Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109973 articles
Browse latest View live

BENKI YA EXIM YATAMBA TUZO YA MWAJIRI BORA

$
0
0



Kaimu Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki hiyo Bw David Lusala (kushoto) akipokea kwa niaba ya benki hiyo tuzo ya mwajiri bora wa ndani wa mwaka 2018 (Best Local Employer of the year 2018) kutoka kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama (kulia) kwenye hafla ya tuzo za Mwajiri Bora (EYA) za mwaka 2018 zilizoandaliwa na Chama cha Waajili Tanzania (ATE) na kufanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mkuu wa Matawi ya Benki ya Exim Bi Elizabeth Mayengoh (wa tatu kulia) akifurahia pamoja na wafanyakazi wengine wa benki hiyo mara baada ya kukabidhiwa tuzo ya kuwa miongoni mwa waajiri wa ndani bora wa mwaka 2018 (Best Local Employer of the year 2018) kwenye hafla ya tuzo za Mwajiri Bora (EYA) za mwaka 2018 zilizoandaliwa na Chama cha Waajili Tanzania (ATE) na kufanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Wengine ni pamoja na Kaimu Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa Benki hiyo Bw David Lusala (katikati) pamoja Meneja Msaidizi wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo Bw Abdulrahman Nkondo.
Wafanyakazi wa benki ya Exim wakifurahia kwa pamoja tuzo hiyo.

DC NAMTUMBO AONYA WANAOJIHUSISHA NA MAFUNZO YA KIGAIDI

$
0
0

*Asema baadhi yao wapo wanafunzi waliomaliza elimu ya msingi, adai anao ushahidi

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Mfaume Kizigo amewahatahadharisha vijana wanaomaliza darasa la saba na kidato cha nne ambao hawakubahatika kuendelea na masomo kuacha kujiunga na mafunzo ya kigaidi.

Kizigo aliyasema hayo kwenye kikao cha ushauri cha Wilaya ya Namtumbo kilichofanyika jana ukumbi wa Halmashauri ya wilaya hiyo ambapo amedai 

kuwepo kwa ushahidi wa wazi wa jeshi la polisi ambao unadai wanafunzi wanaomaliza darasa la saba na wale wanaomaliza kidato cha nne na kutobahatika kuendelea na masomo ndio wanaojiunga na mafunzo hayo ya ugaidi wilayani humo.Hata hivyo kupitia kikao hicho Mkuu wa wilaya huyo aliagiza wanafunzi wote wanaomaliza darasa la saba na kidato cha nne ambao hawatapata nafasi ya kuendelea na masomo na wanapohitajika na taasisi za kidini kwa kisingizio cha kwenda kufanya kazi lazima wapate kibali kutoka katika ofisi yake.

Kwa upande wa Katibu wa Chama cha Wananchi (CUF) wilayani Namtumbo Rashidi Mfaume pamoja na kumpongeza mkuu wa wilaya kwa hatua hiyo lakini alimwomba kuwashirikisha wenyeviti wa serikali za mitaa na vitongoji katika utoaji wa vibali hivyo.Pamoja na hayo kikao hicho cha ushauri cha wilaya kilipitia muhtasari wa maadhimio ya mwaka 2016 ambapo adhimio la kuanzisha Wilaya ya Sasawala wajumbe walidai liindelee kufuatiliwa kulingana na umuhimu wake pamoja na adhimio la kuongezewa jimbo la Sasawala nalo lilibaki kama lilivyopitishwa katika kikao cha mwaka 2016.

Kuhusu azimio la kuyarudisha mashamba yanayomilikiwa na (NAFCO)Shirika la chakula la taifa ambayo kwa sasa hayaendelezwi yarudishwe kwa wananchi pamoja na shamba la Likenangena ambalo nalo awali lilionekana kumilikiwa na wizara ya fedha nalo haliendelezwi .

Mafunzo ya kigaidi wilayani humo yalibainika kufanywa katika misitu ya kijiji cha Mchomoro na Masuguru wilayani humo ambapo Jeshi la polisi Kwa umahiri wake walifanikiwa kuwakamata wahusika na kusambaratisha mafunzo hayo.

DC ARUMERU AZINDUA KAMPENI YA KUHAMASISHA UTALII WA NDANI,AWAOMBA WANANCHI KUTENGA MUDA WA KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII NCHINI

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro amezindua kampeni ya kuhamasisha utalii wa Ndani Kwa kuwataka wananchi kutenga muda wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini .

Mhe Muro amewataka Watanzania wanaotoka katika mikoa ya kanda ya Kaskazini Tanga,Kilimanjaro, Arusha na Manyara ambao Wana tabia ya kwenda nyumbani nyakati za sikukuu ya Xmass na Mwaka mpya kuweka utamaduni wa kutembelea pia Hifadhi za taifa za Wanyama zilizojirani na maeneo yao ikiwemo Hifadhi pekee ya taifa ya Arusha ambayo iko mjini Kabisa .

