Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live

MAHAKAMA YAAMURU WEMA SEPETU ATUPWE GEREZANI SIKU NANE

0
0
Na Karama Kenyunko, globu ya jamii

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru msanii wa filamu nchini na Wema Sepetu kukaa gerezani kwa siku nane wakati akisubiri maamuzi ya dhamana.

Wema ambaye ni Miss Tanzanua 2006 ameingia matatani baada ya kutofika mahakamani hapo mara mbili bila ya sababu na mahakama kutoa hati ya kumkamata kwa kuruka dhamana.

Akitoa maamuzi hayo leo Juni 17.2019 Hakimu Mkazi, Maira Kasonde amesema kwa sababu masuala yaliyoletwa mahakamani hapo yanahusu dhamana, atatoa uamuzi Juni 24, mwaka huu kuhusiana na dhamana ya mshitakiwa 

Akijitetea kwanini asifutiwe dhamana, Wema amedai ni kweli hakufika mahakamani Mei 11 na Juni 14, mwaka huu, na kudai mara ya kwanza alisafiri kikazi nje ya mkoa ambapo alikwenda mkoani Morogoro na kwamba alimpa taarifa wakili wake na mara ya pili, alifika mahakamani lakini alishindwa kuingia kwenye chumba cha mahakama kusikiliza kesi yake kwa sababu aliumwa ghafla tumbo la hedhi.

Ameeleza kuwa, inapofika tarehe ya hedhi mara nyingi tumbo humuuma hivyo alienda hospitali kwa ajili ya kuchomwa sindano ya diclopa. Hata hivyo, aliomba mahakama imsamehe kwa kutokuhudhuria mahakamani.

Wakili wa Serikali, Glory Mwenda alidai mahakamani hapo kuwa, mshitakiwa hana rekodi yakutohudhuria mahakamani hivyo aliomba apewe onyo na kueleza kuwa, endapo mshitakiwa atapata udhuru ni vema kuwapa taarifa wadhamini wake ili kuepuka usumbufu kwa mahakama.

Juni 11, mwaka huu upande wa mashitaka ukiongozwa na Wakili Sylvia Mitanto ulidai mshitakiwa hayuko mahakamani na hakuna taarifa yoyote na hivyo mahakama ikatoa amri ya kukamatwa kwa mshitakiwa huyo baada ya kuruka dhamana.

Wema anakabiliwa na mashtaka ya kusambaza video ya ngono katika mitandao ya kijamii kupitia simu yake ya kiganjani ambapo anadaiwa kati ya Oktoba 15, 2018 katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar Es Salaam, alisambaza video za ngono kupitia akaunti yake ya Instagram, picha ambazo inadaiwa kuwa haina maudhui.
 ALIYEKUWA Miss Tanzania 2006  na Msanii wa Bongo Movie Wema Sepetu akipanda basi la magereza tayari kwa kwenda kuishi huko hadi Juni 24.2019  wakati akisubiri maamuzi ya dhamana, baada ya kukiuka masharti.

ALIYEKUWA Miss Tanzania 2006  na Msanii wa Bongo Movie Wema Sepetu akipanda basibla magereza tayari kwa kwenda kuishi huko hadi Juni 24.2019  wakati akisubiri maamuzi ya dhamana, baada ya kukiuka masharti.

ANDENGENYE AFANYA ZIARA YA KIKAZI MKOANI SHINYANGA KUKAGUA UTENDAJI KAZI

0
0
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini Thobias Andengenye amefanya ziara ya kikazi mkoani Shinyanga kwa lengo la kukagua utendaji kazi wa jeshi hilo na kutoa maelekezo mbalimbali kwa watendaji wa jeshi. 

Andengenye amefanya ziara hiyo ya kawaida mkoani Shinyanga kuanzia Juni 16,2019 hadi Juni 17,2019 ambapo pia amekutana na askari ili kujua baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo wakati wakitekeleza majukumu yao ya kila siku. 

“Nimekuja kufanya ukaguzi wa shughuli za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ili kujua changamoto kwa kujionea mimi mwenyewe kutoa maelekezo mbalimbali ya makao makuu ya jeshi kwa watendaji waliopo mikoani pamoja na kukutana na kuzungumza na wadau wetu,maafisa na askari”,amesema Andengenye. 

Aidha amesema jeshi hilo linaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kukabiliana na majanga huku akiwasisitiza wananchi kuweka kwenye nyumba zao vifaa vya kung’amua na kuzima moto. 


Hata hivyo alibainisha kuwa bado kuna changamoto ya vitendea kazi,upungufu wa watumishi na miundombinu isiyo rafiki inayosababisha washindwe kuyafikia baadhi ya maeneo pale matukio yanapotokea 

“Ili kukabiliana na changamoto ya vitendea kazi serikali inaendelea kuchukua hatua kwa kutenga bajeti ili kununua vitendea kazi ikiwemo magari na vifaa vingine vya uokoaji”,aliongeza. 
Kulia ni Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela akimpokea Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye leo Jumatatu Juni 17,2019. Kushoto ni Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga,Omary Simba. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog 
Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela akimzungumza baada ya Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji nchini, Thobias Andengenye kuwasili ofisini kwake.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye akielezea lengo la ziara yake mkoani Shinyanga.
Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela akielezea changamoto zinazolikabili Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga kuwa ni pamoja na uhaba wa magari na nyumba za askari wa jeshi hilo.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye (kulia),akiagana na Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela.
Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga wakijiandaa kumpokea Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye katika makao makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye akiwasili katika makao makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye akizungumza na Waandishi wa habari na Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye akizungumza na Waandishi wa habari na Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga.
Waandishi wa habari na Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye akizungumza na Waandishi wa habari na Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Shinyanga.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

YALIYOJILI BUNGENI DODOMA LEO

0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika, Stephen Masele kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Juni 17, 2019. Wa pili kushoto ni Mbunge wa Viti Maalum, Latifa Chande. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Mbulu Vijijini, Flatei Massay, kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Juni 17, 2019. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo, Bungeni jijini Dodoma, Juni 17, 2019. 


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masala ya Watu Wenye Ulemavu, Stella Ikupa (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, Bungeni jijini Dodoma, Juni 17, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Pwani, Simiyu watia fora fainali za mita 400 UMISSETA

0
0
Na Mathew Kwembe, Mtwara
Mikoa ya Pwani na Simiyu imeibuka vinara kwenye hatua ya fainali za mbio za mita 400 za mashindano ya  Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari (UMISSETA) yaliyofanyika leo katika viwanja vya Chuo cha ualimu Mtwara.

