Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live

POLISI ARUSHA YABAINI MBINU MPYA YA KUSAFIRISHA MIRUNGI KWENYE MADUMU YA MAJI, YANASA WAWILI

$
0
0
Na Woinde Shizza Michuzi TV, Arusha

JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha limefanikiwa kukamata madumu nane yakiwa yamesheheni dawa ya kulevya aina ya mirungi ambayo ni mbinu mpya inatumiwa na baadhi ya wananchi wanaojihusisha na biashara hiyo kama sehemu ya kulihadaa jeshi hilo.

Akizungumza leo ,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Jonathan Shana amesema kuwa madumu hayo yamekamatwa leo saa nne asubuhi katika eneo la Sakina na kuongeza mirungi hiyo ina uzito wa kilo 140 na watuhumiwa walikuwa wanaitoa Namanga kuleta Arusha Mjini.

Kamanda Shana amewataja washtakiwa hao ni Philipo Mungasi Lairumbe na Mjomba Ngaruma Nairishoo wakiwa na pikipiki aina ya King lion yenye namba MC 404 CEE na nyingine aina ya MC 772 DVT aina ya King lion.

"Tulipata taarifa kuhusu hii staili mpya ya kusafirisha mirungi na ndipo Polisi wetu walipoweka mtego na kufanikiwa kuwakamata katika eneo la Sakina wakati wakija Arusha Mjini,"amesema Kamanda Shana.

Ameongeza kuwa kumekuwepo na mbinu mpya ya kusafirisha mirungi ambapo inawekwa kwenye madumu ya maji na kubeba kama maziwa na kwamba mbinu hiyo imekuwa ikitumika kwa muda mrefu sasa.

Amesema kutokana na tukio hilo Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi zaidi ili kuwabaini wale wote wanaoshirikiana nao na hata kama watakimbia watawakamata na uchunguzi utakapokamilika walioshiriki watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Wakizungumzia kuhusu tukio hilo la kunaswa kwa mirungi hiyo, watuhumiwa hao wamesema wamekuwa wakiitumia mbinu hiyo na hii ni mara ya pili kwao na wanapofikisha mzigo kwa mhusika wanalipwa Sh.80,000.

Wakati huo huo ,Jeshi la Polisi limeendesha msako wa nyumba kwa nyumba katika kuwasaka wahalifu na kufanikiwa kukamata wahalifu 35 wakiwa na vitu mbalimbali ikiwemo TV, radio, simu, sabufa na Laptop.

Amesema miongoni mwa mshtakiwa aliyekamatwa katika msako huo ni Jumanne Mjusi anayedaiwa kufanya uhalifu Mei 16 mwaka huu katika mtaa wa Olasiva uliopo Kata ya Olorieni katika nyumba ya Msafiri Msuya (47)ambaye aliibiwa kiasi cha Sh.milioni sita pamoja na bastola moja aina ya Browning yenye namba B 043601 ikiwa na risasi tisa. 

Kamanda Shana amesema kuwa, Mjusi alikamatwa katika eneo la Ngarenaro baada ya siku mbili ya kufanyika kwa tukio hilo la wizi ambapo alikutwa akiwa na bastola hiyo pamoja na risasi zake isipokuwa fedha hizo.

Amewataka wananchi kutoa taarifa za uhalifu mbalimbali zinazofanyika katika maeneo yao ili kulisaidia jeshi hilo.Pia ametoa onyo kali kwa watu wote wanaoghushi vitambulisho vya uraia na kueleza iwapo mtu yeyote atakamatwa kwa kosa la kughushi hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.
 Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Jonathan Shana akionesha jinsi wasafirisha mirungi wanavyotumia mbinu mpya
 Kamanda akionyesha moja ya muhalifu anaetuhumiwa kusafirisha mirungi  
Mwananchi Abasi Mkindi akizungumza na waandishi wa habari ambapo aliliomba jeshi la polisi kuongeza ulinzi katika mipaka ili madawa ya kulevywa yapitishwe


LSF kutanua wigo wa huduma za msaada wa kisheria Tanzania

$
0
0
Afisa Mtendaji Mkuu mpya wa Legal Services Facility(LSF) Bi. Lulu Ng’wanakilala amesisitiza kuwa vipaombele vya shirika hilo ni kuhakikisha upatikanaji madhubuti wa huduma za msaada wa kisheria pamoja zinatolewa kwa wakati.

Lengo hili litawezekana kwa kutanua wigo wa kutoa huduma hizi muhimu ambazo zimewawezesha mpaka sasa mamilioni ya watanzani kupata haki zao tangu shirika hilo kuanzishwa mwaka 2011

Ng’wanakilala, amesema haya jana jijini Dar es saala wakati wa halfa ya Iftar iliyoandaliwa na LSF na kuwashirikisha wadau kutoka katika sekta mbalimbali , Serikali, wadau wa maendeleo , mashirika binafsi na mashirika yasiyo yakiserikali. Huku lengo hasa likiwa ni kumkaribisha na kumuwaga Afisa Mtendaji Mkuu Kees Groenendijk anayeondoka baada ya kuongoza shirika hilo tangu kuanzishwa kwake

“LSF imekuwa na mafanikio mengi ikiwemo mchango wake mkubwa kwa kushirikiana na wadau na Serikali katika kuwepo kwa sheria ya msaada wa kisheria yaani Legal Aid Act, 2017 ambayo inamufaa makubwa kwa mustakabali wa msaada wa kisheria kwa ujumla na si kwa LSF pekee.Agenda yetu kubwa sasa ni kuendelea kushirikiana na Wizara ya katiba na sheria katika utekelezaji wa sheria hiyo ili kuchochea uhakika, ufanisi na ubora wa huduma za msaada wa kisheria nchini”.Alisema

Akiongea kuhusu kazi kubwa iliyofanywa katika kila wilaya Tanzania na Zanzibar mpaka sasa, aliongeza” mkakati wetu mkubwa sasa ni kuangalia ni jinsi gani LSF itakuendelea kuwepo na kujenga zaidi kile kilichofanyika mpaka sasa. Lengo letu kubwa ni kuhakiksha sekta ya msadaa wa sheria

kupitia mtandao wetu mpana wa watoa huduma wa msaada wa kisheria “paralegal” unafikia kila jamii huku tukitilia mkazo uwezeshwaji wa wanawake , uwezeshwaji uchumi na kuondoa umaskini .

LSF tutafanya kazi kwa karibu na sekta mbalimbali hata zile ambazo hatukuwahi kushirikiana nazo kama vile sekta ya madini, kilimo, utalii na sekta binafsi kwa kuhakikisha paralegal wanatatua changamoto za kisheria zinazowakabili kwa namna moja au nyingine”.

