Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110091 articles
Browse latest View live

QNET YAMALIZA MAONESHO YAKE YA KIBIASHARA DAR ES SALAAM IKIWAACHA WATEJA WAKE NA FURAHA

$
0
0
QNET Independent Representative, Eliah Medard Mrosso explaining to customers and visitors about QNET products and services on the second day of QNET Dar es Salaam Expo 2019.
QNET Independent Representative Andrew Yusuf Gerald giving a testimony to crowds about his exceptional experience with QNET and its business on the second day of QNET Dar es Salaam Expo 2019. 
QNET Independent Representative Erasmus Bahati Amani making a business presentation about QNET Products and business model to crowds on the second day of QNET Dar es Salaam Expo 2019.
QNET Independent representatives, prospective customers, business partners and visitors at QNET Dar es Salaam Expo on the second day of the event.

NAIBU WAZIRI MHE. IKUPA NA NAIBU KATIBU MKUU ELIMU PROF. MDOE KATIKA HAFLA YA TUZO ZA I CAN

$
0
0



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akionyesha juu kitabu cha I Can, I Must, I Will kama ishara ya kuzindua toleo maalum kwa wasioona (kiatu cha nukta nundu) leo wakati wa hafla ya utoaji tuza ya I CAN pamoja na chakula cha mchana iliyoandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Persons with Disabilities Foundation katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
7
Balozi wa Marekani Nchini Dkt. Inmi Patterson (kushoto) akimkabidhi hundi ya shilingi milioni mbili za Kitanzania Bi. Rehema Said mshindi wa Tuzo ya I CAN ya Mafanikio katika Michezo iliyotolewa na  Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Persons with Disabilities Foundation katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
9-2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsalimia Bi.Wakonta Kakunda (kulia) ambaye ni Mshindi wa Tuzo ya I CAN ya Mafanikio katika Ujuzi wa Kipekee kwenye hafla ilioandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Persons with Disabilities Foundation katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
14
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa sheria na Katiba Bw, Amon Mpanju katika hafla ya  Tuzo ya I CAN ya heshima inayoandaliwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Persons with Disabilities Foundation iliyotolewa leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
16-2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya I CAN ya heshima kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kutoka kwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Persons with Disabilities Foundation Dkt. Reginald Mengi (kushoto) kwa kutambua mchango wake katika kusaidia watu wenye ulemavu. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
25
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wageni waalikwa kwenye  Tuzo ya I CAN inayoandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Persons with Disabilities Foundation Dkt. Reginald Mengi.
2
Sehemu ya Watu wenye Ulemavu waliohudhuria hafla ya utoaji tuza ya I CAN pamoja na chakula cha mchana iliyoandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Persons with Disabilities Foundation katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

………………………………………………………………………………….

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewahimiza watu wenye ulemavu kutumia fursa zilizopo katika kujikwamua kiuchumi.

 Makamu wa Rais ameyasema hayo leo kwenye hafla ya utoaji tuzo ya I CAN kwa watu wenye ulemavu iliyoandaliwa na Taasisi ya Dkt. Reginald Mengi Foundation, iliyofanyika leo kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.

 “Serikali inapenda kuwahakikishia kuwa changamoto za walemavu zinafanyiwa kazi moja baada ya nyingine.”Alisema Makmu wa Rais. Aidha, Serikali imeendelea kuweka mifumo, taasisi mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu kwa kuhakikisha kuwa kuna miundombinu wezeshi ya elimu, afya na teknolojia ili watu wenye ulemavu kuajirika kwenye viwanda vyetu. “Nitoe rai kwa waajiri na wamiliki wa viwanda kote nchini kuhakikisha kuwa hawabagui wala kunyanyapaa walemavu katika kuijenga Tanzania ya Viwanda ambayo ni jumuishi kwa wote” alisisitiza Makamu wa Rais.

 Makamu wa Rais amesema Serikali inatambua, inathamini na inapongeza jitihada za Dkt. Reginald Mengi pamoja na taasisi yake mpya ya Dkt. Reginald Mengi Persons with Disabilities Foundation ambayo pamoja na mambo mengine inahimiza ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu katika ajira.

 Vilevile Makamu wa Rais aliwaambia wananchi waliohudhuria hafla hiyo kuwa Serikali imeweka mkazo maalum katika masuala ya elimu jumuishi ambapo watu wenye ulemavu watasoma vizuri kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari.
 Kwa Upande mwingine Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Watu Wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa amesema Tuzo za I CAN zimekuwa chachu sana kwa watu wenye ulemavu ambapo alimpongeza na kumshukuru Dkt. Reginald Mengi kwa moyo wake wa kipekee wa kutambua na kuwasaidia walemavu.

 Aidha, amesema Serikali ina mpango endelevu  wa kutoa elimu ya masuala ya ulemavu ikiwa pamoja na kuendelea kufanya jitihada za kuongeza wakalimani wa lugha za alama. Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa James Mdoe amesema sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 inatambua fursa na haki sawa katika kupata elimu hivyo Serikali inaendelea kuboresha miundombinu wezeshi kwa wote wenye mahitaji maalumu.

TFS YAHIMIZA WATANZANIA KUENDELEA KUTUNZA MISITU KWA AJILI YA VIZAZI VYA SASA NA VIJAVYO

$
0
0

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) umewahimiza Watanzania kutunza misitu kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho huku ikifafanua ni vema changamoto zilizopo zikatatuliwa kwa majadiliano na hatimaye misitu ibaki salama.

Hayo yamesemwa na Meneja wa Rasilimali za Misitu Dkt. Masota Abel kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Profesa Dos Santos Silayo baada ya kumalizika kwa kikao cha mazungumzo na majadilano kati ya maofisa wa TFS na ujumbe wa watu 15 kutoka nchini Ethiopia ambao wamekuja nchini Tanzania kujifunza namna nzuri ya utunzaji misitu.

Raia hao wa Ethiopia wametoka katika taasisi mbalimbali zinazohusika na utunzaji misitu na tafiti katika nchi yao na wakiwa nchini wamepata fursa ya kwenda katika maeneo mbalimbali katika mikoa ya Tanga, Morogoro,Iringa na Dar es Salaam.

Dkt.Masota amesema ni vema Watanzania wakahakikisha wanatunza misitu iliyopo nchini Tanzania na kufafanua wageni hao kutoka Ethiopia wamefurahishwa na namna TFS inavyotunza misitu, hivyo ametoa ombi kwa Watanzania kuwa sehemu ya kila mmoja kwa nafasi yake kuitunza kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho kwa maslahi mapana ya Taifa.

"Ujumbe wangu kwa Watanzania watunze misitu.Tuitunze kwa kufuata taratibu zinazostahili na hata kama kunachangamoto nyingine tutumie nafasi za majadiliano kutafuta ufumbuzi na hatimaye ibaki salama. Tuache kuvamia misitu na kuikata, tuache kufanya shughuli za kilimo maeneo ya hifadhi na misitu kwa ujumla.

"Tunapaswa kufahamu misitu tuliyonayo nchini ni keki ya Taifa na hivyo lazima tuitunze na ilete tija kwa ajili ya kizazi kilichopo sasa na kizazi kinachokuja. Kwetu TFS tutaendelea kuweka mikakati ya kuhakiksha misitu inabaki salama lakini wakati huo huo wananchi nao wanalojukumu kama hilo,"amesema Dk.Abel.

Alipoulizwa changamoto kubwa ambayo TFS wanakabiliana nayo, amejibu ongezeko la watu ni moja ya changamoto kwani wengi wanakosa nishati mbadala ya miti ambayo itakidhi mahitaji kama nchi na kukosekana kwa nishati mbadala imesababisha misitu kuvamiwa na kuharibiwa.

Pia ongezeko la watu limesababisha kuwe na mahitaji makubwa ya ardhi na hivyo wengi kuvamia maeneo ya misitu yaliyohifadhiwa. Mabadiliko ya tabianchi nayo yanachoche watu kuvamia misitu kwa lengo la kutafuta ardhi yenye rutuba kwa shughuli za kilimo.

Alipoulizwa kwanini Waethiopia hao wameichagua Tanzania , Dk.Abel amesema kuwa nchi yetu inasifika kwa utunzaji wa mazingira na hivyo wameona ni sehemu sahihi ya kuja kujifunza kuhusu uhifadhi wa misitu .