Mwanariadha Benedicto Mathias na mwenzake Amos Charles walijinyakulia medali za dhahabu na fedha kwa kushika nafasi ya kwanza na ya pili kwa upande wa wavulana huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na mwanariadha Ismail Tosil kutoka mkoa wa Dar es salaam.

Mwanariadha Benedicto alitumia sekunde 51:30 kumaliza mbio hizo, na Amos alitumia sekunde 51: 50 huku Ismail wa Dar es salaam alitumia sekunde 52:48 kwenye mbio hizo za mita 400.

Kwa upande wa wasichana, medali ya dhahabu ilichukuliwa na mwanariadha Tereza Bernard kutoka Simiyu ambaye alitumia dakika 1:01:22, huku nafasi ya pili ikichukuliwa na Emmy Hosea wa Singida aliyetumia dakika 1:02:35 na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Rahel Nila kutoka Simiyu aliyetumia dakika 1:03:34.

Katika mchezo wa mbio za kupokezana vijiti wavulana, hatua ya fainali 4 x 400 nafasi ya kwanza ilichukuliwa na mkoa wa Pwani ambao walifanikiwa kujinyakulia medali ya dhahabu baada ya washiriki wake wane kutumia jumla ya dakika 3:39:08 huku nafasi ya pili ikienda mkoa wa Mara ambapo washiriki wake walitumia jumla ya dakika 3:39:22 na nafasi ya tatu ilichukuliwa na mkoa wa Unguja ambapo washiriki wake wane walitumia dakika 3: 40:22.

Katika fainali za mbio za kupokezana  vijiti 4 x 400 nafasi ya kwanza ilichukuliwa na mkoa wa Pwani ambao kwa pamoja wanariadha wake wanne walitumia dakika 4:16:36 na hivyo kuibuka nafasi ya kwanza, huku nafasi ya pili ikichukuliwa na mkoa wa Simiyu ambapo wanariadha wake walitumia jumla ya dakika 4:21:41 na nafasi ya tatu ilichukuliwa na mkoa wa Singida baada ya wanariadha wake wanne kutumia dakika 4: 25:41

Katika hatua ya fainali za mbio za kupokezana vijiti 4 x 100 kwa wavulana nafasi ya kwanza ilichukuliwa na mkoa wa Dar es salaam, nafasi ya pili ilichukuliwa na Unguja na nafasi ya tatu ilichukuliwa na mkoa Mara.

Mara baada ya kumalizika kwa mbio hizo kulifanyika mbio za mita 100 kwa walimu,ambapo baadhi ya washiriki walitia fora kwenye mbio hizo kufuatia umahiri mkubwa waliouonyesha wa kukimbia licha ya umri wao mkubwa.

Mashindano ya UMISSETA yanatarajiwa kufungwa tarehe 21 juni, 2019 na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Prof Joyce Ndalichako katika uwanja wa Nangwanda sijaona Mtwara.
Mshindi wa kwanza mbio za mita 400 Tereza Benard wa simiyu (mbele) akifuatiwa na mshindi wa pili Emmy Hosea kutoka Singida na nyuma yake ni Rahel Nila kutoka Simiyu mara baada ya kumaliza mbio za mita mia 400 leo asubuhi katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara
   Mshindi wa kwanza Benedicto Mathias kutoka Pwani, wa pili Amos Charles  na wa tatu Ismail Tosil wa Dar  wakimaliza mbio za mita 400 wavulana asubuhi katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara.
Baadhi ya wanariadha wa mbio za kupokezana vijiti kutoka mikoa iliyotinga hatua ya fainali wakipokea maelekezo kutoka kwa wasimamizi wa mchezo wa riadha kabla ya kuanza mbio hizo leo asubuhi katika viwanja vya chuo ncha ualimu Mtwara

MILLYA AWASHUKURU SUKURO NA KITIANGARE KUMALIZA MGOGORO WA MIAKA 20

0
0

Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, James Ole Millya akizungumza juu ya upendo na kuondokana na makundi na ubaguzi ili lengo la kuwa na Simanjiro moja yenye amani na kutobaguana itimie.
Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara, James Ole Millya akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Sukuro alipotembelea eneo hilo.
Mbunge wa jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara, James Ole Millya akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Kitiangare. 

***************************** 




MBUNGE wa Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara, James Ole Millya amewashukuru wananchi wa Vijiji vya Sukuro na Kitiangare waliomaliza mgogoro wao uliodumu zaidi ya miaka 20 wakigombea Kitongoji cha Katikati. 

Mgogoro huo ulishasababisha mtafaruku mkubwa baina ya aliyekuwa mkuu wa mkoa huo Henry Shekifu na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Christopher Ole Sendeka mwaka 2010. 

Ole Millya akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sukuro na Kitiangare aliwapongeza wananchi wa vijiji hivyo viwili kwa kuridhia kwa pamoja na kuachana na malumbano na mgogoro usiokuwa na tija kwao. 

Alisema katika mgogoro huo yeye binafsi alikaa pembeni bila kupendelea kijiji chochote kwani vyote viwili ni vya kwake hivyo hakupaswa kupendelea kimoja aliwaachia wataalamu wagawe vitongoji kama sheria inavyoelekeza. 

“Nawapongeza sana wananchi wa vijiji vya Kitiangare na Sukuro kwani hali ya amani haikuwepo lakini sasa mmemaliza mgogoro wenu na kuridhia kwa pamoja kuishi kama ndugu kwani mlikuwa kijiji kimoja kabla ya kugawanywa,” alisema Ole Millya. 

Alisema hivi sasa hali ya amani na upendo imerejea baina ya vijiji hivyo viwili kama awali na wananchi wanasalimiana kwa furaha, wanaoleana na kunywa maji pamoja. 

Alisema kupitia mfuko wa jimbo anatoa sh6 milioni kwa vikundi vya wanawake wa vijiji vyote viwili na sh4 kwa mradi wa maji kijiji cha Sukuro na darasa la shule ya kijiji cha Kitiangare. 

Mkazi wa kijiji cha Sukuro, Lengai Ole Makoo alipongeza hatua ya kumalizika kwa mgogoro huo usiokuwa na tija uliosababishwa na baadhi ya wanasiasa wa wilaya hiyo. 

Ole Makoo alisema kijiji cha Sukuro kimebakiwa na vitongoji vyake vitano na kijiji cha Kitiangare kimebaki na vitongoji vyake viwili kama ambavyo kanuni, taratibu na sheria zilivyofuatwa wakati kijiji mama cha Sukuro kilipogawanywa. 

“Kijiji cha Sukuro kimebaki na vitongoji vya Katikati, Lembutwa, Lenjani, Mouwara na Lasepa na Kitiangare imebaki na vitongoji vya Loongung na Kitiangare,” alisema. 

Hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti alimpa onyo Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Awadhi Omary na baadhi ya wanasiasa juu ya kutumika kwa maslahi yao katika mgogoro huo.

MABADILIKO MAKUBWA UJIO MPYA WA SHINDANO LA MISS UTALII TANZANIA

0
0
Shindano la Miss Utalii Tanzania, nimoja ya mashindano yenye mafanikio makubwa katika medani za kimataifa barani Afrika, tangu kuanzishwa kwake na kufanyika kwake kwa mara ya kwanza nchini mwaka 2004, hadi lilipo sitishwa na bodi ya mashindano haya Julai 2013,na kufungiwa kwa muda na Baraza la Sanaa la Taifa Oktoba 2013.

Ubora wa shindano hili unatokana na kuwa ndilo shindano pekee nchini ambalo limetwaa mataji katika mashindano yoyote ya dunia na kimataifa tuliyo shiriki kuanzia mwaka 2005 hadi 2013 tulipo shiriki kwa mara ya mwisho. Ni shindano hili pekee ambalo mafanikio yake kimataifa yaliipa Tanzania heshima ya kihistoria ya kuwa wenyeji wa fainali za Dunia ,za Miss Utalii Dunia 2006,zilizo fanyika 11, Machi 2006 katika ukumbi wa Ubungo Plaza, ambapo zaidi ya nchi 100 zilishiriki huku fainali hizo zikionyweshwa LIVE duniani kote kutokea Tanzania.

Kubwa zaidi ni kuwa shindano la kwanza na kwa mara ya kwanza Tanzania kabla na baada ya uhuru kutwaa taji la Dunia la urembo, hivyo kuingiza Tanzania katika ramani ya Dunia ya nchi zenye mafanikio makubwa katika tasnia ya urembo, pale Miss Utalii Tanzania 2004, Witness Manwingi alipo twaa taji la Dunia la Miss Tourism World 2005 – Africa, katika shindano lililo shirikisha nchi 118, huko Harare Zimbabwe. 

Na sasa baada ya mabadiliko ya mfumo wa uongozi na mfumo wa shindano, shindano hili linaandika historia nyingine kubwa ya kuwa shindano la kwanza la kimataifa Tanzania, likishirikisha washirikiki zaidi ya 140,40 wakiwakilisha kanda na mikoa ya Tanzania kuwania taji la taifa la Miss Utalii Tanzania na 100 wakiwakilisha nchi mbalimbali Duniani kuwania taji la kimataifa la Miss Tourism Tanzania International.

Kwa miaka zaidi ya mitano, tangu shindano hili lilipo fanyika kwa mara ya mwisho, uongozi na bodi ya shindano hili kwa kushirikiana na asasi mbalimbali za kitaifa na kimataifa, ikiwemo Baraza la Sanaa la taifa (BASATA) na taasisi ya kimataifa ya World Beauty Pageant Association (WBPA) tume kuwa tukifanya marekebisho na maboresho mbalimbali ya mfumo wa uongozi, mfumo wa mashindano, kanuni na taratibu za mashindano, kwa kuzingatia vigezo na maelekezo ya BASATA na WBPA,lakini pia kufikia Viwango vya kimataifa vya mashindano ya urembo na mitindo.

Matokeo ya juhudi hizo ni mabadiliko ya kihistoria ambayo yamelifanya shindano hili sasa kuwa pekee nchini lenye mfumo wa kitaasisi wa uongozi, mfumo wa kimataifa wa mashindano, kanuni na taratibu za mashindano zinazo kidhi viwango vya kimataifa na kitaifa, yenye kuzingatia tamaduni, mila na desturi za kitanzania na kiafrika, hivyo shindano hili kuwa la kimataifa la Miss Tourism Tanzania International Pageant. Mabadiliko ambayo yamekidhi masharti na vigezo vyote vya Baraza la Sanaa la taifa (BASATA),ikiwemo ya kuboresha mfumo wa uongozi na wa mashindano, hivyo kulifanya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), kubariki mabadiliko na maboresho hayo ,na kulifungulia na kuruhusu kuendeleza kufanyika shindano hili kwa barua yake tarehe 22 Januari,2019 yenye kumbukumbu namba BST/PR/MT784/27. Kufuatia Baraza la Sanaa la Taifa kubariki maboresho na mabadiliko hayo:

Shindano hili sasa ni shindano la kimataifa la Miss Utalii Tanzania (Miss Tourism Tanzania International Pageant), litakuwa na washiriki wa kitaifa na wa kimataifa wakiwakilisha nchi zao. Fainali za kimataifa za Miss Utalii Tanzania, (Miss Tourism Tanzania International Pageant), zitafanyika Tanzania kila mwaka, na kushirikisha zaidi ya washiriki miamoja (100) kutoka nchi miamoja (100) duniani kote, hii ni fulsa nyingine kwa Tanzania kujitangaza kimataifa na katika nchi zote ambazo zita shiriki shindano hili, ikiwa ni faida zaidi kwa Tanzania kuliko kupeleka washiriki kushiriki mashindano katika nchi nyingine.

Shindano hili sasa limekuwa na kalenda ya kudumu ya mashindano, likiwa ni sehemu ya maazimisho ya kitaifa ya sherehe za uhuru wa Tanzania, ambapo fainali za kanda zitafanyika kati ya Julai na Novemba,za kitaifa na kimataifa zitafanyika siku ya mkesha wa sherehe za uhuru tarehe 8 Disemba kila mwaka. Kalenda hii ya mashindano imezingatia uwepo wa mashindano mengine nchini na kimataifa kila mwaka. 

Washiriki wa fainali za kanda ni wawakilishi wa mikoa katika kila kanda, ambao ni washindi wa 1-5 wa kila mkoa, ambao wata patikana kwa njia ya udahili mahususi utakao fanyika chini ya bodi za kanda za mashindano haya, ambazo zinaundwa na wakurugenzi wa mashindano wa kanda, maafisa utamaduni, maafisa ustawi wa jamii, maafisa Maliasili na Misitu wa mikoa iliyopo katika kanda husika. Washiriki wa fainali za kitaifa na kimataifa ni washindi 1-5 wa kanda, na washindi wa 1,2 au wa tatu wa shindano lolote la kitaifa kutoka nchi zote duniani.

