Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

TANZIA


SERIKALI YAIAGIZA BODI YA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI KUDHIBITI MAADILI YA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI

$
0
0
Na Josephine Majura, WFM, Dodoma


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Susana Mkapa, ameiagiza Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi nchini (PSPTB), kuhakikisha kuwa inadhibiti maadili ya wafanyakazi wa sekta ya ununuzi na ugavi ili fedha za serikali zinazotumika kwenye ununuzi ziwe na tija kwa wananchi.

Bi. Mkapa ametoa maagizo hayo Jijini Dodoma, katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Naibu Katibu Mkuu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mipango wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Richard Mkumbo, wakati akifunga kongamano la tisa la wataalam wa ununuzi na ugavi kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara.

Bw. Mkumbo amebainisha kuwa licha ya vitengo vya matumizi mabaya ya fedha za umma kupitia sekta ya ununuzi na ugavi, ikiwemo rushwa kuendelea kupungua, Bodi inatakiwa kuhakikisha kuwa vitendo vya rushwa vinadhibitiwa ipasavyo.
Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mipango wa Wizara hiyo, Bw. Richard Mkumbo, akifunga Kongamano la Tisa la Bodi ya Wataalam wa ununuzi na ugavi (PSPTB), kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Susana Benard Mkapa, ukumbi wa DCC, Dodoma.
Baadhi ya Washiriki wa Kongamano la Tisa la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPSTB), wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa hafla ya kufunga kongamano hilo la siku tatu lililofanyika Jijini Dodoma na kuwashirikisha wataalam 650 kutoka Tanzania Bara.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi Sr. Dkt. Hellen Bandiho, akisoma hotuba ya ukaribisho kwa mgeni rasmi Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Richard Mkumbo (hayupo pichani), wakati wa hafla ya kufunga Kongamano la Tisa la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), iliyofanyika katika ukumbi wa DCC, Jijini Dodoma
Kamishana wa Idara ya Sera ya Ununuzi wa Umma wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Frederick Mwakibinga (kushoto), na mjumbe wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) Dr. Laurent Shirima, wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi, Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Richard Mkumbo, wakati akifunga kongamano la Tisa la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), katika ukumbi wa DCC, Jijini Dodoma.
Baadhi ya Washiriki wa Kongamano la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPSTB), wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi, Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Richard Mkumbo, wakati akifunga Kongamano la Tisa la Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), katika ukumbi wa DCC, Jijini Dodoma.

PSPTB Yapongezwa Kwa Kusimamia Maagizo ya Serikali

KWA MARA YA KWANZA TANZANIA YAPATA MADAKTARI BINGWA WA UPASUAJI UBONGO,MGONGO NA MISHIPA YA FAHAMU

MICHUZI TV: SHILOLE AFUNGUKA MAZITO CHID BENZ KUDHALILISHWA

MICHUZI TV: Mpenzi wa MONI CENTROZONE, NAI afunguka haya usiku wa WOLPER/

Hafla ya kuwapongeza Waalimu Kata ya Mecco Manispaa ya Ilemela yafana

$
0
0


Diwani Kata ya Mecco Manispaa ya Ilemela, Godlisten Kisanga (CCM) akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha pamoja na waalimu wote wa Shule tatu za Msingi (Nundu, Nundu D na Nyamwilekelwa) katika Kata hiyo iliyolenga kuwapongeza waalimu hao kwa juhudi zao za kuimarisha ufaulu kwa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba.
Afisa Elimu Kata ya Mecco Manispaa ya Ilemela, Mwl. Agnes Mugyabuso (kushoto), Shule zilizofanya vizuri kwa kila somo katika Kata hiyo kwenye mtihani wa darasa la Saba mwaka huu ambapo Shule hizo zilikabidhiwa cheti cha pongezi na Diwani wa Kata ya Mecco, Godlisten Kisanga.
Diwani Kata ya Mecco Manispaa ya Ilemela, Godlisten Kisanga (kulia), akimkabidhi Cheti cha pongezi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nyamwilekelwa, Mwl. Lyatura Mukama (kushoto) baada ya Shule yake kuibuka kidedea kwenye masomo ya Kiswahili na Kiingereza.
Diwani Kata ya Mecco Manispaa ya Ilemela, Godlisten Kisanga (kulia), akimkabidhi Cheti cha pongezi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nundu D, Mwl. Lucas Robert (kushoto) baada ya Shule yake kuibuka kidedea kwenye masomo ya Hisabati na Maarifa ya Jamii.
Utaratibu huu wa kushindanisha Shule za Msingi Kata ya Mecco umelenga kuongeza kiwango cha ufaulu kwa alama A na B tu.

