa China na mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi amesifu mahusiano mema na ya kirafiki baina ya Tanzania na China na kuongeza kuwa Tanzania imekuwa Rafiki wa kweli wa China kwa wakati wote.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameishukuru Serikali ya China sambamba na kueleza kuwa kipaumbele cha Tanzania ni kudumisha na kuendeleza mahusiano mazuri ya kidiplomasia,kisaiasa na kiuchumi yaliyopo baina ya Nchi hizo mbili kwa manufaa ya pande zote mbili.

Pia Prof. Kabudi ameipongeza Serikali ya China na Nchi za Afrika kwa kuandaa mpango kazi wa kimkakati ambao umeanisha maeneo kumi ya kipaumbele yakiwemo uendelezaji wa sekta ya viwanda na miundombinu ambayo kwa nchi za Afrika hususan Tanzania ndio kipaumbele cha kwanza. Maeneo mengine ya kipaumbele ni pamoja na uendelezaji wa biashara na uwekezaji kati ya China na Afrika pamoja na ushirikiano katika maeneo ya ulinzi na usalama kwa kutaja machache.

Halikadhalika, Prof Kabudi ameisifu Serikali ya China kwa kubainisha hatua kubwa nane zitakazosaidia utekelezaji wa Mpango Kazi wa Beijing (2019 – 2021). Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kuanzisha program maalum ya ujenzi wa maeneo maalum ya viwanda (Industrial park), ujenzi wa miundombinu ya nishati, usafirishaji na mawasiliano,mpango maalum wa ujenzi wa vyuo vya ufundi na vituo vya kutolea mafunzo ya stadi kwa ajili ya kuandaa nguvu kazi ya kufanya kazi viwandani.

Katika hatua nyingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amehudhuria mkutano kati ya mawaziri wa mambo ya nje kutoka nchi 53 za Afrika na taasisi za fedha za China ambazo ni pamoja na Mfuko wa Maendeleo kati ya China na Afrika (CAD FUND), Benki ya Exim ya China pamoja Benki ya Maendeleo ya China yenye lengo la kutoa ufafanuzi na utaratibu wa fedha kiasi cha Dola bilioni 60 zilizoahidiwa na Serikali ya China wakati wa Mkutano Mkuu wa Wakuu wa Nchi za Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) uliofanyika mwezi Septemba, 2018 jijini Beijing. 

Awali, katika ya ufunguzi wa mkutano huo,mchumi mkuu wa Benki ya Maendeleo ya China Liu Yong amesema China ina matumaini makubwa kuwa Afrika itaendelea kiuchumi na kwamba wataendelea kushirikiana na Nchi zote kwa kuwa malengo yao ni kuona nchi za Afrika zinaendelea kupitia ushirikiano baina ya China na Afrika.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
BEIJNG - CHINA.
24 Juni 2019

IMELDA MARCOS MKE WA RAIS ALIYEFAHAMIKA ZAIDI KWA KUMILIKI VIATU VIPATAVYO JOZI 3,000

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
IMELDA Marcos ambaye pia amewahi kuwa mke wa Rais wa Ufilipino Ferdinand Marcos  aliyetawala katika miaka ya 1965 na kutolewa kwa nguvu madarakani mwaka 1986 anashikilia rekodi ya kumiliki viatu vingi zaidi vinavyofikia jozi 3,000.

Mtandao wa Rappler wa nchini humo umeeleza kuwa Imelda amekuwa mpenzi wa viatu, vito vya dhahabu pamoja na nguo za nakshi ambapo baada ya kupinduliwa kwa mumewe aliacha maelfu ya jozi za viatu hivyo katika ikulu ya Malacanang na baadaye viatu hivyo vikapelekwa katika makumbusho maalumu iitwayo Makumbusho ya viatu ya Marikina.

Rappler imeeleza kuwa Imelda amekuwa anafahamika kwa mambo makuu mawili maarufu zaidi kwanza ni kuwa mke wa Rais dikteta wa nchi hiyo Ferdinand Marcos na kumiliki viatu vingi zaidi ambavyo vimeweka historia duniani kote.

Aidha imeelezwa kuwa jozi 3,000 za viatu zimethibitishwa na mamlaka husika licha ya viatu hivyo  kutoonekana bora zaidi kama vilivyotolewa katika Ikulu ya Malacanang mwaka 1986.

