Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110133 articles
Browse latest View live

SHIRIKA LA RELI TANZANIA-TRC LAPATA FURSA YA KUSHIRIKI MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA BARANI AFRIKA NCHINI KENYA, NAIROBI.

$
0
0
Shirika la Reli Tanzania-TRC limepata fursa ya kushiriki katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma Barani Afrika, yaliyozinduliwa rasmi na Mh.Rais Uhuru Kenyata katika viwanja vya KICC nchini Kenya, Nairobi leo Juni 21 2019.

Lengo la maadhimisho haya kwa nchi za bara la Afrika ni kubadilishana ujuzi, kujifunza katika ufanisi wa kazi katika sekta za Umma ili kuleta tija na ubunifu zaidi katika maeneo ya kazi kutoka nchi tofauti barani Afrika.

Maadhimisho haya ya wiki ya utumishi wa umma barani Afrika yamesisitizwa na kauli mbiu wa Uhusiano kati uwezeshaji vijana na usimamizi wa masuala ya uhamiaji, kujenga utamaduni wa utawala Bora, matumizi ya Tehama na ubunifu katika utoaji huduma jumuishi. 

Kupitia maadhimisho haya TRC imepata fursa ya kuelezea ubunifu na matumizi ya Tehama katika kutoa huduma. 

Huduma zitolewazo na TRC, yaani kutoa huduma za Usafiri wa Abiria, Mizigo na kukodisha nafasi kwa kampuni za serikali na sekta binafsi ndani ya Tanzania na Nje katika behewa za TRC nje na ndani kwa ajili ya matangazo kwa kua Treni za TRC zina masafa marefu na mafupi,Hivyo fursa ya kutangaza na kuongeza uelewa kuongezeka kwa umma endapo kama wadau watapenda kupata huduma hiyo.

Pia TRC iliendelea kutoa Elimu zaidi kuhusu miradi mikubwa miwili yaani Mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa ambao mpaka sasa umefikia zaidi ya 51% Kwa awamu ya kwanza Daresalaam-Mwanza katika kipande cha Daresalaam-Morogoro na Kipande cha pili Morogoro-Makutopola mradi huu umefika zaidi ya asilimia 12% katika usanifu na ujenzi.

Mradi wa uboreshaji wa Reli ya kati mpaka sasa umefikia zaidi ya 12% kwa ukarabati wa njia na madaja, na miradi mingine midogo kama ufufuaji wa njia ya Reli , Tanga, Arusha, Moshi ambao unatarajia kuanza rasmi huduma ya treni za abiria mwezi wa 9, 2019 na treni za mizigo kuanza mwezi wa 7, 2019.

Vile vile TRC inaendelea na maandalizi ya mradi wa huduma ya treni za mijini za kisasa kwa jiji la Daresalaam na Dodoma.

Katika maadhimisho haya ya Wiki ya Utumishi wa barani Afrika yaliyofanyika nchini Kenya, Nairobi waafrika kutoka nchi tofauti kama Kenya, Afrika kusini, Nigeria walipongeza juhudi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Jemedali Rais Dr.John Pombe Magufuli kwa uthubutu Alioufanya kwa kutekeleza miradi mikubwa kwa kutumia pesa ya ndani ambayo inapatikana kwa walipa kodi Tanzania na kusisitiza Rais Magufuli kuwa mfano Bora wa kuigwa katika utendeji kwa maslahi ya Nchi na Taifa kwa ujumla.

Maadhimisho haya ya Utumishi wa umma barani Afrika kwa upande wa Tanzania yaliwakilishwa na taasisi 3 zilizo chini ya serikali kuu ambapo maadhimisho haya yameandaliwa na kuongozwa na Ofisi ya Rais Utumishi, Taasisi zilizoshiriki ni Shirika la reli Tanzania-TRC, Mamlaka ya chakula na Dawa-TFDA, Bohari ya Dawa Tanzania-MSD.
Kaimu Mkuu Kitengo cha Habari  na Uhusiano TRC Bi Jamila Mbarouk  akitoa  Maelezo na ufafanuzi  kwa mdau Denis Alphonse kuhusu miradi inayosimamiwa na TRC pamoja na huduma zitolewazo katika maadhimisho   ya wiki ya utumishi wa umma  katika viwanja vya KICC leo juni  21, 2019 jijini Nairobi,nchini Kenya.
 Mhandisi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC),Tito Mateshi akitoa akifafanua jambo kwa Bi Catherine  Erasto kuhusu miradi inayosimamiwa na TRC pamoja na huduma zitolewazo katika maadhimisho  ya wiki ya utumishi wa umma katika viwanja vya KICC   jijini Nairobi nchini Kenya,  leo Juni  21, 2019.
 Pichani ni watumishi kutoka taasisi tatu tofauti, Shirika la Reli Tanzania -TRC, Mamlaka ya chakula na Dawa-TFDA,Bohari ya dawa Tanzania -MSD zilizoshiriki katika maadhimisho  ya wiki ya utumishi wa umma barani Afrika  pamoja na  Balozi wa  Kenya  nchini Tanzania Dkt.Pindi Chana (wanne kulia) wakiwa  mbele ya banda la Tanzania katika viwanja vya KICC, jijini Nairobi ,nchini Kenya  leo Juni 21,2019.
Picha ya pamoja na Wakurugenzi kutoka ofisi ya Rais Utumishi Tanzania walipotembelea banda la Shirika la Reli Tanzania-TRC siku ya ufunguzi rasmi wa maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa barani Afrika katika viwanja vya KICC  jijini Nairobi nchini Kenya, leo Juni  21, 2019.

WAZIRI BASHUNGWA AWAHAKIKISHIA WAKULIMA WA TUMBAKU MASOKO

$
0
0
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa (kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi wa Mahusiano kutoka kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) Bw. Godson Killiza aliyefika Ofisi ndogo za Wizara Dar es salaam kwa mazungumo.Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa (kulia) akiagana na Bw. Godson Killiza Mkurugenzi wa mahusiano wa kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) aliyefika Ofisi ndogo za Wizara Dar es salaam kwa mazungumoWaziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa wa tatu (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi kutoka TCC na Watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara.
……………..

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa amesema Serikali itatafuta wanunuzi wa zao la Tumbaku endapo Kamapuni iliyokuwa inanunua awali ya TLTC haitaendelea na ununuzi huo.

Amesema kuwa tayari Kampuni ya GTI imekubali kushirikiana na Serikali kununua zao hilo kutoka kwa wakulima msimu ujao.Mhe. Bashungwa ameyasema hayo leo alipokutana na wawakilishi wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) ambapo aliahidi kufanya mazungumzo na Waziri wa Kilimo kwa lengo la kujadiliana namna ya kupata kampuni itakayoweza kununua zao la tumbaku kutoka kwa wakulima.

‘’Tutazungumza na kampuni ya awali iliyokuwa ikinunua tumbaku kama watakubali kuendelea kununua zao hilo au kama hawawezi basi serikali itatafuta wanunuzi wengine watakaonunua zao hilo kwa wakulima msimu ujao,’’ alisisitiza.

Aliongeza kuwa wadau wengi wameipongeza serikali kwa kuwa na bajeti rafiki iliyosikiliza wadau wa viwanda na biashara kuhusu masuala ya tozo na kodi mbalimbali.

Bashungwa alisema Serikali itaendelea kuondoa vikwazo vilivyokuwepo kwenye sekta ya biashara kwa lengo la kuleta unafuu na kukuza biashara, ajira na mazingira rafiki kwa wafanyabiashara wa sekta binafsi.
Naye, Mkurugenzi wa Mahusiano Godson Killiza kutoka TCC alisema kitendo cha serikali kupunguza kodi ya bidhaa mbalimbali ni jambo linaloleta faida kwa wafanyabiashara watanzania kutumia malighafi za ndani kuzalisha bidhaa.

