Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

NMB yatoa msaada wa madawati 150 na vifaa tiba wilayani Mkuranga

$
0
0
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mwandege Wilayani Mkuranga wakibeba madawati na viti mara baada ya kukabidhiwa na viongozi wawakilishi wa Benki ya NMB.Benki ya NMB imezipiga jeki shule tatu za sekondari na kituo cha afya wilayani Mkuranga vifaa vyenye thamani ya milioni 20.
 Mkuu wa Kitengo cha Biashara za Serikali wa NMB, Bi. Vicky Bishubo (aliyesimama) akiwasalimu wakazi wa Mkuranga kabla yakukabidhi  madawati 150 na viti vyake kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga,  Filberto Sanga (mwenye suti ya khaki) katika hafla ya makabidhiano yaliofanyika Sekondari ya Mwandege. Benki ya NMB imezipiga jeki shule tatu za sekondari na kituo cha afya vifaa vyenye thamani ya milioni 20.

Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga,  Filberto Sanga  akitoa neno la shukrani kwa NMB katika hafla ya makabidhiano yaliofanyika Sekondari ya Mwandege baada ya kupokea msaada wa madawati 150 na viti vyake.Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara za Serikali wa NMB, Bi. Vicky Bishubo.  Benki ya NMB imezipiga jeki shule tatu za sekondari na kituo cha afya vifaa vyenye thamani ya milioni 20.



BENKI ya NMB imekabidhi msaada wa madawati 150 na meza zake kwa shule tatu za sekondari pamoja na vifaa tiba na vitendea kazi katika Kituo cha Afya cha Kisiju Wilaya ya Mkuranga vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 20.

Shule zilizonufaika na msaada huo wa madawati pamoja na meza zake 150 yote yakiwa na thamani ya shilingi milioni 15 ni Sekondari ya Mwandege, Vikindu na Kiimbwanindi zote za Wilaya ya Mkuranga.

Akikabidhi msaada huo leo Wilayani Mkuranga kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga,  Filberto Sanga, Mkuu wa Kitengo cha Biashara za Serikali wa NMB, Bi. Vicky Bishubo alisema kituo cha afya kimekabidhiwa vitanda vitano na magodoro, kitanda kimoja maalum cha kujifungulia na mashuka 53 ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kuboresha huduma za afya.

Bi. Bishubo alisema thamani ya msaada wote yaani madawati na viti vyake 150 pamoja na vifaa tiba ni shilingi milioni 20 na Benki ya NMB itaendelea kuchangia huduma za kijamii maeneo mbalimbali kadri hali inavyoruhusu.

Aidha alisema licha ya benki yao kupokea maombi mengi ya msaada wa kijamii imekuwa ikitoa kipaumbele kwenye sekta ya elimu, afya pamoja na misaada ya hali na mali yanapotokea majanga kwa wananchi.

"Ndugu mgenia rasmi kwa mwaka 2019, Benki ya NMB imetenga zaidi ya shilingi bilioni moja (1) kwa ajili ya kuchangia maeneo ya jamii ikiwemo kusaidia sekta ya afya na elimu. Kiasi hiki kinatufanya kuwa benki ya kwanza katika kuchangia maendeleo kuliko benki yoyote nchini Tanzania.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Bw. Sanga akipokea msaada huo aliishukuru Benki ya NMB kwa msaada wake kwani upendo waliouonesha kwa Wanamkuranga utaendelea kudumu na kuiendeleza wilaya hiyo kimaendeleo.

Alisema msaada wa madawati umenusuru idadi kubwa ya wanafunzi ambao awali walishindwa kuendelea na masomo kwa shule zao kukosa madawati lakini sasa zimefunguliwa baada ya kupokea msaada huo na wanafunzi wanaendelea na masomo.

"...Wilaya yetu ilikuwa na shule tatu ambazo zilikuwa na changamoto kubwa ya madawati baada ya kuzianzisha, lakini msaada huu wa madawati na viti 15o kwa kweli umetufaa na umekuja kwa wakati muafaka," alisema Mkuu huyo wa Wilaya ya Mkuranga.


JOSEPH KABASELE ‘GRAND KALLE’ GWIJI WA MUZIKI ALIYEWABEBA WENGI

$
0
0
Na Moshy Kiyungi

Pasipo kuyataja majina ya gwiji wa muziki wa rhumba Joseph Kabasele ‘Grand Kalle, utakuwa hujakamilisha upaswavyo kusimulia historia ya muziki huo toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Nguli huyo licha ya kwamba hatunaye duniani, jina na sifa zake zitabaki kuwa historia ya muziki nchini humo. Kabasele alikuwa ni baba na nyota kuu ilioleta maendeleo na mabadiriko makubwa kwenye muziki wa rumba DRC.

Kwa mujibu wa Wasifu wake unaeleza kuwa alizaliwa Desemba 16,1930 mjini Matadi huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Baba yake alikuwa akiitwa mzee Andre Tshimala na mama yake aliitwa Hortense Malula. Joseph Kabasele ndiye aliyekuwa kitinda mimba kwenye familia ya watoto sita.

Yaelezwa kuwa ndiye aliyekuwa mwanamuziki wa kwanza kuvitumia vyombo kadhaa vya muziki na kusababisha yatokee mabadiriko makubwa kwenye sekta hiyo ya muziki. Vyombo hivyo ni pamoja ja tarumbeta, Clarinet, Saxophoni na ngoma.

Mwanamuziki huyo alifahamika pia kwa majina ya ‘Grand Kalle’ , mwanamuziki wa kwanza huko Jamhuri ya Kidemorasia ya Kongo kutumia gitaa la umeme. Joseph Kabasele alikuwa Mkongomani wa kwanza kumiliki bendi yake binafsi ya African Jazz iliyoundwa mwaka 1953, pamoja na studio yake ya Surboum kwa ajili ya kurekodia muziki.

Sifa nyingine za mhenga huyo ni kwamba ndiye aliyemlea kimziki mwanamuziki Rochereau Tabu Ley pamoja kamkuza kimziki aliyekuwa mpiga gitaa mahiri nchini Kongo Dokta Nico Kasanda. Grand Kalle na bendi yake ya African Jazz, walikuwa wakwanza kusafiri kwenda nje ya nchi yao ya DRC.

Walifika katika nchi za za Ulaya, Ubelgiji,Ujerumani, Italia, Ufaransa na zingine nyingi kwa ajili ya kufanya maonesho. Kwenye miaka 1960, Kabasele alitungua kibao kilicho kubalika popote pale Barani Afrika cha Independance Cha Cha. Kibao hicho kilikuwa kikiisifia nchi yake ya Kongo kupewa Uhuru kutoka mikononi mwa Wakoloni.

Kupitia studio yake aliweza kufika Ulaya tena akiambatana na mwanamuziki Franco Luambo Makiadi na kundi lake lote la T.P. OK. Jazz pia akawanunulia seti ya vyombo vipya vya muziki. Grand Kalle alisoma shule ya msingi ya Institute Saint Joseph, iliokuwa ikimilikiwa na ma Padre, Jijini Kinshasa.

Akiwa shuleni humo, alijiunga na kwaya la Kanisa Katoliki akiwa na umri mdogo wa miaka 8. Kabasele alitokea kuwa mwimbaji mzuri huku akitumia kwa umaridadi sauti yake ya Tenor, huku akiendelea na masomo ya Sekondari kwenye Shule ya (Ecomoraph). Umaarufu wake ulipelekea kuwa kivutio na kipenzi cha wengi wakiwemo wanafunzi pia wanafunzi wenzake shuleni humo.

Licha ya uimbaji wa nyimbo, Kabasele pia alikuwa akipenda michezo na kupelekea kupendwa sana na watu hususan wanawake. Wahenga walinena kuwa “kila kizuri kina ubaya wake” Pamoja na sifa zote hizo, Kabasele alikuwa na tabia mbaya ya utovu wa nidhamu. Mapadre waladiriki kuchukua hatua ya kumfukuza Shule.

Katika kipindi cha Ukoloni, shule takriban zote zilikuwa zikimilikiwa na Mapadre, kwahiyo ikamjia vigumu kwa Grand Kalle kupata shule nyingine itakayo mkubali. Kwakuwa hapakuwa na shule inayo mkubali, ilimbidi atafute kazi. Nguli huyo akabahatika kupata ajiria kama Katibu kwenye makampuni tofauti Jijini Kinshasa.

Mwaka 1947, kutokana na ushawishi wa rafiki yake Georges Dula aka ‘Geoder’, alipelekea kwenda kujiunga na kundi la muziki la OTC. Bila kusita alikubaliana na pendekezo hilo, kwa kuwa aliona kwamba njia yake ya kuwa ‘Nyota’ inaanza kufunguka. Kuna kipindi Grand Kalle alifanikiwa kutoa wimbo Palmolive, ambapo aliwasifia wasichana kwamba ni warembo na wananukia manukato mazuri kama ya Sabuni Palmolive.