MICHUZI TV: MSIKILIZE LAVA LAVA AKIFUNGUKA KUHUSU MAPENZI NA MUZIKI


NSFF YAJIPANGA KUPELEKA TAIFA KWENYE UCHUMI WA VIWANDA

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

SHIRIKA la taifa la hifadhi ya jamii (NSSF) limeshiriki katika maonesho ya tatu ya bidhaa za viwanda vya Tanzania yaliyozinduliwa rasmi leo katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es salaam kwa kutoa huduma kwa wajasiriamali ikiwa ni mchakato kwa kukamilisha azma ya ujenzi wa Tanzania ya viwanda.

Akizungumza na blogu ya jamii Afisa mwandamizi kitengo cha sekta isiyo rasmi  (NSSF) Abas Cothema amesema kuwa, wameungana na shirika la kuhudumia viwanda vidogo vidogo nchini (SIDO)  katika maonesho hayo ya bidhaa za viwanda zinazozalishwa nchini ikiwa ni  kuunga mkono  jitihada za Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Magufuli iliyodhamiria kujenga Tanzania ya viwanda.

Amesema kuwa NSSF imeshiriki maonesho hayo ili kuhakikisha wanawapatia hifadhi ya jamii wajasiriamali ili waweze kukingwa dhidi ya majanga yanayosababisha  upotevu wa kipato na kuwapa pensheni ya uzeeni, pensheni ya ulemavu, pensheni ya  urithi na bima ya afya ambazo vyote hivyo ni muhimu katika ujenzi wa Tanzania mpya ya viwanda.

Cothema amesema kuwa mwanachama akishiriki kwa kuchangia ada ya kima cha shilingi 20,000/= kwa muda wa miezi mitatu atapata bima yeye na wategemezi wake wanne yaani watoto wanne walio na umri chini ya miaka 18 na watoto wanaosoma walio chini ya miaka 21 pamoja na mtegemezi wake na malengo ya kufanya hivyo ni kumkinga mwanachama na majanga ya maradhi na magonjwa ili aweze kuendelea na shughuli za ujenzi wa uchumi ambao Serikali umejizatiti kuufikia pia kufanya hivyo ni kusaidia serikali katika kutoa huduma kwa wananchi wake.

Ameeleza kuwa NSSF wana miradi mbalimbali ya kiuchumi ambayo imelenga kuwasaidia wananchi wa hali zote ikiwa ni pamoja na  viwanja vilivyo katika maeneo ya kiluvya na visiga ambavyo hupatikana kwa gharama ambayo kila mwananchi anaweza kumudu hata kwa mkopo au kwa malipo ya muda mrefu.

Pia amesema kuwa wanashirikiana bega kwa bega na serikali na wadau mbalimbali katika kuhakikisha azma ya ujenzi wa Tanzania ya  viwanda na kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 inafikiwa.
Naibu wa Viwanda Biashara na Uwekezaji,Mhandisi Stella Manyanya aliyeambatana na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara,Edwin   Rutageruka, akisalimiana na mmoja wa afisa wakitego cha sekta isyo rasmi wa (NSSF) wakati alipotembelea Shirika la Taifa la hifadhi ya jamii (NSSF)  leo jijini Dar es Salaam katika  maonyesho Tatu ya Bidhaa za Viwanda.
Naibu Waziri wa Viwanda biashara na uwekezaji,Mhandisi Stella Manyanya (kushoto) akisisitiza jambo kwa,Abbas Cothema Ofisa Matekelezo kutoka Kitengo cha Hiari-NSSF alipotembelea banda la NSSF ndani ya maonyesho ya tatu ya bidhaa za wiwanda vya hapa nchini yaliyo funguliwa leo jijini Dar es Salaam.
Ofisa Matekelezo kutoka Kitengo cha Hiari-NSSF    Abbas Cothema akizungumza na Michuzi blog  katika maonyesho ya tatu ya bidhaa za wiwanda vya hapa nchini yaliyo funguliwa leo jijini Dar es Salaam.

