Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109941 articles
Browse latest View live

NEWS ALERT: MAPIPA 75 YA MAFUTA YA DIZELI YAKAMATWA BANDARI BUBU KAWE BEACH,KINONDONI JIJINI DAR

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo (kulia) akikagua mapipa 75 ya mafuta ya dizeli yaliyokamatwa katika bandari bubu eneo la Kawe Beach, Dar es Salaam leo katika operesheni yake ya kupambana na magendo, nyumba kwa nyumba, mtaa kwa mtaa, ufukwe kwa ufukwe, mtu na mtu ili kukomesha biashara hiyo.
Mapipa 75 ya mafuta ya dizeli yaliyokamatwa katika bandari bubu eneo la Kawe Beach, Dar es Salaam leo katika operesheni yake ya kupambana na magendo, nyumba kwa nyumba, mtaa kwa mtaa, ufukwe kwa ufukwe, mtu na mtu ili kukomesha biashara hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo (kulia) akikagua mapipa 75 ya mafuta ya dizeli yaliyokamatwa katika bandari bubu eneo la Kawe Beach, Dar es Salaam leo katika operesheni yake ya kupambana na magendo, nyumba kwa nyumba, mtaa kwa mtaa, ufukwe kwa ufukwe, mtu na mtu ili kukomesha biashara hiyo.


Serikali wilayani Kinondoni, jijini Dar es S Salaam, leo imefanikiwa kuvamia bandari bubu ikiwa imehifadhi shehena ya mapipa 75 ya mafuta ya dizeli yaliyoingizwa nchini kinyemela ili kukwepa kodi. 

Mafuta hayo yamenaswa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo aliyeongozana na maofisa wa TRA, EWURA na vyombo vya usalama. 

Mfuta hayo yamekutwa yamehifadhiwa katika nyumba moja iliyopo Mtaa wa Kolekole, Kawe Beach, yenye namba KAW/MZN/1542. 

Chongolo alisema, mafuta hayo yamethibitika kwamba ni mafuta ya dizeli na Mamlaka ya Udhibiti wa Mafuta (EWURA) na kwamba pia wamejiridhisha ni dizeli na yameingia nchini kinyemela bila kufuata utaratibu. 

Alisema mapipa yako 75 ni sawa na lita 17,000 ambapo thamani yake kwa tathimini ya wali ni zaidi y ash.milioni 20. Ofisa Mfawidhi wa Kitengo cha Kuzuia Magendo cha Mamlaka ya Mapato Tanzania b(TRA) Hafidhi Abdallah, alisema wali tarifa ya kuwepo shehena ya mafuta katika eneo hilo tangu Januari 31 mwaka huu katika nyumba hiyo. 

Alisema wahusika walifanikiwa kutoroka na wanaendelea kuwasaka na kwamba mafuta hayo yatataifishwa .

TAMASHA LA PASAKA: MSAMA AWAONYA WASANII KUHUSU USAJILI NA VIBALI BASATA

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MAWAZIRI, WAKURUGENZI/WATENDAJI WAKUU WA SERIKALI LEO JIJINI DODOMA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Hussein Mwinyi (kutoka kushoto), Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Alphaxard Lugola, Waziri wa Katiba na Sheria Paramagamba Kabudi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Augustine Mahiga, ofisini kwake Mlimwa jijjini Dodoma Februari 3, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akioneshwa jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania Richard Mayongera, ofisini kwake Mlimwa jijjini Dodoma Februari 3, 2019. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akizungumza na Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga, ofisini kwake Mlimwa jijjini Dodoma Februari 3, 2019

Wananchi wa Igando Waanza Kupata Huduma ya Umeme

RAIS DKT.SHEIN AZUNGUMZA NA WAZIRI WA KILIMO NA MUSUALA YA ARDHI WA MISRI IKULU ZANZIBAR

$
0
0
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Waziri wa Kilimo na Masuala ya Ardhi wa Jamuhuri ya Kiarabu wa Watu wa Misri.Dkt.Ezzaldin O.Abusteit, alipofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzi, akiongozana na Ujumbe wake na kulia Balozi wa Misri Nchini Tanzania Mhe. Gaber Mohamed.(Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Waziri wa Kilimo na Masuala ya Ardhi wa Jamuhuri ya Watu wa Misri. Dkt. Ezzaldin.O.Abusteit, alipofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo na Rais Ikulu Zanzibar.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiongozana na mgeni wake Waziri wa Kilimo na Masuala ya Ardhi Jamuhuri ya Kiarabu ya Watu wa Misri.Dkt. Ezzaldin O.Abusteit, wakitoka katika ukumbi baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika Ikulu Zanzibar.3-2-2019.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiagana na mgeni wake Waziri wa Kilimo na Masuala ya Ardhi wa Jamuhuri ya Kiaranu ya Watu wa Misri Dkt. Ezzaldin .O. Abusteit, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika Ikulu Zanzibar.3-2-2019, anayefuata Balozi wa Misri Nchini Tanzania Mhe. Gaber Mohamed.(Picha na Ikulu)

RAIS WA UTPC AWATAKA WANAHABARI NCHINI KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA(NHIF)

$
0
0
Na Editha Karlo,Kigoma

RAIS wa umoja wa  vilabu vya waandishi wa habari Tanzania(UTPC) Deogratius Nsonkolo ,amewahimiza wanahabari watumie fursa ya umoja wa vilabu vyao, kujiunga na huduma ya mfuko wa  Bima ya afya (NHIF) kwaajili ya kupata kadi za matibabu na kuwa na uhakika matibabu wanapougua wao na familia zao.

Nsokolo ameyasema hayo jana Kigoma mjini wakati akifunga  Kikao kazi cha  wanahabari na viongozi wa mfuko wa bima ya afya ngazi ya Taifa  na mkoani humo lengo la kikao hicho ni kujenga mahusiano ya utendaji kazi baina ya Mfuko wa bima ya Afua Taifa(NHIF)na wanahabari wa Kigoma.

Alisema ni wajibu wa wanahabari kwa kupitia kalamu zao kuelimisha jamii umuhimu wa kujiunga na mfuko huo ili wawe na uhakika wa matibabu pale wanaugua.

