Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

MAHAKAMA YA WATOTO KISUTU YAPOKEA MASHAURI 118 YA JINAI KWA MWAKA 2018

$
0
0
Kwa mwaka 2018 Mahakama ya watoto ya Kisutu ilipokea jumla ya mashauri 118 ya jinai na makosa 295 ya madai yalipokelewa na kufanyiwa kazi na matukio ya kesi za watoto yakiwa wengi wa watoto hao ni wale ambao wamekinzana na Sheria na pili ni wale ambao Sheria inawakuta na makosa. Hayo yamebainishwa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Mahakama ya Kisutu Bi. Agness Mchome wa jijini Dar es Salaam wakati akitoa maelezo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu Maendeleo ya Jamii) Dkt. John Jingu alipotembelea katika Mahakama ya Watoto Kisutu jijini Dar es Salaam.

Hakimu Agness Mchome amewataka wazazi kutimiza wajibu wao wa malezi kwa watoto ili kuwaepusha na mashitaka yanayozuilika kwani watoto wanaofikishwa mahakamani ni wale ambao wazazi au walezi wao hawakutimiza wajibu wao wa kutoa malezi stahiki.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu ameridhishwa na utendaji kazi wa Mahakama ya Watoto ya Kisutu jijini Dar Es Salaam kwani imekuwa ikifanya kazi nzuri ya kusaidia kurekebisha maadili ya watoto nchini.

Dkt. Jingu amesisitiza wazazi kuzingatia malezi bora na kutoacha watoto kuangalia televisheni na mitandao ya kijamii wakati wote ambapo kwa kiasi kikubwa mitandao ya kijamii na video zisizo na maadili zinachangia kuharibu maadili ya watoto nchini.
 Katibu Mkuu Wizara yaAfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) (kushoto) Dkt. John Jingu akisisitiza jambo wakati wa ziara yake ya kufuatilia utekelezaji wa kazi za Maendeleo na Ustawi wa Jamii na Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika Mkoa Dar es salaam (katikati) ni Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi Bi. Rehema Kombe na kulia ni Afisa Ustawi wa Jamii wa mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sufiani Mdolwa.
Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Given Sure (kulia) akitoa maelezo kuhusu utekelezaji wa kazi za Idara ya Maendeleo ya Jamii ya Mkoa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii) Dkt. John Jingu (hayupo pichani) na kulia ni Afisa Ustawi wa Jamii wa mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sufiani Mdolwa. Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MAKOSA YA UBAKAJI NA KUPATIKANA NA SILAHA YALIONGEZEKA MKOANI PWANI 2018-WANKYO

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, PWANI 

MAKOSA ya ubakaji yametajwa kuongezeka kutoka 206 kwa mwaka 2017 na kufikia 271 mwaka 2018,mkoani Pwani .

Aidha kupatikana na silaha mwaka 2017 yalikuwa makosa tisa ambapo mwaka uliopita yameongezeka na kufikia 26 .

Akielezea tathmini ya hali ya uhalifu katika kipindi cha mwaka 2018 ikilinganisha na mwaka 2017 ,kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Wankyo Nyigesa alisema tathmini ya kijumla inaonyesha wamepunguza matukio 151 makubwa .

Alisema, makosa ya ubakaji yameonekana kupanda kutokana na uelewa kwa jamii na mwamko wa kuripoti matukio hayo polisi. Wankyo alieleza, matukio ya mauaji yalikuwa 61 ikilinganisha na matukio 70 yaliyoripotiwa mwaka 2017 ."Makosa ya kufanya biashara ya kusafirisha binadamu mwaka 2018, yalikuwa 03 ikilinganishwa na makosa 05 yaliyorekodiwa mwaka 2017"alifafanua Wankyo. 

Kamanda huyo alisema kuwa, makosa ya unyang 'anyi wa kutumia silaha mwaka 2017 yalikuwa 21 na mwaka 2018 makosa hayo ni 13.Unyang'anyi wa kutumia nguvu mwaka 2017 yaliriporiwa makosa 126 ,wakati mwaka 2018 makosa ya namna hiyo yameripotiwa makosa 52 .

Alisema, jeshi hilo pia limefanikiwa kudhibiti uingizaji bidhaa kupitia bandari bubu wilayani Bagamoyo kwa kukamata makosa 27,watuhumiwa 31 pamoja na madumu 5,435 ya mafuta ya kula aina mbalimbali .

"Sukari kutoka nchi za nje mifuko 78, mabello 20 ya nguo za mitumba aina mbalimbali ikiwemo manne ya khanga na vyombo vya moto vilikamatwa ikiwa ni pamoja na pikipiki sita na magari matatu. "alieleza Wankyo.

kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Wankyo Nyigesa  akitoa ufafanuzi .

BALOZI SEIF AZINDUA BARABARA PEMBA

$
0
0
     Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewakumbusha Wananchi wanaoishi pembezoni mwa Miundombinu ya Barabara Nchini kuwa walinzi kwa kutoa Taarifa kwa vyombo husika dhidi ya wale wanaoharibu kwa makusudi miundombinu hiyo iliyojengwa kwa gharama kubwa.

