Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

KUNA MAFANIKIO MAKUBWA MKOANI MTWARA NDANI YA MIAKA 3 YA JPM-RC MTWARA

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii, Mtwara

Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa, amesema ndani ya miaka mitatu ya awamu ya tano chini ya Rais Dr John Pombe Magufuli wamefanikiwa kupandisha kiwango cha Elimu na kuwaondoa wanyonyaji wa wakulima wa korosho maarufu kwa jina la 'Kangomba' Pamoja na kuimarisha huduma za Afya katika mkoa huo.

Byakanwa Amesema hayo leo Mkoani Mtwara alipokuwa akitoa Mukhtasari wa Mafaniko ya Serikali ya awamu ya tano katika sekta mbalimbali kwenye mkoa wa Mtwara.

"katika sekta ya elimu kulikuwa na dhana ya kuwa wanafunzi awapendi shule lakini tangu nimefika nimeweza kuweka mipango ya kuhakikisha kuwa elimu inakuwa katika hali sawa kwa kutengeneza mpango kazi ambao umeweza kusaidia kuongeza ufaulu kutoka mkoa wa Mwisho kitaifa mpaka kuwa mkoa wa nane kitaifa" amesema Byakanwa.

RC Byakanwa amesema kila mwalimu Mkuu amepewa mpango kazi hivyo Mimi sijapiga ngoma marufuku wala shughuli za kitamaduni hivyo nimewataka walimu watimize wajibu wao na kuacha kuwasingizia wakazi wa mtwara kwani walipoamua kufundisha ufaulu umeongezeka.

Katika hatua nyingine Rc Byakanwa amesema wameamua kusimamia zao la Korosho katika miaka hii mitatu lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha wanamnufaisha zaidi mkulima wa korosho pamoja na kuwaondoa watu hao ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakipata fedha haramu kupitia michezo hiyo.
Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa, akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya Miaka mitatu ya mkoa huo katika serikali ya awamu ya tano
Sehemu ya Waandishi wa Habari walioshiriki Mkutano wa Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa Kuelezea Miaka mitatu ya Rais Magufuli.


NAIBU WAZIRI MAMBO YA NJE AKARIBISHA KAMPUNI KUTOKA UTURUKI KUJA KUWEKEZA NCHINI

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ameipongeza Serikali ya Uturuki kwa kuendelea kuimarisha ushirikiano na Serikali ya Tanzania hususan katika kukuza biashara, uwekezaji na utalii.

Mhe. Dkt. Ndumbaro ametoa pongezi hizo wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 18 Novemba 2018 kuhusu ziara ya ujumbe wa Makampuni 7 makubwa ya uwekezaji kutoka Uturuki.

Mhe. Dkt. Ndumbaro alisema kuwa, ziara ya ujumbe huo nchini ambayo itafanyika kuanzia tarehe 18 hadi 24 Novemba 2018 ni mwendelezo wa jitihada za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Uturuki na wadau mbalimbali katika kutekeleza diplomasia ya uchumi ambayo pamoja na mambo mengine inalenga kwenye kutafuta na kuleta wawekezaji wenye nia ili wawekeze katika maeneo mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kukuza uchumi na kuinua kipato cha wananchi.

Akielezea ziara hiyo, Dkt. Ndumbaro alieleza kuwa, ujumbe wa wawekezaji kutoka Makampuni hayo ya Uturuki hapa nchini utatembelea mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Simiyu. Alisisitiza kwamba ujumbe huo umechagua mikoa hiyo kwa malengo mahsusi ya kuwekeza katika sekta ya viwanda ikiwemo Kiwanda cha nguo, kiwanda cha sukari, kiwanda cha saruji, kiwanda cha vifaa vya ujenzi, kiwanda cha kuongeza thamani bidhaa na uwekezaji kwenye sekta ya nishati kwa mkoa wa Simiyu. 

Aidha, kwa mkoa wa Dodoma ujumbe huo una nia ya kuwekeza katika ujenzi wa maduka makubwa (shopping malls), ujenzi wa majengo mbalimbali (real estate) na ujenzi wa hoteli zenye hadhi ya kimataifa. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo) pichani kuhusu ziara ya ujumbe wa Makampuni 7 makubwa ya uwekezaji kutoka Uturuki itakayofanyika nchini kuanzia tarehe 18 hadi 24 Novemba, 2018. Ujumbe huo utatembelea mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Simiyu kwa ajili ya kuangalia fursa za uwekezaji katika ujenzi wa viwanda vya nguo, kiwanda cha kuongeza thamani bidhaa za kilimo, ujenzi wa maduka makubwa na hoteli za kimataifa. Mkutano huo na waandishi wa habari ulifanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 18 Novemba, 2018. 
Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Davutoglu nae akizungumza wakati wa mkutano huo kuhusu ziara ya ujumbe kutoka Uturuki huku Mhe. Dkt. Ndumbaro akisikiliza
Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Ali Davutoglu (kushoto) akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga (katikati) pamoja na Afisa kutoka Ubalozi wa Uturuki wakifuatilia mkutano kati ya Dkt. Ndumbaro na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) 
Mkutano ukiendelea 