"Wageni wetu wamekiri na kukubali kazi nzuri ambayo inafanywa na Serikali yetu kupitia TFS katika kutunza misitu, wameeleza namna kile ambacho wamejifunza watakavyokwenda kwao kuweka mikakati itakayowawezesha kuitunza misitu yao.Ethiopa misitu yao imeendelea kuharibiwa .Tunaweza kusema hawana misitu tena.Kwao eneo kubwa limebaki kuwa jangwa, ndio maana wanasema hata asali yao wanafuga katika mabanda .Hivyo hata asali yetu inabaki kuwa bora na ya asili kuliko ya kwao,"amesema.

Kuhusu ujumbe wa TFS kwa wageni hao waliotoka Ethiopia, Dkt.Abel amesema wanashauri waje kuwekeza nchini Tanzania kwani kuna maeneo mengi ya kuwekeza yakiwemo katika sekta ya misitu na viwanda.

Kwa upande wa wageni hao wamesema Serikali ya Tanzania kupitia TFS wamefanya kazi kubwa na nzuri katika kuhakikisha misitu inatunzwa vizuri na kubwa zaidi ni namna ambavyo kuna utaratibu mzuri wa usimamizi.

Akizungumza wakati akitoa shukrani kwa TFS na Serikali ya Tanzania kwa niaba ya wenzake Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti cha Central Ethiopia EV+ & Forest Wondnossen Tsadik amesema kikubwa ambacho wamejifunza ni namna ambavyo sekta ya misitu inavyoangaliwa kwa ukaribu zaidi.

"Tumeona hapa misitu inasimamiwa na TFS ambayo iko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, hii inafanya kuwepo na ukaribu wa kufuatilia hatua kwa hatua kuhusu uhifahi.Kwetu sisi mambo ya misitu yamechangwa na mambo ya kilimo.Tunaipongeza Tanzania kwa namna ambavyo inasimamia misitu yake,"amesema.

Pia amesema wakiwa katika maeneo mbalimbali ambayo wamekwenda wamepata nafasi ya kukutana na watalaam wa masuala ya misitu pamoja na watafiti wa kada mbalimbali ambapo wamebadilisha uzoefu na wanaamini kila mmoja atakuwa amejifunza kutoka kwa mwingine.

Wakati huo huo Ofisa kutoka Idara ya Ununuzi wa mbegu ICRAF nchini Ethiopia Kedra Mohammed amesema pamoja na mambo mengine amejifunza ukarimu wa Watanzania na kuhusu ziara yao imekuwa ya mafanikio makubwa kwani kuna mengi wamejifunza.
 Meneja wa Rasilimali za Misitu kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Dk.Masota Abel akifafanua jambo kwa Waethiopia ambao wamekuja nchini kujifunza utunzaji wa misitu na kubadilisha uzoefu,Aliyekaa ni Meneja wa Kituo cha Uzalishaji mbegu za miti-TFS cha Morogoro Dk.Hamza Katety
 Mkurugenzi wa Kituo cha Utafititi cha Central Ethiopia EV+& Forest Wondnossen Tsadik akizungumza wakati wa kikao cha majadiliano kati yao na TFS baada ya kumalizika kwa ziara waliyoifanya katika mikoa  ya Tanga,Morogoro,Iringa na Dar es Salaam
 Baadhi ya wageni waliotoka nchini Ethiopia kuja nchini Tanzania kujifunza kuhusu utunzaji misitu wakimsikiliza Meneja wa Rasilimali za Misitu kutoka TFS Dk.Masota Abel (hayupo pichani)
 Raia kutoka nchini Ethiopia wakifuatilia mazungumzo

 Sehemu wa ugeni wa watu 15 kutoka taasisi mbalimbali za uhifadhi misitu na tafiti wakifuatilia majadiliano katika Ofisi za TFS zilizopo jijini Dar es Salaam

WAKALA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA YAHOFIA MITI YA MPINGO, MNINGA, MVULE,MKANGAZI KUTOWEKA NCHINI

$
0
0
WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umesema kwa sasa umechukua hatua mbalimbali za kuhakikisha miti bora ya asili iliyopo nchini inaendelea kuwepo kwani tayari kuna tishio la miti hiyo ikiwemo ya Mpingo, Mninga,Mkongo na Mvule kutoweka nchini.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Meneja wa Kituo cha Uzalishaji Mbegu za Miti-TFS mkoani Morogoro Dk.Hamnza Katety amesema wanapotafuta miti hiyo hata mahali ambako waliamini ipo wanaikosa.

"Kuna miti tuliyozoea kuiona katika nchi yetu na sasa imeanza kupotea .Miti hiyo maarufu imekuwa adimu kuipata na hata ikipatakana haiko kwenye ubora unaostahili.Mninga,Mkongo, Mvule na Mkakangazi imeanza kupotea kabisa.

"Hatua ambazo TFS tunachukua ni kuhifadhi mbegu bora za miti hiyo, tuna mashamba ya mbegu bora ambayo yameanzishwa.Tayari miti ya mvule, mkongo na mkangazi imepandwa katika vishamba vidogo,"amesema Dk.Katety.

Ametoa rai kwa Watanzania kuhakikisha wanashiriki kuitunza miti hiyo ambayo ni alama katika nchi yetu na huenda ni mpango wa Mungu kwa kuweika katika ardhi ya Tanzania.

Akizungumzia mbegu bora, Dk.Katety amesema kupitia Kituo cha uzalishaji wa mbegu za miti Morogoro ambacho kipo chini ya TFS Wizara ya Maliasili na Utalii kitaendelea kuzalisha mbegu bora na kushauri ni vema wananchi wakapata ushauri kabla ya kununua mbegu.Amesema matarajio ya TFS ni kuhakikisha kunakuwa na mashamba mengi ya mbegu bora za miti ambapo itasaidia kupunguza gharama kubwa inayotumika kununua mbegu kutoka nchi nyingine na hasa Zimbabwe.

Amesema tayari wageni wameanza kutambua mashamba ya mbegu yaliyopo nchini na hivyo katika siku zijazo nchi itaingiza fedha kwa kuuza mbegu.

"TFS tumewapokea wageni kutoka Ethiopia wamekuja kujifunza kuhusu utunzaji wa misitu.Eneo ambalo limewavutia ni mashamba ya madogo ya mbegu tuliyonayo kwani yameandaliwa katika kiwango cha kimataifa. Tunaamini kwa miaka mitatu au minne ijayo mbegu zitatoka kwetu hapa hapa na kuuza kwa wengine.

"Lakini lengo si kuuza tu mbegu bali kuboresha mashamba ya miti kwa kuwa na mbegu bora na kwa kutumia mbegu bora kiasi cha uzalishaji kitaongozeka na hivyo kuongeza pato la taifa.Kwa sasa ni vigumu kupanua ukubwa wa mashamba bali ni kuongeza uzalishaji.Lengo letu ni kuongeza pato la nchi kwa kuongeza uzalishaji wa miti.Hatua ambazo tunazichukua katika kuzalisha mbegu bora umewafanya raia hao wa Ethiopia kutoa pongezi kwa wataalam wetu.Tunaamini tutashirikiana nao,"amesema Dk.Katety.

Kuhusu wapi zinapatikana mbegu bora, amesema ni vema kwa wanaohitaji mbegu wakaenda katika ofisi za TFS ambazo zipo katika ngazi ya wilaya na mikoa ambako watapata maelekezo ya wapi wanaweza kupata mbegu bora.

Mamia wapongeza Gharama Ndogo za Usafiri wa Treni, Wasema Huduma ya Vyakula SARANDA Ni ya Kuvutia

KATIBU TAWALA ARUSHA AONGOZA MATEMBEZI YA UHAMASISHAJI UMMA UMUHIMU WA AFYA YA KINYWA NA MENO

$
0
0
Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Mhe. Richard Kwitega akizungumza jambo na Wananchi na Wanafuzi kutoka shule mbalimbali ikiwemo Shule ya Msingi Meru ya wanafunzi wenye usikivu hafifu katika viwanja vya Shule ya Msingi Meru Mkoani humo katika matembezi ya Uhamasishaji wa Umma kuhusu umuhimu wa Afya ya Kinywa na Meno yaliyoanzia katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mrisho Gambo , ambapo kilele itakuwa Machi 20, 2019, Mgeni Rasmi ni Waziri wa (TAMISEMI) Suleiman Jaffo. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) 


NA KHAMISI MUSSA

Ambapo Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Mhe. Richard Kwitega "alisema"

Awali ya yote nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kushiriki kwenye matembezi haya yenye umbali wa kilometa 2.5 yaliyoanzia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kuishia katika viunga vya uwanja wa shule ya msingi Meru.

