Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110167 articles
Browse latest View live

StarTimes waipeleka ST Kids Swahili Shule ya Msingi Tabata

$
0
0
Kampuni ya Star Media (T) Ltd kupitia chapa yake ya StarTimes imeendelea kutembelea shule za msingi jijini Dar es Salaam, ikiwa ni katika kutambulisha maudhui ya chaneli mpya ya watoto, ST Kids ambayo yameingiziwa sauti za Kiswahili. 

Jumanne hii walitembelea shule ya Msingi Tabata iiliyoko Ilala jijini Dar es Salaam ambapo wawakilishi wa StarTimes walikutana na kuzungumza na wanafunzi wa darasa la 2, 3, 4 na 5 kutoka shule hiyo.

Pamoja na kuzungumza na wanafunzi wawakilishi wa StarTimes walitoa zawadi kwa ya king’amuzi na Dish kwa uongozi wa shule na zawadi mbalimbali kwa wanafunzi walioweza kujibu vizuri maswali yaliyoulizwa.

“Tumepokea vizuri ugeni wa StarTimes hapa shuleni kwetu na kwa zawadi waliyotupatia. Pia wamewapatia changamoto nzuri wanafunzi wetu kwa maswali waliyowauliza.” Mwl. Mkuu wa Shule ya Msingi Tabata Bi. Rosalia P. Mrema.

ST Kids ni chaneli ya kwanza Tanzania ya watoto ambayo vipindi vyake vinapatikana kwa lugha ya Kiswahili, lengo likiwa ni kuwawezesha watoto kuburudika na katuni na maudhui mengine kwa lugha ambayo wanaifahamu vizuri ili kusaidia ukuaji wao miongoni mwa familia na jamii zao.
“Lengo letu kutembelea shule hizi ni kutambulisha maudhui mapya yanayopatikana katika chaneli ya ST Kids ambayo yako katika lugha ya Kiswahili.

Vipindi ni vizuri kwa watoto kwani vinawafundisha stadi mbali mbali za maisha na pia vinaleta uhusiano mzuri baina yao na wazazi kwani wanaweza kuelezea hisia zao kupitia vipindi hivyo” Samwel Gisayi - Afisa Mahusiano, StarTimes Tanzania.
Kampeni hii ya kutembelea mashule jijini Dar es Salaam itaendelea hadi mwisho wa mwezi wa tano na itafikia jumla ya shule 7 katika Wilaya 3 za Mkoa wa Dar es Salaam.

Chaneli ya ST Kids inapatikana katika kifurushi cha UHURU kilichoboreshwa kwa watumiaji wa dikoda ya Antenna na kuanzia kifurushi cha SMART kwa watumiaji wa dikoda ya Dish.
 Mtangazaji wa Efm radio, Dina Marios(kushoto) akimkabidhi zawadi ya dekodam ya Startimes Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Tabata Rosalia P. Mrema wakati wa kutambulisha maudhui ya chaneli mpya ya watoto, ST Kids ambayo yameingiziwa sauti za Kiswahili.
 Meneja Maudhui  wa StarTimes Tanzania, Zamaradi Nzowa(kulia) pamoja na Mtangazaji wa Efm radio, Dina Marios wakimwonesha vifaa mbalimbali vinanyotumika kwenye king'amuzi cha Startimes  Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Tabata Rosalia P. Mrema(katikati) wakati wa kutambulisha maudhui ya chaneli mpya ya watoto, ST Kids ambayo yameingiziwa sauti za Kiswahili katika shule hiyo leo.
Picha ya pamoja

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI YA KUONGEZA KASI YA UFUGAJI SAMAKI

$
0
0
*Wastani wa mtu mmoja kwa mwaka ni kula samaki kilogram 20.

Na Chalila Kibuda  Michuzi TV
Serikali imesema kutokana kuwapo kwa uhaba wa samaki nchini imeweka mikakati ya kuongeza kasi ya ufugaji wa samaki hao kwa ajili ya kutosheleza katika soko la ndani na nje ya nchi.

 Kwa wastani mtu mmoja anatakiwa kula samaki Kilogramu 20 kwa mwaka, lakini nchini mtu mmoja anakula Kilogramu 7.9  kwa mwaka wakati samaki ana virutubisho vingi katika mwili wa binadamu.

 Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Utunzaji Viumbe Maji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Nazael Madala, wakati akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wadau wa viumbe hai wakiwamo watafiti, wafugaji na wanafunzi kwa lengo la kijadili namna ya kuboresha sekta hiyo na umuhimu wa sekta binafsi katika kuwekeza katika uzalishaji wa samaki ardhini.

“Nchini tani 350,000 hadi 380,000 za samaki zinazalishwa kwa mwaka ambazo hazitoshelezi kulingana na mahitaji yaliyopo na kukabiliana na  na uhaba  wizara inahimiza wavuvi na wadau wengine kujikita kwenye ufugaji wa samaki," amesema Dk. Madala.

 Amesema kupungua kwa samaki kunatokana na  kuwepo kwa uvuvi haramu, uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia ya nchi na kufanya samaki kupungua  kwa zaidi ya miaka 20 bila kuongezeka. .

 Kwa upande wake, Katibu wa Chama Cha Wakuzaji wa Viumbe Maji Tanzania(AAT),Geoffrey Rucho, amesema  lengo la mkutano huo ni kuhakikisha utafiti uliofanywa kuhusu hali halisi ya viumbe hai nchini na kuwakutanisha wadau kujadili kutaleta  mabadiliko chanya katika sekta hiyo kwa kuongeza uzalishaji wa samaki na kufikia malengo ya wizara.