LSF mpaka sasa ina jumla ya paralegal 4000 wanaotoa elimu juu ya maswala ya sheria na kutoa msaada wa kisheria kwa jamii nchi nzima. Mamia na maelfu ya wanawake, wanaume na Watoto wamefaidika na wanaendelea kufaidiaka na huduma hizi zinazosimamiwa na mashirika yanayotoa huduma za kisheria , paralegal na wadau washirika chini ya ufadhili wa DANIDA na DFID “ni matumaini yetu kwamba ushirikiano wetu kwa pamoja utawezesha LSF kutanua huduma zake na kuwafikia watu wengi zaidi na kuboresha Maisha yao kijamii na kiuchumi kwani huduma hizi za msaada wa kisheria ni bure”

Ms. Ng’wanakilala alianza kazi rasmi mwezi huu na ataongoza shirika lilodumu kwa miaka 8 kwa kuboresha mahusiano na serikali katika ngazi zote na kuwawezesha wananchi kupata haki zao kwa manufaa ya maendeleo yao na ya nchi kwa ujumla.

 Mkurugenzi Mtendaji Mpya wa Shirika la Legal Services Facility (LSF), Lulu Ng’wanakilala, akiongea na wadau wa sekta ya huduma wa msaada wa kisheria jijini Dar es Salaam jana wakati wa hafla/futari maalum iliyoandaliwa kumkaribisha rasmi katika nafasi ya uongozi wa juu wa shirika hilo. 

 Wadau wa sekta ya huduma ya Msaada wa kisheria wakifatilia mazungumzo wakati wa hafla/futari maalum iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana ya kumkaribisha rasmi Mkurugenzi Mtendaji Mpya wa Shirika la Legal Services Facility (LSF), Bi. Lulu Ng’wanakilala katika shirika hilo. 
 Picha ya pamoja

NAIBU SPIKA AKUTANA NA MKURUGENZI UNDP

$
0
0
Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akizungumza na Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Ndugu Verity Nyagah alipomtembelea ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. 

NAIBU WAZIRI KANYASU AAGIZA TAWA IUNDE TUME KUCHUNGUZA KIFUTA MACHOZI WILAYANI BUNDA

$
0
0

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sarakwa wilayani Bunda mkoani Mara kuhusu umuhimu wa kutoa taarifa mapema kwenye ofisi za kijiji wakati wanyamapori wakali na waharibifu wanapoharibu mazao. 
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Sarakwa wakimsikiliza Naibu Waziri waMaliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu wakati wa mkutanao wa hadhara uliofanyika katika eneo la Shule ya ,msingi ya Sarakwa mara baada ya kusikiliza malalamiko yao kuhusu malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akisalimiana na baadhi ya watumishi wa wilaya ya Bunda mkoani Mara mara baada ya kuwasili katika ofisi ya Mkuu wa wilaya kwa ajili ya kikazi ya siku moja. 
Mbunge wa jimbo la Bunda vijijini, Boniface Getere akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sarakwa kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu kuzungumzia kuhusu umuhimu wa kutoa taarifa mapema kwenye ofisi za kijiji wakati wanyamapori wakali na waharibifu wanapoharibu mazao yao. 
Mwenyekiti wa kijiji cha Sarakwa, Samson Kapeta akizungumza na wananchi wake kabla ya kumkaribisha na Mbunge wa jimbo la Bunda vijijini, Boniface Getere kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho. 

…………………… 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu ameiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) iunde timu ya kuchunguza uhalali wa malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi kilichotolewa kwa wananchi walioathiriwa na wanyamapori wakali na waharibifu wa mazao katika maeneo mbalimbali nchini. 

Mhe. Kanyasu ametoa agizo hilo mara baada ya kupokea malalamiko na madai kutoka kwa baadhi ya wananchi wa vijiji 4 vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, wilayani Bunda mkoani Mara ambao mazao yao yaliliwa na kuharibiwa na wanyamapori wakali wamekuwa hawalipwi huku wasiostahili ndo wamekuwa wanalipwa . 

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Sarakwa, Mariwanda ,Unyali na Kihomboi vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Bunda mkoani Mara, Mhe. Kanyasu amesema kuwa mara baada ya uchunguzi kukamilika wale watakaobainika kupokea fidia hiyo wale wasiostahili watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kuzirudisha fedha hizo.

‘’Nataka niwambie, wale waliopokea kifuta jasho na kifuta machozi kutoka serikalini wakati hawastahili lazima hizo fedha wazitapike” Amesisitiza Mhe. Kanyasu 

Aidha, Mhe. Kanyasu amesema licha ya fidia hiyo kuendelea kulalamikiwa kuwa kidogo ikilinganishwa na hali halisi ya maisha ya sasa, wananchi ambao mazao yao yameharibiwa wanatakiwa kulipwa fidia kwa mujibu wa sheria iliyopo na sio vinginevyo. 

Katika hatua nyingine Mhe. Kanyasu amewataka wananchi wanaoharibiwa mazao yao na wanyamapori wakali na waharibifu wakiwemo tembo watoe taarifa ndani ya muda wa siku tatu katika ofisi za vijiji katika maeneo yao ili hatua za malipo ziweze kufanyika kwa muda. 


Pia, Kanyasu amewaeleza wananchi hao kuwa Serikali imeanza kupitia upya utaratibu wa kifuta jasho na kifuta machozi ili kiweze kuendana na gharama za maisha ya sasa. 

Kwa upande wake Bw. Abel Hadawi, mmoja wa wananchi ambaye mazao yake zaidi ya ekari 20 yaliharibiwa mwaka jana, amemweleza Naibu Waziri huyo kuwa amaekuwa akijaza fomu kwa ajili ya kulipwa fidia lakini kila malipo yanapokuja jina lake limekuwa halimo. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Kikosi Dhidi ya Ujangili (KDU) kanda ya Ziwa, Emmanuel Nkya amewaeleza wananchi hao kuwa wanachotakiwa kufanya ni kujaza fomu nne ili kuwe na nakala kuanzia ofisi ya kijiji hadi makao makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii. 

Naye Mbunge wa Bunda vijijini, Boniface Getere amemwomba Naibu Waziri Kanyasu kuyashughulikia malalamiko ya wananchi wote wanaostahili kulipwa kifuta jasho na kifuta machozi kwa kuwa wengi wao wameathiriwa na kubaki omba omba kufuatia mazao yao kuharibiwa.

MAWAKALA WA FORODHA ARUSHA WAMUOMBA WAZIRI MKUU KUINGILIA KATI MGOGORO ULIOPO KATI YAO NA WAKALA WA VIPIMO

$
0
0
Na Woinde Shizza Michuzi TV, Arusha

CHAMA cha Mawakala wa Forodha(TAFFA) tawi la Namanga mkoani Arusha wamemwomba Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa kuingilia kati mgogoro kati yao na Wakala wa Vipimo (WMA) unaowalazimisha kulipia tozo mpya inayotozwa kwa kila bidhaa badala ya kutumia utaratibu wa awali wa kulipia tozo kwa mzigo wote.

Aidha wamesema hawapo tayari kufanya kazi na wakala hao hadi hapo watakapo onyeshwa hiyo sheria mpya ambayo wanalazimishwa kuitekeleza bila kuwepo kwa makubaliano yoyote kitendo ambacho kinawaumiza wao. 

Wametoa ombi hilo leo kwenye kikao chao kilichoongozwa na Mwenyekiti wa TFFA Ismail Lukas ambacho kilichofanyika Namanga, wilayani Longido ambapo wamesema walikuwa wakitumia sheria ya zamani ya mwaka 2016 ambayo walikuwa wakilipia asilimia 0.2 ya thamani ya mzigo ambapo kiwango cha chini cha malipo ilikuwa shs 100,000 kwa mzigo.

