Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109573 articles
Browse latest View live

SALAMU ZA POLE KUFUATIA AJALI ILIYOUA WATU 19 SONGWE

0
0
Sehemu ya Majeneza 19 yaliyotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe kufuatia ajali iliyohusisha magari matatu, mkoa pia umewezesha usafiri wa miili ya marehemu hao. 
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus E. Mwangela akitoa salamu za pole kwa niaba ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa ndugu, jamaa na marafiki wa wafiwa, kufuatia ajali ya gari iliyosababisha vifo 19. 
Ndugu, jamaa na marafiki wa wafiwa, kufuatia ajali ya gari iliyosababisha vifo 19 wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus E. Mwangela akitoa salamu za pole. 
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus E. Mwangela akikagua majeneza kabla hayajakabidhiwa kwa wafiwa, kufuatia ajali ya gari iliyosababisha vifo 19. 
 

SALAMU ZA POLE 

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus E. Mwangela anatoa salamu za pole kwa niaba ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa ndugu, jamaa na marafiki wa wafiwa, kufuatia ajali ya gari iliyosababisha vifo 19 ikiwa wanaume ni 15 na wanawake wanne. 

Brig. Jen. (Mst) Mwangela amesema kutokana na ajali hiyo iliyotokea usiku eneo la Senjele Wilayani Mbozi ikihusisha magari matatu yaliyokuwa yakielekea Mbeya kugongana, serikali Mkoani Songwe imetoa majeneza 19 pamoja na usafiri kwa ajili ya kuhifadhi miili ya marehemu. 

“Rais Magufuli amenituma niwape pole na ametuelekeza kama Mkoa kusimamia Mamlaka za Usalama barabarani kufanya uchunguzi na hatua zinazo stahili kuchukuliwa, pia ameelekeza tujipange vizuri kukabiliana na matukio ya ajali za barabarani”, amesema Brig. Jen. (Mst) Mwangela. 

Brig. Jen. (Mst) Mwangela amesema chanzo cha ajali hiyo kimetokana na gari la abiria aina ya coaster kugongwa na gari la mizigo lililokuwa nyuma yake kisha coaster kugonga gari la mizigo lililo kuwa mbele yake na kupelekea gari la abiria kubanwa katikati ya magari mawili ya mizigo. 

Aidha ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe, kuweka utaratibu maalumu wa magari kupita kwa kupokezana katika maeneo yote yenye miteremko mikali, kuwepo ukaguzi wa magari kabla hayajaanza kushuka au kupanda mlima pamoja na kuweka ulinzi wa maeneo hayo. 

“Mungu ametupa akili za kufanya kazi na akili hizi tuzitumie kuzuia ajali ndani ya Mkoa wa Songwe, hivyo nawasihi watumiaji wote wa vyombo vya moto kuhakikisha wanafuata sheria za usalama barabarani ili kuweza kuepuka ajali kama hizi”, amesisitiza Brig. Jen. (Mst) Mwangela. 

Mapema jana Brig. Jen. (Mst) Mwangela amefika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Songwe ambapo miili ya marehemu ilikuwa imehifadhiwa ili kuwafariji wafiwa waliofika kutambua miili ya ndugu zao.

BENKI PUNGUZENI RIBA ZA MIKOPO MNAYOITOA-MAJALIWA

0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka benki nchini zipunguze viwango vya riba zinazotozwa kupitia mikopo mbalimbali wanayoitoa kwa wananchi.

Aliyasema hayo jana jioni (Ijumaa, Februari 22, 2019) alipozungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Bomang’ombe wilayani Hai.

Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Kilimanjaro kwa ziara ya kikazi alisema kitendo cha benki kutoza riba kubwa kinawaumiza wajasiriamali nchini.

Pia, Waziri Mkuu aliwataka wananchi hususani, vijana, wanawake na wenye ulemavu kuchangamkia fursa ya mikopo inayotolewa katika Halmashauri.

Alisema kila halmashauri inatakiwa itenge asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya kuwawezesha vijana, wanawake na wenye ulemavu kupata mitaji.Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu amewataka wakulima wa kahawa wabadilike na kuondoa miti ya zamani na kupanda mipya ili waongeze tija.

Waziri Mkuu alisema wakulima hao wanaweza kuweka utaratibu wa kuondoa miche ya zamani kwa awamu na kupanda mipya, hivyo kupata mavuno mengi.

DKT SHEIN AWAHIMIZA WAUMINI WA KIISLAM KUIMARISHA MAHUSIANO YAO KULETA USTAWI WA JAMII

0
0
Rais waZanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Al – Hajj Ali Mohamed Shein alisema katika kuimarisha mapenzi baina ya Waumini wa Dini ya Kiislamu na kuleta Ustawi wa jamii ni vyema zikatumika fursa za mikusanyiko ya kupeana nasaha juu ya athari ya mambo yanayoweza kuiharibu jamii.

Alisema migogoro na mivutano inayojichomoza miongoni mwa Waumini akitolea mfano baadhi ya Misikiti haitoi taswira nzuri na hatma yake amani hutoweka ambayo ni muhimu kwa ustawi wa Jamii na kupelekea kuwakosesha Waumini kufanya Ibada kwa utulivu.

Al – Hajj Dr. Ali Mohamed Shein alitoa katuli hiyo katika Hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati akiifungua Rasmi Ijitimai ya Kimataifa inayofanyika katika Kijiji cha Kidoti Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Alisema kuhitilafiana mitazamo ni jambo ambalo lilikuwepo tokea zama za Kiongozi wa Waumini wa Dini ya Kiislamu Mtume Muhammad {SAW}, lakini Waumini wenyewe walikuwa wakikaa pamoja {Shura} katika kutafuta muwafaka wa hitilafu inayojitokeza na baadae waliendelea na Ibada zao kama kawaida.

Rais wa Zanzibar alisema Ijitimai ni miongoni mwa Vielelezo vinavyoonyesha mshikamano na Umoja wa Waumini wa Kiislamu ambao Mola Mtukufu huongeza Baraka na kuleta neema zake kwa Waja hao walioamua kushikamana katika kufanya mambo ya kheir.

Alieleza kwamba utaratibu wa kupeana mawaidha lazima uendelee kwa namna mbali mbali kupitia Ijitimai kama hizi na hata Misikiti kwa vile maisha ya Wanaadamu wakiwemo Waumini yanakabiliwa na changamoto mbali mbali ambazo zinaweza kupelekea Watu kutoka kwenye njia sahihi ya Mwenyezi Mungu.

“ Utaratibu huu wa Waumini kupeana mawadisha ni ishara ya kauli ya Mwenyezi Mungu katika Maandiko yake matukufu alipousifia Umma wa Nabii Muhammad {SAW} kwamba ni umma bora kutokana na kujamrishana mema na kukatazama yaliyo maovu na kumuamini Mwenyezi Mungu”. Al – Hajj Dr. Shein alikuwa akiikariri aya ya 110 ya Suratul Al – Imran.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliwanasihi Waislamu kutoitumia vibaya kinyume na makusudio neema waliyoipata ya mkusanyiko wao unaosaidia kuimarisha imani zao kupitia mihadhara inayotolewa na Masheikh na Walimu mbali mbali.

Akizungumzia vitendo viovu vya udhalilishaji vilavyolitia aibu Taifa, Al – Hajj Dr. Ali Mohamed Shein alitahadharisha wazi kwamba Ustawi wa Jamii hauwezi kupatikana iwapo Akina Mama na Watoto wanaishi kwa hofu kutokana na kufanyiwa vitendo hivyo.

Alisema Jamii imekumbwa na Mtihani mkubwa wa kuibuka kila kukicha kwa kesi zinazotokana na vitendo vya udhalilishaji vinavyoleta maudhi vikitendeka kinyume na Mafundisho ya Dini yenyewe ambapo vile vile ni kinyume na Haki za Binaadamu.

“ Mwenyezi Mungu ametuonya kuacha kufanyiana vitendo vya maudhi miongoni mwetu kwa kutuambia – na wale wanaowaudhi wanaume Waislamu na Wanawake Waislamu pasipo na kufanya kosa lolote, bila shaka wamebeba dhulma kubwa na dhambi zilizo dhahiri”. Dr. Shein alikariri Quran Tukjufu aya ya 58 ya Suratul Ahzab.