 Naye Mtaalamu wa viumbe hai, Profesa  Philip Bwathondi, alisema viumbe hao wa majini kama samaki wamepungua kwa sababu watumiaji wameongezeka na vifaa vya kuvulia vimeongezeka.

Amesema njia ya kuongeza viumbe hao ni kuanza kufuga na kusaidia wavuvi wengine kujikita kwenye kufuga na kuongeza uzalishaji.

Bwathondi Amesema njia nyingine ni kufuga samaki wadogo ambao wakifika umri wa ukuaji wanamwagwa kwenye eneo moja la ukuaji ili kupunguza upungufu uliopo,  kwani kuna tofauti ya samaki wa baharini na wakufungwa, wale wanaofugwa ni wazuri zaidi kwa sababu wanapewa vyakula bora.
  Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Ukuzaji Viumbe Wizara ya Mifugo , Uvuvi Kajitanus Osewe akichangia mada kwenye mkutano wa viumbe hai wakiwamo watafiti, wafugaji na wanafunzi kwa lengo la kijadili namna ya kuboresha sekta hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
 Wadau wakiwa katika mkutano wa wadau wa viumbe hai wakiwamo watafiti, wafugaji na wanafunzi kwa lengo la kijadili namna ya kuboresha sekta hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Picha ya pamoja  ya pamoja ya wadau wa wadau wa viumbe hai wakiwamo watafiti, wafugaji na wanafunzi kwa lengo la kijadili namna ya kuboresha sekta hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Ukuaji wa Viumbe Hai wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt Nazael Midala akizungumza na waandishi katika mkutano wa wadau wa samaki uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Serikali kutoa elimu ya kwa Wadau wa Sanaa

$
0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM
Serikali ya ahidi kuendelea kutoa elimu kwa wadau wa Sanaa nchini iliwaweze kutambua haki na thamani ya kazi zao kufuatia changamoto ya wadau  hao kuuza kazi zao pamoja na umiliki.

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri Juliana Shonza alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Kinondoni Maulid Mtulia (CCM) lililohoji serikali inamkakati gani wa kuwasaidia vijana wanaofanya kazi za sanaa na haki zao.

“Serikali kupitia Bodi ya Filamu Tanzania na Baraza la Sanaa la Taifa imetoa elimu kwa wadau 5200 kuhusu masuala ya hakimiliki,hakishiriki,mikataba na makubaliano kupitia mafunzo ya kuwajengea uwezo ili waweze kuwa walinzi wa kwanza wa kazi na haki zao kwa kuingia mikataba yenye maslai,”alisema Shonza.

Akiendelea kuzungumza  wakati huo wa maswali na majibu bungeni Naibu Waziri huyo alitoa wito kwa wadau wote wa Sanaa kuhakikisha wanasajili kazi zao COSOTA ilikuzilinda na kuweka mazingira mazuri yatakayovirahisishia vyombo vya serikali kusimamia haki zao.

Pamoja na hayo kulikuwepo na swali la nyongeza kutoka wa Mbunge wa Mikumi Joseph Haule (CHADEMA) lililohoji kuwa serikali inampango gani wa kuifanyia marekebisho sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki ya mwaka 1999 inayosimamiwa na COSOTA kufuatia sharia hiyo kuonekana kuwa inamapungufu.

Kufuata swali hilo la nyongeza  Naibu Waziri huyo alifafanua kuwa kwasasa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo ipo katika mchakato wa kuihamishia COSOTA katika wizara hiyo kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara kwani kumekuwepo na changamoto nyingi kutokana na taasisi hiyo kuwa nje ya wizara na mchakato huo utakapo kamilika serikali itajipanga kufanya marekebisho ya sharia ya Hakimiliki na Hakishiriki.

Hata hivyo serikali iliendelea kutoa wito kwa wasanii wa kazi za filamu kuandaa kazi zenye ubora na kutumia njia ya mtandao kusambaza kazi zao kufuatia ukuaji wa teknolojia ili kuepuka changamoto iliyopo kwasasa ya kutembeza CD mkononi . 
Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mheshimiwa Juliana Shonza akijibu swali bungeni Jijini Dodoma leo Mei,14 2019 lililohoji Serikali ina mkakati gani wa kuwasadia vijana kupata haki stahiki katika kazi zao za Sanaa.

WAZIRI MKUU AWASIMAMISHA KAZI WAKURUGENZI SABA TUME YA UMWAGILIAJI

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi Wakurugenzi saba wa Tume ya Umwagiliaji akiwemo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa tume hiyo ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazowakabili.

“CAG afanye haraka uchunguzi wa kina, tunataka kujua ni nani alikuwa mlango wa ubadhirifu huu. Hatutamuonea mtu, wote watakaothibitika kuhusika na matumizi mabaya ya fedha watachukuliwa hatua.”

Waziri Mkuu amechukua hatua hiyo leo (Jumanne, Mei 14, 2019) wakati wa kikao na viongozi wa tume hiyo kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Mawaziri, Manaibu Waziri na Makatibu Wakuu. 

Mbali na kuwasimamisha kazi wakurugenzi hao, pia Waziri Mkuu ameagiza watumishi wengine 21 wa tume hiyo wachukuliwe hatua za kinidhamu kutokana na utendaji usioridhisha kwenye miradi mbalimbali inayosimamiwa na tume hiyo.

Waziri Mkuu amesema Serikali imechukua hatua hiyo kutokana na udhaifu wa kiutendaji ndani ya tume hiyo ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za miradi, rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, upendeleo na kukosa umakini. “Hatua kali zitachukuliwa dhidi ya ubadhirifu uliofanyika katika miradi ya umwagiliaji.”