Rappler imeeleza kuwa viatu vya malkia huyo wa urembo kwa sasa  vinapatikana katika makumbusho ya Marikina ambako kuna jozi 720 huku jozi 253 zikiwa zimeuzwa na jozi 467 zimehifadhiwa.

Imeelezwa kuwa mamlaka iliamuru viatu hivyo vihamishiwe mjini mwaka 1996 ambapo FirstLady huyo aliandika na kueleza kuwa hakuwa na usemi.

Makumbusho hiyo iliyoanzishwa mwaka 2001 imekuwa ikihifadhi viatu hivyo huku ripoti  iliyochapishwa mwaka 2010 katika jarida la Gurdian ilieleza kuwa kuna zaidi ya makasha 150 ya nguo, vito, na viatu ambavyo vimeharibika kutokana na changamoto ya uhifadhi.

Makumbusho hayo ya viatu  yamekuwa yakitembelewa na wanafunzi na watalii na vimepangwa kwa rangi katika makumbusho hiyo ya Marikina.

Sehemu iliyopangwa viatu hivyo vimechukua sehemu kubwa ya ghorofa hiyo ikiitwa "Imelda's Footwear."

 Imeelezwa viatu  hivyo vimetengenezwa kutoka kampuni (brand) mbalimbali na hivyo vikiwemo viatu vya kuogea, vya kuvaa chumbani na vingi vikiwa vimetengenezwa nje ya Ufilipino ikiwemo nchini Taiwan na Ufaransa.

TANZANIA YAWA MWENYEJI WA MAFUNZO YA UKAGUZI WA KODI

$
0
0

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo akifungua rasmi mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na African Tax Administration Forum (ATAF). Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika
Meneja wa Mafunzo ya Ukaguzi wa Kodi kutoka African Tax Administration Forum (ATAF) Caroline Mutayabarwa akizungumza wakati wa hafla fupi ya ufunguzi wa mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na ATAF ambapo jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika. Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na yatamalizika tarehe 28 Juni, 2019.
Baadhi ya Wakaguzi wa Kodi kutoka Mamlaka za Mapato Afrika wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na African Tax Administration Forum (ATAF) ambapo jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika. Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na yatamalizika tarehe 28 Juni, 2019
Wakaguzi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na African Tax Administration Forum (ATAF) ambapo jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika. Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na yatamalizika tarehe 28 Juni, 2019.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya menejimenti ya TRA, wakufunzi na wakaguzi wa kodi mara baada ya ufunguzi rasmi wa mafunzo ya ukaguzi wa kodi ambayo yameandaliwa na TRA kwa kushirikiana na ATAF ambapo jumla ya wakaguzi wa kodi 50 wameshiriki mafunzo hayo kutoka Mamlaka za Mapato mbalimbali Barani Afrika. Mafunzo hayo ya wiki moja yanafanyika jijini Dar es Salaam na yatamalizika tarehe 28 Juni, 2019. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO)

Vodacom watunukiwa tuzo ya NEEC

$
0
0


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Kassim Majaliwa (Kulia) akimpongeza na kumkabidhi tuzo Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Bi Rosalynn Mworia (kushoto) kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo katika kuinua wananchi kiuchumi wakati wa semina ya uwezeshaji wananchi kiuchumi uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Bi. Rosalynn Mworia akizungumza na wadau mbalimbali wa masuala ya kiuchumi katika semina ya uwezeshaji wananchi kiuchumi iliyofanyika jijini Dodoma mwishoni mwa wiki.

TANZANIA YASAINI MKATABA WA KUPATIWA FEDHA ZA MSAADA BILIONI 60 ZA KITANZANIA KUTOKA SERIKALI YA CHINA

$
0
0
Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi  (Mb) akibadilishana nyaraka na Makamu Mwenyekiti wa Shirika la Kimataifa la Misaada ya Maendeleo la China Bw. Zhou Liujun, mara baada ya kusaini nyaraka hizo. Zoezi hilo limefanyika Beijing,China. June 24, 2019
 Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na ujumbe wake akiwa kwenye mkutano pamoja na mwenyeji wake ambaye ni Waziri wa mambo ya nje wa China na na Mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi na ujumbe wake. Mkutano huo umefanyika Beijing,China. June 24, 2019.

 Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiteta na mwenyeji wake ambaye ni Waziri wa mambo ya nje wa China na na Mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi na ujumbe wake mara baada ya kumaliza mkutano baina yao. Mkutano huo umefanyika Beijing,China. June 24, 2019.


