Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110028 articles
Browse latest View live

MGOYI:SERIKALI IMEJENGA MAZINGIRA YA AJIRA KWA VIJANA KUPITIA MAPINDUZI YA VIWANDA

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii Mikumi

Serikali imejenga mazingira kwa vijana kupitia mapinduzi ya viwanda kwa serikali ya awamu ya Tano chini Rais Dkt John Pombe Magufuli ambapo ndio suluhisho ya vijana wenye ujuzi kutumika katika viwanda hivyo.

Hayo aliyasema Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi katika mahafali ya 21 ya Chuo VETA Mikumi ,amesema kuwa mafunzo ya VETA ndio uwanja mpana katika soko la ajira kwa vijana kujiajiri au kuajiriwa.

Amesema vijana waliohitimu ni zaidi 315 ambapo wanaenda katika soko la ajira hivyo wanaweza kujiunga katika vikundi na kuanza kuzalisha kile walichokipata kwa miaka waliosoma chuoni hapo. Wanachuo 315 wamehitimu mafunzo kwa ngazi ya (Level) II na III, kati yao wavulana walikuwa 209 na wasichana 106.

Amesema vijana hao wanahitaji mazoezi ya kutosha ili kuweza kupambana na soko la ufundi katika Jumuia ya Afrika Mashariki hivyo ili waweze kuwa na vigezo hivyo walimu wanahitaji kuongeza nguvu za ziada kwa vijana hao hasa walioko bado katika masomo. Mgoyi aliwaasa vijana kutokuitegemea sana serikali katika kuwatafutia ajira na badala yake watumie fursa ya mafunzo walio pata VETA Kwenda kutengeneza kampuni na kujiajiri wenyewe na kuajiri wenzao.

Aliwaasa vijana kutokuwa waoga katika katika kazi zao kwa yale walio fundishwa na kuwa wajasili ili waweze kuwaambia wateje na kuwaaminisha wateja ya kuwa wao ni bora, kwani wateja hawawezi kuwaamini kama wao watashindwa kuwaaminisha. Mkuu wa Wilaya huyo ameiomba VETA kuchangamkia fursa za uzalishaji mali kama wanavyofanya Jeshi ni katika ujenzi wa uchumi wa viwanda .

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adm Mgoyi akipata maelezo kwa mwafunzi wa Kozi ya Uselemala Chuo cha VETA Mikumi Mariam Anderson wakati wa mahafali ya 21 ya Chuo hicho.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi akizungumza katika mahafali ya 21 ya Chuo cha VETA Mikumi yaliyofanyika katika Viwanja vya Chuo hicho.
Mkurugenzi wa Kanda ya Mashariki wa VETA Geofrey Sabuni akizungumza kuhusiana na mikakati ya VETA katika utoaji ujuzi kwa vijana katika kmahafali ya 21 ya Chuo cha VETA Mikumi yaliyofanyika katika Viwanja vya Chuo hicho.
Aliyekuwa Mkuu wa Chuo cha VETA Mikumi Christopher Ayo akitoa salam kwa wahitimu ambao alikuwa nao wakati akihudumu cheo hicho katika chuo  katika mahafali ya 21 ya Chuo cha VETA Mikumi yaliyofanyika katika Viwanja vya Chuo hicho.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha VETA Mikumi Emmanuel Munuo akitoa taarifa ya chuo katika mahafali ya 21 ya Chuo cha VETA Mikumi yaliyofanyika katika Viwanja vya Chuo hicho.
Mchoro wa Ramani waliochora wanafunzi wa kozi ya ujenzi katika Chuo cha VETA Mikumi.


Naibu Waziri Mavunde Aahidi Ushirikiano Baina ya Ofisi Yake na CBE Katika Kukuza Ujuzi kwa Vijana

$
0
0


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde akimkabidhi zawadi mmoja ya wanafunzi aliyeongoza katika taaluma alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 53 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) leo jijini Dodoma.Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Anthony Mavunde akitoa tamko la kuwatunuku wahitimu wa ngazi Astashahada, Stashahada na Shada katika fani za Uhasibu, Biashara, Masoko na Ununuzi toka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 53 ya Chuo hicho leo jijini Dodoma.
Baadhi ya wahitimu wa Shahada ya Uhasibu wakifurahia burudani kutoka kwa mwanadada aliyekuwa akionyesha kipaji cha kuchezea mpira katika mahafali ya 53 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) leo jijini Dodoma.
Baadhi ya wahitimu wakitunukiwa shahada zao wakati wa mahafali ya 53 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) leo jijini Dodoma. (Na: Mpiga Picha Wetu).

BILIONI 2 ZIMEKWISHATOLEWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO

$
0
0

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii Mtwara

SERIKALI Kupitia Benki ya kilimo Tanzania(TADB) imetoa kiasi cha Shilingi Bilioni 2 kwa wakulima wa korosho wa mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma katika malipo ya kundi la kwanza la watu ambao wamehakikiwa kupitia vyama vya msingi na vyama vya ushirika.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Novemba 17, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga, amesema TADB imeanza kulipa wakulima wote walioakikiwa katika mikoa tajwa kupitia vyama vyao vya Msingi na ushirika kwa kuhakikisha fedha hizo zinawafikia wakulima moja kwa moja kupitia akaunti zao.

"zoezi la ulipaji limeanza jana na kwasasa tumewafikia wakulima zaidi ya 2168 kutoka mikoa mitatu tulionza nayo hivyo tunategemea kuendelea kulipa mpaka kufikia jumatatu tutakuwa tushalipwa wakulima wengi sana kama ilivyoagizwa na Rais Dk . John Pombe Magufuli kutaka fedha hizo ziende kwa wakulima moja kwa moja bila ya makato"amesema Waziri Hasunga.

katika hatua nyingine Waziri wa Kilimo ametangaza kuwa jumla ya Tani 20 za korosho zimekamatwa kutoka ghala la mtu binafsi la Olam lililoko mkoani Mtwara ambapo zilikuwa zinahamishwa kwenda kwenye eneo la ununuzi wakati zikiwa ni za mwaka jana.

amesema korosho hizo zilikabidhiwa katika Chama cha Msingi cha Mnyawi kwa lengo la kuchanganywa kinyemela na zile zinazopelekwa kwenye maghala makuu.“Jana (juzi) tulikamata tani 20 zilizokuwa zimepenyezwa katika vyama vya msingi, tusingependa lijirudie hivyo, wananchi wawe makini kuhakikisha korosho zinazoletwa katika vyama vya msingi ni zile za Watanzania ili korosho yetu peke yake iendelee kununuliwa na Serikali,” amesema Hasunga.

Amesema korosho zitakazokamatwa kutoka nje au kuingizwa kinyemela kwenye vyama vya msingi zitataifishwa na wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.Jumanne wiki hii tani nyingine tisa zilikamatwa katika eneo la Newala baada ya kuingizwa kinyemela toka nchini Msumbiji.Aidha juzi pia yalikamatwa magunia 152 ya korosho katika Wilaya ya Nanyumbu yaliyoingizwa nchini kutoka Msumbiji.
Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga,akizungumza na Waandishi wa Habari juu kiasi cha shilingi Bilioni mbili zilizotolewa katika awamu ya kwanza
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ) Luteni Jenerali , Yacoub Mohamedi akizungumza na waandishi wa habari leo Mkoani Mtwara juu ya Zoezi la ulipaji na ukusanyaji wa korosho. 
Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga,akizungumza na Waandishi wa Habari juu kiasi cha shilingi Bilioni mbili zilizotolewa katika awamu ya kwanza
Baadhi ya Malori yaliyopo katika Mkoani Mtwara kwa ajili kubeba korosho na kuzipeleka katika maghala Maalum yaliyotengwa. 
WMajengo ya Bodi ya Korosho kama yanavyonekana kwa nje mkoani Mtwra ambapo kwa sasa macho na masikio ya wanahabari wanayaangazia hapo kujua mfumo mzima wa ulipwaji unakwendaje.