Amesema hali ya kilimo cha umwagiliaji nchini hairidhishi na Serikali haijafurahishwa na utendaji wa Tume ya Umwagiliaji licha ya kuwekeza nguvu kubwa, hivyo inataka kuona mabadiliko.

“Miradi mingi inayotekelezwa na Tume ya Umwagiliaji nayo ina hali mbaya zaidi. Miradi mingi ya tume hiyo imejikita katika mafunzo, semina na warsha badala ya kujenga na kuendeleza skimu za umwagiliaji.”

Waziri Mkuu amesema tume hiyo imeshindwa kusimamia miradi takribani 10 katika maeneo mbalimbali nchini na kusababisha sekta ya umwagiliaji kushindwa kupata mafanikio yaliyotarajiwa kutokana na ubadhirifu.

Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na mradi wa umwagiliaji wa Luiche unaokadiriwa kumwagilia hekta 3,000 ambao upo katika hatua za awali za utekelezaji lakini tayari pamekuwepo na matumizi mabaya ya fedha za mradi.

“Kaimu Mkurugenzi Mkuu alitoa kibali na kulipa fedha taslimu masurufu ya jumla ya sh. milioni 100.7 kwa Wahandisi wa Makao Makuu, Maafisa wa Idara ya Mipango, Tathmini na Ufuatiliaji kwenda kufanya ukaguzi badala ya kujenga. Mkaguzi wa nje alihoji uhalali wa malipo hayo na hajapata majibu hadi leo.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga akamilishe mchakato wa kuwapata wajumbe wa bodi wa tume hiyo ambayo imemaliza muda wake.

Pia amemtaka Waziri huyo ahakikishe Wizara ya Kilimo inaisimamia tume kukamilisha ujenzi wa skimu zote za umwagiliaji zilizoanza kujengwa miaka ya nyuma zikiwemo za wakulima wadogo.

Kadhalika, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Kilimo afanye mabadiliko ya muundo wa tume hiyo na kuwa na maafisa wa umwagiliaji katika ngazi za mikoa na wilaya ili kusogeza huduma kwa wananchi.

Awali, Waziri wa Kilimo alisema skimu zinazofanya kazi hazizidi 10 kati ya 2,678 hali iliyosababishwa na kuwepo kwa dosari katika usimamizi na pia matumizi ya fedha za miradi katika Tume ya Umwagiliaji si mazuri.

Kwa upande wake, Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa alisema miradi mingi ya umwagiliaji ilifeli kwa sababu ya ilijengwa chini ya kiwango hususani mabwawa na pia haikuwa ikilingana na kiasi cha fedha kilichokuwa kinatolewa. “Mradi wa kutumia sh. bilioni mbili wanatumia sh. bilioni nne.”

Kikao hicho kimehudhuriwa na Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Kilimo, Omar Mgumba, Naibu Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa, Makatibu Wakuu wa Wizara hizo pamoja na maofisa wengine wa Serikali.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watendaji wa Tume ya Umwagiliaji kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 14, 2019. Kushoto ni Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga na wa tatu kulia ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa. Wa pili Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mhandisi Mathew Mtigumwe na kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Umwagiliaji, Eliakim Chitutu. (PIcha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Baadhi ya Watendaji wa Tume ya Umwagiliaji wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 14, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga mara baada ya kumaliza kuongea na  watendaji wa Tume ya Umwagiliaji kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 14, 2019.

TAASISI ZA KIDINI NA JUMUIA ZA KIJAMII KUANZA KUHAKIKIWA KUANZIA MEI 20 HADI 30,2019

Profesa Kitila Asaini Mkataba wa Mradi wa Maji wa Miji 29

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo (kushoto) akisaini Mkataba wa mradi wa maji katika miji 29, kulia, ni Meneja Mkazi wa kampuni ya WAPCOS kutoka India. Bw. Chandrasekhal Kombathula. Kampuni ya WAPCOS imepewa muda wa miezi miwili kumaliza kazi ya awali ili Wakandarasi wawepo katika eneo la mradi kuanza kazi. Mradi huo wenye thamanani ya Dola za Marekani milioni 500.

Wizara ya Maji imesaini mkataba wenye thamani ya Shilingi Bilioni 15.6 na Kampuni ya WAPCOS kutoka India ili kuanza kutekeleza mradi wa maji wa miji 29.

Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo, pamoja na Meneja Mkazi wa Kampuni ya WAPCOS Ltd, Bw. Chandrasekhar Kombathula wamesaini mkataba huo, wenye sehemu mbili, jijini Dodoma.

Profesa Mkumbo akizungumza katika hafla fupi ya utiaji saini amesema kazi hiyo inafanyika ukiwa ni mkopo wenye masharti nafuu kutoka Serikali ya India kupitia Benki ya Exim ya India wenye thamani ya jumla ya Dola za Marekani milioni 500.

Amesema mkataba uliosainiwa leo ni hatua ya awali na unahusu kazi mbili (lots) ambazo ni kuandaa taarifa ya kina kuhusu miradi yote wa miji 29 (detailed design) ikiwemo maeneo maji yatakapopatikana na ya pili ikiwa kuandaa nyaraka za zabuni ili kuwapata Wakandarasi watakaotekeleza mradi.

 Kampuni ya WAPCOS imetakiwa kumaliza kazi hiyo ndani ya kipindi cha miezi miwili baada ya kusaini mkataba huo leo. Wakandarasi wa kutekeleza mradi wanatakiwa wawe eneo la kazi ifikapo Septemba 2019. Mradi wa maji wa miji 29 unatarajia kuhudumia zaidi ya wananchi milioni mbili.
                                    
