Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109936 articles
Browse latest View live

SERIKALI YATOA MWEZI KWA WIZARA, BODI YA MAZAO MCHANGANYIKO KUKAMILISHA MALIPO KWA WAKULIMA WA KOROSHO

$
0
0
*Februari 5 wawe wamekamilisha uhakiki na malipo kwa wakulima wa korosho
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo pamoja na Bodi ya Mazao Mchanganyiko wahakikishe hadi Februari 5 mwaka huu wawe wamekamilisha uhakiki na kuwalipa wakulima wote wa zao la korosho.

Pia amesema Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa mazao makuu ya biashara kuanzia hatua ya uzalishaji hadi masoko yake likiwemo zao la korosho kwa lengo la kuwapatia tija wakulima.

Amesema zao la korosho ambalo awali soko lake halikwenda vizuri kutokana na utaratibu uliokuwa ukitumiwa na wafanyabiashara kwa kutenda bei ndogo na wakulima wenyewe kugomea bei hiyo.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Januari 27, 2019) wakati akizungumza na wadau wa zao la korosho mkoani Mtwara, lengo likiwa ni kupata taarifa juu ya mwenendo mzima wa bidhaa hiyo kwa msimu wa mwaka 2018/2019.

Amesema Serikali ilitoa nafasi kwa wafanyabishara kufanya    marekebisho ili waweze kununua bidhaa hiyo kwa bei nzuri bila mafanikia hali iliyopelekea Serikali kuamua kununua korosho zote ili wakulima wapate tija.

Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba amesema kuwa, taarifa iliyotolewa na timu ya uhakiki ilisema msimu wa 2018/2019 matarajia yalikuwa ni kuvuna tani 150,000 kutokana na kushuka kwa uzalishali.

“Lakini kwa kazi nzuri iliyofanywa na timu nzima ya Wizara, wilaya na mkoa na timu ya uhakiki hadi sasa korosho tulizozipokea ambazo ziko katika maghala ni zaidi ya tani laki mbili.”

Amesema zoezi hilo limewapa tija kubwa katika zao hilo tofauti na taarifa zilizowafikia hapo awali, ambapo wanatarajia baada ya zoezi hilo kumalizika watafikisha zaidi ya tani 200,000 ikiwa ni nyongeza zaidi ya tani 100,000.

Amesema, Wilaya inayoongoza kwa uzalishaji mkubwa hapa nchini ni Tandahimba amabpo wamefikia asilimia 96 ya uhakiki hadi kufikia jana huku zoezi la malipo kwa korosho zote zilizohakikiwa kwa mkoa wa Mtwara yamefikia asilimia 83.

Hata hivyo, Waziri huyo amesema kuwa fedha za kununulia korosho hizo zipo kwa kuwa Serikali imejipanga vizuri. Jumla ya sh bilioni 700 zimetengwa kwa ajili ya zoezi hilo ambapo hadi sasa zaidi ya sh. bilioni 400 zimeshalipwa wakulima waliohakikiwa hadi juzi.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika  kikao alichokiitisha cha wadau wa zao la korosho kilichofanyika mjini Mtwara, leo Januari  27, 2019. Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Omary Mgumba. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Baadhi ya washiriki wa kikao cha wadau wa zao la korosho wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakati alipozungumza katika kikao hicho alichokiitisha mjini Mtwara, Januari 27, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa mkoa wa Mtwara wakati alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Mtwara ambako aliongoza kikao cha wadau wa zao la korosho, Januari 27, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


UJUMBE WA MFUKO WA SHEIKH KHALIFA FUND FOR ENTERPRISE DEVELOPMENT WATEMBELEA ZANZIBAR

$
0
0
MKURUGENZI wa Mfuko wa ‘KhalifaFund’ Naizar Cheniour, amesema mfuko huo umeazimia  kuwawezesha vijana wa Zanzibar katika nyanja mbali mbali za kiuchumi ili kuweza kujiajiri na kuinua hali zao za maisha.

Mkurugenzi huyo amesema hayo leo wakati  alipozungumza na waandishi wa habari, mara baada ya ujumbe wa Mfuko huo ulipowasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume.

Ujumbe huo upo nchini kwa ziara maalum, ikiwa ni muendelezo wa mazungumzo na Serikali, yenye lengo la kufanikisha utekelezaji wa programu mbali mbali katika sekta za biashara, ujasiriamali, miundombinu na nyenginezo.

Alisema Mfuko umelenga kuwawezesha vijana wa Zanzibar katika upatikanaji wa rasilimali fedha, utaalamu na masuala ya kiufundi ili waweze kujiajiri kupitia shughuli za ujasiriamali na hivyo kuweza kujitegemea.

Aliwataka vijana na Wazanzibari kwa ujumla kutarajia mafinikio makubwa kutokana na  program mbali mbali zitakazotekelezwa kupitia Mfuko huo.

Alisema mfuko wa KhalifaFund, una uzoefu mkubwa katika utekelezaji wa programu za maendeleo na shughuli za kiuchumi, ambapo umekuwa ukifanya kazi hizo katika nchi mbali mbakli duniani.

Mapema, Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Viwanda, Dk. Juma Ali Juma alisema ujio wa Viongozi wa Mfuko wa’ KhalifaFund’  umelenga kukamilisha mazungumzo yaliofikiwa katika kikao kilichopita ili kuwa tayari kwa utekelezaji wa yale yalioafikiwa.

Alisema mfuko huo wa kifedha, wenye makao makuu yake Abu Dhabi ,UAE utatowa msukumo mkubwa  katika utekelezaji wa program mbali mbali za kimaendeleo na kiuchumi, sambamba na kuwawazesha vijana kupitia kazi za ujasiriamali.

Alisema wakati ukiwa nchini utakutana na kufanya mazungumzo na taasisi mbali mbali za Serikali pamoja na kutembelea maeneo tofauti.

Hii ni mara ya pili kwa viongozi wa Mfuko wa ‘KhalifaFund’ kuja nchini kwa ajili hiyo, ambapo kabla ulipata fursa ya kutembelea sekta tofauti za maendeleo na kiuchumi Unguja na Pemba.

Aidha, ujio wa mfuko huo unafutia ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein aliyoifanya Umoja wa nchi za Falme ya Kiarabu (UAE) Januari mwaka uliopita. 
 