Benki ya Azania Yazindua Rasmi Tawi lake Dodoma.

$
0
0
Benki ya Azania imezidi kujitanua baada ya hii leo kuzindua tawi lake jipya jijini Dodoma ikiwa ni muendelezo wa mkakati wa benki hiyo katika kukuza mtatandao wa matawi yake sambamba na kuunga mkono jitihada za Mh Rais John Magufuli kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda, kupitia huduma bora za kibenki.

Akizungumza kwenye hafla fupi ya Uzinduzi wa tawi hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Charles Itembe alisema kwa sasa benki hiyo ina matawi kumi na tisa ikiwemo tawi hilo jipya lililopewa jina la Sokoine- Dodoma ikiwa ni ishara ya benki hiyo kutambua mchango wa Waziri Mkuu wa zamani, Hayati Edward Moringe Sokoine katika ustawi wa taifa kwa ujumla.

“Malengo yetu ya kimkakati kwa sasa ni kukuza mtatandao wa matawi ya benki yetu , angalau matawi matatu kwa mwaka, na pia kukuza nafasi yetu ya umiliki wa soko( Market share) angalau kwa 3% ndani ya miaka mitatu.’’ Alisema Bw Itembe. Alisema nia ya benki hiyo ni kuwa katika hadhi ya Mabenki Makubwa daraja la kwanza( Tier One ) ndani ya miaka hii mitano ya kimkakati wa kibiashara.

Akizungumzia uamuzi wa kufungua tawi hilo jijini humo, Bw Itembe alisema: “Dodoma ni katikati ya nchi, pili ni makao makuu ya shughuli za kiserikali na pia ni mkoa unaokuwa kwa kasi kibiashara.’’ Aidha, alibainisha kuwa kupandishwa hadhi kwa manispaa ya Dodoma na kuwa jiji kumeiweka benki hiyo katika nafasi nzuri kwa kuwa ukuaji wa jiji hilo unaendana sambamba na mahitaji ya kifedha.

“Katika kuunga mkono sera ya Mh Rais John Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda, ni lazima kuwa na mbinu ya kuweza kukuza kipato kupitia kufanya biashara na benki zenye msingi imara… Azania Benki tupo tayari kushirikiana na wananchi na serikali katika kufanikisha hilo,’’ alisema.

Akizungumza muda mfupi kabla hajazindua rasmi tawi hilo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji mbali na kuipongeza menejimenti ya benki hiyo, alitoa changamoto kwa taasisi za fedha hapa nchini ikiwemo benki hiyo kuhakikisha zinajipanga kikamilifu kukabiliana na suala la mikopo chechefu sambamba na kupunguza gharama za uendeshaji ili ziweze kuwahudumia wateja wake kwa gharama za chini zaidi ikilinganishwa na hali ilivyo sasa.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi jipya la benki ya Azania linalofahamika kwa jina Sokoine-Dodoma wakati wa hafla fupi ya uzinduzi huoiliyofanyika jijini Dodoma leo. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Charles Itembe (kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo, Bw Eliud Sanga. 
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki ya Azania Bw Eliud Sanga (wa pili kushoto) akikabidhi zawadi maalum aliyoandaliwa iliyoandaliwa kwa ajili ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji (wa pili kulia) wakati wa hafla hiyo. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Charles Itembe (kulia). 
 Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Azania ,  Charles Itembe akizungumza kwenye hafla hiyo. 
 Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Azania wakifuatilia matukio mbalimbali ikiwemo hotuba ya Naibu Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji wakati wa hafla hiyo.

KATIBU MKUU KIONGOZI ATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA MJI WA SERIKALI IHUMWA DODOMA.