Imetolewa na
 Kitengo cha Mawasiliano 
14 Mei, 2019

Vita ya biashara baina na China na US yachukua sura mpya

HABARI ZA UMOJA WA MATAIFA LEO


University of Dar es Salaam Convocation call Prime Minister Majaliwa

$
0
0
On the 2nd of  May, 2019, the President of the University of  Dar es Salaam  Convocation, Ambassador Mwanaidi S. Maajar led the Convocation delegation to pay a courtesy call to one of its Prominent Alumni, the Prime Minister of the United Republic of Tanzania Hon. Kassim Majaliwa Majaliwa at his office in Dar es Salaam. 

The visit was part of the efforts of the UDSM Convocation to cultivate a relationship with its Alumni a cross the world. Hon. Majaliwa is Alumnae of 1998, Bachelor of Education in Physical Education. Hon. Kassim Majaliwa advised the Convocation to establish a system where recommendations from members of the Convocation can gain authority and influence higher education transformations and in turn increase the relevance of the Convocation. 
The President was accompanied by Mr. John Ulanga (Member of the Convocation Executive Committee), Dr. Lulu. T. Kaaya (Director of Internationalization, Convocation and Advancement- UDSM) and Mr. Daniel M. Stephen (Convocation Liaison Officer - UDSM).
 The Prime Minister Kassim Majaliwa receives a present from Mr. John Ulanga, a Member of the Convocation Executive Committee of the University of  Dar es Salaam  Convocation
 The Prime Minister Kassim Majaliwa receives the President of the University of  Dar es Salaam  Convocation Ambassador Mwanaidi S. Maajar
 Prime Minister Kassim Majaliwa poses with  President of the University of  Dar es Salaam  Convocation, Ambassador Mwanaidi S. Maajar, Mr. John Ulanga (Member of the Convocation Executive Committee), Dr. Lulu. T. Kaaya (Director of Internationalization, Convocation and Advancement- UDSM) and Mr. Daniel M. Stephen (Convocation Liaison Officer - UDSM).
 The Prime Minister Kassim Majaliwa greets  Mr. Daniel M. Stephen (Convocation Liaison Officer - UDSM).
The Prime Minister Kassim Majaliwa greets Dr. Lulu. T. Kaaya, the Director of Internationalization, Convocation and Advancement- UDSM

Rais Dkt Magufuli atengua uteuzi wa mkuu wa mkoa wa Katavi,amteua Mkuu wa Wilaya ya Tunduru kushika nafasi hiyo.

BEI YA VYAKULA SOKO LA GONGO LA MBOTO

$
0
0
Baadhi ya wananchi wa jiji la Dar es salaam, wakiwa katika soko la  Gongo la mboto  wakijipatiamahitaji yao kufuatia kuanza kwa Mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Kwa mujibu wa wananunuzi hao,wameiambia Michuzi  Tv kwa nyakati tofauti kuwa bei ya bidhaa hizo  zina unafuu wa bei ambapo fungu moja la viazi limauzwa shilingi 1000 mpaka 2000 magimbi 1000 mpaka 3000 na Nazi kuanzia mia tano mpaka 1000  (Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)

Wafanya biashara wa viazi katika  soko  la  Gongo la mboto wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam wakisubiri wateja wanaotoka sehemu mbalimbali,ambapo fungu moja la viazi limauzwa shilingi 1000 mpaka 2000 magimbi 1000 mpaka 3000 na Nazi moja  kuanzia mia tano mpaka 1000.    

TRA YATAKIWA KUIMARISHA UKAGUZI WA MASHINE ZA EFD

$
0
0
Afisa Elimu kwa Walipakodi TRA Kanda ya Kaskazini Eugenia Mkumbo amesema kuwa Mamlaka hiyo inatoa fursa kwa wafanyabiashara wanaolalamikia kukadiriwa kodi ya juu kuliko kipato chao.
Mkui wa Wilaya ya Arusha Gabriakizindua wiki ya mlipa kodi iliyofanyika eneo la stendi kuu ya Mabasi ya mikoani,ambapo ameitaka TRA 
Baadhi ya wananchi waliojitokezankatika uzinduzi wa wiki ya Elimu kwa mpiga kodi iliyoansaliwa na Mamlaka ya Matapo nchini TRA Jijini Arusha



Na Vero Ignatus ,Arusha.

Mamlaka ya Mapato TRA mkoa wa Arusha imetakiwa kuimarisha ukaguzi wa mashine za kielektroniki ili kuwabaini wafanyabiashara wanaokwepa kodi na kuikosesha serikali mapato ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua Kali za kisheria. 

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro amesema hayo wakati akizindua wiki ya mlipa kodi iliyofanyika eneo la stendi kuu ya Mabasi ya mikoani,ambapo ameitaka TRA kuhakikisha kuwa wanakagua na kuwabaini wafanyabiashara wasiotoa risiti na kuikosesha serikali mapato jambo ambalo ni uhujumu uchumi.

Aidha amewataka Wafanyabiashara kutoa taarifa za siri juu ya baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wanaokwepa kodi ili hatua Kali zichukuliwe juu yao.
Kaimu Meneja wa TRA mkoa wa Arusha Irine Donald amesema kuwa wataendelea kushirikiana n wafanyabiashara katika kutatua changamoto na kero zao ili waweze kufurahia kulipa kodi ya serikali.

Kwa upande wao wafanyabiashara Elisante Mungure na Winifrida Massawe Wafanyabiashara. wamelalamikia uwepo wa wamachinga mbele ya maduka yao huku wakiuza bidhaa zinazofanana hivyo kukosa soko la bidhaa zao.

