Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live

MAGAETI YA LEO JUMATATU FEBRUARI 25,2019


NAIBU WAZIRI NISHATI AKERWA NA MKANDARASI MBABAISHAJI

$
0
0
 Na Veronica Simba – Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amekemea vikali utendaji kazi mbovu wa Mkandarasi State Grid, anayetekeleza mradi wa umeme vijijini Mkoa wa Lindi, kutokana na kufanya kazi chini ya kiwango na kutokamilisha wigo wake kwa wakati kama mkataba unavyoelekeza.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nangambi Naipuli, Kata ya Mingumbi, wilayani Kilwa, Mkoa wa Lindi, jana Februari 24, mwaka huu, Naibu Waziri alisema Serikali imemvumilia kwa muda mrefu Mkandarasi huyo, ambaye pia anatekeleza mradi huo katika Mkoa wa Morogoro.

Kufuatia utendaji huo duni wa mkandarasi husika, Naibu Waziri alikataa kuwasha umeme katika kijiji hicho, kama ilivyokuwa imepangwa, na kuelekeza kuwa atafanya zoezi hilo pale ambapo idadi ya wananchi waliounganishiwa umeme itakapokuwa ya kuridhisha, tofauti na idadi ndogo ya waliounganishiwa sasa ambayo ni watano tu.

“Huu ni utapeli mtupu, mimi sitafanya kazi hii. Siwashi umeme na naenda kutoa taarifa kwenye mamlaka zinazohusika kwamba mkandarasi anababaisha.”

Akifafanua, Naibu Waziri alieleza kuwa Mkandarasi huyo amekuwa mwenye kiburi na asiyejirekebisha na kwamba taarifa za utendaji wake mbovu tayari zinafahamika hadi wizarani hivyo hakuna haja ya kuendelea kumvumilia, bali ni lazima hatua stahiki zichukuliwe dhidi yake.

Kufuatia hali hiyo, Afisa Tawala wa Wilaya ya Kilwa, ambaye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo, Christopher Ngubiagai, alimtaka Mkandarasi husika kuripoti ofisini kwake siku ya Jumatano, Februari 27 mwaka huu, akiwa na Hadidu za Rejea ili pamoja na mambo mengine, akaeleze amejipanga vipi kukamilisha kazi husika ndani ya muda wa makubaliano.

Awali, Naibu Waziri Mgalu alitembelea na kukagua Kituo cha kufua umeme kwa kutumia gesi asilia cha Somanga kilichopo wilayani Kilwa, ambapo alieleza kwamba Serikali imedhamiria kupeleka umeme wa uhakika na wa kutosha katika mikoa yote ya Kusini.

Aidha, Naibu Waziri alitembelea pia vijiji vya Kisangi na Mkwanyule pamoja na Kilwa Kisiwani ambapo alizungumza na wananchi kuhusu masuala mbalimbali ya umeme pamoja na kupokea kero zao.

Akiwa Kilwa Kisiwani, alimsisitiza Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Umeme Jua mahala hapo, ambaye ni Kampuni ya Green Leaf, kuhakikisha anakamilisha kazi hiyo kwa wakati, kabla ya Juni 30 mwaka huu, ambapo Mkataba wake utakwisha.

Naibu Waziri yuko katika ziara ya kazi ya siku Nne mkoani Lindi, ambayo aliianza jana, Februari 24, mwaka huu. Katika ziara hiyo, amefuatana na wataalamu mbalimbali kutoka wizarani, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
 Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu (mwenye kinasa sauti), akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nangambi Naipuli, Kata ya Mingumbi, wilayani Kilwa, Mkoa wa Lindi, jana Februari 24, mwaka huu, akiwa katika ziara ya kazi.
 Mkazi wa kijiji cha Mkwanyule, Kata ya Masoko, wilayani Kilwa, Rehema Sudi (kulia), akitoa maoni yake kuhusu masuala ya umeme, kwa Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (mwenye kilemba), wakati wa ziara yake eneo hilo jana, Februari 24, mwaka huu.
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (mwenye kilemba – katikati), akiwa katika usafiri wa Boti ndogo pamoja na Ujumbe wake, kuelekea Kilwa kisiwani, mkoani Lindi, jana Februari 24, mwaka huu akiwa katika ziara ya kazi.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (mwenye kilemba cha kijani), akiwasili Kilwa kisiwani, mkoani Lindi, kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme na kuzungumza na wananchi, akiwa katika ziara ya kazi, jana Februari 24, mwaka huu.

KILUWA YATENGA DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI 150,KUJENGA KIWANDA CHA MABEHEWA NCHINI

$
0
0
WAKATI Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Magufuli, ikidhamiria kuinua uchumi kwa kutumia miundombinu ya usafirishaji, wadau wa maendeleo wamekuwa wakitumia fursa zilizopo kunufaisha watanzania.

Miongoni mwao ni Mkurugenzi wa Makampuni ya Kiluwa Group, Mohamed Kiluwa ambaye amedhamiria kuanzisha kiwanda cha kutengeneza mabehewa ya treni yaliyochakaa kwa kutumia reli ya kisasa na ya zamani.

Akiwa katika hafla ya kubadilishana nyaraka za makubaliano hayo aliyoingia na Kampuni ya Africa Jambo Group ya nchini Afrika Kusini, katika Jiji la Johannesburg hivi karibuni Kiluwa alisema anataka kufanya kitu cha kipekee katika ardhi ya Tanzania kinyume na matarajio ya wengi.

“Hiki tunachotaka kukifanya hakijawahi kufikiriwa na wengi lakini kitaleta tija katika uchumi wa nchi, tunafahamu tunapoelekea ni Tanzania ya viwanda na uchumi wa kati. Tutahitaji mbinu bora za usafirishaji malighafi na bidhaa, reli ni njia rahisi na salama kusafirishia mizigo,” alisema Kilua.

Alibainisha,  kiwanda hicho kitakuwepo katika eneo la uwekezaji Kiluwa Free Processing Zone mkoani Pwani, ambapo taarifa ya awali ya utekelezaji wa mradi huo inabainisha utakuwa katika awamu tatu.

Kila awamu itatoa ajira kwa watu  wapatao 980, mradi huo unalenga katika soko la ndani ya Tanzania na Afrika kwa ujumla. Vilevile wakazi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki watakuwa sehemu ya wanufaika kwa kuwa baadhi ya mizigo itakwenda katika nchi jirani za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi hadi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) pamoja na nchi za ukanda wa kusini mwa Afrika.

“Ifahamike tumetenga kiasi cha Dola za Kimarekani Milioni 150, kwa ajili ya kukamilisha mradi huu ambao utaleta mapinduzi makubwa katika sekta ya viwanda nchini pamoja na usafirishaji,” alisema Kiluwa.

Naye, mwakilishi wa Kampuni ya Africa Jambo Group, Marthinus Christian Landman alisema wameamua kuwekeza Tanzania kwa sababu wanajua ni eneo muhimu linalokua kwa kasi kiuchumi kutokana na malengo makubwa yaliyowekwa na serikali iliyopo madarakani.

“Siku zote mfanyabiashara anaangalia eneo ambalo atanufaika, tunaangalia zaidi faida kabla ya kukamilisha mikataba, tumejiridhisha kwa sasa Tanzania ni sehemu sahihi na salama kiuewekezaji kwa sababu Rais Dk. John Magufuli amedhamiria kuona watu wanafanya kazi, hakuna kona kona wala rushwa,” alisema Landman.  
  Mkurugenzi wa Makampuni ya Kiluwa Group ,Mohamed Kiluwa (kulia) na Mwakilishi wa Kampuni ya Africa Jambo Group ya nchini Afrika Kusini,Marthinus Christiaan LandMan wakibadilishana nyaraka za mkataba wa makubaliano ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza mabehewa ya treni ya zamani (Analogy) na ya Kisasa (Standard Gauge) nchini Tanzania. Makubaliano hayo yamefanyika nchini Afrika Kusini mwishoni mwa wiki,na kwamba mradi huo utakuwa na awamu tatu,ambapo kila awamu itatoa ajira ya Wafanyakazi  wapatao 980,mradi huo ukifanikiwa utalenga soko la ndani na nje.
 Mkurugenzi wa Makampuni ya Kiluwa Group ,Mohamed Kiluwa na Mwakilishi wa Kampuni ya Africa Jambo Group ya nchini Afrika Kusini,Marthinus Christiaan LandMan wakisaini nyaraka za mkataba wa makubaliano ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza mabehewa ya treni ya zamani (Analogy) na ya Kisasa (Standard Gauge) nchini Tanzania. Makubaliano hayo yamefanyika nchini Afrika Kusini hivi karibuni,na kwamba mradi huo utakuwa na awamu tatu,ambapo kila awamu itatoa ajira ya Wafanyakazi  wapatao 980,mradi huo ukifanikiwa utalenga soko la ndani na nje.