Kwaupande mwingine niwashukuru pia waandaaji wa shughuli hii ya tukio hili lenye uhai mzima wa tasnia ya afya ya kinywa na meno, asanteni sana.

Aidha, nitumie nafasi hii kwakuwapongezeni nyote mlioshiriki kwenye matembezi yaha asubuhi hii, Ninawashukuru sana kwa kujumuika nasi katika shughuli hii muhimu yenye lengo la kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa afya ya kinywa na meno Tanzania.

Ndugu wananchi, Ninapenda kuchukua nafasi hii kuwaarifu kuwa matembezi haya yaliyoratibiwa na Chama cha Wataalamu wa Afya ya Kinywa na MenoTanzania (TDA) yanayofanyika kila mwaka kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya afya ya kinywa na meno Duniani.

Kama ilivyo kwa sherehe mbalimbali za maadhimisho, Sherehe hizi huambatana na kauli mbiu na kauli mbiu ya mwaka huu ni "SEMA AHH: CHUKUA HATUA ZINAZOZINGATIA AFYA YA KINYWA NA MENO" Kauli mbiu hii ni mwendelezo wa kampeni ya kipindi cha miaka mitatu zilizoanzishwa mwaka jana 2018 na Shirikisho la Vyama vya Afya ya Kinywa na Meno Duniani chini ya kibwagizo cha kauli mbiu kisemacho "Sema Ahh", kwa mwaka jana 2018 kauli mbiu ilikuwa "Sema Ahh; Fikiri Kinywa Fikiri Afya"ikilenga kutoa elimu kwa jamii kuhusu mahusiano ya afya ya kinywa na afya ya mwilikwa ujumla.
Madaktari na Wanafunzi wakiwa katika maandamano hayo 

Rais Mwandamizi wa Chama cha Wataalamu wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania, Dkt. Deogratias Kisala akizungumza jambo wakati wakati wa matembezi ya Uhamasishaji wa Umma kuhusu umuhimu wa Afya ya Kinywa na Meno yaliyoanzia katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mrisho Gambo , ambapo kilele itakuwa Machi 20, 2019, Mgeni Rasmi ni Waziri wa (TAMISEMI) Suleiman Jaffo.


Kwa upande wa Rais Mwandamizi wa Chama cha Wataalamu wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania, Dkt. Deogratias Kisala "alisema" Magonjwa ya fizi na kutoboka kwa meno ni maradhi ambayo huwapata watu wengi sana ulimwenguni.

Tafiti zilizofanywa na shirikisho la afya ya kinywa na meno duniani zinaonyesha kwamba tatizo la kutoboka kwa meno ndio linaathiri watu wengi Duniani. Aidha, nchini mwetu, inaripotiwa kuwa kati ya watu 10 wenye umri wa miaka 45 na zaidi, watu 8 wanakabiliwa na matatizo ya ugonjwa wa fizi. 

Magonjwa ya kinywa na meno yanaweza kuzuilika kwa kufuata njia sahihi za usafishaji wa kinywa, kusafisha meno mara mbili kwa kutwa, kutumia dawa ya meno yenye madini ya floridi na kumuona daktari wa meno angalau mara moja kwa mwaka Kinga ni bora kuliko tiba na gharama za matibabu ni kubwa kuliko gharama za kinga

Tunatumaini wananchi wamepokea jumbe mbalimbali zilizokuwa kwenye mabango wakati wa matembezi yetu ya leo, Chama cha wataalamu wa afya ya kinywa na meno tukishirikiana na Serikali na wadau wetu tumeratibu shughuli mbalimbali za uhamasishaji wa afya ya kinywa na meno nchini kote.

Toka tarehe 14 Machi shughuli za kutoa elimu, uchunguzi wa afya ya kinywa na meno na matibabu bila malipo kwa nananchi yanayoendelea kutolewa katika mikoa mbalimbali nchini. Kitaifa, maadhimisho yanafanyikia mkoani hapa, katika mkoa wa Arusha na tutatoa huduma katika shule za watoto wenye mahitaji maalumu za Meru, Uhuru, Makumbuso, Shangarawe na pia tutatoa huduma kwa wananchi katika kituo cha Afya cha Themi ifikapo Kilele cha maadhimisho hayo ni siku ya tarehe 20, Machi.

Tunategemea kuwa tumetoa huduma kwa watu takribani 4000 hapa mkoani Arusha na wananchi zaidi ya elfu arobaini na saba (47000) nchini kote
Ndugu mgeni rasmi, Mwaka jana maadhimisho kama haya tulitoa huduma za elimu ya afya, ushauri na matibabu kwa zaidi ya watu elfu thelathini na nane (38000) nchini kote.

Hii ilipelekea chama chetu kupewa tuzo ya kimataifa inayojulikana kama "Most Educative Award" inayotolewa na Sirikisho la Vyama vya Afya ya Kinywa na Meno Duniani (FDI), Zawadi hii imeliletea heshima kubwa sana nchi yetu.Napenda kutoa shukurani za dhati kwa serikali yetu kwa ushirikiano mkubwa inayo tupa katika kuboresha huduma ya afya ya kinywa na meno nchini.

Aidha tunaipongeza serikali kwa kupitisha na kuufanyia kazi muswada wa sheria ya madaktari, madaktari wa meno na wataalamu wa Afya shirikishi ya mwaka 2017 tunatumaini sheria hiiitasaidia kuboresha huduma za Afya kwa jamii na kuongeza ufanisi na tija kwa wataalamu wa Afya 
Mtunza hazina wa Chama cha Wa Afya ya Kinyewa na Meno Tanzania, Dkt. Arnold Mtenga (kulia) kishiriki maandamano hayo

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MACHI 18,2019

Germany Tuebingen festival and GAIEXPO 2019

$
0
0
9th International Africa Festival Tübingen, Germany –27 July to 4th August 2019
East African and Southern Region at Focus
Call for participation

Live music performers, groups, traders, exhibitors, food vendors, Small & Medium sized companies, Journalist, sponsors and collaborators, interested in participating at the 9th edition International Africa Festival Tübingen, Germany can now send in their applications.  

 Each year, the festival bring thousands of people irrespective of their countries together to celebrate Arts & music, young & old talent and tradition vs modernity in an extraordinary ten-day event, 2019 shall focus on East and Southern Africa region.
The International Africa Festival Tübingen, Germany is a highlight and melting pot for Africans in and out of Germany.
    
The call for applications is open until 31Jun 2019

The festival will feature traditional and modern live performances on stage offering diverse and original music from across the African continent and the diaspora.  
The selection committee shall meets in April to finalize the line-up, after which all applicants will be notified of their status before May 2019
For those selected, the Festival will cover the following expenses for participating artists
·        A modest honorarium
·        Per diems for meals
·        Accommodation in Tübingen
·        Artist profile in festival programs, press releases, website and social media
·        Please note that artists from outside the region may be required to find their own travel sponsors.
To apply, send the following:
·        Artist profile/biography
·        Latest audio release (send two CDs by post, or maximum three songs via We Transfer / Dropbox)
·        DVD of live performance, or one clip via We Transfer / Dropbox (if available)
·        Two high-resolution promotional photos
·        Stage plan and technical rider (if available)
Supporting documents must be clearly labeled and sent by email: kontakt@afrikafestival.net  

coordinator for  east Africa +255(0)787457743 (Shamsa)

 

WAZIRI MHAGAMA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI OFISI YA WAZIRI MKUU

