Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110170 articles
Browse latest View live

UPELELEZI KESI YA KITILYA NA WENZAKE BADO HAUJAKAMILIKA

$
0
0
Na Karama Kenyunko blogu ya Jamii.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa na upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili,  aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya na wenzake kuwa wanawasiliana na wachunguzi ili wajue upelelezi umefikia wapi.

Mbali na Kitilya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kampuni inayoshughulikia  Uwekezaji wa Mitaji na Dhamana (Egma), washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni aliyekuwa Miss Tanzania (1996), Shose Sinare na Ofisa wa benki ya Stanbic, Sioi Solomon.

Wakili wa Serikali, Patrick Mwita ameeleza hayo leo Novemba 9.2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi wakati kesi dhidi ya washtakiwa hao ilipoletwa kwa ajili ya kutajwa. Wakili Mwita amedai upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika, bado wanaendelea kuwasiliana na wachunguzi.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 16, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa na kuangalia kama upelelezi umekamilika ama la.
Washitakiwa wote kwa pamoja  wanakabiliwa na mashitaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha.

Wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Machi 2013 na Septemba 2015 wakati wa mchakato wa mkopo wa dola za Marekani milioni 550   kwa  Serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard Uingereza.

Wanadaiwa kuwa  Machi 2013 jijini Dar es Salaam walijipatia Dola za Marekani milioni sita , wakionyesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji upatikanaji wa mkopo  na zililipwa kupitia  Kampuni ya Egma T Ltd.
Washitakiwa  hao wanadaiwa kutakatisha fedha kwa kuhamisha, kuchukua na kuweka kiasi cha Dola za Marekani milioni sita katika akaunti tofauti tofauti  za benki.
Kati ya  Machi 2013 na Septemba 2015, wanadaiwa  kuwa waliweka pesa hizo katika akaunti mbalimbali zilizomilikiwa na kampuni ya Egma na kwamba walipaswa kufahamu kuwa pesa hizo ni mazao ya uhalifu wa kughushi

WAZIRI MKUU AKUTANA NA BALOZI WA PALESTINA NCHINI

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefanya mazungumzo na Balozi wa Palestina nchini Tanzania, Mheshimiwa Hamdi Abuali na kusema Serikali itahakikisha inaimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Palestina.

Akizungumza na Balozi huyo ofisini kwake Bungeni, jijini Dodoma leo (Ijumaa, Novemba 9, 2018), Waziri Mkuu amesema Serikali itaendeleza ushirikiano huo ulioasisiwa na hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na aliyekuwa kiongozi wa Palestina,Yasser Arafat.

“Tanzania na Palestina zina historia ya kutosha. Tunatambua mahusiano mazuri yaliyopo kati nchi zote mbili, ambayo yalikuwepo kuanzia Serikali ya awamu ya kwanza chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimul Julius Nyerere.”

Waziri Mkuu amesema Tanzania na Palestina zimekuwa zikishirikiana kuboresha na kuimarisha sekta mbalimbali ikiwemo ya afya, ambapo madaktari bingwa kutoka Palestina wamekuwa wakija nchini na kuhudumia wananchi kwenye hospitali mbalimbali.

Amesema Serikali imedhamiria kuendeleza sekta ya viwanda nchini kama mkakati wa kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025, hivyo ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wafanyabiashara kutoka nchini Palestina waje kuwekeza kwenye viwanda.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema Tanzania ina vivutio vingi vya utalii ikiwa ni pamoja na uwepo wa mlima Kilimanjaro, mbunga zenye wanyama wa aina mbalimbali na fukwe nzuri za bahari, hivyo amewakaribisha watalii kutoka Palestina waje kuangalia vivutio hivyo

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Balozi wa Palestina nchini Hamdi Abuali, ofisini kwake Bungeni jijini Dodoma Novemba 9, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Balozi wa Palestina nchini Hamdi Abuali, alipomtembelea ofisini kwake Bungeni jijini Dodoma Novemba 9, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Taarifa kuhusu fursa za ufadhili wa masomo ya muda mfupi kutoka Serikali ya Singapore na Israel

$
0
0

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea fursa za ufadhili wa masomo ya muda mfupi kutoka Serikali ya Singapore kupitia Programu ya Ushirikiano ya nchi hiyo (SCP) na Serikali ya Israel kupitia Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Israel (MASHAV).

Maelekezo ya kalenda ya kozi ambazo zimetolewa chini ya ufadhili wa Programu ya Ushirikiano ya Singapore inapatikana kupitia tovuti yao ya http://www.scp.gov.sg.


Taarifa ya kina kuhusu nafasi za masomo chini ya ufadhili wa MASHAV inapatikana kupitia tovuti ya 
http: // mashav.mfa.go.il/MFA/mashav/Courses/Pages/default.aspx.


Kupara sehemu ya kalenda ya kozi chini ya ufadhili wa Programu ya Ushirikiano ya Singapore kwa mwaka 2018 na 2019 

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA AASA JAMII KUACHA KUTENDA UHALIFU ILI KUPUNGUZA MSONGAMANO MAGEREZANI