Mhe Muro amewapongeza Wafanyakazi na Mhifadhi Mkuu wa Arusha National Parks Kwa uamuzi wao wa kuhamasisha utalii wa ndani Kwa kupunguza Ada ya viingilio pamoja na kufanya maandalizi ya kutoa Usafiri maalum utakaobeba wananchi na kuwapeleka kwenye hifadhi ili kutoa nafasi Kwa wananchi wengi zaidi kutembelea hifadhi ya Wanyama Arusha  
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro akizindua  kampeni ya kuhamasisha utalii wa Ndani kwa kuwataka wananchi kutenga muda wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini 
  Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro akizungumza na baadhi ya Wananchi wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha utalii wa Ndani kwa kuwataka wananchi kutenga muda wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini
  Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro akiwa na furaha tele baada ya kuzindua kampeni ya kuhamasisha utalii wa Ndani kwa kuwataka wananchi kutenga muda wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

MICHUZI TV; Shilole afunguka kwa Mhe. Rais Magufuli, aitaka Igunga.!

TAZAMA LIVE RAIS MAGUFULI AKIWEKA JIWE LA MSINGI UPANUZI WA BARABARA YA KIMARA-KIBAHA

BancABC yadhamini mkutano wa chama cha Wanawake wafanyabiashara Tanzania (Tanzania Women Chamber of Commerce – TWCC)

$
0
0
BancABC Tanzania ambayo ni kampuni tanzu ya Atlas Mara na ambao imeorodhesha kwenye soko la hisa la London, mwishoni mwa wiki ilidhamini mkutano wa kila mwezi wa chama cha wanawake wafanyabiashara Tanzania (Tanzania Women Chamber of Commerce TWCC) mkutano ambao uliwaleta pamoja wanachama zaidi ya 250 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kuzungumzia maendeleo yao na changamoto ambazo wanakubana nazo.

Akiongea wakati wa mkutano huo, Mkurugenzi wa Kitengo cha Digitali BancABC Tanzania Silas Matoi alisema kuwa benki ya BancABC inatambua ni umuhimu wa wanawake kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi na ndio sababu benki yake imeweka mikakati ya kuendelea kuwawezesha na kufikia hatua ya leo ya kuungana na Chama cha Wanawake wafanyabiashara Tanzania (TWCC) kwenye mkutano wake huu wa kila mwezi.

Matoi alisema kuwa kwenye mkutano huo BancABC imeweza kutambua kuwa wanachama wa TWCC huwa wanashiriki maonyesho mengi nchini China akitolea mfano kuwa kwa mwezi wa Oktoba na Aprili mwaka huu, wanachama 150 walishiriki baadhi ya maonyesho ya biashara nchini China. Hata hivyo, Malai alisema kuwa wakati wa safari zao nchi China wananchama hao wamekuwa wakikubana na changamoto kadhaa na hasa linapokuja suala ya kubadilisha fedha na hasa inapotokea dharura.

Ninayo furaha kuwafahamisha ya kuwa BancABC Tanzania inayo suluhiso ya jinsi ya kupata fedha za kigeni mnapokuwa safarani China. Tunayo kadi ya malipo ya kabla – YUAN pre-paid Visa card, ambayo itawawezesha kufanya malipo kwa kwa fedha za China. 

Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa benki ya BancABC Tanzania Upendo Nkini akizungumza na wanachama wa chama hicho wakati wa mkutano wa chama hicho ambao uliwaleta pamoja wanachama zaidi ya 250 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kuzungumzia jinsi ya kufanya biashara na changamoto wanazokutana nazo. Mkutano huo ulifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na kudhaminiwa na benki ya BancABC Tanzania. 
Mkuu wa Kitengo cha Digitali BancABC Tanzania Silas Matoi akiwazilisha mada wakati wa mkutano wa chama cha Wanawake wafanyabiashara Tanzania (Tanzania Women Chamber of Commerce) ambao uliwaleta pamoja wanachama zaidi ya 250 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kuzungumzia jinsi ya kufanya biashara na changamoto wanazokutana nazo. Mkutano huo ulifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na kudhaminiwa na benki ya BancABC Tanzania. 

Wafanyakazi wa benki ya BancABC wakimsikiliza kwa makini mmoja wa mwanachama wa chama cha Wanawake wafanyabiashara Tanzania (Tanzania Women Chamber of Commerce) Anna Simbeye wakati wa mkutano wa chama hicho ambao uliwaleta pamoja wanachama zaidi ya 250 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kuzungumzia jinsi ya kufanya biashara na changamoto wanazokutana nazo. Mkutano huo ulifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na kudhaminiwa na benki ya BancABC Tanzania.
 

Mkuu wa Kitengo cha Digitali BancABC Tanzania Silas Matoi akiwazilisha mada wakati wa mkutano wa chama cha Wanawake wafanyabiashara Tanzania (Tanzania Women Chamber of Commerce) ambao uliwaleta pamoja wanachama zaidi ya 250 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kuzungumzia jinsi ya kufanya biashara na changamoto wanazokutana nazo. Mkutano huo ulifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na kudhaminiwa na benki ya BancABC Tanzania. 

WAKULIMA WA PAMBA IGUNGA WAAGIZWA KUONDOA VICHAKA VINAVYOKARIBISHA PANYA MASHAMBANI

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT
WAKULIMA wa Pamba wilayani Igunga wameagizwa kuhakikisha wanasafisha na kuondoa vichaka na magugu yaliyopo kando kando mwa mashamba yao ili kuhakikisha panya na wadudu waharibifu hawageuzi maeneo hayo kuwa maficho na kuingia mashambani kwa ajili ya kula mbegu zilizopandwa.

