Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109591 articles
Browse latest View live

Ajali ya kufukiwa kwa kifusi yaua wachimbaji watatu Arusha


PROF. OLE GABRIEL AFURAHISHWA NA HOSPITALI YA RUFAA YA WANYAMA SUA

0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo Profesa. Elisante Ole Gabriel amefurahishwa na shughuli zinazofanywa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo hususan uwepo wa Hospitali ya Rufaa ya Wanyama.

Hospitali hiyo ni taasisi pekee nchini inayosaidia kutoa ushauri, tiba na chanjo kwa wanyama wa kufugwa na waporini ambao wamepewa rufaa kutoka katika Hospitali ndogo ndogo za wanyama, taasisi za serikali na binafsi ambazo huhifadhi na kuwatunza wanyama hao ambao hupatikana kisheria.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya siku moja chuoni hapo leo Aprili 23, 2019, Prof. Gabriel amesema alipata fursa ya kuzunguka nchi za Afrika Mashariki lakini hakuwahi kusikia uwepo wa Hospitali ya Rufaa ya Wanyama na hivyo kuwataka waandishi wa habari kwa kushirkiana na kitengo cha Mawasiliano na Masoko kuhakikisha Umma unafahamu kuhusu Hospitali hiyo kuwepo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.

“Nimefurahishwa na Hospitali ya Rufaa ya Wanyama hapa SUA ambayo ni kwa Tanzania nzima, ni vyema tukauhabarisha Umma kuhusu hili na ikibidi Waziri aweze kutembelea Hoapitali hii, kiukweli nimefurahishwa sana na mambo niliyoyaona hapa SUA na nashukuru ziara yangu hii sikukosea kuifanya hapa”. Alisema Prof. Gabriel.

Pia aliongeza kuwa SUA inaweza kuwa zaidi ya eneo la mafunzo kwani kuna utalii ndani yake ambapo aliwashauri watumishi wa Ndaki ya Tiba ya Wanyama na Sayansi za Afya kuanzisha programu ya Utalii ambapo watu wakija kufanya mafunzo ya tiba ya wanyama wapate kujionea mambo ya Utalii yaliyopo katika Ndaki hiyo na hata Ndaki nyingine. 

Aidha, Prof. Gabriel alipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya Hospitali hiyo na kujionea shughuli zinazofanywa ambapo alipata fursa ya kuona wanyama wakipatiwa tiba ikiwemo upasuaji wakiwa katika uangalizi wa madaktari maalum wa wanyama.

“Sikuwa najua kama paka anaweza akafanyiwa upasuaji na kukatwa mguu na bado akaendelea kuwa hai hivyo natoa wito kwa wananchi wote kutumia Hospitali hii kuleta wanyama wao ili waweze kupatiwa matibabu mbalimbali, mimi nimefanikiwa kuona paka aliyefanyiwa operesheni na kukatwa mguu pamoja na mbwa ambao wote wako katika hali nzuri”, alisema Prof. Gabriel.

Katibu Mkuu huyo pia alipata fursa ya kuzungumza na Menejimenti ya Chuo na kuwataka kuendelea kuzalisha wahitimu bora na kuwafanya kuwa ni wahitimu waliofundishwa kwa vitendo zaidi kuliko nadharia huku akishauri kuwa Chuo kitoe uelewa kwa wanafunzi kuwa sekta ya mifugo ni sekta inayoajiri zaidi ya asilimia 50 ya wataalam wa mifugo na kutambua kuwa ni vyema wajijengee hari ya kutaka kujiari ili nao waweze kuja kuajili wengine pia.

“Ili tumuenzi Rais wetu John Pombe Joseph Magufuli ambaye ameonyesha msukumo wa pekee ni vyema tuhakikishe wahitimu wetu wanakuwa na uelewa kwa vitendo na si nadharia tu ili kutatua changamoto za wanafunzi”, alishauri Prof. Gabriel.

Aliongeza kuwa chuo kinatakiwa kuongeza nguvu katika kutoa mafunzo ya biashara (Business knowledge) hususan katika upande wa tiba ya wanyama na Sayansi ya wanyama ili kuwapa wataalam ujuzi wa masuala ya biashara.

“Nina hakika tukiongeza mafunzo ya biashara kwa wataalam wetu itasaidia kupata wanafunzi wa tofauti sana ambao mara baada ya kumaliza Chuo wakienda mtaani hawatapwaya katika utendaji kutokana na taaluma waliyopewa kwani biashara ndio kila kitu”, aliongeza Prof. Gabriel.

Prof. Gabriel amesisitiza Chuo hicho kihakikishe kinawagusa wafugaji wa chini kwa kushirikiana na Wizara kuwapeleka wanafunzi kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo katika sehemu halisia za kujifunzia.
“Chuo kishirikiane na Wizara pamoja na Tamisemi kuandika barua ili kuomba Wilaya mbalimbali zikubali kuwapokea wanafunzi wetu na kuwapatia maradhi badala ya kuwaacha wanafunzi hao kwenda mahali ambapo hawatapata nafasi ya kujifunza kwa vitendo wakijaribu kukwepa gharama za kujihudumia wawapo katika mafunzo na hivyo kuangalia wapi wana jamaa ambao wanaweza kupata hifadhi”, alisisitiza.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chubunda alimshukuru Katibu Mkuu kwa ujio wake na mchango wa mawazo ambapo alisema kwa kiasi Chuo kimeshaanza kushughulikia baadhi ya masuala hususani kuwa na mahali halisia pa kujifunzia na hivyo kuanzisha mashamba darasa ya mazao ya kimkakati kwa ajili ya wanafunzi na jamii kwa ujumla.