Wamesema wanachopinga ni WMA kuamua kuwatoza malipo ya shilingi laki moja kwa kila aina ya bidhaa (item ) badala ya mzigo mzima Kama sheria inavyoelekeza .

"Tunamwomba Waziri Mkuu aje Namanga kuja kuzungumza na sisi kuhusu huu mgogoro kwani tukiendelea na utaratibu huu tutakosa wafanyabiashara kwani hakuna mtu aliye tayari kupata hasara kwani jinsi tunavyopandishiwa gharama za tozo ndivyo hivyo hivyo bei za bidhaa zitakavyopanda,"amesema Ismail.

Kwa upande wake Meneja wa Tawi wa kampuni ya EDPAC Wilson Mkanza amesema kwa hivi sasa hawapo tayari tena kufanya shughuli yoyote bila kupata muongozo wa sheria mpya inayowalazimu wao kutumia utaratibu mpya wa kulipa tozo ya laki moja kwa kila bidhaa badala ya mzigo Kama utaratibu wa awali. 

Amesema kuwa walipokea barua mnamo may 15 mwaka huu ya ufafanuzi wa kanuni ya ada za ukaguzi wa bidhaa zilizofungashwa zinazoingia nchini kutoka nje ya nchi kutoka kwa kaimu meneja wa wakala wa vipimo mkoa, Dismas Maturine inayohusu wao kulipia bidhaa moja moja badala ya kutozwa kwa mzigo mzima kama ilivyokuwa hapo awali bila kushirikishwa chochote kabla ya kupewa barua hiyo. 

Wakati huo huo Janeth Mero kutoka kampuni ya Beam Tanzania Ltd alisema kuwa, uwepo wa utaratibu huo wa kulipa kwa kwa mzigo mmoja mmoja unatengeneza mazingira ya rushwa, hivyo kuwataka kuendelea kwa ule utaratibu uliokuwepo wa awali ili waendelee kulipa bila migogoro yoyote.

Mkurugenzi wa Ufundi kutoka wakala wa vipimo makao makuu, Stella Kahwa alisema kuwa, amesikiliza malalamiko hayo na yamepokelewa na yanaendelea kufanyiwa kazi na kusema kuwa, utaratibu utakaoendelea kutumika ni ule uliokuwa ukitumika awali wa kulipia laki moja kwa mzigo.
 mawakala wakisikiliza mwenyekiti kwa makini
 mwenyekiti wa Chama cha mawakala wa forodha( TAFFA)Ismail Lukas akiongea na wanachama wenzake. 
Mkurugenzi wa ifundi Stella kahwa akiongea na waandishi ofisini kwake

WAZIRI MKUU AITAKA AKDN IKAMILISHE MJADALA NA NHIF

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongoza mazungumzo kati yake, na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wa pili kushoto) pamoja na Viongozi wa Taasisi ya Aga Khan, Ofisini kwa Waziri Mkuu, Bungeni jijini Dodoma, Mei 28, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (AKDN) ukamilishe majadiliano yao na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kuhusu matumizi ya kadi za NHIF kwenye hospitali zao ili Watanzania wengi zaidi waweze kunufaika.

Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Mei 28, 2019) alipokutana na viongozi kadhaa wa taasisi hiyo pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, ofisini kwake bungeni jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua mchango unaotolewa na taasisi ya AKDN katika kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya.“Nilijionea kazi kazi kubwa inayofanyika pale Hospitali ya Aga Khan Machi, mwaka huu, niliongea na wagonjwa na kupata maoni yao, lakini kikubwa tu mpunguze gharama na muimarishe huduma zenu,” amesema.

Amewapongeza viongozi hao kwa utoaji wao wa huduma kwenye sekta nyingine kama elimu, maji na kilimo. “Tunategemea mtaendelea kuimarisha huduma hizo ili ziwasaidie Watanzania wengi zaidi,” amesisitiza.

Viongozi hao walikutana na Waziri Mkuu ili kumuarifu juu ya mpango wa taasisi hiyo wa kuanzisha kituo maalum cha matibabu ya saratani nchini (Specialised Cancer Care Facility) ambao unatarajiwa kugharimu dola za marekani milioni 15. Kituo hicho kitaendeshwa kwa ubia baina ya hospitali za Ocean Road, Muhimbili, Bugando na Aga Khan.

Kwa upande wake, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Ummy Mwalimu alimweleza Waziri Mkuu kwamba hospitali za Ocean Road na Bugando zinatoa huduma za radiotherapy na chemotherapy, wakati hospitali ya KCMC inatoa huduma ya chemotherapy tu. “Hospitali ya Rufaa ya Mbeya bado huduma hizo zinaadaliwa ili ziweze kutolewa,” alisema.

Hata hivyo, Waziri Ummy alisema hivi sasa kwa nchi nzima, kuna vituo zaidi ya 120 ambavyo vinatoa huduma ya utambuzi wa saratani (cancer screening).

Mapema, akitoa maelezo kuhusu mpango wa kujenga kituo hicho, Mwakilishi Mkazi wa AKDN, Bw. Amin Kurji, alisema wameshawasiliana na hiospitali zote tajwa na sasa wanashirikiana na wataalamu wa wizara ya afya ili kukamilisha suala hilo.

“Tatizo la saratani hapa nchini ni kubwa kwa sasa. Lakini tunataka watu watambue kwamba ukiugua saratani haimaanishi kwamba utakufa mara moja (it’s not a death sentence). Inaweza kutibika endapo mgonjwa atawahi kupata matibabu,” alisema Bw. Kurji.

Alisema kwa sasa hivi hapa nchini hakuna kituo maalum cha matibabu ya saratani nchini lakini kitu cha pekee kuhusu kituo hicho ni uwepo wa huduma zinazotembea za upimaji na utoaji tiba hadi mikoani. “Huduma hizi zitakuwa zinatolewa kwenye mikoa yote kupitia njia ya mtandao, ilhali vituo vikuu vya Dar es Salaam na Mwanza vitakuwa vikitoa majibu kwa madaktari husika,” alisema.

Alisema lengo lao pia ni kutoa elimu juu ya kuzuia, upimaji wa mapema na upatikanaji wa tiba (prevention, early diagnosis and cure).


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
41193 – DODOMA. 
JUMANNE, MEI 28, 2019.