"Hata sisi waandishi tunapaswa kuwa mfano katika suala hili la kujiunga na mfuko wa bima ya afya,kunabaadi hawana mikataba  ya kazi kwenye vituo vyao vya wanavyo fanyia kazi hivyo ni vyema tukanyima kwa fedha chache tunazopata tukajiunga kwani ugongwa ukija hauna taarifa unaweza ugumua huna hata mia ila ukiwa na kadi ya nhif unapata matibabu,"Alisema

Alisema inatakiwa sasa klabu za waandishi nchini ziweke mkakati wa kila mwanachama atoe fedha kwa utaratibu utakaokubaliana kila mtu atoe kidogokidogo hadi  kiasi cha fedha sh.76,800  na zipelekwe katika mfuko wa NHIF waweze kupata kadi za matibabu.

 Meneja Uhusiano wa Mfuko wa bima ya afya NHIF Taifa Anjela Mziray asema NHIF ina mahusiano mazuri na klabu za waandishi wa habari katika Mikoa yote hiyo ni kwaajili ya kufanya kazi kwa pamoja kama timu hali kama hiyo inachochea wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya afya ya CHF au NHIF.

"Niwaombe hata nyie Waandishi tumieni fursa ya Kikoa kujiunga na mfuko wa bima ya afya ,Serikali inataka kila mwananchi apate huduma bora za afya kuanzia vipimo na dawa kwa wakati,athari ya kutokuwa na bima ya afya ni janga kwa familia kukimbiana linapokuja suala la mchango wa kumtibia mgonjwa mfano,tatizo la kusafisha  figo Kwa mwezi unahitaji uwe na fedha si chini ya sh.milioni moja kwa mwananchi wa maisha ya kawaida ataweza?lakini ukiwa na kadi ya bima ya afya una kuwa na uhakika wa matibabu"Alisema

Ofisa Uthibiti na Uhakiki wa ubora NHIF mkoani Kigoma  Dkt . Daniel Kihaya amesema waandishi wa habari  wathubutu kutoa habari zenye kuibua uwajibikaji baina ya watumishi wa afya,mwanachama na huduma za mfuko huo ili,kukomesha tabia ya watumishi wa afya wanaokwamisha dhana ya bima ya afya kwa maslahi yao binafsi.

"Waandishi ni watafiti nyie muwe mnapita pita huko kwenye zahanati na hospital muibue mambo mbalimbali wanayafanya watoa huduma wasiowaaminifu kwa wanachama wa mfuko tukishirikiana tutakomesha tabia mbaya mbaya zote"alisema

Takimu inaonyesha hadi sasa wananchi waliojiunga na mfuko wa bima ya afya ya NHIF na CHF ni 32% kwa nchini nzima,lengo  kufikia 50%ifikapo mwaka 2020 huku Mfuko wa NHIF ukiwa ni miongoni mwa mfuko bora unaotambulika kimataifa kwa utoaji  wa huduma bora ya Afya (ISO ,901/2015) .

 Kaimu Meneja wa NHIF kigoma Emanuel Kileo ataja moja ya matarajio ya kuongeza wigo wa wanachama ni pamoja na ujio wa  uzinduzi wa kampeni ya  Ushirika afya na kusisitiza kutokana na mashirikiano  na vyombo vya habari na wandishi wake watafanikiwa  kuibua na kutokomeza kero ya ulaghai wa utoaji huduma kwa watumiaji wa Mfuko huo.

Meneja mahusiano wa mfuko wa bima ya afya Taifa(NHIF)Angela Mziray akiongea jambo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi baina ya waandishi wa habari wa Mkoa wa Kigoma na maofisa wa mfuko wa bima ya afya.

Sehemu ya waandishi wa habari wa Mkoa wa Kigoma wakisikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na maofisa wa mfuko wa bima ya afya (NHIF)

TanTrade yawashauri wazalishaji wa zao la Muhogo kuzalisha kitaalam

$
0
0


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Dkt Edwin P.Mhede akiongea na wadau wa Zao la Muhogo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa Zao la Muhogo ulioratibiwa na TanTrade na kufanyika katika ofisi za Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Zao la Muhogo wakiwa kwenye Mkutano wa wadau wa Zao la hilo ulioratibiwa na kufanyika katika ofisi za Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) jijini Dar es Salaam.
Mama MWANTUMU MAHIZA akizungumza na Wadau wa Muhogo baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji na Wachakataji wa Muhogo Tanzania
Mwenyekiti Msaidizi wa Chama cha Wazalishaji na Wachakataji wa Muhogo Tanzania Bw.Burton Mwankuru Nsape(Kushoto) akiwa na Katibu Msaidizi Bw.Victor Vedasto Kabegu(Kulia)
Afisa Masoko wa Kampuni ya EADL kwa kushirikia na TAEPZ akitangaza kununua Zao la Muhogo wakati wa mkutano na wadau wa zao hilo ulioratibiwa na kufanyika katika ofisi za Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) jijini Dar es Salaam.
Wajumbe wa Kamati ya Muda ya Uongozi wa Chama cha Wazalishaji na Wachakataji wa Muhogo Tanzania chenye lengo la kuwa na sauti ya pamoja katika kuendeleza zao hilo wakiwa katika picha ya pamoja kwenye mkutano wa Wadau wa Zao la Muhugo ulioratibiwa na kufanyika katika ofisi za Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) jijini Dar es Salaam.
Afisa Kilimo Mwandamizi kutoka Wizara ya Kilimo Bi Upendo Mndeme akizungumza kwenye mkutano wa mkutano wa wadau wa Zao la Muhogo ulioratibiwa na kufanyika katika ofisi za Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) jijini Dar es Salaam.

…………………………………………………………………….

Wazalishaji wa Zao la Muhogo nchini wameshauriwa kuzalisha zao hilo kitaalam, kwa ubora, kiwango kinachohitajika kwenye soko na kwa kutumia mbegu bora inayozalisha mavuno mengi.

Rai hiyo imetolewa na Dkt Edwin P.Mhede Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa Zao la Muhogo ulioratibiwa na kufanyika katika ofisi za Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) jijini Dar es Salaam.

“Wengi mnafahamu kuwa changamoto katika zao hili ni upatikanaji wa mbegu bora, aina ya mbegu inayoweza kukabiliana na magonjwa mbalimbali mabadiliko ya tabia nchi yanayosababisha uhaba wa upatikanaji wa mavuno ya kutosha na uzalishaji mdogo unaochagizwa na kilimo cha mashamba madogo madogo” alisema Mhede

Alisisitiza kwa kuiomba Wizara ya Kilimo na Vituo vya Utafiti vya Kilimo kuendelea kutafiti juu ya changamoto hizi na kuimarisha huduma za ugani zenye kulenga uzalishaji wa tija ili kupata mazao mengi zaidi.