Mwaka 1950, wazo likamjia aende kujaribia kipaji chake kwa Mr.Moussa Benatard, ambaye alikuwa mfanyabiashara Myahudi tena mmiliki wa Studio ya OPIKA. Baada ya Myahudi huyo kumfanya majaribio, akaona kwamba Kabasele anacho kipaji, ila anastahiki asaidiwe, aongozwe, afundishwe namna ya kuimba kwenye Studio.

Ndipo alipowekwa chini ya usimamizi wa mpiga gitaa mashuhuri Zacharie Elenga ‘Jimmy’. Wakafanikiwa kutoa vibao vingi vya Ondruwe , Maboko Likolo, Baninga Baninga, Makombo ya Jimmy na Putulu Emata. Baada ya kuona amepata mafanikio ya nyimbo hizo kuwa mazuri, Grand Kalle akazidi kujipa moyo kwa kuchapa kazi vilivyo, akiwa na nia ya kutaka kujitegemea.

Mwaka 1951, Wazo likamjia la kuunda bendi yake binafsi na ilipotimu mwaka 1953, chini ya usimamizi wake wakaunda bendi ya African Jazz. Bendi hiyo ilikuwa na wanachama kama Roger Izedi, aliyekuwa mwimbaji na upiganji wa Marakasi, Etienne Diluvila aliyekuwa mwimbaji na Bettry, Nicolas Kasanda aliyekuwa akilicharaza gitaa la Solo, Charles Mwamba, Albert Dinga na Albert Taumani walikuwa pia ni wapiga magitaa.

Wengine ni pamoja na Isaac Musekiwa na Dominique Kuntina waliokuwa wakipuliza saxophone, Willy kwa upande wa tarumbeta , Antoine Kaya na Depuissant walikuwa wakizidunda tumba. Mwaka 1954, Grand Kalle bendi yake ya African Jazz walipata tenda ya kwanza na kwenda kutumbuiza katika jiji la Bangui nchini Afrika ya Kati kwenye uzinduzi wa ukumbi wa Dancing Bar Le Rex.

Ziara yao hiyo ilimletea furaha kubwa Grand Kalle sio kimapato, bali kuona yeye na kundi lake African Jazz wanakubalika hadi Kimataifa. Kabasele na kundi lake wakapata sifa nyingi kutokana na nyimbo nzuri kama Parafifi iliyorekodiwa na African Jazz mwaka 1957, Nzela Mosika, Ce n’est pas la peine de divorcer maintenant na nyingine nyingi.

Mwaka 1959, Orchestra African Jazz ikawa kwenye kipindi kigumu kutokana na utumiaji mbaya wa Pesa. Yasemekana Joseph Kabasele alitokea kuwa mbinafsi aliyeshindwa kuwajali wanamuziki wenziwe. Ujio wa Kijana Tabu Ley Rochereau kwenye bendi hiyo, ukaleta nguvu mpya.

Ley akaja na wimbo wake wa Kellya, uliopendwa sana na mashabiki wa muziki wa rhumba. Kundi hilo likaja kupumua kipesa wakati waliposafiri kwenda Ulaya mwaka 1960, kutoa motisha ya kuwasapoti Wanasiasa wa Kongo wakati wa mazungumzo ya Uhuru wa nchi yao yaliyofanyika Jijini Brussels, nchini Ubelgiji.

Safari yao hiyo ya Ulaya iliwaletea sifa nyingi na mafanikio makubwa. Africana Jazz wakatoa vibao vilivyo weka simulizi kwenye historia ya rhumba nchini Jamhumri ya Kidemokrasia ya Kongo hadi leo hii. Nyimbo walizoachia wakati huo zilikuwa za Indépendance Chacha na Table Ronde, zilizokuwa utunzi wake Joseph Kabasele ‘Grand Kalle’

Nyingine zilikuwa za Naweli Boboto na Sentiment Emonani, utunzi wake Vicky Longomba, Tosekana na Mawonso Pamba zilizotungwa na Dechaud Muamba , Sophia Motema na Merengue Soubidou mtunzi akiwa Niko Kasanda. Waliporudi Kinshasa mwaka 1961, pakatokea mzozo ulio sababisha baadhi ya Wanamuziki wa bendi hiyo ya Orchestra African Jazz kujiondoa.

Wanamuziki hao ni pamoja na Dokta Nico Kasanda, Dechaud, Vicky Longomba, Brazzos na wengine wengi. Licha ya kuondokewa na wanamziki hao bendi hiyo ilifaanikiwa kwa mara nyingine kupanda ndege na kwenda Jijini Brussels. Wakiwa huko wakarekodi baadhi ya nyimbo kupitia Studio yake Surboum.

Baadaye bendi ilirudi Kinshasa kwa mbwembwe, sifa zao zikawa nyingi mno. Uongozi wa bendi ya African Jazz chini ya uongozi wa Grand Kalle, ilimsajili mwanamuziki Manu Dibango. Manu Dibango alikuwa maarufu kwa upulizaji wa saxophoni. Mwaka 1962 Grand Kalle akatafuta suluhisho lipatikane ili wanamuziki wote walio jiondoa warudi kwenye bendi yake.

Hatimaye muafaka ukapatikana, ndipo akina Dokta Nico Kasanda, Dechaud Muamba na wengine, wakakubali kurudi katika bendi. Tabu Ley Rochereau alitoa ushauri wa kuchukuliwa kwa mwimbaji Mujos, akitokea bendi T.P. OK. Jazz.

Mwaka 1963, pakatokea kwa mara nyingine tena mgawanyiko mkubwa, sababu ikiwa ni wanamuziki kupiga kelele kutopewa pesa ingawa kazi wanaifanya ipasavyo. Takriban Wanamuziki wote walijiondoa akiwemo Tabu Ley Rochereau, wakaenda kuunda bendi yao mpya ya African Fiesta. Kitendo hicho kilimuumiza sana Grand Kalle, lakini alijipa moyo, akaanza kuisuka upya bendi yake ya African Jazz.

Rafiki na mfadhili wake Jean Foster Manzikala, alimnunulia vyombo vipya vya muziki. Kikosi cha wanamuziki wa bendi hiyo wakati huo kiliwajumuisha akina Nedule Papa Noël, Kambele Damoiseau, Jeannot Bombenga, Mathieu Kuka, Nsita Rolly, Alex Mayukuta, Casino Mutshipule, Munange Maproko na Yuma Michel Sax.

“Sikio la kufa halisikii dawa” usemi huo ulionekana dhahir baada ya katokea purukushani nyingine iliopelekea wanamuziki kujiondoa. Bendi hiyo ya African Jazz ikawa ndicho chanzo cha kuangamia kimuziki. Kwenye Miaka ya 1969-1970, Joseph Kabasele alihama jiji la Kinshasa, akaweka maskani yake jijini Paris nchini Ufaransa.

Akiwa jijini humo, alishirikiana vymema na wanamuziki akina Manu Dibango, Don Gonzalo, Lutula Edo Clary, Jeannot Bombenga, wakaunda bendi iliyopewa majina ya African Team. Bendi hiyo ikatoa vibao vingi vikiwemo vya Gauche-droite égal débordement, Africa mbiance, Bana Congo na Cuba, Laurent Fantôme na Cambridge. Nyingine zilikuwa wa Mayi ya Piyo,Safari Muzuri, Disciplini na KDL na Edona Souzy

Hata hivyo bendi hiyo ya African Team haikudumu kwa siku nyingi, nayo ikasambaratika. Kati ya miaka ya 1973 na 1980, Joseph Kabasele akawa adimu sana jukwaani, alifanya onesho lake la mwisho kwenye ukumbi wa hotel Intercontinental, jijini Kinshasa.

Baada ya Hapo, Hali yake kiafya ikawa inazorota, na kipesa akawa anadidimia vibaya sana. Joseph Kabasele ‘Ggrand Kalle’ aliyefahamika zaidi kama mzee wa msimamo, mzee wa kanuni, Baba wa rumba, alifariki dunia Desemba 11, 1983)akiwa na mri wa miaka 53 Jijini la Paris nchini Ufaransa.

Mwenyezi Mungu ailaze Roho yake mahala pema, Amina.

Mwisho.Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba:

0767331200, 0736331200, 0713331200 na 0784331200

ZAHIR ZORRO AMERITHISHA WANAWE FANI YA MUZIKI

$
0
0
Na Moshy Kiyungi
Wimbo wa ‘Arua’ aliouimba kwa ujasiri mkubwa Zahir Alli Zorro, ulimuongezea sifa nyingi mno Afrika ya Mashariki. Katika wimbo huo Arua ulikuwa ukiwakaribisha mashujaa wetu waliokwenda mstari wa mbele kupigana vita na nduli Idd Amin wa Uganda. Zahir wakati huo alikuwa mtunzi, mwimbaji mahiri na mwenye uwezo mkubwa wa kulicharaza gitaa la solo katika bendi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Wana ‘Kimulimuli’ iliyokuwa jijini Dar es Salaam.