Katazo La Matumizi Ya Mifuko Ya Plastiki Lasimamisha Masomo Kwa Wanafunzi Mkoani Tabora

$
0
0
Na, Editha Edward-Tabora 

Wanafunzi wa Shule Mbalimbali Za sekondari zilizopo Katika Manispaa ya Tabora Mjini leo wamesitisha masomo ikiwa lengo kubwa ni kufanya Maandamano ya kuhamasisha katazo la matumizi ya Mifuko hiyo 

Hayo yamejili Mapema leo hii Katika Maandamano yaliyofanywa na Wananchi katika makundi Mbalimbali wakiwemo wajasiriamali na Wananchi wa kawaida ambao ndio watumiaji wakuu wa Mifuko hiyo

Rajabu Hamis, Magreth Yohana ni baadhi ya Wanafunzi waliojitokeza Katika Maandamano hayo ambapo wamesema wataendelea kuhamasisha wazazi wao na walezi wao ili kuhakikisha waunga mkono juhudi Za Serikali ya Awamu ya Tano

Matrida James ambae ni Mwlimu wa Shule Ya Wasichana (Tabora Girls) Amesema kuwa Wananchi wa Tabora wanalojukumu la kufahamu kuwa Mifuko ya Plastiki imepigwa Marufuku kwa Sababu inasababisha Uharibifu wa Mazingira

"Mifuko ya plastiki inasababisha Uharibifu wa Mazingira na Afya ya binadamu ambapo mifuko hii inapelekea kupata maradhi mbalimbali pia inachangia kwa vifo vya wanyama endapo watatafuna vipande vya mifuko ya Plastiki "Amesema Matrida

Kwa upande wa Wajasiriamali waliojitokeza katika maandamano hayo wametoa hisia zao kwa kuiomba Serikali kupitia Wizara husika kuhakikisha wanasimamia mfumuko wa bei katika uuzaji wa vifungashio mbadala vitakavyoletwa

Tamko la kusitisha matumizi ya mifuko ya plastiki lilitolewa na Wizara ya Mazingira na Muungano ambayo ipo chini ya Makamu wa Rais Ikiwa lengo kuu Kutunza mazingira ya nchi na Tayari Kuanzia June 1 Mwaka huu litaanza kufanya Kazi kwa Asilimia 100.
Wanafunzi wa Shule mbalimbali Za sekondari manispaa ya Tabora mjini wakionesha Mabango yanayohamasisha Uungwaji Mkono wa Katazo la Matumizi ya Mifuko ya Plastiki.

Taswa FC yawashukuru waandaaji wa Ndondo Cup

$
0
0


Dar es Salaam. Uongozi wa timu ya waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa FC) umewashukuru waandaaji wa mashindano ya Ndondo Cup pamoja na kushindwa kuingia katika hatua inayofuata.

Mwenyekiti wa Taswa FC, Majuto Omary alisema kuwa wamejifunza mengi katika mashindano hayo na kuahidi kushiriki tena msimu unaofuata baada ya kuwajengea wachezaji moyo wa kujiamini katika mashindano yam waka huu.

Majuto alisema kuwa lengo la Taswa FC lilikuwa kutoa changamoto kwa timu nyingine pamoja na ukweli kuwa wanafanya mazoezi mara moja tu kwa wiki tofauti na timu nyingine.

“Tumeonja ladha ya mashindano pamoja na kushika nafasi ya tatu katika kundi letu. Tumethubutu kushindana na kupanua wigo wa timu yetu na kuingia katika historia mpya, sasa tunarejea katika majukumu yetu ya kuyatangaza mashindano kupitia kalamu zetu,” alisema Majuto.

Alisema kuwa kitendo cha waandaaji waandaaji kuhakikisha kila mechi inakuwa na daktari ambaye hutoa huduma kwa majeruhi wa timu zote kimewafurahisha sana na kuwataka waandaaji wengine kuiga mfano huo.

“Tumecheza mechi zote bila kukosa. Hii ni historia kwetu, kwani kuna timu za madaraja ambazo zimeshindwa kumaliza mashindano na kufungwa mabao mengi zaidi yetu, kwetu sisi historia, kwa sasa tunaweza kuyazungumzia mashindano kwa undani zaidi kwani tunayajua vilivyo. Katika shughuli yoyote changamoto hazikosekani, Taswa FC inawaomba waandaaji kutumia changamoto kama njia ya kupata mafanikio,” alisema.

Alifafanua kuwa hata wao (Taswa FC) walipata changamoto nyingi, lakini kubwa kitendo cha makipa wao kuogopa mechi na kujiamulia kutofika uwanjani.

“Tumewachukulia hatua za kinidhamu pamoja na kuwasimamisha kwa muda usiojulikana. Si wazalendo kwa timu yetu. Wachezaji na viongozi wamepitisha adhabu hiyo mara baada ya mechi na Ukwamani na kufungwa mabao 2-0,” aliongeza Majuto.

TCRA yawafikia Wakazi wa Mafinga katika utoaji wa Elimu ya Usajili wa laini kwa kutumia alama za vidole

$
0
0
Wakazi wa Mafinga na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi katika kampeni  ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu Mitandaoni  na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa ajili  ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa kuweka alama za vidole kwa laini za simu.

 Mkuu wa TCRA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Mhandisi  wa TCRA Asajile John amesema ni fursa kwa wananchi wa Mafinga kupata huduma kutokana na kuwa na mnyororo wadau wa  mawasiliano. 

Amesema kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano. 
Asajile amesema kuwa wananchi wasio kuwa na Vitambulisho vya NIDA wahakikishe  wanapata katika usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole. 
"TCRA iko karibu na wananchi katika utoaji wa elimu za utumiaji wa bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma hiyo"amesema John.

 Mwananchi akihudumiwa uwekaji wa alama za vidole katika usajili laini za simu wakati wa kampeni  ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu Mitandaoni  na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa ajili  ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa kuweka alama za vidole kwa laini za simu.

Wananchi wakisoma vitabu vya muongozo vya TCRA mamna ya kutumia bidhaa za mawasiliano wakati wa kampeni  ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu Mitandaoni  na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa ajili  ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa kuweka alama za vidole kwa laini za simu.

 Wananchi wa Mafinga na Maeneo ya jirani wakiwa katika Mnada uliokwenda sambamba   na Mnada kwa Mnada karibu tukuhudumia wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) pamoja na wadau mbalimbali katika utoaji wa  elimu wa usajili laini za simu kwa kutumia alama za vidole.
Wadau mbalimbali wa Mnada kwa Mnada karibu tukuhudumie wakitoa huduma katika Mnada wa Mafinga wakitoa huduma za bidhaa za mawasiliano.

SHIRIKA LA OKOA MOYO WA MTOTO KUTOKA ISRAEL YAKUTANA NA UONGOZI WA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na wajumbe wa bodi wa shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart (SACH) la nchini Israel wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo ya siku saba inayofanyika katika taasisi hiyo. Jumla ya watoto 20 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa bila kufungua kifua kupitia tundu dogo kwa kuziba matundu yaliyopo kwenye moyo na kuzibua mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye moyo. 
: Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na wajumbe wa bodi wa shirika la Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart (SACH) la nchini Israel wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo ya siku saba inayofanyika katika taasisi hiyo. Jumla ya watoto 20 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa bila kufungua kifua kupitia tundu dogo kwa kuziba matundu yaliyopo kwenye moyo na kuzibua mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye moyo.
Mjumbe wa bodi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart (SACH) la nchini Israel Riva Grinshpan akizungumza na menejimenti ya taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wajumbe wa bodi hiyo wakati wa kambi maalum ya matibabu ya moyo ya siku saba inayofanyika katika taasisi hiyo. Jumla ya watoto 20 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa bila kufungua kifua kupitia tundu dogo kwa kuziba matundu yaliyopo kwenye moyo na kuzibua mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye moyo.

