Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110160 articles
Browse latest View live

//michuzi2.rssing.com/chan-7007653/article5221-live.html


Busara Promotions sasa yaja na ‘Sauti Zetu’ Maonyesho ya Ngoma za asili

$
0
0
Busara Promorions ni Taasisi inayoandaa tamasha la muziki la Sauti za Busara mara moja kwa mwaka ndani ya Mji Mkongwe, tunapenda kutangaza mipango mipya ya maonyesho yatakayofanyika kisiwani hapa mwezi wa Tisa na Kumi: Maonyesho haya yanajulikana kwa jina la “Sauti Zetu”

Tamasha hili dogo limeandaliwa ili kusherekea na kutangaza utamaduni wa Zanzibar na kuwapatia nafasi wasanii na wanamuziki wazawa. Vikundi vitakavyoshiriki katika maonyesho haya vitapata nafasi ya kushiriki katika tamasha la Sauti za Busara februari 2014, Rebecca Corey Mkurugenzi Mtendaji wa Busara Promotions alisema kuwa watapata nafasi ya kujulikana kitaifa na kimataifa na kujenga mahusiano kwa utamaduni wa ndani wa Zanzibar.

Journey Ramadhan, Mmoja wa waandaji wa Busara Promotions, alisema”maonyesho haya ya kikanda ni muhimu kwa Busara ili kuongeza uelewa wa kazi zetu katika mikoa mingine ya Zanzibar ( Nje ya Mji Mkongwe) na kujenga mahusiano mazuri na watu na wasanii wa kisiwa hiki. Pia ni muhimu kwa wasanii kwa sababu itasaidia kukuza vipaji vyao, kuwafanya wawe wajasili na kuwaongezea miundombinu. 

Pia ni nafasi muhimu kwa watazamaji wa nje ya Mji Mkongwe kuona ambavyo Sauti za Busara inavyowatangaza wasanii wazawa, katika maonyesho haya yote pamoja na tamasha la Sauti za Busara. ’Sauti Zetu’ itawaonyesha watazamaji kuwa vikundi vitakavyo shiriki katika maonyesho haya ya Mikoa yao ni wasanii bora.”

Maonyesho haya ya kikanda “Sauti Zetu” yatafanyika wiki hii Jumamosi tarehe 21 Septemba 2013 Nungwi na yatashirikisha vikundi vya ngoma za asili kama vile: Kidumbaki, Dumu, Mchikicho, na Pungwa. Maonyesho haya yataanza saa tisa mpaka kumi na mbili katika shule ya msingi ya Nungwi. Kiingilio ni BURE kabisa.

Maonyesho haya yameandaliwa kwa ushirikiano na Maafisa Utamaduni wa Wilaya za Kasikazini A, Kasikazini B na Afisi ya shehia ya Nungwi.

Kati ya mwezi wa tisa na wa kumi Busara Promotions itaandaa maonyesho mengine katika Mikoa ya Mjini Magharibi (Kisonge) na Kusini (Jambiani). Tarehe husika itatangazwa hapo baadae.

Busara Promotions ipo katika maandalizi ya toleo ya 11 la tamasha la muziki la Sauti za Busar, litakalo fanyika kuanzia tarehe 13 mpaka 16 February 2014, ndani ya Mji Mkongwe, Zanzibar.

Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na Mkurugenzi mtendaji wa Busara Promotions, Rebecca Corey, kupitia barua pepe hii: rebecca@busara.or.tz.

MSAADA TUTANI

$
0
0
Ndugu JOSEPH MACHELE kupitia ndugu ISSA MICHUZI(Na Michuzi Blog)...Salaamu!Awali ya yote niwape pole ya majukumu yenu binafsi na ya kitaifa.

Ndugu zangu, nimefurahi sana leo kuona kwenye blog yako kuhusu usalama wa ndugu zetu wanaoishi Mexico kufuatia kimbunga kilichoikumba Marekani.

Mimi niko kwa sasa Marekani kimasomo katika Jimbo la IOWA katika Chuo Kikuu hapa.Ni mpenzi mkubwa wa kupata taarifa za nyumbani na kwingineko kupitia blog hii maalufu ambayo waTanzania wengi wa hapa Marekani tunaitumia kwa kupata habari za nyumbani.ASANTE KWA HILI.