Mikoa yote ya Tanzania bara na visiwani imegawanywa katika kanda maalum nane (8) za mashindano haya, kwa kuzingatia uwiano wa kijiografia, kitamaduni na uwepo wa vivutio vya utalii katika mikoa husika kama ifuatavyo: Miss Tourism Northern Zone (Manyara, Arusha, Kilimanjaro), Miss Tourism Southern Zone (Ruvuma, Lindi, Mtwara, Morogoro), Miss Tourism Swahili Coast Zone (Coast, Dar es Salaam, Tanga), Miss Tourism Western Zone(Kigoma, Tabora, Katavi), Miss Tourism Lake Zone (Kagera, Mwanza, Mara, Geita, Simiyu), Miss Tourism Central Zone (Dodoma, Singida, Shinyanga), Miss Tourism Southern Highlands (Mbeya, Rukwa, Iringa, Njombe), Miss Tourism Eastern Zone (Unguja na Pemba).

Fainali zote za kanda zita rushwa mbashara (LIVE) kupitia Televisheni na mitandao ya kijamii kitaifa na kimataifa, huku ikitangaza vivutio vya utalii, Utamaduni, Uwekezaji, Wanyamapori, Mazingira na kuhamasisha utalii wa ndani, kitamaduni, kimichezo na kimikutano ya kanda na mikoa yote ya kanda husika. Fainali za taifa na kimataifa zitarushwa mbashara (LIVE) kimataifa na kuangaliwa LIVE na watazamaji zaidi ya milioni 750 duniani kote, huku vivutio vya Tanzania vya utalii, utamaduni, uwekezaji, Mazingira, Misitu, Wanyama pori na fukwe vikitangazwa kitaifa na kimataifa duniani kote. Fainali za ngazi zote za kanda, Taifa na kimataifa, zitafanyika katika awamu mbili, ya Fainali za Tuzo za Utalii, Hifadhi za taifa, Hifadhi za Bahari, Mapori ya akiba, Utalii wa ndani, Utamaduni, Vipaji ,Jamii, Wanyamapori, Mazingira, Uwekezaji, Mitindo, Michezo, Wadhamini, Biashara, Viwanda na Uchumi.

Tofauti na mashindano mengine ya urembo nchini, shindano hili ni la urembo wa kitalii na kitamaduni ambalo ni zaidi ya shindano la urembo kwani ni tafsiri ya vitendo ya sera za Taifa za Utalii, Utamaduni, Uwekezaji, Mazingira, Misitu, Wanyama Pori, Michezo na Mazingira, ambalo lina lenga katika kuhamasisha na kutangaza Utalii, Utamaduni na Utalii wa Kitamaduni, Uwekezaji na Mianya ya Uwekezaji, Wanyamapori na Vita Dhidi ya Uwindaji Haramu, Mazingira na Uharibifu wa Mazingira, Michezo na Utalii wa Michezo, Kumbi za Mikutano na Utalii wa Mikutano, Hifadhi za Bahari na utalii wa Bahari, Vita dhidi ya Tamaduni kongwe na Potofu, Ujasiliamali na Ujasiliamali wa Kitalii ,vita dhidi ya Ujinga, Umasikini na Maradhi, Viwanda na Bidhaa za Tanzania.

Mavazi ya mashindano haya ni yale yaliyo buniwa na wabunifu wa Kitanzania kwa malighafi zinazo zalishwa na kupatikana Tanzania tu, ambayo haya mdhalilisha mvaaji wala mtazamaji na yenye kuzingatia mila ,desturi na tamaduni za kitanzania. Sifa kuu za washiriki wa shindano hili ni pamoja na kuwa msichana kwa asili mwenye Elimu isiyo pungua kidato cha sita, cheti cha chuo au zaidi, mwenye ngozi ya asili, uraia wa nchi yake kwa mujibu wa sheria, urefu wa angalau sentimita 168 japo ni vyema zaidi ikiwa ni sentimita 174 au zaidi, afya njema ya akili na mwili, tabia njema, tegemeo na mfano wa kuigwa katika jamii, dira, dhamira na mguso nafsi kwa jamii na Taifa ya kushiriki shindano hili (Vision, Mission and Platform).

Bodi mpya ya mashindano inaundwa na Erasto Gideon- Mwenyekiti Mtendaji, Georgina Saulo- Mkurugenzi wa Mashindano na Matukio, Wakili Msomi Noel Shani- Mkurugenzi wa Sheria na Mahusiano ya Kimataifa, Wakili Msomi Jonson Kaijage- Mkurugenzi wa Protokali, Mahusiano na mawasiliano ya Umma , Wakili Msomi Anna Marealle-Mkurugenzi wa Ufundi,Utafiti na Ushauri, na Judith Masawe-Mkurugenzi wa Mafunzo, Viwango na Ukuzaji Vipaji. Shindano hili kuanzia mwaka huu, litaratibiwa na Taasisi ya Africa Tourism Promotion Centre (ATPC), ambayo ina uzoefu mkubwa wa uratibu wa matamasha na matukio ya promosheni za utalii kitaifa na kimataifa, ikiwemo ya World Tourism Awards, Tanzania Tourism Awards, Miss Tourism University World, National Parks International Marathon, World Great Safari Tour, Tanzania Great Safari Tour, Wildlife International Marathon, World Tourism Music Awards, Tanzania Tourism Music Awards, na Ant Poaching International Marathon, Cultural , Conference and Sports Tourism International Life Party. Kabla ya hapo shindano hilo lilikuwa likiratibiwa na Miss Tourism Tanzania Organisation moja kwa moja, kabala ya kuanza mfumo mpya wa mashindano haya ya kipekee nchini.



Miss Utalii Tanzania Alama ya Urithi wa Taifa, Utalii ni Maisha – Utamaduni ni Uhai


























JE WAJUA KIJIJI KINACHOONEKANA KWA MWEZI MMOJA KILA MWAKA NCHINI INDIA

0
0
 Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
CURDI ni kijiji kinachopatikana katikati ya milima huko magharibi mwa Ghats karibu na mto Salaulim, kijiji hicho kiliwahi kuendelea kiasi cha kujizolea umaarufu sana katika jimbo hilo la Goa.

Jarida la Indian Express limeeleza kuwa kijiji hicho kilianza mwaka 1980 na hufunikwa kwa maji katika miezi ya Aprili hadi Mei.

Jarida hilo limeeleza kuwa kijiji hicho ni kivutio kikubwa kutokana na uwepo wa fukwe mbalimbali za kuvutia.

Kinachostaahabisha na kuvutia wengi kuhusiana na kijiji hicho ni kupotea kwake kwa muda wa siku 335 sawa na   miezi 11 kwa kuzama kwenye maji na kuibuka baadaye.

Wakazi waishio Curdi huamishiwa katika vijiji jirani na baada ya kijiji hicho kuibuka hurudi na kusherekea urejeaji wa kijiji chao huku mabaki ya nyumba na mali zilizoachwa zikionekana.

Wafanyabiashara wahakikishiwa usalama katika Biashara zao.

