Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109933 articles
Browse latest View live

TANZANIA PRESS PHOTOGRAPHERS INVITED TO JOIN IN WORLD PRESS EXHIBITION


Habari za UN, Jnauari 24, 2019

RWLI TV: MTO MKONDOA WAPATA DAWA ,WAHANDISI WAANZA KUUDHIBITI USIHARIBU TUTA LA RELI KILOSA GULWE

Ajali kazini

$
0
0
Mmoja wa waendesha pikipiki wa kata Bupu Wilaya ya Mkuranga mkoa wa  Pwani akiwa amepakia mzigo wa mkaa katika pikipiki  huku akiwa hajavaa  kofia ngumu pamoja na viatu  jambo ambalo ni hatalisha  kwa usalama wake kama anavyo onekana pichani (Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
 Ajali kazini.
wasamalia wema wakafika na kumsaidia kunyanyua pikipiki yake  pamoja na Mizigo aliyokuwa amebeba.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 25,2019

TIMUYA USULUHISHI WA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI YATUA MKURANGA

$
0
0
Timu ya kitaifa ya kushughulikia migogoro ya wakulima na wafugaji imefanya ziara wilayani Mkuranga ,lengo ikiwa ni kutatua migogoro ya aina zote  za ardhi na kuiainisha.

Akizungumza wakati wa ziara wilayani Mkuranga mkoa wa pwani,kiongozi wa timu ya serikali ya ufuatiliaji wa migogoro ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi Dkt.Martin Ruheta amesema timu hiyo sio ya kisiasa bali ni ya kitendaji na matarajio yao mpaka ifikapo 2020 itakuwa imepatiwa suluhu kama sio kwisha kabisa.

Aidha Dkt.Ruheta amewaahidi wanachi hao kuwa watahakikisha migogoro yao inapatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa sababu tume yao ipo makini.

Kwa upande wake katibu wa mbunge wa jimbo la Mkuranga Omary kisatu amewaomba wanachi hao kuwa na imani na tume hiyo."wakulima na wafugaji naomba muendelee kudumisha amani na utulivu iliyopo,tume hii ni ya kitaifa ya kuhakikisha haki ya mkulima na mfugaji inapatikana ."alisema Kisatu

Hata hivyo tume hiyo inaundwa na watu mbalimbali akiwemo Ofisa kutoka ofisi ya Rais,Wizara ya Ardhi,Wizara ya mambo ya ndani ya nchi,Ofisa wa ardhi na wa maliasili,lengo kuu ni kuhakikisha migogoro  ya ardhi inakwisha nchini
 Kiongozi wa Timu ya Serikali ya ufuatiliaji na Utatuzi wa Migogoro na watumiaji wengine wa Ardhi Dkt.Martin Ruheta akizungumza na wakulima pamoja na wafugjia wa kata ya Bupu wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
Kiongozi wa timu ya Serikali  ya ufuatiliaji,Utatuzi  wa Migogoro ya watumiaji wa Ardhi, Dkt.Martin Ruhete(kushoto) akiteta jambo na  Katibu wa Mbunge wa jimbo la Mkuranga,Omary Kisatu.
Katibu Mkuu wa  Chama cha wafugaji Tanzania, Magembe  Makoye akiwasihi wafugaji wa kijiji cha Matanzi kata ya Beta wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani, kutulia na kusubiri taratibu za serikali.

EXCLUSIVE: MWANAFUNZI ALIYEONGOZA KIDATO CHA NNE KITAIFA ATOA SIRI YA MAFANIKIO

EXCLUSIVE: PIKIPIKI YA KIBABE MADE IN MBEYA


AWEZO AITISHA MKUTANO KUJADILI CHANGAMOTO YA UPATIKANAJI MAJI CHALINZE.

$
0
0
Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amemtaka Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Kitila Mkumbo kuitisha haraka Mkutano kwa Wadau wote wanaohusika na Mradi wa Maji Chalinze Jumanne ya Januari 29, mkutano utakaojadili changamoto za upatikanaji Maji katika Halmashauri hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada yakutembelea Mradi huo katika eneo la Chalinze, Mhe. Aweso amesema mpaka sasa mradi huo umefika asilimia 78 na Serikali imewekeza zaidi ya Shilingi Bilioni 95 kuhakikisha Wananchi wa Chalinze wanapata Maji yakutosha. 