Tanzania imetia saini Mkataba wa kupatiwa fedha za Msaada wa Shilingi Bilioni 60 za kitanzania kutoka Serikali ya Watu wa China bila ya masharti yeyote ambapo Serikali ya Tanzania itaamua matumizi yake katika miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi wake. 

Mkataba huo umesainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi  ambaye ameiwakilisha Serikali ya Tanzania na Makamu Mwenyekiti wa Shirika la Kimataifa la Misaada ya Maendeleo la China Bw. Zhou Liujun kwa upande wa Serikali ya China. Mkataba huo umesainiwa punde tu mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya Waziri  Prof Palmagamba John Kabudi na Waziri wa Mambo ya Nje wa China na Mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi.

Mazungumzo ya Mawaziri hao yalilenga kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia baina ya China na Tanzania sambamba na  kuibua maeneo ya kipaumbele na kimkakati yatakayotekelezwa kwa ushirikiano baina ya China na Tanzania.

Maeneo hayo ni pamoja na upembuzi yakinifu kwa ajili ya upanuzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ili kuwa  Taasisi Mahiri ya Tiba ya Moyo Kusini mwa Jangwa la Sahara, ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme ya Ruhudji (megawatt 358) na Rumakali (megawatt 222) mkoani yaliyoko mkoani Iringa na Njombe ambayo yote kwa pamoja yatakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa takribani megawati 580,pamoja na upembuzi yakinifu wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa (standard gauge railway) sambamba na ukarabati wa reli ya TAZARA.

Aidha, katika mazungumzo yao, Serikali ya China imeahidi pia kuunga mkono katika ujenzi wa miundombinu muhimu katika mji mpya wa Serikali katika makao makuu Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Nje wa China na mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi amesifu mahusiano mema na ya kirafiki baina ya Tanzania na China na kuongeza kuwa Tanzania imekuwa Rafiki wa kweli wa China kwa wakati wote.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameishukuru Serikali ya China sambamba na kueleza kuwa kipaumbele cha Tanzania ni kudumisha na kuendeleza mahusiano mazuri ya kidiplomasia,kisaiasa na kiuchumi yaliyopo baina ya Nchi hizo mbili kwa manufaa ya pande zote mbili.

Pia Prof. Kabudi ameipongeza Serikali ya China na Nchi za Afrika kwa kuandaa mpango kazi wa kimkakati ambao umeanisha maeneo kumi ya kipaumbele yakiwemo uendelezaji wa sekta ya viwanda na miundombinu ambayo kwa nchi za Afrika hususan Tanzania ndio kipaumbele cha kwanza. Maeneo mengine ya kipaumbele ni pamoja na uendelezaji wa biashara na uwekezaji kati ya China na Afrika pamoja na ushirikiano katika maeneo ya ulinzi na usalama kwa kutaja machache.

Halikadhalika, Prof Kabudi ameisifu Serikali ya China kwa kubainisha hatua kubwa nane zitakazosaidia utekelezaji wa Mpango Kazi wa Beijing (2019 – 2021). Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kuanzisha program maalum ya ujenzi wa maeneo maalum ya viwanda (Industrial park), ujenzi wa miundombinu ya nishati, usafirishaji na mawasiliano,mpango maalum wa ujenzi wa vyuo vya ufundi na vituo vya kutolea mafunzo ya stadi kwa ajili ya kuandaa nguvu kazi ya kufanya kazi viwandani.

Katika hatua nyingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amehudhuria mkutano kati ya mawaziri wa mambo ya nje kutoka nchi 53 za Afrika na taasisi za fedha za China ambazo ni pamoja na Mfuko wa Maendeleo kati ya China na Afrika (CAD FUND), Benki ya Exim ya China pamoja Benki ya Maendeleo ya China yenye lengo la kutoa ufafanuzi na utaratibu wa fedha kiasi cha Dola bilioni 60 zilizoahidiwa na Serikali ya China wakati wa Mkutano Mkuu wa Wakuu wa Nchi za Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) uliofanyika mwezi Septemba, 2018 jijini Beijing. 

Awali, katika ya ufunguzi wa mkutano huo,mchumi mkuu wa Benki ya Maendeleo ya China Liu Yong amesema China ina matumaini makubwa kuwa Afrika itaendelea kiuchumi na kwamba wataendelea kushirikiana na Nchi zote kwa kuwa malengo yao ni kuona nchi za Afrika zinaendelea kupitia ushirikiano baina ya China na Afrika.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
BEIJNG - CHINA.
24 Juni 2019

BASI LA HAI EXPRESS LAPATA AJALI,DEREVA ATAKIWA AJISALIMISHE

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,PWANI

WATU wanne wamejeruhiwa baada ya kutokea ajali ya gari la abiria aina ya higer kampuni ya Hai express huko barabara kuu ya Dar es salaam -Morogoro,eneo la Kwamatias Kibaha .