$
0
0


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi.Maimuna Tarishi akimuonesha Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi michoro ya ramani ya ujenzi wa Majengo ya Ofisi za Serikali Ihumwa wakati wa ziara yake eneo la Ihumwa Desemba 6, 2018.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi akiuliza jambo kuhusu ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mhandisi kutoka SUMAJKT, Zabron Mahenge wakati wa ziara yake eneo lililotengwa kwa ujenzi wa Ofisi za Serikali la Ihumwa Dodoma.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi akionesha jambo kwa Mhandisi kutoka TBA, Amon Nghamba wakati wa ziara yake katika eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ihumwa Dodoma .
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi akimsikiliza Msanifu Majengo Moses Wadelanga wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa ujenzi wa Majengo ya Ofisi za Serikali Ihumwa Dodoma.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi akimsikiliza Msanifu Majengo Moses Wadelanga akifafanua jambo juu ya ujenzi wa Majengo ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika eneo la Ihumwa Jijin I Dodoma. 

MKUTANO KAZI BAINA YA WADAU WA MAENDELEO, MAAFISA WA SERIKALI NA WATENDAJI TASAF WAMALIZIKA KWA MAFANIKIO JIJINI DAR

$
0
0
Na Estom Sanga-DSM 

Mkutano wa Wadau wa Maendeleo ,Maafisa wa Serikali na Watendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF uliojadili kwa kina utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ambao unatekelezwa na Serikali kupitia TASAF umemalizika jijini Dar es Salaam. 

Mkutano huo ambao hufanyika kila baada ya miezi sita , umefanyika kufuatia ziara ya washiriki hao katika wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza na Unguja ambako walikutana na Walengwa wa Mpango huo na kujionea namna Walengwa wanavyoendelea kunufaika na huduma zinazotolewa na Mpango huo kuboresha maisha yao. 

Miongoni mwa mambo yaliyofanywa katika mkutano huo ni pamoja na kuweka mkakati wa utekelezaji wa awamu ya pili ya Mpangowa Kunusuru Kaya Maskini inayotarajiwa kuanza Mwezi Aprili hapo mwakani ambayo italenga zaidi katika kuwashirikisha Walengwa kufanyakazi za maendeleo kwenye maeneo yao na kisha kulipwa ujira. 

Akizungumza na Washiriki wa Mkutano huo Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF,Bw. Ladislaus Mwamanga ametoa wito maalumu kwa wadau na maafisa wa Mfuko huo kufanya kazi kwa bidii na kuweka mbele maslahi ya taifa ili lengo la serikali la kuwapunguzia kero ya umaskini wananchi liweze kufikiwa kwa ufanisi. 

Bwana Mwamanga amesema utekelezaji na mafanikio ya Mpango huo unategemea kwa kiwango kikubwa jitihada za pamoja hasa ikizingatiwa kuwa wananchi wanaolengwa ni wale ambao kwa kiwango kikubwa wamekuwa wakiishi katika hali ya umaskinina wengine kukata tamaa jambo ambalo amesema linapaswa kukabiliwa kwa nguvu za pamoja. 
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bw. Ladslaus Mwamanga (katikati) akiongoza mkutano wa Wadau wa Maendeleo, Maafisa wa Serikali na TASAF kwenye ukumbi wa Mfuko huo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa Wadau ,Serikali na TASAF wakiwa kwenye ukumbi wa Mikutano wa TASAF jijini DSM katika mkutano uliojadili utekelezaji wa Shughuli za Mfuko huo na maandalizi ya awamu ya pili ya Mpango huo inayotarajiwa kuanza hapo mwakani.
Mmoja wa Watumishi wa TASAF,Shadrack Mziray akiwasilisha taarifa kwenye Mkutano wa Wadau ,serikali na TASAF jijini Dar es salaam.
Picha ya juu na chini menejimenti ya TASAF na ile ya Benki ya Dunia hapa nchini wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa TASAF, Serikali Na Wadau wa Maendeleo baada kuhudhuria mkutano wao wa pamoja jijini Dar es salaam.

MFANYABIASHARA JIJINI ARUSHA HANSPAUL AHUKUMIWA KULIPA FAINI YA MILIONI 60 AU KWENDA JELA MIAKA 2

$
0
0

NA Vero Ignatus -ARUSHA

MFANYABIASHARA maarufu Jijini Arusha,Kamaljit Hanspaul (58), anayejishughulisha na shughuli mbalimbali na wenzake watatu wamehukumiwa kulipa faini ya Sh Milioni 60 au kwenda jela miaka miwili kila mmoja baada ya kukutwa na hatia ikiwemo kuajiri wafanyakazi watatu raia wa kigeni kufanya kazi nchini bila vibali.

Mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha,washitakiwa wengine ambao uraia uko kwenye mabano Vemula Shivakumar, (27), (India) Sathasivam Krishanth, (29) (India) na Ralph Leonard, (54), (Ujerumani),ambapo watuhumiwa wote wanne walikiri kutenda makosa hayo mwanzoni mwa wiki.

Akisoma hukumu hiyo jana,Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo,Niku Mwakatobe,alisema Mahakama hiyo imemtia hatiani Hanspaul katika mashitaka matatu ambayo ni kuajiri raia watatu wa kigeni ambao hawakuwa na vibali vya kufanya kazi nchini.

Alisema baada ya mshitakiwa huyo kukiri mashitaka hayo Mahakama inamtoza faini ya Sh Milioni 10 kila kosa au kifungo cha miaka miwili,huku washitakiwa wengine wakitozwa faini ya Sh Milioni 10 kila mmoja au kifungo cha miaka miwili baada ya kukutwa na hatia ya kufanya kazi nchini bila vibali.

Washitakiwa wote wanne waliachiwa huru baada ya kulipa faini hiyo Sh Milioni 60,ambapo katika uamuzi wake,Hakimu Niku aliwataka raia hao iwapo wanataka kuendelea kufanya kazi hapa nchini,wafuate taratibu na sheria zilizowekwa.Katika shauri hilo jamhuri ilikuwa ikiwakilishwa na Wakili Khalili Nuda huku utetezi ukiwakilishwa na Wakili Salumi Mushi,ambaye aliiomba Mahakama ipunguze adhabu ikizingatiwa ni mara ya kwanza kwa washitakiwa hao kukutwa na hatia na kuwa washitakiwa watatu ambao ni raia wa kigeni walishaaanza taratibu za kufuatilia vibali vya kufanya kazi nchini.

Naye Wakili Nuda aliiomba Mahakama licha ya watuhumiwa wote kutokuwa na rekodi ya kukutwa na hatia,wanaomba Mahakama iwaadhibu kwa mujibu wa sheria na kuomba iwaagize iwapo wanataka kuendelea kufanya kazi hapa nchini wafuate sheria na taratibu.

Awali katika shauri hilo namba 389 la mwaka huu kabla ya kusomewa hukumu hiyo washitakiwa hao walisomewa maelezo ya awali,ambapo Wakili Nuda alidai mshitakiwa wa kwanza,aliwaajiri Shivakumar, Krishanth na Ralph kufanya kazi kama washauri kwenye kampuni yake ya HansPaul Automechs iliyopo maeneo ya Njiro jijini hapa wakati akijua hawana vibali vya kufanya kazi nchini.

Waziri Kairuki awataka TAWOMA kuchangamkia fursa ya uzalishaji chumvi nchini

WAUGUZI WANAOVUNJA MAADILI YA KAZI KUKIONA CHAMOTO

$
0
0

Na WAMJW - Nanyumbu, Mtwara

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu ametoa onyo Kali kwa Wauguzi wote kwenye vituo vya  kutolea huduma za afya nchini wanaovunja maadili na miiko ya kazi za uuguzi ikiwemo matumizi ya lugha chafu kwa wagonjwa na wanaowapiga akina mama wajawazito wakati wakijifungua.

Ameyasema hayo  wakati alipotembelea Hospitali ya Wilaya Nanyumbu, akiwa katika ziara yake Mkoani Mtwara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya na uhamasishaji kwa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na Bima ya Afya hasa katika msimu huu wa Biashara ya Korosho.

Waziri Ummy alisema kuwa Serikali kupitia Baraza la Uuguzi litawafutia usajili Muuguzi yeyote atakayegundulika ametenda kosa la kumpiga mama mjamzito au kumtolea lugha chafu wakati wa kujifungua.