 “Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Mgufuli kwa kuwekea mkazo uwezeshaji kwenye vyuo na hasa chuo chetu kwa miaka miwili iliyopita kuna mambo makubwa ambayo huko serikali ilikuwa kama imevisusa vyuo vyake na kubaki kama yatima na kusababisha kuchakaa kwa baadhi ya miundombinu ya kufundishia mfano chuo chetu tunategemea mashamba na karakana ambazo kwa sehemu kubwa zilichakaa. Kwa sasa serikali na menejimenti ya chuo imefanya juhudi ya kupata mashamba makubwa ya chuo yaani “Modal farms na tumepanda mazao yote ya kimkakati kama vile zabibu, korosho pamoja na chai” alisema Prof.Chibunda.

Aidha, katika kuimarisha utoaji wa elimu bora Chuo kimeboresha maeneo ya mifugo kama vile ngombe, samaki na maabara kwa lengo la wanafunzi kujifunzia kwa vitendo.

Mvua "iliyokwama" Tanzania hatimye yawasili Kenya....

0
0

Mvua iliyodaiwa kukwama Tanzania hatimaye imeanza kunyesha Kenya kwa kasi, huku wananchi wakiwa hawajajiandaa.

Wafanyabiashara waliokuwa wamepanga bidhaa zao pembezoni mwa barabara za jiji la Nairobi wameshindwa kufanya shughuli zao kutokana na mvua hizo.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la BBC, saa mbili kabla ya mvua hiyo kunyesha, idara ya hali ya hewa Kenya ilitangaza kuwa mvua itanyesha jijini Nairobi na maeneo mengine.

''Sikutarajia kwamba itanyesha na nilipokuwa nikiendelea na biashara yangu ilianza kunyesha  nikalazimika kutafuta hifadhi kwengineko,'' amesema mfanyabiashara mmoja nchini humo.

Wiki iliyopita naibu mkurugenzi wa idara hiyo, Bernad Chanzu alisema hakutakuwa na mvua msimu huu.

Wiki mbili zilizopita idara hiyo ilitangaza kuwa kiangazi kitaendelea mwisho wa mwezi huu huku mawingu ya mvua yakisalia Tanzania kutokana na kiwango cha chini cha upepo wa kusukuma mawingu hayo kuelekea Kaskazini mwa nchi hiyo.

Shangwe wakati Rais Museveni wa Uganda apokea Bombardier CRJ900 mbili za Uganda Airlines

0
0
 Rais wa Ugandam Yoweri Museveni leo amepokea ndege mbili za kwanza wakati nchi hiyo inapofufua Shirika lake la ndege la Uganda Airlines.

Kiongozi huyo alikuwa kwenye uwanja wa ndege wa Entebbe kupokea ndege hizo aina ya Bombardier CRJ900. Museveni alisema kamwe hatoruhusu shirika hilo linaloirejeshea nchini yake hadhi yake liangamie tena

 Rais wa Ugandam Yoweri Museveni leo na Mama Janeth Museveni wakipungia wakati wakiingia kuikagua moja ya ndege hizo
 Rais wa Ugandam Yoweri Museveni leo na Mama Janeth Museveni wakiwa ndani ya  moja ya ndege hizo 

TAARIFA KUTOKA MAMLAKA YA HALI YA HEWA KUHUSU HALI HALISI YA HEWA

WAGONJWA 15 AMBAO MISHIPA YA DAMU YA MOYO IMEZIBA KWA KIWANGO KIKUBWA KUPATA MATIBABU KATIKA KAMBI MAALUM YA KUZIBUA MISHIPA YA DAMU YA MOYO

0
0
Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mwenzao wa  Hospitali ya Meditrina ya nchini India wanafanya kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa  siku tatu ya kuzibua mishipa ya damu  ambayo imeziba kwa kiwango kikubwa (Chronic Total Occlusion) na hivyo kushindwa kupitisha damu vizuri.

Kambi hiyo ni maalum kwa ajili ya  kuwasaidia wagonjwa wenye matatizo hayo ambao bila ya kupata mtaalamu mwenye ujuzi wa hali ya juu wa kuzibua mishipa hiyo wangefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo.

Matibabu hayo yanafanyika kwa kutumia mtambo wa Cathlab ambapo mgonjwa anatobolewa tundu dogo katika paja ambalo linapitishwa vifaa maalum vya kuzibua mishipa ya damu ya moyo (Stent).

Katika kambi hiyo wataalamu wa afya wa JKCI watapata elimu ya jinsi ya kuzibua mishipa ya damu ya moyo ambayo imeziba kwa kiwango kikubwa.

Jumla ya wagonjwa 15 ambao mishipa yao ya damu mmoja hadi mitatu imeziba wanatarajiwa kutibiwa  katika kambi hiyo iliyoanza leo tarehe 23 hadi  25/4/2019. Hadi sasa wagonjwa watano wameshatibiwa na hali zao zinaendelea vizuri.