Katika ziara yake hiyo, Mhe. Aweso amesema ameona changamoto katika uendeshaji wa mradi huo ikiwemo vituo vya Maji zaidi ya 200 lakini 86 ndio vinafanya kazi ya utoaji huduma ya Maji pamoja na changamoto ya uendeshaji ikiwa sambamba nakuwapa Watoto wadogo kusimamia vituo hiyo. 

Mhe. Aweso amewata Watendaji wa Wizara hiyo kuhakikisha wanatafuta Wakandarasi wenye weledi na kazi zao ili kuhakikisha miradi hiyo inasimamiwa ipasavyo bila kusuasua licha ya mradi huo kufika asilimia 78. 

"Mkandarasi anayesimamia mradi huu ni changomoto, hatuwezi kumuachia mpaka amalize mradi huu, tayari amechukua fedha zaidi ya asilimia 62 kwenye Bilioni 95", amesema Aweso

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi wa Maji, Chalinze - DAWASA, Mhandisi Modesta Mushi amesema kuwa mradi huo umefika jumla ya asilimia 78 pamoja na ujenzi wa Miundombinu eneo la mtambo, ujenzi wa matenki kufikisha Maji maeneo tofauti na ujenzi wa vitekeo Maji (Viosk) jumla ya 351 maeneo mbalimbali katika eneo la mradi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Bi. Zainabu Kawawa ameshukuru kuona ziara ya Naibu Waziri wilayani humo, amesema wataendelea kusimamia kuhakikisha Mkandarasi wa Mradi wa Maji, Chalinze anamaliza mradi huo kwa wakati licha kuahidi kumaliza Desemba 31, 2018, amesema wanahitaji kuona usimamizi mzuri katika Vitekeo Maji vilivyopo ili kutoa fursa kwa Wananchi wa Chalinze kupata huduma hiyo ya Maji Safi na Salama. 

Utekelezaji wa Mradi huo wa Chalinze, awamu ya tatu unatekelezwa na Mkandarasi Overseas Infrastructure Alliance (India) Private Limited pamoja na Kampuni ya Platiba kwa gharama ya Dollars za Kimarekani Milioni 41.1 ambao ni Mkopo wa gharama nafuu kutoka Serikali ya India.
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akisaidia uchimbaji moja ya Mfereji utakaotumika kutandika mabomba katika eneo la mradi wa Maji, Chalinze.
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akiwa pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA), Mhandisi Cyprian Luhemeja na Msimamizi wa Mradi wa Maji, Chalinze, Mhandisi Modesta Mushi katika eneo la mradi huo. 
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) (aliyevaa Kofia) akishuka chini pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Bi. Zainabu Kawawa (aliyevaa Koti) baada yakukagua moja ya Tenki lililopo kwenye Mradi wa Maji, Chalinze mkoani Pwani. 
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akiteta jambo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA), Mhandisi Cyprian Luhemeja.
Moja ya Tenki lililopo kwenye utekelezaji wa mradi wa Maji, Chalinze.

MAKAMU WA RAIS AMUWAKILISHA RAIS DKT MAGUFULI SHEREHE ZA KUAPISHWA RAIS WA CONGO

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Congo imeandika historia mpya kwa kukabidhiana madaraka kwa upendo na ana imani Viongozi wataendelea kufanya kazi kwa pamoja kwa ajili ya maendeleo na maslahi mapana ya nchi yao.

Makamu wa Rais ambaye alimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameyasema hayo mara baada ya sherehe za kumuapisha Rais mpya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Felix Tshisekedi.

“Linalofurahisha ni kwamba ni mara ya kwanza kwa nchi hii ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufanya uchaguzi wa kidemokrasia na kukabidhiana madaraka kwa usalama kabisa” alisema Makamu wa Rais.

Uchaguzi huo uliofanyika Desemba 30, 2018, Mhe. Felix Tshisekedi alipata takribani kura milioni 7 sawa na asilimia 38.57 ya kura zilizopigwa ambapo wagombea wenzake kama Martin Fayulu alipata ailimia 34 sawa na kura milioni 6.4, Bw. Emmanuel Ramazani Shadary alipata asilimia 23 sawa na takribani kura milioni 4.4. 

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeandika historia kwa mara ya kwanza tangu ilipopata uhuru kwa kukabidhiana madaraka kwa njia ya Amani.
Rais mpya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Felix Tshisekedi.
Rais mpya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Felix Tshisekedi akiteta jambo na Rais wa zamani wa nchi hiyo Mh.Joseph Kabila.

