Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

Serikali ya Marekani Yazindua Mradi wa Lishe Endelevu Kukuza Lishe Nchini Tanzania

$
0
0
 Serikali ya Marekani ilizindua mradi wa Lishe Endelevu katika eneo la Kizitwe manispaa ya Sumbawanga, mkoa wa Rukwa. Mradi huu mpya utasaidia kupunguza udumavu kwa watoto, kuongeza idadi ya watoto wanaopata milo yenye ubora, na kuboresha lishe kwa wanawake waliofikia umri wa kuzaa.

Lishe Endelevu, inayofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) na kutekelezwa na Save the Children, inaonesha ushirikiano wa muda mrefu kati ya Marekani na Tanzania katika kuboresha maisha ya Watanzania. 

"Serikali ya Marekani inaungana na Serikali ya Tanzania kwa kutambua kuwa watoto wenye afya ni viongozi wa baadae wa Tanzania. Lishe bora itawapa watoto wa Tanzania uwezo wa upeo wao katika afya, elimu, na uzalishaji wa kiuchumi, "alisema Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Andy Karas, wakati wa uzinduzi.

Pamoja na kuboresha utoaji wa huduma za lishe, Lishe Endelevu itasaidia shughuli za maji na usafi ili kusaidia lishe bora. Mradi huu pia utaongeza upatikanaji wa vyakula kwa kukuza mazao mengi yenye virutubisho, teknolojia ya kisasa, na ufugaji wa mifugo wadogo bora kwa afya.

Kwa maelezo ya ziada kuhusu Lishe Endelevu, tembelea tovuti hii:


KATIBU TAWALA ATOA MAELEKEZO KWA TFDA KUWEZESHA WAJASIRIAMALI KUANZISHA VIWANDA VYA CHAKULA MKOA WA MARA

$
0
0
Na  James Ndege - Musoma
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara ameilekeza Mamlaka ya Chakula na Dawa kuanzisha mikakati endelevu ya kuwezesha wajasiriamali wadogo wa mkoa wa Mara  kuzalisha bidhaa zitakazokubalika katika soko la ndani na nje ya nchi wakati alipofungua mafunzo ya siku mbili yanayoendeshwa na TFDA  kwa wajasiriamali wadogo 100 wa usindikaji wa vyakula wa mkoa wa Mara katika ukumbi wa Mikutano wa Mkoa wa Katibu Tawala wa Mara uliopo mjini Musoma kuanzia tarehe 29 – 30 Mei, 2019.

Maelekezo hayo ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara yalitolewa na mwakilishi wake ambaye ni Kaimu Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa huo, Bw. Denis Nyakisunda aliyekuwa Mgeni Rasmi katika ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyokuwa na lengo la kuwezesha ukuaji wa Sekta ya  viwanda nchini vinavyokidhi vigezo vya usalama na ubora ili kupata soko la bidhaa za Tanzania la  ndani na nje ya nchi hivyo kukuza uchumi wa nchi

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Nyakisunda alisema “Ninafurahi kuona TFDA leo wanatoa mafunzo haya muhimu ili ninyi wasindikaji wa mkoa huu muweze kuanzisha viwanda vidogo lakini pia nawaasa TFDA kuweka mazingira rafiki kwa kuwawezesha wajasiriamali wa mkoa wangu kutatua changamoto walizonazo katika uanzishaji wa viwanda vidogo vya vyakula”.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula kutoka TFDA Makao Makuu, Bw, Lazaro Mwambole aliwapongeza wasindikaji hao kwa kujitokeza kwa wingi katika mafunzo hayo na kuwaasa kuzingatia ushauri wa wataalam katika kuzalisha bidhaa zao ili ziweze kusajiliwa na TFDA hivyo kupata soko la ndani na nje ya nchi.

 “Mkizingatia mada za mafunzo zinazotolewa hapa na kushirikiana kwa pamoja, suluhisho la changamoto hizo zitabadilika kuwa fursa. Ofisi ya TFDA Kanda ya Ziwa Mashariki pamoja waratibu wa majukumu ya TFDA katika Halmashauri zenu wapo nanyi siku zote hivyo watumieni kupata huduma na ushauri mara kwa mara” alihitimisha kiongozi huyo.

Mafunzo husika yamefungwa na Meneja wa SIDO wa mkoa wa Mara Bi. Frida Mungulu ambaye alipokea maazimio sita kutoka kwa washiriki ili yafanyiwe kazi katika ngazi mkoa kwa nia ya kupata ufumbuzi wa changamoto za uanzishaji viwanda kwa wajasiriamali hao.
Katika mafunzo hayo, TFDA ilishirikisha Taasisi nyingine za Serikali za Shirika la Kuendeleza Viwanda Vidogo (SIDO), Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Tantrade ili kuwawezesha wasindikaji hao kutambua mambo muhimu yanayotakiwa katika kuzalisha bidhaa zinazokubalika kwa mujibu wa sheria zilizopo. Mafunzo hayo ya TFDA ni endelevu na mkoa wa Mara umekuwa mkoa wa 26 nchini kupata mafunzo ya aina hiyo.
 Mgeni Rasmi katika Mafunzo hayo, Mwakilishi wa  Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Denis Nyakisinda akisisitiza jambo kwa wajasiriamali (hawapo pichani) katika hotuba ya ufunguzi wakati mafunzo ya siku mbili yanayoendeshwa na TFDA  kwa wajasiriamali wadogo 100 wa usindikaji wa vyakula wa mkoa wa Mara katika ukumbi wa Mikutano wa Mkoa wa Katibu Tawala wa Mara
 Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula TFDA, Bw. Lazaro Mwambole akiwasilisha mojawapo ya mada kwa washiriki wakati wa mafunzo ya siku mbili yanayoendeshwa na TFDA  kwa wajasiriamali wadogo 100 wa usindikaji wa vyakula wa mkoa wa Mara katika ukumbi wa Mikutano wa Mkoa wa Katibu Tawala wa Mara. 
Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada katika mafunzo ya siku mbili yanayoendeshwa na TFDA  kwa wajasiriamali wadogo 100 wa usindikaji wa vyakula wa mkoa wa Mara katika ukumbi wa Mikutano wa Mkoa wa Katibu Tawala wa Mara.
 Picha ya pamoja baina ya wajasiriamali na wawakilishi wa taasisi za Serikali katika mafunzo hayo. Waliokaa ni Mgeni Rasmi  aliyemwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara,  Denis Nyakisinda (Katikati), Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Chakula TFDA, Bw. Lazaro Mwambole (wa kwanza kushoto) na Kaimu Meneja wa TFDA Kanda ya Ziwa Mashariki, Bi. Nuru Mwasulama.

WADAU WA AFYA ZANZIBAR WAKUTANA KUTATHMINI ATHARI NA MATOKEO YA KIAFYA

$
0
0
Na Fatma Kassim
WIZARA ya Afya imesema suala la kukabiliana na Majanga si la Wizara ya Afya pekeake linahitaji mashirikiano na taasisi mbalimbali kwa lengo la kukabiliana na majanga yanayoweza kutokea.

Akifungua mkutano wa wadau wa afya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Halima Maulid Salum amesema ushirikiano wa taasisi tofauti katika nchi ndio njia pekee itakayowezesha kuondosha hali ya hatari.

Alifahamisha kwa sasa Zanzibar imejiweka tayari katika kukabilina na hali ya majanga mbalimbali ikiwemo ya maradhi ya miripuko ambapo katika maradhi ya kipindupindu wameweza kupigahatua kubwa ya kuyaangamiza kutoka na ushirikiano uliopo baina ya taasisi mbalimbali ikiwemo Halmashauri na Wilaya.

Amesema Wizara ya afya itahakikisha inashirikiana na wadau wote ikiwemo washirika wa maendeleo wakiwemo Shirika la Afya Duniani WHO katika kujiweka tayari na hali ya majanga ya maradhi ya miripiko yatakapo tokea ili yasiweze kuleta athari nchini.

Amezitaka Tasisi zote husika kupanga mipango madhubuti itakayo saidia kukabiliana na hali yoyote ya hatari, majanga sambamba na kuondosha kabisa maradhi na kuepuka miripuko.

Nae Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Afya Duniani aliyopo Zanzibar Dk. Andemichael Ghirmay amesema kutokana na majanga yanayongezeka Duniani kote ni vyema kuwepo kituo cha kuratib matukio ya kiafya Wizara ya Afya alishauri.