NAIBU SPIKA AICHANGIA YANGA

$
0
0
   Naibu Spika  Mheshimiwa Dkt Tulia Ackson akikabidhi fedha kiasi cha Shilingi milioni moja kwa Wabunge mashabiki wa Timu ya Soka ya Yanga iliyopokelewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mheshimiwa Anthony Mavunde, Ofisini kwake Bungeni mjini Dodoma. Fedha hizo ni kwa ajili ya kuichangia Timu ya Yanga.

 Naibu Spika  Mheshimiwa Dkt Tulia Ackson akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi fedha kiasi cha Shilingi milioni moja kwa Wabunge mashabiki wa Timu ya Soka ya Yanga kwa ajili ya kuichangia timu hiyo, Ofisini kwake Bungeni mjini Dodoma .

(PICHA NAOFISI YA BUNGE)

   


MBWANA SAMATTA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI, DKT. HASSAN ABAASI

$
0
0
SERIKALI imesema itaendelea kumsaidia kwa hali na mali Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, anayechezea Klabu ya Genk ya Nchini Ubelgiji Mbwana Samatta ili kuhakikisha kuwa anafungua milango ya uwekezaji na kuiweka juu ramani ya Soka la Tanzania katika anga la kimataifa.
Akizungumza leo Jumanne (Mei 28, 2019) Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam na Nahodha huyo waTaifa Stars, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi alisema Samatta ameonyesha njia iliyoshindwa kufikiwa na wachezaji wengi wa miaka ya nyuma waliojaribu kucheza Soka la kulipwa katika vilabu mbalimbali vya Nchi za Nje hususani Bara la Ulaya.
Dkt. Abbasi alisema Serikali ilimteua Sammatta kuwa Balozi wake wa Utalii kutokana na sifa kubwa zilizoletwa na mchezaji huyo nje ya mipaka ya Tanzania kwa kuwa Serikali ina Imani naye kubwa katika kufungua milango ya fursa za uwekezaji hususani katika miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano hapa nchini. 
“Mbwana Samatta ameonyesha njia ambayo ilikuwa ndoto iliyoshindwa kutimizwa na wachezaji wengi wa zamani, hatua hii aliyofikia ni kubwa na imetokana na sifa kubwa ya nidhamu na kipaji cha mchezo huu hili ni funzo kwa wachezaji wetu chipukizi” alisema Dkt. Abbasi.
Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alisema kwa sasa yapo mambo makubwa na mazuri hususani vivutio vya sekta ya utalii, hivyo kupitia nafasi yake ya Ubalozi Serikali itatoa msaada wowote unaohitajiwa na mchezaji huyo ili kuhakikisha kuwa vivutio vya Tanzania vinabainishwa na hivyo kutangaza mambo mazuri ya Tanzania.
Aidha Dkt. Abbasi alisema Ofisi yake imeandaa mikakati mbalimbali ya mawasiliano ya kitaifa katika kuisema nchi katika maeneo mbalimbali hivyo kumtaka mchezaji huyo kutumia majukwaa hayo kwa ajili ya kuona namna bora ya kutumia fursa hizo ili kuitangaza Tanzania nje ya mipaka yake.
Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alimtaka mchezaji huyo kuwasiliana naye iwapo kutakuwepo na changamoto yoyote anayoweza kuipata katika kutekeleza majukumu yake ya nafasi ya Ubalozi kwani kwa sasa Serikali ya Awamu ya Tano imefungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha kuwa Tanzania inapiga hatua katika kuwaletea maendeleo wananchi wake.
Kwa upande wake, Nahodha huyo wa Taifa Stars, Mbwana Samatta alisema akiwa nchini Ubelgiji tayari amefanya juhudi kubwa katika kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini, ambapo mwanzoni mwa mwezi ujao madaktari 5 wa timu hiyo wanatarajia kuja nchini kwa ajili ya kutembelea maeneo mbalimbali ya utalii nchini.
Samatta alisema raia wengi wa kigeni wana shauku ya kutembelea Tanzania kutokana kusikia na kuona uzuri wa vivutio mbalimbali vya utalii ikiwemo Wanyama, hivyo akiwa Balozi wa Utalii afanya kila liwezekanalo  kukaa karibu na viongozi na wachezaji wa klabu yake ya KRC Genk kuwaeleza uzuri wa Tanzania ili na wao waonesha nia ya kuitembelea Tanzania.
“Wachezaji wengi hususani wale wa kiafrika waliopo nje hususani Bara la Ulaya wanaipenda sana Tanzania, na hi inatokana na sifa tuliyonayo, na hivyo kwa kutumia nafasi yangu ya Ubalozi nitaendelea kushawishi waitembelee Tanzania” alisema Samatta.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Samatta Tours, Hamis Waziri aliishukuru Serikali kutokana na jitihada mbalimbali inazofanya kwa ajili ya kuhamasisha sekta ya utalii nchini na kusema taasisi hiyo itakuwa tayari kutangaza matukio mbalimbali kwa ajili ya kulitangaza jina la Tanzania.
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi jarida la Nchi Yetu Tanzania, Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) anayekipiga katika Klabu ya KRC Genk ya Nchini Ublegiji Mbwana Samatta amara baada ya mazungumzo baina yao katika Ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO) leo Jumanne (Mei 28, 2019) Jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, (wa tatu kulia) Dkt. Hassan Abbasi akiwa katika picha ya pamoja na Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na Mshambuaji wa Klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji (katikati) mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo baina yao katika Ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO leo Jumanne (Mei 28, 2019) Jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, (wa tatu kulia) Dkt. Hassan Abbasi akizungumza na Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na Mshambuliaji wa Timu ya KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Samatta wakati wa mazungumzo baina yao katika Ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO) leo Jumanne (Mei 28, 2019) Jijini Dar es Salaam.
 Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na Mshambuaji wa Kalbu ya KRC Genk ya Ubelgiji akifafanua jambo ka Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, (wa tatu kulia) Dkt. Hassan Abbasi wakati wa mazungumzo baina yao katika Ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO) leo Jumanne (Mei 28, 2019) Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Samatta Tours, Hamisi Waziri akifafanua jambo kwa Mkurugenzi   wa Idara ya Habari (MAELEZO) Dkt. Hassan Abbasi wakati wa mazungumzo baina yao katika Ofisi za Idara ya Habari (MAELEZO) leo Jumanne (Mei 28, 2019) Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Mbwana Samatta.
(PICHA NA MAELEZO)

MATUKIO KATIKA PICHA YA WAZIRI MKUU LEO BUNGENI

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani Bungeni jijini Dodoma Mei 28, 2019.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani akiteta na Naibu wa Waziri wake, Subira Mgalu, Bungeni jijini Dodoma, Mei 28, 2019.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani akielekea kwenye eneo maalum la kusoma Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara yake kwa mwaka 2019/2020, Bungeni jijini Dodoma, Mei 28, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Elimu ,Sayansi, Tekinolojina na Ufundi, Profesa, Joyce Ndalichako, Bungeni jijini Dodoma, Mei 28, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Mjaliwa akisalimiana na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Mei 28, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

CCM WILAYA YA KUSINI UNGUJA YAKAGUA VITUO VYA AFYA JIMBO LA MAKUNDUCHI.