Imetolewa na:

Anna Nkinda
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete

Rais Magufuli ateua Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi Mkuu wa TASAC

RUKSA WANANCHI JIJI LA MBEYA KUWASILISHA KERO ZAO MBELE YA RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI-MWENYEKITI WA CCM MBEYA

0
0
Na EmanuelMadafa,Mbeya

MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbeya mjini Humphrey Nsomba, amesema ni ruksa wanachi wa jiji la Mbeya kuwasilisha kero zao mbele ya rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli ambaye anatarajia kuwa mgeni rasmi kwenye sikuku za mei mosi zitakazo kitaifa Jijini Mbeya .

 Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ujuo wa rais Magufuli jiji la Mbeya, Nsomba amesema kuwa  chama cha mapinduzi Mbeya mjini kimejipanga kikamilifu kumpokea kiongozi huyo mkubwa, kwani ujio wake utakuwa chachu ya maendeleo.

“Tumefurahi sana sisi kama Chama Wilaya ya Mbeya Mjini kuhusu ujio wa Mh Rais Katika Sherehe za Mei Mosi ambazo kitaifa zitafanyika  Jijini Mbeya,kwa Upendo huu ambao ametupa sisi wanambeya   tutajitokeza kwa wingi kwani tunahamu  kubwa ya kumuona na kusikia mambo mazuri kutoka kwake.”Mwenyekiti wa CCM  Wilaya ya Mbeya Mjini ,Afrey Msomba..

Amesema kitendo cha Rais Magufuli kukubali kuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo za Mei mosi ni heshima kubwa kwa Chama Cha Mapinduzi na Mkoa wa Mbeya kwa Ujumla.

Amesema Rais Magufuli ametoa kiasi cha Shilingi Bilioni 12 kwa ajili ya ujenzi wa barabara sita za Jiji la Mbeya pamoja kutoa Fedha za ujenzi wa Kituo cha Iyunga na Nzovwe hivyo wanakila sababu ya Kumshukuru.

Kufuatia hatua hiyo Mwenyekiti huyo wa Ccm Wilaya ya Mbeya mjini amewataka wakazi wa Jiji la Mbeya bila kujali itikadi ya vyama vyao kujitokeza kwa wingi katika sherehe hizo za Meimosi ambazo zitafanyika katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine Jijini hapa .

DR.GEODAVE KISAMBALE :WATANZANIA DUMISHENI AMANI MLIOPEWA

0
0


Na Woinde Shizza Michuzi TV , Arusha 

Watanzania wametakiwa kudumisha amani na upendo uliopo katika nchi yetu kwani ndio zawadi pekee tulioachiwa na mwenyezi mungu.

Hayo yamebainishwa na nabii mkuu Wa kanisa la Ngurumo ya upako Dr Geordave Kisambale jijini hapa wakati akiongea na waumini Wa kanisa hilo katika ibada ya Chuo cha unabii iliofanyika kosongo jiji hapa. 

Alisema kuwa watanzania tunayo amani ambayo tumezawadiwa na mungu ivyo niwajibu Wa kila MTU kuienzi ,kuidumisha pamoja na kuilinda.

"Unajua mungu anatupendelea sana Watanzania ametupa amani ya nchi yetu ,ametufanya tunaishi kwa upendo angalieni nchi zingine wanapigana kila siku ,kuna vita ndugu kwa ndugu hawapendani lakini sisi watanzania tunaishi kwa amani hivyo ni vyema amani hii tuliopewa tuilinde kama vile mboni ya jicho letu" alisema Geodave

Aidha aliwataka watanzania kutoruhusu mtu yeyote yule kuingilia amani yetu na kuivuruga kwani hii ni zawadi ya pekee tuliopewa na mwenyenzi mungu.

Pia alimtaka kila Mwananchi kupitia imani yake kuendelea kuombea nchi yetu ya Tanzania iendelee kuwa na amani pia aliwakumbusha kuwaeka viongozi wetu Wa kitaifa akiwepo Rais Wa Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania katika maombi kila siku ili mungu aendelee kuwaongoza na kuwapigania.

Aidha amewataka watanzania kutii Sheria za nchi bila vurugu, huku akisisitiza wanasiasa kutopandikiza Chuki miongoni mwa wananchi badala yake wawaunganishe na kuwafanya kitu kimoja.
Nabii Dr Geodave kisambale akihudumia waumini wake .

MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL 24,2019

IRINGA HAKUNA KIWANDA CHA KUTENGENEZA UUME BANDIA-DC KASESELA

0
0
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiongea na waandishi mbalimbali ofisini kwake juu ya kusambaa kwa habari ambayo ilitungwa na mtu mmoja.



NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

Siku chache baada ya kusambaa kwa picha zinazomuonesha Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiwa ameshika viungo bandia vya kiume na kuzua Taharuki katika jamii, Mkuu huyo wa Wilaya ametolea ufafanuzi.

Akizungumza na Wandishi wa habari ofisini kwake leo Kasesela amesema kuwa taarifa zilizosambaa mtandaoni juu ya uzalishaji wa viungo bandia vya kiume, zimeleta changamoto huku akiwataka wananchi kuondokana na dhana potofu za kuchukua habari za mitandaoni na kuupotosha umma.