 KATIBU Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda Zanzibar Ndg.Juma  Ali Juma, akisalimiana na Afisa wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development Ndg. Abdulah Al Jarwani, wakati wakiwa sili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, kwa ziara ya siku tatu kutembelea Miradi mbalimbali Zanzibar.(Picha na Ikulu)
 KATIBU Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda Zanzibar Ndg Juma Ali Juma, akizungumza na Ujumbe wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development ya Abudha Dhabi UAE, ulipowasili Zanzibar kwa ziara ya Siku Tatu ukiongozwa na Mkurugenzi Nizar Cheniour, mwenye fula nyeusi. wakiwa katika ukumbi wa VIP uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, baada ya kuwasili kwa ziara ya siku tatu Zanzibar.(Picha na Ikulu)
 KIONGOZI wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development wa Abu Dhabi UAE, ukiongozwa na Mkurugenzi Ndg. Nazar Cheniour, akizungumza na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, kutembelea Miradi mbalimbali ya Maendeleo Zanzibar.(Picha na Ikulu)
 AFISA wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development Ndg. Ali Al Saad, akipata maelezo ya kutoka kwa Mkurugenzi wa Ushirika wa Fakirice Milling Enterprises wa Kisongoni Ndg. Yussuf Faki Yussuf, akitowa maelezo ya usagaji wa mpuga katika ushirika wao wakati walipotembelea ushirika huo leo.(Picha na Ikulu)
KATIBU Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda Ndg Juma Ali Juma, akitowa maelezo kwa Kiongozi wa Ujumbe wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development Ndg. Nizar Cheniour, walipotembelea Ushirika wa Fakirice Milling Enterprises Kisongoni,unaojishughulisha na kukoboa mpunga.(Picha na Ikulu)

MKUU WA OPERESHENI MAALUM ZA JESHI LA POLISI NCHINI ATETA NA KIKOSI CHA KUPAMBANA NA UHALIFU MKOA WA RUVUMA

$
0
0
 Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas, akizungumza na kikosi Maalum cha kupambana na uhalifu katika viwanja vya Kikosi cha kutuliza Ghasia mkoani Ruvuma, baada ya kuwasili katika ziara yake ya kikazi. (Picha na Jeshi la Polisi) 
 Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas katikati kulia kwake ni Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Ruvuma Kamishna Msaidizi ACP Pili O. Mande na kushoto kwake ni Mkuu wa Kikosi cha kutuliza Ghasia Mkoa wa Ruvuma ACP Omar K. Omari wakiwa katika picha ya pamoja na kikosi maalum cha kupamban na uhalifu mkoani humo. 
Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas, akishiliki mazoezi ya pamoja na kikosi maalum cha kupamba na uhalifu Mkoa wa Ruvuma baada ya kuwasili katika ziara yake ya siku moja mkoani humo. 
(Picha na Jeshi la Polisi) 

NMB YATOA MSAADA WA VIFAA TIBA MKOANI MOROGORO KUUNGA MKONO JUHUDI ZA MAKAMU WA RAIS KUBORESHA HUDUMA YA AFYA MAMA NA MTOTO

$
0
0

 Katibu wa Makamu wa Rais Bw. Juma S. Mkomi akipokea Vifaa Tiba vya kujifungulia wakina mama kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kutoka kwa Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Mashariki Bi. Aikansia Muro ikiwa sehemu ya Benki hiyo kuunga mkono juhudi za Makamu wa Rais katika kuboresha huduma ya afya ya Mama na Mtoto leo katika hospitali ya rufaa ya Morogoro ambapo Makamu wa Rais alitoa zawadi kwa watoto 36 waliozaliwa tarehe 27, Januari kama kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
  Katibu wa Makamu wa Rais Bw. Juma S. Mkomi akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Rufaa ya Morogoro Dkt. Lucy Nkya moja ya mabeseni yenye mahitaji muhimu kwa watoto waliozaliwa leo ikiwa zawadi kutoka kwa  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa watoto 36 waliozaliwa leo tarehe 27, Januari kama kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Rufaa ya Morogoro Dkt. Lucy Nkya akionyesha juu moja ya mabeseni yenye mahitaji muhimu kwa watoto waliozaliwa leo kama ishara ya kumshukuru Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka  watoto 36 waliozaliwa leo tarehe 27, Januari ikiwa ni kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Januari 27 kwa kushirikiana na Benki ya NMB, wametoa Vifaa Tiba vya kujifungulia katika wodi ya Mama na Mtoto, pamoja na vifaa tiba hivyo aliwazawadia  watoto 36 waliozaliwa siku ya  katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro .

Makamu wa Rais aliwakilishwa na Katibu wake Bw. Juma S. Mkomi ambaye amesema kuwa Makamu wa Rais amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha huduma ya afya ya mama na mtoto inaboreshwa.

“Suala la kuboresha huduma ya mama na mtoto limeelezewa kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 lakini Makamu wa Rais kwa upekee amelipa kipaumbele kwa sabau ni moja kati ya ahadi zake kuu wakati kampeni” alisema Katibu huyo wa Makamu wa Rais.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt. Rita Lyamuya amemshukuru Makamu wa Rais kwa kuwakumbuka watoto waliozaliwa hospitalini hapo ambapo alisema kuwa watoto 36 wamezaliwa katika siku ya leo na kwa kipindi cha robo mwaka watoto  1779 walizaliwa  kati ya hao waliozaliwa kwa upasuaji ni 586.

Aidha, Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Mashariki Aikansia Muro amesema Benki ya NMB inaunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano katika kuboresha huduma zote za kijamii hususani sula zima la  afya na elimu na wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha huduma za kijamii ambapo leo wamemuunga mkono Mhe. Makamu wa Rais kwa kutoa Vitanda vinne vya kujifungulia, Vifaa vya kumsaidia mama kujifungulia (delivery kit) 8, pamoja na vifaa vingine ambavyo kwa ujumla vinagharimu shilingi milioni 5.

Kwa Upande mwingine Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro Bw. Clifford Tandari ameishukuru Serikali kwa kutenga shilingi bilioni 8.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali 3 na vituo vya afya 11 katika mkoa wa Morogoro.

WAZIRI AWATAKA WALIMU WAKUU KUTOA USHIRIKIANO ILI KUANZISHA CLUB ZA VIJANA MASHULENI

$
0
0
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewataka walimu wa kuu wa Shule za Sekondari Nchini kushirikiana na Shirika la FEMA Hip kuanzisha club za vijana katika shule zao ili kutoa fursa za vijana mashuleni kupata elimu ya Afya ya uzazi na kujitambua.

Waziri Ummy amesema hayo wakati wa maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa shirika hilo ambalo kwasasa lina uwezo wa kuwafikia vijana 15,000 kila mwezi na kuwalimisha masuala mbalimbali ya kiafya ikiwemo kujikinga na maabukizi ya ukimwi.

Aidha Waziri Ummy aliongeza kuwa yeye amekuwa mdau mkubwa katika kuhakikisha vijana Nchini wanapata elimu ya uzazi nchini ikiwezekana hata mtoto wa darasa la tano na kuwafanya kutambua angalau kulinda mwili wao kwani siku hizi watoto wanapevuka katika umri mdogo.

Aliongeza kuwa mwelekeo wa Serikali ni kuwa na uchumi wakati lakini hatuwezi kufikia hapo kama bado kati ya wasichana 100 wasichana 27 wanapata mimba katika umri mdogo hivyo kuwa na mzunguko wa umasikini usio kwisha.

Aliwapongeza FEMA kwa kuanza kupunguza masuala ya elimu ya Afya na uzazi nakuanza kujielekeza katika masuala ya uwezeshaji wa wa vijana kiuchumi kwani kama utampatia elimu bila kuwawezesha kiuchumi matatizo yao yanabaki palepale.

Amelitaka shirika hilo kuanzisha pia masuala ya elimu ya lishe kwa kuwa Tanzania kwasasa inakabiliwa na tatizo la udumavu ambapo kila watoto 100 watoto 34 wenye umri chini ya miaka 5 wamedumaa.