"Tunataka kumjua huyo, ambae ni hodari sana wakupiga wanawake wajawazito, makofi wakati wakujifungua, kwa kweli huyo ni wa kumfukuza kazi, Mimi mkiniletea namfutia Leseni yake kabisa, hafanyi kazi Serikalini, hafanyi kazi Sekta Binafsi" alisema Waziri Ummy.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya wananchi wa Nanyumbu (hawapo kwenye picha), wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji wa huduma za Afya na uhamasishaji kwa wananchi kujiunga na Bima ya Afya Mkoa wa Mtwara.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akipitia ubao wa matangazo ya gharama za matibabu katika Hospitali ya Rufaa Nanyumbu, akiwa katika ziara yake ya kukagua hali ya utoaji wa huduma za Afya na uhamasishaji kwa wananchi kujiunga na Bima ya Afya Mkoa wa Mtwara.
Waziri wa Afy, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisoma cheti cha mtoto aliyefikishwa na baba yake Hospitali ya Wilaya Nanyumbu ili kupata huduma za Afya.
Wananchi wa Nanyumbu wakiongozwa na Wazee waliojitokeza kumsikiliza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu pindi alipokuwa katika ziara yake ya kukagua hali ya utoaji wa huduma za Afya na uhamasishaji kwa wananchi kujiunga na Bima ya Afya Mkoa wa Mtwara.


Takukuru: Wananchi toeni maarifa za maendeleo ya miradi

$
0
0

Wananchi wameombwa kutoa taarifa mapema kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa miradi ya maendeleo wanaoitilia shaka kugubikwa na ufisadi ili kuokoa matumizi mabaya ya fedha za umma. Akizungumza wakati wa kongamano la kujadili utatuzi wa changamoto ya maji, kuanzia ufuatiliaji wa rasilimali fedha na utekelezaji wake,  ufuatiliaji wa maji lililoandaliwa na asasi ya Pakacha Group na kufadhiliwa na The Foundation For Civil Society, Elly Makala, Mkuu wa dawati la Elimu kwa Umma  (Takukuru ) Wilaya ya Kinondoni amesema ikiwa wananchi watatoa taarifa mapema , itakuwa ni rahisi kuchukua hatua mapema.

“Tutaokoa fedha nyingi za serikali zilizotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, ikiwemo miradi ya maji, Barabara na ujenzi wa vituo vya afya,” amesema Makala. Amesema takukuru ina majukumu mbalimbali, ikiwemo kutoa elimu ya madhara ya rushwa katika maendeleo ya nchi na wananchi wake. Hivyo ameongeza ni wajibu wa wananchi kushirikiana na viongozi kuanzia ngazi ya kata katika dhana nzima ya maendeleo, ikiwemo kuhoji mapato na matumizi ya miradi iliyomo maeneo yao.

Ameipongeza Pakacha kwa elimu wanayoitoa kwa wananchi wa Manispaa ya Ubungo juu ya ufuatiliaji ya miradi ya maji na dhana nzima ya ushiriki na ushirikishwaji wa wananchi. Upatikanaji wa maji umekuwa na changamoto katika kata za Kwembe, Msigani na Kibamba, hivyo asasi ya Pakacha, kwa ufadhili wa The Foundation For Civil Society kulazimika kutoa elimu kwa wananchi juu ya ufuatiliaji na utunzaji wa vyanzo vya maji.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Japan yaadhimisha Siku ya Taifa

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Joseph Kakunda (Mb.) akihutubia kwenye maadhimisho ya siku ya Taifa la Japani ambapo katika hotuba yake ameipongeza Japan kwa kuendeleza ushirikiano na Tanzania katika sekta mbalimbali zinazo changia maendeleo ya nchi kama vile ujenzi wa miundombinu, Elimu na Afya. Aidha, Mhe. Kakunda ameihakikishia Japan kuwa Tanzania itaendelea kudumisha na kuimarisha ushirikiano pamoja na kuendeleza urafiki wa kidiplomasia kati ya Mataifa hayo mawili. Hafla hiyo imeudhuriwa na Mabalozi mbalimbali na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa yaliyopo nchini Tanzania. Maadhimisho hayo yamefanyika katika makazi ya Balozi Masaki, jijini Dar es Salaam 
Balozi wa Japan nchni naye akitoa hotuba kwenye maadhimisho ya siku ya Japan.
Balozi wa Japani akiwa katika picha ya pamoja na wageni waalikwa walio hudhuria maadhimisho hayo.