Mfanyabiashara alia Mali zake kuzuiwa polisi

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud,Manyara

Mfanyabiashara ,Furaha Lazaro (52),amelilalamikia jeshi la Polisi Mkoani Manyara ,katika kituo kidogo cha Polisi ,Mererani wilayani Simanjro kwa kushikilia Mali zake za Dukani zenye thamani ya sh,mil.9 bila sababu za msingi kwa muda wa mwaka mmoja.

Akiongea na Vyombo vya habari Jana ,Lazaro ambaye ni Mkazi wa mji mdogo wa Marerani ,amelituhumu jeshi hilo kwa kushikilia Mali zake baada ya kumhisi anajihusisha kununua bidhaa ambazo ni zao la uhalifu jambo ambalo si kweli.

"Naendesha Duka langu kwa fedha za mkopo kama mjasiriamali mdogo sasa Polisi wanashikilia Mali zangu tangia mwaka jana bila sababu ya msingi ,nitalipa na nini mkopo "alilalamika mama huyo

Alifafanua kuwa septemba tisa,mwaka jana Polisi wa kituo cha Mererani,walivamia Duka lake na kukusanya bidhaa mbali mbali yakiwemo Magodoro 15,Jenereta,mitungi ya gesi,Sabufa,Ving'amuzi ,mataili na Rimu Magari na kuondoka navyo hadi kituo cha Polisi.

Kadhalika askari hao pia walimkamata mfanyabiashara huyo na kuondoka naye hadi kituo cha Polisi na kuwekwa mahabusu wakimtuhumu kununua na kuuza Mali za wizi.

Akiongeza kuwa akiwa mahabusu alikuwa kiteswa kwa kipigo na askari wa upelelezi wakimlazimisha kueleza Mali anazouza amekuwa akizipata wapi jambo ambalo alidai Mali hizo huzinunua kwa Wateja wake wanaomletea zikiwa na risiti ama barua kutoka kwa Afisa Mtendaji.

"Mimi ni mjasiriamali huwa nauza bidhaa chakafu kama Mabati ,Milango ,Mgodoro na huwa nanunua zikiwa na risiti ama barua kutokana kwa Mtendaji na si vya wizi kama ambavyo Polisi wanahisi" Alisema Mama huyo.

Alisema baada ya mateso na kipigo cha muda mrefu akiwa mahabusu askari hao waliamua kumfungulia kesi na kumpeleka mahakamani katika mahakamanya Mwanzo Wilayani simanjiro kwa kosa la kuhisiwa kuuza bidhaa za wizi ,hata hivyo kesi hiyo ilimalizika baada ya kukosekana ushahidi.

Baada ya kesi kumalizika alianza kufuatilia Mali zake kituo cha Polisi bila kurudishiwa huku Polisi wakiendelea kumzungusha wakidai kuwa bado wanaendelea kuchunguza wakisubiri watu kuja kutambua Mali walizoibiwa.

Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara,Agustino Senga alipohojiwa juu ya madai hayo alisema kuwa mama huyo bado anakesi nyingine mahakamani inayohusiana na Mali hizo.

"Huyo mama amekuwa akinunua vitu vya wizi na baadhi ya bidhaa zake tunazo na zipo kwenye mikono salama asubiri tukamilishe uchunguzi ,tunasubiri watu waje kutambua Mali zao walizoibiwa,tukikamilisha tutamrudishia" Alisema kamanda senga.

Hata hivyo alimtaka mama huyo kuwa mtulivu na kuacha kuhangaika kuandika barua ngazi mbalimbali za juu kwani pindi Polisi watakapojiridhisha hahusiki na tuhuma hizo atarejeshewa Mali zake.

WABUNGE WA BUNGE LA UGANDA WATEMBELEA BUNGE LA AFRIKA Inbox x

$
0
0
Wabunge wa Bunge la Uganda wametembelea Bunge la Afrika ‘Pan - African Parliament’ katika makao yake makuu Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini ili kujifunza namna bunge hilo linavyofanya kazi. 

Ujumbe huo wa wabunge nane kutoka Uganda ukiongozwa na Mheshimiwa,Ongalo Obote Kenneth umepokelewa leo Jumanne Mei,14 2019 na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele ambaye anatoka Tanzania,Kanda ya Mashariki ya Afrika.

Mhe. Kenneth alisema lengo la kufika katika Bunge la Afrika ambalo wabunge wake wanaendelea na Mkutano wa pili wa kawaida wa bunge la tano la tano ni kujifunza namna bunge hilo linavyofanya kazi.

“Tumefurahi kufika hapa kuona na kujifunza mambo kadha wa kadha kuhusu Bunge la Afrika, ikiwemo historia yake,muundo wake na namna wanavyoendesha shughuli zao na kuzungumzia masuala ya Afrika,kwa kweli bunge hili ni imara kupitia viongozi wake akiwemo,Mheshimiwa Masele ambaye ni kijana lakini ana uwezo mkubwa wa kuongoza taasisi hiyo kubwa Afrika”,alisema Mhe. Kenneth.

Kwa upande wake, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika, Mhe. Stephen Masele amewapongeza wabunge hao kwa kuona umuhimu wa kutembelea bunge hilo kujifunza kuhusu bunge na siasa za Afrika.

“Nimefurahi kupokea ujumbe wa wabunge wa bunge la Uganda wanaotoka katika kamati mbalimbali,mmejionea jinsi tunavyoendesha shughuli za bunge la Afrika,wamefahamu kuhusu historia ya bunge,historia ya Umoja wa Afrika (AU),ukombozi Afrika na mambo mengine”,alisema Mhe. Masele.