Ameiomba Wizara ya afya kwa kushirikiana na sekta mbalimbali Kuchukua hatua za makusudi za kuanzisha vituo vya dharura sehemu tofauti ambavyo vitatumika katika kukabiliana na majanga mbalimbali pindipo yatatokea.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Halima Maulid akifungua warsha ya wadau wa kutathmini athari za matukio ya Kiafya uliofanyika katika ukumbi wa Kitengo Shirikishi cha Afya ya Uzazi na Watoto Kidongochekundu Mjini Zanzibar.
 Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Ofisi ndogo ya Zanzibar Dr. Andemichael Ghirmay akisoma hutuba yake katika Mkutano wa wadau wa afya na kutoa pendekezo la kuwepo kituo cha kuratib matukio ya kiafya Wizara ya Afya.
 Dkt. Mlenge Mgendi akiwasilisha rasimu ya mwazo ya ripoti ya wadau wa Afya ya kutathmini athari na matukio ya kiafya Zanzibar.
 Baadhi ya wadau wa Mkutano wa kutathmini athari na matukio ya kiafya Zanzibar wakifuatulia mkutano huo.
Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Halima Maulid (watano kutoka kushoto) katika picha ya pamoja na wadau wa afya kutoka taasisi mbalimbali. Picha na Makame Mshenga.

SERIKALI KUJA NA MBINU ZA ZIADA KUKABILIANA NA UGONJWA WA MNYAUKO WA MIGOMBA-MHE BASHUNGWA

$
0
0
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) akijibu swali bungeni leo tarehe 31 Mei 2019 wakati wa mkutano wa kumi na tano wa Bunge la Bajeti Jijini Dodoma. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo) 
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Kulia) pamoja na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) wakifuatilia kipindi cha maswali na majibu bungeni leo tarehe 31 Mei 2019 wakati wa mkutano wa kumi na tano wa Bunge la Bajeti Jijini Dodoma.



Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma

Kwa kipindi cha Mwaka 2006 - 2014, Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Uongozi wa Mkoa wa Kagera umetoa mafunzo ya kutokomeza ugonjwa wa mnyauko wa migomba kwa wakulima na maafisa ugani kwenye wilaya zote zilizoathirika. 

Serikali imekuwa ikiendesha kampeni ya kung’oa migomba yote iliyoathirika, kukata Ua Dume na kuiteketeza. Halmashauri zote za Wilaya za Mkoa wa Kagera ziliweka sheria ndogo ndogo za kuwataka wakulima kung’oa na kuchoma au kuzika migomba yote iliyoathirika. Zoezi hilo lilipunguza ueneaji wa ugonjwa huo kwa asilimia 70. 

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa (Mb) ameyasema hayo leo tarehe 31 Mei 2019 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe Jasson Samson Rweikiza Mbunge wa Bukoba vijijini aliyetaka kufahamu Serikali ina mpango gani kuchukua hatua za makusudi za kupambana na ugonjwa huo na kutokomeza kabisa.

Bashungwa alisema kuwa Serikali inaendelea kufanya tafiti za kuzalisha miche bora ambayo haina vimelea vya ugonjwa wa unyanjano kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) ikishirikiana na Shirika la Belgium Technical Cooperation. 

Aidha, hadi sasa miche bora milioni sita (6) imezalishwa na kusambazwa kwa wakulima katika Mikoa ya Kagera na Kigoma. 

Bashunwa ametoa wito kwa wakulima kote nchini kutumia mbegu bora za migomba aina ya Shia 17, Shia 23, Nshakara, Nyoya, na Kinohasha zinazozalishwa katika taasisi za utafiti kama Chuo kikuu cha Kilimo Sokoine, Mikocheni, Uyole, Kibaha, Maruku na Tengeru ili kuongeza tija katika uzalishaji na kutosafirisha ndizi zilizofungashwa na majani ya migomba kutoka mashamba yaliyoathirika. 

Aliutaja ugonjwa huo wa Mnyauko wa migomba ambao kitaalamu unaitwa unyanjano wa migomba kuwa husababishwa na vimelea aina ya bacteria ambao hushambulia aina zote za migomba na jamii yake. 

Ugonjwa huo husambazwa na ndege, nyuki, binadamu, ngedere na tumbili; miche iliyoathirika; vifaa vya shambani vilivyotumika kwenye migomba iliyoathirika na vifungashio vya kusafirishia ndizi.

KIPINDUPINDU CHAUA MMOJA ILALA, 13 WAPATIWA MATIBABU

$
0
0
Said Mwishehe,Globu ya jamii


WATU 14 wameugua kipindupindu na mmoja kati yao amefariki dunia kwa ugonjwa huo katika Halmashauri ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia kuibuka kwa ugonjwa huo, Kaimu Meya wa Halmashauri ya Ilala Omar Kumbilamoto amesema baadhi ya wagonjwa wametoka maeneo ya Buguruni.

"Kipindupindu kimeingia kwenye manispaa yetu kwani tayari kuna watu 14 wameugua ugonjwa huo na mmoja kati yao amefariki dunia, wengine wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa na watu wanne bado wanaendelea kubapata matibabu,"amesema Kumbilamboto.

Amefafanua sababu za kuibuka kwa ugonjwa huo unatokana na mvua ambazo zimenyesha siku za karibuni na kibaya zaidi kuna baadhi ya watu waliokuwa wanafungulia maji machafu kwenye maji ya mvua, hivyo kusababisha kipindupindu.

Kumbilamoto amesema kutokana na kuibuka kwa ugonjwa huo wamechukua tahadhari ili usiendelee huku manispaa hiyo ikiweka mikakati ya kukomesha ugonjwa huo.

Pia amesema wananchi wanapaswa kubadili tabia kwa kutochafua mazingira kwani magonjwa mengi ya mlipuko chanzo chake ni uchafu.

Wakati huo huo Kaimu Meya huyo amesema Halmshauri ya Ilala tayari imeshatoa Sh.milioni 52 kwa ajili ya kununua dawa za kutibu ugonjwa wa Dungeu.

"Halmashauri ya Ilala imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa wa Dengue,"amesema Kumbilamoto na kuongeza fedha nyingi zinatumika kwa ajili ya kuhakikisha afya za wananchi zanakuwa salama.

USWISI KUBORESHA MAISHA YA VIJANA KWA KUIMARISHA UJUZI KUPITIA MAFUNZO YA UFUNDI STADI

$
0
0
*Bilioni 55 zatolewa ili kuwajengea vijana ujuzi

AWAMU ya kwanza  ya programu ya kuwasaidia vijana nchini katika kuboresha maisha yao kupitia programu za kuimarisha ujuzi imezinduliwa rasmi leo huku shirika la maendeleo na ushirikiano la Uswisi (SDC) likitoa shilingi bilioni 55 kwa kipindi cha miaka 12 katika kuboresha maendeleo ya mafunzo ya ufundi stadi nchini Tanzania.

Akizungumza katika warsha hiyo ya uzinduzi Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako amesema kuwa mafunzo hayo yatanufaisha vijana wengi na takribani vijana 15,000 watafikiwa na mafunzo hayo huku akieleza kuwa kupitia sekta ya elimu vijana watapata nafasi ya kujifunza kilimo bora na cha kisasa ili kutengeneza ajira nyingi zaidi.

 Amesema kuwa mradi huo utakuwa karibu na sekta binafsi ili kuwawezesha vijana kupata ajira huko, na kusisitiza  kuwa mafunzo yanayotolewa lazima yaendane na mfumo wa soko la sasa na kuwa kupitia mradi huo wataboresha mifumo ya ufundishaji na ujifunzaji kwa vyuo 16 vya maendeleo ya wananchi ili kuweza kuendana na mafunzo ya kiteknolojia na hiyo ni kutoa mafunzo kwa wakufunzi  ili waweze kuwanoa wanafunzi na kuwafanya wawe wabobezi katika ujuzi wa fani wanazozisomea tangu wakiwa shuleni.

Vilevile ameishukuru Serikali ya Uswisi kwa ushirikiano waliouonesha kwa serikali kwa kutoa bilioni 55 za kuendeleza ujuzi na vijana kupata ajira au kuajirika kwa urahisi zaidi na amehaidi kuwa watanzania wengi wafanufaika na mradi huo.

Kwa upande wake Balozi wa Uswisi nchini Florence Tinguely Mattli amesema kuwa programu hiyo ni mkakati wa taifa wa maendeleo ya stadi na ufundi mkakati unaolenga kuimarisha na kukuza fursa za maendeleo ya stadi zinazotokana na mahitaji ya ajira, huku akieleza matarajio makubwa ya programu hiyo nchini ni kuendeleza ujuzi na kuwawezesha vijana kujiajiri na kuajiriwa kirahisi zaidi.