Kauli hiyo imetolewa jana wilayani Igunga na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati akiwa katika ziara yake ya kuelimisha na kuhamasisha wakulima wa zao la pamba kuzingatia kanuni 10 za kilimo cha zao hilo baada ya baadhi ya wakulima kudai uwepo wa panya wanaoshambulia mbegu za pamba walizopanda.

Alisema wadudu na panya ambao wameanza kuingia katika mashamba ya wakulima na kushambulia mbegu ambazo  wamepanda wanatokea katika vichaka vichaka vilivyoachwa kando kando ya mashamba hayo. Mwanri alisema wakati juhudi za kuwasiliana Wizara ya Kilimo ili kupata dawa ya kuwaangamiza panya na wadudu hao wanaoshambulia mbegu zilizopandwa ni vema wakulima wakahakikisha mashamba yao ni masafi.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akitoa elimu ya kanuni 10 za kilimo bora cha pamba jana katika Kijiji cha Kitangile wilayani Igunga. Kijiji hicho ndio mara ya kwanza kinaanza kulima zao hilo.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akitoa elimu ya kanuni 10 za kilimo bora cha pamba na umuhimu wa kung'oa maotea ya msimu uliopita jana katika Kijiji cha Mwabakima  wilayani Igunga. 
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akionyesha baadhi ya maotea yaliyokutwa katika shamba la mmoja wa wakulima wakati akitoa maelezo juu ya kuzingatia kanuni 10 za kilimo cha zao hilo jana katika Kijiji cha Mbutu wilayani Igunga.
.Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Choma cha Nkola wilayani Igunga wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Tabora (hayupo katika picha ) wakati akitoa maelezo juu ya kuzingatia kanuni 10 za kilimo cha zao hilo jana  wilayani Igunga ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha kilimo cha pamba.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

JESHI LA MAGEREZA LAZINDUA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO (2019-2023) DHIDI YA HIV/AIDS NA TB

$
0
0
Kamishna wa Huduma za Urekebishaji wa Jeshi la Magereza Augustine Mboje,ambaye alimuwakilisha Kamishna Jenerali wa Magereza (wa tatu toka kulia) akikata utepe kuzindua Mpango Mkakati wa miaka mitano dhidi ya HIV,AIDS na TB.
Kamishna wa Huduma za Urekebishaji wa Jeshi la Magereza Augustine Mboje,ambaye alimuwakilisha Kamishna Jenerali wa Magereza, akifungua kikao cha Mpango Mkakati wa miaka mitano dhidi ya HIV,AIDS na TB kwenye ukumbi wa kivukoni katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam tarehe 18 December 2018. Aliyekaa ni Kamishna wa Mafunzo Zanzibar, Ally Abdala.
Kamishna wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar, Ally Abdala akichangia mada kwenye mjadala wa Mpango Mkakati wa miaka mitano dhidi ya HIV, AIDS na TB.
Daktari Fulgency Binagwa akitoa semina ya Mpango Mkakati wa miaka mitano dhidi ya HIV,AIDS na TB kwenye ukumbi wa kivukoni katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Afisa Mradi Kitaifa wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayopambana dhidi ya madawa ya kulevya na uhalifu Bi. Immaculate Nyoni akimshukuru  Kamishna wa Huduma za Urekebishaji wa Jeshi la Magereza Augustine Mboje kwa kuzindua Mpango Mkakati dhidi ya HIV,AIDS na TB.
 Kamishna wa Huduma za Urekebishaji wa Jeshi la Magereza Augustine Mboje (wa tatu toka kushoto,walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau waliowezesha kukamilika kwa Mpango Mkakati wa miaka mitano dhidi ya HIV,AIDS na TB katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Picha zote na Jeshi la Magereza

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Naibu Waziri wa Nishati aendelea kuwasha umeme vijijini mkoani Ruvuma

$
0
0
Na Teresia Mhagama, Ruvuma
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, ameendelea na ziara  ya ukaguzi wa miradi ya umeme mkoani Ruvuma ambapo leo amewasha umeme Kijiji cha Palangu na Mang’ua pamoja mtaa wa Luhila Seko katika Wilaya ya Songea ambavyo vimepata umeme kupitia mradi wa usambazaji umeme vijijini wa Awamu ya Tatu (REA III) mzunguko wa kwanza na mradi wa Makambako – Songea.

Huo ni muendelezo wa kazi ya ukaguzi na uzinduzi wa miradi ya umeme vijijini mkoani Ruvuma aliyoianza tarehe 17 Disemba, 2018 kwa kuwasha umeme katika Vijiji Saba vilivyopo katika Wilaya ya Tunduru na Namtumbo ambapo wateja zaidi ya 200 wameunganishwa na huduma ya umeme.

Aidha, kuunganishwa kwa umeme katika Vijiji Palangu, Mang’ua pamoja na Mtaa wa Luhila Seko, wilayani Songea kumewezesha wateja zaidi ya 230 kuunganishwa na huduma hiyo huku wengine wakitumia umeme huo kwa shughuli za kiuchumi kama kusaga na kukoboa nafaka.