“Naomba niendee kuwaomba radhi watanzania kwa ajili ya jambo ambalo lilileta taharuki kwenye mitandao ya kijamii hasa nchi ya jirani zetu hapo Kenya lilipokelewa tofauti na nilivyokuwa hapo awali” alisema Kasesela 

Kasesela aliwataka watanzania kuacha kufuatia mambo ya ajabu na kuyapa nafasi kwenye mitandao ya kijamii kuliko kupata mambo ya kujenga nchi na yenye tija.

“Jamni ile habari ilitungwa na ni habari ya hovyo sana kwa kuwa nililishwa habari ambayo mimi sijaisema kwenye chombo chochote kile kwenye vyombo vya habari hivyo hiyo habari ni ya kupuuza tu” alisema Kasesela

Kasesela amewashauri watanzania kuhakikisha wanafatilia taarifa zenye kuleta maendeleo na zenye kujenga katika jamii inayomzunguka.“Kwa sasa habari nyingi ambazo zinazungumzwa hivi sasa ni habari ambazo ni za hovyo hovyo mno ndio maana leo wamesema kuwa wilaya ya Iringa kuna kiwanda hicho kitu ambacho sio kweli” alisema Kasesela .

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela amelaani kitendo cha Dawson Kagine kusambaza taarifa zisizo za kweli na kuongeza kuwa mkoani Iringa kuna kiwanda cha kuzalisha vifaa vya elimu ya mapambano dhidi ya Ukimwi. 

PROF. GABRIEL AFURAHISHWA NA HOSPITALI YA RUFAA YA WANYAMA SUA

0
0

SUA, Morogoro

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo Profesa. Elisante Ole Gabriel amefurahishwa na shughuli zinazofanywa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo hususan uwepo wa Hospitali ya Rufaa ya Wanyama.

Hospitali hiyo ni taasisi pekee nchini inayosaidia kutoa ushauri, tiba na chanjo kwa wanyama wa kufugwa na waporini ambao wamepewa rufaa kutoka katika Hospitali ndogo ndogo za wanyama, taasisi za serikali na binafsi ambazo huhifadhi na kuwatunza wanyama hao ambao hupatikana kisheria.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya siku moja chuoni hapo leo Aprili 23, 2019, Prof. Gabriel amesema alipata fursa ya kuzunguka nchi za Afrika Mashariki lakini hakuwahi kusikia uwepo wa Hospitali ya Rufaa ya Wanyama na hivyo kuwataka waandishi wa habari kwa kushirkiana na kitengo cha Mawasiliano na Masoko kuhakikisha Umma unafahamu kuhusu Hospitali hiyo kuwepo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.

“Nimefurahishwa na Hospitali ya Rufaa ya Wanyama hapa SUA ambayo ni kwa Tanzania nzima, ni vyema tukauhabarisha Umma kuhusu hili na ikibidi Waziri aweze kutembelea Hoapitali hii, kiukweli nimefurahishwa sana na mambo niliyoyaona hapa SUA na nashukuru ziara yangu hii sikukosea kuifanya hapa”. Alisema Prof. Gabriel.

Pia aliongeza kuwa SUA inaweza kuwa zaidi ya eneo la mafunzo kwani kuna utalii ndani yake ambapo aliwashauri watumishi wa Ndaki ya Tiba ya Wanyama na Sayansi za Afya kuanzisha programu ya Utalii ambapo watu wakija kufanya mafunzo ya tiba ya wanyama wapate kujionea mambo ya Utalii yaliyopo katika Ndaki hiyo na hata Ndaki nyingine.

Aidha, Prof. Gabriel alipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya Hospitali hiyo na kujionea shughuli zinazofanywa ambapo alipata fursa ya kuona wanyama wakipatiwa tiba ikiwemo upasuaji wakiwa katika uangalizi wa madaktari maalum wa wanyama.

“Sikuwa najua kama paka anaweza akafanyiwa upasuaji na kukatwa mguu na bado akaendelea kuwa hai hivyo natoa wito kwa wananchi wote kutumia Hospitali hii kuleta wanyama wao ili waweze kupatiwa matibabu mbalimbali, mimi nimefanikiwa kuona paka aliyefanyiwa operesheni na kukatwa mguu pamoja na mbwa ambao wote wako katika hali nzuri”, alisema Prof. Gabriel.

Katibu Mkuu huyo pia alipata fursa ya kuzungumza na Menejimenti ya Chuo na kuwataka kuendelea kuzalisha wahitimu bora na kuwafanya kuwa ni wahitimu waliofundishwa kwa vitendo zaidi kuliko nadharia huku akishauri kuwa Chuo kitoe uelewa kwa wanafunzi kuwa sekta ya mifugo ni sekta inayoajiri zaidi ya asilimia 50 ya wataalam wa mifugo na kutambua kuwa ni vyema wajijengee hari ya kutaka kujiari ili nao waweze kuja kuajili wengine pia.

“Ili tumuenzi Rais wetu John Pombe Joseph Magufuli ambaye ameonyesha msukumo wa pekee ni vyema tuhakikishe wahitimu wetu wanakuwa na uelewa kwa vitendo na si nadharia tu ili kutatua changamoto za wanafunzi”, alishauri Prof. Gabriel.

Aliongeza kuwa chuo kinatakiwa kuongeza nguvu katika kutoa mafunzo ya biashara (Business knowledge) hususan katika upande wa tiba ya wanyama na Sayansi ya wanyama ili kuwapa wataalam ujuzi wa masuala ya biashara.