WAZIRI MKUU ATEMBELEA KITUO CHA AFYA NKOWE,RUANGWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaametembelea kituo cha afya cha Nkowe na kuwataka wananchi wakilinde na kukienzi kwa kuwa ndio mkombozi wao kiafya.Amesema kwa sasa wananchi hao hawana sababu ya kulipa nauli kwenda Ruangwa kufuata huduma za vipimo na matibabu katika hospitali ya wilaya hiyo.

Waziri Mkuu ametembelea kituo hicho cha afya leo (Jumapili, Novemba 18, 2018) akiwa katika ziara yake ya kikazi Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.Ametaja baadhi ya huduma zinazopatikana kwa sasa kwenye kituo cha Afya Nkowe ambazo awali hazikuwepo kuwa ni pamoja na upasuaji, maabara, mama na mtoto.“Rais Dkt. John Magufuli anataka kila Mtanzania apate huduma za afya karibu na makazi yake ili asilipe nauli au kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.”

Waziri Mkuu amesema amefurahishwa na huduma zinazotolewa kituoni hapo, ambapo amewataka watumishi waendelee kuwahudumia wananchi vizuri.Baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika kituo hicho cha afya wameishukuru Serikali kwa kuboresha huduma za afya nchini, ambapo kwa sasa wanatibiwa karibu na makazi yao. Awali, Mganga Mfawidhi wa kituo hicho, Dkt. Paul Mbinga alisema kituo hiko kinahudumia jumla ya wakazi 5,264 wa kata ya Nkowe pamoja na wananchi wa kata za jirani za Chienjele, Nandagala, Likunja na Mnacho. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa amembeba mtoto aliyezaliwa katika kituo cha Afya cha Mkowe wilayani Ruangwa na Bibi Asia Abdallh (kushoto) wakati alipotembelea wodi ya wazazi katika Kituo hicho Novemba 18, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mtambo wa utakatishaji vifaa vya  upasuaji katika Kituo cha Afya cha Mkowe wilayani Ruangwa, Novemba 18, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi khanga Muuguzi wa Kituo cha Afya cha Mkowe wilayani Ruangwa, Grace Nanguka ikiwa ni zawadi ya watumishi wote wa Kituo hicho wakati alipokagua ujenzi na ukarabati wa Kituo hicho, Novemba 18, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Walimu na baadhi ya wanafunzi wa Shule za Msingi za wilaya ya Ruangwa kwenye ukumbi wa Narung’ombe, Novemba 18, 2018. Kulia ni Mkewe Mary, kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi na wapili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Ruangwa, Hashim Ngandirwa.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

BILIONI 50 ZATOLEWA KUKARABATI UWANJA WA NDEGE MTWARA

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii ,Mtwara 

Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi inakarabati Uwanja wa ndege wa Mtwara kwa kiasi cha Sh bilioni 50 hili uweze kurahisisha huduma za usafiri wa anga.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisa Uendeshaji wa uwanja huo, Zitta Majinge amesema Ukarabati huo unahusisha ujenzi wa barabara ya kuingia uwanjani yenye urefu wa kilomita 1.2, maegesho ya ndege na njia za kurukia na kutua ndege.

Akizungumza jana, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa, alisema ukarabati huo unafanywa na Kampuni ya Beijing Constraction Engineering Group ( BCEG)."ukarabati huo unafanywa na Kampuni ya Beijing Constraction Engineering Group (BCEG) kwa muda ya miezi 24. Mkandarasi yupo katika hatua za maandalizi na ujenzi wa kambi ya ofisi ya mhandisi mshauri,"amesema

Amesema mradi huo ulisainiwa Novemba 11 mwaka jana na kuanza rasmi Juni 26 mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Septemba 2020.Naye Ofisa Uendeshaji wa uwanja huo, Zitta Majinge, alisema urefu wa njia ya kuruka na kutua ndege kwa sasa ni mita 2,258 na kutokana na ukarabati huo zitaongezwa mita 542 wakati upana utaongezeka kutoka mita 35 hadi 45.

Amesema ndege zenye uwezo wa kutua uwanjani hapo kwa sasa ni zile zenye uzito wa tani 70 na kwamba baada ya ukarabati huo wanatarajia zitatua ndege zenye uzito wa tani 300."Ukarabati ukikamilika kiwanja kitakuwa na uwezo wa kuhudumia ndege kubwa zaidi. Hivi sasa makampuni mengi yanaomba kuja lakini yanashindwa kutokana na miundombinu mingi kuchoka hasa njia za kurukia na kutua ndege," amesema Majinge.