ZIARA YA WAZIRI MUU KASSIM MAJALIWA WILAYANI NACHINGWEA

$
0
0



 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia upinde aliopewa na wazee wa kijiji cha Kilimarondo wilayani Nachingwea ikiwa ni ishara ya kumtakia ulinzi wakati wote anapotimiza majukumu yake ya kulitumikia taifa.  Alikuwa katika mkutano wa hadhara aliouhutubia kijijini hapo, Novemba 17, 2018.
AAA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia upinde aliopewa na wazee wa kijiji cha Kilimarondo wilayani Nachingwea ikiwa ni ishara ya kumtakia ulinzi wakati wote anapotimiza majukumu yake ya kulitumikia taifa.  Alikuwa katika mkutano wa hadhara aliouhutubia kijijini hapo, Novemba 17, 2018.
AAAAAA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akimsikiliza Mwenyekiti wa kijiji cha Mtua, wilayani Nachingwea, Anthony Makota   wakati  aliposoma taarifa kuhusu matatizo yanayokikabili kijiji hicho mbele ya   Waziri Mkuu ambaye alisimama kijijini hapo kuwasalimia wananchi, Novemba 17, 2018 . Kulia ni Mbunge wa Nachingwea, Hasan Masala. Picha na Ofisi ya Wazri Mkuu)

MAGUNIA 45 YA KOROSHO YAKAMATWA PWANI YAKISAFIRISHWA -WANKYO

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,PWANI

JESHI la polisi mkoani Pwani wanalishikilia lori dogo kwa tuhuma za kukutwa na korosho magunia 45 yenye uzito wa kilogramu 81 .

Korosho hizo zinadaiwa zilikuwa zikisafirishwa kwenda kwenye chama cha msingi cha ushirika kinyume na agizo la Rais Dk John Magufuli kutaka korosho zote kusafirishwa na magari ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).

Kamanda wa polisi mkoani Pwani ,Wankyo Nyigesa alisema ,gari hilo linahisiwa kusafirisha korosho hizo kuwa hazijapatikana kihalali.Alieleza, tukio hilo lilitokea novemba 16 mwaka huu ambapo askari kwa kushirikiana na Mrajisi Msaidizi mkoa wa Pwani Angela Nalimi.

"Gari hilo aina ya Canter lenye namba za usajili T 731DGG lilikuwa likizipeleka korosho hizo zikiwa kwenye magunia yenye nembo ya chama kikuu cha ushirika mkoa wa Pwani (CORECU) kwenda chama cha ushirika cha msingi cha Misugusugu wilayani Kibaha," alisema Nyigesa.Baada ya uchunguzi kukamilika watuhumiwa na gari lao watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili ikiwa watabainika walikuwa wanunuzi wasio ruhusiwa na serikali.
Kamanda wa polisi mkoani Pwani ,Wankyo Nyigesa

MICHUZI TV:BILIONI 2 ZAKABIDHIWA KWA WAKULIMA ZAIDI YA 2000 WA KOROSHO

MICHUZI TV: JWTZ WAKO KAMILI KATIKA ZOEZI LA UKUSANYAJI KOROSHO

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 18,2018


POLISI PWANI YAMSAKA MWANAMKE ALIYEMPIGA MWANAE WA MIAKA MITANO HADI KUMSABABISHIA KIFO -NYIGESA

$
0
0

NA MWAMVUA MWINYI, PWANI
JESHI la polisi mkoani Pwani ,linamtafuta mwanamke ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja kwa tuhuma za kumpiga hadi kumuua mtoto  wake Halima Ramadhani (5) kwa tuhuma za kuunguza pazia la chumbani.

Kamanda wa polisi mkoani humo Wankyo Nyigesa alithitisha kutokea kwa tukio hilo la kusikitisha huko Kikongo wilaya ya Kipolisi Mlandizi wilayani Kibaha

Alisema mama huyo ,  alimuua mwanaye kwa kipigo akimtuhumu mwanaye huyo kuunguza pazia hilo kwa kutumia kibatari.

"Baada ya kukuta pazia hilo limeungua mama yake alimshambulia na kupelekea kifo cha mtoto huyo na alipoona hali mbaya alikimbia," alisema Nyigesa.

Alisema,mtoto huyo alifariki alipofikishwa katika kituo cha Afya Mlandizi siku hiyo hiyo majira ya saa nne usiku.