“Bunge la Afrika lina wabunge kutoka nchi mbalimbali barani Afrika,wenye tamaduni na lugha tofauti tofauti,ninaamini kwa siku zote mtakazokuwa hapa bungeni,mtafaidika vya kutosha kuhusu siasa za Afrika”,aliongeza Mhe. Masele.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akiwa ofisini kwake katika Makao Makuu ya Bunge la Afrika,Midrand,Johannesburg, Afrika Kusini akizungumza na Ujumbe wa wabunge kutoka Bunge la Uganda waliotembelea Bunge la Afrika leo Mei 14,2019. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog.
Kushoto ni Mhe. Masele akizungumza na Ujumbe wa wabunge kutoka Bunge la Uganda (kulia) waliotembelea Bunge la Afrika.
Wabunge wa Bunge la Uganda wakimsikiliza Mhe. Masele. 
Kiongozi wa Ujumbe huo wa wabunge kutoka Uganda Mhe. Ongalo Obote Kenneth akielezea lengo la ziara yao kutembelea Bunge la Afrika.
Picha ya pamoja,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele na wabunge wa bunge la Uganda.
Mbunge kutoka Uganda,Mhe. Mugoya Kyawa(kulia) akiteta jambo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe.Stephen Masele.Picha zote na Kadama Malunde- Malunde1 blog

SERIKALI KUVUTIA UWEKEZAJI KUPITIA SEKTA YA UTALII Inbox x

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha

Serikali imeeleza kuwa itatumia sekta ya utalii na watalii wanaokuja kutembelea nchini kushawishi uwekezaji mkubwa na kutangaza kufungua milango ya fursa ya uwekezaji nchini kwa lengo la kuinua uchumi na kuongeza fursa za ajira kwa vijana.

Hayo yameelezwa na Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Uwekezaji Angela Kairuki kwenye Kongamano la kuvutia wawekezaji lililofanyika Jijini hapa ambapo alibainisha mkakati huo wa serikali ya awamu ya tano kuongeza wigo mpana wa wawekezaji wakubwa kuvutiwa kuja kuwekeza nchini.

Amesema kuwa Tanzania itaendelea kupokea wageni wengi wanaokuja kwa ajili ya utalii na kuwatumia kutangaza fursa za utalii kama walivyofanya kwa wageni kutoka China ambao wapo nchini kwa siku nne kutembelea vivutio vya utalii ikiwemo Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro na Serengeti sanjari na Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara.

Amebainisha kuwa huu ni mkakati wa serikali ya awamu ya tano katika kupanua ushirikiano kwa lengo la kukuza biashara hususani ya madini na utalii kuongeza wigo wa mapato ya nchini na kutumia fursa ya rasilimali tulizojaaliwa

“Niombe ndugu zangu watanzania tuweze kuitangaza vizuri nchi yetu hususani nyinyi waandishi wa habari mmeona waandishi wenzenu kutoka China wanaitangaza nchi yetu hii itasaidia kuongeza watalii na kuitangaza Tanzania na rasilimali ilizonazo kwa manufaa ya sasa na baadae”

Awali akiongea kwenye kongamano hilo Naibu waziri wa nchi sera bunge ajira vijana na watu wenye ulemavu Anthony Mavunde ameishukuru wizara ya uwekezaji kwa kuja na mkakati huo wa kuongeza na kutangaza kuvutia uwekezaji nchini kwani anaona kupitia uwekezaji wataweza kupambana na changamoto ya mfumuko wa ongezeko la ajiri kwa vijana wanaomaliza vyuoni.

Amesema kuwa uwekezaji mkubwa utafungua fursa pana ya kuweza kuongeza wafanyakazi kwenye kada mbali mbali na sasa serikali kupitia watalii itafungua milango kwa wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza nchini kwani miongoni mwa watalii wengi wanaokuja wano fursa nzuri za kuwekeza nchini.

“Serikali inapenda wafanyakazi kutoka nje ya nchi kuja kufanyakazi nchini kwa kufuata sheria zilizopo na si kwamba inakataa wafanyakazi hao kwani wanaleta ujuzi mpya na kuongeza ufanisi kazini ila wafuate taratibu za kupata vibali tena sasa upatikanaji wake umeboreshwa”

Nae Mkurugenzi wa Taasisi ya uwekezaji nchini TIC Jofrey Mwambe amesema kuwa mpango wao ni kuweka mkakati wa kuongeza wawekezaji kuwekeza nchini na mkutano huo umeonyesha mafanikio makubwa kwa kampuni iliyowaleta wageni hao italeta wageni wengine mwaka huu takribani 10 elfu kutoka nchini China.

Amesema kuwa hiyo ni faida kwa watalii hao wanaokuja kutembelea vivutio vya utalii nasi tukaitumia nafasi hiyo kutangaza fursa za uwekezaji ikiwa ni mkakati wa kuongeza wigo wa uwekezaji nchini kusaidia kuinua pato la taifa.

Aidha kwa Mujibu wa Mkurugenzi wa taasisi ya sekta Binafsi Godfrey Simbeye amesema kuwa ujio wa wageni hao na wawekezaji kutoka taifa la China kwao ni faraja kwa ukuaji wa sekta binafsi kuongeza wigo wa pato la taifa na uchumi kwa ujumla.