Mwaka 1978 nchi yetu ilivamiwa na majeshi ya Uganda, nchi iliyokuwa ikiongozwa na Rais Idd Amin Dada. Kitendo hicho kimfanya Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Tanzania, ambaye pia alikuwa Rais, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kuyaamrisha majeshi yetu kupigana vita, ambavyo hatimaye vilimuondoa madarakani Idd Amin.

Baadhi ya bendi za muziki humu nchini zilitunga nyimbo za kuyahamasisha nakupongeza majeshi yetu kwa ushindi. Baada ya ushindi huo, mkoa wa Ziwa Magharibi au West Lake Region (kwa lugha ya Kiingereza) wakati huo, ukabadilishwa jina ukaitwa mkoa wa Kagera. Historia ya Zahir Alli Zorro katika muziki inaonesha kuwa amechangia katika kunyanyua tasnia ya muziki wa Tanzania.

Zahir ni mmoja kati ya wanamuziki wakongwe aliyeingia kwenye gemu la muziki mwaka 1968 na hadi sasa anaendelea ‘kupeta’ kwenye tasnia hiyo. Ni baba wa familiya ya mke na watoto wawili ambao nao ni wasanii Banana na dada yake Maunda Zorro. Watoto hao wamedhihirisha usemi wa “mtoto wa nyoka ni nyoka”, hivi sasa wanatamba katika muziki wa kizazi kipya ‘Bongo Flava’.

Wasifu wake katika muziki alisema kuwa awali alijiunga na bendi ya muziki ya Super Vea chini ya Maestro Musama Andrew, baadaye akajiunga na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) na aliajiriwa katika kitengo cha OP TANU M19 mwaka 1973 hadi 1989. Zorro alibainisha baadaye alijiunga na bendi ya Sambuluma, iliyokuwa ikiongozwa na Mbangu Nguza ‘Vicking’, ambako alitunga wimbo uliovuma sana kwa jina la Cleopatra mwaka 1991.

Safari ya muziki ya Zahir alimfikisha kupiga hodi katika bendi ya Washirika iliyokuwa ikitumia mtindo wa ‘Watunjatanjata' mwaka 1992 hadi 1996. Mkongwe huyo aliunda bendi yake ya Mass Media, ambayo haikudumu kwa kipindi kirefu, licha ya kuachia nyimbo kadhaa ambazo zilikuwa simulizi mitaani.

Zahir Ally Zorro alizaliwa Aprili 24, 1954 katika hospitali ya Ocean road jijini Dar es Salaam. Kwa upande wa elimu, alisema kuwa alipata elimu ya awali katika shule ya Wazazi iliyokuwa inayoitwa TAPA mwaka 1959, iliyokuwa katika jengo la Taasisi, karibu kabisa na mnara wa Mwalimu Nyerere mjini Tabora.

Zahir alianza elimu ya msingi mjini humo ambako alihitimu masomo hayo mwaka 1968. Baada ya masomo yake ya elimu ya msingi aliingia kwenye tasinia ya muziki, ambayo amedumu nayo hadi sasa. Nguli huyo anao mpango wa kuwamwagia ujuzi wa muziki kwa vijana wa Tanzania, ambao watakuwa na ari ya kujifunza.

Zahir alisema mikakati yake kwa ujumla ni pamoja na kuirudisha bendi ya Mass media ambayo awali aliwahi kufanya nayo kazi kabla ya kuvunjika. Lengo lake kubwa la kuirejesha bendi hiyo ni pamoja na kuanzisha kituo ili aweze kutoa elimu ya muziki aliyonayo kwa wanamuziki chipukizi wanaopenda kujifunza kazi hiyo.

Vilevile mkongwe huyo anakusudia kutunga nyimbo zake binafsi kwa kwa ajili ya kutoa albamu yake. Zahir Alli alitamka kuwa licha ya mkakati huo, pia anatarajia kutoa kitabu kitakachoitwa SHADOUX ambacho kitachapichwa na Kampuni ya magazeti ya Global Publishers.

"Kazi ya kutunga nimekamilisha na kilichobakia kazi ya kuchapa ambapo kampuni ya Global ndio itafanya kazi hiyo," alisema Zorro. Pamoja na mikakati hiyo alibainisha kuwa changamoto zinazowakabili ni uhaba wa fedha kwa ajili ya kununulia vyombo vya muziki. Zorro alisema kuwa kwa sasa vyombo vya muziki vipo vingi sana madukani hapa nchini lakini ukosefu wa fedha kwa ajili ya kununulia ndiyo tatizo kubwa.

Aidha alisema kuwa kuna utofauti kidogo na zamani ambapo fedha zilikuwepo lakini hakukuwa na vyombo vya muziki. Zahir Alli Zorro nyimbo zake kamwe hazitachuja masikioni mwa wasikilizaji kwa kuwa zilikuwa na ujumbe madhubuti kwa jamii. Baadhi ya nyimbo hizo za Tikisa, Cleopatra, Haifai Kabwe na Arua uliokuwa ukiwakaribisha mashujaa wetu waliokwenda mstari wa mbele kupigana vita na nduli Idd Amin wa Uganda.

Zahir bado yupo na wakati mwingine hushirikiana na mwanawe Banana anayemiliki bendi iitwayo B.Band.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba: 0784331200, 0767331200, 0736331200 na 0713331200.

SAFARI YA MWISHO YA MWIGIZAJI KING MAJUTO

$
0
0
Na Moshy Kiyungi
Mwigizaji mkongwe wa filamu na vichekesho nchini Tanzania Amri Athuman maarufu King Majuto, alifariki dunia Agosti 8, 2018 saa mbili kamili usiku katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Afisa habari wa Muhimbili Aminiel Eligaisha ambapo alisema Mzee Majuto alifariki akiwa anaendelea na matibabu ambayo yalianza Julai 31, 2018.

''Hali yake ilibadilika majira ya saa tisa alasiri ya leo hivyo kuhamishwa kutoka jengo la Sewahaji kwenda ICU. Ilipofika saa 1.30 jioni, hali yake ilibadilika zaidi na madaktari walijitahidi kuokoa maisha yale bila mafanikio. Ilipofika saa mbili alikata roho'', alisema Eligaisha. King Majuto alianza kuumwa muda mrefu akisumbuliwa na tatizo la nyonga ambapo mapema Mei 2018, alipelekwa nchini India kwaajili ya matibabu.

Safari hiyo iliwezeshwa na msamaria mmoja aliyejitolea tiketi za watu wawili za kwenda nchini humo. Alirejea toka India Juni 2018, ambapo alifikia katika hospitali ya Muhimbili lakini baadaye alipata nafuu, aliruhusiwa kurudi nyumbani. Mkongwe huyo alitangaza kustaafu kuigiza baada ya kutoka India.

King Majuto akiwa nyumbani kwake hali yake ilibadilika, akarudishwa tena Muhimbili. Aidha King Majuto aliwahi kutibiwa katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam kabla ya kupelekwa India kwa ajili ya matibabu zaidi. Atakumbukwa kwa kazi zake nyingi za vichekesho ambazo alizifanya kwa uhodari mkubwa na kuwa kivutio kwa mashabiki wengi.

King Majuto alisaidiwa kwakiasi kikubwa na mwigizaji mwenzake Sharo Millionea, kuingia mikataba na makampuni mengi yaliyokuwa yakimuingizia fedha. Milionea alifariki kwa ajali ya gari akielekea nyumbani kwa kwa wazazi wake mkoani Tanga.

Wasifu

Amri Athuman’ King Majuto’ alizaliwa mwaka 1948 jijini Tanga. Alisoma shule ya msingi Msambwini, mkoani Tanga ambapo alianza kuigiza 1958 akiwa na umri wa miaka 9. Licha ya vichekesho, King Majuto alikuwa na talata za utunzi, uigizaji pia ni mwandishi wa miswada.

Nguli huyu Amri Athman ndiye aliyekuwa muigizaji wa kwanza kuandaa kazi zake katika mikanda na kuuza akiwa na Kampuni ya TFC (Tanzania Film Company). Kupia uigizaji wake King Majutoalijizolea mashabiki lukuki waliokuwa wakifuatilia vichekesho vyake kwenye maonesho mbalimbali.

Pamoja na umri kuonekana ulikuwa umemtupa mkono, mkongwe huyu wa sanaa ya Komedi, Amri Athuman ‘King Majuto’ aliwahi kutamka kuwa bado hakuna wa kumpiku katika tasnia hiyo. Aliwahi kutamka kwamba kumekuwapo na wachekeshaji wengi wanaoonekana kuja kwa kasi kutaka kumfunika, lakini hilo halitakuja kutokea kwasababu anaamini uwezo wake ni mkubwa katika fani hiyo.

