Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live

KIDAO KUHUDHURIA SEMINA YA FIFA NCHINI MALAWI.

$
0
0
Na Agness Francis, Michuzi Tv.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Kidao Wilfred pamoja na Mkurugenzi wa Mashindano TFF Salum Madadi wanatakiwa  kushiriki kwenye semina ya FIFA ya siku mbili huko nchini Malawi. 

Uongozi wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) umetanabaisha kuwa semina hiyo itakayofanyika Blantyre nchini  humo ambayo inatarajia kuanza leo  Mei 15 na kumalizika kesho Mei 16 mwaka huu itahusiana na miundo mbinu

Uongozi huo umesema kuwa Washiriki 34 kutoka nchi mbalimbali watashiriki katika semina hiyo inayosimamiwa na  FIFA, huku ajenda kubwa ikiwa ni masuala ya miundo mbinu ya uboreshaji wa viwanja vya  mpira wa miguu.

Mbali na Tanzania tu nchi nyingine kutoka barani Afrika  zimealikwa kuhudhuria mkutano huo wa FIFA.

"Nchi hizo ambazo ni Uganda,Seychelles,Sudan Kusini,Misri,Eswatini,Eritrea,
Gambia,Lesotho,Cape Verde,Liberia,Msumbiji,Somalia,Afrika Kusini na Wenyeji wao Malawi" umesema uongozi wa TFF.
Mtendaji mkuu wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania  (TFF)   Wilfred Kidao. 

MATUKIO MBALIMBALI YA BUNGENI LEO JIJINI DODOMA

$
0
0
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi akisisitiza kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali inapotwaa maeneo ya wananchi kwa ajili ya matumizi ya Jeshi ikiwemo kuwalipa fidia wananchi hao, ameyasema hayo Bungeni Jijini Dodoma leo Mei 15, 2019.
 Waziri wa Nishati Dkt.  Medard Kalemani akieleza mikakati ya Serikali katika kuhakikisha kuwa wananchi wa mikoa mbalimbali ikiwemo Mtwara, Lindi na Dar es Salaam wanaunganishiwa huduma ya gesi majumbani ili kuchochea maendeleo .
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi mhe.  Dkt Angelina Mabula akisisitiza jambo kwa  Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira mhe. Mussa Sima leo Bungeni Jijini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali na majibu.
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo kwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi leo Bungeni Jijini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Nishati mhe. Subira Mgalu akisisitiza wakandarasi wote kutekeleza miradi ya usambazaji umeme vijijini (REA) kwa wakati ili kutimiza azma ya Serikali kufikisha umeme kwa wananchi wote Vijijini.
 Sehemu ya wageni waliofika Bungeni wakifuatilia kipindi cha maswali na majibu leo Bungeni Jijini Dodoma.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Mei 15, 2019. Katikati ni Mbunge wa Busega, Dkt. Raphael Chegeni. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Busega, Dkt. Raphael Chegeni kwenye viwanja vya Bunge jijini Dodoma, Mei 15, 2019. 

chama cha wataalamu waliobobea kupambana na ufisadi wakutana kujadili njia za kumaliza ufisadi

$
0
0
Na Woinde Shizza,Michuzi TV-Arusha

CHAMA cha wataalamu waliobobea katika kupambana na Ufisadi duniani (ACFE)kimejipanga kuanza kutumia teknolojia za kisasa katika kubaini na kuchunguza uhalifu huo unaoonekana kushika kazi katika nchi mbalimbali duniani.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo katika mkutano mkuu wa chama hicho,unaofanyika tawi la Tanzania, jijini Arusha ,Rais wa ACFE ,Emanuel Johanness alisema lengo kubwa la mkutano huo ni kuangalia mapambano ya ufisadi katika siku za usoni kutokana na aina ya ufisadi kuhamia kwenye kiteknolojia zaidi.

Alisema taarifa yao ya mwaka jana 2018 imeonyesha kuwa katika kesi 2690 za ufisadi zilizoripotiwa kutoka nchi 125 duniani katika sekta mbalimbali 23, imeonyesha kuwa kiasi cha dolla za kimarekani billion 7 zimepotea kutokana na ufisadi unaofanyika kwenye taasisi za umma ,makampuni na sekta binafsi.

Alisema kuwa njia sahihi inayotumika kwa sasa kubaini ufisadi ni pamoja na kupewa taarifa za siri kutoka kwa wananchi wazalendo ,ambapo pamoja na mafanikio hayo ipo haja kwa chama hicho kupeana mbinu mbadala ikiwemo matumizi ya teknolojia za kisasa kubaini ufisadi.

“Kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo wahalifu hawa wanavyozidi kugundua mbinu mpya za kufanya ufisadi,na ndio maana katika mkutano huu tumealika mwenzetu kutoka nchi ya Afrika kusini kuja kutupatia uzoefu wa namna wao wanavyopambana na ufisadi kwani nchi yao imefanikiwa kwa kiwango kikubwa zaidi na mapambano hayo na walianza mda mrefu kupambana na wahalifu hawa”alisemaJohaness

Akizungumzia kasi ya ufisadi hapa nchi alisema bado ni kubwa na alibainisha kuwa ufisadi mkubwa unaoongoza hapa nchi ni pamoja na rushwa,ubadhilifu wa fedha na kughushi na kwamba hatua ya serikali kuanzisha mahakama ya mafisadi itasaidia sana kupunguza uhalifu huo na kuokoa fedha za serikali kutokana na baadhi ya waalifu kukutwa na hatia na mali zao kutaifishwa .

Hata hivyo chama hicho kwa upande wa tawi la Tanzania kimefanikiwa kwa kiasi kikubwa kubaini matukio ya ufisadi kutokana na wanachama wake zaidi ya 200 kutoka katika sekta nyeti hapa nchini jambo ambalo limefanikisha kupata taarifa za siri na kuzifanyia uchunguzi haraka.

Kwaupande wake mmoja wa washiriki kutoka mamlaka ya mapato Tanzania TRA Salum Kessy alisema kuwa serikali ilivyoanzisha mahakama ya ufisadi ni miongoni mwa hatua nzuri kwani hata wao wanavyofanya uchunguzi ukikamilika wanapata pa kuwapeleka wahalifu hao.

Alisema kuwa iwapo watanzania tutaungana kwa pamoja zikiwemo taasisi za kiserikali pamoja na binafsi kukemea ufisadi basi tutapunguza kwa kiasi kikubwa tatizohili na sio kupunguza tu bali tunaweza kulimaliza kabisa tatizo hili.

Mkutano huo mkuu unafanyika kwa siku tatu hapa nchini na unashirikisha wataalamu kutoka nchi tano za afrika ambazo ni Kenya ,Nigeria ,Afrika kusini ,Uganda,Zambia na wenyeji Tanzania na kwamba chama hicho cha wataalamu waliobobea katika kupambana na ufisadi kina wanachama toka nchi zaidi 160 duniani na mkutano huo unatarajia kutoka na jibu moja utakaotoka na mbinu itakaomaliza ufisadi katika nchi mbalimbali duniani.
 Rais wa chama cha wataalam waliobobea katika kupambana na ufisadi ( ACFE) ,Emanuel Johanness akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Arusha.
  Washiriki wa mkutano huo wakiendelea kufuatilia kwa makini  

 

KESI YA MBOWE NA WENZAKE YAENDELEA KUUNGURUMA MAHAKAMA YA KISUTU

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Michuzi Tv
SHAHIDI wa Tatu katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi Tisa wa Chadema, ameieleza mahakama kuwa alimshuhudia Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe akichukua kipaza sauti  na kutoa tamko la kuwashinikiza  viongozi wenzie na wafuasi wa Chadema kuandamana kuelekea katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni kuchukua barua.

Shahidi huyo, E 6976 Koplo Rahimu Msangi, ameeleza hayo leo, Mei 15, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba wa  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati akitoa ushahidi wake dhidi ya viongozi hao.

Mbali na Mbowe washtakiwa wengine ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Vincent Mashinji, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu na Naibu Katibu Mkuu Bara na Mbunge wa Kibamba, John Mnyika.

Wengine ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Akiongozwa na wakili wa serikali Wankyo Simoni, Koplo Msangi amedai,  Februari 16,2018 huko Mwananyamala, katika viwanja vya Bauibui ambapo Chadema walikuwa wakifanya mkutano wa Kampeni alimshuhudia Mbowe akichukua kipaza sauti hicho kutoka kwa aliyekuwa Mgombea wa Ubunge jimbo la kinondoni (hakumtaja jina) aliyekuwa amepanda jukwaani akinadi sera zake na kisha kuanza kutoa tamko hilo.

Akieleza tukio hilo, Koplo Msangi amesema, siku hiyo yeye akiwa na maaskari wengine walifika eneo hilola buibui baada ya kupata maelekezo kutoka kwa Inspekta Mohamed Ngereje kuwa wafike pale, na wakiwa pale waliwashuhudia viongozi wa Chadema wakitoa maneno yanayoashiria uvunjifu wa amani.