Alisema bajeti ya serikali ya 2019/2020 italeta faida katika ukuaji wa uchumi, kukuza biashara na kupunguza gharama za uzalishaji kwa kampuni nyingi.

Killiza alisema ongezeko la Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa asilimia nane katika biashara yao imesaidia kuongeza ulipaji wa kodi kutoka Sh bilioni 227 mwaka 2017 hadi Sh bilioni 234 mwaka jana.

TANGA UWASA WATEKELEZA AGIZO LA MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU KWA VITENDO

$
0
0

AFISA Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorrah Killo kulia akifanya mazoezi na watumishi wa mamlaka hiyo leo(Ijumaa) jioni
Sehemu ya watumishi wa Tanga Uwasa wakiwa kwenye mazoezi katikati ni Kaimu Afisa Rasilimali Watu wa Tanga Uwasa Theresia Sanga
Mazoezi yakiendelea
AFISA Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorrah Killo kulia akiwa na watumishi wenzake wakishiriki mazoezi hayo
Mazoezi yakiendelea kama inavyoonekana

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) wameanza utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais Samia Suluhu kwa kufanya mazoezi siku tatu kwa wiki baada ya muda wa kazi kwisha.

Mazoezi hayo hufanyika Jumanne, Jumatano na Ijumaa ambayo yameonekana kuwa chachu kwa watumishi ambao wamekuwa wakishiriki

Akizungumza mara baada ya kumalizika mazoezi ya leo Kaimu Afisa Rasilimali Watu wa Tanga Uwasa Theresia Sanga alisema wameamua kufanya mazoezi hayo ili kuweza kuimarisha miili yao na kuiweka imara pia husaidia kupunguza msongo wa mawazo.

Alisema pia kupitia mazoezi hayo mbali ya kuimarisha miili yao lakini pia yanajenga umoja na kuweka kujenga ushirikiano kwenye kazi hali inayosaidia kutekeleza majukumu yao vema.

“Lakini pia mazoezi yanaondoa msongo wa mawazo hivyo ni jambo zuri huku akiwahamasisha watumishi kuhakikisha kila wakati wanashiriki kwani yanafaida kubwa kiafya”Alisema

Awali akizungumza Afisa Uhusiano wa Tanga Uwasa Dorrah Killo alisema mazoezi hayo ni mazuri kwa sababu yanawapa umoja na kupelekea kupendana ikiwemo kuongeza hari ya uwajibikaji.

Bodi na Menejimenti ya TCRA yafanya ziara katika Maktaba ya Kisasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi James Kilaba kitabu wakati Bodi  na Menejimenti ya Mamlaka  hiyo ilipotembelea Maktaba Mpya na ya Kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam inayotumia mfumo wa Kielektroniki kuhifadhi na kusoma Vitabu na Majarida mbalimbali jijini Dar es Salaam.
 Bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wakiangalia Mfumo unavyafanya kazi katika  Maktaba Mpya na ya Kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam inayotumia mfumo wa Kielektroniki kuhifadhi na kusoma Vitabu na Majarida mbalimbali wakati walipofanya ziara katika Chuo hicho ambapo TCRA ilichangia kitabu vya Teknolojia ya Mawasiliano 800 katika mkataba hiyo.
 Bodi na Menejimenti ya TCRA wakiwa katika ziara ya Chuo Jijini cha Dar es Salaam wakati walipofanya ziara ya kuangalia maktaba ya kisasa ya Chuo hicho.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi James Kilaba akikabidhiwa vitabu vya Teknolojia ya Mawasiliano  katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Picha ya Pamoja ya Bodi na Menejimenti ya TCRA na Watendaji wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mara baada ya kumaliza ziara katika Chuo hicho jijini Dar es Salaam.

KUMBUKUMBU

$
0
0

Edmund Lawrence Mushi
07/12/1973 - 22/06/2015
Leo tarehe 22/06/2019 umetimiza miaka minne tangu ututoke,Unakumbukwa na watoto wako Luis(Anwary) na Jermaine,Unakumbukwa na Baba yako mzazi Mzee Lawrence Mushi(Kimbori).Pia unakumbukwa na wadogo zako Rudolf(Dofu),Claudia,Gaudence,Fulgence,Renatus(Kulwa),Martha(Manka/Dotto) na Maria(Mkakeni)
Unakumbukwa pia na ukoo wote wa Kimbori na Massawe,Pamoja na Ndugu jamaa na Marafiki,Pia Unakumbukwa na Tanzania Houston Community(THC) in Houston-Texas.Pumzika Kwa Amani Kaka Yetu Edmund.
    Bwana Alitoa,Bwana Ametwaa jina lake Lihimidiwe.
          Amen🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽🙏🏽

Wafanyakazi wa Benki ya Dunia wafanya usafi wa fukwe jijini Dar es Salaam

$
0
0
Wafanyakazi wa  Benki ya Dunia ofisi Tanzania  wakiongozwa na Mkurugenzi wao,  Bella Bird, wamefanya  usafi kwenye fukwe za bahari eneo la Coco Beach jijini Dar Es Salaam. 
Usafi huo ulifanyika kama jitahidi za Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira.

“Ujumbe wetu kwa jamii ni wawe na wajibu wa kuepuka uchafuzi,  kuondoa utamaduni wa kutupa taka ovyo na kua na tabia ya kuchakata. Tumefurahi Serikali imechukua hatua kubwa kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki na tunatumaini wataendelea kudhibiti",alisema Bird.
Aliendelea kusema kwamba upungauaji wa taka za mifuko ya plastiki hakika ni kitu kikubwa kwa Tanzania kusherehekea. Pia alisema hatua itayofuata ni kupiga marufuku mirija ya vinywaji kwa kua haina matumizi yoyote muhimu kwa karne hii.

Nao wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania walisema kila mmoja ana jukumu la kutunza mazingira.
"Wote tunajukumu kwenye  hizi taka. Makampuni ya vyakula na vinywaji  yashiriki kutoa elimu kwa jamii, kupanga usafi, kuweka pipa za taka na kusaidia uzoaji taka kama jukumu la kampuni kwa jamii",walisema wafanyakazi hao.

Nae, Carlos Mdemu ambaye ni mratibu wa  'Nipe Fagio' alisema “kuweka pipa za taka maeneo ya fukwe na mtaani ni mpango mzuri, lakini kwenye baadhi ya maeneo tumeona mapipa yanajaa na hakuna  anayekuja kuyazoa, kwahiyo watu wanabidi wajue majukumu yao pia”.
 Mdemu aliendelea kusema “kuwatoza faini  kwa kutupa taka ovyo inafanywa na Manispaa ya Ilala na ni nzuri. Lakini kuongeza ufahamu inaweza kua muhimu zaidi ili kwamba watu wengi wakiwa wanajua, unapunguza nguvu ya kuwatoza faini”.

Kuhusiana na taka za plastiki Mdeme alisema “kwa sasa, taka yenye changamoto tuliyoona ni chupa za plastiki zenye rangi na vifungashio vya chakula (aiskrimu n.k).  Chupa za plastiki za rangi hazikusanywi kwa ajili ya kuchakata kwasababu hazina soko kwa  wakusanyaji”.
“Hapo nyuma tulipofanya usafi wa fukwe, tuligundua hesabu za taka za mifuko ya plastiki ni zaidi ya asilimia 50. Hii imebadilika, leo tumekusanya si zaidi ya asilimia 10” alisema Carlos Mdemu.  