Balozi Mattli amesema kuwakupitia programu hiyo watashirikiana na sekta binafsi pamoja na  vyuo vya mafunzo stadi VETA ili kuweza kuyafikia malengo yaliyowekwa kwa urahisi zaidi huku wanawake wakipewa kipaumbele zaidi na kuahidi kuwa kupitia mafuzo hayo watanzania wajiandae kupokea huduma bora zenye viwango bora zaidi na hiyo ni kupitia kauli mbiu ya Hapa Kazi Nzuri Tu!

Uswisi imekuwa na ushirikiano mkubwa na serikali ya Tanzania  na imekuwa ikichangia katika kuendeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo tangu mwa 1960 kwa kutoa shilingi bilioni 51 kila mwaka katika kusaidia sekta za elimu, afya, kilimo, utawala bora, ajira na mapato.
Balozi waUswisi nchini Florence Tinguely Mattli  akizungumza kuhusu programu ya kuwasaidia vijana nchini katika kuboresha maisha yao kupitia programu za kuimarisha ujuzi huku shirika la maendeleo na ushirikiano la Uswisi (SDC) likitoa shilingi bilioni 55 kwa kipindi cha miaka 12 katika kuboresha maendeleo ya mafunzo ya ufundi stadi nchini Tanzania iliyofanyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Prof. Joyce Ndalichako akizungumza wakati wa uzinduzi wa programu ya kuwasaidia vijana nchini katika kuboresha maisha yao kupitia programu za kuimarisha ujuzi huku shirika la maendeleo na ushirikiano la Uswisi (SDC) likitoa shilingi bilioni 55 kwa kipindi cha miaka 12 katika kuboresha maendeleo ya mafunzo ya ufundi stadi nchini Tanzania.
Profesa Samuel Wangwe akiwasilisha mada wakati wa uzinduzi wa programu ya kuwasaidia vijana nchini katika kuboresha maisha yao kupitia programu za kuimarisha ujuzi uliofanyika leo katika ukumbi wa hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wadau wakichangia mada kwenye uzinduzi wa programu ya kuwasaidia vijana nchini katika kuboresha maisha yao kupitia programu za kuimarisha ujuzi uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa elimu wakiwa kwenye mkutano wa uzindizi wa programu ya kuwasaidia vijana nchini katika kuboresha maisha yao kupitia programu za kuimarisha ujuzi utakadumu kwa miaka 12 uliofanyika leo katika ukumbi wa hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Picha ya Pamoja

SERIKALI INAWAKARIBISHA WAWEKEZAJI BINAFSI KUKIFUFUA KIWANDA CHA GENERAL TYRE ARUSHA

$
0
0
Waziri wa viwanda na Biashara, Josephat Kakunda 
Na.Vero Ignatus,Arusha.

SERIKALI inakaribisha Wawekezaji wa Sekta binafsi wanaotaka kufufua kiwanda cha matairi cha General Tyre kilichopo Jijini Arusha, kupeleka barua zao na kufanya mazungumzo kwenye Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC), ili waweze kuingia ubia na serikali kwa ajili ya kufufua kiwanda hicho haraka iwezekanavyo.

Waziri wa Viwanda na Biashara Josephat Kakunda ameyasema hayo Jijini hapa alipotembelea kiwanda hicho na kukagua eneo la kiwanda hicho, amesema bwatapokea barua hizo na mapendekezo ya wawekezaji wa sekta binasfi hadi Agosti mwaka huu na wapo waliopeleka tayari, ili waanze mchakato wa kukifufua kwa ajili ya kuwezesha watu zaidi ya 5000 kupata ajira.

Waziri Kakunda dhamira ya serikali kufufua viwanda vyote ambavyo vimekufa na hadi kufikia Juni mwakani wawe wameanza utaratibu wakufufua viwanda hivyo na mtu asiyefahamu NDC ilipo aende ofisi z aMkuu wa Mkoa Arusha atapewa maelekezi sahihi.

Kakunda amesema Tanzania ilikuwa na viwanda 156 kati ya hivyo 88 vinafanya kazi,68 vinamatatizo na 20 vimefutwa katika orodha ya viwanda sababu ya wamiliki kuuza kwa mtindo wa rejareja.

“Lakini viwanda 48 vilivyobaki kati ya hivyo 16 vimerejeshwa serikali ambapo kati ya hivyo 32 vipo tayari katika mchakato wa kuvifufua kwa kushirikiana na sekta binafsi na wale wenye viwanda kama wanafahamu vimekufa na hawana mpango wowote wa kuvifufua serikali tutawanyang’anya ifikapo Juni Mosi mwaka huu,ila kama wanampango w akufifufua hawana shida nao, lengoi ifikapo Juni mwakani tuanze utaratibu wa kuvifufua,”alisema

Amesema kwa viwanda ambavyo vimegeuzwa makanisa hawana shida na makanisa ila watachukua na makanisa hayo watalazimika kuomba wamiliki wa viwanda waliowapatia maeneo hayo kuwapatia maeneo mengine ya kanisa.

Aidha ameipongeza serikali ya Mkoa wa Arusha kwa kulinda eneo la kiwanda hicho na kuhakikisha halijaharibiwa.Kakunda amesema kufufuka kwa kiwanda hicho sio itasaidia ajira Tanzania pekee bali hata Afrika Mashariki na Kati na nchi za Kusini mwa Afrika watanufaika.

Kuhusu katazo la mifuko alisema serikali imeweka mazingira bora ya kuhakikisha wananchi wanapata mifuko mbadala na siyo iliyokatawa kwa kuongeza uzalishaji kwenye viwanda 15 vilivyopo nchini.

“Kama jana nimetembelea kiwanda cha Hai Mkoani Kilimanjaro ambacho kinazalisha mifuko 680,000 kwa siku na pia kuagiza kiwanda cha Mgololo Iringa kiongeze uzalisha mara tatu wa malighafi za kutosha ili wenye viwanda waweze kutengeneza zaidi mifuko ya karatasi na mingine,”alisema.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo alisema serikali mkoani hapa, ipo tayari kutoa ushirikiano kwa serikali katika ufufuaji wa kiwanda hicho na hata ikibidi kukiwepo na uhitaji wa eneo la ziada kwa ajili ya kiwanda hicho watasaidia kupatikana.

Waziri Jafo atoa maelekezo maalumu kwa Ma-RC, Ma DC na Wakurugenzi

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jafo amewaagiza wakuu wa Mikoa minne iliyopo kwenye mradi wa “lishe Endelevu” kuhakikisha kuwa mikataba hiyo ya utekelezaji wa afua za lishe inawashukie wakuu wa Wilaya, nao wasainiane na wakurugenzi wa halmashauri, nao pia waishushe kwa watendaji wa kata na watendaji hao wasainiane na watendjai wa vijiji na mitaa ili utekelezaji wa mikataba hiyo kuwa shirikishi bila ya kubagua eneo lolote la utawala. 

Amesema kuwa pamoja na utekelezaji wa mradi huo, Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa niaba ya Makamu wa Rais alisainishana mkataba wa utekelezaji wa afua za lishe na wakuu wa Mikoa yote nchini ili kuchochea utekelezaji wa shughuli za lishe hapa nchini, mkataba ambao una viashiria kumi ambavyo vinampima Mkuu wa Mkoa kila baada ya miezi sita na utadumu kwa kipini cha miaka minne kuanzia januari 2018 hadi 2021

“Kwa vile eneo hili ni eneo la mradi maalum, nitatamani sana niweze kuona katika mbao za vijiji vyetu ambavyo miradi hii inatekelezeka, tuwe na taarifa licha ya taarifa ya mapato na matumizi, kuwe na taarifa ambayo inasema katika Kijiji X, Kijiji cha Milepa, Kijiji cha Wampembe ama Kijiji kingine inaonesha watoto wenye udumavu ni wangapi na watoto wenye upungufu wa damu ni wangapi, hili jambo ninlazima tushikane kila mtu atomize wajibu wake kuhakikisha ajenda ya lishe tunaisimamia kwa nguvu zote,” Alisisitiza.

