Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110153 articles
Browse latest View live

KAMATI YA KUDUMU YA MIUNDOMBINU YA BUNGE YAIELEKEZA WIZARA YA UJENZI KUWASILISHA RIPOTI MATUMIZI YA FEDHA ILIYOWEKEZWA KATIKA MRADI WA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA 

KAMATI ya kudumu ya miundombinu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeielekeza wizara ya ujenzi kuwasilisha majibu ya msingi ya kimaandishi kuhusu matumizi ya fedha iliyowekezwa katika mradi wa mfumo wa anwani za makazi na postikodi. 

Aidha imeomba serikali iwekeze fedha ya kutosha kwenye mradi huo ambao utasaidia kutoa utambuzi katika maeneo husika na wageni kukuta miundombinu mizuri hasa ya mawasiliano. 

Akitoa maelekezo hayo, mwenyekiti wa kamati hiyo, Suleimani Kakoso wakati kamati ilipotembelea na kukagua miundombinu ya mfumo wa anwani za makazi na postikodi kata ya Tumbi, Kibaha mkoani Pwani, alisema ingefaa kuboreshwa katika raslimali fedha ili uweze kufanyiwa kazi haraka. 

Alifafanua, ripoti itakayowasilishwa na kueleza kinaga ubaga kuhusu mapato na matumizi itairahisishia kamati kujua changamoto zilizopo na wapi waongeze msukumo kwa lengo la kufanikisha utekelezaji wa mradi. 


Pamoja na hayo, Kakoso ameitaka jamii ilinde miundombinu iliyopo katika miradi mbalimbali inayowekezwa na serikali kwani nguzo moja inayojengwa katika mradi huo inagharimu sh. 156,000 gharama ambayo ni kubwa.

Nae naibu waziri wa ujenzi ,uchukuzi na mawasiliano, Elias Kuandikwa alisema, mradi utarahisisha ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo mbalimbali nchini.

Kuandikwa alielezea, mfumo huo wa anwani za makazi utaiwezesha Serikali kuwahudumia wananchi wake kirahisi ikiwa ni pamoja na kutoa ulinzi, kurahisisha mawasiliano miongoni mwa wananchi na Serikali.

Naibu katibu mkuu, wizara ya ujenzi, uchukuzi na mawasiliano (MAWASILIANO) dkt. Jim Yonazi aliongeza kuwa ,katika nchi nyingi za viwanda na nchi zilizoendelea suala la miundombinu ikiwemo mfumo huo ni muhimu na linaeleweka kwa kila mtu katika kuanzisha, kukuza na kuendeleza uchumi wa viwanda.

Alisema, mfumo una mahitaji makuu matatu ikiwemo nguzo zilizosimikwa kwenye barabara zenye majina, vibao vilivyobandikwa kwenye nyumba /jengo na postikadi limekamilika kila kata/wadi inapostikadi yake.

"Unaweza kupata postikadi ya kata yoyote kupitia simu yako ya mkononi kwa kupiga *152*00#chagua 3 (ajira na utambuzi)"alifafanua dkt. Yonazi. 

Mkandarasi na mkuu wa chuo cha ufundi (VETA) Dodoma ,Ramadhani Mataka alisema wanaendelea na kazi vizuri na faida wanayoitoa ni ajira pamoja na kulipa kodi serikali na walishatoa mil 2.8 kulipa kodi. 

Kwa upande wake, msimamizi wa mradiambae pia ni mhandisi mkurugenzi wa huduma ya mawasiliano wizara ya ujenzi, Clarence Ichwekeleza, anasema wametekeleza mradi katika kata 112.

Alieleza wamepokea bilioni mbili ambapo bilioni 1.2 awamu ya kwanza na awamu ya pili sh. milioni 727.




MSAADA WA CHAKULA.DAWA NA VIFAA VYA KUJIHIFADHI VYAWASILI HARARE,ZIMBABWE.

$
0
0
Msaada wa Chakula, Dawa na vifaa vya kujihifadhi umewasili Harare nchini Zimbabwe baada ya kupelekwa na ndege za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania {JWTZ} kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa maafa yaliyosababishwa na kimbunga Idai  ambacho kimeikumba sehemu ya nchi hiyo.

Pamoja na kusababisha mafuriko, vifo na maelfu ya kaya kukosa makazi, kimbunga hicho kimesababisha kaya nyingi kuhitaji chakula, dawa na mahali pa kujihifadhi kwa haraka.

Nchi nyingine zilizokumbwa na kimbunga hicho ni Msumbiji na Malawi ambako maelfu ya watu wamepoteza maisha na mamilioni kukosa makazi.

Jana Machi 19, 2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alitoa msaada wa tani 214 za chakula, Dawa tani 24 na vifaa vya kujihifadhi vikiwemo blanketi, shuka, vyandarua na magodoro ambavyo vilipelekwa katika nchi hizo kwa ndege na Malori ya Jeshi.

 

MHE. BALOZI MAKILA JAMES ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA, WASHINGTON, D.C

$
0
0
Mhe. Balozi Makila James, Naibu Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki na Sudan alimtembelea Mhe. Balozi Wilson Masilingi na kufanya mazungumzo kuhusu kuendeleza kuimarisha mahusiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nchi rafiki ya Marekani.
 
