Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live

Balozi wa Tanzania, Ujerumani awasilisha hati za utambulisho nchini Bulgaria

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambaye anawakilisha pia nchini Bulgaria , Mhe. Dkt. Abdallah Posi akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Bulgaria, Mhe. Rumen Radev. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu ya nchi hiyo hivi karibuni.
Mhe. Balozi Dkt. Posi akizungumza na Mhe. Rais Radev mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho
Mhe. Balozi Dkt. Posi akiagana na Mhe. Rais Radev mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho




Mhe. Balozi Dkt. Posi akiwa mbele ya gwaride la heshima alipowasili Ikulu ya Bulgaria kwa ajili ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais wa nchi hiyo.

Muhimbili kusuka upya mfumo wa kliniki

$
0
0
Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) umesema unaangalia jinsi ya kuboresha mfumo wa kliniki ili wagonjwa wahudumiwe kwa wakati baada ya kufika katika hospitali hiyo kupata huduma za matibabu.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Prof. Lawrence Museru wakati akizungumza na madaktari bingwa wa Muhimbili kuhusu namna bora kuboresha huduma za matibabu katika hospitali hiyo.
Hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wa nje 1,500 kwa siku. Pia, kuna wagonjwa 1,200 hadi 1,300 wamelazwa wodini wakati wote. Aidha wagonjwa wa nje walio wengi wanapenda kuja asubuhi hata kama kliniki zao zinaanza mchana.
Prof. Museru amesema hatua hii ina lengo la kuboresha huduma katika kliniki hizo ni  kuondoa msongamano wakati mgonjwa au wagonjwa wakisubiri kuona madaktari bingwa wa hospitali hiyo.

“Wakuu wa idara kupitia kwa madaktari mtuletee mapendekezo ambayo tutaangalia jinsi ya kujenga mazingira bora ambayo wagonjwa watatumia muda mfupi kumuona daktari. Tunataka mgonjwa asikae muda mrefu kwenye foleni,”amesema Prof. Museru.

Pia, Prof. Museru amewaahidi wataalam hao kwamba Uongozi wa Hospitali chini ya Bodi ya Wadhamini utaendelea kuboresha mazingira ya kufanyia kazi na kutoa huduma bora kwa wananchi mbalimbali wanaofika hospitali hapo kupata matibabu.

“Naomba tuendelee kutumia vizuri na kikamilifu miundombinu iliyopo ili kuongeza tija na wananchi wametuamini ndiyo maana wengi wamekuwa na matumaini makubwa sana na huduma tunazotoa” alisema Prof. Museru.

Prof. Museru amewashukuru sana watoa huduma na wafanyakazi wote kwa ujumla wao kwa namna ambavyo wanajituma na kufanya kazi kwa bidii hali iliyoifanya Hospitali kufanya mageuzi makubwa katika utoaji wa huduma bora za afya hapa nchini hususani katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Akizungumzia upatikanaji wa dawa katika hospitali hiyo, mkurugenzi huyo amesema licha ya dawa kupatikana kwa zaidi ya asilimia 95 hospitali yake  inaendelea kuimarisha utoaji wa dawa kwa wagonjwa ili kuhakikisha kila mgonjwa anayetibiwa anapata dawa kwa wakati.

Katika mkutano huo madaktari walijadili njia za kuimarisha utoaji wa huduma bora za matibabu kwa wagonjwa mbalimbali samabamba na kukubaliana kufanya kazi kwa juhudi ili kufikia malengo yaliowekwa na hospitali hiyo ya kutoa huduma bora za ubingwa wa juu nchini.

Hospitali ya Taifa Muhimbili ina wafanyakazi 2,705, kati yao madaktari ni 328, ambapo madaktari bingwa ni 186 na 142 ni madaktari wa kawaida. Aidha, Hospitali ina wauguzi 946 na waliobaki ni wafanyakazi wa kada nyingine.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Lawrence Museru akizungumza na madaktari bingwa wa hospitali hiyo jinsi ya kuboresha mfumo wa kliniki ili wagonjwa wahudumiwe kwa wakati.
Baadhi ya madaktari bingwa wa Muhimbili na wataalam wengine wa hospitali hiyo wakiwa kwenye mkutano huo leo.
Mkuu wa Idara ya utunzaji wa Kumbukumbu wa Muhimbili, Geofrey Semu akichangia mada jinsi ya kuboresha mfumo wa kliniki katika mkutano huo leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Prof. Museru (wa tatu kushoto) akimsikiliza Geofrey Semu wakati akichangia mada kwenye mkutano huo. Wengine baadhi ya wakurugenzi katika kurugenzi za hospitali hiyo.
Daktari Bingwa wa Afya ya Kinywa na Meno, Dkt. Deo Kilasara akizungumza kwenye mkutano huo leo.
Baadhi ya madaktari bingwa wakifuatilia michango ya mada mbalimbali kwenye mkutano huo.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Dharura na Ajali, Dkt. Patrick Shao akichangia mada jinsi ya kuboresha mfumo wa kliniki katika hospitali hiyo.
Habari na Picha na John Stephen, 
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)


Waziri Mbarawa aivunja bodi ya maji mji mdogo wa kibaigwa kutokana na uendeshaji mbovu wa miradi ya Maji

Habari za Umoja wa Mataifa kutoka New York, Marekani

VOA SWAHILI: Habari mbalimbali za dunia kwa ufupi.

