Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110118 articles
Browse latest View live

MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 16,2018


MSHINDI WA NYUMBA ALIA KWA UCHUNGU KUFUATIA USHINDI WA BIKO

$
0
0
Mshindi wa nyumba na sh milioni 20 wa Biko, Prisca Msuya wa Mbezi jijini Dar es Salaam, amelia kwa uchungu mbele ya waandishi wa habari wakati anakabidbiwa hundi ya ushindi wake wa fedha na nyumba kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) iliyopo Kigamboni, huku akishuhudiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Biko, Charles Mgeta.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, mama huyo ambaye ni mjasiriamali mdogo wa duka, alisema kitu kinachomliza ni kushinda nyumba na sh milioni 20 kutoka Biko, huku akitokea kwenye maisha duni ya kuishi kwenye chumba na sebule. 

“Siamini macho yangu kwamba kweli nimeshinda nyumba kutoka Biko, maana maisha yangu ya nyuma anayajua Mungu, ingawa tangu Biko inaanza nilikuwa namuomba Mungu ili niweze kushinda zawadi za juu ikiwamo sh milioni 10, jambo ambalo Mungu amenitimizia mara mia moja. “Kwakweli namshukuru sana Mungu kwa zawadi hii pamoja na kuwaombea Biko katika mtazamo wao wa kuleta utajiri kwa watu wake, hivyo Watanzania wote naomba tucheze Biko kwa sababu ndio michezo halali unaoweza kutoa mamilioni pamoja na nyumba,”Alisema. 

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Biko, Charles Mgeta, alisema mchezo wao umeanzishwa kwa lengo moja la kuwakwamua Watanzania, wakiwamo wadau wa kubahatisha, akisema kila mtu anapoibuka na ushindi anazunguukwa na watu wanaotumia ushindi huo kuboresha maisha yao kwa pamoja. “Leo hii tunamkabidhi dada Prisca fedha na nyumba, ila tunaamini wapo watoto wake, mume na ndugu ambao kwa namna moja ama nyingine watakuwa wamekwamuliwa na mchezo wetu wa Biko. 

Mkurugenzi Mkuu wa Biko, Charles Mgeta wa pili kutoka kulia akimkabidhi hundi ya sh milioni 20 na nyumba iliyopo Kigamboni mshindi wao Prisca Msuya wa katikati aliyeibuka kidedea kwenye droo kubwa iliyochezwa juzi Jumatano. Wengine ni Afisa Leseni wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Catherine Lamwai kushoto akifuatiwa na Kajala Masanja Balozi wa Biko pamoja na Meneja Mauzo wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Tuntufye Mwambusi. Picha na Mpigapicha Wetu.

Mkurugenzi Mkuu wa Biko, Charles Mgeta akimkabidhi hundi ya sh milioni 20 na nyumba iliyopo Kigamboni mshindi wao Prisca Msuya aliyeibuka kidedea kwenye droo kubwa iliyochezwa juzi Jumatano. 

ALIYEKUWA MBUNGE WA TEMEKE ABDALAH MTOLEA AOMBA KUJIUNGA NA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

$
0
0
Wakati tarehe ya mwisho ya kupokea viongozi wa upinzani wanao omba kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikifika leo hii, Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Temeke kwa tiketi ya Chama cha CUF Abdalah Mtolea amejivua uanachama wa CUF na kujiuzuru Ubunge wa Jimbo la Temeke, huku akieleza chanzo kikiwa migogoro isiyoisha katika Chama cha CUF kwa zaidi ya miaka miwili sasa. Tukio la kujivua uanachama wa CUF na kujiuzuru ubunge lilitokea ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wakati akichangia hoja katika mjadala uliokuwa unaendelea mapema leo.

Ndugu Abdalah Mtolea jioni ya leo ametangaza nia yake ya kuomba kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) akieleza msingi wa uamuzi huo ukiwa umejengwa katika ukweli kwamba wengi ya wapiga kura wake wamemshauri kujiunga na CCM.