Alisema wapo baadhi ya Watu waliojitoa mshipa wa fahamu kwa kuiba alama zilizowekwa Bara barani, kuchimba Mchanga au udongo pembezoni mwake jambo ambalo kama Wananchi hawatakuwa tayari kutoa ushirikiano wao kwa vyombo vya Dola  ile azma ya Serikali ya kuimarisha Sekta ya Mawasiliano inaweza kufifia.

Balozi Seif Ali Iddi alitoa kumbusho hilo wakati wa hafla ya kuizindua rasmi barabara ya Kilomita Tatu iliyojengwa kwa Kiwango cha Lami kuanzia Wawi -Mabaoni  hadi Mgogoni Chake Chake Pemba ikiwa ni mwanzoni mwa Shamra shamra za Maadhimisho ya kusherehekea Miaka 55 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Alisema uzoefu unaonyesha wazi kwamba mahala popote palipojengwa Miundombinu ya Bara bara katika kipindi kifupi hutoa fursa kwa Wananchi wake kunawirika Kiuchumi kutokana na harakati za Kibiashara zinazoambatana na ujenzi wa Makaazi bora yanayolingana na uwepo wa Bara bara husika.
 Balozi Seif akizungumza na Wananchi wa Wilayua ya Chake chake katika hafla ya uzinduzi wa Barabara ya Wawi – Mabaoni – Mgogoni ndani ya shamra shamra za maadhimisho ya Sherehza kutimia Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mwakilishi wa Jimbo la Wawi Mheshimiwa Hamadi Ali Rashid { Gerei } akitoa shukrani kwa Serikali kwa niaba ya Wananchi wa Jimbo lake kutokana na Utekelezaji sahihi wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2015 -2020 katika Sekta ya Mawasiliano. Picha na – OMPR – ZNZ.
  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiizindua Barabara ya Kilomita Tatu ya Wawi – Mabaoni – Mgogoni ikiwa ni shamra shamra za Mapinduzi ya Zanzibar kutimia Miaka 55.
 Muonekano wa Barabara ya Wawi Mabaoni – Mgogoni iliyozinduliwa na Balozi Seif imeigharimu Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zaidi ya Shilingi Bilioni 1.9.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

HALOTEL YAJIVUNIA MAFANIKIO YA MWAKA 2018, WAKATI IDADI YA WATEJA WAKE IKIFIKIA MILIONI 4 NCHINI KOTE

$
0
0

• Thamani ya HaloPesa hadi 356%
. Malengo kuwafikia wateja wa Halopesa 1.5 million 2019

2018 ulikuwa mwaka mzuri kwa Kampuni ya Halotel Tanzania ikiwa moja ya Kampuni ya Mawasiliano iliyosajiliwa nchini ikifanikiwa kuongeza idadi ya wateja na mawasiliano katika maeno mbalimbali nchini.

Takwimu zilizopo zinaonyesha watumiaji wa mtandao wa Halotel hadi Septemba imeweza kufikia wateja Milioni 4 ikikua kutoka wateja 3.7 Milioni Septemba Mwaka 2017 .Halkadhalika idadi ya watumiaji wa Halopesa ikionekana kuongezeka kwa kasi kutoka watumiaji 358,217 Septemba Mwaka 2017 hadi watumiaji 800,000 Septemba Mwaka 2018.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam leo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni Nguyen Van Son, kuongezeka kwa mafanikio hayo ya Kampuni hiyo hususani katika huduma za watumiaji wa Halopesa kumetokana na mpango wa utoaji huduma kwa wateja uliozinduliwa na Kampuni mapema Mwaka 2018.

“Kwa kifupi kampuni imeweza kukua katika utoaji wa huduma zake mbalimbali kwa kipindi chote cha mwaka uliopita, katika kipindi hicho Halotel imezindua huduma mbalimbali ikiwemo huduma shirikishi inayomwezesha mteja kutuma au kupokea Fedha kutoka Halopesa kwenda katika akaunti yake au mtandao mwingine wowote wa simu; pia tulizindua huduma ya utoaji mkopo ijulikanayo kama ‘HaloYako’.

“Aidha katika kipindi hicho pia tulikuja na mpango wa ulipaji malipo mbalimbali Serikalini kumwezesha mteja kuondokana na usumbufu mbali na hiyo pia tumeweza kumrahisishia mteja kuweza kutuma fedha katika benki zaidi ya 20 zilizopo nchini” alisema Son.HaloPesa ilikuwa na mawakala hai wapatoa 10,367 Mwaka 2017 lakini hadi tunapozungumza hivi sasa idadi hiyo imeongezeka na kufikia Mawakala 155,000 nchini kote

Aidha alisema mapato yaliyotokana na thamani ya manunuzi ya HaloPesa pia yaliongezeka hadi kuifikia 183%, "Tuliona kiwango cha 356% katika thamani ya manunuzi ya HaloPesa na ongezeko kwa 167% alisema.


Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mawasiliano ya Halotel, Nguyen Van Son, akizungumza mbele ya Waandishi wa habari leo jijini Dar kuhusu mafaniklio iliyopata katika kipindi cha mwaka 2018, ikiwemo kuimarika kwa huduma ya Halopesa na kwa mkongo wa mawasiliano wa kampuni hiyo ambao umefikisha katika vijiji zaidi ya Kumi na tatu elfu nchi nzima,kulia ni
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Kampuni ya Mawasiliano ya Halotel, Mhina Semwenda.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Kampuni ya Mawasiliano ya Halotel, Mhina Semwenda, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam, leo kuhusu mafanikio iliyopata katika kipindi cha mwaka 2018, ikiwemo kuimarika kwa huduma ya Halopesa na kwa mkongo wa mawasiliano wa kampuni hiyo ambao umefikisha katika vijiji zaidi ya Kumi na tatu elfu nchi nzima. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji , Nguyen van Son.