$
0
0
Na Lucas Mboje, Iringa;
KAMISHNA Jenerali wa Jeshi la Magereza Magereza nchini, Phaustine Kasike ametoa rai kuwa ili kupunguza msongamano magerezani ni vema jamii ikaacha kufanya matukio mbalimbali ya uhalifu hapa nchini.
Rai hiyo imetolewa leo na Kamishna Jenerali Kasike wakati akitoa ufafanuzi mbele ya wanahabari wa Mkoani Iringa kuhusu madai ya uwepo wa msongamano wa wafungwa katika magereza mbalimbali yaliyopo nchini ambapo ameeleza kuwa si kweli kwamba magereza yote yana msongamano bali msongamano uliopo magerezani ni kwenye baadhi ya magereza yenye kuhifadhi mahabusu.
Amesema suala la msongamano limekuwa ni tatizo kubwa ambapo takwimu za Jeshi la Magereza zinaonesha kuwa idadi ya mahabusu waliopo magerezani ni wengi na hali hiyo inatokana na wingi wa matukio ya uhalifu kwenye eneo husika na kule ambako hakuna uhalifu mwingi basi nako kwenye magereza hakuna msongamano mkubwa wa wafungwa/mahabusu.
Ameongeza kuwa Jeshi la Magereza litaendelea kushirikiana na vyombo vya haki jinai ikiwemo Jeshi la Polisi, Mahakama na Ofisi ya DPP ili kuhakikisha kuwa kunakuwa na usukumaji wa kesi mbalimbali za mahabusu waliopo magerezani.
“Tutajitahidi kuendelea kushirikiana kwa pamoja katika jukwaa letu la haki jinai ili kuangalia namna bora zaidi ya kuweza kutatua tatizo la ucheleweshaji wa kesi za mahabusu waliopo magerezani”. Amesema Jenerali Kasike.
Kuhusu uhamisho wa Gereza Iringa kwenda eneo la la Mlolo, Kamishna Jenerali Kasike amesema tayari Jeshi hilo limekwishaanza kutekeleza maelekezo ya Serikali ambapo hivi sasa lipo katika mchakato wa kuhamishwa kadri hali ya kibajeti itakavyoruhusu. 
“Tumekwishaanza ufyatuaji wa tofali za ujenzi wa nyumba za maafisa na askari sambamba na ujenzi wa mabweni ya wafungwa unaendelea katika eneo hilo hivyo Gereza Iringa litahamishiwa katika eneo la Mlolo ili kupisha huduma za kijamii”. Amesisitiza Jenerali Kasike.
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, CGP. Phaustine Kasike yupo mkoani Iringa  kwa ziara ya kikazi ambapo leo ametembelea magereza ya Iringa na Pawaga. Ziara hizi ni mwendelezo wa ziara zake  za kikazi zenye lengo la kukagua magereza yote Tanzania Bara na kuzungumza na Maafisa na askari pamoja na kujua changamoto mbalimbali wanazokutana nazo wakati wakitekeleza majukumu yao.

 . Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akiwasili katika Gereza la Iringa leo Novemba 9, 2018 tayari kwa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua shughuli mbalimbali za uendeshaji wa Jeshi hilo.
 Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akizungumza na Mahabusu na Wafungwa wa Gereza Iringa(hawapo pichani) alipofanya ziara ya kikazi leo Novemba 9, 2018.

 Askari wa vyeo mbalimbali wa Gereza Pawaga wakifuatilia kwa makini maelekezo ya Kamishna Jenerali wa Magereza alipotembelea gereza hilo leo Novemba 9, 2018.

 Mkuu wa Magereza Mkoa wa Iringa, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Hassard Mkwanda akimuongoza Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike kutembelea maeneo mbalimbali ya Gereza la Wilaya Iringa.


 6 Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akikagua maandalizi ya shamba ya kilimo cha mpunga katika eneo la Gereza la Pawaga Mkoani Iringa. Gereza Pawaga limepewa malengo ya kulima ekari 375 za mpunga ili kuwezesha mpango wa kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike akikagua moja la ghala la kuhifadhia mpunga unaozalishwa katika Gereza la Kilimo Pawaga(Picha na Jeshi la Magereza).

MICHUZI TV: SERIKALI YATOA TAMKO KUHUSU SWALA LA KOROSHO

TAKUKURU WATAJA WAFANYABIASHARA WANAOFANYA UDANGANYIFU KATIKA BIASHARA.

$
0
0
 Na.Khadija Seiif,Globu ya jamii.

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wametaja makosa  ya baadhi ya wafanyabiashara nchini ambao wanajihusisha na udanganyifu kupitia matumizi ya mashine za Kieletroniki (EFD).

Naibu Mkurugenzi wa TAKUKURU Brigedia Jenerali John Mbungo akizungumza na wanahabari amesema Kodi ndio chanzo cha mapato kwa taifa lolote na Kodi hiyo inayotumika kuboresha huduma za kijamii na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Mbungo amefafanua zaidi kuwa TAKUKURU imeendelea kutoa elimu kwa wafanyabiashara na wananchi wote kwa ujumla waliojitokeza maeneo yenye mkusanyiko mkubwa wa wafanyabiashara kupitia magari ya matangazo maeneo ya Kariakoo,Buguruni,Gongo la Mboto,Tabata,Ilala,Mwenge,Tegeta na Tandika.

Vilevile wachunguzi kutoka taasisi hiyo waliendelea katembea maeneo tajwa na kufanya uchunguzi kujua iwapo bado kuna wafanyabiashara wanaokaidi maelezo hayo ya matumizi sahihi ya kisiti zinazotolewa na mas8hine za EFD na kuendelea kufanya udanganyifu.

Aidha,Mbungo ameeleza katika zoezi hilo wamebaini makosa ya udanganyifu ikiwemo wafanyabiashara wanaotoa risiti zenye kiasi tofauti na kiasi cha pesa halisi kilichotolewa ili kununua bidhaa husika, baadhi ya wafanyabiashara hawatoi kabisa risiti za kielekroniki baada ya kufanya mauzo. 

Na kwa upande mwingine Taasisi ya kuzuia na kupamabana na Rushwa(TAKUKURU) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) watawachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika kuendelea na tabia hiyo ya udanganyifu wenye lengo la kuikosesha serikali yetu mapato.