Rais wa Zanzibar aliwanasihi Waumini na Wananchi wote kuungana pamoja na Serikali katika mapambano dhidi ya vitendo vya udhalilishaji wanavyofanyiwa Wanawake na Watoto bila ya kuwaonea muhali wale watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo viovu.

Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hivi sasa inatekeleza Mpango Mkakati wa Miaka Mitano wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji na kumuomba kila Mwana Jamii atimize wajibu wake katika mapambano hayo ili kupatikana Ustawi bora wa Jamii nzima.

Al – Hajj Dr. Ali Mohamed Shein aliishukuru na kuipongeza Jumuiya ya Fiysabilillahi Tablih Markaz kwa mafanikio yake katika kutekeleza malengo ya kuanzishwa kwa Taasisi hiyo tokea iliposajiliwa rasmi Mnamo Mwaka 1999.

Alisema mafanikio mengi yamepatikana yakiwemo kumudu kuendeleza mikusanyiko ya Ijitihai kila Mwaka, kuanzishwa Ujenzi wa Majengo ya Skuli mbali mbali pamoja na Ujenzi wa Msikiti uliopo Kidoti ambao tayari umeshafikia hatua kubwa.

Hata hivyo aliunasihi Uongozi huo kwamba changamoto zinazojichomoza zisiwakatishe tamaa bali ziwe chachu ya kuungana na kubuni mikakati ya kupata nyenzo ya kufikia malengo ya Miradi waliyojipangia.

“ Nina matumaini makubwa kwa Uongozi wa Taasisi hii mna uwezo wa kutuvusha kutoka hapa tulipo, ili kwenda mbele zaidi, iwapo mtaendelea kutuhamasisha tuchangie mambo haya ya kheir”. Alisema Al – Hajj Dr. Ali Mohamed Shein.

Alisisitiza kwamba mafanikio huenda pole pole ingawa huhitaji uhamasishaji, kuhimizana na kuendelea kuelimashana juu ya umuhimu wa kuchangia katika masuala hayo yakiwa miongoni mwa Sadakatul Jaariya.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi alielezea matumaini yake kwamba Waumini watakaopata chakula cha roho katika kipindi hicho cha Siku Tatu kwenye mjumuiko huo wataondoka na hazina kubwa ya maarifa , imani na ucha Mungu kwa kuanza maisha mapya yanayoendana na mafundisho watakayoyapata.

“ Tuondoke hapa tukiwa Mabalozi wema na wale wanaotoka nje ya Zanzibar warudi wakitusifu kwa sifa njema, ukarimu na hali ya amani wanayoishuhudia wakati wote wanapokuwa Nchini”. Alisema Dr. Shein.

Alifahamisha kwamba haitakuwa vyema kwamba wanaijitihmai hao waondoke katika mkusanyiko huo wa kheir wakiwa kama walivyokwenda, na yale mazuri waliyojifunza kuyaacha huko kidoti.

Akitoa Taarifa ya Ijitimai hiyo Mwenyekiti wa Jumuiya ya Fiysabililah Tablih Markaz Amir Ali Khamis Mwinyi alisema hiyo ni Ijitimai ya 23 tokea kuanzishwa kwake ambao kwa Kidoi imefikia ya Tatu.

Amir Ali alisema Mada Nne zitakazowasilishwa na Wataalamu mahiri zimepangwa katika Ijitimai hiyo akizitaja kuwa ni pamoja na Umuhimu wa Umoja, Amani, Maendeleo pamoja na Familia inayojitambua.

Alisema lengo la kuanzishwa kwa Ijitimai hiyo ni muendelezo wa utekelezaji wa amri ya Mwenyezi Muungu ya kuandaliwa kwa mikusanyiko ya kuamrishana mema na kukatazana mabaya.

Amir Ali alifahamisha kwamba kazi hiyo ya Allah inakwenda sambamba na Jumuiya hiyo kuendelea kuwalea Watoto wanaoishi katika mazingira magumu ambao kwa sasa wamefikia 1011 ambapo Kijiji cha kidoti pekee kina Watoto 56.

Alifahamisha kwamba katika kufikia malengo hayo Jumuiya hiyo imekusudia kuendelea na Miundombinu ya kukamilisha majengo yake yaliyopo katika eneo hilo la Majengo liliopo Kidoti.

Alieleza kuwa hatua zinachukuliwa katika kuyakamilisha Majengo Saba kwa ajili ya Waumini wa Kike, Jengo la Ghorofa kwa ajili ya Wageni pamoja na kukamilisha Msikiti Mkuu unaotarajiwa kuchukuwa Waumini Elfu 5,5000 kwa sala moja.

Akitoa salamu ya Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir Mwakilishi wake Sheikh Jongo amesisitiza suala la kuimarishwa Amani mingoni mwa Waumini na Wenanchi wote.

Sheikh Ahmed Jongo alisema kitendo cha kudumisha amani ndio silaha pekee itakayowasaidia Waumini kuendelea kufanya Ibada zao kwa uhakika na utulivu zaidi.

Akimkaribisha mgeni rasmi kuwawaaidhi waumini waliohudhuria Ijitimai hiyo Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Oman Kabi alisema suala la kumuabudu Mwenyezi Mungu ni kitu cha msingi katika maisha ya kila Siku ya Muumini aliyeshiba Taqwa.

Alisema Malaika uwa Mwenhyezi muungu mara zote hutanda kila pembe ya Dunia kufuatilia ibada zinazotekelezwa na Waja walioamini kumsujudia Mwenyekiti Muungu Mmoja asiya na mshirika.

Zaidi ya Waumini Elfu Tano Wake na Waume kutoka Nchi za Zambia, Uganda, Kenya, Rwanda, Malawi, Mikoa ya Tanzania Bara na Wenyeji Mikoa Kumi ya Visiwa vya Unguja na Pemba wamehuduria Ijitimai hiyo ya 23.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akilakiwa na Viongozi wa Dini ya Kiislamu alipowasili Kidoti kwa ajili ya kuifungua Ijitimai ya Kimataifa kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Al – Hajj Dr. Ali Mohamed Shein.
 Balozi Seif akiifungua Ijitimai ya Kimataifa kwa niaba ya Rais wa Zanzibar hapo katika Msikiti Mkuu wa eneo la ijitimai hiyo Kidoti Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Fiysabilillah Tablih Markaz Amir Ali Khamis Mwinyi akitoa Taarifa ya Ijitimai katika hafla ya ufunguzi wake uliofanywa na Balozi Seif kwa niaba ya Rais wa Zanzibar.
 Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Qabi akijiandaa kumkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kuifungua Ijitimai ya Kimataifa hapo Kidoti. 
Balozi Seif  akitembea kuwasalimia Waumini Wanawake wa Dini ya Kiislamu pamoja na kukagua eneo litakalojengwa Majengo yao ndani ya viwanja vya Fiysabilillah Tablih Markaz Kidoti.Picha na – OMPR – ZNZ.

Dkt Macheyeki aitaka kampuni ya Neelkanth kuachana na uagizaji wa malighafi kutoka nje ya nchi

0
0
Na Greyson Mwase, Pwani. 

Kamishna wa Tume ya Madini, Dkt. Athanas Macheyeki ameitaka kampuni inayojishughulisha na uzalishaji wa chumvi ya Neelkanth Salt Limited iliyopo Wilayani Mkuranga mkoani Pwani kuachana na uagizaji wa malighafi zinazotumika katika kuzalisha chumvi kutoka nje ya nchi na badala yake ijikite kwenye matumizi ya malighafi zilizopo nchini na kusisitiza kuwa kufanya hivyo kunazorotesha soko la ndani. 

Dkt. Macheyeki alitoa agizo hilo mapema leo tarehe 22 Februari, 2019 kwenye ziara yake katika kiwanda hicho ikiwa ni sehemu ya ziara ya Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula katika mkoa wa Pwani yenye lengo la kutembelea wachimbaji wa madini pamoja na kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili. 

Aliyasema hayo mara baada ya kuelezwa kuwa kampuni hiyo imekuwa ikiagiza malighafi ya chumvi kwa asilimia kati ya 60 na 70 kutoka katika nchi za Namibia, India na Afrika ya Kusini. 

