Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live

ATOMIC JAZZ ILIVYOACHIA BOMU KWA JAMHURI JAZZ

$
0
0
Na Moshy Kiyungi
Jangwa la Mkoa wa New Mexico, huko nchini Marekani July 16, 1945, kulifanywa jaribio la mwanzo la kuliripua bomu la Atomic ambalo liliibadilisha dunia yetu. Bomu hilo lilikuwa na nguvu mara elfu mbili zaidi kuliko bomu lolote lililokuweko hapo kabla.

Bomu la mwanzo la atomic lilitengenezwa huko Los Alamos, katika maabara ya siri iliyokuweko katika milima ya New Mexico. Mwanafizikia Robert  Oppenheimer aliiongoza shughuli hiyo katika kipindi cha chini ya miaka miwili. Hapa nchini Tanzania kulianzishwa bendi ya muziki wa dansi iliyobeba jina la Atomic Jazz.

Ilikuwa ‘nguvu’ mithiri ya bomu la Atomic kwa bendi pinzani ya Jamhuri Jazz zote zikiwa makazi katika mji wa Tanga wakati huo. Atomic Jazz ilikuwa na wanamuziki mahiri waliweza kupiga muziki uliokuwa ukileta ushindani mkubwa kwa Jamhuri Jazz. Jiji la Tanga ambalo wakati huo ulikuwa mji, ndilo linalotajwa kwamba ndiko muziki wa dansi uliingia ukitokea katika mji wa Mombasa nchini Kenya.

Yaelezwa kwamba muziki huo ulianza kwanza kwa kuundwa klabu ambapo watu walialikana kwenda kucheza aina mbalimbali za muziki wa Kizungu. Mtindo maarufu uliotumiwa wakati huo unaojulikana kama Ballroom dancing. Aina hizi za klabu zilianzia katika mji wa Mombasa nchini Kenya na kuingia nchini humu kupitia Tanga, kisha kupelekwa Dar es Salaam.

Klabu iliyokuwa maarufu mjini Tanga wakati huo iliitwa ikiitwa Tanga Young Comrades Club. Siku zilivyokuwa zikisonga mbele, klabu nyingine ikaanzishwa, ikaitwa New Generation Club ambayo ilianzisha matawi miji mbalimbali. Atomic Jazz ilikuwa ni moja kati ya bendi zilizowika kwa muziki nchini wakati huo.

Zingine zilizotamba wakati huo ni za mahasimu wao Jamhuri Jazz, Kilwa Jazz, Western Jazz na Dar Jazz zote za kutoka mkoani Pwani wakati huo, sasa ni mkoa wa Dar es Salaam. Morogoro Jazz, Cuban Marimba za mkoani Morogoro, Tabora Jazz na  Kiko Kidds zilizokuwa mkoani Tabora, zilikuwepo zikifanya ushindani mkubwa katika muziki.

Mji wa Tanga wakati huo ulikuwa na vikundi vingine maarufu vya muziki wa dansi na taarabu zikitoa burudani maridhawa kwa wakazi wake mji huo na viunga vyake. Vikundi hivyo ni pamoja na bendi White Star, Amboni Jazz, Lucky Star, Black Star na kadhalika. Ikumbukwe kwamba vikundi hivyo vilitoa wanamuziki wengi wa dansi na taarabu ambao baadhi yao bado wapo katika tasnia ya muziki wa dansi na taarabu.

Bi. Shakila Bint Said na Bi. Asmahani waliokuwa waimbaji mashuhuri wa muziki wa taarabu, walitoka katika kundi la Lucky Star pamoja na mwanamuziki wa bendi ya The Kilimanjaro ‘Wana Nje nje’ Waziri Alli ni mfano wa wakongwe walitoka mjini Tanga. Bila ya kuwasahu ndugu wawili George na Wilson Peter Kinyonga walianzia safari yao ya kwenda Kenya wakiwa katika bendi ya Jamhuri Jazz.

Huko wakauda bendi ya Simba Wanyika hatimaye Les Wanyika na nyinginezo. Miaka ilivyokuwa ikisonga mbele, bendi zingine za Jamhuri Jazz na Atomic Jazz zikaanzishwa katika mji huo. Bendi hizo zilikuwa zikishindana kutoa burudani kwa wapenzi na mashabiki wake waliokuwa katika mji huo sanjari na  viunga vyake.

Makala haya yanaizungumzia bendi ya Atomic Jazz, iliyokuwa ikipiga muziki wake ikitumia mtindo wa ‘Kiweke’ uliokuwa maarufu hususani kwa wapenzi na mashabiki wa bendi hiyo. Atomic Jazz alikuwa na wanamuziki wengi ambao kwa pamoja  walileta changamoto kubwa dhidi ya wapinzani wao wakubwa bendi ya Jamhuri Jazz.

Bendi hiyo ilikuwa ikimilikiwa na Bwana Julius Kiluwa, aliyeweza kukusanya wanamuziki mahiri katika tasnia ya muziki wa dansi. Baadhi ya wanamuziki hao ni John Mbula aliyekuwa akipuliza Saxophone, Rodgers aliyekuwa  mwimbaji wakati John Kiluwa alikuwa mpiga tumba.

Huyo John alikuwa ni ndugu wa mmiliki wa bendi Julius Kiluwa. John Kijiko alikuwa akiliungurumisha gitaa la solo, Hemed Mganga alikuwa akisimama kwenye gitaa la rhythm. Hemed pia aliwahi kupiga muziki katika bendi ya Orchestra Makassy na ndie baba mzazi wa mwimbaji wa kizazi kipya Kassim Mganga.

Gitaa zito la besi lilikuwa likiungurumishwa na Mohamed Mzee. Kama nilivyokujuza awali kwamba Atomic Jazz ilikuwa na wanamuziki wenye weledi mkubwa katikia muziki. Waliweza kutunga na kupiga nyimbo nyingi ambazo zilirekodiwa wakati huo.

Baadhi ya nyimbo hizo zilikuwa ni za Ufukara umezidi, Vipi mpenzi wangu, Mahakimu, Madoo mpenzi wangu, Mimi ni mtoto wa Watu, Nakujutia Salima, Nakupenda ni Raga, Dunia ina mambo, Usitamani kitu na Wataka nini mpenzi.

Wimbo wa ‘Mado mpenzi wangu’ ulijijengea heshima kubwa kufuatia ujumbe uliokuwa ukijieleza. Ulikuwa na ujumbe wa kweli kutoka kwa mwanamuziki mmoja kwenda kwa mpenzi wake. Wimbo huo ulikuwa ni utunzi wa mpenzi wa Atomic Jazz, aliyekuwa amekubuhu kwa kuihusudu bendi hiyo wakati huo.