“Nina hakika tukiongeza mafunzo ya biashara kwa wataalam wetu itasaidia kupata wanafunzi wa tofauti sana ambao mara baada ya kumaliza Chuo wakienda mtaani hawatapwaya katika utendaji kutokana na taaluma waliyopewa kwani biashara ndio kila kitu”, aliongeza Prof. Gabriel.

Prof. Gabriel amesisitiza Chuo hicho kihakikishe kinawagusa wafugaji wa chini kwa kushirikiana na Wizara kuwapeleka wanafunzi kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo katika sehemu halisia za kujifunzia.

“Chuo kishirikiane na Wizara pamoja na Tamisemi kuandika barua ili kuomba Wilaya mbalimbali zikubali kuwapokea wanafunzi wetu na kuwapatia maradhi badala ya kuwaacha wanafunzi hao kwenda mahali ambapo hawatapata nafasi ya kujifunza kwa vitendo wakijaribu kukwepa gharama za kujihudumia wawapo katika mafunzo na hivyo kuangalia wapi wana jamaa ambao wanaweza kupata hifadhi”, alisisitiza.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chubunda alimshukuru Katibu Mkuu kwa ujio wake na mchango wa mawazo ambapo alisema kwa kiasi Chuo kimeshaanza kushughulikia baadhi ya masuala hususani kuwa na mahali halisia pa kujifunzia na hivyo kuanzisha mashamba darasa ya mazao ya kimkakati kwa ajili ya wanafunzi na jamii kwa ujumla.

“Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Mgufuli kwa kuwekea mkazo uwezeshaji kwenye vyuo na hasa chuo chetu kwa miaka miwili iliyopita kuna mambo makubwa ambayo huko serikali ilikuwa kama imevisusa vyuo vyake na kubaki kama yatima na kusababisha kuchakaa kwa baadhi ya miundombinu ya kufundishia mfano chuo chetu tunategemea mashamba na karakana ambazo kwa sehemu kubwa zilichakaa. Kwa sasa serikali na menejimenti ya chuo imefanya juhudi ya kupata mashamba makubwa ya chuo yaani “Modal farms na tumepanda mazao yote ya kimkakati kama vile zabibu, korosho pamoja na chai” alisema Prof.Chibunda.

Aidha, katika kuimarisha utoaji wa elimu bora Chuo kimeboresha maeneo ya mifugo kama vile ngombe, samaki na maabara kwa lengo la wanafunzi kujifunzia kwa vitendo.

AU WAANDAA MKAKATI WA SOKO HURU LA BIDHAA KWA NCHI ZA BARA HILO

0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha

Jumuiya ya Afrika (AU) ipo katika mkakati wa kukamilisha uwepo wa soko huru la bidhaa ambapo Kwa sasa ipo kwenye mchakato wa baadhi ya bidhaa kufunguliwa Kwa zaidi ya asilimia 90 ambapo Tanzania inatarajiwa kunufaika katika soko hilo.

Akizungumza katika kongamano lililowakutanisha wataalamu wa biashara kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika mwakilishi wa wizara ya viwanda na biashara Thomas Mcharo alisema kuwa nchi hizo wanachama wataweza kuchagua bidhaa ambazo zitaweza kufunguliwa baada ya mkataba kuanza kufanyakazi ambapo Tanzania ipo njiani kuridhia mkataba huo.

Alisema kuwa uwepo wa Tanzania katika kongamano hilo ni kuona na kuufahamu zaidi mtangamano huo hivyo wakati wowote kuweza kuingia ikiwa ni faida ya nchi kwani Sera ya viwanda inaendana na masoko ya bidhaa tutakazozalisha hapa nchini

"Unajua Sera ya serikali ya awamu ya Tano ni uchumi wa Kati wa viwanda na kongamano hili tunajadili mkataba wa kubadilishana biadha katika nchi za Afrika utaona faida Kwa nchi katika kukuza biashara za bidhaa zetu"

Kwa upande wake mwakilishi wa mwenyekiti wa meza ya majadiliano ya biashara kutoka umoja wa nchi za Afrika Alexander Rubanga alisema kuwa kuondoa tozo hizo zotasaidia kukuwa Kwa biashara katika mataifa ya Afrika.

Aliziomba nchi ambazo hazijaridhia mkataba huo kuona umuhimu wa kuwepo makubaliano kuhusu soko la pamoja la bidhaa litakalosaidi bara la Afrika kukua kiuchumi.

Awali mtaalamu wa majadiliano kutoka time ya umoja wa Afrika Dkt.Halima Noor Abdi alisema kuwa mpaka sasa ni nchi 52 zimekwisha weka sahihi ambapo nchi zingine bado zinaendelea na majadiliano kuhusiana na umoja huo.

Amesema kuwa faida kubwa ya kujiunga na mkataba huo wa mtangamano utaidia nchi moja kuweza kuzalisha bidhaa ambazo zitaweza kuuzwa kwenye nchi nyingine barani humo.