 Na kwa wanunuzi kuepuka udanganyifu huo kupita baadhi ya Wafanyabiashara ambao bidhaa na stakabadhi havilandani hivyo waepuke kupokea stakabadhi hizo na kwa sasa baadhi ya wafanyabiashara wameanza mahojiano kama vile Masai Shop,Malya Shop,Kanda Trading Company,Kiwanso builders corner,Kipata cafeteria, Mchapa kazi home appliance .


Naibu Mkurugenzi waTaasisi ya kuzuia na kupamabana na Rushwa (TAKUKURU)  Brigedia Jenerali John Mbungo amewataja baadhi ya wafanyabiashara nchini ambao wanajihusisha na udanganyifu kupitia matumizi ya mashine za Kieletroniki (EFD). 

PUMA ENERGY TANZANIA YAZINDUA MRADI WA SKY IS THE LIMID PROJECT KWA LENGO LA KUAMSHA MOYO WA UJASIRI NA KUJIWEKEA MALENGO KATIKA KUFANIKIWA

$
0
0
KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Energy (T) LTD kwa kushirikiana na Kampuni ya Air Tanzania Limited imezindua mradi unaojulikana kama “Sky is the Limit Project”wenye lengo la kuwatambulisha na kuwapa uelewa wanafunzi wa shule za msingi wasio na fursa au uwezo wa kuufikia kwa urahisi ulimwengu wa anga ili kuwapa uelewa kuhusu sekta hiyo yenye kuvutia.

Imeelezwa lengo la mradi huo ni kuwahamasisha watoto wanaotoka mazingira ya kawaida sana ya vijijini kwa kuwatia moyo katika masomo yao ili wajue na kuvutiwa na sekta ya anga na maeneo mengine ya fursa za kazi za nje ya maeneo wanaoishi.

Katika kufanikisha mradi huo zaidi ya wanafunzi 40 kutoka Shule za msingi za wilayani Kisarawe wamepata fursa ya kutembelea Shirika la Ndege la Air Tanzania pamoja na kushuhudia namna Kampuni ya mafuta ya Puma inavyohifadhi mafuta ya ndege katika Uwanja wa Ndege Terminal One jijini Dar es Salaam.

Meneja Masoko wa Mafuta ya Ndege Tanzania kutoka kampuni ya Mafuta ya Puma Illuminata Yateri amesema leo jijini Dar es Salaam kuwa kama neon linavyojieleza la Sky is the Limit , mradi huo unataka kuamsha moyo wa ujasiri na kujiwekea malengo ya juu katika kufanikiwa.

Amefafanua mradi huo wa Sky is the limit utawapa wototo kutoka shule za msingi waliochaguliwa kutoka kwa jumuiya zisizo na fursa na uzoefu wa sekta ya anga kwa ukaribu zaidi, kwa kufanya ziara ya elimu inayofanywa katika miundombinu ya uwanja wa ndege kama ugavi wa mafuta ya ndege,huduma zinazotolewa kwenye ndege ,udhibiti wa safari za ndege, kupata habari mbalimbali za ndege kupitia watalaam wa sekta ya ana wanaohusika.

“Watoto watajua shughuli za kampuni ya mafuta ya Puma kuhusu biashara ya mafuta ya ndege jinsi yanavyouzwa kwenye ndege za ndani na za kimataifa.Kampuni ya Puma Tanzania ambayo ndio inayoongoza katika soko la kuuza mafuta ya ndege nchini imekuwa mshirika wa muda mrefu katika sekta ya anga katika kuunga mkono maendeleo ya kiuchumi ya Serikali ya Awamu ya Tano.
 ????????????????????????????????????
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo (wa pili kulia) na Meneja Masoko wa mafuta ya Ndege Puma Tanzania, Illuminata Yateri (katikati) wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Mawasilino wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) Josephat Kagirwa (kulia) alipokuwa akizungumza na wanafunzi kutoka Shule za Msingi wilayani Kisarawe walipofanya ziara ya mafunzo uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam jana ikiwa ni adhimisho la mradi ujulikanao kama Sky is the limit.
????????????????????????????????????
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo (wa pili kulia) akizungumza na wanafunzi wa shule za msingi kutoka wilaya yake wakati wa ziara ya kimafunzo kutembelea karakana ya ndege jijini Dar es Salaam jana kwa kushirikiana na Kampuni ya Puma Energy Tanzania katika kuhudumia utoaji wa mafuta ya ndege chini ya mradi ujulikanao kama Sky is the limit.
????????????????????????????????????
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo akimfunga vifungo mmoja wa wanafunzi wakati walipofanya ziara katika uwanja wa ndege wa JNIA katika mradi mradi ujulikanao kama Sky is The Timit
????????????????????????????????????
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo, Meneja Masoko wa mafuta ya Ndege Puma Tanzania, Illuminata Yateri na wanafunzi wa Shule za Msingi wilayani Kisarawe, wakimsikiliza Injinia wa Ndege kutoka Shirika la Ndege Tanzania (ATC), Nkhambi Salanga walipofanya ziara ya kimafunzo katika mradi wa Sky is the limit katika uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam jana.

BASATA YAVUTIWA NA MAFANIKIO YA MSANII NANDY


WATEJA WA ZAMANI DAWASA WAANZA KUREJESHEWA HUDUMA YA MAJI KUPITIA KAMPENI YA TUNAWAHITAJJ

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

MAMLAKA ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) imeendelea kuwapokea na kuwarudisha huduma ya maji kwa wateja waliokatiwa huduma hiyo kutokana na kushindwa kulipa bili zao.