Ameyasema hayo alipokuwa akizindua mradi wa Lishe Endelevu unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani (USAID) unaotekelezwa katika Mikoa minne ya Iringa, Dodoma, Morogoro pamoja na Rukwa ikiwa ni mchango wa Serikali ya Marekani katika kuisaidia Serikali ya Tanzania kufikia lengo la kupunguza tatizo la udumavu kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano kutoka asilimia 34 hadi asilimia 28 ifikapo mwaka 2021.

Akitoa salamu za mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo alitaja baadhi ya mambo yanayopelekea wananchi wa Mkoa wa Rukwa, hususan watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano kuwa na hali duni ya lishe huku akisistiza Utamaduni na mazoea ya wananchi wengi kutumia aina fulani za vyakula hususan nafaka kwa muda mrefu bila kuchanganya na makundi mengine ya vyakula, hivyo kukosa virutubishi muhimu.

“Wananchi wengi hasa wanaoishi Vijijini kutokuwa na Elimu ya kutosha kuhusu masuala ya lishe bora.Baadhi ya akinamama na familia kwa ujumla, kutozingatia taratibu za unyonyeshaji na ulishaji bora kwa watoto wenye umri chini ya miaka miwili. Baadhi ya akina mama wenye watoto wadogo kukosa muda wa kutosha wa kuwahudumia watoto wao kwa lishe bora,” Alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirila la Maendeleo la Watu wa Marekani Andrew Karas aliishukuru serikali kwa kuweka kipaumbele juhudi za kuhakikisha inapunguza hali ya udumavu nchini kwa kutekeleza afua mbalimbali kuanzia ngazi ya kitaifa hadi kwenye halmashauri huku akimpongeza mgeni rasmi wa shughuli hiyo Suleima Jafo na Wizara ya TAMISEMI kwa kutoa kipaumbele maboresho ya lishe.

“Sisi sote tunatambua mchango wa Lishe katika maendeleo jumuishia na maendeleo endelevu, tunavyojua Tanzania inaendelea kukumbwa na viwango vya juu vyua utapiamlo Mkoani Rukwa zaidi ya nusu ya watoto waliochini ya miaka mitano wana udumavu ambayo ni asilimia kubwa zaidi nchini, utapiamlo una athari mbaya kwa mtu binafsi, familia na taifa, unaathiri maendeleo ya Kimwili na pia kiakili, lishe duni huchangia kuwa na uwezo mdogo wa kujifunza,” Alisema.

Mradi huu unalenga kuongeza na kuboresha upatikanaji na utoaji wa huduma bora za lishe katika vituo vya afya na jamii, uzalishaji na ulaji wa vyakula vyenye virutubishi kwa wingi katika ngazi ya kaya, udhibiti wa usawa wa kijinsia katika mapato na matumizi ya rasilimali za nyumbani ili kuhakikisha upatikanaji wa vyakula mchanganyiko.

Shirika la maendeleo la Watu wa marekani limetenga zaidi ya dola za kimarekani milioni 19 ili kutekeleza mtadi wa lishe Endelevu kwa kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka 2018 hadi 2022 katika Mikoa minne na Halmashauri 22 za Tanzania Bara na kulenga kufikia zaidi ya wanawake milioni 1.5 walio katika umri wa kuzaa, watoto milioni 1.1 walio chini ya umri wa miaka mitano na vijana walio katika rika la baleghe 330,000 wenye umri wa miaka 15-19.
 - Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jafo (kushoto) akimkabidhi mkataba wa utekelezaji wa mradi wa Lishe Endelevu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo katika hafla ya uzinduzi wa Mradi huo uliofanyika kitaifa mkoani Rukwa.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jafo (kushoto) akimkabidhi mkataba wa utekelezaji wa mradi wa Lishe Endelevu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ali Hapi katika hafla ya uzinduzi wa Mradi huo uliofanyika kitaifa mkoani Rukwa.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jafo (katikati Mwenye suti) katika picha ya pamoja na wakuu wa mikoa ya Songwe, Katavi, Iringa na Rukwa pamoja na makatibu Tawala wa Iringa, Morogoro pamoja na Waganga Wakuu wa mikoa ya Dodoma na Rukwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga muda mfupi baada ya uzinduzi wa kitaifa wa mradi wa Lishe Endelevu.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo (wa pili toka kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ali Hapi (wa pili toka kushoto) wakitia saini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa lishe Endelevu unaodhaminiwa na Shirika la maendeleo la Watu wa Marekani (USAID) muda mfupi kabla ya uzinduzi rasmi huku nyuma yao kukiwa na makatibu tawala wa mikoa hiyo inayotekeleza mradi huo.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jafo (mwenye suti) akiwasalimia wananchi walifika kupata huduma katika banda la Taasisi ya Jakaya Kikwete kutoka kitengo cha Afya ya Moyo.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jafo (mwenye suti) akiwatunza wanafunzi wa shule ya Sekondari Kizwite waliokuwa wakitoa burudani ya wimbo wao wa Lishe Endelevu katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa lishe Endelevu uliofanyika kitaifa Mkoani Rukwa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi (wa Kwanza kushoto) pamoja na Mkuu wa mkoa wa Katavi Juma Homera wakikituza kikundi cha Kwaya cha Laela kilichokuwa kikitoa burudani katika viwanja Ndua Mjini Sumbawanga kulifanyika hafla ya uzinduzi wa kitaifa wa mradi wa Lishe Endelevu.

RAFIKI YANGU WA MUDA MFUKO RAMBO REST IN PEACE,SITAKUHTAJI TENA

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii 

SIKUMBUKI ni lini kwa mara ya kwanza Mfuko wa Plastiki maarufu kwa mfuko wa Rambo uliingia nchini.Sikumbuki. Ndio. 

Ila ninachokumbuka mfuko wa Rambo kwa hapa nchini umeishi kwa muda mrefu sana.Kuna watu tunao hapa nchni wamezidiwa umri na mfuko wa Rambo. 

Na kwa sehemu kubwa watu wamekuwa wakiitumia kubebea bidhaa mbalimbali.Wapo waliokuwa wanaitumia kubebea vyakula, wapo waliokuwa wanaitumia kubebea nafaka na wapo waliokuwa wanaitumia kwa matumizi mbalimbali. 

Ama kweli mfuko wa Rambo ulikuwa rafiki wa kila mtu.Hukuwa mbishi kwani kila aliyehitaji kukutumia alikupata.Kwa umri wako hapa nchini Tanzania wengi wamekutumia.Walikuamini kwani hukuwa mrahisi rahisi.Wewe mfuko wa Rambo ulikuwa mgumu tena mgumu haswaa .Ngoja nitumie lugha rahisi mfuko wa Rambo ulikuwa imara sana. 

Wakati unaingia nchini mfuko wa Rambo umaarufu wako ulishika kasi kama moto wa kifuu.Unajua kwanini jina lako la Rambo ni jina maarufu kwani kabla ya hapo tayari wengi wetu tulikuwa tunalisikia na kuliona kwenye filamu za mapigano. 

Kuna jamaa anaitwa Sylvester Stallone a.k.a Rambo.Huyu ni jamaa hajawahi kuja nchini Tanzania lakini maarufu sana.Filamu zake nyingi zimepata nafasi ya kutamba katika nchi yetu.Nusu ya kizazi cha Watanzania kimewahi kutazama au kusikia uwezo wa Rambo. 

Katika mabanda ya kuonesha video miaka ile ya nyuma nyuma , haipiti wiki bila kuoneshwa picha la Rambo.Ndio maana mfuko wa plastiki uliokuwa na picha ya Rambo aliyevalia kitambaa cha usongo kichwani ikapata umaarufu. 

Kuanzia hapo kila mtu akienda kununua bidhaa hataki tena kubeba kikapu kisa kuna mfuko wa Rambo.Kila mahali Rambo...yaani Rambo Ramboo.Mitaani huko mifuko ya Rambo ikawa inazagaa.Ni kweli kwa wakati ule wengi wetu tuliamua tu kutaza faida ya mfuko wa Rambo katika kubebea vitu mbalimbali. 

Hatukuwahi kuwaza madhara yake.Kila mmoja aliamini mfuko wa Rambo poa tu, Mbona freshi yaani kama naweza kubebea machungwa au ndizi zikafika nyumbani salama tatizo liko wapi? Maskini ya Mungu hatukuwa tunajua madhara yake. 

Uwepo wa mifuko ya plastiki ukiwemo huo wa Rambo madhara yake ni makubwa.Tena makubwa sana na hasa katika eneo la kimazingira.Ni mifuko ambayo imesababisha madhara makubwa ndani ya jamii yetu.Mifugo mingi imekufa kwasababu tu ya kula plastiki.Mitaro ya kupitisha maji taka nayo mingi imeziba kisa mifuko ya plastiki. 