Habari za UN Januari 23, 2019

DC MURO AFANYA ZIARA YA UKAGUZI UJENZI WA MADARASA KATA YA BWAWANI,ARUMERU

$
0
0
Mkuu Wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro amendelea na ziara yake ya kukagua ujenzi wa madarasa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza katika kata ya Bwawani.

Dc Muro akiwa katika ziara hiyo ameeleza kuwa wanafunzi zaidi ya 245 mpaka sasa wote waliopangwa kuingia kidato cha kwanza mwaka 2019 katika shule ya Sekondari Bwawani wamepata nafasi ya  kuendelea na masomo yao bila hata mmoja wao kukosa.

Ziara  ya Mkuu wa wilaya  Ndugu Jerry Muro imelenga kufahamu upatikanaji wa Elimu bora  kwa wanafunzi waliochaguliwa kidato cha kwanza kwa mwaka huu.

Pia Dc Muro amewapongeza wananchi wa kata ya bwawani kwa jitihada zao kuweza kujenga madarasa mawili kwa kipindi cha muda mfupi na kuanzia wiki ijayo wanafunzi wataanza kutumia madarasa hayo.

Sambamba na hapo Mkuu wa Wilaya hiyo ametoa wito kwa wananchi wote na wadau  mbalimbali wa maendeleo Wilayani Arumeru kuendelea kuchangia ujenzi wa madarasa pasipo kuvunjwa moyo na Baadhi ya wanasiasa wanaojaribu kuhujumu zoezi la ujenzi wa madarasa.
 Mkuu Wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro akitoa maelekezo kwa watendaji,wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa madarasa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza katika kata ya Bwawani.
 Mkuu Wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro akikagua ujenzi wa madarasa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza katika kata ya Bwawani.

INTRODUCING "SIRINGI" by Nick Maujanja


TANESCO YAJIVUNIA TEKNOLOJIA YA KISASA KATIKA KUTOA HUDUMA YA UMEME

$
0
0
Na Said Mwishehe,Arusha

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limesema kwa sasa huduma zake nyingi zinatolewa kidigitali kutokana na kukua kwa teknolojia na hivyo kwa kutumia mitambo iliyopo inawawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi.

Tanesco imesisitiza inatambua kazi ya kukua kwa teknolojia na hivyo nayo imeamua kujikita katika kuweka mitambo hiyo ya kisasa ili kwenda na kasi ya ukuaji wa teknolojia katika kuhudumia wananchi na kwa sasa utendaji kazi umekuwa wa ufanisi zaidi kutoka na uwepo wa mitambo ya kisasa.

Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco, Leila Muhaji amewaambia wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini waliopo kwenye ziara ya kutembelea miradi ya umeme inayotekelezwa na Serikali katika Mkoa wa Arusha, amesema shirika hilo kwa sasa haliko nyuma katika kukua kwa teknolojia na hivyo mitambo mingi ambayo imefungwa kwenye vituo vya kusambaza umeme.

"Kama tulivyoona ni kwamba Tanesco tunakwenda sambamba na ukuaji wa teknonolojia, vituo vyetu vingi vimekuwa vya kidigitali .Kwa hapa Arusha vituo vyetu vingi mitambo ambayo imefungwa ni ya kisasa ukilinganisha na miaka ya huko nyuma.Watalaamu wetu wakiwa ofisini kupitia mitambo iliyopo kama kuna tatizo lolote kwenye njia ya umeme kompyuta itaonesha na hivyo inakuwa rahisi kushughulikia tatizo,"amesema Muhaji.

Amefafanua "Hivyo ikitokea gari imegonga nguzo ya umeme, mti umeegemea waya au vyovyote vile kupitia mitambo iliyopo itaonekana moja kwa moja, hii inasaidia kushughulikia matatizo mapema na hivyo kuondoa hata malalamiko kwani kabla mteja hajafika Tanesco kutoa taarifa , tayari watalaamu wetu wameshaona na kuchukua hatua."

Akizungumzia Mradi wa Kukarabati na Kuimarisha Mifumo ya Umeme Tanzania(TEDAP) Muhaji amesema kwa Mkoa wa Arusha kupitia mradi huo wamefanya maboresho makubwa kwa kutengeneza vituo vipya ambapo imesadia kuufanya mkoa huo kuwa na umeme wa ziada.

Ameongeza kwa sasa Arusha haina tatizo la umeme na ndio maana wanahamasisha watu kuwekeza kwa kujenga viwanda huku akiwahamasisha wananchi ambao wanahitaji kuunganishwa umeme kufika kwenye shirika hilo kutoa maombi yao.

Pia amesema Serikali kupitia Tanesco inatekeleza miradi mbalimbali ya umeme nchini ukiwamo mkoa wa Arusha na hivyo kuna kila sababu ya jamii kufahamu utekelezwaji wa miradi hiyo lakini zaidi amewahamasisha wanaotaka kuwekeza kupitia sekta ya viwanda hivi sasa nchi ina nishati ya umeme wa uhakika.

