Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109610 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU ACHUKIZWA NA WANAFUNZI KUKATISHWA MASOMO

0
0

*Ni baada ya wanafunzi 72 wa kike kupewa ujauzito wilayani Nyang’hwale

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amechukizwa na vitendo vya watoto wa kike kukatisha masomo yao kwa kupata ujauzito wilayani Nyang’hwale ambapo jumla ya wanafunzi 72 wamepata ujauzo katika kipindi cha miaka mitatu cha kuanzia mwaka 2016 hadi 2018.

Kutokana na wilaya hiyo kuwa na idadi kubwa ya watoto wa kike wanaokatisha masomo kutokana na ujauzito, Waziri Mkuu amemuagiza Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale Hamim Gwiyama kufanya operesheni katika kila kijiji na kubaini waliowapa wanafunzi ujauzito na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumatano, Novemba 28, 2018) alipozungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba, ,kijiji cha Kalumwawilaya ya Nyang’hwale, akiwa katika ziara yake mkoani Geita.

“Jambo lingine litakalowawezesha kukabiliana na tatizo la ujauzito kwa wanafunzi wa kike ni kuanzisha miradi ya ujenzi wa mabweni ili watoto wa kike waweze kusoma bila ya kupata vishawishi vinavyosababisha wao kupata ujauzito.”

Waziri Mkuu alisema Serikali haiwezi kuacha jambo hilo likiendelea, hivyo aliwataka wananchi washirikiane katika kuwalinda watoto wa kike na Serikali itawachukulia hatua watendaji wote ambao katika maeneo yao watoto wa kike watabainika kuwa na ujauzito.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

DC MURO AENDELEA KUPAMBANA NA MGOGORO WA CHUO KIKUU CHA MOUNT MERU SAFARI HII ATOA YA MOYONI KWA WAZIRI WA KAZI MHE MHAGAMA

0
0
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro ameendelea na juhudi zake Za utatuzi wa migogoro na safari hii amemuomba Mhe Jenista Mhagama ambae ni Waziri wa Nchi ofisi ya waziri Mkuu anaeshughulikia masuala ya kazi kuingilia kati mgogoro huo ili kunusuru hatima Za maisha ya wafanyakazi wanaodai mishahara Kwa miezi tisa sasa .

Hatua ya Dc Muro imekuja Mara baada ya wafanyakazi hao kuvamia ziara ya Mhe Mhagama akiwa katika Wilaya ya Arumeru wakati wa Uzinduzi wa kongamano la maafisa Maendeleo ya jamii nchini ambapo Mara baada ya kutembelea mabanda ya maonyesho kundi la wafanyakazi wa chuo Cha Mount meru lilimvamia Mhe Waziri Mhagama wakiwa na mabango wakitaka kujua hatima ya madai yao ambayo Mhe Mkuu wa Wilaya ya Arumeru amekuwa akipambana kuwasaidia wafanyakazi hao pasipo kuchoka.

Kutokana na tukio hilo, ilimlazimu Mhe Mhagama kutoa maelekezo kwa kamishna wa kazi nchini ambae alimtaka kuunda kamati ya wataalamu kutoka wizarani ambayo itaungana na Mhe Jerry Muro Mkuu wa Wilaya ya Arumeru katika kuhakikisha changamoto hiyo inatatulia haraka iwezakanavyo hatua ambayo ilipokelewa Kwa shangwe na wafanyakazi wa chuo kikuu Cha Mount ~Meru.
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro ameendelea na juhudi zake Za utatuzi wa migogoro na safari hii amemuomba Mhe Jenista Mhagama ambae ni Waziri wa Nchi ofisi ya waziri Mkuu anaeshughulikia masuala ya kazi kuingilia kati mgogoro huo ili kunusuru hatima Za maisha ya wafanyakazi wanaodai mishahara Kwa miezi tisa sasa .
 
 Baadhi ya Wafanyakazi wakiwa wamebeba mabango yao yenye jume mbalimbali.
 

WAKAZI WA PANGANI HUKO KIBAHA MJINI WACHOSHWA NA MASHAMBA PORI YANAYOTUMIKA KUWA VIFICHO VYA UHALIFU

0
0
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA 

BAADHI ya wananchi wa kata ya Pangani ,Kibaha Mjini mkoani Pwani, wameitaka serikali ya wilaya na mkoa kuangalia namna ya kufuta umiliki wa mashamba makubwa ambayo hayaendelezwi na kusababisha kutumika kama vificho vya wahalifu na kuokotwa miili ya wafu na walionusurika kufa.

Wameeleza kwa kipindi cha miezi sita miili zaidi ya kumi zimeokotwa kwenye mtaa huo ambapo kati yao wengine walinusurika kifo na kuokolewa na wengine wakiwa wamefariki dunia. 

Diwani wa kata ya Pangani , Agustino Mdachi aliyasema hayo kufuatia mwili wa mtu mmoja mwanaume aliyekufa kuokotwa kwenye mtaa wa Pangani .Alieleza ifikie wakati wamiliki hao wasiangaliwe nyadhifa ama majina yao ili kunusuru maisha ya watu. "Miili ya watu imekuwa ikiokotwa mara kwa mara,wengine wanaookolewa wakiwa wametupwa hivyo tunaitaka serikali kuyafutia hati mashamba haya ili yagawiwe kwa wananchi waweze kuyaendeleza likiwemo shamba la serikali la mifugo la Mitamba", alisema Mdachi.