Akizungumza katika kikao cha waandishi wa habari, watumishi na baadhi ya wanachama wa CCM katika Ofisi ya Makao Makuu ya CCM Jijini Dodoma, Ndugu Mtolea ameeleza sababu zinazopelekea kuomba kujiunga na CCM na kuwa amevutiwa na Mageuzi makubwa ya Kiuongozi na kazi nzuri inayofanywa na CCM na Serikali yake chini ya Ndugu John Pombe Joseph Magufuli Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kikao hicho cha waandishi wa habari, watumishi na baadhi ya wanachama wa CCM kimehudhuriwa pia na Kamaradi Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM ambaye amemwelekeza kwenda katika tawi lililo karibu na makazi yake Wilayani Temeke, Jijini Dar es Salaam ili afuate utaratibu wa kuomba uanachama wa CCM.



Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM
Ndugu Bashiru Ally akizungumza jambo wakati wa kikao cha Watumishi na baadhi ya Wanachama wa CCM,kushoto aliyekubwa Mbunge wa Temeke kwa Tiketi ya CUF Ndugu Abdalah Mtolea
  Ndugu Bashiru Ally Katibu Mkuu wa CCM na kushoto na aliyekubwa Mbunge wa Temeke kwa Tiketi ya CUF Ndugu Abdalah Mtolea Wakifurahia Jambo
Kikao cha Watumishi na Baadhi ya Wanachama wa CCM na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Bashiru Ally Kakurwa ambacho kilipata bahati ya kupokea kauli ya Ndugu Mtolea kuomba kujiunga na CCM.

MKUU WA JESHI LA MAGEREZA AKUTANA NA RC NJOMBE KABLA YA KUHITIMISHA ZIARA YAKE

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini (CGP) Phaustine Kasike akielezea malengo ya ziara yake ya kikazi mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe alipotembelea Ofisi za Mkoa huo.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike akikagua mashamba ya chai ya Gereza Njombe kabla ya kuhitimisha ziara yake, leo Novemba 15, 2018.
Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP. Phaustine Kasike akiagana na baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi Mkoani Njombe ambao waliongoza msafara wa Kamishna Jenerali katika vituo vyote alivyotembelea Mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Christopher Ole Sendeka (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike(wa pili toka kulia) pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Njombe. Wa pili toka kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Njombe, Bw. Erick Shitindi ( Picha na Jeshi la Magereza).
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Christopher Ole Sendeka akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini (CGP) Phaustine Kasike alipotembelea Ofisi za Mkuu wa Mkoa kabla ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi, leo Novemba 15, 2018.

VODACOM TANZANIA FOUNDATION YAKABIDHI VIFAA VYA KULINDA MAISHA YA WATOTO NJITI HOSPITALI YA RUFAA DODOMA

$
0
0

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kulia) akizungumza wakati makabidhiano ya mashine ya kusaidia kupumua kwa Watoto njiti ilivyotolewa na taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation kwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ili kusaidia kupunguza vifo vya Watoto Njiti. Kushoto ni Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation Rosalynn Mworia, Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel (kati).

Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation Rosalynn Mworia, akikabidhi mashine ya kusaidia kupumua kwa Watoto njiti kwa Waziri wa Madini Angellah Kairuki (wa pili kulia) na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayesimamia Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na walemavu Anthony Mavunde (kulia) katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ili kusaidia kupunguza vifo vya Watoto Njiti. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel, Bi Doris Mollel.
Afisa Muuguzi Msaidizi kutoka Kitengo cha kuhudumia Watoto Njiti Constancia Mankupe akielezea kwa vitendo namna mashine ya kusaidia kupumua kwa Watoto njiti inavyofanya kazi, mashine hii ni mojawapo kati ya vifaa tiba vyenye thamani Sh 25 m vilivyotolewa na taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation vilivyokabidhiwa kwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ili kusaidia kupunguza vifo vya Watoto Njiti. Kulia kwake ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayesimamia Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na walemavu Anthony Mavunde na Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel, Doris Mollel.