Alinukuliwa akitamka kwa: “Uvumilivu, nidhamu na ubunifu niwapo kazini ndiyo siri pekee ya mafanikio niliyonayo kwenye Komedi na ndiyo inayosababisha niendelee kuwa bora siku hadi siku,” alisema King Majuto. Alijigamba kuwa fani hio ya uigizaji na vichekesho aliweza kuvuna mambo mengi, vikiwamo ubunifu na msimamo kutoka kwa aliyekuwa gwiji mwenzie, marehemu Said Ngamba ‘Mzee Small’.

King Majuto alimuelezea ‘Mzee Small’ walikutana kwa mara ya kwanza mwaka 1973, mtaa wa Moshi uliopo Ilala, jijini Dar es Salaam. Akielezea namna alivyolipata jina la ‘King Majuto’, alisema alipokuwa kwenye kundi la DDC Kibisa, aliigiza michezo mingi ambayo mwisho ilimalizika kwa ‘kujuta’. Watu kuamua kumpachika jina hilo ambalo limedumu hadi alipofariki dunia,

King Majuto wakati wa uhai wake alikuwa akikerwa mno kwa uzembe, Wasanii wavivu katika kazi ya sanaa, waliokuwa na kawaida ya kujivutavuta kufika ‘Lokesheni’. Hakusita kutamka msanii analiyekuwa akimvutia katika sanaa ya uigizaji, aliwataja waigizaji Jacob Stephen ‘JB’ na Brother K. wa kipindi cha ‘Futuhi’.

“Faida niliyokwishaipata kwenye uigizaji ni kusomesha watoto wake, kujenga nyumba tatu, kununua magari matano, kumiliki shamba na mifugo,” alitamka enzi za uhai wake.

Aidha King Majuto alikuwa akijivunia kuwaibua wasanii wengi katika maigizo. Faida nyingine alizozipata kutokana na uigizaji kuwa ni kuanzisha kundi lake binafsi liitwalo King’s Entertainment. Kundi hilo lenye wasanii 75, ambalo maskani yake yapo CCM Hall, jijini Tanga.

King Majuto alikuwa baba wa familia yenye watoto 12 ambao takriban wote ni waigizaji kama alivyo yeye, isipokuwa mtoto wake wa kwanza aitwaye Athuman aliyeamua kuingia kwenye muziki akipiga gitaa.

King Majuto alikuwa msanii huru tangu 1983, baada ya kupitia vikundi mbalimbali vya sanaa vya JKT, JWTZ, Zimamoto na Bandari. Alipoulizwa juu ya kugombea nafasi za kisiasa, King Majuto alisema kuwa hana ndoto za kuwa mwanasiasa, na ameahidi kubakia kuwa mwigizaji sababu kwa kuwa vitu hivyo haviingiliani.

Licha ya kazi yake hiyo, Majuto pia ni mkulima bora mwenye shamba kubwa la mbogamboga linalomfaa kwa matumizi ya nyumbani. Aidha anashamba maeneo ya Kiruku, mkoani Tanga, lenye mazo ya Mananasi, Machungwa, Mihogo, Minazi na Miembe ambayo yameanza kumletea faida. Mwili wa Amri Athuman ‘King Majuto’ uliwekwa kwenye nyumba yake ya milele kijijini kwake huko mkoani Tanga.

Mungu aipumzishe roho yake pahala pema peponi, Amina.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba: 0767331200, 0713331200, 0736331200 na 0784331200

Neema kwa Wakulima wa Ufuta,Namtumbo,Wavuna Bilioni 5.5

BURIANI MOSE SENGO FAN FAN

$
0
0
Na Moshy Kiyungi
Tasnia ya muziki wa rumba kwa mara nyingine tena imekumbwa na msiba mwingine wa nguli wa muziki wa rhumba, Mose Sengo Fan Fan. Kifo chake kilitokea zikiwa ni siku mbili kabla maziko ya aliyekuwa mwanamuziki mkongwe wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Lutumba Simaro Massiya aliyezikwa Mei 05, 2019 jijini Kinshasa.

Fan Fan ambaye alikuwa amefikisha umri wa miaka 75, alifariki kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni mshtuko wa moyo, akiwa nyumbani kwake barabara ya Thika, jijini Nairobi, Kenya. Kwa mujibu wa mke wake alisema mumewe alifariki kwa ugonjwa wa moyo kuwa kuvimba, na wanatajia kumzika Juni 08, 2019.

Enzi za uhai wake Fan Fan licha ya kucharaza gitaa, pia alikuwa mtunzi mzuri wa nyimbo katika bendi mbalimbali zalizozipitia kupiga muziki. Kuthibitisha hilo Mose Fa Fan alitunga wimbo wa ‘Papa Lolo’, uliokuwa maarufu na kuweza kutikisa anga za muziki barana Afrika kutokana na mipigo na ujumbe mzito kwa jamii.

Nguli huyo alikuwa Nairobi kwa ajili ya kurekodi nyimbo zake mpya kwa kushirikiana na wanamuziki Paddy Makani na Disco Longwa. Tabu Osusa ambaye alikuwa rafiki na producer wa mwanamuziki huyo alisema kuwa Fan Fan alikuwa akipenda kutembelea Kenya kila mwaka. Mose Sengo alikuwa akitokea London, Uingereza ambako ndiko yalikuwa makazi yake.

Kifo cha Fan Fan kilitokea huku wananchi wa DRC walikuwa wakijiandaa kumzika mwanamuziki nguli Lutumba Simaro Massiya aliyefariki dunia Machi 30, 2019, katika hospitali moja jijini Paris nchini Ufaransa akiwa na umri wa miaka 81.

Kama alivyokuwa Lutumba, Fan Fan naye alikuwa ni miongoni mwa wanamuziki wa mwanzo waliokuwa wakiunda kundi la T.P.OK Jazz, iliyokuwa ikiongozwa na Franco Luanzo Luambo Makiadi. Kifo cha Mose Sengo Fan Fan kimemuweka kwenye orodha ya magwiji kadhaa waliofariki baada ya kufanya mambo makubwa katika tansinia ya muziki ulimwenguni.

Magwiji wengine wa muziki wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo waliotangulia mbele za haki ni akina Papa Wendo, John Bokelo, Joseph Kabasele ‘Grand Kale’, Dokta Nico Kasanda, Vicky Longomba, Franco Luambo Lwanzo Makiadi, Kabasele Yampanya ‘Pepe Kalle’, Madillu System, Baba Gaston ‘Ilunga wa Ilunga Omer, Jimmy Monimambo, Fred Mayula Mayoni, Dindo Yogo na wengine wengi.

Enzi za uhai wa Mose Sengo Fan Fan, aliwahi kuishi nchini Tanzania na kupiga muziki katika bendi za Orchestra Makassy, Super Matimila na Tancut Orchestra ya Iringa. Aliyekuwa kiongozi na mmiliki wa bendi ya Orchestra Makassy, Mzee Makassy, ambaye sasa amestaafu kupiga muziki, alisema kuwa kifo cha Fan Fan kimemstua na kumpa simanzi kubwa kwakuwa waliwahi kufanya kazi katika bendi yake.

“Nimesikitishwa sana kawa taarifa hizi.Tulifanya kazi pamoja kwa muda mrefu mchango wake ulikuwa mkubwa…”alisema Mzee Makassy. Alisema kwamba alikuwa amewasiliana na Fan Fan kwa mara ya mwisho miaka mitatu iliyopita, katika mazungumzo yao, alimuahidi kwamba angelikunja nchiniTanzania katika ziku za karibuni.

Kwa upande wake Tshimanga Kalala Assosa, mwanamuziki aliyewahi kufanya kazi na Fan Fan katika bendi ya Orchestra Makassy, alionesha kuwa na majonzi zaidi kwa kuwa alikuwa na ahadi ya kurekodi nyimbo mpya za Fan Fan hivi karibuni. “Kifo chake kimenipa mshtuko mkubwa sana kwa sababu nilizungumza naye saa chache kabla ya kifo chake kumfika” alisema Assosa.

Aliongeza “Katika mazungumzo yetu, alinieleza kuwa amekwishalipia gharama zote katika moja ya studio za jijini Arusha. Tulikuwa na mpango wa kuingia studio jijini humo kwa ajili ya kurekodi baadhi ya nyimbo zake mpya…” alisema Assosa. Mose Sengo Fan Fan aliyezaliwa Oktoba 16, 1945, huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), alianza kujihusisha na muziki mwanzoni mwa miaka ya 1960.

Alijifunza muziki tangu akiwa mwanafunzi kwenye shule moja ya kanisa Katoliki nchini humo DRC. Baadaye alikwenda kupiga muziki katika bendi za Somo Somo, Orchestra Revulution na kisha akachukuliwa kujiunga katika kikosi cha T.P.OK Jazz, ambako alikabidhiwa gitaa la pili la solo.