Hata hivyo Mdachi alisema ,wameshachukua hatua ya kuwaita wamiliki wa mashamba hayo ili kuwaeleza vitendo vinavyotokea lakini baadhi yao wamekuwa hawajitokezi .

Nae mwenyekiti wa mtaa wa Pangani Jitihada Ndiali alisema,eneo hilo kwa sasa limefanywa kama dampo au sehemu ya kutupia maiti pia madereva bodaboda kuporwa pikipiki zao kisha kutupwa .Mwenyekiti wa mtaa wa Miwale ,Amos Mkwawa alisema kuwa maeneo hayo pia ni changamoto kwa wanafunzi wa kike ambao wapo hatarini kubakwa.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka aliwaomba wamiliki husika kujitokeza kwenda kuyaendeleza maeneo yao. Jitihada za kumtafuta kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP )Wankyo Nyigesa ili aeleze ama kuthibitisha kuhusu maiti hiyo iliyookotwa hazikuzaa matunda kutokana na kuwa kikaoni.
 BAADHI ya wananchi wa kata ya Pangani ,Kibaha Mjini mkoani Pwani, wakiwa kwenye mkutano wao kuhusu serikali ya wilaya na mkoa kuangalia namna ya kufuta umiliki wa mashamba makubwa ambayo hayaendelezwi na kusababisha kutumika kama vificho vya wahalifu na kuokotwa miili ya wafu na walionusurika kufa.

WAZIRI UMMY AAGIZA HOSPITALI ZOTE ZA RUFAA ZA MIKOA KUTOA MATIBABU YA KINYWA NA MENO.

0
0
Na WAMJW - MARA.

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amemwagiza Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya kuhakikisha kuwa kabla ya March 30, 2019 Hospitali zote za Mikoa kutoa Huduma za matibabu ya kinywa.

Ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano wa Mwaka wa Madaktari wa Kinywa wenye lengo la kujadili njia bora za kuboresha huduma za Afya ya kinywa na meno na namna ya kuikuza kada hiyo, tukio lililofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Waziri Ummy alisema kuwa "hatuwezi kusema kuwa Afya ya kinywa na meno ni muhimu alafu leo ni Hospitali za rufaa za Mikoa 10 kati ya 28 ndio zinavitendea kazi" alisema Waziri Ummy.Pia Waziri Ummy aliwahasa Wananchi kupambana dhidi ya magonjwa ya kinywa na meno kwa kujiepusha matumizi ya sigara, tumbaku, unywaji wa pombe kupita kiasi, ulaji wa vyakula na vinywaji vyenye sukari.

"Magonjwa ya kinywa na meno yana visababishi vyake ikiwemo uvutaji wa sigara,sigara, tumbaku, unywaji wa pombe kupita kiasi, ulaji wa vyakula na vinywaji vyenye Sukari" alisema Waziri Ummy.Kwa upande mwingine Mhe. Ummy amewataka madaktari wa kinywa na meno kuwahamasisha wananchi ili kufahamu umuhimu wa kupiga mswaki japo mara mbili kwa siku ili kujiepusha katika hatari yakupata magonjwa ya kinywa na meno.

"Mnatuambia kwamba angalau tupige mswaki mara mbili kwa siku, hapo mnakazi kubwa sana ya kutushawishi, hivyo niwaombe tushirikiane nasi ili kuhakikisha kwamba tunaongeza elimu na hamasa kwa jamii katika suala hiki" alisema Waziri Ummy.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiambatana na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Mara, wakiendelea na ukaguzi wa jengo la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa inayoendelea kujengwa.
 Muonekano wa Jengo la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara inayoendelea kujengwa, ikiwa ni jitihada   za Serikali ya awamu ya tano kuboresha Sekta ya Afya nchini.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu (aliyesimama katikati) akiteta jambo na kamati kuu ya usalama ya Mkoa iliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe.Adam Malima wakati wa ukaguzi wa jengo la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara inayoendelea kujengwa.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee hma Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Madaktari wa Afya ya kinywa na meno (hawapo kwenye picha) wakati akifungua mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Zaidi ya wahitimu 297 wamehitimu katika Chuo cha VETA Kihonda

0
0
Zaidi ya wahitimu wapatao 297 katika chuo cha VETA Kihonda wamehitimu mafunzo yao katika fani mbalimbali miongoni mwao wavulana 49 na wasichana 248,mahafali hayo yalifanyika  katika chuo cha VETA Kihonda mnamo tarehe 23,November 2018,Mahafali hayo yaliuzuriwa na Mgeni rasmi ndugu Beda Marwa Mjumbe wa bodi ya VETA kanda ya mashariki.

Akizungumza wakati wa Mahafali hayo aliyekuwa Mgeni rasmi katika mahafali hayo ndugu Beda Marwa ambaye ni Mjumbe wa bodi ya kanda ya Mashariki aliwaomba wanafunzi watumie vizuri elimu waliyo pata ya Ubunifu kwa kuzalisha bidhaa zenye ubora wa hali ya juu ili kushindana na mafundi wengine walio wazoefu.

Alisema taifa linatambua umuhimu wa kuwepo kwa Vyuo vya Ufundi Stadi vyenye kuwaandaa wataalamu katika nyanja mbalimbali za ufundi.  Alisema Vyuo hivi ni sehemu muhimu ya kuwaandaa vijana kukabiliana na soko la ajira, na vijana kupata ujuzi wa kujiajiri wao wenyewe.

