Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109572 articles
Browse latest View live

NEWS ALERT: Paul Walker dead at 40: 'Fast and Furious' star killed in fiery car crash

0
0
The star of "The Fast and the Furious" movie franchise and a friend identified as Roger Rodas died in Southern California after the Porsche they were in crashed, his rep confirmed to the Daily News. Police said speed was a factor. Walker was attending a charity event in Santa Clarita, about 30 miles north of Los Angeles, when the accident happened. 

Paul Walker, 40, died in a car accident in California on Saturday afternoon. Here, Walker attends the "Fast & Furious 6" world premiere in London, England, on May 7. 

Actor Paul Walker — a self-styled adrenaline junkie best known for his role in “The Fast and the Furious” movies — was killed Saturday in a fiery single-car wreck in Southern California.

The 40-year-old Walker was riding in a red Porsche GT about 3:30 p.m. when the sports car flew off the road and slammed into a tree in Santa Clarita, authorities and witnesses said. The car burst into flames.

Click here to Read more 

KUSAINIWA KWA MIRADI MIKUBWA MITATU YA UJENZI WA BARABARA KWA KIWANGO CHA LAMI ITAKAYOJENGWA KATIKA MIKOA YA DODOMA, MANYARA NA MTWARA

0
0
Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mnamo siku ya Jumatatu ya tarehe 02 Desemba 2013 utasaini mikataba mitatu ya barabara zitakazojengwa kwa kiwango cha lami katika mikoa ya Dodoma, Manyara na Mtwara.

Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli atakuwa Mgeni Rasmi katika hafla hiyo ya kusainiwa kwa mikataba ya ujenzi wa miradi hiyo mitatu mikubwa ambayo utekelezaji wake umekuwa ukisubiriwa kwa hamu.

Miradi itakayohusika ni:
i.    Mayamaya – Mela (km 99.35)
ii.    Mela- Bonga (km 88.8)

Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Mayamaya hadi Bonga yenye urefu wa kilometa km 188.15 umegawanywa katika sehemu mbili ambazo zitakuwa na mikataba miwili tofauti inayojitegemea. Mikataba hiyo itajumuisha ujenzi wa sehemu ya Mayamaya – Mela (km 99.35) na Mela – Bonga (km 88.8).

Kujengwa kwa sehemu hii kati ya Mayamaya na Bonga katika mikoa ya Dodoma na Manyara kutakamilisha barabara ya lami inayounganisha miji ya Dodoma na Babati kwa upande wa mkoa wa Manyara. Sehemu kati ya Dodoma – Mayamaya (km 43.6) ujenzi wake unaendelea kwa kiwango cha lami na kuanzia Babati hadi Bonga (km 19.2) tayari imekwishakamilika.

iii.    Mangaka – Mtambaswala(km 65.5)

Kipande cha barabara kati ya Mangaka hadi Mtambaswala (km 65.5) mkoani Mtwara ni sehemu ya barabara inayoanzia Masasi hadi Mtambaswala (km 120.6) ambako kuna Daraja la Umoja linaounganisha nchi yetu na Msumbiji. Tayari sehemu ya kati ya Masasi na Mangaka (km 55.1) imekwishajengwa kwa kiwango cha lami na hivyo kusainiwa kwa sehemu hii ya Mangaka hadi Mtambaswala kutaifanya barabara hiyo yote kukamilika kwa kiwango cha lami.

Hafla ya kusaini mikataba hiyo mitatu itafanyikia Protea Court Yard Hotel, Ocean road, Upanga jijini Dar es Salaam kuanzia saa 4:00 asubuhi.

KCB BANK YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WAJASIRIAMALI

0
0
 Kaimu Mkuu wa masoko ya rejareja wa KCB Bank, Juma Abdul akizungumzia huduma za benki hiyo kwenye semina ya siku moja ya ujasiriamali iliyoandaliwa na benki ya KCB tawi la Zanzibar kwenye hoteli ya Grand Palace mjini Zanzibar 
 Meneja wa Tawi, KCB bank Zanzibar, Cosmas Mwankemwa akizungumza na washiriki wa  wa semina ya ujasiriamali iliyoandaliwa na benki hiyo kwenye hoteli ya Grand Palace mjini Zanzibar.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHEREHESHA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI MNAZI MMOJA DAR ES SALAAM, LEO.