Hatua hiyo imekuja baada ya DAWASA kuanzisha kampeni mpya ya Tunawahitaji inayowataka wateja wote wa zamani kurudishiwa huduma za maji na wakubaliane watalipa katika mfumo gani.

Kampeni hiyo iliyozinduliwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema kuwa kampeni ya 'Tunawahitaji' lengo kuu ni kuona wateja wote takribani 10000 waliokatiwa maji wanaanza kupata tena huduma hiyo.

Luhemeja alisema kuwa amewaagiza maafisa wote wa utawala wafanye hivyo haraka,lengo la Tunawahitaji ni kuwatafuta wateja wa zamani na wapya ili waunganishiwe maji na hiyo ni kampenibya kudumu.Kampeni hiyo itawahusisha wateja wote waliokatiwa huduma ya maji na kupitia kwa mameneja wa mikoa yote ya DAWASA kwa pamoja wakubaliane watalipa kwa miezi mingapi madeni ambayo wanadaiwa.

Kwa upande wa mameneja kutoka Mikoa mbalimbali ya DAWASA , wamethibitisha wateja wenye madeni ya muda mrefu kuanza kwenda kwenye ofisi zao kukaa nao chini na wakubaliane katika ulipaji.Meneja Mkoa wa Kinondoni amethibitisha hilo na kusema muitikio wa watu umeanza kuwa mkubwa na wengi wakionekana kuelewa lengo la Mamlaka katika kuhakikisha watu wote wanatumia maji safi na salama kupitia kampeni ya Tunawahitaji.

Na kutoka ofisi za Boko, wateja 16 tayari wamesharudishiwa huduma ya maji baada ya kukaa pamoja baina ya DAWASA na wateja na wamekubaliana namna ya kulipa madeni yao huku wengine wakiendelea kujitokeza.Baadhi ya wananchi wamefurahia kampeni ya Tunawahitaji kwani itawapata tena fursa ya kupata maji safi na salama kutoka DAWASA baada ya kukatiwa maji kutokana na ulimbikizwaji wa madeni hapo awali.
Moja wa wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es salaam (DAWASA) akitoa elimu kwa wananchi inayohusu kampeni ya Tunawahitaji itayowapa fursa wananchi kurudishiwa maji.

MAKAMU WA RAIS AENDELEA NA ZIARA WILAYANI ROMBO

$
0
0



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka Watumishi wa Serikali Wilayani Rombo kufanya kazi kwa kushirikiana.

Makamu wa Rais ameyasema hayo jana  mara baada ya kupokea taarifa ya Wilaya hiyo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Mhe. Agnes Hokororo.

“Wote tunajenga nyumba inayoitwa Tanzania katika nafasi yako yoyote ulipo unajenga nyumba inayitwa Tanzania, kwa itikadi yako yoyote uliyonayo unajenga nyumba inayoitwa Tanzania tunatawaliwa na sheria moja, tunataliwa na miongozo hiyo hiyo ya Serikali, kanuni na mambo mengine na hiyo hiyo Serikali”.

Katika ziara yake Wilayani Rombo Makamu wa Rais alikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya Rombo, mradi wa maji Shimbi Mashariki,kukagua shamba la Miti Rongai.

Makamu wa Rais ambaye yupo kwenye ziara ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo pia alipata nafasi ya kuwasalimu wananchi wa Tarakea waliojitokeza barabarani kumsalimia na alihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya shule ya msingi Keni-Mengeni.

Kwa upande mwingine Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo amesema kuwa Serikali hii inafanya jambo la kihistoria kwa kukamilisha ujenzi wa vituo vya Afya 350.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungungumza na Watumishi wa Wilaya ya Rombo mara baada ya kupokea taarifa ya Wilaya hiyo. Makamu wa Rais yupo kwenye ziara ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo mkoani Kilimanjaro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
2 4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo juu ya mradi wa ujenzi wa jengo la Utawala la Halmashauri ya Rombo kutoka kwa Mhandisi wa Halmashauri Mhandisi Boniface Vedasto. Makamu wa Rais yupo kwenye ziara ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo mkoani Kilimanjaro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
5 6
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimu wananchi wa Tarakea waliojitokeza kumsalimia wakati alipokuwa njiani kuelekea kwenye shamba la miti Rongai. Makamu wa Rais yupo kwenye ziara ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo mkoani Kilimanjaro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 10
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua kitalu cha miche wakati alipotembelea shamba la miti la Serikali lililopo Rongai Rombo. Makamu wa Rais yupo kwenye ziara ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo mkoani Kilimanjaro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais). 

Mongella amtaka Mkurugenzi Ilemela kununua vifaa tiba katika Kituo cha Afya Karume

$
0
0
Mkuu wa Mkoa Mwanza, Mhe. John Mongella jana amefanya ziara katika Kituo cha Afya Karume, Manispaa ya Ilemela na kushtushwa na uhaba wa vifaa tiba kwenye majengo mapya yaliyojengwa na serikali kupitia utaratibu wa “Force Account”.Mhe. Mongella ametoa muda wa siku saba kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela na Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo kuhakikisha majengo hayo yanaanza kufanya kazi kama ilivyokusudiwa.

Bofya Video hapa chini kutazama.

DC Jokate Mwegelo avunja ukimya uzinduzi wa Album ya NANDY.

CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAENDELEA KUKEMEA UMIMI, UBINAFSI NA MAKUNDI NDANI YA CCM ILI KUIMARISHA UIMARA, UMOJA NA UMADHUBUTI WA CCM

$
0
0
Katika kikao cha Halmashauri Kuu Maalumu ya CCM Wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara Ndg. Humphrey Polepole Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinakemea vikali umimi, ubinafsi na makundi ndani ya CCM ili kuimarisha uimara, umoja na umadhubuti wa CCM.