Alisema kuwa Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 pamoja na Marekebisho yake ya Mwaka 2017 inawataka wachimbaji wa madini nchini kutumia bidhaa za ndani ya nchi badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi na kuitaka kampuni hiyo kuendelea kujipanga zaidi katika kuhakikisha baadaye inaondokana na matumizi ya malighafi za kutoka nje ya nchi. 

Aliendelea kusema kuwa, katika kujiandaa na matumizi ya malighafi ya chumvi kutoka ndani ya nchi, kampuni inatakiwa kutoa elimu kwa wazalishaji wa chumvi katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Kilwa ili waweze kununua chumvi iliyo bora na kuondokana na matumizi ya malighafi ya chumvi kutoka nje ya nchi na kuinua uchumi wa wazalishaji hao wa chumvi. 

Katika hatua nyingine, Dkt. Macheyeki aliitaka kampuni hiyo kuhakikisha inawasilisha mpango wa manunuzi ya bidhaa na huduma kutoka wananchi wanaoishi karibu na kiwanda hicho (local content plan) pamoja na kiapo cha uadilifu Machi 15 mwaka huu kwenye Ofisi za Mtendaji Mkuu wa Tume ya Madini zilizopo jijini Dodoma. 

Aidha, Dkt. Macheyeki aliitaka kampuni hiyo kuwasilisha mpango wa kuongeza ujuzi kwa wafanyakazi wake ili baadaye waweze kushika nafasi za wataalam kutoka nje ya nchi kwenye Ofisi za Tume ya Madini mapema kama Sheria ya Madini inavyowataka. 

Aliendelea kufafanua kuwa, Serikali inapenda kuona wawekezaji katika sekta ya madini wanafanya kazi katika mazingira mazuri ili waweze kulipa kodi mbalimbali Serikalini. 

“Ndio maana tozo nyingi zilizokuwepo kwenye madini ya chumvi zimeondolewa, tunataka mzalishe kwa faida, lakini wito wangu kwenu ni kuhakikisha mnafuata Sheria ya Madini pamoja na kanuni zake, Tume ya Madini ipo tayari kuwasaidia muda wowote,” alisisitiza Dkt. Macheyeki. 

Awali akizungumzia changamoto za kampuni hiyo, mmoja wa wataalam kutoka kampuni hiyo, Tanmay Purohit alisema kuwa kumekuwepo na changamoto ya kukatika kwa umeme na kuongeza kuwa wameshaiomba Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuwekewa umeme katika mashamba ya chumvi yaliyopo katika eneo la Shungubweni wilayani humo na kuwekewa gesi kwa ajili ya matumizi ya kiwandani hapo. 

Alisema kuwa wamekuwa wakitumia gharama kubwa ya kuendesha mitambo kwa kutumia dizeli pindi umeme unapokatika kiwandani hapo na katika mashamba ya chumvi. 
Mmoja wa watendaji kutoka katika kampuni inayojishughulisha na uzalishaji wa chumvi ya Neelkanth Salt Limited iliyopo Wilayani Mkuranga mkoani Pwani, Mahendra Prasad (katikati) akielezea shughuli zinazofanywa na kampuni hiyo kwa Kamishna wa Tume ya Madini, Dkt. Athanas Macheyeki (kushoto) mara alipofanya ziara katika kampuni hiyo tarehe 22 Februari, 2019 lengo likiwa ni kufanya ukaguzi pamoja na kutatua kero mbalimbali. 

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 23,2019

WAZIRI MBARAWA AAGIZA TAASISI ZA SERIKALI ZIFUNGIWE MITA ZA LUKU

0
0


WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa akizungumza baada ya kupokea taarifa ya mkoa wa Tanga wakati wa ziara yake leo
WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa kushoto akimsikiliza kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Saidi wakati akielezea hali ya upatikanaji wa maji kwa mkoa wa Tanga wakati wa ziara yake
WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa kulia akisaini kitabu cha wageni wakati alipofika Ofisi za Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Mhandisi Geofrey Hilly



WAZIRI wa Maji Proffesa Makame Mbarawa ameagiza taasisi zote za serikali zifungiwe mita za luku ili ziweze kwenda na matumizi mazuri ya maji ili kupunguza changamoto za kutokulipa kwa wakati bili za maji na kujikuta zikiingia kwenye madeni makubwa.

Proffesa Mbarawa aliyasema hayo leo wakati wa ziara yake mkoani Tanga ambapo alisema mita za luku litasaidia kuweza kuondokana na kasumba za watu kumwaga maji hivyo na hivyo kuweza kusimamia matumizi ya maji kwenye maeneo yao.

“Ndugu zangu mita za luku msiwapelee wateja sugu bali wapelekeeni hata wale watu wengine ambao wapo kwenye maeneo mbalimbali lakini pia Jeshi la Polisi sio wabaya wanalipa bili lakini wawekeeni mita za luko isipokuwa ndani ya kituo cha Polisi msiweke”Alisema Waziri Mbarawa.

“Lakini hatupelekei wateja sugu tunakosea kwa sababu hii inaweza kupelekwa kukote kwa sababu inaweza kusimamia matumizi ya maji ndani ya mwezi husika…..nirudir Jeshi la Polisi sio wabaya wanalipa bili zao lakini wawekeni mita sio mwanzo maeneo mengi Mtwara,,Iringa nao wanatumiakwenye kota zao wawekeeni mita hizo”Alisema Waziri Mbarawa.Aidha pia mita hizo la luku zitaweza kusaidia kuweka matumizi mazuri ya maji na mambo ya kuanza kulalamika hawalipi tuwafungie traasisi zio nyingi mita moja laki mbili ukchukua wateja 20 karibuni milioni nne na mapato yatakayopatikana ni makubwa.

Hata hivyo alsema serikali imejipanga kuhakikisha changamoto ya huduma ya maji hapa nchini inatatuliwa ili wananweza waweze kunufaika na huduma hiyo muhimu kwa ukuaji wa uchumi na maendeleo.Katika ziara hiyo Waziri Mbarawa alitembelea maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye chanzo cha Maji cha Mabayani,Mtambo wa kusafirishia maji eneo la Mowe na eneo la Horohoro wilayani Mkinga.

MAKAMU WA RAIS AZITAKA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUHAKIKISHA ZINATOA ASILIMIA 10% YA MAPATO YAKE KWA WANAWAKE,VIJANA NA WAZEEibu wa sheria.

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi wa vikundi vya ujasiriamali ambayo vimekabidhiwa hundi ya shilingi milioni 40 kama sehemu ya 10%ya mapato ya Halmashauri ambapo vikundi 11 vimefaidika na mkopo huo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Sikonge ambaye pia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Joseph Kakunda(kulia) mara baada ya kuwasili Sikonge mkoani Tabora ikiwa sehemu ya ziara yake ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akimwagilia mei wa kumbukumbu alioupanda mara baada ya kuweka  jiwe la msingi  la ujenzi wa Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora.
 Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhe. Joseph Kakunda akihutubia wananchi katika uwanja wa TASAF Sikonge mkoani Tabora.
 Sehemu ya Wananchi wa Sikonge, mkoani Tabora waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara ambao Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alikuwa mgeni rasmi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya TASAF wilayani Sikonge mkoani Tabora
 
 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha zinatoa asilimia 10% ya mapato yake kwa Wanawake, Vijana na Walemavu kwa mujibu wa sheria.

Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati akihutubia wananchi katika Viwanja vya TASAF wilaya ya Sikonge mkoani Tabora ikiwa ni siku ya tatu ya ziara yake ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo.

“Niagize Halmashauri zote kuhakikisha zinatoa fedha hizo kama ilivyopangwa bila riba yeyote kwani fedha hizi zipo kisheria na kwa kutozitoa ni kuvunja sheria”alisema Makamu wa Rais.

Aidha, amesisitiza Halmashauri kuweka utaratibu mzuri kuhakikisha fedha zinazokopeswa kwa vikundi zinarejeshwa kwa kuwa lengo la fedha hizo ni kuwanufaishwa walengwa zaidi huku akishauri kuwepo na makundi yenye mradi unaoleta tija kwa manufaa ya wengi.