Fan Fan alidumu katika bendi hiyo kwa kipindi kirefu cha miaka 27, tangia mwaka 1967 hadi 1994. Akiwa na bendi hiyo alitoa mchango mkuwa kwa kutunga baadhi ya nyimbo na kulicharaza gitaa. Fan Fan ndiye aliyecharaza gitaa la solo katika vibao vya Djemelasi na Testament vya bendi ya T.P.OK Jazz, ambazo zilitamba sana wakati huo.

Upigaji wake wa gitaa hilo kwenye vibao hivyo umefanana kwa kiasi kikubwa na upigaji wa Franco, kiasi kwamba mashabiki na wapenzi wa muziki huo, waliamini kuwa Franco ndiye aliyecharaza gitaa hilo. Baada ya kujigundua kwamba anaweza kufanya vizuri zaidi akiwa kwenye bendi nyingine, Fan Fan akaamua kwenda nchini Zambia na baadaye akaingia nchini Tanzania.

Akiwa nchini humu, alijiunga kwa mara ya kwanza katika bendi ya Orchestra Makassy, ambako alishiriki kurekodi nyimbo mbalimbali zikiwemo za Morema na Muungano. Mwaka 1979, Fan Fan akawa mmoja wa waanzilishi wa kundi la Super Matimila akiwa pamoja na marehemu Ramadhani Mtoro ‘Dk. Remmy Ongara’.

Nguli huyo kwa kipindi kifupi alipiga muziki katika bendi ya Tancut Alimasi ya mjini Iringa. Mose Sengo Fan Fan baadaye aliondoka nchini kwenda Uingereza ambako alifanya makazi ya kudumu hadi mauti nyalipomfika. Akiwa nchini humo, alikuwa akishirikiana na baadhi ya wanamuziki wenzake kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Jamhuri ya Kongo Brazzaville kurekodi nyimbo nyingi.

Fana Fan mwaka 1993 aliondoka Uingereza akaenda nchini Ubelgiji, ambako alianzisha kundi la Bana OK. Kundi hilo liliwashirikisha wanamuziki kadhaa wa zamani wa bendi ya T.P.OK Jazz kiwemo Papa Noel, wakarekodi albamu moja. Mwaka 1995, alirekodi albamu nyingine akiwashirikisha wanamuziki waliokuwa wakiunda kundi la Somo Somo.

Alirekodi albamu nyingine iliyokuwa na jina la Bayekeleye, ikiwa na nyimbo saba za miondoko ya rhumba mwaka 2005. Hadi mauti yanamfika, Fan Fan alikuwa anatamba na kwa kibao chake Papa Lolo, alichokirekodi nchini Kenya, ambacho kinaelezea kukithiri kwa matukio ya ushirikina katika jamii.

Wakati wa enzi za uhai wake alishiriki katika matamasha mbalimbali ya muziki katika jiji la London, Uingereza, Ubelgiji na Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mungu aipumzishe roho yake pahala pema peponi, amina.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba: 0713331200, 0736331200, 0784331200 na 0767331200.

WATALAAM CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI WAFANYA TAFITI KUTIBU SELIMUNDU

$
0
0
SELIMUNDu(Sickle cell) ni chembe nyekundu ya damu ni mviringo, husafiri kupitia mishipa midogo kabisa ya damu kwa urahisi.

Kwa wagonjwa wenye selimundu, chembe zao za damu huvunjika na kupoteza umbo hilo la mviringo na kuchukua umbo la ndizi au mundu(zana ya mkulima).

Chembe hizo nyekundu za damu zenye umbo la mundu hukwama katika mishipa midogo ya damu mwilini na mtiririko wa damu kwenda sehemu fulani ya mwili unapopungua huku oksijeni ikizuiwa na kusababiaha maumivu makali ya ghafla.

Kutokana na hali hiyo, maumivu makali katika mifupa na vifundo, maumivu yasiyotabirika ambayo yanaweza kutokea mara chache au mara nyingi kama kila mwezi kwa mgonjwa mwenye natatizo hayo.

Hata hivyo,Tanzania inashika nafasi ya tatu katika nchi za Afrika ikiongozwa na Nigeria ambapo mpaka sasa idadi ya watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo inakadiriwa kufikia 11,000.

Kutokana na ukubwa tatizo hilo, wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi(Muhas) wameamua kufanya utafiti na kutafuta njia ya kuutibu ikiwa ni pamoja na kupandikiza uboho(born marrow) na vinasaba kwenye mifupa

Akizungumza kuhusu ugongwa huo , Daktari wa Watoto wa Hospitali ya Rufaa ya Mloganzila jijini Dar es Salaam Mosses Karashani anasema hivi karibuni kumekua na ongezeko la rufaa kwa watoto wanaougua ugonjwa huo kuanzia miezi sita hadi miaka 14 ambapo kati yao, nusu ni wale walio chini ya miaka minane.

"Mtoto ambaye wazazi wao wote wawili(baba na mama) wana vinasaba vya selimundu, kuna uwezekano wa asilimia 25 kupata ugonjwa huo na mtoto ambaye mzazi mmoja hana vinasaba vya ugonjwa huo hawezi kupata ugonjwa huo," anasema Dk. karashani.

Anaongeza kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto walimua kuanzisha kliniki ya watoto wa ugonjwa huo siku ya Jumanne na Alhamisi hospitalini hapo ili waweze kupata huduma bora za matibabu.

Anasema katika siku hiyo zaidi ya watoto 20 wanafika hospitali hapo kupatiwa huduma za matibabu kuanzia umri wa miezi sita hadi miaka 14, ambapo kati yao, nusu yake ni wale wenye umri chini ya miaka 8, jambo ambalo linaonyesha wazi kuwa, tatizo la ugonjwa huo ni kubwa.

Anasema kuwa, watoto wanaougua kwenye ugonjwa huo baadhi yao wanapitia kwenye changamoto mbalimbali ikiwamo ya kukimbiwa na mzazi mmoja au unyanyapaa huku wazazi wengine wakizani mtoto wao amelogwa.

Anasema kuwa, katika nchi zinazoendelea ikiwamo Marekani na India, mtoto mara baada ya kuzaliwa anafanyiwa vipimo maalumu 'screening' ili kubaini matatizo aliyonayo, jambo ambalo linasaidia kuanza matibabu mapema kwa pale anapoonekana ana matatizo.

Anafafanua kuwa vipimo hivyo ni muhimu kwa sababu vinasaidia kujua maradhi ambayo mtoto anaweza kuzaliwa nayo hivyo basi wakati umefika kwa Serikali kuboresha Sera za afya na kuanzisha mpango maalumu wa kuwafanyia vipimo maalumu watoto hao mara baada ya kuzaliwa.

Anasema kuwa, hali hiyo itasaidia kutambua matatizo ya mtoto kuanzia tumboni hadi anapozaliwa, jambo ambalo linaweza kupunguza ukubwa wa tatizo.

WAZIRI MWAKYEMBE KUZINDUA MBIO ZA KIMATAIFA ZA RIADHA MKOA WA ARUSHA

$
0
0
Na John Woinde Shizza, Arusha

WAZIRI wa Habari,Sanaa, Utamaduni na Michezo Dk.Harrison Mwakyembe anatarajiwa kuzindua mbio za kimataifa za riadha za John Stephen Akwari zinazotarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 9 mwaka huu mkoano hapa.

Akizungumza leo mkoani Arusha Mkurugenzi Mtendaji wa mbio hizo,Sylvestar Orao amesema maandalizi yote ya mbio hizo yamekamilika na kutoa mwito kwa wadau wa mchezo huo kutoka ndani na nje ya nchi kujitokeza kushiriki.

Amesema mbio zenye kauli mbiu "Sisi wote ni wakimbiaji,maisha ni mbio" yameandaliwa mahususi kwa ajili ya kumuenzi mwanariadha wa kwanzakabisa kupeperusha vema bendera ya Tanzania kimataifa mzee Jahn Stephen Akwari.

"Katika mbio hizo kutakuwa na mbio za kilomita 21,kilometa tano na kilometa mbili kwa watoto na kwamba vituo vya kujiandikisha vipo katika uwanja wa kumbukumbu ya Sheik Amri Abeid Karume wa mjini hapa na kingine kipo Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam," amesema Orao.

Kwa upande wake Mshauri wa kiufundi wa mbio hizo John Bayo amewataka watu kujitokeza kwa wingi katika mbio hizo kwani michezo hudumisha

amani upendo na umoja na kwamba michezo ni mazoezi ambayo humwepusha mtu na magonjwa mbalimbali.Bayo ameongeza katika mbio hizo mshindi wa kwanza hadi kwa 10 kwa mbio zote watapatiwa zawadi na medali mbalimbali kulingana na aina ya mbio.

MKAA ENDELEVU WAFANIKIWA KUIINGIZIA HALMASHAURI, VIJIJI NA WANANCHI SH. BILIONI TATU KUANZIA MWAKA 2014 HADI 2019

$
0
0
NA SULEIMAN MSUYA

MRADI wa Kuleta Mageuzi Katika Sekta ya Mkaa Tanzania (TTCS) maarufu 'mkaa endelevu' umefanikiwa kuingizia halmashauri, vijiji na wananchi zaidi ya shilingi bilioni 3 kuanzia 2014 hadi sasa.