Amesema changamoto nyingine ni kuwapo kwa pori kubwa ambalo wakati mwingine limekuwa na wanyama wakali na kusababisha utendaji kazi kuwa mgumu.Hata hivyo amesema wako kwenye hatua za kupunguza msitu huo ili waanze mchakato wa ujenzi wa uzio.Uwanja huo uliojengwa mwaka 1950 kwa mwaka unahudumia zaidi ya abiria 10,000.
Ofisa Uendeshaji wa uwanja wa Ndege wa Mtwara , Zitta Majinge akizungumza na Waandishi wa habari waliofika katika uwanja huo kuona upanuzi wa uwanja huo.
Ofisa Uendeshaji wa uwanja wa Ndege wa Mtwara , Zitta Majinge akifafanua jambo kwa Waandishi Wahabari
Sehemu ya jengo la Utawala la uwanja wa Ndege wa Mtwara 

MGUNDUZI WA VIDONDA VYA TUMBO HUYU HAPA, ALIMEZA BAKTERIA KUWEZA KUTAFUTA DAWA

$
0
0
DAKTARI Barry Marshall  ambaye pia ni mshindi wa tuzo ya Nobel aliyoipata kutokana na kugundua chanzo cha vidonda vya tumbo kwa kufanya majaribio katika mwili wake.

Wataalamu wengi wa Afya miaka ya nyuma waliamini kuwa bacteria hawezi kuishi ndani ya tumbo la mwanadamu kutokana na joto pia tindikali na asidi iliyopo humo. Hivyo basi iliaminika kuwa ugonjwa wa vidonda vya tumbo unatokana na mawazo au kutokula kwa muda mrefu.

Dkt. Barry akiwa na miaka 32 aligundua kuwa vidonda vya tumbo husambazwa na bacteria anayeitwa Helicobacter pylori na alipojaribu kuwashirikisha wataalamu wengine alipingwa  na hakuna aliyeamini kuwa bacteria huyo anaweza kuishi katika tumbo la binadamu kutokana na mazingira ya tindikali.

Barry Hakukata tamaa aliendelea na majaribio ili kuweza kugundua dawa ya kutibu kabisa vidonda vya tumbo na alipokwama ni jinsi ya kufanya majaribio, kwani taratibu hazikumruhusu kujaribu nadharia zake za bacteria anayepelekea vidonda vya tumbo. 

Daktari huyo  alifanya maamuzi magumu ya kuwameza vimelea hao wajulikanao kama Helicobacter pylori, chini ya uangalizi wa rafiki yake aitwaye Robin Warren na baada ya wiki kadhaa alikuwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Hii iliwahadaha walimwengu wa wataalamu wa afya, na alipojaribu kutumia dawa alizoziandaa mwanzo hazikufanya kazi. Akiwa mgonjwa sana hatimaye aligundua antibayotiki inayotibu vidonda vya tumbo. 

Ilipofika mwaka 2007 alitunukiwa tuzo ya ya Nobel kwa ujasiri huo uliohatarisha maisha yake.

JYOTI KISANJI MWANAMKE MFUPI ZAIDI MWENYE NDOTO YA UIGIZAJI

$
0
0
NCHINI India Jyoti Kisanji Amge aliyezaliwa mwaka 1993 imethibitika kuwa ndiye mwanamke mfupi zaidi anayeishi na makazi yake ni huko Nagpur nchini India.

Akizungumza na jarida la Wider World Ranjana ambaye ni mama mzazi wa Jyoti amesema kuwa binti yake huyo alionekana na matatizo hayo alipofika miaka 5 na kwa mujibu wa madaktari walisema kuwa na tatizo la dwarfism linalofahamika kama achondroplasia na wakathibitisha kuwa kimo chake hakiwezi kuongezeka.

Jyoti alivuma sana mwaka 2009 alipoonekana kwenye televisheni ya Fuji ambapo katika kipindi hicho alipimwa na kugundulika kuwa na futi 2 pekee na ikathibitika kuwa ni mwanamke pekee anayeishi na wakati huo alikuwa na miaka 15 na alieleza kuvutiwa kwake na masuala ya urembo na alieleza kuwa ana ndoto za kuja kuwa muigizaji.

Hadi kufika Desemba 2011 alipofikisha miaka 18 historia yake ilizidi kukua na kuwa mwanamke mfupi zaidi anayeishi.