 Wakihitimisha usafi katika fukwe za Coco Beach wafanyakazi hao walisema "tumeacha alama ndogo ukilinganisha na kinachotakiwa kufanywa. Lakini hii ndiyo sababu kwanini tumefanya na kwanini wote inabidi tuunganishe mikono na kuacha alama kubwa zaidi.
"Tunatekeleza tunachokisema, Benki ya Dunia Tanzania tunasema hapana kwa plastiki, weka fukwe na bahari yetu safi, sema hapana kwa matumizi ya plastiki, saidia mapambano dhidi uchafuzi wa plastiki" walisema wafanyakazi hao.
 Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia (WB) nchini, Bella Bird (kushoto) akiwa amejumuika na baadhi ya wafanyakazi wa Benki hiyo baada ya kuhitimisha zoezi lililofanyika katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia (WB) nchini, Bella Bird (wa pili kulia) akipata maelezo kutoka kwa Carlos Mdemu (wa tatu kushoto) ambaye ni Mratibu wa Nipe Fagio baada ya kuhitimisha zoezi hilo lililofanyika katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach wafanyakazi hao walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.Pichani walioinama chini ni vijana wa Nipe Fagio wakijaribu kufanya tathmini ni taka gani zaidi zimejitokeza kwa wingi wakati wa zoezi la usafi katika fukwe hizo.
 Mratibu wa Nipe Fagio, Carlos Mdemu na vijana wake wakichambua sehemu ya taka za plastiki ziliookotwa na wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam huku Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia (WB) nchini, Bella Bird na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wakitafuta ufumbuzi wa kuhakikisha bahari inakuwa safi na salama kwa viumbe wanaoishi baharini.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania wakiokota taka za plastiki zikiwemo chupa za vinywaji vya MO Energy vya kampuni ya MeTL na mifuko ya lambalamba za Ukwaju zinazotengenezwa na kampuni ya Azam iliyokuwa imetapakaa katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe  hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania wakionyesha taka za plastiki ikiwemo miraji na mifuko ya lambalamba bidhaa za Ukwaju zinazotengenezwa na kampuni ya Azam iliyokuwa imetapakaa katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe  hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania wakiwa wamebeba mifuko ya kuhifadhi taka walipokuwa katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe  hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.
 Ofisa Habari wa Benki ya Dunia nchini, Loy Nabeta akionyesha mifuko plastiki ya lambalamba za kampuni ya Azam iliyokuwa imezagaa katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe  hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania wakirejea na mifuko iliyosheheni taka za plasitiki baada ya kuhitimisha zoezi hilo eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi  wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na mifuko ya kuhifadhia taka baada ya kuhitimisha zoezi lililofanyika katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.
Baadi ya taka za mifuko plastiki ya lambalamba za kampuni ya Azam pamoja na chupa za vinywaji vya kampuni ya MeTL zilizochambuliwa na vijana wa Nipe Fagio baada ya wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya  Tanzania kumaliza zoezi la usafi katika fukwe za bahari ya Coco Beach ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.

CHUO KIKUU ARDHI WATOA ELIMU MAADHISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

$
0
0
MHADHIRI wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) Paul Kitosi akifafanua jambo kwa sehemu ya wageni waliotembelea maonesho ya kazi zinazofanywa na chuo hicho wakati wa maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Goba jijini Dar es Salaam leo. 
 MHADHIRI wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), Shule ya Sayansi ya Mazingira na Tekinolojia, Addo Michael Ndimbo akimwelezea mfumo wa usafishaji maji mmoja wa wageni waliotembelea maonesho ya chuo hicho katika maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Goba jijini Dar es Salaam Juni 20 2019.
 MHADHIRI Msaidizi wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) Dennis Gapser akitoa maelezo kwa sehemu ya wageni waliotembelea maonesho ya kazi zinazofanywa na chuo hicho wakati wa maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Goba. (Picha na Robert Okanda)   
 MHADHIRI wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), Dkt. Zakaria Ngereja akimwelimisha mkazi wa Dar es Salaam aliyekuwa na kiu ya kupata taarifa sahihi za maswala ya ardhi alipotembelea maonesho ya chuo hicho katika maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma Goba. 
 MHADHIRI wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), Dkt. Benedict Malele akifafanua jambo kwa baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam walioshiriki maonesho ya maswala ya ardhi yaliyoandaliwa na ARU eneo la Zahanati ya Goba katika maadhimisho ya wiki ya utumishi jijini humo.

BODI YA TCRA, MENEJIMENT NA KAMATI YA MAUDHUI WATEMBELEA MAKTABA MPYA YA KISASA UDSM NA JENGO JIPYA LA KIWANJA CHA NDEGE CHA JULIU NYERERE TERMINAL 3 TBIII

$
0
0

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

BODI ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), pamoja na Menejimenti ya Mamlaka hiyo, zimemefanya ziara kwenye kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere ili kujionea jengo jipya la kiwanja hicho, Terminal III (TBIII), pamoja na Maktaba mpya na ya kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani.

Ziara hiyo iliyofanyika Ijumaa Juni 21, 2019 pia iliwahusisha wajumbe wa Kamati ya Maudhui ya TCRA.

Akizungumzia nia ya ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James M. Kilaba alisema, Mamlaka kama Mdhibiti na Msimamizi wa Mawasiliano nchini, imeona ni vema kutembelea taasisi hizo mbili kwani kuna mambo ya msingi yanayofanywa na taassi hizo yanahusiana moja kwa moja na huduma zinazotolewa na TCRA.

“Lengo la ujio wetu hapa Terminal III nikuangalia katika hatua hizi ambazo ujenzi umekamilika ni mahitaji yapi ambayo bado ili sisi tuongeze ushiriki wetu ili kuyakamilisha hususan katika mifumo ya mawasiliano.” Alsiema Mhandisi Kilaba.

Alisema wakiwa hapo TBIII wamepata fursa ya kuulizia hali ya mawasiliano kama imekamilika ambapo watoa huduma, TTCL, Airtel, Vodacom, Tigo, Zantel, Halotel na hata Internet kama wako tayari.

“Huduma hizi ni muhimu sana na zinatakiwa ziwe kwenye maeneo kama haya kwa sababu zinawezesha hata kufanya utalii kuwa rahisi, mgei anapoingia hapa na anataka kwenda eneo Fulani la utalii lazima awasiliane, lakini pia TCRA inatoa masafa kwa ajili ya kuongozea ndege zinapotua na kuruka na lengo hasa ni kuhakikisha hakuna muingiliano katika huduma hizo." Alibainisha Mkurugenzi huyo Mkuu wa TCRA.

"Kuja kwetu kumetupa fursa ya kujifunza mengi kama ambavyo watanzania wanaweza kushuhudia kuwa kiwanja hiki ni kizuri, kinapendeza na mawasiliano yapo yanaendelea kukamilishwa na tumejionea hata Wifi point ipo.” Alifafanua Mhandisi Kilaba.

Aidha kuhusu Maktaba mya ya kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mhandisi Kilaba alisema, Maktaba hiyo inatumia huduma za TCRA kwani moja ya huduma zitolewazo ni pamoja na Maktaba mtandao (e-library) na hili ni jambo jema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TCRA, Dkt.Jones Killimbe alisema, ziara hiyo imekuwa ni ya mafanikio makubwa kwani imewezesha timu nzima ya TCRA, Wajumbe wa Bodi, Menejimenti, Wajumbe wa Kamati zinazosaidia kutekeleza majukumu kwenye mamlaka kwa pamoja wameelimika sana.

“Kiwanja hiki katika lugha ambayo ningeiazima ni flagship project….ni mradi wa kimkakati wa taifa hili... nikisema kimkakati ni kwasababu mojawapo ya masuala ya kiuchumi ya nchi yetu ni utalii, na nadhani huu utakuwa mlango mkubwa sio dirisha…utakuwa mlango mkubwa wa utalii na mchango wa utalii kwenye uchumi wetu utaongezeka sana.” Alisema Dkt. Killimbe.