Pamoja na kuwasha umeme katika Vijiji hivyo, Naibu Waziri alikagua kazi ya usambazaji umeme katika Vijiji vya Liula, Mpangula na Litapwasi na kumsisitiza mkandarasi, kampuni ya Namis kufanya kazi kwa kasi na umakini ili kuondoa malalamiko ya wananchi ya kucheleweshewa huduma ya umeme.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwasha rasmi umeme katika Kijiji cha Palangu wilayani Songea, mkoani Ruvuma. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Songea, Pololiti Mgema.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu ( wa pili kulia) akiwasha rasmi umeme katika Kijiji cha Mang’ua wilayani Songea, mkoani Ruvuma. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Songea, Pololiti Mgema.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (wa tatu kulia) akiangalia kazi ya ukoboaji na usagaji wa nafaka katika Kijiji cha Mang’ua wilayani Songea, mkoani Ruvuma baada ya  kijiji hicho kupata umeme. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Songea, Pololiti Mgema.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (wa pili kulia) akikagua mitambo ya umeme katika kituo cha kupoza umeme cha Songea ambacho kimejengwa kupitia mradi wa umeme wa Makambako-Songea na kimeanza kusambaza umeme wa gridi kuanzia mwezi wa Tisa mwaka huu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Watanzania waaswa kuwa wamoja

$
0
0
Watanzania wametakiwa kuwa wamoja na kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli kwa kumuombea  dua  katika kipindi hiki ambacho nchi inapitia kipindi cha mabadiliko makubwa ya kiuchumi huku Serikali ikikataa kupokea misaada yenye masharti ya kudhalilisha mila na desturi za Watanzania.

Hayo  yamesemwa  na  Naibu  Waziri  wa  Mambo  ya  Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad  Masauni,  wakati akimuwakilisha Rais  Dkt. John  Magufuli katika  Dua  Maalumu ya Kumuombea  Rais Magufuli na Kuombea Amani Uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa, iliyoandaliwa  na  Taasisi  ya Kidini ya Maridhiano  Tanzania, katika Ukumbi wa Mikutano wa Sabasaba,jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa maombi hayo Naibu Waziri Masauni alisema nchi sasa inapitia kipindi cha mabadiliko makubwa ya kiuchumi yanayosimamiwa na Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli lengo ikiwa ni kuifanya Tanzania isiwe tegemezi na kupewa masharti yanayodhalilisha mila, tamaduni na dini zetu.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati wa Dua Maalumu ya Kumuombea Rais kwa kutimiza Miaka mitatu madarakani na Kuombea Uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa.Kulia ni Askofu Silvestre Gamanywa na Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania iliyoandaa maombi hayo, Asha Kassim.Maombi hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Sabasaba, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Sheikh Nurdin Mangochi akizungumza wakati wa Dua Maalumu ya Kumuombea Rais kwa kutimiza Miaka mitatu madarakani na Kuombea Uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa..Maombi hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Sabasaba, jijini Dar es Salaam.
 Askofu Silvestre Gamanywa akizungumza wakati wa Dua Maalumu ya Kumuombea Rais kwa kutimiza Miaka mitatu madarakani na Kuombea Uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa.Maombi hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Sabasaba, jijini Dar es Salaam.
Viongozi wa dini wakiwa katika Dua Maalumu ya Kumuombea Rais kwa kutimiza Miaka mitatu madarakani na Kuombea Uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa. Maombi hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Sabasaba, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

NMB YAITOA MABATI 229 KUPIGA TAFU UJENZI WODI YA WAKINA MAMA HOSPITALI YA WILAYA YA MUHEZA

$
0
0
BENKI ya NMB nchini imetoa mabati 229 kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya wakima mama katika hospitali ya wilaya ya Muheza ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt John Magufuli kuhakikisha wananchi wanaondokana na changamoto za afya kwenye maeneo yao.

Hafla ya makabidhiano hayo yalifanyika mjini Muheza na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo akiwemo Katibu wa UWT Mkoani Tanga Sophia Nkupe na Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo.

Akizungumza baada ya kupokea mabati hayo Katibu wa UWT huyo aliishukuru na kuwapongeza benki ya NMB kwa kuwakubalia ombi lao la kuwasaidia mabati kwa sababu wamekuiwa mstari wa mbele kusaidia lakini wanafanya hivyo kuunga mkono juhudui za Rais katika dhamirta yake ya kuhakikisha huduma za afya zinakuwa bora,.