Aliongeza kwa kusema kuwa kwa muda mrefu zao hili lilikuwa linategemewa kama zao la chakula pekee lakini kutokana na maendeleo ya uchumi na teknolojia kukuaa katika nchi zinazoendelea zimekuwa zikitumia Zao la Muhogo kutengenezea wanga ambao unatumika kwa matumizi mbalimbali viwandani vikiwemo viwanda vya karatasi, vinywaji na bidhaa kama nguo na makaratasi na kwa nchi nyingine wanatumia kuzalishia nishati mbadala aina ya Ethanol na kuzalisha sukari ya viwandani yenye ubora wa juu.

Naibu Katibu Mkuu aliendelea kusema kuwa Zao la Muhogo ni zao rasmi la biashara hivyo linasaidia katika kuongezea pato la taifa. Kwa takwimu zilizopo katika kipindi cha mwaka 2015/16 Zao la Muhogo lilichangia asilimia 13.63 ya pato la taifa huku likiajiri wakulima wadogo zaidi ya milioni 1.3 Kati ya mwaka 2012 na 2016 kiasi cha tani 59,447,754 za Muhogo chenye thamani ya Dola za Marekani 4,804,926 uliuzwa nje ya nchi.

Kwa upande wa masoko serikali inaendelea kuimarisha mfumo mzuri ambao utasaidia upatikanaji wa masoko hasa nje ya nchi. Zipo hatua zilizofanyika kwa nchi kama ya China yenye uhitaji wa Zao hilo kwa kuwa na mikataba ya pamoja uliohusu punguzo la ushuru wa forodha kwa bidhaa za Tanzania kuingia soko la China, mkataba wa itifaki ya Muhogo wa namna ya uingizaji wa zao hilo nchini China na kupitia mahusiano kati ya nchi na nchi. Na matokeo ya juhudi hizi zimeonekana kwa makampuni mbalimbali kutoka China kama vile Epoch Agriculture, Foshang Guangji Co. Ltd na Dar Canton Co Ltd zinazojishughulisha na ununuzi wa Muhogo na zikijiandaa kwa ujenzi wa viwanda nchini.

Nae Bw Edwin Rutageruka, Mkurugenzi wa TanTrade alisema kuwa lengo la mkutano huo ni kujadili changamoto zinazolikabili Zao la Muhogo ili kujua jinsi ya kulikabili ingawa changamoto kubwa katika uzalishaji wa Muhogo ni namna ya kuliongezea thamani ili kuepuka changamoto za kimasoko

Aidha aliongeza kwa kusema kuwa TanTrade itasimamia uanzishwaji na usajili wa Chama cha Wazalishaji na Wachakataji wa Muhogo Tanzania, lengo ni kuwa na sauti ya pamoja katika kuendeleza zao hilo. Chama hicho kitakuwa chini ya uangalizi wa TanTrade na makao makuu yake yatakuwa katika ofisi za TanTrade.

Bi Upendo Mndeme Afisa Kilimo Mwandamizi kutoka Wizara ya Kilimo amewashauri wazalishaji wa Zao la Muhogo ili liwe la Kibiashara hasa katika nchi ya China lazima wazingatie vigezo vilivyoainishwa katika itifaki ya soko la Muhogo ambapo baadhi ya vitu ni bidhaa za Muhogo zisiwe na visumbufu vya wadudu na magojwa, wazalishaji na makampuni ya kuuza Muhogo nchini China kutambulika Kisheria, ubora wa bidhaa, bidhaa zifungashwe kulingana na matakwa ya soko la China, ukaguzi wa bidhaa kabla ya kuvuna na Wizara ya Kilimo au Kampuni/ Taasisi iliyopata kibali cha Wizara kwa ajili ya kazi hiyo n.k

Baadhi ya Viwanda vya ndani vilivyojitokeza kununua Zao la Muhogo wamethibisha utoshelezi wa soko la ndani na uhitaji wao wa Zao hilo na wamehakikisha kuwa watalipandisha thamani Zao hilo kabla soko la nje kuwa na uhitaji mkubwa zaidi

Hadi sasa mikoa inayozalisha Muhogo kwa wingi ni Mwanza, Mara, Kagera, Shinyanga, Lindi, Morogoro, Tanga, Dar es Salaam, Pwani na Kigoma

Zaidi ya watu 130 wanufaika na uchunguzi wa awali wa kuangalia uvimbe kwenye matiti

$
0
0
Madaktari kutoka Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania-MEWATA- Dkt. Selina Mathias (kushoto) pamoja na Dkt. Deograsia Mkapa (kulia) wakiwaelekeza wananchi waliojitokeza kufanyiwa uchunguzi wa awali wa kuangalia uvimbe kwenye matiti bila kufanya upasuaji.
Baadhi ya wananchi wakisubiri kufanyiwa uchunguzi wa awali wa kuangalia uvimbe kwenye matiti katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila. Huduma hiyo imetolewa bure na Madaktari wa hospitali hiyo kwa kushirikiana na Madaktari wa MEWATA. 
Mtaalam wa Radiolojia kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila Dkt. Roselyne Okkelo (kushoto) akimpatia maelekezo Bi. Tima Kombo kabla ya kufanyiwa uchunguzi wa awali wa kuangalia uvimbe kwenye matiti. 
Dkt. Selina Mathias kutoka MEWATA (kulia) akimpima urefu na uzito Bi. Mage Hasunga mkazi wa Kigamboni.
Mtaalam wa Radiolojia kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila Dkt. Fadhili Seleman akitumia mashine ya Utrasound kumpima mteja ili kuthibitisha uvimbe ulioonekana.

Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania (MEWATA) leo wamehitimisha zoezi la kutoa huduma ya uchunguzi wa awali wa kuangalia uvimbe kwenye matiti bila kufanya upasuaji na kuhudumia watu zaidi ya 130. 

Akizungumzia zoezi hilo mtaalam wa Radiolojia wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila Dkt. Lulu Sakafu amesema zoezi hilo limefanyika bure kuanzia Februari 02 hadi Februari 03,2019. 