Makamu wa Rais ametoa wito kwa wakulima wa tumbaku mkoani Tabora kutoharibu mazingira kwa kukata miti kwani hasara ya kukata mti ni kubwa kulikoni faida wanayoipata hivyo amewashauri kutumia teknolojia mpya ya Solar na Umeme kama ilivyoshauriwa na wataalamu.

Wakati huohuo Mbunge wa Jimbo la Sikonge ambaye pia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Joseph Kakunda amesema mpaka 2021 kwa mara ya kwanza vijiji vyote wilayani Sikonge vitapata umeme wa uhakika.

Mheshimiwa Kakunda ameleeza namna wananchi wa Jimbo lake walivyoridhishwa na kasi ya maendeleo ambapo Serikali imetoa pesa katika miradi ya afya, miradi ya elimu na kuboresha miundombinu ya barabara.

Pia alielezea Vipaumbele ambavyo wamejiwekea jimboni kwake katika kukuza fursa za kimaendeleo, vipaumbele hivyo ni kuanzisha viwanda vya usindikaji mazao ya kilimo, pili viwanda vya vifaa vya majumbani na ujenzi na tatu ni viwanda vitakavyoajiri watu wengi kwa wakati mmoja.

Kwa upande mwingine Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko amesema Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kurudisha uchumi wa madini kwa Watanzania.“Wananchi changamkieni kuwekeza kwenye uchumi wa madini, lipeni kodi kwa maendeleo ya Taifa letu”. alisema Waziri huyo.

Katika ziara hiyo Makamu wa Rais aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Halmashauri ya wilaya hiyo,alikabidhi hundi ya shilingi milioni 40 kwa vikundi 11 vya ujasiriamali na kuzungumza na wananchi.

Makamu wa Rais ameongozana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba, Waziri wa Madini Mhe. Doto Biteko, Naibu Waziri Maji Mhe. Juma Aweso, Naibu Waziri Ujenzi Mhe. Elias Kwandikwa, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelline Mabula na Naibu Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara.

HOSPITALI ZOTE NCHINI ZATAKIWA KUWA NA ICU YA WATOTO WACHANGA

0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiongea na mama Mjamzito wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akieleza Waandishi wa Habari (hawapo kwenye picha) umuhimu wa kifaa kinacho rekodi mahudhurio na muda wa watumishi kufika ofisini (Biometric) wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akimjulia hali mama aliyetoka kujifungua, wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akimtazama mtoto njiti, aliyepakatwa na mamaye, wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na Madaktari Bingwa wa Hospitali teule ya Mkoa wa Pwani Tumbi, baada ya kumaliza ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali hiyo.


……………………….


NA WAMJW – PWANI


WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameziagiza Hospitali za rufaa zote nchini kuwa na ICU kwaajili ya watoto wachanga ili kupunguza vifo vifo vyao.

Waziri Ummy amesema hayo wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji wa huduma za Afya katika Hospitali teule ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.

Waziri Ummy ameagiza hayo kupitia kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo kuwa ahakikishe watoto wachanga lazima wawe na ICU yao ili kuhakikisha vifo vya Watoto wachanga vinapungua nchini.

“Watoto wachanga wagonjwa, wawe na ICU yao, lengo letu kama Serikali ni kupunguza Vifo vya Watoto wachanga, kwasababu tukipunguza vifo vya Watoto wachanga, tutakuwa tumepunguza vifo vya Watoto wanye umri wa chini ya miaka mitano” alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa karibu 40% ya vifo vya watoto ni watoto wachanga na katika kila Watoto 100, Watoto 40% ni Wachanga, hivyo Serikali inaendelea kuchukua jitihada za makusudi ili kupunguza vifo hivi, ikiwemo kusisitiza kila Hospitali nchini kuwa na ICU.

“Karibu 40% ya vifo vya watoto ni watoto wachanga na katika kila Watoto 100, Watoto 40% ni Wachanga, kwahiyo Daktari ni lazima tulifanyie kazi agizo hilo” alisema Waziri Ummy.Licha ya changamoto alizokutana nazo Waziri Ummy amesema kuwa Serikali inatarajia kujenga jengo mahususi kwaajili ya huduma za Dharura katika Hospitali zote za Rufaa za Mikoa nchini ili kuokoa maisha ya wagonjwa, hasa waliopata ajali.

“Nafurahi kusema, Serikali imeahapata fedha kwahiyo tutakuwa na jengo mahususi kwaajili ya huduma za Dharura na wagonjwa wa ajali, na hii tunataka iwe katika Hospitali za Rufaa za Mikoa zote ili mgonjwa aweze kuokolewa maisha muda mfupi anapofika Hospitali” alisema Waziri Ummy.

Pia, Waziri Ummy ameridhishwa kwa kiasi kikubwa juu ya hali ya upatikanaji wa dawa nchini, huku akiwatoa hofu Mwananchi kuwa Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) ina dawa zakutosha.

Aliendelea kusema kuwa Serikali imeainisha fani nane nane za kipaumbele ili kuwa na madaktari Bingwa wawili katika kila fani ikiwemo, Daktari Bingwa wa Watoto, Daktari Bingwa wa magonjwa yakina mama na uzazi, Daktari Bingwa wa upasuaji wajumla, Bingwa wa upasuaji wa mifupa, Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani (Physician) n.k

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa katika Mkoa wa Pwani Serikali imejenga na kuboresha vituo vya Afya zaidi ya 16, Hospitali za Wilaya 3, na kuboresha Hospitali ya Mikoa ili kuwa na huduma za wagonjwa mahututi na wagonjwa wa Dharura.

Mbali na hayo Waziri Ummy amewahasa Mwananchi kujiunga na mfuko wa Bima ya Afyà ili kujihakikishia matibabu wakati wa ugonjwa, jambo litalosaidia kuokoa gharama kubwa za matibabu pindi Mwananchi anapopata ugonjwa.

“Nitoe Wito kwa Wananchi kujenga utaratibu wakujiunga na Bima ya Afya, kwasababu ndio njia ya uhakika yakujihakikishia matibabu kabla hawajaugua” alisema Waziri Ummy.

Matrekta ya Ursus na Mapinduzi ya Kilimo

WAZIRI MKUU ATOA SIKU 16 KWA MKURUGENZI ROMBO

0
0


WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ametoa siku 16 kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo, Magreth John awe amepeleka asilimia 20 sawa na sh milioni 114 ya kijiji cha Holili kabla ya Machi 10 mwaka huu, fedha hizo zinatokana na mauzo ya madini ya pozolana.

Ametoa maagizo hayo leo (Jumamosi, Februari 23, 2019) wakati akizungumza na watumishi wa Kituo cha Pamoja cha Forodha cha Holili pamoja na wananchi wa kijiji cha Holili, akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Kilimanjaro. Kituo hicho kipo katika mpaka wa Tanzania na Kenya.

Waziri Mkuu alitoa maagizo hayo baada ya wananchi wa kijiji cha Holili kuwasilisha malalamiko yao kupitia mabango wakimuomba awasaidie ili Halmashauri hiyo iweze kulipa fedha zao zinazotokana na mapato ya mauzo ya madini hayo yanayochimbwa kijijini kwao.

“Mkuu wa wilaya (Agness Hokororo) simamia kuhakikisha kiasi hicho cha fedha kinakwenda kwa wananchi na Mkuu wa Mkoa (Dkt. Anna Mgwira) nataka nipate taarifa kuwa fedha hizo zimeshalipwa kwa uongozi wa kijiji husika.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka watendaji katika maeneo mbalimbali nchini kuwa wamepelekwa huko kwa ajili ya kuwahudumia wananchi, hivyo hawana budi kutenga muda wa siku tatu kwa wiki na kwenda maeneo ya vijijini kusikiliza kero zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amesema hali ulinzi na usalama katika mpaka huo si nzuri, Serikali imeamua kuimarisha ulinzi kwenye mpaka huo, hivyo ni muhimu kwa wananchi washirikiane katika kuulinda mpaka huo.