HATUNA TENA TATIZO LA UMEME KATIKA UZALISHAJI WETU,TUNAIPONGEZA TANESCO-WATEJA MKOANI ARUSHA

$
0
0
*Ni kauli ya wateja wakubwa mkoani Arusha wanaomiliki viwanda vikubwa
*Wakiri kuimarika kwa umeme imekuwa chachu kwao kuongeza uzalishaji
Na Said Mwishehe,Arusha

HATUNA tena za umeme katika Mkoa wa Arusha!Hivyo nidvyo ambavyo wamiliki wa viwanda ambavyo vinazalisha bidhaa mbalimbali mkoani Arusha wanavyoeleza baada ya Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO), kuboresha upatikanaji wa umeme.

Wakizungumza mbele ya wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari ambao wamepata nafasi ya kutembelea viwanda vilivyopo mkoani Arusha jana na kupata nafasi ya kuzungumza na baadhi ya wamiliki wa viwanda hivyo wamekiri kwa sasa hali ya umeme inaridhisha kwai huko nyuma hali ilikuwa mbaya na ilisababisha hata uzalishaji wa bidhaa kutofanyika kwa kiwango ambacho walikuwa wanakitarajia.

Wamiliki hao wamesisitiza kuwa kuimarika kwa upatikanaji wa umeme wa uhakika wameongeza uzalishaji huku wengine wakifafanua wameamua kuanzisha na viwanda vingine kwani hivi sasa Serikali kupitia TANESCO imefanya kuwe na uhakika wa kufanya uwekezaji kwani kama hakuna umeme basi hakuna uwekezaji hasa wa viwanda.


Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha Lodhia Steel Industries, Sailesh Pandit amesema kiwanda chao kinatumia umeme wa megawati saba ambapo kwa mwezi wanailipa TANESCO kati ya Sh.milioni 500 hadi 600 kwa mwezi kutokana na uzalishaji wake.

Amefafanua zamani kulikuwa na shida sana yaumeme lakini sana miaka miwili mitatu iliyopita maana umeme ulikuwa unatakatika mara kwa mara lakini sasa hali ni tofauti na hivyo lazima tuwapongeze Serikali na TANESCO kwa juhudi zao za kuboresha umeme.

”Ni kweli huko nyuma kulikuwa na shida ya umeme na sote ni mashahidi lakini leo hii hatuna tatizo la umeme tena.Kama tulipaza sauti kulalamika na hivyo hivyo tupaze sauti zetu kupongeza,”amesema Pandit.

Kuhusu ushirikiano wa kikazi kutoka kwa wafanyakazi wa Tanesco na kiwanda chake, amesema wanashirikiana vema na muda wote linapotokea Tanesco hata ikiwa usiku wa manane hupatiwa ufumbuzi wa haraka na kwa muda mfupi.
“Kwakweli sina cha kusema au kibaya chochote, namna ninavyofanya kazi nao ni very friend manner, mimi ninaweza kumpigia simu Injinia hata saa nane usiku, sina umeme ata respond simu yako hapo hapo na kuchukua hatua wakati kipindi cha nyuma haikuwa hiovyo.

Kwa upande wake Meneja Utawala na Rasilimali Watu wa Kiwanda cha nguo cha Sunflag, Magesa Charles, amesema kwa sasa huduma za umeme zimeboreshwa kwa kiasi kikubwa licha ya kuwepo matatizo madogo ambayo hayathiri shughuli za uzalishaji kama ilivyokuwa miaka miwili iliyopita.

Wakati huo huo Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha A to Z, Viral Shah, amefafanua hakuna tatizo la kukatika kwa kama huko nyuma ila kuna wakati umeme unapungua nguvu.

“Kwa ujumla kumekuwa na maendeleo mazuri ya hali ya umeme ukilinganisha na kipindi cha nyuma, mwito wetu ni kufanyia kazi mapungufu hayo.Hapa kwetu tunatumia megawati 9 hadi 10 kwa mwezi na tunalipa bili zetu Tanesco Sh.bilioni 1.1 kwa kila mwezi na hapa tuna viwanda tisa,” amesema Shah.