Naomba kukutanishwa na ndugu yangu aliyetajwa na Joseph Machele kuhusiana na usalama wao kutokana na kimbuka cha Marekani kwamba yuko na wako SALAMA.

Mtu huyo aliyetajwa kwa jina NYABENDA MPORAKUMUGERO ni ndugu yangu yaani MJOMBA.Pia kwa kuongezea zaidi ni kuwa anaitwa LEONIDAS NYABENDA NGENZEBHUKE MPORAKUMUGERO.

Nitafurahi sana kama nikimpata kwa mawasiliano hasa baada ya kuona katajwa kwenye sehemu hii ya Michuzi blog. Nitafurahi kumpata na kuwasiliana naye;

Email yangu ni kibambizi@gmai.com.Nitatoa namba yangu ya simu nikipata email yake na kuwanza kuwasiliana.

ASANTE;
Deo'Gracias Kibambizi.

UKWELI KUHUSU SAYANSI YA KIAFRIKA A.K.A NDUMBA NAMGAI

$
0
0
Sayansi maana yake ni maarifa . Tunapo zungumzia dhana ya sayansi ya kiafrika , tunakuwa tunamaanisha matumizi ya maarifa ya kiafrika katika kukabiliana  na mazingira ya mwanadamu pamoja na changamoto mbalimbali zinazo mkabili .

Tafiti mbalimbali za ki akiolojia na ki-anthropolojia zinaonyesha kuwa sayansi ya kiafrika imekuwapo kwa takribani miaka bilioni mbili sasa, hii  ikiwa na maana kuwa sayansi ama ustaarabu wa kiafrika ndio ustaarabu mkongwe kupita ustaarabu mwingine wowote ule katika sayari ya dunia.

Hata ustaarabu wa jamii mbalimbali duniani kama vile waajemi, wayunani (Ugiriki ya kale ), wamisri, wasumeri ( Mesopotamia/babiloni ) ya kale nakadhalika, unatokana na ustaarabu ambao msingi wake ni sayansi ya kiafrika.

• Sayansi ya kiafrika imethibitika kumsaidia mwanadamu katika kukabiliana na mazingira yake kwa zaidi ya asilimia tisini na tisa (99%).

• Kwa bahati mbaya sana, sayansi ya kiafrika imepewa jina baya kwa kuitwa uchawi na kupigwa vita mbaya tangu mamia ya miaka iliyopita, lengo kuu likiwa ni kumuondolea mwanadamu uwezo wa kiungu ulio wekwa ndani yake wa kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazo mkabili katika maisha yake ya kila siku.

COSTECH PARTICIPATES INTO YOUNG SCIENTISTS TANZANIA EXHIBITIONS

$
0
0
The Tanzania Commission for Science and Technology(COSTECH) today participated in the Young Scientists Tanzania Exhibition at Diamond Jubilee Hall Dar es salaam. 

COSTECH as a Government institution entrusted with responsibilities of promoting and coordinating Research, Science, Technology and Innovation participates in this event as one of its duties to boost the country’s economical development through Research, Science and Technology.Young Scientists Tanzania is a unique event in Africa, providing a platform for young people from across Tanzania to demonstrate their innovation and showcase their scientific talents.

Young Scientists which now is in its 49th year, helps to popularize science amongst young people and encourage them to seek practical solutions to the problems they face in everyday life.
COSTECH Engineer Andrew Mzava who also is a Judge during the Tanzania Young Scientists Exhibitions examines projects of the Young Scientists at Diamond Jubilee Hall.
COSTECH Public relations Officer,Theophil Laurian Pima explains to a Kilakala Secondary School teacher how COSTECH supports Research, Science, Technology and Innovation in Tanzania mainland and Isles
A cross section of the Ordinary School Students demonstrates how their projects work. The centerpiece of YST is an attractive annual exhibition and competition in which schools and students can participate. Schools and teachers that wish to get involved are supported through cross regional workshops, where they receive mentoring and practical advice on experimental methods suitable for their environment.

