Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110102 articles
Browse latest View live

WASANII WAFURAHISHWA NA KUSIFU KASI YA UJENZI WA RELI YA KISASA YA UMEME (SGR)

$
0
0
Mataruma yakiwa tayari kwa ajili ya kupangwa kwenye tuta ili kutandika reli.
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akizungumza na wasanii mbalimbali, Wachezaji wa zamani na waandishi wa habari mara baada ya kufika katika kambi kubwa ya Soga mkoani Pwani wakati wa ziara ya kutembelea na kujionea jinsi shughuli za ujenzi wa reli ya kisasa ya umeme Starndard Gauge Railway (SGR) kutoka Dar es salaam kwenda Morogoro unavyoendelea.

Wakiongeza katika ziara hiyo wasanii mbalimbali wamesifu juhudi za sreikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa utekelezaji mzuri wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2015-2020 kwa jinsi inavyotekelezwa na serikali kwa kasi kubwa na kuleta matumaini kwa watanzania.

Mradi huo unajengwa na kampuni ya Yapi Merkezi kutoka nchini Uturuki na kwa sasa ujenzi huo umefikia asilimia 42 ambapo kazi mbalimbali zinaendelea kama vile kujenga madaraja, kupasua miamba ya milima kuunganisha tuta katika vipande mbalimbali, kutandika mataruma na reli na kusimika pia nguzo za umeme katika maeneo ambayo tayari yameshatandikwa reli.
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC)Bw. Masanja Kadogosa wakati akitoa maelezo mbalimbali kwa wasanii mbalimbali waliotembelea mradi huo.PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-SOGA PWANI
Baadhi ya wasanii wakiwa katika eneo la Soga.
 
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC)Bw. Masanja Kadogosa wakizungumza na waandishi wa habari mbalimbali ndani ya treni.
Irene Uwoya pamoja na mwenzake wakiwa wameketi kwenye reli ya kisasa ya umeme SGR baada ya kufika eneo la Soga mkoani Pwani.
Ujenzi wa madaraja ukiendelea.
Mratibu wa ziara hiyo mchekeshaji Steve Nyerere akizungumza jambo na mwigizaji Irene Uwoya.
Mitambo mbalimbali inayotumika katika ujenzi huo.
Baadhi ya maeneo yakiwa yamesimikwa nguzo za umeme.
Hii ndiyo treni ya Delux ya TRC iliyowachukuwa wasanii mbalimbali pamoja na waandishi wa habari kwa ajili ya kutembelea mradi huo.
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC)Bw. Masanja Kadogosa wakimsikiliza Babu Tale Meneja wa WCB wakati akizungumza katika kambi ya Soga mkoani Pwani.
Wasanii mbalimbali wakiwa katika kambi ya Soga.
Wasanii Mchizi Mox kushoto na Mtunis ambaye ni muigizaji wa filamu wakipozi kwa picha,
Waigizaji Welu kushoto na Maya wakipozi kwa picha.
Meneja Msoko wa shirika la bima la taifa NIC Elisante Maleko akionyesha reli ya kisasa ya umeme SGR kipande kilichokamilika Shirika la bima la NIC ndilo limeikatia bima kampuni ya Yapi Merkezi inayojenga mradi huo.
Meneja Msoko wa shirika la bima la taifa NIC Elisante Maleko akiwa pamoja na wafanyakazi wenzake kutoka NIC.
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC)Bw. Masanja Kadogosa wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasanii katika kambi kubwa ya Soga mkoani Pwani.

Mfumuko wa Bei Waendelea Kushuka hadi asilimia 3.0 Mwezi Januari 2019

$
0
0
Na; Frank Mvungi- MAELEZO

Mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi Januari, 2019 umeshuka hadi asilimia 3.0 kutoka asilimia 3.3 ya mwezi Desemba mwaka 2018.

Akizungumza wakati akiwasilisha hali ya mfumuko wa bei leo Jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Sensa ya Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Ephraim Kwesigabo, amesema kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwezi Januari, 2019 umepungua ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo mwezi Desemba, 2018.

“Kupungua kwa mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi Januari 2019 kunatokana kupungua kwa bei za bidhaa za vyakula katika mwezi huo ikilinganishwa na bei za mwezi Januari 2018.” alisisitiza Kwesigabo

Akifafanua, Kwesigabo amesema kuwa mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi Januari umeendelea kupungua hadi kufikia asilimia 0.7 kutoka asilimia 1.0 iliyokuwa mwezi Desemba, 2018.

Aliongeza kuwa baadhi ya bidhaa zilizochangia kupungua kwa mfumuko wa bei wa mwezi Januari 2019 ni pamoja na mchele asilimia 3.9, mahindi13.9, unga wa mahindi 8.9, mtama 5.1, unga wa muhogo 6.8, maharage 4.2, choroko 10.5, mihogo mibichi 5.6, viazi vitamu kwa asilimia 3.3, magimbi 18.6 na ndizi za kupika 13.3

Kwa upande wa nchi za Afrika Mashariki, mfumuko wa bei nchini Kenya umepungua hadi asilimia 4.70 kutoka asilimia 5.71 kwa mwezi Desemba 2018, nchini Uganda mfumuko wa bei kwa mwezi Januari umeongezeka hadi asilimia 2.7 kutoka asilimia 2.2 kwa ya mwezi Desemba 2018.

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ni Taasisi ya Serikali iliyoanzishwa kwa sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 na kupewa majukumu ya kutoa, kusimamia, na kuratibu upatikanaji wa Takwimu rasmi nchini ikiwa ni pamoja na takwimu za mfumuko wa bei kwa ajili ya matumizi ya Serikali na wadau wa takwimu.
Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Ephraim Kwesigabo akisisitiza kuhusu kushuka kwa mfumuko wa Bei hadi asilimia 3.0 kwa mwezi Januari 2019 ikilinganishwa na asilimia 3.3 kwa mwezi Desemba 2018.

WIZARA YAKUTANA NA WATAALAM WA MAENDELEO YA JAMII, USTAWI WA JAMII NA ELIMU MKOANI NJOMBE

$
0
0


Kiongozi wa Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Hanifa Selengu (kulia) akifafanua jambo kwa Wataalam kutoka Halmashauri ya Mji wa Njombe na halmashauri ya Wilaya ya Njombe katika ujio wa timu hiyo kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Maendeleo ya jamii wa Mkoa wa Njombe Bw. Cassian Nkunga akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bw.Abraham Kaaya akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Mji wa Njombe Bi. Enembora Lema akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bw. Averino Chaula akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Mji wa Njombe Bw. Hosea Yusto akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Mwanasheria kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bw. Denis Bashaka akifafanua jambo katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Ustawi waJamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) (wa pili kushoto) Bi. Mwanaisha Moyo akifafanua jambo katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa wakati Timu kutoka kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

……………………….

Na Mwandishi Wetu Njombe

Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) wamekutana na Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha na mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.

Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti wa Timu hiyo Bi. Hanifa Selengu amesema kuwa Wizara imeuunda Timu hiyo kwa lengo la kuunga mkono juhudi za Mkoa wa Njombe katika kutafuta namna bora ya kukomeshana mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani humo na kuwezesha wataalam wa mkoa kwa kushirikiana na wadau kwenda kwa jamii kutoa elimu juu ya kuachana na mila zisizofaa hasa zinazoangamiza watoto.

Ameongeza kuwa lengo la kukutana na Wataalam hao ni kuandaa jumbe maalum zitakazotumika katika jamii ili kutoa hamasha kwao kuzingatia umuhimu wa malezi kwa watoto na kuachana na mila zisizofaa katika jamii elimu itakayowasaidia kutimiza majukumu yao ya kupambana na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Akizungumza katika kikao hicho Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Njombe Bw. Cassian Nkunga amewataka Maafisa hao kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoa maoni yao ili yawezeshe kutengeneza jumbe maalum zitakazotumika katika jamii ili kutoa hamasha kwao kuachana na mila zisizofaa katika jamii hasa zinazoangamiza watoto.

Akitoa Taarifa ya utendaji kazi ya Idara ya Ustawi wa Jamii kwa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Afisa Ustawi wa Jamii Bw. Averino Chaula amesema kuwa Idara ya Ustawi wa Jamii ya Wilaya imeshirikiana na wadau wa watoto katika kutoa elimu kwa jamii kila mara na waliongeza nguvu kubwa mara baada ya kutokea kwa mauji ya watoto mkoani Njombe.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bw. Abraham Kaaya ameshauri elimu kutolewa kwa jamii kwa kuwataka wanajamii kuvunja ukimya kwa kutoa taarifa ya vitendo vyote vya ukatili dhidi ya watoto.

Kwa upande wake Mwanasheria kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bw. Denis Bashaka amesisitiza suala la kujikita katika kufichua tatizo linalosababisha kutokea kwa mauaji hayo na kuangalia namna bora ya kuzifikia jamii kutoa elimu na kuzingatia Sheria, Sera na Miongozo katika kuandaa jumbe hizo.

Wizara imekutana na Wataalam wao kutoka Idara ya Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu mkoani Njombe kutengeneza jumbe maalaum zitakozotumika katika Jamii, Vyombo vya Habari katika kutoa elimu juu ya kuzingatia malezi bora kwa watoto na kuachana na mila zisizofaa hasa zinazoangamiza watoto.