Binafsi nikiri nilikuwa na urafiki mkubwa na mifuko ya plastiki lakini baada ya Serikali yangu ya Awamu ya Tano kuamua kueleza madhara yake kwa kweli sitakaa niitumie tena. 

Kwani kuna ubaya gani unapoamua kumuweka kando rafiki ambaye uliamini ni msaada kumbe ana madhara makubwa katika maisha yako na kama si yako basi ya anayekuja.Potelea mbali sitaki tena urafiki na mifuko ya plastiki. 

Nitatafuta mfuko mbadala wa kubebea bidhaa zangu.Samahani kama nitakuwa nimekukwaza unayesoma hii kitu.Naomba tu niseme huko unakokwenda mfuko wa plastiki nenda ukapumzike kwa amani(RIP mfuko Rambo). 

Kwa mujibu wa watalaamu na wanamazingira wanaeleza wazi mfuko wa plastiki unapotengenezwa unakaa kwa miaka 500.Yaani chukulia mfuko wa plastiki ambao umetengenezwa mwaka huu 2019, utakuwepo duniani kwa muda gani. 

Mimi, wewe na atakayezalizwa miaka 100 ijayo ataukuta na ataucha.Basi bora ungekuwa hauna madhara.Ukweli madhara ni makubwa makubwa sana. Kwanza nikumbushe tu, kesho ni marufuku kuzalisha, kutumia, kuuza au kununua mfuko wa plastiki.Ukiona unaupenda sana basi mwisho wako iwe leo.Ndio leo ndio mwisho. 

Serikali kupitia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa imetoa katazo la kisheria kwamba kunzia Juni 1,2019 mifuko ya plastiki ni marufuku kuonekana mtaaani, majumbani, viwandani na maeneo yote ya shughuli za kiuchumi.Wafanyabiashara wa Kariakoo jijini Dar es Salam mmeishi na mfuko wa Rambo na ule uliopewa jina la Kariakoo kwa muda mrefu. 

Iwe mwisho ...sio nakuja kununua bidhaa unanipa mfuko wa plastiki sitakuelewa.Na nitakuwa mnoko kweli, nikiuona tu nakuchongea kwa wenye mamlaka. 

Watanzania wote tuunge mkono jitihada hizi za Serikali za kukomesha mifuko ya plastiki.Tena nikung'ate sikio Tanzania sio wakwanza kwani nchi zaidi ya 127 duniani zimepiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki.Yaani tunakoelekea tunakwenda pazuri sana.Natamani kutumia ule msemo wa SISI TANZANIA MPYA...TUKO VIZURI ila naogopa maana unawenyewe. Tukatae kutumia mifuko ya plastiki. 

Wanaokubaliana nami tuwasiliane:0713833822 

Vyama na Mashirikisho ya Michezo Vyaelekezwa Kusimamia Utaratibu wa Upimaji Afya za Wanamichezo

$
0
0
Na Shamimu Nyaki -WHUSM
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza amevielekeza Vyama na Mashirikisho ya Michezo nchini kuwa na utaratibu wa kutoa elimu ya afya  na kinga  kwa wanamichezo  ili kulinda afya za wanamichezo hao kabla, wakati na baada ya mIchezo.

 Shonza ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma alipokua akijibu swali la msingi la Mhe. Haji Khamis Mbunge wa Nugwi aliyetaka kufahamu Serikali kupitia Vyama vya Michezo imeweka utaratibu gani wa kuhakikisha upimaji wa afya za wanamichezo linalopewa kipaumbele.
Naibu Waziri ameeleza kuwa Kitengo cha Kinga na Tiba kilichopo katika Wizara yake kwa kushirikiana na Chama cha madaktari wa Michezo nchini (TASMA) kinafanya kazi kubwa ya kutoa elimu pamoja na huduma ya afya kwa wanamichezo.

"Kitengo cha Kinga na Tiba cha Wizara jukumu lake ni kutoa elimu ya afya kwa wanamichezo pamoja na kutoa huduma ya upimaji wa afya kwa wanamichezo kila wanaposhiriki michezo au mashindano mbalimbali, hivyo vyama vya michezo na mashirikisho vinapaswa kuzingatia maelekezo hayo," alisema Mhe. Shonza.

Aidha Naibu Waziri huyo amongeza kuwa Sera ya Maendeleo ya Michezo ya mwaka 1995 sehemu ya 10.1 imeelekeza kuwa ni lazima mchezaji achunguzwe afya yake na kuwekewa kumbukumbu zote za kiafya kwa kipindi chote anapokuwa kambini na ahudumiwe na kuwekewa kumbukumbu zote za kiafya kwa kipindi chote anapokuwa kambini na ahudumiwe na Daktari mwenye taaluma ya tiba ya wanamichezo.

Vilevile  Shonza amesema kuwa Wizara iko tayari kutoa ushirikiano katika jitihada za kutoa ushauri wa kitaalamu ili kuimarisha afya za wanamichezo muda wote wanapokuwa uwanjani katika mazoezi au mashindano mbalimbali.
Hata hivyo Naibu Waziri Shonza alipojibu swali la nyongeza la Mhe.Sophia Mwakagenda aliyeuliza ni lini mabondia watapatiwa Bima ya Afya alieleza kuwa Shirikisho la ngumi hapa nchini tayari limeelekezwa kuwa na utaratibu wa kuwatafutia Bima mabondia hao.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza akijibu swali wakati wa kikao cha 40 cha Bunge leo jijini Dodoma.

MSAADA WA WADAU

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Kamishna Msaidizi wa Polisi,Juma Bwire (kushoto) akipokea msaada wa Samani za Makabati 3, viti 15 na Meza 3 kutoka kwa Taasisi ya SOS Children Village Tanzania tawi la Iringa vya thamani ya Tsh 2,700,000/= ambavyo vitatumika kwenye Kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto ngazi ya Kata. Picha na Datus Mahendeka wa Jeshi la Polisi. 

MWILI WA TSHIEKEDI WAWASILI KONGO BAADA YA MIAKA MIWILI TANGU KIFO CHAKE

$
0
0

Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
MWILI wa aliyekuwa Waziri mkuu na kiongozi mkubwa wa upinzani nchini Kongo Etienne Tshisekedi umewasili nchini humo ukitokea Ubelgiji ikiwa imepita miaka miwili tangu kufariki kwake.

Kuwasili kwa mwili wake umezua hisia kubwa wakati ukiwasili baada ya kusubiriwa kwa miaka miwili kutokana na zuio la kiongozi huyo kurejea nchini.


 Maelfu ya watu walijitokeza katika uwanja wa ndege mjini Kinshasa wakiimba wakati jeneza lililobeba mwili wa kiongozi huyo likishushwa huku likiwa limefunikwa bendera ya nchi hiyo.


Mazishi ya kiongozi hayo yatafanyikwa kwa heshima kubwa ikiwa kijana wake ndiye Rais wa sasa wa nchi hiyo.  

WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KATIKA SHEREHE ZA KUMWAPISHA RAIS WA MALAWI PROFESA ARTHUR MUTHARIKA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na , Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Malawi, Ben Botolo baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Chileka uliopo Blantyre Malawi kumwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika sherehe za kumwapisha Rais wa Malawi, Profesa  Arthur Peter Mutharika, Mei 31, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Malawi,  Bw. Ben Botolo wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Chileka uliopo Blantyre nchini Malawi kuwakilisha, Rais Dkt John Pombe Magufuli katika sherehe za kumwapisha Rais wa Malawi, Profesa, Arthur Peter Mutharika, Mei 31, 2019. 
  Waziri Mkuu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na , Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Malawi, Ben Botolo baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Chileka uliopo Blantyre Malawi kumwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika sherehe za kumwapisha Rais wa Malawi, Profesa  Arthur Peter Mutharika, Mei 31, 2019. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Rais wa Malawi, Profesa Arthur Peter Mutharika wakati Rais huyo alipohutubia baada ya  alipoapishwa kwenye Uwanja wa Kamuzu mjini Blantyre, Mei 31, 2019. Mheshimiwa Majaliwa alimwakilisha Rais Dkt John Pombe Magufuli katika sherehe za kumwapisha Rais huyo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa zamani wa Malawi, Bakili Muluzi katika sherehe za kumwapisha Rais wa Malawi Profesa Arthur Peter Mutharika zilizofanyika kwenye uwanja wa Kamuzu mjini Blantyre, Mei 31, 2019.