Hivyo, Waziri Mkuu ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuwakamata na kuwachukulia hatua watu wote watakaokamatwa wakipita au kuingiza mizigo kupitia njia zisizo rasmi kwa sababu hao ndio wanaopitisha silaha.

Waziri Mkuu amesema wananchi wa Tanzania na Kenya hawajazuiwa kufanya biashara upande wowote bali wanatakiwa wafuate sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika nchi husika ikiwa ni pamoja na kutumia njia rasmi.

Amewataka viongozi na watendaji waliopo maeneo ya mipaka huo wa Holili wawe makini kwa sababu mpaka huo hauko salama na kuna mambo mengi yanayoendelea ambayo yapo kinyume cha sheria.

MAKAMU WA RAIS AAGIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA MWANGA WA JUA(SOLAR) KATIKA UKAUSHAJI WA TUMBAKU

0
0
NA TIGANYA VINCENT,TABORA

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan ameziagiza wadau wa zao la tumbaku kuhakikisha wanatumia teknolojia ya kisasa na mabani ya kisasa katika kukaushaji wa tumbaku.

Hatua itasaidia kuepusha uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji wa miti mikubwa kwa ajili ya ukaushaji wa tumbaku kwa kutumia mabani ya kizamani.

Makamu wa Rais alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara katika uwanja wa TASAF wilayani Sikonge ikiwa ni siku tatu ya ziara yake mkoani Tabora .

Alisema miti inayokatwa kwa ajili ya matumizi ya ukaushaji wa tumbaku kwa kutumia katika ukaushaji wa zao hilo ina thamani kubwa kuliko faida wanayopata kutokana na mauzo ya zao hilo.

Makamu wa Rais alisema mauzo ambayo mtu angepata kutokana na uuzaji wa miti ule ule ambao umetumika kuchomea tumbaku ni makubwa kuliko yake ambayo anayapata kupitia uchomeaji tumbaku.

Alisema ni vema wadau wakahakikisha wanashirikiana na Mwekezaji ambaye ameonyesha nia ya kuwekeza katika matumuzi ya teknolojia inayotokana na mwanga jua (solar) na umeme wakati wa kukausha tumbaku ili kupunguza ukataji wa miti kwa ajili ya kupata nishati ya ukaushaji wa zao.

Aidha Makamu wa Rais aliwaagiza wadau wa tumbaku wanapowapokea wanunuzi wa zao hilo wahakikishe wanaweka kipengele cha upandaji miti na utunzaji wa mazingira kabla ya kuingia nao mkataba.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri alisema kuwa ipo haja ya hatua za makusudi zikachukuliwa kuhakikisha kilimo cha zao la tumbaku haliendelei kuwa chanzo cha uharibifu wa mazingira kwa ajili ya kuukoa Mkoa huo kugeuka Jangwa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Tumbaku Tanzania (TTB) Hassan Wakasuvi alimuomba Makamu wa Rais, Ofisi yake isaidie katika ujenzi wa mabani ya kisasa yanayotumia nishati ya jua na umeme wakati wa ukaushaji wa tumbaku katika maeneo mbalimbali nchini.

Alisema katika andiko ambao baadhi ya wadau watakwenda nalo China kwa ajili ya kutafuta masoko zaidi ya zao hilo wamependekeza wanunuzi wanunue tumbaku iliyozalishwa na umeme na mwanga wa jua(solar).

Wakasuvi alisema kwa hali ya wakulima walio wengi hivi sasa wanatumia kuni na hivyo matumizi ya teknolojia hiyo mpya hawawezi kumudu bila kupata msaada wa ujenzi wa teknolojia hiyo mpya.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan ameziagiza halmashauri nchini kuhakikisha mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato yake ya ndani kwa ajili vikundi inakuwa na tija na sio kama ilivyo sasa.

Hatua itavisaidia vikundi kupata fedha ambazo zitaviwezesha kutekeleza miradi yenye tija kwa wanavikundi na kuwawezesha kurejesha.

Makamu wa Rais alilazika kutoa kauli hiyo baada ya kutoa mkopo wa milioni 40 kwa vikundi 11 vya Halmashauri ya Sikonge.

Alisema kwa kiasi hicho kwa watani wa idadi ya vikundi , kila kikundi kitapata wastani wa milioni 3 ambazo ni kiasi kidogo kwa ajili ya shughuli zao.

Makamu alisema ni vema Halmashauri zinapotoa mikopo zihakikishe kuwa fedha wanatoa katika vikundi zitaleta matokeo mazuri na zitakuwa endelevu kwa ajili ya kuwaendeleza wao na hatimaye kuzirejesha ili ziwasaidie wengine.

Makamu wa Rais aliongeza kuwa Halmashauri hiyo inaweza kuanza na vikundi vichache kwa kuviwezesha ununuzi wa mizinga na ununuzi wa ng’ombe wa kisasa kwa ajili ya kuanzisha ranchi ambao watawasaidia wakopaji kuuzia viwanda malighafi badala ya kuwapa fedha kidogo ambazo haziwasaidii.

H-TOWN OLD SCHOOL REUNION USIPIME MTANANGE WA SIMBA NA YANGA KUPIGWA JUMAMOSI

0
0

HOTELS HOUSTON KARIBU NA UKUMBI
-Palace Inn                                         
9317 W Sam Houston Pkwy   
Houston, TX 77099
Ph # 713 777 4622

-Holiday Inn
11160 South Fwy
Houston, TX 77031
Ph # 281 530 1400

-Scottish Inns & Suites
9610 W Houston Pkwy S,
Houston, TX 77099
Ph # 281 564 9100

-Frontier Inn
11230 Southwest Fwy,
Houston, TX 77032
Ph # 281 496 9000

-Symphony Inn & Suites
11744 Southwest Fwy,
Houston, TX 77031
Ph # 281 933 5550

-Comfort Inn Southwest
11230 Southwest Fwy,
Houston,TX 77031
Ph # 281 498 9000

Courtyard By Marriott
12655 Southwest Fwy,
Stafford,TX 77477
Ph # 281 491 7700

Comfort Suites
7707 W Sam Houston Pkwy S,
Houston, TX 77072
Ph # 713 774 7707

-Hilton Garden Inn
6855 W Sam Houston Pkwy S,
Houston, TX 77072
Ph # 713 270 6100

-Home 2 Suites by Hilton
11121 Fountain Lake Dr,
Stafford, TX 77477
Ph# 346 309 2240

-Comfort Inn & Suites
11050 Southwest Fwy,
Houston, TX 77074
Ph # 281 568 6969

-Crowne Plaza Houston
9090 Southwest Fwy,
Houston, TX 77074
Ph# 713 995 0123

TANGA UWASA WATAKIWA KULILINDA BWAWA LA MAJI LA MABAYANI

0
0
Waziri wa Maji Proffesa Makame Mbarawa kushoto akizungumza wakati alipofanya ziara yake wilaya ya Tanga kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi. 
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi k,ushoto anayemsikiliza kwa umakini ni Waziri wa Maji Proffesa Makame Mbarawa
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly akisistiza jambo wakati wa ziara hiyo 
Afisa Raslimali watu wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Haika Ndalama akizungumza wakati wa ziara hiyo 
Waziri wa Maji Proffesa Makame Mbarawa katika akitazama mitambo ya uzalishaji wa maji Moye Jijini Tanga kushoto ni nMkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly kulia ni Msimamizi wa shughuli za Uzalishaji Maji katika kituo cha kuzalishia Maji Mabayani Faraji Nyoni 
Waziri wa Maji Proffesa Makame Mbarawa mwenye kofia katikati akiangalia namna maji kwenye kituo cha Kuzalishia maji cha Mabayani Jijini Tanga wakati alipokitembelea ikiwa ni ziara yake kulia ni msimamizi wa shughuli za Uzalishaji Maji katika kituo cha kuzalishia Maji Mabayani Faraji Nyoni,Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly,Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Said 
Msimamizi wa shughuli za Uzalishaji Maji katika kituo cha kuzalishia Maji Mabayani Faraji Nyoni kushoto akimuonyesha Waziri wa Maji Proffesa Makame Mbarawa jambo wakati wa ziara hiyo 
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly kushoto akimuelezea jambo Waziri wa Maji Proffesa Makame Mbarawa kulia wakati alipotembelea kituo hicho 
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly kushoto akimuelezea jambo Waziri wa Maji Proffesa Makame Mbarawa kulia wakati wakitoka kwenye kituo hicho



MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) imetakiwa kuhakikisha wanalilinda bwawa la maji la mabayani kwa kuliwekea mipaka ili kuepusha kuvamiwa na wananchi wanaoishi karibu nalo. 