Shirika la FEMA limitimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake na limekuwa likijihusisha na utoaji na uhamasishaji vijana kujikinga na ukimwi, kuwapa matumaini wa wathirika wa ugonjwa wa ukimwi, kutoa elimu ya Afya uzazi kwa vijana, kuwawezesha vijana kubuni namna bora za kujiwezesha kiuchumi kupitia club za FEMA Hip mashuleni lakini pia kwa kupitia vyombo vya habari.
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu pamoja na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Stella wakichangia mada wakati wa hafla ya kutimiza miaka 20 ya Shirika la FEMA jana jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu pamoja na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Stella wakichangia mada wakati wa hafla ya kutimiza miaka 20 ya Shirika la FEMA jana jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy pamoja na Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika la FEMA Sauda Simba Kilumanga akiangalia bidhaa za jarida la FEMA wakati wa hafla ya kutimiza miaka 20 ya Shirika la FEMA jana jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy pamoja na Mwenyekiti wa Bodi wa Shirika la FEMA Sauda Simba Kilumanga wakiingia ukumbini tayari kuanza   ya kutimiza miaka 20 ya Shirika la FEMA jana jijini Dar es Salaam.  

KUWAHUDUMIA WAKIMBIZI NI JUKUMU LA WATU WOTE SIO NCHI MOJA

$
0
0
Kuwahudumia Wakimbizi ni jukumu la Wote sio la Nchi moja
Kazi ya kuwahudumia wakimbizi ni Ubinadamu na ni jukumu la kimataifa na ni kitu cha kushangaza kuona nchi zilizoendelea zinaziachia nchi masikini kubeba mzigo wa kugharamia wakimbizi.

Kauli hiyo ilitolewa na Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza wa Baraza la Wakimbizi Duniani (World Refugees Council-WRC), Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kuwasilisha ripoti ya Baraza hilo kwenye Umoja wa Mataifa New York, Marekani tarehe 24 Januari 2019.

Rais Mstaafu alitanabainisha kwamba Baraza lao lilipokea msimamo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kukataa mpango wa kukopa Benki ya Dunia ili kuwahudumia wakimbizi wakati yenyewe inadaiwa mikopo ya kimaendeleo iliyonayo. Serikali inaamini kazi ya kuhudumia wakimbizi ni ya kibinadamu kwa kushirikiana na Jumuiya ya Kimataifa badala ya kuibebesha nchi moja mzigo wa madeni.

Taarifa hiyo imebainisha kuwa tatizo la wakimbizi limekuwa kubwa sana duniani wakati huu kuliko wakati wowote ule tangu vita vya Pili vya Dunia. Mathalan, kuna idadi ya watu milioni 68.5 waliopoteza makwao (Internally displaced persons) mwaka 2017 na kati yao, milioni tatu wamepoteza makwao kwa sababu ya mabadiliko ya hali ya hewa na uchafuzi wa mazingira. 

Ripoti inaeleza kuwa, kumekuwa na ongezeko kubwa la wakimbizi na wanaopoteza makwao kusini mwa jangwa la Sahara ambao walifikia milioni 18.4 mwaka 2017 ukilinganisha na idadi ya milioni 14.1 mwaka 2015. Ripoti inabainisha kuwa ongezeko hilo limetokana na sababu mbalimbali zikwemo upvotevu wa amani katika nchi zao.

Ripoti inazidi kubainisha kuwa asilimia 30 ya watu wote duniani mwaka 2017 walikuwa wakimbizi na waliopoteza makwao ukilinganisha na asilimia 23 ya mwaka 2015. Kati ya idadi hiyo, wanaotoka Afrika, asilimia 79% wanatoka katika nchi za Somalia, Nigeria, Sudan kusini na Jamhuri ya Afrika ya Kati. 

Ripoti imeeleza nchi zinazopokea wakimbizi wengi kuwa ni pamoja na Uganda, wakimbizi milioni moja na laki nne; Ethiopia, laki Tisa; Tanzania laki tatu na ishirini na Sita elfu; na Rwanda elfu 84. Baadhi ya nchi zimechukua wakimbizi hao ikiwemo Marekani, Canada, Australia na Finland ingawa idadi yao ni ndogo mno. 

Katika ripoti hiyo, baraza limetoa mependekezo mbalimbali ya kukabiliana na tatizo la wakimbizi duniani. Mapendekezo makubwa ni pamoja na kudhibiti nchi ambazo zinachochea au kuanzisha migogoro kwa kuweka mfumo thabiti wa kimataifa, kuongeza usuluhishi wa migogoro, kutowanyanyapaa wakimbizi kwa kujenga ukuta na kusaidia juhudi za kutafuta amani katika maeneo yenye migogoro. 

Baraza la Wakimbizi duniani ni chombo kilichoundwa na wataalamu mbalimbali wakiwemo wanasiasa, watafiti na watunga sera kwa lengo la kufanya utafiti wa kina utakaosaidia kubuni njia na mbinu za kitaalamu na za ubunifu zitakazosaidia kukabiliana na kumaliza kabisa tatizo la wakimbizi duniani. 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma 
27 Januari 2019 
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti Mwenza wa Baraza la Wakimbizi Duniani (World Refugees Council, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (mstari wa mbele wa kwanza kushoto) akiwa na viongozi mbalimbali jijini New York baada ya Baraza hilo kuwasilisha ripoti kwenye Umoja wa Mataifa ya namna ya kukabiliana na tatizo la wakimbizi duniani. Picha inaonesha kitabu cha ripoti iliyowasilishwa. 
Mheshimiwa Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Mhe. Balozi Modest J. Mero (kushoto) na viongozi wengine wa Baraza la Wakimbizi Duniani. 

WAZAZI NA WALEZI WILAYANI MUHEZA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA WATOTO WAO

$
0
0


Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kushoto akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo katikati ni Katibu wa CCM wilaya ya Muheza Moyo

Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo kushoto akiingia shuleni hapo kwa ajili ya kushiriki ujenzi wa bweni la w katika shule ya msingi mbaramo yenye watoto wenye mahitaji maalum.

Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu akishiriki ujenzi huo

msingi ukiwa umechimbwa
sehemu ya wanafunzi wa shule hiyo wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo


WAZAZI na walezi wilayani Muheza wametakiwa kusimamia nidhamu za watoto wao ili kuepukana na suala la mmomonyoko wa maadili ambalo lina wakabili baadhi ya watoto hapa nchini.

Wito huo ulitolewa hivi karibuni na Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo ametoa kauli hiyo wakati wa ziara yake wilayani humo ambapo pamoja na mambo mengine ametembelea eneo la ujenzi wa mabweni katika shule ya msingi mbaramo yenye watoto wenye mahitaji maalum.

Alisema iwapo wazazi watawajibika ipasavyo kuhakikisha wanasimamia maadili hayo watawasaidia vijana wao kuweza kuepukana na tabia ambazo sio nzuri ambazo wanaweza kuzipata kutokana na makundi mengine. Hata hivyo pia alisema serikali ya Awamu ya Tano inafanya jitihada kubwa ya kuboresha miundo mbinu ya watoto kujisomea hivyo wazazi wanapaswa kusimamia suala zima la nidham kwa wototo wao .