DC MUHEZA ATOA MAAGIZO KWA MKURUGENZI WA HALMASHAURI HIYO

$
0
0
Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Rivets Resa Limited ya Mkoani Arusha Bahati Kittoh kulia akimkabidhi vifaa tiba Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto vyenye thamani ya milioni 400 kwa ajili ya kusambaza kwenye vituo mbalimbali vya Afya wilayani humo kushoto ni Mganga Mkuu wa wilaya ya Muheza (DMO) Flora Kessy katikati ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu 
Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu katika akiwa na Mganga Mkuu wa wilaya ya Muheza (DM) Flora Kessy kulia na Mkurugenzi wa Taasisi ya Rivets Resa Limited ya Mkoani Arusha Bahati Kittoh kushoto 
MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa tiba hivyo
Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu akizungumza ambapo pamoja na mambo mengine aliishukuru Taasisi hiyo kwa kusaidia vifaa tiba
Mkurugenzi wa halmashauri ya Muheza akizungumza kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Muheza Balozi Adadi Rajabu kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Rivets Resa Limited ya Mkoani Arusha Bahati Kittoh
Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Rivets Resa Limited ya Mkoani Arusha Bahati Kittoh akizungumza kulia ni DMO wa wilaya ya Muheza Flora Kessy
wakiangalia mashine ya kufanyia mazoezi 
sehemu ya vifaa vilivyotolewa 


MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Mhandisi Mwanasha Tumbo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha vifaa vilivyotolewa na Taasisi ya Human Bridge ya nchini Sweeden vina sambazwa kwenye vituo vya afya kabla ya Machi 15 mwaka huu ili viweze kusaidia kutoa huduma. 

Agizo la Mkuu huyo wa wilaya alilitoa wakati akipokea vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya milioni 400 vilivyotolewa na Taasisi hiyo kupitia taasisi ya Rivets Resa Limited ya Mkoani Arusha kwa ajili ya kuhakikisha wanaboresha huduma za Afya kwenye maeneo yao. 

Alisema vifaa hivyo vipelekwe kwenye vituo vinavyotoa huduma kwa sasa na vile ambavyo havijakamilika havitapelekewa huko pindi vitakapokamilika huku akieleza kwenye maeneo ya changamoto ya umeme watasimamia kuhakikisha umeme unapatikana ili vifaa hivyo viweze kutumika kwenye matumizi yaliyokusudiwa. 

“Nikuagize Mkurugenzi wa Halamshauri hakikisheni vifaa hivi vinapelekwa kwenye vituo vya Afya vilivyopo wilayani hapa kabla ya Machi 15 mwaka huu kwa lengo la kuweza kusaidia kutoa huduma za Afya”Alisema DC huyo. 

Alisema haikuwa kazi rahisi kuweza kutengeneza orodha ya vifaa hivyo huko akipongeza juhudi kubwa zilizofanywa na mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kuwa karibu sana kuhakikisha vifaa hivyo vinafika wilayani humo 

“Lakini pia niseme kwamba hizo ni jitihada za serikali ya awamu ya tano kutokana na uchapakazi wake umekuwa chachu ya kuwavutia wadau mbalimbali wa maendeleo kuweza kuchangia na kuunga mkono harakati za wananchi kuweza kupata mafanikio kupitia sekta mbalimbali “Alisema 

“Tunawapongeza kwa kuguswa kwao kuona wasaidie kutoa vifaa tiba hivyo vya kutolea huduma kwa wilaya ya Muheza…vifaa vya sh.milioni 400 sio kitu kidogo tunawashukuru hatuna cha kuweza kuwalipa zaidi ya kuwaombea endeleeni kuisaidia wilaya ya Muheza ili iweze kuondokana na changamoto ya vifaa tiba”Alisema DC Mhandisi Mwanasha. 

Awali akizungumza katika makabidhiano hayo Mganga Mkuu wa wilaya ya Muheza Flora Kessy alisema halmashauri hiyo iliomba vifaa tiba hivyo kwenye Taasisi ya Human Bridge ya nchini Sweeden yeye February 2 mwaka jana lengo likiwa kuweza kukabiliana na changamoto ya uhaba wa vifaa tiba na vitandanishi katika vituo vya kutolea huduma za afya wilayani humo. 

Alisema kwamba vifaa hivyo vitasaidia kuboresha huduma za Afya na vitasambazwa kwenye vya kutolea huduma vitasambazwa kwenye kituo cha Afya cha Mkuzi ambapo watapeleka vifaa mbalimbali ikiwemo ultra sound,vitanda, magodoro, wheel chairs,vifaa vya upasuaji,vifaa vya macho na vifaa vya masikio . 

“Lakini pia halikadhalika vitapelekwa kwenye vituo vya Afya Ubwari ambazo ni kitanda cha chumba cha upasuaji,mashine ya usingizi,taa ya chumba cha upasuaji,mashine ya kusaidia upumuaji na ultrasound ikiwemo vituo vyengine vya afya kulingana na uhitaji kupitia taarifa za walezi wa zahanati husika”Alisema. 

“Kipekee niishukuru taasisi ya human bridge kupitia Taasisi ya Rivetsresa Limited iliyopo Arusha kwa kutupatia msaada wa vifaa tiba bila malipo yoyote…hakika hatuna cha kuwalipa lakini tutaendelea kuwaombea kwa Mungu pia tunahaidi kuendelea kuvitunza vifaa hivi”Alisema DMO huyo. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Bahati Kittoh wataendelea kuisapoti serikali ya awamu ya tano katika kuhakikisha changamoto ya vifaa tiba wanavitoa kila wakati vinapohitajika ili kuondokana na vikwazo ambavyo vilivyopo. 

“Kwanza nashukuru uongozi wote kuanzia DC pasipo yeye tusingeweza kujua mahitaji yenu DC aliweza kushughulikia mara moja ili kuweza kupatikana vifaa hivyo na Mbunge wa Jimbo la Muheza Balozi Adadi Rajabu..kwani tunaleta vifaa hivyo kwa sasabu vinahitaji sana kwa ajili kuwahudumia wananchi”Alisema. 

Aidha alisema wataendelea kuipa misaada ya namna hiyo wilaya hiyo ili kuhakikisha vikwazo vya vifaa tiba wanavyokumbana navyo wanashirikiana kuweza kuvitatua ili kuwawezesha wananchi kupata huduma bora za afya. 

Hata hivyo aliwataka kuhakikisha wanavitunza vifaa hivyo kwa ajili ya kuwasaidia kwani wao wanafanya kazi na serikali wataendelea kuisapoti serikali kwa vyotote itakavyokuwa ili kuhakikisha mafanikio yanapatikana. 

VIJANA WATAKIWA KUWA NA UTAMADUNI WA KUCHANGIA DAMU.

$
0
0
Vijana wa Kanisa la Living Water Center Kawe chini ya Apostle Onesmo Ndegi na Apostle Lilian Ndegi lililopo katika Manispaa ya Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam wameshiriki katika zoezi la kuchangia damu katika kilele cha wiki ya vijana kanisani hapo.    
                               
Vijana hao waliamua kushiriki katika zoezi hilo mapema leo siku ya Jumapili ikiwa ni katika kuunga mkono juhudi mpango wa Taifa wa Damu Salama chini ya Wizara ya Afya wa kutoa damu ili kuokoa uhai wa wahitaji wa damu katika hospitali nchini.    
   
Akiongoza zoezi la uchangiaji damu Mchungaji wa Vijana Kanisani hapo Albert Monyo aliwataka vijana katika jamii kuwa na moyo wa kutoa damu ili kuwasaidia wenye uhitaji maana kwa kufanya hivyo kunasaidia kupunguza uhitaji mkubwa wa damu uliopo kwenye hospitali nyingi hapa nchini.

Naye Afisa muhamasishaji Damu Salama kanda ya Mashariki Mariam Juma alitoa rai kwa waamini wa madhehebu mbalimbali na wanajamii kwa ujumla kujenga tabia ya kuwa wanachangia damu mara kwa mara bila kusubiri dharula.        

Alisema uhitaji wa damu bado ni mkubwa na Ofisi ya Damu Salama bado hijawahi kuziba pengo la upatikanaji wa damu ya kutosha kwa asilimia mia moja.
Vijana wakitolewa damu



  Baadhi ya Vijana wachangiaji damu wakimsikiliza Afisa Mshauri kutoka Damu Salama katika majadiliano kabla ya kutoa damu.

Albert Monyo Mchungaji wa Vijana kanisani hapo akimsikiliza Afisa Mshauri kutoka Damu Salama katika majadiliano kabla ya kutoa damu.