Manyanya : OSHA kazi yenu inaonekana kila sehemu

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa Wakala wa Afya wa Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) kazi yao inaonekana kila sehemu ya viwanda wanamuambia Usalama kwanza kwa kupata vifaa ni kisha kuingia. Manyanya  ameyasema hayo wakati alipotembelea banda la OSHA wakati alipotembelea banda la OSHA katika maonesho ya Tatu ya bidhaa za viwanda Tanzania yanayofanyika katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam amesema kuwa OSHA wamefikisha elimu kwa wenye viwanda na sehemu zingine juu ya usalama mahala pa kazi.

Amesema kuwa viwanda vyote alokopita wamejizatiti katika usalama wa wafanyakazi wao kwa kuwa na vitu vya usalama kuanzia nje hadi ndani katika mitambo. Aidha amesema kuwa OSHA waendelee na utoaji elimu kila siku katika kulinda Afya na madhara mengine katika sehemu za kazi.

Nae Afisa Habari wa OSHA Eliuter Mbilinyi amesema wamekuwa wakitoa elimu ya Afya katika sehemu mbalimbali katika kuhakikisha wafanyakazi wanakuwa salama. Amesema OSHA  lengo kubwa ni kuwalinda wafanyakazi katika vifo pamoja na madhara mengine yanayotokana na mitambo. Amesema Viwanda ni wadau muhimu ambao wanatakiwa kuzinagatia kanuni na viwango katika sehemu ya kazi pamoja na kufanyiwa usajili.
 Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya akizungumza katika banda la OSHA wakati alipotembelea maonesho ya Tatu ya bidhaa za viwanda Tanzania yanayofanyika katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
 Wananchi wakipata huduma katika banda la OSHA katika maonesho ya Tatu ya bidhaa za viwanda Tanzania yanayofanyika katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
 Mmoja wa mwananchi akipata huduma katika la Wakala wa Afya wa Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) wakati alipotembelea banda la OSHA katika maonesho ya Tatu ya  bidhaa za  viwanda Tanzania yanayofanyika katika viwanja vya da Sabasaba jijini Dar es Salaam. 
Afisa Habari wa mwaka Wakala wa Afya wa Usalama Mahala pa Kazi OSHA Eliuter Mbilinyi akizungumza na waandishi habari katika maonesho ya Tatu ya bidhaa za viwanda Tanzania yanayofanyika katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.

Taasisi ya Dk Mengi kutoa tuzo kwa walemavu

$
0
0
Taasisi ya Dr Reginald MENGI ya kusaidia watu Wenye ulemavu imeamua kutoa tuzo kwa Watu Wenye ulemavu ili kuihamasisha jamii kutambua kuwa  watu hao wana uwezo wa kufanya makubwa.
Akitangaza utoaji wa tuzo hizo za " I can", jijini Dar es salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Dr Reginald MENGI Persons with Disabilities, Bi. Shimimana Ntuyabaliwe amesema Tuzo za mafanikio katika maeneo saba tofauti zitatolewa kwa washiriki watakaoshinda baada ya kupitia mchakato wà uteuzi.
Amesema tuzo hizo zimewalenga watu wenye ulemavu waliofanikiwa kwenye nyanja za elimu, siasa, uongozi, ujasiriamali, Sanaa na burudani, michezo, na ujuzi wa kipekee na ametaja sifa za watu wanaostahili kuwania tuzo hizo.
Amesema washindi watatangazwa na kukabidhiwa tuzo hizo, na fedha taslimu tarehe 2 February mwakani wakati wa tafrija ya kila mwaka  ya chakula cha mchana kwa watu wenye ulemavu inayoandaliwa na Dr Reginald Mengi.
Amewataka watu wenye sifa watume mapendekezo yao kwenye Taasisi hiyo kwa njia za barua pepe (info@drmengifoundation.org) , whatsapp +255 692 141 979 na vituo vya ITV/Radio one, ambapo mwisho wa kupokea  mapendekezo hayo ni  January 18, 2019.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Dr Reginald MENGI Persons with Disabilities Foundation Bi. Shimimana Ntuyabaliwe akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu utoaji tuzo za I Can kwa Watu wenye Ulemavu waliofanikiwa kwenye nyanja za elimu, siasa, uongozi, ujasiriamali, Sanaa na burudani, michezo, na ujuzi wa kipekee katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za Makao Makuu wa IPP jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ofisa Mifumo ya Habari wa Taasisi ya Dr Reginald MENGI Persons with Disabilities, Bw. Francis Bazil na kulia ni Meneja wa Utawala na Fedha wa Taasisi ya Dr Reginald MENGI Persons with Disabilities, Bw. Peter Sarungi,