‘’Tumetoa huduma hii kwa siku mbili ambapo jana tumewafanyia uchunguzi watu zaidi ya 70 na leo tumewafanyia uchunguzi watu zaidi ya 60, kwa wale ambao wamekutwa na matatizo tumewapangia tarehe ya kurudi kwa ajili ya kuwafanyia uchunguzi zaidi’’. Amefafanua Dkt. Sakafu. 

Kwa upande wake Daktari kutoka MEWATA, Dkt. Selina Mathias ametoa wito kwa wananchi kujenga utamaduni wa kuchunguza afya zao mara kwa mara ili kupata matibabu kwa wakati.

MTOTO MWINGINE ADAIWA KUCHINJWA TENA NJOMBE

$
0
0


NJOMBE 

Mtoto mwenye umri wa miaka 7 anaefahamika kwa jina la Recho Malekela mkazi wa kitongoji cha Lung’angali kijiji cha Matembwe wilayani Njombe ameuawa kwa kuchinjwa koromoe na kutupwa katika msitu uliojirani na nyumbani kwao. 

Mtoto huyo wa darasa la pili katika shule ya msingi Matembwe ameuwawa ikiwa siku mbili zimepita tangu kikosi maalumu cha kiinteligensia kiwasiri mkoani Njombe kuongeza nguvu katika kuwasaka watu wanaotekeleza mauaji hayo ya kikatili dhadi ya watoto wadogo ambayo yaliomengi yanahusishwa na visasi pamoja imani za kishirikina. 

Akizungumza nyumbani kwa marehemu mara baada ya kushiriki mazishi ya mtoto Rachel na kutoa rambrambi kwa wafiwa Mbunge wa viti maalumu kupitia CCM Neema Mgaya amewata wananchi kuachana na tabia ya kushambulia watu watuhumiwa wa matukio hayo ya ukatili dhidi ya watoto pindi wanapo wabaini na badala yake wawafikishe katika vyombo vyenye dhamana ya ulinzi ili wahojiwe na kusaidia kubaini mtandao wa wauaji hao. 

Mgaya anatoa kauli hiyo ikiwa tayari watu wawili wameuawawa na wananchi wenye hasira kali wilayani Ludewa na Mmoja Wilayani Wanging’ombe baada ya kuhisiwa kujihusisha na matukio ya utekaji hatua ambayo imefanya jeshi la polisi kukosa taarifa kutoka kwa watuhumiwa. 

Awali akizungumza katika ibada ya kuaga mwili wa marehemu mkuu wa wilaya ya Njombe Ruth Msafiri amesema serikali imeshitushwa na mauaji yanayoendelea na kwamba tayari kikosi kilichosheheni wataalamu mbalimbali wa upelelezi kilichotumwa na mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Saimon Siro kimeanza kazi ya kuwabaini wahusika huku kikiwa tayari na kimewashikiria watu kaadhaa kwa mahojiano. 

Msafiri amesema mauaji yanayoendelea yanachafua sura ya amani na kudai kwamba damu ya mtoto Rachel itawatafuta popote walipo wauaji na kuwafikisha katika vyombo vya sheria . Baba mkubwa wa marehemu akizungumza na mwandishi wetu amesema mtoto huyo alitekwa mchana wa february mosi akiwa anatoka shambani jirani na nyumbani kwao baada ya kutumwa na mama mzazi kwenda nyumbani kupika maharage. 

Nae Bryson Mlote mwenyekiti wa kijiji cha Matembwe anaeleza historia ya matukio kama hayo kijijini hapo ambapo anasema inaelezwa miaka ya zamani kulitekelezwa matukio kama hayo na kwamba taarifa za kutekwa zianza kusambaa jioni ya februari mbili ambapo zoezi la kumtafuta lilianza saa kumi na mbili na kufanikiwa kumpata majira ya saa nne usiku katika msitu uliojirani na nyumba yao akiwa amekatwa shingoni na kitu chenye ncha kali. 

CAF: Gor yazima kidomodomo cha Zamalek ya Misri

$
0
0
Mabinga wa ligi ya soka nchini Kenya Gor Mahia walionyesha umahiri wao kwa kutoka nyuma na kupata ushindi mkubwa wa 4-2 dhidi ya klabu ya Zamalek kutoka Misri katika kombe la Shirikisho barani Afrika Caf katika mechi ya kundi D iliochezwa katika uwanja wa michezo wa kasarani jijini Nairobi.

Mshambuliaji wa Gor Mahia Jacques Tuisenge alifunga magoli mawili huku Nicholas Kipkurui akiongeza bao jingine na kufanya mambo kuwa 3-2 huku naye Ibrahim Hassan akiwafungia wageni hao magoli mawili kabla ya Denis Oliech kuingia kama mchezaji wa ziada na kuipatia Gor Mahia ushindi mkubwa 4-2 baada ya kucheza kwa utulivu.

Kipkurui alipofunga goli lake la kwanza la kimataifa alilazimika kutolewa katika kipindi cha pili baada vya kupata jeraha na nafasi yake ikachukuliwa na Oliech ambaye aliwapatia mabeki wa Zamalek matatizo makubwa.

Ushindi huo unaiweka Gor ahia katika nafasi nzuri katika kundi hilo huku wakitafuta tiketi ya kufuzu katika robo fainali ya michuano hiyo.

Katika uwanja wa Kasarani, mashabiki wa Gor Mahia walijitokeza kwa wingi, wakiwa na hamu ya kuiona timu yao iklipiza kisasi cha mwaka 1984 dhidi ya Wamisri hao ambao waliisababisha K'Ogalo kufungiwa katika michuano hiyo kwa miaka miwili.

Hali ilionekana kuwa mbaya mapema kunako dakika ya saba wakati timu hiyo ya nyumbani ilipofungwa bao la mapema kufuatia makosa ya Boniface Oluoch. lkaini Tuyisenge alisawazisha baada ya dakika 27 kabla ya kufunga tena baada ya pasi nzuri kutoka kwa Francis Kahata.

KUSOMA ZAIDI BOFYA BBC Swahili.

KISOMO CHA BI ZAINAB M. MWINYI NEW YORK

$
0
0

Ustadh Hajj Khamis na Ustadh Abbas wakiongoza kisomo cha Mama yake Ally Jecha Bi. Zainab M. Mwinyi kilichofanyika Mt Vernon New York siku ya Jumamosi. Ally Jecha ni Staff wa Tanzania Mission New York City.
Bi Zainab alifariki huko nyumbani Zanzibar, Tanzania.