$
0
0
Na Nyamagory Omary wa PMO
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amefungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi yake upande wa Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu uliofanyika mapema mwishoni mwa wiki hii.
Akifungua mkutano huo uliofanyiaka Machi 16, 2019 katika Ukumbi wa mikutano wa Magadu mkoani Morogoro waziri aliwataka watumishi wa ofisi hiyo kuendelea kufanya kazi kwa kuzingatia weledi na ubunifu ili kuendelea kuleta tija na utendaji wenye kuleta maendeleo nchini.
“Naamini mkutano huu unalenga kugusa maeneo yote ya utendaji kazi ikiwemo kubainisha changamoto, fursa na jinsi ya kujipanga ili kuongeza tija na ufanisi katika maeneo yetu ya kazi,”alisema Mhagama
Waziri aliwaeleza watumishi kuutumia mkutano huo kama chombo muhimu cha kuendelea kujadili na kuweka maazimio yanayotekelezeka kwa kuzingatia umuhimu wa chombo hicho kilichopo kisheria katika kusaidia watumishi wa umma.
“Tumieni mabaraza haya kama eneo muhimu la kujadili na kutoa mapendekezo juu ya kuboresha mazingira ya kazi ili kuendelea kuwa na weledi katika kutekeleza majukumu ya ujenzi wa Taifa,”alieleza Mhagama
Waziri aliongezea kuwa, matumizi sahihi ya mkutano huo ni kuona namna  utavyosaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazokabili Idara, Vitengo pamoja na Taasisi zilizopo chini ya Ofisi hiyo na kuwa na  maoni, ushauri na mapendekezo yanayotekelezeka ili kufikia malengo waliojiwekea kwa mwaka wa fedha ujao 2019/2020
Pamoja na hayo Waziri alipongeza utendaji wa watumishi wa ofisi yake hususan Idara ya Kazi, inayoshughulikia masuala ya vibali vya kazi na kuendelea  kuboresha mifumo na mazingira wezeshi ili kuendelea ,kulinda mazingira ya kazi na ajira nchini.
“Pamoja na idara zote kuendelea kufanya vyema, kipekee naipongeza Idara ya kazi kwa mabadiliko mapya ya kiutendaji kwa kuzingatia ilikuwa Idara inayotupa shida hususani upande wa vibali vya ajira, tunashukuru kwa mageuzi makubwa yaliyofanyika katika Idara hiyo kwa kuwa na usimamizi mzuri na kulinda mazingira ya ajira na kuleta manufaa nchini,”alieleza Mhagama
Sambamba na hilo waziri aliwapongeza watendaji wa Ofisi kwa ujumla kwa nafasi zao kwa kuwepo na mafanikio makubwa ya kiutendaji pamoja na mchango wa kila mtumishi katika utoaji wa huduma bora bila upendeleo kwa wananchi wote kwa haki na usawa.
“Sina budi kuwapongeza kwani kila mmoja wetu ametimiza majukumu na kuwa na mchango mkubwa katika kutimiza majukumu ya serikali yetu kwa kuendelea  kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015/2020,”alisisitiza Waziri Mhagama.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Andrew Massawe aliahidi kuendelea kusimamia maagizo na ushauri wa waziri kwa watumishi wa ofisi yake ili kuleta matokeo chanya yanayotarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika kuboresha mazingira ya utendaji kwa watumishi ikiwemo kuendelea kupambana na rushwa mahali pa kazi na kuzingatia haki na usawa kwa watumishi wote.
Aidha Katibu Mkuu aliongezea kuwa, uwepo wa mabaraza hayo ni kwa mujibu wa sheria na  agizo Na. 1 la mwaka 1970 ambalo linaelekeza utaratibu wa kuundwa kwa mabaraza katika Taasisi na Ofisi za Umma kwa kuzingatia sheria mbalimbali za Kimataifa ikiwemo zile za Shirika la Kazi Dunia (ILO)
“Kwa kuzingatia lengo la kuanzishwa kwa mabaraza haya ni pamoja na kuona utekelezaji wa Bajeti za Ofisi zetu pamoja na kutoa mapendekezo katika kuboresha utekelezaji wa bajeti zetu za kila mwaka,”alisisitiza Massawe
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akihutubia watumishi wa Ofisi yake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika Machi 16, 2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa Magadu Mkoani Morogoro.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akihutubia watumishi wa Ofisi yake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Magadu Mkoani Morogoro.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Bw.Andrew Massawe akizungumza jambo wakati wa mkutano wa baraza la wafanyakazi wa ofisi yake Machi 16, 2019
 Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) wakifuatilia mkuatano huo.
 Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) wakifuatilia mkuatano huo.
 Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) wakifuatilia mkuatano huo.
 Mkurugenzi wa ajira Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Ally Msaki akichangia jambo wakati wa mkutano huo.
 Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Sera na Mipango Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Bw. Godfrey Chambo akichangia jambo wakati wa mkuatano huo.
 Mkurugenzi wa Sera na Mipango Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Bw. Gabriel Saelie akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2018/2019 pamoja na Mada ya mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2019/ 2020 wakati wa mkutano huo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa ofisi yake mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo, uliofanyika Mkoani Morogoro. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

HOROHORO: WAKAZI WA MAENEO YA MPAKANI WAAHIDI KUSHIRIKIANA NA IDARA YA UHAMIAJI KATIKA UDHIBTI NA USIMAMIZI WA MPAKA

$
0
0
Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji nchini, Mrakibu Ally Mtanda akizungumza na wananchi wa Horohoro wakati wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Idara ya Uhamiaji kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) uliyofanyika katika Uwanja wa Horohoro Customs katika Kijiji cha Horohoro mwishoni mwa wiki.

Wakazi wa vijiji vya mpakani Wilayani Mkinga wasema wako tayari kushirikiana na Idara ya Uhamiaji katika suala zima la Udhibiti na Usimamizi wa mpaka. Wamesema hayo katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Idara ya Uhamiaji kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) uliyofanyika katika Uwanja wa Horohoro Customs katika Kijiji cha Horohoro.

Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Horohoro Border Ndugu Mery Mery Mirio aliishukuru Idara ya Uhamiaji kwa kukutana na Wananchi ili kutoa elimu na kujadili changamoto zilizopo maeneo ya mpakani.

Awali akimkaribisha Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Mrakibu Ally Mtanda alisema kwamba, Idara ya Uhamiaji imeamua kwa dhati kabisa kuwashirikisha Wananchi katika Suala zima la Ulinzi na Usimamizi wa Mpaka kwani wao (wananchi) ndio wanafahamu mambo yote yanayoendelea mpakani kuliko maafisa Uhamiaji.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Horohoro Border Ndugu Mery Mery Mirio akiongea wakati wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Idara ya Uhamiaji kwaa kushirikiana na shirika la uhamiaji la Kimataifa (IOM) katika mpaka waa Horohoro, wilayani Mkinga mkoa wa Tanga.

“Ndugu wananchi, tumekuja hapa ili kutoa elimu na kuwashirikisha katika Ulinzi na Usimamizi wa Mpaka, nyinyi ndio mnaofahamu watu wanaovusha wahamiaji haramu, wanaofanya magendo ya usafirishaji binadamu na wanaoishi na kuwauzia ardhi wahamiaji haramu. Tumeamua kuja kwenu kuwapa elimu ya uraia, umuhimu wa kushirikiana na idara ya Uhamiaji katika udhibiti na usimamizi wa mpaka tukiamini kuwa ninyi ndio wenye nchi na ndio mnaotakiwa kunufaika na Haki zinazotolewa na serikali kwa raia wake pamoja na rasilimali za Taifa. Kwahiyo mnao wajibu wa kuilinda nchi yenu ili iendelee kuwa salama.” Alieleza Mtanda.

Baadhi ya wananchi waliotoa maoni walisema kwamba wako tayari kushirikiana na Idara ya Uhamiaji kuwafichua wahamiaji haramu wanaoingia nchini. “Kwa maelezo hayo aliyotoa afande, nipo tayari kushiriki katika kuilinda nchi yangu kwani leo nimefahamu madhara yanayoweza kulikumba Taifa kwa kuwahifadhi wahamiaji haramu ikiwa ni pamoja na uwepo wa migogoro ya ardhi, kuongezeka vitendo vya kihalifu, ugaidi, usafirishaji madawa ya kulevya, na kupungua kwa na nafasi za ajira na huduma za jamii.” Alisema Mzee Ally ambaye ni Mkazi wa Horohoro kijijini.

Akifunga mkutano huo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Horohoro Border, aliishukuru Idara ya Uhamiaji kwa kutoa elimu kwa wananchi na kuitaka idara hiyo kuwa na utaratibu wa kukutana na wananchi mara kwa mara kwani wananchi wana taarifa nyingi lakini wanakuwa waoga kufika ofisi za Uhamiaji. “Kwa mkutano huu, nimeshukuru sana, wananchi hapa wameingia hamasa na uzalendo wa kuilinda nchi yao, zamani walikuwa wanaona suala la ulinzi wa mpaka ni la vyombo vya dola pekee” Alisema Mwenyekiti huyo.

Mkutano huo ulikuwa ni kuhitimisha Warsha ya Siku tatu ya Ushirikishishwaji wa Wananchi katika Ulinzi na Usimamizi wa Mipaka iliyoanza tarehe 13 Machi na kufikia tamati leo siku ya Ijumaa, Machi 15, 2019.