Nkupe alisema pia wana mpongeza Rais Dkt John Magufuli kwa juhudi kubwa anazofanya kuhakikisha wananchi wanaondokana na changamoto mbalimbali ikiwemo za huduma ya afya na nyenginevyo

“Lakini pia nikushukuru Mh DC Mhandisi Mwanasha Tumbo kwa juhudi zako unazozifanya kuhakikisha wilaya ya Muheza inapata maendeleo makubwa pia niwaombe NMB mtusaidie wakina mama kwa sababu tunateseka sana wanachombezwa na taasisi mbalimbali za mikopo yenye riba kubwa”Alisema Katibu huyo wa UWT.
  Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel kushoto akimkabidhi mabati 229 Katibu wa UWT Mkoani Tanga Sophia Nkupe kwa ajili ya ujenzi wa wodi wakina mama hospitali ya wilaya ya Muheza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo
 Katibu wa UWT Mkoani Tanga Sophia Nkupe kulia akimkabidhi 229 Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo mabati 229 kwa ajili ya ujenzi wa wodi wakina mama hospitali ya wilaya ya Muheza kushoto ni Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel
 Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akimkabidhi mabati 229 Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza kwa ajili ya ujenzi wa wodi wakina mama hospitali ya wilaya ya Muheza kushoto ni Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Cosmas Gabriel
  Katibu wa UWT Mkoani Tanga Sophia Nkupe akizungumza katika halfa hiyo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo

BATA WAPEWE THAMANI KAMA JAMII ZINGINE ZA NDEGE ILI KULETA UFUGAJI WENYE TIJA

$
0
0
Na Khadija Seif, Globu ya Jamii

UMOJA wa wafugaji bata nchini wamekutana na kuzindua tamasha la uchomaji wa  nyama ya Bata  katika ukumbi wa police officers mess jijini Dar es salaam.

Akifungua hafla hiyo ya tamasha la uchomaji nyama ya bata Afisa mifugo wa jamii ya ndege Deodratus Nestory kutoka Manispaa ya Kinondoni  
 amewapongeza  wafugaji hao na kusema kuwa ni   nadra sana kukuta tamasha la uchomaji nyama ya bata kwani imeshazoeleka mbuzi choma na kuku choma.

Nestory amesema kuwa "Umoja huu upo kwa ajili ya  kutia watu hamasa ili waweze kutambua thamani ya nyama ya bata, na Manispaa ya Kinondoni itatoa semina kwa wafugaji wote wa mbuzi,ngombe, kuku na bata ili waweze kupata masoko kwa urahisi na  kuwapa ushirikiano kutoka Serikalini kuanzia Manispaa hadi Wizara husika ya Kilimo na ufugaji" amesema Nestory.

Pia Nestory amefafanua kuwa kufikia mwakani  watafungua chama cha wafugaji wa jamii ya ndege ambacho kitatambulika kisheria
Ili waweze kupata mkopo kutoka mabenki tofauti na kuwawezesha kupanua soko na ufugaji wenye tija.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyowakutanisha wafugaji wa Bata kutoka sehemu mbalimbali yakiwemo Kawe, Kibiti,Morogoro,kigamboni na Bunju  Mwenyekiti wa chama hicho Riziki osward amesema sasa ni wakati wa kumpa thamani bata pamoja na nyama ya bata kwani jamii bado haina mwamko katika Kula kwa wingi nyama hiyo.

Hata hivyo osward amefafanua zaidi kuwa lengo la tamasha hilo sio tu Kula nyama peke yake bali hata kujifunza  namna bora ya kufuga bata hao hasa katika kuanzia malisho ,madawa na chakula.

Pia ameeleza kuwa mikakati ya Umoja wa wafugaji bata itahakikisha inatoa elimu kwa wafugaji na kuwasaidia ili kuweza kupanua soko na kumpa thamani bata kwani bado kuna desturi iliyojengeka juu ya bata kuwa ni mchafu japo bata ana thamani kubwa kuliko kuku .

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI PWANI CHAKUSANYA MIL. 228.4 ZA MADENI

$
0
0


NA MWAMVUA MWINYI, PWANI 

JESHI la polisi mkoani Pwani, kupitia kikosi cha usalama barabarani limekusanya kiasi cha sh. milioni 228.440 za madeni ya makosa ya usalama barabarani .

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, kamanda wa polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa alisema ,fedha hiyo imepatikana kutokana na madereva waliofanya makosa kipindi cha nyuma kutakiwa kufanya hivyo . 

Alieleza, kwa muda mrefu kumekuwepo na tabia kwa madereva wanaofanya makosa na kuandikiwa kulipa tozo la serikali kwa njia ya POSS mashine kushindwa kufanya hivyo kwa dhana ya kuwa hawataweza kubainika kwa kuwa mfumo mpya wa ulipaji wa tozo humtaka dereva husika kwenda kulipia yeye ndani ya siku saba. 

Wankyo aliwataka, madereva ambao wanatambua kuwa wanadaiwa kulipa mara moja kwani hatutakuwa na muhali nao pindi watakapowakamata.Kamanda huyo alifafanua ,wanaendelea kupambama na mabasi yanayosafiri kupitia barabara za mkoa wa Pwani kwa kuyakagua na kuona kama yana ubora wa kufanya usafirishaji wa abiria. "Kudhibiti ujazaji ndani ya mabasi kwa kuweka abiria kwenye vigodoro, uzidishaji wa nauli kwa abiria kwa kushirikiana na SUMATRA, malori na kuyafanyia ukaguzi wa kina katika maeneo yao ya maegesho na yanapopita kwenye barabara zetu "alisisitiza. 

Wankyo alisema ,watadhibiti usafiri wa magari madogo aina ya Noah yanayobeba abiria kwa kushirikiana na SUMATRA yasizidishe abiria na yasiende umbali wa kilometa zaidi ya 50#.Pamoja na hayo wana mikakati waliyojiwekea kuendelea pia kutoa elimu kwa madereva wa pikipiki katika wilaya zote wapatao 444.