MASHINDANO YA AFCON YATUMIKE KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII WETU

$
0
0
Na Ivon Samson-MAELEZO 

Hayawi hayawi sasa yamekuwa ni siku 66 pekee zimebaki mashindano ya AFCON kuanza ifikapo April 14, 2019, ambapo pazia la michuano ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 litafunguliwa. 

Mkurugenzi wa Baraza la Michezo la Taifa-BMT,Yusuph Dingo, amesema kuwa mpaka sasa maandalizi yanaenda vizuri na yamekamilika kwa asilimia kubwa.ikiwemo miundombinu ya viwanja, usafiri, na hoteli ambazo wageni watafikia. 

Dingo, amesema “Michuano hiyo ambayo itakayofanyika Jijini Dar-es-salaam, itajumuisha timu nane katika makundi mawili, ambapo kundi A kuna wenyeji Tanzania, Nigeria, Angola na Uganda. Aidha, kundi B litajumuisha mataifa ya Guinea, Cameroon,Morocco na Senegal.Hii ni kwa mara ya kwanza kwa Tanzania kuandaa michuano hii na imewekeka historia mpya kwa nchi za Afrika Mashariki”. 

Aidha, viwanja vitatu pekee ndiyo vitatumika kwenye michuano hii ambavyo ni uwanja wa Taifa,Uhuru na Azam Complex unaomilikiwa na klabu ya Azam FC.Hakika hii fursa hadhimu kwa wapenda mchezo wa soka hapa nchini Tanzania kushudia mataifa ya kigeni yakija kwenye ardhi yetu ya 

Dingo Alienda mbali zaidi kwa kueleza kwamba hii fursa kubwa zaidi kutokea nchini kwetu hivyo ni vyema tukajipanga vizuri ili wageni wakija waje kuona uzuri, sifa nzuri ya Tanzania na mabalozi wazuri kusimulia mazuri ya nchi yetu. 

"Tumejipanga vyema sana pia tutashirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania-TTB kuhakikisha tunatangaza vivutio vyetu vya utalii vilivyopo kwani hii fursa pekee na ukizingatia watu wengi wanaingia nchini kwetu.Tuna ndege za kisasa hivyo hizo zinakuwa chachu kwa wageni ambao watapenda kwenda mikoa mbalimbali yenye vivutio. 

Naye Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Micheza Tanzania-TFF Ammy Ninje, amesema kuwa maandalizi ya timu yetu yanaenda vizuri na wiki mbili zijazo kikosi hicho cha Serengeti Boys kitaenda nchini Uturuki ili kuweka kambi ya kujiandaa na michuano hiyo. 

Aidha, TFF wamepanga kuongeza mwalimu kwenye benchi la ufundi ili aweze kushirikiana na mwalimu Oscer Mirambo na Hemedi Moroco ili kufanya vijana wapate mazoezi zaidi na hatimaye kupata ushindi katika michuano hiyo. 

Timu ya Serengeti Boys inajumuisha wachezaji………ambao wamechaguliwa kutokana na vijana walioshiriki michezo mbalimbali ya Kopa Cocacola, Umoja wa Michezo wa Shule za Sekondari Tanzania .-UMISETA 

08 Februari 2019

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKUTANA NA WATENDAJI WA TASISI YA UTAFITI ZAO LA MICHIKICHI

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika kikao kati yake na Mawaziri wa Kilimo, Viwanda na Biashara  na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji pamoja na Watendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Zao la Michikichi,  alichokiitisha kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Februari 8, 2019.  Kulia kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angela Kairuki na kushoto kwake ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Maimuna Tarishi. Wapili kulia ni Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga  na kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Innocent Bashungwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika kikao kati yake na Mawaziri wa Kilimo, Viwanda na Biashara na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji pamoja na watendaji wa Taasisi ya Utafi wa zao la Michikichi alichokiitisha kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma, Februari 8, 2019.  Kulia kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angela Kairuki na kushoto kwake ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Maimuna Tarishi. (Picha na Ofisi ya Waziri  Mkuu)

Wadau wa Sekta ya Madini Wajadili Rasimu ya Mwongozo wa Ufungaji Migodi Dodoma.

WATUMISHI OFISI YA MWANASHERIA MKUU WATAKIWA KUTUNZA MITI WALIYOIPANDA

$
0
0
Kila jambo jemba huanza ni dua au sala, kabla ya kuaza kwa zoezi la upandaji miti, watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mafanya maombi mafupi kumwomba Mungu aikuze miti hiyo. Pichani watumishi wakiwa wameinamisha vichwa kumwomba Mungu ashushe baraka zake katika kazi yao.
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dr. Evaristo Longopa akipanda mti aina ya Ashok wakati zoezi la upandaji miti kwa watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Jumla ya miti 75 ilipandwa katika eneo linalozunguka kiwanja inapojengwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, katika Mji wa Serikali huko Ihumwa nje kidogo ya Jiji la Dodoma. Dr. Longopa alitoa wito kwa watumishi hao kuwa wasiishie kupanda tu bali pia kuitunza ili ikue na kupendezesha mandhari ya Ofisi na kuhifadhi mazingira.
Watumishi wakiwa wametawanyika wakiendelea na zoezi la kupanda miti aina ya Ashok na Miti Dodoma katika kwanja panapojengwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali zaidi ya miti 600 ikiwamo ya matunda inatarajiwa kupandwa katika eneo hilo.
Baada ya kupanda miti Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliwaongoza watumishi katika kuangalia kazi ya ujenzi wa Ofisi yao ilivyokuwa ikiendelea. Pichani Naibu Mwanasheria Mkuu akiongozwa na Injinia Suma Atupele kukagua kazi ya ujenzi inavyoendelea.
Naibu Mwanasheria Mkuu akiangalia mabati yatakayotumika kuenzekea Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali huku Injia Suma Atupele akitoka maelezo


Na Mwandishi Maalum, Dodoma 

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dr. Evaristo Longopa amewataka watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhakisha kwamba, miti waliyoipanda leo inatunzwa ipasavyo na kukua ili ipendezeshe mandhari ya Ofisi na kuhifadhi mazingira. 

Dr.Longopa ametoa wito huo leo, Ijumaa, wakati alipowaongoza watumishi wa Ofisi yake katika zoezi la upandaji miti, katika kiwanja inapojengwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika Mji wa Serikali huko Ihumwa nje kidogo ya Jiji la Dodoma. 

Miti ambayo imepandwa katika zoezi hilo ni 75 kati ya 640 inayotarajiwa kupandwa katika eneo hilo. Miti hiyo 75 ni aina ya Ashoki na Miti Maji au maarufu kama miti Dodoma imepandwa kama sehemu ya mpaka wa kiwanja cha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. 

“Watumishi wenzangu, leo tunazindua zoezi la kupanda miti 75 kati ya 640 ikiwamo ya matunda ambayo tutapanda katika eneo letu. Upandaji huu wa miti unayo malengo tuseme mawili, kwanza kupendezesha mandhari ya eneo la Ofisi yetu ili yawe ya kuvutia na pili ni kuhifadhi mazingira. Niwatake basi tusiishie kupanda tu bali kila mmoja wetu ahakikishe anatunza miti hii ili iweze kukua na kustawi”. Akasema Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. 

Pamoja na Naibu Mwanasheria Mkuu kuongoza na kushiriki zoezi hilo, wangine walioshiriki ni pamoja na Mkurugenzi wa Mipango Bi. Nkuvililwa Simkanga na Bw. Jackson Nyamihula ambaye n Mkurugenzi wa Utawala na Raslimali watu. 

Kwa upande wao watumishi hao wakionesha kufurahia zoezi hilo la upandaji miti, baadhi walipendekeza kwamba kila aliyepanda mtu aweke alama yake ili kuhakikisha kwamba kila mmoja anautunza mti wake. 

Baada ya zoezi la upandaji miti, Naibu Mwanasheria Mkuu alikwenda kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Ofisi ambapo mmoja wa ma – Injinia anayesimamia ujenzi huo Injinia Suma Atupele alimweleza Naibu Mwanasheria Mkuu kwamba kazi inaendelea vizuri ambapo kazi mbalimbali zikwamo za uchapiaji na upakaji rangi na nyinginezo nyingi zimekuwa zikiendelea kwa kasi ya kuridhisha. 

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali 
Dodoma

Viwanda 3,504 Vimeanzishwa Nchini

$
0
0
Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.

Jumla ya viwanda 3,504 vimeanzishwa nchini kutokana na juhudi za kujenga uchumi wa viwanda zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano tangu iingie madarakani hadi kufikia Desemba, 2018.

Hayo yameelezwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Chumbageni, Mhe. Ussi Salum Pondeza juu ya viwanda vingapi vimeanzishwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda.

"Kati ya viwanda hivyo 3,504 vilivyoanzishwa, vinajumuisha viwanda vidogo sana 2,500, viwanda vidogo 943, viwanda vya kati 51 na viwanda vikubwa 10," amesema Mhandisi Manyanya.

Amesema wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina imekuwa ikifanya tathmini ya viwanda 156 vilivyobinafsishwa na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa kwa viwanda 68 ambavyo havijaendelezwa.

Aidha amesema, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilijiridhisha na mapendekezo yaliyotolewa na kuiwezeshsa Ofisi ya Msajili wa Hazina kuchukuwa hatua.

