Anaandika Abdullatif. Yunus.
Mkuu wa Mkoa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti ameongoza mamia ya wakazi wa Mkoa Kagera Kuupokea na kuusindikiza Mwili wa Marehemu Ruge Mutahaba mpaka Nyumbani kwao Kabale.
Awali imewasili Ndege ya Abiria ikiwa na Wanahabari, watu mashuhuri na wasanii kabla ya kuwasili Ndege ya Serikali iliyobeba Mwili wa Marehemu pamoja na Waombolezaji mbalimbali wakiwemo wafiwa.
Mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Bukoba, na kupokelewa na wananchi kutoka maeneo mbalimbali wakiwemo Sheikh wa Mkoa Kagera Haruna Kichwabuta, Mkuu wa Wilaya Bukoba Deodatusi Kinawiro, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Bukoba atakapozikwa Ruge, Viongozi Mbalimbali pamoja na Wanachama wa CCM Mkoa wa Kagera, Msafara huo ulianza safari ya Kuelekea Kijijini Kiziru - Kabale kwa kupitia Barabara Kashai, Uganda, Kibeta, Magoti, Hadi Nyumbani Kabale. Tayari Mwili huo umewasili salama Na umepumzishwa Nyumbani huku Kwaya zikiendelea kutumbuiza na watu mbalimbali wanafika kusaini katika kitabu cha Waombilezaji.
Kesho Mwili wa Marehemu Ruge unatarajiwa kutolewa Nyumbani hapo kwa Msafara kuelekea Viwanja vya Gymkhana ampapo shughuli nyingine zitaendelea huko ikiwemo kuaga, na Ibada kabla ya Kurejeshwa tena Kiziru kwa Msafara kwa ajili ya Mazishi.
Mwili Wa marehemu Ruge Mutahaba tayari umekwisha wasili nyumbani kwao kijijini Kiziru Bukoba mkoani Kagera leo,ambapo watu mbalimbali wamejitokeza kumpokea,huku msafara huo ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti .
Sanduku lenye mwili wa Marehemu Ruge Mutahaba ukipokelewa uwanja wa ndege wa Bukoba 'Bukoba Airport',na kupokelewa na watu mbalimbali huku Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti akiongoza mapokezi hayo.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera,Brigedia Jenerali Marco Gaguti amefika uwanja wa ndege kuongoza mapokezi ya mpendwa wetu Ruge Mutahaba. Kabla Brigedia Jenerali Marco Gaguti kufika hapa Kagera alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe kipindi kile alikuwa ni Kanali kabla ya kupanda cheo amefanya kazi za kizalendo bega kwa bega na Ruge Mutahaba mojawapo ikiwa ni Fursa na Ile ya Umoja wa Mataifa Kigoma Programu ya pamoja.
Wazazi wa Marehemu Ruge,Prof Mutahaba na Mkewa akiwasili uwanja wa ndege wa Bukoba.
Mtoto wa kwanza wa Marehemu akifarijiwa baada ya kuwasili Bukoba.
Sanduku lenye mwili wa Marehemu Ruge Mutahaba likipokelewa uwanja wa ndege wa Bukoba 'Bukoba Airport',na kupokelewa na watu mbalimbali huku Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti akiongoza mapokezi hayo.