Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

MRADI WA LTA WAMALIZA MIGOGORO YA ARDHI KATIKA KIJIJI CHA MAGUBIKE KWA KUTOA HATI MILIKI ZA KIMILA

$
0
0
NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

Migogoro ya ardhi katika kijiji cha magubike kata ya nzii wilaya ya iringa imebakia kkama historia baada ya mradi wa feed the future (LTA) kufanikiwa kupima ardhi na kuwakabidhi hatimiliki ya kimila kwa wananchi wa kijiji hicho.

Akizungumza wakatika wa kukabidhi hati hizo za kimila mwenyekiti wa halmashauri ya iringa Stephen Mhapa alisema kuwa kutolewa kwa hatimikili za kimila kunamaliza migogoro ya ardhi kwa wananchi wote waliopata hati hizo.

“Sasa tunaelekea kipindi cha kilimo ambapo ndio kuna kesi nyingi za mipaka ya ardhi, hivyo uwepo wa mradi huu wa LTA umetusaidia kumaliza kabisa migogoro ya ardhi naomba kuchukua nafasi hii kwa niaba ya serikali kuwashukuru kwa kazi mliyoifanya” alisema Mhapa 

Mhapa aliwaomba viongozi wa mradi wa LTA kuhakikisha wanapima vijiji vyote vya halmashauri ya wilaya ya Iringa ili kuondoa migogoro yote ambayo imekuwa ikirudisha nyuma maendeleo ya wananchi.

“Kama serikali ikisema ipime ardhi yote ni kazi nzito,kazi hii ilitakiwa kufanywa na serkali kutokana na ukosefu wa rasilimali fedha na rasilimali watu imekuwa tatizo kubwa kwa serikali hivyo lazima mpongezwe kwa kazi yenu mnayoifanya” alisema Mhapa
Mwenyekiti wa halmashauri ya iringa Stephen Mhapa akiwa na mkurugenzi wa mradi wa feed the future Malaki Msingwa wakati wa kukabidhi hati miliki za kimila kwa wananchi wa kijiji cha Magubike kilichopo kata ya Nzii mkoani Iringa 
Mwenyekiti wa halmashauri ya iringa Stephen Mhapa akiwa na mkurugenzi wa mradi wa feed the future Malaki Msingwa wakimkabidhi hati mmoja wa wananchi wa kijiji cha Magubike
Mwenyekiti wa halmashauri ya iringa Stephen Mhapa akiwa na mkurugenzi wa mradi wa feed the future Malaki Msingwa wakicheza nyimbo za asili pamoja na wananchi wa kijiji cha Magubike wakati wa ugawaji wa hati za kimila.



KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

Operesheni Nzagamba Awamu ya Pili yaondoa watumishi wazembe Kibaha

$
0
0
                        Na Frank Mvungi- MAELEZO
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina ameagiza Kuondolewa mara moja kwa watumishi wa Wanaosimamia Kituo cha Ukaguzi Kibaha Mkoani Pwani kwa kushindwa kusimamia rasilimali za Sekta ya Mifugo na Uvuvi. Akizungumza leo Jijini Dodoma wakati  wa kikao cha Tathmini ya Operesheni Nzagamba Awamu ya Pili iliyofanyika  kati ya mwezi Oktoba na Novemba 2018 ikilenga Kuinua mchango wa Sekta ya Mifugo katika Pato la Taifa Waziri Mpina amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali yatokanayo na biashara ya Mifugo na Mazao yake.

“ Watumishi wote walioshiriki katika Operesheni Nzagamba Awamu ya Pili wamefanya kazi kubwa na kwa uzalendo mkubwa hivyo nawapongeza kwa kuwa mmeonesha kuwa tunao uwezo wa kusimamia rasilimali zetu ili zitoe mchango stahiki katika pato la Taifa”.Alisisitiza Mhe. Mpina. Akifafanua amesema watumishi wasio waadilfu na wanaoshindwa kutekeleza majukumu yao hawana nafasi katika Wizara hiyo ndio maana ameagiza kuondolewa mara moja kwa watumishi wanaofanya kazi ya ukaguzi wa rasilimali hizo katika kituo cha Kibaha.
Aliongeza kuwa Operesheni Nzagamba awamu ya Pili, 2018 imedhihirisha kwamba usimamizi thabiti wa Sheria, Kanuni na Taratibu katika Sekta ya Mifugo unaweza kuleta tija kwa kuongeza uzalishaji bora wa mazao ya mifugo ambayo ni malighafi ya Viwanda na hivyo kuchangia ipasavyo katika kuendeleza uchumi wa Viwanda.