$
0
0
MWENYEKITI wa CCM Wilaya ya Kusini Unguja Abdulaziz Hamad Ibrahim akiwa na Kamati ya Siasa wakikagua Sehemu ya Kuchomea Takataka (Kinu Moshi) za Kituo cha Afya Kibuteni katika ziara hiyo ya kukagua Utekelezaji wa Ilani.
MWENYEKITI wa CCM Wilaya ya Kusini Unguja Abdulaziz Hamad Ibrahim akizungumza na Uongozi wa Kituo cha Afya cha Kajengwa katika ziara ya Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo ya Kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Vituo vya Afya vilivyopo katika Jimbo la Makunduchi.
MWENYEKITI wa CCM Wilaya ya Kusini Unguja Abdulaziz Hamad Ibrahim akizungumza na Uongozi wa Kituo cha Afya cha Muyuni (hawapo Pichani) juu ya Ziara hiyo ya Kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Kituo hicho.



NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

MWENYEKITI wa CCM Wilaya ya Kusini Unguja Abdulaziz Hamad Ibrahim, ameitaka Halmashauri ya Wilaya hiyo kutatua Changamoto zinazovikabili Vituo vya Afya katika Jimbo la Makunduchi ili kwenda sambamba na Matakwa ya Ugatuzi katika Sekta ya Afya Nchi.


Maelekezo hayo ameyatoa leo katika Ziara ya Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo ya kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya Mwaka 2015/2020 katika Vituo vya Afya Vilivyomo ndani ya Jimbo la Makunduchi Unguja.

Alisema Serikali imefikia uamuzi wa kufanya Ugatuzi katika Sekta ya Afya kwa kuzipatia Mamlaka ya usimamizi Hslmashauri za Wilaya kwa lengo la kuimarisha Huduma za Afya ili Wananchi wapate huduma bora na kwa wakat mwafaka.

Mwenyekiti huyo aliipongeza Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya kwa wameimarisha upatikanaji wa Vifaa Tiba na huduma mbali mbali za msingi za Afya, lakini bado Vituo vingi vinakabiliwa na Changamoto ya Miundombinu Duni ya Majengo hali inayosababisha usumbufu kwa Wananchi na Watumishi wa Afya.

Abdulaziz alisema Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo wanatakiwa kufanya ziara za mara kwa mara katika Vituo vya Afya kwa lengo la kuratibu changamoto zinazovikabili Vituo hivyo ili viendelee kutoa Huduma Bora za Afya.

Katika maelezo yake Mwenyekiti huyo kwa niaba ya Kamati ya Siasa ya Wilaya hiyo, alimshukru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kwa kusimamia ipasavyo Mfumo wa Utoaji wa Huduma za Afya Bure kwa Wananchi.

“Tumetembelea Vituo vya Afya mbali mbali vilivyopo katika Jimbo la Makunduchi na kujionea namna vinavyotoa Huduma za Afya kwa Wananchi lakini pia tumebaini uwepo wa Changamoto ndogo ndogo na tumetoa maelekezo kwa wahusika zitatuliwe kabla ya Mwaka 2020.”alisema Mwenyekiti huyo wa CCM Abdulaziz.

Aidha alisema Chama Cha Mapinduzi Wilayani humo kitaendea kuisimamia Serikali itekeleze kwa ufanisi Ilani ya Uchaguzi hasa katika masusla ya utoaji wa Huduma za Afya ili kila Mwananchi apate fursa hiyo bila vikwazo.

Wakizungumza kwa Wakati tofauti Maafisa Utabibu wa Vituo vya Afya katika Jimbo hilo waliipongeza Serikali Kuu kwa kufanya Ugatuzi ambao umeongeza upatikanaji wa Huduma Bora za Afya kwa Wananchi wa Vijijini.

Maafisa hao walizitaja Changamoto zinazowakabili kuwa ni pamoja na Uchakavu wa Majengo ya Vituo, Ukosefu wa Uzio, Ukosefu wa Huduma za Usafiri kwa Watumishi wanaoishi mbali na Vituo hivyo, ukosefu wa Walinzi kwa baadhi ya Vituo.

Ziara hiyo imefanyika katika Vituo vya Afya vya Mtende,Kibuteni,Kizimkazi Mkunguni, Kizimkazi Dimbani pamoja na Muyuni.

NAIBU SPIKA AICHANGIA YANGA

$
0
0
 Naibu Spika  Dkt Tulia Ackson akikabidhi fedha kiasi cha Shilingi milioni moja kwa Wabunge mashabiki wa Timu ya Soka ya Yanga iliyopokelewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mheshimiwa Anthony Mavunde, Ofisini kwake Bungeni mjini Dodoma. Fedha hizo ni kwa ajili ya kuichangia Timu ya Yanga.
 Naibu Spika  Dkt Tulia Ackson akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi fedha kiasi cha Shilingi milioni moja kwa Wabunge mashabiki wa Timu ya Soka ya Yanga kwa ajili ya kuichangia timu hiyo, Ofisini kwake Bungeni mjini Dodoma .

(PICHA NAOFISI YA BUNGE)
   


FOUR WAYS NA GIRLS QUEENS KUINGIA KAMBINI RASMI KUJIANDAA NA CASTLE AFRICA 5S 2019

$
0
0
TIMU Four Ways Park Fc yenye makazi yake Kinondoni jijini Dar es Salaam na Girls Queens yenye makazi yake Msimbazi Kariakoo jijini Dar es Salaam wameingia kambini leo rasmi kujiandaa na mashindano ya Castle Africa 5s(5 – aside) yanayotarajia kuanza kutimua vumvi Juni 7 na 8,2019 katika Uwanja wa Taifa wa Zamani(Shamba la Bibi) jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Balozi wa Castle Lager Africa nchini Tanzania, Ivo Mapunda amesema timu zote ziko vizuri tayari kwa kuwakilisha Watanzania katika fainali za Kimataifa na ushindi ni lazima kulingana na maandalizi waliyonayo na watakayoendelea nayo.

Mwaka huu Tanzania tutawakilishwa na timu ya Wanaume kutoka Four Ways ya Kinondoni na timu ya Wanawake ya Girls Queens kutoka Msimbazi Kariakoo kwa ujumla timu zote ziko sawa na ziko tayari kwa fainali hizo na leo rasmi sasa wanaingia kambini kwa kujiandaa na fainali hizo.

Nae Meneja wa Bia ya Castle Lager, Pamela Kikuli alizitaji Nchi shiriki zinazotarajiwa kushiriki mashindano hayo ya Africa 5s kuwa ni Africa Kusini, Zambia, Zimbabwe, Swaziland, Lethoto, Uganda, wenyeji Tanzania na chi alikwa ya Nigeria.

Kikuli alisema Nchi hizo zikiwakilishwa na timu ya Wanaume na Wanawake zinatarajiwa kuwasili nchini Juni 5,2019 tayari kwa fainali za Castle Africa 5s.Juni 6,2019 timu zitakabidhiwa vifaa vya michezo katika Hoteli ya Lamada jijini Dar es Saalaam tayari kwa kuanza mashindano rasmi Juni 7 na 8,2019.