Marwa aliwaomba wanafunzi kutambua ya kwamba kazi nyingi za mafundi ni kazi zinazoonekana kwa kila mtu hivyo kama watakuwawanafanya vizuri kazi zao na kwa kiwango cha juu kizuri tayari inaweza kuwa ni  sehemu mojawapo ya kujitangaza na kujipatia ajira binafsi kwa urahisi zaidi.
Naye Mkurugenzi wa VETA kanda ya Geofrey Sabuni aliwapongeza vijana kwa kufikia hatua nzuri kimaisha ya kumaliza masomo yao katika chuo cha VETA Kihonda na kuwashauli kwenda kuwa mabarozi wazuri huko mtaani waendako katika kuitangaza VETA.
Mr.Sabuni alisema jukumu kwabwa la VETA ni kuhakikisha wanawaandaa wanafunzi kuwa mafundi bora katika ujenzi wa taifa,
Aliongeza kwa kusema  VETA wanajitahidi katika kuhakikisha tunaandaa watu mahili wa kufanya kazi kwa kuhakikisha wanaa andaa mitahara inayo endana na mabadilioko ya soko la ajira kwa kuhakikisha vyuo vya VETA vinakuwa na  ,walimu wa kutosha,pomoja na Vitendea kazi mazubuti.
Naye kaimu Mkuu wa Chuo cha VETA Kihonda ndugu Kashindye k.Maganga alisema nimatarajio ya Chuo kutokana na mafunzo waliyoyapata wahitimu, wanatarajia watakuwa wabunifu, waangalifu,waaminifu,hodari na watakuwa tayari kujiendeleza kwa mafunzo ya ngazi nyingine za masomo.

aliongeza kwa kusema katika kuhakikisha wanawafikia Vijana wengi zaidi hasa katika fani zile zenye huitaji zaidi chuo kimeanzisha program ya wanafunzi wa mchana (Evening Class) katika fani za umeme wa magari, umeme wa majumbani, ufundi wa magari, ufundi wa bomba na ukerezaji wa vyuma.

Maganga alisema “chuo kimeweza Kuongezeka udahili kwa wafunzi wa kozi ndefu na fupi, kutoka idadi ya wanafunzi 480 hadi 600 kwa kozi ndefu na kutoka wanafunzi 970 hadi 1,200 kwa kozi fupi kwa mwaka”.

Maganga alichukua fursa hiyo kuishukuru Serikali kwa kuweza kuwapatia vifaa mitambo ya kisasa ya  kufundishia katika fani ya Kilimo (Agro-Mechanics) na kuhahidi kuvitumia kwa uhangalifu lakini pia kuitumia kufanya uzalishaji wa mazao mbali mbali katika chuo hicho pamoja na kuwafundishia wanafunzi.

WIKENDI LIVE HAPPENINGS THIS SATURDAY AY NAFASI ART SPACE DAR ES SALAAM

WAZIRI WA AFYA UMMY ATOA MAAGIZO UPATIKANAJI WA VIFAA TIBA ZA KINYWA NA MENO

0
0
Na Frankius Cleophace Mara
Waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto. Ummy Mwalimu  amemuagiza katibu mkuu wa afya kuhakikisha kila Hospital za Rufaaa za Mikoa  yote Tanzania  kuwa na vifaa tiba  vya kinywa na meno kabla  ya machi 30, 2019.

Kauli hiyo imetolewa wakati akifungua mkutano wa madaktari bingwa wa kinywa na meno Tanzania katika ukumbumbi wa mwekezaji wa mkuu wa mkoa wa Mara. Waziri ummy amesema kuwa kufanya hivyo nikuhakikisha wanaondoa changamoto katika hospitali zote nakuowaondolea wananchi usumbufu  wanaoupatapa kipindi wakitembea  zaidi ya kilomita 200 kuitafuta huduma ya kinywa na meno.

Pia amesema kuwa lengo la serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inawahudumia na kuwajali wananchi wote nakuhakikisha wanapata huduma zote katika maeneo yaliyokaribu nao ambapo amewakikishia Madaktari bingwa kuanzia hospital za wilaya katika mkutano ujao itakuwa tayari wameshatekeleza adhima hiyo. Naye mkuu wa Mkoa wa Mara Adamu Malima amewapongeza madkatari Bingwa wa kinywa na meno kwa kuupa kipaumbele Mkoa wa Mara katika utaoji wa huduma hiyo huku akimuomba waziri kuangalia namna ya kusaidia wananchi wa mkoa huo katika utoaji wa huduma hiyo.

Awali akitoa Taarifa mbele ya waziri wa Afya Rais wa madaktri wa kinywa na meno Ambege Mwakatobe amesema kuwa pamoja na jitihada zao zote wanakwamishwa na changamoto ya upungufu wa watalamu wa kinywa na meno ambapo baadhi ya maeneo Nchini Tanzania yanakosa upatikanaji wa huduma hiyo  pia hakuna chuo ambacho kinafundisha wahudumu hao wa kinywa na meno. Zoezi la kuendelea kutoa huduma ya tiba ya kinywa na meno kwa baadhi ya Maeneo katika wilaya za Mkoa wa Mara zinaendelea ili kuweza kuwanusuru wagonjwa wa Meno.
 Waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu akizungumza na madaktari katika mkutano wa madaktari bingwa wa kinywa na Meno uliofanyika katika ukumbi wa Mwekezaji Mkani Mara.
  Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima akiongea na madaktari hao katikati ni Waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu na wakwanza kulia ni Rais wa madaktri wa kinywa na meno Ambege Mwakatobe.
 Rais wa madaktri wa kinywa na meno Ambege Mwakatobe  akizungumza katika mkutano huo.
 Daktari Merina Njelekela ambaye ni mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi  akiongea katika Mkutano huo wa madakri bingwa wa kinywa na Meno uliofanyika mkoani Mara.