Alielezea, lengo kuu likiwa ni kuhakikisha wanapunguza ajali kwa waendesha pikipiki ambao wengi wao wamekuwa hawakidhi vigezo vya kuendesha vyombo vya moto, kutojua sheria na kanuni za usalama barabarani na udereva wa kujihami.

WIZARA YA ARDHI YASHIRIKI KUPAMBANA NA VVU/UKIMWI

$
0
0

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mathias Kabundunguru amewaongoza watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika Upimaji hiari wa Virusi Vya UKIMWI (VVU) na UKIMWI na magonjwa mengine wakati wa Mafunzo maalum ya Afya katika mahali pa kazi, yaliyofanywa na Timu ya Wataalam wa Afya kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ofisi za Wizara ya Ardhi – Dodoma.

Magonjwa mengine yaliyofanyiwa upimaji ni pamoja na Kisukari, Shinikizo la damu (Pressure) na Uwiano wa Urefu na Uzito (Body Mass Index /BMI).

Akiongea na Watumishi wa Wizara katika Mafunzo hayo. Bwn. Kabundunguru alisema; “ Mafunzo ya Afya kwa Watumishi ni muhimu na yanalenga kuwapa uelewa zaidi na kuwawezesha Watumishi kupima Afya, kutambua hali za Afya zenu mapema na kuwawezesha kuishi kulingana na hali ya afya zenu huku mkiendelea kutoa huduma katika Utumishi wa Umma”.

Naye Afisa mwitikio wa Taasisi za umma (Public institutions response officer, Dkt. Hafidh Ameir kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS); Pamoja na mambo mengine, alieleza kuwa dhumuni Kuu pia la Mafunzo ni kuwaarifu watumishi wa umma kuhusu umuhimu wa kuchukua tahadhari ya magonjwa husika, hususani VVU na UKIMWI. Alisema; “ Watumishi wa umma wanasisitizwa kutambua kwamba mbali ya kuwa suala la afya dhaifu huathiri uwezo wao wa kufanya kazi kwa ufanisi, pia linawaathiri wao binafsi, hivyo watumishi wenyewe wanawajibika pia kujali afya zao.
kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mathias Kabundunguru, akifuatiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Utawala; Gideon Malabeja na Afisa Utumishi Mwandamizi; Joyce Mlowe katika ufunguzi wa Mafunzo Maalum ya Afya mahali pa kazi yaliyotolewa na Timu ya Wataalam wa Afya kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ofisi za Wizara ya Ardhi – Dodoma. 
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mathias Kabundunguru akiwa kwenye zoezi la upimaji wa VVU/UKIMWI baada tu ya Mafunzo maalum ya Afya mahali pa kazi yaliyotolewa na Timu ya Wataalam wa Afya kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ofisi za Wizara ya Ardhi – Dodoma. 
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mathias Kabundunguru akiwa kwenye zoezi la upimaji wa Uwiano wa Urefu na Uzito (Body Mass Index /BMI) baada tu ya Mafunzo maalum ya Afya mahali pa kazi yaliyotolewa na Timu ya Wataalam wa Afya kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ofisi za Wizara ya Ardhi – Dodoma.

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUWA TAYARI KUFANYA KAZI MAHALI POPOTE NCHINI ILI KUWAHUDUMIA WANANCHI

$
0
0
Watumishi wa umma wametakiwa kuwa tayari kufanya kazi mahali popote na katika mazingira yoyote nchini ili waweze kuwahudumia wananchi ambao ndio walengwa wakuu wa huduma zinazotolewa na Taasisi za Umma. 

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) alipokutana na watumishi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa lengo la kufahamu majukumu ya Idara hiyo na kuhimiza uwajibikaji.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema, kitendo cha watumishi wa umma kuwa tayari kufanya kazi mahali popote na katika mazingira yoyote bila kujali maslahi binafsi kinaashiria uzalendo kwa Taifa na kinatoa haki kwa wananchi katika maeneo yote hususan ya pembezoni kupata huduma bora wanayostahili.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa ameitaka Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma kutorubuniwa na baadhi ya watumishi na waajiri wanaoomba vibali vya uhamisho kwa maslahi binafsi hivyo kuathiri utoaji huduma kwa umma.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akisisitiza uwajibikaji kwa watumishi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (hawapo pichani) alipoitembelea idara hiyo kwa lengo la kufahamu majukumu ya idara na kuhimiza uwajibikaji. 
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na watumishi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora alipoitembelea idara hiyo kwa lengo la kufahamu majukumu ya idara na kuhimiza uwajibikaji. 
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Mathew Kirama (wa pili kutoka kulia) akifafanua majukumu ya Idara yake kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (kulia) alipoitembelea idara hiyo kwa lengo la kufahamu majukumu ya idara na kuhimiza uwajibikaji. 


KUAHIRISHWA KIKAO CHA BARAZA LA VYAMA VYA SIASA KILICHOPANGWA KUFANYIKA DESEMBA 22, 2018 ZANZIBAR

$
0
0

Natumia fursa hii kuwafahamisha wajumbe wote wa Baraza la Vyama vya Siasa kuwa, nimepokea taarifa rasmi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa, tarehe 20 Disemba, 2018 kutakuwa na zoezi la uteuzi wa wagombea Katika Jimbo la Temeke Dar-es Salaam na Kata 48 zilizopo katika maeneo ya Wilaya mbalimbali za Tanzania Bara.