Amehudhuria matamasha mbalimbali na kukutana na aliyekuwa mwanaume mfupi zaidi duniani Chandra Dangi na amewahi kutokea katika wimbo wa Bhangra Singh na katika makala ya Bodyshock iliyojulikana kama Two Foot Tall Teen.

WAUZAJI WA VIFAA VYA MAWASILIANO,MAFUNDI WATENGENEZAJI SIMU ZA MKONONI WOTE WANATAKIWA KUWA NA LESENI KUTOKA MAMLAKA HUSIKA-TCRA

$
0
0
Na. Vero Ignatus, Arusha

Mamlaka ya mawasiliano Nchini kanda ya kaskazini imeendesha semina ya siku moja kuhusu huduma za utangazaji kwa chanel zinazotazamwa bila kulipia 

Akizungumza katika semina hiyo Mkuu wa Kanda ya Kaskazini Francis Msungu amesema leo ngo kuu la serikalini kuwataka watoa huduma kujenga miundo mbinu ya Minara hapa nchini na hii itapelekea watanzania wengi watapata ajira. Katika semina hiyo iliyojumuisha viongozi mbalimbali wa serikali ngazi ya mkoa washiriki kuweza kuuliza maswali nje ya mada yanayohudu vifaa vya mawasiliano, simu, tekevisheni pamoja na radio.

Mamlaka hiyo ya Mawasiliano iliweza kutoa ufafanuzi kwamba maduka yanayouza vifaa vya mawasiliano vya eletroniki wauzaji wake wanatakiwa kuwa na leseni kutoka mamlaka ya mawasiliano sambamba na ile ya biashara.Msungu amesema kuwa mafundi wanaotengeneza simu za mkononi wanapaswa pia kwa mujibu wa sheria wawe na kibali kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Nchini.

Ndiyo maana tumeshauri wananchi kupitia viongozi kwamba unapopeleka kutengeneza simu yako kabla hujampa mtu kuitengeneza hakikisha je anacho kibali kinachomruhusu kufanya hiyo shughuli hiyo?
Unapokwenda dukani kununua kifaa chako cha mawasiliano radio, televisheni ni haki yako kujua je huyu anayeniuzia ametathimishwa kufanya hiyo kazi?

Amesema lengo kubwa la Mamlaka kuwataka watu hawa kuwa na leseni ni kumlinda mtumiaji wa hizo huduma(mlaji).Unapoenda kununua kifaa chako hakikisha umepewa risiti na sasa risiti hiyo imeongezewa kazima iwe na Efd ya TRA, lazima uwe na garantiii kama kunatokea lolote uweza kufidiwa kile kifaa na kupatiwa kingine hiyo ndiyo nia njema ya serikali kuweka huo utaratibu. Alisema

Amesema baadhi ya mafundi wanapotengeneza vifaa vya wateja wao asilimia kubwa wanabadilisha namba tambulishi na kupewa namba ya mtu mwingine ambapo amesema hilo ni tatizo.Kwa usalama wa nchi hili swala la msingi sana najua namba ya simu kitamvulishi ni kitambulisho muhimu kwa watumiaji wa simu hivy kuweni makini, hata vocha mnapozitumia msizitumie hovyo. Alisema
Muwezeshaji wa Warsha hiyo Injinia Jan Kaay (TCRA) akiendekea kutoa elimu kwa washiriki.
Wakwanza kulia ni mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro ndiye akiyefungua warsha hiyo ya siku moja ya watumishi na viongozi mbalimbali wa serikali mkoani Arusha katika ukumbi wa Goldenrose.
Baadhi ya washiriki wa warsha hiyo wakiendelea kufuatilia kwa makini.

Makamba awataka wataalam elekezi mazingira kubadilika kiutendaji

$
0
0
WAZIRI wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira),Bw.
January Makamba amewataka wataalamu elekezi wa tathmini ya athari kwa mazingira kubadilika kiutendaji ili tasnia hiyo iendelee kukua na
kutoa mchango stahiki katika maendeleo ya taifa. 

Akifungua Mkutano wa Pili wa Mwaka wa Chama cha Wataalamu Elekezi wa
Tathmini Athari kwa mazingira, ukaguzi na vibali vya awali jijijni
Dar es salaam mwishoni mwa wiki, Bw. Makamba alisema wataalamu elekezi wa mazingira wana umuhimu mkubwa katika ujenzi wa uchumi,lakini lazima wabadilike namna ya utendaji wao wa kazi.

‘’Katika changamoto za namna ya ufahamu na ufanywaji wa
tathimini na ukaguzi wa mazingira nyie kama chama mnauwezo wa
kujipanga kuanzisha programu za mafunzo na kubadilishana uzoefu (
Capacity Building) kwa kufanya hivo itasaidia kuboresha na kuimarisha
uwezo wenu wa kiutendaji,’’ alisema Waziri Makamba.