Koplo Msangi ameendelea kudai kuwa, mbowe baada ya kuwatangazia wanachama wake waandamane, alishuka chini na kushikana mikono na viongozi wenzake waliokuwepo eneo hilo na kuandamana wakipitia mbarabara ya Mwananyamala, Kinondoni Studio hadi barabara ya Kawawa huku wakiimba nyimbo ambazo maneno yake yalisikika 'hatuogopi, hatushikiki, tutaandamana hadi kieleweke', .

Amedai, wandamanaji walionekan kuwa na hasira nanwalikuwa wameshika mawe,marungu na chupa za maji ambapo walipofika eneo la Mkwajuni,polisi walitoa irani ya kuwataka watawanyike lakini walikaidi na badala yake waliwarushia polisi mawe,na marungu ambapo yeye alipigwa jiwe eneo la shingoni na baada ya hapo hakufahamu kilichoendelea na kujikuta yupo hospitali amelazwa.

Ameeleza kuwa, alilazwa katika Hospitali ya Polisi (barracks)  iliyopo barabara ya Kilwa na aliposhtuka alikumbuka kwamba alikuwa na silaha aina ya SMG ambayo wakati huo hakuwa nayo lakini alikuja kuelezwa na Inspekta Ngereji kuwa, silaha take ipo kituo cha polisi cha Osterbay

WAJASIRIAMALI WADOGO NA WAKATI WAPATIWA MAFUNZO CHUO KIKUU DAR ES SALAAM

$
0
0
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Shule Kuu ya Biashara (UBDS) kupitia Kituo cha Ubunifu na Ujasiriamali cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDIEC) kwa kushirikiana na ufadhili wa European Investment Bank (EIB) kimetoa mafunzo kwa wajasiriamali wadogo na wakati juu ya ufahamu kwenye biashara na mipango kabla ya kuanza biashara.

Miongoni mwa masuala waliyofundishwa ni pamoja na kujua mipango ya kibiashara, vyanzo vya fedha, kujua masoko, namna ya kuwa na bidhaa bora na jinsi ya kuuza kwa faida pamoja na kufundishwa namna bora ya kuandaa maandiko ya kibiashara.

Mafunzo hayo ya siku tatu yalianza tarehe 13 na kumalizika Tarehe 15 Mei 2019 yameshirikisha wajasiriamali kutoka ndani na nje ya Dar es Salaam ili kuweza kutoa nafasi na wigo mpana kwa wajasirimali kujikumbusha mbinu na namna bopra za kuboresha baishara zao.
 Wajasiriamali wadogo na wakati wakifuatilia maelekezo kutoka kwa mwezeshaji (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya namna ya kuboresha biashara zao pamoja na kufahamu mbinu za kujua masoko, bidhaa na namna ya kuuza na kupata faida. Mafunzo hayo yametolewa na Kituo cha Ubunifu na Ujasiriamali cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDIEC) kwa kushirikiana na ufadhili wa European Investment Bank (EIB) katika jengo la Shule kuu ya Biashara kuanzia tarehe 13 hadi 15 Mei, 2019.
 Wajasiriamali wadogo na Wakati wakifuatilia kwa makini mafunzo ya Ujasiriamali yaliyoendeshwa na Kituo cha Ubunifu na Ujasiriamali cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDIEC) kwa kushirikiana na ufadhili wa European Investment Bank (EIB) katika Jengo la Shule kuu ya Biashara chuo kikuu cha Dar es Salaam.
 Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Mteja kutoka Benki ya Access Alexander akiwaeleza wajasiriamali wadogo na wakati huduma zinazotolewa na benki ya Access, na namna bora ya kutunza fedha katika akaunti tofauti zilizopo katika benki hiyo pamoja na kuwafundisha mbinu za kuwekeza na kukuza mitaji ili waweze kukopesheka kwa urahisi.

MMONYOKO WA MAADILI CHANZO CHA UKATILI NDANI YA FAMILIA

$
0
0
Kwa kipindi cha Miezi tisa Julai 2018 hadi Machi 2019 Jumla ya Mashauri ya ndoa 16832 yalipokelewa ikilinganishwa na mashauri 13382 ya mwaka 2017/18 hali ambayo ni sawa na ongezeko la 34% ya migogoro ya ndoa hapa Nchini.

Akiongea kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu Mkurugenzi wa Watoto wa Wizara hiyo Mwajuma Magwiza aliitaja changamoto ya maadili ya mmomonyoko wa maadili kuwa chanzo cha migogoro ya ndoa hapa Nchini.

Magwiza aliongeza kuwa Vitendo vya ukatili kwa watoto ndani ya familia vimekithiri huku wahausika wakubwa wa vitendo hivyo wakiwa wanafamilia hili likijionesha katika takwimu za Jeshi la polisi za mwaka 2017 zinaonesha kuwa Jumla ya matukio ya ukatili kwa watoto 13457 yameripotiwa na Jeshi la polisi.