Akieleza kwa kina suala hilo Ndg. Polepole amesema umimi, ubinafsi na makundi ni kinyume na Katiba, Kanuni na Taratibu nzuri za CCM na kuwa ndani ya CCM Makundi hayana nafasi hususani katika kipindi hiki ambacho muelekeo wa CCM ni kushughulika na utatuzi wa shida za wananchi.

Aidha Ndg. Polepole amewataka wanaCCM na Viongozi kuwa wamoja, kushikamana, kushirikiana na kupendana ili CCM izidi kuwa imara na iendelee kuwa hudumia wananchi ipasavyo.

“Chama hiki nikikubwa kuliko mtu mmoja, hatuwezi tukaruhusu tabia za hovyo ambazo tumezikataza, tabia za makundi, hata Ndg. Magufuli Mwenyekiti wetu mpendwa hapendi makundi kwa sababu makundi hayatujengi na yanadhoofisha umoja wa  Chama chetu” amesema Ndg. Polepole

Wakati uo huo Ndg. Polepole amewapongeza sana Viongozi wote wa CCM kwa kufanikisha kupatikana kwa ushindi wa CCM Wilaya ya Serengeti ambapo CCM imepita bila kupigwa kwenye nafasi ya Ubunge  na udiwani na kuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuongoza Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.
  Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Ndg. Humphrey Polepole akizungumza jambo kwenye kikao cha Halmashauri Kuu Maalumu ya CCM Wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara ,ambapo alieleza kuwa  Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinakemea vikali umimi, ubinafsi na makundi ndani ya CCM ili kuimarisha uimara, umoja na umadhubuti wa CCM.
 Ndg. Polepole akiambatana na Viongozi wa CCM Wilaya na Mkoa wakiongozwa na Ndg. Samweli Niboye (Namba tatu) Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara walikagua  eneo la ujenzi wa chujio la Maji Mugumu katika Bwawa la Manchira  ambapo Ndg. Polepole pamoja na Viongozi wa CCM wamesikitishwa sana na namna ambavyo mradi huo unavyosuasua licha ya kuwa Serikali ya CCM imekwisha weka fedha ya kutosha kwenye mradi huo.


Monalisa afanya maajabu kwa NANDY,usiku wa The African Princess.

Mabinti watakiwa kutumia tehama kuondoa changamoto katika jamii

$
0
0
Na mwandishi wetu
KAIMU Balozi wa Marekani nchini Dk.  Inmi Patterson amewataka mabinti wa Tanzania kufikiria taifa lao na namna ambavyo wanaweza kusaidia kuondoa changamoto mbalimbali zinazokabili jamii yao.
Kauli hiyo ameitoa katika jukwaa la kufunza wasichana wajasiriamali lililoshirikisha mabinti wa sekondari wa mkoa wa Dar es salaam; pamoja na mambo mengine walishiriki katika shindano la ubunifu wa programu za kompyuta.
Jukwaa hilo linalojulikana kama Girls Entrepreneurship Summit (GES) 2018 linachagiza mabinti kutumia Tehama kutatua matatizo yaliyopo katika jamii.
Jukwaa hilo lililoandaliwa na ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani nchini limelenga kusaidia mabinti kuchangia utatuzi wa matatizo kwa kuwa wabunifu katika ujasiriamali.
Kaimu Balozi huyo aliwataka mabinti hao kuwa na uvumilivu katika kukabiliana na changamoto zilizopo na kujenga mtandao ambao utawasaidia kuendelea mbele zaidi kiuchumi.
Alisema mtaji mkubwa wa wajasiriamali ni ubunifu na wazo ambalo linatakiwa kufanyiwa kazi bila kuogopa changamoto zilizopo.
 Mapema katika hotuba yake Mwanzilishi mwenza wa Apps &Girls, Carolyne Ekyarisiima alisema kwamba jukwaa hilo na mashindano hayo yamelenga kuhakikisha kwamba binti anawezeshwa katika ulimwengu wa kidijiti  kwa kumsogezea vishawishi mbalimbali vinavyompa motisha kuwa mbunifu kwa kutumia tehama.
 Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Dk. Inmi Patterson akizungumza na mabinti wa shule za sekondari za mkoa wa Dar es Salaam wakati wa jukwaa la kufunza wasichana wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani na kufanyika katika ukumbi wa American Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa.
 Afisa anayeshughulikia Utamaduni kutoka Ubalozi wa Marekani, Bw.  Jeffrey Ladenson akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Dk. Inmi Patterson (hayupo pichani) kufungua jukwaa la kufunza wasichana wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani na kufanyika katika ukumbi wa American Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa.
 Mwanzilishi mwenza wa Apps & Girls, Bi. Carolyne Ekyarisiima akizungumzia shindano la ubunifu wa programu za kompyuta ambalo limelenga kuhakikisha kwamba binti anawezeshwa katika ulimwengu wa kidijiti wakati wa jukwaa la kufunza wasichana wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani na kufanyika katika ukumbi wa American Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Nancy Kaizilege akifafanua jinsi  gani vijana wanavyoweza kubuni miradi inayolenga kufikia malengo ya maendeleo endelevu wakati wa jukwaa la kufunza wasichana wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani na kufanyika katika ukumbi wa American Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa
 aadhi ya wasichana 156 kutoka shule 25 za Dar es salaam walioshiriki jukwaa la kufunza wasichana wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani na kufanyika katika ukumbi wa American Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa.
Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Dk. Inmi Patterson katika picha ya pamoja na wasichana 156 kutoka shule 25 za Dar es salaam wakati wa jukwaa la kufunza wasichana wajasiriamali (Girls Entrepreneurship Summit -GES 2018) lililoandaliwa shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama ‘Apps and Girls’ kwa kushirikiana na Ubalozi wa Marekani na kufanyika katika ukumbi wa American Corner uliopo Maktaba Kuu ya Taifa.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