Mhe. Wilson Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Marekani na Mexico akiwa na Mhe. Balozi Makila James, Naibu Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki na Sudan.
Mhe. Wilson Masilingi, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Marekani na Mexico akiwa na Mhe. Balozi Makila James (Deputy Assistant Secretary of State for East Africa and the Sudans) na Bw. Michael Fraser Msaidizi wake, katika picha ya pamoja na maafisa wa Ubalozi Bw. Dismas Assenga, Brigedia Jenerali Adolph Mutta, Bi. Swahiba Mndeme, Bi. Jean Msabila na Bw. Mugendi Zoka.

DID YOU KNOW THESE THINGS HAD NAMES?

$
0
0

1. The space between your eyebrows is called
a glabella.
2. The way it smells after the rain is called
petrichor.
3. The plastic or metallic coating at the end of your shoelaces is called an aglet.
4. The rumbling of stomach is actually called a wamble.
5. The cry of a new born baby is called a vagitus.
6. The prongs on a fork are called tines.
7. The sheen or light that you see when you close your eyes and press your hands on them is called phosphenes.
8. The tiny plastic table placed in the middle of a pizza box is called a box tent.
9. The day after tomorrow is called
overmorrow.
10. Your tiny toe or finger is called minimus.
11. The wired cage that holds the cork in a bottle of champagne is called an agraffe.
12. The 'na na na' and 'la la la', which don't really have any meaning in the lyrics of any song, are called vocables.
13. When you combine an exclamation mark with a question mark (like this ?!), it is referred
to as an interrobang.
14. The space between your nostrils is called columella nasi.
15. The armhole in clothes, where the sleeves are sewn, is called armscye.
16. The condition of finding it difficult to get out of the bed in the morning is called dysania.
17. Unreadable hand -writing is called griffonage.
18. The dot over an “i” or a “j” is called tittle.
19. That utterly sick feeling you get after eating or drinking too much is called crapulence.
20. The metallic device used to measure your
feet at the shoe store is called Bannock device.

HOW MANY OF THE ABOVE DID YOU ALREADY KNOW? HAHA HAHAAAA!

ELIMU MUHIMU KWA UHIFADHI : JE WAJUA ADHABU NA FAINI YA KUGONGA WANYAMAPORI HIFADHINI?.

$
0
0

Muhimu kufahamu kwamba adhabu na faini ya 
kugonga wanyamapori  hifadhini

1: Tembo = USD  15,000 au shilingi Milioni 34.6
2: Twiga = USD 15,000 au shilingi Milioni 34.6
3: Simba = USD 4,900 au shilingi Milioni  11.3
4: Chui = USD 3,500 au shilingi Milioni 8
5: Nyati =USD 1900 sawa na shilingi milioni 4.2
6 :Pundamilia = USD 1200 au shilingi milioni 2.7
7: Fisi = USD 550 au shilingi milioni 1.2
8: Ngiri = USD 450 au shilingi milioni 1
9: Swala = USD 390 au shilingi Laki 9
10: Nyani = USD 110 au shilingi Laki 254

11: Ukipata ajali hifadhini shilingi 200,000 na ukizidisha 
mwendo faini yake shilingi 30,000

Ni muhimu kuwa na tahadhari pindi uingiapo au upitapo
 kwenye maeneo ya hifadhi,  Day speed ni 70km/h na 
night speed ni 50km/h.

Kuwa makini, chukua tahadhari!