“ Ni mategemeo yangu kuwa wananchi mtakuwa wazalendo kwa nchi yetu kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za Kufanya biashara ya mifugo pia kutoa taarifa pale mnapobaini utoroshaji wa mifugo kwenda nchi jirani bila kulipiwa ushuru na tozo stahiki ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya watu hao”. Alibainisha Mhe. Mpina. Pia aliwaasa Watumishi wa Wizara hiyo na wale wa Halmashauri kuhakikisha kuwa wanasimamia kwa makini utekelezaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu zote zinazosimamia biashara ya Mifugo na Mazao yake hususan mabadiliko ya Kanuni mpya iliyotolewa mwezi Agosti, 2018.
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Luhaga Mpina akizungumza wakati wa uwasilishwaji wa Taarifa ya Tathmini ya Matokeo ya Operesheni Nzagamba awamu ya pili leo Jijini Dodoma.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof Elisante Ole Gabriel akizungumza wakati wa uwasilishwaji wa Taarifa ya Tathmini ya Matokeo ya Operesheni Nzagamba awamu ya pili  katika ukumbi wa St.Gasper Leo Jijini Dodoma.
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Luhaga Mpina akifuatilia uwasilishwaji wa Taarifa ya Tathmini ya Matokeo ya Operesheni Nzagamba awamu ya pili  leo Jijini Dodoma.Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof Elisante Ole Gabriel,Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Prof Siza Tumbo.     
 Baadhi ya Maafisa wa Polisi walioshiriki  Operesheni Nzagamba awamu ya pili  wakifuatilia kwa makini Hotuba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Luhaga Mpina (hayupo)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA    

WIZARA, IOM WAJADILI CHANGAMOTO ZA KUWARUDISHA WAKIMBIZI WANAOTAKA KUREJEA MAKWAO

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa (IOM), Dkt. Qassim Sufi (kulia), alipofika Ofisi Ndogo ya Wizara kujadili changamoto mbalimbali za kusafirisha wakimbizi wanaoendelea kurejea makwao baada ya kuimarika kwa amani katika nchi zao. Mazungumzo hayo yamefanyika leo jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa (IOM), Dkt. Qassim Sufi (kulia), akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, alipofika Ofisi Ndogo ya Wizara kujadili changamoto mbalimbali za kusafirisha wakimbizi wanaoendelea kurejea makwao baada ya kuimarika kwa amani katika nchi zao. Mazungumzo hayo yamefanyika leo jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Washindi wa Tigo Jigiftishe Moshi na Arusha wakabidhiwa fedha zao

$
0
0
 Mratibu wa Usambazaji na Tigo Pesa Mkoa wa Kilimanjaro Wolfgan Miraro akimkabidhi mfano wa Hundi ya Shilingi milioni moja  mmoja wa washindi wa Promosheni ya Jigftishe Yussuph Miraro kutoka mkoani Arusha. 

 Mratibu wa Usambazaji na Tigo Pesa Mkoa wa Kilimanjaro Wolfgan Miraro akimkabidhi mfano wa Hundi ya Shilingi milioni moja mmoja wa washindi wa Promosheni ya Jigiftishe mkazi wa Moshi mkoani Kilimanjaro Hilda Lema.

 Mratibu wa Usambazaji na Tigo Pesa Mkoa wa Kilimanjaro Wolfgan Miraro akimkabidhi Mkazi wa Moshi mjini, mkoani Kilimanjaro Albina Mmbaga mfano wa Hundi ya Shilingi milioni moja baadaya kufanikiwa kuibuka mshindi wa Promosheni ya Jigiftishe.

Mratibu wa Usambazaji na Tigo Pesa Mkoa wa Kilimanjaro Wolfgan Miraro (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa zawadi ya shilingi milioni moja wlizoshinda kupitia promosheni ya Tigo Jigiftishe kutoka mkoa wa Kilimanjaro na Arusha muda mfupi baada ya kuwakabidhi zawadi zao mjini Moshi jana.