Aidha bendi ya Atomic Jazz iliweka jina la wimbo huo kwenye jarada la santuri. Msomaji wa makala haya kwa ridhaa yako naomba usome ubeti wa kwanza wa wimbo wa Dunia ina mambo. “Dunia ina mambo mengi, ya furaha na shida, kila uonapo raha ukumbuke mwisho utapata tabu, hasa sisi vijana wa leo mambo yetu ni mengi shida zikikufikia unalialia na kupata tabu…”

Haya ni maneno mazuri yenye mafundisho kwa vijana wa wakati ule na hata wa hivi sasa. Ni matumaini yangu kwa vijana wanaoinukia katika tasnia ya muziki kuzisaka nyimbo za wanamuziki wa zaman, wazisikilize yawezekana wakaambulia mambo mengi yakuwasaidia katika muziki.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 3,2019

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI NA SALAMA NCHINI

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Hassan Suluhu akiwasha Mwenge wa Uhuru kuashiria uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2019, Mkoani Songwe.
????????????????????????????????????
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Hassan Suluhu akihutubia wananchi wa Songwe walioshiriki kwa wingi katika uwanja wa Kimondo – Forest, Wilayani Mbozi kushuhudia uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Mwaka 2019.
????????????????????????????????????
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa Mkoa wa Songwe waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.
????????????????????????????????????
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Songwe walioshiriki kwenye hafla ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka 2019.
????????????????????????????????????
Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Serikali ya Zanzibar, Mhe. Balozi Ali Karume akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwenye Uwanja wa Kimondo, Wilayani Mbozi Aprili 2, 2019.
????????????????????????????????????
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali (Mst.), Nicodemus Mwangela akieleza jambo kuhusu Mkoa wa Songwe.
????????????????????????????????????
Sehemu ya Vijana wenye dhamana ya kukimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2019 (waliosimama mstari wa mbele).
????????????????????????????????????
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Hassan Suluhu akiwa pamoja na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa wakifuatilia matukio ya vijana halaiki. (Kulia) ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (Kushoto) ni Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Serikali ya Zanzibar, Mhe. Balozi Ali Karume.
????????????????????????????????????
Vijana wa Halaiki wakionesha picha ya Mwl. Julius K. Nyerere wakati wakiimba nyimbo ya kumsifu kwenye hafla ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.
????????????????????????????????????
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Hassan Suluhu akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bw. Mzee Mkongea Ali. (Kulia) ni Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa.
????????????????????????????????????
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali (Mst.), Nicodemus Mwangela akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bw. Mzee Mkongea Ali baada ya kukabidhiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Hassan Suluhu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge zilizofanyika Aprili 2, 2019 Mkoani Songwe katika Uwanja wa Kimondo.
????????????????????????????????????
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama pamoja na Viongozi mbalimbali walipokuwa wakicheza na kufurahi wakati wanakwaya ya JKT Mlale walipokuwa wakiimba nyimbo na kutoa burudani kwa wananchi wa Songwe waliohudhuria uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wananchi wa songwe wakifuatilia hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Hassan Suluhu (hayupo pichani). Makamu wa Rais alikuwa Mgeni rasmi katika hafla hiyo ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2019. 
PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU
(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)
…………………………


Na OWM (KVAU) – SONGWE

Serikali imedhamiria kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi waishio mijini kufikia asilimia 95 na vijijini asilimia 85 ifikapo 2020.

Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mama Samia Hassan Suluhu wakati wa uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Aprili 2, 2019 zilizofanyika uwanja wa Kimondo – Forest Mlowo, Wilaya ya Mbozi, Mkoani Songwe.

Kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu 2019 isemayo “Maji ni Haki ya kila Mtu, Tutunze Vyanzo Vyake na Tukumbuke Kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa”

Makamu wa Rais amesema kuwa dhamira ya Serikali inayoongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ni kuboresha huduma za jamii ikiwemo sekta ya elimu, afya, barabara, umeme vijijini, usafiri wa anga, uvuvi, kilimo, viwanda na upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wote.

“Sera yetu ya Maji ya mwaka 2002 inasisitiza upatikanaji wa maji safi na salama ambayo ni muhimu kwa maisha ya kila mtu, shughuli za kiuchumi na ustawi wa mazingira,” alisema Makamu wa Rais.

Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa maji safi, alieleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza ujenzi wa miradi mbalimbali ya maji nchini ikiwemo mabwawa ya kimkakati na kuboresha miundombinu ya uzalishaji na usambazaji maji safi.

Aidha, Makamu wa Rais alitoa wito kwa Wananchi kuhakikisha wanatunza vyanzo vya maji kwa kuacha kufanya shughuli za kibinadamu kando ya vyanzo hivyo.

Kupitia hadhara ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Makamu wa Rais, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi na kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao ni muhimu katika kuleta maendeleo ya watu na huduma za kijamii.

Awali Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama alisema kuwa Mwenge wa Uhuru ndio msingi mkubwa wa amani, Mshikamano, Uzalendo na Umoja tulionao katika Taifa.

“Tunu hii imekuwa ni kichocheo cha maendeleo kwa wananchi na wamekuwa wakihamasika kushiriki katika kuandaa na kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo ya kijamii na kiuchumi iliyopo katika maeneo yao,” alisema Mhagama.

Waziri Mhagama aliongeza kwa kuwashukuru wadau mbalimbali waliosaidia kufanikisha tukio hilo muhimu la Kitaifa.

Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali (Mst.), Nicodemus Mwangela alishukuru Serikali kwa kuchagua Mkoa wa Songwe kuwa wenyeji wa Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka 2019.

WAZIRI WA MADINI UGANDA AFURAHISHWA NA USIMAMIZI WA SEKTA YA MADINI NCHINI

$
0
0



 Waziri wa Madini Nchini Uganda, Peter Lokeris na Naibu Waziri wa Madini Nchini Tanzania, Stanslaus Nyongo (katikati) wakiangalia namna kifusi cha mchanga kinavyotolewa kwenye Mgodi wa Dhahabu wa Blue Creef  uliopo Wilayani Geita Mkoani Geita unaomilikiwa na Christopher Kadeo tarehe 02 Aprili, 2019
PICHA NA 2 A
Waziri wa Madini Nchini Uganda, Peter Lokeris (wa pili kulia) akifafanua jambo kwenye Mgodi wa Dhahabu wa Blue Reef  uliopo Wilayani Geita Mkoani Geita unaomilikiwa na Christopher Kadeo mara baada ya yeye pamoja na ujumbe wake kufanya ziara kwenye mgodi huo. Katikati ni Naibu Waziri wa Madini Nchini Tanzania, Stanslaus Nyongo.
PICHA NA 3 A
Mkurugenzi wa kampuni ya Tan-Discover Mineral Consultancy Co. Ltd, Peter Kaheshi (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa Waziri wa Madini Nchini Uganda, Peter Lokeris (kulia) mara baada ya yeye pamoja na ujumbe wake kufanya ziara katika kituo cha mfano cha Rwamgaza kwa ajili ya kutoa mafunzo ya namna bora ya uchimbaji na uchenjuaji wa madini kilichopo katika eneo la Rwamgaza Wilayani Geita Mkoani Geita.
PICHA NA A
Mtaalam kutoka Mgodi wa Dhahabu wa Busolwa uliopo Wilayani Geita Mkoani Geita, Felix Adolf Ishebabi  (katikati) akielezea shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu zinavyofanywa na mgodi huo kwa Waziri wa Madini Nchini Uganda, Peter Lokeris, Naibu Waziri wa Madini Nchini Tanzania, Stanslaus Nyongo pamoja na wajumbe kutoka Uganda na Tanzania kwenye ziara hiyo.
PICHA NA 5A
Afisa Migodi Mkazi wa Mkoa wa Geita, Ernest Maganga (kulia) akielezea namna biashara ya madini inavyofanyika kwenye Soko la Madini la Geita kwa Waziri wa Madini Nchini Uganda, Peter Lokeris (kushoto) na Waziri wa Madini Nchini Tanzania, Stanslaus Nyongo (katikati) pamoja na wajumbe kutoka Uganda na Tanzania kwenye ziara hiyo
……………..


Na Greyson Mwase, Geita

Waziri wa Madini Nchini Uganda, Peter Lokeris ames ema kuwa amefurahishwa na usimamizi wa sekta ya madini nchini Tanzania na kusisitiza kuwa Uganda bado itaendelea kutuma wataalam wake pamoja na wachimbaji wadogo wa madini nchini Tanzania kwa ajili ya kujifunza namna bora ya uchimbaji na uchenjuaji wa madini.