Students then generate ideas for their projects based on the realities faced in their communities, tackling topics as wide ranging as nutrition, climate change, sustainable agriculture, gender inequality, disease, clean water and sustainable energy, all of which have major implications for the development of the Tanzanian economy and society.

 In the process of their research, students and schools are also linked up with appropriate mentors from academia, the government, development and private sectors, and encouraged to view their research in the context of the global scientific community

VIWANJA VINAUZWA VIKAWE-KIBAHA.

$
0
0
VIWANJA VILIVYOPIMWA VINAUZWA,VINA UKUBWA TOFAUTI TOFAUTI,VIPO VIKAWE KIBAHA,UKITOKEA BAGAMOYO ROAD MAENEO YA BAOBAB SECONDARY.

NI UMBALI WA KILOMETA NANE MPAKA KWENYE VIWANJA.WANAOTAKA KUVIONA NI KILA JUMAPILI SAA NNE  ASUBUHI,SAFARI INAANZIA MWENGE.

KWA MAELEZO ZAIDI PIGA 0756877173

NAPE AWACHONGANISHA CHADEMA NA WAKULIMA WA PAMBA

$
0
0


 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa wilaya ya Bariadi kwenye Viwanja vya Sabasaba.

~. Adai wamechukizwa na viwanda vya nguo,nyuzi ,nyama na ajira.
~. Asema misaada ya China ni ukombozi mkubwa unaowakera Chadema.
~. Awataka kanda ya ziwa kuujua unafiki huo wa Chadema.


Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye ameeleza kusikitishwa kwake na hatua ya Chadema kukerwa na hatua za Balozi wa China na serikali ya China kwa ujumla katika kushiriki katika hatua za kuwakwamua watanzania katika umasikini.



Nape alisema hayo jana alipokuwa akiwahutubia wananchi wa mji wa Bariadi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya CCM sabasaba Mkoani Simiyu.



Alisema hoja kuwa ambayo imewakera na kuwasumbua Chadema ni hatua zinazochukuliwa hivi sasa kwa pamoja kati ya Serikali ya CCM na Serikali ya China ambayo hivi sasa inaelekea kuzaa matunda ya kutoa mwanya wa ajira zaidi ya elfu- 25 viwandani.



"Tayari tushaingia makubaliano na serikali ya China ya kuwekeza katika viwanda vya kuongeza thamani ya mazao kama Pamba, ufuta, alzeti na mazao ya mifugo ikiwemo ngozi za ng'ombe, hivyo wananchi, chuki na hasira ya Chadema dhidi ya Balozi wq China inasababishwa na mafanikio hayo ya kutatua matatizo ya wananchi" alisema Nape.



"ushahidi wa hasira za Chadema unadhihilishwa na ukweli kwamba tayari wawekezaji wa viwanda hivyo vya kuongeza thamani ya mazao washawasili nchini na wengine wameshaanza ujenzi wa viwanda hivyo mjini Shinyanga, na kwamba vitaanza kazi ya uzalishaji mwezi desemba mwaka huu" Aliongeza.



Nape aliwataka watanzania kuzipuuza shutuma za Chadema dhidi ya Balozi wa China na kusisitiza kuwa hasira yao imesababishwa na hofu ya mtaji wao wa kutumia udhaifu na umasikini wa watanzania hasa vijana wasi na ajira kama mtaji wao wa kisiasa.



"Chadema wamechanganyikiwa, kwa sababu siku zote wamekuwa wakitegemea kuendesha chama chao kwa mgongo wa umaskini wa watanzania, sasa kasi ya kutengeneza ajira kupitia ujenzi wa viwanda, na mchakato wa kuwezesha kuongeza bei ya mazao ili kuwakwamua wakulima kutoka katika umaskini umewachanganya" Alisisitiza Nape.



Mwishoni mwa wiki iliyopita Balozi wa China alishiriki katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Abdurlahaman Kinana kwa kukagua maendeleo ya ujenzi wa viwanda vinavyojengwa na wawekezaji toka nchini China katika mikoa ya kanda ya ziwa ikiwemo vile vinavyojengwa mjini Shinyanga jambo linalolalamikiwa na Chadema.

