Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109602 articles
Browse latest View live

MPINA AREJESHA SERIKALINI MALI ZILIZOIBWA, ZAIDI YA BILIONI 118 ZA TAFICO NDANI YA MWEZI MOJA.

0
0

Waziri wa Mifugo naUvuvi Mh. Luhaga Joelson Mpina(mwenye mkasi) akikata utepe wa Ofisiya TAFICO katika uzinduzi rasmi wa ofisi na Menejimenti ya mpito ya kusimamia hatua za kufufua TAFICO Menejimenti hiyo ilizinduliwa  Julai 1/2018,anayefuata ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumuya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji, Mheshimiwa MahamoudMgimwa wa kwanza kuliani Kaimu Meneja Mkuu wa TAFICO Esther Mndeme. 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Joelson Mpina akitoa hotuba yake wakati wa uzinduzi rasmi wa ofisi na Menejimenti ya mpito ya kusimamia hatua za kufufuaTAFICOMenejimenti hiyo ilizinduliwa na tarehe 01/07/2018; kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji, Mheshimiwa MahamoudMgimwa. 


Ataka zilizo baki zisalimishwe kwa hiari haraka.
· Asisitiza kuendelea kuzisaka nchi nzima 

NA JOHN MAPEPELE, DODOMA

WIZARA ya Mifugo na Uvuvi imetaifish amali za Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) zenye thamani ya shbilioni 118 zilizokuwa zinamilikiwa nawat ukinyemela kisha kuzirejesha serikalini ikiwa ni miongoni mwa mikakati ya Serikali ya awamu ya tano ya kulifufua shirika hilo. 

Zoezi hilo limefanyika katika kipindi cha ndaniyasiku 30 

Pia Serikali inaendelea na uhakiki wa mali hizo popote zilizopo ambazo na zozote zitarejeshwa ili kuwezesha shirika hilo kuanza kazi baada ya menejimenti yake kuundwa mwishoni mwa mwaka jana. 

Akijibu hoja za wabunge kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Kamati ya Kudumu ya Bunge Kilimo, Mifugo na Maji bungeni mjini Dodoma, Waziri wa Mifugo naUvuvi, Luhaga Mpina Serikali ya awamu ya tano iko kwenye hatua za mwisho za kulifufuashirikahilo. 

Pia Serikali inajiandaa kununua meli mbili kubwa ambazo zifanya kazi ya uvuvi katika ukanda wa uchumi wa bahari kuu ilikukidhi matakwa ya wabunge ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakiitaka Serikali kuwekeza kwenye ukanda huo. 

AidhaWaziri MpinaalisematayariSerikaliya apanimeshaahidikutoashbilioni 4.3 kwaajiliyakufufuamiundombinuyaShirika la Uvuvi ikiwemomajokofuyakuhifadhisamaki, gari la barafu, melimojayauvuvinakujengagati la kuegeshameli za shirikahilo. 

“Kumekuwa na kilio cha wabunge cha miaka mingi kutakaSerikali iingie kwenye uvuvi wa bahari kuu,nataka kuwahakikishia Serikali ya awamu yatano tunaingia kuvua kwenye uvuvi wa bahari kuu na mipango iko vizuri”alisemaMpina 

Kuhusu ujenzi wa bandari yaUvuvi, Waziri Mpina alisema tayari mtaalamu mwelekezi anaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na kwamba mara baada ya kukamilika kazi hiyo ujenzi wa bandari ya uvuvi utaanza . 

Waziri Mpina amesisiti za kuwa mbali nakulifufua shirika la uvuvi, Serikali ya awamu ya tano inakwenda kufufua viwanda vya kuchakata mazao ya mifugo nakujenga vingine vipya katika maeneo mbalimbali nchini. 

“Hivi sasa ujenzi wakiwanda kikubwa cha kuchakata mazao ya mifugo kinakwenda kujengwa eneo la Ruvu ambacho kitakuwa na machinjio ,kitasindikanyama, kitasindikangozi, kitasindika mazao ya ngozi ukiingiza mfugo unatokana kiatu”alisemaMpina 

Alisema, tayariWizaraimefanyamkutanotarehe 5/2/2019 naujumbewa Waziri waKilimona Ardhi waMisriMheshimiwa, DktEzzidine Abu Stiet, ulioongozwanaBaloziwaMisrinchiniMheshimiwa, Mohammed Gaber Abdulwafa. 

“Tumekubaliana kuwa, utiaji wa saini mkataba huo utafanyika tarehe 24/2/2019 hapa nchini. Baina ya Kampuni ya Ranchi za Taifa(NARCO) kwa upande wa Tanzania na Kampuni ya Uwekezaji kwa Nchi za Afrika ya nchini Misri ijulikanayo kama “The National Egyptian Company for Africa Investment” (NECAI) kwa niaba ya Serikali ya Misri” alisisitiza 

Pia Serikali itaanza ujenzi wa mnada wa kimataifa wa mifugo Ruvu na kwamba tayari wamekutanana Waziri waMifugo wa Misri kukubaliana ujenzi wa kiwanda hicho uanze Machi mwaka huu. 

Vile vile viwanda vingine vya kuchakat amazao ya mifugo vinajengwa Longido, Tan Choice Kibaha chenye uwezo wa kuchinja ngombe zaidi 1,000 na mbuzi 4,000 nakiko kwenye hatua ya mwisho kukamilishwa huku Kampuniya KOMU ya Kahama nayo ikiwa kwenye hatua za mwisho za kuanza ujenzi wa kiwandaChato 

Hivyo Serikali ya awamu ya tano iko kazini matatizo ya wananchi kukosa soko la mifugo sasa yamefika mwisho kwani wafugaji wengi watapata masoko ya uhakika ya mifugo yao hapanchini. 

Kuhusu huduma za mifugo, Waziri Mpina alisema zoezi la uogeshaji wa mifugo ambao lilisimam akwa muda mrefu lakini kwasasa Serikali ya awamu ya tano inaogesha mifugo kila kona ya nchi na tayari wizara imegawa dawa kwenye majosho yote 1, 409 yanayo fanyakazi na kwamba wizara itaendelea kutoa dawa kwa ajili ya uogeshaji. 

Alisema wafugaji walikuwa wanateswa kuogesha ng’ombe mmoja sh 2,000 lakini sasa hivi watakuwa wanachangia gharama ndogo kwa kila ng’ombe sh 50 tu.Kuhusu operesheni za kulindarasilimali za mifugo na uvuvi, Waziri Mpina alisema wabunge wameishauri Serikali kuhusu uwekezaji wa viwanda lakini Serikali inawajibu wa kuwalinda wawekezaji wa ndani. 

“Tunazungumza uwekezaji, leo hivin ania nayeweza kuja kwenye uwekezaji kwenye nchi ambayo haiwezi kulinda rasilimali zake, na ni atakayejenga kiwanda hapa cha kusindika samaki wakati samakiwote wanatoroshwa kwenda nje ya nchi bila hata kufuatautaratibu unaokubalika ninani”alihoji Waziri Mpina, 

“Nani leo atakayekubali kuwekeza kuzalisha vifaranga, kuku, ngombe wa maziwa katika nchi ambayo maziwa yanatoka nje ya nchi hayana vibali hayajalipi wa kodi yoyote, hayajapimwa ubora na ya nauzwa na yanashindana na viwanda vya ndani nani atakayejenga viwanda hapanchini”alihoji. 

Pia Waziri Mpina alisema na nia takayejenga viwanda katika nchi ambayo inaruhusu mpaka vituv ilivyoishamuda wa matumizi kuuzwa nchini na kushindana na wazalishaji wa ndani na nia takubali. 

“lazima tukubali doria zinazoendelea zinalenga kuwalinda wazalishaji wandani ili waweze kuzalisha vizuri leo nenda kawaulize wazalishaji wa viwanda vya maziwa wa meamua kuongeza uzalishaji kwasababu kuna ulinzi madhubuti hakuna mtu ataingiza kimzahamzaha maziwa kutoka nje ya nchi”alisema Mpina. 

Aidha Waziri Mpina alisema katika vitu ambavyo alivichukia kuliko vyote miaka ya nyuma niwatukuleta vitu vilivyokwisha muda wamatumizi ambao wamepita njia za panya alafu waziri mhusika anakuja bunge ninayeye analalamika juu ya mambo hayo. 

“Wakatiyeyendioanauwezowakuwashika, sisi tutawashika na hatutakubali kuruguza wawekezaji wetu hapa nchini”alisema. Hivyo aliwaomba wabunge kuunga mkono juhudi za Serikali za kulinda rasilimali hizo kwa ajili ya manufaa ya wananchi wote kwani rasilimali hizo zikitoweka hata wao hawawezi kunufaika. 

“Nani anaye wahurumia wavuvi ni mtu ambaye anaruhusu watu wakavue kwa nyavu haramu alafu baadae mvuvi anaenda kuvua kwa gharama kubwa anarudi bila samaki au ni yule anayelinda mwisho wavuvi wa kienda kuvua wakarudi na samaki wengi ili wawe matajiri nani anayewatetea wavuvi na huo ndio msingi hasa doria hizo”alisemaMpina. 

EDWIN MTEI: "GENIUS" ALIYEZALIWA KIMAAJABU KWENYE MASHAMBA YA MAHINDI NA MAHARAGE!!!

0
0
1. Usuli:

1.1 Mama MTEI azaa na Binamu wa Mume wake:

Bi.NGIANAELI NGEKALIO, mama yake EDWIN MTEI,  alikuwa ameolewa na Bw. VICTOR SHAMBARI MTEI ambaye alifariki mwaka 1928. Bw. VICTOR alikuwa akiishi jirani kabisa na binamu yake aliyeitwa Bw. ELIAPENDA NGAPANYI MTEI. Baada ya Bw. VICTOR kufariki, Bw. ELIAPENDA akawa akifika mara kwa mara nyumbani kwa mama yake MTEI kumfariji na kumsaidia kazi mbalimbali kwani aliachwa na watoto 2. Matokeo ya ziara hizo za kumfariji ni mama huyo kupata ujauzito!.