JWTZ WAANZA UTEKELEZAJI WA AGIZO LA RAIS WILAYA YA NEWALA MKOANI MTWARA

$
0
0

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii Newala, Mtwara

Mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo leo amepokea ujumbe wa Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ )ambao umeanza kukagua Maghala yote ya kuhifazia korosho katika Wilaya hiyo kama ilivyoagizawa na Rais John Pombe Magufuli kufuatia Wafanyabiashara kutaka kuwalangua wakulima kwa kununua kwa bei isiyokuwa na Maslahi.

Ujumbe huo ambao ulipata nafasi ya kutembelea Maghala yote Makubwa ambayo yapo katika Wilaya yake hili waweze kuanza zoezi la kununua korosho kwa kuwalipa wananchi kupitia benki ya kilimo.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Newala mkoani Mtwara, Daniel Zenda amesema sababu kubwa ya kupungua kwa uzalishaji wa zao la korosho msimu huu ni kutokana na mvua iliyonyesha katikati ya msimu na kusababisha dawa ya Sulpher kushindwa kufanya kazi vizuri.

Akitoa muhtasari kwa vyombo vya habari jana mjini Newala juu ya shughuli zilizofanyika hadi sasa tangu serikali kutoa mwongozo wa ununuzi wa korosho, Zenda alisema propaganda zinaoenezwa kuwa upungufu wa uzalishaji umetokana na wakulima kutokupewa fedha za ushuru wa kusafirisha nje ( export levy) hazina ukweli wowote.

"Upungufu wa uzalishaji wa korosho haujasababishwa na kukosekana kwa fedha za export levy kama inavyoelezwa na baadhi ya wanasiasa badala yake mavuno yamepungua kwasababu mvua zilinyesha katikati ya msimu na kusababisha athari kwa dawa ya sulpher kushindwa kufanya kazi vizuri kwenye mazingira hayo," alisema Zenda.

Mkuu wa Wilaya ya Newala AkiongozaUjumbe wa Kikosi cha Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Ambao wamefika Wilayani hapo kwa ajili ya kukagua Maghal ya Korosho hili waanze zoezi la ununuzi na kulipa fedha kwa wakulima kama ilivyoagizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr . John Magufuli kuwa Korosho zote zitanunuliwa na jeshi .
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiwa ndani ya Ghala la Kiwanda cha Ubanguaji wa korosho Microfonix kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiwa ndani ya Ghala la Agro focus kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakiwa ndani ya Kiwanda cha Ubanguaji wa korosho Microfonix kilichopo Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara na kushuhudia zoezi la usafishaji wa korosho.
Wafanyakazi wa Kiwanda cha Ubanguaji wa Korosho cha Microfonix wakiendelea na kazi ya ubanguaji wa korosho na kusafisha katika Kiwanda hicho.

KIPINDI CHA BBC DIRA YA DUNIA

MICHUZI TV: FEDHA ZA KOROSHO ZA JPM ZITAENDA MOJA KWA MOJA KWA WAKULIMA -TANECU


MAWAZIRI WAKUTANA KUELEKEA UZINDUZI WA CHANELI YA RUNINGA YA UTALII

MICHUZI TV:WAKULIMA NEWALA WAMSHUKURU RAIS MAGUFULI KWA KUWAMWAGIA MABILIONI

SERIKALI YAWAPANDISHA MADARAJA WATUMISHI WA UMMA 113,520 WALIOAJIRIWA TANGU MWAKA 2012

$
0
0
Serikali imewapandisha madaraja watumishi wa umma 113,520 walioajiriwa mwaka 2012 katika awamu tatu, ambapo ya kwanza walipandishwa vyeo Watumishi 28,049 waliokuwa wameidhinishiwa vyeo kabla ya zoezi la uhakiki wa watumishi hewa na uhakiki wa vyeti kuanzia mwezi Juni, 2016, awamu ya pili ilianza mwezi Novemba, 2017 na ilihusisha watumishi 59,967 ambao taarifa zao zilikuwa kwenye Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS) kabla ya zuio na awamu ya tatu ilianza mwezi Aprili, 2018 na ilihusisha Watumishi 25,504 ambao barua zao zilikuwa hazijaingizwa kwenye Mfumo. 