Tunawaomba watanzania wapenda michezo wajitokeze kuja kuzishangilia timu zao zinazowakilisha nchi katika Fainali hizo za Castle Africa 5s.Mwisho Kikuli alisema fainali hizo zinatarajiwa kuhudhuria na Balozi wa Castle Africa 5s, Samwel Eto’o hivyo tujitokeze kwa wingi kuja kumshuhudia mchezaji mkongwe wa Zamani pamoja na kupiga nae picha.

wameibuka mabingwa katika Bonanza kubwa la Soka lililofanyika mwishoni mwa wiki katika Viwanja vya Posta Kijitonyama kwa udhamini wa Kampuni ya Bia nchini (TBL) kupitia bia yake ya Castle Lager na hivyo kuzawadiwa Kikombe, Medali za dhahabu, Pesa taslimu shilingi 1,500,000/=, Caton ya bia ya Castle Lager pamoja na kuwakilisha nchi katika fainali za Caslte Africa 5s zinazotarajiwa kufanyika mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano hayo.
Baloziwa Castle Lager Africa 5s, Ivo Mapunda (kushoto) akizungumza na wachezaji wa timu ya Four Ways Fc ya Kinondonina Girls Queens ya Msimbazi Kariakoo zinazowakilisha nchi kwenye fainali za mashindano ya Castle Africa 5s wakati wa uzinduzi wa Kambimaalumu ya maandalizi ya mashindano hayo yanayotaraji wakufanyika Juni 7 na 8,2019 katika Uwanja Taifawa Zamani jijini Dar esSalaam. Jumlaya Nchinane(8) zinatarajiwa kushiriki fainali hizo mwenyeji akiwani Tanzania.
Wachezaji wa Four Ways Fc ya Kinondonina Girls Queens ya Msimbazi Kariakoo zote za jijini Dar es Salaam wakifanya mazoezi wakijiandaa na fainali za mashindanoya Castle Africa 5s yanayotarajiwa kufanyika Juni 7 na 8,2019 katikaUwanjaTaifa wa zamani nijijini Dar esSalaam. Jumla ya Nchi nane(8) zinatarajiwa kushiriki fainali hizo mwenyejiakiwani Tanzania.

TAASISI YA LSF LATOA ELIMU KWA WANAHABARI NAMNA LINAVYOFANYA KAZI NA JAMII IKIWEMO NA KUTAMBUA HAKI ZAO NA SHERIA

$
0
0
Pichani aliyesimama ni meneja mawasilano wa shirika lisilo la kiserikali linalotoa ushauri wa msaada wa kisheria la Legal Services Facility (LSF) Jane Matinde leo akitoa mada kuhusu shirika hilo namna ambavyo linavyofanya kazi na jamii kuhusu kutambua haki zao na sheria lakini pia kuboresha ushirikiano kati ya shirika hilo na waandishi wa habari ambapo yanayoendeshwa na shirika hilo. 
Pichani ni waandishi wa habari wa mikoa ya Kusini Lindi, Mtwara na Ruvuma leo wakiwa katika mafunzo ya siku moja kuhusu kuboresha ushirikiano kati ya shirika lisilo la kiserikali linalotoa ushauri wa msaada wa kisheria la Legal Services Facility (LSF) na waandishi wa habari yanayoendeshwa na shirika hilo. 
Pichani aliyesimama ni mwezeshaji wa mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari wa mikoa ya Kusini Lindi, Mtwara na Ruvuma Nevile Meena ambaye pia ni katibu wa Jukwaa la wahariri nchini (TEF) leo akitoa mada kuhusu kuboresha ushirikiano kati ya shirika lisilo la kiserikali linalotoa ushauri wa msaada wa kisheria la Legal Services Facility (LSF) na waandishi wa habari mafunzo ambapo yanayoendeshwa na shirika hilo lakini pia namna ambavyo wanapaswa kutoa elimu kwa jamii kuhusu kutambua haki zao na sheria. (PICHA NA FATNA MWINYIMKUU)

GURU PLANET YATOA MAFUNZO YA MIFUKO MBADALA KWA WAJASILIAMALI

$
0
0

IKIWA zimebaki siku nne za katazo la serikali la kutokomeza mifuko ya platiki (rambo) vikundi mbalimbali vya ujasiriamali vimeanza kutumia fursa hiyo kwa kutengeneza mifuko ya karatasi.

Kampuni ya Guru Planet iliyopo Tabata jana iliwakusanya wajasiriamali kwa kutumia mikono waliweza kujifunza na kutengeneza mifuko ya karatasi kwa lengo la kusambaza madukani na sehemu za biashara.

Akizungumza na waandishi wa Habari Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Nickson Martin alisema lengo kuwafanya wajasiriamali kujiari lakini pia kuendana na kasi ya kuacha kutumia mifuko hiyo ya rambo.

"Hapa wajasiriamali wengi baada kuona tangazo wamejitokeza na kuanza kujifunza kutengeneza mifuko hiyo ambapo tunamshukuru Mungu kwa hilo ila asilimia 90 ni akina mama na 10 akina baba kwa pamoja wataanza kupata masoko yaliyowazunguka mitaani mwao ili kuweza kuendana na kasi ya katazo,"

"Hata hivyo naamini soko ni kubwa mno hivyo kila mtu ajira hii imeanzia pale alipo na naamini watafanikiwa,"alisema Martini.Mwalimu wa mafunzo ya kutengeneza mifuko hiyo Bilhuda Mohamed alisema soko ni kubwa na huduma hiyo imeanzia kwa Dar es Salaam lakipi pia lengo kufika mikoani kote.

Wajasiriamali mbalimbali waliopata mafunzo hayo akiwemo Ester Sinduka (70) anasem alilisikia tangazo akiwa mkoani Mwanza na alipopata fursa kuja Dar es Salaam akaona ni vyema kujifunza ili akaweze kuwafundisha wajukuu zake jinsi ya kutengeneza mifuko hiyo.

Mafunzo hayo yameelewa kuwa na mwendelezo ambapo yatakuwa yanafanyika jumatatu,Alhamisi na jumamosi katika ofisi za Guru Tabata.
Mkurugenzi wa Tasisi ya Guru Planet, Nikson Martn akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa mafunzo ya utengenezaji wa mifuko mbadala kwa Wanawake wajasiliamali wa Mkoa wa Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Tasisi ya Guru Planet, Nikson Martn akionyesha baadhi ya mifuko ambayo inatengenezwa na Wanawake Wajasiliamali
Mwalimu wa ujasiliamali kutoka Guru Planet,Bilhuda Mohamed, akionyesha baadhi ya vifaa vya kutengeneza mifuko mbadala
Mwalimu wa ujasiliamali kutoka Guru Planet,Bilhuda Mohamed akiwa katika Mafunzo ya Vitendo na Wanafunzi na wanafunzi kutengeneza mifuko mbadala
Wajasiliamali wakijifunza kwa vitendo namana ya kutengeneza mifuko mbadala

JUMANNE KISHIMBA ATAKA IUNDWE TUME KUCHUNGUZA GHARAMA ZA UZALISHAJI MGODI WA BUZWAGI...AWATOLEA UVIVU WATAALAM

$
0
0
Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MBUNGE wa Jimbo la Kahama Mjini Jumanne Kishimba (CCM), ameamua kumshauri Waziri wa Madini au Spika wa Bunge Job Ndugai kuunda Tume au Kamati ambayo itajikita kuchunguza gharama za uzalishaji katika Mgodi wa Buzwagi.