MALIPO HEWA YA KOROSHO YABAINIKA NEWALA

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya Newala Mhe Aziza Mangozongo akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama katika Kuhakiki Majina ya Wakulima katika Makonga Amcos na kubaini Watu wawili(2),Karani wa Chama cha Msingi Makonga Asma Rajabu kwa kosa la  kumuandikia malipo Hewa  ya kilo Hewa 221kg ya korosho na Mohamed Hamisi Namkunga ambaye ameandikisha Majina Hewa tofauti Mara Tatu na Account Hewa kwa lengo ya kufanya Malipo Hewa.Mh.Aziza amesema huo ni mtindo mpya wa Kangomba. 

Mkuu Wa Wilaya Newala amethibitisha kukamatwa kwa watu hao leo  na kusema Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi ili Sheria ichukue mkondo wake.

Aidha  amewataka Viongozi wa Vyama vya Msingi/Amcos na Makarani kuwa Wazalendo na kuandika Malipo sahihi kwa Wakulima.

Newala tutahakikisha kwa Kila hatua tunakuwa makini mpaka Mwisho. 

Imetolewa 
Mwansishi Wetu
Newala.

Agizo la Rais Magufuli laanza kutekelezwa wilayani Ukerewe

KONGAMANO LA UWT LAFANA,LATOA TUZO KWA MWENYEKITI WAO RAIS DKT MAGUFULI KWA UTEKELEZAJI THABITI WA ILANI YAO YA CHAMA

$
0
0
 
  Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Idara ya Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole akipokea tuzo ya pongezi kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli, baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Gaudentia Kabaka katika Kongamano la Jumuiya hiyo , kumpongeza Rais Dk. Magufuli kutimiza miaka mitatau tangu aingie madarakani na pia kwa utekelezaji thabiti wa Ilani ya CCM, lililofanyika katika Ukumbi wa PTA, Temeke, Dar es Salaam, Novemba 17,2018. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Mwalimu Queen Mlozi.
  Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Idara ya Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole akisoma ujumbe ulioandikwa kwenye tuzo hiyo ya pongezi  kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli, baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT) Gaudentia Kabaka katika Kongamano la Jumuiya hiyo , kumpongeza Rais Dk. Magufuli kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM, lililofanyika katika Ukumbi wa PTA, Temeke, Dar es Salaam, Novemba 17,2018. 
Katibu Mkuu wa UWT Taifa Mwalimu Queen Mlozi akishereheka pamoja na washiriki mbalimbali waliofika kwenye kongamano hilo lililofana kwa kiasi kikubwa,huku likihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama.
 
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya CCM ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Gaudentia Kabaka akielekezwa jambo na Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo Mwalimu Queen Mlozi, katika Kongamano la kumpongeza Rais Dk. Magufuli kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM, lililofanyika katika Ukumbi wa PTA, Temeke, Dar es Salaam, Novemba 17,2018.
Baadhi ya  Washiriki wakishangilia wakati wa Kongangamano la Jumuiya ya Chama Cha Mapinduzi ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kumpongeza Mwenyekiti wao CCM, Rais Dk. John Magufuli kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM, lililofanyika Novemba 17,2018 katika Ukumbi wa PTA, Temeke, Dar es Salaam. 
  Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Idara ya Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole alipokuwa akiwasili katika  katika Kongangamano la kumpongeza Rais Dk. Magufuli kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM, lililofanyika katika Ukumbi wa PTA, Temeke, Dar es Salaam, Novemba 17,2018.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli Apongezwa kwa Kuwezesha Wanyonge

$
0
0

Frank Mvungi- MAELEZO, Njombe

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amepongezwa kwa kuendelea kuwawezesha wajasiriamali kupitia Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) .

Akizungumza wakati akifunga mafunzo ya siku 10 kwa wajasiriamali zaidi ya 700 wa Mjini Njombe Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Christopher Ole Sendeka amesema kuwa swala la urasimishaji Biashara kwa wajasiriamali ni takwa la Kisheria na pia ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ibara ya 58 ambapo Biashara zote zinatakiwa kuendeshwa katika mfumo rasmi na Serikali ya Awamu ya Tano imeweka mkazo mkubwa ili kuwainua wajasiriamali wanyonge.