JUMUIYA YA ZAPHA + YAFANYA WARSHA YA SIKU MOJA KUJADILI WATOTO WANAOSHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU ZANZIBAR

$
0
0
Mwezeshaji wa warsha Bw. Mwalimu Wilson-olesira alie simama akizungumza na washiriki wa warsha ya kujadili mchango wa jamii katika kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu, katika ukumbi wa zamani wa Radio uliopo Rahaleo Mjini Zanzibar. Warsha hiyo ya siku 1 imeandaliwa na (ZAPHA +).
Afisa vituo vya kulelea watoto yatima Idara ya Ustawi wa Jamii Zanzibar Lahdad Haji Chum akichangia katika mjada wa nini tufanye kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu katika warsha ya siku moja iliyoandaliwa na (ZAPHA +) katika ukumbi wa zamani wa Radio Zanzibar.
Maryam Charles Samwel mmoja ya vijana wanaosaidiwa kimasomo na (ZAPHA +) akizihamasisha Jumuiya nyengine kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu magumu katika warsha ya siku moja iliyoandaliwa na (ZAPHA +) katika ukumbi wa zamani wa Radio Zanzibar uliopo Rahaleo Mjini Unguja.
aadhi ya washiriki wa warsha ya siku moja iliyo jadili mchango wa jamii katika kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu, huko katika ukumbi wa zamani wa Radio Zanzibar uliopo Rahaleo Mjini Unguja. (Picha na makame Mshenga-Maelezo)

MWENYEKITI WA CHADEMA ALIYETIWA MBARONI ASHINDA RUFAA NA KUACHIWA

$
0
0
 Mwenyekiti CHADEMA kijiji cha Ivalalila Makete Godfrey Mahenge akizungumza mara baada ya kutoka jela.

======
Na Edwin Moshi, Michuzi Media, Makete

Jeshi la polisi nchini limeaswa kutenda kazi kwa haki bila kushurutishwa na mtu yeyote kwani lisipofanya hivyo haki haitatendeka kwa kila raia kama katiba inavyosema

Rai hiyo imetolewa hii leo na mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Makete Shaaban Mkakanze wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Ivalalila wilayani hapo waliojitokeza kumpokea mwenyekiti wa CHADEMA kijijini hapo aliyekuwa gerezani mara baada ya kuachiwa huru
 
"jeshi la polisi ni zuri sana pale litakaposimamia haki, lakini wanapokwenda kinyume kwa kweli wanageuka mwiba mchungu kwa wananchi" alisema Mkakanze 

Mkakanze amesema hukumu iliyotolewa na mahakama ya mwanzo makete mjini Juni 28 mwaka huu dhidi ya mwenyekiti huyo imeonekana kuwa na mapungufu mengi ambayo amesema atayataja katika mkutano wa hadhara utakaofanyika muda wowote kuanzia sasa, hivyo ndiyo maana wameibuka kidedea katika rufaa waliyokata

Amesema wao kama chama hawatakatishwa tamaa na mambo kama hayo na badala yake wataendelea kupigania haki za wananchi pale wanapoonewa na ikibidi hata kupoteza maisha wakati wakipigania haki zao

"Chadema sisi si watu wa vurugu, lakini sisi tunasimamia haki na maendeleo ya wananchi bila kujali  itikadi za vyama, hata yeyote tupo pamoja nae kama anatenda haki na kile anachotakiwa kuwafanyia wananchi lakini anapokwenda kinyume sisi hatutakubali na badala yake tutapambana mpaka kieleweke" alisema Mkakanze

Naye mwenyekiti wa CHADEMA kijiji cha Ivalalila ambaye alikuwa gerezani Bw Godfrey Mahenge amesema hana cha kusema zaidi ya kumshukuru Mungu na wananchi wa kijiji hicho ambao walikuwa naye pamoja tangu wakati wa kesi hadi gerezani na kusema kwa sasa ametoka na wembe ni ule ule wa kupigania haki za wananchi wake

Amesema kwa sasa hana mengi ya kuongea zaidi atakuja kuzungumza kwenye mkutano wa hadhara ambao utaandaliwa kwa ajili ya wananchi hao ambapo anatarajia kueleza yote yaliyomkuta ili wananchi wake wajue, huku akitoa rai kwa waandishi wa habari kutangazia umma kuwa hivi sasa yuko huru na kesi zote ameshinda