Kwa Mkuu wa wilaya ya Muheza Mwanaasha Tumbo amesema kuwa kupitia kampeni ustawi wao ni wajibu watajenga madarasa na mabweni kwa ajili ya watoto walemavu ambayo wameshaanza kuitekeleza katika shule ya msingi mbaramo. Katika kuunga mkono jitihada hizo mbunge wa Jimbo la Muheza Balozi Adadi Rajab pamoja na mambo mengine ameahidi kutoa mifuko Saruji ili kuhakikisha mabweni hayo yanakamilika kwa wakati ili kutoa fursa kwa wanafunzi kusoma bila kuwepo kwa vikwazo

TAARIFA KUHUSU ZIARA YA KAMPUNI ZA UWEKEZAJI KUTOKA AUSTRIA

$
0
0

Yah: Ziara ya Kampuni kubwa za uwekezaji kutoka Austria na India

Ujumbe wa Makampuni 16 makubwa ya uwekezaji kutoka Austria utafanya ziara ya kikazi hapa nchini kuanzia tarehe 28 hadi 30 Januari, 2019. 

Ziara ya ujumbe huo nchini ni mwendelezo wa jitihada za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambao unawakilisha pia nchini Austria na wadau mbalimbali katika kutekeleza diplomasia ya uchumi. Pamoja na mambo mengine, diplomasia ya uchumi inalenga kwenye kutafuta na kuleta wawekezaji wenye nia ili wawekeze katika maeneo mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kukuza uchumi na kuinua kipato cha wananchi. 

Makampuni hayo ya Austria yana nia ya kuangalia fursa za uwekezaji hapa nchini katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, mawasiliano ya simu, umeme wa kutumia maji na usafirishaji. 

Ukiwa nchini, ujumbe wa Kampuni 8 umeomba kuonana na kufanya majadiliano na viongozi wa Wizara mbalimbali tarehe 29 Januari, 2019 jijini Dodoma akiwemo Mhe. Japhet Ngailonga Hasunga (Mb.), Waziri wa Kilimo; Mhe. Dkt. Medard Kalemani (Mb.), Waziri wa Nishati; Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb.), Waziri wa Fedha na Mipango; Mhe. Ummy Mwalimu (Mb.), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto na Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. 

Lengo la ujumbe huo kukutana na Mawaziri hao ni kutaka kufahamu kuhusu kazi na miradi mbalimbali inayosimamiwa na kutekelezwa na wizara hizo ili waone namna ya kuwekeza katika maeneo hayo. Aidha, ujumbe huo utashiriki kwenye Kongamano la Biashara lililoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Chama cha Wafanyabiashara, Wakulima na Wenyeviwanda Tanzania (TCCIA) na Ubalozi wa Austria. Kongamano hilo litafanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam tarehe 28 Januari 2019. 

Serikali ya Tanzania na Austria zina mahusiano ya kidiplomasia ya muda mrefu tangu uhuru ambapo Austria imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali kupitia mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) hapa nchini hususan katika sekta ya kilimo, afya na kuwajengea uwezo wanawake. Ziara ya ujumbe wa makampuni hayo ni dalili njema za kuanza kuimarika zaidi kwa mahusiano kati ya Tanzania na Austria. 

Wakati huohuo, Ujumbe wa wawekezaji kutoka Kampuni ya Bureau Facility Services Pvt Ltd (CISB) ya India utafanya ziara hapa nchini kuanzia tarehe 29 Januari hadi 05 Februari 2019. Ziara hiyo ina lengo la kukamilisha utaratibu wa kuwekeza katika maeneo kadhaa ikiwemo ujenzi wa kiwanda cha madawa, kutafuta fursa ya kuwekeza kwenye miundombinu kama vile barabara na madaraja na ujenzi wa nyumba na hoteli. Wajumbe hao wanatarajia kukutana na kufanya mazungumzo na Mawaziri na Viongozi Wakuu Waandamizi wa sekta husika. 

Ujumbe huo wa watu watatu utaongozwa na Bw. Alban Rodricks kutoka CISB ambaye alishafanya ziara hapa nchini mara kadhaa. Aidha, Ujumbe huo unatarajiwa kukutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Hamisi Kigwangala (Mb.), Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Ummy A. Mwalimu (Mb.), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto na Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe (Mb.), Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na Mhe. Angellah Kairuki (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji. 


Katika ziara yao hiyo fursa mbalimbali za kiuwekezaji zinatarajia kuibuliwa pamoja na kujadiliana namna bora ya kushirikiana kati ya Tanzania na India. 

Imetolewa na: 
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, 
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, 
Dodoma. 
27 Januari 2019

BREAKING NEWZZZZZ: RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI WA MAJAJI, WAKUU WA WILAYA WAWILI NA MA-DAS KUMI LEO

SERIKALI YATOA MWEZI KWA WIZARA, BODI YA MAZAO MCHANGANYIKO

$
0
0
Februari 15 wawe wamekamilisha uhakiki na malipo kwa wakulima wa korosho

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo pamoja na Bodi ya Mazao Mchanganyiko wahakikishe hadi Februari 15 mwaka huu wawe wamekamilisha uhakiki na kuwalipa wakulima wote wa zao la korosho.

Pia amesema Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa mazao makuu ya biashara kuanzia hatua ya uzalishaji hadi masoko yake likiwemo zao la korosho kwa lengo la kuwapatia tija wakulima.

Amesema zao la korosho ambalo awali soko lake halikwenda vizuri kutokana na utaratibu uliokuwa ukitumiwa na wafanyabiashara kwa kutenda bei ndogo na wakulima wenyewe kugomea bei hiyo.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Januari 27, 2019) wakati akizungumza na wadau wa zao la korosho mkoani Mtwara, lengo likiwa ni kupata taarifa juu ya mwenendo mzima wa bidhaa hiyo kwa msimu wa mwaka 2018/2019.

Amesema Serikali ilitoa nafasi kwa wafanyabishara kufanya marekebisho ili waweze kununua bidhaa hiyo kwa bei nzuri bila mafanikia hali iliyopelekea Serikali kuamua kununua korosho zote ili wakulima wapate tija.

Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba amesema kuwa, taarifa iliyotolewa na timu ya uhakiki ilisema msimu wa 2018/2019 matarajia yalikuwa ni kuvuna tani 150,000 kutokana na kushuka kwa uzalishali.“Lakini kwa kazi nzuri iliyofanywa na timu nzima ya Wizara, wilaya na mkoa na timu ya uhakiki hadi sasa korosho tulizozipokea ambazo ziko katika maghala ni zaidi ya tani laki mbili.”

Amesema zoezi hilo limewapa tija kubwa katika zao hilo tofauti na taarifa zilizowafikia hapo awali, ambapo wanatarajia baada ya zoezi hilo kumalizika watafikisha zaidi ya tani 200,000 ikiwa ni nyongeza zaidi ya tani 100,000.

Amesema, Wilaya inayoongoza kwa uzalishaji mkubwa hapa nchini ni Tandahimba amabpo wamefikia asilimia 96 ya uhakiki hadi kufikia jana huku zoezi la malipo kwa korosho zote zilizohakikiwa kwa mkoa wa Mtwara yamefikia asilimia 83.