Ziara hiyo imewezesha wajumbe kupata maelezo ya kina ya kukamilika kwa huduma mbalimbali kwenye jengo la TBIII hali kadhalika kwenye maktaba ya ksiasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaa,
 Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jones Killimbe (mwenye shati jeupe), Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Mhandisi James M. Kilaba, (kulia), wajumbe wa Bodi na Kamati ya Maudhui ya TCRA wakiongozwa na Msimamizi wa Mradi wa ujenzi wa jingo la Terminal 3 (TBIII) la kiwanja cha ndege cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Juni 21, 2019.
 Dkt. Jones Killimbe (kushoto) na Mhandisi Kilaba, wakitembelea eneo la kusubiri abiria la jingo la TBIII kabla ya kuingia ndani ya ndege. 
 Muonekano wa nje wa eneo la kuondokea abiria kwenye jingo jipya la TBIII la kiwanja cha ndege cha Julkius Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Ujumbe wa TCRA ukipatiwa maelezo na Mhandisi Barton Komba (kulia), kuhusu wapi abiria anapaswa kuelekea mara tu baada ya kuingia eneo la kuondokea abiria.
 Mandhari ya sehemu ambayo abiria wa kawaida watakuwa wakisubiri kabla ya kupanda ndege.
 Eneo la udhibiti wa Pasipoti mara tu baada ya abiria kuwasili kwenye kiwanja hicho.
 Mhandisi Komba (kushoto), akimpitisha Mkurugenzi Mkuu wa TCRA eneo litakalotumika kudhibiti pasipoti.
 Mjumbe wa Kamati ya Maudhui ya TCRA, Bw. Jacob Tesha, akizunhumza jambo ili kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya huduma kwenye jingo hilo.
 Eneo la ku chek-inn.
 Picha ya pamoja.
 Msimamizi wa Maktaba mpya na ya kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (eneo la nyaraka za serikali), akitoa maelezo kwa ujumbe wa TCRA ukiongozwa na Mwenyekiti wa bodi, Dkt. Jones Killimbe (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Mhandisi James M. Kilaba (mwenye nguo za kibuluu), wakati wa ziara ya kutembelea maktaba hiyo.

 Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui, TCRA), Bi. Valerie Msoka (kushoto) na mmoja wa wajumbe wa Kamati hiyo, Bw. Dreck Murusuri, wakiangalia jinsi maktaba ya kielektroniki (e-library)ya Maktaba ya kisasa ya UDSM inavyofanya kazi.
 Mkurugenzi Mkuu, TCRA, Mhandisi James M. Killaba (wapili kulia), akiangalia kwa makini jinsi maktaba ya kielektroniki (e-library) ya Maktaba ya kisasa ya UDSM inavyofanya kazi.
 Mwenyekiti wa bodi, Dkt. Jones Killimbe (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Mhandisi James M. Kilaba (mwenye nguo za kibuluu), pamoja na ujumbe wakiouongoza, wakiwa kwenye chumba cha maktaba ya kielektroniki (e-library) ya Maktaba hiyo ya kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Maktaba mpya ya kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dkt.Esther Ndenje Sichalwe (katikati), akiongoza ujumbe wa TCRA ulipotembelea maktaba hiyo Juni 21, 2019.
 Dkt. Sichalwe (kulia), akizungumza na Kaimu Mkuu wa Kitenmgo cha Mawasilian, Uhusiano na Elimu kwa Umma, TCRA, Bw. Semu Mewakyanjala, wakati wa ziara hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Mhandisi James M. Kilaba, (kushoto), akimkabidhi Mkurugenzi wa Maktaba mpya ya kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Esther Ndenje Sichalwe (kulia), machapisho mbalimbali yanayoeleza shughuli za Mamlaka hiyo.
 Picha ya pamoja ya ujumbe wa TCRA mara baada ya kutembelea maktaba hiyo.

MWAKYEMBE AMTAMBULISHA RASMI KAIMU KATIBU MTENDAJI WA BODI YA FILAMU.

$
0
0
* Dkt. Kiagho Kilonzo ahaidi kuleta mabadiliko na kuhakikisha 
Filamu inakuwa jukwaa rasmi la uchumi hapa nchini.

Na.Khadija seif,Globu ya jamii

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe  mapema leo amekutana na Bodi ya Ushauri ya Bodi ya Filamu nchini katika ofisi za  Bodi ya Filamu na kumtambulisha kwa Wajumbe wa Bodi hiyo Kaimu Katibu Mtendaji  mpya wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt. Kiagho Kilonzo.

Katika kikao hicho Mhe. Mwakyembe alipongeza jitihada chanya zilizoanza kufanywa  na Naibu Katibu Mtendaji huyo katika kipindi kifupi cha kuteuliwa kwake na kumtaka  kufanya kazi kwa bidii na weledi wa hali ya juu katika kuhakikisha Sekta ya Filamu na  Michezo ya Kuigiza inasonga mbele na kuwa sehemu ya pato kwa Taifa na Wanatasnia 
wenyewe.

“Sekta ya Filamu na Michezo ya Kuigiza ni moja ya Sekta kubwa na muhimu 
zinazoweza kukuza pato la nchi na kupunguza umaskini kwa raia wake, hivyo Bodi ya  Filamu ni wajibu wenu kutengeneza mazingira rafiki yatakayo wezesha Sekta hii  kukuwa hapa nchini na kupunguza umaskini kwa Watendaji wake” Dkt. Mwakyembe  alisema.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mtendaji mpya wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt.  Kiagho Kilonzo alimshukuru Waziri Mwakyembe kwa kushiriki katika kikao hicho cha  kutambulishwa kwake kwa Wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Bodi ya Filamu  na kumuahidi kuendelea kufanya kazi nzuri itakayoimarisha na kukuza Tasnia ya  Filamu kwa kushirikiana na Wajumbe hao wa bodi ya Ushauri inayoongozwa na  Mwenyekiti wake Profesa Frowin Nyoni, kushirikiana na Wadau mbalimbali wa Sekta ya  Filamu na kuimarisha umoja wa vyama vya Watendaji katika Filamu ili kuhakikisha 
Filamu inakuwa jukwaa rasmi la uchumi hapa nchini.

“kwa pamoja tutashirikiana katika kuifanya Sekta ya Filamu na Michezo ya Kuigiza  inakuwa na mchango chanya kwa Taifa letu na sio sehemu au jukwaa la kuharibu  maadili ya kitanzania, hivyo tunaahidi kuifanya Sekta hii kuzidi kuimarika ili iweze kuwa  jukwaa la moja kwa moja la pato la mtu binafsi na Taifa kwa ujumla”. 

Hata hivyo bodi ya Ushauri ya Bodi ya Filamu kwa sasa ina wajumbe 8 ikiongozwa na Mwenyekiti Profesa. Frowin Nyoni na Katibu Dkt. Kiagho Kilonzo ambaye ni Naibu Katibu Mtendaji wa Bodi.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe  (katikati) akisisitiza jambo wakati wa Kikao cha kumtambulisha kwa Wajumbe wa Bodi  ya Ushauri ya Bodi ya Filamu Tanzania Kaimu Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu  Tanzania Dkt. Kiagho Kilonzo (kulia) katika Ukumbi wa mikutano wa Bodi hiyo iliyopo  Mtaa wa Samora Posta jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo 
Profesa Frowin Nyoni.

Dkt. Gwajima Ataka Huduma Tembezi za Afya kuwa Jukumu la Pamoja

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt.Dorothy Gwajima akizungumza katika kikao cha wadau wa Afya kilichofanyika katika ukumbi wa Takwimu Jijini Dodoma.\Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Zainabu Chaula akizungumza katika kikao cha wadau wa Afya Kilichofanyika katika Ukumbi wa Takwimu Jijini Dodoma.Wadau wa Afya wakifuatilia kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Takwimu Jijini Dodoma.
……………………. 

Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI
Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dkt. Dorothy Gwajima amewataka wadau wote wanaotoa huduma Tembezi za Afya kuunganisha nguvu kwa pamoja ili huduma hiyo iweze kufikishwa katika Halmashauri zote Nchini. 

Dkt.Gwajima ameyasema hayo wakati wa kikao cha wadau wa Afya kuwasilisha Taarifa mbalimbali za utekelezaji wa miradi kilichofanyika katika Ukumbi wa Takwimu Jijini Dodoma. 

Akizungumza katika kikao hicho Dkt. Gwajima amesema huduma Tembezi za Afya ni muhimu kufikishwa katika Ngazi ya Jamii ili wananchi waweze kupata matibabu kutoka kwa madaktari bingwa tena kwa gharama nafuu. 

“Huduma hizi zimekuwa zikitolewa na Taasisi tofauti kwa nyakati tofauti na kila Taasisi analenga eneo Fulani ambalo anachagua hivyo kuna maeneo ambayo yamekuwa yakinufaika na huduma hizi mara kwa mara lakini kuna sehemu nyingine hazifikiwi kabisa sasa ni umefika wakati wa kukaa pamoja na kuunganisha nguvu ya wadau wote pamoja na Serikali na kupelekwa huduma hii katika Halmashauri zote ili kila mwananchi mwenye uhitaji anufaike nayo”
Kupitia Kikao hiki cha leo tutaunda Kamati ya Uendeshaji ambayo itahusisha Wataalamu wa OR-TAMISEMI, Wizara ya Afya, Asassi zisizo za Kiserikali pamoja na wadau wanaotekeleza Afua za Afya ambao watakuja na hadidu za rejea zitakazotuongoza katika kutekeleza azima yetu hii kwa ufanisi aliongeza Dkt.Gwajima. 

Pia Dkt. Gwajima alisema kuwa “Tunajua tuna vituo vya kutolea huduma vya lakini si wakati wote vituo hivyo vinakuwa na madaktari Bingwa na kwa mwananchi wa kawaidia kusafiri mpaka kukutana na madaktari bingwa ni gharama hivyo tukisogeza huduma hizi tutawatibu wananchi wetu hata yale magonjwa ambayo walikuwa wameyakatia tamaa”Alisema Dkt. Gwajima. 

Dkt. Gwajima aliongeza kuwa Huduma hizi Tembezi zina faida zake kwanza gharama za kuwekeza katika huduma hii ni ndogo lakini inawafikia watu wengi tena kwa muda mfupi. Unafuu huu wa gharama sio kwa sisi kama watoa huduma lakini pia kwa wagonjwa ambao ndio wanufaika wa huduma hii yaani ugonjwa ambao angeweza kutumia zaidi ya shilingi milioni moja anaweza kupata huduma hiyo hiyo kupitia Kliniki Tembezi kwa elfu thelathini tu. 

“Huduma tembezi ni msaada kwa wanyonge, wananchi wanaugua magonjwa makubwa ambayo hata akisafiri kumfuata Daktari Bingwa anaweza akafia njiani kabla hata hajakutana na huyo Daktari, kupitia huduma hii watakutanishwa na Madaktari bingwa kwa urahisi na nafuu zaidi na hapo tutakuwa tumegusa maisha ya watanzania na kuwaongezea siku za kuishi maana wangeweza kufa kwa kukosa huduma za Afya stahiki kwa magonjwa yanayowasumbua” Alisema Dkt. Gwajima. 

Tusipowafuata na kuwatibu wananchi wataendelea kunywa miti shamba na kwenda kwa waganga na hata wakati mwingine kupoteza maisha yao kwa kukosa matibabu stahiki hebu tuwafikie wote kupitia huduma hii ya Kliniki Tembezi alimalizia Dkt. Gwajima. 

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainabu Chaula amesema agenda kuu katika Sekta la Afya ni Huduma ya Afya kwa Wote na hakuna mtu atakayeachwa nyuma hivyo ni lazima tuifikishe huduma hii ya Kliniki Tembezi kwa wananchi wote. 

“Tunapoelekea katika Uchumi wa Kati ni wajibu wetu kuhakikisha kila mwananchi anakuwa na Afya Njema ili aweze kushiriki kikamilifu katika kujitafutia kipato sasa hii kazi kwetu itakua rahisi tukiunganisha nguvu na rasilimali katika kutoa huduma hii ya Afya Tembezi tushirikiane kikamilifu kuleta tabasamu kwa watanzania” Alisema Dkt. Chaula. 

Akiwasilisha Taarifa ya Huduma za Afya Tembezi Mratibu wa Huduma hiyo Dkt. Mombeki Domisian amesema tangu walipoanza kutoa huduma hii katika Mkoa wa Singida imeokoa maisha ya watanzania, imetoa elimu ya Kinga, imepeleka utaalamu na zaidi imetoa ushauri kwa wagonjwa kulingana na ugonjwa husika.

KATIBU MKUU AALCO AITEMBELEA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA JIJINI DODOMA.

$
0
0


Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akiwa na Prof. Kennedy Gastorn (kushoto) na Prof. Sifuni Mchome (kulia) alipokutana na Prof. Gastorn ambaye ni Katibu Mkuu wa AALCO alipowatembelea Wizarani jijini DODOMA.
Prof Gastorn (kulia) akimkabidhi Prof.Mchome zawadi ya kitabu alichoandika kuhusu Afrika Mashariki.
Prof.Mchome akiagana na Prof.Gastorn aliyewatembelea katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma
……………………..

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Mashauriano ya Masuala ya Kisheria ya Nchi za Asia na Afrika (ASIA-AFRICAN LEGAL CONSULTATIVE ORGANISATION(AALCO) PROF. Kennedy Gastorn ameitembelea wizara ya Katiba na Sheria jijini Dodoma.

Katika ziara hiyo Prof. Gastorn amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Augustine Mahiga na Katibu Mkuu Prof. Sifuni Mchome katika Ofisi za Wizara zilizoko Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Prof. Gastorn na wenyeji wake wamezungumza masuala mbalimbali juu ya kuimarisha umoja huo na jinsi ya kunufaisha nchi wanachama.

AALCO ilianzishwa mwaka 1956 kwa lengo la kuwa chombo cha ushauri na ushirikiano katika masuala ya sheria za kimataifa kwa nchi za Asia na Afrika.

Toka kuanzishwa kwake AALCO imewezesha nchi wanachama kushirikiana na kubadilishana uzoefu katika masuala mbalimbali ya sheria za kimataifa na kimechangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya sheria za kimataifa.

Tanzania ilijiungana umoja huo 1973 .