Albert Monyo Mchungaji wa Vijana Kanisani hapo alipowaongoza vijana katika zoezi la uchangiaji damu





Afisa mshauri kutoka damu salama akimshauri mmoja wa wachangiaji damu katika zoezi hilo
Mmoja wa wachangiaji wa damu akioesha kadi yake ya wachangiaji mara kwa mara
Mmoja wa wachangiaji wa damu akioesha kadi yake ya wachangiaji mara kwa mara
Maafisa kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama walioendesha zoezi hilo.

Maafisa kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama walioendesha zoezi hilo

CAMARADA BRIGEDIER GENERAL HASHIM MBITA: A DISTINGUISHED TANZANIAN AND AN ILLUSTRIOUS SON OF THE AFRICAN SOIL.

$
0
0

"I hope a free Africa will remember the little I did for this continent. I am a satisfied man because I played my part".
HASHIM MBITA, 24.8.2014.


1. Introduction:

CAMARADA, Rt. Brig. Gen. HASHIM IDD MBITA, chose to sleep forever on 26.4.2015 at the Lugalo Millitary hospital, Dsm after a long illness. Brig. Gen. MBITA did not die, to borrow an English catchphrase, "Soldiers never die, they simply fade away". Brig. Gen. MBITA simply faded away. He chose to fade away on the date that Tanganyika and Zanzibar were united to create the United Republic of Tanzania. Thus, in my humble view, UNITY is the message he left behind.

President JAKAYA MRISHO KIKWETE stated:

"There are very few people that have served the country the way Mzee MBITA has served this nation. He also led the liberation efforts of our brethren in the Southern African countries for 20 years until they all achieved their independence. There is not a freedom fighter in Mozambique, Angola, Zimbabwe, Namibia and South Africa who did not know the contribution made by Mzee MBITA. His death has robbed us of a true son of the African soil. He was a man of his own kind"

There are certain individuals life and fate make us stumble upon not to learn from them as they breath, but rather that we may marvel at their collossal nature when they are no longer with us. Such is the case with Brig. Gen. MBITA.

The Dot.com generation knows very little or nothing about this Big man. Currently, one can hear a story here and there of what this fallen hero did. With the passing of time and if no effort is made towards writing his Big Story, then Brig. Gen. MBITA could be just a smoke that just passed over the sky!.

The Billion-dollar question is who was this Unique Tanzanian who served his country with honour and distinction?

2. Birth of a Jewel:

HASHIM IDD MBITA was born on 2.11.1933 at Songoro, Gongoni, Tabora.

3. Primary Education:

MBITA studied at Town primary school and passed his exams with flying colours.

4. Secondary Education:

MBITA joined Tabora boyz secondary school, known for nurturing luminaries for post-independence government, in 1950 and he completed his A Leve studies in 1957.

5. MBITA Joins the Cooperatives Department:

MBITA joined the Cooperatives Department in Mwanza in 1957.

6. MBITA Joins TANU:

MBITA joined the Tanganyika African National Union (TANU) in 1958 and was always a humble party cadre before moving to public relations as a journalist.

7. MBITA Joins the Ministry of Information:

MBITA, a journalist by profession, worked with the Department of Information, Ministry of Information as the Director of Information.

8. MBITA Attends Millitary Training in the UK:

Given Mwalimu NYERERE's overhaul and re-branding of the army after the 1964 mutiny, MBITA was sent to UK for millitary training and then was appointed political commissar in the army.

9. MBITA Becomes Press Secretary to Mwalimu NYERERE:

MBITA, thereafter, moved to the State House to become Press Secretary to Mwalimu NYERERE and was later TANU's Secretary General.

10. MBITA Becomes TANU's Secretary General:

In 1970, MBITA was appointed TANU Secretary General.

11. MBITA Appointed Executive Secretary of OAU in 1972:

In 1972, MBITA was appointed Executive Secretary of the the OAU Coordinating Committee for the liberation of Africa.

MBITA's work was guarded by the 9-nation Committee with a Non-Executive Chairman. He had to link up and work with the OAU Secretary General and occassionally with the rotating chairmen.

Nurturing these relationships and balancing between the demands from Addis and from the Committee of Nine was not easy.

MBITA mobilized materials and training for the liberation forces of the remaining countries still under colonial rule, all of whom gained independence during his tenure including Guinea-Bissau 1974, Cape Verde 1975, Angola 1975, Zimbabwe 1980, Namibia 1990 and South Africa 1994.

As Committee Administrative Chief, Brig. Gen. MBITA was singulary the person most hated by the likes of Ian Smith in Rhodesia and F.W De Clerk of South Africa. As such, the regimes considered Brig. Gen. MBITA the Trouble-maker Numero Uno! His life was thus in great danger and in fact several schemes hatched to illiminate him unsuccesfully.

12. MBITA: Mission Accomplished, 1994!

The Liberation Committee closed down in August 1994 with MBITA submitting a Final Report under the title: "MISSION ACCOMPLISHED"

At the final meeting of the OAU Liberation Committee in Arusha, Mwalimu NYERERE heaped praises on Brig. Gen. MBITA for his outstsnding contribution for liberation of the continent.

A 9-Volume history of Southern Africa Liberation struggles known as the HASHIM MBITA PROJECT was published in his honour in Dsm in 2014 as Southern African Liberation Struggles: Contemporaneous documents(1960-1964).

13. MBITA Appointed TZ Ambassador to Zimbabwe:

Once Brig. Gen. MBITA was done with the libetation mission, he was assigned to several other tasks including being a diplomat.

Thus, when relations between TZ and Zimbabwe deteriorated over a Tanzanian envoy's stance over the seizure of white farms, Brig. Gen. MBITA was dispatched by president BEN MKAPA as High Commissioner to smoothen relations. He served as Ambassador from 2003 to 2006 and did a commendable job.

14. Brig. Gen. MBITA Fades Away, 2015:

That Brig. Gen. MBITA faded away on 26.4.2015, a day of significant proportions to TZ is an unblemished indicator of the impact this Great man had on African politics and its quest for freedom from colonial rule. He was one of the last remaining African heroes.

15. MBITA: Showered with Praise & Awards

The late Brig. Gen. MBITA was one of the heroes of African Liberation. His heart belonged not only to TZ but also to Africa, his motherland:

15.1 Zimbabwe:

Zimbabwe awarded Brig. Gen. MBITA the highest national honour that could be given to a foreigner- "THE ROYAL ORDER OF MUNHUMUTAPA", in recognition of his outstanding role, during the SADC summit at Victoria Falls.

Brig. Gen. MBITA was represented by his beautiful daughter, Ms SHEILLA MBITA, a BOT employee. It read:

"We in Zimbabwe are glad that Hon. MBITA was able to appreciate this honour although he was not feeling well. His daughter came to receive the honour".
SIMBARASHE MUMBENGWEGI, Foreign Minister.

15.2 South Africa:

President JACOB ZUMA, on 8.12.2015, bestowed MBITA with the Order of the Companions of Oliver Tambo in Gold, during the 2018 National Orders Awards ceremony:

"For his exceptional and gallant support of African liberation movements and his tireless efforts in ensuring that the struggle for freedom throughout the African continent bore fruit".


15. 3 Joachim Chissano:

Former president JOACHIM CHISSANO who was MBITA's close friend and who had once visited and stayed with MBITA in his house in Tabora for a couple of days, said:

"During his prime, Camarada MBITA was outwardly a good natured man, but in the job, he was tough, no-nonsense, results demanding, high discipline-enforcement army officer. He was a Millitary per excellence".

15.4 Keneth Kaunda:

"Brig. Gen. HASHIM MBITA was the Headmaster of the Africa Liberation movement's Highest school".

15.5 Sam Nujoma

SAM NUJOMA, Namibian founding President, described Brig. Gen. MBITA as "courageous" and "symbol of freedom from colonialism and occupation".

15.6 Joseph Kabila:

"The late HASHIM MBITA was not only a national of his mother country, Tanzania, but also a denizen of the African continent".

15.7 AU:

On 30.1.2016, President ROBERT GABRIEL MUGABE of Zimbabwe, the then outgoing chairperson of SADC and AU, presented "THE HASHIM MBITA PROJECT" to the African Union.

The Publication is composed of 10 Volumes which document the history of the Liberation struggles in Southern Africa to be accessible to all citizens of the continent.

15.8 SADC

"This Award is for the important role Brigedier General MBITA played in regional liberation during his 20 year tenure as the Executive Secretary of the Liberation Committee of the OAU".

16. Journeying with MBITA:

As a Milambo High School Form 5 student, back in the day, I once had the privilege of travelling with Hon. MBITA in the Central Line train First Class Compartment from Dsm to Tabora. Though it was a 24 hour journey but it felt like a two hour journey as the Big man told me a lot of stories such as how he was executing his duties, criss-crossing the continent to foresee liberation struggles and various challenges he was facing. It was simply, the best journey of my life!.

17. Conclusion:

Very unfortunately, Tanzania has been drowsed with that heavy blanket of sleepness as despite having several universities, none has awarded Brig. Gen. MBITA with an honourary doctorate for his invaluable contribution to Africa.