0
0
MKUU wa Jeshi la Polisi mkoani Mwanza Jumanne Murilo amewahakikisha usalama wa pesa na mali zao.Akizungumza na  wafanyabiashara katika Jukwaa la business club,Jeshi lake limejipanga imara kuhakikisha wanafanyabiashara hawasumbuliwi na wahalifu.

 Aliwaomba wafanyabiashara mkoani hapa kuhakikisha wanatumia vyema jukwaa la Business Club katika kuhakikisha wanajenga uchumi imara wa nchi.
'"tumejipanga na tunapambana kuzuia uhalifu kabla haujatokea kuliko kukabiliana nao ukishatokea " Murilo alisema.

Alisema wafanyabiashara wasiwe na wasiwasi bali wahakikishe wanafanya biashara zao kwa uhuru kwakuwa jeshi lake limejipanga vyema kuhakikisha hakuna masuala ya uhalifu.Kwa upande wake,mkuu wa kitengo cha Biashara cha benki ya NMB makao makuu,Donatus Richard alisema benki yao itaendelea kutoa elimu kwa wafanyabiashara kupitia ‘Business Club’

Alisema kupitia elimu watakazokuwa wanatoa kwa wafanyabiashara zitakuwa zikiwasaidia sana wafanyabiashara katika shughuli zao za kila siku.Donatus alisema kwa sasa benki yao itaendelea kuwa karibu na wateja wao na alisema wataendelea kutoa mafunzo mbali mbali kwa wateja wao yakiwemo masuala ya masoko pamoja na kodi.

Alisema semina zao pia zimewasaidia wateja wao kuwa karibu na wateja wenzao ambapo jambo linalodumisha uhusiano mwema katika ufanyaji biashara zao.

Alisema kwa sasa benki yao ipo katika mikakati ya kuwapeleka wafanyabiashara 10 nchini China kwajili ya kuwenda kujifunza mambo ya kibiashara katika tamasha la biashara litakalo fanyika nchini humo katika mwezi wa 10,mwaka huu.Mmoja ya wafanyabiashara,Kejja Misungwi alisema anaiomba benki ya NMB kuhakiksha wanaendelea kutoa semina za mara kwa mara kwa wateja wao jambo ambalo litawasaidia wateja kupata elimu za biashara zitakazowawesha upatakinaji wa faida katika biashara zao.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Jumanne Muliro, akizungumza na wajasiliamali na wafanyabiashara ambao ni wajumbe wa NMB Business Club ya mkoani Mwanza, jinsi walivyojipanga kuwalinda watu,mali na biashara zao wakati wa mkutano wa kuwajengea uwezo wajumbe hao,kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela Godfrey Mzava na Mkuu wa kitengo cha Biashara wa NMB Makao Makuu Donatus Richard(kulia).
Mkuu wa kitengo cha Biashara wa NMB Makao Makuu Donatus Richard, akizungumza na wajasiliamali na wafanyabiashara ambao ni wajumbe wa NMB Business Club ya mkoani Mwanza, wakati wa mkutano wa kuwajengea uwezo wajumbe hao,kushoto ni Mwenyekiti wa Club hiyo anayemaliza muda wake Mathiasi Rwechungura na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela Godfrey Mzava.

MFANYABIASHARA AFIKISHWA KORTIN KWA KUDAIWA KUSAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA

0
0
Na Karama Kenyunko globu ya jamii.

MFANYABIASHARA Andres Uribe amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka moja la  kusafirisha dawa za kulevya aina ya Cocaine Hydrochloride.

Uribe amefikishwa mahakamani hapo leo Juni 17,2019 ambapo amesomewa shtaka lake tmbele ya Hakimu Mkazi, Augustine Mmbando.

 Wakili wa Serikali, Gloria Mwenda amedai kuwa Agosti 11, 2014 katika Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere (JNIA), mshtakiww alisafirisha dawa za kulevya aina ya Cocaine Hydrochloride zenye uzito wa gramu 904.7 ambayo yana thamani ya Sh milioni 63.3.

Hata hivyo, mshtakiwa hakutakiwa kujibu chochote mahakamani hapo kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za dawa za kulevya.

Kwa mijibu wa upande wa mashitaka,  upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na  kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai Mosi, mwaka huu kwa kutajwa na mshitakiwa amerudishwa rumande.
 MFANYABIASHARA Andres Uribe alipofikishwa  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo  akikabiliwa na shtaka moja la  kusafirisha dawa za kulevya aina ya Cocaine Hydrochloride.

Waalimu Vyuo Vya Uuguzi, Maabara, Utabibu Tabora Waomba Mikopo Serikalini.

0
0
Na, Editha Edward-Tabora

Waalimu wa Vyuo vya Uuguzi, maabara, Utabibu pamoja na Afya ya jamii wameiomba Wizara ya Afya Maendeleo Ya jamii jinsia wazee na Watoto  kuangalia uwezekano wa kufanya mapitio ya sheria ya mikopo kwa Vyuo vya afya ngazi ya Astashahada na Astashahada  kupata mikopo ili iweze kukidhi  kutoa Elimu dhidi ya wanafunzi wanashindwa kumudu gharama za masomo

Ameyasema Hayo mkuu wa chuo cha Sayansi za Afya Nkiga Mkoani Tabora Robert Masano  katika mahafali ya Tano yaliyofanyika leo katika chuo hicho

Dkt. Jackson Kaluzi Mwenyekiti wa bodi ya taasisi ya sayansi Nkiga amesema"kama inawezekana Serikali iangalie suala hili katika Jicho la tatu kwa Sababu hawa ni watanzania hapa Tunaona wakati mwingine vijana wanapata shida kulipa ada inabidi wakati mwingine, Mwanzoni tulikuwa na ufadhili kutoka ulaya Lakini kadri siku zinavyoenda inaonekana hatupati ufadhili wa kutosha "Amesema Kaluzi

Hindu  Salumu na Amani Azack ni baadhi ya wahitimu wa Ngazi ya Astashahada na Stashahada ya Uuguzi na  maabara katika chuo hicho wamesema Tatizo la mikopo linawapelekea baadhi ya wanafunzi kurudi nyumbani kwa kukosa Ada na  na wengine kurudia muhula na kukosa pesa ya mahitaji  madogo madogo

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwaipopo amesema amelipokea suala hilo na ataliwakilisha sehemu husika ili kila Mwanafunzi anayesomea fani za utabibu Uuguzi Afya ya jamii waweze kupewa 
 Mkuu wa chuo cha Sayansi Nkinga Robert Masano akieleza ugumu uliopo katika kuendesha kozi hizi za afya bila mikopo.
 Darubini zinazotumika kupima vijidudu visivyoonekana kwa macho ya kawaida.
 Wahitimu wa fani ya utabibu Uuguzi maabara na Afya ya Jamii wa chuo cha Sayansi za Afya Nkiga wakitunukiwa vyeti.