SHIRIKA LA MCT LAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI

$
0
0

Shirika la Miracle Corners Tanzania(MCT) kwa kushirikiana na Kampuni ya Colgate Palmolive na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Vyuo vya Tabibu Meno (Mbeya na Tanga) wameadhimisha siku ya afya ya kinywa na meno Duniani.
Maadhimisho haya huadhimishwa kote duniani kila ifikapo tarehe 20 mwezi Machi kila Mwaka. Kwa mara ya kwanza maadhimisho haya yalianza kuadhimishwa nchini Tanzania mwaka 2014 katika mkoa wa Dar es Salaam.
Kila maadhimisho hubeba kauli mbiu yake ambayo hutumika kuhamasisha watu kutunza afya ya kinywa na meno,ambapo
Kauli Mbiu ya mwaka huu ni “Sema Ahh :Chukua hatua zinazozingatia afya ya kinywa na meno”.
Maadhimisho haya yameadhimishwa kwenye mikoa miwili ya Mbeya na Tanga ambako Shirika la MCT linafanya kazi zinazolenga afya ya kinywa na meno.
Madhumuni ya maadhimisho hayo ni kutoa elimu ya afya ya kinywa na meno, uchunguzi wa kinywa na meno, kupunguza uwezekano wa meno kuharibika kwa kupaka dawa ya floridi pamoja na kugawa dawa za meno na miswaki kwa wanafunzi wa shule za msingi.
Katika kuadhimisha siku ya Afya ya Kinywa na Meno Duniani, Shirika la MCT limetoa elimu na huduma ya afya ya kinywa na meno zoezi ambalo lilifanyika siku ya Jumatatu hadi Jumatano jijini Tanga na Mbeya.
Kupitia zoezi hilo jumla ya watu 1,226 wakiwemo watu wazima na wanafunzi wa shule za msingi katika jiji la Tanga walifikiwa huku Jumla ya wanafunzi 246 wa shule za msingi jijini Mbeya wamepatiwa huduma siku ya kilele cha maadhimisho tarehe 20 mwezi Machi,2019.
Wataalam mbalimbali wa huduma za afya ya kinywa na meno ikiwa ni pamoja na wanafunzi walio katika mafunzo kwa vitendo kutoka Vyuo vya Tabibu wa meno vilivyopo Tanga na Mbeya wakisimamiwa na wakufunzi wao wameshiriki maadhimisho haya.
Aidha MCT pia imetoa elimu ya afya ya kinywa na meno kupitia vyombo mbalimbali vya habari zikiwemo radio na vituo vya televisheni ambavyo ni Radio Free Africa, Baraka FM, Sweet FM, Bomba FM, TK FM na Tanga Television.
Wanafunzi pamoja na wakufunzi wao kutoka katika chuo cha Tabibu meno Tanga wakiwa katika maadhimisho ya siku ya afya ya kinywa na meno duniani.
Uchunguzi wa kinywa na meno ukiendelea.
Uchunguzi pamoja na matibabu yakiendelea – Tanga.
Wanafunzi wakipata elimu zaidi juu ya afya ya kinywa na meno.
Joseph Haule ambaye ni mwanafunzi aliyepo katika mafunzo kwa vitendo kutoka Chuo cha Tabibu Meno Mbeya akionyesha njia sahihi ya kupigwa mswaki.
Joseph Haule akiendelea kutoa maelezo kuhusu upigaji sahihi wa mswaki.
Mwanafunzi akionesha njia sahihi ya kupiga mswaki baada kupata elimu.
Wanafunzi wakifurahia zawadi ya dawa ya meno na mswaki kutoka Kampuni ya Colgate Palmolive.
Wa kwanza kushoto ni Mkufunzi kutoka Chuo cha Tabibu Meno Tanga,Dkt. Digna Komba akifuatiwa na Mratibu wa afya ya Kinywa na meno jiji la Tanga Dkt. Gideon Joshua na Afisa Mradi wa MCT mkoa wa Tanga,Sara Mtagwa wakitoa elimu ya kinywa na meno kwa njia ya Radio TK Fm mkoani Tanga.
Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Idara ya kinywa na meno hospitali ya Kanda ya Rufaa Mbeya - Dkt. Hery Mwakayoka, akifuatiwa na Afisa Mradi kutoka MCT - Fredrick Meena, Meneja wa Shirika la MCT - Jane Shuma na Mkuu wa Chuo Tabibu Meno Mbeya - Dkt. Ibrahim Kasambala (wa kwanza kulia) baada ya kumaliza kutoa elimu ya afya ya kinywa na meno kupitia Radio Sweet Fm Mbeya.
Picha ya pamoja ya washiriki wa maadhimisho ya siku ya afya ya kinywa na meno duniani - Mbeya.
Wanafunzi wa Chuo cha Tabibu Meno mkoani Tanga pamoja na wanafunzi wa shule za msingi.
Wanafunzi walio katika mafunzo kwa vitendo kutoka Chuo cha Tabibu Meno mkoani Mbeya wakiwa katika picha ya pamoja.

KANGI LUGOLA AFANYA ZIARA YA KIKAZI GEREZA MAHABUSU SEGEREA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola (wa kwanza kushoto) akikaribishwa na Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike(kulia) nje ya viwanja vya Gereza la Mahabusu Segerea. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani Meja Jenerali Jacob Kingu.

 Afisa wa zamu wa Gereza la Mahabusu Segerea, Mkaguzi Ambrose Kasanga (wa tatu kushoto) akimpa taarifa ya Gereza Waziri Kangi Lugola

 Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Mkuu wa Gereza Segerea.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola(wa pili kulia) akikagua jengo la zahanati ya ndani ya Gereza ambalo liko kwenye hatua za mwisho za ujenzi.

Waziri Kangi Lugola akifanya mazungumzo na baadhi ya Mahabusu Ndani ya Gereza la Segerea.

VOA SAHILI: Duniani Leo March, 20th 2019


BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO 20.03.2019

TANGAZO LA AJIRA SHULE YA SEKONDARI BULUBA

$
0
0
EMPLOYMENT  OPPORTUNITY                                                   

Buluba Secondary School (BSS) is a Private school owned by SHIRECU (1984) LTD Shinyanga Region Cooperative Union. Currently the school is offering Advanced level and Ordinary level education with almost ten combinations for advanced level. The School is located at Shinyanga with almost 500 students both advanced and ordinary level students. SHIRECU (1984) LTD the owner of the school is therefore looking for the competent and experienced headmaster/headmistress to lead the school.

INTRODUCTION

·         Job Title: Headmaster/Headmistress

·         Department: Administration

·         Report to: SHIRECU(1984) General Manager

MAIN PURPOSE

To lead the school and maintain discipline among student and teachers in order for the school to achieve better performance.

PERSONALATTRIBUTES

·         Team player with the ability to work independently

·         High level of integrity, honesty and sense of responsibility

·         Self motivated and able to endure long working hours in new  challenging environments

·         Committed to deliver work ofa high quality that meet and exceed industry standards

·         High level administrativekills

·         Demonstrate high level of customer cares kills

ROLES AND RESPONSIBILITIES:

A) ADMINISTRATION AND FINANCE

·         The reporting of maintenance needs in his/her section of the school plant to the General Manager and ensure that his/her section of the School buildings, its furniture and fixtures, office equipment, playgrounds, school garden and other properties are properly and carefully maintained.