Wafanyabiashara wajazwa mamilioni kwa kufanya miamala

$
0
0
Kampuni ya Selcom kwa kushirikiana na Mastercard imetoa zawadi ya Sh milioni tatu kwa wafanyabiashara wanaotumia huduma ya Masterpass QR katika kupokea malipo mbalimbali kwenye maeneo yao ya biashara. 

Zawadi hizo zimetolewa jana katika promosheni ya “Shinda Mtaji” iliyoanza rasmi Novemba mwaka huu kwa lengo la kuwarahisishia wafanyabiashara hao kutumia huduma ya Masterpass QR kufanya miamala mbalimbali. 

Akizungumza promosheni hiyo, Meneja Masoko wa Selcom, Juma Mgori alisema promosheni hii inamuwezesha mfanyabiashara kujishindia Sh milioni moja kila wiki kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Novemba mwaka huu hadi Januari mwaka 2019. 

Aidha, aliwataja wateja walioshinda milioni moja kila mmoja kuwa ni Boaz Wales, Hamisi Kilenga wote wa mkoani Dar es Salaam na mfanyabiashara mmoja kutoka Arusha. 

Alisema kila mfanyabiashara atakayejiunga na Masterpass QR na kuanza kupokea miamala kutoka kwa wateja, ataingia moja kwa moja kwenye droo ya promosheni kwa wiki hiyo na kupata nafasi ya kujishindia hivyo kumuwezesha kujiongezea mtaji wa biashara yake. 

“Masterpass QR ni huduma inayomuwezesha mteja kufanya malipo ya bidhaa na huduma mbalimbali kutoka kwenye akaunti ya simu au akaunti ya benki kwa kuingiza Pay Number ya mfanyabiashara au ku-skani kodi ya QR iliyopo kwenye eneo la mfanyabiashara kwa kutumia Smartphone. 
Mmoja wa washindi wa promosheni ya ‘Shinda mtaji’, Godfrey Kitende akionesha hundi ya Sh milioni moja aliyoshinda baada ya kukabidhiwa jana na Kampuni ya Selcom inayoshirikiana Mastercard kutoa zawadi kwa wafanyabiashara wanaotumia huduma ya Masterpass QR.
Mmoja wa washindi wa promosheni ya ‘Shinda mtaji’, Godfrey Kitende akipokea hundi ya Sh milioni moja kutoka kwa Meneja Masoko wa Kampuni ya Selcom, Juma Mgori. Kampuni hiyo inashirikiana Mastercard kutoa zawadi kwa wafanyabiashara wanaotumia huduma ya Masterpass QR




MICHUZI TV: WAZIRI MKUU ATEMBELEA TIC AITAKA IMALIZE URASIMU

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKABIDHI TUZO ZA MASHINDANO YA TEHAMA YA HUAWEI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa China Nchini, Mhe. Wang Ke wakati alipowasili kwenye Hoteli ya Hayyat Regency jijini Dar es salaam, Kutoa Tuzo za Mashindano ya TEHAMA ya HUAWEI, Desemba 5, 2018.  Wapili kushoto ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa  Joyce Ndalichako   na kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini katika bango wakati alipowasili kwenye hoteli ya Hayyat Regency jijini Dar es salaam kutoa Tuzo za Mashindano ya TEHAMA ya HUAWEI, Desemba 5, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi walioshiriki katika sherehe za Utoaji Tuzo za Mashindano ya TEHAMA ya HUAWEI kwenye hoteli ya Hayyat Regency jijini Dar es salaam, Desemba 5, 2018. Kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi, Atashasta Nditiye, Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya HUAWEI nchini, Frank Zhou na  Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Tuzo Mshindi wa Kwanza wa Mashindano ya TEHAMA ya HUAWEI, Emmanuel  Chaula wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam katika sherehe za kukabidhi Tuzo hizo kwenye hoteli ya Hayyat Regency jijini Dar es salaam, Desemba 5, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipokabidhi Tuzo za Mashindano ya TEHAMA ya HUAWEI kwenye hoteli ya Hayyat Regency jijini Dar es salaam, Desemba 5, 2018.
   Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Viongozi wa Kitaifa na Kimataifa wakiwa katika picha ya pamoja na washindi wa Mashindano ya TEHAMA ya HUAWEI baada ya kuwakabidhi tuzo za ushindi washindi hao kwenye hoteli ya Hayyat Regency jijini Dar es salaam, Desemba 5, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozana na Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke (wapili kulia) na Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati alipotoka kwenye ukumbi wa hoteli ya Hayyat Regency jijini Dar es salaam baada ya kutoa Tuzo kwa washindi wa Mashindano ya TEHAMA ya HUAWEI, Desemba 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Vodacom na TECNO wazindua simu ya TECNO Camon 11 kuwawezesha wateja wao kumaliza mwaka kidijitali