Brig. Gen. MBITA's story has to be written. We should not allow this unique history slip through our fingers!
 





 

UNESCO yawakutanisha wadau kujadili mpango mkakati wa mradi wa BEAR ll

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo(katikati) akifungua kikao cha kujadili pamoja na kupitisha mpango mkakati wa mradi wa BEAR ll wenye lengo la kuleta elimu bora kwa mataifa ya Afrika kwenye mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos
 Mkuu wa Kitengo cha Elimu katika Shirika la UNESCO nchini, Faith Shayo akiwasilisha mpango mkakati wa mradi wa BEAR ll kwa wadau kutoka MoEST, Wizara wa Kilimo, UNESCO, NACTE, TCCA, ATE, VETA pamoja wadau wa maendeleo  wenye lengo la kuleta elimu bora kwa mataifa ya Afrika kwenye mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam 
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos(kushoto) akitolea ufafanuzi baadi ya vipengele vya mpango mkakati wa mradi wa BEAR ll wenye lengo la kuleta elimu bora kwa mataifa ya Afrika kwenye mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo.
Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Dk. Noel Mbonde(kulia) akichangia mada wakati wa majadiliano pamoja na kupitisha mpango mkakati wa mradi wa BEAR ll wenye lengo la kuleta elimu bora kwa mataifa ya Afrika kwenye mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam.
Ofisa mipango ya Elimu wa Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Jennifer Kotta  akichangia mada wakati wa majadiliano pamoja na kupitisha mpango mkakati wa mradi wa BEAR ll wenye lengo la kuleta elimu bora kwa mataifa ya Afrika kwenye mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau kutoka MoEST, Wizara wa Kilimo, UNESCO, NACTE, TCCA, ATE, VETA pamoja wadau wa maendeleo wakichangia mada wakati wa kujadili mpango mkakati wa mradi wa BEAR ll wenye lengo la kuleta elimu bora kwa mataifa ya Afrika kwenye mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Elimu katika Shirika la UNESCO nchini, Faith Shayo akijibu maswali ya  wadau wakati wa kujadili mpango mkakati wa mradi wa BEAR ll wenye lengo la kuleta elimu bora kwa mataifa ya Afrika kwenye mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam.
Majadiliano yakiendelea
Mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo  akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki kutoka MoEST, Wizara wa Kilimo, UNESCO, NACTE, TCCA, ATE, VETA pamoja wadau wa maendeleo wakati wa kikao cha kujadili pamoja na kupitisha mpango mkakati wa mradi wa BEAR ll wenye lengo la kuleta elimu bora kwa mataifa ya Afrika kwenye mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam.

INTRODUCING:MTAALAM WA DAR BY MH.TEMBA FT.KISAMAKI


SERIKALI KUPELEKA MAJI SAFI NA SALAMA VIJIJI VILIVYOPO KARIBU NA VYANZO VYA MAJI

$
0
0
WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa akizungumza mara baada ya kutembelea chanzo cha Maji cha Amani wilayani Muheza wakati wa ziara yake mkoani Tanga
 WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa kushoto akimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu
MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa ziara hiyo


 WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa akishuka kwenye tanki kubwa la kuhifadhia maji eneo la Kilapula Jijini Tanga ambayo yatatoka eneo la Pongwe kuelekea wilayani Muheza kupunguza changamoto ya uhaba wa maji kwenye wilaya hiyo
 Mabomba yakiwa yameweka eneo hilo mradi huo mkubwa ukiendelea kutekelezwa
 Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly kushoto akiwa na katibu wa Mbunge wa Jimbo la Muheza kulia kushoto ni PRO wa Mamlaka hiyo Dorrah Killoh
 WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa kulia akionyeshwa kitu kwenye ramani na Mhifadhi wa Misitu ya Amani wilayani Muheza Mwanaidi Kijazi katika wakati alipotembelea chanzo kikubwa cha Maji wilayani Muheza cha Amani kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo  kulia ni Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly
WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa katikati akisisitiza jambo kwa viongozi wa wilaya ya Muheza mara baada ya kutembelea chanzo hicho

WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa amesema serikali kupitia mamlaka za maji watahakikisha wanapeleka huduma ya maji safi na salama kwenye vijiji vilivyopo karibu na vyanzo vya maji ili waendelee kuvitunza viweze kusaidia vizazi vya sasa na vijavyo.

Mbarawa aliyasema hayo wakati alipotembelea chanzo cha Maji cha Amani wilayani Muheza mkoani Tanga ikiwa ni ziara yake ya siku ya pili mkoani hapa ambapo aliwataka wananchi kulinda vyanzo

Alisema haitakuwa na maana iwapo wananchi hao wanaendelea kuvitunza vyanzo vya maji lakini hawana maji safi na salama hivyo watahakikisha nao wanapata huduma hiyo muhimu kwa ustawi wa maisha yao na jamii zao.

Alieleza kwa sababu mwaka 1962 maji yaliyo yakipatikana kwa mtu mmoja yalikuwa mita za ujazo 7862 hivi sasa mtu mmoja kwa mwaka anaweza kutumia maji yaliyopo mita za ujazo 1800 lakini siku hizo kulikuwa na watu milioni 10.6 lakini leo hii watu zaidi ya milioni 50 na watu wanazidi kuongezeka.

“Ndugu zangu Serikali kupitia mamlaka za Maji tutahakikisha wananchi wanaoishi karibu na vyanzo vya maji wanapata huduma ya maji safi kwa maana haitakuwa na maana kama wataendelea kuvitunza vyanzo hivyo wakati wao hawapati maji safi na salama “

“Lakini pia nisisitize kwamba tuhakikishe vyanzo vya maji vilivyopo tunavilinda kwa nguvu zote kwani vinazidi kupungua kutokana na uharibifu wa mazingira pia wananchi wakielimishwa wanaweza kuvitunza, “Alisema.

Aidha aliwataka wananchi hao kuhakikisha wanaendelea kuvitunza vyanzo vya maji ili viweze kusaidia vizazi vya sasa na baadae kwani bila kufanya hivyo chanzo hicho kinaweza kukauka.

“Lakini kitakapokauka watu watafikiria kwenda mto Pangani na huko kunaweza pia kukauka hivyo kuna umuhimu wa kuhakikisha vyanzo hivyo vinatunzwa kwa lengo la kuendelea kuwepo “Alisema.

Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo katika taarifa yake alimueleza Waziri Mbarawa kwamba hali ya upatikani maji wilayani humo eneo la mjini ni asilimia 35 kwa mjini na kipindi cha kiangazi asilimia 18.

Alisema kwa upande wa vijiji upatikanaji wa maji ni asilimia 65 inakuwa ni nafuu kwa sababu baadhi ya maeneo kuna maji yanatiririka sehemu ambazo kumejengwa vyanzo vya maji na hivyo kuyapata kirahisi.

“Mradi wa maji eneo la Muheza mjini ulijengwa mwaka 1977 ukitumia chanzo cha Mkurumuzi kilichopo Magoroto huku kililenga kuwapata huduma hiyo wakazi 8000 lakini kwa sasa sasa wapo wakazi 32000.

Mkuu huyo wa wilaya alimueleza waziri huyo kwamba mpango wao kwa sasa ni kuhakikisha wanapata chanzo cha uhakika ili kupata maji ili kuondosha changamoto kubwa ya wilaya hiyo.

“Kwani mh Waziri wakati wa kiangazi wananchi wananua ndoo moja ya maji kwa sh.1000 jambo ambalo ni changamoto kubwa na hilo linaweza kupatiwa ufumbuzi kwa miradi mikubwa “Alisema

Naye kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu alisema eneo hilo la chanzo lilikuwa kwenye hali mbaya baada ya kuvamiwa na watu waliokuwa wakitafuta madini kabla ya kushirikiana na watu wa maliasili na serikali ya wilaya kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na kulirudisha kwenye hadhi yake.

Alisema pia waliwapeleka wataalamu ili kuangalia kama kweli kuna mamdini kwenye eno hilo ili kama wanaweza kuruhusu uchumbaji wa madini ufanyike bila kuathiri chanzo cha maji hivho hivyo taarifa yao bado tunaisubiri.

“Lakini pia niwashukuru Tanga Uwasa wameanza mikakati ya kuwapa maji vijiji vyote vinavyozunguka chanzo hicho kuhakikisha nao wananufaika na hduuma hiyo muhimu badala ya kutumia maji yanayo tiririka “Alisema.



REPSSI YAENDELEA NA KAMPENI KUTOKOMEZA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI

$
0
0
Mkurugenzi Mkazi wa Repssi Tanzania, Edwick Mapalala akiongea na vijana kijiweni kuhusu athali za mimbaMkurugenzi Mkazi wa Repssi Tanzania, Edwick Mapalala akiongea na vijana kijiweni kuhusu athali za mimba

Baadhi ya wanafunzi wakimsikiliza Mkurugenzi Mkazi wa Repssi Tanzania, Edwick Mapalala 

Mwandishi wetu, Pwani.