WAZIRI LUGOLA APIGA MARUFUKU POLISI KUWAKAMATA WAENDESHA BODABODA WAKIWA HAWAJAVAA SARE

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA-Bukoba.

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amepiga marufuku tabia ya baadhi ya Askari Polisi nchini kukamata pikipiki wakiwa hawana sare za Jeshi.

Akizungumza na mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa uhuru, Mayunga, mjini Bukoba Mkoani Kagera, leo, Lugola alisema polisi wanapaswa kufuata utaratibu wa kijeshi hasa wanapokamata vyombo vya moto na siyo kuvunja utaratibu.

Lugola aliongeza kuwa, bodaboda zinazovunja sheria za usalama barabarani zinapaswa kukamatwa bila kuwaonea huruma, ila ni kosa Polisi kuwanyanyasa vijana hao ambao wanapata ridhiki kupitia biasahara hiyo. “Mnapaswa kukamata hizi bodaboda zinapofanya makosa, tabia ya kukurupuka huku mkitafuta fedha zisizo halali, huko ni kuwaonea waendesha bodaboda,” alisema Lugola.

Pia Lugola aliwataka waendesha bodaboda mjini Bukoba na Tanzania kwa ujumla wafuate sharia za usalama barabarani zikiwemo kuvaa kofia ngumu, kutokubeba abiria zaidi ya mmoja na pia wakiendesha wanapaswa kuwasha taa. Lugola ameanza ziara yake ya siku nane mkoani humo akitembelea Wilaya zote za Mkoa huo akisikiliza kero za wananchi pamoja na kufuatilia maagizo yake aliyoyatoa kwa vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo ndani ya Wizara yake.







Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na mamia ya wananchi mjini Bukoba Mkoani Kagera, katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Uhuru, Mayunga mjini humo, leo. Lugola licha ya kuwa amewataka waendesha bodaboda wafuate sheria za usalama barabarani, lakini ametoa onyo kwa Polisi mjini humo kuacha kuwakamata waendesha bodaboda wakiwa hawajavaa sare. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akimsikiliza Mkazi wa mjini Bukoba alipokuwa anaeleza kero yake mara baada ya Waziri huyo kuwaita wananchi hao mbele waweze kutoa kero zao, mara baada ya kumaliza kuzungumza na wananchi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Uhuru, Mayunga mjini humo, leo. Lugola licha ya kuwa amewataka waendesha bodaboda wafuate sheria za usalama barabarani, lakini ametoa onyo kwa Polisi mjini humo kuacha kuwakamata waendesha bodaboda wakiwa hawajavaa sare. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akimsalimia Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Bashiru Ally, wakati alipoonana naye Uwanja wa Ndege wa Bukoba, leo. Lugola yupo Mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi akitembelea Wilaya zote, akisikiliza kero mbalimbali za watumishi wa Wizara yake pamoja na wananchi mkoani humo. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akitoka Kituo Kikuu cha Polisi cha mjini Bukoba mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Kituo hicho, leo, kwa kufuatilia utendaji kazi wao. Katikati ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Revocatus Malimi, na kulia ni Mkuu wa Jeshi la Magereza Mkoani humo, ACP Raymond Mwampashe. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 

MICHUZI TV :MAMBOSASA ASEMA DAR IKO SALAMA,HAKUNA 'PANYA ROAD'

$
0
0



Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema Jiji hilo liko shwari na hakuna tukio lolote la uvunjifu wa amani ambalo linahusishwa na uwepo wa 'Panya road'.

Akizungumza leo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amewahakikishia wananchi wa Jiji hilo kuwa hali ni shwari na hakuna tukio ambalo limetokea hasa kwenye siku ya mkesha wa mwakya mpya wa 2019.

"Tumeona moja ya gazeti likisema 'Panya road watikisa Dar'.Ukweli hakuna tukio limehusisha panya road siku ya mkesha wa mwaka mpya.Dar iko salama sana , hivyo taarifa hizo hazina ukweli wowote,"amesema Kamanda Mambosasa na kusisitiza Jeshi la Polisi Kanda Maalum limejipanga kuhakikisha usalama upo wa kutosha.

Amefafanua katika siku ya mkesha wa mwaka mpya kulikuwa na makundi ya watu mbalimbali wakiwamo wanaosheherekea mwaka mpya,makundi ya watu waliotoka Kanisani na maeneo mengine, hata hivyo hakukuwa na tukio ambalo limefanywa na hao wanaodaiwa kuwa panya road kwani hakuna panya road .

"Tupo kwa ajili ya kuhakikisha hali ya usalama inakuwa salama,hivyo asitokee mtu mmoja kwa utashi wake awatia hofu wananchi kwa kudai kuna panya road wakati hakuna," amesema Kamanda Mambosasa na kuongeza kuwa wananchi wasiwe na hofu na kuwatataka waendelee na shughuli zao kama kawaida za ujenzi wa uchumi wao na Taifa kwa ujumla kwa mwaka huu wa 2019.