$
0
0
Vodacom, kampuni nambari moja ya mawasiliano ya simu nchini imeungana na kampuni ya Tecno kuwaletea wateja wao toleo jipya la simu aina ya Tecno Camon 11, leo jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huu ni harakati ya Vodacom kuhakikisha jitihada zake za kuwezesha maisha ya kidijitali kwa wateja wao, kwa kupitia simu janja zinafanikiwa. 

Akizungumza na waandishi wakati wa uzinduzi wa simu hiyo, Meneja Uhusiano wa kampuni ya TECNO Bw. Eric Mkomoya alisema, “Tumedhamiria kuhakikisha kila Mtanzania anamiliki simu janja na kwa pamoja tunalifanya taifa la Tanzania kuwa la kidigitali”. Uzinduzi huu uliohudhuriwa na wateja lukuki utawawezesha watumiaji wa matoleo ya awali wa simu za TECNO Camon kuweza kubadili simu zao ili kujipatia toleo hili jipya kwa kuongeza kiasi kidogo cha pesa. 

Simu hii inapatikana kwa bei ya shilingi laki nne tu (Sh. 400,000) na inakuja na Intaneti ya GB 15 ambapo mteja anapata GB tano kwa miezi mitatu mfululizo. TECNO Camon 11 ina kamera ya mbele yenye uwezo wa mega pixel 16 na kamera mbili za nyuma yenye uwezo wa mega pixel 13 na 2 kwa picha bora zaidi. Simu hii pia ina uwezo wa 4G LTE pamoja na uwezo wa kuhifadhi laini mbili za simu.

Pamoja na hayo, simu hii ina flashi iliyotengenezwa kwa rangi maalumu kuweza kusaidia mwanga kutoka vizuri huku ikiwa na kioo chenye ukubwa wa inchi 6.2 chenye uwezo wa FHD. Maduka yote ya TECNO yatatoa si huduma za TECNO tu bali pia kusajili laini za Vodacom. 
Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania PLC, Jacquiline Materu (wa pili kushoto) akimkabidhi zawadi ya simu mpya ya Tecno Camon 11Pro, kwa mhamasishaji wa Tecno Abdallah Sultan 'Dullivan' wakati wa uzinduzi wa simu hiyo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Simu hiyo itauzwa katika maduka ya Vodacom kwa kiasi cha TSh. 400,000. Kushoto ni Meneja wa Maduka ya rejareja ya Vodacom, Happiness Macha na  Meneja Uhusiano wa Tecno Erick Mkomoya kulia.
Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania PLC, Jacquiline Materu (katikati) akiwaonesha waandishi wa habari ( hawapo pichani) simu mpya ya Tecno Camon 11pro wakati wa uzinduzi wa simu hizo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Simu hiyo itauzwa katika maduka ya Vodacom kwa kiasi cha TSh. 400,000. Kushoto ni Meneja wa Maduka ya rejareja ya Vodacom, Happiness Macha na Meneja Uhusiano wa Tecno Erick Mkomoya.
Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania PLC, Jacquiline Materu (wa pili kushoto) akimkabidhi mpiga picha wa ITV Goodluck Maruti (kulia) zawadi ya simu mpya ya Tecno Camon 11pro, mara baada ya kuibuka mshindi wakati wa uzinduzi wa simu hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam. Simu hizo zitakazouzwa katika maduka ya Vodacom kwa kiasi cha TSh. 400,000 tu. Kushoto ni Meneja wa Maduka ya rejareja ya Vodacom, Happiness Macha na Meneja Uhusiano wa Tecno Erick Mkomoya.