0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi Mpango Mkakati wa 3 wa Kitaifa wa Kudhibiti Ukimwi (NMSF3), wakati wa sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashid, (wa pili kulia) ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mwantum Mahiza, Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya kudhibiti Ukimwi Tanzania, Dkt. Fatma Mrisho
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi moja kati ya Vitabu vya Mkakati wa 3 wa Kitaifa wa Kudhibiti Ukimwi (NMSF3), Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Alhad Mussa, baada ya ya kuzindua mpango mkakati huo wakati wa sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani, zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo.

mchekeshaji Eric Omondi toka kenya atua dar leo, kuburudisha leo usiku Golden tulip hotel

0
0
 Mchekeshaji Eric Omondi toka Kenya akiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mchana huu tayari kuvunja mbavu wadau kwenye onesho la kufunga mwaka la Vuvuzela Entertainment linaloanza saa moja leo hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam
 Mchekeshaji Evans Bukuku akimpokea Eric Omondi toka Kenya alipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mchana huu tayari kuvunja mbavu wadau kwenye onesho la kufunga mwaka la Vuvuzela Entertainment linaloanza saa moja leo hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam
 Evans: Dah!  Jamaa kumbe shotiiii
Eric: Dah!v Madhee kumbe mtoliiii 
Wakila pozi kabla ya kukwea Bajaji kuelekea Uchumi Supermarket iliyoko Quality Centre kununua makubazi maana alisahau kubeba
 Wadau wa Uchumi wakimhudumia Eric
 Eric na Evans wanaonesha kadi ya Uchumi Supermarket
 Eric akisonga ugali. Kumbe alikuwa hajala...
HEMBU CHEKI VIBWEKA VYA ERIC OMONDI JUKWAANI HAPA CHINI.....

Article 12

Kilimanjaro Stars yaibamiza Somalia bao 1-0 leo

0
0
 Hii ni timu ya kilimanjaro Stars wakiwa katika Picha ya pamoja Kabla ya mchezo huo kuanza jijini Nairobi. Mashindano ya CECAFA  Senior Challenge Cup 2013 yanaendelea hapa Kenya NA Kilimanjaro Stars Leo 1/12/2013 wamecheza na timu ya  Taifa ya Somalia na  kuifunga bao 1-0.
 Mpira ukiwa Kati Mara baada ya Kilimanjaro Stars kufunga goli hilo
Katika mchezo Huo Bwana innocent Shiyo mwenye tai nyekundu alimuwakilisha Mh, BALOZI Batilda Burian. Kulia ni BALOZI wa Somali nchini Kenya.

Kambi ya siku tatu ya huduma za meno bure Zanzibar yatangazwa

0
0
 MRATIBU wa Kambi ya siku tatu ya huduma za meno bure zitazotolewa Zanzibar kuanzia disemba 5-7, Ali Jivraji (katikati) akitoa maelezo ya Kambi hiyo kwa Waandishi wa Habari wa vyombo mbali mbali (hawapo pichani) katika Hoteli ya Beit al Salaam iliyopo Shangani mjini Zanzibar, kulia Mkurugenzi  mauzo wa Hoteli ya Doubletree ya Dar es Salaam, Florenso Kirambata ambao ni wadhamini wa kambi hiyo na Mkurugenzi wa Zanzibar Help Foundation Dk. Feroz Jafferji.(
MKURUGENZI Mauzo wa Hoteli ya Doubletree ya Dar es Salaam, Florenso Kirambata ambao ni wadhamini wa kambi ya siku tatu ya huduma za meno bure inayotegemewa kuanza tarehe 5-7 mwezi huu akitoa ufafanuzi kwa Waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wakiitangaza kambi hiyo, kulia kwake Mratibu wa kambi hiyo,  Ali Jivraji na Mkurugenzi wa Zanzibar Help Foundation, Dk. Feroz Jafferji. Mkutano huo ulifanyika katika Hoteli ya Beit al Salaam iliyopo Shangani mjini Zanzibar.
Picha zote na Haroub Hussein).