Dk Mpango afagilia ripoti ya maendeleo ya binadamu

0
0
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Phillip Mpango amesema Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu nchini Tanzania ya Mwaka 2017 (THDR) inayozungumzia  “Sera ya Kijamii Katika Muktadha wa Mageuzi ya Kiuchumi”, ina mchango mkubwa katika kuchambua masuala yanayohusu maendeleo ya binadamu na nafasi yake katika uandaaji wa mipango ya maendeleo, utengenezaji wa bajeti, ufuatiliaji na tathmini.

Alisema hayo katika hotuba yake iliyosomwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Khatibu Kazungu wakati wa uzinduzi wa ripoiti hiyo mjini Dodoma jana.“Kwa mtazamo wangu, dhana hii ya kufungamanisha maendeleo ya watu na mageuzi ya kiuchumi sio tu kwamba ni dhana sahihi bali pia inaendana na Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2016/17 – 2020/21.’ Alisema Dk. Mpango .

Aidha, alisema dhana ya kufungamanisha maendeleo ya watu na mageuzi ya kiuchumi ni dhana ambayo imekuwa ikizingatiwa katika mipango ya ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka mmoja mmoja pamoja na miongozo ya uandaaji wa bajeti za serikali.

Dk. Mpango alisisitiza kwamba kwa kuzingatia umuhimu wa kujenga uchumi jumuishi, kutokuacha mtu yeyote nyuma katika mchakato wa maendeleo na kufungamanisha maendeleo ya watu na mageuzi ya uchumi, serikali ya Tanzania imetoa umuhimu mkubwa katika utoaji wa huduma za jamii ili kuinua hali za watu wake.Waziri Mpango alisema kwamba sekta ya afya, elimu na miradi ya kimkakati kama ujenzi wa reli ya kisasa ni sehemu ya juhudi zinazofanya kuwezesha uchumi jumuishi.
 Mshehereshaji George Mulamula (kushoto) wa uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya Tanzania (THDR) ya mwaka 2017 akiitambulisha meza kuu wakati wa hafla ya uzinduzi huo uliofanyika ukumbi wa mikutano wa Kambarage kwenye jengo la Treasury Square mjini Dodoma. Kutoka kulia kwenda kushoto ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bi. Natalie Bouckly, Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Khatibu Kazungu, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida pamoja na Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa ESRF, Prof. Sylvia Temu.
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Khatibu Kazungu akisoma hotuba ya ufunguzi kwa niaba ya Waziri mwenye dhamana ya wizara hiyo Dkt. Phillip Mpango wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya Tanzania (THDR) ya mwaka 2017 uliofanyika ukumbi wa mikutano wa Kambarage kwenye jengo la Treasury Square mjini Dodoma.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akitoa neno la ukaribisho kwa mgeni rasmi na wageni waalikwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya Tanzania (THDR) ya mwaka 2017 uliofanyika ukumbi wa mikutano wa Kambarage kwenye jengo la Treasury Square mjini Dodoma.
 Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bi. Natalie Bouckly ambao ni wafadhili wa ripoti hiyo akitoa salamu za Umoja wa Mataifa wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya Tanzania (THDR) ya mwaka 2017 uliofanyika ukumbi wa mikutano wa Kambarage kwenye jengo la Treasury Square mjini Dodoma. Kulia ni Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa ESRF, Prof. Sylvia Temu.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

IDARA YA MAKUMBUSHO NA MAMBO YA KALE ZANZIBAR IMAWAGA WAFANYAKAZI WALIOMALIZA MUDA WA KUFANYA KAZI

0
0
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale  anaeshughulikia masuala ya Habari Dkt. Saleh Yussuf Mnemo akizungumza katika khafla ya kuwaaga wafanyakazi hao iliofanyika  ukumbi wa Palace Museum Forodhani Mjini Zanzibar.
 Mkurugenzi  Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale Zanzibar Salum Kitwana Sururu akitoa shukurani zake kwa Wafanyakazi hao (hawapo pichani) na kuwatakia kheri katika maisha yao.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar  anaeshughulikia masuala ya Habari  Dkt. Saleh Yussuf Mnemo akimkabidhi cheti maalum Bi. Jokha Ali Simba mmoja ya wafanyakazi waliostahafu Idara ya Makumbusho ya Mnazimmoja Mjini Zanzibar.
 Katibu Mkuu Chama cha Wafanyakazi Zanzibar (ZAPSU) Mwatumu Khamis Othman akimkabidhi saa ya ukutani mzee  Mussa Vuai Pakia  katika khafla ya kuwaaga wafanyakazi hao iliofanyika  ukumbi wa Palace Museum Forodhani Mjini Zanzibar.
 Baadhi ya Wafanyakazi wa  Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale waliohudhuria katika ghafla ya kuwaaga wafanyakazi wenzao waliomaliza muda wa kufanya kazi katika Idara hiyo.
 Wafanyakazi walioangwa baada ya kumaliza utimishi wao wa kazi katika Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale Zanzibar.
Picha na Abdalla Omar Habari  -  Maelezo Zanzibar.