Hata hivyo, Waziri huyo amesema kuwa fedha za kununulia korosho hizo zipo kwa kuwa Serikali imejipanga vizuri. Jumla ya sh bilioni 700 zimetengwa kwa ajili ya zoezi hilo ambapo hadi sasa zaidi ya sh. bilioni 400 zimeshalipwa wakulima waliohakikiwa hadi juzi.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
41193 – Dodoma, 
JUMAPILI, JANUARI 27, 2019. 
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika  kikao alichokiitisha cha wadau wa zao la korosho kilichofanyika mjini Mtwara, Januari  27, 2019. Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Omary Mgumba. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Baadhi ya washiriki wa kIkao cha wadau wa zao la korosho wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakati alipozungumza katika kikao hicho alichokiitisha mjini Mtwara, Januari 27, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa mkoa wa Mtwara wakati alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Mtwara ambako aliongoza kikao cha wadau wa zao la korosho, Januari 27, 2019. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa mkoa wa Mtwara wakati alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Mtwara ambako aliongoza kikao cha wadau wa zao la korosho, Januari 27, 2019. 
 Baadhi ya washiriki wa kIkao cha wadau wa zao la korosho wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakati alipozungumza katika kikao hicho alichokiitisha mjini Mtwara, Januari 27, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

UGONJWA WA UKOMA HAUNA UHUSIANO NA IMANI ZA KISHIRIKINA-Dkt Ndugulile -

$
0
0
Na WAMJW -Mvomero, Morogoro.

“Ugonjwa wa ukoma hausababishwi na imani za kishirika bali ni vimelea vya magonjwa ambavyo huingia ndani ya mwili na kusababisha ukoma”

Hiyo ni kauli ya Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipokuwa akizungumza na waathirika wa ugonjwa wa ukoma pamoja na wananchi katika maadhimisho ya siku ya Ukoma Duniani, wilayani Mvomero, katika Mkoa waMorogoro.

Dkt. Ndugulile amewaasa wananchi kuachana na imani za kishirikina kwa kuamini kuwa ya kwamba ugonjwa huo unahusika moja kwa moja na imani hizo za giza.

“Dhana ya kwamba ugonjwa huu ni wa kurogwa siyo kweli, ugonjwa wa ukoma hausababishwi na mtu kulogwa wala kutupiwa jini bali ni vimelea ambavyo huingia mwilini na kusababisha ugonjwa wa ukoma, ni watu kama mimi na wewe” anasema Dkt Ndugulile.

Aidha Dkt Ndugulile ametumia nafasi hiyo kuwaelimisha wananchi kuwa ugonjwa wa ukoma unatibika na kusema kuwa dawa za kutibu ugonjwa huo zipo na kuwaondolea hofu ya kuwa ugonjwa huo kutotibika. Hata hivyo Dkt. Ndugulile ametoa rai kwa wananchi wote kujitokeza mapema katika vituo vya kutolea huduma za afya kupata huduma za matibabu pindi wanapohisi kuwa na dalili za ugonjwa wa ukoma.

“Mtu yeyote ambaye anaanza kuona mabadiliko kwenye ngozi yake, anapata mabaka ambayo hayaelewi au kupoteza hisia pindi unapojigusa ni muda wa kwenda hospitalini kufanya uchunguzi na kama utagundulika kuwa na vimelea vya ugonjwa wa ukoma utapewa matibabu” alisisitiza Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile amewataka wananchi kuwa mabalozi wa kuwaelimisha watu wengine juu ya dalili na athari za ugonjwa wa ukoma. “Niwaombe ndugu wananchi tuendelee kutoa elimu kuhusiana na ugonjwa huu ni ugonjwa ambao tunaweza tukauzuia na tusiwe na athari kwenye jamii na tusingependa kuona kwenye zama hizi watu wanapata athari za kudumu na wanapoteza viungo, hisia katika sehemu za miili yao au kuharibika ngozi kwa sababu ya kutopata matibabu mapema” alifafanua Dkt Ndugulile.

Naibu Waziri huyo wa Afya amesema kuwa Serikali ipo katika hatua nzuri za kutokomeza ugonjwa wa ukoma nchini licha ya changamoto ambazo zipo katika baadhi ya maeneo sugu ambayo ugonjwa huo umeonekana kuwa ni tatizo. “Takwimu zinaonyesha kuwa takribani watu 1993 huugua ugonjwa wa ukoma kila mwaka huku mikoa ya Lindi, Rukwa, Mtwara, Pwani, Tanga, Geita, Dodoma, Tabora, Kigoma na Mkoa wa Morogoro ikiwa na idadi kubwa ya wagonjwa” alisema Dkt. Ndugulile.

Sasa hivi tumepiga hatua kubwa, tunajua jinsi gani ugonjwa unaambukizwa, na namna ya kuutibu pamoja na kujikinga dhidi ya maambukizi mapya, naamini kwa mikakati iliyopo tunaweza kuutokomeza ugonjwa huu.

Akizungumiza mikakati iliyopo Dkt Ndugulile amesema kuwa pamoja na elimu ambayo wamekuwa wakiitoa, Serikali imehamishia nguvu kwenda kwenye jamii moja kwa moja kuwabaini wagonjwa wa ukoma. “Hatusubiri watu watufate, tumewekeza nguvu nyingi kwenye jamii na kuwafikia huko huko maeneo wanayoishi” alisema Dkt Ndugulile.

Kwa upande mwingine, Dkt Ndugulile amezindua Mpango wa Kingatiba ya Ugonjwa wa Ukoma mahususi kwa wale ambao wamekuwa wakiishi na wagonjwa wa ukoma ili waweze kujikinga kutopata ugonjwa huo na kutoa rai kwa wananchi wote ambao wamekuwa wakiishi na wagonjwa wa ukoma kujitokeza katika vituo vya huduma za afya kumeza dawa hizo za kujikinga na ukoma.

“Mtu mwenye ukoma na ambaye amekunywa dawa za kingatiba hawezi kusambaza ugonjwa huu na tunaweza kuishi na kushirikiana naye kufanya shughuli mbalimbali kimaendeleo” alisema Dkt Ndugulile na kuwaasa wananchi kuacha tabia za kuwanyanyapaa wenye ukoma.

Dkt Ndugulile ameipongeza taasisi ya GLRA kutoka Ujerumani inayojihusisha na kuwatunza watu wenye ukoma kwa kuwaanzishia miradi ya ujasiriamali na kuwaunganisha wahanga wa ugonjwa huo na jamii pamoja na kuwapongeza pia wagonjwa wa ukoma kujishughulisha na shughuli za uzalishaji kipato kuliko kuwa omba omba barabarani.

Awali akitoa salamu zake Rais wa Taasisi ya GLRA Bw. Patric Meisen amesema kuwa anafuraha kuona Tanzania na Ujerumani zikiwa na mahusiano mazuri na kuahidi kuendelea kuwasaida waathirika wa ugonjwa ukoma nchini.

“Tumekuwa tukifanya kazi na wataalam wa afya katika kuwatunza waathirika waugonjwa wa ukoma, hatujaishia hapo tuu, tumewasaidia waathirika wa ugonjwa huu kwa kuwapatia mitaji itakayowasaidia kujiongezea kipato ambacho kitawasaidia” alisema Bw. Meisen.