Lokeris aliyasema hayo jana tarehe 02 Aprili, 2019 mara baada ya kutembelea migodi ya wachimbaji wadogo na wa kati ya madini iliyopo Wilayani Geita Mkoani Geita, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku nne nchini Tanzania yenye lengo la kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa katika Sekta ya Madini kupitia Wizara ya Madini hususan katika kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini.

Akiwa ameongozana na ujumbe wa maafisa waandamizi kutoka Serikali ya Uganda pamoja na wawakilishi wa wachimbaji wadogo aliwasili mkoani Geita na kupokelewa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Geita ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Geita pamoja na Naibu Waziri wa Madini Nchini Tanzania, Stanslaus Nyongo.

Ziara hiyo pia ilihusisha wataalam kutoka Wizara ya Madini. Tume ya Madini, vyombo vya ulinzi na usalama vya mkoa pamoja na waandishi wa habari.

Akielezea hali iliyopelekea nchi ya Uganda kuichagua nchi ya Tanzania kama sehemu ya kujifunza kuhusu Sekta ya Madini, Lokeris alisema kuwa, baada ya kutanya utafiti katika nchi za Aftika Mashariki, walibaini kuwa nchi ya Tanzania ni nchi iliyopiga hatua kubwa kwenye usimamizi wa sheria na kanuni za madini hali iliyopelekea wananchi wengi kunufaika nayo hususan wachimbaji wadogo wa madini.

Aliendelea kusema kuwa, Sekta ya Madini Nchini Uganda ndio inaanza kukua, hivyo wameona ni vyema kuja Tanzania kwa ajili ya kujifunza na kwenda kuimarisha Sekta ya Madini ili baada ya miaka kadhaa angalau iwe inakaribiana na nchi ya Tanzania.

Akielezea mikakati ya matumizi ya uzoefu mkubwa ujumbe huo ilioupata kutoka kwa nchi ya Tanzania, Waziri Lokeris alisema hatua ya kwanza itakayofanywa na Serikali ya Uganda kupitia Wizara yake ya Madini ni kuhamasisha wachimbaji wadogo wa madini kuunda vikundi na kuwapatia leseni.

Aliongeza kuwa, mara baada ya kuwapatia leseni hatua itakayofuata itakuwa ni kuwaleta Tanzania kwa ajili ya mafunzo ambapo watajifunza kupitia wachimbaji wadogo wa madini wa Tanzania waliofanikiwa kwenye shugfhuli za uchimbaji na uchenjuaji wa madini.

Aliendelea kueleza kuwa, nia ya Serikali ya Uganda kupitia Wizara yake ya Madini ni kuhakikisha sekta hiyo inakua kwa kasi na kuanza kuzalisha dhahabu na kuuza nyingine nje ya nchi na kujipatia mapato makubwa.

“Tumefurahishwa na usimamizi mzuri kwenye sekta ya madini hususan kwenye eneo la uwezeshaji wa wachimbaji wadogo, tumeona namna wanavyochenjua madini huku wakizingatia sheria na kanuni za mazingira,”alisisitiza Waziri Lokeris.

Naye Naibu Waziri wa Madini Nchini Tanzania, Stanslaus Nyongo akielezea mafanikio ya sekta ya madini nchini alieleza kuwa, mafaniko yaliyopatikana ni pamoja na uboreshaji wa sheria mpya ya madini pamoja na kanuni zake inayotambua madini kama mali ya watanzania na kusisitiza kuwa wachimbaji wadogo wamekuwa wanufaika kwa kiasi kikubwa.

Aliongeza kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Madini imeondoa tozo mbalimbali zisizo za lazima hali iliyopelekea wachimbaji wadogo kuzalisha madini kwa gharama nafuu na kulipa kodi na tozo mbalimbali serikalini.

Alieleza mafanikio mengine kuwa ni pamoja na uanzishwaji wa masoko nchini kama njia mojawapo ya kudhibiti utoroshwaji wa madini kwa kuhakikisha wachimbaji wa madini wanakuwa na soko la uhakika la kuuzia madini yao kwa bei yenye faida.

Naye mmiliki wa mgodi wa dhahabu wa Blue Reef uliopo katika eneo la Rwamgaza Wilayani Geita mkoani Geita ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Wachimbaji wa Madini Mkoa wa Geita (GEREMA), Christopher Kadeo akizungumza na ujumbe huo uliofanya ziara kwenye mgodi wake akielezea mchango wa mgodi wake katika jamii iliyopo jirani alisema mgodi wake tangu ulipoanzishwa mwaka 1991 mpaka sasa umefanikiwa kuajiri watumishi 160 na vibarua takribani 200.

Alieleza mafanikio mengine kuwa ni pamoja na uboreshaji wa huduma za jamii kama vile afya, elimu, ulinzi kupitia ujenzi wa vituo vya polisi na kusisitiza kuwa mgodi umekuwa ukishirikiana kwa karibu zaidi na Tasisi nyingine za Serikali kama vile Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Chuo cha Madini Dodoma (MRI), Chuo Cha Ufundi Dar es Salaam (DIT), Wizara ya Madini, Tume ya Madini na mashirika mengine ya kimataifa.

Aidha, aliongeza kuwa mgodi wake umewahi kupewa tuzo ya utunzaji bora wa mazingira na Rais wa Awamu ya Tatu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin Mkapa.

Akielezea mikakati ya mgodi wake kwenye shughuli za uchimbaji wa madini alisema mgodi wake unatarajia kufanya utafiti zaidi ili kugundua madini zaidi na kuunganisha leseni zake tano unazomiliki na kutoka kwenye uchimbaji wa kati hadi mkubwa.

DC KIGAMBONI AWATAKA WANANCHI NA KAMPUNI WALIOJENGA KWENYE HIFADHI YA BARABARA WAZINGATIE SHERIA

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Sara Msafiri amewataka wananchi pamoja na Kampuni zilizojenga katika hifadhi ya barabara kuzingatia sheria na taratibu za wakala wa Barbara nchini TANROADS ili kuepuka usumbufu wa kuvunjiwa na kuisababishia serikali hasara.

Kauili hiyo ya Mkuu wa Wilaya MSAFIRI imekuja baada ya kubaini baadhi ya wawekezaji kujenga kituo cha mafuta katika hifadhi a barabara na kuongeza kuwa serikali imekuwa ikiweka mazingira bora ya uwekezaji ili pande zote mbili ziweze kunufaika.

Akiwa katika ziara ya kukagua vituo vya kuhifadhia na kusambaza mafuta ndani na nje ya nchi vilivyopo Wilayani humo amesema, ameridhishwa na ukarabati wa Tanki la Mafuta la Kampuni ya TAZAMA ambalo linajengwa kwa ushirikiano wa Tanzania na Zambia hivyo linapswa kuendelezwa kutokana na historia yake baina ya nchi hizo mbili.

Kwa upande wake Meneja wa Mkoa wa TAZAMA upande wa Tanzania ABRAHAM SAMWEMA amesema ujuio wa mkuu wa Wilaya utasaidia kutatua migogoro iliyopo kati yao na wananchi wanaovamia eneo la bomba la mafuta huku kaimu mkurugenzi wa jeshi la zimamoto na uokoaji CASTORY WILLA akizitaka Kampuni za mafuta kuwa na vifaa bora vya kuzuia milipuko ya moto katika maeneo ya kazi

Ziara hiyo ya siku nne ya Mkuu wa Wilaya wa Kigamboni inahitimishwa Ijumaa kwakuzikutanisha Kampuni za Mafuta na Gesi zilizopo katika wilaya hiyo.
Meneja wa Uhandisi TAZAMA Mhandisi Patrick Mnzava (kulia) akimwelezea Mkuu wa wilaya ya Kigamboni,Sara Msafiri mtambo kusafirisha mafuta ghafi kwenda Zambia unavyo fanya kazi leo katika ziara ya kukagua vituo vya kuhifadhi mafuta leo jijini Dar es Salaam. 
Meneja wa Uhandisi TAZAMA Mhandisi Patrick Mnzava (alienyosha mkono) akifafanua jambo mbele ya Mkuu wa wilaya ya Kigamboni,Sara Msafiri katika ziara ya kukagua vituo vya kuhifadhi mafuta leo jijini Dar es Salaam. 
Mkuu wa wilaya ya Kigamboni,Sara Msafiri akiwa ameongozana na kamati ya ulinzi ya wilaya hiyo wakikagua mitambo mbalimbali ya kampuni ya mafuta ya TAZAMA katika ziara ya kukagua vituo vyakuhifadhi mafuta leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
picha ya pamoja.