1.2 Kuzaliwa kwa EDWIN MTEI:

EDWIN MTEI alizaliwa asubuhi ya siku ya Jumanne, tarehe 12.7.1932 baba yake akiwa ni Bw. ELIAPENDA NGAPANYI MTEI. Siku hiyo, mama yake akiwa mja mzito na akiwa na rafiki na jirani yake, Bi. NDEAMBILIASIA, waliamka asubuhi sana na kwenda eneo la Rawuya kwenye shamba la mahindi na maharage lililokuwa kilometa 8 toka Marangu. Baadae asubuhi hiyo, Bi. NGIANAELI akajifungua mtoto EDWIN na mchana akarejea kibabe nyumbani huku baby MTEI akiwa amebebwa na Bi. NDEAMBILIASIA. Wanawake enzi hizo hawakuwa mayai, walikuwa ngang'ari kinoma!.

1.3 "Baba yake "Kuuchuna"

Bw. ELIAPENDA NGAPANYI MTEI, baba yake, hakutaka kabisa ijulikane kuwa dogo EDWIN ni mwanae kwani mwanzoni mwa mwaka huo, 1932, alikuwa amefunga ndoa na Bi. LUCY MAWOLLE. Vivyo hivyo, mama yake nae alifanya siri sana na hakupenda watu wajue kuwa EDWIN ni mtoto wa Bw. ELIAPENDA NGAPANYI MTEI, ingawa "mzee baba huyo" huyo alikuwa akipeleka matunzo.

2. Elimu:

2.1 Elimu ya Vidudu/Msingi:
MTEI alisoma "shule ya vidudu" Ngaruma Lutheran Church, 1941 akiwa na miaka nane. MTEI alikuwa akitoka shule anakwenda kuchunga mbuzi na maisha yao yalikuwa ya kubangaiza na ya kifukara sana huku wakiishi kwenye nyumba ya majani. Mwaka 1943, MTEI alihamia Marangu Native Authority Primary School ambako alisoma na WILBERT KLERUU aliyekuwa anatoka umbali wa 10 Kms kwenda na kurudi kila siku. Bw. KLERUU alikuwa ni mwenye kiu kubwa ya elimu. Baadae akawa mmoja wa watanganyika wa mwanzo kuwa na PHD na akawa RC Mtwara na Iringa, kabla ya Mnyalukolo SAID MWAMWINDI kufanya yake tarehe 25.12.1971.

2.2 MTEI "Apasua pepa" Darasa la 4;

MTEI alifanya mtihani STD IV Exams for Nothern Province mwaka 1944. Matokeo yalitangazwa na Headmaster mzungu, G.W. GINNER wa Old Moshi Sec. School  Januari, 1945. MTEI akashika namba moja na hivyo kuitwa kujiunga na Old Moshi. 

Tarehe 31.1.1945, MTEI akafika shuleni hapo na kupokelewa na Mwalimu ERASTO MANG'ENYA aliyekuja kuwa Waziri na Spika wa Bunge. Shuleni hapo alisoma na Bw. CLEOPA MSUYA, aliyekuja kuwa PM na Bw. HERMAN SERWATT, mbunge pekee aliyekuja kuishinda TANU, DANIEL MFINANGA aliyekuja kuwa Balozi, Bw. SOLOMON ELIUFOO na Bw. ISRAEL ELINAWINGA waliokuja kuwa Mawaziri na WILBERT KLERUU.

Mwaka 1946 kulikuwa na mtihani wa taifa wa STD VI kwa nchi nzima ili kwenda STD VII. Kwavile MTEI alifiwa na baba yake Mei 1945, ambaye alikuwa akimsaidia kulipa karo, ikawa kimbembe! Hata hivyo, kwavile MTEI alikuwa "amepasua pepa", ikabidi Headmaster amnusuru na kufanya kitu kisicho cha kawaida kwa kuwaandikia Machifu wa Kichaga!.

Mwezi Octoba 1950, MTEI alifanya "STD X Territorial Exams" na kufaulu vizuri sana na akachaguliwa kujiunga na Tabora Boyz Sec School. Januari 1951 'akakwea gogo" kwenda shule yake mpya ambako alipokelewa na Headmaster JOHN CRABBE, na akakutana na wanafunzi wengine akina GEOFREY MMARI, aliyekuja kuwa Vice Chancellor, Udsm, OSCAR KAMBONA na JOB LUSINDE waliokuja kuwa Mawaziri na MARK BOMANI aliyekuja kuwa AG.

2.3 MTEI "Apasua pepa" Darasani 1952 & 1953 Tabora Boyz

MTEI alikuwa si mtu wa spoti-spoti kwani kwa miaka miwili mfululizo akiwa shuleni hapo, 1952 na 1953, alishika nafasi ya 1 darasani licha ya kusoma na utitiri wa "Vipanga!.

2.4 MTEI "Kipanga" wa "debates"

MTEI, licha ya "kuwatimulia vumbi" wenzake darasani, alikuwa ni "kiboko wa kutema yai" na "mkali wa debates" shuleni hapo. Hii ilipelekea mwishoni mwa 1952, Headmaster J. CRABBE aandike "EDWIN MTEI is an Excellent debator" .

2.5 MTEI "Kipanga" nchi nzima (TANGANYIKA ONE)

Mwezi Octoba 1952, MTEI akafanya mtihani wa Cambridge Overseas School Certificate Exams. Huu ulikuwa ni mtihani kwa wanafunzi wa Tanganyika, Kenya na Uganda. MTEI 'aliipasua pepa' hii kwa si tu kupata ufaulu wa Daraja la Kwanza, bali pia yeye ndiye alikuwa Mwanafunzi Bora Tanganyika!. Hivyo akachaguliwa kwenda kusoma chuo kikuu cha Makerere, Uganda ambako alikutana na watanganyika wengine akiwapo PAUL SOZIGWA.

2.6 MTEI Ashinda Insha ya History Makerere

MTEI aliendelea na moto wake ambapo mwaka 1956, kulikuwa na History Essay competition iliyojumuisha nchi nyingi ambapo MTEI aliibuka mshindi na kupewa kabati lililojaa vitabu vyenye thamani ya £200.

Mwaka 1957, MTEI alifanya mtihani wa mwisho kumaliza chuo na kufaulu vizuri na kukabiziwa shahada na kisha akarejea nchini.

3. MTEI Akutana na Mwalimu NYERERE kwa mara ya kwanza

MTEI alikutana na Mwalimu NYERERE jijini Dsm kwa mara ya 1 mwaka 1959 baada ya kupelekwa na rafiki yake, MWANJISI. Mwalimu alimwambia MTEI kuwa ipo siku wakoloni wataondoka na Watanganyika watajitawala wenyewe.

4. MTEI Aenda kufanya kazi KENYA:

Baada ya kuona Bongo hamna dili kwani serikali ya kikoloni haikumpa kazi yoyote akaamua "kuishia" zake Kenya.

5. Mwalimu NYERERE Amteua MTEI Katibu Mkuu Fedha:

Mwezi Agost 1964, Mwalimu alimteua MTEI kuwa Katibu Mkuu Wizara ya fedha. Mh. MTEI akafanya jambo la kizalendo kwa kuhakikisha kampuni ya kizalendo ya MECCO inapewa kandarasi ya kujenga Benki Kuu ya TZ.

6. Mwalimu amteua MTEI kuwa Gavana-Mteule

Mwanzoni mwa 1965, nchi za TZ, KN & UG zilikubaliana kila nchi itoke kivyake kwani hakukuwa na dalili ya kuwa na Federation.  Mwalimu akamteua MTEI kuwa Gavana-mteule mwezi Octoba 1965. Majukumu yake makubwa yalikuwa kutayarisha fedha ya TZ, kushughulikia sheria ya kuundwa Benki Kuu, kuajiri "experts" na kuandaa mafunzo mujarab ya wafanyakazi wazalendo. Baadaye, Mwalimu akamteua Mh. MTEI kuwa Gavana wa BOT.

7. Mh. MTEI Awaibua BALALI na YONA:

Mh. MTEI akiwa Gavana mdogo kuliko wote katika historia ya TZ(34) aliibukia US alikomkuta Bw. DAUDI BALALI akisoma chuo kikuu cha Howard. MTEI alivutiwa sana na uwezo mkubwa wa BALALI na akamshauri asomee masomo yanayoendana na BOT. Baada ya kumaliza chuo, Mh. MTEI akamwajiri BALALI BOT na akawa kijana hodari sana. Mh. MTEI pia alimuibua DANIEL YONA na kumuajiri pia. Baadaye, Mwalimu alimchukua YONA ili kwenda kuongoza benki ya THB baada ya Mh. MTEI kumsifia sana.

8. Mwalimu NYERERE Ajipunguzia mshahara, Gavana MTEI Afuata Nyayo:

Mwalimu aliamua kujipunguzia mshahara wake wa Buku-Tano hadi Buku-Nne Jero_ kwani kulikuwa na kutofauti kubwa. Mh. MTEI, ambaye yeye na Mwalimu tu ndio walikuwa wakilipwa pesa ndefu, alifanya uzalendo wa hali ya juu sana kwa kuamua nae kujipunguzia. Mh. MTEI angekuwa kama viongozi wengi wa sasa wanaojali matumbo yao tu, asingejipunguzia kwani Mkataba wake ulikuwa na kipengele mahsusi kuwa hakuna mamlaka yoyote iwezayo kumpunguzia.

Hii ikapelekea mishahara ya viongozi wengine nayo kupunguzwa.

9. Mwalimu amteua Mh. MTEI kuwa Katibu Mkuu wa EAC

Mwalimu alimteua Mh. MTEI kuwa Katibu Mkuu wa EAC mwaka 1975 ambapo alihudumu kwa miaka 2 hadi 1977.

10. Mwalimu NYERERE Amteua Mh. MTEI kuwa Waziri wa Fedha:

Mwalimu alimteua Mh. MTEI kuwa Waziri wa Fedha mwezi Februari 1977.