BISMILLAH 
INNA LILLAHI WA INNA ILAYHI RAJ'OON


Ally Jesha akitoa shukrani kwa wa Community ya Watanzania New York baada ya kisomo


Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa, Mhe. Modest J. Mero akipata Ukodac na Ally Jesha baada ya Kisomo.




TEHAMA imerahisisha upatikanaji wa huduma – NHIF

$
0
0
5
6
Washiriki wa Mkutano wa NHIF na Wanahabari  wa Kigoma wakifuatilia ufafanuzi wa hoja zinazohusu huduma za Mfuko.
Meneja Uhusiano wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Anjela Mziray akizungumza katika mkutano wa Mfuko na Wanachama wa Chama cha Wanahabari wa Mkoa wa Kigoma.
2
Kaimu Meneja wa NHIF Kigoma, Bw. Emmanuel Kileo akiwasilisha mada kwa wanahabari wa Mkoa wa Kigoma.
3
Washiriki wa Mkutano wa NHIF na Wanahabari  wa Kigoma wakifuatilia ufafanuzi wa hoja zinazohusu huduma za Mfuko.
4
Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabari Mkoa wa Kigoma, Bw. Deogratius Nsokolo akifafanua jambo juu ya mchango wa wanahabari katika utekelezaji wa shughuli za Mfuko.
7
Picha ya pamoja kati ya Maofisa wa NHIF na Wanahabari wa Mkoa wa Kigoma

……………………………………………………………………………….

Na Grace Michael, Kigoma
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umeimarisha utekelezaji wa majukumu na kurahisisha huduma kwa uwekezaji kwenye mifumo ya TEHAMA inayomwezesha mwanachama kupata huduma kwa haraka zaidi pamoja na Watoa huduma kuwasilisha madai yao kwa haraka.
Maboresho haya yamefanyika na yanaendelea kufanyika kwa lengo la kuwarahisishia wanachama upatikanaji wa huduma na kuondokana na changamoto ambazo awali zilikuwepo za ucheleweshaji wa huduma mbalimbali ikiwemo utoaji wa vitambulisho na upatikanaji wa taarifa za wanachama.

Akizungumza katika mkutano baina ya NHIF na Wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Kigoma, Meneja Uhusiano wa Mfuko, Bi. Anjela Mziray alisema kuwa uimarishaji wa mifumo ya huduma unaofanywa na Mfuko umewezesha kutatua changamoto za upotevu wa muda kwa wanachama wanapokuwa vituoni, kurahisisha utambuzi wa mwanachama kabla ya huduma, lakini pia kurahisisha uwasilishaji na ulipaji wa madai ya Watoa Huduma.

“Lengo la Mfuko ni mwanachama wetu apate huduma kwa haraka na aweze kuwasiliana nasi kwa haraka anapohitaji, uimarishaji huu wa Mifumo ambao umefanyika na unaoendelea kufanyika, kwanza kabisa unawezesha upatikanaji wa taarifa za wanachama kwa haraka wanapokuwa katika vituo vya kupata huduma na inapotokea changamoto yoyote inatatuliwa kwa haraka zaidi tofauti na awali,” alisema Bi. Mziray.

Alieleza kuwa Mfuko sasa unaendelea na jitihada za kuwaunganisha watoa huduma wengi zaidi na mifumo hiyo ili waweze kuwasilisha madai yao kila siku mara huduma inapotolewa kwa mwanacha bila kusubiri mwisho wa mwezi. Hii inasaidia kushughulikia dai la mtoa huduma kila linapowasilishwa na hivyo kupunguza muda unaotumika kuchakata madai na hivyo kuongeza ufanisi. 

“Kwa sasa tayari kuna baadhi ya Watoa huduma ambao wameanza kutumia mfumo wa uwasilishaji wa madai kwa Mfuko kila siku na hatua hii mbali na kurahisha malipo lakini pia inaziba mianya ya udanganyifu na kuwezesha ulipaji wa madai halali yaliyotumiwa na wanachama,” alisema Bi. Mziray.
Akizungumzia suala la kuongeza wigo wa wanufaika wa huduma za NHIF, alisema kuwa Mfuko kwa sasa uko katika hatua za mwisho za kuanzisha utaratibu ambao utawezesha watu wengi kujiunga na kunufaika kwa namna mbalimbali kulingana na mahitaji yao.

 “Mipango yetu ni kuhudumia asilimia 50 ya wananchi ifikapo mwaka 2020 na badae kuwafikia wananchi wote hivyo maboresho na uimarishaji wa huduma tunaoufanya ni kujipanga na utoaji wa huduma kwa wananchi wote ili kila mtanzania aweze kupata huduma za matibabu kwa utaratibu rahisi wa bima ya afya,” alisema Bi. Mziray.

Naye Kaimu Meneja wa NHIF Mkoa wa Kigoma, Bw. Emmanuel Kileo alisema kuwa uwepo wa Ofisi ya NHIF mkoani hapo imesaidia kwa kiasi kikubwa kusogeza huduma kwa wananchi ambapo kwa sasa maofisa wa Mfuko wanawafikia wananchi mpaka ngazi ya kijiji na kuwapatia elimu ya umuhimu wa kujiunga na huduma.

Wakichangia hoja juu ya huduma za Mfuko, wanahabari wa Mkoa wa Kigoma, wameupongeza Mfuko kwa jitihada kubwa ambazo zimefanyika hususan katika kuyafikia makundi mbalimbali na kuboresha huduma za matibabu kwa wanachama wake.