"Nawaomba waandishi wa habari kama mlivyotangaza wakati nafungwa naomba mtangaze pia na jinsi nilivyoshinda rufaa na kuwa huru" alisema Mahenge

Mnamo Juni 28 mwaka huu mahakama ya mwanzo makete mjini ilimtia hatiani kwa kosa la kutukana polisi hivyo kuhukumiwa kifungo cha miezi 9 gerezani hali iliyomlazimu kukata rufaa na kushinda rufaa hiyo

Tanzania convention-Trade and investment forum UK 2013 meet with the Tanzania high commissioner in UK

$
0
0
The chief coordinator of The Tanzania convention-Trade and investment forum UK 2013 and director Newdeal Africa Mr Ayoub Mzee mt with the Tanzania high commissioner H.E Peter Kallaghe and the entire Mission team for a briefing on the forthcoming Tanzania convention-Trade and investment forum UK 2013 to be held in London from the 6-7 December 2013.

The Forum, will focus on Tanzania as one of Africa’s leading business and investment destinations, while taking the theme:’Unleashing Tanzania’s potential as a pole of global growth under the subtheme: ‘Ijuwe Tanzania yako ya leo’.

Tanzania’s business opportunities are attracting high levels of international interest and the reform of our country’s economy to make it more private sectors friendly is already paying dividends. Now is the optimal time to come to this event to meet with the Ministers and officials and hear the success stories of other international private sector leaders that are already operating in our country.


This Forum will bring together the decision makers you need to meet to do business in Tanzania as well as focusing on key issues essential to the continued growth and development of our country and continent. Present will be investors and UK business community who are interested I doing business in Tanzania.


We are very keen and committed to support and develop Tanzania together and we welcome any suggestions , Exhibition, Sponsorship and partnerships proposals .To register for participation kindly send your emails to: newdealafrica@yahoo.co.uk or visit our website www.newdealafrica.co.uk

Mavazi na Urembo kutoka kwa Mdau Freddy Macha

$
0
0
-Na Freddy Macha
LOGO -fashion Sept 7- by Sara Abood 
  Mchoro wa shughuli uliobuniwa na Sara Abood. 

Wabunifu mavazi wanne toka Tanzania walioshiriki maonesho ya mavazi Ubalozi wetu London Jumamosi Septemba Saba wamechaguliwa kuingia dimba la kimataifa London Fashion Week, Februari mwakani. Wasanii hao waliopewa nafasi ya kujitangaza kupitia jitihada za Jumuiya ya Wanawake Uingereza (TAWA) ukishirikiana na Ubalozi ni mseto wa wafanyabiashara wakongwe na vijana wanaoanza fani hii ya urembo. Mama Joyce Kallaghe-pic by Felipe Camacho 
  Mama Joyce Kallaghe, ni mtangazaji mzuri wa mavazi ya Kitanzania ughaibuni. Picha na Felipe Camacho. Akifungua shughuli hii, mkewe Balozi, Mama Joyce Kallaghe alikumbusha hii ni nafasi nzuri kwetu. “ London Fashion Week” ni tafrija maarufu inayofanyika sambamba Paris, New York, Milan mwezi Februari na Septemba kila mwaka toka 1984. Mbali na msaada wa TAWA na Ubalozi, mwekezaji mkuu wa shughuli hii ni British Council- shirika linaloendeleza vipaji nchi zaidi ya 100 duniani kwa miaka 75 sasa. Mada ya maonesho iliitwa “Fahari Passion 2013” na mchoro wake uliobuniwa na Bi. Sara Abood unaonyesha uso wa mwanamke na rangi za bendera ya taifa.
Khanga dress tight 
Khanga inavyojigamba na kupendeza. Picha na Abubakar Faraji

MZAZI MWENZA WA MTOTO HUYU ANAMTAFUTA MWANAE

$
0
0
7 months ago I gave birth to twin boys. They are the most precious little guys you can imagine. I need your help. The guy I had these wonderful babies with are unknown to me, and he does not know about the twins. Therefore I need all of your help to pass this forward. The boy in the picture is the man I'm looking for - Todau he his 25 years old and that picture is the only one I have.