BALOZI SEIF AHIMIZA NIDHAMU MICHEZONI

0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi msaada wa seti za Jezi Mwenyekiti wa Timu ya Soka ya Muembe Ladu Omar Zubeir katika lengo la kuendeleza Michezo Nchini,Wa kwanza kutoka Kushoto ni Kocha wa Timu ya Soka ya Muembe Ladu Ramadhan Madundo na wa kwanza kutoka Kulia ni Katibu wa Timu hiyo Mohamed Mbarouk.
Mwenyekiti wa Timu ya Soka ya Muembe Ladu Omar Zubeir akimshukuru Balozi Seif kwa msaada huo wa Jeziutakaoleta faraja kwa Uongozi wa Klabu hiyo pamoja na Wachezaji wenyewe.


Balozi Seif Ali Iddi akisisitiza umuhimu wa kudumishwa nidhamu Michezoni ili wachezaji wajijengee heshima itakayowatanulia hatma njema kimichezo ikiwemo suala la ajira mara baada ya kukabidhi msaada wa Jezi.Picha na – OMPR – ZNZ.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema suala la nidhamu michezoni ni jambo la msingi linalomjengea sifa na mafanikio mazuri mchezaji katika maisha yake Kimichezo.

Amesema mchezaji anapofikia hatua ya kutegemewa na Viongozi pamoja na walimu wake kutokana na kipaji alichojaaliwa analazimika kulinda heshima hiyo ili imfikishe daraja analokusudia kufikia hasa suala la ajira.

Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar wakati akiukabidhi Msaada wa seti mbili za Jezi pamoja naahadi ya Mipira Minne kwa Timu ya Soka ya Muembe Ladu katika azma ya kuunga mkono jitihada za kuendeleza Sekta ya Michezo Nchini.

Alisema nidhamu ndio silaha pekee inayomfikisha kwenye mafanikio Mchezaji au mtu yoyote katika malengo yake akatolea mfano baadhi ya Wachezaji wa Tanzania ambao kwa sasa wanacheza mpira wa kilipwa katika Timu za Mataifa mbali mbali Duniani.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliupongeza Uongozi wa Timu ya Soka ya Muembe Ladu kwa jitihada unazochukuwa wa kuwaendeleza Vijana wao Kimichezo na kuweka Historia ya Timu hiyo katika medani ya Soka.

Akipokea Msaada huo Mwenyekiti wa Klabu ya Soka ya Muembe Ladu Omar Zubeir alimshukuru Balozi Seif kwa uamuzi wake wa kuisaidia Klabu hiyo msaada utakaoleta faraja kwao na hata wachezaji wenyewe.

Omar Zubeir alisema Timu ya Soka ya Muembe Ladu na Ujamaa zina Historia ndefu ya kuwa Timu Moja kipindi cha nyuma isiyosahaulika kwa wapenda soka Nchini kitendo ambacho Kizazi cha sasa kinapaswa kuifuatilia Historia hiyo.

Othman Khamis Ame & Rashida Abdi
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.

Kimbunga Kenneth: Mamlaka za Hali ya Hewa Msumbiji, Tanzania zatoa tathmini

0
0
Kumezuka hofu ya kimbunga kwenye upwa wa magharibi wa Bahari ya Hindi hususan katika nchi za Msumbiji na Tanzania.
Mtandao uliobobea kwenye masuala ya hali ya hewa wa AccuWeather wa nchini Marekani umeripoti kuwa mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa katika bahari ya Hindi huenda ukapelekea kutokea Kimbunga kitakachopewa jina la Kenneth.
Iwapo kimbunga hicho kitatokea, kinatazamiwa kuathiri maeneo ya kuanzia Lindi kusini mwa Tanzania mpaka Pemba kaskazini mwa Msumbiji.
Mtandao huo pia umebainisha kuwa mgandamizo huo wa baharini unaweza kupoteza makali na kimbunga kisitokee, ila badala yake mvua kubwa zinaweza kutokea na kuathiri maeneo hayo.
"Mvua kali zinazoweza kusababisha mafuriko na mmomonyoko wa udongo katika maeneo kama Masasi na Tunduru nchini Tanzania, pia Marrupu na Montepuez kwa upande wa Msumbiji," imeeleza taarifa ta AccuWeather.
Kusoma zaidi Bofya Hapa>>>>

Coppa Italia: Nafasi ya pekee kwa timu hizi kushinda Coppa Italia

0
0
Vigogo wa Serie A Juventus wameimiliki Coppa Italia kwa miaka kadhaa ya hivi karibuni na wameshinda mara nne mfululizo hadi msimu uliopita. Lakini baada ya kutolewa na Atalanta kwenye robo fainali, jambo moja liko wazi: Jina la Juventus halitaandikwa kwenye Kombe la Coppa Italia baada ya mchezo wa fainali Mei 15.

Usiku wa leo na kesho michezo ya pili ya nusu fainali itapigwa, timu zote zina nafasi baada ya michezo ya kwanza yote kuisha kwa sare. Lazio mara ya mwisho wameshinda taji hilo mwaka 2013, katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali walilazimishwa suluhu nyumbani dhidi ya AC Milan. Klabu hiyo ya jijini Rome imekuwa na matokeo dhaifu hata kwenye ligi msimu huu, na pengine Coppa Italia ndiyo tiketi yao ya kushiriki kwenye mashindano ya Ulaya msimu ujao.