Akitoa  shukrani kuhitimisha mkutano huo, Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabari wa Kigoma Bw. Deogratius Nsokolo alisema watauendeleza uhusiano uliopo baina yao na Mfuko huu  hususan katika kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kuwa na bima ya afya kabla ya kuugua.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 4,2019

NDITIYE AKABIDHI KOMPYUTA SHULE ZA SEKONDARI MPANDA

$
0
0
 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (katikati) akikabidhi kompyuta kwa Mbunge wa Mpanda Mjini, Sebastian Kapufi (wa pili kulia) kwa ajili ya shule za sekondari mjini humo. Wakishuhudia, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote, Mhandisi Albert Richard na Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Abdallah Malela (wa pili kushoto)

 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akifafanua jambo kwa viongozi wa Mkoa wa Katavi, Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda na waalimu wa sekondari (hawapo pichani) kuhusu ukuaji na maendeleo wa sekta ya Mawasiliano nchini. Kulia kwake ni Mbunge wa Mpanda Mjini, Mhe. Sebastian Kapufi na kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Abdallah Malela 

 Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote, Mhandisi Albert Richard akitoa maelezo ya kompyuta walizotoa kwa shule za sekondari za Mpanda. Walioketi wakimsikiliza, wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye na  katikati ni Mbunge wa Mpanda Mjini, Sebastian Kapufi

 Afisa Elimu wa Shule za Sekondari wa Manispaa ya Mpanda, Enelia Lutungulu akisoma risala ya shukrani kwa Serikali kwa niaba ya waalimu na wanafunzi wa shule kwa kuzipatia shule hizo kompyuta 25. Walioketi wakimsikiliza wa kwanza kushoto ni Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye na  katikati ni Mbunge wa Mpanda Mjini, Sebastian Kapufi
 Waalimu wa shule za sekondari, viongozi na watendaji wa mkoa wa Katavi na Manispaa ya Mpanda wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (hayupo pichani) wakati akiwahutubia kabla ya kukabidhi kompyuta kwa ajili ya shule za sekondari za Mpanda

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akisisitiza jambo kwa Afisa Usalama Msaidizi wa Uwanja wa Ndege wa Katavi, Fredrick Valentine(wa kwanza kulia) wakati akikagua miundombinu na hali ya uwanja huo akiwa ziarani mkoani humo. Mbunge wa Mpanda Mjini, Sebastian Kapufi (wa tatu kulia) akifuatilia kwa makini mazungumzo hayo .


Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (aliyesimama mbele amefunga mikono) akiwa kwenye picha ya pamoja na waalimu wa shule za sekondari, viongozi na watendaji wa mkoa wa Katavi na Manispaa ya Mpanda. Wan ne kulia ni Mbunge wa Mpanda Mjini, Sebastian Kapufi na wa tano kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Abdallah Malela



Ubalozi wa Tanzania Ujerumani wamjibu Tundu Lissu


DC MURO AWAFUNDA MAAFISA TARAFA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI

$
0
0
Na Imma Msumba na Elinipa LUPEMBE, Arumeru

Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhe. Jerry Muro, amewataka Maafisa watendaji wa kata na vijiji wilayani humo, kufanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma, kwa kuweka mbele maslahi ya taifa ya kuwahudumia wananchi katika maeneo yao.

Mkuu huyo wa wilaya ametoa rai hiyo, wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha maafisa tarafa na Maafisa watendaji wa kata na vijiji wa halmashauri zote mbili za wilaya ya Arumeru, chenye lengo la kuwakumbusha na kuwajengea uwezo watalamu hao katika kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.

Amesema, kama wilaya wamemekubaliana kuanzisha programu maalumu ya mafunzo kwa watendaji hao, kwa kushirikiana na chuo kilichopo ndani ya wilaya hiyo, chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru, baada ya kugundua uhitaji wa mafunzo kwa watalamu hao, mafunzo yatakayowawezesha kuwa na uelewa wa pamoja katika kuteleleza majukumu yao.

Amesema kuwa Maafisa hao huajiriwa kutoka kwenye kada tofauti, jambo ambalo wakati mwingine, linalopelekea changamoto ya kukwamisha baadhi ya kazi, kupitia mafunzo hayo yatawawezesha kuwa na uelewa wa pamoja na kufahamu majukumu yao na mipaka ya kazi yao, kufanya kazi kwa uadilifu, kujiamini, kuongeza ari na morari ya kazi, pamoja na kuweka mbele uzalendo kwa maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.

"Tumegundua kuna umuhimu kupata mafunzo kwa watendaji wote, yatakayowakumbusha na kuwawezesha kutambua namna sahihi ya utekelezaji wa kazi zenu za kila siku, hii imetokana na baadhi ya watendaji kushindwa kutekeleza majukumu yenu kwa usahihi na kusababisha malalamiko mengi kwa wananchi" amesema Mkuu huyo wa wilaya.8

Hata hivyo Mhe. Muro amewasisitiza watendaji hao kusimamia hali ya usalama katika maeneo yao, kwa kutambua wageni wanaoingia na kutoka katika maeneo yao, kuhamasisha wananchi kushiriki kuchangia maendeleo katika maeneo yao, huku kipaombele kikiwa ni ujenzi wa vyumba vya madarasa hususani kwenye shule za sekondari, lengo likiwa ni kuunga mkono jitihada za serekali la kutoa elimu bila maliopo linalotoa fursa ya kila mtoto kupata nafasi ya kusoma mpaka kidato cha nne.

"Kazi kubwa ya mwaka huu ni kujenga vyumba vya madarasa, ninawaomba Maafisa Watendaji, tuelekeze nguvu zetu kuhamasisha jamii kujikita katika kujenga madarasa, nataka nione kila Tarafa ina shule ya kidato cha 5-6 na kila kata ya kidato cha 1-4" amesema Mhe. Muro

Kwa upande wao wakurugenzi wa halmashauri zote mbili, wamewataka Maafisa Watendaji hao kusimamia shughuli za maendeleo kwa kuendana na kasi ya serikali iliyopo madarakani,serikali ya awamu ya tano, kuwa waadilifu katika kutekeleza kazi zao, kutoa huduma sawa kwa wananchi na kusimamia haki, na kuongeza kuwa hawatosita kuwachukulia hatua wale wote watakaofanya kazi kinyume na maadili.

Kikao kazi hicho, kiliambatana na mafunzo yaliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Maendeleo ya Jamii kutoka chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru, Mkufunzi Douglas Mwadolago, mafunzo yaliyolenga kuwajengea uwezo watendaji hao ya mbinu bora za kuhamasisha jamii, kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao.

Hata hivyo watendaji hao, wamesifu juhudi zinazofanywa na halmashauri zao kupitia ofisi ya mkuu wa wilaya, na kusema kuwa mafunzo hayo yanawaongezea ujuzi na maarifa zaidi ya kutekeleza kazi zao na kuahidi kwenda kutumia maarifa waliyoyapata katika kazi zao za kila siku.

Afisa Mtendaji wa kijiji cha Kikuletwa kata ya Mbuguni, halmashauri ya Meru, Flora Maghimbi amesema kuwa, amefurahishwa na mafunzo hayo na kuahidi kwenda kuyafanyia kazi, huku akiahidi pia kutekeleza maagizo yaliyotolewa kwa kuwa yote yanalenga maslahi ya jamii wanayoihudumia.