Call to Design Corporate Logo for the EAC 20 Anniversary

0
0

East African Community


Consultancy ON DESIGN OF THE EAC 20TH ANNIVERSARY CORPORATE LOGO


1.0Introduction


The EAC is set to mark its 20thAnniversary with various activities and events culminating into EAC Day on 30thNovember, 2019, the date of the 21st Ordinary Summit of the EAC Heads of State.


2.0 Objective


For purposes of publicity and branding, the Community requires a logo to brand its 20th Anniversary celebrations. The EAC Secretariat intends to engage a creative artist or graphic designer to come up with a logo for the anniversary.


The graphic designer will be required to provide the following:


i)   Three designs of the proposed 20th Anniversary Logo from which the Secretariat can select;

ii)  Three soft copies of the proposed 20thAnniversary Logo from which one will be selected for use during the 20thAnniversary;

iii)Three hard copies of the proposed logo; and

iv)Designs that are usable in multimedia channels (print, electronic, social media, etc.)


4.0 Qualification / Competencies required


(a)  A Senior Expert/Design Firm who has at least 10 years previous experience in graphics design, new brand creation and logos development

(b)  A Senior Expert/Design Firm who has directed or supported at least two re branding activities

(c)  A Senior Expert/Design Firm who has strong experience in creating visual campaigns 

(d)  Bachelor’s Degree in Graphics design, brand development, business administration or other relevant fields. A Master’s Degree will be preferred but is not mandatory. 

(e)  Must be an East African national/East African based Brand Design Firm


5.0 Submission Requirements


(a)  Application Letter/Expression of Interest

(b)  CV of key experts to be involved with references for previous assignments

(c)  Previous design portfolio (new logo/brand design development, not more than 20 pages)

(d)  Proof of minimum two previous similar assignments undertaken.


Interested Brand Design Experts/Firms should submit Technical and Financial proposals by email to Procurement@eachq.org not later than 26th June, 2019.


Ofisi ya Waziri Mkuu Yawajengea Uwezo Watumishi Wake Wanaotarajia Kustaafu

Waziri Mwakyembe Azindua Kampeni ya Kuichangia Timu Ya Taifa “Taifa Stars”

0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amezindua rasmi kampeni maalumu ya kuchangia timu ya Taifa “Taifa Stars” inayoshiriki mashindano ya Kombe la Maifa ya Afrika (AFCON) yanayotarajiwa kuanza Juni 21 nchini Misri.
Waziri Mwakyembe amesema watanzania hawana budi kuchangia kiwango chochote na kwamba fedha hiyo itakuwa salama na itawafikia wachezaji hao bila ya mizengwe yoyote.

"Watanzania kote nchini wanaweza kuichangia timu yao  kupitia akaunti zifuatazo BMT N BC 011101000978, Sport Development Fund, CRDB 01J1019956700 na Voda *150*00#5595298. Ukichangia, ujumbe unaopata utume  kwenda 0735 414043 jina litakuja Oscar Zabloni ambye ni mweka hazina ,'' amesema Dkt. Mwakyembe.

Amesema wote watakaochangia watapewa cheti  maalumu na  kiongozi wa kitaifa ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao katika kuhakikisha timu yetu ya Taifa inafanya vizuri katika mashindano hayo.

Naye mwenyekiti wa kamati ya kusaidia Taifa Stars, Paul Makonda amesema siku ya Jumamosi Juni 22, 2019 mkoa wa Dar es Salaam utafanya maombi maalum kwa ajili ya  kuiombea timu ya Taifa Stars ambayo inatarajia kushuka dimbani siku ya Jumapili Juni 22 dhidi ya timu ya Taifa ya Senegal.
Pamoja na mambo mengine Makonda amezitaka kampuni 41 zilizoahidi kuchangia Taifa Stars kutoa michango hiyo.

"Jumamosi ya Juni 22,2019 Mkoa wa Dar es Salaam tutafanya maombi maalum kuiombea timu ya Taifa Stars, na pia nitumie nafasi hii  kuyakumbusha  makampuni  yaliyoahidi kuichangia Taifa Stars sasa wachangie kupitia akaunti hizo,'' amesema Makonda.
Timu ya Taifa Stars iko kundi C, pamoja na timu za Senegal, Algeria na Kenya ambapo siku ya Jumapili inatarajia kutupa karata yake ya kwanza dhidi Senegal.

Tayari Stars imeshacheza mechi mbili za kirafiki za kujipima nguvu, huku ikipoteza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Misri 1-0 na kutoka sare ya goli 1-1 dhidi ya Zimbabwe.
 Katibu wa Kamati ya kuisadia timu ya Taifa “Taifa Stars”, Mhandisi Hersi Said (kulia)  akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa harambee maalum ya kuichangia timu hiyo mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe na katikati ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Paul Makonda.
 Mwenyekiti wa Kamati ya kuisaidia timu ya Taifa “Taifa Stars”, Paul Mokonda akimkaribisha Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya kuichangia timu ya Taifa inayoshiriki mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) nchini Misri.
 Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (wa pili kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya kampeni maalum ya kuichangia timu ya Taifa “Taifa Stars” inayoshiriki mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) nchini Misri.
 Mbunifu wa mavazi akionesha kwa waandishi wa habari vazi maalum kwa ajili ya washangiliaji wa timu ya Taifa “Taifa Stars”, inayoshiriki mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) nchini Misri.
 Mwenyekiti wa Kamati ya kuisaidia timu ya Taifa “Taifa Stars”, Paul Mokonda (katikati) akijaribu vazi maalum kwa ajili ya washangiliaji na mashabiki wa timu ya Taifa “Taifa Stars”, inayoshiriki mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) nchini Misri.
 baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini uzinduzi wa kampeni maalum ya kuichangia timu ya Taifa “Taifa Stars” inayoshiriki mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) nchini Misri.
Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (wa tatu toka kushoto) akimkabidhi cheti Mwenyekiti wa Kamati ya kuisaidia timu ya Taifa “Taifa Stars”, Paul Mokonda kwa kutambua mchango wake katika kufanikisha kufuzu kwa timu hiyo katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) nchini Misri.
Picha na WHUSM – Dar es Salaam.
17/06/2019


TCRA yaweka kituo kimoja katika usajili wa laini za simu kwa alama za vidole katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam

0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Katika kuadhimisha wiki ya Utumishi kwa Umma Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA Kanda ya Mashariki kwa kushirikiana na Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa  NIDA pamoja na kitengo cha polisi makosa ya mtandaoni wamefungua kituo cha pamoja kwa lengo la kuwarahisishia wananchi usajili laini  za simu kwa kutumia alama za vidole.