Prof. Gastorn ni Mtanzania na alichaguliwa kushika nafasi hiyo Agosti 2016.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 22,2019

MNAPASWA KUDUMISHA NIDHAMU YA MATUMIZI YA FEDHA BAADA YA KUSTAAFU- PINDA

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mizengo Pinda akimuonesha Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi sehemu ya mimea ya zabibu aliyolima katika shamba lake la hekari 10 kwa ajili biashara wakati wa ziara ya watumishi wa ofisi hiyo wanaotarajia kustaafu mwaka huu walipomtembelea kujifunza mafanikio yake. Mmoja wa wastaafu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Nisetas Kanje akiuliza swali kwa Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda walipomtembelea nyumbani kwake eneo la Zuzu Dodoma kwa lengo la kujifunza Stadi za maaisha pindi watakapostaafu ikiwa ni moja ya shughuli anazofanya baada ya kustaafu Muonekano wa moja ya mabwawa ya kufugia samaki aina ya sato katika shamba la Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mizengo Pinda lililopo Kijiji cha Zuzu Jijini Dodoma ikiwa ni moja ya shughuli anazofanya baada ya kustaafu. Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mizengo Pinda akiwaonesha waastafu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu moja ya Bwawa la kufugia samaki aina ya kambale lililopo katika shamba lake eneo la Zuzu Jijini Dodoma walipomtembelea ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa mafunzo yaliyotolewa na ofisi hiyo kwa wastafu hao katika kuiadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma inayoendelea. Muonekano wa sehemu ya shamba la zabibu linalomilikiwa na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe.Mizengo Pinda eneo la Zuzu Jijini Dodoma ikiwa ni moja ya shughuli anazofanya baada ya kustaafu. Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mizengo Pinda akiwaonesha baadhi ya watumishi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu wanaotarajia kustaafu mwaka huu ufugaji wa kuku walipomtembelea katika makazi yake eneo la Zuzu Jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya kujifunza namna ya kufanya ujasilimali watakapostaafu. 
Katibu Mkuu (Ofisi ya Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi akizungumza jambo wakati wa kikao kifupi cha watumishi wa ofisi yake wanaotarajia kustaafu (hawapo pichani) pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mizengo Pinda walipomtembelea katika makazi yake eneo la Zuzu Jijini Dodoma. 
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mizengo Pinda akiwaonesha baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Wazri Mkuu wanaotarajia kustafuu mwaka huu sehemu ya miti ya miembe aliyolima katika shamba lake eneo la Zuzu Dodoma, wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu (Ofisi ya Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi. Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wanaotarajia kustaafu walipomtembelea nyumbani kwake eneo la Zuzu Jijini Dodoma Juni 20,2019.Kushoto kwake ni Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi.
(PICHA ZOTE NA OFISI NA WAZIRI MKUU) 
………………….


Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mizengo Pinda amewaasa watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wanaotarajia kustaafu hivi karibuni kudumisha nidhamu katika matumizi ya fedha baada ya kustaafu utumishi wa umma na kujikita katika shughuli za uzalishaji. 
Akizungumza katika makazi yake yaliyopo Zuzu Jijini Dodoma wakati watumishi hao walipomtembelea Juni 20, 2019 kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali za uzalishaji katika sekta ya kilimo na mifugo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kustaafu pamoja na kuadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma , Mhe Pinda amesema kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa watumishi wote wanaotarajia kustaafu kujenga utamaduni wa nidhamu katika matumizi ya rasilimali ikiwemo fedha watakazopata kama kiinua mgongo. 

” Nidhamu ya maisha baada ya kustaafu ni muhimu sana hivyo niwaase mjitahidi kuacha baadhi ya masuala ambayo mnafanya kwa sasa kama starehe na mambo yote yanayoendana na kupoteza muda wenu badala yake mjikite katika uzalishaji” Alisisitiza Mhe. Pinda .

Aliongezea kuwa ni vyema watumishi hao wakajenga utamaduni wa kufanya kazi za uzalishaji na kujikita katika usimamizi wa miradi ya uzalishaji watakayoanzisha kwa lengo la kujiongezea kipato na kukuza uchumi . 
Pia aliwaasa watumishi hao kuzingatia mawazo kutoka kwa watumishi ambao wameshastaafu na wamefanikiwa kimaisha baada ya kustaafu. 

“Kila mmoja wenu akatekeleze miradi ya kujikwamua kiuchumi kwa kuzingatia mafao atakayopata badala ya kutaka kufanya mambo kwa mashindano bali kila mtu ajikune kulingana na mkono wake unapoweza” 
Kwa upande wake Katibu mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi Maimuna Tarishi amesema kuwa mafunzo yakuwajengea uwezo wa kujiandaa kustaafu, yameandaliwa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma. 

Aliongeza kuwa watumishi hao wamefarijika kuona shughuli za uzalishaji anazofanya Waziri Mkuu mstaafu Mhe. Mizengo Pinda na kuwa ni mfano kwa watumishi wa umma wanaostaafu na kuanza kujikita katika uzalishaji mali . 

Ofisi ya Waziri Mkuu imeandaa mafunzo ya siku 5 kwa watumishi wake wanaotarajia kustaafu ili kuwapa mbinu za kisasa zinazolenga kuwawezesha kuendelea na maisha yao baada ya kustaafu huku wakiendeleza shughuli za uzalishaji zitakazowawezesha kuendesha maisha yao ya kila siku na kuweza kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza baada ya kustaafu.

CHANGAMOTO YA MAJI TABORA,NZEGA,IGUNGA KUWA HISTORIA

$
0
0
Bomba la Maji kwenda miji ya Tabora, Nzega na Igunga pamoja na Vijiji zaidi ya 120 likiunganishwa katika eneo la Solwa. Nzega wataanza kupata maji ya Ziwa Victoria mwezi wa saba, Igunga mwezi wa tisa na Tabora wataanza kupata maji kutoka Ziwa Victoria Novemba mwaka huu. Picha kwa hisani ya Maji Tanzania.

HALOTEL YAIPIGA JEKI TAIFA STARS AFCON

$
0
0

Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Mama Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Afisa uhusiano kampuni ya simu Halotel Stella Pius wakati akizungumza katika harambee ya kuchangia Taifa Stars iliyofanyika jijini Dar es Salaam.Halotel ilichangia shilingi Million 10, Kutoka kushoto ni Afisa Mawasiliano wa Halotel Hindu Kanyamala na Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Susan Mlawi. 

Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Mama Samia Suluhu Hassan akimpongeza Afisa uhusiano kampuni ya simu Halotel Stella Pius mara baada ya kuzungumza na kuchangia katika harambee ya kuchangia Taifa Stars iliyofanyika jijini Dar es Salaam.Halotel ilichangia shilingi Million 10, Kutoka kushoto ni Afisa Mawasiliano wa Halotel Hindu Kanyamala na Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Susan Mlawi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan, Katibu Mkuu wa Wizara Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi Susan Paul, wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Halotel katika harambee ya kuchangia timu ya Taifa Stars ambapo kampuni hiyo ilichangia Milioni 10/.

BALOZI JOSEPH SOKOINE AONGOZA WATUMISHI WA MAKAMU WA RAIS KUFANYA USAFI MAKULU DODOMA

$
0
0
Ofisi ya Makamu wa Rais katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma leo imefanya usafi katika eneo la Makulu jijini Dodoma kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji, NEMC, Wadau mbali mbali wa mazingira pamoja na Wananchi wa Makulu.
Wananchi na Wadau wa Mazingira wakishiriki zoezi la usafi katika eneo la Makulu, Dodoma ambapo taka za mifuko ya plastiki zilipewa kipaumbele, zoezi hili liliandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Wakazi wa Makulu jijini Dodoma wakiwa na vifaa vyao vya usafi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine (hayupo pichani) kabla ya kuanza kwa zoezi la usafi lililoratibiwa na Ofisi yake ikiwa Sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Wananchi na Wadau wa Mazingira wakishiriki zoezi la usafi katika eneo la Makulu, Dodoma ambapo taka za mifuko ya plastiki zilipewa kipaumbele, zoezi hili liliandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Patrobas Katambi akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali, Wadau wa mazingira na Wananchi mara baada ya kumaliza zoezi la usafi katika eneo la Makulu Dodoma, zoezi hilo liliratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma ikiwa sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Patrobas Katambi akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali, Wadau wa mazingira na Wananchi mara baada ya kumaliza zoezi la usafi katika eneo la Makulu Dodoma, zoezi hilo liliratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma ikiwa sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine (mwenye kofia) akiongoza watumishi wa ofisi yake pamoja na wananchi wa Makulu, Dodoma kufanya usafi ikiwa sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Balozi Joseph Sokoine (mwenye kofia) akiongoza watumishi wa ofisi yake pamoja na wananchi wa Makulu, Dodoma kufanya usafi ikiwa sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

KATIBU MKUU MASSAWE AHIMIZA USHIRIKIANO KWA WATUMISHI

$
0
0

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Ofisi hiyo, Bw. Peter Kalonga akieleza jambo kwa watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani) ikiwa ni sehemu ya maaadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe akizungumza na Watumishi wa ofisi hiyo (hawapo pichani) alipokutana nao kujadili utendaji kazi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. 
Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Ofisi hiyo wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (hayupo pichani) walipokutana Jijini Dodoma. 
Mmoja wa Watumishi wa Ofisi hiyo Bi. Grace Kigula akielezea baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo katika utendaji walipokutana na Katibu Mkuu wa ofisi hiyo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. 

Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Andrew Massawe alipokutana nao kusikiliza maoni na changamoto wazokabiliana nazo katika utendaji kazi wao.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (katikati) akifafanua jambo kwa wadau (hawapo pichani) alipokutana nao kwa lengo la kujadiliana pamoja na kusikiliza maoni, ushauri na changamoto wanazokutana nazo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2019. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Johanes Majura na kulia ni Mwanasheria kutoka Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzan Ndomba. 
Naibu Katibu Mkuu, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Johanes Majura (kushoto) akifafanua jambo kuhusu masuala ya vyama vya wafanyakazi wakati wa mkutano huo uliofanyika ghorofa la PSSSF, Jijini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe. 
Mwanasheria kutoka Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzan Ndomba akielezea kuhusu baadhi ya Sheria zinazowaongoza Waajiri nchini wakati wa kikao na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (katikati) alipokutana na wadau mbalimbali wa ofisi hiyo. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Johanes Majura 
Baadhi ya wadau wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (haupo pichani) walipokutana kujadili masuala mbalimbali kuhusu sekta ya Kazi, Maendeleo ya Vijana, Ajira, Huduma kwa Watu wenye Ulemavu, Hifadhi ya Jamii na masuala ya Vyama vya Wafanyakazi. 
Mmoja wa wadau kutoka Kampuni ya RECO Engineering Ltd, Bw. Abubakar Mukadam akichangia mada kuhusu masuala ya vibali vya kazi walipokutana na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (haupo pichani) ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma. 
Sehemu ya ya wadau wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (haupo pichani) walipokutana kujadili masuala mbalimbali kuhusu sekta ya Kazi, Maendeleo ya Vijana, Ajira, Huduma kwa Watu wenye Ulemavu, Hifadhi ya Jamii na masuala ya Vyama vya Wafanyakazi. 

PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU 
(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU) 
…………………….. 
Na; Mwandishi Wetu 
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe amewaasa watumishi wa ofisi hiyo kufanyakazi kwa ushirikiano ili waweze kutumiza malengo waliyojiwekea. 
Hayo ameyasema wakati alipokutana na watumishi wa ofisi yake Dodoma kwa lengo la kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma inayofanyika kila mwaka kuanzia Juni 16 hadi 23 kwa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kwa lengo la kuonesha mchango wa Watumishi wa Umma katika maendeleo ya nchi zao na Bara la Afrika kwa ujumla ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni; 
“Uhusiano kati ya uwekezaji wa vijana na usimamizi wa masuala ya uhamiaji: Jenga utamaduni wa Utawala bora, matumizi ya TEHAMA na Ubunifu katika utoaji wa huduma jumuishi.” 
Katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo ipo kisheria Katibu Mkuu huyo alisema kuwa Ofisi hiyo ina majukumu makubwa ya kiutendaji hivyo watumishi wanawajibu wa kufanyakazi kwa kushirikiana na kujenga umoja. 
“Ushirikiano katika kazi ni muhimu na husaidia kuboresha mifumo ya kiutendaji ikiwemo kuwa na mikakati endelevu ya ofisi, mawasiliano mazuri, kujenga mahusiano mazuri na wadau na kutoa huduma bora kwa wananchi,” alisema Massawe. 
Sambamba na hilo aliwasihi watumishi wa ofisi hiyo kufanyakazi kwa bidii, weledi, uzalendo na kuwa wabunifu katika kutekeleza majukumu yao na utoaji wa huduma kwa wadau na wananchi. 
Pia amewashauri watumishi hao kuepukana na vitendo vya rushwa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na maadili ya Utumishi wa Umma katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingatia haki na usawa. 
Aidha, Katibu Mkuu alikutana na kufanya kikao na wadau mbalimbali wa nje na alipokea maoni na mrejesho wa huduma zinazotolewa na Ofisi ya Waziri kuhusu sekta ya Kazi, Maendeleo ya Vijana, Ajira, Huduma kwa Watu wenye Ulemavu, Hifadhi ya Jamii na masuala ya Vyama vya Wafanyakazi. 
Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Bw. Peter Kalonga aliafiki yaliyosemwa na kuahidi kuahidi kufanyia kazi maagizo hayo ikiwemo suala la ushirikiano na mawasiliano katika utendaji kazi baina ya watumishi ili kuimarisha mshikamano baina ya watumishi. 
Kwa upande wake alisema kuwa kikao hiko kimewezesha watumishi wa ofisi hiyo kubadilishana taarifa zaidi za kiutendaji na kitasaidia kuimarisha ushirikiano

SERIKALI KUIMARISHA MAFUNZO KWA WALIMU WA MICHEZO-

$
0
0

JOSEPH MPNAGALA-MTWARA

Serikali imesema itaendelea kuimarisha Mafunzo kwa walim wa michezo ili kuweza kuwa na Walim watakaoweza kuibua Vipaji vya wanafunzi Mashuleni na kuweza kusaidia Taifa katika michezo mbalimbali.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi na Prf.Joyce Ndalichako wakati akifunga mafunzo ya Copa cocacola UMISETA yaliyomaliziaka katika Uwanja wa Umoja Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara.

Prf.Ndalichako amesema michezo ya umiseta imekuwa ikiibua vipaji mbalimbali kutoka kwa vijana na wapo waliofanikiwa katika ngazi ya kitaifa na kimataifa hivyo serikali itaendelea kuimarisha michezo.

“Tunafaham Kwamba michezo inasaidia kuimarisha afya michezo inasaidia kupunguza na kuepusha kupata magonjwa yasiyoambukiza lakini kwa wanafunzi Michezo inasaidia kuchangamsha akili”amesema PRf Ndalichako.

Naye Meneja Maendeleo ya Biashara Kampuni ya Coca Cola Yassin Hussein amesema ili kuhakikisha Mazingira yanatunzwa kampuni yake imeanzisha kampeni ya Rejesha na Ushinde ambapo Wanafunzi wanashindana kukusanya Chupa za zilizotumika.

“Kampeni yetu ya cocacoLA vijana wameweza kukusanya Chupa za Plastic zilizotumika zoezi ambalo tumelianzisha mwezi June na litamalizika mwezi wa Nane ili kuhakikisha tunatunza mazingira na nchi yetu inabaki salama”amesema Yassin.

Michezo ya Umeseta imeshirikisha Mikoa26 ambapo Fainali zilikutanisha Timu ya Songwe na Ruvuma ambapo Timu ya Ruvuma Ilishinda kwa mikwaju ya penati 10 kwa 9 .

Baadhi ya wanfunzi wa kutoka shule mbalimbali za sekondari wakionesha ishara ya kumalizika kwa mashindano ya Copa Coca Cola ambayo yalimalizika katika Uwanja wa Umoja Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara
Wachezaji na mashabiki wa timu ya Mkoa wa Ruvuma wakimnyanyua Juu Kipa wa Timu hiyo baada ya Kufanikiwa kupangua Mkwaju wa Mwisho uliyoipa Timu ya Mkoa wa Ruvuma Ushindi.