Awali, Wilaya ya Arumeru inaundwa na halmashauri mbili, halmashauri ya Arusha na Meru, ikiwa na jumla ya Tarafa 6, kata 53 na vijiji193.
.
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro akizungumza na Maafisa Watendaji wa kata na vijiji,  wakati wa kikao kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.
 Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Meru Emanuel Mkongo, akizungumza na Maafisa Watendaji wa kata na vijiji,  wakati wa kikao kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha. 
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Dc Dr. Wilson Charles Mahera, akizungumza na Maafisa Watendaji wa kata na vijiji,  wakati wa kikao kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Arusha.

RELI YA ZAMANI YAANZA KUKARABATIWA,ZOEZI LAFIKIA 10% ,TRENI SASA KUKIMBIA KM 70 KWA SAA

HABARI ZA UN: Mhandisi mwanamke wa Air Tanzania afunguka!

Response of the Embassy of the United Republic in Germany on Accusations raised by Hon. Tundu Lissu through DW News Africa

$
0
0

  
The Embassy has noted with concern unsubstantiated accusations made by a Tanzanian Member of Parliament Hon. Tundu Lissu, during an interview on DW News Africa aired on 28th January, 2019.  

While requesting an opportunity to appear on the same program in the near future to reply to some of the one-sided allegations, the Embassy wishes to put the record straight on the following matters raised by the MP:     


Attack on His Life and On-going Accusations 

It is regrettable that the Hon. Tundu Lissu, Member of Parliament , who is still on treatment, would embark on a tour abroad to propagate such serious allegations against his own country. The people of Tanzania and indeed his constituents would have expected him, if now recovered and able to travel, to go back home and continue his representative and other public duties. 

Nevertheless, it is well acknowledged that the attack on MP Tundu Lissu by unknown gunmen near his residence in the country’s political capital of Dodoma on 17th September, 2017, was very unfortunate. Such events are rare in peaceful Tanzania but may happen in any country. It was on the same fateful day, in the city of Dar es Salaam, that a retired highranking army officer was also attacked by unknown gunmen and sustained serious injuries too. 

The President of the United Republic of Tanzania issued a statement to condemn the senseless acts and ordered a thorough investigation immediately. At different times the President sent the Vice-President, a former President and other senior government leaders to visit the Hon. Lissu in hospital, some in Dodoma, Nairobi and Brussels. It is ill-advised that the MP would now turn these well-meaning gestures of the President into yet unwarranted attacks.  

The wish of the law enforcement agencies is to have an audience with the Hon. Member of Parliament in order for him to recollect some of the important events concerning the matter. Investigation started immediately after the incident and his primary account is crucial for effective investigation that may lead to successful prosecution.  

Until now, law enforcers have not secured the co-operation of the Member of Parliament and his driver to give important insights into the unfortunate circumstances of the day. 

Investigators in Tanzania are still keen and waiting for the Hon. Lissu and his driver, the two key eyewitnesses, to give their account of the events preceding the attack. 

  

On the Leader of the Opposition being in Prison

The leader of the opposition, Hon. Freeman Mbowe, has not been convicted to serve a prison sentence. The granting or revocation of bail is a judicial process regulated by the Criminal Procedure Act. The Resident Magistrate’s court in Dar es Salaam revoked his bail after he had breached bail conditions by being absent in court without justified cause. After series of appeals against the decision, the matter is still pending in court, awaiting the decision of the Court of Appeal of Tanzania. 

The Embassy wishes to affirm that Tanzania will continue to be a stable democratic country. Since independence to-date, the country has actively upheld the rule of law, enhanced democratic principles and human rights, by among others, acceding to regional and international human rights instruments.  

Since 1992, the country has remained one of the few countries in Africa that have continued to enjoy peaceful multi-party democracy. The fact that the Hon. Lissu is a Member of Parliament from an opposition party speaks loud to how far the country has given space to democracy. 

The Embassy reaffirms the unwavering commitment of the reform-minded President, Dr. John Pombe Magufuli, and his Government, to cementing democratic principles, upholding the rule of law and accelerating the country’s anti-corruption drive. All these are necessary elements of the social, political and economic development agenda that the President has set for the benefit of the people of Tanzania.   


On President’s Statement on Opposition Parties 

During the interview, Hon. Tundu Lissu had accused the President of the United Republic of Tanzania for encouraging political violence by stating that the President did declare  that he wanted to see no opposition party by the year 2020. 

The Embassy states that the accusations of Hon. Tundu Lissu are unfounded. In any multi party democracy, the survival or otherwise of political parties depends on how they are able to sale their ideology and/or manifesto to the public. Based on this fact, Mr. Tundu Lissu and members of his party have occasionally stated that they will eliminate CCM from the political scene. It is therefore highly exaggerated for Hon. Tundu Lissu to conclude that the government is committing murders against opposition politicians based on the President’s statement. Furthermore, the argument by Hon. Tundu Lissu does not explain acts of murder and violence which have been committed against members of the ruling party CCM, civil servants, and police officers. It is unfortunate that Hon. Tundu Lissu was not only biased in his arguments, but also tried unethically to capitalise politically on innocent lives. 


On Hon. Tundu Lissu facing several criminal cases

Members Parliament, just like any other citizens are not immune from criminal prosecutions in case of commission of offences. Hon. Tundu Lissu is facing several criminal cases, and the independence of the judiciary requires that determination of any case pending in court should not be influenced by persons or entities outside the judiciary. It is unfortunate that Hon. Tundu Lissu intentionally hides the fact that Tanzania has a record of respecting judicial decisions, even those given in favour opposition politicians.

Furthermore, the enforcement of criminal laws is not based on political affiliation as claimed by Hon. Lissu. It is for this reason that on different occasions, some members of parliament, including those from the ruling party were either arrested or charged in court following accusations of having committed different and unrelated offences.   For example, in December 2017, Hon. Sadifa Juma Khamis, a member of parliament from the ruling party CCM was arrested and later charged by the anti-corruption bureau in Tanzania, the PCCB. There are also several examples of CCM politicians who were arrested or charged for various offences. It is therefore wrong and bias for Hon. Tundu Lissu to argue that opposition members of parliament are targeted. 