Siku ya Ukoma Duniani huadhimishiwa kila jumapili ya mwisho wa mwezi Januari, ambapo kwa mwaka huu 2019, maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika Wilayani Mvomero, Mkoa wa Morogoro yakiwahusisha wadau mbalimbali wa Sekta ya afya huku kauli mbiu ikiwa ni “Tutokomeze Ubaguzi, Unyanyapaa na Chuki dhidi ya Waathirika wa Ukoma”

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia)akisalimiana na Mzee Anthony Martin (kushoto) wakati alipotembelea makazi ya wasiojiweza ya Chazi, Katika Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akisalimiana na Rais wa Taasisi ya GLRA bw. Patric Meisen kutoka Ujerumani inayowahudumia waathrika wa ukoma nchini.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akisalimiana na Bi. Christina Mohammed (kulia) mhanga wa ugonjwa wa ukoma katika makazi ya watu wasiojiweza ya Chazi yaliyopo Wilayani Mvomero, Morogoro.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia) akisalimiana na wazee waliopata msaaada wa viatu vya kutembelea toka Taasisi ya GLRA inayowasaidai watu wenye ugonjwa wa ukoma nchini.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akitoa kingatiba kwa mtoto aliyekuwa akiishi na mgonjwa wa ukoma. Kingtiba hiyo itamlinda dhidi ya ugonjwa wa ukoma imezinduliwa na Dkt. Ndugulile katika maadhimisho ya siku ya Ukoma Duniani yaliyofanyika Wilayani Mvomero, Morogoro.




Picha ya pamoja, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulike (wa nne kutoka kushoto, walioketi) akiwa na wadau wa Sekta ya Afya nchini.

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Majaji wa Mahakama ya Rufani, Mahakama Kuu, Wakuu wa Wilaya 2 na DED 10

Benki ya DTB-Tanzania yaendesha Warsha kwa Wateja wake jijini dodoma

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe akiwasili kwa ajili ya hafla ndogo ya chakula na vinywaji kwa wateja na wadau wa DTB Tanzania iliyofanyika katika hoteli ya Nashera mjini Dodoma hivi karibuni. Pamoja nae kutoka kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu ya TTCL Waziri Kindamba, Mwakilishi wa hoteli hiyo Phoebe Geoffrey na Meneja Maendeleo na Biashara wa DTB Tanzania Magusa Nhende. 
Baadhi ya wageni waalikwa, maafisa wa Serikali na wateja wa DTB Tanzania katika hafla ndogo ya chakula na vinywaji kwa wateja na wadau wa DTB Tanzania iliyofanyika katika hoteli ya Nashera mjini Dodoma hivi karibuni.
Mgeni ramsi, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe akitoa hotuba fupi katika hafla ndogo ya chakula na vinywaji kwa wateja na wadau wa DTB Tanzania iliyofanyika katika hoteli ya Nashera mjini Dodoma hivi karibuni.
Mkuu wa kitengo cha TEHAMA wa DTB Tanzania, Bi. Stella Masha (mwenye mtandio wa pinki) akimkaribisha Mgeni rasmi, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dk. Harrison Mwakyembe kuhudhuria hafla ndogo ya chakula na vinywaji kwa wateja na wadau wa DTB Tanzania iliyofanyika katika hoteli ya Nashera mjini Dodoma hivi karibuni. Kutoka kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu ya TTCL Waziri Kindamba na Katibu wa Waziri Andrew Magombana.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe akisalimiana na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba wakati wa hafla ndogo ya chakula na vinywaji kwa wateja na wadau wa DTB Tanzania iliyofanyika katika hoteli ya Nashera mjini Dodoma hivi karibuni.





Meneja Maendeleo na Biashara wa DTB Tanzania, Magusa Nhende akizungumza na wateja wenye biashara ndogondogo na wadau wa benki hiyo kutoka mji wa Dodoma na vitongoji vyake katika semina ya siku moja iliyojadili kwa kina kanuni za uendeshaji wa biashara na udhibiti wa mapato, sharia ya kazi na mwenendo wa Uchumi Tanzania. Warsha hiyo iliandaliwa na DTB Tanzania kwa kushirikiana na PKF Associates jijini Dodoma hivi karibuni.


Mtendaji wa Kampuni ya PKF Associates, Muntansir Gulamhussein akizungumza na wateja wenye biashara ndogondogo na wadau wa DTB Tanzania kutoka mji wa Dodoma na vitongoji vyake katika semina ya siku moja iliyojadili kwa kina kanuni za uendeshaji wa biashara na udhibiti wa mapato, sharia ya kazi na mwenendo wa Uchumi Tanzania. Warsha hiyo iliandaliwa na DTB Tanzania kwa kushirikiana na PKF Associates jijini Dodoma hivi karibuni. Kulia ni Meneja wa Maendeleo na Biashara wa DTB Tanzania, Magusa Nhende.

 

Benki ya DTB-Tanzania, leo imeendesha warsha ya siku moja kwa wateja wake wenye biashara ndogondogo na kati waliopo katika mji wa Dodoma na vitongoji vyake. Warsha hii ya siku moja iliyofanyika katika hoteli ya Nashera, iliandaliwa kwa ushirikiano na kampuni ya PKF Associates; ambao ni wataalam wa utunzaji mahesabu, kodi na uendeshaji wa biashara.

Maswali yaliyojadiliwa kwa kinaga ubaga ni kanuni za uendeshaji wa biashara na udhibiti wa mapato, sharia ya kazi na mwenendo wa Uchumi Tanzani na dunia kwa ujumla.

Waendesha warsha kutoka PKF Associates walichanganua kwa undani marekebisho mbalimbali na miongozo katika ulipaji wa kodi na mambo mbali mbali yanayohusisha sheria za kazi nchini. Wageni waalikwa (wateja wa Benki ya Diamond Trsut) walipata kujua bidhaa na huduma mbalimbali zitolewazo na benki, zikiwemo dhamana za benki, mikopo mbalimbali, mikopo ya bima, huduma za kutuma na kupokea fedha ndani na nje ya nchi.

Akiongea na waandishi wa habari katika warsha hiyo, Mkurugenzi mtendaji na Meneja mkuu wa DTB Tanzania, Ndugu Viju Cherian, alisema “Tumeweka lengo la kufanya warsha kama hii katika miji yote tuliyo na matawi ili kuzungumza na wafanyabiashara wadogo na wa kati mikakati mizuri ya biashara bora: kuweka rekodi za biashara, kanuni za biashara na upangiliaji wa matumizi ya mikopo ya kibenki, ambazo ni vitu muhimu katika uendeshaji wa biashara”.

Wageni waalikwa katika warsha hiyo walipata nafasi ya kuzungumza na viongozi kutoka DTB-Tanzania na kubadilishana ujuzi wa kazi pamoja na ubunifu wa biashara katika sekta mbalimbali kwa mfano Biashara, Viwanda, Usafirishaji, Ujenzi. “Warsha hii ni sehemu muhimu sana katika kukuza uchumi na sekta ya biashara ndogondogo na kati na inahitaji kupewa kipaumbele.Tumetoa mikopo zaidi ya Shs. bilioni 285 kwa biashara ndogondogo na kati. Hii ni asilimia 40% ya mikopo yote iliyotolewa na benki yetu”. Ndugu Viju aliongeza.

DTB Tanzania kwa sasa ina matawi 28 nchini, 14 kati ya hayo yakiwa jijini Dar es Salaam kama ifuatavyo (Mtaa wa Jamaat, Masaki, Morocco, Magomeni, Mbezi, Mbagala, Nyerere, Kariakoo, Tawi la Nelson Mandela, Upanga lililo barabara ya Umoja wa Mataifa na Tawi la CBD lililo kwenye makutano ya barabara za Samora na Mirambo) jingine ni Tawi Mbezi Chini lililo Kata ya Kawe na tawi jipya kabisa la Mlimani City. Matawi mengine yakiwemo matawi mawili kwa miji ya Mwanza na Arusha na tawi moja katika miji ya Dodoma, Kahama, Mbeya, Morogoro, Moshi, Mtwara, Mwanza, Tabora, Tanga na visiwa vya Zanzibar.