Katika ajali hiyo dereva wa gari hiyo,Juma Abdallah alitoroka baada ya kusababisha ajali kizembe ,ambapo anatakiwa kujisalimisha katika jeshi la polisi mkoani humo ,kabla hajatafutwa.

Akielezea kuhusu ajali hiyo,kamanda wa polisi mkoani ,Wankyo Nyigesa alieleza imetokea majira ya saa 1:30 asubuhi Juni 24 mwaka huu.

Alisema, gari hilo la abiria lenye namba za usajili T.329 DGC ikiendeshwa na Juma alitoroka ikiwa na abiria 48 ikitokea Dar es salaam kuelekea Mbeya,kupitia Kibaha Mji iliacha njia na kupinduka na kusababisha abiria wanne kupata majeraha.

Kati ya abiria hao watatu ni wanawake ambao wametibiwa na kuruhusiwa na mmoja mwanaume ambae anaendelea na matibabu katika hospital ya rufaa ya Tumbi .

"Chanzo cha ajali ni dereva wa gari hilo kujaribu kuyapita magari mengine barabarani katika eneo lililozuiliwa darajani hivyo kushindwa kulimudu na kuliangusha "alifafanua Wankyo.

Wankyo alibainisha ,alimtaka dereva huyo ajisalimishe mwenyewe ili achukuliwe hatua za kisheria.

Kamanda huyo aliwaasa madereva,kuacha kukiuka sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali zembe.


BABA ADAIWA KUBAKA NA KULAWITI BINTI YAKE MAILMOJA TANGINI,KIBAHA-WANKYO

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA

JESHI la polisi mkoani Pwani,linamshikilia Suleiman Issa Ngorombwe (43) mfanyabiashara na mkazi wa Mailmoja Tangini ,Kibaha,kwa kudaiwa kumbaka na kumlawiti binti yake wa miaka 11.

Kamanda wa polisi mkoani Pwani,Wankyo Nyigesa alieleza kwamba,tuhuma ziliripotiwa katika kituo cha polisi Kibaha Mjini Juni 20 majira ya asubuhi ambapo walimkamata mtuhumiwa.

"Baada ya upelelezi wa tuhuma hii kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani "

Alieleza,jeshi la polisi linaendelea kukemea vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na vya kinyama vinavyofanywa na baadhi ya watu kwenye jamii.

Wankyo alisema,vitendo vya aina hiyo huanzia ngazi ya familia hivyo alitoa rai kwa wananchi kutoa ushirikiano wa kuripoti taarifa za matukio kama hayo ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria na iwe fundisho kwa wengine.

MGODI WA GEITA GOLD MINING (GGM) WATUNUKIWA TUZO NA TANAPA

$
0
0
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi-Mawasiliano TANAPA,Pascal Shelutete akieleza sababu za Tanapa kutoa tuzo kwa kampuni ya AngloGold Ashanti Ltd kutokana na mchango wake kwa shirika wa kutangaza Mlima Kilimanjaro pamoja na kuongeza pato la shirika .
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi-Mawasiliano TANAPA,Pascal Shelutete akikabidhi tuzo maalumu kwa wakuu wa mikoa ya Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghwira na Geita,Robert Gabriel kwa ajili ya kukabidhi kwa Makamu wa Rais wa Kampuni ya AngloGold Ashanti wanaomiliki mgodi wa dhahabu wa Geita,Simn Shayo. 
Wakuu wa mikoa ya Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghwira na Geita,Robert Gabriel wakimkabidhi tuzo maalumu iliyotolewa na TANAPA kwa Makamu wa Rais wa Kampuni ya AngloGold Ashanti wanaomiliki Mgodi wa dhahabu wa Geita,Simn Shayo.









Na Dixon Busagaga.Moshi


SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limeitunuku Kampuni ya AngloGold Ashanti Ltd tuzo maalumu kutokana na mchango wake wa kutangaza Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro kupitia changamoto a kupanda mlima ikilenga kuchangisha fedha za Mapambano ya Virus vya Ukimwi lijulikanalo kama “Kili Challenge”

Tuzo hiyo imetolewa wakati wa hafla ya mapokezi ya washiriki 64 waliopanda mlima Kilimanjaro,wengine wakizunguka mlima huo kwa Baiskeli,hafla iliyofanyika katika lango la kushukia la Mweka na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa serikai wakiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira aliyekuwa mgeni rasmi.