SERIKALI YATOA BARAKA ZOTE KWA WASHINDI WA PROMO YA TIGO AFCON,YAWAKABIDHI BENDERA YA TAIFA

$
0
0

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk Yusuf Singo (kushoto) akiwa na baadhi ya washindi wa Promosheni ya Soka la Afrika inayoendeshwa na kampuni ya Tigo muda mfupi baada ya kuwakabidi bendera ya Taifa kwa ajili ya kwenda kushuhudia Michuano ya Mataifa ya Afrika yanayofanyika nchini Misri. Wa kwanza kulia ni Afisa Biashara Mkuu wa Tigo Tarik Boudiaf


 Afisa Biashara Mkuu wa Tigo Tarik Boudiaf (kati kati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla fupi ya kuwakabidhi bendera ya Taifa baadhi ya washindi wa promosheni ya Soka la Afrika watakaokwenda Misri kushuhudia michuano ya mataifa ya Afrika. Kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk Yusuf Singo na kushoto ni Meneja Mawasiliano wa Tigo Woinde Shisael.

 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk Yusuf Singo (kati kati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla fupi ya kuwakabidhi bendera ya Taifa baadhi ya washindi wa promosheni ya Soka la Afrika watakaokwenda Misri kushuhudia michuano ya mataifa ya Afrika. Kulia ni Afisa Biashara Mkuu wa Tigo Tarik Boudiaf na kushoto ni Meneja Mawasiliano wa Tigo Woinde Shisael.

 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk Yusuf Singo (kushoto) akimkabidhi Kalaghe Rashid (kulia) mbaye ni mmoja wa washindi wa Promosheni ya Soka la Afrika inayoendeshwa na kampuni ya Tigo bendera ya Taifa kwa ajili ya kwenda kushuhudia Michuano ya Mataifa ya Afrika yanayofanyika nchini Misri. Anayeshuhudia katikati ni Afisa Biashara Mkuu wa Tigo Tarik Boudiaf.

 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk Yusuf Singo (kushoto) akimkabidhi Godfrey Muta (kulia) mbaye ni mmoja wa washindi wa Promosheni ya Soka la Afrika inayoendeshwa na kampuni ya Tigo bendera ya Taifa kwa ajili ya kwenda kushuhudia Michuano ya Mataifa ya Afrika yanayofanyika nchini Misri. Anayeshuhudia katikati ni Afisa Biashara Mkuu wa Tigo Tarik Boudiaf




SHULE YA MFANO DODOMA HAIENDANI NA VIWANGO VYA MFANO

$
0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo(Katikati) akiwasilia katika eneo la ujenzi wa shule ya mfano katika Mkoa wa Dodoma inayojengwa katika kata ya IpagalaWaziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akitoa maelekezo wakati wa ziara yake kukagua maendeleo ya shule ya mfano ya Mkoa wa Dodoma inayojengwa katika Kata ya Ipagala Jijini Dodoma. 
……………………. 
Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(Mb) amesema ujenzi unaoendelea wa shule ya mfano inayojengwa Mkoani Dodoma haiendani na viwango vya mfano ambavyo mtu yeyote akija atatambua kuwa hiyo ndio shule ya mfano. 
Akikagua maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo ya Msingi inayojengwa katika Kata ya Ipagala Jijini Dodoma wakati wa ziara yake Waziri Jafo ameyasema alitegemea kukuta kitu kitofauti na alichokikuta eneo la ujenzi kwa sababu Dodoma ndio Makao Makuu ya Nchi. 
“Ujue mpaka shule inapewa hadhi ya kuwa ya mfano inatakiwa iwe ya utofauti mkubwa sana na shule za kawaida kuanzia kwenye ramani ya majengo, ukubwa wa eneo, muonekano wa majengo yanayojengwa, mandhari, viwanja vya michezo na kila kitu kitakachowekwa katika shule hiyo” Amesema Jafo 
Aliongeza kuwa Sasa kwa hapa Ipagala kwanza ukiingia tu unaanza kuona eneo la shule limezingirwa na makazi ya watu kwa karibu sana halafu majengo yanayojengwa yote ni ya chini kama mabehewa ya Treni hamuoni kwa eneo lililopo hapa hamtapata nafasi ya kutosha kwa ajili ya kufanya vitu vingine vya Msingi. 
Aidha Mhe. Jafo alifafanua kuwa “eneo mlilonalo la Ekari saba sio dogo kwa ujenzi wa shule ya kawaida lakini sio lakini kubwa kwa ujenzi wa shule ya mfano yaan hapa mlitakiwe mpate ekari hata thelathini kuwe na nafasi ya kutosha kisha mjenge majengo ya gorofa, vipatikane viwanja vya michezo vizuri, maeneo ya kupumzikia watoto na nyumba za walimu ziwe pembeni kidogo sio vitu vyote visongamane katika eneo moja; 
Hii ni shule ya mfano inatakiwa kuwa na muonekano ambao kila mtu akija hapa atakubali kuwa kweli hapa ni eneo la mfano na wengine watakuja kujifunza kwaiyo sitafurahia kuona vitu vya kawaida kawaida tu lazima mjue kujiongeza”. 
Aliongeza kuwa sitegemei kuona shule hii inafanana na shule ya Msingi Chaduru au Nzuguni B lazima iwe tofauti katika kila kitu, mkifanya mchezo nyie Dodoma ndio mtakuwa tofauti na wenzenu wote wanaojenga shule hizi za Mfano na watawazidi endeleni kufikiria kawaida tu. 
Akizungumza katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Belnith Mahenge alikiri kuwa wataalamu wa Dodoma hawakupanua mawazo yao katika kuangalia namna bora ya kutekeleza ujenzi wa shule ya mfano katika Mkoa wa Dodoma. 
“Nikiri tu kuwa tumekosea na baada ya ziara hii ya Mhe. Waziri tukaa pamoja na wataalamu wetu kuangalia namna gani tunaweza kurekebisha kasoro hizi zilizojitokeza katika ujenzi huu wa Shule ya Mfano ili iwe na ubora unatakiwa katika shule hizi” Alisema Mahenge. 
Naye Mkurgenzi wa Elimu Ofisi ya Rais TAMISEMI Julius Nestory ametaja vigezo vya shule za Mfano kuwa ni Uwepo wa Vyumba vya madarasa kuanzia 17 tofauti na shule za kawaida ambazo zina vyumba sita mpaka tisa na shule hiyo itajengwa eneo lenye idadi kubwa ya watu ambapo pia kutakua na idadi kubwa ya wanafunzi. 
Nestory aliendelea kutaja vigezo vya shule ya mfano kuwa ni uwepo wa miundombinu muhimu kama Nyumba za Walimu, Maktaba, Ukumbi wa Mikutano, Jengo la Utawala, vyoo vya kutosha pamoja na viwanja vya michezo. 
Alimaliza kutaja maeneo ambayo shule hizo zitajengwa Nchini kuwa ni Dodoma eneo la Ipagala, Kigome kule Buhigwe, Geita, Mtwara katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na Mara kwenye shule aliyosoma Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere ambayo ni Shule ya Msingi Mwisenge. 
Naye Afisa Elimu Msingi Jiji la Dodoma Joseph Mabeyo amesema walipokea Tsh Mil 706 mnamo mwezi April 2019 na ujenzi unaondelea utahusisha vyumba vya madarasa 17, Maktaba, Bwalo la chakula, nyumba za walimu, matundu ya vyoo pamoja na Jjengo la Utawala na ujenzi huo unategemea kukamilika Mwezi Agosti, 2019.
Viewing all 110133 articles
Browse latest View live




Latest Images