ASLAY UMRI MDOGO SIFA KIBAO

$
0
0
Na Moshy Kiyungi
Sifa kubwa aliyonayo Aslay ni uwezo wa kutunga, kuimba na kurekodi nyingi kwa kipindi kifupi. Ni msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka nchini Tanzania maarufu kama ‘Dogo Aslay’, ambaye tungo za nyimbo zale zimekuwa zikiwakuna wapenzi wa muziki wa huo, ndani na nje ya nchi.

Nyimbo za kijana huyu zimejikita zaidi katika mapenzi, ambazo kundi kubwa la wasikilizaji hupendelea sana kuzisikiliza. Majina yake kamili anaitwa Isihaka Nassoro, alizaliwa Mei 06, 1995, akapata elimu ya msingi katika shule ya Yussuf Makamba kati ya mwaka 2003 na 2009, kabla ya kuingia sekondari ya Tandika mwaka 2010 alikosoma hadi kidato cha nne.

Pindi umuonapo Dogo Aslay, ukalinganisha na mashairi anayotunga na kuimba nyimbo, utabaini kwamba haziendani na umri wake, lakini kupitia kipaji chake, anafanya vitu vikubwa kama hivyo. Alianza kufahamika kuanzia mwaka 2011 baada ya kuachia ngoma yake ya Nakusemea, aliyoitoa akiwa chini ya msimamizi wake Mkubwa Fella. Baadae akatoa nyimbo kadhaa kabla ya kuundwa rasmi bendi ya vijana ya Yamoto.

Bendi hiyo ya Yamoto ilidumu tangu 2013 hadi 2017 ilipovunjika kwa sababu mbalimbali. Kuanzia 2017, Aslay akawa msanii wa kujitegemea bila bendi wala usimamizi wa Mkubwa Fella. Amebaki akiwa na meneja wake wa zamani Chambuso. Aslay ametoa nyimbo nyingi mfululizo hali ambayo imewachanganya baadhi ya watu hata wasanii wenzake.

Alielezea kwanini aliamua kufanya hivyo, sababu kubwa ni kwamba hana nyimbo nyingi alizofanya akiwa msanii wa kujitegemea, zaidi ya zile alizokuwa na bendi ya Yamoto. Ili asiimbe za Yamoto akiwa kwenye matamasha, kaamua kutoa nyimbo nyingi. Baadhi ya nyimbo ni pamoja na Angekuona, Usiitie Doa akimshirikisha mama Khadija Kopa, Muhudumu, Baby, Likizo, Pusha Natamba na Huna.

Awali ilitazamika kama Mkubwa Fella ndiye hasa mmiliki wa muziki wa kizazi kipya, lakini kupitia Aslay, Chambuso anasema si lazima yeye ndiye awe meneja bora wa muziki huo. Aslay alimemtaja kaka yake Idd kuwa ndiye aliyegundua kipaji chake na kumkutanisha na mdau wa muziki kutoka TMK, Said Fella ‘Mkubwa’, baada ya kumuona akipenda kuimbaimba kila alipokaa.

kufanya vizuri zaidi katika muziki wa dansi la kizazi kipya akiwa na kundi la Yamoto Band.

Yamoto Band.

Ndani ya kituo cha Mkubwa na Wanawe, Aslay alipokelewa na kunolewa kikamilifu na baadhi ya wakali aliowakuta, wakiwamo Yusuph Chambusso na Fella mwenyewe.

Mwaka 2011 akishiriki onesho la nchi za Majahazi maarufu kama (ZIFF), aliweza kulitendea haki ipasavyo onedho hilo kwa kuimba kibao ‘Zuwena’ ambacho ni cha marehemu Marijani Rajabu ‘Jabali la Muziki’.

Mwaka huohuo, 2011 akachomoka na ngoma yake ya kwanza, iliyotokea kutikisa vilivyo na kuteka nafsi za wengi, hususan watoto na wanawake, inayokwenda kwa jina la ‘Nakusemea’. Mwaka uliofuata, 2012 Aslay alirekodi kibao ‘Umbea’ alichomshirikisha Chegge Chigunda kabla ya kuachia kete nyingine tena iliyojulikana ‘Bado Mdogo’.

Baada ya kushuka na kupanda huko, ndipo mwishoni mwa mwaka 2013, lilipoundwa kundi la Yamoto Band kwa kushirikisha pia vijana wengine watatu ambao ni Beka, Maromboso na Enock Bella. “Changamoto kubwa tunayoipata ndani ya Yamoto Band kupendwa na kuchukiwa, kwasababu tulitokea kukubalika ghafla basi wapo waliotupenda na wengine kutuonea kijicho,” alisema Aslay katika mahojiano maalumu.

Malengo ya baadae ya Dogo Aslay ambaye hakutegemea kama atatoka kimuziki, ni kumiliki kituo chake mwenyewe cha kuibua na kukuza vipaji vya wasanii, kama ilivyo kwa bosi wake, Fella. Aidha alieleza siri ya kuibuka kuwa mwimbaji, Aslay anayevutiwa na Banana Zorro katika muziki, alisema kwamba alipitia madrasa ya Aswabirina, Temeke, jijini Dar es Salaam.

Huko alikufundishwa jinsi ya kughani nyimbo za Kaswida, na kumfanya ajiamini mbele ya kadamnasi pasipo hofu yeyote. Aslay alitamka kuwa kukosa ushirikiano kwa baadhi ya wasanii wa muziki na hali ya kuibuka kwa bifu, ni kati ya mambo yanayo mkera nyota huyo mpya asiyependa majivuno.

Safu hii inakutakia kila la heri ili uweze kufikia malengo uliyojipangia ili mradi ‘usilewe sifa’ zitakuponza.

Mwandishi wa makala hii anaptikana kwa namba: 0784331200, 0767331200, 0736331200 na 0713331200.

CHUO KIKUU HARVARD WAMTUNUKU SHAHADA YA UDAKTARI WA HESHIMA ANGELA MERKEL

$
0
0
KANLESA wa nchini Ujerumani Angela Merkel ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima ya Chuo Kikuu maarufu cha Harvard.

Rais wa Chuo cha Havard Larry Bacow ambaye ndiye aliyemtunukia Merkel tuzo hiyo amesema kuwa Kansela huyo wa Ujerumani ni mwanasiasa mwenye nguvu barani Ulaya.

Wakati wa sherehe za kutunukiwa kwa Shahada hiyo ya Udaktari, chuo hicho kimemsifu Merkel kwa matamshi yake "Tutaweza kulisimamia hili" wakati wa mgogoro wa wakimbizi ulioanza mwaka 2015 nchini Ujerumani wakati aliporuhusu idadi kubwa ya wakimbizi na kukabiliwa na ukosoaji mkubwa nchini mwake.

Akizungumza kwenye hotuba yake kwa wanafunzi, wakati wa mahafali ya 368 ya chuo hicho cha Havard, Merkel amewaonya wanafunzi dhidi ya kuchanganyikiwa na kuuchukulia uongo kuwa ukweli na ukweli kuwa ni uongo.

JIMMY REEVES ALITAMBA KWA MUZIKI WA COUNTRY

$
0
0
Na Moshy Kiyungi

Muziki wa Country hapa nchini si maarufu sana kama ilivyo mingine. Naandika makala haya huku nafsi ikinisuta mbele ya msomaji wai wa gazeti hili, huenda akawa haufahamu muziki huo. Kazi kubwa ya vyombo vya habari ni kupasha habari na kuburudisha. Kwa matinki hiyo, sina bundi kukujuza au kukumbusha kwa wewe uliyesahau enzi za ujana wako alivyokuwa akifuarahia burudani.

Katika makala ya leo hapana shaka mzee mwenye zaidi ya umri wa miaka 50, akisoma majina ya Jim Reeves, atakuwa umeguswa vilivyo. Jim Reeves alikuwa mwanamuziki toka nchini Marekani, aliyekuwa amejikita katika miondoko ya muziki wa ‘Country’ na muziki wa kawaida akiwa mtunzi halikadhalika uimbaji.

Katika maisha yake ya muziki, aliweza kuweka rekodi ya kuupandisha ‘chati’ muziki wake kati ya miaka ya 1950 hadi ya 1980. Nyimbo za Jim Reeves husikika sana katika baaadhi ya sherehe zinazowajumuisha wazee hususani katika mikoa ya Nyanda za Kaskazini, nyakati za sikukuu za Krismasi na mwaka mpya.