Akimwakilisha Kamishna Mkuu wa Uhifadhi -TANAPA ,Dkt Allan Kijazi katika hafla hiyo,Kamishna Msaidizi Mwandamizi –Mawasiliano TANAPA,Pascal Shelutete alisema mbali na GGM kutumia Mlima Kilimanjaro kuchangisha fedha lakini pia kwa kiasi kikubwa wameshiriki katika kuutangaza Mlima huo.

"Niwashukuru wenzetu was Geita Gold Mining kwa kipindj Cha miaka 17 Sasa tangu walivyoanza zoezi hili,wamekuwa wakichangia pato la Shirika kupitia Mlima lakini pia kwa upande mwingine zoezi hili limekuwa likisaidia Sana kuutangaza Mlima Kilimanjaro ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu."alisema Shelutete.

"Tumeona ni vyema tunatambua mchango huo hasa ambapo tukio hili Lina fikisha miaka 17 kwa kutoa tuzo maalum kwa wenzetu hawa wa GGM "aliongeza Shelutete.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Anna Mghwira alisema mlima Kilimanjaro ni dhamana iliyotolewa na Mungu kwa watanzania hivyo serikali wajibu wake mkubwa ni kuhakikisha kwamba unaendelea kubaki salama na kuenziwa.

“Sisi watu kama serikali ni kuhakikisha kwamba Mlima Kilimanjaro unaendelea kubaki na kuenziwa ili uendelee kufaidisha nchi yetu na Dunia kwa ujumla na katika kuhakikisha hilo linatekelezeka tumeweka utaratibu maalumu wa kuhakikisha hauchafuliwi wala kuharibiwa kwa namna yoyote ile.”alisema Dkt Mghwira .

Dkt Mghwira alitumia nafasi hiyo kuwahimiza Serikali za wilaya zinazopakana na hifadhi ya taifa ya Mllima Kilimanjaro pamoja na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kukaa kwa pamoja kumaliza migogoro baina ya wananchi na hifadhi hiyo.

“Naomba kuhimiza kwa Serikali za wilaya pamoja na TANAPA kupitia KINAPA ya kwamba Migogoro yote inayohusu eneo la Mlima imalizwe,kuna migogoro ya Half Mile, inazungumzwa kila wakati na ni kama haiishi.”alisema Dkt Mghwira.

Aidha Dkt Mghwira aliwaomba wageni kutoka nje ya nchi kutoingilia masuala yanayohusu Mlima Kilimanjaro na badala yake watumie muda wao kuijifunza kutoka kwa watanzania kwani wao ndio wenye kuufahamu vizuri mlima huo.

“Niombe pia wageni ambao wanakuja kwetu hasa wale ambao wanakuja kwa shughuli za kijamii wajifunze kutoka kwetu ,wasituingilie sana kwenye eneo hili ,….hapa na pale tumekutana kila wakati na mazingira ya wageni kujiingiza mno kwenye masuala ya mlima.”alisema Dkt Mghwira .

“Wamekuwa wakijiingiza katika shughuli zinazofanyika hapa na kuteletea utata mgumu ,kwa sababu tunavyoshughulika na wageni wa nje ya nchi mahusiano yake yanakuwa tofauti kidogo na namna ya kufanya maamuzi”aliongeza Dkt Mgwira.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Kampuni ya AngloGold Ashanti kupitia mgodi wa Dhahabu Wa Geita,Simon Shayo alisema zadi ya Bil 13 zimekusanywa katika kampeni hiyo tangu ianze na kuungwa mkono na zaidi ya mashirika yasiyo ya kiserikali 40.

“Tunafurahi kweli na tunashukuru kwa washirika wetu wote na tutaendelea kushirikiana kufanya kila liwezekanalo na kwa ambao pia wangependa kujiunga katika vita hivi hii inamaanisha wakihamsika wapandaji zaidi itasababisha watu binafsi na jamii zaidi kuunga mkono na mpango wa Kili Challenge.”alisema Shayo.