Shirika linalojihusisha na masuala ya kijamii na kisaikolojia kwa watoto (REPPSI) limeendelea kufanya kampeni ya kutokomeza tatizo la ndoa na mimba za utotoni mkoani Pwani.

Kampeni hiyo inafanyika ili kuhakikisha watoto wa kike wanatimiza ndoto zao za kielimu ili kushiriki katika mkakati wa Serikali wa Tanzania ya viwanda.

Akizungumza na wakazi wa Kibiti Mkoani Pwani, Mkurugenzi Mkazi wa REPSI Tanzania, Edwick Mapalala alisema tatizo la mimba na ndoa za utotoni bado kubwa na kwamba linahitaji jitihada za pamoja kupambana nalo.

“Mfano ni hizi kampeni za kutoa elimu na kuihamasisha jamii kumthamini mtoto wa kike zinasaidia kwa hiyo kama tutaendelea nazo jamii itaelewa, watoto watatimiza ndoto zao,” alisema.

Mapalala alisema katika kampeni hizo wanazoshirikiana na Shirika la Pasada linalojihusisha na masuala ya Ukimwi chini ya Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam na Pwani, vijana hasa madereva bodaboda wamefikishiwa elimu kuhusu thamani ya mtoto wa kike.

Baadhi ya viongozi wa vijiji na kata walikiri kuwa ndoa za utotoni ni changamoto kubwa lakini wanaendelea kupambana nayo.

Mratibu wa Elimu Kata ya Salala, Wilayani Kibiti Erasmus Assenga alisema kwa mwaka huu tu wanafunzi wawili wa Sekondari katika kata hiyo wameacha masomo kwa mimba.

“Kwa hiyo kampeni hii ni muhimu kwa sababu watoto wa kike wenyewe wanafikishiwa elimu, jamii hasa wanaume wanaelezwa na wanajua umuhimu wa kuwathamini,” alisisitiza.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii wa Pasada Ester Mbwana alisema anaamini kuwa baada ya kampeni hizo kutakuwa na mafanikio makubwa kwa sababu, jamii inaelewa na imekubali kusaidia katika ulinzi wa mtoto.

MTENDAJI MKUU TEMESA ZIARANI MIKOA YA IRINGA, NJOMBE, MBEYA, RUKWA NA KATAVI

$
0
0

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akikagua mojawapo ya mashine iliyopo katika karakana ya wakala huo mkoa wa Njombe wakati wa ziara yake ya kukagua utendaji kazi, kushoto ni Kaimu Meneja wa Temesa Mkoa wa Njombe Mhandisi Saidi Mawazo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akiichunguza mashine ya kuchongea vipuri vya mitambo mbalimbali wakati akikagua chumba cha kuhifadhia mashine hizo katika karakana ya mkoa wa Mbeya. Kulia ni Meneja wa TEMESA mkoani humo Mhandisi Sunday Kyungai.
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mkoa wa Katavi Mhandisi Stembrige Rushatila katikati akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Mhandisi Japhet Y. Maselle kushoto eneo la karakana wanapotegemea kupaboresha ili kuongeza uzalishaji wakati wa ziara ya mtendaji mkuu kukagua miundombinu ya karakana za wakala.  
Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mkoa wa Iringa Mhandisi Ian Makule kulia akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala huo Mhandisi Japhet Y. Maselle mashine ya kisasa ya kutoa na kubadilishia matairi ya magari iliyopo katika karakana ya mkoa huo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa TEMESA mkoa wa Iringa mara baada kuzungumza nao na kusikiliza changamoto wanazokutana nazo katika utendaji kazi. Kulia kwake ni Meneja wa TEMESA Mkoani humo Mhandisi Ian Makule.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akitoa msisitizo wakati akizungumza na wafanyakazi wa wakala huo mkoani Rukwa alipokua ziarani kukagua utendaji kazi. Pembeni yake ni Meneja wa Mkoa huo Mhandisi Fidol Tumbi.PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO - (TEMESA)

Posted: 24 Feb 2019 11:30 AM PST
  Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akionesha hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa tenki la maji ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali.
 Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akionesha hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa jengo la Wizara ya Nishati linalojengwa ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma wakati wa ziara yakukagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali.
 Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akionesha hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa jengo la Wizara ya Fedha na Mipango linalojengwa ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma wakati wa ziara yakukagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali.
 Muonekano wa hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa jengo la Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora katika mji wa Serikali Ihumwa jijini Dodoma. 
  Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akiongea na mafundi katika jengo la Ofisi ya Makamu wa Rais linalojengwa ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma wakati wa ziara yakukagua maendeleo ya ujenzi wa mji wa Serikali.


 Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuratibu Zoezi la Serikali Kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akiongea na Mkandarasi na Mshitiri katika jengo la Wizara ya Kilimo linalojengwa ndani ya mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma 

UTOAJI ELIMU JUU YA SHERIA MPYA YA UDHIBITI WA UZITO WA MAGARI KWA WASAFIRISHAJI WAENDELEA KILA KONA

$
0
0
 Afisa kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Omary Kinyange, akitoa elimu kwa madereva wa malori kuhusu utumikaji wa sheria mpya ya Afrika Mashariki ya Udhibiti wa Uzito wa magari katika mzani wa Makambako uliopo mkoani Njombe. Sheria hiyo inatarajiwa kuanza kutumika tarehe 1 Machi, 2019

 Afisa kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Omary Kinyange, akitoa elimu kwa madereva wa malori kuhusu utumikaji wa sheria mpya ya Afrika Mashariki ya Udhibiti wa Uzito wa magari katika mzani wa Makambako uliopo mkoani Njombe. Sheria hiyo inatarajiwa kuanza kutumika tarehe 1 Machi, 2019

 Afisa kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Omary Kinyange, akitoa elimu kwa madereva wa malori kuhusu utumikaji wa sheria mpya ya Afrika Mashariki ya Udhibiti wa Uzito wa magari katika mzani wa Makambako uliopo mkoani Njombe. Sheria hiyo inatarajiwa kuanza kutumika tarehe 1 Machi, 2019


Muonekano wa lori likipima uzito katika mzani wa Makambako, mkoani Njombe. Wasafirishaji wanaendelea kupewa elimu ya Sheria mpya ya Udhibiti wa Uzito wa magari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki itakayoanza kutumika tarehe 1 Machi, 2019


Bridging the gap of Soft Skills; Have we thought of Extra Curriculum Skills? UWEZO AWARD project Case.

$
0
0

By Noelle Mahuvi, 
Country Director at Great Hope Foundation.