Maadhimisho hayo ni muhumu kupata huduma za mawasiliano katika mwamvuli mmoja pamoja na kupunguza gharama za usafiri.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam katika Viwanja vya Mnazi Mmoja kwenye maadhimisho hayo  Kaimu Mkuu wa TCRA Kanda ya Mashariki  Mhandisi Jumanne Ikuja amesema kuwa usajii huu utasaidia  kukomesha wizi wa mtandaoni kwani kila mwananchi atatakiwa kumiliki laini moja kwa kila Mtandao wa kampuni ya simu.

Aidha amewata wananchi wanaopoteza vitambulisho vyao kuhakikisha kuwa wanaripoti polisi ili kuweza kurudishiwa vitambulisho vingine katika kuepuka  kutumiwa kwenye matukio ya kihalifu.

Mhandisi Ikuja  amewasisitiza wananchi kufika katika viwanja vya mnazi ili kupatiwa huduma mbalimbali zinazohusiana na Mawasiliano kwani zoezi hilo ni la wiki moja kuanzia Juni 17- 21 mwaka huu.

Kwa upande wake  Mkaguzi Msaidizi wa polisi Kitengo Cha makosa ya mtandaoni Inspekta Edga Masawe amewatahadharisha wa anchi kuacha kutumia simu ambazo wamezinunua kiholela haswa kutoka kwa watu pamoja na zile wanazoziokota ikiripotiwa ni unachukuliwa kama mhalifu.

Hata hivyo amesema kuwa kupitia maadhimisho ya wiki ya utumishi watatoa elimu kwa wananchi kuhusu sheria za mtandaoni pamoja na  madhara ya matumizi mabaya ya mtandao ikiwemo matumizi ya lugha isiyokuwa na staha na picha zisiokuwa na maadili na maneno ya uchochezi.
 Kaimu Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi Jumanne Ikuja akizungumza na waandishi habari kuhusiana na TCRA na wadau wengine kuungana katika kutoka huduma za usajili wa laini za simu kwa alama za vidole katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.
 Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Kitengo cha Makosa Mtandaoni Edga Massawe akizungumza kuhusiana na Makosa Mtandaoni kwa waandishi habari na kutaka wananchi waende kupata maelezo  katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.
 Wananchi wakipata huduma katika kampuni za simu.
 Wananchi wakipata huduma katika kampuni ya simu ya TTCL katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.
 Afisa wa TCRA Kanda ya Mashariki Annastella Mchomvu akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea banda TCRA katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.



Picha mbalimbali za matukio katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam.

Klabu Ya Yanga Kupatiwa Uwanja Kigamboni

0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kulia) akifafanua jambo kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) wakati Mkuu wa mkoa huyo alipokuwa akipokea nyaraka mbalimbali toka kwa viongozi wa Yanga ili kukamilisha ununuzi wa kiwanja cha klabu hiyo mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga Bw. Omar Kaya.
 Baadhi ya viongozi wa klabu ya Yanga wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (hayupo pichani) wakati Mkuu wa mkoa huyo alipokuwa akipokea nyaraka mbalimbali toka kwa viongozi hao ili kukamilisha ununuzi wa kiwanja cha klabu hiyo mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kulia) akipokea baadhi ya nyaraka toka Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Dkt. Mshindo Msolla ili kukamilisha ununuzi wa kiwanja cha klabu hiyo mapema hii leo jijini Dar es Salaam, wanaoshuhudia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (wa pili kulia) na Kaimu Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga Bw. Omar Kaya.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwapongeza viongozi wa klabu ya Yanga (hawapo pichani)  kwa hatua waliyofikia katika ununuzi wa uwanja, kulia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga Bw. Omar Kaya.

IDDI NADO ASAINI MIAKA MIWILI AZAM FC

0
0
KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imekamilisha usajili wa winga Idd Seleman 'Nado', kutoka Mbeya City.

Nado ambaye ataanza kuitumikia timu hiyo msimu ujao, amesaini mkataba wa miaka miwili leo jioni mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim Amin 'Popat' na Mratibu wa timu, Phillip Alando.

Usajili wa winga huyo aliyeifungia Mbeya City mabao 10 msimu uliopita, ni sehemu ya mapendekezo ya Kocha Mkuu mpya wa Azam FC, Etienne Ndayiragije.

Huo ni usajili wa kwanza mpya kwa Azam FC, ambayo kwa mujibu wa ripoti ya kocha mpya, anahitaji nyota wapya wanne tu, wawili wakiwa wazawa na wawili kutoka nje.

Nado anatarajia kuungana na wachezaji wengine wa Azam FC waliopo kwenye kikosi hicho, katika maandalizi ya msimu mpya yatakayoanza Alhamisi hii.

Ufafanuzi wa Tuhuma Dhidi Ya Maafisa wa Takukuru

BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 17.06.2019

Bandari kiwira kuongeza Mapato hadi shilingi 3.6bn/- kwa mwaka

0
0
Na Humphrey Shao, Kyela
Upanuzi wa bandari ya Kiwira iliyopo wilayani Kyela mkoani Mbeya unatarajia kuongeza mapato ya bandari za Ziwa Nyasa kutoka wastani wa Sh milioni 300 kwa mwaka hadi kufikia Sh bilioni 3.6.

Hayo yameelezwa na Meneja wa Bandari za Ziwa Nyasa, Abeid Galus, wakati akizungunza na waandishi wa habari waliofika kuangalia Miradi ya Maendeleo inayofanywa na mamlaka ya bandari katika Ziwa Nyasa.

"Upanuzi huu unahusisha ujenzi wa sakafu ngumu katika eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 11,000 ambalo litakuwa na uwezo wa kuhifadhi makaa ya mawe tani 10,000 kwa wakati mmoja.  Upanuzi huo utaongeza kasi ya upakuaji wa meli tofauti na sasa ambapo meli husubiria malori yanayobeba makaa ya mawe kupeleka viwandani" amesema Galusi.

Amesema kwa sasa meli moja yenye uwezo wa tani 1000 inatumia siku tisa kushusha mzigo badala ya siku moja kama ukishushwa eneo na kuhifadhia wakati ukisubiri malori ya kuubeba.

"Ujenzi huu wa eneo la kuhifadhia mizigo utaiongezea bandari mapato kwa zaidi ya mara 100," amesema Galus.

Amesema kwa sasa bandari hiyo inahudumia wastani wa tani 5000 kwa mwaka na kiingiza mapato ya wastani wa Sh milioni 230.