AZAM YAENDELEZA REKODI YA KUTOKUFUNGWA UWANJA WA NYUMBANI

$
0
0
KLABU ya Azam FC, imetumia vema dakika 25 za mwisho ikitoka nyuma na kuichapa Stand United mabao 3-1 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Ushindi huo unaifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi 36 ikiwa na nafasi ya pili baada ya kushinda mechi 11 na sare tatu, ikizidiwa pointi mbili na vinara Yanga waliokuwa nazo 38.Mchezo huo ulianza kwa kasi kubwa, timu zote zikionyeshana ushindani mkubwa na haikushangaza dakika 45 za kwanza kumalizika kwa timu zote kuwa nguvu sawa, pande zote zikipoteza nafasi za kufunga mabao.

Stand United ilitangulia kupata bao la uongozi dakika ya 52 kupitia kwa Hafidh Musa, bao ambalo liliongeza kasi ya mashambulizi kwa Azam FC.

Mabadiliko yaliyofanywa na Kocha Mkuu wa Azam FC, Hans Van Der Pluijm, ya kuwaingiza kipindi cha pili mshambuliaji Yahya Zayd na winga Enock Atta, yalizaa matunda baada ya wachezaji hao kuhusika kwenye mabao yote matatu ndani ya dakika 25 za mwisho za kipindi cha pili yaliyopindua uongozi wa Stand.

Dakika ya 65, Atta aliisawazishia Azam FC kwa bao safi la kichwa akimalizia krosi iliyopigwa na Zayd, na hilo linakuwa bao lake la kwanza msimu huu.Alikuwa ni Atta tena aliyehusika kwa bao pili la Azam FC baada ya kuangushwa ndani ya eneo la hatari na mwamuzi, Huseein Athuman, kutoka Katavi kuamuru upigwe mkwaju wa penalti uliofungwa vema na Zayd dakika ya 71.

Zayd aliihakikishia ushindi Azam FC kwa kuifungia bao la tatu dakika ya 85 akitumia vema pasi ya kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’, likiwa ni bao lake la tano msimu huu.Mara baada ya mchezo huo, kikosi cha Azam FC kinatarajia kuendelea na mazoezi kesho Jumatano kujiandaa na mchezo ujao wa ligi dhidi ya Mbao utakaofanyika Ijumaa hii saa 1.00 usiku.

MICHUZI TV: RAIS DKT MAGUFULI AMJULIA HALI RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA PILI MZEE MWINYI

TGNP WAADHIMISHA NA KUJADILI SIKU 16 ZA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
KATIKA kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) wamefungua kongamano la kampeni ya siku 16 za kupambana na ukatili wa kijinsia. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kongamano hilo Mkurugenzi mtendaji wa TGNP, Lilian Liundi amesema kuwa Wanawake ni nguvu kazi ya Taifa na pasipo kumthamini hakutokuwa  na Maendeleo ambayo yatakua na usawa wa kijinsia na haki sawa.

Amesema kuwa kampeni ya kupinga ukatili wa kijinsia hasa kwa mwanamke ni usalama wake na ni jukumu la kila mmoja katika kutokomeza ukatili wa kijinsia na hasa kuwalinda wanawake katika janga hilo. Kuhusiana na  rushwa ya ngono makazini hasa kwa waajiri kwenda kwa waajiriwa bi. Lilian amesema kuwa kupitia kampeni hiyo hali hiyo itavunjwa na kupigwa vita kwani elimu itatolewa kwa pande zote ili kuhakikisha kuwa kila mmoja anakuwa na uhuru na ujasiri wa kusema pindi anapokutana na changamoto hizo.

Aidha amesema kuwa wao kama TNGP mtandao wataendelea kuunga mkono juhudi zote zitakazofanywa na na TAKUKURU na vyombo vingine vya dola katika kuhakikisha vita hiyo inafanikiwa na ametoa wito kwa serikali na wadau wengine kushirikiana katika kuhakikisha janga hilo la ukatili linatokomea kabisa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Lilian Liundi akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano la siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ambapo ameeleza kuwa wapo bega kwa bega na serikali pamoja na vyombo vya dola katika kuhakikisha janga hilo linatokomea kabisa wakati wa kongamono hilo lililofanyika katika viwanja vya TGNP Mtandao  leo jijini Dar es Salaam.
Wadau pamoja na wadua mbalimbali kutoka vitovu vya jinsia  na Clabu za jinsia Mashuleni wakiwa kwenye kongamono la kupinga ukatili wa kijinsia lililofanyika katika viwanja vya TGNP Mtandao  leo jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa kamati ya wanawake (TUCTA) Rehema Ludanga akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kugmfunguliwa kwa kongamano hilo ambapo amesema kuwa taasisi binafsi zinaongoza kwa rushwa ya ngono mahali pa kazi wakati wa kongamono hilo lililofanyika katika viwanja vya TGNP Mtandao  leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