On banning of political activities

Political parties in Tanzania are free to organize their statutory processes (like elections, constituent activities etc). Politicians, like Hon. Lissu can conduct their political activities while adhering to the laws which protect not only public order, but also the rights of other citizens. It is important to note that multi-party democracy thrives only in a place where there is law and order. Prohibition of unorganised or violent demonstration is in accordance with the law, whose existence is not limited to politicians alone. 

Dr. Abdalah S. Possi

AMBASSADOR



Je, unafahamu kwamba unaweza kujiajiri kupitia Jumia?

$
0
0
Je, unafahamu kwamba unaweza kujiajiri kupitia Jumia?
  • Pata kamisheni kwa kuuza bidhaa zinazopatikana Jumia.
  • Zaidi ya mawakala 600 wamekwishajiunga.

Timiza ndoto zako za kibiashara kwa kujipatia kipato zaidi na zaidi! Kuwa bosi wako mwenyewe kwa kufanya shughuli zako na kujiingizia kipato bila ya mtu kukusimamia. Ndiyo kauli mbiu ambayo Jumia inaitumia kwa sasa katika kuwahamasisha vijana wa kitanzania kutumia fursa zilizoletwa na teknolojia kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa pekee.

Kampuni hii ambayo inajishughulisha na kuuza bidhaa kwa njia ya mtandaoni Tanzania imeanzisha programu inayokwenda kwa jina la ‘Jumia JForce.’ Huu ni mtandao wa wataalamu wa ushauri wa mauzo ambao hujiingizia kipato kwa kuwasaidia wateja kufanya manunuzi ya bidhaa zinazopatikana kwenye tovuti ya Jumia. Kwa sasa kuna mawakala takribani 600 waliotapakaa Tanzania nzima.
Changamoto ya ajira ni kubwa duniani kote na sio nchini Tanzania pekee au barani Afrika kwa ujumla. Kwa mujibu wa Ripoti ya Mtazamo wa Uchumi wa Afrika ya mwaka 2019 iliyotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika, imeainisha kuwa nguvu kazi ya Afrika inatarajiwa kuongezeka kwa 40% zaidi kufikia 2030. Inaendelea zaidi kwa kufafanua kuwa, endapo mienendo iliyopo sasa ikiendelea, ni nusu pekee ya nguvu kazi mpya inayoingia ndiyo itakayopata ajira, na ajira nyingi zitakuwa kwenye sekta zisizo rasmi. Hii ina maanisha kwamba vijana takribani milioni 100 watakuwa bila ya ajira.

Akifafanua namna Programu ya Jumia JForce inavyoweza kuwa mwarobaini wa changamoto ya ajira kwa vijana, Nahodha wa Wakala wa Mauzo wa Jumia - Tanzania, Bi. Elizabeth Samson amesema kuwa, “Kuwa bosi wako mwenyewe, ‘kamwe usiseme haiwezekani.’

Mwaka mmoja nyuma kama angekuja mtu na kuniambia kuwa unaweza kujiingizia kipato cha zaidi ya laki moja na kuendelea kwa kujifanyia shughuli zako mwenyewe, ningemwambia apeleke hizo hadithi kwa ndege wa mwituni. Mtu pekee ambaye anaweza kukuzuia kufanya hivyo ni wewe mwenyewe. Kwa mafunzo na nyenzo zinazopatikana Jumia JForce, ni rahisi kuanza kuingiza kipato mara moja na kukuza mapato yako kwa urahisi, hakuna kuwekeza mtaji kabisa. Kama wakala wa JForce, unaweza kuwa vile unavyotaka kuwa, ishi ndoto zako na ujenge mustakabali wa baadaye!”

Programu ya mawakala wa mauzo kutoka Jumia ina malengo ya kuwapatia uwezo na kuwaimarisha watu wanaotarajia kuwa wajasiriamali kwa kuwapatia msaada wa kukuza biashara zao. Jiunge kwa kulipia gharama ndogo na kisha uanze kuingiza kipato kwa kuuza bidhaa za Jumia zinazokuzunguka.

Faida 5 za kujiajiri kupitia Jumia JForce

Unajiingizia kipato chako mwenyewe. Unapata kamisheni kwa kuuza bidhaa zinapatikana katika tovuti ya Jumia kutoka kwa wauzaji tofauti. Unalipwa kutokana na juhudi zako za kuweza kuwashawishi wateja wengi zaidi kununua bidhaa: kadri unavyofanya kazi, ndivyo unavyolipwa zaidi!

Bosi ni wewe mwenyewe. Ukiwa kama wakala wa programu ya mauzo, una uhuru kamili na udhibiti wa shughuli uzifanyazo. Jenga biashara yako yenye kukunufaisha wewe mwenyewe. Hakuna cha kukuzuia! Pia, unaunda timu yako mwenyewe ya mawakala wa mauzo ambayo itakuwa inaripoti kwako na kuisimamia.

Unapatiwa mafunzo bure. Kadri unavyokua ndivyo unavyozidi kujiongezea malipo ya kamisheni. Utapatiwa ujuzi na mafunzo ya hali ya juu. Utanahakikishiwa kwamba unakuaa mfanyabiashara uliyewezeshwa kikamilifu.

Unafurahia kile unachokifanya. Uza bidhaa na uzawadiwe. Pata maarifa mapya na ujijengee uwezo wa kujiamini. Kutana na watu wapya na utengeneze marafiki wapya. Pata fursa ya kuhudhuria matukio ya Jumia kama vile hafla, semina na warsha mbalimbali.

Faida. Pata fursa ya kujua promosheni za kila siku. Furahia kujipatia kipato kupitia kulipwa kamisheni. Shiriki bure mafunzo yote ya Jumia na ujipatie ujuzi wa kazi yako! Hauhitajiki kuwa na uzoefu, bali msukumo na shauku kubwa ya biashara!

Unasubiri nini kuichangamkia fursa hii? Ikiwa ndio mwanzo wa mwaka wa 2019 ambao umejaa fursa lukuki siku za usoni ni vema kufanya maamuzi ya kujiunga sasa. Kwasababu hivi punde kampeni mbalimbali za mauzo zinatarajiwa kuzinduliwa ikiwemo ya msimu wa wapendao au ‘Valentine’s’ ambayo inatarajiwa kuanza Februari 4 mpaka 16.  
Viewing all 109941 articles
Browse latest View live




Latest Images