Akizungumzia hali hiyo, Meneja Mwandamizi wa Miradi wa Tanesco, Mhandisi Emmanuel Munirabona, ameeleza kama shirika watafuatilia kwa kina kujua hasa nini chanzo cha tatizo hilo la kupungua kwa umeme katika kiwanda hicho.
“Tumefanya maboresho makubwa ya mitambo yetu ikiwa ni pamoja na kupanua vituo sita vya kupoza umeme jijini Arusha, ambavyo vimewezesha wateja wakubwa kufunguwa laini zinazojitegemea ili kuondoa uwezekano wa kukatika kwa umeme na hivyo kuathiri shughuli za uendeshaji.

“ TANESCO tumeamua kuhakikisha tunatafuta ufumbuzi wa changamoto zote kama zipo , lengo letu ni kuhakikisha Tanzania ya viwanda inatekelezwa kwa vitendo na hii itatokana na uwepo wa umeme wa uhakika.

“Ndio maana tumeendelea kuboresha huduma zetu na lengo lake ni kuona hatuna matatizo ya umeme na tayari tumefanikiwa , hivyo tuendelee kutoa rai wawekezaji waje tu nchini kwetu kuwekeza kwani tunao umeme wa kutosha,”amesema.
 Meneja Rasilimali Watu wa Kiwanda cha Sun Flag kilichopo mkoani Arusha akitoa ufafanuzi  kuhusu bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo
 Mfanyakazi wa kiwanda cha TANELEC ambacho kinatengeneza trasfoma akiendelea na majukumu yake katika kiwanda hicho kilichopo Themi mkoani Arusha
 Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha TANELEC wakiendelea na kazi ya kusuka transfoma
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha A to Z  Viral Shah akifafanua jambo kwa wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari waliotembelea kiwandani hapo kuona shughuli za uzalishaji
 Mmoja wa wafanyakazi wa kiwanda cha A to Z mkoani Arusha akiendelea na kazi kiwandani hapo
 Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda cha A to Z wakiendelea na majukumu yao wakati wa hariri wa vyombo vya habari nchini pamoja na maofisa wa Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) walipofanya ziara kiwandani hapo kuona shughuli za uzalishaji pamoja na hali ya upatikaji umeme kwa sasa
 Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha TANELEC mkoani Arusha Zahir Saleh akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari(hawapo pichani) baada ya kutembelea kiwanda hicho ambacho kinatengeneza matransfoma ya umeme nchini
Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda cha TANELEC Zahir Saleh akiwaongoza wahariri na maofisa wa TANESCO kuelekea ndani ya kiwanda hicho ambacho kinatengeneza matransfoma ya umeme.Kiwanda hicho ni moja ya wateja wakubwa wa utumiaji umeme mkoani Arusha

Watumiaji wa Tigo Pesa App kufurahia Huduma Hiyo Pasipo Mbs Zao kutumika

$
0
0

Afisa Biashara Mkuu wa Kampuni ya Tigo Tarik Boudiaf, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya inayojulikana kama #AppanaChezea Tigo Pesa App.

Mkuu wa Huduma za Kifedha wa Tigo Pesa Hussein Sayed akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya inayojulikana kama #AppanaChezea Tigo Pesa App.

Meneja bidhaa, Tigo Pesa App Ian Ludovick akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya inayojulikana kama #AppanaChezea Tigo Pesa App.


Pakua au huisha App yako ya Tigo Pesa bure

Wateja wanaotumia #AppanaChezea Tigo Pesa App kufurahia faida nyingi ikiwamo kurudishiwa ada ya malipo, Mbs na muda wa maongezi

Kampuni ya simu inayoongoza katika maisha ya kidigitali Tanzania, Tigo, imeanza mwaka 2019 kwa kutangaza uzinduzi wa App ya Tigo pesa katika kampeni inayojulikana kama #AppanaChezeaTigo PesaApp campaign.

Kampeni ya #Appana ChezeaTigo Pesa App inaenda sambamba na filosofia ilinayojikita kwenye uvumbuzi na kumjali mteja kwa kutoa suluhisho za kidijitali zinazoendana na matakwa ya wateja tofauti tofauti hapa nchini.

Kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu, Kampuni ya Tigo imewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye mfumo wa malipo ya kidijitali ukilenga kuwapatia wateja huduma za kifedha zinazoendana na dunia ya kisasa. #AppanaChezea Tigo Pesa App campaign ni hatua mpya ya kuboresha uzoefu wa wateja wanaotumia na watakaotumia huduma ya Tigo Pesa. Pamoja na uzoefu huo mpya na wa kipekee, wateja watakaotumia Tigo Pesa App katika kipindi chote cha promosheni watafurahia faida lukuki kama kurudishiwa ada ya kufanya malipo, Mbs pamoja na muda wa maongezi.