The Institute of social work is pleased to welcome you to the International Social work Conference to be held from 8th to 10th May 2019

$
0
0


The Institute of social work is pleased to welcome you to the International Social work Conference to be held from 8th to 10th May 2019, at the Institute's Information Resource Center. The conference will bring together local and international academicians, policy makers, practitioners, students from related fields and social work service users who will share and discuss about Economic Transformation in Africa under the theme "The Role Of Social Work in Enhancing Inclusive and Sustainable Economic Transformation".
This conference will integrate how social work as a profession and academic discipline enhances inclusive and sustainable economic transformation that will bring resolutions to significantly inform the desired economic transformation, in the short and long run.

JOHNNY BOKELO ISENGE

$
0
0
Na Moshy Kiyungi, Dar es Salaam. Machi, 2019.

Johnny Bokelo alizaliwa mwaka 1939 nchini Kongo, nje kidogo ya jiji la Kinshasa. Familia yake ilikuwa ni ya wanamuziki. Johnny alikuwa mdogo wa Paul Ebengo’Dewayon’ Isenge.

Mwanamuziki mwingine aliyekuwa mkubwa sana nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, toka mwanzoni mwa miaka ya 50, alikuwa Dewayon.

Alikuwa na bendi inaitwa Watam, ambako  Johnny Bokelo,  alipoanzia akipiga muziki akiwa na mtoto mwingine wakati huo akiwa na miaka 12, aliyekuja kutikisa ulimwengu wa muziki Franco Luambo Luanzo Makiadi


Bokelo aliendelea kupiga katika bendi alizoanzisha kaka yake Paul Ebengo’Dewayon’ Isenge.


Bendi hizo ni kama Konga Jazz na Orchèstre Cobantu, lakini mwaka 1958 John akaanzisha bendi yake, Orchestra Conga Success, akiwa na mdogo wake Mpia Mongongo, maarufu kwa jina la Porthos Bokelo.

Mpia wakati huo alikuwa mpiga gitaa la rhythm kwa umahiri mkubwa sana. 

Kaka yao Dewayon, akaja kujiunga na kundi hilo 1960, lakini miaka miwiwli baadae mwaka 1962,  Johny na kaka yake Dewayon wakatengana. 

Bokelo alifanikiwa kulijenga kundi lake kuwa na nguvu, likawa kwa namna fulani linafanana sana kimirindimo ya T.P.OK Jazz.

Hata tungo nyingine zilikuwa ni za kujibu tungo za T.P.OK Jazz au kuzungumzia mada ambayo imeanzishwa na  wenzao hao. 

Kuna wakati Bokelo alianzisha kuimba nyimbo alizozipa jina la Mwambe no 1 na 2 mpaka 5. Katika nyimbo hizo alikuwa akiongea na kushangaa jamii inaelekea wapi. Upigaji wa gitaa wa Bokelo, Dewayon na Franco ulishabihiana, pengine ni kutokana na wote kuanzia bendi ya Watam.

Mwaka 1968 Johnny Bokelo akabadili jina la kundi lake la Conga Success na kulita Conga 68, akaanzisha label yake, akaanza kutoa santuri. Kitendo hicho kilimuongezea kipato japo wanamuziki wake walitishia kuachana nae.

Walidai kuwa hawakuwa wanapata fedha zozote kutokana na mradi huo.

Santuri nyingi wakati huo alikuwa akiziachia kwanza kutoka nchini Ufaransa, ili kupata mapato zaidi. 

Kati ya 1972 mpaka 1974 Bokelo Isengo alikuwa anatumia muda mwingi zaidi akiwa studio. Kwenye mwaka 1970 viwanda vya kutengeneza santuri vya Kinshasa vikawa vimechoka hivyo bokelo akaanza kupeleka master zake ili kutengeneza santuri. 

Mwaka 1980 Bokelo aliachana kabisa na shughuli za muziki.

Ni miaka 24 imepita tangu kifo cha Johnny Bokelo Isenge, kilichotoke Januari 15, 1995, baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Mwisho.

Mungu alilaze roho yake pahala pema peponi, amina.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba: 0713331200, 0736331200, 0767331200 na 0784331200.

BILEKU MPASI ALIYEJIKWAMUA KATIKA MUZIKI

$
0
0
Na Moshy Kiyungi, Dar es Salaam. Machi, 2019

Bileku Mpasi ni mwanamuziki  aliyethubutu kuunda kundi la wanamuziki wa dansi katika jiji la Kinshasa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mara baada ya kifo cha ‘bosi’ wake Pepe Kalle. Huko nyuma tulishudia wanamuziki wengi wakipotea katika anga za muziki pasipo kufahamika sababu za mzingi mara baada ya viongozi wa bendi zao kufariki dunia.

Bendi ya T.P.OK. Jazz ilitoweka baada ya kufariki kwa kiongozi mkuu wa bendi hiyo marehemu Franco Luambo Makiadi. Wanamuziki waliosalia walijaribu kuiendesha, lakini ilishindikana licha ya kuwepo kwa wanamuziki wakubwa akina Lutumba Simaro Masiya, Kiambukuta Joscky, Madillu System na wengine wengi.

Katika makala hii itamzungumzia Djouna Mombafu ‘Bileku Mpasi’.

Bileku alipokuwa katika bendi ya Empire Bakuba ya Kabasele Yampanya ‘Pepe Kalle’, alikuwa kama mnenguaji na ‘mfokaji’. Watanzania tulimshudia miaka ya 1990, ambapo Pepe Kalle na kundi zima la Empire Bakuba walipoachia burudani humu nchini.

Bileku alikuwa akiongoza safu ya wanenguaji wafupi ‘Mbilikimo) akina Emoro na Jolly Bebbe. Bendi hiyo ilisambaratika baada ya kifo cha Pepe Kalle, Bileku akafanya jitihada binafsi ya kuanzisha kundi lake la Orchestra Big One.

Bendi hiyo hivi sasa ni gumzo katika jiji la Kinshasa, na viunga vyake, wakitamba na albamu ya Tonnerre de Brest yenye kibao kikali cha ‘6600 Volts’.

Bileku Mpasi akiongoza kundi hilo, wamefanikiwa kufyatua albam nyingi kwa kipindi kifupi, zilizopelekea kupata mialiko lukuki ndani na nje ya nchi yao hususan za Ulaya.

Amekuwa kivutio akionekana kwenye video zake nyingi kwa kuimba na kunengua akishirikiana na wanenguaji mbirikimo, Djuma Fatembo na Jolly Bebe.

Baadhi ya album alizoachia mwanamuziki huyo ni pamoja na Moun Baka Bouger, Karachiga, Tatou, Djouna Big One 6600Volts, Cupidon Brise, Tonnere de Best Onze Onze na Bilibili Bino Moko.

Zingine ni Medaile, Ndule Dekin, Keba na Mopepe, Sur Moradoe, Fin du Match na nyingine nyingi.

Wasifu wake

Bileku Mpasi yasemekana kuwa alizaliwa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mwishoni mwa miaka ya 1940, akapewa majina ya Bileku Jean-Pierre Matonet

Alichukuliwa na Pepe Kalle kama mnenguaji na rapa wa bendi hiyo. Juhudi zake zilimuwezesha kupanda chati haraka na kuwa maarufu, pengine hata zaidi ya waasisi wenyewe.

Kupanda kwa mafanikio yake kulitokana na umahiri wake mkubwa wa kucheza, kurapu na baadae akawa akiimba.

Hali hiyo ilimfanya Pepe Kalle kufikiria kumpa nafasi ya hisa zake katika bendi hiyo ya Empire Bakuba.

Pepe Kalle alitokea kumpenda sana Bileku na kumuamini, kama alivyofanya marehemu Franco Makiadi  kwa marehemu Madilu System, enzi za uhai wao walipokuwa pamoja katika bendi ya T.P. OK Jazz.

Kasi yake ya kucheza na kurapu kwa wakati mmoja, ndiyo kwa sasa imeigwa na marapa mbalimbali wa makundi ya muziki wa rumba, kuanzia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kongo Brazzaville hadi humu nchini.

Bileku Mpasi alikuwa akichuana na nyota wa kurap kama Robert Ekokota Wenda wa Wenge Musica BCBG, kabla ya kuibuka wengine kadhaa waliofuata nyayo zao.

Historia yake katika muziki.

Bileku Mpasi alianza  shughuli zake za muziki katika mji wa Kalemi kabla ya kwenda katika mji mkuu wa nchi hiyo wa Kinshasa mwishoni mwa miaka ya 1970.

Aliwahi kufanya shughuli za unenguaji katika bendi ndogondogo mnamo miaka ya 1980, kabla ya ‘kunyakuliwa’ na Pepe Kalle.