Mhandisi Manyanya amesema hatua iliyochukuliwa na Ofisi ya Msajili ni kuvirejesha viwanda 14 Serikalini na juhudi za kuvitafutia wawekezaji wengine walio tayari kuviendeleza zinaendelea.

Ameeleza kuwa, kwa mujibu wa hali ya uchumi ya mwaka 2017, mchango wa sekta ya viwanda katika Pato la Taifa ni asilimia 5.5 ikilinganishwa na asilimia 4.9 mwaka 2016, sawa na ongezeko la asilimia 0.6.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya 

Kiwanda cha Kuunga Trekta Chawakomboa Wakulima Wadogo

$
0
0
Trekta aina ya URSUS likiendelea na kazi yakulima mashamba ya wakulima katika Wilaya ya Malinyi mkoani Morogoro.
Kazi ya uunganishaji matrekta katika Kiwanda cha Kuunganisha Trekta kilichopo Kibaha mkoani Pwani ikiendelea ikiwa ni juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kufufua na kukuza sekta ya Kilimo hapa nchini ambapo matrekta zaidi ya 200 yameunganishwa na kuuzwa kwa wakulima mbalimbali nchini.
Moja ya Trekta aina ya URSUS likiwa limekamilika. 
Matrekta yaliyounganishwa yakiwa tayari kuuzwa.

Sehemu ya majembe ya matrekta ya URSUS yakiwa tayari yameunganishwa Kiwandani Kibaha mkoani Pwani.
Trekta aina ya URSUS likiendelea na kazi yakulima mashamba ya wakulima katika Wilaya ya Malinyi mkoani Morogoro.
 
Mkulima kutoka Wilaya ya Gairo, Haji Salum akifanyia majaribio ya kuendesha trekta aina ya URSUS mara baada yakukabidhiwa trekta hilo alilonunua kutoka Kiwanda cha kuunganisha matrekta kilichopo Kibaha mkoani Pwani. (Picha na MAELEZO)

Na: Lilian Lundo - MAELEZO

Kiwanda cha Kuunganisha Trekta Aina ya URSUS kilichopo Mkoani Pwani kimekuwa mkombozi mkubwa kwa wakulima wadogo kutokana na masharti nafuu ya ukopeshaji wa trekta hizo.

Kutokana na urahisi wa upatikanaji wa trekta hizo umepelekea kuongezeka kwa idadi ya wakulima wenye trekta ambazo zimekuwa zikiwalimia wakulima wadogo wadogo kwa gharama nafuu.

Akizungumia Trekta hizo, Mkulima wa zao la Mahindi na Alizeti kutoka Gairo, mkoani Morogoro, Haji Salum ambaye alikutwa kiwandani hapo akichukua trekta aliyoinunua kwa mkopo, ameeleza kuwa anafuraha kubwa ya kumiliki chombo hicho ambacho atakitumia kulimia mashamba yake pamoja na wakulima wenzake.

"Ninayofuraha kubwa kupata chombo hiki ambacho sikutarajia kukimiliki katika maisha yangu. Ninamshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kauli mbiu yake ya ujenzi wa viwanda ambayo imetuwezesha hata sisi maskini kumiliki trekta," amesema Salum.

Mkulima huyo anayemiliki heka 120 za mashamba ya mahindi na alizeti mkoani humo amesema, kwa kulima mashamba yake peke yake anauwezo wa kurejesha fedha ambazo zimebaki kukamilisha malipo ya trekta hiyo anayoimiliki.

Mkulima huyo amewashauri Watanzania kujitokeza kwa wingi kununua trekta hizo kwani masharti yake ni nafuu na zipo kwa ajili ya kila Mtanzania hata wale wenye kipato cha chini.

Aidha, mmiliki mwingine wa trekta hizo kutoka Wilaya ya Malinyi, Mkoa wa Morogoro Jacob Mbifile ameishukuru Serikali kwa kupata trekta kwa gharama nafuu ambayo anaitumia kulima mashamba yake pamoja na kuwalimia wakulima wenzake kwa kuchangia kiasi kidogo kwa ajili ya marejesho ya mkopo na uendeshaji wa chombo hicho.

"Kwa sasa tunalima kwa wakati, kutokana na uwepo wa trekta nyingi, tofauti na ilivyokuwa zamani, ambapo wakulima wengi walikuwa wakipata huduma ya kulimiwa kwa kuchelewa kutokana na uchache wa trekta uliokuwepo hivyo kusababisha kuvuna mazao machache kutokana na kuchelewa kupanda," ameeleza Mbifile.

Kwa upande wake, Mkulima wa zao la Mpunga Wilayani humo, Ladislaus Kidunda amesema kabla ya uwepo wa trekta hizo, kulikuwa na uhaba mkubwa wa trekta hivyo kusababisha foleni kubwa ya kusubiri trekta ili kulimiwa.

"Kipindi cha nyuma tulikuwa tukipata huduma ya kulimiwa kwa trekta kwa tabu sana kutokana na wamiliki wa trekta hizo kuwapa kipaumbele wale wenye mashamba makubwa kuanzia heka 10 na kuendelea. Tofauti na ilivyo sasa ambapo wamiliki wamekuwa wengi hata sisi wenye heka mbili au tatu tunaweza kupata huduma hiyo kwa wakati," amesema Kidunda.

Nae Msimamizi Mkuu wa Kiwanda hicho, Godwin Mubi amesema mpaka tarehe 15 Januari mwaka huu, jumla ya trekta 261 zimenunuliwa kwa njia ya mkopo katika mikoa ya Manyara, Mwanza, Dodoma, Ruvuma, Singida na Morogoro na mikoa mingine ikiwa kwenye mchakato wa kununua trekta hizo.

"Tunakopesha trekta hizi kwa kila Mtanzania anayehitaji, ambapo hutakiwa kutoa asilimia 25 ya gharama ya trekta na gharama inayobaki atairudisha kwa kipindi cha miaka miwili. Njia nyingine ni ile ambayo mkulima anaonesha dhamira ya kupata trekta, hivyo hulipia milioni 3 hadi 4 na kiasi kinachobaki hurejesha katika kipindi cha miaka miwili," amesema Mubi.

Aidha Mubi ameeleza, spea za trekta za Ursus zipo na zinapatikana kwa wingi nchini hivyo Watanzania watembelee kiwandani hapo kujua namna ya kumiliki trekta hizo kwani masharti na gharama yake ni nafuu.

Kiwanda cha Kuunganisha Trekta za Ursus ni kiwanda kinachosimamiwa na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) ambapo huunganisha Trekta zinazokuja kwa vipande kutoka nchini Poland. Kiwanda hicho kilianza rasmi kufanya kazi Aprili, 2017 ambapo ni moja ya matunda ya kauli mbiu ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya ujenzi wa viwanda.

BREAKING NEWS: Ajali iliyotokea Bukoba, imeelezwa kutokea idadi kubwa ya vifo, eneo la Nyangonye

TANZANIAN LEADERS & PUBLIC FIGURES OWE IT TO THE NATION TO WRITE THEIR AUTOBIOGRAPHIES!!!

$
0
0
"An Autobiography is a self-written lifestory. A writer who writes an Autobiography is like a painter who paints a self-portrait. An Autobiography provides an opportunity for learning. As almost all the World Leaders and the Most Influential people in this century have published their Autobiographies, I urge my fellow Presidents and other Influential People in Africa to write their Autobiographies too"
NELSON ROLIHLAHLA MADIBA MANDELA, 7.3.1997.

Introduction:

Writing an Autobiography is pretty standard practice these days all over the world. In the West, since time immemorial, it is an unwritten law that Presidents and other Public Figures document their ups and downs, detailing crucial hitherto untold stories. H.E ABRAHAM LINCOLN, the 16th US President and arguably the Most brilliant US President ever, for example, wrote three Autobiographies!.

Autobiographies, since they are personal accounts, have become the most accurate source of information about Public leaders' success and failure secrets. For them, this is not only an opportunity to tell their lifestories but also it is an opportunity to put the record straight regarding various issues including controversies that were misrepresented or opinions they could not air while holding certain positions. It is their means to excercise their right to reply.

In the African continent, where for decades history was mostly narrated by oral tradition, few Public leaders have published their Autobiographies. In BONGOLAND, as shown herein below, about 99% of serving and past leaders have not published their Autobiographies!.

In my humble view, the absence of these Autobiographies denies the current and future generations in BONGOLAND the right to hear it from the horse's mouth considering that this country has gone through numerous undocumented momentous happenings.

1. H.E Mwalimu Julius Kambarage NYERERE:


The Founding Father of our nation, the late Mwalimu NYERERE, served as the first President of our beautiful country. When died on 14.10.1999, he left a good number of books. However, I have noted with grave concern that although Mwalimu was a man of great knowledge and wisdom, he died without having written his Autobiography!.


I fail to understand as to why Mwalimu, of all people, did not deem necessary to leave the world with anything in the form of an Autobiography bearing in mind that H.E President BENJAMIN WILLIAM MKAPA said, on the occassion of State funeral, on 21.10.1999, that "Mwalimu NYERERE was a voracious reader of books who had unquenchable thirst for knowledge and an unending desire to impart knowledge to others".