11. Mh. MTEI Aenda US, apewa masharti chechefu na IMF

Mh. MTEI alikwenda US kutafuta misaada. Hii ilikuwa baada ya hali kuwa ngumu kwani katika vita ya Kagera tulikuwa tukitumia $ 500,000 kwa siku kwa mwaka mzima. Mh.MTEI akapewa masharti na IMF ya kushusha thamani ya shilingi na kurekebisha mashirika hoehae ya umma, na aliporejea Mwalimu akayakataa masharti hayo ya IMF.

12. Mh. MTEI Aupeleka Ujumbe wa IMF Msasani:

Tarehe 29.11.1979, Mh. MTEI aliupeleka Msasani ujumbe wa IMF uliokuwa ukiongozwa na Bw. BO KARLSTROM ili "kumkata shule" Mwalimu.

Ujumbe huo, ukiwa Msasani, ulimwaga mwembwe zake ukiamini umekonga moyo wa Mwalimu. 

13. Mwalimu "Ajikata",  Auacha Solemba Ujumbe wa IMF

Mwalimu alipoona Watasha hao wanaongea "vepa" tupu, "alijifanya kama anajikuna" kisha, ghafla bin vuu, bila kuaga, akaenda nje nyuma ya nyumba karibu na baharini yaani bichi, akawa anapunga upepo na kuwaacha Watasha seblen!.

14. Mh. MTEI Amuibukia Mwalimu Bichi:

Mh. MTEI akaona Kama Mbwai, Mbwai tu hivyo akamfuata Mwalimu hukohuko bichi na kumuomba arudi. Mwalimu, akiwa amefura kwa hasira, akamwambia Mh. MTEI kuwa hawezi kuacha nchi yake ikiongozwe toka Washington. Mwalimu alisema- "Mimi nikikataa kitu msimamo wangu unabaki pale pale, sitaki nigeuke Mnara wa chumvi. Waambie hao jamaa zangu warudi makwao kwani nimewasikia ila sikubaliani nao".

Mh. MTEI alijaribu kumsihi Mwalimu arudi seblen japo awaage wageni ili kuwaonesha ukarimu wa Watanzania lakini Mwalimu hakutaka kuona pua wala sikio la mtu yeyote wa IMF!. Hivyo, Mh. MTEI kwa unyoonge akarudi seblen na kisha 'akajikata" na ujumbe wake.

15. MH. MTEI Akimbilia Ofisini na Kuandika Barua ya Kujiuzulu

Mh. MTEI alikuwa amekasirishwa mno, hivyo akatoka nduki na gari yake hadi Wizarani. Alipofika tu huku akitweta, akaandika kwa mkono barua ya kujiuzulu na kuiweka juu ya meza ili J3, Katibu Muhtasi akija aichape.

16. Mh. MTEI AMPA "UBUYU" Mh. MALECELA

Mh. MTEI, baada ya kuandika barua hiyo, aliamua kuwasiliana na Waziri wa Kilimo, Mh. JOHN MALECELA, juu ya dhamira yake hiyo ambapo Mh. MALECELA alistuka sana!. Mh. MALECELA akamweleza kuwa mmiliki wa Tanganyika Plantation Company anataka kuiuzia Govt kiwanda hicho kwa bei ya ubwete ila alipwe fasta.

Mh. MTEI alimjibu Mh. MALECELA kuwa jambo hilo haliwezekani kwani nchi imefulia vibaya sana na kwamba aliishaliongelea hilo na Gavana CHARLES NYIRABU kiisha wakaagana, kila mmoja "akasepa" kivyake.

Baadae kidogo, Mh. MTEI alipigiwa simu na Mh. MALECELA kwamba wote 2 wanaitwa na Mwalimu Msasani hivyo wakaenda.

Mh. MALECELA alitaka kiwanda hicho kinunuliwe akiungwa mkono na Mwalimu, huku MTEI akisisitiza kuwa nchi haina mbumba za kigeni.

Kikao kilipoisha, hasira ya Mh. MTEI ilikuwa ipo juu mno hivyo akakimbiza gari kwenda ofisini kwake kwa mwendo ambao hata Michael Schumacher angesubiri! Akaichukua ile barua aliyoandika kwa mkono akatoka nayo ofisini.

17. Mwalimu Amtumbua Mh. MTEI:

Mh. MTEI, alipomaliza tu kushuka ngazi za Wizara ya fedha, akakutana na Bw. BATHAO ambaye alikuwa msaidizi wa Mwalimu ambaye alimkabidhi barua toka kwa Mwalimu. Mh. MTEI, bila kuisoma, akaichukua na kuiweka ndani ya gari kisha akasaini Dispatch book na kuelekea Msasani.

18. Mh. MTEI Ajiuzulu, Mwalimu Amkubalia:

Mh. MTEI alimkabidhi Mwalimu barua ya kujiuzulu na Mwalimu akaisoma kwa makini na utulivu kisha akamuuliza kama alikuwa ameisoma barua yake. Mh. MTEI alikiri aliipokea lakini hakuisoma kutokana na uharaka wa kwenda kumuona. Mwalimu akamkubalia Mh. MTEI kujiuzulu.

19. Mwalimu Amwagiza Bw. SOZIGWA Kuutangazia Umma

Mwalimu alimuagiza Bw. PAUL SOZIGWA, Katibu wake, kuwa amekubali kujiuzulu kwa Mh. MTEI hivyo umma utaarifiwe hivyo.

Mwalimu na Mh. MTEI wakaagana vizuri kwa kukumbatiana.

Bw. SOZIGWA akaandika barua fupi kisha akaipeleka Shihata, Upanga na umma ukatangaziwa.

Bendi ya Kimulimuli ya Mafinga ikatunga wimbo wa kumpongeza Mwalimu - Tumekataa kuyumbishwa na Mataifa Makubwa.

Baada ya wiki kadhaa  Mwalimu akatangaza miezi 18 ya kujifunga mikanda.

20. Mh. MTEI Auza nyumba, Aenda Kuishi Tengeru;

Baada ya kujiuzulu, Mh. MTEI aliona "togwa limeingia nzi hapa mjini" hivyo akauza jumba lake na kununua shamba kubwa Tengeru, nje kidogo ya Arusha na kuhamia huko.

21. Mwalimu Ampa Ulaji Mh. MTEI "Mamtoni"

Miaka 3 baada ya kujiuzulu, Mwalimu alimteua Mh. MTEI kuwa "Executive Director" wa IMF Africa, US, akiziwakilisha nchi za Afrika zinazotwanga un'gen'ge. Mh. MTEI, naada ya kuifanya kazi hiyo kwa welefi akizunguka dunia nzima, hatimaye akarejea nchini mwishoni mwa 1986.

22. Rais MWINYI Amteua MSUYA Waziri wa Fedha

Rais ALI HASSAN MWINYI aliyechukua uongozi baada ya Mwalimu, mwaka 1986 alimteua Mh. CLEOPA DAVID MSUYA kuwa Waziri wa Fedha na akaruhusu soko huria na kulegeza masharti mengi ya biashara.

23. Mh. MSUYA Aenda Mamtoni Apewa Masharti ya IMF:

Mh. MSUYA "alitia timu" Washington kujadiliana na IMF na kukubaliana na masharti yao kisha akarejea nchini. Kisha tarehe 10.6.1986, Mh. MSUYA aliongoza ujumbe mzito wa mkutano wa siku 2 Paris akiwa pamoja na Mh. PAUL BOMANI, Waziri wa Kilimo,  Gavana CHARLES NYIRABU na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Mh. GILMAN RUTIHINDA.

24. Mh. MWINYI Aitisha "Cabinet" Kujadili Masharti ya IMF:

Mh. MWINYI aliitisha kikao cha Baraza la Mawaziri kujadili masharti ya IMF. Katika kikao hicho, Mh. MSUYA alieleza makubaliano yake na IMF na Baraza likaafiki kwa kauli moja na kumuelekeza Mh. MSUYA akaandae bajeti itakayoendana na makubaliano hayo.


25. Mh. MWINYI Akosa Usingizi, "Amtwangia" simu Mh. MSUYA:

Siku 3 baadae "machale yakamcheza" Mh. MWINYI hivyo akampigia simu Mh. MSUYA na kumueleza; "Sijapata usingizi kabisa toka juzi kutokana na haya makubaliano uliyokuja nayo, je tunaweza kukutana tena tukayajadili upya katika Baraza la Mawaziri?"

26. Mh. MSUYA Amchimba Mkwara Mh. MWINYI kuwa Atajiuzulu kama Mh. MTEI:

Mh. MSUYA alikubaliana na Rais MWINYI na hivyo siku moja kabla Bajeti kusomwa, 18.6.1986, Rais MWINYI aliitisha "Cabinet meeting".

Mh. MSUYA, bila kupepesa macho, kutikisa pua wala maskio, akatiririka "Mh. Rais, kama kuna hata mmoja katika Baraza hili la Mawaziri ambaye hatakubaliana na bajeti hii niliyoiandaa kutokana na masharti tuliyokubaliana na IMF, basi NITAJIUZULU ili uteue Waziri mwingine wa Fedha unaemtaka".

Rais MWINYI alieleza kwamba Mawaziri wote waongee kwa ukweli toka mioyoni mwao na kila mmoja aseme kama anakubaliana na masharti hayo.

Kila Waziri alieleza msimamo wake ambapo Mawaziri wengi walikubaliana na masharti hayo isipokuwa wachache akiwemo Waziri wa viwanda kwani wakati huo kulikuwa na "songombingo la kufa mtu" la maandamano nchini Jamaika na Moroko kupinga masharti ya IMF hivyo kuhofia yangefika Bongo. Mh. MWINYI "alimpiga shule" Waziri huyo kuwa viwanda vichache vilivyosalia vilikuwa vikifanya kazi kwa 25% tu na hivyo vilikuwa hatarini kufungwa. Hivyo, Baraza la Mawaziri likapitisha kwa mara nyingine masharti hayo. Kesho  yake, alhamis, tarehe 19.6.1986, bajeti ikasomwa.