IGP SIRRO AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA NBC

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Theobald Sabi, wakati alipomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es salaam leo 05/12/2018, kwa lengo la kuendelea kujenga ushirikiano baina ya benki hiyo na Jeshi la Polisi. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Theobald Sabi, pamoja na watendaji wengine wa benki hiyo wakati walipomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi hilo jijini Dar es salaam leo 05/12/2018, kwa lengo la kuendelea kujenga ushirikiano baina ya benki hiyo na Jeshi la Polisi. Picha na Jeshi la Polisi.



BENKI YA I&M KUWAWEKA KARIBU WATEJA WAKE KATIKA MSIMU HUU WA SIKUKUU

$
0
0
Na Agness Francis, Globu ya Jamii
Benki ya I & M inaendelea kutoa zawadi kwa wateja wake katika droo  ya pili JIDABO na I & M bank chini ya usimamizi kutoka Bodi ya Taifa  ya Michezo ya Kubahatisha iliyochezeshwa leo ambapo washindi  watano wamepatikana kutoka sehemu mbali mbali hapa nchini 

Akizungumza na Waandishi wa  Habari leo Jijini Dar es  Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Wateja na reja reja, Ndabu Swere amesema kuwa  promosheni hiyo iliyoanza mwezi Octoba na kuendelea mpaka Disemba kwa kila mwezi kutaja washindi watano wa droo hiyo. 

Ndabu amesema washindi watano waliopatikana leo ni sehemu ya washindi 15 ambao watapatikana katika kipindi chote cha miezi mitatu ya promosheni ya "JIDABO na I&M". Aidha Ndabu amesema kuwa mpaka  sasa wameshapata jumla ya washindi 10 na kubakiza wengine  5 ambao watapatikana katika droo ya mwezi huu

"Ili kuweza kushiriki Promosheni hii mteja anapaswa afungue akaunti ya Akiba, biashara, mtoto katika tawi lolote la Benki ya I & M katika kipindi chote cha promosheni, kwa mteja ambaye tayari ana Akaunti ya Benki hiyo anapaswa kuhakikisha kuwa ana akiba ya kiasi cha fedha  shilingi 200000, akiwa anamiliki akaunti ya biashara, au 100000, Ikiwa anamiliki Akaunti nyingine zinazohusika katika promosheni," amesema Ndabu.
 Mkuu wa kitengo cha Wateja wa reja reja wa Benki ya I & M Ndabu Lilian Swere akiwataja washindi watano wa droo ya pili ya Promosheni ya JIDABO na I& M Bank iliyochezwa leo Jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko na Mawasiliano Emmanuel Kiondo, Benki ya I & M akiwa na mmoja ya mfanyakazi wa Benki hiyo wakichezesha droo ya pili iliyofanyika leo na kuwatangaza washindi  watano wa Promoshei ya JIDABO na I & M Bank chini ya usimamizi kutoka bodi ya Taifa ya Michezo ya Kubahatisha.