Lakini ili kufanikisha hilo wanahitaji kuwafunga Milan walau goli moja usiku wa leo, ambapo wenyeji wao wamekuwa wagumu sana kuruhusu magoli. Golikipa wa timu ya taifa ya Italia Gianluigi Donnarumma na Pepe Reina – ambao wameshirikiana kulinda lango la Milan bado hawajaruhusu bao hata moja kwenye Coppa Italia, hii itawaongezea presha washambuliaji wa Lazio. Pia Lazio wanatakiwa kufikiria namna ya kumzuia mshambuliaji wa AC Milan Krzysztof Piątek, ambaye anaongoza kwa magoli kwenye shindano hilo akiwa na jumla ya mabao nane hadi sasa.

Kama mashabiki waliotazama mechi ya kwanza ya Lazio na Milan walinyimwa burudani ya magoli basi mchezo wa Fiorentina na Atalanta uliwapa burudani yote, timu hizo zilifungana jumla ya magoli sita. Aisee!! Fiorentina na Atalanta wote wana muda mrefu sana hawajashinda taji hilo, Fiorentina mara ya mwisho wameshinda mwaka 2001 wakati Atalanta wameshinda mara moja tu na ilikuwa mwaka 1963.

Atalanta ambao bado wanagombania nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao watakuwa na mchezo mwingine mwisho wa wiki. Beki wa Atalanta Andrea Masiello, ambaye alikuwa nje ya uwanja kwa mwezi mzima akiuguza majeraha alisema wataingia katika michezo yote wakitafuta ushindi. “Hatutaki kufanya mahesabu kabla ya mechi, kila mchezo tutauchukulia uzito na umuhimu wake kama ulivyo.

“Ni lazima tuendelee kufanya tulichofanya msimu huu, Tuna imani na utaratibu tuliojitengenezea kwani ndio ambao umetupatia matokeo,” aliwaambia waandishi wa habari.
Mchezo wa AC Milan vs Lazio utapigwa leo saa 3:45 Usiku na ule wa Atalanta vs Fiorentina utapigwa kesho Alhamisi saa 3:45 Usiku, zote zitakuwa MUBASHARA kupitia StarTimes World Football pekee katika kifurushi kilichoboreshwa cha UHURU kwa watumiaji wa Antenna na SMART kwa wateja wanaotumia dish.

RC Wangabo asisitiza kasi katika ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Sumbawanga

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo amemtaka Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kusimamia kwa karibu,  umakini na kuongeza kasi ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya sumbawanga baada ya kuona kusuasua kwa ujenzi huo tangu kuanza kwake tarehe 19 Januari, 2019 ambapo wananchi walijitokeza kuchimba misingi ya majengo saba ya hospitali hiyo.

Amesema kuwa muda mwingi umepita tangu kuanza kwa ujenzi huo na hadi sasa ilistahili uwe umefikia hatua ya lenta na matokeo yake bado ipo kwenye hatua ya jamvi pamoja na changamoto zilizokuwepo na kuongeza kuwa hali hiyo inawakatisha tamaa wananchi kwa kuona jengo halipandi tangu kuanza kushiriki kwao kwenye ujenzi huu na kutahadharisha kuwa kwa sasa hakuna sababu ya kusuasua katika ujenzi huo.

“Kuna haja kwa halmashauri kusimamia ujenzi huu kwa karibu kuanzia sasa hivi kasi iongezeke mara mbili hata tatu kwa ile iliyokuwepo kwasababu kuapanga matofali kwenda juu hata siku mbili ytatu unafika kwenye lenta lakini kutoka kule kwenye msingi kunahitaji uangalifu na kupanga vizuri zaidi, kwahiyo Mkurugenzi narudia tena simamia vizuri ujenzi wa hapa na kwa ukaribu zaidi,” Alisisitiza.

Ameyasema hayo alipotembelea eneo la ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Sumbawanga inayojengwa katika Kijiji cha Mtowisa, Kata ya Mtowisa, bonde la ziwa Rukwa na kuwataka mafunzi wote waliokabidhiwa kujenga majengo saba ya hospitali hiyo kuhakikisha wanafikia ngazi ya lenta ifikapo tarehe 10 Mei, 2019 na kuongeza kuwa asiyefikia hatua hiyo atawajibishwa.

Wakati akisoma taarifa ya ujenzi wa hospitali hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Fani Musa aliwashukuru wananchi kwa kujitolea kwao kwa kazi za songambele zilizookoa shilingi 18,600,200 ikijumuisha kazi za kuchimba misingi ya majengo na mtaro wa kupeleka maji eneo la ujenzi, kusogeza tofali na ujazaji wa kifusi kwenye majengo hayo.

“Kwa ujumla kazi inaenda vizuri kwa mujibu wa ratiba ya kazi na tunatarajia kuikamilisha kwa wakati kama ilivyoelekezwa. Halmashauri inahitaji ushirikiano wa viongozi wote uendelee kama sasa ili kufikia mafanikio na kukamilisha ujenzi huu wa hospitali kwa muda uliopangwa,”Alisema