Profesa Mwandosya amjulia hali Father Mwang'amba hospitalini India alikolazwa naye

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Prof Mark Mwandosya akimjulia hali Father Joseph Mwan'gamba aliyemwagiwa tindikali Zanzibar,  wote  wawili wakiwa wamelazwa  Apollo Hospital, Hyderabad, India

Bodi ya Chakula, dawa na vipodozi Zanzibar yateketeza bidhaa zilizoisha muda wake

0
0
WAFANYAKAZI wa Bodi ya Chakula, dawa na vipodozi Zanzibar (ZFDB) wakiwa katika harakati za kuangamiza vyakula vilivyomaliza muda wake wa matumizi pamoja na dawa zilizokua hazina kiwango kwa matumizi ya Binaadamu vilivyokamatwa katika maduka mbali mbali pamoja na vingene katika bandari ya Zanzibar vikiingizwa Nchini. Vyenye zaidi ya tani 40 viliangamizwa katika eneo la Kibele Wilaya ya Kati Unguja.(Picha na Haroub Hussein).

HALI YA MVUA ZANZIBAR LEO

0
0
 KUFUATIA mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo mbali mbali ya mji wa Zanzibar leo asubuhi Barabara nyingi zimejaa maji na kusababisha watumiaji kupata usumbufu kutokana na wasi wasi wa kuharibika kwa njia hizo pichani gari zikipita kwa tabu katika eneo la Mwanakwerekwe .(Picha na Haroub Hussein).
 Mabwawa kila pahala
 Hali ya mvua katika maeneo ya Jang'ombe Unguja leo.
 Maji kila kona
Biashara nyingi zimesimama

DK.Shein Mgeni Rasmi Kilele cha Siku ya Ukimwi, Paje.

0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akivalishwa (Redreben) alama maalum ya Ukimwi,na Zainab Khamis, Mhamasishaji Tume ya Ukimwi Zanzibar,wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika Paje Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja, ambapo kila ifikapo tarehe 1 Disemba
hufanyika maadhimisho
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji,alipokuwa akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kushoto),kuzungumza na wananchi wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani yaliyoafnyika leo katika Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) alipokuwa akizungumza na wananchi wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi Duniani yaliyoafnyika leo katika Kijiji cha Paje,Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja,(kushoto)  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji, na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja,Dk.Idrisa Muslim Hija
Baadhi ya wananchi walioalikwa katika hafla ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi,wakisoma majarida yaliyotolewa katika maadhimisho hayo  yaliyofanyika Paje Wilaya ya Kusini,Mkoa wa Kusini Unguja,mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, Picha  na Ramadhan Othman,Ikulu.

News alert: watu wanne wapoteza maisha, 63 wajeruhiwa katika ajali ya treni ya abiria New York Leo

0
0
Watu wane wamekufa na wengine 63 kujeruhiwa baada ya Treni ya abiria kuacha reli na kupinduka katika sehemu yenye kona kali maeneo ya Bronx jijini New York, Marekani, mamlaka zimeeeleza.
Gavana Cuomo amesema marehemu watatu wamekutwa nje ya treni na mmoja ndani yake, Hakutaja majina kwa kuwa familia zao bado kujulishwa, na kwamba majeruhi 11 wako mahututi, akiwemo dereva wa treni hilo.
Msemaji wa Metropolitan Transportation Authority, Bi Marjorie Anders amesema sehemu hiyo yenye kona kali iko katika eneo la mwendo mdogo, na kwamba kifaa cha mawasiliano kijulikanacho kama  black box kitafafanua treni hio ilikuwa inasafiri kwa mwendo gani.
Ripota wa Globu ya Jamii aliyekuwa eneo la tukio anafuatilia kujua kama kuna Mtanzania aliyehusika katika ajali hiyo, ikizingatiwa kwamba New York kuna Watanzania wengi wanaoishi jijini humo.