Amesema uendeshaji wa uchumi ni muhimu sana kwani serikali ikiweka mazingira mazuri kwa kuvutia wawekezaji watanzania watapata mitaji kutokana na wawekezaji hao kuja kuweza ila serikali zao nazo ziliweka mazingira maziru ya kibiashara kwa wananchi wa mataifa hayo, “Tunaiomba serikali kuona umuhimu wa mazingira mazuri ya kuwekeza kwa wananchi wa Tanzania tunaishukuru serikali yetu ya awamu ya tano kuanza kuona umuhimu huo na kuiga mataifa kama ya wenzetu kutoka nje”

Wizara Ya Kilimo Yaapa Kusafisha Wala Rushwa Wote na Wanaokwamisha Kilimo Cha Tumbaku Urambo Tabora

$
0
0

Na, Editha Edward-Tabora

Waziri wa kilimo Mhe, Japhet Hasunga amezitaka bodi zote zilizopo chini ya Wizara yake kuanza kujitathimini kama zimeshindwa kuwaondolea kero ya Rushwa kwa Wakulima zijiondoe kabla ya mwezi wa saba mwaka huu

Kauli hiyo ameitoa akiwa Wilayani Urambo Mkoani Tabora wakati wa Ufunguzi wa soko la zao Tumbaku kitaifa huku akisema Wizara hiyo ina mpango wa Kusafisha watu wote ambao Wanaojihusisha na Rushwa na kukwamisha kilimo cha zao hilo

"Mwaka huu tunaanza mabadiliko makubwa ndani ya wizara ya kilimo ili Kusafisha watu waliozoea Rushwa wakafanye kazi sehemu nyingine siyo kilimo na niwaase bodi msiegemee upande wowote ule hakikisheni mnasimamia sheria"Amesema Hasunga

Mwenyekiti wa bodi ya Tumbaku nchini (TTB) Hassan Mwakasavi ameiomba Serikali kuhakikisha inawatafutia masoko ya zao hilo ili Wakulima walime kilimo cha zao hilo wakiwa na uhakika wa masoko yasiyo na Madeni na Usumbufu

"Ombi langu kwa viongozi itendeeni haki zao la Tumbaku ili Wananchi wanufaike na zao hili kwani ni zao zuri linalo stahimili ukame "Amesema Mwakasuvi

Aidha pamoja na kukabiliwa na Changamoto mbalimbali Katika uzalilishaji wa zao la Tumbaku bado linachangia pato la Taifa kwa kuingiza Fedha za kigeni zaidi ya dola za kimarekani Milioni 195.8 Katika msimu wa kilimo cha Mwaka jana.
Waziri wa kilimo Japhet Hasunga akisititiza jambo kwenye Ufunguzi wa Zao La Tumbaku Mkoani Tabora
Pichani ni Shehena ya zao la Tumbaku likiwa kwenye ghala

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA BUNGENI LEO

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki, Bungeni jijini Dodoma, Mei 14, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Tanzania Tunao Uwezo Mkubwa wa Kuzalisha Mifuko Mbadala - Makamba

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba akielezea mbele ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa katika kikao chao leo Jijini Dodoma. Waziri Makamba alisisitiza umuhimu wa ushirikiano baina ya viongozi wakati wa utekelezaji wa Operesheni ya Marufuku ya Matumizi ya Mifuko ya Plastiki nchini inayotarajiwa kuanza tarehe 1/6/2019.[/caption]

Na: Mwandishi Wetu

Tanzania inao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko mbadala ambayo itatosheleza kufanikisha azma yake ya kupiga marufuku biashara na matumizi ya mifuko ya plastiki.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, mhe. Januari Makamba wakati akizungumza na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa leo Jijini Dodoma.

Makamba amesema kuwa ni jambo la kushangaza kuona asilimia 100 ya mifuko ya karatasi inayotumika nchini Rwanda na asilimia hamsini nchini Kenya inazalishwa Tanzania huku Tanzania ikitumia zaidi ya asilimia 80 ya mifuko ya plastiki inayozalishwa nje ya nchi jambo linalokinzana na dhana ya kukuza uchumi wa viwanda. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba akielezea mbele ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa katika kikao chao leo Jijini Dodoma. Waziri Makamba alisisitiza umuhimu wa ushirikiano baina ya viongozi wakati wa utekelezaji wa Operesheni ya Marufuku ya Matumizi ya Mifuko ya Plastiki nchini inayotarajiwa kuanza tarehe 1/6/2019. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo akizungumza wakati wa kikako baina yake na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa katika kikao chao leo Jijini Dodoma

“ Tunao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko mbadala, wazalishaji wa mifuko hiyo wameithibitishia Serikali kuwa wanao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko hiyo ambapo Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi kimesema kitaongeza uzarishaji zaidi ya maratatu huku wawezkezaji zaidi ya 50 wakiwa wameagiza mashine za kuzalishia mifuko hiyo,”Alisema Waziri Makamba.

Makamba aliongeza kuwa nchi ya Tanzania inaweza kufanikiwa katika zoezi hili kwa kuwa inazalisha mifuko mbadala ya karatasi ambayo hutumiwa kwa kiasi kikubwa na nchi jirani za Rwanda huku kenya wakitumia asilimia kubwa ya mifuko kutoka Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi cha hapa nchini, Kenya ikitumia asilimia 50, jambo linalotoa tafsiri kuwa tunaouwezo wa kuzalisha mifuko mbadala itakayotosheleza,” Alisema Januari Makamba.

