Naibu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Michezo Wizarani Bw.Moshi Makuka |
Naibu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Michezo la Wizarani (SHIMIWI) Bw. Moshi Makuka amesema shirikisho hilo linatarajia kufanya mkutano wa tathmini wa mashindano ya SHIMIWI ya mwaka huu mjini Morogoro tarehe 13 na 14 Desemba, 2013.
Akiongea ofisini kwake Bw.Makuka alisema kuwa lengo kuu la mkutano huo ni kujadili changamoto zilzojitokeza kwenye mashindano ya mwaka huu.
“Lengo ni kujadili changamoto zilizojitokeza katika mashindano ya SHIMIWI ya mwaka huu na kuzipatia ufumbuzi kwa ajili ya kuboresha michezo ya mwaka ujao” alisema Bw.Makuka.
Aidha,Bw Makuka aliwataka Wenyeviti wa vilabu,Makatibu wa Vilabu na Maafisa Michezo kufika bila kukosa ili kukuza michezo serikalini.
“Wenyeviti,Makatibu na Maafisa Michezo wa vilabu wahudhurie kwa wingi ili waje kutoa changamoto zao walizokutana nazo katika michezo ya mwaka huu” alifafanua Bw.Makuka.
Shirikisho la Michezo Wizarani (SHIMIWI) kila mwaka huandaa michezo inayowakutanisha watumishi wa serikali kutoka katika Wizara,Idara zinazojitegemea,Wakala wa serikali na Ofisi za Wakuu wa Mikoa ambapo kwa mwaka huu yalifanyika mjini Dodoma kuanzia tarehe Septemba 21 hadi Oktoba 5.
Wajumbe wanaotakiwa kuhudhuria mkutano huo ni Mwenyekiti, Katibu na maafisa michezo wote kutoka vilabu vya SHIMIWI. Hadi sasa mikoa ya Dodoma na Kilimanjaro imeshatuma maombi ya kushiriki, na mikoa mingine inahimizwa kufanya hivyo mapema iwezekanavyo>
Wajumbe wanaotakiwa kuhudhuria mkutano huo ni Mwenyekiti, Katibu na maafisa michezo wote kutoka vilabu vya SHIMIWI. Hadi sasa mikoa ya Dodoma na Kilimanjaro imeshatuma maombi ya kushiriki, na mikoa mingine inahimizwa kufanya hivyo mapema iwezekanavyo>