"Tumeamua kufanya ziara hii ya kuwaleta wahariri wa vyombo vya habari , kwanza waone kazi ambayo Serikali ya Awamu ya Tano inafanya katika kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme nchini, pili wawe wajumbe wa kutoa taarifa kwa Watanzania kuhusu kazi inayofanyika na hasa uwepo wa umeme wa ziada katika Mkoa huu wa Arusha.Miradi ya TEDAP inafanyika pia kwenye mikoa mingine kadhaa ukiwamo wa Dar es Salaam ambako nako kuna miradi ya umeme ambayo inatekelezwa na mingine imekamilika,"amesema Muhaji.

Mtaalam wa masuala ya umeme akifafanua jambo kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini(hawapo pichani) baada ya kutembelea kituo cha umeme cha Sakina kilichopo Ngatamtoni mkoani Arusha

Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO)Leila Muhaji(kushoto) akimsikiliza Meneja wa shirika hilo mkoa wa Arusha Mhandisi Herini Mhina(kulia) kuhusu huduma ya usambazaji umeme mkoani hapa wakati wa ziara ya wahariri wa vyombo vya habari walipotembelea moja kituo cha umeme ambacho kimejengwa kupitia mradi wa TEDAP.Katikati ni Meneja Mwandamizi Miradi Mhandisi Emmanuel Manibora.

RAIS DKT. MAGUFULI NA VIONGOZI WA DINI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM KATIKA PICHA

Message on the occasion of International Day of Education

$
0
0
Today marks the first International Day of Education, as proclaimed by the United Nations General Assembly last December. This significant decision recognizes the capital role of education in “Transforming our world: the 2030 Agenda for Sustainable Development”.

Without inclusive and equitable quality education and lifelong opportunities for all, countries will not succeed in breaking the cycle of poverty that is leaving millions of children, youth and adults behind. We will not succeed in mitigating climate change, adapting to the technological revolution, let alone achieve gender equality, without ambitious political commitment to universal education.

This day is the occasion to reaffirm fundamental principles. Firstly, education is a human right, a public good and a public responsibility. Secondly, education is the most powerful force in our hands to ensure significant improvements in health, to stimulate economic growth, to unlock the potential and innovation we need to build more resilient and sustainable societies. Lastly, we urgently need to call for collective action for education at global level.

Headline figures point to the challenges: 262 million children and youth do not attend school; 617 million children and adolescents cannot read and do basic math; less than 40% of girls in sub-Saharan Africa complete lower secondary school while some 4 million children and youth refugees are out of school, their lives disrupted by conflict and loss.

Because the world is not on track to achieve Sustainable Development Goal 4, we need a surge in global cooperation and collective action. Our challenge is to make education work for everyone, by promoting inclusion and equity at every level, to leave no one behind. This calls for special attention to girls, to migrants, displaced persons and refugees; to support teachers and make education and training more gender responsive. It urgently requires scaled up domestic resources and international aid, because the cost of not investing will dig divides, inequalities and exclusion across societies.

Invited to facilitate the observance of International Education Day, UNESCO calls on governments and all partners to make education a leading priority. We all have a stake in education, let’s act together to fulfil its promise.

MIRADI YA TEDAP YAIMARISHA UPATIKANAJI,USAMBAZAJI UMEME KWA WATEJA ARUSHA

$
0
0
Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii
SHIRIKA la Umeme Tanzania(TANESCO)limesema kwamba kutekelezwa kwa mradi wa Kukarabati na Kuimarisha Mifumo ya Umeme Tanzania(TEDAP) umesaidia kuimarisha upatikanaji wa umeme wa uhakika hasa katika mikoa mbalimbali ambayo TEDAP inatekelezwa.

Kwa Mkoa wa Arusha TEDAP imesaidia kuufanya mkoa huo kuwepo kwa umeme wa uhakika na kwamba kutokana na ukarabati na uimarishwaji wa mifumo ikiwemo ya usambazaji umeme imeifanya TANEACO Mko wa Arusha kuwa na umeme wa unaotesheleza wateja na kuwepo na akiba ambayo haitumiki.

Akizungumzia utekelezaji wa TEDAP Mkoa wa Arusha,  Menaja Mwandamizi wa Miradi kutoka Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) Mhandisi Emmanuel Manirabona amesema katika mkoa huo kuna mafanikio makubwa na kwamba ndio maana wanahamasisha watu wawekeze kwani kuna umeme wa uhakika.

Amefafanua kupitia TEDAP wamerabati kituo cha umeme cha Mt.Meru, kituo cha Njiro B, kituo cha Sakina, kituo cha Themi, kituo cha Unga Ltd, kituo cha T/School na Kituo cha Kiltx.na kwamba uwepo wa vituo hivyo na uboreshwaji wake umeongeza ufanisi  wa utoaji huduma ya nishati ya umeme kwa wateja wao.

"Kutekelezwa kwa TEDAP ndani ya Mkoa wa Arusha umepiga hatua kubwa ya upatikanaji wa umeme wa uhakika,leo hii Arusha hata malalamiko ya wateja yamepungua kwani hata tatizo la kukatika kwa umeme halipo kama ilivyokuwa huko nyuma," amefafanua.

Mhandisi Manirabona amesema kupitia miradi ya  TADEP imesaidia kuifanya TANESCO kufanya kazi zake kwa uharaka zaidi hata pale linapotokea tatizo la umeme kupitia mitambo iliyopo inasaidia kupata taarifa ya tatizo la umeme kabla ya mteja kufika ofisi za shirika hilo kutoa taarifa.