Reeves alipata kuwa maarufu na akajulikana kama mwanamuziki wa midundo ya ‘Nashville’ (ambayo ni mchanganyiko wa muziki wa zamani wa Country na ule wa kisasa). Wasifu wa nguli huyo unaonesha kuwa majina lake halisi alikuwa ikiitwa James Travis aka “Jim”.

Mwanamuziki huyu alizaliwa Agosti 20, 1923, katika kitongoji cha Galloways huko Texas, nchini Marekani. Reeves alikuwa akitoka katika jamii ya watu waliokuwa nje ya mji karibu na Carthage.

Aidha Jim alitambulika ‘Muungwana Jim’ Alifariki kwa ajali ya ndege Julai 31, 1964 akiwa na umri mdogo wa miaka 40 katika ajali ya ndege binafsi. Nyimbo zake ziliendelea kupanda chati kwa miaka kadhaa hata baada ya kifo chake. Jim Reeves alikuwa mwanachama wa muziki wa ‘Country’ na pia ule wa Texas Country Halls of Fame.

Alifanikiwa kupata nafasi ya kwenda kusoma msomo ya juu ‘Scholarship’ ambapo alijisajili kusomea masuala ya kuhutubia na maigizo. Baada ya miezi sita katika masomo hayo, aliachana nayo akaamua kwenda kufanya kazi katika Yadi ya kutengeneza Meli huko Houston, huko huko Marekani.

Licha ya kuwa na weledi katika muziki, Reeves pia alikuwa mwanariadha aliyewahi kuchezea ligi za Semi- Professional kabla hajaingia mkataba na St. Louis Cardinals, timu ya shamba. Mwaka 1944 alicheza kama right- handed Pitcher.

Aidha alicheza ligi ndogo kwa miaka mitatu kabla hajaumia na kupata maumivu katika misuli iliyohitimisha juhudi zake za kuendelea na michezo. Reeves alianzia kufanya kazi kama mtangazaji wa redio. Kila wimbo umalizikapo kuupiga redioni, yeye akawa anaimba wimbo huo.

Mwishoni mwa miaka ya 1940, aliingia mikataba na baadhi ya Makampuni madogo ya kurekodi, huko Texas, lakini hakupata mafanikio. Muziki wa Magharibi ulimfanya kuhamasika sana hususani alipokuwa akiwasikia wanamuziki kama Jimmie Rodgers na Moon Mullicann. Waimbaji wengine maarufu wakati huo aliokuwa akiwatamani ni akina Bing Crosby, Eddy Arnold na Frank Sinatra.

Mapenzi hayo makubwa katika muziki yalimpelekea kuwa mwanachama wa bendi ya Moon Mulican. Jim aliweza kucheza mitindo ya mwanzoni ya bendi ya Mullican, ambapo nyimbo zake kama ‘Each Beat of My Heart’ na ‘My Heart’s Like a Welcome Mat’ mnamo miaka ya 1940 mwishoni na mwanzoni 1950, zilitamba wakati huo.

Aliweza ‘kukopi’ akiimba nyimbo za mwanamuziki mkongwe walomtangulia katika tasnia hiyo kama ‘Mexican Joe’. Nyimbo ambazo zilishika namba moja mwaka 1953. Kutoka mwaka 1955 mpaka mwaka 1969 Reeves akiwa na nyimbo zake hizo, ziliendelea kushika ‘ukanda’ hata baada ya yeye kufariki.

Nyimbo zake za kwanza za ‘Country’ zilizompa mafanikio zilikuwa ni pamoja na ‘I Love You’ aliouimba akishirikiana na Ginny Wright, na ‘Mexican Joe’ ‘Bimbo’ Jim aliafanikiwa kufyatua albamu yake katika studio za Abbott Records, ikatoka Novemba, 1955 iliyojulikana ‘Jim Reeves Sings’.

Mapema mwaka 1955, Reeves aliingia mkataba wa miaka 10 na Kampuni ya RCA Victor chini ya Steve Sholes. Katika mkataba huo, alitoa rekodi za kwanza za Reeves akitumia Kampuni ya RCA na pia akasaini mkataba na mwanamuziki Elvis Presley, katika Kampuni hiyohiyo.

Alipokuwa akirekodi mwanzoni akiwa na Kampuni ya RCA, Reeves bado alikuwa anaimba kwa mtindo wa sauti ya juu ambapo ilionekana ndio kipimo cha nyimbo za ‘Country’ Wanamuziki wa Magharibi kwa wakati huo. Jim alisaidia sana kuanzisha mtindo mpya ya muziki wa ‘Country’ akitumia ‘violin’ na ‘mpangilio wa kupendeza wa background ikijulikana kama ‘Nashville’ sound.

Baadae alianza kupunguza sauti yake wakati akiimba na kutumia ‘Pitch’ ya chini akiimba huku midomo yake ikikaribia kugusa kipaza sauti, ingawaje waliokuwa wanamrekodi (RCA) walikuwa wanailalamikia hali hiyo. Mwaka 1957 kwa maelekezo ya ‘Produysa’ wake Chet Arkins, alitumia mtindo huo katika toleo la wimbo wa maonesho wa ‘Penzi lililopotea’ uliokusudiwa uimbwe na mwimbaji wa kike.

Katika kipindi chote miaka yote ya 1950 na hadi 1960 mwanzoni, Jim Reeves alifanikiwa kuachia nyimbo zake kali zizoshika ‘chati’ za ‘Anna Marie’ na ‘Blue Boy’ No. 2 za mwaka 1958. Nguli huyo alifyatua vibao vingine vya ‘Billy Bayo’ mwaka 1959 na ‘He will have to go’ wa mwaka 1960, ‘Adious Amigo’ (namba mbili, 1962), ‘Welcome to my World’ (namba mbili, 1964) na ‘I guess I’m crazy’ (namba moja kwa wiki saba, 1964).

Pia alikuwa na kikosi na idara ya nyimbo za dini katika jukwaa lake. Wimbo wake, ‘Danny Boy’ akijitambulisha kwamba wazazi wake wametokea Irish. Wimbo ‘But You Love Me Daddy’ ukirekodiwa wakati mmoja akiwepo ‘Steve’. Huyo alikuwa ni mtoto wa umri wa miaka minane. Mtoto huyo alikuwa ni wa mpiga gitaa la besi, Bob Moore.

Wimbo huo uliingia katika ishirini bora huko Ulaya baada ya miaka kumi. Rekodi za Reeves mara nyingi zilikuwa na utamanifu wa kipekee, kama ‘I Love you Because’ na ‘I won’t forget You’. Zote hizo zilikuwa katika chati huko Ulaya kwa wiki 39 mfululizo.

Alipata umaarufu kama muimbaji wa kiume mwenye sauti ya kupendeza na nzito kiasi na yenye madaha. Nyimbo kama ‘Adios Amigo’ ‘Welcome to My World’ na ‘Am I Losing You’ zinaonesha hilo. Reeves nyimbo zake za Chrismasi zikijirudia rudia na kupendwa sana hasa zikiwa ni pamoja na ‘Chrismasi’, ‘Blue Chrismas’ na ‘An Old Chrisimasi Card’.

Hali kadhalika alikuwa hodari kwa kuukweza na kuzipa umaarufu nyimbo nyingi za ‘Injili’ kama. Alizipa kipaumbele nyimbo hizo za ‘We Thank Thee’ ‘Take My Hand, Precious Lord’ ‘Across The Bridge’ ‘Where We’ll Never Grow Old’ na nyingine nyingi.

Reeves aliibua na mafanikio makubwa baada ya ‘kujaladia’ kuimba utunzi za Joe Allison, ukiwemo wa ‘He’ll have to Go’. Katika nyimbo za ‘Country’ ambazo ziligonga vichwa vya watu kuanzia February 08, 1960 na kuendelea kwenye chati kwa wiki 14 mfululizo.

Mwana historia wa muziki wa Country, Bill Malone alionesha kwamba ni katika namna nyingi Reeves aliendeleza utamu na ubora katika muziki wa ‘Country’ kimpangilio na ‘melodi’ safi na ujumbe unaogusa mioyo ya watu.

Kwa nyongeza, Malone alimsifia Reeves kwa staili yake ya kuimba ambayo anaishusha chini sauti yake, inakuwa kama ya kubembeleza na ndio maana watu wengi wanatamka kwamba Jim Reeves alikuwa mwimbaji mwenye sauti ya mguso.