Ufafanuzi huo, umetolewa Bungeni leo na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary M. Mwanjelwa (Mb) wakati akijibu swali la Mhe. Joram Hongoli (Mb) kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora lililohusu watumishi wa umma walioajiriwa 2012 kutopandishwa madaraja mpaka hivi sasa.

Dkt. Mwanjelwa amesema, watumishi walioajiriwa Mwaka 2012 walistahili kupandishwa madaraja kuanzia mwaka 2016/2017 kipindi ambacho Serikali ilikuwa ikifanya zoezi la uhakiki wa watumishi hewa na uhakiki wa vyeti, hivyo mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo Serikali ilianza kuwapandisha watumishi hao kwa awamu hizo tatu kwa kuzingatia vigezo stahiki na kuongeza kuwa watumishi wengine ambao wamekidhi vigezo wataendelea kukasimiwa katika bajeti ya mishahara ili waweze kupandishwa vyeo katika mwaka huu wa fedha 2018/2019. 

Aidha, Dkt. Mwanjelwa ameainisha kuwa, watumishi 31,188 walioajiriwa na TAMISEMI mwaka 2012, kati ya hao watumishi 15,320 wamepandishwa vyeo na kubadilishiwa mishahara, na watumishi 3,349 waajiri wao wamewapandisha vyeo lakini majina yao yapo UTUMISHI kwa ajili ya kupitia taarifa zao kabla ya kuwabadilishia mishahara na watumishi 1,064 waliopandishwa vyeo wamebainika kuwa na hoja mbalimbali ambazo waajiri wanapaswa kuzikamilisha na kurejesha majina yao UTUMISHI kwa ajili ya kuwaidhinishia mishahara, watumishi 4,552 hawapo tena katika Utumishi wa Umma na watumishi 6,903 bado hawajapandishwa vyeo ambapo Serikali inatarajia kuwapandishwa vyeo wakati wowote katika mwaka huu wa fedha 2018/19.

Suala la upandishwaji vyeo kwa Watumishi wa Umma linazingatia vigezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na utendaji kazi mzuri, kukidhi sifa zilizoainishwa katika Miundo ya Maendeleo ya Utumishi, uwepo wa nafasi wazi na bajeti iliyotegwa. Kwa mujibu wa Miundo ya Maendeleo ya Utumishi, mtumishi anapaswa kutumikia cheo kimoja si chini ya miaka mitatu kabla hajafikiriwa kupandishwa cheo. Aidha, iwapo mtumishi ameajiriwa kwa mara ya kwanza atapaswa kumaliza mwaka mmoja wa kuthibitishwa kazini kisha ndipo atumikie cheo hicho si chini ya miaka mitatu, hivyo kwa kuzingatia sifa mtumishi anaweza kupandishwa cheo baada ya miaka 3, 4, 5 au hata saba kutegemea na kukidhi vigezo stahiki.

IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
OFISI YA RAIS (UTUMISHI)
TAREHE 15 NOVEMBA, 2018.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary M. Mwanjelwa (Mb) akijibu swali la Mhe. Joram Hongoli (Mb) Bungeni leo, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora lililohusu upandishwaji wa madaraja kwa watumishi wa umma walioajiriwa mwaka 2012.

NHC YAWATAKA WALIOPEWA HATI MRADI WA SAFARI CITY KUANZA UJENZI ILI HUDUMA ZIWAFIKIE

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha

Shirika la taifa la Tafa (NHC)Limewataka wale wote walikabidhiwa hati za viwanja walivyopewa katika la eneo la Safari City lililopo kata ya Mateves nje kidogo ya jiji la Arusha kuhakikisha wanaendeleza maeneo yao ili kuhakikisha huduma muhimu za umeme na maji zinasogezwa katika mji huo mpya.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya Hati ya umiliki wa eneo na kibali cha ujenzi kwa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira(AUWSA) iliyofanyika katika kata ya matever jijini hapa Mkurugenzi wa shirika la nyumba la taifa(NHC)Dkt.Maulidi Banyani amesema kuwa shirika hilo katika kuhakikisha linafikia malengo ya kusogeza huduma zake kwa jamii ya watanzania wa vipato vyote na kupunguza gharama za ujenzi kuendana na mazingira.