Mkuu wa wilaya ya Kigamboni,Sara Msafiri wa (kwanza kushoto) akizungumza na wafanyakazi wa kampuni ya mafuta ya TAZAMA katika ziara ya kukagua vituo vya kuhifadhi mafuta leo jijini Dar es Salaam.

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA MHAMASISHAJI WA TIMU YA TAIFA STARS PETER MOLLEL ALMAARUFU KAMA PIERRE LIQUID JIJINI DODOMA

$
0
0
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja wakifurahi jambo na Mhamasishaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Taifa Stars, Ndg. Peter Mollel alimaarufu kama Pierre Liquid ( wa tatu kushoto) walipokutana leo katika Hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, kabla ya kumualika Bungeni kwa ajili ya kusikiliza Vikao vya Bunge vilivyoanza jana Jijini Dodoma. Wa tatu kulia ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (kushoto), Mbunge wa Vijana kutoka Mkoa wa Dodoma, Mhe. Miriam Ditopile (wa pili kulia) na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dodoma, Ndg. Billy Chidabwa
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto) akifurahi jambo na Mhamasishaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Taifa Stars, Ndg. Peter Mollel (wa pili kulia) alimaarufu kama Pierre Liquid walipokutana leo katika Hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, kabla ya kumualika Bungeni kwa ajili ya kusikiliza Vikao vya Bunge vilivyoanza jana Jijini Dodoma. Kulia ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson na Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Mhamasishaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Taifa Stars, Ndg. Peter Mollel alimaarufu kama Pierre Liquid walipokutana leo katika Hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, kabla ya kumualika Bungeni kwa ajili ya kusikiliza Vikao vya Bunge vilivyoanza jana Jijini Dodoma. Katikati ni Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai
Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kulia) akisalimiana na Mhamasishaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Taifa Stars, Ndg. Peter Mollel alimaarufu kama Pierre Liquid (Kushoto) walipokutana leo katika Hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, kabla ya kumualika Bungeni kwa ajili ya kusikiliza Vikao vya Bunge vilivyoanza Jana Jijini Dodoma. Katikati ni Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai na Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai.(PICHA NA DEONISIUS SIMBA - OFISI YA BUNGE)

Sasa ni zamu ya Iringa Kuipokea BOMBARDIER

Kutotengwa rasilimali za kutosha kufikia Usawa wa Kijinsia ni Ndoto

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Shirika la TGNP Mtandao limesema kuwa kutotengwa rasilimali za kutosha, kutolewa  na kutekelezwa kwa wakati itakuwa ndoto kufika usawa wa kijinsia na maendeleo endelevu pamoja na ufanisi wa mikataba ya Kimataifa, sera na bajeti yenye mrengo wa kijinsia.

Hayo yameelezwa Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP Mtandao Bi.Asseny Muro kwenye ufunguzi wa mdahalo kabla ya bajeti kuu ya Taifa ya mwaka 2019/2020 ambapo amesema TGNP imekuwa mstari wa mbele katika kutetea masuala ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji Wanawake.

Aidha ameongeza kuwa wakati TGNP ikitimiza miaka 25 tangu ianzishwe imekuwa na mikakati mingi ambayo imekuwa ikitumika katika kuleta maendeleo kwa jamii, hasa usawa wa kijinsia na haki ya jamii, uchambuzi wa sera, mipango na bajeti kwa mrengo wa kijinsia pamoja na mafanikio ya mabadiliko ya kimtazamo na kimaoni kwa Wanawake kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Utafiti na Uchambuzi wa sera na Bajeti kutoka TGNP Happiness Maluchu amesema mdahalo huo umehusisha wadau wa  makundi mbalimbali ikiwemo makundi maalumu na wachambuzi wa sera za kibajeti ili kuhakikisha kuwa katika ujenzi wa uchumi wa viwanda watu waliopembezoni ikiwemo makundi maalumu na wale wa vijijini hawaachwi nyuma.

Hata hivyo amesema kuwa katika utekelezaji wa bajeti ambazo zimepita changamoto kubwa ipo kwenye ufikishwaji wa fedha kwa kiwango ambacho kimepangwa kwenye utekeleza wa mipango iliyowekwa hivyo kukwamisha ukamilishaji wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo.
 Mkuu wa Idara ya Utafiti na Uchambuzi wa Sera na Bajeti Happiness Maluchu akizunguma katika warsha ya kujadili Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2019/2020 kwa kuangalia usawa wa kijinsia lililofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mwanaharakati Janeth Mawinza akizungumza kuhusiana na wanawake kutoshirikishwa katika mipango mbalimbali ya serikali katika warsha ya TGNP iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau mbalimbali katika warsha ya TGNP

JESHI LA POLISI KIGOMA LAFANIKIWA KUUWA MAJAMBAZI 24, KUKAMATA SILAHA 14 AINA YA SMG NA RISASI 350.

$
0
0


Jeshi la Polisi Tanzania limeendesha Operesheni sehemu mbalimbali za nchi ili kupambana na wahalifu waliokuwa wanavamia majumani na kuteka magari njiani kwa kutumia silaha za moto. 

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi Nchini CP, Liberatus Sabas amesema operesheni hiyo iliyofanika katika Mkoa wa Kigoma imefanyika ndani ya miezi mitatu ambayo ilianza mwezi wa kwanza mpaka mwezi wa tatu mwaka huu na kufanikiwa kukamata silaha 14 aina ya SMG na risasi 350 pamoja na mafanikio hayo Jeshi la Polisi limefanikiwa kuua majambazi 24 katika majibizano ya kurushiana risasi na polisi ambapo katika mapambano hayo askari wawili walijeruhiwa na majambazi ila mpaka sasa wanaendelea na matibabu. 

Aidha kamishna Sabas, amesema wahalifu hao wanaotoka nchi za jirani ambazo hazina utulivu wa kisiasa, huku akiwaonya wahalifu hao wanaotoka nchini jirani kuwa wajue wataingia ila hawatatoka na wakae wakijua hakuna mwalifu atakaebaki salama pia akiwataka wale wanaoingia nchini kwa kutumia miamvuli ya wakimbizi na wao hawatakuwa salama kwani wakae wakijua Tanzania ni kisiwa cha amani. 

Kamishna Sabas amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano baina yao na Jeshi la Polisi ili kukabiliana na wahalifu wa ndani na wale wanaotoka nje ya nchi na kuwatumia salamu kuwa Tanzania si sehemu salama kwa wahalifu.