Hayo yalisemwa na Waziri wa Maji Proffesa Makame Mbarawa wakati alipolitembelea bwawa hilo ikiwa ni ziara yake mkoani Tanga ambapo alisema hilo linatokana na bwawa hilo kuwa ndio tegemezi kubwa kwa mji wa Tanga na maeneo ya karibu. 

Alisema ni muhimu kulindwa kwa eneo hilo la kwenye mabwawa hayo ikiwemo kutumia sheria za mita 500 kutoka kwenye bwawa hilo ili lisiweze kuvamikwa na wananchi ambao kila siku wamekuwa wakisaka ardhi kwa ajili ya matumizi. 

“Ndugu zangu wataalamu jambo kubwa ni kuhakikisha wanalilinda eneo hili la kwenye mabwawa hayo lakini pia sheria inasema mita 500 au waziri anaweza kutoa maelekezo ni muhimu kupata mita 500 zinafaa kubwa hasa maeneo ya chini kabla ya wananchi hawajavamia kwani bwawa linaweza kupasuka na kusababisha watu kupoteza maisha”Alisema Waziri Mbarawa. 

Alisema lazima kuwepo kwa mita hizo kutokana na kwamba iwapo wananchi wataishi karibu sana na na bwawa hili ikitokea siku bwawa limepasuka maji yanaweza kusambaa sehemu kubwa mifano ipo mingi mabwawa yanapasuka na watu kupoteza maisha .“Maeneo ya chini ya mabwawa wananchi waiishi jambo ambalo ni hatari kwani bwawa linapopasuka kuna madhara makubwa yanaweza kuwakumba yakiwemo ya kupoteza maisha ….lakini pia ni vema kabla ya wananchi hawajavamia tuweke alama zetu za mabwawa hasa sasa hivi tusije kukaa kama tukapata shida kama tunazozipata bwawa la mindu”Alisema Waziri Proffesa Mbarawa. 

“Bwawa hili lazima lilindwe liwekewe mipaka wajuia wapi mwisho wa bwawa kwani bila kufanya hivyo tukiliacha ardhi kila siku inapungua wananchi wanasaka ardhi hasa kwenye maeneo yenye maji maji hivyo baadae tunaweza kuja kupambana na wananchi kuhusu eneo hilo kama hatutalilinda lakini nashukuru mamlaka kunipa fursa ya kutembelea bwawa la mabayani na ndio tegemezi kubwa kwa mji wa Tanga na maeneo ya karibu kwa ajili ya kupata maji”Alisema 

“Kama alivyosema mtaalamu bwawa lina lita milioni 7.7 kuhifadhi lina uwezo wa kuzalisha maji kwa mji wa Tanga miezi mitano kama ilivyoeleza bila matataizo lakini changamoto kubwa ni magugu hivyo sisi tutaona namna ya kutumia utaalamu wa jinsi ya kuyatoa lengo likiwa bwawa hili liendelea kutumika muda mrefu halina shida lina uwezo mzuri,”Alisema . 

Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo,Msimamizi wa shughuli za Uzalishaji Maji katika kituo cha kuzalishia Maji Mabayani Faraji Nyoni bwawa hilo linapokea Mto Zigi unaotoka Amani wilayani Muheza limejengwa mwaka 1976 na 1978 likaanza kazi rasmi kutumika. Alisema bwawa hilo lina kina cha urefu wa mita 24 na lina uwezo wa kuhifadhi maji lita milioni 7.7 maji hayo yana uwezo wa kuwatosheleza miezi mitano hata kama hakuna mvua itakayokuwa ikinyesha kwa kipindi hicho. 

“Lakini changamoto kubwa ni watu wanalima kwenye eneo hilo…watu wanakata miti,bwawa limezunguwa na vijiji vitano na wapo wafugaji hivyo wanakwenda kulishia mtoni bado hairuhusiwi kisheria mamlaka kupitia sheria za vijiji waliunda kamati shirikishi ya vijiji imeweza kusaidia sana kupunguza kidogo tatizo hilo “Alisema . 

Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Geofrey Hilly alisema mpango wa mamlaka hiyo kwa mwaka ujao wa fedha ni kuhakikisha wanabadilisha bomba urefu wa kilomita zaidi ya 50 kuondoa ya zamani ili kuepusha maji kupotea kwa njia ya mivujo. 

Alisema hilo linatokana na mabomba kupasuka mara kwa mara kunakosababishwa na uchakavu wake hivyo wakaona umuhimu wa kjuyabadilisha ili kuweza kuendana na wakati uliopo. 

Rais wa Sudan Omar al-Bashir yatangaza hali ya hatari na kuwafuta magavana wa majimbo

0
0
Rais wa Sudan Omar al-Bashir ametangaza hali ya hatari nchini humu na kufutilia mbali utawala wa majimbo na uongozi wake.

Katika hotuba yake kwa taifa rais Bashir alisema kuwa maandamano yanayoshuhudiwa nchini yanalenga kuvuruga amani na kuhujumu utawala wake.

"Natangaza hali ya hatari kwote nchini kwa mwaka mmoja."

"Natangaza kuvunjiliwa mbali kwa utawala wa majimbo katika ngazi zote hadi za mikoa."

Waandamanaji walimiminika katika mji wa Omdurman baada ya tangazo hilo, lakini waliyoshuhudia wanasema maandamano hayo yalizimwa na polisi kwa kutumia bomu ya machozi.

Saa kadhaa baada ya tangazo hilo rais Bashir amewateua wakuu wa vikosi vya usalama kuchukua nafasi ya magavana waliyofutwa kazi.

Katika hotuba yake kwa taifa bwana Bashir ameliomba bunge kuahirisha mchakato wa marekebisho ya katiba ambao ungemruhusu kugombe muhula mwingine madarakani.

Bashir pia alisema kuwa maandamano yanayoshuhudiwa nchini yanalenga kuvuruga amani na kuhujumu utawala wake.

Ripoti za awali kutoka shirika la kitaifa la ujasusi (NISS) ziliashiria kuwa Bashir huenda akajiuzulu.


DKT. MWANJELWA AMPA ONYO KALI AFISA UTUMISHI HALMASHAURI WILAYA YA KIBAHA KWA KUMTOLEA LUGHA CHAFU MSTAAFU

0
0




Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Mji Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao chenye lengo la  kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao, kabla kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Halmashauri hizo mkoani Pwani.
IMG_2001
Baadhi ya watumishi wa umma wa Halmashauri ya Mji Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha  wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (hayupo pichani), wakati wa kikao kazi cha watumishi hao na Naibu Waziri huyo chenye  lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao, kabla ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Halmashauri hizo mkoani Pwani.
IMG_2003
Katibu Tawala Mkoa wa Pwani, Bi. Theresia Mbando akitoa neno la utangulizi kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) kuzungumza na watumishi wa Halmashauri ya Mji Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao  chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao, kabla kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Halmashauri hizo mkoani Pwani.
IMG_2004
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akitoa onyo kwa Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Bi. Ruth Mwelo ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu  wa Halmashauri hiyo kwa kumtolea lugha chafu mstaafu aliyekuwa akidai haki yake, onyo hilo amelitoa wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao.

……………………
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) amempa onyo kali Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Bi. Ruth Mwelo ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu  wa Halmashauri hiyo kwa kumtolea lugha chafu mstaafu aliyekuwa akidai haki yake na kumtaka afisa huyo ajirekebishe haraka iwezekanavyo.