Waziri Makamba alisema suala la tathimini za athari kwa mazingira
linapewa kipaumbele ili kwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu
ya Tano ya kujenga Uchumi wa Kati na Viwanda ifikapo mwaka 2025.
“Kuna changamoto kadhaa kwenye usajiri wa wataalam elekezi wa
mazingira kuhusu ulipwaji wa ada za mwaka ambapo serikali inapoteza
mapato yake. Taarifa ya NEMC inaonyesha kuwa mwaka 2018 wataalam
binafsi wanadaiwa jumla ya shilingi milioni 600, na makampuni
yanadaiwa jumla ya milioni 250 kama ada za mwaka,” alisema.


Kamishna wa Bima, CAG wateta kuhusu sheria mpya ya bima

$
0
0
Kamishna wa Bima Nchini, Dkt. Baghayo Saqware amefanya mazungumzo na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Juma Assad yaliyolenga kukuza ushirikiano wa usimamzi wa sekta ya bima na ukaguzi wa hesabu za serikali.

Akizungumza na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali mwishoni mwa wiki, Dkt. Saqware alisema Mamlaka ya Usimamizi wa shughuli za Bima (TIRA) imefanya mabadiliko madogo ya sheria ya bima Na. 10 ya Mwaka 2009 katika kifungu cha 133, kinachotaka majanga yote ya yapewe kinga na makampuni ya Bima yaliyosajiliwa na Mamlaka, na kuomba Ofisi ya CAG kuweka utaratibu wa ukaguzi wa utekelezaji wake kwenye miradi ya serikali.

“Ndugu CAG, mabadiliko haya yanataka majanga yanayotokana na
uendashaji wa shughuli zote za kiuchumi na kijamii kukatiwa bima na
makampuni yenye usajili nchini, ndiyo sababu serikali imeona ni vema
tushirikiane katika kuhakikisha taasisi zetu zinakidhi matakwa ya
sheria hii” alisema Dkt. Saqware.

Serikali ya Awamu ya Tano inatekeleza miradi mingi na mikubwa ya
kimkakati hivyo ni fursa adhimu kwa kwa sekta ya bima kushiriki
kikamilifu katika kuhakikisha miradi hii inapatiwa kinga dhidi ya
majanga yanayoweza kuathiri na kuchelewesha utekelezaji wa Miradi
hiyo
.

Solomon Mkubwa akonga nyoyo za wakazi wa Mwanza, RC Mongella afurahia

RAIS WA ZANZIBAR DK.SHEIN AZUNGUMZA NA MAKAMU MWENYEKITI WA BUNGE LA JAMUHURI YA WATU WA CHINA

$
0
0

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Watu wa Jamuhuri ya China Mhe. Cai Defeng, alipowasili Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo wa Rais wa Zanzibar leo tarehe 18/11/2018


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Ujumbe wa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Watu wa Jamuhuri ya China, Ikulu Zanzibar, akitambulishwa na Makamu Mwenyekiti wa Bunge Mr. Cai Defeng katikati.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Watu wa Jamuhuri ya China Ikulu Zanzibar,kulia Makamu Mwenyekiti wa Bunge la China Mr. Cai Defeng na Ujumbe wake walipofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo leo,18/11/2018

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Watu wa China Mr. Cai Defeng alipofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo.akiwa na Ujumbe wake

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Ali Mohamed Shein, akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Watu wa Jamuhuri ya China na Ujumbe wake na Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, baada ya mazungumzo yao Ikulu Zanzibar.tarehe 18/11/2018
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na mgeni wake Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Watu wa Jamuhuri ya China Mr. Cai Defeng akimuonesha mandhari ya visiwa vya Zanzibar wakiwa nje ya ukumbi wa mkutano baada ya mazungumzo yao Ikulu Zanzibar.leo tarehe 18/11/2018.(Picha na Ikulu

Kampuni ya TanzaRice yaja na bidhaa ya mchele kuchochea ajira kwa vijana

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

Kampuni ya TanzaRice International Ltd imesema kuwa mchele una fursa ya ajira kubwa lakini watu bado hawana uelewe ya kufanya biashara hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa kampuni hiyo Deo Mbasa amesema kuwa wamefanya utafiti na kuona biashara hiyo inaweza kuwakomboa wananchi kiuchumi kwa kuuza mchele huo kupitia kampuni.

Amesema kuwa wajasiriaali wakijiunga na kampuni hiyo wanaweza kupata mchele na kuuza kwa jamii inayowazunguka.Mbasa amesema kuna faida ya kuuza mchele kwani kinachotakiwa ni uaminifu wa mtu kwa kuchukua mchele bila ya kuwa na hela mara baada ya kujiunga na kampuni hiyo.