Introducing "Doin It Refix" by P Mawenge Feat Tifa Flow...

Introducing "SAFARI" (Official Audio) by AY feat King Kikii

0
0
#SAFARI, Ay feat King KiKi, Produced by Marco Chali, Mj Records.

KORTI YATAKA UPELELEZI KESI YA UHUJUMI UCHUMI INAYOMKABILI ALIYEKUWA MFANYAKAZI MSTAAFU TAZAMA,WENZAKE UKAMILIKE MAPEMA

0
0
Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa utetezi katika kesi ya kesi ya Uhujumu uchumi inayomkabili mfanyakazi mstaafu wa Shirika la Mafuta Tanzania na Zambia(Tazama), Samwel Nyakirang'ani(63) na wenzake 11 kukamilisha mapema upelelezi dhidi ya kesi hiyo ili kigundua nani anahusika na nani hausiki kwenye kesi hiyo.

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ameeleza hayo leo Novemba 29, 2018 wakati kesi hiyo ilipokuja kwa kutajwa.

Kabla ya kueleza hayo Wakili wa Serikali Patrick Mwita alidai kuwa upelelezi katika shauri hilo haujakamilika, jalada bado lipo katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), kwa ajili ya kulichambua na kisha kulitolea maamuzi kuangalia washtakiwa gani washtakiwe na washtakiwa gani waachiwe huru.

Kutokana na hayo, Hakimu Simba ameutaka upande wa mashtaka wajitahidi kumaliza shauri hilo mapema kwani shauri lenye watu wengi kama hili ni vema ikajulikana mapema kwani inawezekana baadhi yao hawahusiki.Nyakirang’anyi na wenzake wanakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kujiunganishia isivyo halali bomba la mafuta, mali ya Mamlaka ya Bandari Tanzania ( TPA), katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu

 Kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 10 kwa ajili ya kutajwa na kuangalia upelelezi kama utakuwa umekamilika ama la.Washtakiwa wote wapo rumande kutokana DPP kuwasilisha hati ya kuzuia dhamana.Mbali Samweli, washtakiwa wengine katika kesi  hiyo namba 1/2018 ni Nyangi Mataro( 54) Mwalimu wa Shule ya  Msingi Ufukoni na mkazi wa Kisiwani Mkajuni Kigamboni.

Mfanyabaishara, Farijia Ahmed(39)mkazi wa Soko Maziwa Kigamboni, Malaki Mathias(39) mkazi wa Magogoni, Kristomsi Angelus(25) mkazi wa Soko Maziwa,  Fundi Ujenzi Pamfili Nkoronko(40) mkazi wa Tungi Kasirati na Henry Fredrick (38) mkazi wa Tungi Kigamboni.Wengine ni Audai Ismail (43) ambaye ni mkazi wa Kibaha, Chibony Emmanuel, Roman Abdon, Amina Shaban na Zubery Ally.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka matatu ya uhujumu uchumi kwa  kujiunganishia isivyo halali bomba la mafuta, kinyume cha sheria  ya Uhujumu uchumi.Katika shtaka la kwanza, kati ya mwaka 2015 hadi Januari 8, 2018 katika eneo la Tungi Muungano wilaya ya Kigamboni, washtakiwa kwa pamoja wanadaiwa kujiunganishia bomba la mafuta ya dizeli lenye upana wa inchi moja kutoa katika bomba lenye upana wa inchi 24, bila kuwa na kibali kutoka Mamlaka ya Bandari nchini(TPA).

Pia wanadaiwa kuharibu miundo mbinu ambapo wanadaiwa kutoboa  bomba la hilo, ambalo  lilikuwa likitumika kufirisha mafuta,  mali ya Mamlaka ya Bandari nchini( TPA).Aidha washtakiwa wanadaiwa kuharibu  bomba la mafuta mazito( Crude oil) lenye upana wa Inchi 28, ambalo lilikuwa likitumika kusafirisha mafuta ghafi, mali ya Mamlaka ya Bandari nchini( TPA).

wafanyakazi bora wa mwezi Oktoba wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wapongezwa

0
0
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Happiness Kusekwa akipokea zawadi ya Daktari bora wa mwezi Oktoba kutoka kwa Mkurugenzi wa Tiba ya Moyo na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo Peter Kisenge wakati wa hafla fupi ya utoaji zawadi kwa wafanyakazi bora iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo. Zawadi hizo zilitolewa na kampuni ya dawa za binadamu ya Samiro
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Huduma ya Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akimkabidhi zawadi ya mfanyakazi bora wa mwezi Oktoba Afisa Muuguzi Msaidizi Keyness Erasmus Mng’anya wa JKCI wakati wa hafla fupi ya utoaji zawadi kwa wafanyakazi bora iliyofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo. Zawadi hizo zilitolewa na kampuni ya dawa za binadamu ya Samiro. Picha na: Genofeva Matemu - JKCI

NMB YAMWAGA MSAADA WA VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU ZA JWTZ, WANAJESHI WATOA TAMBO

0
0

TIMU za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zimepokea msaada wa vifaa vya michezo kwa ajili ya kuboresha timu zao mbalimbali zinazoshiriki katika Ligi Kuu Bara na michuano ya mbalimbali ya majeshi.