POLISI MKOA WA PWANI WANAWASHIKILIA WATU WANNE KWA TUHUMA ZA WIZI

$
0
0
Na  Mwandishi Wetu, Kibaha Pwani
WATU wanne  wanashikiliwa na  Jeshi  la Polisi Mkoa wa Pwani  kwa tuhuma za  uvunjaji wa nyumba  usiku na  kuiba katika  maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani ambapo jumla ya mali zote zilizokamatwa zina thamani kiasi cha Shilingi Mil. 18,800,000.

Watuhumiwa  hao wamekamatwa  kufuatia msako  mkali ulioendeshwa na  makachero wa kupambana  na makundi yanayojihusisha na matukio ya uvunjaji na kuiba mali za watu  katika nyakati za usiku na mchana.

Yamesemwa  hayo  na Kamanda  wa Jeshi  la Polisi Mkoa wa Pwani   ACP  Nyigesa Wankyo  amesema kuwa  majina ya watuhumiwa  yamehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi na kufanikisha kuukamata  mtandao wote wa walioshirikiana  nao katika matukio ya uvunjaji.

RPC   Wankyo alisema kuwa katika msako huo wamefanikiwa  kukamata vitu  mbalimbali  amabvyo ni luninga  kumi   za aina  mbalimbali ( zote Flat Screen) , jenereta kubwa mbili zenye thamani ya sh.6, 500,000, jenereta hizo ni aina ya  Euro Power  EP.6500E na Boss  BG-2500.

Vitu vingine vilivyokamatwa  katika msako huo ni  pamoja na  deki mbili,ving'amuzi viwili, spika mbili  music system mbili, home theatre, rimoti sita, speaker twiter mbili, flash moja, kapeti za chini ya sakafu mbili, stendi moja ya vyombo na extention moja.

Aidha Kamanda amesema  kuwa wamemkamata mtuhumiwa mmoja akiwa na lita 200 za mafuta ya dizeli  ambapo alikutwa na madumu kumi yenye ujazo wa lita 20  mafuta hayo alikua ameiba katika karakana ya mradi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) iliyopo eneo la Soga  Wilaya ya Kipolisi Mlandizi.

Pia amewaasa  wale wote  wanaohujumu  mradi wa  mkubwa wa ujenzi wa reli ya kisasa kwa kuiba mafuta  kuacha mara moja tabia hiyo kwani Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani  hawatakuwa na muhali  nao na mtu  yeyote atakayejaribu kujihusisha  na vitendo  vya wizi  tutawakamata  na kuwafikisha mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.

"Mtuhumiwa huyo alikamatwa katika kijiji cha  Mperamumbi akiwa amepakia  mafuta  hayo  kwenye pikipiki aina ya SANLG namba MC.197BJD.Mtuhumiwa anashikiliwa  kwa mahojiano zaidi  kwa lengo la  kubaini walem wote ambao  amekuwa  akishirikiana nao katika wizi huo  wa  mafuta  na atafikishwa  Mahakamani kujibu tuhuma hizo mbili zinazomkabili" alisema Wankyo.

Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani  limekamata bhangi kiroba kimoja  kilichokua kinasafirishwa kwenda kuuzwa, katika tukio hulo mmiliki wa  pikipiki  yenye namba za usajiliMC951  BSA anaombwa  kujisalimisha  kwenye kituo  chochote cha Polisi ndani ya siku  tatu vinginevyo atasakwa  popote  pale aliko ili kujibu  tuhuma za kusafirisha  bangi ambayo aliitelekeza ikiwa  kwenye  pikipiki  hiyo  baada ya  kugundua  anafuatiliwa na  askari  wa jeshi la polisi.

"Kutokana na  matukio haya Jeshi  la Polisi  Mkoa wa Pwani  tunatoa wito  kwa wananchi  kuwa  wabia  katika  suala zima  la  ulinzi  shirikishi kwenye maeneo  tao ili  kuweza  kukabiliana  na matukio ya uvunjaji wa sheria..Pia tunatoa  rai kwa  wananchi  wa Mkoa wa Pwani kuwafichua  wale wote wanaoshirikiana  na wahalifu  kwenye maeneo  yao kwani  haiwezekani  mahali pakavunjwa  katika mtaa bila  ya kuwepi na wenyeji  wanaowafahamu alisema  RPC Wankyo.

"Natoa wito kwa  wananchi kuacha tabia ya  kununua  vitu vya mikononi bila kupewa risiti  ya kile  wanachokinunua, wale wote ambao  watakutwa  na mali  ya wizi  nao tutawachukulia hatua  kali za  kisheria  ili iwe mfano kwa wengine"alisema Kamanda huyo.
 Kamanda  wa Jeshi  la Polisi Mkoa wa Pwani   ACP  Nyigesa Wankyo akiwa na baadhi ya maofisa wa Jeshi la Polisi  akizungumza na waandishi wa habari

MAKAMU WA RAIS ATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MAREHEMU MERCY MENGI

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Mercy Mengi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Moshi mjini, kushoto kwa Makamu wa Rais ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Anna Mghwira. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa mkono wa pole Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Mzee Reginald Mengi mara baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Mercy Mengi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Moshi mjini.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro ambaye alikuwa moja ya waliohudhuria ibada ya kuuaga mwili wa marehemu Mercy Mengi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Moshi mjini.

 Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Mzee Reginald Mengi akizungumza na mwanae Bw. Abdiel Mengi wakati wa Ibada ya kuuaga mwili wa Marehemu Mercy Mengi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Moshi mjini.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Dkt. Maria Kamm (kulia) ambaye alikuwa moja ya waliohudhuria ibada ya kuuaga mwili wa marehemu Mercy Mengi katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Moshi mjini.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

PROF. KAMUZORA AWATAKA WAKULIMA WA KASULU KUZALISHA KWA TIJA

$
0
0

NA MWANDISHI WETU
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera na Uratibu Prof.Faustin Kamuzora amewataka wakulima wa Wilaya ya Kasulu kulima kwa tija ili kuondokana na changamoto wanazokabiliana nazo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa masoko.

Ametoa kauli hiyo Novemba 08, 2018 alipofanya ziara katika maeneo ya Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara Local Investment Climate (LIC) ikiwemo Mradi wa Umwagiliaji wa Tittye Wilayani Kasulu mkoani Kigoma ili kukagua na kujiridhisha ubora na faida zitokanazo na mradi huo.

“Wakulima wa Wilaya ya Kasulu hamna budi kubadili mitazamo katika uzalishaji kwa kuanza kuweka mikakati ya kuzalisha kwa tija ili kuondokana na changamoto za kukosa masoko ya mazao ikiwemo Mpunga na mihogo hivyo ni wakati muafaka kuwatumia maafisa kilimo waliopo ili kupata mbinu mbadala za matumizi mazuri ya pembejeo za kisasa ili kuzalisha kwa tija”.Alisema Prof.Kamuzora

Aliongezea kuwa wakulima wanapaswa kuondokana na dhana potofu ya kilimo cha asili kinachohusisha dhana ya kulima kwa dawa za kienyeji ambazo wamekuwa wakizitumia kwa muda mrefu bila kuleta matunda wanayotarajiwa.

“Ni vyema sasa kuachana na kilimo cha matumizi ya dawa za kienyeji na hatimaye muone namna bora ya kuwatumia wataalam wa masuala ya kilimo ili  kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia ili kuzalisha kwa tija.”Alisisitiza Prof.Kamuzora

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe.Kanali Simon Anange aliahidi kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Katibu Mkuu huyo pamoja na kutoa rai kwa wakulima wa Kasulu kuendelea kuzalisha kwa tija ili kuendana na soko lililopo.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof.Faustin Kamuzora (wa kwanza kushoto) akiuliza jambo kwa Mkurugenzi wa Kasulu Vijijini Mhandisi Godfrey Kasekenya alipotembelea kukagua mradi wa Umwagiliaji wa mashamba ya mpunga wa Titye uliojengwa na Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (Local Investment Climate -LIC) unaoratibiwa na Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) uliopo Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoama Novemba 08, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe.Kanali Simon Anange akizungumza jambo wakati wa kikao cha pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof.Faustin Kamuzora alipotembelea ofisini kwake kwa lengo la kupata taarifa za miradi inayotekelezwa chini ya uratibu wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC).
Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara Bi.Oliver Ligula akichangia jambo wakati wa kikao na Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Mhe.Kanali Simon Anange pamoja na baadhi ya Watendaji wa Wilaya hiyo walipotembelea kukagua utekelezaji wa Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara ( Local Investment Climate -LIC) katika Wilaya hiyo.
Afisa wa Baraza la Biashara la Taifa na Mratibu wa shughuli za Mabaraza ya Biashara Kigoma Bw. Ano Mwamsiku akieleza mafanikio ya mabaraza ya biashara kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof.Faustin Kamuzora (hayupo pichani) wakati wa kikao cha pamoja na Watendaji wa Wilaya ya Kasulu walipotembelea kupata taarifa za utekelezaji wa miradi ya LIC.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kupokea taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Umwagiliaji ya mashamba ya mpunga ya Titye inayofadhiliwa na Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (Local Investment Climate -LIC) Wilayani Kasulu Mkoani  Kigoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Misri wakutana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi

$
0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Zanzibar imejitolea na kuwa tayari kuendelea kushirikiana na Misri katika kudumisha uhusiano wa muda mrefu uliojikita katika masuala ya Utamaduni unaofanana pamoja na Maendeleo ya Kiuchumi.
Alisema pande hizo mbili bado zina fursa zaidi ya kushikamana katika misingi iliyoachwa na Viongozi waasisi wa Mataifa ya Misri na Tanzania, mshikamano unaohitaji kuelekezwa katika ushirikiano wa Sekta za Kilimo, Elimu, Utalii pamoja na Viwanda.
Balozi Seif Ali Iddi alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na Ujumbe wa Wafanyabiashara waandamizi kutoka Taasisi mbali mbali za Kibiashara wa Nchini Misri aliokutana nao katika Ukumbi wa Majengo ya Kasri ya Kifalme iliyopo Mizingani Forodhani Mjini Zanzibar.
Alisema Makampuni na Taasisi za Kibiashara za Nchini Misri zina nafasi ya kuangalia fursa za uwekezaji zilizopo Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kwa vile Zanzibar binafsi imeshaamua kuimarisha Sekta ya Utalii ikienda sambamba na muelekeo wa Ujenzi wa miundombinu ya Viwanda.
“ Zanzibar na Misri bado zinahitaji kuendelea kushirikiana katika Sekta za Uchumi ili kuimarisha  uhusiano wa pande hizo zinazofanana Kiutamaduni”. Alisisitiza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
Balozi Seif alisema hatua hiyo inayoweza kuungwa mkono na Wafanyabiashara hao wa Misri kupitia Taasisi na Makampuni yao imelenga kuimarisha Sekta ya Uchumi kwa kupunguza changamoto inayowakabili Vijana ya ukosefu wa ajira, kundi ambalo ndio nguvu kazi ya Taifa.
Alisema Sekta ya Utalii na Viwanda iwapo Wafanyabaiashara hao wataamua kwa makusudi kusaidia kuongeza nguvu zao za  Uwezeshaji na Taaluma yanaweza kustawisha Pato la Taifa na kuibua fursa nyingi zaidi za ajira.
Mapema Kiongozi wa Msafara wa Ujumbe huo wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Misri ambae pia ni Rais wa Shirikisho la Taasisi za Kibiashara Nchini humo Dr. Sharif  El – Gabaly alisema Zanzibar ni muhimu kwa Misri kutokana na mfanano wa mazingira ya Kiutamaduni ya Wananchi wake.
Dr. Sharif  alisema ziara yao ya siku Mbili Visiwani Zanzibar imewapa faraja kubwa ya kufurahia utajiri wa Bidhaa za Viungo zinazozalishwa na Wakulima wa Zanzibar wenye kuonyesha ukomavu wa kujituma katika masuala ya kazi za ujasiri amali zinazowapatia kipato.
Alisema yapo mambo mengi waliyojifunza katika ziara yao hiyo ambayo imewapa Wafanyabiashara hao wazo la kuwashawishi Wataalamu wa Makampuni na Taasisi zao kuchangamkia fursa za Uwekezaji zilizopo Zanzibar katika Sekta za Utalii na Viwanda.
Katika mazungumzo hao Viongozi wa Ujumbe huo wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Misri wamefikiria wazo la kuanzisha Kituo cha Biashara Zanzibar kitakachoshughulikia uratibu wa Bidhaa zinazozalishwa Nchini Misri kupatikana Visiwani Zanzibar.
Ziara ya Viongozi hao imepata Baraka kwa kusaini Mkataba wa Ushirikiano wa Kibiashara kati yake na Chama cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Wakulima Zanzibar.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Ujumbe wa Wafanyabiashara wa Nchini Misri uliopo Zanzibar kwa ziara ya Siku Mbili.
 Balozi Seif  Kulia akiwashawishi Wafanyabiashara wa Misri kufikiria wazo a kuanzisha miradi yao Visiwani Zanzibar wakati akibadilishana nao mawazo.
 Kiongozi wa Msafara wa Ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Misri ambae pia ni Rais wa Shirikisho la Taasisi za Kibiashara Nchini humo Dr. Sharif  El – Gabaly akimueleza Balozi Seif faraja ya ujumbe wake kutokana na mazingira mazuri ya Uwekezaji yaliyopo Zanzibar.
 Balozi Seif Kulia akimpatia zawadi ya baidhaa za Viungo Kiongozi wa Msafara wa Ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Misri   Dr. Sharif  El – Gabaly baada ya kumaliza mazungumzo yao wakishuhudiwa kati kati na Waziri wa Biashara na Viwanda Zanzibar Balozi Amina Salum Ali.
 Kiongozi wa Msafara wa Ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Misri   Dr. Sharif  El – Gabaly Kulia akimkabidhi zawadi Balozi Seif  ya Bidhaa zinazozalishwa Nchini Misri.
Balozi Seif  wa Nne kutoka Kushoto waliokaa vitini akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Misri pamoja na wale wa Wizara ya Biashara na Viwanda Zanzibar.
Ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Nchini Misri ulipokutana kwa mazungumzo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwenye ukumbi wa majengo ya Kasri ya Kifalme Mizingani Forodhani Mjini Zanzibar. 
Picha na Habari na OMPR ZANZIBAR

UBALOZI WA POLAND WAADHIMISHA MIAKA 100 YA UHURU

$
0
0
Balozi Ramadhan Mwinyi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisoma hotuba katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Taifa ya Poland iliyofanyika kwenye makazi ya Balozi jijini Dar Es Salaam tarehe 09 Novemba 2018. 
Mhe. Krzysztof Buzalski, Balozi wa Poland nchini akisoma hotuba katika hafla ya kuadhimisha miaka 100 ya uhuru wa Poland 
Baadhi ya wageni mbalimbali walioshiriki hafla hiyo wakisikiliza kwa makini hotuba za viongozi 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi alikuwa Mgeni Rasmi katika sherehe za kutimiza miaka 100 ya Uhuru wa Taifa la Poland. Sherehe hizo zilifanyika katika makazi ya Balozi wa Poland, Mhe. Balozi Krzysztof Buzalski yaliyopo Oystberbay, Jijini Dar es Salaam tarehe 09 Novemba 2018

Katika Sherehe hizo, Naibu katibu Mkuu pamoja na mambo mengine alifafanua kuwa uhusiano baina ya Poland na Tanzania ni wa kihistoria na kuwa unaimarika siku hadi siku. 

Pamoja na kuishukuru Poland kwa uwekezaji katika maeneo mbalimbali ikiwemo kilimo, amemuomba Balozi Buzalski, kuongeza jitihada katika kuvutia wawekezaji zaidi wa Poland kuja kuwekeza hapa nchini na kusaidia kutangaza vivutio vya utalii wa Tanzania nchini Poland.

Naibu Katibu Mkuu amemhakikishia Balozi wa Poland kuwa Wizara na Serikali kwa jumla itampa ushirikiano wakati wowote atakapohitaji ili kufanikisha malengo kwa manufaa ya mataifa yote mawili. 

Viewing all 110170 articles
Browse latest View live




Latest Images