"Hatuwezi kila kitu tunafikiria mtaji wakati ukiwa na uaminifu unaweza kufanya biashara hata kama hauna mtaji na baadae ukawa umejikwamua kiuchumi"amesema Mbasa.
 Mkurugenzi wa TanzaRice Deo Mbasa akitoa maada wakati wa mafunzo ya wajasiriaali .
Mjasiriamali wa bidhaa ya Mchele kupitia kampuni hiyo Even John akizungumza mafanikio ya biashara ya mchele.
 Bidhaa ya mchele ikioneshwa kwa wajasiriamali katika mafunzo yaliyoandaliwa na kampuni ya TanzaRice
 washiriki wa wajasiriaali wa Mchele wakiwa katika mafunzo yaliyoandaliwa na kampuni ya TanzaRice
Mkurugenzi wa Kampuni ya TanzaRice Deo Mbasa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na fursa iliyopo katika bidhaa ya mchele.

DCB YAWASHAURI WABUNGE KUNUNUA HISA ZA BENKI HIYO

$
0
0
BENKI ya Biashara ya DCB ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Godfrey Ndalahwa,  wametembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma ikiwa ni muendelezo kampeni ya kuhamasisha uuzaji wa hisa zake kwa Wabunge na watanzania wote.

Akizungumza wakati akimtambulisha Mkurugenzi mtendaji  huyo pamoja na ujumbe wake, Spika wa Bunge Job Ndugai aliwatangazia wabunge hao taarifa za uzinduzi huo na ya kwamba hisa zinaweza kununuliwa katika matawi ya benki hiyo, mawakala wa Solo la Hisa (DSE) kwa bei pungufu ya shs 265 na ya kwamba benki hiyo sasa ni benki ya biashara.

DCB ilizindua zoezi la kuuza hisa zake Novemba 12 mwaka huu huku mwanahisa namba moja Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa akiwa mteja wa kwanza  kujitokeza kununua hisa.

TAASISI YA DORIS MOLLEL YAWAPA SOMO WABUNGE JUU YA WATOTO NJITI

$
0
0
KILA ifikapo Novemba 17, Dunia huadhimisha siku ya mtoto njiti (World Prematurity Day) na kwa umuhimu wake, Taasisi isiyo ya kiserikali ya Doris Mollel yenye jukumu la kuhakikisha Mtoto Njiti anapata mahitaji yote muhimu na kukua iliendesha semina kwa Wabunge wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya umuhimu wa kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti).

Semina hiyo iliyoandaliwa kwa ushirikiano na Umoja wa wabunge wanawake Tanzania (TWPG) ilifanyika mwishoni mwa wiki kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma. Katika semina hiyo, Taasisi ya Doris Mollel ilipendekeza ombi kwa Serikali la kurekebisha sheria ya likizo ya Uzazi ili wazazi wenye watoto njiti waweze kupata muda wa kutosha kulea watoto wao ambao asilimia kubwa huwa na changamoto nyingi pindi wazaliwapo, hivyo huhitaji uangalizi wa hali ya juu kutoka kwa wazazi wao.

Maadhimisho ya Siku ya Mtoto Njiti kwa mwaka huu yalikuwa na kauli mbiu ya Saidia  wazazi wenye watoto njiti na watoto wagonjwa.

Pamoja na semina hiyo, Taasisi ya Doris Mollel pia imekabidhi vifaa tiba katika Hospitali ya wilaya ya Kongwa, Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma pamoja na Hospitali kuu ya kambi ya wakimbizi, Nyarugusu ambayo itakabidhiwa wiki hii.

Shuguli za maadhimisho ya mtoto Njiti mwaka 2018 zimefanikishwa kwa Ushirikiano na Wizara ya Afya pamoja na wadau wengine wa maendeleo kama Vodacom Tanzania Foundation, Benki ya DTB, Benki ya CBA, Asas Dairies, Ashton Media, Walt Printers n.k. 

 
Pichani ni Sehemu ya Wabunge wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa pamoja na Ujumbe kutoka Taasisi ya Doris Mollel pamoja na washirika wengine katika semina hiyo.
Daktari bingwa wa watoto wachanga kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Augustine Massawe akitoa mada katika semima kwa Wabunge wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya umuhimu wa kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma.
Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), Doris Mollel akizungumza jambo mbele ya Wangunge wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa semina iliyozungumzia umuhimu wa kuwasaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), iliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni jijini Dodoma.
Sehemu ya Wabunge Wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakifatilia mada hiyo.

MRITHI WA PROFESA MAJI MAREFU AANZA KUUNGURUMA KOROGWE VIJIJINI

$
0
0
MBUNGE wa Korogwe vijijini ndugu Timotheo Mnzava, Novemba 18, 2018 amefanya mkutano wake wa kwanza na wananchi mara baada ya kuapishwa rasmi katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma Novemba 6, 2018.