MAKOSA YA UBAKAJI NA KUPATIKANA NA SILAHA YALIONGEZEKA MKOANI PWANI 2018-WANKYO

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, PWANI 
MAKOSA ya ubakaji yametajwa kuongezeka kutoka 206 kwa mwaka 2017 na kufikia 271 mwaka 2018, mkoani Pwani. Aidha kupatikana na silaha mwaka 2017 yalikuwa makosa tisa ambapo mwaka uliopita yameongezeka na kufikia 26 .

Akielezea tathmini ya hali ya uhalifu katika kipindi cha mwaka 2018 ikilinganisha na mwaka 2017 ,kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP)  Wankyo Nyigesa alisema tathmini ya kijumla inaonyesha wamepunguza matukio 151 makubwa. Alisema, makosa ya ubakaji yameonekana kupanda kutokana na uelewa kwa jamii na mwamko wa kuripoti matukio hayo polisi. 

Wankyo alieleza, matukio ya mauaji yalikuwa 61 ikilinganisha na matukio 70 yaliyoripotiwa mwaka 2017. "Makosa ya kufanya biashara ya kusafirisha binadamu mwaka 2018, yalikuwa 03 ikilinganishwa na makosa 05 yaliyorekodiwa mwaka 2017"alifafanua Wankyo. 

Kamanda huyo alisema kuwa, makosa ya unyang 'anyi wa kutumia silaha mwaka 2017 yalikuwa 21 na mwaka 2018 makosa hayo ni 13. Unyang'anyi wa kutumia nguvu mwaka 2017 yaliriporiwa makosa 126 ,wakati mwaka 2018 makosa ya namna hiyo yameripotiwa makosa 52 .

Alisema, jeshi hilo pia limefanikiwa kudhibiti uingizaji bidhaa kupitia bandari bubu wilayani Bagamoyo kwa kukamata makosa 27,watuhumiwa 31 pamoja na madumu 5,435 ya mafuta ya kula aina mbalimbali. "Sukari kutoka nchi za nje mifuko 78, mabello 20 ya nguo za mitumba aina mbalimbali ikiwemo manne ya khanga na vyombo vya moto vilikamatwa ikiwa ni pamoja na pikipiki sita na magari matatu. "alieleza Wankyo.  

VIJANA WATAKIWA KUSAIDIA WATOTO YATIMA NA WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU

$
0
0

NA DENIS MLOWE, IRINGA

MWENYEKITI wa Serikali za vyuo vikuu vya Kikatoriki chini, Anord Mvamba ametoa wito kwa vijana kujenga utamaduni wa kutembelea vituo vinavyowalea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu sanjari na kutatua changamoto wanazokabiliana nazo hatua itakayowasaidia kufikia malengo yao.

Ametoa rai hiyo juzi mara baada ya kujumuika pamoja na watoto wanaolelewa katika kituo cha kulelea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu cha Tosamaganga kilichoko wilaya ya Iringa mkoani Iringa wakati akiadhimisha siku ya kuzaliwa kwake.

Mvamba alisema kuwa kundi la watu wasiojiweza wanahitaji kupata misaada kutoka kwa jamii inayowazunguka na hasa vijana ambao wamekuwa wakitumia sehemu ya fedha katika mambo ya starehe zaidi kuliko kuwajali yatima ili wapate furaha.

Aliongeza kuwa ni vema kuona umuhimu na haja ya kuwasaidia ili wapate faraja hivyo na katika kusherehekea kumbukizi ya kuzaliwa kwake ameona umuhimu kama kijana kutoa sadaka na kusheherekea na watoto ho kwa wa vitu mbalimbali vikiwemo, chumvi, sukari, sabuni na vifaa vya shule.

Mvamba ambaye pia ni rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Ruaha Iringa (RUCU)alisema kuwa endapo vijana wengi wakijenga tabia ya kuwatembelea watoto yatima na wanaoshi katika mazingira magumu itakuwa fursa kwao kujifunza zaidi na kuwa na moyo wa huruma katika kuwasaidia kuliko kupoteza fedha nyingi katika starehe ambazo ni za muda mfupi tofauti na kuwekeza katika watu.

Aidha ameitaka jamii kujitolea kwa dhati kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji, ikiwa pamoja na kuwatembelea ili kujenga upendo kwa makundi maalumu yenye uhitaji kwa lengo la kupunguza changamoto zinazoyakabili makundi hayo.

Kwa upande wake,Sister Helena Kihwele ni msimamizi mkuu wa kituo cha watoto Yatima cha Tosamaganga alisema kituo kina jumla ya watoto 60 ambao hawajafikisha mwezi mmoja hadi miaka sita, na kuwa changamoto kubwa ni walezi kuwasahau watoto mara baada ya kukabidhiwa kituoni hapo.

“Changamoto hii inatusumbua sana maana baadhi ya walezi hawaji kuwasalimia wala kuwachukua watoto sasa tunapata shida wakati wanapotakiwa kurudi nyumbani, maana umri wa mwisho wa kukaa kituoni hapa ni miaka 6,” alisema Kihwele

Alisema kituo kinapokea watoto wasio na mama au wenye mama ambaye ni anatatizo la akili, na kuwa baadhi ya ndugu ndiyo wamekuwa wakiwatelekeza watoto mara tu wanapowafikisha kituoni hapo.