“ Nawapongeza MKURABITA na Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa kufanikisha mafunzo haya kwa wajasiriamali yanayolenga kuwajengea uwezo ili waweze kurasimisha Biashara zao na pia kuanzishwa kwa Kituo Kimoja cha Urasimishaji Biashara hapa Njombe itakuwa ukombozi kwa wajasiriamali wetu”; Alisisitiza Ole Sendeka.

Akifafanua Mhe. Ole Sendeka amesema kuwa kuanzishwa kwa Kituo cha Urasimishaji na Uendelezaji wa Biashara Mjini Njombe kumewashirikisha wadau kama MKURABITA, TRA, SIDO na Benki mbalimbali ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kukabiliana na tatizo la Ongezeko la Biashara ndogo na za kati zisizo rasmi na ambazo zinakuwa kwa kasi.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka akifunga mafunzo kwa wajasiriamali zaidi ya 700 wa Mjini Njombe yaliyoratibiwa na Ofisi ya Rais, Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) yakilenga kuwajengea uwezo wajasiriamali hao ili waweze kurasimisha Biashara zao. Hayo yamejiri leo tarehe 17/11/2018 Mjini  humo. 
Sehemu ya Wajasiriamali hao zaidi ya 700 wa Mjini Njombe wakifuatilia hafla ya ufungaji mafunzo hayo iliyofanyika mjini humo ambapo Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Christopher Ole Sendeka alikuwa mgeni rasmi. Mafunzo hayo  yamelenga kuwajengea uwezo wajasiriamali hao ili waweze kurasimisha Biashara zao. 
Mratibu wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) Bi. Seraphia Mgembe akizungumzia faida za mafunzo waliyopata Wajasiriamali zaidi ya 700 wa mjini Njombe yakilenga kuwajengea uwezo ili warasimishe Biashara zao na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi. 
Mmoja wa wajasiriamali walinufaika na mafunzo yakuwajengea uwezo ili waweze kurasimisha Biashara zao Bw. Lucas Kawongo akifurahia cheti alichotunukiwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe wakati akifunga mafunzo kwa  wajasiriamali zaidi ya 700 wa Mjini Njombe. 
Mhasibu wa Mapato kutoka Halmashauri ya Mji wa Njombe Bw. George C. Mwasera akipokea cheti cha kuhitimu mafunzo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais- MKURABITA yakilenga kuwajengea uwezo wajasiriamali ili warasimishe Biashara zao.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka akiwasili ukumbini  kufunga mafunzo kwa wajasiriamali zaidi ya 700 yaliyoandaliwa na MKURABITA yakilenga kuwajengea uwezo wajasiriamali hao ili warasimishe biashara zao. 