Bileku akiwa katika bendi hiyo ya Empire Bakuba, aliweza kuonesha kuwa anacho kipaji cha kuimba.

Wanamuziki waimbaji wa bendi hiyo Pepe Kalle, Dilu Dilumona na Papy Tex, walimpika hadi akawa mwimbaji hodari.

Ukali wake katika kunengua wakati huohuo akiimba, ulipekelekea kuwafunika baadhi ya magwiji wa uimbaji wa kundi hilo, akiwemo Papy Tex, wakaweka ‘Bifu’ dhidi yake.

Baada ya kifo cha Pepe Kalle Novemba mwaka 1998, kulitokea mtafaruku kama uliotokea katika bendi ya T.P. OK Jazz baada ya kifo cha Luambo Makiadi ‘Franco’ juu ya mustakabali wa bendi hiyo.

Familia ya Franco Makiadi ilimpa uongozi wa bendi ya T.P.OK. Jazz Madilu Sysytem. Kitendo ambacho wakongwe wa bendi hiyo akina Lutumba Simaro Massiya na Kiambukuta Joscky, wakaamua kujiengua na kwenda kuunda bendi yao ya Bana OK.

Ilidaiwa kwamba wanamuziki waliosalia katika bendi ya Empire Bakuba walikuwa na nia ya kuiendeleza bendi hiyo. Waliokuwa na waasisi wa wamiliki wake, Dilu Dilumona na Papy Tex, walianzisha ‘zengwe’ baada ya kufahamika kuwa Bileku Mpasi, alikuwa amepewa usimamizi wa hisa za Pepe Kalle.

Katika njia ya kuepusha shari, Bileku Mpasi na muungurumishaji wa gitaa la zito, Gode Lufombo, waliamua kujiondoa na kuiacha Empire Bakuba.

Wakaenda kujiunga katika kundi la Delta Force, ambalo lilikuwepo hata kabla ya kifo cha Pepe Kalle.

Walipiga muziki katika bendi hiyo ya Delta Force, tangu mwaka 1999 hadi 2002.

Baadae Bileku Mpasi aliamua kujiondoa na kuwa msanii wa kujitegemea na kufanikiwa kufyatua albamu yake ya kwanza ya ‘Tonnerre de Brest’.

Albamu hiyo ina kibao matata cha ‘6600 Volts’, kilichotolewa mwaka 2004 na kumfikisha Bileku kwenye fainali za tuzo za muziki Afrika za Kora (Kora Music Awards), ingawa hakufanikiwa kubeba tuzo yoyote.

Miongoni mwa vibao vilivyomo kwenye albamu hiyo iliyompa mafanikio makubwa kabla ya kuunda Orchestra Djouna Big One.

Bendi hiyo ilitamba kwa albamu zake nyingine mpya za ‘100% TVA’, ‘6600 Volts’ na ‘Cupidon Brisé’.

Bileku Mpasi  na kundi lake waliachia albam zingine za ‘Fin Du Match’, ‘Karachiga’, ‘Nez a Nez’, ‘Mihona’, ‘ ‘Onze Onze’, ‘Respect Pepe Kalle’ na ‘Tatou’.

Bileku anakumbukwa na Watanzania kwa kuchangia kuibua vipaji vya madansa wa Kitanzania wakati huo alipotinga nchini. Madansa hao ni pamoja na Kokoriko aliyeshabihiana naye kwa unenguaji hata mavazi, Maxi Prest na Mrisho Mpasi.

Baadhi ya wanamuziki wetu hapa nchini wameanzisha bendi zao ambazo zinafanya vizuri katika ‘game’ la muziki.

Hapa nawazungumzia Hussein Jumbe na kundi lake la Talents Band, Banana Zorro, Mafumu Bilal, Lady Jdee, Deo Mwanambilimbi na kundi lake la Kalunde Band, Kanku Kelly na kundi la The Kilimanjaro Connection, Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kiki’ kundi lake la La Capitale na wengine wengi.

Wito wa makala hii kwa wanamuziki wetu humu nchini, wawe wabunifu kwa kutengeneza vyao badala ya kukopi vya wenzao.

Mwisho.

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa namba 0784331200, 0713331200, 0736331200 na 0767331200.

KATIBU MKUU UVCCM AWATAKA VIJANA KUTUMIA VYEMA FURSA ZA UONGOZI

$
0
0
*Awataka kutokuwa wabeba pochi na mikoba bali wagombee nafasi za uongozi na kulitumikia taifa

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha  Mapinduzi (Uvccm) Mwalimu Raymond Mwangwala amewataka vijana nchini kuacha tabia ya kuwa wabeba pochi za watu kwa kusindikiza safari za uongozi kwa watu wengine  na kuwataka kuomba nafasi za uongozi kuanzia ngazi za Serikali za mitaa ambazo zipo mbioni kuelekea kwenye uchaguzi utakaofanyika  mapema mwaka huu 2019.

 Akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Kampeni ya Dar ya Kijani yenye lengo la kutoa hamasa kwa vijana wa UVCCM kushiriki kikamilifu katika kugombea nafasi za uongozi na kurudisha mitaa yote ya Jiji la Dar es Salaam kwenye himaya yao,  Mwalimu amesema kuwa Dar lazima iwe mfano na vijana wajitokeze na kuwa sehemu ya historia ya ujenzi wa Taifa la Tanzania chini ya Jemedari mkuu na Mzalendo, Rais Dkt. John Joseph Magufuli.

Katika mkutano huo uliohudhuriwa na  vijana toka wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam, Mwangwala ametoa rai kwa Mikoa yote nchini  kuiga kampeni za namna hiyo zinazolenga zinazojenga Ari, hamasa na moyo wa kukiimarisha Chama Cha Mapinduzi.

Aidha amewakumbusha Vijana kutumia vizuri mitandao ya kijamii kwa kuendesha kampeni mbalimbali lakini kujibia upotoshwaji unaofanywa  na upinzani. Amewataka Vijana kufanya tafiti ili kusaidia kupata ufumbuzi wa matatizo mbalimbali ili kuzidi kuendeleza taifa zaidi.

Pia ameomba kamati za maadili kuwafukuza wanachama wa CCM wanaoendekeza siasa za makundi na kuchafuana ndani ya Chama.

Mwalimu ametoa salamu za Mwenyekiti za UVCCM Taifa, Kheri James kwa wanachama hao na  kueleza kuwa kiongozi huyo mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi anavyofanya kazi usiku na mchana ili kuifanya UVCCM kubaki na heshima iliyojijengea.


Awali, akimkaribisha katibu mkuu, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar Es Salaam, Musa Kilakala ameeleza kuwa Umoja huo umejipanga kuchukua mitaa yote ya jijini Dar es salaam kupitia kampeni hiyo ya Dar ya Kijani ambayo  itatoa majibu kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019.

Kongamano la "Ifanye Dar iwe Kijani" limeendeshwa na UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Chuo kikuu cha Dar es salaam tawi la Elimu (DUCE.)
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mwalimu Raymond Mangwala akizungumza na vijana wa umoja huo kanda ya Dar es salaam katika kongamono la  Dar ya kijani, na kuwataka vijana hao kulitumikia taifa kwa kugombea nafasi za uongozi, leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wakifuatilia mada katika kongamano la Dar ya kijani ambalo viongozi wa umoja huo kwa kushirikiana na wanachama hao wamejizatiti kuzitumikia vyema nafasi za uongozi katika kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Joseph Magufuli katika kujenga taifa, leo jijini Dar es Salaam.

BREAKING NEWS:MAHAKAMA YABARIKI UWENYEKITI WA PROFESA LIPUMBA

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imekubaliana na uamuzi wa Msajili wa Vyama vya Siasa wa kumtambua Profesa Ibrahimu Lipumba  kuwa Mwenyekiti halali wa Chama cha Wananchi CUF.

Aidha imetupilia mbali maombi yaliyofunguliwa na  Maalimu Seif  Sharifu Hamad aliyeomba mahakama kutoa amri ya kubatilisha barua ya Msajili wa Vyama ya kumtambua Profesa Lipumba kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.

SERIKALI YAPANIA UWEKEZAJI UTALII KANDA YA ZIWA

$
0
0
Serikali imesema kuwa itaendelea kuweka mazingira rafiki, kuwahamasisha na kuwavutia Wawekezaji watakaosaidia kuwapeleka watalii katika maeneo ya Kanda ya Ziwa ili kukuza Sekta ya Utalii Katika maeneo hayo.