It is estimated that by 2020, African Population shall be 1.3bln and 47% of this are the young people 24 of years age and below. This has made African continent to be defined as a continent of young people. This vibrant young group seems to be a great human resource for the social-economical development of the continent, however when unemployment is their biggest hurdle, their future seems to be filled with uncertainties and vulnerabilities. I will take a case of my home, Tanzania where as 64% of the population in 2020 is expected to be below 24 years, and like many other African states, unemployment of this group comes up on everyday discussions and debates. It has been observed that out of 800,000–1,000,000 people getting to the labor market yearly from learning institutions, only 50,000 has an assurance of being absorbed in the formal sector. The rest just work to find their place in the labor market.
A close observation on youth unemployment has seen that, the harshness of the situation is not very much on the less educated ( the Primary School graduates and dropouts). These people seem to find ways to adjust themselves in the market. They easily get absorbed with anything that the market is providing as a source of income. It falls on secondary schools and the University graduates. They seem to have a bigger challenge, meeting the expectations of the market despite of spending some 13–17 years at school. It is even worse for them to employ themselves because, they seem handicapped in visualizing opportunities and turning them into source of employment. The few who cross the bridge, they get badly knocked down, because of poor set/package of Soft Skills, that they never had a chance to learn at school. Things like team work, self-identity understanding, leadership skills, perseverance, goal setting, spotting opportunities on the labor market, problem solving, creativity and innovation are scarcely found on these graduates. Generally, the skills mismatch between the graduates and the expectations of the market seems to be quite high.
The underlying question has always been, how one could have mastered the hard skills, that needed much time and effort and fail to have a package of these soft skills?
What has gone wrong?
How could this be possible?
On this article I would like to share my experience of working with students, helping them to develop skills through extra curriculum activities.
I have had a privilege of working with Secondary Schools through Great Hope Foundation ( GHF) an NGO working on the area of youth development and empowerment in Tanzania. I have been coordinating UWEZO AWARD PROJECT, for the past three years. The project is a competition for Secondary School Students, to do Community Change Projects. A single Community Change Project was fully chosen by students and they were supposed to do activities that give them a chance to explore their talents, build skills and bring positive impact to the community. GHF aimed at motivating students to do Community Service as a methodology for them to learn the benefit of volunteering. “UWEZO” is a Swahili word, meaning capacity/potential/ability, and the project was named UWEZO AWARD because it gave student a chance to bring out their potential, specifically those ability that you hardly see them through books and classroom tasks. Outstanding Community Change Projects are awarded every year, to motivate students to keep the spirit up.
In 2016, GHF involved 20 Secondary Schools in the project. Students were given three months to do the project. Out of 20 Secondary Schools that participated, Zanaki Secondary School was the overall winner, and received an outstanding recognition. Students developed a talent show Bonanza asking all their fellow to participate at a fee of 200 TZS, and the fund collected was used to renovate their school dispensary by painting and they bought bedsheets, mattresses, and tablemats. All of them were ladies, and were in form six at that time, when they had graduated from high school, a lady known as Diana went on to open a fashion designing label and Theckla who was leading the team, was motivated to start a non profit known as Tanzania Eagles as she was going to Mzumbe University. I had some moments with Thekla asking her what was her biggest lesson she picked from their Community Change Project and she said
“ the whole process of our project made me understand that, we the young generation ( students) can have a remarkable contribution to our society through our talents. We just organized a project in a month and we were able to paint our school dispensary that has never been renovated for quite sometime. I have learnt on how to work as a team to reach our agreed common goal. I think we need to have this competition at a national level”
GHF had an amazing case in 2017 when the project was expanded to reach 50 Secondary Schools in Dar es Salaam. Wailes Secondary School from Temeke was among the schools that received outstanding Recognition, as their Community Change Project had a remarkable impact. They grew vegetables and sold, and the fund collected was used to partly contribute in building the school wall. The excitement of accomplishing such their project, charged their spirit and started their own business of soap making and selling the soap to the school Community, specifically teachers. When I spoke to Charles Michael, who was the leader of the project, he said,
“ I knew that I can accomplish much in my life, I had so many ideas and had a lot of energy. But my participation in Uwezo Award, ignited my potential in a way that, I couldn’t wait for me to finish school to start a business. I organized my fellow students we started our soap making business. This has been a great opportunity for me. I shall keep this business after school. Our Community Change Project won in UWEZO AWARD 2017 because we wanted to win in the very first place. For sure now I know I can do entrepreneurship.”
GHF expanded the scope of the project to reach 100 Secondary Schools in 2018 and students kept on doing better Community Change Projects. Kibasila Secondary School Community Change Project was among the project that was recognized with Outstanding Recognition, taking second position out off 100 Secondary Schools . Students went all the way doing five different activities to make a single Community Change Project. They organized themselves to design small wallets out of Kitenge ( African Print) and sold them. The fund was used to paint their school gate. They organized a fashion show to showcase their designs. They bought new Vitenge ( African Print) and made clothes for Children at the Orphanage Centre and they made dust-masks and distribute them for free to women who were cleaning the road at Temeke. Students gave the following feedback on the reports. When GHF interviewed Primus who was the head of the project from the school he said
“ We didn’t know that our participation in the project will give us a chance to learn so much about ourselves. It is amazing how we have been able to come together as a team. I have learnt about team work. I have known how to use my talents for the benefit of my community. I have learnt how to lead others, and achieve our set goal regardless of the challenges I face. As a leader I have learnt to respect each and every idea of the team members and use them for the benefit of the team. I am now bold and more daring. The list is endless. I am so proud of my participation in UWEZO AWARD 2018. It has been a life changing experience for me.”
Up to 2018 GHF had managed to reach 170 Secondary Schools in Dar es Salaam and Coastal Region. Students went quite some miles to do Community Change Projects that had a remarkable impact to their school. To name a few Kibada Secondary School from Kigamboni created and furnished a resting room for students who fall sick at school, because before that, they used to sleep under the tree. Kibamba Secondary School made a door for their class to stop people from stealing their chairs. The list could go on and on. The top skills that students confessed to attain by participating in UWEZO AWARD project was working in a team, leadership, goal setting, hardworking, creativity, time management, selling and self identity discovery. This observation has been the most interesting to GHF as little did the team knew that the Community Change Projects will equip young generation with such a set of soft skills.
This is the reality you understand better, by being on the field, as they say experience is always a better teacher. We learnt the benefits of extra Curriculum activities, beyond our usual or normal expectations. The passion and commitment we saw within students was amazing. They requested more and more of these activities for them. Unfortunately Extra Curriculum activities benefits are not clearly understood by parents and even school administrators. There is a lot of resistances towards allowing students do these extra curriculum activities. Majority of Parents feel, it is a wastage of time, if they are paying fees for their child, all they want to hear is an A or B on their achievement, anything out of that is irrelevant and unwanted. Teachers are also under the pressure of delivering, when a school has underperformed, the first activity is normally to burn all social clubs at their schools. “students waste time on these”. Majority of Private schools, seem less interested because, for them education is business. No single parent picks a school because of the great extra curriculum activities the school is offering. No way, they pick and pay the fees because they just want an assurance that, their child will pass with some reasonable grades. Hence extra Curriculum activities is something they may choose not to pay much attention ( if at all they will give it attention). 95% of schools participating in UWEZO AWARD are Government Schools. The permission we got from the government for working with Secondary Schools was clearly written that, none of the activities should be allowed to interfere with schools schedules and timetable because Extra Curriculum activities have not been integrated in the daily school calendars.
Soft skills development to students needs a transformation of the key elements of how we measure the KPI when it comes to education. Recently I have seen the Government, bringing some added programs to reduce the problem. The efforts being added are add-on to the normal curriculum. But most of them are under the same traditional way of learning; trainings and workshops. Having this as a starting point is fine, but I believe we need to go beyond that. Education should be organized to bring a graduate with a package of both soft + hard skills. Am saying this with due respect, getting a GPA of 4.5 tells us that you are extremely brilliant and we should rely on you probably on a number of things. But if with that level of intelligence you can’t work in a team, you can’t set goals and achieve them, poor communication skills, then the impact of your intelligence will be demeaned by the lack of these set of soft skills. Imagine how much you could have accomplished if you had both, soft & hard skills?
May be we can start with Extra Curriculum activities to bridge the gap. Repackaging them in a way they shall sound attractive to the young generation. UWEZO AWARD could be that small light at the end of the tunnel but I believe there are so many ways of organizing extra curriculum activities at Schools, from Primary to Universities and Colleges in a way that, they can bridge the missing gap. Mwl Nyerere started “Elimu ya Kujitegemea” and we lost it down the Road. This is what he said,
“ to transmit from one generation to the next the accumulated wisdom and knowledge of the society, and to prepare the young people for their future membership of the society and their active participation in its maintenance or development is what Education for Self-Reliance meant. “
As old as it is, it still one of the best perspective to benchmark our education with this quote. In the face of a heavy debate of what to do with the skills mismatch between our youth and the labor market, Extra Curriculum activities could be a great starting point if it is re-packaged innovatively.

KOROSHO ZA SERIKALI ZAANZA KUBANGULIWA WILAYANI TUNDURU

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera akimsikiliza Mfanyakazi wa kiwanda cha kubangua Korosho cha Korosho Africa Ltd Tunduru Mkoani Ruvuma Issa Kahesa kulia alipokuwa akimueleza kazi ya ubanguaji wa korosho za Serikali inavyoendelea katika kiwanda hicho.
Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha kubangua korosho cha Korosho Africa Ltd wakiendelea na kazi kiwandani hapo ambapo hadi kufikia jana zaidi ya wananchi 200 wamepata ajira.
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera aliyeinama akiangalia ubora wa korosho za Serikali zinazobanguliwa katika kiwanda cha kubangua korosho cha Korosho Africa Ltd kilichopo Tunduru Mkoani Ruvuma.
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera akiangalia korosho zilizobanguliwa katika kiwanda cha Korosho Africa Ltd ambacho kimeingia mkataba na Serikali kwa ajili ya kubangua korosho za Serikali zilizonunuliwa katika msimu wa 2018/2019 kutoka kwa wakulima wa wilaya ya Tunduru,kulia ni mfanyakazi wa kiwanda hicho Issa Kahesa

REPSSI YAENDELEA NA KAMPENI KUTOKOMEZA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI

$
0
0
Mkurugenzi Mkazi wa Repssi Tanzania, Edwick Mapalala akiongea na vijana kijiweni kuhusu athali za mimbaMkurugenzi Mkazi wa Repssi Tanzania, Edwick Mapalala akiongea na vijana kijiweni kuhusu athali za mimba
Baadhi ya wanafunzi wakimsikiliza Mkurugenzi Mkazi wa Repssi Tanzania, Edwick Mapalala


Mwandishi wetu, Pwani.