Ameeleza kuwa limeingia makubaliano na AUWSA na kuwapatia eneo lenye ukubwa wa squaremita elfu 13 kwa ;lengo la ujenzi wa ofisi kuu ya kanda,Karakana,Bohari na Kituo cha Taarifa za mita hatua hiyo itasaidia kupunguza tatizo la maji katika eneo hilo baada ya mamlaka hiyo kuonyesha nia ya kusogeza huduma hiyo kupitia mradi huo.

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi wa AUWSA Mhandisi Humphrey Mwiyombela amelishukuru shirika la nyumba kwa kuwapatia eneo hilo nakuhaidi kujenga jengo lenye ukubwa wa ghorofa sita litakalotumika kama ofisi kuu ya kanda ambalo litafungwa mitambo maalumu ya kupokea taarifa za mbali mbali katika mtandao wao wa huduma za maji.
Mkurugenzi wa shirika la nyumba la taifa Dkt.Maulidi Banyani akiwa na Kaimu mkurugenzi wa Auwsa Mhandisi Humphrey Mwiyombela wakikabidhiana hati ya kiwanja na kibali cha ujenzi wa ofisi za AUWSA kwenye eneo la Safari City nje Kidogo ya jiji la Arusha Picha na mahmoud ahmad wa globu ya jamii Arusha.


MKIWAENDEKEZA WATOTO MTATENGENEZA “BOMU”- POLISI

$
0
0
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha

Imeelezwa kwamba tabia ya wazazi kutoa ahadi ya zawadi kwa kila wanachofanya watoto wao ni kibaya na kinawajengea mazingira magumu watoto hao baadae hasa pindi hali ya uchumi inapobadilika.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto mkoa wa Arusha Inspekta Happyness Temu wakati alipokuwa anafafanua aina za malezi katika kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa hewani kila siku Asubuhi katika kituo cha Redio cha Triple “A” kilichopo jijini hapa.

Inspekta Happyness alisema kwamba, baadhi ya wazazi wamekuwa na tabia ya kutoa ahadi ya fedha au vitu kwa watoto wao kwa nia ya kutoa hamasa ili wafanye vizuri aidha katika masomo au shughuli zozote hali ambayo kimalezi si sahihi kwani inaweza kusababisha mtu kuwa tabia tofauti pindi atakapokuwa mkubwa.

“Tabia hii inawafanya watoto wanapokuwa kwenye malezi wawe na matumaini kwamba kila kizuri wanachofanya lazima mwishoni kiendana na zawadi na hivyo mtoto anasababishiwa tamaa, mfano ukimaliza ugali wote nakununulia keki”. Alisema Inspekta Happyness.

Alisema pindi anapokuwa mtu mzima hali hiyo itamuathiri kwa kuwa atakuwa anataka kupewa asante ya kitu au fedha kutoka kwa kila atayemhudumia mara baada ya kumaliza kazi kitu ambacho si sahihi.

Alisema pongezi kwa mtoto sio lazima iendane na kuahidiwa na kupewa kitu au fedha bali inaweza kufanyika kwa njia ya maneno tu na ikamridhisha kwani si kila wakati mzazi unaweza ukawa na uwezo ule ule kiuchumi kuna wakati unashuka au mtoto anakuwa mikononi mwa walezi wengine ambao uwezo wao ni mdogo.
Pichani ni Mkuu wa Kitengo cha dawati la Jinsia na Watoto mkoa wa Arusha,Inspekta Happyness Temu.

ATHMANI AENDELEA KUOMBA MSAADA WA MATIBABU KWA WATANZANIA

$
0
0
NA YEREMIAS NGERANGERA,NAMTUMBO

Athmani Amani mkazi wa kijiji cha Naikesi kata ya kitanda wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma anawaomba watanzania kumsaidia fedha za kugharimia matibabu ya mtoto wake Shaziri Athmani (12) anayesumbuliwa na tatizo la moyo kuwa mkubwa.