Alivitaja vitendo hivyo kuhusisha ukatili wa kingono wenye matukio 3,583, mimba za utotoni 1,323 akiongeza kuwa taarifa jeshi hilo imeonesha matukio ya mikoa ya kipolisi yenye ukatili mkubwa kuwa ni kinondoni matukio 2,426, Dodoma 1,283, Tanga 164, Tameke 984 na Arusha Matukio 972.

Wakati huo huo Serikali imewataka baadhi ya Wazazi Nchini kuacha tabia ya kutoa kipaumbele cha elimu kwa watoto wa kike kama ilivyo kwa watoto wa kiume jambo ambalo linakwamisha juhudi za Serikali katika kuhakikisha usawa wa kijinsia unatekelezwa katika nyanja zote bila ubaguzi wa kijinsia.

Akisoma hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Dodoma Mhandisi Happiness Mgalula ambaye pia ni Katibu Tawala Masaidizi Mkoa wa Dodoma aliongeza kuwa ni lazima elimu itolewe kwa kuzingatia usawa wa kijinsia.

Aidha Mgalula amewataka wazazi na walezi kutoa kipaumbele cha elimu kwa watoto wote bila kujali jinsia ikiwa ni hatua muhimu ya kutekeleza ahadi ya Rais kwa vitendo ya utoaji elimu bure kwa wanafunzi hapa Nchini.

Mgalula aliongeza kuwa Tanzania bado inakabiliwa na tatizo la mila potofu akizitaja mila hizo kuwa ni kuwa ni mimba na ndoa za utotoni, haki ya wanawake kumiliki ardhi, vipigo kwa wanawake akiutaja mkoa wa Dodoma kuwa wa pili kitaifa katika vitendo vya ukatili hapa Nchini.

Aidha Mugarula amewataka wanafamilia kuhakikisha wanakuwa ana Afya bora kwa kuhakikisha wanakuwa na vitambulisho vya Bima ya Afya, Elimu na akina mama wajawazito kuhakikisha wanaenda hospitali ili kupata huduma ya Afya kwa mama na mtoto.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Dodoma Happy Hiza amesema Mkoa wa Dodoma umefanikiwa kutoa elimu juu ya Makosa ya Jinai kwa maafisa Ustawi na Maendeleo ya jamii na katika ngazi ya Jamii ili kuwezesha elimu ya malezi na makuzi kwa watoto katika jamii.
 Wanafunzi wa kikundi cha Brass Band kutoka Shule ya Msingi St. Home wakiongoza Maandamano ya Wanafunzi wenzao katika kilele cha Mazimisho ya Siku ya Familia Duniani yaliyofanyika leo katika Mkoa wa Dodoma.
 Mkurugenzi wa Idara ya Watoto wa Wizara ya Afya kutoka Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Mwajuma Magwiza akitoa hotuba kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara yake wakati kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani yaliyofanyika leo katika Mkoa wa Dodoma.
 Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Dodoma Happiness Mgalula akitoa hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma wakati wa kilele cha Mazimisho ya Siku ya Familia Duniani yaliyofanyika leo katika Mkoa wa Dodoma.
 Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Dodoma Happiness Mgalula akivalishwa skafu na Skauti wa Mkoa wa Dodoma mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Nyerere Square katika Maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani .
Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Dodoma Happiness Mgalula akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.

MAHAKAMA YAMFUTIA MASHTAKA KIGOGO WA UDART

$
0
0
Na Karama Kenyunko,Michuzi TV
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemfutia mashtaka mkurugenzi wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es Salaam (UDART) Robert Kisena (46) na mkewe Frolencia Mashauri nisha kukamatwa tena na kuunganishwa katika kesi moja yenye  mashitaka 19 ikiwemo kusababisha hasara kwa UDART ya Bil.2.41.

Awali washtakiwa hao  walikuwa wakishtakiwa  pamoja na wenzao watatu mbele ya Mahakimu Thomas Simba na Augustine. Mbali na Kisena na Mkewe, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Kulwa Kisena(33), Charles Newe(47) na raia wa China, Cheni Shi (32).

Baada ya kufutiwa mashitaka yao chini ya kifungu namba 91 (1) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai (CPA) sura ya 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 walikamatwa na kuunganishwa katika kesi moja.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwizire  Wakili wa Serikali, Grory Mwenda amedai washtakiwa wanakabiliwa na mashitaka 19 likiwemo la  Kuongoza genge la uhalifu, kujenga kituo cha mafuta bila kibali, kuuza mafuta sehemu zisizoruhusiwa, Wizi wa mafuta, utakatishaji fedha wa Bil.1.2, kughushi na kusababisha hasara ya Bil.1.4.