·         Monitor staff attendance on a daily and monthly basis.

·         With the other members of the Executive Committee, to be responsible for all employees in his/her section of the school in accordance with the rules laid down by the Governing Council.

·         At the time of handing over charge, the headmaster/headmistress/ shall prepare detailed “handing over notes” and a report aimed at a complete orientation to the incumbent.

B) EDUCATION PLANNING AND IMPLEMENTATION

Be responsible for:

·         Preparation of the School timetable through the academic office, allocation of duties and teaching load of the teachers in his/her section.

·         Providing necessary facilities to the teachers in his/her section in the discharge of their duties.

·         Discipline in his/her particular section of the school, in consultation with the General Manager.

·         Plan the year’s academic work in consultation with the staff and hold staff meetings at least once a month to (inter alia) review the work done during the month and assess the progress of the students.

·         Supervise classroom teaching and secure co-operation and coordination amongst teachers of the same subject areas as well as inter subject co-ordination.

·         Plan and specify a regular timetable for the scrutiny of student’s written work and home assignments and ensure that the assessment and corrections are carried out effectively and on time.

·         Monitor and regulate students discipline together with teachers as well

·         Develop and organize the Library resources and reading facilities in his/ her section of the school and ensure that the students and teachers have access to books and journals of established value and usefulness.

·         Ensure that a growing social awareness (concern and compassion for others in need) is developed in the students, through on-going, planned outreach programmers’.

·         Send the progress reports of the students regularly to the parents or guardians.

·         Send an Annual Report of his/her section to the General Manager to appraise him of achievements and challenges, and areas of needed support in his/her section of the school.

C) HUMAN RELATIONS DEVELOPMENT

·         Help and guide teachers to promote their professional growth, and towards this end actively encourage their participation in courses designed for in-service training and development. This should be done in consultation with the Principal and the Executive Committee.

·         Communicate and reinforce school values, beliefs and objectives frequently to staff, students and parents.

·         Encourage opportunities for communication between and among staff, students and parents through regular meetings.

·         Be responsible for his/her own professional and personal development by availing of relevant resource opportunities which will expose him/ her to the new trends in education, school management, communication and personal skill development.

·         Motivate, guide and supervise the work of the teaching staff of the school.

D) POLICY / PLANNING

·         In consultation with the General Manager and School Board, develop and document an Annual Plan for his/her section of the school which must reflect the overall school vision and mission and ensure staff participation in and ownership of the plan.

QUALIFICATION AND EXPERIENCE:

We are looking for a graduate candidate with a background in:

·         Bachelor degree in Education from any recognized University.

·         His/her should have an experience of almost 5 five years in managerial position mostly as a headmaster/headmistress.

·         His/her should be not less than 35 years of age.

APPLICATION INSTRUCTIONS

Submit your application letter together with an updated CV to

General Manager,

Shinyanga Region Cooperative Union-SHIRECU (1984) LTD

P.O. Box 349, Shinyanga

Apply through:Shireculimited@yahoo.com

REMUNERATION

The post carries an attractive remuneration and fringe benefits , according to Buluba Secondary School Scheme of Service.

APPLICATION DEADLINE:

Sunday, the 11st of APRIL 2019 at 17:00pm

Location: Shinyanga Town

Postal Address: P.O. Box 349, Shinyanga

TEL/FAX 255282762525

Email: Shireculimited@yahoo.com

 

MAANDALIZI YA TAIFA STARS YANOGA

HABARI ZA UMOJA WA MATAIFA KUTOKA NEW YORK, MAREKANI

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MACHI 21, 2019

SIKU MWALIMU NYERERE NA MZEE KARUME WAKIPOKUWA MAREFA WA MPIRA WA MIGUU

WANANCHI WAONYWA KUTOTUMIA VIBAYA MATAMKO YA RAIS WA NCHI, KUKWEPA KODI

$
0
0
Na. Edward Kondela

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amewataka wananchi hususan wafugaji kutotumia matamko ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli vibaya kwa kutafuta mianya ya kutolipa kodi.

Prof. Gabriel amebainisha hayo akiwa katika mnada wa upili wa Meserani uliopo wilaya ya Monduli Mkoani Arusha mara baada ya kufanya ziara ya kukagua utendaji kazi wa watumishi waliopo katika mnada huo na kusikiliza kero za wafugaji.

Akizungumza na wananchi mara baada ya kufanya ziara hiyo Prof. Gabriel amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika kipindi cha mwezi mmoja itashirikiana na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli kutoa tafsiri sahihi ya mfanyabiashara mdogo anayestahili kukatiwa kitambulisho cha biashara ndogo ndogo (machinga) cha Shilingi Elfu Ishirini kwa mwaka, kilichotolewa na Rais Magufuli kutokana baadhi ya wafugaji kutaka kufahamu endapo wanastahili kupatiwa vitambulisho.