Onyo hilo amelitoa wilayani Kibaha, wakati wa kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji, kabla ya kutembelea wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika wilaya hizo ili kujiridhisha na utekelezaji wake.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema, haiwezekani afisa huyo mwenye dhamana ya kusimamia Sheria, Kanuni na Taratibu za kiutumishi ndio awe kikwazo cha utendaji kazi katika Halmashauri hiyo kwa kutoa lugha chafu dhidi ya wanaofuta huduma ofisini kwake, na kuongeza kuwa, afisa huyo ndiye anayestahili kuwa kwenye Kamati ya Maadili ili kutoa miongozo ya uadilifu na kusimamia maadili ya watumishi kwa ujumla katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amemtaka afisa huyo kutotumia cheo chake vibaya na badala yake asimamie vema nidhamu na masilahi ya watumishi wa umma.
Sanjari na hilo, Mhe. Dkt. Mwanjelwa amemtaka afisa huyo kuacha tabia ya kutoa siri za ofisi na kutokuwa mchonganishi miongoni mwa watumishi wenzie kwani matendo hayo hayapaswi kufanywa na mtumishi yeyote nchini.

Aidha, Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema ameamua kuweka bayana  mapungufu ya afisa huyo mbele ya watumishi wenzie ili ajifunze kutokana na matendo yake yasiyoridhisha na aweze kubadili mwenendo wake mbaya wa kimaadili.
Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) ameendelea kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma nchini, kwa kutoa onyo kwa watumishi wote wanaobainika  kukiuka Kanuni za Maadili ya Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma.

MSAMA PROMOTIONS YATOA MSAADA WA VYAKULA VITUO SITA VYA YATIMA NA WASIOJIWEZA

0
0
Kuelekea Tamasha la Kihistoria la Pasaka kwa mwaka 2019, Kampuni ya Msama Promotions imetoa msaada katika vituo Sita vya Watoto wasiojiweza  ili kujikimu kimaisha.

Msama Promotions imetoa msaada huo kwenye vituo vya Sifa (Bunju), Zaidia (Sinza), Maunga (Mkwajuni), Honoratha (Temeke), Watoto Wetu Tanzania na Mwandaliwa (Boko).

Akizungumza na Waandishi wa Habari baaada ya kutoa msaada huo, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Alex Msama amesema Tamasha hilo linafanya kazi yake pamoja na kuisaidia jamii isiyojiweza.

"Kama kawaida yetu Kampuni ya Msama Promotions kujali Watoto Yatima, kuwasaidia kwa kiwasomesha kuwapa mambo mbalimbali ikiwemo Chakula na Malazi", amesema Msama.

Pia, Msama ametoa wito kwa Kampuni nyingine kuwasaidia Watoto hao wasiojiweza ili kujikimu kimaisha kama ilivyo kwa Watoto wengine waliokuwa na wazazi wao.

Tamasha hilo la Kihistoria linatarajiwa kufanyika April 21, 2019 katika jiji la Dar es Salaam ambapo linatarajiwa kuzunguka mikoa 10, likiwa na lengo la kuombea Taifa pamoja na Viongozi wake akiwemo Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama akijiandaa kugawa msaada wa vyakula katika vituo sita ambavyo ni Sifa (Bunju), Zaidia (Sinza), Maunga (Mkwajuni), Honoratha (Temeke), Watoto Wetu Tanzania pamoja na Mwandaliwa (Boko).
Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama akikabidhi msaada wa vyakula kwa baadhi ya vituo vya watoto wasiojiweza,Msama ametoa msaada huo kwa vituo sita ambavyo ni Sifa (Bunju), Zaidia (Sinza), Maunga (Mkwajuni), Honoratha (Temeke), Watoto Wetu Tanzania pamoja na Mwandaliwa (Boko).
Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari mara baada ya kutoa msaada kwa vituo sita vya jijini Dar,ikiwa ni sehemu ya fedha zilizokuwa zikipatikana katika tamasha la pasaka,ambalo hufanyika kila mwaka,likianzia jijini Dar na kuendelea katika mikoa zaidi ya 10
Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama akifurahia jambo na mmoja wa watoto mara baada ya  kutoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo vyakula  kwa vituo sita vya jijini Dar,ikiwa ni sehemu ya fedha zilizokuwa zikipatikana katika tamasha la pasaka,ambalo hufanyika kila mwaka,likianzia jijini Dar na kuendelea katika mikoa zaidi ya 10
Mara baada ya kutoa msaada wa vyakula na vitu mbalimbali,Mkurugenzi wa Kampuni  ya Msama Promotions , Alex Msama pia alipata wasaa wa kula chakula cha pamoja na baadhi ya watoto hao waishio katika mazingira magumu.

WASANII WAKONGWE WABWAGWA TUZO ZA SZIFF

0
0
  Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Tulia Akson Mwansasu akikabidhi tuzo ya Msanii Bora wa kike, Mtoto Kutoka Iringa aliyecheza Filamu ya Kesho
 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Tulia Akson Mwansasu akizungumza wakati wa ufunguzi usiku wa Tuzo za Sinema Zetu Film Festival zilizofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.
 Mseamaji wa Klabu ya Simba Haji Manara akikabidhi Tuzo kwa Muongozaji wa Filamu John Kallaghe
 Wema Sepetu akizungumza Jambo na Wadau wa Muziki waliofika katika tuzo hizo za Sinema zetu
 Baadhi ya Viongozi wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wakifuatilia Tuzo za Sinema Zetu zilizofanyika Mlimani City.
 Washehereshaji wa Tuzo hizo Baruani Muuza na Elizabeth Michael wakiwa jukwani wamependeza
 Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo akitoa neno kama Mlezi wa Tuzo hizo na kukaribisha msimu wa tatu
 Muigizaji Maarufu katika Sinema ya Sultan Shaazad Mustafa akiwasili katika ukumbi wa Mlimani City Mahali ambapo Tuzo za Sinema zetu zilifanyika.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AZUNGUMZA VIONGOZI WA CCM WETE PEMBA.

0
0

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mojhamed Shein, akizungumza na Viongozi wa CCM wa Wilaya ya Wete Pemba wakati wa mkutano wa majumuisho wa ziara yake katika Wilaya Wete uliofanyika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete Pemba.(Picha na Ikulu).

RAIS DK. SHEIN AWATAKA WAZAZI, WALEZI KUWEKA MAZINGIRA BORA KWA WATOTO KUPATA ELIMU

0
0

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiangalia moja ya meza mpya zilizoagiziwa kwa ajili ya matumizi ya Skuli za Sekondari na Msingi Zanzibar, baada ya kufungua madarasa manne ya Skuli ya Sekondari ya Mchanga Mdogo Wilaya ya Wete Pemba akiwa katika ziara yake kutembelea Miradi ya Maendeleo.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiangalia moja ya meza mpya zilizoagiziwa kwa ajili ya matumizi ya Skuli za Sekondari na Msingi Zanzibar, baada ya kufungua madarasa manne ya Skuli ya Sekondari ya Mchanga Mdogo Wilaya ya Wete Pemba akiwa katika ziara yake kutembelea Miradi ya Maendeleo.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akikata utepe kuashiria kufungua jengo jipya la Skuli ya Sekondari ya Mchanga Mdogo Wilaya ya Wete Pemba leo.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akiwasili katika viwanja vya Skuli ya Mchanga Mdogo akiwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Riziki Pembe Juma kushoto, wakielekea katika jengo ljipya la Madarasa ya Skuli ya Sekondari ya Mchanga Mdogo kwa ajili ya uwekaji jiwe la msingi, akiwa katika ziara yake Kisiwani Pemba.(Picha na Ikulu)
WANAFUNZI wa Skuli ya Sekondari na Msingi ya Mchanga Mdogo Wilaya ya Wete Pemba, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwahutubia wakati wa hafla ya ufunguzi wa Madarasa ya Skuli ya Sekondari Mchanga Mdogo Pemba.
WANANCHI wa Kijiji cha Mchanga Mdogo Wilaya ya Wete Pemba wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia baada ya hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi Skuli ya Sekondari ya Mchanga Mdogo Pemba.

WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Riziki Pembe Juma akihutubia kabla ya kumkaribisha mgeni rasmin kuwahutubia Wananchi wa Kijiji cha Mchanga Mdogo Wilaya ya Wete Pemba, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Jengo la Skuli ya Sekondari Mchanga Mdogo
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Madarasa Mapya ya Skuli ya Sekondari Mchanga Mdogo Wilaya ya Wete Pemba, akiwa katika ziara yake kutembelea Miradi ya Maendeleo Kisiwani Pemba.
WANAFUNZI wa Skuli ya Msingi Mchanga Mdogo Wilaya ya Wete Pemba wakiimba Wimbo wa Sisi Sote Tumengomboka wakati wa hafla ya ufunguzi wa majengo ya Skuli ya Sekondari Mchanga Mdogo Kisiwani Pemba leo.
 