Msaada huo wenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 10 umetolewa na Benki ya NMB Tanzania, leo Jumatatu jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Kanali Damian M. Majare ambaye ni Kaimu Mwenyekiti wa Kanda ya Ngome.Akizungumza katika hafla hiyo, Kanali Damian M. Majare alisema vifaa hivyo vitawawezesha kujiimarisha kukabili michuano ya majeshi inayotarajiwa kuanza mapema mwakani.

Kwa upande wake, Kanali Erasmus Bwegoge ambaye ni Mkurugenzi wa Utimamu wa Mwili, Michezo na Utamaduni kutoka JWTZ amesema timu zitakazonufaika na msaada huo ni pamoja na timu za Ruvu Shooting, JKT Tanzania, Green Warriors, Mlale JKT ya Songea, Mgambo Shooting na baadhi ya timu ambazo zinashiriki Ligi Daraja la Kwanza.

Naye Kaimu Mkuu wa Wateja Wadogo kutoka Benki ya NMB, ambao ndiyo wametoa msaada huo, Salie Mlay amesema kuwa wanalenga kuona Timu za JWTZ zikiongeza mwamko katika mashindano mbalimbali hususan mashindano ya majeshi ili waweze kuliwakilisha taifa kikamilifu.

Kaimu Mkuu wa Wateja Wadogo kutoka Benki ya NMB, Salie Mlay (kushoto) akimkabidhi moja ya jezi zilizokabidhiwa Kanali Damian M. Majare(katikati).

Kaimu Mkuu wa Wateja Wadogo kutoka Benki ya NMB, Salie Mlay (kushoto) akimkabidhi mipira Kanali Damian M. Majare (katikati). 

Meza kuu ilivyoonekana mbele.

WAZIRI MHAGAMA ATOA MAAGIZO 5 KWA KAMATI YA USIMAMIZI WA MENEJIMENTI YA MAAFA YA MKOA WA DAR ES SALAAM

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama amefanya ziara ya siku moja mkoani Dar es salaam, lengo la ziara hiyo ni kukagua miundo mbinu ya kukabiliana na maafa ya mafuriko pamoja na kutaka kujua mikakati ya kamati ya Usimamizi wa menejimenti ya maafa mkoani humo ya kukabiliana na maafa hayo.

Katika ziara hiyo Waziri Mhagama emetembelea wilaya zote za mkoa wa Dar es salaam hususan katika maeneo ambayo mkoa huo umeboresha miundo mbinu ya kukabiliana na maafa ya mafuriko. Maeneo hayo ni Jangwani, Mto Mbezi, Mto Ng’ombe, Mto Bungoni na mfereji wa Mtoni kwa Azizi Ally. Pamoja na kuridhishwa na jitihada zilizofanywa na mkoa wa Dar es salaam za kuboresha miundombinu ya kukabiliana na maafa ya mafuriko, pia na mikakati ya kukabiliana na maafa hayo waliyomueleza, Waziri Mhagama ametoa maagizo 5 kwa kamati ya Usimamizi wa menejimenti ya maafa ya mkoa huo kuyatekeleza  ili menejimenti ya maafa ya mafuriko mkaoni Dares salaam iwe endelevu.

“Nimeridhishwa na juhudi zilizofanywa na serikali kuu chini ya uongozi wa Dkt.Joh Pombe Magufuli za kuboresha miundo mbinu ya kakabiliana na maafa ya mafuriko, na nimeona jinsi serikali ya ngazi ya mkoa na wilaya zote zinavyo jitahidi kujenga uwezo   wa kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na maafa. Pamoja na jitihada hizo ninge penda kuishauri  na kuielekeza kamati na Mkuu wa mkoa ayasimamie maelekezo yangu.” Amesisitiza  Mhagama

Mhagama ameiagiza Kamati ya Usimamizi wa menejimenti ya maafa kusimamia suala la uharibifu wa mazingira hususani maeneo ya mito na mabondeni kwa mujibu wa sheria ya menejimenti ya maafa ya mwaka 2015. Aidha alifafanua kuwa Maafa mengi ya mafuriko mkoani humo yanatokana na uharibifu wa mazingira unaochangiwa na  ujenzi  katika maeneno yasiyo stahili kama kingo za mito na mabondeni hali ambayo huzuia maji kutiririka na kusababisha mafuriko.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aliye kuwa akimueleza juu ya ujenzi wa mfereji wa mto Ngo’mbe, wakati wa ziara yake  ya kukagua miundo mbinu ya kukabili maafa ya mafuriko mkoani Dar es Salaam.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza, Bibi, Nuru Damson, mkazi wa Dar es Salaam, aliye kuwa akimueleza  jinsi ujenzi wa mfereji wa mto Ngo’mbe, ulivyowasaidia kutopata athari za maafa ya mafuriko wakati wa ziara yake  ya kukagua miundo mbinu ya kukabili maafa ya mafuriko mkoani Dar es Salaam. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akioneshwa ujenzi wa miundombinu ya kukabili maafa ya mafuriko mkoani Dar es saaam na  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, wakati wa ziara yake  ya kukagua miundo mbinu hiyo mkoani humo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

WATEJA WA TIGO SASA KUFANYA MALIPO KWA KUTUMIA MFUMO WA KIELETRONIKI WA MALIPO SERIKALINI (GePG)

0
0
Fanya malipo ya haraka, urahisi na kwa usalama zaidi kwa zaidi ya idara 300 za serikali, mawakala na mamlaka za udhibiti kwa Tigo Pesa 

Wateja wa Kampuni ya Tigo, sasa wanaweza kufanya malipo kutumia mfumo wa Kielektroniki wa Malipo Serikalini (GePG) baada ya kampuni hiyo kuongeza malipo ya Serikalini kwenye App yake ya Tigo Pesa. 