Changamoto nyingine zinazowakabili watoto ni baadhi ya wazazi kushindwa kuwaendeleza kielimu watoto, kwani baadhi ya walezi huwa hawana mwamko wa kuwaendeleza watoto hao, na hivyo kusababisha watoto hao kutoendelea na masomo.
Mwenyekiti wa Serikali za vyuo vikuu vya Kikatoliki chini, Anord Mvamba ambaye pia ni Rais wa Serikalia ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Ruaha Iringa, (RUCU) akimkabidhi moja vitu mbalimbali mlezi wa kituo cha kulelea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu cha Tosamaganga kilichoko wilaya ya Iringa mkoani Iringa Helena Kihwele wakati akiadhimisha siku ya kuzaliwa mwanzoni mwa ka. (picha na Denis Mlowe)

UCSAF YALETA CHANGAMOTO CHANYA KWA KAMPUNI ZA SIMU ZA MKONONI

$
0
0
Mkurugenzi Uendeshaji wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Mhandisi Albert Richard amemweleza Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye kuwa UCSAF imeleta changamoto chanya kwa kampuni za simu za mkononi zinazotoa huduma za mawasiliano nchini
Richard ameyasema hayo wakati wa ziara ya Nditiye ya kukagua changamoto za mawasiliano kwenye maeneo mbali mbali wilayani Sengerema mkoani Mwanza.  Richard amefafanua kuwa awali kampuni za simu za mkononi nchini zilisita kuwekeza kwenye vijiji mbali mbali ambavyo havina mawasiliano nchini kwa kuwa havina mvuto wa kibiashara ambapo kampuni hizo zilikuwa zinakwenda maeneo ya mijini yenye mvuto wa kibiashara
“Ila sasa Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano tunashirikiana na kampuni za simu za mkononi kufikisha huduma za mawasiliano vijijini na kampuni zimepata mwako,” amesema Richard. Ameongeza kuwa Serikali imekuwa inatoa ruzuku kwa kampuni hizo ili waweze kujenga minara kwa lengo la kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma za mawasiliano
Nditiye amesema kuwa amefanya ziara ya siku tatu ya kukagua mawasiliano kwenye maeneo mbali mbali wilayani Sengerema ili kuona changamoto za mawasiliano ambapo amekiri uwepo wa changamoto za mawasiliano kwenye Wilaya hiyo kwenye baadhi ya kata ambapo ina jumla ya kata 21 na kubaini uwepo wa ukosefu wa mawasiliano kabisa kwenye baadhi ya maeneo, mawasiliano ya kusuasua na mahitaji ya kuongeza nguvu ya usikivu wa mawasiliano kwenye baadhi ya maeneo
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa tatu kulia) akisikiliza kwa makini taarifa kutoka kwa Afisa Mtendaji Kata ya Katwe, Wilaya ya Sengerema, Mwanza, Deus Ngodagula Masasi (aliyenyoosha kidole) kuhusu ukosefu wa mawasiliano kwenye kisiwa cha Maisome wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya mawasiliano wilayani humo. Naibu Katibu Mkuu – Sekta ya Mawasiliano Dkt. Jim Yonazi (aliyeshika ramani) akiwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji, UCSAF, Mhandisi Albert Richard (wa kwanza kushoto).
Naibu Katibu Mkuu – Wizara Ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Sekta ya Mawasiliano Dkt. Jim Yonazi (aliyeinua mkono) akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa kwanza kulia) wakati wa ziara yake ya kukagua changamoto ya mawasiliano kisiwani Maisome, Mwanza. Anayesikiliza wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya TCRA, Dkt. Jones Kilimbe.
Diwani wa Kata ya Bangwe, wilayani Sengerema, Mwanza, Yonas Magikulu akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa kwanza kulia) wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya mawasiliano Wilayani humo. Wa kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara Ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Sekta ya Mawasiliano Dkt. Jim Yonazi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

DC MUHEZA:NITASHIRIKIANA NA WANAMICHEZO KUHAKIKISHA TUNAPATA TIMU YA LIGI KUU

$
0
0

MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Mwanasha Tumbo amesema atashirikiana na wanamichezo ili kuhakikisha wanaweza mazingira mazuri yatakayowezesha kupatikana timu ambayo itaweza kushiriki ligi madaraja ya juu ikiwemo Ligi kuu.

Mwanasha aliyasema hayo wakati fainali michuano ya kombe la Kabunda Cup iliyokuwa ikichezwa kwenye viwanja vya Vikonge Mtindiro wilayani Muheza ambapo alisema ili kuweza kuhakikisha wanafanikisha jambo hilo wataendelea kuhamasisha vijana kujikita kwenye michezo.

Alisema licha ya kuhamasisha michezo kutokana na kwamba ni ajira ambayo inaweza kuwainua vijana kuichumi na kupata maendeleo lakini pia aliwahaidi kuwajengea kiwanja cha mpira chenye matofali ili waweze kuonyesha umahiri wao na hatimaye wilaya hiyo iweze kupata mafanikio kwenye soka.