DTB Tanzania ni kampuni tanzu ya makampuni ya DTB (DTB Group) yanayoendesha shughuli za kibiashara katika ukanda wa Africa Mashariki nchini Kenya, Uganda na Burundi. DTB Tanzania pia ni kampuni tanzu ya Mfuko wa Aga Khan wa Maendeleo ya Kiuchumi (The Aga Khan Fund for Economic Development – AKFED) ambayo ni tawi la Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (Aga Khan Development Network -AKDN)

MDAU WA MAENDELEO ACHANGIA MILIONI 15 KUSAIDIA UJENZI WA MADARASA WILAYANI TUNDURU

$
0
0


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Nalika Said Masudi kulia,akikabidhi shlingi milioni 15 kwa mkuu wa wilay ya Tunduru mkoani Ruvuma Juma Homera ili kusaidia ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule za sekondari Namwinyu,Ligunga na Matemanga,katikati ni mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Tunduru Gaspar Balyomi na mwenyekiti wa halmashauri hiyo Mkwanda Sudi

SHONZA AZINDUA MIRERANI TANZANITE MARATHON

$
0
0
Muandaaji wa michuano ya riadha ya Mirerani Tanzanite Marathon, Charles Mligo (Mnyalu) akizungumza kwenye uzinduzi wa mashindano hayo.
Muandaaji wa michuano ya riadha ya Mirerani Tanzanite Marathon, Charles Mligo (Mnyalu) akizungumza kwenye uzinduzi wa mashindano hayo
Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, mhandisi Zephania Chaula akimkaribisha Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza ili kuzindua michuano ya riadha ya Mirerani Tanzanite Marathon. 
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza akizindua mashindano ya riadha ya Mirerani Tanzanite Marathon yaliyofanyika mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Yefred Myenzi akionyesha medali ya shaba baada ya kuwa miongoni mwa washindi wa kilomita tano katika michuano ya Mirerani Tanzanite Marathon. 
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza akiongoza mbio za kilomita tano katika michuano ya riadha ya Mirerani Tanzanite Marathon yaliyofanyika mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.
Baadhi ya wakazi wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakishuhudia mbio za Mirerani Tanzanite Marathon zikitaka kuanza. 
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza akiwa na baadhi ya wanariadha walioshiriki mbio za Mirerani Tanzanite Marathon yaliyofanyika mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. 

…………………………….

MWANARIADHA mwanajeshi wa JWTZ Faraja Damas ameng’ara kwenye mbio za Mirerani Tanzanite Marathon kilomita 21 zilizozinduliwa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza, baada ya kushika nafasi ya kwanza kwa kutumia muda wa saa 1:14.

Katika mbio hizo zilizofanyika mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Michael Joseph alishika nafasi ya pili kwa kutumia saa 1:34.

Mshindi wa tatu alikuwa Stephano Huche aliyetumia muda wa saa 1:34 huku Failuna Mtanga akishika nafasi ya kwanza kwa wanawake katika kilomita 21 kwa kutumia saa 1:09. 

Angelina Daniel alishika nafasi ya pili kwa wanawake kilomita 21 kwa saa 1:14 na nafasi ya tatu ni Rosalina Fabian kwa saa 1:16 na mbio za watoto kilomita tano wanafunzi wa shule ya awali na msingi ya Blue Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani, Sarah Barakael, Clara Flavian na Shangwe Isack, walingara kwa kuongoza michuano hiyo. 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza akizungumza wakati akizindua mbio hizo aliwataka maofisa michezo wa mikoa na wilaya kufuatilia vipaji vya michezo mashuleni na kutokaa maofisini. 

Shonza alisema vipaji vingi vipo kwenye ngazi za shule hivyo maofisa michezo wa wilaya na mikoa wafuatilie hilo kwa manufaa ya sekta ya michezo nchini. 

Alisema ana wapongeza waandaaji wa mashindano hayo ambayo japokuwa ni mara ya kwanza lakini wamejitahidi kuepuka changamoto mbalimbali ambazo huwa zinajitokeza kwenye michezo mbalimbali. 

Mkuu wa wilaya ya Simanjiro mhandisi Zephania Chaula alisema mashindano hayo yametumika kuweka historia ya mashindano makubwa ya riadha kufanyika kwenye eneo la mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro. 

Mhandisi Chaula alisema katika wilaya hiyo hakujawahi kufanyika mashindano ya riadha ila kupitia Mirerani Tanzanite Marathon jina la Simanjiro linaingia kwenye historia ya kufanyika mashindano makubwa. 

Katibu wa shirikisho la riadha Tanzania, Wilhelim Gidabuday alisema baadhi ya wakenya walizuiwa kushiriki michuano hiyo baada ya kukosa vibali. Gidabuday alisema hawana nia mbaya ya kuwazuia wakimbiaji hao wanne wa Kenya ila kutokana na kutokuwa na vibali hivyo hawakuruhusiwa kushiriki. 

Muandaji wa mashindano hayo ya Tanzanite Mirerani Marathon, Charles Mligo (Mnyalu) alisema lengo la mashindano hayo ni kuunga mkono jitihada za Rais John Magufuli kwa kutangaza utalii wa madini ya Tanzanite. 

Mnyalu alisema baada ya Rais Magufuli kuagiza ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite kujengwa nao wakaamua kuanzisha mashindano hayo ili kutangaza madini ya Tanzanite ambayo hapa duniani yanapatikana mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara pekee

UJUMBE WA MFUKO WA SHEIKH KHALIFA FUND FOR ENTERPRISE DEVELOPMENT WATEMBELEA ZANZIBAR

$
0
0
MKURUGENZI wa Mfuko wa ‘KhalifaFund’ Naizar Cheniour, amesema mfuko huo umeazimia kuwawezesha vijana wa Zanzibar katika nyanja mbali mbali za kiuchumi ili kuweza kujiajiri na kuinua hali zao za maisha.

Mkurugenzi huyo amesema hayo leo wakati alipozungumza na waandishi wa habari, mara baada ya ujumbe wa Mfuko huo ulipowasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume.

Ujumbe huo upo nchini kwa ziara maalum, ikiwa ni muendelezo wa mazungumzo na Serikali, yenye lengo la kufanikisha utekelezaji wa programu mbali mbali katika sekta za biashara, ujasiriamali, miundombinu na nyenginezo.

Alisema Mfuko umelenga kuwawezesha vijana wa Zanzibar katika upatikanaji wa rasilimali fedha, utaalamu na masuala ya kiufundi ili waweze kujiajiri kupitia shughuli za ujasiriamali na hivyo kuweza kujitegemea.Aliwataka vijana na Wazanzibari kwa ujumla kutarajia mafinikio makubwa kutokana na program mbali mbali zitakazotekelezwa kupitia Mfuko huo.