May be Mwalimu was uncomfortable with his domestic scorecard or may be events like the 1964 army mutiny, the blanket nationalizations, the two treason cases, the forcible removals of peasants or the acute shortage of commodities,  would have been embarassing episodes to narrate!.

Mwalimu, in his heyday as President of TZ,  did a commendable job. He took over a country with 85% of its adults illiterate. The British ruled Tanganyika for 42 years and when they left, there were only 2 engineers and 12 doctors. But when Mwalimu steped down in October 1985, there was 91% literacy and nearly every child was at school and hundreds of engineers, doctors and lawyers had been trained! Furthermore, Mwalimu was the archtect of our unique Union and the one who fused TZ's 120 tribes into a cohesive state.

On the international scene, Mwalimu was one of Africa's independence heroes and a leading light behind the creation of the OAU on 25.5.1963. On several occassions during his presidency, Mwalimu sent his armed forces abroad, either to expel an invader (Uganda), to stablize a friend (Seychelles) or to shore up another friend (Mozambique).

In his retirement, he did more than any other person to chaperone TZ into Multi-party politics, often in the teeth of opposition from bigwigs within his party, CCM. On this basis, surely, Mwalimu ought to have documented his life.

On a number of occassions when confronted, Mwalimu used to say that he was averse to writing his Autobiography claiming that his life amounted to nothing to write home about!.


Just before Mwalimu died, three intellectuals; to wit, Prof. AHMED MOHIDDIN, Prof. HAROUB OTHMAN and former ambassador FERDINAND RUHINDA, had approached him to seek his consent to assist him to write his Autobiography. After lenghthy discussions, Mwalimu finaly obliged and duly granted his consent. The modus operandi  was that the trio were going to sit with him whenever he had time and write his own words and then he would go through the manuscript because they wanted it to be his own work. They were just going to assist him to write. It is just sad that he departed before the project could take off. 


It is our loss that Mwalimu passed on without having written an Autobiography!.

2. H.E Alhaj Ali Hassan MWINYI;

H.E MWINYI, who served as the 2nd President of TZ, is yet to write the story of his life and it seems, at 94, it will remain a secret known to him and a few close allies!. This is sad bearing in mind that H.E MWINYI, who is the only person in history to serve as President in both parts of the Union, has an avalanche of stories to tell.

During his tenure as President, he was admired by many people who nicknamed him "Mzee Rhuksa" as it was during his presidency that TZ made some of the crucial decisions towards the liberization of its economy that paved the way for economic growth after he had inherited a near bankrupt country!.

His tenure was, on the other hand, clouded by a number of challenges such as the IMF conditions, the push for ERPs and a series of unending strikes at Udsm like the infamous 1991 Kunji that, inter alia targeted him personally, with some radical students calling him names "Matusi ya nguoni"!.

Furthermore, between 1990 and 1995, he rode the waves of the Multi-party system introduced in 1992 and also faced rabel MPs from his own party, CCM, popularly known as G55 who were strongly demanding a Tanganyika government within the Union, forcing Mwalimu to step in and majestically silence all the dissenters!.


Living in the shadow of Mwalimu was, ipso facto, a challenge. We all remember how Mwalimu used to frequently launch thinly-veiled attacks on MWINYI's leadership, accusing it of corruption and failing to defend the Union.


In view thereof, it is unfortunate that H.E MWINYI has not published his Autobiography hence denying us important detailed information regarding his lifestory.

3. H.E Benjamin William MKAPA:

H.E MKAPA served as the 3rd President of TZ. Though I believe that his recollections are worth penning, it seems and I stand to be corrected, he has chosen to follow the path of his two predecesors. This is, indeed, very sad as he is the one I was expecting to be a trailblazer considering his background in journalism and the fact that it is well documented that he is a bookworm/a great lover of books!.

H. E MKAPA, just like his predecessors, weathered many storms ranging from the first Multi-party General elections in 1995 to the MV Bukoba disaster on 21.5.1996. 

Moreover, it was during his tenure that Mwalimu died on 14.10.1999 and it was a monumental task to ensure that the father of the nation was laid to rest peacefully. H.E MKAPA faced a bloody demonstration in Zanzibar on 27.1.2001 organized by CUF to protest the victory of then President AMANI ABEID KARUME. Dozens of demonstrators were killed and hundreds fled to Somalia and Europe.

There is also the much talked about privitization excercise. Moreover, there were his days as the Managing Editor of the Daily News and in 1974 when Mwalimu, after he had recognized his talents and potential , appointed him his press Secretary. Then there is his life as a diplomat and Foreign Affairs Minister. Furthermore, Tanzanians want to hear from the horse's mouth as to how he defeated Hon. JAKAYA MRISHO KIKWETE in the second round of voting in 1995 without forgetting the accident which occured in October 1995 when he narrowly survived a road accident in Mwanza while campainging when a defective bus almost hit his car. 38 people were killed in the bizzare accident, the majority being CCM members who had lined the Mwanza-Musoma road to see his entourage. Tanzanians want all untold stories, eversince he was born in Ndanda, Masasi on 12.11.1938, documented!.


H.E MKAPA's failure to publish his Autobiography means his lifestory will be buried in the sand! I strongly advise him to put pen to paper and write about his life as he has had a remarkable life full of ups and downs, joys and sorrows, as he himself revealed at St. Immaculate, Upanga on his 80th birthday, last year.


I believe he has so many interesting untold stories that he never had the chance to tell. This is now his golden opportunity. Although he is now 80 years old but, without any shadow of doubt, he is in full control of his faculties and has a razor-sharp memory.

Your Excellency, BWM, the ball is in your court!.

4. Tanzania's Ex-Prime Ministers:

With the exception of Dr. SALIM AHMED SALIM, none in the list of Tanzanians who have been privileged to serve as PMs and are still alive todate, namely Hon. CLEOPA DAVID MSUYA, Hon. JOHN SINDE WARIOBA, Hon.JOHN SAMWEL CIGWEYIMISI MALECELA, Hon. FREDRICK TRUWAY SUMAYE and Hon. EDWARD NGOYAYI LOWASSA, has published his Autobiography. Why they have chosen the code of silence is the Billion-dollar question!.

Dr. SALIM, a trusted protege and emissary of Mwalimu, wrote his 106 page Autography titled "SALIM AHMED SALIM: SON OF AFRICA" which was launched in January 2016.

I believe that all the abovenamed PMs have some wonderful and insightful stories to tell the current as well as the future generations.

Apart from these PMs, other Public leaders such as ambassadors and ministers have not published their Autobiographies either.

Worse still, they are not alone. Also in the list are famous athletes, artists, footballers and prominent people in the bussiness community whose success and failure are worth documenting. Hon. REGINALD ABRAHAM MENGI and Sir JAYANTILAL "ANDY" CHANDE are the only exceptions.

5. Our Influential & Inspirational Women in Tanzania:

At a time when gender equity is a global agendum, who would not want to read an inspirational account of the life of (1) Dr. ASHA ROSE MIGIRO, notable as the only woman in TZ to get a First Class Hons Degree in Law at Udsm & former UN Deputy Secretary General, (2) Mama TABITHA IJUMBA MWAMBENJA SIWALE, the First Female Minister in TZ, (3) Hon. ANNE SEMAMBA MAKINDA, the First Female Speaker in the TZ male-dominated National Assembly, (4) Hon. SABETHA JOHN MWAMBENJA, the First Female MD & CEO of a Commercial bank in TZ (5) Hon. JULIE CATHERINE MANNING, the First Female Judge in  East Africa, (6)Dr. GETRUDE IBENGWE MONGELA, the First President of the Pan African Parliament, (7) Prof. ESTHER MWAIKAMBO, the First Female doctor in TZ, (8) Hon. AMINA SALUM ALI, the First Female African Union Ambassador to US, (9) Hon. Ambassador FATUMA TATU NURU, the First TZ Female Ambassador, (10), Ms ELIZABETH OLOTU, the First Female Pilot in TZ, (11) Hon. ANNA MARGARETH ABDALLAH, the First Female DC & RC in TZ and the one and only Mama MARY KAMM, the First Tanzanian Female to get a degree?!.

These are incredible women who broke new ground and achieved FIRSTS in various fields. They have a lot of life experiences to share with the world hence we can't wait for their unique Autobiographies!.

6. There is light at the end of the tunnel!

Hon. FREDRICK TRUWAY SUMAYE has promised to write an Autobiography, to quote him verbatim:
"I will definately write an Autobiography but I have not yet started. I am seriously thinking about it. People have the right to know and there is a lot they can learn from us".

Betterstill, while Hon. SUMAYE is seriously thinking about it, H.E JAKAYA MRISHO KIKWETE will, later this year, launch his Autobiography titled : "THE JOURNEY OF MY LIFE: FROM A BAREFOOT SCHOOLBOY TO PRESIDENT". But what prompted him to write the said Autobiography? He says:

"After retiring from my presidency in 2015, I sat with my family, friends and former workmates who pushed me to write something. In April 2018, at the New York University, I was advised by one of my professors to write down my memoir.  My Autobiography is focused on history and political issues and I am positive that historical and political academicians will like it".

CONCLUSION:

Tanzanian leaders & other Public figures (Politicians, Celebrities & other Influential People) owe it to the nation to write their Autobiographies for enlightening other people especially the Dot.com generation and for posterity.