Msama atoa msaada wa magodoro kituo cha watoto yatima Luhila Pachane,songea mkoani Ruvuma

0
0

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Msama Promotions,Alex Msama(kulia) akikabidhi msaada wa Magodoro kwa Sheikh Abdushakur Omary, kwaajili ya kituo cha Luhila Pachane,kilichoko Songea  mjini,kinacholea  Watoto  Yatima na wanaoishi katika mazingira magumu, Sheikh Abdushakur,ni mlezi wa kituo hicho,pia ni Katibu wa Bakwata Mkoa wa Ruvuma. 
 =======  =====  ======
Na Mussa Mkama
MKURUGENZI Mtendaji wa Msama Promitions Alex Msama amekabidhi msaada wa magodoro yenye dhamani ya zaidi ya Shilingi milioni 4 kwa kituo cha watoto yatima Luhila Pachane kilichopo Songea Mkoani Ruvuma.
 
Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya ofisi za Msama Promotions Kinondoni Jijini Dar es Salaam jana Msama alisema msaada huo umetoka kwenye mfuko wa Tamasha la Krismas ambalo linatarajiwa kuanza Desemba 25 jijini hapa na mikoa mingine.
Tamasha hilo la Krismas linatarajia kufanyika katika mikoa mitano, ambapo ni Dar es Salaam, Morogoro, Tanga, Arusha na Dodoma.
 
Msama alisema kuwa kutokana na maombi ya kituo hicho na kuguswa na hali waliyokuwa nayo ya yatima hao kulala katika mkeka, aliamua kunyofoa sehemu ya fedha zilizokuwa kwenye mfuko wa Tamasha la Krismas na kuamuo kuwasaidi watoto hao ili nao waweze kujisikia wapo katika jamii ya Watanzania.
 
“Nimeamua kufanya hivyo kutokana na kuguswa na hali halisi waliyonayo yatima hao wa kituo cha Luhila Pachane huko mkoani Ruvuma nikaamua kunyofoa fedha katika mfuko wa Tamasha la Krismas kwa ajili ya kuwasaidi ili nao wajisikie wako pamoja na Watanzania wenzao” alisema Msama na kuongeza kuwa;
 
“Msaada huo wa magodoro hayo ni zaidi ya shilingi milioni 4, hivyo ninaimani kubwa sasa kwa msaada huu yatima wataniombea kwa Mungu ili Tamasha la Krismas liwe la mafanikio kwani lengo la tamasha hilo ni kuweza kujenga kituo cha kisasa cha watoto yatima na wasiojiweza kwani kiwanja tumeshakiona kipo pale maeneo ya barabara ya Pugu Jijini Dar es Salaam.
 
Akizungumza baada ya kukabidhiwa msaada huo Mlezi wa kituo hicho ambaye pia ni Katibu wa Bakwata mkoa wa Ruvuma Shekh Abdushakur Omary alisema anamshukuru Msama kwa wema wake aliouonyesha wa kusaidia jamii ya Watanzania wote bila kubagua dini, kabila wala rangi.
 
“Msama ni mtu wa aina yake hana ubaguzi anashughulikia maombi ya Watanzania wote bila kuangalia dini, kabila, rangi wala utaifa wake kwani amaamini kuwa wote ni wamoja, hivyo naomba nizidi kumuombea aendelee kuwa na moyo huo wa kujitolea kwa ajili ya watu wa taifa lake wasiyojiweza” alisema Omary.
 
Hata hivyo aliomba Wizara husika kuharakisha upatikanaji wa hati ya kiwanja kile kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kisasa cha kutolea misaada (Center)  pamoja na kiwanda cha kisasa cha kuzalishia kazi za wasanii  kwa manufaa ya Taifa na watu wake, kwani kwa kufanya hivyo itakuwa imesaidia Watanzania wengi wenye ndoto ya kuwa wasanii wakubwa nchini.
 