Mkutano huo ambao ulifanyika katika kata ya Makuyuni, Mnzava amewahakikishia wananchi wa jimbo la Korogwe vijijini kutatua kero sugu zilizopo ndani ya jimbo ambapo zile zilizo juu ya uwezo wake kuendelea kuikumbusha serikali kutatua ili wananchi wapate maisha bora. 

Aidha Mnzava ameainisha changamoto ya Elimu, Maji, afya na Miundombinu ya barabara ndio vipaumbele ambavyo ataanza kuvishughulikia katika kipindi chake cha kuiongoza Korogwe vijijini. 

Mnzava amewahakikishia wananchi kuhusu Korogwe mpya na yenye matokeo chanya inayoenda sambamba na dhamira ya Mh. Rais Dkt John Pombe Magufuli ya kuifikisha Tanzania katika uchumi wa kati ifikapo 2025. 

Mnzava alimalizia kwa kumshukuru rais Magufuli, Wananchi pamoja na chama cha mapinduzi kwa imani waliyonayo juu yake na kumchagua kuwa mbunge atakayeiongoza Korogwe vijijini na kuleta maendeleo yenye tija na endelevu. 

SERIKALI YARAHISISHA UKUSANYAJI WA TAKWIMU ZA VIFO VINAVYOTOKEA KATIKA NGAZI YA JAMII NCHINI.

$
0
0
NA WAMJW-IRINGA 

SERIKALI kupitia Wizara ya afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imerahisisha ukusanyaji wa takwimu za vifo vinavyotokea kwenye ngazi ya jamii nchini kwa kugawa vifaa maalumu vya kukusanyia takwimu hizo kwa Maafisa afya katika kata za mkoa wa Iringa. 
Hayo yamezungumzwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati akikabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu hizo kwa Maafisa Afya leo Mkoani Iringa.
“Takwimu zitakazokusanywa kuhusu vifo na Maafisa hawa wa afya kutokana na Mifumo hii zitawasaidia madaktari kujadili changamoto pamoja na sababu za vifo hivyo ili kupata ufumbuzi wa matatizo hayo na kuweza kupunguza idadi ya vifo nchini” alisema Dkt. Ulisubisya. 
Aidha,Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa takwimu hizo zikikusanywa kikamilifu zitasaidia kutoa elimu kwa jamii na kupunguza imani za kishirikina kwa wananchi kwani zitaleta picha sahihi ya kugundua vyanzo vya vifo hivyo kwenye jamii husika. 

Hata hivyo Dkt. Ulisubisya amewataka maafisa hao kutumia vifaa hivyo kwa matumizi ya kazi ya kukusanyia takwimu na sio matumizi binafsi na kama itatokea afisa afya yeyote atakayehama kituo cha kazi basi arudishe ofisini kwa ajili ya mtumishi mwingine atakayekuja. Kawa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa iringa Bw. Fikira Kissimba amesema kuwa mfumo huo wa ukusanyaji taarifa zitasaidia pia uandikishwaji wa mirathi ya marehemu wakati ndugu husika anapokwenda kufungua mirathi yake mahakamani. 

Naye Mratibu wa usajili wa Takwimu wa Masuala muhimu ya Binadamu nchini kutoka wizara ya afya Dkt. Gregory Kabadi amesema kuwa jumla ya Kompyuta kibao (Tablets) zilizogawiwa ni 106 kwa kila kata ya mkoani Iringa na thamani yake ni takribani shilingi Milioni 61.5. Aidha , Dkt Kabadi amesema kuwa zoezi hilo limeanza kwa majaribio katika halmashauri tano kwenye mikoa mitatu ikiwemo Pwani,Tanga na Morogoro na kufanya tathimini ya utekelezaji wa mifumo hiyo katika mkoa wa Iringa kabla ya kutumika nchi nzima. 