“Mheshimiwa rais alikuwa amelenga hasa wale wafanyabiashara wadogo wadogo na tunachoamini tutaendelea kulifanyia kazi lakini suala la machinga kwamba naye mfanyabiashara wa ng’ombe kuhusishwa katika sifa za mfanyabiashara ndogondogo bado ni gumu kulitolea majibu, lakini ushauri tusitumie matamko ya rais vibaya tusitafute kichaka cha kujificha kwamba nawe ni machinga, wewe mwenyewe fikiria na jitafakari tulipe kodi na tujenge nchi yetu.” Alisema Prof. Gabriel

Akizungumza na wafugaji hao Prof. Gabriel amepokea kilio cha wafugaji kuwa wamekuwa wakiuza ng’ombe kwa makadirio au matakwa ya mnunuzi kutokana na kutokuwepo kwa mizani ili waweze kuuza ng’ombe kwa kilo badala ya bei ya kukadiria kati ya mfugaji na mnunuzi wa ng’ombe, kitendo ambacho wafugaji hao wamesema kimekuwa kikiwafanya wasiuze mifugo yao kwa bei yenye tija kwao.

“Lengo letu ni kuhakikisha minada yote hasa ya upili na ile ya mipakani inatumia mizani, mnada wa Kimesera mzani wake uko tayari unatakiwa kufanyiwa marekebisho ili kuondokana na bei ya kukisia katika kipindi cha mwezi mmoja.” Alisema Prof. Gabriel

Aidha katibu mkuu huyo, amewataka wafugaji kufuga kisasa kwa kuhakikisha wanawapatia ng’ombe malisho bora ili wapate mazao bora ya mifugo yao huku Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikihakikisha inaendelea kuimarisha matibabu ili mifugo iwe na afya bora.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema pia licha ya uwepo wa masoko ya mifugo hususan ng’ombe hapa nchini, wizara inajikita katika kutafuta masoko ya mifugo nje ya nchi.

“Tunachoangalia hivi sasa ni kuangalia na masoko ya nje ya nchi lakini hauwezi kuuza ng’ombe nje ya nchi ambaye hana afya bora na tunaamini tukiendelea hivi hata mchango wetu wa wizara kwenye uchumi wa viwanda utakuwa ni mzuri.” Alisema Prof. Gabriel

Naye Bw. Kandidi Mlinyi ambaye ni msimamizi wa mnada wa Meserani amesema kuwa wamekuwa wakikumbwa na changamoto ya upatikanaji wa maji katika ukanda wa Wilaya ya Monduli hivyo kuwa na mazingira magumu ya upatikanaji wa huduma hiyo mnadani.

Kauli hiyo imeungwa mkono na baadhi ya wafugaji ambao wamesema ng’ombe wanaposafirishwa kutoka maeneo mbalimbali kuja katika mnada huo, kwa wastani wanakunywa maji lita 20 hadi 60 lakini kutokana na ukosefu wa maji ng’ombe wanakuwa katika mazingira magumu hali inayosababisha ng’ombe hao kuchoka kwa kuwa wanapoteza maji mengi mwilini.

Katika ziara hiyo ya Katibu Mkuu Prof. Gabriel wafugaji wamepongeza utendaji kazi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuwa viongozi na watendaji wa wizara wamekuwa wakifika mara kwa mara kwa wananchi wakiwemo wafugaji ili kutatua kero zao.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika uongozi wa mnada wa Meserani kwa siku zaidi ya ng’ombe 500 huuzwa na kusafirishwa kwenda katika mikoa mbalimbali wakati wa msimu ambao unakuwa na ng’ombe wengi kuanzia mwezi Machi hadi Julai kila mwaka.
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gariel akikagua ubora wa baadhi ya ng'ombe waliofikishwa katika mnada wa Meserani.
 Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel (kulia) akiwa kwenye mazungumzo na baadhi ya wafugaji kwenye mnada wa Meserani.
 Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel akiongozana na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa wizara hiyo Dkt. Felix Nandonde (aliyevaa suti) katika mnada wa Meserani

MRADI WA MAJI WA BILIONI 15.8 KUKAMILIKA HIVI KARIBUNI LONGIDO

$
0
0

Baadhi ya wakinamama kutoka kijiji cha kijiji cha Engikaretia wilayani Longido  wanavyoonekana wakiteka maji 

Na. Vero Ignatus, Longido

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Uvuvi na mifugo na Maji imetembelea na kukagua mradi ya maji mji mdogo wa Longido ili kuona umefikia hatua gani kimaendeleo

Akisoma ripoti ya maendeleo ya mradi huo Mkurugenzi wa AUWSA Jijini Arusha Mhandisi Ruth Koya amesema kuwa serikali kupitia wizara ya maji na umwagiliaji inatekeleza mradi wa maji safi na salama katika mji mdogo wa Longido ambapo chanzo chake ni mto Simba uliopo Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro

Amesema mradi huo unategemewa kugarimu kiasi cha shilingi Bilioni 15.8 ambapo hadi sasa kiasi cha shilingi bilioni 12.3 kimeshalipwa kwa mkandarasi. 