Akiongea wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Mkuu wa Huduma za Kifedha wa Tigo Hussein Sayed alisema mteja yeyote wa Tigo anayemiliki simu janja ana kila sababu ya kutumia Tigo Pesa App yenye kukidhi vigezo vya kimataifa vya App na hivyo kumhakikishia mteja urahisi na usalama wa hali ya juu anapofanya miamala yake. Tigo Pesa App pia haitumii data.

“Leo tunayofuraha kuwaletea watumiaji wa simu janja habari njema. Mteja anapopakua au kuhuisha App yake ya Tigo Pesa, atapata dakika za muda wa maongezi na Mbs bure. Pamoja na ofa hii, mteja wa Tigo atakapotuma pesa kwa mteja mwingine wa Tigo atarudishiwa gharama alizotumia kutuma pesa,” alisema Hussein

Kwa mujibu wa Hussein, Tigo Pesa App imetengenezwa kwa kuzingatia usalama wa hali ya juu kwa mteja anapokuwa anafanya miamala yake. Kupitia App hiyo, mteja wa Tigo pia ataweza kufanya malipo kwa zaidi ya taasisi 300 za Serikali ikiwamo Wizara, Mashirika, Mamlaka mbali mbali na watoa huduma za Serikali

Afisa Biashara Mkuu wa Tigo Tarik Boudiaf alisema “Moja kati ya vipau mbele vya Tigo ni kurahisisha maisha ya wateja wake. Kuangalia salio kupitia Tigo Pesa App pia ni rahisi na ni bure. Kununua kifurushi au muda wa maongezi kumerahisishwa zaidi kwa kuwa unachohitajika kufanya ni kufuata hatua tatu rahisi na utakuwa umekamilisha zoezi hilo. Hii ndiyo sababu watu 9 kati ya 10 wanaotumia Tigo Pesa wameridhika na huduma hii na wanawashauri wasiotumia kuitumia,”

Ikiwa rahisi,haraka na yenye ufanisi kwenye matumizi # AppanaChezea Tigo Pesa App campaign inawaletea wateja App bora na rahisi kutumia kuliko App nyingine zinazofanana nayo zilizopo sokoni. Tigo inamshauri kila mteja kuwa sehemu ya safari ya maisha ya kidijitali kwa kutumia huduma za kidijitali za kifedha zinazotolewa na Tigo. Uvumbuzi huu unaendelea kuwawezesha wateja na wafanyabiashara wa Kitanzania kupata huduma za kifedha pamoja kwa njia ya kidijitali na kuyafanya maisha yao yawe rahisi.

TAARIFA WA UMMA

AWESO AITISHA MKUTANO KUJADILI CHANGAMOTO YA UPATIKANAJI MAJI CHALINZE.

$
0
0
Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amemtaka Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Kitila Mkumbo kuitisha haraka Mkutano kwa Wadau wote wanaohusika na Mradi wa Maji Chalinze Jumanne ya Januari 29, mkutano utakaojadili changamoto za upatikanaji Maji katika Halmashauri hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada yakutembelea Mradi huo katika eneo la Chalinze, Mhe. Aweso amesema mpaka sasa mradi huo umefika asilimia 78 na Serikali imewekeza zaidi ya Shilingi Bilioni 95 kuhakikisha Wananchi wa Chalinze wanapata Maji yakutosha. 

Katika ziara yake hiyo, Mhe. Aweso amesema ameona changamoto katika uendeshaji wa mradi huo ikiwemo vituo vya Maji zaidi ya 200 lakini 86 ndio vinafanya kazi ya utoaji huduma ya Maji pamoja na changamoto ya uendeshaji ikiwa sambamba nakuwapa Watoto wadogo kusimamia vituo hiyo. 

Mhe. Aweso amewata Watendaji wa Wizara hiyo kuhakikisha wanatafuta Wakandarasi wenye weledi na kazi zao ili kuhakikisha miradi hiyo inasimamiwa ipasavyo bila kusuasua licha ya mradi huo kufika asilimia 78. 