Katika kosa la utakatishaji fedha linamkabili Robert Kisena na Chen Shi inadaiwa Aprili 8,  2016 katika benki ya NMB Kisena akiwa Mkurugenzi wa UDART alihamisha Sh.Mil 594.92 kwenda kwenye akaunti nyingine ya Kampuni ya Longway Engineering Company wakati akijua fedha hizo ni zao haramu lililotokana na makosa ya kughushi.

Pia  washitakiwa wote wanadaiwa kati ya Mei 25, 2015 na December 2016 wakiwa Dar es Salaam waliisababishia hasara UDART  ya Bil.2.41.

Aidha katika kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu linalomkabili Kisena na Shi imedaiwa June 9, 2016 katika tawi la NMB Ilala washtakiwa kwa nia ya  ovu waijipatia Mil.603.25 kutoka UDART kwa kuonyesha kiwango hicho kimelipwa kwa ajili ya ujenzi wa uzio wa  Kituo cha UDART Kimara, Ferry  (Kivukoni), Ubungo na Morocco.

Hata hivyo, washitakiwa hawakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo. Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika. Kesi imeahirishwa hadi Mei 28, 2019 kwa ajili ya kutajwa.

TUME YA NGUVU ZA ATOMIKI TANZANIA YAWASHAURI WAFANYABIASHARA KUPIMA BIDHAA ZAO

$
0
0
TUME  ya Nguvu za Atomiki Tanzania(TAEC) imewashauri wafanyabiashara nchini kuendelea kupima bidhaa zao ili kuhakikisha mionzi yake ni salama na ambayo haitaleta madhara.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania Profesa Busagala alipowasilisha mada katika mkutano wake na baadhi ya wafanyabiashara wa jijini Mwanza ambapo amesema kwa kupima bidhaa zao ni jambo la kufuata sheria.
 
 Pia amezungumza nao kuhusu majukumu ya tume kisheria ili kuongeza uelewa na kujadiliana hatua mbalimbali ambazo zitaisaidia kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Mwanza na wafanyabiashara wote wanaolizunguka ziwa Victoria.
 
Katika mkutano huo ,wamejadili masuala mbali mbali ya Tume ya Atomiki Tanzania ikiwa ni pamoja na kuangalia mapungufu mbalimbali na hatimaye kuchukua hatua stahiki ili kuweka ustawi mzuri kati ya wafanyabiashara wa Mwanza na maeneo menginine nchini na kuyafanyia kazi kwa lengo la uboreshaji.

Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania ( TAEC) ambayo ndio mamlaka pekee yenye dhamana ya Udhibiti wa mionzi na uhamasishaji Salama wa matumizi ya teknolojia ya Nyuklia hapa nchini.

Hata hivyo katika mkutano huo Prof. Busagala amewaeleza wafanyabiashara hao kuwa athari za mionzi zinaweza kuleta madhara makubwa endapo kutakuwa na ukiukwaji wa kisheria
 
Prof. Busagala amesisitiza umakini na ushirikiano mkubwa unahitajika ili kuendelea kudhibiti na kuna ulazima mkubwa wa kupima bidhaa hizo ili kukidhi matakwa ya sheria ya Nguvu za Atomiki (Atomic Act No 7) na Sheria za Kimataifa kwani kwa kutokufanya hivyo kutakuwa na ukiukwaji sheria iliyopo ya udhibiti wa mionzi ili kutosababisha madhara yanayoweza kusababishwa na vimelea vya mionzi kwa wananchi na mazingira
 Wakiwa katika picha ya pamoja.

VOA SWAHILI: Duniani Leo May 15, 2019

HABARI ZA UMOJA WA MATAIFA KUTOKA NEW YORK MEI 15, 2019

GAVANA SHILATU ALIA NA KANDARASI ZA UJENZI TARAFA YA MIHAMBWE WILAYANI TANDAHIMBA, MTWARA

$
0
0
Wakandarasi wanaoshinda kandarasi za ujenzi wametakiwa kuacha urasimu na  ubabaishaji  kwenye utekekezaji wa kazi wanazolipwa na Serikali  na miradi yote itakayokosa ubora wa viwango isipokelewe.

Pia imeelezwa kwamba  si busara kwa kampuni za ujenzi  zilizopitishwa chini ya taratibu za kisheria, kushinda zabuni na kulipwa fedha  za umma zishindwe kujenga kwa viwango na kumaliza kwa wakati. 