Mhandisi Koya amesema kuwa lengo kuu la mradi ni kuongeza upatikanaji wa maji katika mji mdogo wa Longido kutoka 15%za sasa ambazo ni sawa na wakazi 2, 510 hadi kufikia 100%sawa na wakazi. 16 712 ambapo kiasi hicho kitatosheleza kwa 100% hadi kufikia wakazi 26,145 mwaka 2025

Ameiambia kamati hiyo ya Bunge kuwa mradi huo unauwezo wa kuzalisha kiasi cha lita za ujazo 2,160 kwa siku na mahitaji ya maji ni lita za ujazo 1462 hivyo itaongeza upatikanaji wa huduma ya  maji katika mji mdogo wa Longido wenye jumla ya wakazi 16, 712 kwa sasa, na kufikia wakazi 26, 145 kwa mwaka 2025

Aidha amesema kuwa mradi huo utaondoa magonjwa yanayosababishwa na ukosefu wa maji safi na salama kwa kijiji cha Engikaretia mbapo utahudumia wakazi wapatao 1294

Kwa upande wake mwenyekiti wa Kamati uya kudumu ya bunge ya Uvuvi, Mifugo na Maji  Mahmoud Mgimwa amesema kuwa mradi huo unapokamilika siyo wa serikali bali wenye jukumu la kuutunza na kuulinda ni wananchi wa Longido. 

Amewahakikishia wananchi hao kuwa tayari kamati hiyo imeshazungumza na serikali kuwa ifikapo machi 30 mwaka huu mradi huo utakuwa umeshakamilika na kwamba watarudi tena kwenda kuhakikisha kama kuna mgao wa maji katika maeneo yao. 

'' Leo tumekuja kukagua na kuona tumefikia kwa asilimia ngapi, na mkiona kuna uharibifu wa aina yeyote na nyie mkaa kimya na nyie mtakuwa sehemu ya uharibifu''alisema Katibu huyo
Aidha Kamati hiyo ya Kudumu ya Bunge imemuagiza DC wa Longido pale atakapoona uharibifu wowote kwenye eneo la mradi kuwachukulia hatua za kisheria watu wote waliopo eneo hilo.

 Akizungumza bi Lucy Martini mkazi wa Longido ameiomba kamati hiyo kuhakikisha mradi huo uwe unatoa maji mara zote isijeikawa ni kwa siku moja tu halafu hapo baadae tatizo la. Maji likarudi palepale. 
 Mkurugenzi wa AUWSA jijini Arusha akitoa taarifa ya mradi wa maji mji mdogo wa Longido kwa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Uvuvi, Mifugo na Maji leo wilayani Longido. 
Mkurugenzi wa AUWSA jijini Arusha Mhandisi Ruth Koya akiwa na Katibu wa Kamati ya Bunge ya Uvuvi, Mifugo na Maji 
Mradi wa maji katika kijiji cha Engikaretia kilichopo mji mdogo wa Longido utakaogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 15.8 ambapo hadi sasa tayari makandarasi ameshalipwa shilingi bilioni 12.3 
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Uvivu, Mifugo na maji akizungumza na wananchi mji mdogo wa Longido leo,kushoto kwake ni Kaimu katibu mkuu wizara ya maji Emmanuel Kalobelo naibu katibu Mkuu Wizara ya maji  mradi Emmanuel Kalobelo. Picha na Vero Ignatus.
Mkuu wa wilaya ya Longido akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akinamama waliokuja kuteka maji katika kijiji cha Engikaretia mji mdogo wa Longido leo Picha zote na Vero Ignatus 

SHIRIKA LA MCT LAADHIMISHA SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI

$
0
0

Shirika la Miracle Corners Tanzania(MCT) kwa kushirikiana na Kampuni ya Colgate Palmolive na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Vyuo vya Tabibu Meno (Mbeya na Tanga) wameadhimisha siku ya afya ya kinywa na meno Duniani.

Maadhimisho haya huadhimishwa kote duniani kila ifikapo tarehe 20 mwezi Machi kila Mwaka. Kwa mara ya kwanza maadhimisho haya yalianza kuadhimishwa nchini Tanzania mwaka 2014 katika mkoa wa Dar es Salaam.
Kila maadhimisho hubeba kauli mbiu yake ambayo hutumika kuhamasisha watu kutunza afya ya kinywa na meno,ambapo Kauli Mbiu ya mwaka huu ni “Sema Ahh :Chukua hatua zinazozingatia afya ya kinywa na meno”.

Maadhimisho haya yameadhimishwa kwenye mikoa miwili ya Mbeya na Tanga ambako Shirika la MCT linafanya kazi zinazolenga afya ya kinywa na meno.Madhumuni ya maadhimisho hayo ni kutoa elimu ya afya ya kinywa na meno, uchunguzi wa kinywa na meno, kupunguza uwezekano wa meno kuharibika kwa kupaka dawa ya floridi pamoja na kugawa dawa za meno na miswaki kwa wanafunzi wa shule za msingi.

Katika kuadhimisha siku ya Afya ya Kinywa na Meno Duniani, Shirika la MCT limetoa elimu na huduma ya afya ya kinywa na meno zoezi ambalo lilifanyika siku ya Jumatatu hadi Jumatano jijini Tanga na Mbeya.

Kupitia zoezi hilo jumla ya watu 1,226 wakiwemo watu wazima na wanafunzi wa shule za msingi katika jiji la Tanga walifikiwa huku Jumla ya wanafunzi 246 wa shule za msingi jijini Mbeya wamepatiwa huduma siku ya kilele cha maadhimisho tarehe 20 mwezi Machi,2019.