KAIMU MTENDAJI MKUU TEMESA AFANYA ZIARA KUKAGUA USALAMA WA VIVUKO MIKOA YA KUSINI

$
0
0


Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle (wan nne kulia) akitoa maelekezo kwa mafundi wakati akikagua fitokombo (‘crankshaft’) mashine ya kuchonga vipuri vya injini za magari katika karakana ya TEMESA mkoa wa Mtwara wakati wa ziara yake mkoani humo kukagua utendaji kazi na kusikiliza kero mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi wa wakala huo.Wa pili kulia ni Kaimu Meneja wa TEMESA mkoa huo Rocky Sabigoro.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akimpa maelekezo Mkuu wa Kivuko Kilambo Namoto ndugu Dhulkif Hamdan kulia wakati wa ziara yake ya kukagua usalama wa vivuko katika mikoa ya kusini. Kivuko cha MV. KILAMBO kinatoa huduma kati ya Kilambo na Namoto mkoani Mtwara.
Abiria wa kivuko cha MV. KITUNDA kinachotoa huduma kati ya Kitunda na Lindi mjini wakimsikiliza kwa umakini mfanyakazi wa kivuko hicho wakati akiwapa elimu ya jinsi ya kuvaa boya la kujiokolea pindi inapotokea ajali ya maji.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akitoa maagizo kwa Meneja wa TEMESA mkoa wa Lindi Mhandisi Grayson Maleko kulia wakati akikagua ujenzi wa jengo la abiria kusubiria kivuko (‘waiting lounge’) katika kivuko cha Lindi kitunda. Majengo hayo pamoja na vyoo yanajengwa pande zote mbili za kivuko na yanatarajiwa kumalizika hivi karibuni na kuanza kutumiwa na abiria wa kivuko hicho.
Abiria wa kivuko cha MV. KITUNDA kinachotoa huduma kati ya Kitunda na Lindi mjini mkoani Lindi wakishuka kutoka kwenye kivuko hicho baada ya kuwasili kutokea Kitunda. Kivuko hicho kimekua msaada mkubwa kwa wakaazi wa maeneo hayo ambao kabla ya ujio wa kivuko walikua wakivuka kwa kutumia mitumbwi midogo ambayo ilikua ikihatarisha usalama wao kwa kiasi kikubwa.
Kivuko cha MV. KITUNDA kikielea majini wakati kikikaribia maegesho ya Lindi Mjini kutokea Kitunda. Kivuko hicho kimekua msaada mkubwa kwa wakaazi wa maeneo hayo ambao kabla ya ujio wa kivuko walikua wakivuka kwa kutumia mitumbwi midogo ambayo ilikua ikihatarisha usalama wao kwa kiasi kikubwa.

MHAGAMA AFUNGUA RASMI OFISI NDOGO ZA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI MKOANI KAHAMA

$
0
0

Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye Ulemavu Mhe Jenista Mhagama akimkabidhi Meneja wa NSSF Kahama Ndugu Winston Mundigile Ufunguo wa Ofisi Ndogo alipofungua rasmi kituo cha uwezeshaji wananchi kiuchumi Mkoani Kahama. Taasisi mbalimbali zimepewa ofisi ndogo ili kutoa elimu na rasilimali nyingine ili kuwakwamua wananchi wa Wilaya ya Kahama Kiuchumi
Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye Ulemavu Mhe Jenista Mhagama akisalimiana na Baadhi ya Wafanyakazi wa NSSF Kahama katika Ofisi Ndogo ya NSSF alipofungua rasmi kituo cha uwezeshaji wananchi kiuchumi Mkoani Kahama. Taasisi mbalimbali zimepewa ofisi ndogo ili kutoa elimu na rasilimali nyingine ili kuwakwamua wananchi wa Wilaya ya Kahama Kiuchumi 

MAJALIWA AWAPONGEZA WALIMU NA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI WILAYANI RUANGWA KWA KUFANYA VIZURI KATIKA MTIHANI WA DARASA LA SABA

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe Mary (kulia) wakimpongeza Mwanafunzi Halfani Abdallah Ngonde aliyemaliza Elimu ya Msingi katika Shule ya Nanjaru wilayani Ruangwa na ambaye aliibuka kuwa mwanafunzi bora wa Mkoa wa Lindi katika Matokeao ya Mtihani wa Darasa la Saba kwa mwaka huu. Waziri Mkuu alikuwa katika mkutano wa kuwapongeza walimu wa na baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi za wilaya ya Ruangwa ambayo imefanya vizuri na kuwa ya kwanza katika mkoa wa Lindi. Mkutano huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Narung’ombe katika Halmashauri ya Ruangwa, Novemba 18, 2018. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MAKAMU WA RAIS AMTEMBELEA NA KUMPA POLE WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE.SUMAYE

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amemtembelea na kumpa pole Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Frederick Sumaye nyumbani kwake Endasak, Hanang kufuatia kufiwa na Mama yake mzazi.Bibi Elizabeth Gisa Sumaye alifariki tarehe 7 Novemba 2018. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo akisaini kitabu baada ya kumtembelea na kumpa pole Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Frederick Sumaye nyumbani kwake Endasak, Hanang kufuatia kufiwa na Mama yake mzazi.Bibi Elizabeth Gisa Sumaye alifariki tarehe 7 Novemba 2018.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

BALOZI ADADI AWAFUNDA VIJANA TAMASHA LA UTAMADUNI WA BONDE

$
0
0
MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu amewataka vijana wilayani humo kuacha kuvaa suruali na kuzishusha chini maarufu kama milegezo, mini sketi kwani kufanya hivyo kunapelekea kuondoa utamaduni wa kitanzania hususani za watu wa bonde kupotea badala yake wavae nguo za asili zenye heshima. 