Waziri Makamba amesema kuwa wazalishaji wa mifuko mbadala wameithibitishia Serikali kuwa wanao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko hiyo ambapo Kiwanda cha Karatasi Mufindi kitaongeza uzalishaji zaidi ya mara tatu kinavyozalisha sasa huku wawekezaji zaidi ya 50 wakiwa wameagiza mashine kwa ajili ya kuzalishia mifuko hiyo. Baadhi ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba(hayupo pichani) alipokuwa akiwaeleza kuhusu utekelezaji wa Operesheni ya Marufuku ya Matumizi ya Mifuko ya Plastiki nchini inayotarajiwa kuanza tarehe 1/6/2019 Baadhi ya Watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba (hayupo pichani) alipokuwa akiwaeleza kuhusu utekelezaji wa Operesheni ya Marufuku ya Matumizi ya Mifuko ya Plastiki nchini inayotarajiwa kuanza tarehe 1/6/2019. (Na: Ofisi ya Makamu wa Rais)

Katika hatua nyingine Waziri Makamba alitumia fursa hiyo kutoa rai kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa kushirikiana kwa karibu na mamlaka zingine zitakazo husika katika zoezi la kutokomeza biashara na matumizi ya bidhaa za Plastiki zilizopigwa marufuku.

Akizungumzia marufuku hiyo Makamba amesema kuwa katika awamu ya kwanza marufuku hiyo inahusisha mifuko ya plastiki tu huku bidhaa zingine zinazotumia plastiki vifungashio vya plastiki kuendelea kutumika wakati utaratibu ukiendelea. Alizitaja bidhaa hizo kuwa ni bidhaa za chakula, kilimo na dawa.

Utekelezaji wa katazo hilo la matumizi ya bidhaa za plastiki nchini linafuatia utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyotoa tarehe 26, April, 2019 katika maadhimisho ya Muungano jijini Dodoma.

BEI ZA MCHELE SOKO LA BUGURUNI

$
0
0
 Bei za bidhaa mbalimbali katika soko Buguruni wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam,kamazinavyo onekana katika picha.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)

  Bei za mchele katika soko la Buguruni wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam  kama inavyo onekana katika picha.

Watakiwa kuhakikisha wanazingatia matumizi Bora ya ardhi

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud,Arusha

SERIKALI imewataka wafugaji na wakulima kuhakikisha kuwa wanazingatia matumizi bora ya ardhi,ikiwa ni pamoja na kuepukana na uharibifu wa mazingira unasababishwa na shughuli za kibinadamu kwa lengo ya kuepukana na tatizo la mabadiliko ya tabianchi.

Mkuu wa Wilaya ya simanjiro,Zephania Chaula,ameyasema hayo jana
alipokuwa akizungumza katika warsha ya siku mbili iliyofanyika jijini
hapa iliyolenga kuelimisha jamii juu ya athari za uharibifu wa
mazingira.

Amesema kuwa wakati umefika kwa jamii hususani ya wafugaji na
wakulima,kuhakikisha kuwa wanazingatia matumizi bora ya ardhi,ikiwa ni
pamoja na kulinda maliasili ya nchi hii kwa manufaa ya kizazi cha sasa
na cha baadaye.

“Nawashauri wafugaji kuhakikisha kuwa wanaboresha nyanda za
malisho,wafugaji wanatakiwa wawe na maeneo maalumu ya malisho  kwa
lengo la kuepukana na changamoto ya uharibifu wa mazingira,ikiwa ni
pamoja na kufuga mifugo michache kwa njia za kisasa na kuepukana na
tabia ya kuhamhama kwani inachangia uharibifu wa mazingira”alisema
Chaula.

Alitoa wito kwa wananchi kutumia nishati mbadala lengo likiwa ni
kuepukana na tabia ya ukataji miti ovyo kwa ajili ya kuni  na kutoa
wito kwa wananchi kuhakikisha kuwa wanajenga tabia ya kupanda miti
kabla ya kukata miti.

Kwa upande wake Meneja Msaidizi wa Mradi kwa kuboresha nyanda za
mifugo na wanyamapori,Kanda ya kaskazini,kutoka shirika la TNC,Lucas
Yamati,alisema kuwa warsha hiyo ya siku mbili inawashirikisha
wakurugenzi wa halimashauri,wazee wa kimila kutoka jamii ya
wafugaji,wananchi wanaoishi katika maeneo ya hifadhi za wanyamapori
pamoja na viongozi wa vijiji.

“Wengine ni wataalamu kutoka taasisi za utafiti wa
wanayamapori,mamlaka za usimamizi za wanyamapori viongozi wa serikali
na kwamba lengo la warsha hii ni kuweza kuwafanya wanajamii kuboresha
njanda za malisho,kuweka matumizi bora ya ardhi pamoja na haki za
akina mama na watoto katika katika suala zima la lishe na afya.

Amesema kuwa warsha hiyo inawaweka pamoja makundi hayo kwa lengo la
kujadili namna ya kukabilina na mabadiliko ya tabia nchi ikiwa ni
pamoja na kuwataka wakulima kuacha kulima kiholela pamoja na wafugaji
kuacha kufuga kiholela

Kwa upande wake Mjumbe  wa baraza la wanawake kutoka kata ya
Terrat,Wilayani Simanjiro, Nerikoki Charles  amesema kuwa anatarajia
kupitia warsha hiyo wao kama wafuagaji wataweza kufikia maisha bora na
wataepukana na mila potofu ikiwemo suala la mimba za utotoni na
ukeketaji.

Kadhalika aliiyomba Serikali na wadau mbalimbali kujitokeza kwa wingi
kuzisaidia jamii za kifugaji katika kuwajengea vituo vya afya kwani
wamekuwa wakitumia umbali mrefu kufuata huduma za afya ikiwemo baadhi yao kujifungulia njiani.

Viewing all 110167 articles
Browse latest View live




Latest Images