"Mkandarasi anayesimamia mradi huu ni changomoto, hatuwezi kumuachia mpaka amalize mradi huu, tayari amechukua fedha zaidi ya asilimia 62 kwenye Bilioni 95", amesema Aweso

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi wa Maji, Chalinze - DAWASA, Mhandisi Modesta Mushi amesema kuwa mradi huo umefika jumla ya asilimia 78 pamoja na ujenzi wa Miundombinu eneo la mtambo, ujenzi wa matenki kufikisha Maji maeneo tofauti na ujenzi wa vitekeo Maji (Viosk) jumla ya 351 maeneo mbalimbali katika eneo la mradi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Bi. Zainabu Kawawa ameshukuru kuona ziara ya Naibu Waziri wilayani humo, amesema wataendelea kusimamia kuhakikisha Mkandarasi wa Mradi wa Maji, Chalinze anamaliza mradi huo kwa wakati licha kuahidi kumaliza Desemba 31, 2018, amesema wanahitaji kuona usimamizi mzuri katika Vitekeo Maji vilivyopo ili kutoa fursa kwa Wananchi wa Chalinze kupata huduma hiyo ya Maji Safi na Salama. 

Utekelezaji wa Mradi huo wa Chalinze, awamu ya tatu unatekelezwa na Mkandarasi Overseas Infrastructure Alliance (India) Private Limited pamoja na Kampuni ya Platiba kwa gharama ya Dollars za Kimarekani Milioni 41.1 ambao ni Mkopo wa gharama nafuu kutoka Serikali ya India.
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akisaidia uchimbaji moja ya Mfereji utakaotumika kutandika mabomba katika eneo la mradi wa Maji, Chalinze.
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akiwa pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA), Mhandisi Cyprian Luhemeja na Msimamizi wa Mradi wa Maji, Chalinze, Mhandisi Modesta Mushi katika eneo la mradi huo. 
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) (aliyevaa Kofia) akishuka chini pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Bi. Zainabu Kawawa (aliyevaa Koti) baada yakukagua moja ya Tenki lililopo kwenye Mradi wa Maji, Chalinze mkoani Pwani. 
Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) akiteta jambo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA), Mhandisi Cyprian Luhemeja.
Moja ya Tenki lililopo kwenye utekelezaji wa mradi wa Maji, Chalinze.

MRADI WA SGR : UJENZI WA TUTA JIPYA,MAKARAVATI NA UWEKAJI WA RELI WAENDELEA KWA KASI KIDETE-GODEGODE MKOANI MOROGORO

$
0
0
 Kazi ya Kuhamisha kipande cha reli chenye urefu wa Kilometa 1.3 ikiendelea eneo la Kidete - Godegode umbali wa KM 337 - 338 ili kudhibiti mafuriko ya mto Mkondoa  yanayoathiri miundombinu ya reli na kupelekea kusitishwa kwa Huduma za Usafiri wa reli mara kadhaa wakati wa mvua kubwa. Kazi inajumuisha ujenzi wa tuta jipya la reli, ujenzi wa Makalavati pamoja na uwekaji wa reli katika tuta jipya hivi karibuni Januari 2019.

 Muendesha mtambo akiendelea na kazi ya kuweka kifusi na kupanga mawe kwenye kingo ya mto Mkondoa kwa ajili ya kudhibiti mafuriko ya mto Mkondoa  yanayoathiri miundombinu ya reli na kupelekea kusitishwa kwa Huduma za Usafiri wa reli mara kadhaa wakati wa mvua kubwa.
 Sehemu ya Mto Mkondoa ikiwa imewekewa kingo za mawe kwa ajili ya kudhibiti mafuriko ya mto Mkondoa  yanayoathiri miundombinu ya reli na kupelekea kusitishwa kwa Huduma za Usafiri wa reli mara kadhaa wakati wa mvua kubwa.
Kazi ya Kuhamisha kipande cha reli chenye urefu wa Kilometa 1.3  ikiendelea eneo la Kidete - Godegode umbali wa KM 337 - 338 ilikudhibiti mafuriko ya mto Mkondoa  yanayoathiri miundombinu ya reli na kupelekea kusitishwa kwa Huduma za Usafiri wa reli mara kadhaa wakati wa mvua kubwa. Kazi inajumuisha ujenzi wa tuta jipya la reli, ujenzi wa Makalavati pamoja na uwekaji wa reli katika tuta jipya hivi karibuni Januari 2019.

BREAKING NEWZZZZ: MAHAKAMA YA KISUTU YAMWACHIA HURU TIDO MHANDO.

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Imemuachia huru Mkurugenzi wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Tido Mhando, aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya madaraka inayomkabili baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yake.