Kimsingi, matukio yote mawili, uteuzi wa wagombea wa ubunge na udiwani uliopangwa kufanyika tarehe 20 Disemba, 2018 na kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa kilichopangwa kufanyika tarehe 21 na 22 Disemba, 2018 ni muhimu na hayo yote yanahusisha wadau walewale. Tofauti ni kuwa, ni rahisi kuahirisha kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa kuliko kuahirisha siku ya uteuzi wa wagombea.

Hivyo, Kwa mujibu wa Kanuni ya 16(4) ya Kanuni za Baraza la Vyama vya Siasa, nimeshauriana na wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Baraza la Vyama vya Siasa na tumeamua kuahirisha kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa mpaka baada ya uchaguzi mdogo wa tarehe 19 Januari, 2018, ili kuwezesha Vyama vya Siasa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mdogo wa tarehe 19 Januari, 2018.

Tunaomba samahani kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

TAASISI YA MOYO YA JAKAYA YAFANYA UPASUAJI KWA ZAIDI YA WATOTO 1000

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii

TAASISI ya moyo ya Jakaya Kikwete imefanikisha kufanya upasuaji kwa zaidi ya watoto 1000 ikiwa ni upasuaji mkubwa kwa watoto 600 na upasuaji mdogo kwa zaidi ya watoto 400. Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mbio za Heart Marathon kwa mwaka 2019 Rais wa Tanzania Health Summit (THL) Dkt. Omary Chillo amesema kuwa mbio hizo zitafika kilele Aprili 28, 2019 katika viwanja vya Coco Beach ikiwa ni mara ya nne tangu kuanzishwa kwake na kusema kuwa malengo ya kuendesha mbio hizo ni kusaidia juhudi za serikali za kupunguza magonjwa yasio ya kuambukiza kwa kupitia michezo na kuchangia fedha kwa ajili ya watoto wanaohitaji upasuaji katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)

Aidha amesema kuwa zawadi zitakazotolewa ni pamoja na fedha taslimu zenye jumla ya thamani ya zaidi ya shilingi milioni 16 kwa wakimbiaji watakaokimbia mbio za kilomita 21, kilomita 5 na mita 700 kwa watoto na ameziomba taasisi mbalimbali nchini kuchangia na kushiriki katika mbio hizo kupitia tovuti yao ya www.heartmarathon.com ili kuweza kuokoa maisha ya watoto na wananchi kutoka katika janga la magonjwa yasiyoambukizwa.

Kwa upande wake Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete Dkt. Naiz Majani amesema kuwa wanaungana na taasisi ya Tanzania Health Summit katika mbio hizo ili kuweza kuwachangia watoto wenye matatizo ya moyo kuweza kupata matibabu.

Dkt. Majani amesema kuwa kuanzia mwaka 2015 matibabu ya moyo yalianza kufanyika hapa nchini na hasa katika masuala ya upasuaji na hadi kufikia sasa jumla ya watoto 1040 wamepata matibabu ambapo watoto 600wamefanyiwa upasuaji mkubwa na zaidi ya watoto 400 wamefanyiwa upasuaji mdogo.

Pia amesema kuwa serikali imejipanga katika kuhakikisha matibabu yanatolewa nchini na hadi sasa wameshapatiwa wodi maalumu kwa ajili ya matibabu ya watoto pekee.Pia mmoja wadhamini hao kutoka Nexlaw Advocate, Wakili Upendo Mmbaga amesema kuwa ni mara ya pili wanadhamini mbio hizo ikiwa ni moja ya majukumu yao ya kusaidia huduma za afya hasa kuhusiana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Aidha amewapongeza THS kwa kutoa hamasa kwa jamii na amezishauri taasisi na mashirika mbalimbali kushiriki katika kuelimisha umma kuhusiana na magonjwa hayo na wao kama Nexlaw Advocate wametoa jumla ya shilingi milioni 7 ili kuweza kufanikisha mbio hizo.


Rais wa Taasisi ya Tanzania Health Summit (THS) Dkt. Omary Chillo akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na msimu wa mbio za Heart Marathon kwa mwaka 2019 na kueleza kuwa tangu kuanza kwake 2016 zaidi ya watu 3000 wamekimbia na watu 1000 wamefanyiwa vipimo vya magonjwa yasiyoambukizwa, leo jijini Dar es Salaam.



Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Dkt. Naiz Majani akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mbio za Heart Marathon na namna taasisi hiyo ilivyofanikiwa na kufanya upasuaji kwa watoto zaidi 1000, leo jijini Dar es salaam


Upendo Mmbaga (kulia) akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 7 Rais wa taasisi ya Tanzania Health Summit (THS) Dkt. Omary Chillo na kuhaidi kuendelea kushirikiana nao ili kufanikisha azma ya uelewa wa magonjwa yasiyo ya kuambukizwa kwa jamii na kuongeza nguvu katika juhudi za serikali za kukabiliana na magonjwa hayo, leo jijini Dar es salaam.(Picha na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii)


NAIBU WAZIRI OMARY MGUMBA AFANYA KIKAO NA WATUMISHI WA TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI DAR

$
0
0
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe.Omary Mgumba, Amefanya Kikao na watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Mapema leo Jijini Dar es Salaam akiwa safarini kikazi kuelekea Mkoani Ruvuma.
 