Tarehe 25.6.1986 wakati wa kujibu maswali ya wabunge waliohoji kuhusu kubadili msimamo wa Mwalimu kuhusu IMF, Mh. MSUYA, kwa weledi wa hali ya juu, alidadavua : "Hatuna adui wa kudumu bali tuna maslahi ya kudumu ya Watanzania. Tumewahi kuvunja uhusiano na nchi moja na baadae tukarejesha".

Hatimaye, thamani ya shilingi ikapunguzwa toka $1= TZS 17/= hadi $ 1= TZS 40/= (25%).

27. Prof. MBILINYI Aeleza Mwalimu Hakuambilika kuhusu IMF:

Prof. SIMON MBILINYI, aliyekuwa mshauri wa Mwalimu ameeleza kuwa ilikuwa vigumu kumbadili Mwalimu kuhusu msimamo wa kushusha thamani ya shilingi kwakuwa alikuwa hakubaliani kabisa na IMF & WB. Prof. MBILINYI anaeleza - "Bosi alikuwa akitaka ushauri kutoka kwetu, lakini ukitoa ushauri unaoendana na WB au IMF atakujibu "toka hapa"!


28. Prof. MBILINYI Aelezea Tofauti ya Mwalimu na MWINYI Kuhusu IMF

Prof. MBILINYI aliyekuwa pia mshauri wa Mh. MWINYI ameeleza: "Ilikuwa vigumu kumshauri Mwalimu kwakuwa alikuwa na msimamo thabiti kuhusu IMF, lakini ilikuwa kazi nyepesi kidogo kwa Rais MWINYI. Rais MWINYI alikuwa na fikra huria, ilikuwa rahisi kwetu kubuni sera kwani alikuwa huru kuchanganya kanuni za Kijamaa na Kibepari ili mradi nchi isonge mbele".

29. Rais MWINYI Ampa Mh. MTEI Ulaji:

Rais MWINYI, kwa kutambua uwezo mkubwa alionao Mh. MTEI, alimteua kwenye "Boards & Commissions" nyingi ambako alitoa mchango mkubwa.

30. Mh. MTEI Aaanzisha CHADEMA, 1992

Mh. MTEI, mwezi Julai 1992, alianzisha CHADEMA, chama kikuu cha upinzani nchini ambapo alienda Butiama na kumuonesha Mwalimu Katiba ya chama hicho ambapo Mwalimu aliisifia.

Huyu ndiye "Kipanga" EDWIN MTEI, mzalendo aliyetoa mchango mkubwa kwa taifa lake.

Tafakuri Tunduizi:

 Je, Mh. MTEI alikosea kuhusu masharti ya IMF mwaka 1979?


LONGIDO YAENDESHA MSAKO WA KUWAKAMATA WAZAZI WASIOWAPELEKA WATOTO SHULE

0
0

Mkuu wa wilaya ya Longido Frank Mwaisumbe akiongea na wadau wa elimu wilayani humo kwenye kilele cha siku ya Taaluma iliyofanyika kiwilaya kwenye ukumbi wa halmashauri jana picha na Mahmoud Ahmad Longido
Waalimu na wadau mbalimbali wa elimu wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi mkuu wa wilaya hiyo Frank Mwaisumbe mwenye shati jeusi katikati wakati akitoa hotuba yake kwenye sherehe za siku ya Taaluma kiwilaya jana wilayani Longido picha na Mahmoud Ahmad Longido
Katibu tawala akimkaribisha mkuu wa wilaya hiyo kuongea na wadau wa elimu kwenye maadhimisho ya siku ya taaluma jana wilayani Longido picha na Mahmoud Ahmad Longido


Na Ahmed Mahmoud Longido

Wilaya ya Longido imejipanga kuendesha Msako wa kuwakamata wazazi ambao hawajawaandikisha watoto wao shuleni kwani kwa kufanya hivyo wanavunja sheria ya elimu na sheria ya watoto kutokana na idadi ndogo ya watoto wanaoandikishwa katika shule mbalimbali jambo ambalo linawasukuma kufanya msako huo.

Mkuu wa Wilaya ya Longido Frank James akizungumza katika Maadhimisho ya Wiki ya Elimu ,amesema kuwa msako huo ambao utafanyika majumbani na iwapo watabaini kuna wanafunzi hawajaandikishwa watawachukulia hatua ikiwemo kuwakamata na kuwafungulia mashtaka kwa kuwanyima watoto haki ya kupata elimu.

Aidha amesema kuwa msako huo utahusisha maeneo ya malisho kwani wafugaji wengi hawapendi kuwaandikisha watoto ili waweze kuwatumia watoto kuchunga mifugo yao badala ya kwenda shule jambo ambalo serikali haitalifumbia macho.

Ametanabaisha kuwa uwepo wa asilimia ambazo wilaya ilijiwekea hauwiani na watoto walioandikishwa kuingia Darasani wilayani huo ambapo 56 asilimia pekee ndio walioandikishwa kuingia darasa la kwanza ambapo wa kidato cha kwanza ni asilimia 32 hii imetufanya kuanza kwa msako wa nyumba kwa nyumba na atakayebainika kuwaficha watoto tutamchukulia hatua kali.

“Niwaombe wadau wa elimu na wazazi kuwapeleka watoto shule kabla msako haujaanza rasmi tena kwa hiyari yao kwani tukimkuta motto anachunga mifugo yeye na mifugo yake tutawakamata na mzazi au mlezi hatua kali tutachukuwa kwa hili hatutamvumilia yeyote” alisisitiza Mwaisumbe

Afisa Elimu shule ya Msingi Wilaya ya Longido Natang`aduaki Mollel amesema kuwa wilaya hiyo imefanya vizuri katika mitihani ya kitaifa licha ya changamoto ya utoro,ndoa za utotoni na umbali mrefu wa kufika mashuleni hivyo wataweka mikakati thabiti kuhakikisha kuwa wanafanya vizuri kila mara.

Amesema kuwa mikakati ya wilaya hiyo ni kuondokana na mapungufu mbali mbali yanayoikabili jamii kupata elimu kwa kushirikiana na wazazi na walezi kuhakikisha elimu wilayani humo inapewa kipaumbele cha kwanza ikiwemo kuwapeleka watoto shule na waalimu kutimiza wajibu wao ili kuipaisha wilaya hiyo.

Niwasihi sana wazazi na walezi kushirikiana kwa pamoja kuhakikisha elimu wilayani hapa inazidi kupaa na kushika nafasi za juu tusione tumefanikiwa bado ni safari ndefu ya kufikia mafanikio tunaohitaji ni ushirikiano pekee na kutimiza wajibu ndio vitatufanya kufanikiwa”alisema Mollel

Kwa upande wao Walimu Ephata Mwalimu Mkuu shule ya msingi Longido..na Sabato Petro Mkuu wa Shule ya Sekondari Ngarnaibor waliotoka katika shule za Msingi na sekondari zilizofanya vizuri wamesema kuwa ushirikiano mzuri kati ya wazazi,walimu na Viongozi wa kiserikali umesaidia kuleta tija na kuwafanya watoto wasome kwa bidii

WALIOFAULU KIDATO CHA NNE STONE TOWN INTERNALINAL SCHOOL ZANZIBAR WATAKIWA KUONGEZA JUHUDI

0
0

Katibu Tawala Mkoa Mjini Magharibi Hamida Mussa Khamis akimkabidhi cheti mwanafunzi Rahma Juma Juma mmoja kati ya wanafunzi wawili waliopata daraja la kwanza Skuli ya Stone Town International.
Mwanafunzi Asia Juma Ali (kushoto) na Nathania Sleiman wakighani utenzi kwenye sherehe ya mahafali yakuwapongeza wanafunzi wa kitado cha nne waliomaliza Stone Town International School iliopo Kilimani Mjini Zanzibar mwaka jana.
Mkurugenzi wa Stone Town International School Bi. Jamila Gulam Hussen akisoma hutuba katika mahafali ya kidato cha nne yaliyofanyika skulini kwao Kilimani Mjini Zanzibar.
Mjumbe wa Bodi ya Ushauri Tasisi ya Elimu Zanzibar Charles Lubega akielezea umuhimu wa elimu katika mahafali ya Stone Town International School pamoja na kumkaribisha mgeni rasmi kuwahutubia wahitimu wa kidato cha nne na wanafuzi wanaoendelea na masomo.
Mgeni rasmi Katibu Tawala Mkoa Mjini Magharibi Hamida Mussa Khamis akizungumza na wazazi na wanafunzi wa Stone Town International School ya Kilimani katika mahafali ya kidato cha nne ya skuli hiyo.
Wahitimu wa Kidato cha Nne wa Stone Town International School wakiwa katika mahafali yao yaliowashirikisha pia wanafunzi wa darasa la sita yaliyofanyika skulini kwao Kilimani.Picha na Makame Mshenga.

Tembo mzee zaidi duniani afariki dunia

0
0

Dakshayani, anayefikiriwa kuwa tembo wa zamani kabisa duniani, amekufa akiwa na umri wa miaka 88 nchini India.

Kutokana na kichwa cha gaja Muthassi au kijana wa tembo, Dakshayani alishiriki katika ibada za hekalu na maandamano katika Hekalu la Chengalloor Mahadeva katika jimbo la kusini la Kerala.

Lakini mtunzaji na mwenye kumtibu tembo huyo alionekana naye mapema wiki hii akiwa amesimama naye huku akimpa chakula na inasemekana tembo huyo mzee alikufa Jumanne.

Wahifadhi wa tembo huyo walianza kumlisha mananasi na karoti miaka ya hivi karibuni baada ya kukabiliwa na tatizo la kushindwa huku na kule na kushindwa kuonekana hadharani na katika shughuli za kijamii kwa miaka kadhaa sasa.