Mtoto Shaziri Athamani ni mwanafunzi wa darasa la nne shule ya msingi Naikesi iliyopo kata ya Kitanda wilayani Namtumbo awali alikuwa anasumbuliwa na kuvimba miguu hali iliyokuwa inamkosesha masomo yake darasani mara kwa mara kuanzia mwaka 2016.

Mwaka huo huo mwezi septemba baba yake alilazimika kumpeleka Hospitali ya Mkoa Songea kuangalia tatizo la kuvimba kwa miguu ya mtoto huyo na baada ya kupata vipimo wakashauriwa kuenda Hospitali ya Peramiho .

Bwana Athamani alidai kuwa hakuwa na fedha za kumpeleka mtoto peramiho kwa kipindi hicho na badala yake alirudi naye nyumbani Naikesi kwenda kuuza mifugo lakini fedha hizo hazikumwezesha kukidhi mahitaji ya kumtibu mwanae katika Hospitali ya Peramiho baada ya kufika katika Hospitali hiyo na kumaliza fedha yake yote aliyokuwa nayo katika vipimo pekee .

Baada ya kupatiwa vipimo na kubaini Tatizo la mwanae alirudi na mwanae mpaka kijijini kwake kujipanga upya kwa ajili ya matibabu ya mwanae na kujitahidi kwa kile anachokipata anunue dawa kwa ajili ya mwanae huyo.

Pamoja na jitihada hizo hali ikaendelea kuwa sio nzuri na ndipo alipolazimika kufanya kazi za kulima mashamba ya watu ili apate fedha za kumtibu kijana wake na mwaka huu mwezi oktoba alimpeleka kijana wake huyo peramiho na baada ya kufika peramiho na kupatiwa vipimo alishauriwa na madaktari kumpeleka mtoto huyo Hospitali ya Muhimbili Dar es salaam.

Hata hivyo mzazi huyo aliomba msaada vyombo vya habari kumsaidia tatizo lake ili aweze kuchangiwa na wasamaria wema ampeleke mtoto wake muhimbili ambapo vyombo vya habari vilimsaidia na aliweza kusaidiwa michango iliyomwezesha kumfikisha kijana wake muhimbili na kupatiwa matibabu ya awali.

Anawashukuru Watanzania wote waliomchangia kijana wake na kuweza kupata matibabu ya awali lakini anawaomba waendelee kumchangia kwani kila baada ya miezi mitatu anatakiwa kumpeleka kijana wake huyo hospitalini hapo na yeye hana uwezo wa wa fedha za kumpeleka hospitali kijana wake huyo mara kwa mara muhimbili zaidi ya kuwategemea wasamaria wema .

Kijana huyo baada ya kupata matibabu ya awali ameanza kuonesha hali ya matumaini tofauti na ilivyoawali kabla ya kumpeleka Muhimbili kwa matibabu ya awali alisema mzazi huyo.
Athmani Amani mkazi wa kijiji cha Naikesi kata ya kitanda wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma anawaomba watanzania kumsaidia fedha za kugharimia matibabu ya mtoto wake Shaziri Athmani (12) anayesumbuliwa na tatizo la moyo kuwa mkubwa.

FEDHA ZA KOROSHO KULIPWA MKULIMA MOJA MOJA


MICHUZI TV: BAADA YA MBUNGE ABDALLAH MTOLEA KUJIONDOA CUF, PROF. LIPUMBA AZUNGUMZA HAYA....

ZANZIBAR KUADHIMISHA SIKU YA TAKWIMU AFRIKA.

$
0
0
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar 16.11.2018

Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeandaa Mdahalo mkubwa utakaofayika Novemba 19, kwa lengo la kuongeza uelewa wa Wananchi juu ya umuhimu wa Takwimu katika maendeleo ya Taifa.

Mtakwimu Mkuu wa Serikali Mayasa Mahfudh Mwinyi aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake Mazizini kuhusu shamrasharma za maadhimisho ya siku ya Takwimu Afrika.

Amesema Takwimu zina umuhimu mkubwa katika kupanga maendeleo ya Taifa hivyo wananchi wanapaswa kujua kwa undani wake ili kutoa mashirikiano kwa ofisi hiyo.Amesema Ofisi ya Takwimu itaendelea na jukumu lake la kufanya Tafiti katika nyanya mbalimbali ikiwemo za kiuchumi, kimaendeleo na kijamii na kuishauri Serikali na Taasisi binafsi kuhusu mwelekeo wa kiuchumi.