He is half danish and half tanzanian. I don't have much information about him, only that his mother is from Tanzania and his father is Danish and he lives in Denmark. If this reach you, if I'm that lucky, please I want you to know that I'm not here to claim anything.

I just want you to get a chance to get to know them, because they are awesome. Please you guys, this is important to me, share this and hopefully someday this will pass the eyes of someone that recongnize him in some way or even someone that knows him and can pass this on to him directly. If you know anything about the man in the picture, please contact me. Send me a PM or an email - needyourhelpdenmark@gmail.com

Share this, like it or comment so as many people as possible can see this.

I will be foreller greatful to you.

UJUMBE WA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA TANGA MH CHIKU GALAWA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Chiku Galawa akimkaribisha Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mh. Jaji Aloysius Mujulizi ofisini kwake mkoani Tanga.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Chiku Galawa akiwa na ujumbe wa Tume ulioongozwa na Mwenyekiti Mh. Jaji Mujulizi (wa pili kushoto), Katibu Mtendaji wa Tume Bi. Winfrida B. Korosso ( wa pili kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Bw. Peter Kalonga ( wa kwanza kushoto) na Katibu Msaidizi wa Tume Bi. Agnes Mgeyekwa.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Bw. Benedict Ole Kuyan akizungumza wakati Katibu Mtendaji wa Tume Bi. Winfrida Korosso alipomtembelea ofisini kwake mkoani Tanga wakati Tume ikiwa katika Kikao chake cha Baraza la Wafanyakazi mkoani humo, Kulia ni Katibu Msaidizi wa Tume Bi. Agnes Mgeyekwa (Picha Zote na Munir Shemweta- LRCT)

EAC ELECTION OBSERVER MISSION TO THE 16th -18th SEPTEMBER 2013 PARLIAMENTARY ELECTIONS IN THE REPUBLIC OF RWANDA

$
0
0
The East African Community's Observer Mission has issued a preliminary statement on the Parliamentary Elections in the Republic of Rwanda which took place 16th – 18th September 2013.

The Mission was in the country at the invitation of the Government of Rwanda and the National Electoral Commission. It was led by Hon. Musa Sirma, Former Minister for EAC Affair’s, Republic of Kenya and comprised 40 members drawn from the East African Legislative Assembly (EALA), Electoral Management Bodies (EMBs), Civil Society Organisations (CSOs), and National Human Rights Commissions from 4 EAC countries namely Burundi, Kenya, Tanzania and Uganda.

The Mission’s assessment of the elections was primarily based on the Constitution and other legislation governing elections in Rwanda. The assessment was also predicated on international principles and standards governing the conduct of democratic elections including the African Charter on Democracy, Elections and Governance (2007) and the EAC Principles for Election Observation and Evaluation (2012).

The Mission's preliminary statement (attached) contains preliminary findings, recommendations and conclusions made by the Mission based on independent observation, interaction with electoral stakeholders including the National Electoral Commission, political parties, civil society organisations, security agencies, the media, international and domestic observers present in Rwanda, among others. As the electoral process is still ongoing, this statement limits itself to the assessment made upto the three-day polling and counting processes, as at 18th September 2013.

Having consulted with stakeholders from 9th – 13th September, on 14th September 2013, eight teams of Observers were deployed to all the five provinces of Rwanda. Each team was equipped with questionnaires as an aid for systematic collection of data on activities pertaining to pre-polling, polling and counting processes as well as announcement of provisional results.