INTRODUCING "WASHA" BY BARNABA CLASSIC

MABORESHO UJENZI WA RELI YA ZAMANI (MGR): UJENZI WA TUTA JIPYA,MAKARAVATI NA UWEKAJI WA RELI WAENDELEA KWA KASI KIDETE-GODEGODE MKOANI MOROGORO

$
0
0
 Kazi ya Kuhamisha kipande cha reli chenye urefu wa Kilometa 1.3 ikiendelea eneo la Kidete - Godegode umbali wa KM 337 - 338 ili kudhibiti mafuriko ya mto Mkondoa  yanayoathiri miundombinu ya reli na kupelekea kusitishwa kwa Huduma za Usafiri wa reli mara kadhaa wakati wa mvua kubwa. Kazi inajumuisha ujenzi wa tuta jipya la reli, ujenzi wa Makalavati pamoja na uwekaji wa reli katika tuta jipya hivi karibuni Januari 2019.

 Muendesha mtambo akiendelea na kazi ya kuweka kifusi na kupanga mawe kwenye kingo ya mto Mkondoa kwa ajili ya kudhibiti mafuriko ya mto Mkondoa  yanayoathiri miundombinu ya reli na kupelekea kusitishwa kwa Huduma za Usafiri wa reli mara kadhaa wakati wa mvua kubwa.
 Sehemu ya Mto Mkondoa ikiwa imewekewa kingo za mawe kwa ajili ya kudhibiti mafuriko ya mto Mkondoa  yanayoathiri miundombinu ya reli na kupelekea kusitishwa kwa Huduma za Usafiri wa reli mara kadhaa wakati wa mvua kubwa.
Kazi ya Kuhamisha kipande cha reli chenye urefu wa Kilometa 1.3  ikiendelea eneo la Kidete - Godegode umbali wa KM 337 - 338 ilikudhibiti mafuriko ya mto Mkondoa  yanayoathiri miundombinu ya reli na kupelekea kusitishwa kwa Huduma za Usafiri wa reli mara kadhaa wakati wa mvua kubwa. Kazi inajumuisha ujenzi wa tuta jipya la reli, ujenzi wa Makalavati pamoja na uwekaji wa reli katika tuta jipya hivi karibuni Januari 2019.

NAIBU WAZIRI MABULA AKERWA WADAIWA SUGU KODI YA ARDHI KUTOFIKISHWA MAHAKAMANI

$
0
0
Na Munir Shemweta, DODOMA
NaibuWaziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angelina Mabula ameshangazwa na halmashauri za wilaya ya Mpwapwa na Kongwa mkoani Dodoma kushindwa kuwafikisha katika Mabaraza ya Ardhi na Nyumba wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi pamoja na baadhi yao kupelekewa ilani za madai.

Dk Mabula ameziagiza halmashauri hizo mbili kuhakikisha zinawafikisha wadaiwa hao katika Mabaraza ya Ardhi kwa hatua zaidi ambapo alielezea kuwa huko maamuzi yake ni mawili ambapo mdaiwa anatakiwa kulipa ama kunyanganywa miliki yake kufidia deni.

Naibu Waziri wa Ardhi alitoa agizo hilo jana alipozitembelea wilaya hizo mbili ikiwa ni mfululilzo wa ziara zake kutembelea halmashauri mbalimbali kwa nia ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, halmashauri hizo zina wamiliki wengi wa viwanja wasiolipia kodi ya ardhi na hivyo kuzifanya kudai kiasi kikubwa cha fedha lakini idara za ardhi zinashindwa kuwachukulia hatua jambo linaloikosesha serikali mapapto.

Naibu Waziri wa Ardhi alisema, halmashauri ya wilaya ya Kongwa inadai jumla ya shilingi milioni 152 kutoka kwa wamiliki wasiolipa kodi huku ile ya Mpwapwa ikidai milioni 128,013,696.90.

Afisa Ardhi Msaidizi wa Halmashauri ya wilaya ya Kongwa Anjelina Ndemera alisema halmashauri yake pamoja na kuwa na madeni kutoka kwa wadaiwa wa kodi ya pango la ardhi lakini haikuweza kutoa ilani za madai kwa wadaiwa hao.

Kwa upande wa wilaya ya Mpwapwa, Mkuu wake wa Idara Anderson Mwamengo alisema halmashauri hiyo ina wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi mia tatu na thelathini  ambao wameandikiwa na kukabidhiwa ilani hizo.