……………………………………………………………………………………..
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wazazi na walezi kote nchini kuwasaidia na kuwatengenezea mazingira bora watoto wao ili waweze kusoma bila taabu.

Kwa nyakati tofauti, Dk. Shein amesema hayo leo wakati alipofungua jengo la madarasa manne katika skuli ya sekondari Mchangamdogo pamoja na kuweka jiwe la msingi la jengo la madarasa manne katika skuli ya msingi Bopwe, Wilaya ya Wete Pemba.

Huo ni muendelezo wa ziara zake za kukaguwa miradi mbali mbali ya maendeleo pamoja na utekelezaji wa Ilani ya CCM. Dk. Shein aliwataka wazazi an walezi kuepuka kuwatuma watoto kupita kiasi katika masuala yasio na mnasaba wa elimu, kwa msingi kuwa hayaendani na umri walionao, hususan katika suala zima la kujiendeleza kitaaluma.

Alisema wapo baadhi ya wazazi na walezi wanaowatumikisha vibaya watoto wao katika kazi za kujikimu kimaisha ikiwemo biashara, hivyo kuwatwisha mzigo usioendana na wakati wao. Aidha, aliwataka walimu kufanikisha dhana ya ulezi wa wanafunzi kwa kuwabidisha kitaaluma, sambamba na kuwataka kuondokana na vitendo vyote vya uharibifu dhidi ya wanafunzi, ikiwemo udhalilishaji wa kijinsia.

“Mwalimu na mwanafunzi ni mtu na mzee wake mnapaswa kujenga urafiki na sio uadui’, alisema. Vile vile Dk. Shein aliwataka walimu kufanyakazi zao kwa misingi ya taaluma ya ualimu pamoja na kuzingatia maadili ya kazi hiyo, akiweka wazi azma ya Serikali ya kuwachukulia hatua walimu wote watakaobainika kukiuka miongozo na sheria za kazi.

Katika hatua nyengine, Dk. Shein aliwataka wanafunzi kusoma kwa bidii na jitihada zote, akibainisha kutokuwepo kwa sababu zozote zile zitakazomfanya mwanafunzi kushindwa kusoma vizuri kutokana na mazingira bora yaliowekwa na Serikali.

Alisema Serikali itaendelea kuimarisha sekta ya elimu, kwa kukamilisha madarasa saba yanayohitajika katika skuli ya Sekondari Mchangamdogo ili kukidhia mahitaji ya wnaafunzi, sambamba na mahitaji ya skuli zote nchini, kw akuyapatia vifaa vya kufundishia pamoja na samani.

Dk. Shein alirudia kauli yake kwa kusema lengo la Serikali ni kuwajengea mazingira bora wanafunzi ili kuhakikisha inapata wataalamu katika fani zote, akibainisha kuwa wataalamu ndio chachu ya maendeleo ya taifa lolote Duniani.

Alisema Serikali ya awamu ya saba itaendelea kusimamia upatikanaji bora wa elimu bila malipo katika skuli za maandalizi, msingi na sekondari na kubainisha jukumu la Serikali la kuwaondolea dhima wazazi katika uchangiaji wa vifaa.

Dk. Shein aliwahakikishia wazazi na wanafunzi kuwa serikali itaendelea kutekeleza ahadi ya upatikanaji wa elimu na taaluma yenyewe kwa kuimarisha miundombinu na upatikanaji wa samani zote ili kuwawekea mazingira bora ya kielimu wanafunzi. Aidha, alisema pamoja na serikali kukosa uwezo wa kutosha wa kutoa elimu bure katika masomo ya Vyuo Vikuu, itaendleea kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wa elimu ya juu.

Nae, Waziri wa Nchi, (OR), Serikali za Mitaa, Tawala za Mikoa na Idara maalum za SMZ, Haji Omar Kheir, alisema Wizara yake itatimiza jukumu la kusimamia sekta ya elimu katika ngazi ya maandalizi na msingi, akibainisha madarasa manne ya Skuli ya msingi Bopwe (yaliowekewa jiwe la msingi) kuwa ni miongoni mwa madarasa 60 yalioendelezwa na Wizara hiyo kupitia mfumo wa Ugatuzi.

Aidha, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Riziki Pembe Juma aliipongeza Serikali katika kusimamia vyema sekta ya elimu pamoja na kuwajengea mazingira mazuri wanafunzi ya kupata elimu.

Mapema, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Madina Majaka , alisema ujenzi wa jengo la madarasa manne katika skuli ya Sekondari Mchangamdogo umegharimu zaidi ya shilingi Milioni 34.4, ambapo utapunguza mlundikano wa wanafunzi madarasani, akibainisha haja ya kupatikana madarasa mengine saba ili kuondokana kabisa na kadhia hiyo.

Aidha, Katibu Mkuu, Wizara nchi (OR), Serikali za mitaa, Tawala za Mikoa na Idara maalum za SMZ, Radhia Rashid alisema ujenzi wa jengo la madarasa manne katika skuli ya msingi Bopwe utagharimu shilingi Milioni 53.6 hadi utakapokamilika, fedha zinatokana na Bajeti ya serikali pamoja na michango ya wananchi.

WAKATI HUO HUO, RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein alisema Serikali imefanya kazi kubwa na ngumu katika kuliimarisha zao la karafuu na hatimae kuleta tija kwa wananchi, hususan wa kisiwa cha Pemba. Alisema bado zao hilo lina umuhimu mkubwa katika uchumi wa Zanzibar , na kusisitiza azma ya serikali katika kuliendleeza kibiashara.

Dk. Shein alisema hayo katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Wete, alipozungumza na Viongozi na wanachama wa CCM, pamoja na kupokea taarifa ya Utekelezaji wa kazi za Maendeleeo Wilaya Wete kwa kipindi cha Agosti 2017 hadi Disemba, 2018. Alisema amefurahishwa sana na hali ya amani na utulivu iliyopo katika Wilaya hiyo na Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa ujumla, hatua iliyotoa fursa kwa wananchi kufanya shughuli zao za maendeleo bila vikwazo.

Aidha, alilipongeza Baraza la Mji wa Wete kwa kukusanya vyema mapato hadi kufikia asilimia 96.6 ya malengo lililopangiwa. Sambamba na hilo Dk. Shein alisema ameridhishwa na hatua za Wilaya hiyo kusajili wanafunzi katika skuli za msingi na maandalizi, kwa kigezo kuwa huo ndio msingi bora wa elimu kuelekea ngazi za elimu ya sekondari.

Alisema changamoto za maji katika maeneo ya Uvinje na Kiuyu Mjini yatapatiwa ufumbuzi, na kuonya tabia ya ubinafsi iliopo kwa baadhi ya watendaji wa Mamlaka ya Maji (ZAWA), Wilayani humo inayodhoofisha upatikanaji wa huduma hiyo. Aidha, Dk. Shein akaukumbusha uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, kukamilisha ujenzi wa Chuo cha Amali Mtamwe ambapo ujenzi wake ulianza takriban miaka minane iliyopita, ukiwa umesita.

Mapema, Waziri wa Nchi (OR), Serikali za mitaa, Tawala za Mikoa na Idara maalum za SMZ, Haji Omar Kheir aliwataka wananchi wanaojishughulisha na biashara za magendo, ikiwemo ya zao la karafuu kuacha mara moja, akibainisha kuwa Serikali itachukuwa hatua za kisheria pamoja na kutaisha mali za wahusika.

Nae, Mkuu wa Wilaya ya Wete, Abeid Juma Ali, alisema miongoni mwa changamoto zilizoikabili Wilaya hiyo atika kipindi hicho ni pamoja na upungufu wa wafanyakazi katika sekta ya Afya, upungufu wa madarasa na walimu katika skuli za msingi na sekondari.

Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Viewing all 109573 articles
Browse latest View live




Latest Images