Hayo yamesemwa na Meneja Mradi wa TTCS, Leonard Charles wakati akiwasilisha mada kwa maofisa mbalimbali kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Serikali Kuu walikutana mkoani Morogoro.

Meneja huyo amesema mradi wa TTCS unatekelezwa katika vijiji 30 vya wilaya za Mvomero, Kilosa na Morogoro chini ya usimamizi wa Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania (TFCG), Mtandao wa Jamii wa Kusimamia Misitu Tanzania (Mjukita), Shirika la Kuendeleza Nishati Asili Tanzania (TaTEDO) na kufadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uswisi (SDC).

Amesema katika mradi huo vijiji 22 vimeanza kunufaika katika pande mbili ambazo ni kiuchumi na utunzaji wa mazingira huku nane vikiwa katika mchakato.

Ameongeza hadi kufikia mwezi Mei 2019 vijiji vimeweza kikusanya mapato halali zaidi ya shilingi bilioni 1.4, wachomaji mkàa shilingi bilioni 1.2 na halmashauri shilingi milioni 500.

Ametaja baadhi ya vijiji ambavyo vimenufaika na mradi ni Ulaya Mbuyuni, Matuli, Kitunduweta, Mlilingwa, Ulaya Kibaoni, Diguzi na vingine.

Leonard amesema mradi wa mkaa endelevu ulianza Machi 2012 katika vijiji 10 lakini baada ya kuonekana mafanikio wamelazimika kuongeza vijiji hadi kufika 30.

"Mradi wa TTCS maarufu mkaa endelevu umefanya mapinduzi makubwa kiuchumi, kijamii na maendeleo katika vijiji vilivyopo kwenye mradi kama kuboresha sekta ya afya, elimu, maji, kilimo na mitaji," amefafanua.

Ameongeza mafanikio ya mradi yamezingatia kutoa elimu kwa jamii husika, watendaji na wafanya maamuzi hivyo kurahisisha utekelezaji.

Amesema pia utekelezaji unazingatia uwepo wa mpango wa matumizi bora ya ardhi za vijiji, kutenga maeneo madogo ya mradi na kuvuna kwa kutumia vitalu.Pia mradi umefanikisha ujenzi wa ofisi za vijiji hali ambayo inarahisisha usimamizi wa mradi.

Kwa upande wake Ofisa Uhusiano wa TFCG, Bettie Luwuge amesema warsha hiyo ya siku tatu imelenga kujenga uelewa kwa pande zote ili kurahisisha utunzaji wa misitu nchini.

Luwuge amesema rasilimali misitu ikitunzwa kwa ushirikiano wa wadau wote inaweza kubadilisha jamii kiuchumi na maendeleo.

"Tumeamua kukutanisha maofisa kutoka sekta ya kilimo, misitu, maliasili na sheria wa wilaya 19 lengo ni kuweza kubadilishana mawazo namna ya kutunza misitu yetu ili iwe endelevu," amesema.

Amezitaja  wilaya husika kwa warsha hiyo ni Kigoma, Kilwa, Tabora, Namtumbo, Handeni, Kilindi, Mvomero, Morogoro, Kilosa, Lindi, Liwale, Tunduma, Kilolo, Ruangwa, Nachingwea, Mpwapwa, Songea, Nyasa, Mbinga.

Awali akifungua warsha hiyo Ofisa Misitu wa Mkoa wa Morogoro, Joseph Chuwa alisema warsha hiyo itasaidia kuongezea uelewa maofisa hao kuhusu utunzaji misitu ya vijiji.

Chuwa alisema rasilimali mali misitu ikitunzwa kwa dhana ya uendelezaji itasaidia jamii kuinuka kiuchumi.
Meneja Mradi wa TTCS, Charles Leonard akitoa mada kuhusu Mkaa endelevu  kwa maofisa mbalimbali kutoka wilaya 19 nchini.

KMC YAACHANA NA KOCHA ETTIENE NDAYIRAGIJE

$
0
0
Klabu ya KMC imetangaza rasmi kuachana na kocha wake raia wa Burundi, Ettiene Ndayiragije baada ya kumaliza mkataba klabuni hapo.

Taarifa iliyotolewa leo na Mwenyekiti wa Bodi ya timu hiyo Benjamini Sitta imeeleza kuwa mkataba wa mwalimu huyo ulimalizika mara baada ya kuhitimishwa kwa msimu wa 2018/19 lakini kocha mwenyewe hakuwa tayari kuongeza mkataba. .

“Baada ya majadiliano ya pande zote mbili, Mwalimu Ndayiragije aliomba kutoongeza mkataba ili aweze kupata changamoto mpya sehemu nyingine. Bodi na uongozi wa KMC umeridhia ombi na matakwa ya mwalimu,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

KMC imetoa shukrani zake kwa kocha huyo kutokana na mchango mkubwa alioutoa kwa timu msimu huu akiiwezesha kumaliza katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara na kupata nafasi ya kuiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

“Tunamtakia kila lenye kheri katika maisha yake mapya ya huko aendako na uongozi unaendelea na mchakato wa kumpata mwalimu mpya,” imemalizia taarifa hiyo.

Kocha huyo anahusishwa kujiunga na Azam FC, huku tetesi zikieleza kuwa KMC wapo kwenye mazungumzo na kocha wa Lipuli FC Selemani Matola kuchukua mikoba hiyo.

NIDHAMU YAWAONDOA MKUDE, AJIBU KIKOSI CHA TAIFA STARS YA AFCON 2019

$
0
0
Kocha Mkuu wa TaifaStars Emmanuel Amunike ametaja kikosi chake cha  wachezaji 32 wanaoondoka nchini leo kuelekea Misri kwaajili ya kambi ya wiki mbili kabla ya kutaja kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 kitakachoshiriki AFCON2019 kuanzia Juni 21 mwaka huu.

Katika kikosi hicho Kocha Amunike amewaacha wachezaji saba kutoka kwenye orodha ya wachezaji 39 wa kikosi cha awali kilichotangazwa mapema mwezi Mei akitumia kigezo za nidhamu na kujituma kwao mazoezini.

Wachezaji walioachwa ni Ibrahim Ajibu (Yanga), Jonas Mkude (Simba SC), Ally Ally (KMC), Kennedy Juma (Singida United), Ayoub Lyanga (Coastal Union), Kassim Khamis (Kagera Sugar) na Shomari Kapombe (Simba SC). Wachezaji 32 wanaoondoka leo ni:

Magolikipa
1. Aishi Manula - Simba SC.
2. Metacha Mnata - Mbao FC.
3. Suleiman Salula - Malindi FC.
4. Aron Kalambo - Tz Prisons.
5. Claryo Boniphace - U20.

Mabeki
6. Hassan Kessy - Nkana FC. 
7. Vicent Philipo - Mbao FC.
8. Gadiel Michael - Yanga SC.
9. Abdi Banda - Baroka FC
10. Ally Mtoni - Lipuli FC.
11. Mohamed Hussein - Simba SC.
12. Agrey Moris - Azam FC
13. Kelvin Yondan - Yanga
14. Erasto Nyoni - Simba SC.
15. David Mwantika - Azam FC.

Viungo wa kati
16. Feisal Salum - Yanga SC.
17. Himid Mao - Petrojet. 
18. Mudathir Yahya - Azam FC.
19. Frank Domayo – Azam FC
20. Fred Tangalu - Lipuli FC.

Viungo wa pembeni
21. Yahya Zayd - Ismailia.
22. Miraji Athuman – Lipuli FC.
23. Farid Musa – Tenerife.
24. Shiza Kichuya – ENPPI.
25. Saimon Msuva – Difaa El Jadidi.

Washambuliaji
26. Shaban Chilunda - Tenerife.
27. Rashid Mandawa – BDF.
28. Mbwana Samatta – KRC Genk.
29. Thomas Ulimwengu – JS Saoura.
30. John Bocco – Simba SC. 
31. Kelvin John – U17.
32. Adi Yusuph – Blackpool.

AZAM YAMUONGEZEA MKATABA KIPA MWADINI ALLY

$
0
0
 Kipa wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Mwadini Ally, ameongeza mkataba mpya wa mwaka mmoja kuendelea kuitumikia timu hiyo. 

Mwadini aliyeanza kuitumikia Azam FC tokea mwaka 2011 akitokea Mafunzo ya Zanzibar, amesaini mkataba huo rasmi leo mchana, akiwa mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu, Abdulkarim Amin 'Popat' na Mratibu wa timu, Phillip Alando.

Mchezaji huyo mwandamizi wa timu hiyo, anazidi kuongeza idadi ya wachezaji waliosaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia Azam FC, wengine wakiwa ni mabeki David Mwantika, Bruce Kangwa, Abdallah Kheri na mshambuliaji Donald Ngoma.