Maeneo 17 Dar Kufungwa CCTV Kamera

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, akiongoza Kikao cha wadau kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali, kujadili Mradi wa kuweka Kamera za Kudhibiti Uhalifu(CCTV Kamera) katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dodoma. 
 Washiriki wa Kikao cha Wadau wa kujadili Mradi wa Kuweka Kamera za Kudhibiti Uhalifu(CCTV Kamera) katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam,Faraji Ntembo na Faizer Mbange(kushoto), wakipitia moja ya nyaraka inayohusu mradi huo wakati wa kikao hicho kilichoongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu. Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dodoma. 
Mshiriki wa Kikao cha Wadau wa kujadili Mradi wa Kuweka Kamera za Kudhibiti Uhalifu (CCTV Kamera) katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam,Wankyo Nashon akichangia hoja, kushoto  ni mshiriki  Lina Rujweka. Kikao hicho kimefanyika  leo  jijini  Dodoma. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

PIERRE LUQUID ATINGA BUNGENI KIBABE...WAZIRI MKUU KUMPA TIKETI YA KUSAFIRI NA TAIFA STARS

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

HAKAMATIKI kabisa na atabaki kuwa kileleni!Ndivyo unavyoweza kuelezea kuhusu Peter Mollel a.k.a Pierre Luquid baada ya leo Machi 3, 2019 kutinga Bungeni kwa mualiko maalum wa Spika wa Bunge Job Ndugai.

Pierre anapata mualiko huo katika kipindi ambacho jina lake limekuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii .Kwa siku kadhaa Pierre amekuwa akijadliwa sana lakini leo hii ameibukia Bungeni.

Kabla ya kuingia bungeni leo mapema asubuhi Pierre alipata nafasi ya kukutana na mwenyeji wake Spika Ndugai ambapo walisalimiana na kisha kama kawaida  yake akatoa kibwagizo kwa kumwambia hivi "Ndugai ooooo...utabaki kuwa juu mawinguni" .Kibwagizo hicho kilimfanya Spika aliyekuwa ameambatana na Naibu Spika Dk.Tulia Akson na maofisa wengine wa Bunge kubaki wakicheka.

Katika kudhihirisha Pierre nyota yake imeng'aa na hakuna wa kuizima kwa sasa amepata nafasi ya kuzungumza na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye amemuhakikishia Pierre ambaye anajulikana kama Mhamasishaji wa Taifa Stars kuwa kutakuwa kuna tiketi yake ya ndege ya kwenda kushiriki na timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' iliyofuzu mashindano ya AFCON 2019.

Waziri Mkuu ameyasema hayo alipokuwa anazungumza na Pierre katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.Pierre amekwenda Dodoma kwa kutumia ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania na akiwa kwenye ndege hiyo aliamua kupiga picha akionesha ile ishara yake ya kubaki kileleni.

Kwa kukumbusha tu Pierre ni moja ya watu mashuhuri kwa sasa ambaye ametoa mchango mkubwa katika kuhakikisha anahamasisha Watanzania kujitokeza kwa wingi kwenye mechi kati ya Taifa Stars na Uganda ambapo Taifa Stars iliubuka na ushindi.

Wakati Rais Dk.John Magufuli alipokuwa amewaalika Ikulu jijini Dar es Salaam wachezaji wa Taifa Stars, viongozi wa TFF, bondia  Hassan Mwakinyo, Kamati ya Saidia Taifa Stars na wadau wengine wa soka, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alionesha kutambua mchango wa Pierre katika uhamasishaji kuelekea mchezo huo uliofanyika siku kadhaa zilizopita.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Mhamasishaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Taifa Stars, Ndg. Peter Mollel alimaarufu kama Pierre Liquid walipokutana leo katika Hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, kabla ya kumualika Bungeni kwa ajili ya kusikiliza Vikao vya Bunge vilivyoanza jana Jijini Dodoma. Katikati ni Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai

BONDIA ROJAS MASAMU AJIGAMBA KUMCHAKAZA MKWERA SIKU YA PASAKA

$
0
0
Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

BONDIA Rojas Masamu ametamba kumsambalatisha bondia Idd Mkwera katika raundi za awali kwa madai kuwa hataki kuwapa tabu majaji watakaosimamia pambano lao.

Masamu ameiambia Michuzi Blog leo Machi 3,2019 jijini Dar es Salaam kuwa kwa sasa yupo fiti na ana uchu wa kupambana huku akijagamba kumchakaza mpinzani wake Mkwera kwani kipigo atakachompa hatakisahau mpaka anaingia kaburini"Najiamini vya kutosha, nimefanya mazoezina hivyo nina kila sababu za kushinda tena mapema tu.Mkwera ajipange kwelikweli.

"Nipo kambini sasa yapata miezi miwili kwa ajili ya mpambano huu , hivyo asichukulie poa kabisa kwani kwa sasa nimeongeza dozi ya kufanya mazoez.Awali nilikuwa nafanya mazoezi mara mbili kwa siku lakini kwa sasa nafanya mara tatu kwa kuwa nataka kumpiga kwa K,O mbaya ambayo itawashangaza wapenzi na mashabiki wa mchezo wa ngumi,"amesema.

Kwa mujibu wa ratiba ya mpambano huo ambao umeandaliwa na Promota wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ni kwamba litafanyika Siku ya Sikukuu ya Pasaka na kwamba limepewa nguvu na bondia Mtanzania Omari Kimweri 'Lion Boy 'anayeefanya shughuli zake nchini Australia.

Super D amesema kuwa bondia huyo ndiye aliyesabababisha mabondia hao wawili kuwekewa pambano hilo kwani vijana wanatakiwa kuendeleza rekodi zao za masumbwi kila wakati.Ameongeza mbali ya pambano hilo pia siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine kadhaa.

Amesema kuwa bondia Hussein Pendeza atamkabili Juma Ramadhani 'Choki' na Shomari Milundi ataoneshana umwamba na Bakari Mbede wakati Ibrahimu Makubi atavaana na Haruna Ndalo wakati Ramadhani Mbegu 'Migwede' atakabiliana na Rashidi Mnyagatwa.

Pia bondia Salum Tandu atapambana na Gerald Mkude na Sunday Kiwale 'Moro Best' atavaana na Luckman Ramadhani wakati Vicent Mbilinyi atapambana, Shabani Mbogo na Hussein Shemdoe, Shehe Azizi na Ahmadi Kombo atapambana na Sandali Nyambala

Super D amesema mapambano yote hayo yamedhaminiwa na kampuni tanzu ya kizalendo ya Super D Boxing Promotion ambayo ipo nchini Tanzania kwa ajili ya kuinuwa vipaji ya vijana mbalimbali ili kuendeleza vipaji vyao pendwa

na kwa kupitia kampuni ya Super D Promotion imejidhatiti kuweka angalau pambano moja kila baada ya miezi miwili ili kuwasaidia vijana kukuza vipaji vyao na kujiendeleza kupitia mchezo uho wa masumbwi nchini.


Bondia Ramadhani Mbegu 'kushoto' akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Idd Mkwera wakati wa mazoezi ya kujiandaa na mapambano yao yatakayofanyika siku ya pasaka April 21 katika ukumbi wa CCM Mwinyimkuu magomeni Mapipa Mbegu atacheza na Rashidi Mnyagatwa na Mkwera atapambana na Rojas Masamu 
Bondia Idd Mkwera 'kushoto' akioneshana umwamba wa kutupiana makonde naRamadhani Mbegu wakati wa mazoezi ya kujiandaa na mapambano yao yatakayofanyika siku ya pasaka April 21 katika ukumbi wa CCM Mwinyimkuu magomeni Mapipa Mbegu atacheza na Rashidi Mnyagatwa na Mkwera atapambana na Rojas Masamu 
Bondia Sunday Kiwale 'Moro Best' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Shehe Azizi wakati wa maoezi yao ya kujiandaa na mapambano yao yatakayofanyika siku ya Pasaka April 21 katika ukumbi wa CCM Mwinyimkuu Kiwale atapambana na Luckman Ramadhani na Azizi atapambana na Hussein Shemdoe

MTENDAJI MKUU TFS AWATAKA WAAJIRIWA WAPYA NA WAZAMANI KUFUATA SHERIA ZA NCHI WANAPOTEKELEZA MAJUKUMU YAO

$
0
0
Na Ripota Wetu, Globu ya jamii

MTENDAJI Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Profesa Dos Sanatos Silayo amewataka waajiriwa wapya na wazamani wa wakala huo kuhakikisha wanatakeleza majukumu yao kadri sheria za nchi na jinsi maadili yanavyowataka.