Wataalam mbalimbali wa huduma za afya ya kinywa na meno ikiwa ni pamoja na wanafunzi walio katika mafunzo kwa vitendo kutoka Vyuo vya Tabibu wa meno vilivyopo Tanga na Mbeya wakisimamiwa na wakufunzi wao wameshiriki maadhimisho haya.

Aidha MCT pia imetoa elimu ya afya ya kinywa na meno kupitia vyombo mbalimbali vya habari zikiwemo radio na vituo vya televisheni ambavyo ni Radio Free Africa, Baraka FM, Sweet FM, Bomba FM, TK FM na Tanga Television.
Wanafunzi pamoja na wakufunzi wao kutoka katika chuo cha Tabibu meno Tanga wakiwa katika maadhimisho ya siku ya afya ya kinywa na meno duniani.
Uchunguzi wa kinywa na meno ukiendelea.
Uchunguzi pamoja na matibabu yakiendelea – Tanga.
Wanafunzi wakipata elimu zaidi juu ya afya ya kinywa na meno.
Joseph Haule ambaye ni mwanafunzi aliyepo katika mafunzo kwa vitendo kutoka Chuo cha Tabibu Meno Mbeya akionyesha njia sahihi ya kupigwa mswaki.
Joseph Haule akiendelea kutoa maelezo kuhusu upigaji sahihi wa mswaki.
Mwanafunzi akionesha njia sahihi ya kupiga mswaki baada kupata elimu.
Wanafunzi wakifurahia zawadi ya dawa ya meno na mswaki kutoka Kampuni ya Colgate Palmolive.
Wa kwanza kushoto ni Mkufunzi kutoka Chuo cha Tabibu Meno Tanga,Dkt. Digna Komba akifuatiwa na Mratibu wa afya ya Kinywa na meno jiji la Tanga Dkt. Gideon Joshua na Afisa Mradi wa MCT mkoa wa Tanga,Sara Mtagwa wakitoa elimu ya kinywa na meno kwa njia ya Radio TK Fm mkoani Tanga.
Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Idara ya kinywa na meno hospitali ya Kanda ya Rufaa Mbeya - Dkt. Hery Mwakayoka, akifuatiwa na Afisa Mradi kutoka MCT - Fredrick Meena, Meneja wa Shirika la MCT - Jane Shuma na Mkuu wa Chuo Tabibu Meno Mbeya - Dkt. Ibrahim Kasambala (wa kwanza kulia) baada ya kumaliza kutoa elimu ya afya ya kinywa na meno kupitia Radio Sweet Fm Mbeya.
Picha ya pamoja ya washiriki wa maadhimisho ya siku ya afya ya kinywa na meno duniani - Mbeya.
Wanafunzi wa Chuo cha Tabibu Meno mkoani Tanga pamoja na wanafunzi wa shule za msingi.
Wanafunzi walio katika mafunzo kwa vitendo kutoka Chuo cha Tabibu Meno mkoani Mbeya wakiwa katika picha ya pamoja.

WAFUGAJI TUMIENI MBEGU ZINAZOZALISHWA NAIC KUPATA NG'OMBE WENYE UBORA ZAIDI

$
0
0


Na Vero Ignatus, Arusha

KATIBU Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Elisante Ole Gabriel ameagiza halmashauri zote nchini kutoa elimu kwa wafugaji umuhimu wa utumiaji mbegu bora zinazozalishwa kituo cha Taifa cha Uhimilishaji mifugo kwa njia ya chupa NAIC kilichopo Wilayani Arumeru,Mkoani hapa.

Ametoa agizo katika ziara ya kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo,Mifugo na Maji, ambapo Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega, ambapo Prof.Gabriel amesema ni kufuatia uwepo wa mwamko mdogo wa wafugaji katika utumiaji mbegu hizo.

Amesema kuwa ili kuendana na uchumi wa viwanda ni lazima wafugaji nchi wabadilike na kutumia mbegu hizo ili kupata Ng'ombe wenye nyama bora,maziwa,ngozi na Kwato watakazokidhi malighafi za viwanda.

Prof.Ole Gabriel amesema kwa kipindi cha mwaka jana waliweza kutoa mafunzo kwa wafugaji 58,000 kwa nchi nzima hali iliyosababisha kuzalisha Ndama 10,000 pekee licha ya kituo hicho kuzalisha mbegu 60,000 kwa wiki.

"Idadi ya wagufaji waliopewa elimu ni ndogo na mwitikio wa utumiaji mbegu hizi hauridhishi kwa wafugaji wetu wakati kituo kinazalisha mbegu za kutosha kwa mahitaji ya wafugaji wote nchini,hivyo nawaagiza wataalamu wote watoke ofisini waende kwa wafugaji kutoa elimu juu ya utumiaji mbegu hizi,"alisema

Aidha alitumia nafasi hiyo kuwataka wafugaji kuondokana na dhana potofu kwakutumia mbegu hizo ni kuharibu vizazi vya ng'ombe jambo ambalo sio sahihi ni kukinzana na maendeleo katika sekta ya ufugaji.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega kuwa hali ya usambazaji wa mbegu hizo kwenye vituo vilivyopo kanda saba nchini hauridhishi kutokana na baadhi ya waataalamu kutotimiza wajibu wao wa utoaji elimu kwa wafugaji.