Msimamo huo umetolewa na Afisa Tarafa Mihambwe Wilayani Tandahimba mkoa wa Mtwara Gavana Emmanuel Shilatu  alipokagua ujenzi miradi ya ofisi, soko na choo  katika kiijiji cha Ngongolo  kata ya Miuta. Alisema Wakandarasi wana wajibu wa kutimiza ahadi kama mikataba yao ilivyoeleza, kujenga majengo kumaliza kwa wakati husika kazi zao bila visingizio vyovyote.

"Tabia za uzembe na ubabaishaji mkubwa wa ujenzi chini ya kiwango na miradi mingine kutokuanza kabisa licha ya Mkandarasi kupewa pesa tangu Septemba 2018 inatakiwa ife.

"Ifike mahali  uzalendo utusute na kuona aibu. Tuheshimu fedha za umma na kusimamia matumizi bora. Hatuwezi kupata maendeleo ikiwa tutaongozwa na uzembe au ubadhirifu. Miradi ambayo itakosa kujengwa kwa viwango isipokelewe." Alisema Gavana Shilatu 

Aidha Gavana huyo alitoa agizo kwa Mkandarasi wa ujenzi huo akimtaka kufika kazini mapema na kuiasa Serikali ya Kijiji pamoja na kamati ya ujenzi kuwa makini katika usimamizi miradi  ya maendeleo.

Katika ziara hiyo Gavana Shilatu aliambatana na Mtendaji Kata Miuta, Serikali Kijiji cha Ngongolo pamoja na kamati ya ujenzi Kijiji cha Ngongolo.
 Afisa Tarafa Mihambwe Wilayani Tandahimba mkoa wa Mtwara Gavana Emmanuel Shilatu  akikagua wa ujenzi miradi ya ofisi, soko na choo  katika kiijiji cha Ngongolo  kata ya Miuta. 
 Afisa Tarafa Mihambwe Wilayani Tandahimba mkoa wa Mtwara Gavana Emmanuel Shilatu  akikagua wa ujenzi miradi ya ofisi, soko na choo  katika kiijiji cha Ngongolo  kata ya Miuta. 
 Afisa Tarafa Mihambwe Wilayani Tandahimba mkoa wa Mtwara Gavana Emmanuel Shilatu  akikagua wa ujenzi miradi ya ofisi, soko na choo  katika kiijiji cha Ngongolo  kata ya Miuta. 
Afisa Tarafa Mihambwe Wilayani Tandahimba mkoa wa Mtwara Gavana Emmanuel Shilatu  akikagua wa ujenzi miradi ya ofisi, soko na choo  katika kiijiji cha Ngongolo  kata ya Miuta. 

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA (AFRICAN DEVELOPMENT BANK (AfDB) DKT. AKINWUMI ADESINA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi zawadi ya picha ya Wanyama Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi zawadi ya picha ya Wanyama Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza mgeni wake Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza mgeni wake Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya kupiga picha ya pamoja na viongozi wengine kutoka nchini  na ujumbe kutoka benki hiyo ya AfDB.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari pamoja na mgeni wake Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt. Akinwumi Adesina mara baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam akizungumza na wanahabari. PICHA NA IKULU

WHO IS HUSSAIN YATOA MSAADA WA VYAKULA KATIKA MWEZI MTUKUFU WA RAMADAN HUKO VIGWAZA

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, BAGAMOYO 

SHIRIKA linalosaidia watu wenye maisha duni na kuleta mabadiliko chanya katika jamii  la WHO IS HUSSAIN?, kwa kushirikiana na diwani wa kata ya Vigwaza Mohsin Bharwani ,limetoa msaada wa vyakula kwa kaya 200 zilizopo kwenye kata hiyo,uliogharimu sh.milioni kumi. 

Akikabidhi msaada huo, mratibu msaidizi wa shirika la Who is Hussain?, tawi la Dar es salaam Meesam Bandali alisema,walengwa ni watu wasio na uwezo wakiwemo wenye ulemavu,wazee katika kaya 200 kata ya Vigwaza. 

"Kila kaya kati ya hizo imepatiwa box lenye vitu vilivyogharimu sh. 50,000 ,ikiwemo mchele kilo 3, maharage kilo tatu, sukari kilo 3, majani ya chai, tende na tambi ili kuwasaidia katika mwezi mtukufu wa Ramadan"alifafanua Bandali.   

Awali diwani wa kata ya Vigwaza, Mohsin Bharwani, alilishukuru shirika hilo kwa ujali na kujitoa kwao . 