Kwani uvaaji huo wa nguo unapelekea kupoteza mila na tamaduni ambao uliopo huku akiwataka kubadilika kwa kuhakikisha wanavaa mavazi asili ambayo ni desturi kwa watanzania. 

Hayo yalisemwa na Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu wakati wa Tamasha la Bonde ambalo lilifanyika Kata ya Kicheba wilayani Muheza lililokwenda sambamba na maonyesho ya vitu mbalimbali vya asili ikiwemo vyakula. 

“Tamasha la Bonde linapaswa tuliendeleze kwa vizazi vya sasa na vijavyo waweze kujua tamaduni na mila zao ,lakini pia mambo ya mavazi badala ya kuvaa milegezo, mini sketi huku mavazi na desturi zetu vinapotea tuvae nguo za asili zenye heshima kwani bila kufanya hivyo mavazi na desturi vitapotea”Alisema Mbunge huyo .Mbunge huyo alisema pia ni muhimu tamaduni za kibondei kuhakikisha zinaendelezwa kila mwaka kupitia tamasha hilo kwa kuyafadili ili vijazi vya sasa na vijavyo viweze kujua mila zao huku akiwasisitiza wazee waliopo kutokuondoka nazo maana vijana wanaozaliwa wanaweza kuona mambo hayo hayawezekani. 
Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kushoto akiwa na Zumbe wa Kitulwe Tibua Charles Nkuninga kulia wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye Tamasha la Bonde ambalo lilifanyika Kata ya Kicheba wilayani Muheza lililokwenda sambamba na maonyesho ya vitu mbalimbali vya asili ikiwemo vyakula
Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu akizungumza wakati wa Tamasha hilo 
Afisa Utamaduni wa wilaya ya Muheza Msafiri Charles Nyaluka akizungumza katika Tamasha hilo
Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kushoto akitazama bidhaa mbalimbali vinavyotengenezwa na wakima mama wa Kibondei wakati alipotembelea Maonyesho hayo wakati Tamasha la Bonde lililofanyika eneo la Kicheba wilayani Muheza
MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kulia akilakiwa na wananchi wa Kijiji Kicheba Kata ya Kicheba wilayani Muheza wakati alipokwenda kwenye Tamasha la Bonde. 

Muhimbili Kuvunja Rekodi ya Miaka 15, Watoto 21 Watibiwa

$
0
0

Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imepata mafanikio makubwa baada ya kufanya upasuaji wa kupandikiza vifaa vya kusaidia kusikia kwa watoto 21 ndani ya miezi 17 ukilinganisha na watoto 50 waliopandikizwa vifaa hivyo miaka 15 iliyopita nchini India.

Kila mwaka Serikali ilikuwa ikipeleka wagonjwa nchini India kwa ajili ya kupandikizwa vya vifaa vya kusaidia kusikia na hadi kufikia mwaka 2016, wagonjwa 50 tu walikuwa wamenufaika na huduma hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Masikio, Pua na Koo wa Muhimbili, Dkt. Edwin Liyombo amefafanua kwamba hospitali hiyo itavunja rekodi kwa kuwa hadi sasa tayari wagonjwa 21 ndani ya miezi 17 kuanzia Juni mwaka 2017 hadi Novemba 2018 sawa na asilimia 42 wamepatiwa matibabu tofauti na wagonjwa 50 waliopelekwa India katika kipindi cha miaka 15 iliyopita kuanzia 2003 hadi 2016.

Dkt. Liyombo amesema mwaka 2003 Serikali ilianza kupeleka wagonjwa nchini India kwa ajili ya kupandikizwa vifaa vya kusadia kusikia na kwamba idadi ya wagonjwa imekuwa ikiongezeka. Dkt. Liyombo amesema kwamba gharama ya kutoa huduma hiyo kwa mgonjwa mmoja katika Hospotali ya Taifa Muhimbili ni Tshs. 37 milioni wakati India kwa mgonjwa mmoja ni Tshs. 80 milioni hadi Tshs. 100 milioni.

Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Masikio, Pua na Koo wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Edwin Liyombo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu upasuaji wa kupandikiza vifaa vya kusaidia kusikia kwa watoto 10 ambao umefanywa na wataalam wa Muhimbili kwa kushirikiana na mtaalam kutoka nchini Misri. 
Watoto waliopandikizwa vifaa vya kusaidia kusikia wakiwa wodini baada ya kupatiwa huduma hiyo. 
Pichani ni baadhi ya watoto waliopandikizwa vifaa hivyo.

Dkt. Liyombo akiwaeleza waandishi wa habari jinsi vifaa vya kusaidia kusikia vinavyofanya kazi baada ya mwezi mmoja. 


MAWAZIRI WAKUTANA KUJADILI UTEKELEZAJI WA PROGRAMU YA PAMOJA YA UJENZI WA UCHUMI WA VIWANDA

$
0
0


Mawaziri wa sekta za uchumi wamekutana Jijini Dodoma kujadili utekelezaji wa Programu ya pamoja ya Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda.

Akizungumza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ambaye alikuwa Mwenyekiti wa mkutano huo alisema kuwa Programu ya ujenzi wa uchumi wa viwanda imejikita katika kuweka mazingira wezeshi ya biashara na uwekezaji nchini kwa lengo la kuvutia sekta binafsi na kuongeza fursa za ajira.

“Programu hiyo itakuza uchumi na ujenzi wa viwanda kwa kufuata misingi na kanuni za kibiashara zinazokubalika kimataifa, ikiwakama nyenzo muhimu katika kuhakikisha viwanda vitakavyoanzishwa vinakuwa chachu ya maendeleo hapa nchini,” alisemaMhagama.

Aliongeza kuwa Serikali imedhamiria kutekeleza kwa vitendo azma ya ujenzi wa uchumi wa viwanda ili kufikia malengo ya dira ya Taifa ya maendeleo ya kuiwezesha Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo 2025.
Hata hivyo, Waziri Mhagama alieleza kuwa Programu hii ya pamoja inatokana na kutegemeana kwa mipango na mikakati ya kisekta katika kufikia malengo ya Serikali kwa pamoja.

Aidha, alitoa rai kwa kila mmoja kuhakikisha sekta anayoiongoza inatoa mchango stahiki katika kufikia azma ya Serikali kwa kuweka malengo yanayotekelezeka kwa wakati na kufanya mapitio ya sera, sharia na kanuni.
“Niwaombe wote mliopo hapa kuhakikisha mnatimiza wajibu kwa kutekeleza Programu hii ya ujenzi wa uchumi wa Viwanda ikiwa njia ya uhakika katika kuhakikisha rasilimali za Taifa zinatumika kwa manufaa ya nchi na kuweza kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania” alisisitiza Mhagama. 
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akizungumza jambo wakati akifungua kikao cha Mawaziri wa Sekta za uchumi walipokutana kujadili utekelezaji wa Programu ya pamoja ya ujenzi wa uchumi wa viwanda katika ukumbi wa mikutano wa Waziri Mkuu Bungeni Jijini Dodoma, Novemba 17, 2018.
????????????????????????????????????
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Joseph Kakunda (Mb) akielezea utekelezaji wa Wizara yake wakati wa kikao hiko walipokutana kujadili utekelezaji wa Programu ya pamoja ya ujenzi wa uchumi wa viwanda, Jijini Dodoma.
????????????????????????????????????
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akisisitiza jambo wakati wa Kikao hiko cha Mawaziri wa Sekta za kiuchumi walipokutana kujadili utekelezaji wa Programu ya pamoja ya ujenzi wa uchumi wa viwanda, Jijini Dodoma.
????????????????????????????????????
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa (Mb) akielezea umuhimu wa kila Wizara kutekeleza majukumu kwa haraka ili kutimiza malengo wakati wa Kikao hicho.
????????????????????????????????????
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Sekta Binafsi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Ezamo Maponde akiwasilisha mada kwa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Sekta za Kiuchumi walipokutana Jijini Dodoma.

Viewing all 110028 articles
Browse latest View live




Latest Images