"Serikali inauza mbegu hizi kwa ruzuku ili wafugaji wasiokuwa na uwezo waweze kumudu gharama ya Sh.5000,lakini kuna baadhi ya wataalamu wananunua mbegu hizi na kuziuuza kwa bei kubwa kati ya Sh.15,000 na Sh.40,000,"alisema

Ametoa wito kwa wafanyabiashara binafsi wa mbegu za chupa kuacha kuagiza mbegu hizo nje ya nchi na kuuzia wafugaji mbegu hizo kati ya Sh.50,000 hadi 100,000.Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bungeya Kilimo,Mifugo na Mjai,Mahmoud Mgimwa alisema utumiajo wa mbegu hizo utawezesha wafugaji kufuga kwa tija na kupata soko la uhakika la bidhaa za mifugo yao.

"Kikubwa hapa wafugaji wabadilike kutoka kwenye ufugaji wa maea na kufuga kisasa kwa kutumia mbegu hizi za NAIC ili tushiriki uzalishaji wa malighafi za Viwanda vyetu vinavyoanzishwa kwa wingi nchini,"alisema.

Hadi sasa kiruo hicho kina madume 28 ya aina zofuatavyo katika kituo hicho NAIC.Ng'ombe wa maziwa Ayrshine 6,Friesian7 na Jersey 2.Ngombe wa maziwa na nyama (Dual porpose) Simmental 2 na Mpwapwa 4,Ng'ombe wa nyama, Boran 4 na Binsmara2 na Teaser bull 1.

Ngombe aliyeko tayari kwa ajili ya Uhamilishaji katika kituo cha NAIC
KATIBU Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Elisante Ole Gabriel ameagiza halmashauri zote nchini kutoa elimu kwa wafugaji ili waweze kupata ngombe bora wa nyama, maziwa na ufugaji wenye tija
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza na waandishi wa habari katika kutuo cha NAIC kilichopo Usariver Mkoani Arusha
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bungeya Kilimo,Mifugo na Mjai,Mahmoud Mgimwa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo,Mifugo na Maji waliotembelea katika kituo hicho kujionea jinsi uhamilishaji
Baadhi ya ng'ombe walipo katika kituo cha NAIC kwajili ya Uhimilishaji. Picha na Vero Ignatus.

Introducing "NAFUU" by Lomodo Ft Baraka The Prince

Waziri Kabudi afanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu nchini

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mhe. Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi alipomtembelea katika ofisi ndogo za Wizara zilizopo Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Machi 2019. Mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili masuala mbalimbali ya namna ya kudumisha na kukuza uhusiano baina ya Tanzania na UAE.     
Waziri Mhe. Kabudi akimsikiliza Balozi wa Falme za Kiarabu nchini Mhe.Khalifa Abdulrahman Mohamed Al-Marzooqi walipokutana kwa Mazungumzo Jijini Dar es Salaam
Mazungumzo yakiendelea.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mhe. Prof. Kabudi akutana kwa mazungumzo na Balozi wa UAE nchini

Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amekutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Khalifa Abdulrahman Al-Marzooqi, Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) nchini.

Katika mazungumzo yao yaliyofanyika tarehe 20 Machi 2019 kwenye ofisi ndogo za Wizara zilizopo Dar es Salaam, Prof. Kabudi alimshukuru Mhe. Balozi Al-Marzooqi kwa kupata fursa ya kukutana naye na kwamba, Tanzania inathamini mahusiano na ushirikiano wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Umoja wa Falme za Kiarabu.

Aidha, alimweleza Balozi huyo kuwa, Wizara chini ya uongozi wake itaendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa, mahusiano yaliyopo kati ya nchi hizi mbili yanaimarishwa.

Kwa upande wake, Mhe. Balozi Al-Marzooqi ametumia mazungumzo hayo kumpongeza Mhe. Prof. Kabudi kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kumhakikishia ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha mahusiano yaliyopo yanaimarishwa.

 Mhe. Balozi Al-Marzooqi aliongeza kuwa, Umoja wa Falme za Kiarabu una nia ya kuimarisha mahusiano yaliyopo na umepanga kufungua Ubalozi mdogo (Consulate General) Zanzibar. Pia, Mhe. Balozi alimuarifu Mhe. Waziri kwamba  ana mpango wa kuutembelea Mkoa wa Dodoma ili pamoja na masuala mengine, kujionea eneo walilopewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za ubalozi na makazi kwa lengo la kujipanga kuliendeleza.

Kadhalika, Prof. Kabudi na Mhe. Balozi Al-Marzooqi wamekubaliana kuendeleza ushirikiano kwenye maeneo ya uwekezaji ambapo Balozi huyo ameonesha nia ya kuendelea kushawishi wawekezaji kutoka nchini kwake kuja kuwekeza nchini hususan kwenye sekta za utalii, hoteli, viwanda na utoaji wa huduma. Pia ameahidi kuwashawishi wafanyabishara wakubwa na wadogo kutoka UAE kuja nchini ili kujionea fursa za biashara zilizopo.

Prof. Kabudi amemuhakikishia Balozi Al-Marzooqi kuwa, Tanzania ni eneo bora la uwekezaji na biashara na kwamba, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Wizara zingine zitaendelea kuweka mazingira mazuri ya kupokea wawekezaji na wafanyabiashara kutoka maeneo yote duniani.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
20 Machi 2019
Viewing all 110153 articles
Browse latest View live




Latest Images