"Kuna mitambo ya kisasa ambayo yamerahisisha hata upatikanaji wa taarifa.Chochote ambacho kinafanyika katika mfumo wa umeme tunapata taarifa kwa haraka sana," amefafanua Mhandisi Manirabora huku akisisitiza watu kujenga viwabda Arusha kwani umeme wa uhakika.

Kwa upande wake Msimamizi Mkuu wa Modumo ya Usambazaji Umeme kituo cha usambazaji umemenNjiro Rembrice Mollel ameto ufafanuzi kuhusu namna mifumo ilivyo kwenye kituo hicho namna ambavyo imeboreshwa na hatimaye kirahisisha utoaji huduma ya nishati ya umeme.

Pia amesema kwamba katika kituo hicho wanazo njia tatu za kusambaza uneme ambapo njia moja ni ya 220 kilovolti na njia nyingine mbili za kusambaza umeme zina uwezo wa 132 kilovolti kwa  kila mmoja.

",Katika kituo hiki cha Njiro hatuna tatizo kabisa la umeme,wateja wetu wanapata umeme wa uhakika na usiokatika.Kupitia," amesisitiza huku akifafanua kwa mifumo ya usambazaji umeme waliyonayo ni ya kisasa na hivyo inawarahisiahia katika kutoa huduma kwa wateja.
 Meneja wa Mradi wa Shirika La Umeme TANESCO, Mhandisi Emmanuel Marinabona akielezea jambo wahariri na waandishi waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini kuhusu hatua mbalimbali ambazo mradi wa TEDAP ulipitia kukamilisha upanuzi wa miundo mbinu ya kusambaza umeme na kupunguza changamoto mbalimbali za umeme katika Mkoa wa Arusha leo. Mradi huo unahusisha vituo sita vya umeme pamoja na kituo kikuu cha kusambaza umeme cha Njiro. 
 Kaimu Meneja wa Uhusiano wa shirika la umeme TANESCO, Leilah Muhaji akijibu maswali aliyoulizwa na waandishi wa habari kuhusu hatua mbalimbali ambazo mradi wa TEDAP ulipitia kukamilisha upanuzi wa miundo mbinu ya kusambaza umeme na kupunguza changamoto mbalimbali za umeme katika Mkoa wa Arusha leo. Mradi huo unahusisha vituo 6 vya umeme pamoja na kituo kikuu cha kusambaza umeme cha Njiro. 
Mkuu wa Usambazaji Umeme Mkoa wa Arusha, Mhandisi Donasiano Shamba akielezea jambo wahariri na waandishi waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini kuhusu hatua mbalimbali ambazo mradi wa TEDAP ulipitia kukamilisha upanuzi wa miundo mbinu ya kusambaza umeme na kupunguza changamoto mbalimbali za umeme katika Mkoa wa Arusha leo. Mradi huo unahusisha vituo 6 vya umeme pamoja na kituo kikuu cha kusambaza umeme cha Njiro. 

BREAKING NEWZZZZ: MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2018 YATOKA, YATAZAME HAPA

Muhimbili kusuka upya mfumo wa kliniki

$
0
0
Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) umesema unaangalia jinsi ya kuboresha mfumo wa kliniki ili wagonjwa wahudumiwe kwa wakati baada ya kufika katika hospitali hiyo kupata huduma za matibabu. Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Prof. Lawrence Museru wakati akizungumza na madaktari bingwa wa Muhimbili kuhusu namna bora kuboresha huduma za matibabu katika hospitali hiyo.

Hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wa nje 1,500 kwa siku. Pia, kuna wagonjwa 1,200 hadi 1,300 wamelazwa wodini wakati wote. Aidha wagonjwa wa nje walio wengi wanapenda kuja asubuhi hata kama kliniki zao zinaanza mchana. Prof. Museru amesema hatua hii ina lengo la kuboresha huduma katika kliniki hizo ni  kuondoa msongamano wakati mgonjwa au wagonjwa wakisubiri kuona madaktari bingwa wa hospitali hiyo.

“Wakuu wa idara kupitia kwa madaktari mtuletee mapendekezo ambayo tutaangalia jinsi ya kujenga mazingira bora ambayo wagonjwa watatumia muda mfupi kumuona daktari. Tunataka mgonjwa asikae muda mrefu kwenye foleni,”amesema Prof. Museru. Pia, Prof. Museru amewaahidi wataalam hao kwamba Uongozi wa Hospitali chini ya Bodi ya Wadhamini utaendelea kuboresha mazingira ya kufanyia kazi na kutoa huduma bora kwa wananchi mbalimbali wanaofika hospitali hapo kupata matibabu.

“Naomba tuendelee kutumia vizuri na kikamilifu miundombinu iliyopo ili kuongeza tija na wananchi wametuamini ndiyo maana wengi wamekuwa na matumaini makubwa sana na huduma tunazotoa” alisema Prof. Museru. Prof. Museru amewashukuru sana watoa huduma na wafanyakazi wote kwa ujumla wao kwa namna ambavyo wanajituma na kufanya kazi kwa bidii hali iliyoifanya Hospitali kufanya mageuzi makubwa katika utoaji wa huduma bora za afya hapa nchini hususani katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Akizungumzia upatikanaji wa dawa katika hospitali hiyo, mkurugenzi huyo amesema licha ya dawa kupatikana kwa zaidi ya asilimia 95 hospitali yake  inaendelea kuimarisha utoaji wa dawa kwa wagonjwa ili kuhakikisha kila mgonjwa anayetibiwa anapata dawa kwa wakati. Katika mkutano huo madaktari walijadili njia za kuimarisha utoaji wa huduma bora za matibabu kwa wagonjwa mbalimbali samabamba na kukubaliana kufanya kazi kwa juhudi ili kufikia malengo yaliowekwa na hospitali hiyo ya kutoa huduma bora za ubingwa wa juu nchini.