Bodi ya Travancore Devaswom, ambayo inaendesha hekalu ambalo alikuwa akiishi tembo mzee, inaarifu kuwa tembo huyo ni wa zamani kabisa katika uhamisho na anakadiriwa kuwa na umri wa miaka 88.Hata hivyo, mmiliki wa sasa wa Rekodi ya Dunia ya Guinness kwa tembo wa zamani katika utumwa ni Lin Wang.

Tembo wa bara Asia alikufa kwenye bustani ya wanyama huko Taiwan mwaka 2003 akiwa mimwenye umri wa miaka 86, na kutumikia na wasifu wake uinaarifu kuwa kipindi cha uhai wake aliwahi kulitumikia Jeshi la Uingereza katika Vita Kuu vya Pili vya dunia.

Ndovu mwingine ni Indira, alikufa nchini India katika jimbo la Karnataka mnamo mwaka 2017 na iliripotiwa kuwa alikuwa mzee wa "kati ya miaka 85 ama 90".

KUSOMA ZAIDI  BOFYA BBC  Swahili.

INTRODUCING "CHAMBUA MCHELE" BY KELLAH

RAIS DKT. MAGUFULI ASHIRIKI IBADA YA MISA TAKATIFU YA DOMINIKA YA 5 YA MAKASIA KANISA LA MTAKATIFU PETRO JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishiriki na waumini wengine katika Ibada ya Misa Takatifu ya Dominika ya 5 ya Makasia katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam leo February 10, 2019
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mkono wa amani na masista na waumini wakati wa  Ibada ya Misa Takatifu ya Dominika ya 5 ya Makasia katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam leo February 10, 2019
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Mkate wa Sakramenti Takatifu toka kwa  Paroko wa Parokia ya Oysterbay Padri Dkt. Alister Makubi  wakati wa  Ibada ya Misa Takatifu ya Dominika ya 5 ya Makasia katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam leo February 10, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Paroko wa Parokia ya Oysterbay Padri Dkt. Alister Makubi baada ya kushiriki Ibada ya Misa Takatifu ya Dominika ya 5 ya Makasia katika Kanisa la Mtakatifu Petro jijini Dar es salaam leo February 10, 2019. Katikati ni mmoja wa viongozi wa kanisa hilo  Dkt. Adelhelm James Meru

CHILDREN'S EDUTAINMENT COMMUNICATING GENDER EQUALITY FOR SOCIAL CHANGE

0
0
As Tanzania stands in the midst of the Fourth Industrialisation Revolution, digital forces are changing the way children are educated and how they perceive the world around them. The 5th Sustainable Development Goal calls for gender equality and one avenue to install this principle at an early stage is through educational cartoons that encourage children to normalise equality between the sexes and expand the notion of gender roles in day-to-day life. 

Ubongo is one such non-profit social enterprise launched in Tanzania that is paving the way for edutainment programs in Africa. The programs portray a diverse cast that aims to drive gender equality through characters that are empowered by the education they gain. The shows portray young boys that treat their female counterparts equally and perform domestic and household work. 

Akili and Me a program that was funded by the Human Development Innovation Fund (HDIF) has Akili, a young girl as the main protagonist whose life is filled with adventure and excitement. The program is currently airing in households across East and West Africa with an estimated 2.8 million viewers every week proving that this method of education has the potential to reach and positively affect children across the continent. 

It is important to portray characters in media that young children can identify and connect with and learn from. These approaches will uplift and motivate the generation of today to become the leaders and innovators of tomorrow.


G4S yaimarisha huduma za ulinzi Tanzania kwa kutambulisha teknolojia mpya.

0
0


 Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Einar Jensen akizungumza na wageni waalikwa juzi jijini Dar Es Salaam kwenye hafla ya uzinduzi wa huduma mpya za Teknolojia ya ulinzi wa kisasa zenye kulinda watu na mali zao kutoka kampuni ya G4S Tanzania.
 Henrik Krag kutoka Zonith akiwa na askari wa kampuni ya Q4S akielezea jambo kwa wageni waalikwa
 Inj.Omar Bakar kutoka Tanzania Data Lab akiwasilisha mada kwenye hafla ya uzinduzi wa huduma mpya za Teknolojia ya ulinzi wa kisasa zenye kulinda watu na mali zao kutoka kampuni ya G4S Tanzania.
 Sugandran wa Geo Tab akiwasilisha mada kwa wageni waalikwa
Wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.





· G4S inatoa huduma za ulinzi zinazotumia teknolojia kusaidia taasisi na watu binafsi kulinda watu na mali zao.

Tarehe 8 Februari 2019, Dar es salaam. Wakati ambapo ni muhimu kupunguza gharama za uendeshaji, sio tu kwamba teknolojia itasaidia kufikia malengo haya lakini pia itaweza kutoa manufaa zaidi ya kuaminika na ufanisi. Kwa kuongezea zaidi matuko mengi ya matumizi ya teknolojia inayostahili imeweza kuondoa maofisa wa ulinzi katika maeneo ambayo kuna hatari ya watu kuumia.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa teknolojia mpya ya ulinzi inayotolewa na G4S, Balozi wa Denmark Mhe. Einar H. Jensen alisema kwamba uimarishaji wa usalama wa watu na mali zao katika kanda hili umekuja katika wakati muafaka kwaajili ya kukabiliana na vitisho vilivyoshuhudiwa hivi karibuni. 'Dunia inabadilika kwa kasi sana na mahitaji ya kulinda watu na rasilimali hayajawahi kuwa makubwa kama hivi sasa. Mahitaji ya usalama kwa watu wa Afrika Mashariki vile vile yanazidi kuongezeka. Si muda mrefu tulikabiliana na uvamizi wa kikatili wa magaidi katika hoteli nchini Kenya, tunapaswa kuwa tayari kwa mashambulizi ya aina hiyo katika siku zijazo.

Akitangaza uzinduzi wa bidhaa za kisasa mwaka 2019, Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa G4S Secure Solutions Tanzania, Andrew Lauwo amesema 'Mfumo wa Ulinzi wa ishara ya kengele ya video (A video alarm security system) (Videofied) iliyotengenezwa Ufaransa yenye uwezo wa kuhisi mtu anapoingia na kisha kutuma video ya haraka kwenye control room ya G4S na kwenye simu yako pale mtu anapoingia katika sehemu husika ni bidhaa nyingine iliyoko katika ofa: Mfumo huu unatumia betri na hauna waya na unaweza kufungwa nje au ndani. Mfumo wa VIDEOFIED unatumika zaidi kulinda mali na pia unatumika katika mazingira ya nje kama vile sehemu za kuhifadhia boti, maeneo ya burudani ya nje, katika njia na sehemu nyingine ambako nishati ya umeme hakuna.'

'At the Gate' (Katika Mageti) ni mfumo wa kudhibiti waingiaji ambao unaruhusu ufuatiliaji wa nani anaingia na kutoka katika eneo lako kwa kuskani magari na taarifa za leseni za madereva wanapoingia na kutoka kupitia kifaa cha Android. Kifaa hiki kinafanyakazi kwa kutumia mtandao wa simu au kuunganishwa na Wi-Fi na kutoa vipengele mbalimbali vinavyokutaarifu mgeni anapofika getini, picha nyingi za magari na walioko ndani, taarifa za laptop, silaha,simu za smart, tablets nk. zinazoingia na kutoka katika eneo nk.'. aliongeza.

Akitolea maoni kuhusu mfumo wa kufuatilia magari (Vehicle Tracking Management System) alisema, ‘Geotab kutoka Canada: ni mfumo wa kufuatilia magari na kufuatilia tabia za dereva ambao pia unatoa kifaa cha ufahamu wa dereva (Driver Awareness tool) kinachobadilisha jinsi mafunzo ya mereva yanavyofanyika wakati wa kuendesha kwa kutoa maelekezo ya sauti ya hapo kwa hapo kwa dereva. Zaidi ya eneo halisi gari liliko, taarifa za kasi ya gari idadi ya tripu na umbali ambao tayari ameshasafiri, utendaji wa dereva kama vile kufunga breki kwa haraka, kukata kona na takwimu za utulivu wa kupita kiasi pia zinapatikana. Mfumo huu umetengenezwa kusimamia na kufuatilia utendaji wa gari, tabia za dereva na kuboresha mifumo ya usalama.'

Vilevile alisema kwamba, ‘The Sentinel Perimeter Protection kutoka Afrika ya Kusini ni mfumo wa masafa marefu wa kutambua uvunjaji na kuzuia ambao unatoa ishara ya kengele unapokuwa umekiukwa na kutuma video za tukio kwa kutumia Wi-Fi wakati pia ikiwa inatuma ishara ya tahadhari kwenye Control room yetu na katika simu yako ya mkononi masaa 24/7 Ina uwezo wa kusimamia eneo la mita 150 na vipengele vya ziada vinaweza kuongezwa kwenye mfumo huu kutoa ulinzi wa asilimia 100% katika eneo husika.

Akiongea kuhusu mfumo wa ulinzi kwa kutimia video ulioko katika ofa, Ofisa Mtendaji Mkuu wa ZONITH, Kristian H Stiesmark amesema kwamba 'Ishara ya Kengele ya Hofu Binafsi (Personal Panic Alarms) iliyoundwa na ZONITH, kampuni ya teknolijia ya kiwango cha juu ya watu wa Denmark inatoa kifaa cha kutolea ishara ya kengele ya hofu binafsi cha kufunga mahali na cha kutembea nacho ambacho kinamruhusu mtumiaji kuita msaada kutoka katika kikosi cha kuitikia matukio cha G4S panapotokea vitisho vya kiusalama au huduma ya kimatibabu au dharura ya moto.
 
 Zonith inatoa teknolojia ya kuchagua inayotumia Bluetooth ambayo inaruhusu ishara ya kengele na sehemu ulipo kutumwa kutokea sehemu yoyote ambako mtandao wa GSM unapatikana.'