Aidha amezishauri Taasisi za Serikali na binafsi kuzitumia Takwimu zinazotolewa na ofisi hiyo ili zipige hatua mbele kimaendeleo na kukabiliana na changamoto zao.Alisisitiza wadau wote wanaotaka kufanya tafiti rasmi kwenda katika Ofisi yao kuomba ushauri wa kitaalamu ili Takwimu watakazozipata katika tafiti zao ziwiane na Takwimu ya Ofisi yake.

“Ili kuepuka mgongano wa Kitakwimu nawaomba Wadau wote wanaofanya Tafiti basi waje ofisini tuwasiliane kuboresha Takwimu badala ya takwimu hizo kugongana” alisisitiza Mtakwimu Mkuu.Mbali na kilele Mtakwimu Mayasa alielezea mambo watakayoyafanya ikiwa ni pamoja na kutoa msaada katika nyumba za kulelea watoto Mazizini ambapo Jumapili kutakuwa na Mchezo wa Mpira wa Miguu kati ya Ofisi ya Mtakwimu na Ofisi ya Mdhibiti Mkuu wa Serikali.

Awali Mtakwimu Mwandamizi kutoka Ofisi ya Mtakwimu Abdulmajid Jecha alisema kulingana na Takwimu za uwezekano wa umri wa kuishi kwa Mzanzibari ni miaka 67.Alisema miaka hiyo imeongezeka kutokana na uimarishwaji wa huduma za Afya Zanzibar na matumizi madogo ya ulevi ikiwemo Pombe kwa Wanzanzibari.

Hali hiyo ni tafauti kidogo kwa Tanzania Bara ambapo Makadirio ya kuishi ni miaka 66.“Sababu zinazofanya Makadirio ya kuishi kwa Wazanzibari kuwa juu ukilinganisha na Bara ni uimarishwaji wa huduma za Afya kwa mfano kupungua kwa Malaria ikilinganishwa na Bara lakini hata Ulevi ambao ni chanzo cha magonjwa Zanzibar ni kidogo ukilinganisha na Bara ” alibainisha Abdulmajid Jecha

Hivyo Jecha alishauri watu wazidi kuzitumia Takwimu sahihi zinazotolewa na Ofisi hiyo ili kujipangia mipangilio yao ya maendeleo.Kila ifikapo November 18 ni siku ya Takwimu Afrika ambapo kwa Zanzibar itaadhimishwa November 19 katika viunga vya Ofisi hiyo Mazizini, ili kufikisha ujumbe kwa wananchi wengi.
Mtakwimu Mkuu wa Serikali Mayasa Mahfudh Mwinyi akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake Mazizini kuhusu shamrashamra za maadhimisho ya siku ya Takwimu Afrika.

ZIARA YA MAKAMU WA RAIS MKOANI MANYARA LEO

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi waliojitokeza nje ya kiwanda cha Mbolea cha Minjingu mkoani Manyara.Makamu wa Rais yupo kwenye ziara ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo ambapo asubuhi hii alitembelea kiwanda hicho cha mbolea.

KONGAMANO LA WAHITIMU CHUO KIKUU MZUMBE LAFANA

$
0
0
Rais wa Baraza la Wahitimu Chuo Kikuu Mzumbe, Ludovick Utoh, akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wahitimu wa waliosoma chuoni hapo. Picha zote Kajunason/MMG - Morogoro. Spika wa Bunge mstaafu, Anne Makinda, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano uliowakutanisha wahitimu wa waliowahi kusoma Chuo Kikuu Mzumbe. Makamu Mkuu Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Lughano Kusiluka, akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wanafunzi waliowahi kusoma na kuhitimu katika chuo hicho. Baadhi ya washiriki wa mkutano huo. Baadhi ya washiriki wa mkutano huo. 

TAARIFA KWA WASTAAFU WA NSSF

Viewing all 110118 articles
Browse latest View live




Latest Images