Profesa Silayo ameyasema hayo leo Machi 3,2019 ambapo ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa anawapongeza watumishi hao kupata fursa ya kufanya kazi TFS lakini ni vema wakatambua wanalo jukumu la kutekeleza majukumu yao kwa kufuata misingi ya sheria za nchi. “ Niwapongeze watumishi wapya kwa kupata nafasi ya kufanya kazi nasi, lakini nataka kuwasisitizia suala la uadilifu na maadili katika utumishi si la mzaha, enendeni mkalitumikie taifa na kamwe msisubiri kufanya kazi kwa kusukumwa."

Ameongeza kuwa kila mmoja anatakiwa kufanya kazi kwa hiari, kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo ili kuhakikisha utumishi wa umma unaleta tija iliyokusudiwa, hivyo amefafanua ndio maana wameamua pia watumishi wa zamani kuwapatia amafunzo haya ikiwa ni jitiada za kurejesha uadilifu na maadili miongoni mwao.

Kwa upande wake Mkuu wa Mafunzo ya muda mfupi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Charles Magaya aliyemwakilisha Kaimu Mtendaji Mkuu wa chuo hicho, Dk.Emanuel Shindika ameipongeza TFS kwa kutambua kuwa ili utumishi wa umma uwe wenye ufanisi na wa kuheshimika, watumishi wanapaswa kuzifuata Kanuni za maadili ya utumishi pamoja na kuwa na tabia na mwenendo unaozingatia utoaji wa huduma bora, utiii kwa Serikali, kutoa huduma bila upendeleo, kufanya kazi kwa uadilifu, kuwajibika kwa umma, kuheshimu sheria na matumizi sahihi ya taarifa kwa kuwapa nafasi yakuwafunza watumishi hao.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Profesa  Dos Sanatos Silayo akifafanua jambo wakati anazungumza na waajiriwa wapya na wa zamani wa wakala huo ambapo amewakumbusha kutekeleza majukumu yao kwa kuheshimu sheria za nchi na jinsi maadili ya umma yanavyoelekeza.
 Mkuu wa Mafunzo ya muda mfupi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Charles Magaya aliyemwakilisha Kaimu Mtendaji Mkuu wa chuo hicho, Dk. Emanuel Shindika akifafanua jambo ambapo pia ametoa pongezi kwa  TFS.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) Profesa Dos Santos Silayo (aliyekaa mstari wa mbele katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wapya na wazamani wa wakala huo

Ujumbe wa Libya wakutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Palamagamba Kabudi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof Palamagamba John Kabudi akiwa katika mazungumzo na Kiongozi wa Ujumbe kutoka Libya Mhe. Jamal El Barak

=======================================

Tanzania na Serikali ya Umoja ya Libya, zimekubaliana kuingia katika mazungumzo ya kina yenye lengo la kupitia miradi yote na uwekezaji, iliyokuwa ikifanywa na Serikali ya Libya hapa nchini kabla ya machafuko nchini humo na pia kuangalia maeneo mapya ya uwekezaji ambayo Libya imeonesha nia ya kutaka kuwekeza chini ya Kamati ya pamoja baina ya nchi hizo mbili.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati wa mazungumzo na Kiongozi wa Ujumbe kutoka Libya na kuongeza kuwa baada ya hali ya Libya kutengemaa na Amani kuongezeka wamekubaliana kuingia katika uwekezaji.

“Nimemueleza mgeni wangu kuwa mwaka huu wa 2019 Tanzania tumeutangaza kuwa ni mwaka wa uwekezaji na yeye ameonesha nia ya nchi yake na makampuni ya Libya kutaka kuja kuwekeza hapa nchini,tumejadili pia jinsi ya kufufua kamati ya pamoja kati ya Libya na Tanzania kwakuwa mkutano wa mwisho ulifanyika mwaka 2000 baada ya Kamati hiyo kukutana sasa tutajadili miradi mbalimbali ambayo Libya imewekeza,mitaji iliyoiwekeza lakini pia tutaangalia maeneo mapya wanayopendekeza kuwekeza”.

Aidha Profesa Palamagamba John Kabudi amefafanua kuwa lengo jipya katika sheria za uwekezaji Tazania ni kuhakikishia Nchi inakuwa na mfumo wa sheria na uwekezaji ambao kila upande unapata tofauti na mfumo wa zamani ambao wawekezaji walikuwa wakinufaika na nchi inanyonywa.

Kwa upande wake Kiongozi wa Ujumbe kutoka Libya Mhe. Jamal El Barak amesema wamekuja dhumuni la ujumbe wao kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ni kumjulisha kuwa Serikali ya Umoja wa Libya iko tayari kufufua na kuendeleza mahusiano ya kidiplomasia baina ya nchi hizo baada ya hali ya Amani kutengemaa nchini Libya kutokana na mahusiano ya Tanzania na Libya kuwa ya kihistoria.

Mbali na hayo Mhe Jamal El Barak ameongeza kuwa Libya iko tayari kushirikiana na Tanzania katika sekta mbalimbali za uwekezaji kwa kuwa wanatambaua mazingira ya uwekezaji Tanzania ni mazuri hasa baada ya kuhakikishiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki kuwa mazingira ya uwekezaji yameboreshwa.

“Si mara yetu ya kwanza kuwekeza hapa nchini,kabala ya machafuko nchini mwetu tulikuwa tumewekeza katika sekta mbalimbali na sasa tutaangalia maeneo mapya ya uwekezaji” 

RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA MTWARA-NEWALA-MASASI KM 210 SEHEMU YA MTWARA MNIVATA KM 50 KATIKA ENEO LA NALIENDELE MKOANI MTWARA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na Viongozi wengine wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mkoa wa Mtwara, Wabunge na viongozi wengine akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mitambo itaayotumika katika ujenzi wa Barabara ya Mtwara-Newala-Masasi km 210 sehemu ya Mtwara-Mnivata km 50 katika hafla iliyofanyika sehemu ya Naliendelea mkoani Mtwara.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na Viongozi wengine wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mkoa wa Mtwara, Wabunge na viongozi wengine akivuta utepe kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Barabara ya Mtwara-Newala-Masasi km 210 sehemu ya Mtwara-Mnivata km 50 katika hafla iliyofanyika sehemu ya Naliendelea mkoani Mtwara.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Naliendele mkoani Mtwara kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Barabara ya Mtwara-Newala-Masasi km 210 sehemu ya Mtwara-Mnivata km 50.



 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wanachi wa Naliendele mkoani Mtwara wakati akielekea kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Barabara ya Mtwara-Newala-Masasi km 210 sehemu ya Mtwara-Mnivata km 50.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mbunge wa zamani wa Mtwara mjini Murji mara baada ya kuweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi huo wa barabara.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Nanguruwe mkoani Mtwara wakati akielekaea Newala.
 Wananchi wa Nanguruwe Mtwara vijijini wakishangilia mara baada ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwatatulia sehemu itakapojengwa hospitali katikka eneo hilo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Nanyamba mkoani Mtwara wakati akielekea Newala. PICHA NA IKULU


Mkurugenzi mpya Tony Elumelu aanza majukumu yake

$
0
0
Na Ripota Wetu-Lagos, Nigeria

MKURUGENZI Mtendaji mpya wa Taasisi ya Tony Elumelu ya nchini Nigeria, Ifeyinwa Ugochukwu, ameanza majukumu yake mapya kuanzia Aprili 1, mwaka hu.