WAHASIBU, MAMENEJA TEMESA WAPEWA MAFUNZO MFUMO WA GePG

0
0



Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akipokea muhtasari wa mafunzo ya Mfumo wa Ukusanyaji Maduhuri ya Serikali (GePG) kutoka kwa mhasibu Bi. Sophia Lukas mara baada ya kufunga mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam na kuendeshwa na wakufunzi kutoka Wizara ya Fedha na mipango (Hazina).
????????????????????????????????????
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle akizungumza na wahasibu wa wakala huo kutoka mikoa mbalimbali mara baada ya kufunga mafunzo ya Mfumo wa Ukusanyaji Maduhuri ya Serikali (GePG) yaliyoendeshwa na wakufunzi kutoka Wizara ya Fedha na mipango (Hazina). Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam.
????????????????????????????????????
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akizungumza na wahasibu (hawapo pichani) wakati akifunga mafunzo ya Mfumo wa Ukusanyaji Maduhuri ya Serikali (GePG) yaliyoendeshwa na wakufunzi kutoka Wizara ya Fedha na mipango (Hazina). Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha GePG Bazil Baligumya, Mhandisi Sylvester Simfukwe, Mhandisi Lukombe King’ombe na CPA Hans Lyimo.


……………………………………………………………………………………

NA ALFRED MGWENO- TEMESA

Wahasibu na mameneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA) mwishoni mwa wiki hii wamepatiwa mafunzo ya Mfumo wa Ukusanyaji Maduhuri ya Serikali, mafunzo hayo yaliyotolewa na wawezeshaji kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Hazina kitengo cha (GePG) yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mt. Depot Keko jijini Dar es Salaam na yamelenga kuwapatia uelewa mpana wa matumizi ya mfumo huo na jinsi ya kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza kwenye utekelezaji wa mfumo huo.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle alisema mfumo huo utausaidia sana Wakala kwenye utendaji kazi wake kwani utapunguza gharama za uendeshaji kwakuwa hauna tozo lolote na wakati huo huo mtumiaji atakuwa na uwezo wa kupata taarifa wakati wowote akizihitaji.

‘’Ninaamini mfumo huu utatusaidia kutoa taarifa mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya taasisi yetu hivyo basi tuutumie kama kitendea kazi chetu muhimu katika kuboresha na kuongeza tija kwa maslahi mapana ya Wakala wetu, wizara na taifa kwa ujumla’’, alisema Mhandisi Maselle.

Naye mkufunzi wa mafunzo hayo kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Hazina kitengo cha (GePG) Ndugu Bazil Baligumya alisema mfumo huo utaisaidia TEMESA kuhakiki kwa urahisi malipo yote yatakayokuwa yanafanywa na wateja wake na utarahisisha upatikanaji wa taarifa za fedha zinazohitajika kutoka katika vituo, ‘’tumewafundisha jinsi ya kuandaa ankara za madai, kuangalia na kuhakiki malipo yaliyokwisha fanywa na wateja, namna ya kutambua na kufanya usuluhisho kwa kutumia taarifa itokayo katika mfumo wa (GePG) pamoja na taarifa ya makusanyo kutoka benki na jinsi mfumo unavyoweza kuzalisha taarifa za wateja’’, aliongeza mkufunzi huyo.

Mfumo huo wa ukusanyaji wa maduhuri ya serikali unatambua na kukusanya fedha zote za Umma na kuziweka kwenye akaunti maalumu ya serikali iliyopo Benki kuu (BOT) na umetokana na marekebisho ya sheria ya mwaka (2017 sura ya 348 kifungu cha 6 cha sheria ya fedha kifungu kidogo cha 6a i na ii) inayoelekeza fedha zote za umma kukusanywa kwa mfumo huo. Mfumo wa (GePG) ulianza kwa kutumiwa na jeshi la polisi nchini hususani askari wa barabarani pamoja na Wakala wa Misitu ambapo ulionyesha mafanikio makubwa na hivyo kupata baraka za kuenezwa zaidi katika taasisi na asasi zaidi za serikali ambapo hadi kufikia sasa wadau zaidi ya 500 wameshaunganishwa kwenye mfumo huo.

MABORESHO SHERIA MPYA YA MADINI, MAJENGO NA VAT KUWANUFAISHA WADAU

0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango(Mb) akifafanua hoja wakati wa mjadala wa Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali, uliowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Prof. Adelardus L. Kilangi, Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Medard Kalemani(Mb) wakijadili jambo kabla ya kuwasilishwa kwa Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali, Bungeni Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) akijadiliana jambo na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Medard Kalemani (Mb), bungeni Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango(Mb) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Prof. Adelardus L. Kilangi wakijadili jambo baada ya kuwasilishwa kwa Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali, bungeni Jijini Dodoma.


Na. Josephine Majura, WFM, Dodoma 

Bunge limepitisha Muswada wa Sheria wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba mbili ya Mwaka 2019 ambao umelenga kutatua changamoto za za kodi ikiwemokodi ya Majengo, madini na Kodi uya Ongezeko la Thamani (VAT). 

Muswada huo uliopelekwa Bungeni kwa Hati ya Dharura ulijadiliwa na kupitishwa ambapo Wabunge mbalimbali walipata fursa ya kutoa maoni yao. 

Akizungumza wakati wa kuwasilisha Muswada huo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Prof. Adelardus Kilangi, alisema kuwa marekebisho hayo yameondoa kodi ya zuio (withholding tax) kutoka 5% hadi asilimia sifuri kwenye bei ya kuuzia madini ya aina zote kwa wachimbaji wadogo ili kuwahamasisha wachimbaji hao kuuza madini katika masoko ya madini. 

Alisema marekebisho hayo yanalenga kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali na kuhakikisha mapato yanayotokana na biashara ya madini yanakusanywa ipasavyo. 

Aliongeza kuwa Muswada huo umependekeza kutoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani kwa wachimbaji wadogo wa madini watakaouza madini yao katika masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa madini. 

Aidha, Prof. Kilangi alibainisha kuwa Muswada huo pia umependekeza kila kiwanja kitozwe Kodi ya Majengo badala ya kila jengo lililopo ndani ya kiwanja husika kwa maeneo ya Halmashauri za Wilaya. 

Sheria zilizopitishwa ni pamoja nma Sheria ya Ushuru wa Bidhaa Sura ya 147, Sheria ya Kodi ya Mapato Sura ya 332, Sheria ya Mamlaka za Serikali za Mitaa ya Utozaji wa Kodi ya Majengo Sura ya 289, Sheria ya Madini Sura ya 123 na Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani Sura ya 148. 

“Madhumuni ya marekebisho ya Sheria hizo pamoja na mambo mengine ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuondoa changamoto kwa wachimbaji wadogo wa madini, wakulima wa zabibu ndani ya nchi na viwanda vinavyotumia zabibu hiyo katika uzalishaji pamoja na kuweka viwango mfuto (fixed rate) vya kodi ya majengo.” Alisema Prof. Kilangi. 

Alisema kuwa Serikali imeona upo umuhimu wa kuwasilisha Muswada huu kwa haraka kupitia Hati ya Dharura ili kutatua changamoto mbalimbali ikiwemo kupunguza utoroshwaji wa madini nje ya nchi unaofanywa na wachimbaji wadogo ambao wanakwepa kodi. 

MAUJI YALIYOTOKEA YANAZOROTESHA UCHUMI- DC NJOMBE

0
0
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Ruth Msafiri akizungumza na waumini wa Kanisa la TAG Melinze wakati wa kufunga maombi ya kuuombea mkoa wa Njombe kutokana na mauaji ya Watoto yaliyotokea Mkoani Njombe.
Mwenyekiti wa Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ( Idara za Maendeleo na Ustawi wa Jamii) Bi. Hanifa Selengu akitoa salamu za Wizara kwa waumini wa Kanisa la TAG Melinze wakati wa kufunga maombi ya kuuombea mkoa wa Njombe kutokana na mauaji ya Watoto yaliyotokea Mkoani humo.
Waumini wa Kanisa la TAG Melinze wakimsikiliza MKuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Ruth Msafiri (hayuko pichani) wakati wa kufunga maombi ya kuuombea mkoa wa Njombe kutokana na mauaji ya Watoto yaliyotokea Mkoani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Ruth Msafiri (wa Tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Waumini wa Kanisa la TAG Melinze na Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ( Idara za Maendeleo na Ustawi wa Jamii mara baada ya kufunga maombi ya kuuombea mkoa wa Njombe kutokana na mauaji ya Watoto yaliyotokea Mkoani humo.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.



Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Ruth Msafiri amesema matukio ya utekaji na mauji ya watoto Wilayani Njombe yamesababisha uchumi kuzorota kwa kushuka kwa uzalishaji mali kwa wananchi.

Amesema hali hiyo inatokea kwa kuwa wazazi wanatumia muda mwingi kwapeleka watoto na kuwafuata watoto shule hivyo kupoteza muda na kusimamisha shuguli zao.

Ameyasema hayo jana wakati akifunga maombi katika Kanisa la TAG Milinze yaliyolenga kuombea Wilaya hiyo kuondokana na matukio ya utekaji na mauaji ya watoto.“ Hatuwezi kufikia uchumi wa Viwanda kama matukio haya yataendelea wazazi wanapoteza sana muda katika kuhakikisha watoto wao wanapata ulinzi kwa kuwapeleka na kuwarudisha nyumbani” amesema

“ Niwaambie tu Halmashauri ya Mji wa Njombe inaoongoza katika Halmashauri zote nchini kwa kuwa na kipato kikubwa ana kwa mwaka mwananchi wa hapa ana uwezo wa kuwa na shillingi million 5”

Mkuu wa Wilaya huyo amewataka waumini wa Kanisa hilo na wananchi wa Wilaya na Mkoa wa Njombe kwa ujumla kuombea mkoa wao ili kuondokana na vitendo hivyo vinavyopelekea kuzorotesha shughuli za kiuchumi.

Akitoa salama za Wizara Mwenyekiti wa Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara za Maendeleo na Ustawi wa Jamii) Bi. Hanifa Selengu amesema Serikali ipo pamoja na wananchi wa Mkoa wa Njombe katika kulaani matukio hayo ya utekeaji na mauaji ya watoto yaliyojitokeza.