“Leo nimekuja hapa kuhimitisha Ligi hii kwanza nimefurahishwa sana na viwango ambavyo mmekuwa mkivionyesha kwenye mchezo huu nimeongeza na Diwani wenu hapa na niwahaidi kwamba nitawajengea kiwanja chenye matofali ili hari ya kushiriki kwenye michezo muweza kuendelea nayo na tunaamini siku zijazo tutairudisha Muheza kwenye ramani ya soka “Alisema DC Mwanasha.

MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati akifunga Mashindano ya Kombe la Kabunda Cup

MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akimkabidhi Kombe la Ubingwa wa Mashindano ya Kabunda Cup Nahodha wa timu ya Ushirika Amiri Nko kushoto ni Afisa Michezo wa wilaya ya Muheza Anania Sama
Nahodha wa timu ya Ushirika Amiri Nkoa akiwa ameinua kombe hilo juu mara baada ya kukabidhiwa 
MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akimkabidhi Kitita cha Milioni moja Nahodha wa timu ya Ushirika Amiri Nko baada ya timu yao kuibuka na ushindi kwenye michuano ya Kombe la Kabunda Cup kushoto ni Afisa Michezo wa wilaya ya Muheza Anania Sama .


MICHUZI TV: POLISI KANDA MAALUM DAR YAKANUSHA UWEPO WA PANYA ROAD

DAWASA YATAKIWA KUFANYAKAZI KWA BIDII ILI KUFIKIA MALENGO YAKE

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo ameitaka Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) kusimamia miradi ya maji kwa umakini mkubwa.

Amewataka DAWASA kuhakikisha kufikia 2020 asilimia 85 ya vijijini na asilimia 95 ya mijini inapata maji safi na salama. Mkumbo amesema hayo wakati wa utiaji saini wa makubaliano ya jengo la Maji lililopo Ubungo jijini Dar es Salaama na linalotarajiwa kumalizaika Februari 2020.

Utiaji wa saini hiyo ulihudhuriwa pia na Mwenyekiti wa Bodi ya DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyage na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja. Akizungumza baada ya utiaji wa saini, Mkumbo amesema DAWASA lazima wahakikishe wanasimamia mapato ili kuweza kuendeleza miradi ya maji ili wananchi waweze kufaidika.

Amesema, hafla ya leo sio ya kukabidhiwa jengo tu ila wanatakiwa kusimamia mradi wa Kidunda, visima vya Kimbiji Mpera pamoja na kuwaunganishia wateja wapya. Kwa upande wa Mwenyekiti wa Bodi Mwamunyage amesema changamoto kubwa iliyokuwepo katika mamlaka hiyo ni maeneo ya kufanyia kazi ila baada ya kukabidhiwa jengo hilo wanaamini kwa sasa kazi zitafanyika kwa wakati.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo akizungumza na wanahabari na wageni waalikwa wakati wa utilianaji wa saini wa usimamizi wa jengo la Maji lililokuwa likijengwa na Wizara ya maji na Umwagiliaji na sasa wamekabidhiwa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) kwa ajili ya kulimalizia na kuhamishia ofisi. Picha na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Mwenyekiti wa Bodi ya DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyage akizungumza na wanahabari na wageni waalikwa wakati wa utilianaji wa saini wa usimamizi wa jengo la Maji lililokuwa likijengwa na Wizara ya maji na Umwagiliaji na sasa wamekabidhiwa DAWASA kwa ajili ya kulimalizia na kuhamishia ofisi. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo na kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja. 
Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja akitoa machache.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo (kushoto) akisaini mkataba na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja (katikati) wa kusimimia jengo la Maji House linalotarajiwa kumalizika Februari 2020. Pambeni kulia ni mmoja ya wajenzi wa kampuni ya CCECC ambao ndiyo wakandarasi. Wafanyakazi wa DAWASA na wageni waalikwa wakifuatiliwa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo (kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyage (anayefuata kushoto) wakifurahi pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja (kushoto) mara baada ya kuzindua picha ya jengo la Maji linalotarajiwa kumalizika Februari 2020.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

UFUNGUZI WA NYUMBA YA WALIMU WAFANYIKA ZANZIBAR

$
0
0
 Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo akiwa pamoja na Mshirika wa Maendeleo Mkurugenzi Mkuu wa DSTV Jacqueline Woiso wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa Nyumba ya Walimu Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
  Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo kushoto akimkabidhi Mshirika wa Maendeleo Mkurugenzi Mkuu wa DSTV Jacqueline Woiso zawadi ya Cheti maalum katika ufunguzi wa Nyumba ya Walimu Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
 Mshirika wa Maendeleo Mkurugenzi Mkuu wa DSTV Jacqueline Woiso akitoa hotuba kuhusiana na namna alivyosaidia kumaliza kwa Nyumba ya Walimu katika Ufunguzi wa Nyumba hio Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo akitoa hotuba ya ufunguzi wa Nyumba ya Walimu katika ufunguzi wa Nyumba ya Walimu Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.  
 Nyumba ya Walimu wa Skuli ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja iliofunguliwa na Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya mapinduzi ya Zanzibar.
 Nyumba ya Walimu wa Skuli ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja iliofunguliwa na Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya mapinduzi ya Zanzibar.
PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

Jafo apongeza Ujenzi Ofisi za Halmashauri-KIBITI

$
0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo amewapongeza viongozi wa Wilaya ya Kibiti kwa Ujenzi mzuri wa Ofisi za Halmashauri ya Wilaya Kibiti mradi unao tarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni tatu.