Shirika linalojihusisha na masuala ya kijamii na kisaikolojia kwa watoto (REPPSI) limeendelea kufanya kampeni ya kutokomeza tatizo la ndoa na mimba za utotoni mkoani Pwani.

Kampeni hiyo inafanyika ili kuhakikisha watoto wa kike wanatimiza ndoto zao za kielimu ili kushiriki katika mkakati wa Serikali wa Tanzania ya viwanda.

Akizungumza na wakazi wa Kibiti Mkoani Pwani, Mkurugenzi Mkazi wa REPSI Tanzania, Edwick Mapalala alisema tatizo la mimba na ndoa za utotoni bado kubwa na kwamba linahitaji jitihada za pamoja kupambana nalo.

“Mfano ni hizi kampeni za kutoa elimu na kuihamasisha jamii kumthamini mtoto wa kike zinasaidia kwa hiyo kama tutaendelea nazo jamii itaelewa, watoto watatimiza ndoto zao,” alisema.

Mapalala alisema katika kampeni hizo wanazoshirikiana na Shirika la Pasada linalojihusisha na masuala ya Ukimwi chini ya Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam na Pwani, vijana hasa madereva bodaboda wamefikishiwa elimu kuhusu thamani ya mtoto wa kike.

Baadhi ya viongozi wa vijiji na kata walikiri kuwa ndoa za utotoni ni changamoto kubwa lakini wanaendelea kupambana nayo.Mratibu wa Elimu Kata ya Salala, Wilayani Kibiti Erasmus Assenga alisema kwa mwaka huu tu wanafunzi wawili wa Sekondari katika kata hiyo wameacha masomo kwa mimba.

“Kwa hiyo kampeni hii ni muhimu kwa sababu watoto wa kike wenyewe wanafikishiwa elimu, jamii hasa wanaume wanaelezwa na wanajua umuhimu wa kuwathamini,” alisisitiza.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii wa Pasada Ester Mbwana alisema anaamini kuwa baada ya kampeni hizo kutakuwa na mafanikio makubwa kwa sababu, jamii inaelewa na imekubali kusaidia katika ulinzi wa mtoto.

HALI YA UPATIKANAJI WA UMEME KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM

$
0
0
Februari 25, 2019

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawaomba radhi Wateja wake wa Mkoa wa Dar es salaam kwa kukosa huduma ya umeme kwa siku za hivi karibuni kutokana na maboresho makubwa yanayohusisha matengenezo kinga ya mashine 3 za Kituo cha Ubungo II, pamoja na uwekaji wa transfoma kubwa la MVA 300 kwenye Kituo cha kupoza umeme cha Ubungo ili kukiongezea uwezo na kwenda sambamba na ukuaji wa mahitaji ya jiji la Dar es Salaam.

 Kabla ya matengenezo kuanza mnamo Januari 2019 Kituo hiki cha kupoza umeme cha Ubungo kimekuwa kinapokea umeme kutoka katika vituo vya Uzalishaji umeme vilivyopo upande wa msongo wa kilovolti 220 kupitia transfoma mbili zenye uwezo wa MVA 150 kila moja, zenye kupokea umeme wa msongo wa Kilovolti  220 na kuushusha hadi kuwa msongo wa Kilovolti 132  katika transforma namba sita na namba  saba za kituo cha Ubungo na  vituo vya uzalishaji umeme vilivyoungwa kwenye msongo wa kilovolti 132 ambavyo vimeungwa moja kwa moja kwenye mfumo mkuu wa usambazaji umeme  kwa Dar es Salaam na Zanzibar.

Kutokana na matengenezo yanayoendelea vituo vya uzalishaji umeme vilivyoungwa kwenye msongo wa kilovoti 132 na 33 vimekuwa nguzo kubwa ya upatikanaji wa umeme. Vituo hivyo ni Ubungo II na Tegeta.

Shirika kupitia wataalamu wake tayari limefanya jitihada kubwa za kupunguza athari za upungufu wa upatikanaji wa umeme kwa wakaazi wa Dar es salaam na Zanzibar kwa kufanya yafuatayo: 

Mosi, Kufungua laini ya msongo wa kilovoti 132 kati ya Kilimanjaro na Hale: Hili hufanyika ili kutoruhusu umeme wa kutoka Dar es Salaam na Morogoro kwenda Kilimanjaro hivyo Mkoa huu kuchukulia kwenye upande wa msongo wa kilovolti 220 kutoka Arusha.

Pili , Kuwezesha upatikanaji wa umeme katika baadhi ya  maeneo ya Mkoa wa Dar es salaam, kwa kuunga baadhi ya njia za Usafirishaji  umeme kutoka Kituo cha Kinyerezi, Gongolamboto hadi Mbagala ili kuwezesha maeneo hayo kupata umeme bila kupitia kituo cha Ubungo  ambacho kipo katika matengenezo.

Tatu, Kufungua njia ya umeme ya kilovolti 132 itokayo Kituo cha Kunduchi   hadi Mlandizi na kuunga maeneo hayo katika njia ya umeme ya kilovolti 132 itokayo Morogoro ili kuwezesha jiji la Dar es salaam kuwa na umeme wa uhakika.

Nne, Kufungua laini ya msongo wa kilovolti 132 kati ya Ubungo na Chalinze upande wa Ubungo ili kutozihusisha transfoma za Ubungo kwenye mzigo wa mikoa mingine na hivyo kutumika kuhudumia  wateja wa  Dar es Salaam na Zanzibar pekee.

 Tunatarajia matengenezo haya yanayokwenda kwa awamu yatakamilika ifikapo mwezi Juni 2019.

TANESCO itaendelea kutoa taarifa ya Maendeleo ya kazi ya matengenezo ya kituo cha Ubungo yenye lengo la kuwezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika Dar es salaam na Zanzibar kwa siku zijazo 

Kituo cha miito ya simu 2194400 na 0768 985100

Tovuti: www.tanesco.co.tz, 

Mitandao ya kijamii

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

 Facebook https://www.facebook.com/tanescoyetultd/

IMETOLEWA NA:

OFISI YA UHUSIANO
TANESCO MAKAO MAKUU

WAZIRI JAFO ASEMA DOLA MILIONI 100 ZAHITAJIKA KUBORESHA BONDE LA MTO MSIMBAZI JIJI LA DAR ES SALAAM

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)Sulemani Jafo amesema ndoto yake ni kuona eneo la bonde la Mto Msimbazi jijini Dar es Salaam ambalo limekuwa kero kwa muda mrefu sasa linaboreshwa na kuwa eneo ambalo litakuwa kivutio.

Ametoa kauli hiyo leo Februari 25,2019 wakati anazungumza na maofisa wa ngazi mbalimbali wa Benki ya Dunia ambao wapo nchini na leo na kesho watakuwa kwenye ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayoendelea ndani ya Jiji hilo ikiwemo ya miundombinu ambapo amesema Dola milioni 100 zinahitaji kwa ajili ya kuboresha bonde hilo na hivyo ametoa ombi kwa benki hiyo.

Amefafanua katika bonde la Mto Msimbazi zipo familia ambazo zimepoteza wapendwa wao kutokana na kufa maji kutokana na mafaruko ambayo yamekuwa yakitokea wakati wa msimu wa vua, hivyo anachotamani ni kuona kero iliyopo bonde la Msimbazi inatatuliwa na kubaki eneo salama na kivutio.

"Mimi ni Waziri ni mdogo na ukweli ndoto niliyonayo ni kuona kero ya bonde la Mto Msimbazi inaondolewa na kubaki eneo salama ambalo litakuwa kivutio. Dola Milioni 100 zinahitajika kukamilisha mradi wa kuboresha bonde hilo.Ni matumaini yangu Benki ya Dunia mtashirikiana nasi kama ambavyo tunashirikiana katika miradi mbalimbali ya maendeleo," amesema Waziri Jafo.

Eneo hilo la msimbazi kupitia mradi huo wa uborshwaji wa eneo hilo litakuwa kivutio kutokana namna ambavyo utajengwa kwa kuwa na maeneo ya kupumzika na kubwa zaidi mandhari yake itavutia watu wengi.

Maofisa hao wa Benki ya dunia ambao kabla ya kuanza ziara ya kutembelea miradi ambayo wanaifadhili, walifika ofisi za TAMISEMI ambapo Waziri Jafo ametoa shukrani kwa benki hiyo kwa namna ambavyo inatoa fedha kwa ajili ya kufanikisha uboreshaji wa sekta mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa miundombinu ya barabara,majiji nane,elimu,afya na sekta nyingine.

Wakati huo huo Waziri Jafo amezungumzia namna ambavyo maeneo mengi ya nchi yetu yameboreshwa kutokana na ushirikiano mzuri kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia."Benki hii imetoa Sh.trilioni mbili kwa ajili ya kuboresha miundombinu katika majiji nane pamoja na uboreshaji wa maeneo mengine.