TUME YAENDESHA WARSHA VYUO VYA ARDHI KUHUSU DHANA YA USHIRIKISHWAJI KATIKA UPANGAJI WA MATUMIZI YA ARDHI

0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) Dkt. Stephen Nindi akitoa mada wakati wa warsha ya ushirikishwaji wa wananchi katika upangaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi nchini.
Bwana Kent Nillson kutoka Taasisi ya Lantmateriet nchini Sweeden akitoa mada juu ya uzoefu wa nchini kwao kuhusu upangaji wa matumizi ya ardhi.
Mwanafunzi wa mwaka wa pili Ngeze Valentina wa kozi ya RDP akichangia mada wakati wa majadiliano juu ya ushirikishwaji wa wananchi katika upangaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi. 
Mshiriki wa warsha Kiteri Sophia kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi akitoa maoni yake juu ya ushiriki wa wanawake katika hatua za upangaji wa mipango ya matumizi ya ardhi.
Baadhi ya washiriki wa warsha wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa wakati wa warsha ya upangaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi.



Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) kwa kushirikiana na Taasisi ya Lantmateriet ya nchini Sweden kupitia ufadhili wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Sweeden (SIDA) imeendesha warsha katika Chuo Kikuu cha Ardhi jijini Dar es Salaam na Chuo cha Ardhi mjiji Morogoro iliyohusu ushirikishwaji wa wananchi hasa makundi maalum katika upangaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi nchini.

Katika warsha iliyofanyika Chuo Kikuu Ardhi na kuhudhuriwa na Wakufunzi pamoja na Wanafunzi wa chuo hicho, wawezeshaji walikuwa ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume Dkt. Stephen Nindi; Bw. Kent Nillson kutoka Taasisi ya Lantmateriet na Bi. Lilian Looloitai kutoka Shirika Lisilo la Kiserikali la CORDS ambalo hufanya kazi zake katika Wilaya za Monduli na Longido Mkoani Arusha.

Akitoa mada katika warsha hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Tume alielezea namna gani Sheria, na miongozo mbalimbali inayohusu upangaji wa matumzi ya ardhi inavyotambua na kuhimiza ushirikishwaji wa wananchi na kutaja makandi maalum kama vile wanawake kupewa kipaumbele katika hatua zote za upangaji na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi. 

Pia, Dkt. Nindi alitolea mfano wa Mwongozo Shirikishi wa Upangaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji (Participatory Land Use Management Guidelines) ambao umetamka bayana juu ya uundwaji wa kamati za upangaji na usimamizi wa mipango ya matumizi ya ardhi za vijiji kuwa lazima ziwe na wajumbe wanawake wasiopungua watatu.

Wakielezea uzoefu wao juu ya ushirikishwaji katika upangaji wa matumizi ya ardhi, Bw. Kent Nillson kutoka Taasisi ya Lantmateriet amesema kuwa Sweden ilianza kupangwa toka mwaka 1692 ambapo hadi hivi sasa ushiriki wa wananchi katika shughuli za upangaji na umiliki wa ardhi umeimarika kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wa mwezeshaji kutoka Asasi ya Kiraia ya CORDS, Bi. Lilian Looloitai amesema kuwa, kwa muda mrefu sasa CORDS wamejikita katika uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi katika Wilaya ya Monduli ambapo ushiriki wa wanawake katika zoezi hilo unaonyesha kufanikiwa. Bi. Lilian amesema kuwa kwa sasa kumekuwepo na ongezeko la idadi ya wanawake wanaoshiriki na kutoa maoni katika mikutano ya kijiji pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Warsha kama hii pia imefanyika Chuo cha Ardhi mjini Morogoro ambapo imekuwa chachu ya majadiliano juu ya upangaji wa mipango ya matumizi ya ardhi kwa njia ya ushirikishwaji pamoja na kuwaandaa wanafunzi kwa ajili ya kusimamia sekta ya ardhi kwa kuzingatia masilahi mapana ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

MUUGUZI ASIMAMISHWA KUTOA HUDUMA

0
0
BARAZA LA UUGUZI NA UKUNGA LA MSIMAMISHA AFISA MUUGUZI MKUNGA MSAIDIZI MARTINI CHAMANI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MOUNT MERU ARUSHA KWA MUDA WA MWAKA MMOJA.
 
Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, katika kikao chake cha 196 limemsimamisha Muuguzi Martin Chama kutoa huduma za Uuguzi na Ukunga kwa muda wa mwaka mmoja tangu tarehe 7.02.2019 baada ya kumtia hatiani na makosa mawili kati ya manne yaliyowasilishwa katika Baraza la Uuguzi na Ukunga mwezi Septemba 2018.
 
Makosa hayo ni pamoja na kufika kazini akiwa amelewa na kutaka kuhatarisha usalama wa wagonjwa na ndugu zao kwa kushindwa  kutoa huduma kwa umakini na weledi.
 
Awali ofisi ya Msajili wa baraza la Uuguzi na Ukunga lilipokea tuhuma kutoka Hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mount Meru Arusha kupitia kwa Muuguzi mkuu wa mkoa ambaye pia ni msimamizi wa maadili wa mkoa wa Arusha kwa mujibu wa sheria N0 1ya mwaka 2010.
 
Kwa mujibu wa taarifa hiyo muuguzi huyu  alifika kazini tarehe 26.09.2018  zamu ya usiku majira ya saa tatu husiku akiwa amelewa na alianza kuwasumbua ndugu waliokuwa wakiwaangalia wagonjwa wao kutaka kuendelea kutoa huduma kwa wagonjwa ili hali akiwa amelewa sana hali ambayo ingesababisha kuhatarisha  maisha ya wagonjwa kwa kuwa hakuwa na umakini.
 
Tuhuma hizi ziliwasilishwa na walalamikaji wawili waliokuwa wakiuguza wagonjwa wao.
 
Ofisi ya Msajili ilituma Afisa kutoka baraza la Uuguzi na Ukunga ambaye aliungana na timu ya Mkoani Arusha ikiongozwa na Muuguzi mkuu wa Mkoa wa Arusha.Timu hii ilifanya uchunguzi wa awali na kubaini mapungufu yaliyofanywa na muuguzi huyu ambayo ni kinyume na maadili ya Uuguzi na Ukunga.
 
Taarifa hiyo ilipelekwa katika kikao cha dharura cha bodi cha 195 ambacho pamoja na mambo mengine ilijadili taarifa hii na kuamua shauri hili lisikilizwe  kataka kikao cha bodi cha 196 ambayo itahusisha mtuhumiwa na mashahidi ambao ni walalamikaji na watumishi waliokuwepo siku ya tukio.
 
Shauri hili limesikilizwa tarehe 07.02.2019 ambapo Ushahidi uliotolewa umemtia hatiani bwana Martini kwa kulewa na kushindwa kutoa huduma kwa wagonjwa kwa weledi na kutaka kuhatarisha Maisha ya wagonjwa na ndugu zao.baraza liliadhimia kwa kauli moja kumsimamisha kutoa huduma hizi kwa muda wa mwaka mmoja.
 
Baraza la Uuguzi na Ukunga ni Mamlaka iliyoanzishwa kisheria na kufanya kazi chini ya Sheria inayoitwa The Nursing and Midwifery Actof 2010.Baraza lilianzishwa kwa ajili ya kulinda umma kutokana na huduma zinazotolewa na wauguzi na wakunga nchini na linafanya kazi kwa kusimamia ubora katika mafunzo na kuhakikisha huduma zinazotolewa zinazingatia viwango vilivyowekwa.
 
Imetolewa na
Agnes Mtawa
Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga
09.02.2019

INTRODUCING: FID Q X Isha Mashauzi X Rich Mavoko X Big Jahman - BAMBAM (Official Video)


Mkubwa na Wanawe wakonga nyoyo Sauti za Busara Zanzibar

0
0
Na ANDREW CHALE, ZANZIBAR

KUNDI la wanamuziki wanaokuzwa la Mkubwa na Wanawe usiku wa 7 Februari 2019 limeweza kukonga nyoyo za watu waliojitokeza kushuhudia tamasha la 16 la Kimataifa la Sauti za Busara, kwenye viunga vya Ngome Kongwe, Unguja.

Kundi hilo limeweza kuonesha umahri wao wa kuimba na kucheza jukwaani huku wakiendana sambamba na mapigo na ala za muziki wa bendi ‘live' iliamsha shangwe za mara kwa mara kwa mashabiki waliofurika Ngome Kongwe.

Vijana hao wa waliweza kuimba nyimbo zaidi ya tano (5) ikiwemo ya Stata ukiimbwa na mwanadada Catrima Wegesa huku nyimbo zingine zikiimbwa na Abdala Mustapha 'Kisamaki' huku kijana mdogo kabisa wa kundi hilo Abdul Kadry 'Dogo Kadry' akiwa kivutio kila alipopanda kuimba kwenye jukwaa hilo la Busara.

Dogo Kadry aliweza kuimba nyimbo zaidi ya mbili ikiwemo ule aliyourudua wimbo wa Asu ulioimbwa na Abdul Misambano. pia waliweza kuimba nyimbo za wasanii waliowahi kupitia kundi hilo zikiwemo za ‘Mototo wa udongo’ na ‘Watakubali'. Kundi hilo lililo chini ya muasisi wake, Said Fella ‘Mkubwa Fella’ ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kilungule ya wilayani Temeke, Dar es Salaam hadi sasa lina vijana wanaofanya kazi za Sanaa za Muziki zaidi ya 100.

Miongoni wa wasanii waliowahi kuwa kwenye kundi hilo na kwa sasa wanajitegemea ni pamoja na Dogo Aslay, Mboso na wengine wengineo.Miaka miaka kadhaa iliyopita wasanii hao Dogo Aslay na Mboso waliwahi kushiriki tamasha hilo huku wakiwa vijana wenye umri mdogo ambapo walikuwa kivutio kama ilivyo kwa sasa kwa msanii mpya wa kundi hilo Dogo Kadry ambaye kwenye shoo hiyo aliweza kuonesha uwezo wake licha ya kuwa na umri wa chini ya miaka 15.