AUGUSTINO RAMADHANI: MZALENDO MBOBEVU MWENYE VIPAJI MUJARAB NA REKODI LUKUKI ZA KIPEKEE TZ.

$
0
0

1. Usuli:

Ijumaa ya tarehe 28.12.1945, Vita Kuu ya pili ya dunia ikiwa ndio inamalizika duniani, Mwalimu MATHEW DOUGLAS RAMADHAN na mkewe, Mwalimu BRIDGET ANA CONSTANCE MASOUD, wakazi wa Kisima-Majongoo, Zanzibar walibarikiwa kupata mtoto wa kiume buheri wa afya, AUGUSTINO STEPHEN LAWRANCE RAMADHANI. Mtoto huyu alikuwa ni mtoto wao wa pili kuzaliwa kati ya watoto wao nane ambapo wavulana walikuwa ni wanne na wasichana wanne pia.

Ingawa familia hii ina majina mchanganyiko ya dini ya kiislam na kikristo lakini familia hii ni ya kikristo, madhehebu ya Anglikana.

2. Kuhamia Mpwapwa:

Mwezi April mwaka 1952, Mwalimu MATHEW DOUGLAS RAMADHANI alihamishiwa Mpwapwa, Idodomia kwenda kufundisha, akiwa na familia yake huku AUGUSTINO akiwa na miaka saba.

3. Elimu:

3.1 Elimu ya Msingi:

AUGUSTINO alisoma shule ya msingi Mpwapwa kuanzia mwaka 1952 hadi 1953.

Baba yake akahamishiwa mkoa wa Tabora hivyo AUGUSTINO akasoma "Town school" darasa la tatu na la nne mwaka 1954 hadi 1956.

Mwaka 1957 hadi 1958 AUGUSTINO alisoma shule ya "Kaze Hill" (sasa Itetemia).

Mwaka 1959, Mwalimu MATHEW DOUGLAS RAMADHANI alirudishwa Mpwapwa baada ya kupandishwa cheo na kuwa "Headmaster" hivyo AUGUSTINO alimalizia elimu yake ya msingi Mpwapwa.

3.2 Elimu ya Sekondari:

Baada ya kufaulu vizuri masomo yake ya shule ya msingi, AUGUSTINO alichaguliwa kujiunga na shule maarufu iliyokuwa ikitayarisha vijana wa Tanganyika kuja kushika uongozi wa nchi, "Tabora Boyz" kuanzia mwaka 1960 hadi kumaliza kidato cha sita mwaka 1965. Akiwa shuleni hapo alijifunza mambo mengi ikiwemo kupiga piano ambapo pia alirithi kipaji cha babu yake ambaye pia alirithi jina lake, AUGUSTINO RAMADHANI. Aidha, alijifunza "basketball" aliyoimudu sana kutokana na wajihi wake kwani "amekwenda hewani".

4. Baba yake kufariki katika ajali ya treni UK:

Tarehe 1.3.1961, AUGUSTINO, akiwa kijana mdogo wa miaka 15 na mwanafunzi wa "Tabora Boyz", alipata pigo kubwa kuliko yote katika maisha yake baada ya baba yake, Mwalimu MATHEW DOUGLAS RAMADHANI, aliyezaliwa Zanzibar tarehe 11.9.1951,  akiwa masomoni nchini Uingereza kufariki katika ajali ya treni katika kituo cha Guidebridge Ashton Under-Lyne. Inadaiwa kifo chake kilichagizwa na ubaguzi wa rangi ambao ulikuwa umetamalaki vilivyo nchini Uingereza wakati huo ambapo inadaiwa alisukumwa na kukanyagwa na treni na akazikwa Southern graveyard, UK. AUGUSTINO, licha ya uchungu mkubwa wa kufiwa na mzazi wake huyo aliyekuwa wa kupigiwa mfano kwa maadili, akili na utanashati,  aliingiwa na hofu kubwa kuwa huo ndio ungekuwa mwisho wake kusoma kwa kukosa mtu wa kumlipia ada. Hata hivyo, aliweza kusoma na si tu kumaliza kidato cha sita bali pia kufaulu kwa kiwango cha juu.

5. Kujiunga na Chuo Kikuu:

AUGUSTINO alijiunga na Chuo Kikuu kusomea fani ya sheria, akiwa ni mmoja wa watanzania wa mwanzomwanzo kusomea fani hii ya kipekee.

6. "Kufyekelewa mbali" na Rais NYERERE

Mwaka 1966 kulitokea  mgomo wa kwanza mkubwa katika historia ya chuo hicho. Wanafunzi walikuwa wakipinga masharti ya kujiunga kwa lazma na JKT. Ingawa kuna baadhi ya wanafunzi hawakushiriki mgomo huo akiwemo AUGUSTINO, Rais NYERERE aligadhabishwa mno na kitendo hicho kisicho cha kizalendo hivyo "kuwafukuzilia mbali" wanafunzi wote. Wanafunzi hao, hata hivyo, walirejeshwa chuoni hapo mwezi Julai, 1967.

7. Kukata kadi ya TANU:

AUGUSTINO alikata kadi ya TANU na akawa mwanachama wa "TANU Youth League", akiwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu, mwaka 1969 katika tawi la Temeke.

8. Kumaliza Chuo Kikuu

AUGUSTINO alimaliza elimu ya Chuo Kikuu mwaka 1970 na kufaulu vizuri.

9. Kujiunga na JWTZ

Mwezi Machi 1970, baada ya kumaliza Chuo Kikuu, AUGUSTINO alijiunga na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

10. Kuoa

Licha ya kuwa mkristo, AUGUSTINO alimuoa laaziz wake, Bi. SAADA MBAROUK, ambaye ni mwislam, tarehe 1.11.1975.

11. Kuteuliwa Naibu Mwanasheria Mkuu ZNZ:

Mwaka 1978 ulikuwa ni mwaka wa mafanikio makubwa kwa AUGUSTINO.

Mwanzoni mwaka 1978, Rais wa pili wa Zanzibar, Alhaj ABDOU JUMBE MWINYI, alimteua kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, kikiwa ni moja ya vyeo vya juu kisiwani humo.

Mwaka huohuo wa 1978, AUGUSTINO alipata shahada ya uzamili ya Udsm, katika Sheria za Kimataifa.

12. Kurudishwa JWTZ

Mwezi Machi 1979, Mh. AUGUSTINO alirudishwa JWTZ na katika vita ya Kagera iliyorindima mwaka huo alipelekwa vitani ambako jukumu lake kubwa lilikuwa kuendesha mahakama za kijeshi.

13. Kuteuliwa  Jaji Mkuu ZNZ:

Mwezi Januari 1980, Mh. AUGUSTINO aliapishwa kuwa Jaji Mkuu wa Zanzibar, akiwa Luteni Kanali. Alihudumu cheo hicho hadi mwaka 1989.

14. Kuteuliwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa TZ

Tarehe 23.6.1989, Rais wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa TZ, Alhaj ALI HASSAN MWINYI "Mzee Rukhsa" alimteua Mh. AUGUSTINO kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania.

15. Kujiondoa Uanachama wa CCM

Mh. AUGUSTINO alijiondoa uanachama wa CCM mwaka 1992 baada ya mabadiliko ya Katiba ya nchi yaliyokataza majaji na wanajeshi kuwa wanachama wa vyama vya siasa.

16. Kuteuliwa M/Mwenyekiti NEC

Mwaka 1993, Rais MWINYI alimteua Mh. AUGUSTINO kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Alihudumu kwenye cheo hicho hadi mwaka 2003.

17. Kustaafu Uanajeshi

Mwaka 1997,  Mh. AUGUSTINO alistaafu rasmi JWTZ akiwa na cheo cha Brigedia Jenerali na kuagwa kwa heshma zote za kijeshi katika hafla ya kukata na shoka.

18. Kuteuliwa Jaji wa Mahakama ya Afrika Mashariki

Mh. AUGUSTINO aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Afrika Mashariki mwezi Novemba, 2001 na kuhudumu hadi mwaka 2007.

19. Kuteuliwa M/Mwenyekiti ZEC

Mh. AUGUSTINO aliteuliwa Makamu wa Mwenyekiti Tume ya Uchaguzi, Zanzibar (ZEC) mwaka 2002 hadi 2007.

20. Kusomea Uchungaji:

Mh. AUGUSTINO alisomea uchungaji Chuo Kikuu cha London nchini Uingereza ambapo mwaka 2004 alipata shahada ya uchungaji ( a Bachelor of Divinity).

21. Kuteuliwa Jaji Mkuu wa TZ

Mh. AUGUSTINO alipata heshma ya kipekee alipoteuliwa na Rais KIKWETE kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania mwaka 2007 na akahudumu kwenye cheo hicho hadi tarehe 27.12. 2010 baada ya kufikisha miaka 65, ambao ni muda wa kustaafa kwa lazima kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

22. Kuteuliwa Jaji wa Mahakama ya Afrika

Mwaka 2010, Mh. AUGUSTINO aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu.

23. Kurejea CCM

Mh. AUGUSTINO, baada ya kustaafu, alirejea uanachama wa CCM mwezi Septemba 2011 katika Tawi la CCM, Oysterbay.