Kwa mujibu wa Kishimba ameliambia Bunge kuwa mgodi huo unatakiwa kufungwa au kufukiwa wakati bado una kiwango kikubwa cha dhahabu.

Akizungumza Bungeni Mjini Dodoma wakati akichangia mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Madini wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2019/2020 amesema mbali na kuipongeza Wizara hiyo kwa kazi nzuri, lakini wakati wa ziara ya Makamu wa Rais kwenye mgodi huo, Meneja wa Mgodi huo aliwaambia wanataka kuufunga kutokana na ukubwa wa gharama za uzalishaji.

Kishimba ameelezea kusikitishwa kwake na uamuzi wa kutaka kwenda kuufunga au kuufukia mgodi huo wa Buzwagi wakati bado una kiwango kikubwa cha dhahabu.Pamoja na uamuzi huo meneja huyo aliwaambia kiasi cha dhahabu kilichopo ndani ya mgodi huo. Kwa mujibu wa Kishimba kiasi hicho ni sawa na tani 31 za dhahabu.

Kishimba amesema kuwa alichodai meneja huyo wa mgodi ni kwamba gharama zao za uzalishaji ni kubwa na kwamba tani 31 za dhahabu ni sawa dola za Marekani bilioni moja na laki mbili ambazo ni sawa na Sh.trilioni 28.

"Kuufukia mgodi wa dhahabu wenye Sh. trilioni 28 wakati tuna uwezo wa kufunga Mto Rufiji tukapata umeme ni jambo la kushangaza. Mheshimiwa Spika lazima lawama tuzipeleke kwa wataalamu wetu.

"Kweli ni wavivu wa kufikiri, hauwezi kuletewa ripoti na mtu mmoja tena mwenye mgodi ukakubali kuufukia mgodi wako wenye thamani ya Sh. trilioni 28 ndani wakati wewe una shida ya kujenga treni ya mwendo kasi (SGR) na unataka kuziba Mto Rufiji.

"Haiwezekani Spika, kitu ambacho kinahuzunisha sana Serikali kwenye sheria yetu mpya ina asilimia 16 mle ndani, ina maana na Serikali itapoteza kodi, lakini alichosema meneja wa mgodi ni kuwa gharama zao ni kubwa,"amesema Kishimba.

Ameongeza kuwa "Nitoe ombi kwa Waziri au wewe Spika iundwe Tume au kamati ndogo ambayo itakwenda kuangalia gharama za uzalishaji katika mgodi huu zile ambazo zinaweza kuondolewa, ziondolewe.

"Lakini Serikali kwa upande wake ifikirie, maana Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) peke yake inapata Sh.bilioni 2 kwa mwezi, Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) zaidi ya Sh.bilioni 20, Idara ya Maji tunapata zaidi ya Sh. bilioni 4, hawa na wao wanaweza kupunguza viwango vyao maana kama mgodi utafungwa maana yake na wenyewe hivi viwango vyao havitafanya kazi popote."

Mbunge huyo ambaye amekuwa akisimama imara kutetea wananchi wa jimbo lake na Watanzania kwa ujumla kwenye masuala ya kitaifa, amesema kuhusu mgodi huo amekuwa akizungumza na Waziri mara kwa mara, lakini bado anawasiwasi wataalam waliopo ni wavivu. 

Pamoja na hayo Kishimba ametumia nafasi hiyo kuzungumzia suala zima la madini ambapo amesema utajiri wa Waraabu ni mafuta na wanapata utajiri pale mafuta yanapopanda bei.

"Kwetu sisi tunayo dhahabu, wahasibu wetu wanachanganya bei ya kiwanda na madini, dhahabu haipandi kwa ajili ya gharama za uzalishaji...inapanda kulingana na hali inavyoendelea duniani,"amefafanua Kishimba na kwamba Duniani kote kama kuna hofu au tatizo lolote dhahabu nayo lazima itapanda.

Mbunge huyo amesema kilichoongezeka hapo si kwa sababu ya uzalishaji, bali kwa sababu ya mahitaji duniani tofauti na kiwanda na kuongeza Serikali ya Tanzania kama wahasibu au wataalamu waliopo watakubali, basi kuna utajiri mkubwa pale bei ya dhahabu inapopanda.

Amesisitiza kuwa "Hii fedha Spika siyo fedha ya mwenye mgodi na hawezi kuidai kwa sababu hata dhahabu isipopanda yeye anaendelea na uzalishaji na faida anapata. Waarabu wanatajirika pale bei ya mafuta inapopanda, ile tofauti yote inatakiwa kuwa mali ya Serikali na si ya mwenye mgodi, maana hicho ni akiba ya hiyo nchi si ya mwenye mgodi," amesema.

Kishimba wakati anazungumza Bunge lilikuwa likimsikiliza kwa umakini ambapo pamoja na kuomba kuundwa kwa tume ya kuchunguza mgodi huo amesisitiza umuhimu wa watalaam kuchangamka na kuondoa uvivu uliopo kwani kwa upande wake anaona baadhi ya watalaamu ni tatizo.

TCRA yawafikia Wakazi wa Mafinga katika utoaji wa Elimu ya Usajili wa laini kwa kutumia alama za vidole.

$
0
0
Wakazi wa Mafinga na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi katika kampeni ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu Mitandaoni na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa ajili ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa kuweka alama za vidole kwa laini za simu.

Mkuu wa TCRA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Mhandisi wa TCRA Asajile John amesema ni fursa kwa wananchi wa Mafinga kupata huduma kutokana na kuwa na mnyororo wadau wa mawasiliano. 

Amesema kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano. 

Asajile amesema kuwa wananchi wasio kuwa na Vitambulisho vya NIDA wahakikishe wanapata katika usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole. 

"TCRA iko karibu na wananchi katika utoaji wa elimu za utumiaji wa bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma hiyo"amesema John.
Wananchi wa Mafinga na Maeneo ya jirani wakiwa katika Mnada uliokwenda sambamba na Mnada kwa Mnada karibu tukuhudumia wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) pamoja na wadau mbalimbali katika utoaji wa elimu wa usajili laini za simu kwa kutumia alama za vidole.
Wananchi wakisoma vitabu vya muongozo vya TCRA mamna ya kutumia bidhaa za mawasiliano.
Mwananchi akihudumiwa uwekaji wa alama za vidole katika usajili laini za simu. 
Wadau mbalimbali wa Mnada kwa Mnada karibu tukuhudumie wakitoa huduma katika Mnada wa Mafinga wakitoa huduma za bidhaa za mawasiliano.
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live




Latest Images