Mpaka sasa Mkubwa na Wanawake Crew wameshatoa nyimbo mbalimbali zikiwemo : Tofauti, 2012; Nawashusha Down, 2013; Fanya Yako, 2014; Unanitusi, 2015; Sitakitararira, 2016; Naelewa, 2016; Yerere, 2016Lakini pia baadae waliweza kutoa nyimbo kupitia bendi ya Yamoto ambapo napo walitoa nyimbo mbalimbali .
 Kundi la Mkubwa na Wanawe wakishambulia jukwaa katika onesho lao la jana usiku 7 Februari 2019, kwenye viunga vya Ngome Kongwe, Unguja, Zanzibar
Mmoja wa Wasanii kutoka kundi la Mkubwa na Wanawe, Abdala Mustapha 'Kisamaki' akionesha uwezo wa kuimba na kucheza jukwaani wakati wa tamasha hilo la Sauti za Busara, 7 Februari 2019
 Msanii mwenye umri mdogo katika kundi hilo la Mkubwa na Wanawe, Abdul Kadry 'Dogo Kadry' akiimba kwa hisia nyimbo ya Asu.
 Dogo Kadri akifanya mahojiano baada ya kumalizika kwa  shoo yao hiyo
shangwe zilizokuwa zikiendelea wakati wa shoo hiyo

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMWAKILISHA RAIS DKT MAGUFULI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA ADIS ABABA ETHIOPIA

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini Thabo Mbeki, katika ukumbi wa mkutano wa kimataifa wa (AU) mjini Adis Ababa Ethiopia Februari 10, 2019, (katikati) ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Augustine Mahiga, Waziri Mkuu yupo nchini Ethiopia kumwakilisha Rais Magufuli kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika (AU). 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa kwenye mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika (AU) kumwakilisha Rais Magufuli, mkutano huo uliyofanyika katika ukumbi wa mkutano wa kimataifa wa (AU) mjini Adis Ababa Ethiopia Februari 10, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa kampuni ya Liyan African iliyowekeza nchini Tanzania Hakim El- Shwehdi, kwenye ukumbi wa mkutano wa kimataifa wa (AU) mjini Adis Ababa Ethiopia Februari 10, 2019, Waziri Mkuu yupo nchini Ethiopia kumwakilisha Rais Magufuli kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika (AU), katikati ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Augustine Mahiga.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Augustine Mahiga, ndani ya ukumbi wa mkutano wa kimataifa wa (AU) mjini Adis Ababa Ethiopia Februari 10, 2019, Waziri Mkuu yupo nchini Ethiopia kumwakilisha Rais Magufuli kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika (AU)

SMZ Yakabidhiwa Kiwanja cha Heka 30 Mji wa Serikali Dodoma

0
0
Makamu wa Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Samia Suluhu Hassan akimkabidhi hati ya kiwanja Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ally Idd wakati wa mara baada ya kufungua Kikao Kazi cha Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Muungano na Mapinduzi jana jijini Dodoma. Hati hiyo ya kiwanja chenye ukubwa wa Hekari 30 imetolewa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ili waweze kujenga Ofisi zao Makao Makuu ya Nchi jijini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao kazi cha Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) jana Jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ambaye alimwakilisha Waziri Mkuu, Dkt. Hussein Mwinyi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mohamed Aboud.
Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifuatilia kikao kazi cha Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) jana Jijini Dodoma.
Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanziba wakifuatilia kikao kazi cha Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) jana Jijini Dodoma. (Picha na Frank Shija – MAELEZO)
Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanziba wakifuatilia kikao kazi cha Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Serikali ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) jana Jijini Dodoma. (Picha na Frank Shija – MAELEZO)



Na: Lilian Lundo – MAELEZO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameikabidhi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) hati ya kiwanja chenye ukubwa wa heka 30 kilichopo Mji wa Serikali Jijini Dodoma kwa ajili ya kuanza ujenzi wa ofisi Jijini humo.

Makabidhiano hayo yamefanyika jana wakati wa kikao cha kamati ya pamoja ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kujadili masuala ya Muungano kilichofanyika Jijini Dodoma.

“Serikali ya Mapinduzi Zanzibar tunawakaribisha Dodoma, wenzenu tumeanza na nyie tunawategemea kuwepo Dodoma,” amesema Mhe. Makamu wa Rais.

Kwa upande wake, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi amesema kiwanja kilichokabidhiwa kwa SMZ kina ukubwa wa sawa na viwanja kumi vilivyogawiwa kwa Wizara, kwani viwanja vya Wizara vinaukubwa wa kati ya heka 3 hadi 5 kwa kila wizara.

Ameendelea kusema, utoaji hati kwa SMZ ni muendelezo wa utekelezaji wa Serikali ya Awamu ya Tano ya kuhamishia shughuli zake Jijini Dodoma, ambapo tayari wizara zote zimekwisha hamia Jijini humo na mwezi huu zinatarajia kuhamia Mji wa Serikali, uliojengwa eneo la Ihumwa.

Aidha Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameshatoa hati za viwanja kwa Balozi zote zilizopo hapa nchini ili nazo zihamie Jijini humo ambayo ndiyo Makao Makuu ya Nchi.

MKURUGENZI WA TRC ACHUKIZWA NA UTENDAJI KAZI WA KAMPUNI YA CCECC

0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa (mwenye tisheti nyeupe) akizungumza na mmoja ya wasimamizi wa Kichina ambaye ndiyo wanaokarabati reli ya kati kupitia kampuni ya CCECC wakati anapita kuelekea katika ukaguzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge mwishoni mwa wiki hii. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa (wa kwanza kulia) akizungumza na msimamizi wa Kichina ambao ni wakarabati wa reli ya kati. Ambapo hapa Msimamizi huyo alikataa kuongea nao maana hajui kingereza. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa (mwenye tisheti nyeupe) akipiga simu kwa bosi wake na huyo msimamizi wa kichina ili kuweza kuwaachia njia baada ya huyo mchina kukataa kwa madai ukarabati unaendelea.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa (mwenye tisheti nyeupe) akizungumza na wafanyakazi wa Kitanzania ambao wamepewa ajira na kampuni ya CCECC jinsi wanavyofanyakazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa (wa mbele) akiendelea kukagua ukarabati wa reli ya kati kupitia kampuni ya CCECC wakati anapita kuelekea katika ukaguzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge mwishoni mwa wiki hii. 
Shughuli ya ukarabati wa reli ya kati kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma. 
Msimamizi wa Kichina wa kampuni ya CCECC akiendelea kusimamia kazi.
Baada ya kukaa kwa muda wa takribani saa 1:30 ndiyo ilipoamuliwa kuweka magogo ili treni ipite na waendelee na safari.
Treni ikipita huku ikiwa na usimamizi wa hali ya juu. 

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa amechukizwa na utendaji kazi wa kampuni ya Kichina ya CCECC inayohusika na ukaratati wa reli ya kati. 

Akizungumza mara baada ya kutembelea reli hiyo wakati akipita kukagua mradi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge, Mkurugenzi Masanja Kadogosa amechukizwa na jinsi wafanyakazi wa Kichina wanavyowabagua Watanzania wanaofanya nao kazi. "Leo nimepita kama bahati mbaya na kukutana na haya, kiukweli sijafurahishwa na utendaji kazi wao haiwezekani watu waliopelekwa site hawajui Kingereza sasa wanawezaje kuwasimamia hawa waswahili ambao nao hawajui kichina???," amesema. 

Ameongeza kuwa Kampuni iliyopewa tenda ya kukarabati reli ya Kati ya CCECC wamekuwa wakipeleka wasimamizi wasiojua lugha ya Kingereza jambo linalozorotesha utendaji kazi katika ukarabati huo. Hatua hiyo ilikuja baada ya Mkurugenzi Mtendaji kupita na wasanii na kukuta wanakarabati wakati walipewa taarifa kuwa watapita na wasanii wakielekea mjini Morogoro kukagua mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge. 

Katika hali iliyomchukiza Mkurugenzi Mtendaji Kadogosa ni jinsi wafanyakazi hao wa kichina walivyomdharau kwa kukataa kuongea nae eti hawamfahamu licha ya yeye kujitambulisha kwao hawakujali. "Hivi nyie wafanyakazi kiongozi weni ni nani??? nimekuja hapa nikiwa ni Mtendaji Mkuu wa TRC lakini mnavyonijibu kama hamna kiongozi basi niwafukuze wote hata site,' amesema. 

Ndipo Mtendaji Mkuu alipochukua hatua ya kupiga simu kwa viongozi wao na kuamuru waende ofisini kwake Jumatatu Februari 11, 2019 wakajieleze kwanini wanakuwa na dharau hasa kwa viongozi. 'Binafsi sijafurahidhwa na majibu ya hawa Wachina au wanatuona sisi ngozi nyeusi hatuna thamani kwao??? Niwaombe nyie viongozi wa TRC mlio pamoja na mimi... nawataka Jumatatu mje na hawa mabwana ofisini kwangu," amesema.

 Hatua nyingine Mkurugenzi Mtendaji huyo amewaamuru wafanyakazi wote wanaokarabati reli chini ya kampuni ya kichina ya CCECC kuwa wawazi kusema kero zao ili zitatuliwe. 'Nimeambiwa kuwa wachina wamekuwa wakiwapiga na kuwatukana ila nyie mmekaa kimya hili siwezi livumilia katika shirika langu, nataka wote muwe na usawa,' Amesema. Wafanyakazi wa Kampuni ya Kichina ya CCECC wamekuwa ni wakaidi na hawajui lugha ya kingereza jambo linalozorotesha utendaji kwa vile hawaelewani na vijana wa Kitanzania.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEBRUARI 11,2019

Viewing all 109602 articles
Browse latest View live




Latest Images