“Uwepo wa Msama katika ulimwengu huu kunamuwakilisha Mwenye Mungu, kwani Mungu si mbaguzi kwa watu wake anawapenda wote na anatoa sawa kwa kila mtu, hivyo ndivyo alivyo Msama, kwa moyo mmoja namuombea yeye na taasisi yake isiyokuwa na ubaguzi wa dini kuendelea 
 
kuwa hivyo wakati wote” alisema Omari na kuongeza kuwa;
“Naomba Wizara au Waziri husika kuona umuhimu wa ujenzi wa kituo hicho cha kisasa cha kutolea misaada pamoja na kiwanda cha kuzalishia kazi za wasanii, kwani wapo Watanzania wengi wenye vipaji lakini hushindwa kufanya kazi za kisanii kutokana na viwanda kuwa na gharama kubwa wasizoweza kuzimudu”
 

KINANA NA UJUMBE WAKE AMALIZA ZIARA YAKE WILAYANI CHUNYA,KESHO KUUNGURUMA MBARALI.

0
0
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwahutubia Wananchi na Wanachama wa Kijiji cha Udinde  Mkwajuni mapema leo jioni,Wilayani Chunya mkoani Mbeya,Kinana aliwahimiza wananchi hao kufanya kazi kwa bidii na kujituma katika suala zima la kujiendelea maendeleo yao,alieleza kuwa Serikali haiwezi kumpa ajira kila mtu,isipokuwa inasaidia kwa namna moja ama nyingine kuongeza nguvu katika suala zima la kimaendeleo,hivyo amewataka vijana kutobweteka na kusubiri ajira kutoka serikalini na badala yake wajitume kujikwamua na lindi la umaskini.Ndugu Kinana akiwa sambamba na  ujumbe wake,Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi Nape Nnauye pamoja na Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt Asharose Migiro,wamemaliza ziara yao leo Wilayani Chunya na kesho wanaelekea wilaya Mbarali mkoani Mbeya.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na ujumbe wake wakielezwa jambo namna mradi huo wa maji unavyowasaidia wafugaji wa kabila la Wasukuma.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akimtwisha ndoo ya maji mkazi wa kijiji cha Mteka,Bi.Gegwa Luhende mara baada ya mradi huo kuzinduliwa rasmi,Wakazi wa kijiji hicho ambao ni wafugaji walikuwa na shida kubwa ya upatikanaji wa maji,kufuatia kilio hicho cha Muda mrefu serikali iliamua kuwajengea kisima kama kionekanavyo pichani.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akioneshwa sehemu ya kunyweshea mifugo ya wafugaji hao wa Kisukuma ndani ya kijiji cha Mteka,Kata ya Kapalala,Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana pamoja na  Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt.Asharose Migiro kwa pamoja wakishiriki ujenzi wa bweni la wanafunzi katika shule ya sekondari ya Kapalala kata ya Kapalala,ambalo limejengwa na Wakulima wa Tumbaku kupitia taasisi ya Chunya Development Trust.
Pichani kulia ni Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt.Asharose Migiro akishiriki kufurahia jambo na wanakijiji cha Iudinde,Mkwajuni mapema leo wakati katibbu mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipokuwa akizungumza nao.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na baadhi ya Wanachama na Wananchi wa Mwambani kata ya Mwambani mara baada ya kushiriki ujenzi wa Soko la Mulugo Market Mwambani,Soko hilo linajengwa na Mbunge wa jimbo la Songwe na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Mh Phillip Mulugo katika suala zima la kuwakomboa wananchi wake kuondokana na umaskini na kulifanya jimbo hilo lizidi kufanya vyema katika masuala mazima ya ukuaji wa Uchumi.Ndugu Kinana akiwa sambamba na  ujumbe wake,Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi Nape Nnauye pamoja na Katibu wa NECSiasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt Asharose Migiro,wamemaliza ziara yao leo Wilayani Chunya na kesho wanaelekea wilaya Mbarali mkoani Mbeya. Kwa habari na picha zaidi BOFYA HAPA