"Sisi wanasiasa tunajua hali za wananchi waliopo katika maeneo yetu ambao wana hali duni kimaisha, ikitokea wafadhili kama hawa tunashukuru, nami waliponifuata niliona ni vyema kushirikiana kusaidia baadhi ya kaya ambazo zinaishi kwenye maisha duni"alisema Bharwani. 

Nae msemaji mkuu wa Who is Hussain? Iffet Thawer alibainisha, mjukuu wa mtume Mohammad S.W.A. ambae ni Hussain , alipinga dhuluma hivyo kuwa chanzo cha wao kuhamasika kufanya shughuli za kusaidia jamii ambapo lilianza miaka kumi iliyopita huko London.
Baadhi ya wakazi waliopata msaada huo,  akiwemo Said Imani, Maimuna Iddi  walielezea, vitu hivyo vinaweza kuwafikisha kimatumizi wiki mbili jambo ambalo litakuwa limezisogeza familia hizo kutokana na hali zao. 
Diwani wa kata ya Vigwaza, Mohsin Bharwani, akilishukuru shirika hilo kwa ujali na kujitoa kwao . 
  Msemaji mkuu wa Who is Hussain? Iffet Thawer akiongea wakati wa utoaji wa misaada Vigwaza
 Misaada ikitelemshwa Vigwaza
Wananchi wa Vigwaza wakijipanga kupokea misaada hiyo

JESHI LA POLISI LAWAKAMATA WATU NANE WANAODAIWA KUIBA MALI YENYE THAMANI YA MIL. 300 YA KAMPUNI YA ORGANIA PRODUCTION KIBAHA, PWAN

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA 
JESHI la polisi mkoani Pwani, linawashikilia watu nane wanaodaiwa kuhusika na wizi wa mashine za kutotoloshea vifaranga vya kuku,mashine ya maji, mfumo wa umeme na vyuma mbalimbali vya uzalishaji zenye thamani ya milioni 300, mali ya kampuni ya organia production ltd,iliyoko huko Boko Mnemela Kibaha Pwani. 
Kamanda wa polisi mkoani hapo, Wankyo Nyigesa (pichani) amewaambia waandishi wa habari kuwa, mara baada ya kupata taarifa kutoka kwa meneja wa ulinzi wa kampuni hiyo Ismail Yahaya, walifuatilia kwa kutumia kikosi maalum cha askari wa jeshi la polisi. 

Alieleza, mei 13 mwaka huu walimkamata Musa Omary (17),Abdallah Salehe  (14) na William Pius (15) wakazi wa Pichandege wakiwa na pikipiki yenye namba za usajili MC. 640  CBF aina ya Haojue iliyobeba vyuma ambavyo ni mali iliyoibiwa mei 12 katika kampuni hiyo. 
Baada ya kuendelea na upelelezi mei 14 jeshi hilo lilimkamata Dotto Said (28) ,Martin Michael (35),Mshamu Nassoro (25) na Ramadhani Dossa (25),wakazi wa Pichandege ambao nao wameshiriki kwenye wizi huo. 

"Tumemkamata mtuhumiwa Joseph Mwakasuka mkazi wa Mailmoja, Kibaha ambae ni mnunuzi wa vyuma chakavu ambapo amekamatwa na vyuma mbalimbali vinavyohusiana na mashine ya kutotolea vifaranga vya kuku, cooper wire zilizokuwa ndani ya mfuko, box za control panel nne na mifuniko ya sinki za maji "aliweka bayana. 

WAKATI HUO HUO -Emmanuel Yusuph (36) mkazi wa Chanika Dar es salaam ameuawa na watu wanaodhaniwa ni watumishi wa idara ya misitu Kisarawe. 

Alisema kuwa, kabla ya tukio hilo marehemu na mwenzake John Mwaluko mkazi wa Pugu Kajiungeni alijeruhiwa na watumishi hao kwa kukatwa miguu yote na kitu chenye ncha kali baada ya kukutwa wakichoma mkaa katika msitu huo. 

Wankyo alifafanua, mara baada ya jeshi hilo kupokea taarifa hiyo askari walifika eneo la tukio kwa ajili ya uchunguzi ambapo walifanikiwa kuwakamata Lameck Samamba (28) askari ulinzi wa misitu mkazi wa Kisarawe na Regina Mwakifuna (29)ambae ni ofisa misitu msaidizi. 

Mwili wa marehemu umehifadhiwa hospital ya wilaya ya Kisarawe na majeruhi anapatiwa matibabu hospitalini hapo.