RAIS DKT. SHEIN AZINDUA MRADI WA UCHUNGUZI WA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI ZANZIBAR

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein akitoa hotuba ya uzinduzi wa Mradi wa Uchunguzi wa Saratani ya Shingo ya Kizazi katika ukumbi wa sheikh Idriss Abdulwakil kikwajuni Zanzibar.
 Katibu Mkuu Wizara ya Afya Asha Ali Abdalla akitoa maelezo kuhusiana na Mradi wa Uchunguzi wa Saratani ya Shingo ya Kizazi katika ukumbi wa sheikh Idriss Abdulwakil kikwajuni Zanzibar.
 Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohamed akitoa hotuba ya makaribisho katika hafla ya  uzinduzi wa Mradi wa Uchunguzi wa Saratani ya Shingo ya Kizazi katika ukumbi wa sheikh Idriss Abdulwakil kikwajuni Zanzibar.
 Makamu wa Rais wa Naijing Drum Tower Hospital Dkt Yu Chenggong akitoa hmaelezo kuhusu mradi katika uzinduzi wa Mradi wa Uchunguzi wa Saratani ya Shingo ya Kizazi katika ukumbi wa sheikh Idriss Abdulwakil kikwajuni Zanzibar.
 Bolozi mdogo wa China Alioko Zanzibar Xie Xiaowu akitoa salamu za china katika hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Uchunguzi wa Saratani ya Shingo ya Kizazi katika ukumbi wa sheikh Idriss Abdulwakil kikwajuni Zanzibar.
 Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Uchunguzi wa Saratani ya Shingo ya Kizazi katika ukumbi wa sheikh Idriss Abdulwakil kikwajuni Zanzibar.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Ali Mohamed Shein katikati akimkabidhi Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Mgeni Hassan Juma cheti cha uteuzi wa ubalozi wa Mradi wa Uchunguzi wa Saratani ya shingo ya kizazi katika hafla ya Uzinduzi wa mradi huo ukumbi wa sheikh Idriss Abdulwakil kikwajuni Zanzibar.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Ali Mohamed Shein wapili kulia akionesha kitu wakati akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Huduma za Uchunguzi Hospitali ya Mnazi mmoja Dkt,Msafiri Marijani kuhusiana na maradhi ya Shingo ya kizazi yanayowapata kinamama katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa Uchunguzi wa Saratani ya shingo ya kizazi ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil kikwajuni Zanzibar.
PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR

RAIS DKT. MAGUFULI AMJULIA HALI RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA PILI ALHAJI ALI HASSAN MWINYI ANAYEPATIWA MATIBABU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mhe.Ali Hassan Mwinyi alipomtembelea kumjulia hali  Jijini Dar es Salaam.Disemba 5, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakiomba Dua Maalumu na Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mhe.Ali Hassan Mwinyi, Bi. Sitti Mwinyi (Mke wa Mzee Mwinyi) pamoja na Abdallah Mwinyi (Mtoto wa Mzee Mwinyi) alipomtembelea kumjulia hali Jijini Dar es Salaam.Disemba 5, 2018.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mhe.Ali Hassan Mwinyi alipomtembelea kumjulia hali  Jijini Dar es Salaam.Disemba 5, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Bi Sitti Mwinyi Mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mhe.Ali Hassan Mwinyi alipomtembelea kumjulia hali  Rais Mstaafu Jijini Dar es Salaam.Disemba 5, 2018.PICHA NA IKULU.

Taasisi ya APHFTA yakabidhi vitaa tiba katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita

$
0
0
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG.

Chama cha Watoa Huduma za Afya Binafsi Tanzania (APHFTA), leo kimekabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya Tsh. Milioni 19 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Geita lengo likiwa ni kuboresha huduma ya upimaji Malaria kwa wananchi.

Mkurugenzi wa Miradi APHFTA, Elizabeth Bonareri amesema vifaa hivyo ni pamoja na "Microscope" na kwamba chama hicho pia kimetenga Tsh. Milioni 30 kwa ajili ya kufanya ukarabati wa jengo la maabara ya Hospitali hiyo.

Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Geita, Mhandisi Robert Gabriel, Katibu Tawala Msaidizi, Herman Matemu amesema vifaa hivyo vitasaidia utoaji wa huduma bora kwa wananchi na hivyo kuomba vitumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

Mganga Mkuu mkoani Geita, Dkt. Japhet Simeo amesema juhudi mbalimbali ikiwemo kunyunyizia dawa ya ukoko majumbani, elimu sahihi kuhusu matumizi ya vyandarua vyenye dawa, utunzaji mazingira/ kufyekya nyasi na kufukia madimbwi pamoja na kuwahimiza wananchi kuwahi katika vipimo zimekuwa zikifanyika katika kupambana na ugonjwa wa Malaria ambapo pia ameishukru taasisi ya APHFTA kwa namna inavyoshirikiana na Serikali kupambana na ugonjwa huo.