Article 2

WAFANYAKAZI TBL WASHIRIKI UPIMAJI VIRUSI VYA UKIMWI

0
0
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=142aab752dcc0483&attid=0.2&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P90fuF_-XHOSL6iwje353GN&sadet=1385875932310&sads=Vc0ZF7B53Mozcht61SknwuXmzBY
Muuguzi Mshauri wa kupima maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, Bi. Aulelia Kunambi, akimpima Meneja Raslimali Watu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bw. David Mafuru (kulia), wakati wa zoezi maalumu la kupima Ukimwi kwa hiari kwa wafanyakazi wa Kampuni hiyo, Dar es Salaam.
 https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=142aab752dcc0483&attid=0.3&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P90fuF_-XHOSL6iwje353GN&sadet=1385875980692&sads=neRd3JHhnec9MsnJwgvRXKZzKIU
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bi. Tereza Mbando
 (katikati), akiwasha mshumaa kuzindua zoezi la kupima virusi vya ukimwi kwa hiari kwa wafanyakazi wa Kampuni ya 
Bia Tanzania (TBL), Dar es Salaam kuadhimisha siku ya Ukimwi duniani. Kulia ni Meneja Raslimali watu wa kampuni hiyo, Bw. David Mafuru.
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=142aab752dcc0483&attid=0.4&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P90fuF_-XHOSL6iwje353GN&sadet=1385876009639&sads=25ZHTW_4EXMsfnvw0VNb3omaaT8 
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=142aab752dcc0483&attid=0.5&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P90fuF_-XHOSL6iwje353GN&sadet=1385876031448&sads=tx0ZtOz4uRfXlhpjE_2co63_JVc
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), 
wakiwasha mishumaa baada ya kushiriki katika zoezi la kupima ukimwi kwa hiari, wakati wakiadhimisha siku ya Ukimwi Duniani.
 
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=142aab752dcc0483&attid=0.6&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P90fuF_-XHOSL6iwje353GN&sadet=1385876200263&sads=PqpcJkhLCoDHJcSL5txvE7PpVqQ
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=142aab752dcc0483&attid=0.7&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P90fuF_-XHOSL6iwje353GN&sadet=1385876249949&sads=8_m6GbuxfE6VfUIJ3GE25l-2qbI
Wasanii wa kundi la THT wakitoa burudani kwa wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania TBL, wakati wa zoezi la kupima virusi vya ukimwi kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo, Dar es Salaam.
 

JOY KALEMERA NDIYE MSHINDI WA MISS TANZANIA USA PAGEANT

0
0
 Mlimbwende Joy Kalemera akipungia mashabiki baada ya kushinda mashindano ya Miss Tanzania USA Pageant yaliyofanyika usiku wa Jumamosi Novemba 30, 2013 kwenye ukumbi wa Hollywood Ballroom uliopo Silver Spring , Maryland na Mhe. Balozi Liberata Mulamula ndiye aliyekua mgeni rasmi. Joy Kalemera alipohojiwa na Vijimambo alikua na haya ya kusema.
 Mshindi wa Miss Tanzania USA Pageant Joy Kalamera akipewa maua na aliyekua Miss District of Columbia baada ya kutangazwa mshindi kwenye Miss Tanzania USA Pageant ambapo mashindano haya ya kumtafuta Miss Tanzania USA Pageant ndiyo ya kwanza kufanyika kwenye ardhi ya Marekani. 
 Miss Tanzania USA Pageant Joy Kalemera akiwa mwenye furaha baada ya kutangazwa mshinidi wa Miss Tanzania USA Pageant.
 Balozi wa Tnzania nchini Marekani na Mexico akimvisha taji Joy Kalemera baada ya kutangazwa mshindi wa Miss Tanzania Pageant
 Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa mwenye furaha baada ya shindano hili kufana sana na kuandika historia iliyobeba ukurasa mpya wa kutangaza Tanzania kwenye mashindano haya ya Miss Afrika USA Pageant ambayo Tanzania ilikua na mshiriki wa kwanza mwaka huu ambae ushiriki wake haukupitia ngazi hii.
Joy Kalemera akipongezwa na washiriki wenzake waliokua nae kwenye kinyang'anyiro hiki kilichoanzia miezi miwili iliyopita.
 Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa kwenye picha ya pamoja na mshindi wa kwanza katika historia ya Miss Tanzania USA Pageant Joy Kalemera kulia ni Mkurugenzi na mwanzilishi wa Miss Tanzania USA Pageant Ma Winny Casey.
 Joy Kalemera katika picha ya pamoja na majaji pamoja na mkurugenzi na mwanzilishi wa Miss Africa USA Pageant, Lady Kate (kulia)
 Kutoka kushoto ni Faith Kashaa kutoka Alabama ambaye ndiye mshindi wa tatu, Doreen Rumaya kutoka Pennsylvania mshindi wa pili, Joy Kalemera kutoka New Jersey Miss Tanzania USA Pageant, Julia Nyerere mshindi wa Tano na Namala Elias mshindi wa nne wakiwa kwenye picha ya pamoja
 Miss Tanzania USA Pageant katika picha ya pamoja na washiriki wenzake. Kwa habari na picha zaidi BOFYA HAPA