RAIS SHEIN WA ZANZIBAR AZINDUA MADRASA HIDAYA-TUL ISLAMIYA KIDOTI

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekliti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akikata utepe kuzindua Madrasa Hidayatul Islamia katika Kijiji cha Kidoti Wilaya ya Kaskazini A Unguja,(kulia) Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Pembe Juma Pembe.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekliti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) akifuatana na Mkuu wa Ujenzi wa Madrasa Hidayatul Islamia,Salim Yussuf Mohamed,(kushoto) na Mwalimu Mkuu wa madrasa hiyo Makame Ali Juma,(kulia) pamoja na Viongozi wengine wakati walipotembelea sehemu mbali mbali za madrasa hiyo baada ya kuifungua Rasmi leo huko katika Kijiji cha Kidoti Wilaya ya Kaskazini A Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekliti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipokuwa akizungumza na Wananchi na Wanafunzi wa madrasa Hidayatul Islamia ya Kidoti Wilaya ya Kaskazini A Unguja,Mkoa wa Kaskazini iliyojengwa kwa ufadhili wa wahisani mbali mbali na Nguvu za Wananchi wenyewe.
iongozi waliohudhuria katika ufunguzi wa Madrasa Hidayatul Islamia katika kijiji cha Kidoti Wilaya ya Kaskazini A Unguja,(kutoka kulia) Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Juma Haji Juma,Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum,Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein,Mke wa Makamo wa Pili wa Rais Mama Asha Suleiman Iddi,na Waziri wa Ardhi,Maji,Makaazi na Nishati Ramadhan Abdalla Shaaban,nwakiwa katika hafla ya ufunguzi wa Madrasa Hidayatul Islamia katika kijiji cha Kidoti Wilaya ya Kaskazini A Unguja,uliofanyika leo kijijini hapo.
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Kidoti waliohudhuria katika hafla ya ufunfuzi wa Madrasa Hidayatul Islamia katika kijiji cha Kidoti Wilaya ya Kaskazini A Unguja,uliofanyika leo kijijini hapo,wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekliti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuifungua madrasa hiyo.
Wanafunzi wa Madrasa Hidayatul Islamia ya Kidoti Wilaya ya Kaskazini A,Mkoa wa Kaskazini Unguja,wakiwa katika sherehe za Ufunguzi wa Madrasa yao iliyofunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekliti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao baada ya kuifungua rasmi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Article 23

$
0
0
SERENGETI FREIGHT FORWARDERS LTD
END OF YEAR OFFER!
SALE!         SALE!       SALE!
TUMEPUNGUZA BEI ZA KUSHIP MAGARI KWENDA DAR/MOMBASA
4 X 4 CARS TO MOMBASA NOW FROM  £800
SALOON CARS NOW FROM £700
4 X 4 CARS TO DAR NOW FROM £820
SALOON CARS TO DAR NOW £720
40'HC CONTAINER TO DAR FROM £1850 (this is £500 less )
20' CONTAINER TO DAR/MOMBASA FROM £1,350
BEI ZETU NI ZA KINDUGU WALA HAZINA KIGUGUMIZI
TUNATOA  25 DAYS FREE STORAGE IN MOMBASA
TELEX RELEASE KWA MOMBASA NI FREE

AIR CARGO TO DAR NOW £3.80
INCLUSIVE CLEARANCE
SIMPLY THE BEST IN BUSINESS
WE PROMISED, WE DID IT AND WE ARE MAKING IT EVEN BETTER!
KUCHUKUA MZIGO WAKO DAR ES SALAAM 
MPIGIE AGENT WETU DAR; TORNADO LUKOSI TEL; 0713607116
MZIGO UNANDOKA KILA IJUMAA

ONCE YOU PAY HERE IN UK YOU DONT PAY ANYTHING IN TANZANIA
UKIISHA LIPA UK UNAKWENDA KUCHUKUA ILALA DAR BILA KULIPA TENA

FLIGHTS EVERY WEEK

KWA WALE WANAOTAKA KUNUNUA VITU UK TUTUMIE EMAIL AU TUPIGIE
MINIMUM WEIGHT IS 40K HANDLING/ADMIN FEE £20
KABLA HUJATULETEA MZIGO HAKIKISHA UMEANDAA ORODHA YA VITU UNAVYOTAKA TUKUSAFIRISHIE NA
 NI LAZIMA TUUFUNGUE MZIGO NA KUHAKIKISHA UNACHOSAFIRISHA . KAMA HAUNA PACKING LIST HATUTASAFIRISHA MZIGO.
OUR AGENT IN DAR; TORNADO TEL; +255 713607116