Ifeyinwa anakuwa Mkurugenzi Mtendaji wa tatu na wa kwanza kwa Afrika kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Tony Elumelu, ambapo kabla ya kuchukua nafasi hiyo aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Ushirikiano na Tahmini wa taasisi hiyo.

Desemba mwaka jana Taasisi ya Tony Elumelu ambayo inafanyakazi ya kuwawezesha wajasiriamali wa Kiafrika, ilitangaza uteuzi mpya wa Ifeyinwa kama Mkurugenzi Mtendaji nafasi ambayo ilikuwa ikishikiwa na mtangulizi wake Parminder Vir, ambaye kwa sasa anakwenda kuwa Mkurugenzi wa Bodi ya Ushauri wa Tony Elumelu.

Katika jukumu yake Ifeyinwa alisema atazingatia kuongeza umuhimu wa Programu ya Uwekezaji wa Tony Elumelu ya dola milioni 100 kwa kipindi cha miaka 10 na kuimarisha mahusiano kati ya Afrika na mfumo wa kimataifa wa ujasiriamali, kuwawezesha wajasiriamali wa Afrika na matokeo ya kujenga ajira na mali juu ya bara. 

Pia atachukua jukumu la kuweka nafasi ya TEF Connect- ambalo ni jukwaa la mitandao ya digital kwa wajasiriamali wa Afrika kama kitovu cha kuunda uhusiano wa biashara, kubadilishana uzoefu na kusambaza ujuzi kwa Bara la Afrika.

Katika kipindi cha miaka miwili Ifeyinwa Ugochukwu, alikuwa katika kutoa uzoefu wake hasa kupitia nafasi yakwe yake ya zamani ya Mkurugenzi wa Ushirikiano na Tathmini kabla ya kupata nafasi mpya ya kuongoza taasisi hiyo.

Taariga kwa umma iliyotolewa na Taasisi ya Tony Elumelu, ilieleza kwamba kwa nafasi yake mpya pia ni kiongozi anayethibitishwa na maono ya biashara kwa akili na uwezo wa kuwaleta watu pamoja. 

Ilielezwa kuwa uwezo wake wa namna ya kuisuka taasisi inavyostahili, kulingana na mazingira. Lakini pia ataangazia maendeleo na mazingira ya taasisi kwa kuona namna gani inaweza kupiga hatua zaidi.

Akizungumza kwa niaba ya Bodi ya Wadhamini, Tony Elumelu, Mwanzilishi wa Tony Elumelu Foundation alisema “Tuna hakika kwamba Ifeyinwa ndiye mtu makini wa kuimarisha Taasisi katika awamu yake ya uongozi. Uteuzi wake kama Mkurugenzi Mtendaji utaimarisha taasisi yetu ya kuongeza kiwango cha kujitolea na kufungua fursa katika mazingira ya ujasiriamali kote katika Bara la Afrika.

“Nimekuwa nikisema kuwa hakuna mtu wa ulitengeza Bara la Afrika, na maonyesho zaidi na utekelezaji wa azimio hili ni wajibu wetu wote,” alisema Mwasisi wa taasisi hiyo Tony Elumelu

GULAMALI CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI JULAI MWAKA HUU

$
0
0
* Lalenga kuimarisha sekta ya elimu, Shule  zote za Sekondari katika jimbo la Manonga kushiriki 

Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
LIGI ya mpira kwa wanafunzi wa shule za sekondari katika jimbo la Manonga zinatarajiwa kuanza kutimua vumbi mapema mwezi Julai mwaka huu na hiyo yote ni kwa malengo ya kuimarisha sekta ya elimu jimboni humo.

Mashindano hayo yaliyopewa jina la Gulamali Cup 2019 yamekuja baada ya mbunge wa jimbo hilo Seif Gulamali kuwezeka zaidi katika sekta ya elimu kwa kuhakikisha mazingira ya ujifunzaji na miundombinu ya sekta hiyo yanakuwa rafiki kwa wanafunzi na walimu.

Imeeleezwa kuwa mashindano hayo yatawaweka pamoja wanafunzi na walimu pamoja na kubadilishana mawazo na kuzidi kuboresha sekta ya elimu.

Aidha shule zitakazoshiriki mashindano hayo ni sekondari zote za jimbo hilo ambazo ni Choma, Ziba, Misana, Ngulumwa, Mwashiku, Ndembezi, Nkinga, Mwisi, Simbo, Ichama, Igoweto, Sungwizi, Ibologelo, Mwakipanga, Umoja, Ulaya na shule ya sekondari ya Mtakatifu Thomas.

Ligi hiyo itahusisha michezo mbalimbali na washindi watakaoibuka kidedea kujipatia zawadi kutoka kwa Mbunge wao.

Ikumbukwe kuwa katika matokeo ya kidato cha nne mwaka jana zaidi ya watahiniwa 250 walipata daraja la kwanza hadi la tatu huku ikielezwa  kuwa jitihada za mbunge wa jimbo hilo katika kuweka miundombinu rafiki ya majengo na nyumba za walimu pamoja na kuwalipia ada wanafunzi wanaofaulu kwenda kidato cha tano imekuwa chachu kubwa  kwa wanafunzi na walimu .

KAMPUNI YA KIMATAIFA YAZINDUA MAFUNZO YA KUUZA NA KUNUNUA FEDHA KIMTANDAO

$
0
0
Na Khadija Seif,Globu ya jamii

KAMPUNI ya kimataifa ya kibiashara ya kuuza na kununua fedha kwenye masoko kimtandao (CITL)imeamua kuzindua mafunzo ya mfumo mpya wa kibiashara kwa lengo la kuhakikisha inawasaidia vijana kutambua ni jinsi gani wataweza kujikwamua kiuchumi kupitia biashara hiyo.

Akizungumzia mafunzo hayo jijini Dar es Salaam Mkuu wa Kitengo cha fedha kimtandao wa kampuni hiyo Christopher Shayo amesema mafunzo hayo yataendeshwa kwa lugha ya Kiswahili kwa lengo la kuwafikia watu wengi zaidi ili kufikisha elimu hiyo.

Shayo amefafanua mafunzo hayo yanatarajia kuanza rasmi Aprili 17,2019 na kutarajiwa kuwa na wanafunzi wapatao 100 ambao watajisajiri mapema.

Kwa upande wake Mkufunzi wa mafunzo hayo Jimmy James amesema mafunzo hayo yatakavowafikia watu wa mikoani pamoja na nchi zingine kupitia kwenye tovuti za kampuni ya CITL na badae kuwafikia wanafunzi hao na kuendesha mafunzo kikamilifu .

" Fursa hii ni ya kipekee kwani tumefanya tafiti na kugundua asilimia kubwa ya watu bado hawana uelewa kuhusu biashara ya kuuza na kununua fedha kupitia mtandaoni," amesema James.

NCHI HAINA TAZIZO LA MZUNGUKO MDOGO WA FEDHA - DKT. KIJAJI

$
0
0
Na Josephine Majura, WFM, Dodoma

Serikali imesema kuwa kwa sasa nchi haina tatizo la mzunguko mdogo wa fedha katika soko kutokana na hatua mbalimbali ilizozichukua kukabiliana na tatizo hilo ikiwemo kuongeza ukwasi kwenye uchumi.

Hayo yameelezwa leo Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Momba Mhe. David Silinde (Chadema), aliyetaka kujua sababu za mzunguko mdogo wa fedha.

Dkt. Kijaji alisema kuwa, katika kutatua changamoto ya kupungua kwa mzunguko wa fedha katika soko, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilichukua hatua  mbalimbali za kuongeza ukwasi kwenye uchumi ikiwemo kushusha riba ya Benki Kuu (discount rate) kutoka asilimia 16 kwa mwezi Machi, 2017 hadi asilimia 7, Agosti 2018.