JK azindua Benki ya Azania Tawi la Lamadi Mkoa wa Simiyu

0
0
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Azania Bw.William Erio(kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bwana Charles Singili(kulia) wakifuana kitambaa katika jiwe la msingi kushiria kuzindua Benki ya Azania tawi la Lamadi, Mkoa mpya wa Simiyu  jana.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Azania Bwana William Erio(wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Azania Bwana Charles Singili(kushoto) wakikata utepe kuzindua rasmi Benki ya Azania Tawi la Lamadi jana.Kulia nia mkuu wa Mkoa wa Simiyu Pascal Mabiti. Picha na Freddy Maro

DKT. NCHIMBI AZINDUA RASMI KIWANDA CHA USHONAJI CHA GEREZA KUU BUTIMBA, MWANZA PAMOJA NA MAGEREZA "DUTY FREE SHOP" YA KANDA YA ZIWA LEO

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel John Nchimbi(kushoto) akisoma Kibao cha uzinduzi rasmi wa Magereza "Duty Free Shop" ya Butimba, Mwanza ambayo itahudumia Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa(kulia) ni Kamishna Jenearali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel John Nchimbi(suti nyeusi) akifurahia jambo na Mmoja wa Wafungwa( kushoto) wa Gereza Kuu Butimba, Mwanza ambaye ni fundi Ushonaji wa nguo za aina mbalimbali mara baada ya uzinduzi rasmi wa Kiwanda cha Ushonaji cha Gereza Kuu Butimba. Kiwanda hicho kitakuwa kinatoa huduma ya Ushonaji wa Sare za Maafisa, Askari, Watumishi raia, Wafungwa pamoja na nguo za aina mbalimbali za Taasisi za Serikali na Watu Binafsi katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa( kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel John Nchimbi( suti nyeusi) akiangalia nguo za aina mbalimbali kama ambavyo zinaoonekana katika picha ambazo zimeshonwa na Wafungwa katika Kiwanda cha Gereza Kuu Butimba, Mwanza ambapo Kiwanda hicho kimezinduliwa rasmi leo Disemba 02, 2013(kushoto kwa Dkt. Nchimbi) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja.
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza toka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel John Nchimbi( hayupo pichani) ya uzinduzi rasmi wa Kiwanda cha Ushonaji cha Gereza Kuu Butimba, Mwanza pamoja na Magereza "Duty Free Shop"ya Kanda ya Ziwa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dkt. Emmanuel John Nchimbi(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mwanza mara baada ya kuzindua rasmi Magereza "Duty Free Shop " ya Kanda ya Ziwa iliyopo Gereza Kuu Ukonga leo Disemba 02, 2013(kulia kwa Dkt. Nchimbi) ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(kushoto kwa Dkt. Nchimbi) ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga(wa pili kulia) ni Rais wa Kampuni ya Transit Military Shop Limited, Bw. Sadrudin Virji( wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mwanza, Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Magereza, Raphael Molel( Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Viewing all 109572 articles
Browse latest View live




Latest Images