Hatua hiyo inakuja baada ya kuyapandisha hadhi Mapori ya Akiba ya  ya  Burigi, Biharamulo, Kimisi,Ibanda na Rumanyika kuwa Hifadhi ya Taifa.

Akizungumza kwenye mkutano uliohusisha  Wizara Maliasili na Utalii  na Wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali nchini, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amesema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Sekta binafsi kwa kuwa sekta hiyo ni injini ya Utalii nchini.

 Amesema kuwa mkutano huo una umuhimu mkubwa Katika maendeleo ya sekta hiyo kwa kuwa Serikali  inapata  nafasi ya kuwaelezea Wawekezaji fursa mbalimbali  zinazopatika katika Ukanda huo pamoja na kusikia changamoto zao.

Amesema kufuatia kufanyika kwa mkutano huo Sekta Binafsi itakuwa na kila sababu ya kuwekeza katika Ukanda huo baada ya Serikali kuendelea kuweka mazingira rafiki kwa Uwekezaji

Amesema Serikali imeendelea kuweka Miundombinu wezeshi ambayo imekuwa chachu ya kurahisisha watalii na wageni mbalimbali kutembelea maeneo ya hifadhi.

Mhe.Kanyasu ameyataja maeneo yaliyoboreshwa  kuwa  ni  Barabara,   Uwanja wa ndege wa Mwanza pamoja na  Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Chato ambao umefunguliwa.

Hata hivyo, Mhe.Kanyasu amesema kuwa licha ya   kuwa Tanzania imekuwa ikifanya vizuri kwenye shughuli za Uhifadhi, lakini katika Uendelezaji Utalii bado jitihada za makusudi zinahitajika.

"Tuna vivutio vingi vya utalii lakini idadi ya watalii wanaotembelea vivutio hivyo hairidhishi, tunahitaji kuongeza juhudi katika kuwahamasisha watalii wa ndani na nje ya nchi kutembelea maeneo hayo" Amesisitiza 

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ambaye alikua mwenyeji wa mkutano huo, Prof.Adolf Mkenda amesema kupitia mkutano huo kutasaidia kuchagiza idadi ya watalii kuongezeka kwa kutembelea vivutio vya utalii vinavyopatikana katika ukanda huo.

Amesema kufanyika kwa mkutano huo ni muendelezo wa kutawanya fursa za uwekezaji wa sekta ya utalii nchi nzima.

Akichangia hoja kwenye mkutano huo, Mwenyekiti wa Chama cha Wasafirishaji Watalii ( TATO)Wilbard Chamburo ameiomba Serikali iangalie uwezekano wa kutobadili  mara kwa mara sera na mipango ya kukuza masuala ya Utalii kwa kuwa kuwa hali hiyo inayochangia kuwakatisha tamaa Wawekezaji.

Amesema Wawekezaji wanataka kuwekeza mahali ambako wana uhakika wa kupata  faida itayowasaidia kujiendesha kibiashara pamoja na kulipa kodi stahiki za serikali.

Katika mkutano huo, Wakuu wa mikoa yote ya Kanda ya Ziwa wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Mhe.John Mongela walikua miongoni mwa Washiriki.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungumza  kwenye ufunguzi wa mkutano wa siku moja uliofanyika jana jijini Mwanza  baina ya Wizara ya Maliasili na Utalii  na Wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuhamasisha Utalii Ukanda wa Ziwa 
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella (wa kwanza kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Hifdadhi za Taifa.Alllan Kijazi (kulia) kabla ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine  (wa pili kushoto)  Kanyasu kufungua mkutano baina ya Wizara hiyo na Wawekezaji  uliofanyika jijini Mwanza
 Baadhi ya washiriki wa mkutano baina ya Wizara ya Maliasili na  Utalii hiyo na Wawekezaji  uliofanyika jijini Mwanza
 Baadhin ya Wawekezaji wakubwa walioshiriki mkutano wa kuhamasisha utalii kanda ya Ziwa
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungumza  kwenye  mkutano wa siku moja uliofanyika jana jijini Mwanza  baina ya Wizara ya Maliasili na Utalii  na Wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali nchini ka lengo la kuhamasisha Utalii Ukanda wa Ziwa 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu (mbele) akiwa ameongozana na Naibu waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela(katikati) 
( Wizara ya Maliasili na Utalii) 

SERIKALI KUKARABATI MAENEO YA HARAKATI ZA UKUMBOZI ILI KULINDA HISTORIA - DKT MWAKYEMBE

$
0
0

Na Tiganya Vincent
SERIKALI imesema inatafuta fedha kwa ajili ya kukarabati maeneo yote yaliyopo Tanzania ambayo yaliyotumika katika harakati za kudai uhuru na ukombozi katika nchi mbalimbali barani Afrika ili kutunza historia yake isipotee.
Kauli hiyo imetolewa jana Wilayani Kaliua  na Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe wakati wa ziara yake ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika ikiwemo eneo la Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo.
Waziri alisema kuwa lengo ni kutaka historia ya mashujaa na maeneo waliyotumia isipotee ili kuwafanya  vijana wa sasa na vizazi vijavyo viwe na ukweli wa historia za mashujaa wote.
Alisema ukarabati huo unakwenda sanjari na kutafuta kumbukumbu zote walizotumia  wapigania uhuru mbalimbali kwa ajili kuzitambua na kuzihifadhi rasmi kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo ili kulinda historia isije ikapotea.
Dkt. Mwakyembe alitoa wito kwa watanzania wote wenye taarifa za kumbukumbu mbalimbali zikiwemo picha, vitabu, mashairi, nyimbo, barua na nyaraka mbalimbali zilizotumiwa na wapigania uhuru wa Tanzania na nje ya Nchi kuwasilisha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo au kwa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa ili ziweze kutunzwa kwa ajili ya manufaa ya Nchi na bara la Afrika kwa ujumla.
Aidha aliwataka wananchi na Viongozi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha wanalinda alama zote zilizopo katika maeneo yaliyotumiwa na wapigania uhuru ikiwemo majina katika makaburi na majengo ili kutopotezakumbukumbu za mashujaa.
Katika hatua nyingine, Waziri huyo aliwataka wataalamu mbalimbali wakiwemo Maafisa Utamaduni kuhakikisha wanatumia hazina ya wazee waliopo ambao wanajua historia ya kweli kuhusu harakati za kudai uhuru nchini na mapambano ya ukombozi barani Afrika kupata maelezo na kuyaandika kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ili zisitoweke.
“Tunajua kila mtu atakufa hivyo ni vema tukatumia hazina ya wazee wetu waliopo sasa kupata historia ya kudai uhuru na harakati za ukumbozi zilizofanyika nchini ili kuweka kumbukumbu zote” alisema.
Alisema simulizi ya wazee ni muhimu katika kuhakikisha hakuna mashujaa walioshiriki harakati za kudai uhuru na ukombozi wa bara la Afrika watakaoachwa katika kumbukumbu za historia.
 Mtemi Mirambo wa II (Salumoni Kazikwa) (kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (kulia) kuhusu makaburi mbalimbali  ya ndugu zake Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo wakati wa ziara yake jana ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika.
 Mtemi Mirambo wa II (Salumoni Kazikwa) (mwenye kanzu nyeusi) akimwonyesha  Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (aliyevaa mgolole mweusi) choo kilichotumiwa na Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo wakati wa ziara yake jana ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika ikiwemo eneo la Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo.
 Mtemi Mirambo wa II (Salumoni Kazikwa) (kushoto) akimwongoza Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (kulia) kutoka nje ya makaburi mbalimbali  ya ndugu zake Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo wakati wa ziara yake jana ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika ikiwemo eneo la Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo.
 Mtemi Mirambo wa II (Salumoni Kazikwa) (mwenye kanzu nyeusi) akitoa maelezo kwa Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (aliyejifunga mgolole mweusi) kuhusu kisima kilichotumiwa Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo wakati wa ziara yake jana ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika ikiwemo eneo la Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo.
 Mti uliotumiwa na Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo kama Mahakama wakati wa utawala wake.
 Mtemi Mirambo wa II (Salumoni Kazikwa) (mwenye Kanzu nyeusi) akimwonyesha  Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (aliyejifunga mgolole mweusi) mabaki ya Ghorofa la Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo ambalo limetitia . Waziri alipata maelezo hayo wakati wa ziara yake jana ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika.
 Mtemi Mirambo wa II (Salumoni Kazikwa) (mwenye Kanzu nyeusi) akimwonyesha  Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (aliyejifunga mgolole mweusi) mabaki ya Ghorofa la Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo ambalo limetitia . Waziri alipata maelezo hayo wakati wa ziara yake jana ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika.
 Mtemi Mirambo wa II (Salumoni Kazikwa) (aliyechuchumaa) akimwombea Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (aliyekaa kwenye kigoda) kwenye kaburi la Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo wakati wa ziara yake jana ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika ikiwemo eneo la Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe akizugumza na wananchi kwenye Ikulu ya Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo wakati wa ziara yake jana ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika ikiwemo eneo la Shujaa wa Afrika Mashariki na Kati Mtemi Mirambo.  Picha na Tiganya Vincent