Akiongea katika uzinduzi wa GePG kwa mtandao wa Tigo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, Bernard Mabagala Afisa Mwandamizi wa TEHAMA – Wizara ya Fedha na Mipango alisema kuwa ubunifu na juhudi za Serikali katika kuanzisha mdumo huo wa Kieletronbiki wa Malipo Serikalini (GePG) umerahisisha upatikanaji wa ankara na kufanya malipo kwa wananchi. Pia imeleta faida nyinginezo ikiwemo kuboresha uwekaji wa kumbukumbu, utoaji wa taarifa, kupunguza uvuvaji na ubadhirifu pamoja na kuongeza mapato kwa idara mbali mbali za Serikali. na 

Kupitia mfumo wa GePG Serikali pia imeongeza wigo wa upatikanaji wa huduma kwa wananchi na kuongeza fursa za biashara kwa kampuni zinazotoa huduma za malipo kama Tigo. Wananchi wanaweza kupokea ankara zao moja kwa moja kutoka ofisi na mashirika ya Serikali au kwa njia mbali mbali za kimtandao, na kufanya malipo ya ankara kwa urahisi na mahali popote kwa njia ya simu za kiganjani, benki au kwa njia ya mtandao. 

“Kufanya kazi kwa karibu na Serikali ili kufikisha huduma za kifedha kwa wananchi wengi ni moja kati ya malengo na mkakati wetu,” alisema Hussein Sayed, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za kifedha wa Tigo. 

Mkuu wa Huduma za Biashara na Serikali wa Tigo, Ally Maswanya (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mfumo wa Malipo ya Kieletroniki Serikalini (GePG) ambao utawezesha wananchi kulipia ankara mbali mbali za kiserikali kwa urahisi na moja kwa moja kwa njia ya simu za mkononi kupitia huduma ya Tigo Pesa. Pamoja naye ni Afisa Mwandamizi wa TEHAMA katika Wizara ya Fedha na Mipango, Bernard Mabagala (kushoto) na Mkuu wa Huduma za Tigo Pesa, Hussein Sayed (kati).
Afisa Mwandamizi wa TEHAMA katika Wizara ya Fedha na Mipango, Bernard Mabagala (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Mfumo wa Malipo ya Kieletroniki Serikalini (GePG) unaowezesha wananchi kulipia ankara mbali mbali SerikaliNI kwa urahisi na moja kwa moja kwa njia ya simu za mkononi kupitia huduma ya Tigo Pesa. Pamoja naye ni Mkuu wa Huduma za Tigo Pesa, Hussein Sayed (kati) na Mkuu wa Huduma za Biashara na Serikali wa Tigo, Ally Maswanya (kulia).
Baadhi ya wafanyakazi kutoka kampuni ya Tigo na Serikali wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya uzinduzi wa Mfumo wa Kielektroniki wa Malipo Serikalini (GePG) uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.


Masauni Akabidhiwa Orodha ya watuhumiwa Dawa za Kulevya Zanzibar

0
0
Wananchi wa eneo la Sogea, Wilaya ya Mjini Unguja wamemkabidhi Naibu Waziri  wa  Mambo  ya  Ndani ya Nchi, Mhandisi  Hamad  Masauni, orodha ya watu  wanaoshukiwa  kujihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya Visiwani Zanzibar. Wananchi hao wamekabidhi orodha hiyo baada ya Naibu Waziri Masauni kuwataka waorodheshe majina ya watu wanaowafahamu wakituhumiwa kujihusisha na biashara hiyo ambayo imekuwa ikiaribu nguvu kazi ya Taifa na kusababisha  kuwepo  kwa  matukio ya uhalifu katika sehemu mbalimbali Visiwani humo.

Awali  wakiwasilisha  kero zao kwa nyakati  tofauti wananchi hao waliiomba serikali  kudhibiti  biashara  hiyo  ya dawa za kulevya  kwani  imekua ikishamiri kwa kasi Visiwani humo na wakishangaa ukimya wa mamlaka husika kuacha biashara hiyo ikizidi kuleta madhara katika jamii.
Akizungumza katika Mkutano huo wa hadhara, Naibu Waziri Masauni amewaahidi  wananchi  hao  kuchukua  hatua  madhubuti  kukabiliana  na  wauzaji wa dawa za kulevya huku akitoa maelekezo kwa  Jeshi  la  Polisi  kuwakamata watu  wote waliotuhumiwa  na  uchunguzi  uanze  mara moja.