Hospitali ya Taifa Muhimbili ina wafanyakazi 2,705, kati yao madaktari ni 328, ambapo madaktari bingwa ni 186 na 142 ni madaktari wa kawaida. Aidha, Hospitali ina wauguzi 946 na waliobaki ni wafanyakazi wa kada nyingine.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Lawrence Museru akizungumza na madaktari bingwa wa hospitali hiyo jinsi ya kuboresha mfumo wa kliniki ili wagonjwa wahudumiwe kwa wakati.
 Baadhi ya madaktari bingwa wa Muhimbili na wataalam wengine wa hospitali hiyo wakiwa kwenye mkutano huo leo.
 Mkuu wa Idara ya utunzaji wa Kumbukumbu wa Muhimbili, Geofrey Semu akichangia mada jinsi ya kuboresha mfumo wa kliniki katika mkutano huo leo.
  Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Prof. Museru (wa tatu kushoto) akimsikiliza Geofrey Semu wakati akichangia mada kwenye mkutano huo. Wengine baadhi ya wakurugenzi katika kurugenzi za hospitali hiyo.
  Daktari Bingwa wa Afya ya Kinywa na Meno, Dkt. Deo Kilasara akizungumza kwenye mkutano huo leo.
 Baadhi ya madaktari bingwa wakifuatilia michango ya mada mbalimbali kwenye mkutano huo.
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Dharura na Ajali, Dkt. Patrick Shao akichangia mada jinsi ya kuboresha mfumo wa kliniki katika hospitali hiyo.
 Daktari Bingwa wa Kina mama, Dkt. Geofrey Marandu akichangia mada kwenye mkutano huo leo.

MAMA SHAMIM KHAN ATUNUKIWA TUZO YA HESHIMA NCHINI INDIA

$
0
0
Aliyekuwa Mbunge na Naibu Waziri Mstaafu wa Tanzania, Mama Shamim Khan akitunukiwa Tuzo ya Juu (Pravasi Bharatiya Samman Award ) na Rais wa India, Mhe. Ram Nath Kovind tarehe 23 Januari, 2019. Kushoto kwake ni Waziri Mkuu wa Mauritania, Mhe. Pravid Kumar Jugnauth ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa Mkutano wa 15 wa Diaspora wa India uliofanyika katika mji wa Varanasi, Utter Pradesh nchini humo. 
Rais wa India, Mhe. Ram Nath Kovind akihutubia katika hafla ya kuhitimisha Mkutano wa 15 wa Diaspora wa India [15thPravasi Bharatiya Divas 2019] uliofanyika tarehe 23 Januari, 2019 katika mji wa Varanasi, Uttar Pradesh nchini India 
Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkubwa wa 15 wa Diaspora wa India uliofanyika katika mji wa Varanasi, Utter Pradesh, India 
Picha ya pamoja 
Mama Shamim Khan katika picha ya pamoja na Afisa Ubalozi wa Tanzania, New Delhi, Dkt. Kheri Goloka baada ya kupokea Tuzo tarehe 23 Januari, 2019.




Yah: Mama Shamim Khan atunukiwa tuzo ya juu ya heshima na Mhe. Ram Nath Kovind, Rais wa India 

Mbunge wa zamani na aliyekuwa Naibu Waziri kwenye Wizara mbalimbali nchini, Mama Shamim Khan ametunukiwa Tuzo ya Juu ya Heshima (Pravasi Bharati yan Samman Award) na Rais wa India, Mhe. Ram Nath Kovind. Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa Mkutano wa 15 wa Diaspora wa India (15th Pravasi Bharatiya Divas 2019) uliofanyika kwenye mji wa Varanasi, Uttar Pradesh tarehe 23 Januari, 2019.

Mkutano huo ambao ulifunguliwa na Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi uliwahusisha viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya India akiwemo Waziri Mkuu wa Mauritania, Mhe. Pravid Kumar Jugnauth, Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Mhe. Sushma Swaraj, Waziri wa Nchi anayeshughulikia masuala ya Mambo ya Nje ya India, Mhe. Gen [Dr.) V. K. Singh na Waziri Kiongozi wa Jimbo la Utter Pradesh, Mhe. Yogi Adityanath. 

Mama Shamim Khan ametunukiwa tuzo hiyo kutokana na mchango wake mkubwa kwa jamii hususan katika masuala ya akina mama na kudumisha amani na uhusiano mzuri wa madhehebu ya dini mbalimbali nchini. 

Wakati akimtunuku tuzo hiyo, Rais Kovind alieleza kutambua mchango mkubwa wa Mama Shamim Khan katika kudumisha uhusiano mzuri uliopo baina ya Watanzania wenye asili ya India wanaoishi nchini Tanzania na Serikali ya Tanzania katika kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi baina ya nchi zao. Aidha, alimpongeza kwa utumishi uliotukuka. 