Mawaziri wakutana na Watanzania waishio Namibia

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.), akiambatana na Waziri Ofisi ya Rais, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Issa Haji Ussi Gavu; Waziri wa Viwanda na Biashara, George Kakunda (Mb.) na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) tarehe 17 Machi, 2019, wamepata fursa ya kukutana na jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Namibia na kujadiliana nao masuala mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa vitambulisho vya taifa na hati za kusafiria, maendeleo na hali ya siasa nchini, biashara kwa ujumla na mkakati wa serikali katika kunufaika uanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Miongoni mwa masuala mengine, mawaziri hao wamewataarifu Watanzania hao kuhusu juhudi mbalimbali zinazotekelezwa na serikali ya awamu ya tano katika kuleta maendeleo ambazo ni pamoja na kuimarika kwa ukusanyaji wa mapato na udhibiti wa uvujaji wa mapato; ujenzi wa miundombinu kwa ajili ya kurahisisha usafirishaji wa mazao na bidhaa; ukuaji katika sekta ya viwanda; ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme katika Korongo la Stiglers;kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za kijamii zikiwemo afya na elimu bure na mkakati wa Tanzania kujitanua kibiashara katika eneo la SADC.

Prof. Kabudi amewataka Watanzania hao kuacha kuamini dhana kuwa, chema chajiuza na kibaya chajitembeza na kuanza kuyasemea masuala mbalimbali mazuri ya Tanzania. Ametolea mfano uwepo wa uhitaji mkubwa wa vitu vyenye ubora vinavyozalishwa nchini kama vigae, nepi za watoto, korosho na mvinyo na kuwataka Watanzania hao kuitumia fursa hiyo kuwa mawakala wa bidhaa hizo nje ya nchi.Suala hilo limeungwa mkono na Watanzania hao ambao wameiomba Wizara ya Viwanda na Biashara kuwapa taarifa sahihi za kibiashara na kwa wakati. 

Kuhusu suala la kila Mtanzania kuwa na hati mpya ya kielektronikia ya kusafiria ifikapo mwaka 2020, Prof. Kabudi amewataarifu Watanzania hao kuwa, serikali inaziboresha hati za sasa za kusafiria kwa mujibu wa makubaliano ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Hivyo, ameitaka jumuiya ya Watanzania wanaoishi nje ya Tanzania kuhakikisha wanakuwa na vitambulisho vya kitaifa ambavyo ni moja ya vielelezo muhimu katika kuomba hati hizo mpya za kusafiria.

Prof. Kabudi amewahakikishia Watanzania hao kuwa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kitengo cha Diaspora, kipo wazi muda wote ili kuwasaidia Watanzania wanaoishi nje ya nchi ili kuhakikisha wanapata vitambulisho hivyo vya taifa kwa wakati.

Mawaziri hao wapo nchini Namibia kwa lengo la kuhudhuria mkutano wa Baraza la Mawaziri la SADC ambao umefanyika kuanzia tarehe 15 hadi 17 Machi, 2019. 

Wajumbe walioshiriki katika mkutano huo wakifungua mkutano kwa kuimba wimbo wa taifa.
Kaimu Balozi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini ambao pia unawakilisha nchini Namibia, Richard Lupembe, akimkaribisha Prof. Kabudi kwa ajili ya kufungua mkutano huo.
Sehemu ya Watanzania waishio nchini Namibia wakifuatilia mkutano huo.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, akifurahia jambo wakati wa mkutano huo.Pembeni yake ni baadhi ya Watanzania waishio Namibia.

MKAZI WA YOMBO DOVYA ASHINDA KITITA CHA MILIONI 10 KUTOKA BIKO

$
0
0
Mfanyabiashara mwenye maskani yake Yombo Dovya, jijini Dar es Salaam anayeitwa Ramadhan Kitwemu, amekabidhiwa fedha zake sh milioni 10 alizoshinda kutoka kwenye bahati nasibu ya Biko inayotoa mamilioni na bodaboda kwa Watanzania kila siku, ambapo droo kubwa hufanyika kila Jumatano na Jumapili kwa kucheza sh 500 na sh 1000, huku namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba ni 2456.

Mawaziri wakutana na Watanzania waishio Namibia

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.), akiambatana na Waziri Ofisi ya Rais, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Issa Haji Ussi Gavu;Waziri wa Viwanda na  Biashara, Mhe. George Kakunda (Mb.) na  Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb.) leo tarehe17 Machi, 2019, wamepata fursa ya kukutana na jumuiya ya  Watanzania wanaoishi nchini Namibia na   kujadiliana nao masuala mbalimbali ikiwemo  upatikanaji wa vitambulisho vya taifa na hati za kusafiria,  maendeleo na hali ya siasa nchini, biashara kwa ujumla na mkakati wa serikali katika kunufaika uanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Miongoni mwa masuala mengine, mawaziri hao wamewataarifu Watanzania hao kuhusu juhudi mbalimbali zinazotekelezwa na  serikali ya awamu ya tano katika kuleta maendeleo ambazo ni pamoja na kuimarika kwa ukusanyaji wa mapato na udhibiti wa uvujaji wa mapato; ujenzi wa miundombinu kwa ajili ya kurahisisha usafirishaji wa mazao na bidhaa; ukuaji katika sekta ya viwanda; ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme katika Korongo la Stiglers;kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za kijamii zikiwemo afya na elimu bure na mkakati wa Tanzania kujitanua kibiashara katika eneo la SADC.



Mhe. Prof. Kabudi amewataka Watanzania hao kuacha kuamini dhana kuwa, chema chajiuza na kibaya chajitembeza  na kuanza kuyasemea masuala mbalimbali mazuri ya Tanzania. Ametolea mfano uwepo wa uhitaji mkubwa wa vitu vyenye ubora vinavyozalishwa nchini kama vigae, nepi za watoto, korosho na mvinyo na kuwataka Watanzania hao kuitumia fursa hiyo kuwa mawakala wa bidhaa hizo nje ya nchi.Suala hilo limeungwa mkono na Watanzania hao ambao wameiomba Wizara ya Viwanda na Biashara kuwapa taarifa sahihi za kibiashara na kwa wakati.


 Kuhusu suala la kila Mtanzania kuwa na hati mpya ya kielektronikia ya kusafiria ifikapo mwaka 2020, Mhe. Prof. Kabudi amewataarifu Watanzania hao kuwa, serikali inaziboresha hati za sasa za kusafiria  kwa mujibu wa makubaliano ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Hivyo, ameitaka jumuiya ya Watanzania wanaoishi nje ya Tanzania kuhakikisha wanakuwa na vitambulisho vya kitaifa ambavyo ni moja ya vielelezo muhimu katika kuomba hati hizo mpya za kusafiria.

 Mhe.Prof. Kabudi amewahakikishia Watanzania hao kuwa, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kitengo cha Diaspora, kipo wazi muda wote ili kuwasaidia Watanzania wanaoishi nje ya nchi ili kuhakikisha wanapata vitambulisho hivyo vya taifa  kwa wakati.



Mawaziri hao wapo nchini Namibia kwa lengo la kuhudhuria mkutano wa Baraza la Mawaziri la SADC ambao umefanyika kuanzia tarehe 15 hadi 17 Machi, 2019.

Wajumbe walioshiriki katika mkutano huo wakifungua mkutano kwa kuimba wimbo wa taifa.

 Kaimu Balozi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini ambao pia unawakilisha nchini Namibia, Richard Lupembe, akimkaribisha Mhe. Prof. Kabudi kwa ajili ya kufungua mkutano huo.

Sehemu ya Watanzania waishio nchini Namibia wakifuatilia mkutano huo.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, akifurahia jambo wakati wa mkutano huo.Pembeni yake ni baadhi ya Watanzania waishio Namibia.




Viewing all 110091 articles
Browse latest View live




Latest Images