Kwa upande wake Afisa afya wa kata ya Kitwilu Bw. Wilson Ntagondwa amesema kuwa kupitia mfumo huo waliokabidhiwa itawasaidia kukusanya takwimu kwa urahisi hivyo kupelekea kujua sababu zinazosababisha vifo na kusaidia kupanga maendeleo.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na baadhi ya Wakurugenzi wa halmashauri mbalimbali na Maafisa Afya mkoani Iringa wakati wa kukabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii kwa Maafisa Afya mkoani humo. 
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya katikati akionesha Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii pamoja na Maafisa afya wa kata mbalimbali Mkoani Iringa 
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa iringa Bw. Fikira Kissimba akiongea nna na baadhi ya Wakurugenzi wa halmashauri mbalimbali na Maafisa Afya mkoani Iringa wakati wa kukabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii kwa Maafisa Afya mkoani humo. 
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisyakushoto akimkabidhi Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mafinga Mji bw. Fredrick Kayombo kulia wakati wa kukabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii kwa Maafisa Afya mkoani humo. 
Mkurugenzi Msaidizi wa Ufuatiliaji na Tathimini kutoa Wizara ya Afya Bw. Tumainieli Macha wa kwanza kulia akifuatilia kwa makini maelekezo ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendelo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya hayupo pichani wakati wa kukabidhi Kompyuta Kibao ( Tablets) zanye mfumo maalum wa kukusanyia takwimu za vifo ngazi ya jamii kwa Maafisa Afya mkoani Iringa. 

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 19,2018.

Tigo Fiesta 2018 Dodoma, burudani ,mwanzo mwisho

$
0
0
-Baadhi ya Wabunge wapanda jukwaani kusakata Kwaito, Bolingo
-Bill Nas, Weusi , Whozu, Rosaree waacha historia


Wabunge na viongozi wa Serikali, jana walikuwa ni sehemu ya burudani ya aina yake katika Tamasha kubwa la muziki la Tigo Fiesta 2018, lililofanyika katika uwanja wa Jamuhuri mjini Dodoma.

Tamasha hilo lililofanikiwa kuwavuta mashabiki wa muziki wa bongo fleva kutoka mkoa huo na viunga vyake, lilianza kwa msanii Jay Melody kupanda jukwaani na kutoa burudani safi ‘iliyobamba’na kutengeneza mazingira safi kwa waliomfuatia .

Baada ya wasanii kadhaa kupanda jukwaani i, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi alipanda jukwaani kuongea mawili matatu kabla ya kuomba kuwekewa muziki wa bolingo ambalo alisakata kwa ustadi kmubwa jambo lililozua shangwe za ktosha.

Wakati Katambi akiendelea kusakata bolingo, baadhi ya wabunge wakiongozwa na mbunge wa Sengerema William Ngeleja waliomba kuwekewa muziki wa Kwaito ambao waliusakata kwa ufundi mkubwa na kusababisha shangwe kubwa kutoka kwa mashabiki.
 Baadhi ya Wabunge na viongozi wa Serikali wakisakata muziki katika Tamasha la Tigo Fiesta mwaka 2018 lililofanyika katika uwanja wa Jamuhuri Mkoani Dodoma mwishoni mwa wiki.
 Msanii wa muziki wa Hip Hop Fid Q akiwapagawisha mamia ya mashabiki walioshiriki katika tamasha la Tigo Fiesta mwaka 2018 lililofanyika uwanja wa Jamuhuri mkoani Dodoma.
 Msanii anayefanya vizuri kwenye muziki wa Hip Hop Rich Mavoko,  akiwaburudisha  mamia ya wakazi wa mkoa wa Dodoma na maeneo jirani walioshiriki katika Tamasha la Tigo Fiesta mwaka 2018 lililofanyika katika uwanja wa Jamuhuri Mkoani humo. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

MCHEZO WA MECHI YA YANGA NA NAMUNGO ULIVYOKUWA UWANJA WA MAJALIWA RUANGWA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wapenzi wa mpira wa miguu baada ya kukagua timu za Yanga na Namungo zilizocheza mechi ya kirafiki kwenye uwanja wa Majaliwa katika Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa Novemba 18, 2018. Kulia kwake ni mkewe Mary , wapili kushoto ni Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi. Timu hizo zilitoka sare 1-1. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Andrew Vincent wa Yanga akizuia mpira kwa kichwa huku akizongwa na  Reliant Lusajo wa Namungo katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye uwanja wa Majaliwa katika Halmashauri ya wilaya ya Rungwa Novemba 18, 2018. Timu hizo zilitoka sare 1 – 1
  Kiungo na mshambuliaji wa Yanga, Thaban Kamusoko akijaribu kufunga kwa tikitaka bila mafanikio mbele ya beki wa Namungo FC, Juma Jamal akimkabili katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye uwanja wa Majaliwa katika Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa Novemba 18, 2018. Kushoto ni Kipa wa Namungo FC,  Adam Oseja
 Reliant Lusajo wa Namungo FC  (kushoto) akimiliki mpira huku akizongwa na Juma Abdul wa Yanga katika mechi ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Majaliwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Novemba 18, 2018. Katika mchezo huo timu hizo zilitoka sare  1-1. 
Mashabiki wakishangilia

MICHUZI TV: MIAKA MITATU YA RAIS DKT MAGUFULI TUMEISHUHUDIA KWA VITENDO NA SI KWA MANENO-MABULA

Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images