Ili kukamilisha ujenzi wa majengo saba ya hospitali hiyo ambayo ni majengo ya Utawala, Kufulia, Dawa, OPD, Maabara, Mionzi na Wazazi ni matofali 84,000 yanahitaji ambapo hadi sasa matofali 70,666 yameshafyatuliwa huku shilingi milioni 496 zikiwa zimeshatumika.
 Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo (kulia) akihoji maswali juu ya namna matofali hayo yatakavyopangiliwa ikiwa kuna yanayotakiwa kulala na mengine kusimamishwa kwenye ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Sumbawanga unaoendelea katika bonde la ziwa Rukwa. Wa tatu toka kushoto ni Mkuu wa Wilaya hiyo Dkt. Khalfan Haule. 
 Mkuu wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo akijaribu ubora wa matofali yanayotumika katika ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Sumbawanga katika bonde la ziwa Rukwa. 
  Sehemu ya Jengo la Mionzi likiwa limeanza hatua ya kupandisha ukuta ili kufikia usawa wa lenta ifikapo tarehe 10 Mei, 2019. 
 Sehemu ya jengo la Utawala inayoendelea na ujenzi katika hospitali ya Wilaya ya Sumbawanga inayojengwa katika bonde la ziwa Rukwa.

UVCCM YAKANUSHA TUHUMA ZA KUMFUKUZISHA KAZI DAKTARI ARUSHA

0
0
Na Vero Ignatus
Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi ccm wilaya ya Arusha Mjini Saipulani Abdallah Ramsey amekanusha vikali taarifa zinazoenea kwenye mitandao ya kijamii kuwa CCM imemfukuza kazi mganga mfawidhi wa kituo cha Afya Ngarenaro.

Akizungumza na Vyombo vya habari jijini Arusha Ramsey amesema kuwa kilichofanywa na katibu wa itikadi na uenezi wa CCM kata ya Levolosi ni kusimamia utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Aidha alisema kuwa ipo mitandao ya kijamii iliyotoa taarifa hiyo na kusema ccm imemfukuza kazi daktari huku  swala hilo likizua mjadala kwa jamii nzima.

"Alichokifanya mwenezi ni kusimamia utekelezaji na ndio kazi yetu sisi kama chama tawala alifika katika kituo cha afya Ngarenaro na kukuta hakuna huduma na kumtafuta daktari ambaye hakuwapo pia katika eneo hilo ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma na malalamiko hapo mengi tu na sio kiki za kisiasa muelewe hivyo" alisema Ramsey

Hata hivyo mwenyekiti huyo alisema kuwa ccm haimfukuzi mtu kazi Bali kusimamia mienendo mizima ya uwajibikaji na watanzania wanapata huduma. Alisema kuwa wanashangaa namna ambavyo mjadala huo unakuwa makubwa wakati kazi yao ni kuhoji wataalamu.

Itakumbukwa kuwa ipo video clip ambayo inasambaa mitandaoni kumuonesha katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho akiwasiliana na mganga mfawidhi wa kituo hicho akimtaka kufika kituoni hapo,na mganga huyo kudai kuwa hawezi kufika yupo mbali shambani ambapo tukio hilo pia limesababisha mkurugenzi wa jiji la Arusha Daktari Maulid Madeni kumvua nafasi hiyo na kubaki kuwa daktari wa kawaida.
Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Arusha Mjini Saipulani Abdallah Ramsey .

Jukwaa la kujenga ujuzi kwa wateja wa benki ya Stanbic Tanzania

0
0
 Mtaalamu wa Uchumi kutoka Stanbic Bank, Jibran Quereishi akizungumza katika jukwaa la kujenga ujuzi kwa wateja lilioandaliwa na benki hiyo, kwa ajili ya kuwaonyesha wateja wake fursa mbali mbali zilizopo katika kilimo cha biashara pamoja na utalii, hivi karibuni mkoani Arusha. Benki ya Stanbic iliandaa jukwaa hilo ili kutekeleza ahadi ya kuwasaidia wateja wake kufikia mafanikio yao ya kifedha kwa kupitia fursa mbali mbali zilizopo katika sekta husika.

Akatwa Sehemu Za Siri Na Mpenzi Wake Kwa Kutompa Fedha Ya Sikukuu

0
0
Na, Editha Edward-Tabora

Mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Bilali Khamis (61) mkazi wa Mtaa wa Ushirika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora amekatwa sehemu zake za siri na Mpenzi wake Veronica Ngayawula baada ya Kutompa fedha ya sikukuu ya Pasaka hali iliyopelekea kufanyiwa ukatili huo wa kijinsia

Tukio hili la kikatili limetokea majira ya saa saba usiku wa kuamkia tarehe 22 mwaka huu nyumbani kwa Bilali Khamis 

Juma Maswezi ambaye ni ndugu wa Bilali ameiambia Michuzi Blog kuwa kitendo alichofanyiwa ndugu yake siyo kitu kizuri kwani ni uzalilishaji ulio kinyume na haki za binadamu

George Mgalega ni Mganga Mkuu mfawidhi Hospitali ya Wilaya amesema kuwa amekili kumpokea mgonjwa huyo
"Baada ya kumfanyia uchunguzi tumegundua kwamba ametendewa kitendo hicho kwa kutumia kitu ncha kali kwa hiyo afya yake itachukua muda mrefu sana kuimalika maana  kidonda hiki kimekaa wazi kwa muda mrefu"amesema Mgalega 

Hata hivyo kwa matibabu    na uchunguzi zaidi mzee Bilali amepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Nkiga Igunga huku Mpenzi wake Veronica  Ngayawula akiwa ametokomea kusiko julikana.
Viewing all 109591 articles
Browse latest View live




Latest Images