Naibu Waziri Mgumba amewasitiza watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kufanya kazi kwa bidii, ushirikiano na ueledi ili kutimiza dhima ya Serikali ya awamu ya Tano ili kuleta maendeleo katika uzalishaji wa chakula kupitia kilimo cha Uhakika cha Umwagiliaji kuelekea Tanzania ya viwanda.
 Picha ya Pamoja Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Mhe. Omary Mgumba akiwa na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Tume ya Taifa ya Umwagiaji katika Ofisi za Wizara ya Kilimo Jijini dar es Salaam.
Katika Picha Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Mhe. Omary Mgumba akiongea na watumishi wa Tume ya Taifa ya umwagiliaji (hawapo pichani) katika Ofisi za Wizara hiyo Jijiini Dar es Salaam, kushoto ni Bi Aida Tesha Afisa Utawala Mkuu wa Tume hiyo.
 Katika Picha ni baadhi ya watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba.
 Baadhi ya watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakimsikiliza Naibu Waziri wa Kilimo Mhe . Omary Mgumba.

RC Wangabo atoa tahadhari ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Kalambo

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa tahadhari kwa uongozi wa wilaya ya Kalambo juu ya matumizi na ubora wa hospitali inayotarajiwa kujengwa katika wilaya hiyo ili kusijirudie makosa yaliyofanyika wakati wa ujenzi wa vituo vya afya vinavyoendelea ikiwemo kuchelewesha malipo kwa mfundi pamoja na kuachana na mafundi wasumbufu wanaochelewesha ujenzi.

Akitolea mfano wa ujenzi wa kituo cha afya cha Legeza Mwendo kilichopewa Shilingi milioni 700 na hatimae kufanikiwa kujenga majengo tisa, hivyo kumtaka Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kwa usimamizi wa mkuu wa Wilaya hiyo kuhakikisha wanazitumia vyema Shilingi bilioni 1.85, fedha ambazo zimetengwa na serikali kwaajili ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya.

“Utoaji wa fedha ofisi yako Mkurugenzi mmekuwa mnasuasua, malipo mnasingizia sijui mifumo mifumo, watu hawalipwi kule (kituo cha afya) Mwimbi imekuwa tabu karibu mwaka mzima, hata kule (kituo cha Afya) Legeza mwendo ilikuwa hivyo hivyo, nisingependa hili litokee, malipo lazima yaende vizuri, hata wale mama lishe walikuwa wanadai hawalipwi,” Alisisitiza.

Alisema kuwa kutokana na fedha hiyo iliyotengwa angependa kuona majengo mazuri yenye viwango ili kuupendezesha mji wa Matai ambao ni makao makuu ya wilaya hiyo.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WAKAZI WA KATA YA TUMBI WALALAMIKIA KERO YA UBOVU WA BARABARA ZA NDANI

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA 

WAKAZI wa kata ya Tumbi, Kibaha Mjini mkoani Pwani ,wamelalamikia kero ya ubovu wa miundombinu ya barabara kutoka Royal hospital hadi Mwanalugali na CCM Mkoa kuelekea shule ya Wipaz. 

Aidha, barabara ya kuelekea shule ya msingi Mwanalugali imekuwa mbovu hali inayosababisha wanafunzi kupata shida wakiwa wanakwenda shule. 
Akielezea juu ya changamoto ya baadhi ya barabara za ndani kuwa mbovu ,wakati wa muendelezo wa ziara ya jimbo inayofanywa na mbunge wa jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka ,diwani wa kata ya Tumbi Hemed Chanyika alisema ufanyike uboreshaji wa barabara hizo ili kuondoa usumbufu kwa wananchi. 

Akizungumzia suala la usafiri ,Chanyika alisema, walishafanya utaratibu wa kusogeza huduma hiyo ambapo kuna mabasi yanayofanya safari Mbezi -Mwanalugali lakini imejitokeza tatizo mabasi hayo kushindwa kuendelea na huduma hiyo hatua ambayo inawapa shida wakazi hao. 

Mkazi Hamis, Monika Mnyambirwa, Issa Gwaja, Shomari Gwaji walieleza, barabara hizo zinahitaji kuchongwa, mitaro ,madaraja ,kuwekwa matuta na makalavati.Akijibu juu ya kero hiyo, Koka aliitaka TARURA ihakikishe inakwenda kutatua kero hizo. 

Alielezea kwa mujibu wa TARURA barabara ya Royal hospital -Mwanalugali ipo kwenye mpango na mkandarasi atashughulikia tatizo hilo. "Suala la usafiri, miundombinu ya barabara ni muhimu katika jamii, kwani uinua maendeleo ya eneo husika "alisema Koka. Hata hivyo, Koka alibainisha ataendelea kushirikiana,kusimamia na kuwatumikia wananchi wa Mji wa Kibaha ili kutatua kero zinazowakabili.

Viewing all 109973 articles
Browse latest View live




Latest Images