July 31, 1964, Reeves na mshirika mwenzake wa kibiashara, Meneja Dean Manuel waliondoka Batesville, Arkansas kupitia Nashville wakitumia ndege ya injini moja akiwa Reeves anaendesha. Wawili hao walikuwa wamepata ‘dili’ ya kununua shamba huko Deadwood Texas, Kaskazini mwa Galloway ambayo ni sehemu aliyozaliwa Reeves.

Wakati wanapaa juu kwa ndege akiwa na Brentwood, Tennessee, walikutana na dhoruba ya upepo mkali na mvua kubwa. Katika uchunguzi ilionekana ndege hiyo ndogo ilinaswa katika dhoruba na Reeves alipata mstuko ikaanguka na wao wakafariki.

Mjane wa marehemu, Mary Reeves alianzusha uvumi kwamba Reeves alikuwa akiendesha juu chini na aliongeza spidi ili kukwepa dhoruba. Hata hivyo kulingana na Larry Jordan, maelezo ya mjane wake kwamba Reeves alikuwa anaendesha chini juu haikuwa sahihi.

Kutokana na watu walioiona ajali hiyo jinsi ndege ilivyoanguka na maelezo yaliyomo kwenye tape iliyorekodi mwenendo wa ndege, na pia maelezo ya ripoti ya ajali, kwamba Reeves alikata kushoto katika jitihada zake za kuipata Franklin road, ili afike uwanja wa ndege aweze kutua.

Katika jitihada yake hiyo akazidi kuelekea kule kwenye mvua kubwa. Katika kuhangaika ili akakipate kiwanja ili kutua, spidi ya ndege ikawa ipo chini hivyo akaikwaza ndege.

Reeves alitegemea zaidi hisia zake katika kumuongoza na hakutumia maarifa aliyofundishwa chuoni kuikabili hali kama hiyo. Baada ya masaa 42 mabaki ya ndege yalionekana ikiwa mbele, yaani usoni pamoja na injini vimejikita ardhini. Reeves na mwenzake walikutwa tayari wamekwisha fariki.

Jim Reeves alizikwa katika kipande cha ardhi maalum ubavuni mwa ‘Highway 79’ Texas. Licha ya kufariki Jim Reeves bado umaarufu wake haukupotea, kwa hakika mauzo ya kazi zake yameongezeka baada ya kufariki.

Tangu kipindi cha kifo cha Jim Reeves kulipotokea, Mary alipatwa na matatizo ya kuugua kabla hayajamzidia. Mjane huyo Mary Reeves alifariki akiwa na umri wa miaka 70, Novemba 11, 1999. Iliripotiwa kuwa alikufa akiwa peke yake katika nyumba ya kuuguza wagonjwa.

Kabla ya kifo chake Mary Reeves Davis alishindwa kusimamia mali za Jim kutokana na ugonjwa, zikauzwa kwa ‘United Show of America’ mwaka 1997 kwa thamani ya Dola za Kimarekani milioni 7.3 Jim Reeves aliwekwa kwenye kundi la mwimbaji nyota wa kiume ambaye ametokeza katika midundo ya ‘Nashville Sound’.

Sauti yake laini ya kidume yenye madaha imeendelea kusikika hadi wakati leo. Mungu ailaza roho yake pahala pema peponi, Amina.

Mwandishi wa makala haya anapatikana kwa namba 0784331200, 0713331200, 0736331200 na 0767331200

NCHI ZA KIARABU WATOA TAMKO LA KUISHUTUMU IRAN,WAITAKA KUACHA KUINGILIA UHUSIANO WA NCHI NYINGINE

$
0
0
VIONGOZI wa nchi za Kiarabu wameishutumu Iran na kuitaka kuacha kuingilia mahusiano ya nchi nyingine.

Kwa mujibu wa Mtandao wa DW umesema kuwa shutuma hizo nchi hizo wamezitoa wakati wakihitimisha mikutano miwili ya kilele ya dharura nchini Saudi Arabia baada ya mashambulizi kwenye ukanda wa Ghuba. Iran ililaumiwa kwa mashambulizi hayo.

Taarifa ya kuhitimisha mikutano hiyo imechapishwa mapema leo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya nchi za kiarabu, Arab League, Ahmed Aboul Gheit baada ya mkutano wa jumuia hiyo.

Mikutano ya jumuia hiyo pamoja na Baraza la ushirikiano wa mataifa ya Kiarabu, GCC katika Mji wa Mecca iliitishwa baada ya mashambulizi kwenye meli nne za mafuta katika Pwani ya Umoja wa Falme za Kiarabu, UAE na yale ya ndege zisizo na rubani kwenye mabomba ya mafuta nchini Saudi Arabia yaliyofanywa na waasi wa Houthi wa Yemen wanaoungwa mkono na Iran.

Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje yapitishwa

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi (Mb.) akijibu maswali mbalimbali yaliyoulizwa na wabunge wakati wa kujadiliwa Bajeti ya Wizara yake May 30, 2019 
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango pamoja na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Willium Lukuvi (Mb.) wakimsikiliza Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani ) alipokuwa akijibu maswali Bungeni. 
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Kangi Lugola (Mb.) naye akichangia hoja kwenye Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Willium Lukuvi (Mb.) naye akichangia hoja kwenye Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Baadhi ya Wabunge wakifuatilia kwa hoja zilizokuwa zikichangiwa na wabunge mbalimbali.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damasi Ndumbaro (Mb.) akijibu maswali mbalimbali Bungeni wakati wa kupitisha Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro akifafanua jambo wakati wa uwasilishaji wa bajeti ya wizara hiyo. Aliyekaa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi na nyuma kabisa ni sehemu ya baadhi ya menejimenti ya Wizara hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro wakipongezwa na Wabunge Mbalimbali mara baada ya kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni mjini Dodoma. May 30, 2019. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Damas Ndumbaro (Mb.) akipongezwa na Mhe. Joseph Mbilinyi Mbunge wa Mbeya Mjini. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro, Katibu Mkuu Dkt. Faraji Mnyepe, Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhan Mwinyi wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

KOREA KASKAZINI YADAIWA KUMUUA OFISA WAKE BAADA YA KUSHINDWA MKUTANO WA HANOI

$
0
0
Na Ripota,Kimataifa 

VYOMBO vya habari vya nchini Korea Kusini vimeripoti kuwa Korea Kaskazini inadaiwa kumuua mjumbe wake maalumu kwa ajili ya Marekani Kim Hyok Chol baada ya kushindwa kwa mkutano wa pili wa kilele kati ya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un na rais Donald Trump. 

Kwa mujibu wa Gazeti la Chosun Ilbo limeandika Chol aliyeuandaa mkutano huo wa Hanoi na kumsindikiza Kim kwenye treni yake binafsi ameuawa kwa kupigwa risasi kwa kile kinachotajwa kumsaliti kiongozi huyo wa juu baada ya kufanikiwa kuishawishi Marekani wakati wa majadiliano ya kabla ya mkutano huo wa kilele. 

Gazeti hilo lililonukuu chanzo ambacho hakikutambulishwa limesema Chol, aliuawa Machi, katika uwanja wa ndege wa Mirim pamoja na maafisa wanne waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje baada ya uchunguzi. 

Mkalimani wa Kim kwenye Umoja wa Mataifa naye ametiwa kizuizini baada ya kufanya makosa kwenye mkutano huo wa kilele. 

CHANZO-DW

WAKIMBIZI, WAHAMIAJI 150 WAONDOLEWA NCHINI LIBYA

$
0
0
Na Ripota,Kimataifa 

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi(UNHCR) limewasafirisha kwa ndege wakimbizi na wahamiaji wapato 150 kutoka Mji Mkuu wa Libya Tripoli, kuelekea katika Mji 

Mkuu wa Rome nchini Italia. 

Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji (BBC) ni kwamba waliochukuliwa ni raia kutoka mataifa ya Eritrea, Ethiopia, Sudan na na wengi wanahitaji matibabu na wanakabiliwa na utapiamlo. 

Pia imeelezwa kuwa kuna raia wa nchi hizo ambao ndoto zao ni kwenda nchi za Ulaya lakini huishia nchini Libya ambako hushikiliwa kwenye vituo vya mahabusu katika hali mbaya.Inaelezwa kuwa takribani watu 600 wamepoteza maisha yao katika makabiliano ya hivi karibuni nchini Libya kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO).

Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images