Kwa upande wake, Mama Shamim Khan alimshukuru sana Rais Kovind na kueleza kufarijika kwake kwa kutunukiwa Tuzo hiyo ambayo ni heshima kubwa kwake. Aidha, Mama Shamim Khan alipongeza juhudi za Serikali ya India kwa kuendelea kudumisha ushirikiano wa kidugu na wa muda mrefu uliopo baina ya Tanzania na India na amemuomba Mhe. Rais Kovind kuendelea kusaidia juhudi za Serikali ya Mhe.Rais Dkt. John P. Magufuli katika kuwaletea maendeleo watanzania.

Tuzo hiyo hutolewa kwa raia wenye asili ya India ambao wametoa mchango mkubwa katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi baina ya nchi wanazoishi na India. Hivyo hii imekuwa ni heshima kubwa sio tu kwa Mama Shamim Khan bali kwa Tanzania kwa ujumla. Mama Shamim Khan aliongozana na Afisa Ubalozi wa Tanzania nchini India, Dkt. Kheri Goloka kwenye hafla hiyo. 


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
24 Januari 2019


WANACHAMA WASTAAFU MFUKO WA TAIFA BIMA YA AFYA MKOANI TANGA WAHAKIKIWA

$
0
0

ZAIDI wa Wachama Wastaafu 5000 mkoani Tanga waliondikishwa kwenye Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kuanzia Julai 2009 hadi Septemba 2018 wameanza kuhakikiwa.

Hayo yalisemwa leo na Meneja wa Mfuko mkoani Tanga Ally Mwakababu (Pichani Juu) wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema zoezi hilo lilianza Januari 2 mwaka huu na litamalizika Machi 30 mwaka huu.

Alisema kwamba uhakiki huo unafanyika kwa kipindi cha miezi mitatu huku akiwataka wastaafu mkoani hapa ambao walioandikishwa kufika kwenye ofisi za mfuko huo kwa ajili ya kuhakikiwa. Mwanachama Mstaafu afike ofisini akiambatana na mwenza wake (endapo yupo hai)endapo mwanachama mstaafu amefariki ,mwenza aliyebaki afike kwa ajili ya uhakiki huo “Alisema Meneja huyo.

“Lakini pia mwanachama anapaswa kufika na vitu muhimu ikiwemo kitambulisho cha NHIF, Cheti cha Ndoa (kwa mstaafu mwenye mwenza),Kitambulisho cha Uraia au mpiga kura ,leseni ya Gari au hati ya kusafiria ikiwemo barua ya kustaafu “Alisema Meneja huyo.

Hata hivyo alisema kwamba ofisi inawataka wanachama wastaafu kufika kwa uhakiki ndani ya muda uliowekwa ili kuepuka usumbufu wa kukosa huduma kwa kutokufanya hivyo. 

CHANGAMOTO HALMASHAURI YA BAHI ZAMSONONESHA NAIBU WAZIRI WA ARDHI

$
0
0
Na Munir Shemweta, BAHI
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula amekutana na changamoto kubwa zinazoikabili halmashauri ya wilaya ya Bahi mkoani Dodoma kiasi cha kushindwa kuwabana maafisa ardhi katika halmashauri hiyo.

Akiwa katika ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya Serikali kupitia sekta ya ardhi katika halmashauri mbalimbali nchini jana, Dk Mabula aliikuta halmashauri ya Wilaya ya Bahi ikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ufinyu wa bajeti na  uhaba wa magari.

Hali hiyo imesababisha halmashauri hiyo kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo kama vile kukusanya maduhuli ya serikali kupitia sekta ya ardhi, kuwapelekea wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi hati za madai, kupima na kupanga viwanja pamoja na kwenda kutatua migogoro ya ardhi.

‘’Sekta ya ardhi ni idara nyeti sana ambayo inaweza kuingizia seriali mapato mengi lakini kama haitawezeshwa kufanya kazi ipasavyo kwa kupatiwa rasilimali fedha na vifaa kama magari basi itashindwa kutekeleza majukumu yake na hivyo kuifanya serikali kukosa mapato kupitia sekta hiyo.’’ Alisema Dk Mabula

Mkuu wa Idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Chediel Mrutu alimwambia Naibu Waziri Mabula kuwa, idara yake hajawahi kupatiwa fedha za mgao wa ndani na bajeti yake kwa mwaka ni milioni mbili na laki tano na kubainisha kuwa kiasi hicho wakati mwingine  hakipatikani chote. Kwa mujibu wa Mrutu idara yake haina gari la kuwawezesha kufanya shughuli za ardhi ambazo wakati mwingine hutakiwa kwenda umbali mrefu kushughulikia masuala ya ardhi.

Kufuatia hali hiyo Dkt. Mabula alitaka kufahamu kiasi cha fedha za mgao inazopata idara nyingine kwenye halmashauri hiyo kufuatia katika ziara zake kubaini idara ya ardhi kutengwa na kupewa kiasi kidogo cha fedha ukilinganisha na halmashauri nyingine ambapo kwa upande wa Bahi hakuna tofauti jambo lililomfanya kuishiwa nguvu na kusema halmashauri hiyo inahitaji kusaidiwa.

Dk Mabula alisema kiasi cha milioni mbili na laki tano inazopata halmashauri kwa mwaka haiwezi kufanya kitu kwa idara kama ya ardhi yenye majukumu mengi jambo lililoifanya kukusanya milioni saba tu hadi kufikia desemba mwaka jana huku ikiwekewa malengo ya milioni 47.