Uongozi wa Azam FC chini ya Popat kwa kushirikiana na benchi la ufundi la timu hiyo, wanaendelea na zoezi la kuwabakisha wachezaji waliomaliza mkataba pamoja na usajili wa wachezaji wapya wa kuongeza nguvu kikosini kwa ajili ya msimu ujao.

Kikosi cha Azam FC kwa sasa kipo mapumzikoni na kinatarajia kurejea mazoezini Juni 20 mwaka huu, tayari kuanza maandalizi ya msimu mpya 2019/2020 ikianza na kibarua cha kutetea Kombe la Kagame (CECAFA Kagame Cup) kuanzia Julai 6 mwaka huu jijini Kigali, Rwanda.

AZAM YAMUONGEZEA MKATABA KIPA MWADINI ALLY

$
0
0
  Kipa wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Mwadini Ally, ameongeza mkataba mpya wa mwaka mmoja kuendelea kuitumikia timu hiyo.

Mwadini aliyeanza kuitumikia Azam FC tokea mwaka 2011 akitokea Mafunzo ya Zanzibar, amesaini mkataba huo rasmi leo mchana, akiwa mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu, Abdulkarim Amin 'Popat' na Mratibu wa timu, Phillip Alando.

Mchezaji huyo mwandamizi wa timu hiyo, anazidi kuongeza idadi ya wachezaji waliosaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia Azam FC, wengine wakiwa ni mabeki David Mwantika, Bruce Kangwa, Abdallah Kheri na mshambuliaji Donald Ngoma.

Uongozi wa Azam FC chini ya Popat kwa kushirikiana na benchi la ufundi la timu hiyo, wanaendelea na zoezi la kuwabakisha wachezaji waliomaliza mkataba pamoja na usajili wa wachezaji wapya wa kuongeza nguvu kikosini kwa ajili ya msimu ujao.

Kikosi cha Azam FC kwa sasa kipo mapumzikoni na kinatarajia kurejea mazoezini Juni 20 mwaka huu, tayari kuanza maandalizi ya msimu mpya 2019/2020 ikianza na kibarua cha kutetea Kombe la Kagame (CECAFA Kagame Cup) kuanzia Julai 6 mwaka huu jijini Kigali, Rwanda.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam Fc Abdulkarim Popat akipeana mkono na kipa Mwadini Ally baada ya kuongeza mkataba wa mwaka mmoja wa kuendelea kuitumia klabu hiyo. 

NIDHAMU YAWAONDOA MKUDE, AJIBU KIKOSI CHA TAIFA STARS YA AFCON 2019

$
0
0
Kocha Mkuu wa TaifaStars Emmanuel Amunike ametaja kikosi chake cha  wachezaji 32 wanaoondoka nchini leo kuelekea Misri kwaajili ya kambi ya wiki mbili kabla ya kutaja kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 kitakachoshiriki AFCON2019 kuanzia Juni 21 mwaka huu.

Katika kikosi hicho Kocha Amunike amewaacha wachezaji saba kutoka kwenye orodha ya wachezaji 39 wa kikosi cha awali kilichotangazwa mapema mwezi Mei akitumia kigezo za nidhamu na kujituma kwao mazoezini.

Wachezaji walioachwa ni Ibrahim Ajibu (Yanga), Jonas Mkude (Simba SC), Ally Ally (KMC), Kennedy Juma (Singida United), Ayoub Lyanga (Coastal Union), Kassim Khamis (Kagera Sugar) na Shomari Kapombe (Simba SC). Wachezaji 32 wanaoondoka leo ni:

Magolikipa
1. Aishi Manula - Simba SC.
2. Metacha Mnata - Mbao FC.
3. Suleiman Salula - Malindi FC.
4. Aron Kalambo - Tz Prisons.
5. Claryo Boniphace - U20.

Mabeki
6. Hassan Kessy - Nkana FC. 
7. Vicent Philipo - Mbao FC.
8. Gadiel Michael - Yanga SC.
9. Abdi Banda - Baroka FC
10. Ally Mtoni - Lipuli FC.
11. Mohamed Hussein - Simba SC.
12. Agrey Moris - Azam FC
13. Kelvin Yondan - Yanga
14. Erasto Nyoni - Simba SC.
15. David Mwantika - Azam FC.

Viungo wa kati
16. Feisal Salum - Yanga SC.
17. Himid Mao - Petrojet. 
18. Mudathir Yahya - Azam FC.
19. Frank Domayo – Azam FC
20. Fred Tangalu - Lipuli FC.

Viungo wa pembeni
21. Yahya Zayd - Ismailia.
22. Miraji Athuman – Lipuli FC.
23. Farid Musa – Tenerife.
24. Shiza Kichuya – ENPPI.
25. Saimon Msuva – Difaa El Jadidi.

Washambuliaji
26. Shaban Chilunda - Tenerife.
27. Rashid Mandawa – BDF.
28. Mbwana Samatta – KRC Genk.
29. Thomas Ulimwengu – JS Saoura.
30. John Bocco – Simba SC. 
31. Kelvin John – U17.
32. Adi Yusuph – Blackpool.

FRESH JUMBE AWAOMBA BASATA KUENZI MCHANGO WA MARIJAN RAJAB

$
0
0

*Akoshwa na Diamond na alikiba

Na.Khadija seif,Globu ya jamii.

NGULI wa muziki dansi barani la Afrika kutoka nchini Tanzania fresh jumbe awatia hamasa kubwa wajapani kujifunza kiswahili kupitia muziki wake.

Jumbe amezungumza na michuzi tv na kuweka wazi kuwa kwa kiasi kikubwa sana wajapani wameweza kujua kiswahili kutokana na muziki ambao amekuwa akifanya kwa muda mrefu sana na kupendwa na watu wengi.

"Wajapani,wachina na watu wengine kutoka mataifa mbalimbali wamekua wakivutiwa sana na muziki wangu kupelekea kutamani kujua kilichoimbwa kuanzia kufahamu matamshi mpaka maneno yaliyoimbwa katika wimbo huo,"

Aidha ,jumbe amesema soko la muziki wa Tanzania limepiga hatua kwa kiasi kikubwa sana na kupelekea vijana wengi kuiepeperusha bendera kwa kupitia sanaa mbalimbali hususani muziki.

"Katika nchi ambazo utazitaja basi huwezi kuacha kuitaja Tanzania kuwepo kwa wanamuziki wanaopendwa sana hivyo tunajitoa kifua mbele ukilinganisha na hapo zamani ni wachache ambao tulikua tunafahamika tena kwa nchi chache lakini kwa sasa hakuna nchi ambayo muziki wa bongofleva haujapata kupenya,"

Amewataja Diamond platinum,Alikiba ndio wasanii ambao anavutiwa na kazi zao kutokana na ubunifu wa hali ya juu wakati wa upishi wa nyimbo zao na kuweka vionjo ambavyo vimewazolea mashabiki wengi ndani na nje ya nchi.

Aidha , ameweka bayana sababu zinazopelekea baadhi ya nyimbo zake kuendelea kupendwa ni kutokana na mashairi ambayo yanaishi na kusadifu maisha halisi wimbo kama penzi ni kikohozi,pamela ,conjesta pamoja na mazingira yetu .

Pia ameomba Baraza la sanaa (BASATA) pamoja na wanamuziki wote nchini kuenzi juhudi za marehemu Marijan Rajab kwa kuweka picha au ukumbusho ambao vizazi vijavo vitaweza kutambua mchango wake kupitia muziki wake.

"Bila jitihada zake na uwezo wa kutambua kipaji changu nisingewezakufika huku nilipo na mbali na hilo marijan amewezakutambulisha vizuri nchi ya Tanzania kwa kupitia miondoko ya muziki wa dansi kwa vionjo vya kiafrika zaidi na ustadi mzuri wa kukuza lugha ya kiswahili kwa vibao vyake kama "masudi,mtaa wa Saba,ndoa ya mateso, mwanameka ,namsaka mbaya wangu na vibao vingine vingi",

Kwa sasa fresh jumbe amesema anaendelea na harakati za muziki wa dansi sanjari na kuwa mtayarishaji wa muziki.
.. mwisho


KMC YAACHANA NA KOCHA ETTIENE NDAYIRAGIJE

$
0
0

Klabu ya KMC imetangaza rasmi kuachana na kocha wake raia wa Burundi, Ettiene Ndayiragije baada ya kumaliza mkataba klabuni hapo.

Taarifa iliyotolewa leo na Mwenyekiti wa Bodi ya timu hiyo Benjamini Sitta imeeleza kuwa mkataba wa mwalimu huyo ulimalizika mara baada ya kuhitimishwa kwa msimu wa 2018/19 lakini kocha mwenyewe hakuwa tayari kuongeza mkataba. .
.
“Baada ya majadiliano ya pande zote mbili, Mwalimu Ndayiragije aliomba kutoongeza mkataba ili aweze kupata changamoto mpya sehemu nyingine. Bodi na uongozi wa KMC umeridhia ombi na matakwa ya mwalimu,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

KMC imetoa shukrani zake kwa kocha huyo kutokana na mchango mkubwa alioutoa kwa timu msimu huu akiiwezesha kumaliza katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara na kupata nafasi ya kuiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.