24. Kutunukiwa Tuzo Maalum na Balozi wa Marekani

Tarehe 23.2. 2012, Mh. AUGUSTINO alitunukiwa Tuzo Maalum "Dr. Martin Luther King Award" na Balozi wa Marekani, Mh. ALFONSO LENHARDT kutonaka na utumishi wake uliotukuka na hivyo kuwa Mbongo wa 13 kupokea Tuzo hiyo mujarab.

25. Kuteuliwa M/Mwenyekiti Tume ya Katiba

Tarehe 7.4.2012, Rais KIKWETE alimteua Mh. AUGUSTINO kuwa Makamu Mwenyekiti Tume ya Katiba ambapo alitoa mchango mkubwa.

26. Kusimikwa MCHUNGAJI

Tarehe 28.12.2013, Mh. Jaji AUGUSTINO alitawazwa kuwa Mchungaji wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Zanzibar baada ya kuwa Shemasi kwa miezi sita. Mchungaji AUGUSTINO alitawazwa katika kanisa la Anglikana lililopo minara miwili, Unguja.

27 Kuteuliwa RAIS wa Mahakama ya Afrika:

Tarehe 14.9.2014, Mh. AUGUSTINO alichaguliwa Rais wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu baada ya kuonesha uwezo mkubwa akiwa jaji wa kawaida wa mahakama hiyo ambapo katika uchaguzi alipata kura 9 na hivyo "kumtimulia vumbi" mpinzani wake aliyeambulia kura kiduchu, nne tu! Mh. AUGUSTINO alihudumu katika cheo hicho hadi alipomaliza ngwe yake jumapili ya tarehe 3.9.2016.

28. Rais JK Amtunuku Nishani

Tarehe 9.12.2014, katika maadhimisho ya miaka 53 ya uhuru wa Tanganyika, Rais wa awamu ya nne, Dr. JAKAYA MRISHO KIKWETE, alimtunuku Mh. AUGUSTINO Nishani Maalumu ya utumishi uliotukuka.

29. "Kuingia-"fronti" kinyang'anyiro cha Urais

Mh. AUGUSTINO, aliushangaza umma, tarehe 15.6.2015 pale jijini Idodomia alipochukua fomu ya kugombea urais kupitia CCM na kuwa mmoja wa wagombea 42. Hata hivyo, tarehe 11 Julai 2015 "alichinjiwa baharini" na Kamati Kuu ya CCM iliyochuja majina hayo na kuibuka na majina matano tu ya Dr. ASHA ROSE MIGIRO, Mh. JANUARI YUSUPH MAKAMBA, Mh. BERNAD KAMILIUS MEMBE, Mh. AMINA SALUM ALI na DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI aliyeibuka kidedea.

30. Rekodi zake Kuntu za Kipekee

30.1 Mbongo pekee kuwa Jaji Mkuu Zanzibar na Tanzania;

30.2 Mbongo wa kwanza kuwa Jaji wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu;

30.3 Mbongo pekee kuwahi kuwa Rais wa Mahamaka ya Afrika ya Haki za Binadamu;

30.4 Mbongo pekee kuwa Jaji Mkuu kisha Mchungaji;

30.5 Mbongo pekee kuwa Jaji Mkuu na Brigedia Jenerali;

30.6 Mbongo pekee aliyejaliwa talanta nyingi kwenye tasnia tofauti (Jurist, Basketballer, Pianist, Army officer & Pastor). Mchungaji AUGUSTINO aliwahi kuwa Mwenyekiti wa " Tanzania Basketball Association". 

Mwisho

Huyu ndiye Mh. Mchungaji AUGUSTINO STEPHEN LAWRENCE RAMADHANI ambaye mkewe, Bi. SAADA MBAROUK RAMADHANI ni mwislamu aliyekuwa Luteni Kanali kabla ya kustaafu. Mchungaji AUGUSTINO ana watoto wanne ambapo wawili ni wavulana(FRANCIS & MATHEW) na wawili ni wasichana (MARINA & BRIDGET). 

Kwa hakika, Mchungaji AUGUSTINO ana historia ya kuvutia na ya kipekee!







SMARTLAB YAWAKUTANISHA VIJANA KWA LENGO LA KUWAJENGEA UWEZO

$
0
0



SMARTLAB imeamua kuunda mfumo maalumu ambao utawakutanisha vijana kwa lengo kuwajengea uwezo utakaowawezesha kufanya shughuli mbalimbali za ujenzi wa uchumi wao binafsi na Taifa kwa ujumla.

Miongoni mwa mambo ambayo vijana hao wanafundishwa na kuelekezwa ni katika mambo ya ujasirisamali, ubunifu wa kibiashara, kubuni miradi, kutafuta masoko na kuangalia namna ya masoko ya Tanzania yanavyoweza kutumika kuuza bidhaa zinazozalishwa nchini.

Akizungumza leo Februari 8, 2019 Meneja Mradi wa Smartlab Juliana Kayombo amesema kuwa miongoni mwa vijana ambao wamewakutanisha wamo pia  wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini ambapo kwa pamoja wanatumia nafasi hiyo kujeanga uwezo wa kufanya shughuli mbalimbali.

Amefafanua Smartlab hii ni mara ya tatu kupitia mradi wake wa kuwaunganisha vijana na kupitia Smartlab Founder to Founda wameweza kukutanisha vijana wengi na wapo ambao wamenufaika kwani wapo ambao wameweza kuanzisha kampuni zao na wengine wamefanikiwa kujiajiri na msingi wake ni baada ya kukutana na kupeana maarifa.

“Kupitia Smartlab vijana wa kada mbalimbali wanakutana na kujadiliana mambo mengi yanayohusu ujasiriamali, ubunifu , utafutaji masoko, uwezeshaji na namna ya kutumia fursa zilizopo nchini kuanzisha kampuni,”amesema.

Kwa upande wake Mwanzilishi wa Smartlab ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Smart Codes Limited Edwin Bruno amesema kuwa uwepo wao sasa umetoa nafasi ya vijana kukutana na kujadili mambo ya maendeleo.

“Ukweli ni kwamba sasa vijana wajasiriamali, wabunifu na wavumbuzi wa biashara za hapa nchini wana sehemu moja ya kukutana na kufanya kazi zao ambazo zitakutanisha na kukuza jumuiya za uvumbuzi zilizo tofauti na zenye vipaji hapa Tanzania na Afrika kwa ujumla,”amesema.

Wakati huo huo Mdhamini Mkuu wa Smartlab kutoka Raha Liquid Telecom Kumeil Abdulrasul amesema wanajivunia kuona kumeanzishwa  sehemu moja ambayo itawakutanisha watu wa kada mbalimbali na hasa vijana kwa lengo la kujengeana uwezo na kupeana maarifa kuhusu nini cha kufanya kuanzisha biashara, kampuni na shughuli nyungine za kiuchumi.

“Tumefurahishwa zaidi na hili eneo la ubunifu , kwetu sisi Raha Liquid Telecom moja ya mambo ambayo tumeyapa kipaumbele ni ubunifu ambao umetusaidia kufanya mambo makubwa.Nchi yetu inahitaji kuona tunakuwa na vijana wengi wabunifu ili tuendelee kusonga mbele kimaendeleo,”amefafanua. 






 Mwanzilishi wa SmartLab na Mkurugenzi Mtendaji wa Smart codes,Edwin Bruno akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu wavumbuzi ,Wajasiriamali na wabunifu wa  Tanzania sasa wana sehemu moja ya kukutana na kufanya shughuli  mbalimbali ili  kukuza jumuiya ya uvumbuzi  hapa Tanzania na Africa  kupitia  Smart codes.

Meneja Mradi wa SmartLab, Juliana Kayombo akiwaeleza waandishi wa habari utekelezaji wa miradi huo.leo jijini Dar es Salaam.
Meneja Mradi wa SmartLab, Juliana Kayombo (wa pili kulia) akifafanua jambo katika mkutano huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
Mwanzilishi wa SmartLab na Mkurugenzi Mtendaji wa Smart codes,Edwin Bruno  (kulia) akimshukuru  Mdhamini mkuu  kutoka Raha Liquid Telecom,Kumeil Abdulrasul, Bidhaa.
Wajasiriamali,wabunifu na wavumbuzi wakiwa katika mkutano wa kujadili mambo mbalimbali uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. 

WATU WANNE WAFARIKI AJALI YA GARI BUKOBA MKOANI KAGERA

$
0
0


Watu wanne wamepoteza maisha katika ajali iliyohusisha magari aina ya Canter lenye namba za usajili T223ATK na Hiace yenye namba za usajili T869 CHC kugongana katika Mlima Nyangoye eneo la Hamugembe Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.

Ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia leo Februari 8,2019.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Revocatus Malimi,ambaye amefika eneo la ajali ambayo imetokea katikati ya barabara,amesema watu wanne wamefariki dunia katika ajali hiyo.

"Canter ilikuwa Main Road ikitokea Rwamishenye ikiingia Mjini kati,baada ya ajali hiyo kutokea,magari hayo yalitoka nje ya barabara,bahati mbaya gari aina ya Hiace ilishika moto na watu waliokuwemo waliungua moto,tumeondoa maiti mbili za abiria na dereva mwenye hiyo Hiace pia dereva wa bodaboda aliyekuwa amefunganishwa kwenye hii ajali bahati mbaya amefariki,kwa hiyo jumla ya watu waliofariki katika ajali hii ni watu wanne,mpaka sasa maiti zipo hospitali ya Mkoa hazijatambuliwa"- RPC

"Bado tunaendelea na shughuli ya uokoaji na uchunguzi kubaini hasa nini chanzo cha ajali hii na atakayebainika kusababisha ajali,hatua za kisheria zitachukuliwa",amesema Kamanda Malimi.