Alisema kwa hali waliyo nayo halmashauri ya Wilaya ya Bahi haiwezi kufikia asilimia hamsini ya malengo ya serikali na kuagiza ofisi ya Kamishana Msaidizi Kanda kuangalia namna itakavyoweza kuisaidia idara ya ardhi angalau iweze kutatua baadhi ya changamoto.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Bahi leo Mavika alisema halmashauri yake inakabiliwa na changamoto kubwa ya upatikanaji mapato ambapo alisema kwa sasa inajitahidi  kuhakikisha kiasi kidogo kinachopatikana kinagawanywa kwenye idara zote za halmashauri huku idara ya ardhi ikipewa kipaumbele kutokana na umuhimu wake na kuongeza kuwa halmashauri hiyo kwa sasa ina magari mawili tu jambo linalowawia vigumu kutekeleza majukumu ya kila siku.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mwanahamisi Munkunda alisema ili halmashauri yake iweze kutoka ilipo mikakati madhubuti inahitajika ili kuondokana na hali hiyo ambayo imekuwa ikiwakatisha tama watumishi kutokana na kushindwa kutekeleza majukumu ipasavyo kutokana na changamoto zinazowakabili.
 Naibu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi katika halmashauri ya wilaya ya Bahi mkoani Dodoma alipofanya ziara ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi. Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Bahi Mwanahamisi Munkunda, na wa tatu kushoto ni Mkurugenzi wa Halamashauri ya Wilaya ya Bahi leo Mavika.
 Mkuu wa Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma Mwanahamisi Munkunda akizungumza wakati wa ziara ya Naibu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi.
 Mkuu wa Idara ya Ardhi katika halmashauri ya Wilaya ya Bahi mkoa wa Dodoma Chediel Mrutu akitoa maelezo kuhusiana na sekta ya ardhi  wakati wa ziara ya Naibu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi.
Naibu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula akizungumza wakati akikagua mfumo katika ofisi za ardhi halmashauri ya wilaya ya Bahi mkoani Dodoma alipofanya ziara ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi.

HOSPITALI MKOA WA GEITA YAPEWA SIKU 60 KUFUNGUA DUKA LA DAWA

$
0
0
NA WAMJW-GEITA.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameuagiza uongozi wa Hospitali ya mkoa wa Geita kuhakikisha wanafungua duka la dawa ili kutoa huduma karibu na wananchi pia kuongeza mapato ya Hospitali.

Waziri Ummy ametoa agizo hilo mapema leo wakati alipoitembelea hospitali hiyo ili kuona hali ya miundombinu pamoja na utoaji wa huduma za afya.
“Tumeshaagiza Hospitali zote nchi nzima kuwa na maduka ya dawa ya Hospitali, kwanini hapa hamjafungua duka lenu? Alihoji Waziri Ummy na kuongeza “sasa nawapa miezi miwili uongozi wa Hospitali kuhakikisha mnafungua duka la dawa la Hospitali ili liweze kuwasaidia kupandisha mapato lakini pia kusogeza huduma karibu na wananchi. Alisema Waziri huyo.

Pamoja na hayo Waziri Ummy ameonekana kuridhishwa na hali ya upatikanaji wa dawa wa zaidi ya asilimia 90 na uboreshwaji wa huduma za afya zinazotolewa katika Hospitali hiyo.Kabla ya hapo Waziri Ummy alitembelea ujenzi wa Hospitali Teule ya Mkoa wa Geita ambapo alishuhudia ujenzi huo ukiwa umekamilika kwa asilimia 54 lakini amemtaka mkandarasi anayesimamia ujenzi huo ambaye ni wakala wa ujenzi (TBA) kufanya kazi usiku na mchana ili Hospitali hiyo ianze kufanya kazi ifikapo Mwezi Julai 2019.

Waziri Ummy amekamilisha ziara yake ya mkoa wa Geita kwa kutembelea Hospitali ya Wilaya ya Chato ili kujiridhisha na hali ya utoaji wa huduma za afya na miundombinu pamoja na kuhakikisha kama vifaa na vifaa tiba vinapatikana Hospitalini hapo.

Waziri Ummy ameridhishwa na utolewaji wa huduma za afya lakini ameitaka Hospitali hiyo kuwa na chumba maalum chenye vifaa maalum vya uangalizi wa watoto wachanga mahututi na wale waliozaliwa kabla ya siku (watoto njiti) lengo likiwa ni kupunguza vifo vya watoto wachanga nchini.

Aidha, waziri huyo ameagiza uongozi wa Hospitali hiyo kuanzisha kitengo cha huduma za wagonjwa wa dharura na wale waliopata ajali ikiwa ni agizo la serikali kwa hospitali zote za wilaya na mikoa nchi nzima.Huo ni muendelezo wa ziara za Waziri Ummy katika mikoa ya kanda ya ziwa kutembelea Hospitali mbalimbali kuangalia hali ya miundombinu na utoaji wa huduma za afya.