Alisema mfuko wa KhalifaFund, una uzoefu mkubwa katika utekelezaji wa programu za maendeleo na shughuli za kiuchumi, ambapo umekuwa ukifanya kazi hizo katika nchi mbali mbakli duniani.Mapema, Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Viwanda, Dk. Juma Ali Juma alisema ujio wa Viongozi wa Mfuko wa’ KhalifaFund’ umelenga kukamilisha mazungumzo yaliofikiwa katika kikao kilichopita ili kuwa tayari kwa utekelezaji wa yale yalioafikiwa.

Alisema mfuko huo wa kifedha, wenye makao makuu yake Abu Dhabi ,UAE utatowa msukumo mkubwa katika utekelezaji wa program mbali mbali za kimaendeleo na kiuchumi, sambamba na kuwawazesha vijana kupitia kazi za ujasiriamali.Alisema wakati ukiwa nchini utakutana na kufanya mazungumzo na taasisi mbali mbali za Serikali pamoja na kutembelea maeneo tofauti.

Hii ni mara ya pili kwa viongozi wa Mfuko wa ‘KhalifaFund’ kuja nchini kwa ajili hiyo, ambapo kabla ulipata fursa ya kutembelea sekta tofauti za maendeleo na kiuchumi Unguja na Pemba.Aidha, ujio wa mfuko huo unafutia ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein aliyoifanya Umoja wa nchi za Falme ya Kiarabu (UAE) Januari mwaka uliopita.
KATIBU Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda Zanzibar Ndg.Juma Ali Juma, akisalimiana na Afisa wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development Ndg. Abdulah Al Jarwani, wakati wakiwa sili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, kwa ziara ya siku tatu kutembelea Miradi mbalimbali Zanzibar.(Picha na Ikulu)
KATIBU Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda Zanzibar Ndg Juma Ali Juma, akizungumza na Ujumbe wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development ya Abudha Dhabi UAE, ulipowasili Zanzibar kwa ziara ya Siku Tatu ukiongozwa na Mkurugenzi Nizar Cheniour, mwenye fula nyeusi. wakiwa katika ukumbi wa VIP uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, baada ya kuwasili kwa ziara ya siku tatu Zanzibar.(Picha na Ikulu)
KIONGOZI wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development wa Abu Dhabi UAE, ukiongozwa na Mkurugenzi Ndg. Nazar Cheniour, akizungumza na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, kutembelea Miradi mbalimbali ya Maendeleo Zanzibar.(Picha na Ikulu)
AFISA wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development Ndg. Ali Al Saad, akipata maelezo ya kutoka kwa Mkurugenzi wa Ushirika wa Fakirice Milling Enterprises wa Kisongoni Ndg. Yussuf Faki Yussuf, akitowa maelezo ya usagaji wa mpuga katika ushirika wao wakati walipotembelea ushirika huo leo.(Picha na Ikulu)
KATIBU Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda Ndg Juma Ali Juma, akitowa maelezo kwa Kiongozi wa Ujumbe wa Mfuko wa Khalifa Fund for Enterprise Development Ndg. Nizar Cheniour, walipotembelea Ushirika wa Fakirice Milling Enterprises Kisongoni,unaojishughulisha na kukoboa mpunga.(Picha na Ikulu)

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 28,2019

OHOOOOO...! MWENDESHA PIKIPIKI ANUSURIKA KIFO

$
0
0
Jana katikati ya makutano ya barabara ya Goba na Morogoro eneo la Mbezi jijini Dar es Salaam mwendesha pikipiki aligongwa na gari kama aonekanavyo pichani, dereva huyo wa boda boda alinusurika kifo.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
wasamalia wema wakisaidia kunyanyua pikipiki yake hiyo pamoja na Mizigo aliyokuwa amebeba.

MADIWANI MKURANGA WAKAGUA MAENEO YA UWEKEZAJI.

$
0
0
Mwenyekiti wa kamati ya Uchumi na ujenzi na mazingira,ambae ni Diwani wa kata Tengerea,Shabani Manda akizungumza na wadau mbalimbali wa maendele leo katika ziara ya madiwani ya kutembelea maeneo mbalimba ya uwekezaji katika kata ya Mbezi wilaya ya Mkuranga mkoa Pwani.
Diwani wa kata ya Mbezi,Rashid Selungwi (katikati) akisisitiza jambo mbele ya wadau wa maendeo katika ziara ya madiwani ya kutembelea maeneo mbalimbali ya uwekezaji leo wilaya ya Mkuranga mkoa Pwani.
Madiwani pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo wilaya ya Mkuranga mkoa Pwani, wakimsikiliza Mwenyekiti wa kamati ya uchumi,ujenzi na Mazingira ambaye ni Diwani wa kata ya Tengerea,Shabani Manda alipokuwa akizungumza nao, mara baada ya ziara ya kukagua maeneo mbalimbali ya uwekezaji.

SERIKALI YAFUTA KODI YA PANGO LA ARDHI KWA TAASISI NA MADHEHEBU YA DINI NCHINI

$
0
0
SERIKALI Imefuta kodi ya pango la ardhi kwa Taasisi na Madhehebu ya dini nchini kuanzia mwaka wa fedha wa 2018/2019.

Hatua hiyo imetangazwa leo Jumapili Januari 27, 2019 na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi jijini Mbeya wakati wa ibada ya kuwaweka wakfu viongozi wa Jumuiya Kuu ya Kanisa la Kibaptisti Tanzania (BCT).

Lukuvi amesema Rais Magufuli ameiagiza wizara hiyo kutoyatoza kodi madhehebu ya dini kwa sehemu ambazo zimeandaliwa kwa ajili ya kufanyia ibada.

"Rais ameagiza kuanzia Julai mosi mwaka huu wa fedha madhehebu ya dini yasilipe kodi ya ardhi kwa maeneo ambayo huduma za maombi na ibada zinatolewa, hata hivyo msamaha huu hauhusu maeneo ambayo kuna miradi ya kuingiza fedha ambayo tunajua madhehebu mengi yameanzisha," amesema Lukuvi.

Lukuvi amefafanua maagizo hayo tayari yametolewa kwa makamishna wa ardhi wa kanda na mikoa pamoja na maofisa ardhi wa majiji, manispaa na halmashauri nchi nzima.Hata hivyo, Lukuvi ametoa nafasi ya kukutana na viongozi wa dini ambao wana migogoro ya ardhi kwenye maeneo ambayo wanatoa huduma.

"Najua kuna migogoro mingi kwenye maeneo ambayo mnatoa huduma hivyo nawakaribisha ofisini kwangu Dodoma na kama migogoro itakuwa mikubwa nitafika mpaka eneo la mgogoro," amesema Lukuvi.

“Wizara yangu imepewa jukumu la kutatua migogoro ya ardhi kabla ya mwaka 2020 na tusipotatua migogoro ya dini inaweza kupelekea uvunjifu wa amani nchini hivyo hatutaki kuifuga migogoro iliyopo,” amesema.

Awali, askofu wa kanisa la Baptisti nchini, Arnold Manase amesema kanisa lake ni moja ya madhehebu yanayoongoza kuwa na migogoro ya ardhi na baadhi ya waumini wa kanisa hilo.

"Kwa kuwa waziri mwenye dhamana upo naomba nafasi nije ofisini kwako nikueleze migogoro iliyopo ndani ya kanisa langu ili uangalie namna ya kuitatua maana migogoro imekithiri mpaka kufikia hatua ya kujenga makundi miongoni mwa waumini," amesema Manase.
Viewing all 109936 articles
Browse latest View live




Latest Images