Tupigie kwa namba hizo hapo chini au  tutumie email tafadhali

SIMON  LOUIS +44 (0) 79 506 89 243

HQ -  UNIT 92 THAMES INDUSTRIAL PARK, PRINCESS MARGARET ROAD, EAST TILBURY, RM18 8RHRH
Tell (+44) 01375 855917  Fax (+44) 01708202477

Article 22

KINANA KUKOMESHA UMANGI MEZA WA WATUMISHI WA CHAMA NA SERIKALI

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Ndgugu Stephen Wassira mara baada ya kukagua mradi wa kusambaza maji kwa wilaya ya Bunda
Katibu Mkuu wa CCM akipokelewa na wananchi wa kata ya Kibara katika jimbo la Mwibara alipotembelea kuona jinsi ilani ya uchaguzi inatekelezwa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kuashiria kufungua kwa mradi wa kujenga chuo cha ufundi fundi Stadi katika jimbo la Mwibara,kulia ni mbunge ndugu Kange Ligora na kushoto ni mwenyekiti wa CCM mkoa ndugu Christopher Sanya.

RAIS KIKWETE ATUNUKIWA SHAHADA YA UZAMIVU YA CHUO KIKUU CHA GUELPH JIMBONI ONTARIO, CANADA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe kuelekea ukumbini kutunukiwa Shahada Ijumaa Septemba 20, 2013.
Nyimbo za taifa zikipigwa wakati wa sherehe za kumtunuku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aki Shahada ya Uzamivu katika Chuo Kikuu Guelph jimboni Ontario, Canada, Ijumaa Septemba 20, 2013.
Sehemu ya umati ulioshuhudia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kutunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Chuo Kikuu cha Guelph jimboni Ontario Ijumaa Septemba 20, 2013.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akitunukiwa Shahada ya Uzamivu na Provost na Makamu wa Rais wa Chuo Kikuu cha Guelph jimboni Ontario, Dkt Maureen Mancuso , Ijumaa Septemba 20, 2013.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

WAZIRI DK. NCHIMBI AMTEMBELEA PADRI ALIYEMWAGIWA TINDIKALI HOSPITALI YA MUHIMBILI LEO

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akisalimiana na Padri Joseph Monesmo Magamba wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui, alipofika katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam kumpa pole, baada ya kumwagiwa tindikali na watu wasiojulikana katika Mtaa wa Mlandege Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar wiki iliyopita. Dk Nchimbi alimtoa hofu Padri huyo akimuahakikishia kuwa waliofanya tukio hilo watakamatwa, na serikali itapambana kikamilifu na mtu au kikundi chochote kitakachojihusisha na vitendo vya uhalifu wa kutumia kemikali ya tindikali.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akimsikiliza Padri Joseph Monesmo Magamba,wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui, akitoa maelezo jinsi alivyopata mkasa wa kutiwa Tindikali na watu wasiojulikana, Mjini Unguja, Zanzibar alipofika katika Hospitali ya Muhimbili kumpa pole, ambapo amelazwa na kuapatiwa matibabu. Dk Nchimbi alimtoa hofu Padri huyo akimuahakikishia kuwa waliofanya tukio hilo watakamatwa, na serikali itapambana kikamilifu na mtu au kikundi chochote kitakachojihusisha na vitendo vya uhalifu wa kutumia kemikali ya tindikali.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akimuhakikishia Padri Joseph Monesmo Magamba wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui, Zanzibar jinsi wizara yake itakavyopambana kwa kuwakamata wale wote watakaojihusisha na vitendo vya uhalifu wa kutimia kemikali ya tindikali. Dk Nchimbi alifika hospitalini. Dk Nchimbi alifika katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam kumpa pole padri huyo ambaye anatarajiwa kupelekwa nchini India kwa ajili ya kupata matibabu zaidi. Hata hivyo, Dk Nchimbi alimtoa hofu Padri huyo akimuahakikishia kuwa waliofanya tukio hilo watakamatwa, na serikali itapambana kikamilifu na mtu au kikundi chochote kitakachojihusisha na vitendo vya uhalifu wa kutumia kemikali ya tindikaliPicha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Viewing all 110160 articles
Browse latest View live




Latest Images