Baadhi ya Wanachi wakitoa msaada wa kuinasua miili ya watu iliokuwa imenasa kwenye magari hayo
Watu wanne wamepoteza maisha katika ajali iliyohusisha magari aina ya Canter lenye namba za usajili T223ATK na Hiace yenye namba za usajili T869 CHC kugongana  uso kwa uso  katika Mlima Nyangoye eneo la Hamugembe Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.


TANZANIA NA AZERBAIJAN KUANZISHA USHIRIKIANO WA KIDIPLOMASIA

$
0
0

Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Modest J. Mero (kushoto) akisalimiana na Mwakilishi wa Kudumu wa Azerbaijan katika Umoja wa Mataifa, Balozi Yashar Aliyev jijini New York Marekani. Viingozi hao walikutana kwa ajili ya kusaini Makubaliano ya kuanzisha ushirikiano wa kidiplomasia baina ya Mataifa yao. 
Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Modest J. Mero (kulia) na Mwakilishi wa Kudumu wa Azerbaijan katika Umoja wa Mataifa, Balozi Yashar Aliyev wakiweka saini Makubaliano ya kuanzisha ushirikiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na Azerbaijan jijini New York, Marekani. Wengine katika picha ni maafisa wa ofisi za Balozi, Bi, Lilian A. Mukasa na Bw. Tofig F. Musayev. 
Balozi Mero na Balozi Aliyev wakiagana baada ya kusaini makubaliano ya kuanzisha ushirikiano wa kidiplomasia baina ya mataifa yao. 



MFANYABIASHARA KUJENGA MADRASA KASENYI SENGEREMA

$
0
0

NA BALTAZAR MASHAKA, SENGEREMA.

MKURUGENZI wa kampuni ya Baraka Mining inayojihusisha na uchimbaji wa madini ya dhahabu, almasi na vito, Baraka Chilu ameahidi kujenga madrasa itakayotumika kufundishia elimu ya dini hiyo, kununua pikipiki na mazuria ya msikitini hapo Kijiji cha Kasenyi wilayani Sengerema.

Pia Chilu ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri ya BAKWATA Sengerema alitoa fedha sh. 500,000 za kulipa posho ya miezi miwili ya mwalimu wa dini ya kiislamu, kati ya fedha hizo kiasi cha sh. 150,000 zitatumika kununulia baiskeli ya kumrahisishia usafiri wa kwenda na kurudi kutoa elimu kwenye shule za msingi na sekondari za Nyamahona.

Mgeni rasmi huyo wa maonyesho ya umahiri wa kuhifadhi Kuran na hadithi za Mtume Muhammad S.A.W.lililofanywa na wanafunzi wa madrasa ya Msikiti wa Kasenyi, alilionyeshwa kuguswa na changamoto ya wanafunzi hao kukosa sehemu sahihi ya kujifunzia elimu ya dini kutokan na risala iliyosomwa na katibu wa madrasa hiyo.

"Fanyeni tathmini ya gharama za ujenzi wa madrasa na nitakuwa tayari kuijenga.Kwa kuanzia natoa sh.500,000 za usafiri na posho ya mwalimu na baadaye nitamletea pikipiki mpya,nitanunua sare za wanafunzi wote 30 pamoja na mazuria ya msikitini,"alisema.

Awali akisoma risala Katibu wa Madrasa ya Msikiti wa Kasenyi,Hamidu Basinda alisema wana changamoto ya ukosefu wa jengo la madrasa kujifunzia, posho na usafiri wa mwalimu, sare za wanafunzi na maji kwa matumizi mbalimbali.

"Tunayo changamoto ya madrasa ya watoto kupata elimu ya dini na mazingira, tunatumia msikiti kutoa elimu hiyo, hakuna usafiri wa uhakika wa mwalimu kwenda kutoa elimu ya dini kwenye shule za umma.Changamoto ambazo zinakwamisha uislamu kustawi Kasenyi,"alisema Basinda.

Alisema licha ya uchumi wao mdogo wamefanikiwa kuboresha Msikiti wa Kasenyi kwa kuweka madirisha ya mbao na umeme kwa fedha walizouza mazao (vyakula anuwai) na kuimarisha nguzo za uislamu. 

Aidha, baada ya mfanyabiashara huyo kuahidi kujenga madrasa, Sheikh wa Msikiti wa Kasenyi Swadiki Mchwampaka ili kuunga mkono ufadhili huo aliwashauri waumini wa msikiti kuchangia nguvu zao.

"Shule ni biashara baina ya waja na Mwenyezi Mungu, tunahitaji kushikamana vizuri katika kuendeleza elimu ya dini (kiroho) na watoto ni haki yao kupata elimu ya mazingira na kiroho pia!Lakini pia ibada ndio msingi wa dini,inaleta heri na kukataa maovu,"alisema Sheikhe Mchwampaka na kuongeza;

"Usafiri umepatikana na tumeambiwa tutasaidiwa kujenga madrasa.Sasa na sisi tuchangie nguvu zetu ili kuunga mkono juhudi za mfadhili,."
Jengo la Msikiti wa zamani wa Kasenyi linalotumika kama madrasa ya kufundishia elimu ya dini ya Kiislamu likiwa nimechakaa na kupata nyufa na hivyo kuhatarisha Maisha ya wanafunzi.
  Mkurugenzi wa kampuni ya Baraka Mining, Baraka Chilu (kulia) akimkabidhi fedha sh.500,000 Sheikhe wa Msikiti wa Kasenyi Sheikhe Swadiki Mchwampaka kwa ajili ya posho ya mwalimu wa madrasa na kununulia baiskeli.Chilu ameahidi kujenga madrasa ya msikiti huo. 
  Sheikhe wa Msikiti wa Kasenyi Swadiki Mchwampaka (kulia) akimuonyesha Mkurugenzi wa Baraka Mining, Baraka Chilu (kushoto) jengo la msikiti wa zamani ambalo limechakaa lakini limekuwa likitumika kama madrasa. Picha na Baltazar Mashaka

MASAUNI AFUNGUA SEMINA YA VIONGOZI WA TAASISI ZA KIISLAM JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Serikali imesema haitakua tayari kuona Amani na Utulivu wa Nchi inachezewa huku ikisisitiza uwepo wa Umoja kati ya wananchi bila kujali tofauti ya imani, kabila au itikadi yoyote.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati akifungua Semina ya siku mbili iliyofanyika jijini Dar es Salaam ikiwahusisha Viongozi wa Taasisi za Kiislamu lengo ikiwa ni kuwakumbusha kuhubiri amani katika sehemu zao

Amesema muelekeo na malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kukuza maendeleo katika sehemu mbalimbali nchini lengo ikiwa kuinua maisha ya wananchi nan chi kwa ujumla

“Serikali hii imejidhatiti kuhakikisha maendeleo yanakuja kwa kasi na maendeleo hayawezi kuja ikiwa amani na utulivu haupo, sisi kama serikali tutahakikisha tunalinda amani iliyopo ili wananchi wapate kufanya shughuli za kiuchumi bila wasiwasi wowote” alisema Masauni

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Mussa Salum aliihakikishia serikali kutokuwepo kwa mifarakano kati ya taasisi mbalimbali kama ilivyokuwepo awali huku akisisitiza kuendelea kwa umoja huo ili jamii ipate kuendelea

“Sisi kama Bakwata tunaihakikishia serikali uwepo wa umoja na ushirikiano baina ya baraza na taasisi zingine na tofauti zetu hazipelekei kukoseana au kuvunjiana heshima kwahiyo tunaomba serikali iamini uwepo wa maelewano mazuri tu kwa maendeleo ya nchi hii” alisema Sheikh Mussa

Semina hiyo ya Siku mbili imejumuisha viongozi wa Taasisi mia moja huku mada ya Nafasi ya Taasisi za Kiislam katika Kuleta Umoja na Kuishi kwa Amani itajadiliwa.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Semina ya Viongozi wa Taasisi za Kiislam, ambapo aliwahakikishia uwepo wa Amani na Utulivu nchini.Ufunguzi huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Mussa Salum akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Semina ya Viongozi wa Taasisi za Kiislam, ambapo aliihahakikishia serikali kuwepo kwa maelwano kati ya taasisi mbalimbali za dini lengo ikiwa ni kurahisisha maendeleo nchini.Ufunguzi huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia) akisalimiana na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Mussa Salum baada ya kuwasili katika Ufunguzi wa Semina ya Viongozi wa Taasisi za Kiislam, uliofanyika leo jijini Dar es Salaam
Baadhi ya washiriki wakimsikiliza Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Semina ya Viongozi wa Taasisi za Kiislam, ambapo aliwahakikishia uwepo wa Amani na Utulivu nchini.Ufunguzi huo umefanyika leo jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