Dkt Mabula alisema, pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kuhimiza suala la kulipa kodi na Wizara ya Ardhi kujitahidi kusaidia suala hilo lakini halmashauri hazifanyi jitihada zozote katika kukusanya maduhuli ya Serikali kupitia kodi ya ardhi.

‘’Kila siku inaelezwa pelekeni ilani za madai ya kodi ya ardhi kwa wamiliki lakini hakuna ufuatiliaji wowote unaofanywa na watendaji wa sekta ya ardhi jambo linalorudisha nyuma jitihada za serikali ya awamu ya tano kukusanya maduhuli ya serikali.

Naibu Waziri wa Ardhi aliziagiza halmashauri hizo mbili kufikia tarehe 31 Machi 2019 watendaji wake wa sekta ya ardhi wawe wamewafikisha katika Baraza la Ardhi wadaiwa wote waliopelekewa ilani za madai.

Aidha, Dkt Mabula ameitaka idara ya ardhi kuhakikisha orodha ya wadaiwa wa kodi ya pango la ardhi waliopewa ilani za madai inafikishwa katika kila kikao cha kamati ya Uchumi na Mazingira vya kila robo mwaka ya Baraza la Madiwani katika kila halmashauri lengo likiwa kuitaka kamati husika kuelewa suala hilo na kufanya ufuatiliaji.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Jabir Shekimweri (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpwapwa Paul Sweya na Mkuu wa Idara ya Ardhi  Anderson Mwamengo alipofanya ziara kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Dodoma.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kongwa alipokutana na watendaji wa sekta ya ardhi katika wilaya hiyo wakati wa ziara ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Dodoma.
 Baadhi ya watendaji katika wilaya ya Kongwa wakiwepo wale wa sekta ya ardhi wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alipofanya ziara kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Dodoma.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akikagua Majalada ya ardhi katika halmashauri ya wilaya ya Kongwa alipofanya ziara kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Dodoma.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akitoa maelekezo baada ya kukagua masijala ya ardhi katika halmashauri ya wilaya ya Kongwa alipofanya ziara kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Dodoma. Wa pili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kongwa Deo Ndejembi.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi katika halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa (hawapo pichani) alipofanya ziara ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Jabir Shekimweri, wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpwapwa Paul Sweya na kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Ardhi kanda ya Kati Ezekiel Kitlya.
 Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Deo Ndejembi akimuongoza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula kuelekea Masijala ya Ardhi katika halmashauri ya wilaya ya Kongwa alipofanya ziara kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Dodoma. Katikati ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Omar Nkullo.

Selcom unveils platform for banks fund transfer

$
0
0

BY STAFF REPORTER.

SELCOM Tanzania in collaboration with Business Connexion (BCX), have launched a new digital platform, which will be enable people to transfer cash from one bank to another. Indeed, this is a milestone in the promotion of financial inclusion. 

Selcom who are leading innovators in mobile applications, products and services, including banking in Tanzania, say the platform namely “Qwiksend”, will allow customers to make interbank fund transfers, in real-time, through the various digital access channels that are available to them countrywide.

Selcom Tanzania Executive Director, Sameer Hirji said the goal of unveiling th new platform is to promote financial inclusion in Tanzania, through simplified technology.

“Not only will interbank transfers open up a new avenue of funds transfers, but it will also enable smoother transactions that are cost effective for individuals and small-scale merchants alike,” said 

As of now, interbank transfers involves the traditional physical withdrawal and deposit or alternatively, the mobile transfer route which involves the loading of funds into one’s mobile wallet and then deposit into the beneficiary’s bank account. These routes are tedious and costly to the customer, denying the consumer the benefits of real-time transactions,” he said.

He added that Qwiksend service eliminates the double-charging effect and only charges the sender once, on sending funds. Since the Qwiksend service is managed by Selcom/BCX end-to-end, the service is quick, real-time and reliable. The charges associated with Qwiksend will be significantly cheaper than the current charges of existing transfer options in the market.

“Qwiksend is fully operational and is expected to have over 20 participating banks by the end of March 2019 with the number expected to grow to 40 banks by the end of June 2019. Participation is through open banking Application Programme Interfaces (“APIs”) and settlement is handled by way of existing net-off settlement processes between banks.

“Qwiksend will be available on standard mobile banking (USSD and App), internet banking and various other digital channels offered by banks countrywide, where the only requirement will be to select the recipient's bank and then enter the destination account number, to complete transaction,” He said.
Viewing all 109933 articles
Browse latest View live




Latest Images