Taasisi ya APHFTA kwa kushirikiana na kampuni ya Afya Micro-Finance kwa ufadhili wa wadau wa maendeleo "Comic Relief" inatekeleza mradi wa kupambana na Malaria mkoani Geita ambapo juhudi hizo zimesaidia kiwango cha maambukizi kupungua kutoka asilimia 38.1 mwaka 2015/16 hadi kufikia asilimia 17 mwaka 2017/18.
Baadhi ya mashine (Microscopes) zilizotolewa na taasisi ya APHFA ili kusaidia huduma ya upimaji Malaria katika Hospitali ya Rufa ya Mkoa Geita.
Mkurugenzi wa Miradi taasisi ya APHFTA, Elizabeth Bonareri (kushoto), akimkabidhi Katibu Tawala Msaidizi Mkoa Geita, Herman Matemu (kulia) printa kwa ajili ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo. Mashine hiyo ni miongoni mwa vifaa tiba vilivyotolewa na taasisi ya APHFTA kuboresha huduma hospitalini hapo.
 Katibu Tawala Msaidizi Mkoa Geita, Herman Matemu (katikati) akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel (hayuko pichani) baada ya kupokea vifaa tiba kutoka taasisi ya APHFA

OFFICIAL LYN ASEMA AMEKUJA KIVINGINE KWENYE BONGOFLEVA

$
0
0
MSANII wa michezo ya mrembo husika wa Kwenye wimbo (VIDEO QUEEN) Irene maarufu kama official Lyn  aingia rasmi Kwenye tasnia ya muziki wa Bongofleva.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es salaam Lyn ambae alianza kujulikana Kwenye video ya Msanii Rayvan Kwenye kibao chake cha kwetu alishirikishwa kama video queen amesema rasmi ameingia Kwenye muziki akiwa tayari ameshafanya wimbo unaokwenda kwa jina la Chafu ambao umetoka Leo .

Kisheria natambulika na Baraza la Sanaa  (BASATA) nikiwa kama Muimbaji pia ni Msanii hivyo basi  niwatoe hofu mashabiki zangu alisema Lyn.

Hata hivyo ameeleza utofauti wake na video queen wengine ambao wameshaingia Kwenye tasnia ya muziki kuwa atanyanyua vipaji vya queen video chipukizi na kuwa nafasi kuonekana Kwenye baadhi ya kazi zake za muziki atakazokuwa anafanya kuanzia sasa kwani hata yeye alitokea huko huko na baadae kujulikana.

Hata hivyo Lyn amesema kuwa anaomba mashabiki wake wampokee kwa mikono yote kama walivompokea wakati akiwa video queen ambapo kwa sasa hatoweza kurudi Kwenye kazi hiyo ya zamani.

Pia ametolea ufafanuzi kuhusu wimbo wake mpya wa chafu ambao amefanya Kwenye studio za Black na video amefanya na director hascana nchini south Africa huku Mashairi akitungiwa na Msanii Marioo.

WATOTO 52 NA WATU WAZIMA WAWILI WENYE MATATIZO YA MOYO YA KUZALIWA NAYO WAFANYIWA UPASUAJI KAMBI MAALUM

$
0
0
Wagonjwa 54 wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo wamefanyiwa upasuaji wa moyo wa kufungua na bila kufungua kifua katika kambi maalum ya matibabu inayofanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Matibabu hayo yanafanywa na madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na madaktari wa mradi wa Little Heart wa nchini Saud Arabia ambao ni moja ya mradi wa Afya ulioko ndani ya Taasisi ya Msaada ya Muntada yenye makao makuu yake mjini London nchini Uingereza.

Upasuaji huo umefanyika kwa watoto 52 na watu wazima wawili wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo ambayo ni matundu na valvu .

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salam Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka JKCI Godwin Sharau alisema kwa upande wa upasuaji wa kufungua kifua wamefanya upasuaji kwa watoto 19 kwa kurekebisha valvu, kuziba matundu, kurekebisha mishipa ya moyo ambayo imekaa vibaya na kurekebisha mfumo wa uzungukaji wa damu katika moyo.

Dkt. Sharau alisema watoto waliowafanyiwa upasuaji wanaendelea vizuri na wengine wameshatoka katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) na kupelekwa wodini kwa ajili ya kuendelea na matibabu ikiwa ni pamoja na kuanza mazoezi.

MKURUGENZI MSD APIGIWA SIMU 'LIVE' KUJIBU HOJA ZA WASIKILIZAJI DODOMA JUU YA USAMBAZAJI DAWA

Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images