Waziri Jafo alitoa pongezi hizo Leo hii alipokuwa katika ziara ya kikazi Wilayani Kibiti Mkoani Pwani. Ujenzi huo unaojengwa na mkandarasi SUMAJKT chini ya Mshauri Chuo Kikuu cha Ardhi umemridhisha sana Waziri Jafo kutokana na kuzingatiwa kwa viwango vya ubora katika ujenzi huo. Hata hivyo Jafo ameagiza kuongezwa kwa kasi ya ujenzi ili mradi huo ukamilike kabla ya mwezi Julai, 2019.

Katika ziara hiyo ya kikazi wilayani Kibiti Waziri Jafo alifanikiwa kutembelea mradi huo pamoja na mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Kivinja “A” ambao unagharimu shilingi milioni 400. Katika kuhitimisha ziara yake wilayani humo waziri Jafo ameutaka uongozi wa wilaya hiyo kutumia fursa waliyonayo ya tofali nzuri zenye ubora zinazo zalishwa na SUMAJKT katika ujenzi wa hospitali ya wilaya ambayo wameshapokea shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo.

Aidha, Mbunge wa Jimbo la Kibiti Mhe. Seif Ungando ameishukuru sana Serikali ya DKT. John Pombe Joseph Magufuli kwa msaada mkubwa wa miradi ya maendeleo inayo elekezwa wilayani Kibiti.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo(katikati) akitoa maelekezo wakati akikagua ujenzi wa Ofisi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo aKiwa na viongozi wa Wilaya ya Kibiti wakati wa ziara yake Wilayani humo. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo(katikati) akitoa maelekezo wakati akikagua ujenzi wa Ofisi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti.

Jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti linaloendelea kujengwa. 

MUDA WA KUMUONESHA TRAFIKI LESENI NI MPAKA SIKU TATU KAMA UMESIMAMISHWA NA HUNA.

$
0
0
Na Bashir Yakub. 

Kusimamishwa na trafiki barabarani, na ukawa huna leseni mfukoni kwa muda huo sio kosa. Mwambie huyo trafiki kuwa hilo sio kosa. Sheria inatutaka kutembea na leseni tunapoendesha vyombo vya moto, lakini pia haisemi kuwa utakapokuwa hauna pale unapoombwa na trafiki basi ni kosa. 

Tunaongelea Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168. Wapo watu wameandikiwa faini kisa wameombwa leseni wakasema hawana, au wakasema wamezisahau majumbani. Hawa waliotozwa faini katika mazingira kama haya wameonewa. Na wanastahili kurudishiwa fedha walizotoa haraka. 

Ni kweli kifungu cha 77 cha Sheria ya Usalama Barabarani kinamtaka kila mwendesha chombo cha moto kutembea na leseni barabarani. Ni kweli askari anayo mamlaka kumsimamisha mwendesha chombo cha moto. Na ni kweli pia kuwa askari anayo mamlaka ya kumtaka mwendesha chombo cha moto aoneshe leseni yake. Lakini sio kweli hata kidogo kuwa mwendesha chombo cha moto asipoonesha leseni kwa wakati huo basi tayari ametenda kosa. Sio kweli. 

Kifungu cha 77(1) cha Sheria ya Usalama Barabarani kinasema kuwa mtu hatatiwa hatiani, kwa maana ya kulipa faini au kuandikiwa kosa au kuadhibiwa na chombo chochote ikiwamo mahakama, kwasababu tu hakubeba, au hakutoa/kuonesha leseni pale alipotakiwa kufanya hivyo, isipokuwa ana siku tatu za kutoa au kuonesha leseni hiyo tokea siku hiyo aliposimamishwa. 



WAZIRI WA UTALII AFUNGUA NYUMBA YA WALIMU ZANZIBAR

$
0
0



Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo akiwa pamoja na Mshirika wa Maendeleo Mkurugenzi Mkuu wa DSTV Jacqueline Woiso wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa Nyumba ya Walimu Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
????????????????????????????????????
Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo kushoto akimkabidhi Mshirika wa Maendeleo Mkurugenzi Mkuu wa DSTV Jacqueline Woiso zawadi ya Cheti maalum katika ufunguzi wa Nyumba ya Walimu Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
????????????????????????????????????
Nyumba ya Walimu wa Skuli ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja iliofunguliwa na Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya mapinduzi ya Zanzibar.
????????????????????????????????????
Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo akisalimiana na Mshirika wa Maendeleo Mkurugenzi Mkuu wa DSTV Jacqueline Woiso mara baada ya kuwasili katika Ufunguzi wa Nyumba ya Walimu Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar
????????????????????????????????????
Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo kushoto akimkabidhi Mshirika wa Maendeleo Mkurugenzi Mkuu wa DSTV Jacqueline Woiso zawadi ya Cheti maalum katika ufunguzi wa Nyumba ya Walimu Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
????????????????????????????????????
Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo akitoa hotuba ya ufunguzi wa Nyumba ya Walimu katika ufunguzi wa Nyumba ya Walimu Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo akitoa hotuba ya ufunguzi wa Nyumba ya Walimu katika ufunguzi wa Nyumba ya Walimu Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja ikiwa ni Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

TANZIA

$
0
0
Ndugu Isaac Zumba wa Ngarenaro, Arusha. Anatangaza kifo cha mke wake Amabilis Zumba kilichotokea jana katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mwili unategemewa kuagwa kesho Ijumaa saa sita mchana, Muhimbili hospital-katoliki, na baada ya hapo  kuelekea Arusha kwa ajili ya mazishi siku ya Jumanne tar 8 Januari. Salaam ziwafikie ndugu wote wa  koo za Zumba na Mumba waishio ndani na nje ya nchi.