BBC DIRA YA DUNIA JUMANNE 14.05.2019


WAKALA WA VIPIMO WAFANYA UKAGUZI KITUO CHA MAFUTA TOTAL MLIMANI CITY JIJINI DAR ES SALAAM

VISHOKA WANAOWATAPELI WAFANYABIASHARA ACHENI MARA MOJA:TRA

$
0
0
Irene Donald Meneja msaidizi wa mkoa wa kikodi wa Arusha,Upande wa ukusanyaji wa madeni na ridhaa ya ulipaji kodi.
Mkuu wa wiaya Arumeru Jerry Muro akizungumza katika wiki ya Elimu ya mlipa kodi iliyoandaliwa na TRA Mkoni Arusha.


Na Vero Ignatus,Arusha.

Onyo kali limetolewa kwa Vishoka wanaowatapeli wafanyabiashara kupitia mgongo wa Mamlaka ya Mapato TRA mkoani Arusha waache kufanya hivyo mara moja kwani Mamlaka hiyo itawatachukulia hatua kali za kisheria kwani wanakwamisha ulipaji kodi kwa hiari.

Irene Donald ni Kaimu Meneja wa TRA amesema hayo katika soko la Tengeru alipo alizungumza na walipa kodi katika wiki ya mlipa kodi ,ambapo amesema kuwa kuna baadhi ya watu wanaofahamika kama vishoka ambao hufika TRA na kufanya udanganyifu kwa wafanyabiashara kwa lengo la kujipatia faida huku wakiwaumiza wafanyabiashara.

Jerry Muro ni Mkuu wa Wilaya ya Meru amesema kuwa wafanyabiashara wanapaswa kulipa kodi kwa hiari ili kuchangaia maendeleo ya nchi na kuiwezesha serikali kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi wake.

Baadhi ya wafanyabiashara waliofika kupata elimu ya mlipa kodi Magreth Pallangyo amelalamikia uchafu wa soko la tengeru licha ya kulipa ushuru kwa Halmashauri hiyo hivyo wameiomba serikali itatue changamoto hiyo ili waweze kulipa kodi stahiki.

ANA KWA ANA NA COMEDIAN MR BENEFICIAL

HATUJAIKAMIA SIMBA SC, MTIBWA SUGAR TUTAWAFUNGA - AZAM FC

$
0
0

Na Agness Francis, Michuzi Tv. 

AFISA habari wa klabu ya Azam FC   Jaffary Iddy Maganga (pichani) amesema  baada ya kupoteza Mchezo uliopita dhidi ya Simba kwa kutoka  suluhu ya bila kufungana wanakaibiriwa tena na kibarua kizito cha kumenyana na Mtibwa Sugar ambayo ni timu kongwe na yenye uzoefu iliyopo ligi kuu muda mrefu. 


Afisa habari huyo akizungumza leo Jijini Dar es Salaam amesema kuwa Kutokana na matokeo ya mchezo ulioyopita dhidi ya wekundu wa msimbazi Simba uliopigwa katika uwanja wa Uhuru mei 13 mwaka huu Jijini Dar es Salaam kumezuka maneno kutoka kwa baadhi ya mshabiki na  viongozi wa klabu hiyo kuwa azam fc ilicheza kwa kukamia ili simba isiweze  kushinda na kuchukua ubingwa ligi kuu Tanzania bara. 

"Tulikwenda uwanjani kucheza na Simba kama Azam ikiwa tulishafungwa  bao 3-1 raundi ya kwanza  tukakubalina na matokeo, kwahiyo tulipoingia mchezo wa pili tulisoma wapi tulipotea na tusije tukapotea tena" amesema Jaffary. 

Aliongezea kwa kusema kuwa " Tumecheza na kupata suluhu ya bila kufungana hatukufurahia ile suluhu tulipanga kutoka na Alma 3 uwanjani, isipokuwa sasa ile sare Simba waliona azam walienda uwanjani kwa kuwakamia"amesema Msemaji huyo.  

Aidha amewaomba mashabiki wa soka kuacha kwenda uwanjani na matokeo yao mkononi, mchezo wa mpira una matokeo matatu kufungwa, kufanga au suluhu. 

Pia amesema mara nyingi Azam anapocheza na timu kubwa na kongwe  hapa nchini Simba au Yanga na matokeo yakiwa timu hizo zimefungwa na azam  kilamoja hulalamika kuwa wamewabania na kukamiwa. 

"Azam haipo Katika ligi kuu kwa ajili ya kumbeba mtu uwajani, tupo kwa ajili ya kujenga  jina na status ya klabu yetu,na kwa ajili ya kupambana kama Azam "amesema Jaffary.

Benki ya CRDB kufanya Mkutano Mkuu wa 24 wa Wanahisa wake jijini Arusha

Viewing all 110091 articles
Browse latest View live




Latest Images