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiongozana na Kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita Bw. Josephat Maganga (kulia) wakitoka kukagua jengo la hospitali ya rufaa ya mkoa wa Geita.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiangalia mashine mpya ya X-ray ya kidigitali iliyifungwa katika Hospitali ya wilaya ya Chato wakati alipoitembelea hospitali hiyo kuona hali ya utoaji huduma za afya.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiangalia ramani ya majengo za majengo ya Hospitali ya rufaa ya Geita wakati alipotembelea ujenzi huo. Pembeni ni msimamizi wa ujenzi huo Injinia Grace Elias.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akimjulia hali mtoto aliyekuja kupata matibabu katika Hospitali ya wilaya ya Geita. Katikati ni mama wa mtoto huyo Bi. Jenista Benedicto.

ALIYEKUWA BOSI TRA HARRY KITILLYA,WENZAKE KUSOMEWA MAELEZO YA MASHAHIDI KESI YA UTAKATISHAJI FEDHA FEBRUARI 8 MWAKA HUU

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Februari 8 mwaka huu imepanga kumsomea maelezo ya mashahidi (commital) aliyekuwa Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitillya na mwenzake wawili wanaokabiliwa na mashtaka 58 yakiwemo ya utakatishaji fedha.

Hatua hiyo imefikiwa leo Januari 24,2019 baada ya upande wa utetezi kupinga maombi ya upande wa mashtaka ya kutaka kesi hiyo iahirishwe kwa siku 14 wakieleza kuwa wapo katika hatua za mwisho za kufaili taarifa (fail information), hivyo wanaomba siku hizo kwa ajili ya kukamilisha zoezi hilo. 

Hata hivyo upande wa utetezi ukiongozwa na Wakili Masumbuko Lamwai ulidai "Washtakiwa hao wamekaa ndani miaka mitatu sasa, walifutiwa kesi kiujanja na kuleta tena kesi hii ili wakae tena ndani, hivi ni kitu gani kinazuia commital, wiki iliyopita walisema leo watawasomea na sasa wanasema wapo kwenye hatua za mwisho watueleze hiyo hatua, " alidai Wakili Lamwai. 

Mapema Wakili wa Takukuru Leonard Swai alidai kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa wanaomba tarehe nyingine ili wakamilishe zoezi la kuwasilisha taarifa kwani wapo katika hatua za mwisho. Hata hivyo, hakimu Huruma Shahidi anayesikiliza kesi hiyo, alikubaliana name upande wa utetezi name kesi hiyo itakuja Kwa ajili ya commital Februari 8, mwaka huu. 

Mbali na Kitilya washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni maofisa wa Benki ya Stanbic, Shose Sinare na Sioi Solomon, Kamishna wa Sera ya uchambuzi wa Madeni kutoka Wizara Fedha na Mipango, Bedason Shallanda na msaidizi wake Alfred Misana.

Katika mashtaka hayo washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matatu ya kughushi, moja la kuongoza uhalifu, 49 utakatishaji fedha, mawili ya kutoa nyaraka za uongo, kujipatia fedha kwa njia ya udanyanyifu moja na shtaka moja la kutoa nyaraka kwa nia ya kumdanganya kwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango. 

Wanadaiwa kati ya Machi 15, 2013 na Januari 10, 2014 ndani ya jiji la Dar es Salaam kwa nia ya kudanyanya washtakiwa wote walijipatia Dola za Kimarekani Milioni sita wakionesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji wa upatikanaji wa mkopo na zililipwa kupitia Kampuni ya Egma T Ltd.


KUENDESHA GARI SPIDI NDOGO BILA SABABU ZA MSINGI NI KOSA KISHERIA.

$
0
0

Na Bashir Yakub. 

Wapo watu wanaojua kuwa kuendesha gari kwa mwendo mdogo ndio ustaarabu na ndio jambo zuri linalopendwa sana na sheria. Yeyote mwenye mawazo ya aina hii amekosea sana. Kifungu cha 56 cha Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya `168 kinakataa dhana hii. 

Kifungu hicho kinasema kuwa “dereva wa gari au teela ambaye bila sababu za msingi ataendesha kwa mwendo mdogo(low speed) ambao utaelekea kuwasababishia watumiaji wengine wa barabara usumbufu au utawasababishia usumbufu, atakuwa ametenda kosa na panapo hatia yake atatakiwa kuadhibiwa kwa kulipa faini”. 

Maneno bila sababu za msingi hapo juu humaanisha kuwa kama itatokea mtu anaendesha kwa mwendo mdogo basi kuwepo na sababu za msingi za kufanya hivyo na hapo ndipo anaweza kukwepa kuingia katika kosa hili. 

Sababu za msingi zaweza kuwa foleni kubwa na hivyo huwezi kuongeza mwendo, unaendesha ndani ya msafara rasmi unaotambulika kisheria, maelekezo ya vibao na alama za usalama za eneo hilo yanakuelekeza kuendesha kwa mwendo huo, ubovu wa barabara ambao haukuruhusu kwenda mwendo mkubwa, barabara imezuiwa na waandamanaji au halaiki(population) nyingine ambayo haikuruhusu kwenda haraka. 

Ubovu wa gari unaweza kuwa sababu ya kutembea taratibu lakini sio sababu ya msingi. Sheria hii inaelekeza gari likiwa bovu kutokuendeshwa barabarani kwa maana ya kuwekwa pembeni ili kulirekebisha au kutafuta namna nyingine. 


KUSOMA  ZAIDI sheriayakub.blogspot.com



Viewing all 110025 articles
Browse latest View live




Latest Images