"Kwa namna nchi yetu ilivyojenga Watanzania ambao wameondoka miaka 10 iliyopita wakirudi leo hii wanaweza kupotea kwenye baadhi ya mitaa,kwani imeboreshwa sana.Hata yale maaneo ambayo yalikuwa hayapiti leo hii yana barabara na yanapitika vizuri.Ukweli mitaa mingi imeboreshwa."

Amewaambia maofisa wa Benki ya dunia kuwa Serikali ya Tanzania inatoa shukrani nyingi kwa benki hiyo na kubwa zaidi inatambua namna ambavyo inathamini mchango wao wa kusaidia uboreshaji wa sekta mbalimbali.

Kuhusu ziara ya maofisa hao,amewaambia kuwa watapata fursa ya kuona namna miradi mingi iliyotekelezwa na ile ambayo bado ipo katika hatua mbalimbali kupitia Mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam(DMP).

"Mtapata fursa za kuona namna ambavyo Jiji la Dar es Salaam lilivyoboreshwa kupitia miradi ya DMP.Tunashukuru kwa ushirikiano wenu Benki ya dunia,tuendelee kushirikiana.Rais wetu Dk.John Magufuli ametoa maelekezo Makao makuu ya Serikali yawe Dodoma na Jiji la Dar es Salaam liwe la kibiashara .Hivyo tunaka kuona Jiji hili linavutia kibiashara," amesema Waziri Jafo.

Kwa upande wao maofisa wa Benki  ya Dunia wamemwambia Waziri Jafo kuwa  wamefurahishwa na namna ambavyo utekelezaji wa miradi hiyo na kwamba wataendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kuhakikisha wanaendelea kusaidia fedha za miradi ya maendele

SERIKALI YAAGIZA MSAKO KWA WALIOWAPA MIMBA WANAFUNZI SIHA

$
0
0
*Waziri Mkuu asema kwa mwaka jana wanafuzi 57 walikatishwa masomo 

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameagiza viongozi na wazazi wilayani Siha mkoani Kilimanjaro washirikiane kuhakikisha watu wote waliowapa mimba wanafunzi wanasakwa na kufikishwa kwenye vyombo vya dola.

Amesema katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Desemba mwaka jana jumla ya wanafunzi wa kike 57 walikatishwa masomo baada ya kupata mimba na hadi sasa kesi zilizofunguliwa ni sita tu.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumapili, Februari 24, 2019) alipokuwa akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Isanja, Sanya Juu wilayani Siha wakati akihitimisha ziara yake ya kikazi mkoani Kilimanjaro. 

“Jambo hili halipendezi, kesi sita tu ndio zimefikishwa mahakamani. Hakikisheni wahusika wote waliowapa mimba wanafunzi wanatafutwa popote walipo, wakamatwe na wachukuliwe hatua kali za kisheria.”

Waziri Mkuu alisema Serikali imeweka sheria kali ya kumlinda mtoto wa kike lengo ni kumuwezesha amalize masomo yake ili aweze kujikwamua kiuchumi na aondokane na utegemezi, hivyo ni marufuku kuwakatisha masomo.

Watoto wa kike wanatakiwa kuheshimiwa katika jamii na Serikali itatoa adhabu kali ya kifungo cha miaka 30 jela kwa mtu atakayekatisha elimu ya mtoto wa kike iwe kwa kumuoa, kumpa ujauzo na hata ukikutwa naye nyumbani kwako, katika nyumba ya wageni.

“Tukikukuta na binti wa shule katika kona isiyoeleweka tunakukamata na kukuchukulia hatua za kisheria. Ole wenu vijana, mkibainika mmewapa mimba mabinti wanaosoma, adhabu yake ni miaka 30 jela, sasa tafakari kabla ya kutenda.”

Waziri Mkuu alisema kwa wazazi au walezi watakaowaozesha watoto wa kike ambao bado ni wanafunzi na kwa upande wa wazazi watakaomsindikiza mtoto kwenda kuoa mwanafunzi wote watachukuliwa hatua za kisheria.

“Kuna taarifa nimezipata kuwa baada ya watoto kupewa mimba wazazi au walezi mnamalizana na wahusika kwa kupeana ng’ombe. Sasa tukikukamata unamalizana na mtu aliyempa mimba mwanafunzi na wewe tunakufunga.”

Pia Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwataka wanafunzi wote hususani wa kike wasome kwa bidii ili watimize ndoto zao na wasikubali kushawishika kwa sababu watashindwa kuendelea na masomo yao.

OFISA TAWALA KISARAWE ADAIWA KUOMBA RUSHWA YA MILIONI MBILI

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, KISARAWE 

TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU)wilayani Kisarawe, Mkoani Pwani, imemfikisha mahakamani ofisa tawala wilayani humo, John Mwendamaka kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa ya sh. milioni mbili ikiwa ni kinyume na kifungu cha 15 (1)cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa na. 11/2007.

Ofisa huyo anadaiwa kuomba kiasi hicho, kutoka kwa mtoa taarifa ili aweze kumsaidia mdogo wake kujiunga na mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa. 

John Mwendamaka ambae alifunguliwa kesi ya jinai namba 22 ya mwaka 2019 ni ofisa tawala katika ofisi ya katibu tawala wa wilaya ya Kisarawe. 

Akisoma mashtaka hayo mbele ya hakimu mkazi wilaya ya Kisarawe Devotha Kisoka, mwendesha mashtaka TAKUKURU  Naftali  Mnzava, aliieleza mahakama kwamba mshtakiwa alitenda kosa la kuomba rushwa milioni mbili kwa ajili ya kumsaidia mdogo wa mtoa taarifa kujiunga na mafunzo ya jeshi. 

Aidha mshtakiwa, alikana makosa yote mawili na dhamana ilikuwa wazi hivyo alipata dhamana baada ya kutimiza masharti. 

Kesi hiyo itakuja kwa ajili ya hoja za awali march 5 mwaka huu. 

Hata hivyo,  kamanda wa TAKUKURU mkoani Pwani, Suzana Raymond aliiasa jamii kufuata taratibu, kanuni za sheria za nchi ili kwenda na kasi ya awamu ya tano, chini ya Rais Dkt. John Magufuli.

Pamoja na hayo ,Suzana alisema kuomba na kupokea rushwa ni kosa kisheria hivyo kila mmoja ajiepushe na vitendo hivyo. 

S/M MAENDELEO YAKABILIWA NA MSONGAMANO MKUBWA WA WANAFUNZI ZAIDI YA 200 KATIKA DARASA MOJA-MKAMA

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Kibaha.

SHULE ya msingi Maendeleo ,kata ya Mailmoja Kibaha, mkoani Pwani, inakabiliwa na msongamano mkubwa wa wanafunzi ambapo darasa moja lina wanafunzi 284.

Changamoto hiyo aliitaja ,mwalimu mkuu wa shule hiyo Miriam Mkama wakati mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kata ya Maili Moja Mathayo Mkayala alipofanya ziara kutembelea miradi ya elimu na barabara akiwa na kamati ya siasa ya kata hiyo .

Alisema ,shule hiyo ina wanafunzi wengi ikiwemo wa awali wanafunzi 153, la kwanza wako 284 la pili wako 209, tatu wako 210, la nne wako 171, la tano wako 177, la sita wako 175, saba 158 na memkwa wako sita.

Alitaja changamoto nyingine ,ni upungufu wa vyoo ambapo wavulana 792 wanatumia vyoo vitano mapungufu 26 upande wa wasichana 756 wanatumia vyoo vinne .

Nae mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Maili Moja ,Mathayo Mkayala alisema ,kutokana na hali hiyo kuna kila sababu ya wananchi wa kata ya maili Moja kusaidia ujenzi wa madarasa mapya ili kupunguza msongamano huo ambao unahatarisha wanafunzi kutoweza kusoma vizuri.

"Wanafunzi wamejazana hata namna ya kufundishwa inakuwa ni ngumu hili ni tatizo hivyo wananchi wanapaswa kuliangalia suala hili kwa upekee kwa kujenga madarasa mengine,” alisema Mkayala.

Awali, diwani wa Kata ya Maili Moja ,Ramadhan Lutambi alisema ,changamoto ni kubwa na wameanza mchakato wa kuwaomba wazazi na wananchi kujitolea matofali matatu yamefika 980 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ambapo kwa sasa wameanza darasa moja linalojengwa na wananchi.

Kamati hiyo ya siasa ya kata ya Maiali Moja ilitembelea baadhi ya miradi ya ujenzi wa shule ya msingi Muheza, ujenzi wa madarasa matatu shule ya msingi maendeleo, ujenzi wa vyoo shule ya sekondari Bundikani na ujenzi wa barabara toka shule ya Bundikani kwenda Mpakani.
Viewing all 110078 articles
Browse latest View live




Latest Images