“Hatuwezi  kama  Taifa  tukawa  na vijana ambao hawana faida katika jamii, vijana  ni  nguvu kazi ya Taifa, tutahakikisha majina yaliyoletwa hapa tunayafanyia  kazi na natoa maelekezo kwa Jeshi la Polisi kuhakikisha watuhumiwa hao wanakamatwa na nitahitaji ripoti hiyo ndani ya wiki mbili, haiwezekani watu wachache waharibu nguvu kazi ya Taifa kwa maslahi yao binafsi na familia zao,” alisema  Masauni
Akizungumza katika mkutano huo , Kamishna Msaidizi, Saleh Mohamed Saleh, aliwaomba wananchi kuzifikisha  taarifa  za  uhalifu  katika  vituo  vya  Jeshi la Polisi au Serikali ya Mtaa  ili  hatua ziwe zinachukuliwa ili kuweza kudhibiti  uhalifu  katika  maeneo yao.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad (kulia), akiangalia majina ya watu wanaotuhumiwa kujihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi hao ikiwa ni jitihada za Serikali kudhibiti matukio ya uhalifu  yaliyoanza kushamiri katika maeneo mbalimbali  Visiwani Zanzibar.Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Polisi Jamii Zanzibar, Emmanuel Lukula, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Saleh Mohamed Saleh na Katibu wa Naibu Waziri, George Mwansasu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad (kulia), akizungumza na wananchi wa eneo la Sogea, Wilaya ya Mjini Unguja (hawapo pichani), wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi hao ikiwa ni jitihada za Serikali kudhibiti matukio ya uhalifu  yaliyoanza kushamiri katika maeneo mbalimbali Visiwani Zanzibar.Wengine kutoka kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Polisi, Saleh Mohamed Saleh na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka Zanzibar, Masoud Mabalila. 
 Mwananchi wa eneo la Sogea, Wilaya ya Mjini Unguja, Ally Saleh Ally, akielezea kero ya uhalifu kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad (kulia),wakati wa Mkutano wa Hadhara uliokuwa na lengo la kujadili jinsi ya kukomesha matukio ya uhalifu yanayoanza kushamiri Visiwani Zanzibar.
 Mwananchi wa eneo la Sogea, Wilaya ya Mjini Unguja, Mariamu Said Ali, akielezea kero ya uhalifu kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad (kulia),wakati wa Mkutano wa Hadhara uliokuwa na lengo la kujadili jinsi ya kukomesha matukio ya uhalifu yanayoanza kushamiri Visiwani Zanzibar.
Kamishna Msaidizi wa Polisi, Saleh Mohamed Saleh, akizungumza na wananchi wa eneo la Sogea, Wilaya ya Mjini Unguja (hawapo pichani), wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi hao ikiwa ni jitihada za Serikali kudhibiti matukio ya uhalifu yaliyoanza kushamiri katika maeneo mbalimbali  Visiwani Zanzibar.Kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni. 

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA BALOZI WA FALME ZA NCHI ZA KIARABU

0
0
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akizungumza na Balozi wa Falme za Nchi za Kiarabu Mhe. Khalifa Abdulrahman  Almarzooqi alipomtembelea Ofisini kwake  Jijini Dar es Salaam.
  Balozi wa Falme za Nchi za Kiarabu Mhe. Khalifa Abdulrahman  Almarzooqi akimuelezea jambo Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai alipomtembelea  Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam.
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai katika picha ya pamoja na Balozi wa Falme za Nchi za Kiarabu Mhe. Khalifa Abdulrahman  Almarzooqi mara baada ya kuzungumza naye Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam. PICHA NA BUNGE

DODOMA ITAKAVYOKUWA USIPIME....JIJI LAKE KUFANANISHA NA MIJI YA MAJUU SIO LA DAR

0
0
*Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma aweka wazi mikakati yao
*Aeleza jinsi tamko la Rais lilivyoleta mabadiliko makubwa

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii.

WAKATI Rais Dk.John Magufuli akitarajiwa kuhamia rasmi katika Jiji la Dodoma Desemba mwaka huu, tayari mikakati mbalimbali inaendelea la kuliweka sawa Jiji hilo kuhakikisha linaendana na hadhi ya kuwa makao makuu ya Serikali.

Kwa sasa kuna miradi mbalimbali ya ujenzi wa maendeleo inayoendelea kufanyika kwa kasi kubwa kuhakikisha Jiji la Dodoma linapendeza na kuwa na muonekano wa aina yake ambapo Mkurugenzi wa Jiji hilo Godwin Kunambi ameeleza hatua kwa hatua namna ambavyo wamejipanga.

Akizungumza na Michuzi Blog na Michuzi TV kwenye mahojiano maalumu yaliyofanyika Mjini Dodoma Kunambi amesema kuwa baada ya Rais Dk.John Magufuli kutangaza Dodoma kuwa Jiji na Serikali kuhamia rasmi kuna hatua mbalimbali zimechukuliwa.

"Kuna mambo makubwa ambayo Rais wetu mpendwa ameyafanya baada ya kutangaza Dodoma kuwa Jiji na kuhamishiwa kwa shughuli za Serikali Kuu.Tunakumbuka aliamua kuivunja CDA na shughuli za CDA kuhamishiwa Manispaa ya Dodoma na baadae kuwa Jiji.Niwahakikishie Watanzania baada ya tamko la Rais la kuhamishia Serikali Dodoma kuna mambo makubwa yamefanyika,"amesema.

Amefafanua baada ya tamko hilo, Jiji la Dodoma nalo likaanza kuweka mikakati yake kufanikisha dhamira ya Rais ambapo moja ya mambo ambayo walifanya ni kuandika maandiko kwa ajili ya kupata fedha za kwa ajili ya miradi mitano waliyoamua kuanza nayo katika kuboresha Jiji hilo.

"Maandiko yetu yalisaidia kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa kituo kikubwa cha mabasi ambacho tunaamini kitakuwa cha kwanza kwa ukubwa Afrika Mashariki, soko la kisasa , maeneo ya kupumzika, ujenzi wa miundombinu ya barabara, dampo la kisasa la kuhifadhi taka na eneo la kuegesha malori,"amesema Kunambi.

Viewing all 109610 articles
Browse latest View live




Latest Images