“Tunamtakia kila lenye kheri katika maisha yake mapya ya huko aendako na uongozi unaendelea na mchakato wa kumpata mwalimu mpya,” imemalizia taarifa hiyo.

Kocha huyo anahusishwa kujiunga na Azam FC, huku tetesi zikieleza kuwa KMC wapo kwenye mazungumzo na kocha wa Lipuli FC Selemani Matola kuchukua mikoba hiyo.

SIMBA SC KUTOSHIRIKI KOMBE LA KAGAME

SERIKALI YA DENMARK KUENDELEZA MSAADA PASS KWA AJILI YA WAKULIMA NCHINI..

$
0
0

Na Hussein Stambuli,Michuzi TV Morogoro.

Bolozi wa Denmark nchini Einar Jensen amesema kutokana na namna ambavyo Asasi ya kusaidia sekta binafsi ya kilimo PASS inavyowawezesha vijana kwenye sekta ya kilimo wataendelea kutoa msaada kwa asasi hiyo kwani inamsaada mkubwa wa kuinua maisha ya vijana wajasiliamli wa kilimoTanzania ..

Balozi huyo alitembelea kituo atamizi cha SUA AIC na kujionea namna ambavyo Zaidi ya vijana 20 wanavyojifunza kwa vitendo ujasiliamali wa nyanya na ambapo alilidhidhwa na namna ambavyo PASS wameandaa utaratibu wa kilimo cha zao hilo kisasa.

“hiki wanachokifanya hapa vijana hawa ndicho kinachohitajika kwa kizazi cha sasa ninancho wasihi ni kuhakikisha mnazidi kuwa wavumbuzi na wabunifu Zaidi katika kila mnachokifanya nasisi tutakuwa bega kwa bega nanyi” alisema Balozi Einar

Mkurugenzi mkuu wa wa PASS Nicodemus Boay amesema vijana waliopo katika kituo hicho wanamoyo mkubwa wa kujikomboa kiuchumi kupitia ujasiliamli huo wa nyanya na anaamini kwa mafunzo na taaluma waliyopata wataweza kufika mbali kwani kupitia PASS watadhaminiwa kupata mikopo na kupata mitaji huku lengo likiwa ni vijana hao waweze kuajiri vijana wenzao.

“hawa vijana wakitoka hapa watachagua mahali pakwenda kufanyia shughuli zao na sisi kama PASS tutawashika mkono kuhakikisha wanafanikiwa kwa wanayotarajia kuyafanya katika mipango yao ya siku zijazo” alisema Boay

Meneja maendeleo biashara wa kituo hicho Richard Bruno ameeleza kuwa kuanzia mwezi Februari hadi Mei mwaka huu wameweza kujiingizia kiasi cha shilingi milioni 15 kupitia mradi wa kituo atamizi cha sua AIC hiyo ni kutokana na mavuno ya nyanya katika kipindi cha miezi mine.
 Balozi wa Denmark nchini Einar Jensen  akijadili jambo na kijana mjasiliamli wa zao la nyanya kuhusu uzalishaji wa zao hilo mkoani morogoro
 Bolozi wa Denmark nchini Einar Jensen kushoto kwake mkurugenzi mkuu wa PASS nchini Nicodemus  Boay akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine wa PASS pamoja na vijana wajasiliamali wa kituo atamizi cha  SUA

KUELEKEA MASHINDANO YA AFCON, VODACOM YAZINDUA KAMPENI YA DATA NA AFCON

$
0
0
* Washindi kujipatia tiketi za kushuhudia na kushangilia timu ya taifa (Taifa stars) mubashara huko Misri

Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii

KAMPUNI ya Vodacom Tanzania, leo Juni 7 imezindua rasmi kampeni mpya kwa wateja wao na mashabiki wa timu ya taifa inayoenda kwa jina la Data na AFCON ikiwa ni katika kutoa mchango wao wa kuishika mkono Taifa Stars inayoshiriki mashindano hayo.

Akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa idara ya biashara kutoka vodacom Linda Riwa amesema kuwa ndani ya kipindi cha kampeni hiyo watatoa zawadi kwa watumiaji kumi wa huduma ya soka letu ambao watajipatia tiketi za kuenda nchini Misri  kushuhudia na kushangilia timu ya taifa ikicheza mubashara kabisa.

Amesema kuwa kampeni hiyo imeanza rasmi leo na itamalizika Julai 21 na wateja watakuwa wakipata dondoo za mechi za ligi mbalimbali zinazoendelea duniani huku zawadi nyingine kemkemu zikiwemo muda wa maongezi na hiyo yote ni kwa kupiga *148*84# na kujiunga na huduma ya soka letu.

Bi. Riwa amesema kuwa kampeni hiyo imekuja kutokana na furaha baada ya timu ya taifa kufuzu kuwania kombe la AFCON hivyo wameona ni vyema kushirikiana na wateja wao ili kuweza kutia hamasa na morali zaidi kwa wachezaji na hatimaye kurudi na kombe hilo nyumbani.

Kwa upande wao wateja wa Vodacom; Juma Hamis wa Mbagala na Christian John wa Mwenge Dar es Salaam wameipongeza kampuni hiyo kwa kuonesha ushiriki wao katika masuala ya burudani hasa soka kwa kipindi hiki ambacho taifa limeelekeza macho yake nchini Misri kushuhudia michuano ya AFCON.
 Mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha Vodacom Tanzania, Jacquiline Materu akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Data na AFCON kupitia huduma ya soka letu iliyofanyika leo Juni 7, 2019 jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Meneja wa kitengo cha Vijana wa Vodacom, Abdi Zagar.



DKT. MAGUFULI ASEMA YOTE YALIYOSEMWA NA WAFANYABIASHARA YATAFANYIWA KAZI

$
0
0

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

RAIS Dk.John Magufuli amewahakikishia wafanyabiashara kutoka Wilaya zote nchini kuwa yote ambayo yamezungumzwa kwenye kikao kati yake na wafanyabishara hao yatafanyiwa kazi.

Akizungumza na wafanyabiashara hao leo Ikulu jijini Dar es Salaam ambapo lengo la kikao hicho ilikuwa ni kujadili masuala mbalimbali yakiwemo yanayohusu changamoto za kwenye sekta ya biashara nchini.

Hata hivyo wakati anazungumzia baadhi ya changamoto na mapendekezo ya wafanyabishara hao, Rais Magufuli amefafanua yote yaliyojadiliwa na yanayoendelea kujadiliwa kati ya Serikali na wafanyabiashara yatapatiwa ufumbuzi na kufafanua kwa sasa Wizara ya Fedha na Mipango kuna mpango mkakati ambao wanauandaa na hivyo baadhi ya mambo yataingizwa.

"Wizara ya Fedha kuna mpango mkakati ambao wanaendelea kuuandaa na utakapokamilika utapelekwa Bungeni, hivyo niwahakikishie yote ambayo yamejadiliwa hapa tayataingizwa kwenye mpango huo kabla ya kwenda bungeni,"amesema Rais Magufuli.

Amefafanua kuna baadhi ya mambo ambayo yalizungumzwa mwaka jana kuhusu kupunguzwa kwa bei ya taulo za kike na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa tamko la Serikali ilitangaza kutoa punguzo lakini wafanyabishara hawajapunguza bei.

"Kuna wakati Serikali inakuwa na nia njema kwa kupunguza bei kwa baadhi ya bidhaa kwa mfano taulo za kike tuliamua kupunguza bei kutokana na maombi ya wananchi.Hata hivyo wafanyabishara wameshindwa kupunguza, hivyo lazima muwe na huruma,"amesema Rais Magufuli.

Ametumia nafasi hiyo kuwataka wafanyabiashara pamoja na Serikali kuweka mikakati ya kusonga mbele na kufafanua badala ya kuendelea kulalamika na kuendelea kulalamika kumesababisha Tanzania kuwa chini kwenye uuzaji wa biashara nje ya nchi.

Rais Dk. Magufuli amewataka wafanyabiashara kuaha woga na kueleza kuna vikwazo vingi ambavyo wanavipata kutoka Mamalaka ya Mapato Tanzania (TRA) lakini ukweli ni kwmaba kwenye kikao hicho wameshindwa kueleza kwasababu ya woga.

"Nilitarajia leo hapa wafanyabiashara mngewataja kwa majina watumishi wa TRA ambao wamekuwa wakiwasumbua lakini naona mmekaa kimya kwasababu mnaogopa.Acheni woga, ninyi wafanyabisara na Serikali tukiungana pamoja tutakwenda na tutapiga hatua,"amesema Rais Dk.Magufuli.
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live




Latest Images