WATAALAMU WA UNUNUZI NA UGAVI WATAKIWA KUWA WELEDI KATIKA KUTIMIZA MAJUKUMU YAO

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Ununuzi na Ugavi(PSPTB),Godfred Mbanyi akizungumza na Wanafunzi wa utafiti wa Masuala ya ununuzi wakati wa kufunga semina ya watafiti hao, ambao wanafanya tafiti kwa mujibu wa mtaala wa bodi inavyotaka ili  wasajiliwe na kuhitimu mafunzo ya bodi, Pia mkurugenzi huyo alitumia wasaa huo kuwataka wawe waadilifu na wazalendo katika kazi hili kusaidia Taifa kusonga mbele
Mkurugenzi wa Mafunzo wa PSPTB,Amani Ngonyani akizungumza na Wanafunzi wa utafiti ambao wamemaliza mafunzo na wako tayari kwa ajili ya kuingia Mtaani kufanya tafiti ili waweze kufanya mitihani ya bodi hiyo.
Afisa Mahusiniano wa Bodi ya Ununuzi na Ugavi(PSPTB), Shamimu Mdee akizungumza na Wanafunzi hao kabla ya kumkaribisha kaimu Mkurugenzi wa bodi hiyo kutoa nasaha zake
Mmoja ya Wanfunzi wanokwenda kufanya tafiti  kuhusu masuala ya ununuzi na ugavi ,Noelia Richard akipokea cheti kutoka kwa kaimu Mkurugenzi wa bodi ya PSPTB, Godfred Mbanyi.
Mmoja wa Mwanafunzi wa Masuala ya Ununuzi na Ugavi Moerdekai Lasmon akipokea cheti kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Ununuzi na Ugavi SPTB),Godfred Mbanyi mara baada ya kumaliza mafunzo hayo.
Wanafunzi wa mitihani ya bodi ya Ununuzi na Ugavi (PSPTB) Walioshiriki katika semina ya siku tano iliyofanyika katika Ukumbi wa Msekwa kwenye Shule ya Sheria jijini Dar es Salaam.

RC CHALAMILA-MARUFUKU KUJIITA RAIS MBEYA

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila amesema ni marufuku mtu yeyote tofauti na Rais Dk. John Magufuli kujiita Rais au kiongozi yeyote kuingilia madaraka ya mwingine katika mkoa huo na kwamba kufanya hivyo ni kinyume cha Katiba, sheria na taratibu.

Akizungumza na waandishi wa habari Chalamila amesema upo mtindo wa baadhi ya wabunge kujiita marais na kwamba kufanya hivyo ni kosa kwani mbunge hawezi kuwa Rais na wala hawezi kufanya majukumu ya Rais.

Anasema ni vyema watu wajitambue na kila kiongozi kumiliki majukumu yake pasipo kuingilia nafasi au mhimili mwingine wa dola ili kuepusha migongano na mifarakano katika utendaji kazi wao.

“Nimesema watu wajitambue, ni marufuku wewe mbunge kujiita Rais kwasababu Rais ni Mhimili mwingine. Ni marufuku mimi mkuu wa mkoa kujiita Mbunge, ni marufuku mtendaji wa mtaa kujiita mtendaji wa kata au wa kata kujiita wa mtaa, kila mtu amiliki majukumu yake,” anasema na kusisitiza.

“Rais ni mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hatuna Rais mwingine labda wale ambao wanaandikwa kwa R ndogo na narudia tena Rais hawezi kuwa Mbunge na wala Mbunge hawezi kuwa Rais.

Anasema inashangaza sana kuona mtu kutoka mhimili mmoja wa dola anakwenda kuingilia mhimili mwingine na kwamba kujiita jina la mwingine si haki.Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa alisema licha ya kwamba mkoa huo umetawaliwa na viongozi wa upinzani hususan Halmashauri ya Mbeya mjini lakini wamekuwa wakishirikiana vizuri na serikali katika utendaji kazi.

Anasema linapokuja suala la utekelezaji wa mambo ya maendeleo baraza la madiwani limekuwa likiweka kando itikadio zao za vyama na kuwa kitu kimoja kupigania maslahi ya Taifa.

“Mkoa wetu hauna misigano kutokana na siasa, madiwani wanashirikiana vizuri na serikali na serikali imekuwa ikishirikana vizuri na madiwani katika kutekeleza miradi ya maendeleo bila kujali chama gani kinatawala katika eneo fulani ndiyo maana serikali ilipeleka Sh bilioni 700 katika kata ya Mzavua kwaajili ya ujenzi wa kituo cha afya licha ya kuwa kata hiyo ipo chini ya diwani wa Chadema ambaye ndiye Meya,” anasema Chalamila.

Anasema madiwani hao ndio waliopitisha uamuzi wazo lakela kuhamisha Sh milioni 300 kutoka shule ya Mkapa kwenda shule ya Azimo na kwamba kama kusengekuwa na ushirikiano wangeweza kugoma kupitisha wazo hilo.Hata hivyo alisema ipo haja ya wananchi kuendelea kuelimishwa na kuona kuwa serikali inapeleka maendeleo kwa wananchi si kwasababu ya vyama vyao.

Aliongeza kuwa katika kipindi alichofanya kazi katika mkoa huo amesimamia mambo mbalimbali ikiwemo ulinzi na usalama na kuondoa sifa mbaya ya mkoa huo kuwa mkoa wa mauji.Anasema mkoa huo umeendelea kufanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato, uboreshaji wa elimu na kuongeza ufaulu pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya afya, barabara na maji
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, akiwa katika Mahojiano Maalum na vyombo vitatu vya habari jijini Dar es Salaam 
Baadhi ya Waandishi wa Habari walioshiriki Mahojiano na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila jijini Dar es Salaam

--

WATEJA SITA BENKI YA NMB WAJINYAKULIA SIMU KALI KATIKA PROMOSHENI YA MASTA BATA

$
0
0


Meneja Huduma za Kadi wa Benki ya NMB, Bw. Stephen Jilala akizungumza wakati wa Promosheni ya washindi wa droo ya nane ya kampeni ya matumizi ya 'NMB Mastercard' au 'NMB Masterpass' inayojulikana kama 'MastaBatan iliyofanyika katika Tawi la Benki hiyo la Sinza Mori jijini Dar es Salaa. Kushoto ni Meneja wa Tawi la Benki hiyo la Sinza Mori, Mnkande Zawadi.
Tabitha Luhuja wa Benki ya NMB (wa pili kulia), akizungumza kwa njia ya simu na mmoja wa washindi wa droo ya nane ya kampeni ya matumizi ya 'NMB Mastercard' au 'NMB Masterpass' inayojulikana kama 'MastaBata. Kutoka kushoto ni Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Sinza Mori, Mnkande Zawadi, Sophia Mwamwita, Mkaguzi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Abdallah Hemedy na Bi. Saumu Rajabu kutoka Selcom.
Meneja Mahusiano Kitengo cha Kadi kutoka Makao Makuu ya Benki hiyo, Yusuph Achayo, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu promosheni hiyo.



WATEJA sita wa Benki ya NMB wamejishindia simu janja 'Samsung S9+' baada ya kuchezeshwa droo ya nane ya shindano la Benki hiyo ya kuhimiza matumizi ya 'NMB Mastercard' au 'NMB Masterpass' linalojulikana kama 'MastaBata'. Washindi hao wapya wanakamilisha idadi ya washindi 12 hadi sasa waliojishindia simu kama hizo katika shindano hilo.

Washindi walioshinda na kujinyakulia simu hizo wametajwa kuwa ni Taha Karimjee kutoka maeneo ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam, Gladys Gilbert, Salim Abdallah, Raphael Schuurmans wa Masaki jijini Dar es Salaam, Imara Noah wa Meatu na Burton Anyisile wa Kahama mkoani Shinyanga.

Akizungumzia kuhusu promosheni hiyo Meneja wa Benki hiyo Tawi la Sinza Mori, Mnkande Zawadi alisema wateja hao wamepatikana baada ya kuchezeshwa droo iliyojumuisha wateja wote wa NMB waliolipa au kufanya manunuzi kwa kutumia mfumo wa 'NMB Mastercard' au 'NMB Masterpass' na wao kujishindia zawadi za simu hizo.

Alisema katika droo ya mwisho washindi watatu watapata ofa ya kwenda kula 'Bata' Dubai huku wakiambataba na mtu mmoja wa kila mshindi ambapo jumla yao watakuwa sita na gharama zote za safari hiyo zitalipwa na benki hiyo kwa siku nne watakazo kuwepo nchini humo.

"Tunawaomba wateja wetu ambayo akaunti zao hazifanyi kazi wazifungue katika muda huu uliobaki wa promosheni hii ili waweze kushiriki na kushinda zawadi hizo pamoja na safari hiyo" alisema Zawadi.Meneja Mahusiano Kitengo cha Kadi kutoka Makao Makuu ya Benki hiyo, Yusuph Achayo , aliwaomba wateja wa Benki ya NMB kuendelea kutumia huduma hiyo ili kujiweka katika nafasi kubwa ya kuibuka mshindi na kwenda kula bata Dubai.

Katika droo ya kwanza wateja 100 wa Benki hiyo walifanikiwa kujishindia fedha taslimu shilingi 100,000/- kila mmoja huku wengine sita wakijishindia simu hizo za 'Samsung S9+' zenye thamani ya shilingi milioni 300.
Viewing all 110102 articles
Browse latest View live




Latest Images