KLINIKI YA BIASHARA IPO TAYARI KUTOA HUDUMA, TAGLA YAHAIDI USHIRIKIANO KUKUZA VIWANDA

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
MAONESHO ya tatu ya bidhaa za viwanda vya Tanzania na siku ya viwanda Afrika yamezinduliwa rasmi yakiwa na kauli mbiu ya  "Sasa Tunajenga Tanzania ya Viwanda" huku matumizi ya teknolojia katika kutafuta masoko ndani na nje ya nchi yakisisitizwa.

Akifungua maonesho hayo Naibu waziri wa viwanda, biashara na uwekezaji Mhandisi Stellah Manyanya amesema kuwa, serikali ya awamu ya tano imejizatiti katika kuhakikisha mpango kazi wa kuyafikia maendeleo unafanikiwa na kufikia 2025 wananchi wote wawe na vipato vya kati.

Aidha amesema kuwa uhakika wa masoko kwa bidhaa zinazozalishwa ni muhimu sana hasa kwa kutangaza bidhaa hizo ndani na nje kupitia maonesho ya aina hiyo.

Aidha amezipongeza taasisi 513 zilizoshiriki maonesho hayo na kuahidi kuwa Serikali kupitia Wizara ya viwanda itaendelea kuratibu na kuunganisha sekta zote katika kuhakikisha sekta hiyo inakua imara zaidi.

Pia amewataka wafanyabiashara watumie kliniki ya biashara iliyoanzishwa kwa kupeleka kero zao ili ziweze kutatuliwa na amewataka maafisa biashara ya Halmashauri na Wilaya kusikiliza kero za wafanyabiashara na kuziwakilisha mahala husika.
 Kulia  Mkurugenzi wa masoko na huduma kwa wateja wa Shirika la bima la taifa (NIC), Elisante Maleko akitoa maelezo ya bima ya kilimo kwa Naibu Waziri wa Viwanda biashara na uwekezaji,Mhandisi Stella Manyanya  ambapo akitoa wito kwa wakulima ote nchini  kujiunga na bima ya Taifa katika  maonyesho ya tatu ya bidhaa za wiwanda vya hapa nchini yaliyo funguliwa leo jijini Dar es Salaam.
  Naibu Waziri wa Viwanda biashara na uwekezaji,Mhandisi Stella Manyanya akisalimia na Mkurugenzi wa masoko na huduma kwa wateja wa Shirika la bima la taifa (NIC), Elisante Maleko leo alipotembelea banda la (NIC) katika maonyesho ya tatu ya bidhaa za wiwanda vya hapa nchini yaliyo  funguliwa leo jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na uwekezaji,Mhandisi  Stella Manyanya akimsikiliza Mkurugenzi mtendaji wa wakala wa mafunzo kwa njia ya mtandao,Charles Senkondo alipotembelea banda la banda hilo katika maonesho ya tatu ya bidhaa za wiwanda vya hapa nchini yaliyo funguliwa leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Viwanda biashara na uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya na Mkurugenzi mtendaji wa wakala wa mafunzo kwa njia ya mtandao Charles Senkondo wakiangalia namna ya kufanya mkutano kwa njia ya mtandao leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wananchi waliofika kwenye banda la NIDA ndani ya maonyesho ya Tatu ya Bidhaa za viwanda wakipatiwa elimu juu ya zoezi la usajili, umuhimu wa Vitambulisho vya Taifa na taratibu za kufuata ili kukamilisha hatua za awali za usajili.Picha na Emmanuel Massaka wa MMG)

Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images