"Tunatarajia baada ya upanuzi huu mwaka ujao wa fedha tutahudumia tani 72,000 kwa mwaka na kuingiza mapato ya sh bilioni 3.6,"

Aliongeza kuwa bandari hiyo pia inaongeza gati na kulifanya liweze kuhudumia meli 3 kwa wakati mmoja tofauti na sasa ambapo linahudumia meli moja tu.

Alisema miradi hiyo ambayo inahusisha pia ujenzi wa jengo la mgahawa na ofisi unagharimu bilioni 1.25 na unatarajiwa kukamilika Septemba mwakani.

Aidha Meneja huyo alisema katika kuongwza ufanisi wa huduma za bandari Mamlaka hiyo imenunu mizani mbili ambapo moja itatumika katika bandari ya Kiwira na nyingine katika bandari ya Ndumbi.

"Mizani hii itasaidia kuwa na uhakika wa uzito wa mizigo inayoingia na kutoka bandarini pia itasaidia kuongeza usalama wa vyombo vya majini kwa kutozidisha mizigo na kuondokana na kizama kwa meli," alisema Galus.

Aliongeza kuwa bandark hiyo imeongezewa vifaa vya kifanyia kazi zikiwemo mashine mbili (wheel loader) kwaajili ya kupakia na kushusha makaa ya mawe ambapo moja imepelekwa Ndumbi na nyingine imewekwa Kiwira.

Alisema pia zimenunuliwa kreni kwaajili ya kuinua vitu vizito pamoja na uwepo wa chelezo ambayo inatumika kukarabati meli za TPA pamoja na za taasisi nyingine.
 Waandishi wa Habari was vyombo mbalimbali nchini wakimsikiliza Meneja Bandari za Ziwa Nyasa Abeid Galus alipokuwa akieleezea Miradi ya Bandari za Ziwa Nyasa
 Meneja Bandari za Ziwa Nyasa,Abeid Galus akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya mafanikio yatokanayo na kuboreshwa kwa Bandari za Ziwa Nyasa.
 Meli ya Mv Mbeya ii kama inavyoonekana pichani ikiwa imekamilika kwa asilimia 85 ambapo inataraji kuanza kazi mwezi September mwaka huu.
 Sehemu ya mafundi wanaofanya marekebisho ya kuongeza Gati katika Bandari ya Kiwira Kyela Mkoani Mbeya.
Sehemu ya mafundi wanaofanya marekebisho ya kuongeza Gati katika Bandari ya Kiwira Kyela Mkoani Mbeya.

MAJANGILI WOTE POPOTE WALIPO WATAKIWA KUJISALIMISHA MARA MOJA

0
0

Na woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha 

SERIKALI imewataka majangili wote popote walipo wajisalimishe vinginevyo serikali   itawatumia polisi wa kimataifa kuwakamatwa mmoja mmoja ili kutokomeza vitendo vyote vya ujangili ndani ya hifadhi zote hapa nchini.

Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Hamisi Kingwangala, alipokuwa akifungua mkutano wa kimataifa wa Utalii unaoshirikisha mataifa mbalimbali pamoja na mashirika ya kimataifa yanayohusiana na maswala ya utalii, ulimwenguni na wadau.

 Kigwangala, amesema  kuwa  katika kipindi cha miaka michache kiwango cha Ujangili wa Wanyamapori kwenye hifadhi mbalimbali nchini kimeshuka lakini biashara ya nyara  haramu inaongezeka..

Amesema  wanaouza au kusafirisha nyara ni wale waliokuwa na akiba za nyara kwani hakuna nyara mpya, na wanazisafirisha nje ya nchi na usafirisahaji wa nyara uumeipiku biashara ya usafirishaji wa binadamu ambapo biashara hiyo ya nyara imepanda hadi kushika nafasi ya tatu ya biashara haramu.

Amebainisha kuwa Mkutano huo unaangalia namna ya  kupata taarifa za ujangili  kwenye hifadhi kuangalia  namna ya kufanya kazi ,kushirikiana kupeana  taarifa kutatua migogoro inayojitokeza kati ya wananchi wanaoishi kwa kupakana na hifadhi kwenye maeneo ambako ni mapito ya wanyama pori, kuimarisha miundo mbinu  katika swala zima la kudhibiti ujangili ndani ya hifadhi mbalimbali.

Waziri Kigwangala,amesema  Usalama wa Dunia unategemea usalama wa mazingira Matokeo ya mkutano huo yatapelekwa kwenye mkutano mkuu wa marais utakaofanyika nchini Japani mwezi Augosti mwaka huu na hiyo ni fursa kwa afrika kutokomeza biashara haramu ya ujangili .

Kwa upande wake mkurugenzi msaidizi wa kuzuia ujangili  Robat Mande amesema kuwa mkutano huo inalenga kuimarisha mfumo wa Kiintelejensia ,uzoefu na nyara na mazao ya misitu.

 Amesema Tanzania kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa ni kinara barani Afrika katika kudhibiti vitendo vya Ujangili dhidi ya wanyama pori barani Afrika.

 Mande, ambae pia ni mwenyekiti wa kikosi cha kuzuia ujangili nchini,ameongeza kuwa ujangili huo umedhibitiwa kutokana na kutekeleza falsafa ya ushirikishawaji wa vyombo vingine vya dola pamoja na wadau na wananchi na hivyo kuwezesha kufanya kazi kwa pamoja

Amesema mwaka 2005  Tanzania ilikuwa ni moja kati ya nchi 8 Ulimwenguni ambazo ujangili ulikuwa umekithiri lakini mwaka 2014 kulizinduliwa  mkakati wa kutokomeza ujangili na sasa tupo kwenye nafasi nzuri ya kuwa ni nchi ambayo imetokomeza ujangili.

Alisema Mkutano huu ni wa tatu kufanyika mkutano wa kwanza ulifanyika Nairobi nchini Kenya nmkutano wa pili ulifanyika nchini Thailand mkutano ujao utafanyika Japani.

Nae mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka za usimamizi za wananchi ,WMA, George wambura, amesema yapo maeneo 38  ya hifadhi za wananchi kati yake 22 ndio yanayotumika  kwenye shughuli za uwindaji  na utalii na zimeweza kudhibiti ujangili kwa asilimia 88  na hivyo kuboresha utalii kwenye maeneo mbalimbali,.

Amesema zipo WMA 36,000 ambazo zimekuwa zikisaidia serikali katika kudhibiti ujangili na hivyo kuwezesha wananchi waishio kuzunguka hifadhi hizo kujipatia vipato
Viewing all 109589 articles
Browse latest View live




Latest Images