Shayo aliwashukuru wafadhili wa changamoto hiyo na wote walishiriki kupanda na kwamba jitihada walizoonesha ni muhimu katika kuchochea tukio hilo wakiwemo waendesha baiskeli ambao waliamua kuweka roho zao juu ili kuhakikisha Tanzania kupitia Kili Challenge inafikia sifuri 3 mwaka 2030.

AUNT EZEKIEL ADHIHIRISHA URAFIKI WAKE WA SHIDA NA RAHA KISUTU.

$
0
0

  Na Khadija seif,Globu ya jamii

MSANII wa bongomovie nchini Aunt Ezekiel amemfariji mahakamani wema sepetu.

Aunt Ezekiel ni miongoni mwa rafiki wa karibu wa msanii wema isaack sepetu na mara kadhaa wamekua wakiwa karibu kwenye shida na raha huku kupitia ukurasa wake wa Instagram akionekana kusambaza baadhi ya picha ambazo walikua pamoja huku akimuombea mazuri.

Ambapo ameonekana Leo mahakamani ya kisutu kufatia kesi iliyokua ikimkabili rafiki yake wakaribu Wema Sepetu ambaye amesota gerezani kwa siku 7 kutokana na kukiuka masharti ya dhamana.

Mahakama imemuonya msanii huyo endapo akirudia kukiuka masharti ya dhamana haitasita kumfutia kabisa dhamana hiyo.

Wema anakabiliwa na mashtaka ya kusambaza  video ya ngono katika mitandao ya kijamii kupitia simu yake ya kiganjani ambapo anadaiwa  kati ya Oktoba 15, 2018 katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, alisambaza video za ngono kupitia ukurasa wake wa Instagram, picha ambazo inadaiwa kuwa haina maadili.

Serikali kuboresha viwanja vya ndege

$
0
0
 Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Vedastus Fabian (kushoto) akiwasikiliza Maafisa Naomi Mbilinyi na Gladston Mlay (kulia), kutoka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), katika maonesho yanayokwenda sambamba na Jukwaa la Pili la Kimataifa la Usafiri wa Anga linalofanyika kwa siku mbili mfululizo kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC). 
 Dkt Bartholomew Rufunjo (kulia) leo akipata maelezo mbalimbali kuhusiana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kutoka kwa Mhandisi Astelius John (kushoto), kwenye maonesho yanayokwenda sambamba na Jukwaa la Pili la Kitaifa la Usafiri wa Anga yanayofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC). Wengine pichani ni Afisa Masoko wa TAA, Pendo Mwakilasa akizungumza na Mtendaji Mkuu wa VIA Aviation Ltd, Suzan Mashibe.
 Mhandisi Astelius John na Afisa Masoko, Pendo Mwakilasa wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (kushoto), leo wakiwaeleza masuala mbalimbali ya viwanja vya ndege wadau waliotembelea meza ya maonesho yanayokwenda sambamba na Jukwaa la Pili la Kitaifa la Usafiri wa Anga yanayofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC).

TUME YA NGUVU ZA ATOMIKI TANZANIA (TAEC) KUENDESHA MKUTANO KUIMARISHA UWEZO WA KIKANDA KWA SEKTA ENDELEVU YA MADINI YA URANI

$
0
0
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) kwa kushirikiana na Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani (IAEA) wanaendesha mkutano wa siku tano kwa nchi wanachama wa IAEA kanda ya Afrika, zinazodhibiti usalama wa mionzi.

Lengo kuu la mkutano uliohudhuriwa na jumla ya washiriki 27 kutoka Botswana, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Chad, Congo, Jamhuri ya Demokrasia ya Congo, Misri, Ethiopia, Gabon, Ghana, Madagascar, Malawi, Mali, Nigeria, Sudan na Tanzania ni kujadili  na kutoa miongozo kulingana na viwango vya usalama kwa wasimamizi wa nchi za wanachama wa Afrika juu ya utoaji wa leseni na ukaguzi wa shughuli za mzunguko wa uzalishaji wa madini ya urani.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAEC Injinia John Ben Ngatunga alipokuwa akifungua rasmi mkutano huo katika hotel ya SG Premium Resort ya Jijini Arusha hivi leo,  amewataka washiriki wote kufanya majadiliano ambayo yatasaidia kuelewa miundombinu iliyopendekezwa ya sheria na udhibiti wa madini ya urani na majukumu ya washirika wengine wa udhibiti katika ngazi za kitaifa na kimataifa.


Imetolewa na;

Peter G. Ngamilo
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania

Viewing all 110095 articles
Browse latest View live




Latest Images