“Benki Kuu ilipunguza kiwango cha kisheria cha sehemu ya amana kinachotakiwa kuwekwa Benki Kuu na mabenki ya biashara(Statutory Minimum Reserve Requirement, (SMR)) kutoka asilimia 10 hadi asilimia 8 mwezi April 2017 pamoja na kuruhusu mabenki kutumia asilimia 10.0 ya sehemu ya SMR kama chanzo kimojawapo cha kusaidia hali ya ukwasi kwenye uchumi”, alisema Dkt. Kijaji.

Alisema Benki Kuu ilianzisha utaratibu wa kutoa mikopo ya muda maalumu kwa mabenki pamoja na kununua fedha za kigeni kutoka kwenye soko la jumla la mabenki ili kuongeza ukwasi kwenye uchumi.

Alifafanua kuwa mzunguko wa fedha katika uchumi unaendana na malengo pamoja na mahitaji halisi ya shughuli za kiuchumi zizopo kwa sasa.

Aidha, Dkt. Kijaji alisema Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania inatekeleza Sera ya Fedha inayolenga kusimamia mzunguko wa fedha unaoendana na mahitaji halisi ya uchumi kwa lengo la kudumisha utulivu wa mfumuko wa bei na hivyo kuweka mazingira mazuri ya ukuaji wa uchumi.

Uamuzi wa maombi ya kutaifishwa kwa mali na fedha za Kampuni ya DECI kutolewa Mei 6, mwaka huu

$
0
0
Na Karama Kenyunko, globu ya Jamii.

UAMUZI wa maombi ya kutaifishwa kwa mali na fedha Sh.bilioni 14.1 za iliyokuwa Kampuni ya Development Entrepreneurship for Community Initiative (DECI) kuwa mali ya serikali unatarajiwa kutolewa Mei 6, mwaka huu. Hatua hiyo imekuja baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kupitia Jaji Stephen Magoiga kumaliza kusikiliza hoja za pande zote yaani ule wa Serikali na wa wajibu maombi.

Maombi hayo namba 42 ya mwaka huu yaliwasilishwa mahakamani hapo na Makurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) Biswalo Mganga dhidi ya waliokuwa viongozi wa DECI Jackson Sifael Mtares, Dominick Kigendi, Timotheo Saiguran Ole Loitg’nye na Samwel Sifael Mtares.

Wakati wa usikilizwaji wa maombi hayo, Dpp Mganga katika kuwasilisha hoja zake aliongoza jopo la mawakili watatu wa serikali, wakili wa Serikali Mkuu Poul Kadushi Teophil Mutakyawa na Shadrack Kimaro mawakili wa serikali.

Awali, wakili wa wajibu maombi, Majura Magafu alipinga maombi ya Dpp kwa madai kuwa hakuna ushahidi wa kuthibitisha kama fedha na mali zote za Deci zilitokana na michango ya wanachama (upatu).

Amedai, si kweli kwamba mali za Deci zilipatikana kwa njia isiyo halali kwani kampuni hiyo ilikuwa inafanya kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo watu kwa njia mbalimbali ikiwemo kuwapa mikopo.

Hata hivyo Magafu alipotakiwa kuonyesha  biashara zingine za deci kwa alishindwa kufanya hivyo kwa madai kuwa nyaraka zote zilichukuliwa na polisi wakati ofisi zao zilipovamiwa na kukamatwa wajibu maombi kipindi hicho.

Akiendelea kuwasilisha hoja zake, Magafu amedai, hakuna ushahidi wa  kutosha uliotolewa kuonesha kwamba hizi mali zilipatikana kwa njia ya ujanja ujanja,kitu walichokikubali wakati wa usikilizwaji wa hoja za awali mahakama ya Kisutu  ni kuwa pesa ambazo zipo benki  kama viwanja  na magari vinàmilikiwa na Deci, hakuna sehemu yoyote waliyokiri kwamba mali zile zilipatikana kwa njia isiyo halalai.

Akijibu hoja hizo, DPP amedai kuwa fedha na mali hizo zimethibitika kuwa zilitokana na upatu na ndiyo maana Mahakama ya rufaa katika hukumu yake ilimuelekeza yeye kufungua shauri hilo Mahakama Kuu.

Amedai, Deci haikuwa na shuguli nyingine yoyote  mbali ya kukusanya fedha  na kwamba wajibu maombi hawakuleta ushahidi wa kupinga hilo hivyo   
biashara haramu ya upatu ndiyo ilikuwa kazi yao.

Kuhusu uhusiano wa mali za kanisa na Deci, DPP  amedai kuwa fedha zilizokuwa katika akaunti ya kanisa zilikuwa za Deci kwasababu wakàti huo hawakuwa na akaunti kwa kuwa walikuwa hawajasajiliwa.

Mapema, DPP,  aliwasilisha maombi mahakamani  akiiomba mahakama itoe amri ya kutaifishwa kwa mali za kampuni hiyo yakiwemo magari 11, nyumba na viwanja vinane na fedha ziwe nali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika maombi hayo, DPP anaiomba mahakama hiyo kutoa amri ya kutaifishwa na kuwa mali ya serikali, nyumba namba UKMMD/1237 iliyoko Mwembe Madafu, Ukonga, Dar es Salaam, kiwanja namba 651, kitalu ‘M’ kilichopo Forest area, Mbeya, nyumba iliyoko kiwanja namba 7, kitalu ‘P’  ikiwa na hati namba  033004/23 kilichopo mtaa wa Rufiji, Manispaa ya Mwanza.

Mali nyingine ni ardhi iliyoko katika kiwanja namba 2/283/2 kitalu “E” Mabibo, Kinondoni, Dar es Salaam, kipande cha ardhi ambacho hakijapimwa kilichopo kijiji cha Manyinga, Turiani, Mvomero, Morogoro, kiwanja namba 467 kilichopo kitalu “H” kikiwa na hati ya usajili namba 48170 kilichopo eneo la Tegeta, Dar es Salaam, nyumba iliyoko kiwanja namba MM/19/P kilichopo Manzese karibu na barabara ya Morogoro, Dar es Salaam na nyumba iliyoko katika kiwanja namba KND/MXS/MNM/Z ikiwa na leseni ya makazi namba KND 008337 Kinondoni, Dar es Salaam.

Pia ameomba magari aina ya Toyota Premio lenye namba  T 132 AWJ, Toyota Land Cruiser namba T 480 AUP,   Toyota Rav 4 namba T 274 ATQ, Toyota Mark II namba T 676 AYP, Subaru Legacy namba T 682 AUT, Toyota Ipsum namba T 850 AXY, Toyota Ipsum  T455 ADM, Toyota Mark II T 186 AYX, Mitsubishi Pajero  T 852 AAV, Toyota Lande Cruiser T 789 AUX, Nissan Terrano namba T 899 AYU nayo yataifishwe na kuwa mali ya serikali

Pia, DPP anaomba kutaifishwa kwa fedha zilizoko benki katika akaunti namba 22601601056 iliyoko National Microfinance Bank (NMB), tawi la Msasani  ikiwa n ash. 12,503,068,647.89.

Fedha nyingine taslim ni zilizoko katika akaunti namba 000120100000194/1 iliyoko Dar es Salaam Community Bank (DCB), tawi la Uhuru ikiwa na sh. 1,457,700,462.49 na fedha taslim zilizoko katika akaunti namba 021140019558 iliyoko Kenya Commercial Bank (KCB), tawi la Samora, Dar es Salaam, ikiwa n ash. 57,933,304.10.
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live




Latest Images