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

NISHATI WAUNGA MKONO JITIHADA ZA RAIS KUWEZESHA WACHIMBAJI MADINI WADOGO

$
0
0
Na Veronica Simba – Geita
Wizara ya Nishati inatekeleza mkakati wa kuwaunganishia umeme wa uhakika wachimbaji wadogo wa madini kote nchini, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais John Magufulu kuiwezesha sekta hiyo izalishe kwa tija kwa manufaa yao binafsi na ya Taifa kwa ujumla.

Akizungumza katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi wa kiwanda cha kuchenjua dhahabu, kinachomilikiwa na kampuni ya Padalu, kijijini Lumasa, Chato; Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa eneo hilo, Dkt Medard Kalemani, alisema serikali imefunga transfoma tano zenye uwezo wa KVA 400 hadi 1,000 ili kuwawezesha wachimbaji wadogo wa Geita kuzalisha kwa tija.

“Umeme huu mkubwa utawawezesha wachimbaji kuchimba , kuchenjua na kuongeza thamani dhahabu yao ili kuiongezea thamani, iwapatie faida na waweze kulipa kodi na mrabaha serikalini,” alisema.

Akieleza zaidi, Waziri Kalemani alisema yako maeneo mkoani humo ambayo bado hayajafikiwa na huduma hiyo lakini akabainisha kuwa utaratibu wa kufunga transfoma nyingine tano zenye uwezo uleule, unafanyika ili kuyafikia maeneo ya wachimbaji yaliyosalia ikiwemo Mbogwe na Nyakafuru.
 Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani (kushoto) na Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (kulia), wakifungua kitambaa maalum kilichofunika jiwe la msingi la kiwanda cha uchenjuaji dhahabu cha Padalu, kilichopo Chato Geita, kuashiria uzinduzi rasmi. Hafla hiyo ilifanyika Januari 2, 2019.
 Msimamizi wa Kiwanda cha kuchakata dhahabu cha Padalu, kilichopo Chato Geita, Abel Lucas (kulia), akitoa maelezo jinsi kinavyofanya kazi kwa Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani pamoja na Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko, na ujumbe waliofuatana nao, wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi wa kiwanda hicho, Januari 2, 2019.
 Msimamizi wa Kiwanda cha kuchakata dhahabu cha Padalu, kilichopo Chato Geita, Abel Lucas (kushoto), akitoa maelezo jinsi kinavyofanya kazi kwa Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani (wa kwanza kulia) pamoja na Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko (wa pili – kulia), wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi wa kiwanda hicho, Januari 2, 2019.
 Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani (katikati), akisalimiana na Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko (kushoto), walipowasili kwenye hafla ya uwekaji jiwe la msingi katika kiwanda cha kuchenjua dhahabu cha Padalu kilichopo Chato Geita, Januari 2, 2019. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mhandisi Msafiri Mtemi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
 Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani akizungumza na wananchi, wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi katika kiwanda cha kuchenjua dhahabu cha Padalu kilichopo jimboni mwake, Chato Geita, Januari 2, 2019.
Sehemu ya umati wa wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani (hayupo pichani), wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi katika kiwanda cha kuchenjua dhahabu cha Padalu kilichopo jimboni humo, Chato Geita, Januari 2, 2019.

MFUMO MPYA WA KUTOLEA HUDUMA ZA KIBENKI WAZINDULIWA ZANZIBAR

$
0
0


Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Dk,Sira Ubwa Mamboya akibonyeza kitufe kuashiria Uzinduzi wa Mfumo Mpya wa kutolea huduma za Kibenki uliofanyika katika Makao makuu ya PBZ Mpirani Wilaya ya Mjini Unguja Ikiwa Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Dk,Sira Ubwa Mamboya akisisitiza jambo alipotoa hotuba ya Ufunguzi wa Mfumo Mpya wa kutolea huduma za Kibenki uliofanyika katika Makao makuu ya PBZ Mpirani Wilaya ya Mjini Unguja Ikiwa Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ)waliohudhuria katika Uzinduzi wa Mfumo Mpya wa kutolea huduma za Kibenki uliofanyika katika Makao makuu ya PBZ Mpirani Wilaya ya Mjini Unguja Ikiwa Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Katibu Mkuu Fedha na Mipango Khamis Mussa Omar akitoa hotuba na kumkaribisha mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Mfumo Mpya wa kutolea huduma za Kibenki uliofanyika katika Makao makuu ya PBZ Mpirani Wilaya ya Mjini Unguja Ikiwa Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mkurugenzi mtendaji wa PBZ Juma Ameir Hafidh akitoa hotuba katika hafla ya Uzinduzi wa Mfumo Mpya wa kutolea huduma za Kibenki uliofanyika katika Makao makuu ya PBZ Mpirani Wilaya ya Mjini Unguja Ikiwa Shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images